Quantcast
Channel: UDAKU SPECIAL
Viewing all 104785 articles
Browse latest View live

Kilichojiri Kwenye Kesi ya Wema Sepetu Leo Mahakamani

$
0
0

Kesi ya dawa za kulevya inayomkabili malkia wa filamu, Wema Sepetu yaahirishwa hadi April 11 baada ya upande wa mashtaka kusema kortini Kisutu upelelezi haujakamilika.

Muigizaji huyo ni mmoja kati ya wasanii ambao walitajwa kwenye list ya mkuu wa mkoa wa Dar es salaam Paul Makonda yawatuhumiwa wanaojihusisha na biashara ya dawa za kulevya.

Katika upelelezi wa awali ambao ulifanywa na jeshi la polisi, walidai wamekuta msokoto wa bangi nyumbani kwa muigizaji huyo.

Amber Lulu Awafunda Wanaotafuta Umaarufu Mitandaoni

$
0
0

Mrembo anayepamba video za wasanii bongo ' Amber Lulu amewataka warembo wenzake kubadilisha mfumo wa maisha wa kutafuta umaarufu kupitia mitandao ya kijamii kwa kupiga picha zisizofaa na badala yake wafanye kazi za kusaidia jamii ili wakumbukwe.

Akipiga story kwenye  Planet Bongo Amber anasema amegundua kuwa kutumia sehemu za miili yao kutafuta umaarufu ni kitu kisicho na maana kwa kuwa umaarufu huo unakuja na kupita kitu ambacho mwisho wa siku watakuwa hawana kitu kipya cha kuonesha kwa mashabiki na kubaki kunyooshewa vidole kwa sababu ya picha hizo wanazotafutia kiki.

"Kutumia maungo kwa ajili ya kutafuta umaarufu siyo mpango kwa kuwa upepo huo utapita halafu tutakuwa hatuna cha kuonesha, bado watoto wa kike tuna mambo mengi ya kufanya kwenye jamii na tukaonekana kuliko kuonesha miili yetu ambapo mwisho wa siku tunadharaulika." Amesema Amber

Hii siyo mara ya kwanza video vixen huyo kufunguka suala la kuacha sehemu kubwa ya mwili wazi, Wiki iliyopita Ambar Lulu alisema umaarufu wa kuutafutia kwenye mitandao ya kijamii ni kama upepo kwani hutokea na kupita kwa kuwa warembo wapo wengi na kila mmoja anatafuta njia ya kutokea. 

Makonda Achezewa Sharubu!, Vijana Wamjaribu Mchana Kweupe...!!!!

$
0
0

UKAIDI! Wakati wakazi mbalimbali wa Jiji la Dar es Salaam na vitongoji vyake wakiendelea kutii bila shuruti agizo la kuacha kunywa pombe, kucheza pool na kamari nyakati za kazi, baadhi ya vijana wakaidi wameonekana kupuuza agizo hilo linalotafsiriwa kama kumchezea sharubu Mkuu wa Mkoa, Paul Makonda aliyetoa amri hiyo.

Uchunguzi mahususi uliofanywa na Kitengo Maalum cha Oparesheni Fichua Maovu (OFM) cha Global Publishers kimefichua kuendelea kwa michezo ya pool, uchezeshwaji wa kamari na unywaji pombe katika baadhi ya baa na maeneo maarufu, tena vitendo hivyo vikifanyika mchana kweupe.

Katika uchunguzi huo uliofanywa maeneo mbalimbali ya Dar es Salaam kama Sinza, Manzese, Temeke, Mbagala na Kariakoo, OFM walishuhudia majira ya kuanzia saa nne asubuhi, katika baa kadhaa, wahudumu wakiendelea na utoaji wa huduma za vilevi bila wasiwasi wowote. Sinza Mori katika baa moja maarufu, ilishuhudiwa baadhi ya watu katika bar hiyo wakiendelea kunywa bia kama kawaida kana kwamba bado wanaishi enzi zile za mwaka 1947.

Kule Manzese, katika baa moja kubwa yenye wateja wengi (majina yao yanahifadhiwa kwa sasa) baadhi ya wateja waliwekwa sehemu ambayo siyo rahisi kuonekana na mtu mgeni, huku wahudumu wakiwapelekea vilevi vyao. OFM ilikuta wanywaji wakipewa bia, pombe kali za kwenye chupa na virobo ambavyo vimepigwa marufuku. Temeke Mwembeyanga, katika baa maarufu eneo hilo, OFM pia walikuta agizo la Mheshimiwa Makonda likipuuzwa mchana wa jua kali, kwani watu waliendelea kupata kile roho inapenda bila hofu yoyote.

Licha ya unywaji wa pombe, pia katika eneo la Mbagala Rangi Tatu, OFM iliwaona baadhi ya vijana wakiendelea na mchezo wa pool bila hofu, licha ya kuwa jua lilikuwa likiwaka, kuashiria muda wa watu kuchapakazi.

Lakini katika hali ya kusikitisha, eneo la katikati ya Kariakoo, kwenye baa moja kubwa ya miaka mingi, pamoja na jua kali la mchana, uuzwaji na unywaji wa pombe ulikuwa ukifanyika pasipo kificho, huku vijana wa rika mbalimbali nao wakionekana wacheza pool, katika meza zaidi ya nne zilizomo ndani ukumbi wa baa hiyo.

Licha ya mitungi, pia baadhi ya wateja waliendelea kucheza kamari ya kwenye vibanda maarufu kama casino pasipo hofu licha ya kwamba baa hiyo ipo umbali wa mita chache tu kutoka kilipo Kituo cha Polisi cha Msimbazi, jijini Dar es Salaam. Licha ya Makonda kutoa amri ya kuachwa kwa vitendo hivyo wakati wa saa za kazi, pia viongozi wengine wa ngazi za ukuu wa wilaya, mikoa na mawaziri, wamewahi kutoa maagizo ya kutochezwa kwa pool, kunywa pombe na hata kwa wamiliki wa maeneo yanayoendesha shughuli hizo kufungwa nyakati za kazi.


Baada ya Kusaidiwa Kwenye Nyimbo Yake ya Kwanza,Harmorapa Aaanza Kumpiga Vijembe Juma Nature,Adai Hakumfanyia Poa Hata Kidogo...!!!

$
0
0

Msanii Harmorapa amewaomba wasanii wakubwa waliopo kwenye 'game' ya muziki kuacha tabia ya kuwapiga mkwanja mkubwa 'underground' wakati wanapoenda kuwaomba kufanya nao 'collabo'

Hayo yamekuja baada ya msanii huyo kuombwa pesa ya mavazi na Juma Nature kwaajili ya kufanyia ‘shooting video’ jambo ambalo kwa upande wake limemkwaza kwa namna moja ama nyingine.

“Haipo sawa kwa wasanii wakubwa kutudai sisi ‘underground’ pesa ya kufanyia collabo wakati wanajua bado hata hatuanza kufaidika na muziki wenyewe”. Alisema Harmorapa kwenye kipindi cha eNewz ya EATV

Aidha Harmorapa amesema muda mwingine wasanii wakubwa wanatumia njia ya kutaka pesa ndefu ili mradi wa kwamishe kufanya kazi nao.

Kwa upande mwingine mzee wa kiki za mjini amesema mashairi aliyoyatumia katika wimbo wake amefanya kumjibu ‘dansa’ Mose Iyobo kutoka WCB kwa kile alichokifanya awali cha kumfananisha na sokwe.

