Quantcast
Channel: UDAKU SPECIAL
Viewing all 104694 articles
Browse latest View live

ZIMEBAKI SIKU 4 MSHINDI KUTANGAZWA, JISAJILI SASA NAFASI NI YAKO USIFE MOYO

$
0
0
Umeshawahi Kufikiria Kupata Gari la Bure bila Kulipa Chochote, Basi hii Kampuni ya Cars From Japan Wanakupa Nafasi Hiyo na ww miliki Gari bure.

Chakufanya ni Kubofya Link hapo chini na Ufate Maelekezo ya Jinsi ya Kuweza Kuwa Mshindi wa Gari hilo, Nirahisi sana wala usihofu

Kisha Jisajili kwa Kuweka Jina na Email Yako... USIWE NA WASIWASI HUDUMA HII NI SALAMA KABISA..

Jinsi ya kujiunga:
Bofya hayo maandishi ya rangi ya blue kisha itafunguka kurasa ambayo itakuwa iko hivi.

Kisha Bofya neno APPLY NOW kisha itafunguka hivi.

Kisha utajaza Form hii kisha utaBofya neno NEXT itafunguka kurasa ingine nayo ufate maelezo yake..

Mwisho wa Kujisajili ni 20 / 3 / 2017

Miujiza ya Shekh Sharifu Rashid Je? Unapata Pesa Haika? Kusafisha Nyota na Kurudisha Mke/Mume Aliekuacha

$
0
0

MIUJIZA YA SHEKH SHARIFU RASHID KUTOKA BAGAMOYO PWANI. (RUDISHA MAHUSIANO YAKO NDANI YA MASAA 72 TU) ASANTE KWA KUENDELEA KUMPIGIA SIMU SHEKH SHARIFU RASHID KWA WALE WENYE MATATIZO NA WALE WANAOTOA SHUKRANI: SHEKH SHARIFU RASHID ni mtaalamu wa tiba mbalimbali za asili, anatumia kitabu cha quran dawa za asili dawa za kiarabu, na njiwa, Anakuvutia mpenzi alie kuacha au alie mbali, anazo dawa za mapenzi, nguvu za kiume, chango kwa kina mama, ngiri maji na n.k, anakuvutia mali zilizo potea au kudhulumiwa, pia anatoa Pete za bahati zilizoambatanishwa na jini mali, Wenye matatizo ya uzazi, jini mahaba, mapepo ya kichawi, vifungo vya kimaisha, ndoto mbaya za usiku, uelewa mdogo wa ufahamu shuleni kwa watoto wote, pia anauwezo mkubwa wa kumaliza kazi zilizoachwa na wataalamu wengine ndani ya masaa 48 tu, Pia anatibu kwa njia ya simu popote ulipo. WASILIANA NAE KWA WhatsApp na SIMU NO: +255 718-668347 na +255 767-204308 +255 685-224047 Email shekhsharifurashidi@gmail.com.

USHAURI: ni vyema kupiga simu kuliko kutuma sms ili upate huduma kwa haraka.

Rungwe amtaka Mwakyembe asiivuruge TLS

$
0
0

Mwenyekiti wa CHAUMMA, Hashim Rungwe amemtaka Waziri wa Katiba na Sheria Dkt. Harrison Mwakyembe kuacha kuingilia mambo yanayohusu chama cha wanasheria Tanganyika (TLS) hasa kwenye suala uchaguzi wa kumsaka Rais wa chama hicho


Akijibu maswali ya wananchi kwenye kipindi cha KIKAANGONI kinachorushwa katika ukurasa wa Facebook EATV, Mh. Rungwe amesema kuwa TLS ina utaratibu wake wa kuendeshwa na kamwe haiwezi kupelekwa kama jinsi waziri anavyotaka kwani chama hicho kinaongozwa kwa sheria na kanuni.

