Quantcast
Channel: UDAKU SPECIAL
Viewing all 104429 articles
Browse latest View live

Vita ya Makonda na Gwajima Yafika Lavel Hii..!!!!

0
0

Askofu wa Kanisa la Ufufuo na Uzima, Josephat Gwajima ametaja makosa ya kisheria yaliyomfanya Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam,Paul Makonda kukimbilia Afrika Kusini.

Akizungumza jana kanisani kwake, Ubungo, jijini hapa, Gwajima alidai  kosa la kwanza la Makonda ni kughushi cheti ambacho kinaonyesha yeye ni Paul Makonda wakati akifahamu kuwa yeye ni Daudi Bashite.

“Kosa hilo kwa mujibu wa Gwajima ni kifungo cha miaka saba.Kosa jingine ni kula kiapo cha ukuu wa wilaya na ukuu wa mkoa akisema yeye ni Makonda wakati akijua yeye ni Bashite,” alisema

Gwajima alisema  kosa la hilo la kula kiapo na cheti feki  ni kifungo cha miaka mitatu.

Kosa jingine  alisema ni kupokea mshahara na posho kwa jina la Makonda wakati akifahamu si yeye   na kuongeza kuwa kosa hilo likithibitika atatakiwa kurudisha mishahara na posho zote alizochukua.

Jeshi la Polisi Dar Wakusanya Milioni 840 za Faini Ndani ya Wiki Moja Tu...!!!!

0
0

Jeshi la polisi kanda maalum ya Dar es salaam limefanikiwa kukusanya jumla ya shilingi milioni 840 za faini ya makosa mbalimbali ya barabarani kwa kipindi cha wiki moja ya oparesheni iliyofanywa na jeshi hilo.

Akiongea na waandishi wa habari Ijumaa hii, Kamishna wa Kanda Maalumu ya Dar es Salaam, Simon Sirro amesema kiwango cha mapato hayo ni kidogo na inaashiria kupungua kwa makosa yanayofanywa na madereva.

“Kwa upande wa barabarani tunakwenda vizuri kati ya tarehe 1 mwezi 3 mwaka 2017 mpaka tarehe 9 mwezi wa 3 mwaka 2017 takribani siku hizo 8 tumeweza kukusanya jumla ya shilingi milioni 840 kwahiyo niseme tu kwamba mapato yanapungua hii tu ni kwasababu watu wameanza kutii tu sheria ya usalama barabarani,” Alisema Kamanda Sirro.

Siri Vigogo Kutimuliwa CCM Yavuja...!!!!

0
0

WAKATI Chama Cha Mapinduzi (CCM) kimechukua maamuzi magumu katika historia ya chama hicho tangu kizaliwe kwa kuwafukuza viongozi wa juu wengi kwa wakati mmoja baada ya kubainika kukiuka misingi ya Katiba ya chama hicho, gazeti hili limebaini sababu zaidi za kufukuzwa kwa viongozi hao.

CCM juzi ilitangaza uamuzi mzito wa kuwafukuza uanachama, kuwavua uongozi na kuwapa onyo kali vigogo 22 ambao wamechangia kukihujumu na kukifanya chama hicho kinuke mbele ya jamii.

Kupitia Halmashauri Kuu ya Taifa (NEC), CCM imeamua kuchukua hatua hiyo ya kuadhibu viongozi wake baada ya kupokea ripoti kutoka kwa Kamati Kuu (CC) iliyokutana jana asubuhi ambayo nayo ilipokea ripoti kutoka kwenye Kamati Ndogo ya Maadili naNidhamu ya chama iliyoketi mjini hapa juzi.

Katibu wa NEC, Itikadi na Uenezi wa CCM, Hamprey Polepope ndiye aliyeutangazia umma uamuzi huo na kusema adhabu hizo zimeanza jana. Muda mfupi baada ya kutangazwa kwa uamuzi huo, chanzo cha kuaminika kutoka Dodoma (jina kapuni) kililidokeza gazeti hili kuwa hatua hiyo imetokana na usaliti mkubwa uliofanywa na viongozi hao wakati wa uchaguzi mkuu wa Oktoba 2015.

Chanzo hicho kilisema kutokana na usaliti huo, CCM ilijikuta ikipata wakati mgumu wa kukubalika katika baadhi ya maeneo kutokana na kuonekana kinanuka na kutokubalika kwa wananchi wa maeneo hayo.

Hatua hiyo mbali ya kumpunguzia kura aliyekuwa mgombea urais wake Rais John Magufuli, pia ilikifanya chama hicho kupoteza nafasi nyingine mbalimbali ikiwemo ubunge na udiwani.

Usahihi wa taarifa hizo ulithibitishwa wakati wa mkutano wa Polepole na waandishi wa habari ambapo Katibu huyo wa NEC, Itikadi na Uenezi wa CCM alisema; “Ukiona mwanachama amefukuzwa ndani ya chama maana yake amefanya kosa kubwa.

“Mtu huyo atakuwa amefanya kitendo cha usaliti kilichosababisha chama kunuka au chama kushindwa na wanaCCM kumuona si mwenzetu na hakubaliki tena.” Waliofukuzwa uanachama Polepole aliwataja wenyeviti wa mikoa waliofukuzwa uanachama kuwa ni Mwenyekiti wa CCM wa Mkoa wa Iringa Jesca Msambatavangu, Mwenyekiti wa Mkoa wa Dar es Salaam, Ramadhan Madabida, Mwenyekiti wa Mkoa wa Shinyanga, Erasto Kwilasa na Mwenyekiti wa Mkoa wa Mara, Christopher Sanya.