Rasmi..Diamond Aamua Kumchana Makonda Ukweli wa Moyo Wake..!!!

$
0
0

MSANII wa muziki wa Bongo Fleva,  Nasib Abdul ‘Daimond Platnumz’, amempongeza Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam,  Paul Makonda kwa jitihada zake kuhakikisha Dar es Salaam inakuwa salama.

“Kwanza kabisa Nimpongeze Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam, Makonda kwa jitihada zake. Ukizingatia ni mwaka mmoja tu tokea awe mkuu wa mkoa lakini utendaji wake umezaa matunda mengi na changamoto ni nyingi zinazo mkabili lakini bado amekuwa imara.”, alisema Diamond.

Diamond ameyasema hayo leo katika mkutano  kuhusu vita dhidi ya madawa ya kulevya uliofanyika katika Bwalo la Polisi Oster Bay jijini Dar es Salaam ambako Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam, na viongozi wengine wa serikali na taasisi mbalimbali walihudhuria.

Makonda: Mimi Sio Mwanasiasa, Sitafuti Sifa za Kijinga....!!!!

$
0
0

Mkuu wa mkoa wa Dar ametoa kauli hiyo jana Dar wakati alipowatembelea wahanga wa mafuriko mkoa wa daresalam na kuwataka wahame maramoja maeneo hayo swali ni kweli wanasiasa wanapokua kwny majukumu yao wanatafuta sifa za kijinga??

Picha: Lema Amsindikiza Wema Mahakamani Leo...!!!

$
0
0

Mmh huu ukaribu sasa umekua wa mwendo kasi kwa kweli, sio kwa mahaba hayo

Wewe unamtazamo gani kuhusu picha hii?


Ofisi za TFF Zapigwa Kufuli na TRA...Sababu Hizi Hapa

$
0
0

Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA) imezifungia ofisi za Shirikisho la Mpira wa Miguu Nchini (TFF) leo na kuamrisha kuacha kila kitu ndani, hali hiyo imefikiwa kufuatia deni kubwa la kodi wanalodaiwa TFF. Kampuni ya Yono Auction Mart kwa idhini waliyopewa na TRA walihusika katika kuzifunga ofisi hizo na kuwataka kutotoka na kitu chochote ndani.

Siri Imevuja ...Rais Magufuli Anachukiwa na Hawa na kwa Sababu Hizi...!!!!!

$
0
0

1. Anachukia rushwa ,watoa rushwa wanaotaka kupata madaraka kwa kutoa rushwa !! Watu wengi hawajiamini kiasi ya kwamba wanaona wasipotoa rushwa wanaamini hawawezi kuchaguliwa!! Hawa wakishagawa pesa wanakuwa wamenunua akili za watu!! Wanakuja na ka msemo kuwa tunapendwa sana!!wanajificha ndani ya kichaka cha demokrasia maamuzi ya wengi lazima yafuatwe!! Ukiwabana utasikia wanalia eti katiba ya chama imebakwa!!Hawa lazima wamchukie JPM

2. Wapiga dili: wako watu kwa miaka mingi walijificha ndani ya chama kwa lengo LA kuficha maovu yako mfano kukwepa kodi( wafanyabiashara) ,kufanya biashara haramu ,kujipatia kipato isivyohalali,nk!! Kwa sababu alikosekana msemakweli na MTU Wa kuwakemea ndiyo maana walijificha humo.watu hawa wanafikiri ni enzi za myaka ya 90 kwamba MTU akipendekezwa na CCM lazima atashinda, wanafikiri CCM itatawala milele vyovyote vile! Hawaamini katika kutenda meema ( siyo kutoa rushwa au kupokea rushwa) ili uchaguliwe kwa njia ya haki( kidemokrasia) ! Hawa wamekifitinisha chama kwa wananchi wakawaida!! Hawa lazima wamchulie rais JPM

3. Wapinzani japo siyo wengi ambao ni wachumia tumbo!! Hawa pesa kwanza uzalendo baadae,nchi baadae chama baadae,mwanachi baadae!! Wako tayari kusema uongo na kuutetea kwa sababu wanajua watanzania tunapenda kusikia siyo kufanya utafiti na kujiridhisha juu ya kilichosemwa na MTU huyu!! Hili ni tatizo kubwa katika nchi maskini kama Tanzania!! MTU akisema kitu tunaamini hivo hivo kama mazuzu!!
Wapinzani ambao wao ni kupinga kila JPMu wanakiri huo ndiyo upinzani Wa kweli!! Hawa lazima wampinge rais JPM

4. Watu ambao walitegemea kupitishwa na chama ili wachaguliwe!! Japo siyo wengi lakini nao wanaweza kumchukia rais! Huko nyuma watu waliacha kuamini chama wakaanza kumwamini MTU!! Hili nalo ni shida!! Sasa rais anaposema watu waamini chama kuliko MTU( na huu ndo msingi imara) lazima nao wamchukie rais!!

5. Kuna watu utafikiri waliajiriwa na watu ili kazi yao iwe kukosao kila kitu kifanywacho na rais!! Hawa wanamtumikia mgombea Fulani wa urais.Wanafanya hivyo kutaka kuwaminisha wananchi wasiyotumia akili kufikiri kuwa JPM hafai Mara ni mkurupukaji,anaonea watu,ana double standards katika kushugulikia waovu!! Hawa watu ni hatari kwa maendeleo na mstakabali Wa taifa letu!!

6. Kuna watu wanataka kuendekeza ukabila na udini ndani ya taifa letu!! Kipindi cha uchaguzi liko kabila La mbali ( silitaji) walifurahia mgombea fulani ( simtaji).Nikijiuliza maana yake nini jameni!! Ukabila ni hatari sana kwa Amani endelevu ya taifa!! Burundi hakuna amani kwa sababu ya ukabila nakadhali nchini Rwanda ,Kongo,sudani kusini hakuna Amani kwa sababu ya ukabila! MTU anayetaka kuendekeza ukabila ni wakuchukia kama ukoma!! Hafai kuwa kiongozi wetu!!

7. Watu ambao hawakapata ajira,watu ambao wanavyeti feki,watu waliyofukuzwa ajira, hawa lazima wamchukie JPM! Nafikiri ni muda mzuri kwa serikali yetu kupunguza maadui Wa rais wetu kwa kutoa ajira kwa vijana wetu waalimu ,madaktari,ma injinia nk!

Fahamu Matumizi Mbadala Usiyoyajua ya Unga wa Soda au Baking Soda Tofauti na Kuokea Keki au Kupikia ..!!!!

$
0
0

Najua wengi mnaifaham Baking soda au Bicarbonate of soda kwa lugha ya Kiswahili huitwa magadi soda ,kwa wale msioifahamu,Baking soda au bicarbonate of soda ni hitaji la kawaida kabisa jikoni,hutumika sana katika vyakula vya kuhoka kama keki na mikatepia hutumika katika maandazi,pan cakes,chapatti na vyakula vingine vingi.Hata ivyo Baking soda wakati mwingine hutumika kulainisha vyakula ambavyo ni vigumu kuiva au visivyolainika haraka vinapopikwa kama mahindi yasiokobolewa,mboga za majani za kienyeji kama mgagani, msusa,majani ya kunde yaliyo komaa na kadhalika.Hapa nchini Baking soda ya jina kubwa na kufaamika kwa wengi inaitwa SIMBA.