“Yeye kama Waziri maoni yake ni muhimu, lakini  anasema vijana hawa wawili wana maoni ya kisiasa yaani Lissu na mwenzake lakini wakati huo huo yeye ni waziri na mpaka amefika hapo yupo ndani ya chama cha kisiasa. na amevaa kofia mbili. TLS  haiwezi kuendeshwa kama anavyotaka yeye, huwezi kutengeneza utaratibu nje ya utaratibu. Tuheshimu pia taaluma za watu." Rungwe alifunguka.

Aidha Rungwe ambaye pia ni Wakili wa Mahakama Kuu na Mwanachama wa chama hicho ameongeza kuwa katika chama hicho hakuna sheria ambayo inamzuia mwanasiasa yoyote kugombea nafasi na kuongeza kwamba kuwazuia upinzani wakati waliomo kwenye chama tawala wanaruhusiwa ni kutengeneza chuki ndani ya jamii na nchi kwa ujumla Hashim Rungwe

"Kutengeneza chuki kwa makusudi it's a great crime, hasa chuki ikitengenezwa na viongozi waliopo madarakani, ambao wamepewa dhamana ya kuwaongoza wananchi yeye atuache na TLS yetu, kama itaonesha watu hawa hawaruhusiwi kugombea basi watazuiliwa kwasababu watu wanaochuja wagombea ni sisi wenyewe". Amesema

Hivi karibuni Waziri huyo wa Sheria na Katiba alinukuliwa akisema kuwa serikali haiwezi kuona (TLS) kinajiingiza katika siasa na kuongeza kuwa kama wanataka hivyo, basi serikali haitasita kuifuta Sheria ya TLS Sura ya 307 iliyoanzisha chama hicho cha wanasheria.

Makonda ajitetea kuhusu Wema Sepetu, Gwajima

$
0
0

HATIMAYE Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam, Paul Makonda, ametoa ufafanuzi kuhusiana na sababu za kuwatangaza hadharani watu waliohusishwa na dawa za kulevya wakiwamo Askofu Josephat Gwajima na mshindi wa taji la mrembo wa Tanzania mwaka 2006, Wema Sepetu.

Akizungumza katika hafla ya kutimiza mwaka mmoja tangu ateuliwe na Rais Magufuli kuwa Mkuu wa Mkoa huo kwenye viwanja vya Oysterbay jana, Makonda alisema uwazi katika mapambano dhidi ya dawa za kulevya ni miongoni mwa sababu hizo, nyingine zikiwa ni kujiweka kwake mbali na vishawishi vya rushwa na pia kuwadhihirishia wananchi kuwa taarifa wanazotoa kuhusiana na vita hiyo zimekuwa zikifanyiwa kazi bila kusita.

Gwajima ambaye ni Askofu wa Kanisa la Ufufuo na Uzima lililopo jijini Dar es Salaam, pamoja na Wema ambaye pia ni msanii wa filamu, ni miongoni mwa watu maarufu kadhaa waliotajwa na Makonda katika orodha ya awali ya watuhumiwa 65 wa dawa za kulevya.

Wengine katika orodha hiyo ni pamoja na wanasiasa aliyekuwa Mbunge wa Kinondoni kupitia Chama Cha Mapinduzi (CCM), Iddi Azzan; baadhi ya wamiliki wa hoteli na klabu za usiku na pia wasanii wakiwamo Khalid Mohamed ‘TID’ na Chid Benz.

Watuhumiwa hao walitakiwa na Makonda kujisalimisha katika Kituo Kikuu cha Polisi jijini Dar es Salaam kwa mahojiano kabla ya hatua zaidi za kisheria kuchukuliwa kwa baadhi yao.

Mahakama Yatupilia Mbali Kesi ya Kuzuia Uchaguzi wa TLS

$
0
0

Mahakama Kuu imetupilia mbali kesi ya Kikatiba iliyofunguliwa na Wakili Onesmo Mpinzila pamoja na mambo mengine akipinga Kanuni za Uchaguzi za Chama cha Wanasheria Tanganyika (TLS) za mwaka 2016.


Kesi hiyo imetupiliwa mbali baada ya Mahakama kukubaliana na hoja za mapingamizi ya TLS na Mwanasheria Mkuu wa Serikali ambao ndio waliokuwa wadaiwa katika kesi hiyo.