Alisema katika kundi hilo la waliofukuzwa pia wamo Wajumbe wa NEC (Mnec) wa Wilaya ya Babati Ally Khera Sumaye na Wilaya ya Arumeru Mathias Manga. Wengine ni wenyeviti wa wilaya, ambapo lungu hilo limetua kwa Mwenyekiti wa CCM wa Wilaya ya Arusha Wilfred Ole Soilel Molel, Mwenyekiti wa Wilaya ya Kinondoni, Salum Madenge, Mwenyekiti wa Wilaya ya Longido Makolo Laizer, Mwenyekiti wa Wilaya ya Babati Ally Msuya na Mwenyekiti wa Wilaya ya Gairo Omar Awadh.

Wengine waliokumbwa na adhabu hiyo kubwa na ya juu kabisa kwa CCM ni Mwenyekiti wa Jumuia ya Wanawake (UWT) Taifa na Mbunge wa Viti Maalum, Sophia Simba. Kutokana na tukio hilo Simba pia amepoteza sifa ya kuwa Mbunge wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kupitia jumuiya hiyo.

Hata hivyo siku chache zilizopita mwana CCM huyo alitangaza nia yake ya kutogombea tena nafasi hiyo katika uchaguzi wa chama hicho unaotarajiwa kuanza hivi karibuni na kumalizika ifikapo Desemba mwaka huu.

Hata hivyo katika historia CCM imewahi kuwafukuza uanachama viongozi wa juu zaidi katika uongozi kama ilivyowahi kufanywa mwaka 1988, pale ilipomfukuza Maalim Seif Shariff Hamad akiwa Waziri Mkuu Kiongozi wa Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar.Miaka 10 baadaye yaani mwaka 1998 ilimfukuza uanachama Hamad Rashid Mohammed.

Waliovuliwa nafasi za uongozi, kuonywa Adhabu hiyo ya NEC ya CCM haikushia hapo kwani chama hicho kilitangaza kuwavua nafasi za uongozi baadhi ya viongozi wake kwa makosa hayo ya kukiuka misingi ya Katiba ya chama hicho.

Wajumbe waliovuliwa uongozi ni Mnec kutoka Wilaya ya Tunduru Ajili Kalolo, Mnec wa Wilaya ya Singida Mjini Hassan Mazala na Mnec wa Wilaya ya Kibaha Mjini Valerian Burreta.

Aidha chama hicho kimetoa onyo kali kwa viongozi wengine ambapo waliokumbana na onyo hilo na ambao watakuwa kwenye uangalizi kwa muda wa miezi 30 ni pamoja na Mnec kutoka Wilaya ya Kilwa, Ali Mchumo.

Wengine ni Mwenyekiti wa UWT Mkoa wa Kigoma na Mbunge wa Viti Maalum, Josephine Gezabuke, Mwenyekiti wa Wilaya ya Muleba Muhaji Bushakonyo, Mwenyekiti wa CCM wa Wilaya ya Iringa Mjini Abeid Kiponza na wa Wilaya ya Singida Mjini Hamisi Nguli.

Aidha katika kuonesha kuwa haikufanya mzaha katika kufikia uamuzi huo, CCM pia imetoa adhabu kwa Mjumbe wa Kamati Kuu, Balozi Emmanuel Nchimbi ambaye amepewa onyo kali na kutakiwa kuomba radhi mara moja, huku mjumbe mwingine wa Kamati Kuu ambaye pia ni Mwenyekiti wa CCM Mkoa wa Dodoma na Mbunge wa Bunge la Afrika Mashariki (EALA) Adam Kimbisa akisamehewa.

Nini hatma yao Polepole akizungumzia hatma ya waliopewa adhabu hiyo alisema pamoja na kwamba wamezuiwa kukata rufaa kupinga uamuzi huo wa NEC, lakini bado wanayo fursa ya kuwa wanaCCM au kuwa tena viongozi baada ya kujirekebisha kwa kipindi fulani, kwa mujibu wa Katiba ya chama hicho.

Alisema kwa waliovuliwa madaraka au kupewa onyo watakuwa katika kipindi cha uangalizi kisichopungua muda wa miezi 30 ili kuona kama wataweza kujirekebisha huku akisema kwa waliofukuzwa wanaruhusiwa kuomba tena uanachama wa CCM baada ya kupita miaka minne au miezi 48.

“Kwa hali hiyo hawa walioonywa au kuvuliwa madaraka wanakosa haki ya kushiriki katika uchaguzi wa ndani ya chama utakaofanyika kuanzia mwishoni mwa Machi hadi mwanzoni mwa Desemba mwaka huu na uchaguzi mwingine katika kipindi cha adhabu,” alisema Polepole.

Zanzibar yaundiwa Kamati Akizungumzia hali ilivyo kwa upande wa Zanzibar, Polepole alisema Makamu Mwenyekiti wa CCM Bara, Philip Mangula ataongoza kamati kwenda Zanzabar kuchunguza mwenendo wa chama, uchaguzi na maadili ya wanachama.