Baking soda hupatikana kwa wingi madukani na hata sokoni.kuna ile ambayo imepita kiwandani na kusindikwa kitaalam na kuna ile ya kienyeji ambayo iko kiasili zaidi.

Siri kubwa ambayo wengi hawajui kuhusu baking soda,Ni ambavyo huweza kutumika kufanya shughuli nyingi za usafi.Uwepo wa alkalini ndani ya baking soda huipa uwezo wa kuondoa uchafu wenye asili ya asidi.

1.Kusafisha kibao cha kukatia nyama au mboga.

Kwa wale mnaotumia kibao cha plastiki au mbao kukata nyama mnajua ambavyo kibao hushika uchafu na hata kubadilika rangi,hata baada ya kukiosha.Kutatua tatizo hilo na kufanya kibao chako kiwe safi na cheupe tena,Nyunyuzi baking soda ya kutosha kisha sugua na dodoki adi kibao kiwe safi,kama ni uchafu wa muda mrefu loanisha kibao na maji kisha nyunyuzi baking soda na uache kwa dakika 15 ndipo usugue na dodoki



2.Kuzibua sinki la jikoni.

Sinki la jikoni mara nyingi huziba na kugoma kupitisha maji machafu kwasababu ya mafuta na uchafu wa chakula.Mwaga kikombe kimoja cha baking soda kwenye tundu la sinki,kisha mwaga vikombe vitatu vya maji ya moto sana.Acha kwa angalao masaa manne kabla hujatumia sinki.Ni vyema ukafany ivyo usiku unapoenda kulala kwani sinki halitatumika adi asubuhi.



3.Kukata harufu ya mkojo chooni.

Kama unasafisha choo lakini bado kuna harufu mbaya ya mkojo.Chukua nusu kikombe cha baking soda changanya na nusu kikombe cha vinegar nyeupe kisha mwaga ndani ya choo na unyunyuze kwenye sakafu ,na baada ya nusu saa unaweza kudeki sakafu ili pabaki safi.

4.Kusafisha na kung’arisha sinki,bathtab na tiles.

Ingawa wengi hupenda kuweka tiles,masinki na Bathtubs kwenye nyumba zao,utakubaliana na mimi nikisema wengi hawajui namna ya kuzifanyia usafi,unakuta sinki au tiles nyeupe zimegeuka na kua za rangi ya njano kwa uchafu.

Chukua nusu kikombe cha baking soda changanya na nusu kikombe cha sabuni ya majichanganya vizuri ili kupata kama uji mzito.Kisha tumia kusugua sinki,tiles au bathtub.


5.Kusafisha Oven

Kawaida unapohoka vyakula kama nyama,samaki,mboga za majani na matunda kama nanasi,mchuzi au umajimaji kutoka kwenye vyakula hivi humwagika ndani ya oven.Wakati mwingine unapo rost vyakula ndani ya mafuta kwenye grill,mafuta huruka na kuchafua oven.Kwa kawaida uchafu wa aina hii Uganda haraka sana ndani ya oven.

Ili kusafisha .weka baking soda yakutosha kwenye sehem ya chini kabisa ya oven,kisha iloanishe na maji,usiweke maji mengi,kiasi tu cha kutosha kuloanisha baking soda.Fanya hivi usiku kabla ya kulala na ifikapo asubui uchafu wote ulioganda utakua umelainika,tumia dodoki kusafisha.

6.Kukata /Kuondoa harufu mbaya ndani ya friji.

Kutokana na uwekaji wa vyakula iana mbalimbali vyenye harufu tofauti tofauti mara nyingi friji huwa na harufu isioeleweka.Kwa sisi yunaoishi Tanzania na kukabiliwa na tatizo la umeme,umeme unapokatika kwa muda mrefu friji hutoa harufu.

Chukua boksi la baking soda,lifungue na kisha fungua mfuko wa plastiki uliobeba baking soda ili ukae wazi,kisha weka baking soda hiyo kwenye sehem ya chini ya friji yako,itanyonya harufu yote ndani ya friji na kuiacha ikiwa fresh.Ukiweka boksi lenye baking soda kidogo utendaji wake huwa wataratibu sana,hivyo ni vyema ukaweka boksi jipya.


7.Kukata harufu kwenye nguo mpya 

Mara nyingi unaponunua nguo mpya inakua na harufu ya upya na ndio maana watu wengi hufua nguo mpya kabla hawajavaa.Nguo za mtumba nazo hua na harufu kali inayolazimu kufua kabla hujavaa,hizi zote ni harufu za kemikali zilizotumika katika utengenezaji wa nguo,na kwa nguo za mitumba ni harufu ya madawa yenye kemikali zinazotumika kuhifadhi nguo.

Ili kuondoa harufu hizo,pima kikombe kimoja cha baking soda changanya kwenye maji lita tano ,kisha loweka nguo kwenye maji hayo kwa masaa matatu au zaidi,suuza na uanike.

Kwakua baking soda inaweza fanya yote haya,unakila sababu ya kua nayo jikoni kwako,hasa kwa ajili ya kusafishia kibao cha kukatia Nyama na mboga,pamoja na kuzibua sinki lako la jikoni.Ukweli ni kwamba,kibao cha kukatia nyama kikiwa kichafu,au kimebadilika rangi na mabaki ya nyama yamenata au kuganda kwenye kibao hicho,inatia kinyaa na pia ni hatari kwa afya ya familia yako.Sinki la jikoni nalo likiziba na kuacha kupitisha maji machafu ndio mwanzo wa kurundika viombo vichafu na kua na maji machafu kwenye beseni kila wakati,chanzo kikubwa cha inzi jikoni na magonjwa ya tumbo.

Kama kawaida,naboresha maisha ya familia yako,Kazi yangu ni kukuelimisha tu,utendaji ni juu yako.

Nilivyomdhania Magufuli Kumbe Sivyo...

$
0
0

Na. M. M. Mwanakijiji

Kwa baadhi yetu tuliokataa kuvingirisha mikono yetu kuunga mkono mabadiliko yaliyobinafsishwa kwa mtu mmoja tulijikuta hatuna budi kumuunga mkono Magufuli tukiamini anawakilisha mabadiliko ya kweli. Binafsi niliamini kabisa kuwa Taifa lilikuwa linamhitaji kiongozi kama Magufuli kuweza kulinasua mahali lilipo kuliko kiongozi yule mwingine toka upinzani. Niliamini kabisa kuwa Magufuli akishika madaraka atakuwa na kazi kubwa ya kulirejesha Taifa katika misingi yake ambayo inaonekana ilikuwa imepotea.

Hatua zake mbalimbali za mwanzo kushughulika na kubana matumizi, kupambana na ufisadi na kuondoa watendaji mizigo a.k.a majipu kulinifanya niamini kabisa kuwa Magufuli kazi aliyonayo akiendelea na kasi hiyo basi ndani ya miezi sita tu atakuwa ameleta heshima katika utumishi wa umma, kurejesha heshima kwa Watanzania na fahari ya taifa letu kurudishwa. Niliamini kabisa kuwa Magufuli atafanya kazi hii bila woga, huruma, husuda, wivu, au kusita sita. Kwamba, hatomwangalia yeyote, popote na kwa lolote. Ndani ya miezi sita hivi na kabla ya ujio wa bajeti ya kwanza ya serikali yake basi Magufuli atakuwa ameshaweka alama za namna gani taifa linataka kwenda na kila kiongozi atakuwa amepata ujumbe.