Hoja hizo ambao Mahakama imekubaliana nazo ni pamoja na kwamba mdai hakuwa na mamlaka kisheria kufungua kesi hiyo na kwamba hati yake ya kiapo kilichokuwa kikiunga mkono madai yake ilikuwa na kasoro za kisheria.


Uamuzi huo umesomwa na Jaji Ignasi Kitusi kwa niaba ya jopo la majaji watatu waliokuwa wakisikiliza kesi hiyo. Majaji wengine walikuwa ni Rose Teemba(kiongozi wa jopo) na Beatrice Mutungi.

Kimenukaaa..Lulu Diva Aanika Ukweli Ishu ya Madawa,Amtaja Petiti Man...!!!

$
0
0

NAKIRI! Baada ya jina lake kuwemo katika orodha ya mastaa waliotuhumiwa kujihusisha na madawa ya kulevya, hatimaye msanii Lulu Abbas ‘Lulu Diva’ ameamua kuanika ukweli wake, kwa kukiri kuwa ni kweli ndiye aliyekuwa chanzo cha kukamatwa kwa mpiga picha Petit Man ambaye pia alitajwa kwenye listi hiyo ya Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam, Paul Makonda. 

Akizungumza na Risasi Mchanganyiko juzikati, Lulu Diva alisema kukamatwa kwake kulitokana na picha ya unga mweupe aliyomtumia Petit Man, akimuuliza kilikuwa ni kitu gani, baada ya yeye kuwa ameupiga picha huko Afrika Kusini alikokwenda kikazi.

“Nilikuwa nimeenda Afrika Kusini kwa ajili ya kushuti video, sasa kutokana na gharama kubwa, nikawa nimeomba kwa wadau waniunganishe kwa Mbongo yeyote kule ili kusevu gharama, nikapewa dada mmoja hivi ambaye nilifikia kwake.

“Nikiwa kule nikawa simwelewi mwelewi hivi, kwani mara kwa mara walikuwa wanakuja polisi wanasachi na kuondoka, pia alikuwa anakuja na watu wengi wake kwa waume ambao sikujua wanafanya shughuli gani.

Sasa siku moja alikuja na watu wengi wakawa wamekaa wanaongea, walipoondoka wakaacha unga f’lani mezani. “Sijawahi kuuona hata mara moja, nikaupiga picha, sasa nikasema hebu nimtumie rafiki yangu Petit Man, nikamuuliza hiki ni kitu gani?” alisema binti huyo huku akisema picha hiyo ndiyo ambayo polisi waliikuta kwenye simu ya Petit Man na kumkamata.

“Baada ya kunitaja nilitafutwa siku mbili sikuwepo Dar maana nilivyorudi kutoka huko nilienda nyumbani Tanga kumuona mama yangu, nilivyorudi siku ya tatu usiku wa manane ndiyo nyumba ikazingirwa na polisi, nikachukuliwa na kupelekwa ‘Sentro’ ambapo nilikaa siku kadhaa kabla ya kupelekwa mahakamani.

“Kiukweli sijawahi kutumia au kubeba unga na siujui ila kiherehere changu cha kupiga picha na kuuliza kwa Petit ndicho kilichoniponza, bado naendelea kuripoti polisi kwa mwezi mara mbili kwa ajili ya kupimwa,” alisema Lulu Diva.

Lulu Diva ni miongoni mwa mastaa waliotajwa na Mkuu wa Mkoa wa Dar, Paul Makonda katika orodha ya watuhumiwa wa madawa ya kulevya ambapo walikamatwa na kupandishwa katika Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu na kuachiwa kwa dhamana kwa sharti la kuripoti kituo cha polisi Sentro mara mbili kwa mwezi.

Ahukumiwa Kuchapwa Kiboko Kimoja kwa Kumpa Mwanafunzi Mimba...!!!