Alisema kamati hiyo itakuwa na wajumbe Pandu Amri Kificho, Shamsi Vuai Nahodha, Maua Daftari, Daud Issa, Suleiman Saharani, Steven Wasira, Hadija na Zakhia Meghji. Alisema kamati hiyo itafanya kazi ya kuchunguza hali ya kisiasa, uchaguzi ulivyofanyika Zanzibar na maadili ya wanachama katika kisiwa hiyo, na kwamba taarifa yake itatolewa baadaye.

Ushiriki Mkutano Mkuu Polepole alisema viongozi ambao chama kimewafukuza uanachama, hawataruhusiwa kuingia kwenye mkutano mkuu wa leo, isipokuwa chama kitawapa malazi, chakula na eneo la kulala na kutakiwa kurudi makwao.

“Kwa vile CCM ni chama kinachotambua utu na kuzingatia haki, wajumbe hawa watapatiwa sehemu ya kulala, chakula na haki zao nyingine na kesho (leo) watatakiwa kurudi makwao. “

Tayari viongozi hao ambao walikuwa wakimiliki mali za chama, wahusika wameshawatembelea na kuwajulisha kwamba wanatakiwa kuziacha na kuondoka,” alisema. Polepole alisisitiza kuwa CCM imechukua uamuzi huo wa kihistoria wa kuwaadhibu viongozi wake, kama sehemu ya mkakati wake wa kufanya mabadiliko na kuwa chama cha wanachama zaidi.

Magufuli asisitiza mabadiliko Awali akifungua mkutano wa NEC, Mwenyekiti wa CCM Taifa, Rais Magufuli aliwataka wajumbe wa NEC kukubali mabadiliko yanayofanywa na chama hicho yakiwamo ya kupunguza wajumbe wake 200 kati ya 358 na kubaki wajumbe 158.

Rais Magufuli alisisitiza kwamba wanachama wanatakiwa kukubali mageuzi yanayofanyika ndani ya chama hicho ili kukiletea chama hicho mageuzi ya kweli. “Katika mageuzi haya kuna viongozi na wajumbe wa mkutano watapunguzwa wakiwamo makatibu wa CCM katika ngazi mbalimbali zikiwamo za wilaya na mikoa ambao si lazima wawe wajumbe wa mkutano wa NEC.

“Watu wanasema lazima Makatibu wa CCM Mkoa wawe wajumbe wa mkutano wa NEC, mimi nasema si lazima kama wanataka kuwa wajumbe waende wakagombee uenyekiti,” alisema.

Huku akishangiliwa na baadhi ya wajumbe, Magufuli alisema, kama suala la uwakilishi wa makatibu si lazima, kutokana na ukweli kwamba mwaka jana, wakati Mwenyekiti mstaafu, Jakaya Kikwete akiingia ukumbini waliimba kwamba wana imani na mtu mwingine badala ya Mwenyekiti anayewalipa mshahara.

Mwenyekiti akauliza, kwanini makatibu ambao ni waajiriwa hawakusimama na kupigana au kupinga kitendo cha kuimba kwamba watu wana imani na mtu mwingine wala si Mwenyekiti wao wakati ndiye anayewalipa mshahara.

Magufuli alisisitiza kwamba kama makatibu wanataka kuwa wajumbe, wasuburi wakagombee katika nafasi mbalimbali zikiwamo za uenyekiti, lakini kwa sasa si lazima kuwa wajumbe.

Magufuli: Hatuna Muda wa Kumbembeleza Mtu Kukichangia Chama Chetu...!!!!

0
0

Mwenyekiti wa CCM, Rais Dk John Magufuli amesema chama hicho hakitambembeleza mtu kukichangia katika shughuli mbalimbali.

Akihutubia mkutano Mkuu wa CCM unaofanyika leo Dodoma, Dk Magufuli amewaambia wajumbe wa mkutano huo kuwa kwa miaka yote CCM kimekuwa kikiomba hata kwa watu ambao hawastahili.

“Matokeo yake wamekuwa wakitumia nafasi hiyo kudhalilisha. Hakuna tena omba omba hatutaki kumbembeleza mtu akitaka kutuchangia atuchangie,”amesema.

Amesema kuwa chama hicho kina utajiri unaokiwezesha kujitegemea na kwamba mwanachama atakayetumia mali za chama kwa maslahi binafsi atachukuliwa hatua kali.

Vanessa Mdee Apata Baraka za Mchungaji Gwajima

0
0

#FreeVanessaMdee haijaishia kutrend kwenye midomo ya mashabiki na wasanii pamoja na kwenye mitandao ya kijamii peke yake, weekend hii.


Vee Money ameonekana kuwa special katika mastaa wote waliohusishwa na skendo ya madawa ya kulevya baada ya umma kuonesha kumtetea kwa nguvu zote. Muimbaji huyo pia amepata baraka toka kwa Mchungaji Gwajima ambaye tangu naye ahusishwe na biashara hiyo amekuwa akifurumisha series za mabomu dhidi ya mkuu wa mkoa wa Dar es Salaam, Paul Makonda.

