Quantcast
Channel: UDAKU SPECIAL
Viewing all 104709 articles
Browse latest View live

Nay wa Mitego Aongea Kitu Kuhusu Vanessa Mdee na Sakata la Dawa za Kulevya...!!

$
0
0

Msanii wa muziki wa hip hop Nay wa Mitego amefunguka kwa kumpa pole mwanadada Vanessa Mdee ambaye anashikiliwa na jeshi la polisi kwa tuhuma za kutumia na kusambaza dawa za kulevya.

Muimbaji huyo alijisalimisha kwa jeshi la polisi siku 5 zilizopita baada ya kutajwa kwenye list ya RC Makonda ya watu wanaojihusisha na biashara ya dawa za kulevya na kutakiwa kujisalimisha polisi central kwajili ya mahojiano.

Rapper huyo ameonyesha kuguswa na tukio hilo lililomtokea muimbaji huyo wa wimbo Cash Madame huku akimtaka kuvumilia kwa yote yanayoendelea.

“Vanessamdee Sijui ulipo anzia, but mpaka apa ulipofikia umepambana sana. Nina imani mungu ndo aliye kufanyia wepesi mpaka kua #BrandKubwa na kupata hatua Ulizo nazo. Naamini Mungu Huyu Huyu ndiye atakae kufanyia Wepesi Kwenye yanayo kukabili ivi sasa. Amini izi ni Changa moto tu na ni Mapito ambayo Binadamu tunapitia kwenye Safari ya kuelekea kutimiza Ndoto zetu,” aliandika Nay Instagram.

Aliongeza, “I pray for you my friend Vanessa, naamini brand yako haiwezi haribika kirahisi kwa sababu umepambana sana ni wasichana wachache wenye kuweza ku-fight kama wewe. Mungu ata kusimamia uzidi kusonga mbele, Haya yata pita nina imani utakua strongZaidi. #CashMadame KeepItUp. Napenda kuona Wasichana wakifanikiwa kwa kufanya kazi kwa bidii #VannesaTheBrand wewe ni mwanamke wa shoka. Usiyumbishwe kuwa Mfano. Najivunia uwepo wako kwenye Game,”

CCM ni Kusuka Au Kunyoa Leo...!!!

$
0
0

CHAMA Cha Mapinduzi (CCM) leo kinafanya vikao viwili vikubwa kwa mkupuo vya Kamati Kuu (CC) na Halmashauri Kuu ya Taifa (NEC) mjini hapa.

Vikao hivyo vitafanyika kwa siku moja, baada ya Kamati Kuu kutofanyika jana. Badala yake siku nzima ya jana, ilitumika kwa ajili ya kikao cha Kamati ya Usalama na Maadili ya chama.

Kikao hicho cha Kamati ya Usalama na Maadili cha jana, kiliangalia maadili ya wanachama wake na kiliongozwa na Mwenyekiti wa Taifa wa CCM, Rais John Magufuli.

Pamoja na mambo mengine, kikao hicho hujadili nidhamu za viongozi na baadhi ya wanachama waliokwenda kinyume na maadili ya chama hicho.

Kamati hiyo huhoji wanachama na viongozi na mapendekezo yake, hupelekekwa Kamati Kuu kwa ajili ya hatua zaidi.

Akizungumza na waandishi wa habari mjini hapa, Katibu wa NEC, Itikadi na Uenezi, Humphrey Polepole alisema, vikao hivyo vitafanyika leo, ambapo Kamati Kuu itakutana asubuhi.

Alisema baada ya Kamati Kuu kumaliza kikao chake, mchana Halmashauri Kuu itafanya mkutano wake, ambao ndio utakaoandaa ajenda kwa ajili ya Mkutano Mkuu Maalumu wa chama hicho, utakaofanyika kesho, ambao utafanya mageuzi makubwa katika chama.

Baadhi ya mageuzi hayo ni kubadilisha Katiba na Kanuni za chama pamoja na jumuiya zake, ikiwemo kupunguza wajumbe wake ili kuwa chama cha ufanisi zaidi.

Lema Asimulia Alivyowakuta Watoto Wadogo Gerezani...!!!!

$
0
0

Mbunge wa Arusha Mjini (Chadema), Godbless Lema, amesema akiwa magereza amewakuta watoto wadogo, mmoja wa miaka 14 ambaye amefungwa mwaka mmoja kwa kukutwa na bangi na tayari taarifa zake amepeleka kwa Msajili wa Mahakama Kanda ya Arusha.

Lema aliyasema hayo jana mbele ya maelfu ya wakazi wa Jiji la Arusha waliojitokeza katika mkutano wake wa kwanza tangu atoke gerezani, kwa dhamana.

Machi 3, mwaka huu, Lema aliachiwa kwa dhamana baada ya kukaa gerezani miezi minne tangu alipokamatwa akiwa bungeni mjini Dodoma, Novemba mwaka jana.