$
0
0

Mahakama ya Wilaya ya Hai  Mkoani Kilimanjaro  imetoa hukumu ya kuchwapwa kiboko kimoja mwanafunzi wa kidato cha tatu shule ya sekondari Longoi wilaya hapo baada ya kupatikana na hatia ya kumbaka na kumpa ujauzito mwanafunzi mwenzake wa shule hiyo

Akisoma hukumu hiyo  Hakimu  mkazi Mfawidhi wa mahakama hiyo, Agnes Muhina  mbele ya mwendesha mashtaka wa polisi , Valeria Banda, alisema kuwa anatoa hukumu hiyo baada ya kuridhishwa na ushaidi uliotolewa mahakamani  hapo usioacha shaka yoyote.

Kesi hiyo pia ilikuwa na mashahidi sita wa upande wa mashtaka akiwemo daktari wa hospitali ya Hai,dawati la jinsia na watoto na mama mzazi wa binti huyo, mwalimu na binti mwenyewe.

Ilidaiwa na mwendesha mashtaka wa polisi  kuwa mtuhumiwa alitenda kosa hilo   Oktoba 10, 2015 saa 8.00  mchana katika kijiji cha Mkalama Wilayani humo ambapo alimbaka na kumpa ujauzito mwanafunzi mwenzake wa kidato cha tatu mwenye umri (16).

Meya wa Ubungo Kufungua Kesi Dhidi ya Vyeti Feki..!!!

$
0
0

Mayor wa Ubungo Mh. Borniface Jacob anakusudia kufungua shauri mahakamani la kumtaka mkuu wa mkoa wa Dar es Salaam kuonesha vyeti vyake ili kuondoa utata uliojitokeza hivi karibuni dhidi ya kiongozi huyo wa mkoa. Kesi hiyo inatarajiwa kufunguliwa jumatato ijayo ya tar 20/03/2017.


Yafahamu Makundi Manne ya Binadamu...!!!

$
0
0

Binadamu kama walivyo viumbe wengine, hutofautiana kwa mambo mengi. Kwa kushindwa kutambua tofauti zilizopo baina yao, binadamu wamekuwa ni viumbe wanaoongoza kwa migogoro. Kwa kuzingatia hilo, nimekuandalia mada inayohusu aina na makundi ya binadamu. Naamini baada ya kufahamu tabia na hulka tofauti za binadamu, migogoro isiyo ya lazima itaepukwa.

Binadamu wanagawanywa katika makundi makuu mawili kulingana na uwezo wao wa kufikiri na kuchanganua mambo.Makundi hayo mawili yamegawanyika mara mbili na kutengeneza makundi makuu manne kama ifuatavyo:​

1.Introvert- Hili ni kundi linalojumuisha binadamu wenye uwezo mkubwa kiakili na wanaotafakari mambo kwa kina, Binadamu wanaopatikana katikakundi hili hutofautiana kwa kiasi kikubwa na wengine kutokana na uwezo wao wa akili (Intelligent Quotient). Kundi hili nalo limegawanyika katika makundi makuu mawili ambayo ni:

A. Melancholy: Binadamu katika kundi hili ni wenye upeo mkubwa wa kuvumbua mambo ya kitaalam yanayohitaji akili nyingi na wana uelewa mpana kwenye masomo ya Sayansi na Hesabu. Licha ya uimara huo katika akili zao, binadamu wa kundi hili wana hisia zinazogusika na kuchokozeka kirahisi. 

Wanawake ni wepesi wa kulia pale wanapokerwa hata na jambo dogo, Wana upendo wa dhati lakini wanapotendwa hata kwa jambo dogo, huumia sana kihisia. Wana huruma sana na hawapendi kuona wengine wakionewa. Wana aibu sana wawapo mbele ya watu wengi na ni watunzaji wazuri wa siri.

B. Phlegmatic:
Hili ni kundi la binadamu ambao wana uelewa mpana, wana uwezo wa kuchanganua mambo kwa kina na kujenga hoja lakini hawawazidi binadamu wa kundi la kwanza (Melancholic). Wana hisia ngumu, siyo waoga na wanajijali wao kuliko watu wengine.