Akizungumza mbele ya waumini wa kanisa lake, Gwajima alisema:

Sasa hapo ndio najiuliza, polisi na uhamiaji waseme kwanini wanasuasua na kuna makosa niliyoyataja angalau saba ya jinai wakati wengine wamelala ndani kwa kuhisiwa tu wakiwemo wanamuziki kwa mfano Vanessa Mdee, amelala ndani tu alikuwa nje wakati sisi ametajwa naye ametajwa amerudi ndani leo siku ya tatu Vanessa Mdee leo yuko ndani kwa kuhisiwa tu, lakini huyu mpaka tumetaja Daudi Bashite yupo katorokaje? Huyu kakimbiaje? Vanessa Mdee simfahamu wala simjui lakini alikuwa ana performing zake nje ya nchi kashikwa pale yuko ndani leo, huyu katorokaje? Kwanini wengine wako ndani na wengine wanazunguka mitaa ya South Africa wakati walitakiwa wawe hapa na wao, mbona mimi nilienda kulala tu?

Tangaza Biashara yako Kwenye Blog yetu kwa Bei Rahisi

0
0

Tangaza Biashara yako Hapa kwa bei rahisi...

Tunapokea matangazo madogo madogo kama vile uuzaji wa viwanja, nyumba, magari, Maduka na Biashara nyingine

Piga simu namba 0714604974 kwa maelezo zaidi

Samatta hakamatiki Ubelgiji, wiki moja atupia magoli 5

0
0

Mbwana Samatta hakamatiki. Mchezaji huyo amezidi kuendeleza kasi yake ya ufungaji katika klabu ya KRC Genk.

Jumapili hii nahodha huyo wa Taifa Stars amefanikiwa kufunga goli moja katika ushindi wa mabao 4-0 walioupata Genk wakiwa ugenini dhidi ya KVC Westerlo.

Samatta alifunga goli lake katika dakika ya saba ya mchezo huo huku magoli mengine yakifungwa na Thomas Buffel dakika ya 27, Omar Colley dakika ya 67 na Ruslan Manilovskydakika ya 90.

Mpaka sasa Samatta amefanikiwa kufunga magoli matano ndani ya wiki moja yakiwemo mawili aliyofunga Alhamisi iliyopita katika michuano ya kombe la Europa League.

Mafuriko Yasababisha Jiji la Dar Kusimama....

0
0

Mvua Kubwa iliyonyesha sehemu mbalimbali za Jiji la Dar es Salaam imepelekea maji kujaa na kusababisha adha ya usafiri.
Mwenge, Sinza na Mlimani City ni baadhi ya maeneo yaliyoathiriwa na mvua hii. Wafanyabiashara Mwenge wamepata hasara baada ya maji kuingia madukani na kuharibu bidhaa.

Barabara za Bagamoyo na Mwai Kibaki(Old Bagamoyo) zimejaa maji na kusababisha foleni na kuwakwamisha wasafiri kwa masaa kadhaa.

Vigogo wa CHADEMA Watimkia CCM. Yumo pia Msaidizi wa Mbowe..!!!

0
0

Wakati Mkutano Mkuu wa Chama cha Mapinduzi (CCM) ulipokuwa ukiendelea mkoani Dodoma, baadhi ya waliokuwa wanachama na viongozi wa ngazi za juu wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) pamoja na ACT-Wazalendo wamepokelewa rasmi na CCM baada ya kutangaza kujiunga na chama hicho.

Viongozi hao waliojiunga na CCM jana wamesema sababu kubwa iliyopelekea na kufikia uamuzi huo ni utendaji kazi wa Rais na Mwenyekiti wa CCM, Dkt John Pombe Magufuli.

Miongoni mwa wengi waliopokelewa jana ni pamoja na, Moses Machali Mbunge wa zamani wa Kasulu Mjini kwa tiketi ya NCCR- Mageuzi na baadae kuahimia ACT Wazalendo. Alitangaza kujiunga CCM Novemba mwaka jana ambapo leo amepokelewa rasmi. Dkt Yared Fubusa, Aliyekuwa Mjumbe wa Kamati Kuu ya CHADEMA Mkoa wa Kigoma na Mgombea Ubunge jimbo Kigoma Kaskazini (CHADEMA).

Mwingine ni aliyetangaza kujiunga na CCM na kupokelewa na Mkutano Mkuu leo ni, aliyekuwa Makamu Mwenyekiti wa CHADEMA Taifa, Said Arfi.

Wolper 'Amchamba' Harmorapa Hadi Huruma...!!!!

0
0

STAA wa fi lamu za Kibongo, Jacqueline Wolper ameeleza  kukerwa na mwanamuziki chipukizi, Athuman Omary ‘Harmorapa’ aliyesema amewahi kutoka naye kimapenzi jambo ambalo siyo kweli.

Akichonga na Mikito Nusunusu Wolper alisema mwanamuziki huyo ambaye ameimba kwenye wimbo wake wa Kiboko ya Mabishoo kuwa ameshatoka naye kimapenzi amemkosea heshima  na hata alivyousikia wimbo huo umemshangaza kwa sababu hata Harmorapa mwenyewe anamuona kwenye mitandao ya kijamii na magazetini tu hajawahi kumuona ‘live’.

“Jamani huku ni kukoseana heshima maana huyo Harmorapa hata simfahamu huwa namuona kwenye mitandao na magazetini tu, sasa alivyoimba ametoka na mimi kimapenzi naona kama ni kituko kikubwa sana,” alisema Wolper.

Hivi Ndivyo Samatta Anavyozidi Kuingia Katika Mioyo ya Wazungu Taratibu....!!!