Alisema ameshuhudia pia vijana 65 wa Jiji la Arusha ambao wamekaa miaka minne gerezani kwa tuhuma za ugaidi na kwamba, hadi sasa kesi yao haijaanza kusikilizwa na wamekuwa wakiteswa hadi mmoja kuvunjwa mguu.

“Ndugu zangu kukaa magereza kumenipa ujasiri mkubwa na kumesaidia kujua shida za watu, kwani kuna watu wamefungwa maisha kwa kukutwa na mirungi wakati nchi jirani Serikali inatoa fedha kupanua mashamba ya mirungi,” alisema lema.

Mbunge huyo alisimulia mwanzo mwisho mambo aliyojionea gerezani kwa muda wa miezi minne aliyokaa huko.

Kimenukaa..Jacquline Wolper Afunguka Haya ya Aibu Juu ya Harmonize...!!!

$
0
0

STAA wa filamu za Kibongo, Jacqueline Wolper kwa mara ya kwanza tangu aachane na mpenzi wake, Rajab Abdulhan ‘Harmonize’ ameibuka na kusema amewaachia penzi wajuaji.

Wolper alisema kuwa baada ya kumwagana na Harmonize kwa sasa ameamua kujikita zaidi katika kufanya mambo yake ya kimaendeleo na mambo ya mapenzi na msanii huyo wa Bongo Fleva amewaachia wajuaji ambao anaamini walikuwa wakimtolea macho kitambo.

“Harmonize nimewaachia wajuaji wawe naye, nimeamua kuwa bize na mambo yangu ya maendeleo zaidi, suala la mapenzi nimeliweka pembeni kwanza,” alisema Wolper.

Breaking News..Timua Timua Yaanza CCM,Magufuli Amtimua Uanachama Sophia Simba,Nchimbi na Kimbisa Wapewa onyo Kali..!!!

$
0
0

Mwanachama Mkongwe wa CCM na Aliyekuwa Mwenyekiti wa Jumiya ya Wanawake Taifa UWT,Sophia Simba Amevulia Uanachama wa Chama na Kamati ya Maadili ya Halmashauri kuu ya Taifa ya CCM ,NEC,.

Aidha Balozi Emannuel Nchimbi na Adam Kimbisa Wamepewa Onyo Kali Juu ya Tabia na Mienendo yao Isiyoridhisha dhidi ya chama.

Taarifa Zaidi Zinakuja...

Toyota Alteza Inauzwa Bei Nafuu Kabisa

$
0
0
Toyota Altezza inauzwa bei poa
IPO DAR, Bunju
Namba CBR
Kilometer 110,000
Four Cilinder
Sh Million 7.5
Maelewano yapo
Piga simu 0714604974

Hatarii...Kafulila Aingia Katika Vita ya Makonda,Amtaka Aonyeshe Vyeti Vyake ...!!!!

$
0
0

Aliyekuwa Mbunge wa Kigoma Kusini, David Kafulila ameibuka na kuongea mambo matano kuhusiana na sakata la vyeti feki linalomuandamana Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam, Paul Makonda.Kafulila amesema yafuatayo;

"Kwanza ni ushauri wangu kwamba Makonda amsaidie Rais ama kwa kuonesha vyeti vyake vyote kuondoa utata au ajizulu ili serikali iendelee na mambo mengine. 

"Obama alipotuhumiwa kuhusu uraia wake USA alifanya kazi ndogo tu ya kuweka vyeti vyake vyote hadharani na akawa amefunga utata wa uraia wake. hivyo ni vema Makonda afanye hivyo kama anavyo au akae pembeni kwani nchi ni muhimu kuliko mahusiano yake na Rais.


"Rais anapaswa kujua kuwa hoja ya jinai ya kughushi vyeti inayopigiwa kelele inahusu pia umakini wa mamlaka yake kama mteuzi wa Makonda kwamba kuna shida ya vetting. hivyo kuondoa hilo ni kuchukua hatua stahiki. hakuna namna Rais atamlinda Makonda na akabaki na sifa ya kuwa Rais anaesimamia haki na Usawa. Itafanya aonekane kama waliomizwa na ukali wake katika kusimamia sheria ni kwasababu hawakuwa na ukaribu nae na zaidi itafanya aonekane Rais wa kawaida sana kwa kulinda uovu kwa sababu za binafsi.Hivyo ukimya wa Rais unafanya dhamira yake ya uzalendo ihojike kwani sio kawaida yake.


"Mamlaka kama Sekretariet ya Maadili ya Uongozi ilipaswa kuwa imeshachukua hatua kuondoa wingu hili kwani kinachojadiliwa hapa mbali zaidi ya jinai pia kinahusu uadilifu wa Kiongozi(intergrity). ukimya wa taasisi hii ni mfano mbaya wa namna taasisi zinavopigwa ganzi pindi haki inapotakiwa kutendeka lakini inagusa maslahi ya Rais. huu ni uzoefu niliopata kuona hata kwenye sakata la Escrow.likitokea jambo ambalo Rais ana maslahi taasisi zetu zimekuwa nzito na kigugumizi kuchukua hatua ipasavyo.