Ni wabishi na hupenda kutumia mifano na takwimu katika ubishi wao. Hawayapi mapenzi kipaumbele katika maisha yao nawengi huishi single' kwa muda mrefu. Wanajiamini sana hata kwa mambo ambayo hawayajui.Wengi hupenda kuchunguza na kufuatilia maisha ya wengine na wanafaa kwa kazi za ushushushu.

2. Extrovert: Hili ni kundi kuu la pili linaloundwa na binadamu wenye uwezo wa kawaida wa kiakili. Uwezo wao wa kuchanganua mambo ni wa kawaida, hawajishughulishi kujua mambo yasiyo na manufaa na ni wepesi wa kuridhika hata kwa mafanikio madogo. Kundi hili nalo limegawanyika katika makundi makuu mawili:

A. Sanguine- Kundi hili linaundwa na binadamu wenye uwezo wa kawaida wa kiakili, kufikiri na kuchanganua mambo (wakati mwingine huwa na uelewa mdogo). Ni wacheshi, wanapenda sifa, wanapenda kusikilizwa kuliko kuwasikiliza wenzao na hupenda kuwa wazungumzaji wakuu kwenye kila jambo hata kama hawana ufahamu nalo. Ni wagumu wa kutunza siri.

Hawapendi kujifunza mambo mapya na hata wakifundishwa husahau haraka. Wanapenda sana kuonekana kwa watu kwa kila jambo wanalolifanya hata kama ni dogo. Si waaminifu katika mapenzi na siyo ajabu kuwakuta wakiwa na wapenzi wengi kwa wakati mmoja.

B. Choleric- Kundi hili linaundwa na binadamu wenye sifa zinazokinzana na kundi la Melancholic. Wana uelewa mdogo katika kila jambo na wengi hukatisha masomo yao kutokana kuwa na vichwa vizito. Ni wakali, wakatili na wana wivu kwa mafanikio ya watu wengine

Tabia ya kila kundi, tunaendelea na uchambuzi wetu kwa kutazama tofauti kati ya kundi la Introvert na Extrovert.

Tofauti zote zinaanzia kwenye asili ya kila kundi. Kundi la kwanza (Intovert), asili yake ni kusikiliza na kuufuata msukumo wa nguvu kutoka ndani bila kutegemea mazingira ya nje wakati kundi la pili (Extrovert) husikiliza na kufuata msukumo wa nje ya miili yao. Hisia zao hutegemea mazingira ya nje kuliko ya ndani.

1: Ukimya
Binadamu wanaopatikana katika kundi kuu la kwanza, Introvert ni wakimya sana, wanaona aibu kuzungumza mbele ya binadamu wengi ingawa wanapenda kufanya mambo kwa vitendo. Wanaelewa zaidi kwa vitendo nahawaamini kwa urahisi kile wanachokisikia bila kuona vitendo.

Binadamu wanaopatikana katikakundi la pili ni kinyume chake. Extrovert wanapenda sana kuzungumza na kubishana mbeleya wengine hata kama hawana uhakika juu ya kile wanachokibishia. Ni wepesi wa kuamini maneno ya wengine bilakutafakari kwa kina na hupotoshwa kirahisi. Ni wagumu wa kuonesha vitendo juu ya yale wanayoyasema.

2: Uvumilivu
Binadamu wanaopatikana katika kundi la kwanza, Introvert ni wavumilivu katika mipango ya muda mrefu na hawaoni hasara kulifuatilia jambo moja hata kwa kipindi kirefu. Hawajali linaumiza kichwa kwa kiasi gani ilimradi wafanikiwe. Mara nyingi wanapenda kufanya kazi peke yao na kuwaonesha wengine matokeo.

Kundi la pili ni kinyume chake. Extrovert wanapenda sana kazi nyepesi nyepesi zisizoumiza kichwa na zinazokamilika haraka.Hawapendi kazi ngumu zinazochukua muda mrefu kukamilika na hulka hii inawaweka mbali na mafanikio ya muda mrefu. Wanapenda kufanya mambo katika jumuiya kuficha udhaifu wao na wanapofanikiwa hata kwa kiasi kidogo, hujisifu sana.