Nilifanya makosa.

Nilifanya makosa kwa sababu nilidhani hii ni kazi rahisi kwa Rais. Nilidhani ni kazi ya kutimua huyu, kuondoa yule na kumleta yule mwingine. Nilidhani ni kazi ambayo akimaliza teuzi mbalimbali basi atakuwa ameipanga serikali yake kwa ajili ya kuchapa kazi.

Sasa najua kuwa uamuzi wake wa kushughulika na watu kwanza kabla ya mfumo ni jambo muhimu sana. Ulikuwa ni uamuzi sahihi na unajitahi kutetewa. Watu ndio hutengeneza mfumo; ni watu ndio ambao hukaa chini na kufanya maamuzi mbalimbali yenye kuathiri (kwa uzuri au ubaya) uwepo na utendaji wa mfumo wa utawala. Ukiwa na watu wabovu, wabinafsi na wenye mwelekeo wa ufisadi basi mfumo utakuwa mbovu, wa kibinafsi na wenye uelekeo wa kifisadi kwa sababu moja kubwa; wale wenye kuiwamba ngoma ngozi huivutia kwao! Mfumo wetu wa utawala wa kifisadi ulitengenezwa na watawala wenye mwelekeo wa kifisadi. Matobo (siyo matundu) kwenye sheria zetu vilitengenezwa na watu ambao walijua wakiziba na wao watakuwa wamejizibia.

Magufuli asingeweza kutengeneza mfumo mwingine kwa kutumia watu wale wale walioutengeneza mfumo huu wa sasa na hasa kama watu hao ni wanufaika wa mfumo huu. Ingelikuwa ni sawa sawa na kumtaka Rais awalazimishe watu wakate matawi ambayo wamekalia huku wakijua kwa kufanya hivyo wataangukia mtoni kwenye mamba wengi. Hakukuwa na jinsi nab ado hakuna jinsi ni lazima kuwaondoa hawa na kuwashughulikia ili kuleta watu wenye fikra zinazoakisi mwelekeo wa serikali yake.

Ni kwa sababu hiyo, kumbe kazi ile ya miezi sita kwa kweli haiwezekani. Ni kazi ambayo inapaswa kuwa endelevu na yenye matokeo bora. Tayari tumeanza kuona dalili za yaliyomo ndani ya ripot ya Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu (CAG) na tayari inatisha kama ilivyotisha mwaka 2006 na miaka iliyofuatia. 

Kwa muda mrefu tumekuwa tukijulishwa juu ya uchafu wa watendaji wetu na taasisi zetu na mara karibu hizo zote tumekuwa tukionesha kushtushwa na kusikitishwa tukiamini kuwa labda mwaka unaofuatia mambo yatakua tofauti. CAG aliyepita alikuwa anarudia baadhi ya hoja mwaka baada ya mwaka na wakati mwingine kuhusiana na taasisi au watu wale wale. Na safari hii tusije kushangaa kuwa hata CAG wa sasa anaweza kujikuta amegusa maeneo yale yale; matumizi mabaya ya sheria ya manunuzi ya umma, fedha kutumiwa bila maelezo, kutopatikana kwa vitabu vya masuala ya fedha wakati wa ukaguzi, na upotevu wa fedha za umma kwa namna ambayo inadokeza tu kuwa zimeliwa.

Magufuli basi ana kazi kubwa; kushughulikia viongozi wabadhirifu, wazembe, wezi, na wenye kutumia madaraka yao vibaya na wakati huo huo kupanga na kusimamia serikali yake huku akiuunda upya mfumo uliojaribiwa na kuharibiwa.

Kwa mwendo alioanza nao hakuna shaka yoyote jambo moja lilikuwa sahihi kwa upande wangu; kuunga mkono mabadiliko haya. Wapo wanadhani hali ni ngumu sasa na kuwa serikali inabana naamini bado hatujaona hasa ugumu kwani hadi hivi sasa bado serikali inahangaika na madudu ya nyuma na yanatisha. Kusahihisha uchumi (correcting an economy) ambao umejengwa na kusimamiwa na utamaduni wa kifisadi (corrupt culture) haiwezekani kuwa ni jambo moja.

Ni kwa sababu hiyo naamini:

1. Kuanza kazi kwa mahakama za kushughulikia ufisadi na uhujumu uchumi kunahitajika mara moja

2. Sheria ya CAG ifanyiwe mabadiliko mapema zaidi ili CAG awe na madaraka ya kutoa agizo la kusimamishwa kazi na hata kufikishwa mahakamani kwa mtendaji yeyote wa umma ambaye uchunguzi wake (CAG) unaonesha kuwa kuna uvunjaji wa sheria. Ikiwezekana ofisi ya CAG iwe na Waendesha mashtaka wake kama ilivyo kwa TAKUKURU. Haipaswi madudu yam waka mzima yanasubiri mwaka mwingine kujulikana. CAG anapofanya ukaguzi na kukuta madudu na ushahidi wa kisayansi upo (forensic evidence) basi hatua zichukuliwe mara moja. Siyo awe na uwezo wa kupeleka mashtaka lakini kwa kupendekeza kwa DPP au hata yeye mwenyewe washutumiwa watiwe mbaroni, mali zao zinazohusiwa kupatikana kwa njia haramu kukamatwa ili zije kufilisiwa wakikutwa na hatia.

3. Sheria ya Usalama wa Taifa inahitaji kufanyiwa marekebisho ya haraka – hili ni jambo ambalo limekuwa katika mada zangu kwa karibu miaka kumi sasa. TISS bado ni dhaifu sana na udhaifu wake umechangia sana kutamalaki kwa utamaduni wa kifisadi. Natumaini Magufuli hatochukua muda mrefu kuifumua hii taasisi kwani ndio moyo wa taifa. Ikilegea taifa liko mashakani.

Kuna na mengine mengi ambayo naamini Magufuli atayafanya kwani tayari ameshaanza kuyafanya na kuwa endapo atafanikiwa tutakapofika mwisho wa mwaka huu kama taifa tutashusha pumzi kidogo kwani angalau tutakuwa katika mazingira ya kusema “kweli hakika huyu alikuwa anahitajika”.

Ni wazi pia kutokana na kazi hii ngumu ambayo tunaamini Magufuli anaiweza kutakuwepo na wasema “hapana” na waleta “vikwazo”. Wale ambao wataona maslahi yao yanaguswa na kuwa pale walipokuwa wakihemea sasa panaanza kuondolewa. Watakuwepo watu ambao watajaribu kudhulumu na kuharibu jitihada hizi; raia wa kawaida, watendaji serikalini, wabunge na tusije kushangaa hata watu wake wa karibu. La maana ni kukaza mwenzo na kuendelea kusafisha serikali, kuleta uwajibikani, na nidhamu ili hatimaye Ujenzi Mpya (Reconstruction) wa taifa letu uanze tena kwani pale tulipoacha kulijenga tulianza kulibomoa. Hizi ni Zama Mpya, zama za ujenzi mpya wa taifa letu.

Katika hili, naamini nilikuwa sahihi na bado naendelea kuwa sahihi. Magufuli ni kiongozi wa zama hizi.