"Chuo cha Uvuvi walichomsajili kwa cheti cha form4 ambacho anatuhumiwa kuwa sio chake pamoja na Chuo Kikuu ni taasisi ambazo mjadala huu unahusu heshima ya taasisi hizo. hivyo ilipaswa zijitokeze kuthibitisha au kukanusha. ukimya wao unaashiria hofu yao kwasababu kaguswa mtoto wa mfalme! Huu ni mfano mbaya kabisa kwa taasisi za taaluma kwamba zinaweza kuwa za hovyo kiasi hiki.


"Kibaya zaidi ni ukimya wa NECTA ambao ni mamlaka ya kutoa vyeti. sasa cheti kinachosumbua hapa ni cha form4 ambacho ni mali yao. lakn kwa woga wamekaa kimya kuficha ukweli na kuacha mjadala wa cheti uwe kati ya Askofu na RC na watanzania wakati wao ambao ni mamlaka sahihi kuondoa utata wamekaa kimya kwa hofu ya kugusa mtoto wa mfalme.. Hili ni fundisho la kwani nchi hii haiendelei kwasababu taasisi hizi haziko imara kutimiza majukumu yake kisheria bali zinafanya majukumu yake kwa kadiri ya mapenzi ya mteule wao."

Pichazzz..Hivi Ndivyo Makada wa CCM Walivyomshushia Kipigo cha Paka Mwizi Mbunge wa Chadema Aliyepita Kwenye Jengo la CCM Makuu Dodoma...!!!!

$
0
0


Mbunge wa Chadema Kunti Majala ameokolewa na Polisi Mara baada ya  dereva wake kushushiwa kipigo na makada wa Chama Cha Mapinduzi ,Baada ya Kuendesha Gari Hilo Karibu na Makao Makuu ya CCM Dodoma.
N:B Jengo lipo karibu na barabara magari yanapopita kwahiyo mbunge alikuwa anapita barabarani

Lipumba Aonekana Usiku Akiwa na Vigogo wa CCM Dodoma..!!!

$
0
0

Mwenyekiti wa CUF anayetambuliwa na msajili wa vyama vya siasa Professor Ibrahim Lipumba alionekana jana usiku akiwa katika hoteli waliyopanga vigogo kadhaa wa CCM Zanzibar wanaohudhuria vikao vya chama hicho Dodoma.

Haikuweza kufahamika mara moja kama Lipumba alikuwepo kama mwalikwa ingawa ilishangaza kumuona nyakati za usiku katika hoteli hiyo akiwa na vigogo hao wa CCM Zanzibar.

Lipumba anatuhumiwa na CUF kwamba anakihujumu chama hicho na amekuwa akishirikiana na CCM kutaka kukiangamiza.

Taifa Linalishwa Uongo, Sio Trump Wala Magufuli..!!!!

$
0
0

Kuna upuuzi unaendelea mitandaoni na wabana pua kwamba oooho Trump ampongeza rais wetu kipenzi. Ikulu ya Marekani ndio inaandika kiingereza kibovu vile na inatumia wasapu siku hizi badala ya njia sahihi toka White House Kiingereza kile kina sura na mfanano kabisa wa mwandiko wa ndugu yangu Humphrey Polepole, labda siku hizi amekuwa mwandishi na msemaji wa Donald Trump wa Chamwino pale Dodoma...Lakini Trump yule wa Marekani sijui kama anajua kuwa kuna Tanzania ya Magufuli, ninachofahamu anajua kuna Afrika ya Nyerere, Nkurumah, Mandela, Lumumba, Mugabe, Museven nk..... 

Hotuba ya Donald Trump wakati akisaini sheria ya kuzuia wahamiaji kuingia nchini mwake hakuna mahali alipotamka neno Magufuli, wala hakuna alipomsifu... Nilifuatilia hotuba ile, lakini mtandao wa radio ya Ufaransa ya kiswahili umechomekea maneno hayo nakufanya habari kuwa tofauti kamia propagsnda za aona hii bisa, Ukweli Rais wetu tutamsifu wenywe kwa mazuri yake sio kwakutumia propaganda za aina hii, Bahati mbaya vyombo vya habari vya kimataifa vinavyotumia lugha ya kiswahili vingi vimejaa watanzania wenye ushabiki wa vyama (makada) ambao muda mwingi wanatumika vibaya.