0
0

Baada ya kufunga magoli mawili katika michuano ya Europa League dhidi ya ndugu zao KAA Gent Mshambuliaji na Nahodha wa Tanzania Mbwana Samatta huku KRC Genk wakishinda jumla ya magoli 5-2 na kuandikwa na vyombo mbalimbali barani Ulaya hatimaye jana ameifungia timu yake bao katika ushindi wa magoli 4-0 dhidi ya KVC Westerlo kwenye dimba la Het Kuipje.

Ilichukua dakika ya 7 Mbwana Samatta akifunga goli la uongozi katika timu yake na mnamo dakika ya 27,Thomas Buffel hadi mapumziko wageni walikuwa mbele kwa 2-0.

Kipindi cha pili kilianza kwa timu zote mbili kufanya mabadiliko hata hivyo wageni waliweza kunufaika kwani kunako dakika ya Omar Colley alifunga dakika ya 62 na dakika ya 90,Malinovsky akipingilia msumari wa nne ukiwa mchezo wa kufunga Ligi kuu ya Ubelgiji huku Genk wakifikisha jumla ya pointi 48 kwenye nafasi ya nne ya Msimamo.

Hadi mwamuzi akipuliza kipyenga cha mwisho Genk wameibuka na ushindi wa jumla ya magoli 4-0 huku Samatta akifikisha jumla ya magoli 10.

Wajue Wanaume wa Kiafrika na Hulka Zao Katika Maisha...!!!

0
0

1. Wanaume wakatili zaidi Afrika - Waangola, Warundi na Wanubi (Sudan). Ukiwakosea ni kipigo au kifo. Kwao hakuna msamiati uitwao "Msamaha".
2. Wanaume wanaojali zaidi familia zao Afrika - WaSenegal.

3. Wanaume wanaopigwa zaidi na wake zao - Wakenya (Kati ya wanaume 10 nchini Kenya 7 wanapokea kipigo kutoka kwa wake zao. Chama cha kutetea haki za wanaume hadi sasa kina wanachama laki 8).

4. Wanaume wanaosali zaidi Afrika - Wasomali (kati ya wanaume 10 wa kisomali, 8 huswali swala 5 kila siku. Hata katikati ya vita huwaachi kuswali).

5. Wanaume matapeli zaidi Afrika - Wanigeria (kati ya wanaume 10 wa Nigeria, 6 ni matapeli wa kutupwa. Hata kama ni Askofu ukijilengesha anakutapeli tu).

6. Wanaume wanaopenda dezo na kulelewa zaidi Afrika - Wakongo (hawa wakioa mwanamke mwenye pesa huhamia kwa mke. Wanaitwa "Mario").

7. Wanaume wasomi zaidi Afrika -Washelisheli (Sychelles). Kila wanaume 100, 40 wana degree. Tanzania kila wanaume 1000 watatu wana degree.

8. Wanaume washamba zaidi Afrika - WaEritrea (ukienda kanisani/msikitini na gari jipya wanaahirisha kusali washangae gari kwanza).

9. Wanaume wachawi na Washirikina zaidi Afrika - Wagambia (Rais wao Yahya Jammeh hutumia waganga na wapiga ramli kama sehemu ya walinzi wake).

10. Wanaume wenye mikwara mingi mdomoni lakini waoga kutake "action" - Watanzania.

Lema: Viongozi wa Dini Wakiendelea na Uoga Nitafungua Kanisa, Naliita Godbless Church..!!!!

0
0

Akihutubia mkutano wa hadhara jana tindigani Arusha.Mbunge wa Arusha mjini Godbless Lema amewatupia lawama viongozi wa dini kwa kuwa waoga hata pale wanapoona katiba na sheria za nchi zinakanyagwa wazi wazi.

Lema ameenda mbali na kusema kama viongozi hao hawatabadilika na kuendelea kuwa waoga na wanafiki atafungua kanisa lake na kuliita Godbless lema church!

Amesisitiza haiwezekani viongozi wa dini wanahubiri mbiguni kuna barabara ya dhahabu lakini wao wanakuwa waoga kwenda kuipita barabara hiyo.Asemema viogozi wa dini wamekuwa waoga na uoga ni dhambi mbaya zaidi.

Biashara ya Mahindi ya Kuchoma Yapigwa Marufuku...

0
0

Kutokana na upungufu wa chakula, Mkuu wa Wilaya ya Same, Rosemary Senyamile apiga marufuku biashara ya mahindi ya kuchoma ili kukabiliana na tatizo la njaa.

Je, unahisi kupigwa marufuku kwa biashara ya kuchoma mahindi kutasaidia kupunguza tatizo la njaa ?

Jakaya Azindua Kikwete Foundation. Wamo Sefue, Mkandara, Bakhressa na Waziri wa Malaysia..!!!

0
0

Rais mstaafu wa awamu ya nne, Dr Jakaya Kikwete anazindua taasisi yake muda huu. Miongoni mwa timu ya taasisi hiyo ni Prof Mahalu ambae ni daktari bingwa wa moyo, Mkandara na Ombeni Sefue huku Kikwete akiwa mwenyekiti wa taasisi. Bodi ya taasisi hiyo pia imejumuisha wajumbe wengi kutoka nje ya nchi.

Hii inakuwa taasisi ya tatu inayoanzishwa na kubebwa na majina ya marais wastaafu ikitanguliwa na taasisi za Mwl Nyerere(Mwl Nyerere Foundation) na Mkapa Foundation huku Mwinyi yeye akipita kimya kimya.