Rungwe - Ningekuwa Rais Ningehakikisha Watanzania Wanapata Chakula Wanashiba Ndii,Halafu Mengine Ndio Yangefuata

$
0
0

Mwenyekiti wa chama CHAUMMA Mhe Hashim Rungwe yupo Kikangooni live anaongelea mambo mbalimbali.

Ningekuwa Rais jambo la kwanza ningehakikisha wananchi wote wanapata chakula, wanashiba kwanza mengine baadaye.

Ningefanya bei ya unga iwe shilingi 250, watoto shule wapate chakula, wapate uji, hawawezi kusoma na njaa.

"Chama Cha Mapinduzi hakina utamaduni wa kuwaheshimu watu wengine wenye uwezo ambao wanatoka vyama vingine.

Haya Hapa Maneno ya Mavugo Ambayo Kama Wewe ni Shabiki wa Yanga Unaweza Ukalia Ukiambiwa...!!!!

$
0
0

Straika nyota wa Simba, Mrundi, Laudit Mavugo, ni kama amepania baada ya kutoa kauli ya kishujaa akitamka kuwa watashinda mechi zote sita walizozibakiza kwenye Ligi Kuu Bara.

Kwa maneno hayo, maana yake Yanga ambao ndiyo wapinzani wao wakubwa wasahau kabisa kuhusiana na suala la kutetea ubingwa wao.


Simba hivi sasa inaoongoza kwenye msimamo wa ligi kuu ikiwa na pointi 55, Yanga wakifuatia na pointi 53 huku Azam wakiwa wa tatu wenye 44.


Mechi sita ambazo imezibakiza Simba ni dhidi ya Mbao FC, Toto Africans, Kagera Sugar, Mwadui FC, Stand United na African Lyon.

Mavugo alisema hakuna mechi nyepesi kwao kati ya hizo walizozibakiza, lakini kwa pamoja watapambana kuhakikisha wanashinda zote.

Mavugo alisema watalazimika kushinda mechi hizo zote kwa lengo la kutowaruhusu Yanga wawapite au wawakaribie kwenye idadi ya pointi walizonazo kwa hofu ya kuongeza ugumu.

Aliongeza kuwa, ana matumaini ya kushinda mechi hizo kutokana na ubora wa kikosi chao na morali iliyokuwepo kwenye timu kuhakikisha ubingwa wanauchukua kwenye msimu huu.

"Kila timu inakuwa ina mikakati yake, lakini kwetu Simba tulichopanga hivi sasa ni kushinda mechi zote sita tulizobakiza katika msimu huu wa ligi kuu.


"Ninajua siyo kazi rahisi, lakini bidii na kujituma kwetu ndiyo kutafanikisha hayo yote, ninaamini tuna kikosi bora kitakachofanikisha hayo yote.

"Kingine ni umoja na mshikamano uliopo hivi sasa katika timu yetu kwa kuanzia kwa viongozi, benchi la ufundi na wachezaji hatuwezi kuacha pointi hata moja kwa kuwa wapinzani wetu wanakuja kwa kasi," alisema Mavugo.

Njia 5 za Kudumisha Mahusiano ya Kimapenzi...!!!

$
0
0

Japo inasemwa kuwa mapenzi hayana njia moja ya kufuatwa lakini kuna vitu ambavyo vinajulikana kuchangia katika kuboresha mahusiano baina ya wapenzi.

Mahusiano ya mapenzi yenye kudumu ni sharti yapandwe katika udongo wenye rutuba kama ulivyo mmea,yatahitaji maji ya kumwagilia na mbolea ya kukuzia.  Na zaidi ya yote yanahitaji muda wa kukua kabla matunda kuonekana.

Uaminifu

Kumwamini mwenza wako ni jambo la msingi sana katika kudumisha mahusiano. Usimshuku mpenzi wako kuwa si muaminifu bila ushahidi wowote.

Kushukiwa kukosa uaminifu pasipo ukweli inasononesha sana na kumkosesha raha mpenzi wako.

Imesemwa na wanafalsafa wa mawazo ya binadamu kuwa “Unachofikiri na kuamini kinatokea” hivyo unashauriwa kutofikiri vibaya juu ya mpenzi wako kwani haileti afya katika mahusiano.

Hali kadhalika na wewe uwe mwaminifu na mwenye kusema kweli mara zote. Ongeeni juu ya mipango na mawazo yenu bila kufichana.

Watambulishe kwa mpenzi wako ndugu ,jamaa na marafiki wakaribu ili kumpa mwenza wako amani.

Weka muda kwajili ya Mwenza wako.

Mahusiano mazuri kati ya wapenzi yanahitaji muda wa wapenzi hao kukaa pamoja. Wapenzi wasio na muda wa kukaa wana hatari ya kupoteza mvuto wa mahusiano yao na hivyo kuhatarisha uhai wa mapenzi kati yao.

Kama wapenzi wapo mbali mbali basi wanahitaji kuweka muda wa kuongea kila inapowezekana.

Tafuta muda wa kutoka pamoja,hata kama mtaenda mkahawani kunywa chai au juisi tu,inatosha sana na inawaweka karibu zaidi.

Mawasiliano

Mawasiliano ni muhimu sana baina ya wapenzi.

Hata kama umebanwa na kazi pata dakika chache za kuongea na mpezi wako na kumtaka hali. 

Andika hata ujumbe wa maneno au barua pepe. Mwambie mpenzi wako ulipo kila mara inapobidi ili kumjengea imani na wewe na kumpa amani moyoni. Tuma ramani ya mahali ulipo kama unatumia simu ya “Smart” (Tuma location kwenye whatsapp)

Mawasiliano ni ufunguo wa kudumisha upendo.

Wakati kuwasiliana na mpendwa wako, kumbuka kwamba upendo ni muhimu. Ongea toka moyoni na si kwa ajili ya kutimiza wajibu tu,kwani mpezi wako atajua tu kama hakuna mahaba katika mawasiliano yenu hivyo kutoleta faida ile inayotegemewa.

Mawasiliano mengine ni yale ya kuelezana yaliyo moyoni. Mweleze mwenza wako linalokusibu ili kupata ufumbuzi wa pamoja. Wapenzi wanaoongea kwa utulivu siku zote watakuwa pamoja.
Zawadi

Tafuta kitu cha kumpa mpenzi wako. Si lazima kiwe na thamani kubwa.Inaweza ikawa pipi au matunda tu.

Mnunulie zawadi kila inapowezekana hasa unaposafiri au katika siku yake ya kuzaliwa.

Onyesha Upendo wako

Kila mtu anajinsi yake tofauti ya kuonyesha upendo, lakini vyovyote itavyokuwa ni jambo la muhimu sana kuonyesha hisia zako kwa mpenzi wako.

Mara nyingi wapenzi wa muda mrefu wanasahau juu ya hili.

Maneno kama “Nakupenda”au majina ya mahaba kama “Mpenzi” au ”La-azizi” yanachangia sana kuonyesha mapenzi na kumfanya mwenza wako kujisikia vizuri.

Maneno haya yanaposemwa kwa hisia halisi na toka moyoni yana mchango mkubwa katika kuboresha mahusiano.

Fahamu Sehemu Tano Muhimu za Kumshika Mwanaume Zitakazo Mpandisha Nyege/Hamu ya Kungonoka...!!!