Rais asifiwe kwa mazuri yake mfano mimi namuunga mkono kwa 100% Zanzibar ibebe msalaba wake, Muda wa kubebwa Zanzibar umekwisha ilipe deni la tanesco ili shirika letu liweze kujiendesha... Tumewabeba kwenye bajeti ya Masuala ya Muungano ambapo Bajeti huwa kati ya trilion 2-2.5 lakini Zanzibar huchangia sifuri katika Mfuko huo wa Muungano uitwao JVC committee. Wakati huo bajeti ya Zanzibar ni kati ya 500b hadi 550b lakini pato la Zanzibar ni 150b, hivyo kiasi cha zaidi ya 350b huwa tunawachangia sisi tani kodi zetu zinakwenda kuwahudumia wao kule... Baada ya hapo katika baje ya Muungano hutengwa 34b kwaajili ya Rais wa Zanzibar, hii huitwa pesa maalumu ikitumika kwa shughuli maalumu za kiusalama na mengineyo... Hii inatoka pia kwa walipa kodi wa Tanganyika, Je Zanzibar inachangia nini kwa Tanganyika? Jibu ni sifuri..... Zaidi ni ulinzi wa Bahari na UDUGU.
Hili ndilo linanifanya nimuunge mkono rais wangu kipenzi...

Mafanikio ya Makonda ni Uthibitisho Wa Jiwe Walilolikataa Waashi Litafanywa Kuwa Jiwe Kuu la Pembeni..!!!

$
0
0

Ukiisikia simulizi ya Makonda, alipotoka, alipo na anapokwenda, mtakubaliana na mimi kuwa hii ni kazi ya Mungu katika kuonyesha uwezo wake kwa wanadamu kwa kuufanya muujiza wa Jiwe Walilolikataa Waashi, Litafanywa Kuwa Jiwe Kuu la Pembeni.

Historia Yake Kuzaliwa na Familia
Makonda alizaliwa Februari 15, 1982 majira ya saa 1:30 asubuhi, familia ya mzee Makonda (Baba hatajwi majina) na mkewe, Suzan, walimkaribisha mtoto wao pekee wa kiume katika Zahanati ya Kolomije, wilayani Misungwi mkoani Mwanza.

Elimu ya Msingi, Sekondari na Chuo.
Makonda ni mhitimu wa Chuo Kikuu cha Ushirika Moshi. Kabla ya kwenda Moshi, alipita katika Shule ya Msingi Kolomije na amesoma pia katika Chuo cha Uvuvi, Mbegani, Bagamoyo ambako alisoma hadi ngazi ya Diploma katika masuala ya uvuvi.Hakuna maelezo alisoma wapi Sekondari wala hakuna index number yoyote ya Necta yenye majina yake.

Kabla ya Chuo.
Makonda alianzia kazi ya kuchimba mchanga.
Akaja kazi ya kuchoma mkaa.
Akawa utingo kwenye mabasi stendi
Kisha akawa kondakta yaani Makonda akawa konda.

Ukiwa ni mpakwa mafuta kama Daudi, Mungu atakuinua kutoka chini ulipo na kukupandisha mahali pa juu palipo inuka.
Mibaraka.
Mibaraka kwa Makonda ilianzia siku yake ya kuzaliwa February 15, mwaka 2015 Rais Jakaya Kikwete alipomteua Makonda kuwa Mkuu wa Wilaya ya Kinondoni na kutangazwa Februari 18, mwaka 2015. Kuteuliwa siku yako ya kuzaliwa sio coincidence bali ni mipango ya Mungu.

Mibaraka Zaidi.
Hii ni kazi ya mikono yake kwa baraka za Bwana. (Not necessarily ni kweli)
Inasemekana Mungu amemuwezesha
Makonda kununua jengo (apartment), pale Viva Towers kwa Sh600 milioni. Makonda amempa mke wake gari aina ya Mercedes Benz lenye thamani ya Dola 250,000 za Marekani (Sh550 milioni) kama zawadi ya ‘Birthday’,”
Makonda ana gari aina ya Lexus, lenye thamani ya Sh400 milioni. Makonda anamiliki magari mengine ya kifahari aina ya V8, anajenga maghorofa jijini Mwanza na amekarabati ofisi yake kwa Sh400 milioni zake binafsi.

Japo there is something missing ambayo ni a missing link kwenye story ya Makonda ambayo wazazi hawajaisema, Makonda mwenyewe hajaisema, wala sijaisikia ikisemwa popote, kuhusu elimu ya Sekondari, the bottom line ni the end justify the means.

Huwezi jua!.

Mwacheni Mungu aitwe Mungu.

Paskali

CCM Yawatimua Makada 12,Yupo Sophia Simba na Mwenyekityi wa CCM Dar Es Salaam,Ramadhan Madabida..!!!

$
0
0

Chama cha Mapinduzi kimewafukuza makada 12 wa chama hicho wakiwemo wanachama mkongwe kama, Sophia Simba, Ramadhan Madabida na Jesca Msambatavangu.