Kulingana na taasisi hiyo, itajihusisha na afya hasa ya mama na mtoto, kudhibiti Maleria na lishe bora. Pamoja na hayo taasisi hiyo itajihusisha na elimu hasa ya vijana, kukuza vipaji, ujasiriamali na mafunzo. Mratibu wa taasisi hiyo, Omary Issa ambaye aliteuliwa na JK wakati wa utawala wake kuongoza 'Matokeo makubwa sasa' amesema Kikwete ameamu kutoa utaalamu na maarifa yake kwa watanzania na waafrika kwa ujumla.

Wengine katika taasisi hiyo ni Jack Steve ambae ameshawahi kuwa balozi wa Marekani nchini Tanzania, Aboubakar Bakhresa ambae ni mfanyabiashara, Indriss Jala ambae ni waziri katika serikali ya Malaysia, Kisangugi ambae ni mmarekani mwenye asili ya Tanzania na mfanyibiashara.

Harmorapa Amchana Mose Iyobo Kwenye Interview ‘Nina Hela, Aje Nimwajiri Kama Dancer Wangu’..!!!

0
0

Baada ya kuachia track mpya iliyojaa utata utata hivi, Harmorapa ameweka kila kitu ‘clear’ kilichomfanya kuandika mistari ya kumdiss dancer wa Diamond, Mose Iyobo.

Kupitia kipindi cha Fleva Plus kinachoruka hewani kupitia Sunrise Radio, DJ Dix alimuuliza kuhusu chanzo cha kile kinachoendelea kati yake na dancer huyo kutoka WCB.

Harmorapa hakuona noma na alijibu maswali yote aliyoulizwa. Sauti yake iliskika ikisema kwamba Mose Iyobo aambiwe kwamba anahitaji dancer na angetaka awe ni yeye. Aliongeza kuwa anatumia dollars kwahiyo ana uwezo wa kumuajiri na kumlipa vizuri tu.

“Mwambie Mose Iyobo nahitaji dancer, yeah nahitaji dancer kwa sababu naweza mimi, nahitaji dancer so naweza kumlipa kwa sababu Harmorapa ana dollar na pia anatumia account ya dollar,” alisema.

Katika hatua nyingine, alipoulizwa ni kwa nini aliamua kumdiss jamaa kwenye ngoma yake aliyomshirikisha Juma Nature ‘Kiboko Ya Mabishoo’, alisema…”Yani hata mfano naianza ile ngoma nilivyoiandika na nini, mwanzo haikuwa vile ila baada ya kuja kunianza mimi ndo pale nikapata feelings sana nikajikuta naandika vitu ambavyo vinamdiss pia na yeye ili nimjibu.”

Harmorapa anahisi Mose Iyobo alichokoza nyuki pale alipomfananisha na nyani kwa hiyo kung’atwa ni kitu cha lazima. Katika hatua nyingine, rapper huyo alipinga kinachoonekana kama ana nguvu nyingi kwa upande wa ‘publicity stunt’ kuliko muziki wake.

Hali kadhalika, amewataka mashabiki zake wawe tayari kupokea kazi zake kwa kuwa amejipanga vizuri kimuziki mwaka huu.

Ohooo..Ishakuwa Noma..Wema Sepetu Ajadiliwa Msikitini....!!!

0
0

Makubwa! Wema Isaac Sepetu amezua gumzo baada ya kujadiliwa kwenye msikiti mmoja uliopo Mwenge jijini Dar kufuatia mhadhiri mmoja maarufu aliyefahamika kwa jina moja la Mwaipopo kuelezea namna mwanadada huyo alivyotoa mchango wake kumsaidia marehemu Juma Kilowoko ‘Sajuki’ alipokuwa mgonjwa.

Akizungumza kwenye msikiti huo akiwataka Waislam wamchangie fedha kwa ajili ya matibabu ya maradhi yanayomsumbua, mhadhiri huyo alisema kuwa anawashangaa Waislam kutokuwa na mioyo ya kuwasaidia wenzao wanapokuwa na matatizo wakati dini haitaki hivyo.

“Nimezunguka sana kwenye misikiti mingi lakini msaada ambao nimekuwa nikipata kutoka kwa Waislam wenzagu haukuwa wa kuridhisha, inasikitisha sana.

Kuna wakati yule msanii wa filamu, Sajuki alipokuwa anaumwa, akina Wema walimchangia mapesa na akaenda kutibiwa lakini sisi tumekuwa wagumu katika kutoa,” alisema mhadhiri huyo.

Baada ya kusema, hivyo baadhi ya watu waliokuwa msikitini hapo walianza kunong’ona chinichini wakimjadili Wema huku wengi wakisema kuwa inakuwaje staa huyo awe na moyo wa kutoa kushinda waumini wa Kiislam wengine ambao wamejaliwa utajiri. “Wewe fikiria kama Wema ameweza kutoa pesa zake nyingi tu kusaidia katika matibabu ya Sajuki kipindi kile, Waislam kwa nini tunakuwa wagumu,” alihoji kijana mmoja aliyekuwa msikitini hapo.

Hata hivyo, hoja ya mhadhiri huyo ambaye historia yake inaonesha alikuwa Mkristo ni kwamba, Waislam wanatakiwa kusaidiana katika shida na raha pamoja na kwamba alikosolewa kuwa aliyemsaidia Sajuki fedha nyingi kipindi kile hakuwa Wema bali alikuwa ni Jacqueline Wolper.