$
0
0

wanaume nao huwa na maeneo ya kuwa sisimua na kuwpandisha nyege kwa kasi zaidi huku akipata raha ya ajabu.... leo nitayataja maeneo ambayo mwanaume akiguswa kimahaba huwa yanamsisimua sana na kumfanya ahisi kuchanganyikiwa kimahaba

1/ masikio 
hii ni seheme ambayo hubeba hisia nyingi sana za mwanadamu; hapa mwanamke hebu afanye kama kukunong'oneza kimaha kisha atumie ulimi wake kukugusa masikio ndani,nje na kwa nyuma pia 

2/shingoni
hii ni sehemu yenye hisia sana kwa kila kiumbe kwa sabubu mishipa mingi ya fahamu hukutania hapo
mguso wako wa pole pole kutumia ulimi wako na pumzi ya kimahaba vinaweza mfanya achanganyikiwe zaidi juu yako na kumfanya asahau mengine maana nyege zitampanda kwa haraka zaidi KAZI KWAKO kujua jinsi ya kumwekea na yey "love bite" pia mwanamke unatakiwa uwe fundi wa kutumia ulimi wako na lips hapo kwenye shingo ya mwanaume


3/ Ngozi

ngozi hapa ni namaanisha kushikana/kupapasana kabla ya kungonoka ni jambo zuri sana kwani utaufanya miili yenu isisimuke kwa pamoja na kumfanya mwanaume mzunguko wake wa damu kuongezeka na kuwa wenye kasi hii itamsaidia uume kuwa wenye nguvu na kusimama kwa muda(kumuongezea pumzi ya kutomwaga haraka na hata akimwaga iimpe nguvu ya mboo kutokulala baada ya kumwaga) na pia itampandisha nyege zake sana TUMIA HATA ZAIDI YA DAKIKA ISHIRINI KUSHIKANA/KUPAPAANA NA MWENZI WAKO KABLA YA TENDO

4/ Busu la Denda
hii sio kitu cha kushangaza jinsi gani denda(deep kiss) linavyo sisimua na kuamsha hisia na kuongea hashiki ya kufanya ngono//tendo la ndoa ila mwanamke inatakiwa ujue jinsi ya kumpagawisha mwanaume na Denda kwa kumyonya na kubite lips zake kimahaba tafadhali pia kwa kucheza na na ulimi wake kimahaba na sio kubadilishana mimate tuu mpe raha kuwa fundi kwenye denda asikumbuke kutoka nje kila mara akuwaze wewe tuu 

5/ Sehemu yake ya ndani(uume)
hii ndio sehemu yenye kumchanganya zaidi mwanaume kimahaba na ndiko sehemu hisia zake za kimahaba zimekaa . hapa mwanamke haitaji ujuzi mwingi bali ni kujua ni wakati gani ni mguse eneo hilo na nimguse vipi
mfano; mme simama kwenye ukuta utamgusa kwa kumpapasa juu ya alichokivaa kwa kupandisha mkono na kuushusha huku ukimguga uume wake fanya hivyo mara 8 mpaka 10 kabla ya kuingiza mkono ndani na kuitoa nje ili kuishika vizuri kimahaba na labda kuanza kuinyonya kiufundi na kimahaba zaidi
vivyo hivyo hata mkiwa kitandani usikurupuke kumshika uume wake unatakiwa umlegeze na umchanganye kimahaba kwanza KABLA YA TENDO PENDA KULAMBA KONI KWANZA
maana wanaume wengi hupenda kunyonywa mboo

na kwa kufanya ivyo itakusaidia kutunza uhusiano wako na mwenzi wako
usimbanie sana mwenza wako ujuzi wako na pia usipende kufanyia mapenzi gizani jiamini we ni mkali kwa mwenza wako na maumbile yeko aliyo kuumbia Mungu
jitoe kwa mwenza wako


Hatua Tano za Kufikia Mafanikio Makubwa Bila Kujali Wapi Umeanzia...!!!

$
0
0

Katika maisha kuna watu ambao wamefanikiwa sana na kuna ambao wanasukuma tu maisha siku ziende. Na ukiangalia hawa ambao wamefanikiwa sana kuna ambao walianzia chini kabisa, hawakuwa na elimu kubwa, hawakurithi mali na pia hawakupata watu wa kuwapa mitaji au kuwasaidia. Ila kwa hatua fulani wameweza kufikia mafanikio makubwa sana.

Inawezekana wewe ni mmoja wa watu ambao bado hujafikia mafanikio makubwa unayotazamia. Huenda umejaribu sana ila unaona kama bahati haiku upande wako. Huenda pia unaona kwa elimu ndogo uliyopata hutaweza kufikia mafanikio makubwa. Au kwa kuwa wazazi wako walikuwa masikini hivyo na wewe utaishia kuwa masikini.

Sasa leo nataka nikuambie kwamba yote hayo unayofikiria yanakukwamisha wewe kufikia mafanikio ni ya uongo. Nakuhakikishia unaweza kufikia mafanikio makubwa kama utazijua hatua muhimu za kukufikisha kwenye mafanikio na ukazitumia ipasavyo.

Leo utazijua hatua hizo kwenye makala hii, na kazi yako itakuwa ni kuanza kuzitumia hatua hizi mapema iwezekanavyo ili uweze kubadili maisha yako.

1. Amua ni nini unataka kwenye maisha yako

Hii ndio hatua ya kwanza na muhimu sana ili kuweza kufikia mafanikio makubwa. Cha kushangaza ni kwamba karibu asilimia 90 ya watu hawajui ni nini wanachotaka kwenye maisha yao. Hebu nikuulize ni nini hasa unachotaka kwenye maisha yako? Ukinijibu unataka kuwa na hela nyingi au kuwa tu na mafanikio makubwa basi hujui unachotaka. Unatakiwa ujue ni nini hasa unachotaka kwenye maisha yako. Kama ni fedha, sema ni kiwango gani cha fedha unachotaka na kwa muda gani. Kama unataka kufikia mafanikio makubwa ni lazima ujue mafanikio makubwa kwako wewe ni nini.

Kaa chini sasa na uandike kwenye kitabu chako cha malengo ni kitu gani unachotaka kwenye maisha yako. Kujua unakoelekea ndio mwanzo mzuri wa safari yako.

2. Jua ni gharama gani unatakiwa kulipa ili kufikia mafanikio unayotarajia

Kuna baadhi ya watu wanajua kabisa ni nini wanataka kwenye maisha yao na wamekuwa wakitamani sana kufikia kile wanachotaka. Lakini siku zinakwenda bila ya kuweza kufikia kile wanachotaka. Hii inatokana na watu hao kutojua gharama wanayotakiwa kulipa ili kufikia mafanikio wanayotarajia. Sikiliza utaendelea kuwa hivyo ulivyo kama utaendelea kuishi maisha unayoishi sasa. Na ili uweze kufikia mafanikio makubwa ni lazima uanze kubadilisha mfumo wako wa maisha wa sasa.

Katika kila jambo zuri unalotaka, kuna gharama utahitajika kulipa ili uweze kupata jambo hilo. Kama unataka kuongeza kipato zaidi ya unachopata sasa utahitajika kufanya kazi zaidi na kwa maarifa zaidi. Utahitaji kupunguza matumizi yasiyo ya msingi na pia utahitaji kupunguza muda unaopoteza kwenye mambo yasiyo ya msingi.