Wakati wanachama hao wakifukuzwa wengine wanne wamepewa onyo kali,  sita wamevuliwa uongozi na kuwekwa chini ya uangalizi mkali wa miezi 30, huku mwenyekiti wa chama hicho Dodoma, Adam Kimbisa akisamehewa.

 Uamuzi huo umetolewa baada  wa kikao cha Nec kilichofanyika Dodoma leo (Jumamosi) na kuongozwa na mwenyekiti wake, Rais John Magufuli.

Kwa Mara ya Kwanza..Chadema Watoa Ushauri Huu kwa Wajumbe wa Mkutano Mkuu wa CCM ...!!!!

$
0
0

Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), kimewaomba wanachama wa CCM wanaoanza mkutano mkuu wao maalumu kesho, kuweka mbele uzalendo badala ya ushabiki wa kisiasa.

Akizungumza na waandishi wa habari jijini Dar es Salaam jana, Katibu Mkuu wa Chadema, Dk Vincent Mashinji alisema wanachama wa CCM wanapaswa kuutumia mkutano huo kuisema Serikali yao kuhusu kupuuza mambo ya msingi, ikiwamo malengo ya bajeti iliyopitishwa na Bunge.

Alisema imekuwa kawaida kwa Serikali kupuuza mambo ya msingi na kufanya ambayo hayamo kwenye bajeti huku baadhi ya maeneo yakikosa huduma muhimu.

Dk Mashinji alitoa mfano kuwa, mwaka wa bajeti wa 2016/17 unakaribia kwisha, lakini kiuhalisia utekelezaji wake uko robo ya nne na haujafikia asilimia 40.

Katibu mkuu huyo wa Chadema alisema mbali na hayo, Serikali haitaki kusimamiwa kikamilifu na inauyumbisha mhimili wa Bunge ambapo vikao vya kamati za Bunge vimeshindwa kuanza kama ilivyopangwa awali kwa wiki tatu, badala yake muda umepunguzwa hadi wiki mbili. Aliongeza kwamba bajeti iliyopitishwa imekuwa haiheshimiwi na kuingiziwa matumizi ambayo hayakuwemo ikiwamo Serikali kuhamia Dodoma, kujenga kiwanja cha ndege Chato na Magereza ya Ukonga

Wakati Mwingine Wanasiasa Wawe Wakweli, Katibu Mkuu Umoja wa Mataifa Hakuwa na Ziara Rasmi Tanzania..!!!!

$
0
0

Naona watu wameibeba hii ya Katibu Mkuu wa UN kama "ajenda" tena,huku namuona Mtatiro akirusha makombora,na huku Mbunge Msigwa akirusha kwa upande wa pili.Vijana nao wamebeba mitandaoni kama ajenda ya kumalizia week kimjadala.

Watu wanatakiwa kuelewa tu,mambo mengine sio lazima tuingize siasa saaaanaa.António Guterres hakuwa na ratiba ya ziara ya Tanzania.Ziara yake ilipangwa kufanyika Somalia ili kuonana na Rais mpya kuhusu baa la njaa na ukame unaolikumba eneo hilo.

Sehemu ya pili ikawa Kenya kukutana na Kenyatta,na hii ni kwa sababu,nchini Kenya kuna kambi kubwa sana ya wakimbizi ya Dadaab, inayokaliwa na Wasomali,ambao sera ya Trump ya katazo la Wasomali kuingia US imewaathiri...Umoja wa Mataifa lazima iwahikikishie Kenya ushirikiano ktk kipindi hiki cha mabadiliko ya sera za uhamiaji nchini Marekani.

Maana hivi karibuni,wakimbizi wengi wenye asili ya Somalia ambao walikuwa wafanyiwe "resettlement" na Shirika la Wahamiaji la Kimataifa (IMO),kutoka kambi ya Dadaab kwenda Marekani wamezuiliwa kutokana na sera mpya ya Marekani,hivyo kuwafanya waendelee kusalia Kenya.

Hapa Tanzania alikuwa tu "On Transit",sababu ndege aliyotumia kusafiri ni SwissAir.Schedule ya SwissAir ni Zurich-Nairobi-Dar-Zurich.Na inapotoka Nairobi kuja Dsm kabla ya kwenda Zurich,ndege huwa inakaa Dsm zaidi ya saa moja na nusu.Sasa mtu mkubwa kama Antonio hawezi kukaa muda wote huo ktk ndege wakati anaweza kushuka na kufanya mazungumzo ya kidiplomasia na viongozi wa Tz kama wadau wa Umoja wa Mataifa.

Aina hii ya ugeni ni ya kawaida sana katika viwanja vya ndege ambayo hutumika kama "connection centre".Ukienda Jomo Kenyata International Airport VIP Lounge utakutana na Marais wengi na viongozi wengi maarufu wakipiga soga na Mawaziri wa Mashauriano ya Kigeni wakati wakiwa "on transit".Bole International Airport pale Addis Ababa VIP-Lounge humkuti Waziri Mkuu wa Ethiopia,lakini toka mawio mpaka machweo ya jua,viongozi wa kimataifa huwa "On Transit" kuelekea katika safari zao tarajiwa.