Rose Muhando Asakwa Apelekwe Soba,Adaiwa Kawa Mtumiaji Mkubwa wa Madawa ya Kulevya...!!!!

0
0

Taarifa mbaya ya kusikitisha kutoka kwa staa wa nyimbo za Injili, Rose Muhando zinadai kuwa, mwimbaji huyo anasakwa na uongozi wa Sober House ya Pederef ili waweze kumwokoa kwenye matumizi ya madawa ya kulevya ‘unga’.

Chanzo kilicho karibu na mwanamama huyo ambaye amejijengea jina kubwa kupitia nyimbo zake nzuri kama Nibebe, kimeeleza kuwa Rose ametoweka nyumbani kwake mjini Dodoma baada ya kutopea kwenye matumizi ambapo kuna kiongozi mmoja wa dini ameamua kumsaidia.

“Kuna kiongozi mmoja wa dini hapa Dodoma, ameamua kujitolea kumsaidia Rose baada ya kusikia hali yake ni mbaya. Ameamua kuwatafuta Pederef ili wamsake popote alipo na wakimpata wampeleke soba moja kwa moja na gharama zote yeye atazishughulikia,” kilisema chanzo hicho.

Baada ya kupata habari hizo, mwanahabari wetu alimvutia waya Rose ili kuzungumzia madai hayo ambapo alipopatikana alioomba aachwe kwani alikuwa kanisani, angempigia mwandishi baadaye.

“Nitakupigia baadaye, nipo kanisani…,” alisikika Rose na kukata simu. Hata alipopigiwa tena baadaye, simu yake haikupokelewa.

Hata hivyo, Wikienda ilimtafuta mmliki wa Sober ya Pederef, Nuru Saleh aliyekiri kupewa kazi ya kumtafuta Rose na kumfikisha katika soba yao iliyopo Dodoma na kuanza kumpatia tiba ya kuacha matumizi ya madawa ya kulevya.

“Ni kweli. Sisi ndiyo kazi yetu. Nimepewa hiyo kazi na kiongozi wa dini, naomba nisimtaje lakini tumeshaanza kumtafuta na tukimpata tu, tutampeleka kwenye soba yetu ya Dodoma,” alisema Nuru.

Mara kadhaa Rose amewahi kuripotiwa kuwa anabwia unga lakini mwenyewe amekuwa akikanusha.

Mbeya Kinara Matukio ya Kishirikina..!!!

0
0

MKOA wa Mbeya umetajwa kushika nafasi ya tatu kitaifa, kwa kuwa na makosa mengi ya jinai na mengi ya makosa hayo, yakitokana na imani za kishirikina.

Mkemia Mkuu wa Serikali, Profesa Samwel Manyele,alibainisha hayo kwenye mkutano wa Wadau wa Maabara Kanda ya Nyanda za Juu Kusini, uliokuwa maalumu kwaajili ya uzinduzi wa kusimikwa kwa mtambo mpya wa Energy Dispersive X Ray Fluorescence(EDXRF), ambao ni maalumu kwaajili ya kufanyia uchunguzi wa kimaabara.

Prof Manyele alisema mkoa wa Mbeya, unashika nafasi ya tatu kitaifa kwa makosa ya jinai, ukiongozwa na mikoa ya Mwanza na Dar es Salaam. Lakini, kwa Mbeya hali ni tofauti, kwakuwa matukio mengi yanatokana na imani za kishirikina.

“Hapa kuna ubakaji hasa wa watoto unaohusishwa imani za kishirikina, masuala ya mauaji ya kuzika watu wakiwa hai kwa kuwatuhumu kuwa wachawi, lakini hata biashara nyingi zinazofanyika kwenye mkoa huu zinatajwa kuhusishwa sana na imani potofu za ushirikina sasa ili kupunguza kiwango cha makosa ya jinai ni lazima jamii yenyewe ibadilike” alisema.

Akizungumzia mashine ya ED-XRF, Prof Manyele alisema kusimikwa kwa mtambo huo, kutarahisisha upatikanaji wa majibu ya haraka juu ya uchunguzi mbalimbali wa kimaabara, ambapo mtambo huo una uwezo wa haraka wa kuchunguza na kutoa majibu.

Alisema mashine hiyo itatoa fursa kubwa kwa wanajamii, kwa kuwa muundo wake hautaishia kupimia vinasaba (DNA) tu, bali hata sambuli za madini ardhini, kemikali zilizopo kwenye vyakula, ardhini na kwenye maji hususani ya visima virefu na vifupi.

Aliwataka wakazi wa mikoa ya Nyanda za Juu Kusini, kuitumia mashine hiyo itakayotoa huduma kwa gharama nafuu, tofauti na zile zilizokuwa zikigharamiwa kwa sampuli kukusanywa na kusafirishwa hadi Dar es salaam.

Akimwakilisha mkuu wa mkoa wa Mbeya kwenye mkutano huo, Mkuu wa Wilaya ya Mbeya, William Ntinika, alisema mtambo huo umekuja wakati muafaka, ambao Rais John Magufuli amepiga marufuku usafirishaji wa mchanga wenye madini kwenda nje ya nchi.

 Aliwataka wachimbaji wadogo na wakubwa kuitumia fursa hiyo katika shughuli zao kwakuwa sasa wataweza kujua sehemu iliyo na kiasi kikubwa cha madini kwa sampuli za udongo za maeneo husika kupimwa na si kuchimba kiholela kama inavyofanyika hivi sasa.