Jua ni gharama gani utakayotakiwa kulipa ili kufikia mafanikio makubwa na jipange kulipa gharama hiyo. Kama unafikiri unaweza kufikia mafanikio makubwa kwa kuendelea kuishi unavyoishi sasa unajidanganya. Gharama kubwa utakayotakiwa kulipa kwenye kila hatua kubwa unayotaka kupiga kwenye maisha yako ni kufanya kazi kwa bidii na maarifa.

3. Weka milango na mipango ya muda mfupi na muda mrefu

Baada ya kujua unataka nini kwenye maisha yako na kukubali kulipa gharama ya kupata unachotaka, sasa unahitaji kuwa na malengo na mipango. Ni vigumu sana kufanya jambo kubwa kwenye maisha yako kama huna malengo na mipango. Unahitaji kuwa na malengo ya muda mrefu, mwaka mmoja, miaka miwili, miaka mitano na hata miaka kumi. Malengo haya yaendane na kile unachotaka kwenye maisha yako ili ufikie mafanikio makubwa.

Pia unahitaji malengo ya muda mfupi, miezi sita, miezi mitatu, mwezi, wiki na hata siku. Kila siku hakikisha umeipanga kufanya kitu ambacho kitakusogeza kufikia malengo yako makubwa. Malengo yoyote unayopanga hakikisha unayaandika kwenye kitabu chako cha malengo. Malengo na mipango yako ndio yatakuwa muongozo kwenye maisha yako.

4. Kuwa mwaminifu

Katika safari yako ya kuelekea kwenye mafanikio makubwa, uaminifu ni nguzo muhimu sana. Ukikosa uaminifu utapoteza kila kitu ambacho umekuwa unakijenga kwa bidii na maarifa. Kuna picha ambayo imejengwa na jamii yetu kwamba watu waliofanikiwa ni wezi, wanadhulumu au wanatapeli. Ukweli ni kwamba watu wanaofanikiwa kwa njia hizo, mafanikio yao hayadumu kwa muda mrefu. Utakuwa shahidi yangu kwamba umewahi kuona watu wengi ambao ni wezi na maisha yao yanaishia wapi. Au wanaofanya biashara haramu mwisho wao unakuwa nini.

Usidanganyike hata kidogo kujihusisha na kazi au biashara yoyote ambayo ni kinyume na sheria au kinyume na imani au kisimamo yako binafsi. Uaminifu unalipa, jinsi unavyokuwa muaminifu ndivyo watu wengi wanavyokuamini na ndivyo itakavyokuwa rahisi wewe kufikia mafanikio makubwa.

5. Kuwa mvumilivu

Huu ndio ukweli ambao watu wengi hawapendi kuusikia. Hakuna kitu kwamba utalala masikini uamke tajiri, hakuna na ikitokea hivyo utajiri huo utapotea haraka kama moshi unavyopotea. Unahitaji muda ili kuweza kufikia mafanikio unayotarajia. Na katika muda huo utashindwa mara nyingi sana. Kama utakosa uvumilivu utaona muda huo ni mrefu sana na pia utakata tama kutokana na kushindwa. Na ukishakata tamaa ndio mwisho wa safari yako ya kufikia mafanikio makubwa. Uvumilivu ndio tofauti kubwa kati ya watu waliofanikiwa na ambao wanasukuma tu maisha yaende. Unahitaji kuwa mvumilivu sana na kuendelea kujifunza kutokana na makosa unayofanya.

Fuata hatua hizi tano na zifanyie kazi kila siku. Kama utazifuata kweli baada ya muda utaona mabadiliko makubwa kwenye maisha yako. Uwezo wa kufikia mafanikio makubwa unao, ni wewe tu kuanza kuutumia ili kufikia mafanikio hayo.


+18..Ukimfanyia Haya Mpenzi Wako,Hata Iwe Vipi Hatokusahau Kamwe...!!!

$
0
0

1. KILA siku usisahau kumsifia kwa kumwambia ni kiasi gani alivyo mzuri. Kumbuka kila msichana anapenda kusifiwa hivyo unapomuambia yeye ni mzuri anaona una mthamini kuliko msichana yeyote awaye.

2. Wakati wowote ukipata nafasi muandikie barua au msg kwenye simu mueleze hisia zako kiasi gani unampenda. Kumbuka wasichana hupenda kusikia zaidi kutoka kwa wapenzi wao ni kiasi gani wanapendwa. Haitakiwi iwe tu katika kipindi cha siku ya wapendanao ndio umuoneshe kuwa unampenda. Muoneshe msichana ni kiasi gani yeye ni muhimu sana kwako.

3. Busu la ghafla na kumshika mkono wakati mkitembea pamoja itamfanya yeye kujisikia raha zaidi. Na wakati mwingine msuprise kwa kumtembelea mara kwa mara hi humfanya akuone wewe ni mtu muhimu pale usipokuwa naye karibu na kumfanya kukuhitaji zaidi ukiwa naye mbali

4. Tambua mahitaji yake. Uwe msaada kwake kipindi ambacho mpenzi wako amekasirika kuwa pale kwa ajili yake na ukimpooza kwa sauti ya upole na mahaba. Utashangazwa sana na kiasi gani msaada huo umeleta mabadiliko kwake. Hakikisha unamsaidia katika shida zake hapa ndipo kuna tatizo kwa wavulana wengi. Mapenzi si pesa lakini kuna kipindi ambacho pesa huitajika kulinda penzi lako. Si msichana anapokuomba pesa ina maana ana nia ya kukuchuna au amekupendea pesa kuna shida nyingine inabidi akuombe wewe tena kwa kukupima kama utakuwa tayari kumsaidia.

5. Mchukue mpenzi wako out mara nyingine itamfanya ajisikie furaha sana kwa sababu wasichana hupenda enjoyment na boyfriend zao. Hii haitamfanya mpenzi wako tu kuwa na furaha bali itawafanya nyie kwa pamoja kujuana na kufahamiana zaidi.

6. Kuwa muwazi kwake usimfiche jambo linalokuhusu. Msichana hupenda kutoa ushauri kwa mtu ampendaye hivyo unapokuwa muwazi atajisikia kuthaminiwa nawe na kukuona umemuamini

7. Ukijiona upo busy sana usithubutu kuacha japo kumpigia simu mara mbili kwa siku hata kama ukishindwa kumpigia wakati upo ofisini darasani au kwingineko hakikisha unapopata nafasi japo ujumbe mfupi wa kumwambia unampenda.

8. Mkumbatie mara kwa mara katika tukio la kumbatizi kuna jambo kubwa sana hutokea. Si kwake tu hata kwako mvulana. Hali ya joto lenu huwaweka pamoja kifikra hata pale msipokuwa pamoja.

9. Epuka maugomvi na hasira za mara kwa mara ukiwa nae. Mwanamke hupenda ustaarabu kwa mtu ambaye yupo serious naye hivyo ukionesha hasira kabla hata hujamtongoza unaweza ukamkosa msichana hivihivi wasichana huwaogopa wavulana wenye hasira na wagomvi kwa sababu hupenda kubembelezwa.