Hata kwa kumtazama tu,wale waliowahi kupanda SwissAir First Class,watakubaliana kuwa alichokuwa amekivaa Guterres ni zile pyjamas (pajama) za abiria wa daraja la kwanza ambao hupatiwa ndani ya ndege kwa ajili ya kupumzikia kwa safari ndefu.Dressing code tu ya pyjamas za SwissAir zinaashiria Katibu Mkuu alikuwa "On Transit".Ratiba na Tanzania haikuwepo.

Sio wa kwanza Guterres kupita tu bila kuonana na Rais,wapo viongozi wengi hupita kama "On transit" hapa Dsm,na husalimiana na viongozi wa chini wa serikali.Mfano King Mswati,yeye "refueling point" yake huwa ni Dsm,katika safari zake za kutoka Mbabane kwenda ama Abu Dhabi shopping au sehemu nyingine,kituo chake cha Cattering na refueling ni Dsm.Toka enzi za JK mpaka sasa,huwezi kumkuta JK anakimbizana kumpokea Mswati,bali utamkuta Membe kwa minajili ya kidiplomasia akimsubiri King Mswati.

Uwanja wetu wa Dsm hutumika kwa ajili ya "On Transit Passengers" na "On Transfer Passengers"."On Transit Passengers" ni wale abiria ambao hupita uwanjani wakiwa ndani ya ndege bila kushuka na kuchukua abiria wengine au kushusha na kuunganisha na ndege hiyohiyo kuelekea "destination" iliyokusudiwa.Mfano wa ndege zenye safari ya aina hii Julius Nyerere Int'nal Airport ni SwissAir (Zurich-Nairobi-Dsm-Zurich),Ethiopia Airways (Addis Ababa-Dsm-Znz au Addis-Dsm-Hahaya Comoro),Oman Air (Muscat-Znz-Dsm-Muscat),Mauritius Air nk.

Siku kadhaa kiongozi wa Mauritius alipita Dsm na Mauritius Air na kuunganisha kuelekea Addis Ababa kwenye mkutano wa viongozi wa Afrika.Toka Sir Seewoosagur Ramgoolam Port Louis kupitia Julius Nyerere International Airport mpaka Addis Ababa.

Walikutana tu na Rais wetu ndani ya ndege,wakapeana mkono na kila mtu akarudi kwenye presidential Suit room yake ya "First class".

Hii ni dalili ya uwanja wetu kukua na kuanza kuwa moja ya "Connection" kubwa ya sehemu mbalimbali za Afrika na dunia.Sasa tunapokea abiria wote wa kutoka Msumbiji kwenda Dubai kupitia Dsm,abiria wa Mayote na Comoro kwenda Dubai.Abiria wa kutoka Mauritius kuja Afrika ya Mashariki na Mashariki ya kati ya Asia.

Tuanze kuzoea,kuwa sio kila abiria ni "mgeni rasmi" wa nchi,wengine wanakuwa wapita njia.Waziri Mkuu wa Ethiopia angekuwa anashinda Airport kama kila kiongozi anayepita Bole Int'nal Airport atamsubiri kumpokea.

Mkuu wa Mkoa wa Dsm angekuwa anajipanga kila siku kupokea viongozi na mawaziri mkoani kwake,maana ofisi zote kubwa zipo kwake.Waziri wa Mambo ya ndani akiwa Simiyu ni "mgeni",ila kwenye viunga vya Dsm ni mpita njia tu.

Hence;haikuwa sehemu ya ratiba,ndio maana ni Balozi Mahiga badala ya Rais JPM

Fahamu Mambo Muhimu ya Kuzingatia Mara Baada ya Kumaliza Kufanya Mapenzi..!!!!

$
0
0

Namshukuru Mwenyezi Mungu kwa kunijaalia siha njema na pia kwa kunipa mwangaza wa kuandika hiki ninachokusudia.

Pia niwashukuru wapenzi wasomaji wa safu hii ambao tumekuwa tukiwasiliana na kushauriana hili na lile katika tasnia hii adhimu ya mapenzi. Nawakaribisha sana!

Labda kwa wale wasiofahamu niwaambie tu kwamba dhana ya mapenzi ni dhana yenye wigo mpana sana na ndiyo maana hutasikia hata siku moja tumepumzika kuizungumzia.

Hata hivyo, tunachofanya siku zote ni kukumbushana kwa yale tunayoyafahamu na kushauriana kwa pale tunapohisi wengi hufanya makosa.

Baada ya kusema hayo sasa nigeukie mada yangu ya leo ambayo kwa kiasi kikubwa inawahusu wale walio kwenye ndoa na kikubwa nazungumzia yale ambayo wawili waliotokea kupendana kwa dhati wanatakiwa kuyafanya mara baada ya kumaliza kufanya tendo la ndoa.