Akizungumzia masuala ya Makosa ya jinai yatokanayo na imani za kishirikina,mkuu huyo wa wilaya alikiri kuwa licha ya uwepo wa makanisa mengi katika mkoa wa mbeya hata ukalinganishwa na Taifa la Naijeria hali ya uhalifu ni kubwa ikilinganishwa na mikoa mingine.

“Tulichopanga hivi sasa kama serikali,tumeamua tukutane na viongozi wote wa dini na wadau wengine ili tukae tuzungumzie suala hili.Ukiangalia mauaji kila siku,ubakaji kila kona sasa tumeona tukae na hawa wenzetu ili wanapokuwa kwenye nyumba zao za ibaada wawaambie waumini wao kuwa Mbeya hatuangaliwi vizuri” alisema Mkuu wa wilaya

Timua Timua CCM, Hongera M/Kiti Magufuli, Wapinzani Mjifunze Kutoka CCM...!!!!!

0
0

Mimi ni miongoni mwa watu ninaotatizwa sana na ukiukwaji wa haki unaofanyika popote ndani ya JMT na ni miongoni mwa watu wa mwanzo mwanzo kabisa kumuita rais wetu Dr.John Pombe Magufuli kuwa ni dikiteta.

Katika tumbua tumbua majipu ya rais Magufuli niliunga mkono dhana nzima ya utumbuaji na dhima ya utumbuaji ila sikuunga mkono utekelezaji wa utumbuaji huo kutokana na baadhi ya utumbuaji kufanywa kidikiteta kwa chuki, papara na double standards za hali ya juu kwa kukiuka sheria, taratibu na kanuni.

Lakini kwa hii timua timua ya kuwatimua vigogo wa CCM, nimefarijika sana kwa sababu kumbe huu utumbuaji wa kidikiteta sio kwa serikali tuu bali hata kwa CCM. Hii ni plus kwa Magufuli kuwa katika tumbua tumbua, anatumbua tuu bila kumuangalia mtu usoni kuwa nani ni nani, kama mtu kama Sofia Simba ameweza kutumbuliwa, then kiukweli Magufuli sio mchezo! .

Hakuna ubishi kuwa CCM ni chama kikongwe kinafanya mambo yake kiutu uzima. Kwenye katiba yake kinazo taratibu za nidhamu zilizofuatwa ndani kwa ndani, kimya kimya hadi kufikia hatua ya mwisho ya watu kupigwa chini ndipo umma unaambiwa na kupigwa na surprise. Huu ni ukomavu na ndiko kufanya maamuzi makubwa kiutu uzima. Pongezi ziende kwa Mwenyekiti Magufuli. Wapinzani mjifunze kutoka CCM.

Ugomvi wa Baba na Mama. 
Mara nyingi watoto huwa hawawezi kufahamua kuwa kumbe baba na mama huwa wanagombana mara mara ugomvi wa kimya kimya chumbani. Mara kwa mara wanawake huwa wanachukia na kuwanyima 'chakula' waume zao, hivyo kuna wanaume kibao hulala njaa na hawasemi. Kuna wanawake kibao hubakwa na waume zao na wengine hupokea hadi vipigo lakini hawasemi. Kuna mara kibao baba na mama wamenuniana ila akija mgeni warajikausha. 

Ugomvi ukiwa mkubwa hadi mama kufungasha ndipo hakuna namna lazima watoto watajua. Hiki ndicho kilichofanyika CCM. 

Watuhumiwa wote walijadiliwa toka vikao vya chini kimya kimya. Wakapewa barua za mashitaka yao, wakapewa muda wa kujibu tuhuma, wakaitwa kujieleza, wakahojiwa na kupewa muda wa haki ya kusikilizwa na kujitetea, kisha vikao vikafikia maamuzi kimya kimya na hatimaye ndipo vikao vya maamuzi vikatangaza maamuzi yale. Huu ni ukomavu wa hali ya juu na CCM kinastahili pongezi za dhati kwa hili. 

Siku Polepole akiongea na media, awahakikishie Watanzania kuwa taratibu zilifuatwa vinginevyo kama ule udikiteta wa kukanyaga katiba ya nchi pia umeikanyaga katiba ya CCM hivyo timua timua ile ni muendelezo wa udikiteta ule ule, CCM kitakuwa ni chama cha kidikiteta na kama kinaongozwa kidikiteta na kiongozi dikiteta, then jiulize taifa letu la Tanzania tunalipeleka wapi? .

Chedema utumieni uzoefu na ukongwe wa CCM katika kufanya maamuzi yake kwa kuzingatia katiba zenu, niliwahi kuwashauri hivi kuhusu udikiteta katika kuendesha mambo yenu ya ndani. 

Fanyeni mambo yenu kimya kimya, jifunzeni kwa CCM ili angalau 2020 Watanzania tuweze kuwafikiria tuwajaribishe vinginevyo tutaendelea kiongozwa na chama kikongwe kilichozeeka mpaka basi lakini kila kinapofanya face lift kama hii, kinarudia ujana hivyo hata hapo mlipo kama mnajidhania mmesimama, angalieni msianguke come 2020. 

Hongera sana CCM kwa mabadiliko. Hongera kwa ukomavu.

Jumatatu njema
Viewing all 104429 articles
Browse latest View live




Latest Images