10. Mdekeze. Msichana anapenda kudeka anaenda kudeka sana na kubembelezwa sana hivyo mvulana ukidekewa usikasirike eti huyu msichana kazidi wewe ndio wakati wako wa kumuonesha msuchana wako unampenda mdekeze mpaka aone aibu kudeka siku nyingine. Wasichana wameumbwa kwa jili ya wavulana ndio maana hudeka hii ndiyo silaha pekee na ya mwisho kumpata msichana hata kamasi wako ni wa rafiki yako unaweza ukatumia silaha hii kumpora msichana huyo kwa mwenzio usipojua kudekeza utaachwa pia.

Uchawi Katika Mapenzi Ndio Huu...!!!

$
0
0

Mapenzi  ni  miongoni  mwa  mambo  makuu  yanayo msumbua  mwanadamu. Tangu kuumbwa  kwa  ulimwengu  kuna  mamilioni  ya  watu   ambao  wameuwawa  kwa  sababu  ya  mapenzi, wameua  kwa  sababu  ya  mapenzi ama  wamejiua  kwa  sababu  ya  mapenzi. Wapo  walio  poteza  nafasi  zao  za  kazi  kwa  sababu  ya  mapenzi,  wapo  walio  feli  masomo  yao shuleni  kwa  sababu  ya  mapenzi, wapo  walio  filisika  kibiashara  kwa  sababu  ya  mapenzi, wapo  waliopatwa  na  ulemavu  wa  kudumu  kwa  sababu  ya  mapenzi, wapo  walio  patwa  na  uchaa  kwa  sababu  ya  mapenzi, wapo  walio  tupiwa  magonjwa  mbalimbali  ya  kichawi  kwa  sababu  ya  mapenzi, wapo  waliokosana  na   ndugu , jamaa  na  rafiki  zao  kwa  sababu  ya  mapenzi.

Ongezeko  la  watoto  wa  mitaani, watoto  yatima  katika  nchi  za  dunia  ya  tatu , Tanzania  ikiwemo, ni  miongoni  mwa   viashiria  ya   athari  ziletwazo  na   matatizo  katika  mahusiano.
Ongezeko  la  wanawake  kwa  wanaume  wanao  jihusisha  na  tabia  hatarishi za  kingono, kwa  kiasi  kikubwa  sana, linasababishwa  na  na  kuwepo  kwa  matatizo  katika  mahusiano. 

Hii  inaonyesha  ni  namna  gani  ambavyo  suala  la  mapenzi  lina msumbua  mwanadamu., 

 Kinyume chake  wapo  watu  walio  pata  mafanikio  makubwa  sana  katika  maisha  yao  kwa  sababu  ya  kunyookewa  katika  masuala  yao  ya  mahusiano.

Je  , ni  kwa  nini  basi  mapenzi  yanamuhanganisha  na   kumtesa  mwanadamu kwa  kiasi  hiki?
 Jibu  la  swali  hili  ni  rahisi  sana, hii  ni  kwa  sababu  ya  kukosa  elimu  ya  uhakika  ya  uchawi  kuhusu  mapenzi. Watu wanao fahamu   elimu  ya  uchawi  kuhusu  mapenzi, hawasumbuliwi  kabisa  na  kitu  kinacho  itwa  mapenzi.

Ukitimiza  masuala  maalumu  ya  kiroho  kuhusu  mapenzi , utafurahia  maisha  yako  ya  kimapenzi, utampata mwanamke  yoyote  yule  unaye  muhitaji, utampata  mwanaume  yoyote  yule  unaye  muhitaji  na  utaishi  naye  katika  namna    yoyote  ile  ambayo  wewe  unataka iwe. Atakupa  chochote  anachokitaka, kwa  kiasi, hali, jinsi  na  namna  yoyote  ile unayo  itaka  wewe.  Hata  hivyo, ili, ufanikiwe katika  hili    pamoja  na  mambo  mengine  yote  yale, unatakiwa  kuhakikisha  unafanya  yafuatayo:

1.  Unajiunga  na  madhabahu  maalumu  ya  watu  maalumu , yanayo  ongozwa  na  malaika  maalumu  wanao  toa  ulinzi  maalumu  katika  masuala   ya  kimapenzi kwa  watu  wanao  shiriki  katika  madhabau  hiyo.

2. Kushiriki  ibada  maalumu   katika  madhabahu  husika.
3. Toa  sadaka   maalumu  kwa  madhabau  husika.
4. Hakikisha  unafuata  na  kutimiza  maelekezo  yote  unayo pewa  na  kiongozi  wa  madhabahu  husika.

Hakika  utafurahia  maisha  yako  ya  kimapenzi  katika  siku  zote  za  maisha  yako.. Tafiti  mbalimbali  duniani  zinaonyesha  kuwa  miongoni  mwa  mambo  yanayo  weza  kumfanya  mwanadamau  aweze  kufanikiwa  vizuri   katika  maisha  yake  ni  kuwa  na  tulizo  la  moyo  wake( Yaani  kuwa  na  mwanamke  ama  mwanaume  anaye  mpenda  a  kupendwa  naye  )..

ZIMEBAKI SIKU 5 MSHINDI KUTANGAZWA, JISAJILI SASA NAFASI NI YAKO USIFE MOYO

$
0
0
Umeshawahi Kufikiria Kupata Gari la Bure bila Kulipa Chochote, Basi hii Kampuni ya Cars From Japan Wanakupa Nafasi Hiyo na ww miliki Gari bure.

Chakufanya ni Kubofya Link hapo chini na Ufate Maelekezo ya Jinsi ya Kuweza Kuwa Mshindi wa Gari hilo, Nirahisi sana wala usihofu

Kisha Jisajili kwa Kuweka Jina na Email Yako... USIWE NA WASIWASI HUDUMA HII NI SALAMA KABISA..

Jinsi ya kujiunga:
Bofya hayo maandishi ya rangi ya blue kisha itafunguka kurasa ambayo itakuwa iko hivi.

Kisha Bofya neno APPLY NOW kisha itafunguka hivi.

Kisha utajaza Form hii kisha utaBofya neno NEXT itafunguka kurasa ingine nayo ufate maelezo yake..

Mwisho wa Kujisajili ni 20 / 3 / 2017

Uuwii...Umemsikia Jike Shupa..Eti Anadai Haogopi Ukimwi 'so' Haoni Shida Kubadili Wanaume Kama 'Chupi'

$
0
0

HAMNAZO! Msanii muuza sura katika video za Bongo Fleva, Zena Abdallah ‘Jike Shupa’ ametoa kali ya mwaka baada ya kudai haogopi Ukimwi kwa kuwa ni ugonjwa wa kawaida, ndiyo maana amekuwa akibadili wanaume ovyo bila wasiwasi.

Aliiambia safu ya Za Motomoto News kuwa wanaume wengi wamekuwa wakimtokea na kumhitaji kimapenzi, hivyo kutokana na uwingi wao, anajikuta akishindwa kuwakatalia wote hivyo kuwakubalia, pamoja na ukweli kuwa humpa fedha.

“Sioni shida kubadili wanaume kila siku maana wao wenyewe ndiyo wanaonitamani, siogopi Ukimwi maana kila mtu duniani ameathirika, huo ni ugonjwa wa kawaida kama mwingine, wanaume wanaonitamani ni wengi hivyo nashindwa kuwakataa,  naingia nao kwenye uhusiano siku mbili tatu tunaachana, nakuwa na mwingine,” alisema Jike Shupa.
Viewing all 104785 articles
Browse latest View live




Latest Images