Nalazimika kuandika makala haya baada ya kubaini kuwa wengi wamekuwa wakifanya makosa na kujikuta wakishamaliza kufanya tendo hilo takatifu, kila mmoja anageukie kwake kisha kuuchapa usingizi.

Sisemi kwamba ni lazima kuyafanya haya nitakayoyaeleza leo ila 
yakifanywa huwa na manufaa yake na mara nyingi yanaboresha uhusiano.

Kuoga pamoja

Mtakuwa ni watu wa ajabu kama mtamaliza kufanya tendo hilo kisha kila mmoja kulala na majasho yake. Wapo


wasiojali katika hili na kuona kuoga au kutooga ni uamuzi wa mtu. Elewa linapokuja suala la usafi inashauriwa mkimaliza lazima muoge.

Wapo wanawake ambao wakishamaliza hukimbilia kuwaandalia maji wenza wao, wakishaoga ndipo nawo huenda kuoga. Hivi unaona ugumu gani kwenda kuoga na mwenza wako? Unaijua raha ya kuoga na huyo wako wa maisha?

Wanaofanya hivyo wanajua raha yake na wewe ambaye hujawahi, anza leo. Mmemaliza mambo yenu, chukuaneni kimahaba, elekeeni bafuni kisha ogeshaneni kimahaba.
Baada ya hapo rudini chumbani, mkishajifuta maji pandeni kitandani mkiwa wapesi.

Kusifiana

Hakuna muda maalum uliotengwa kwa ajili ya wanandoa kusifiana. Hilo linaweza kufanyika wakati wowote lakini pale mnapomaliza kufanya tendo la ndoa ni lazima utakuwa na jambo zuri la kumuambia mwenza wako.
Msifie kwa utundu na ubunifu wake. Msifie pia kwa mapenzi matamu anayokupa na ikibidi mpe sifa ya uzuri wake kiasi cha kukufanya kila unapokuwa karibu yake ujisikie amani ya kupitiliza.
Wapo ambao hawana kabisa kasumba ya kuwasifia wala kuwashukuru wenza wao kwa mazuri wanayofanyiwa. Yaani wao wanachukulia kila kitu poa tu bila kujali kwamba kusifiana kunanogesha mambo.

Kuelekezana

Kwenye kale kamchezo, wapo ambao wanakosea, kuelekezana na kukosoana kwa wapenzi ni jambo la kawaida. Yawezekana mwenza wako alifanya kitu ambacho hakikukufurahisha wakati mkiendelea na burudani yenu, mnapomaliza mwambie lakini kwa lugha ya kimahaba na ya upole. Naamini kwa kufanya hivyo atakuelewa na kubadilika.

Zungumzieni maisha

Huu ni wakati muafaka wa kujadili changamoto na malengo katika maisha yenu. Hapa akili zinakuwa zimetulia na kila mmoja anakuwa na mawazo chanya kwa mwenza wake. Jadilini mambo yenu, wekeni mikakati ya kuliboresha penzi na maisha yenu kwa ujumla.

Hayo ni baadhi ya mambo ambayo mnashauriwa kuyafanya pale mnapomaliza kufanya tendo la ndoa.

Yapo mnayotakiwa kuyaepuka ili kutotibua furaha iliyopatikana. Hayo nitakuja kuyaeleza katika makala zinazokuja kupitia ukurasa huu.

Kimenuka...Bashe, Musukuma, Malima mbaroni Kisa Vurugu Vikao vya CCM

$
0
0


Dodoma. Wabunge wawili na aliyekuwa naibu waziri wa fedha, Adam Malima wanahojiwa na polisi mjini hapa kwa kosa la kutaka kufanya vurugu na uchochezi katika vikao vya CCM.

Kamanda wa Polisi Mkoa wa Dodoma, Lazaro Mambosasa amethibisha na kuwataja waliokamatwa kuwa ni Mbunge wa Nzega Mjini, Hussein Bashe na Mbunge wa Geita vijijini ambaye pia ni Mwenyekiti wa CCM Mkoa wa Geita, Joseph Kasheku maarufu kama Musukuma na Malima.

“Hao ndio waliokamatwa na bado tunaendelea na mahojiano na wengine bado tunaendelea kuwatafuta,”amesema Mambosasa.

Amesema  taarifa zaidi atazitoa baada ya uchunguzi wa tukio hilo kukamili

Askofu Achekelea Sadaka Kuongezeka Kanisani..!!!

$
0
0

Askofu wa Kanisa la Kiinjili la Kilutheli (KKKT), Dayosisi ya Pare, Charles Mjema amewapongeza waumini wa usharika huo kwa kuongeza mapato yanayotokana na sadaka.

Askofu Mjema amesema hayo akiwa ni mgeni rasmi wa mkutano mkuu wa 20 wa Dayosisi ya Kaskazini uliofanyika kwenye dayosisi hiyo.

“Nimeona kwenye taarifa yenu hapa mwaka 1995 sadaka ilikuwa Sh9.4 milioni, lakini mwaka jana matoleo yenu kwa ajili ya kazi ya Bwana yamefikia Sh412.9 milioni. Hongereni,” amesema.

Askofu Mjema amesema wapo watu wanaoogopa kuweka malengo makubwa kwa kukosa ujasiri kutokana na kutokuwa na utamaduni wa kumtolea Mwenyezi Mungu.

Awali, Mchungaji Kiongozi wa Usharika wa Karanga wa mjini Moshi wa Dayosisi ya Kaskazini, Fred Njama amesema nchi imekumbwa na tatizo kubwa la ajira kwa vijana wanaomaliza elimu ya juu.

“Naishauri Serikali ione kwa jicho pana kwamba kwa kurundika vijana bila kujua mustakabali wao tunatengeneza bomu ambalo linasubiri kulipuka,” amesema.

Magufuli Awapa Makavu Live Walioimba Wanaimani na Lowassa Mbele ya Kikwete..!!!

$
0
0

Mwenyekiti wa Taifa CCM, Rais John Magufuli amewataka
makatibu wa mikoa wa chama hicho wanaotaka kuingia katika vikao vya
Halmashauri Kuu  (Nec) ya Taifa ya chama hicho wakagombee uenyekiti.

Akizungumza jana (Jumamosi) wakati wa ufunguzi wa kikao cha Nec, Rais Magufuli amesema
kuna watu wanaumuhimu wa kuingia katika vikao vya Halmashauri Kuu na
kwamba wakikosa kutakosekana uwakilishi .

“Nikawaambia mbona mwaka uliopita waliposimama wakimpinga mwenyekiti
makatibu mlikuwepo? Wakati mwenyekiti anawalipa mshahara mbona
hamkumtetea? Mbona hamkusimama kupigana na bado wakaendelea  kuimba
wanaimani na mtu fulani na wengine mkawa mnaitikia,”amesema.

Amesema kwa kuwa mabadiliko ya Katiba na Kanuni ambayo yatapunguza
idadi ya wajumbe wa vikao vya juu vya chama hicho walishayajadili
katika  kikao kilichofanyika Desemba 13 mwaka jana, ni matumaini yake
kuwa kikao hicho hakitachukua muda mrefu kuyajadili.

P-Funk: Diamond Anapaswa Kutulia Kidogo, lasivyo Watu Watamchoka

$
0
0
Producer mkongwe wa Bongo Records, P-Funk Majani, amesema kila siku akiendelea kusikia kuhusu Wasafi, itafika muda atawachoka.



Amedai kuwa ili label hiyo iendelee kufanya vizuri kwa muda mrefu, ni lazima ibadilishe sound, kuja na ladha au wasanii wapya. Amedai pia kuwa pamoja na ukubwa wa Diamond, kama asipotengeneza hali ya watu kummiss, watu watamchoka mapema.

Majani amesema hayo kwenye kipindi cha The Playlist cha Times FM kinachoendeshwa na Lil Ommy.

KUTANA na Mtabibu Ostadhi Khamisi Kutoka Mombasa Kenya Kwasasa Yupo Tanzania Kwa Ajili yako

$
0
0

Kutana na ostadhi khamisi kutoka mombasa Kenya kwa sasa yupo Tanzania ni mtabibu na mtafiti Wadawa za asili anatibia kama vile:
Miguu kuuma
Miguu kufagazi
Miguu kuwakamoto
Chango lauzazi kwakina mama
Dawa ya uzazi wakina mama inapatikana
Kusafisha nyota ili uwe namuonekano kwa kila mtu
Kumrudisha mpenzi wako na liekukimbia ndani yasiku 3 bila yapingamizi yoyote
Kumshika mume au mke asitoke nnje ya ndoa
Pata pete ya Bahati inayo endana na nyota yako
Kurudisha mali ilipotea au kudhurumiwa ndani yasiku 3
Pata utajili usiokuwa namashaliti yoyote
Dawa za nguvu za kiume
Dawa ya biashara inapatikana
Dawa ya kuzuia chuma ulete kwenye biashara inapatikana
 Zindiko la nyumba au shamba
 Anatuliza familia zinazogombana DUWA pamoja navisomo vya ufunguzi wa mwili wako njoo ufunguliwe vifungo ulivyo fungwa kutana na ostadhi khamisi utimiziwe ahadi ulizo hadiwa acha kuteseka acha kuhangaika ostadh khamisi yupupo tanzania kwajili yako...

Call +255718746825 +255754765246 kwa what'sapp +255783708487
Viewing all 104709 articles
Browse latest View live




Latest Images