3: Marafiki
Kundi la kwanza la binadamu (Introvert) huwa na idadi ndogo ya marafiki kutokana na haiba ya ukimya na kuona haya kuzungumza na wengine kwa mambo ambayo wanayaona siyo ya manufaa. Wengi ni wakimya na hawawasiliani sana na wengine kutokana na asili yao, hali inayowafanya wawe na marafiki wachache. Hata hivyo, marafiki wanaokuwa naohudumu nao kwa kipindi kirefu. Kundi la pili ni tofauti kwa sababu ya haiba yao ya uzungumzaji na ucheshi hupata marafiki wengi na kufahamika kwa urahisi kutokana na kupenda kuonekana kwa wengine lakini mara nyingi marafiki wanaokuwa nao hudumu nao kwa kipindi kifupi.

4: Mavazi
Kundi la kwanza (Introvert) hupendelea mavazi ya kawaida yanayowafanya wawe huru kufanya mambo yao. Hawapendikujipamba sana kwa vito au nakshi nyingi, wanapenda kuonekana simple lakini nadhifu. Wanavutiwa na rangi zilizopoa. Kundi la pili ni tofauti. Extrovert wanapenda sana mavazi yanayowafanya waonekane wanazo', hupenda kujiremba kwa mavazi ya bei ghali, vito na vidani vingi kwenye miili yao (hasa wanawake). Wanapenda sana rangi zinazong'aa na kuonekana kwa urahisi. Hii ni kwa sababu popote walipo wanataka wengine wawaone. Huwa hawajali unadhifu bali hupendelea mavazi na vitu vya bei ghali.

Tofauti ya tano na ya mwisho inayohusu uhusiano wa kimapenzi.

5. MAPENZI
Kama tulivyoona katika matoleo yaliyopita, binadamu wa kundi la Extrovert wanaongozwa na nguvu za msukumo na hisia kutoka nje (mazingira wanayoishi). Tuliona kwamba binadamu wanaopatikana katikakundi hili ni waongeaji sana, wacheshi, wanaopenda kuonekana na sifa nyinginezo nyingi.
Tuliona pia kuwa binadamu wanaopatikana katika kundi la Introvert wana sifa zinazokinzana na wale wa kundi la kwanza. Ukimya, kupenda kusikiliza kuliko kuzungumza, ugumu wa kuwasiliana na wengine na kuongozwa na hisia na msukumo kutoka ndani ni baadhi ya sifa zinazowafanya binadamu wa kundi hili wawe tofauti na wengine. Inapotokea binadamu wa kundi la kwanza akawa na uhusiano wa kimapenzi na mwingine kutoka kundi la pili, je, uhusiano wao utadumu? Hili ni swali la msingi tunalopaswa kujiuliza. Migogoro mingi ndani ya ndoa na uhusiano wa kimapenzi husababishwa na wahusika kushindwa kuelewa tofauti zilizopo kati yao na wanaowapenda. Ni makosa kulazimisha mwenzako afanane na wewe bila kuzingatia tofauti za msingi zilizopo baina yenu. Hii ndiyo sababu ya msingi ya kumchunguza na kumwelewa mwenzi wako kabla hamjaingia katika maisha ya ndoa kwani ukishindwa kumuelewa mwenzako utaangukia pua.

Soma mfano ufuatao: Salum na Miriam ni wapenzi waliokaa pamoja kwa miezi kadhaa. Tabia na mwenendo wa Salum unamfanya Miriam ahisi kwamba hapendwi ila analazimisha kupendwa (anajipendekeza). Siku zote malalamiko yake ni kuwa Salum hamjali, hapendi kuzungumza naye mpaka alazimishwe na ni mgumu sana wa kutoa siri zake, hali inayomfanya Miriam ahisi kuwa huenda ana mpenzi mwingine anayempenda zaidi yake.

"Mimi ni mcheshi sana, napenda kufurahi na kupiga stori na marafiki. Nafahamika na kuheshimika na wengi lakini mpenzi wangu yuko tofauti. Ni mkimya sana, anapoongea na mimi haniangalii usoni na mara zote yeye huwa msikilizaji tu bilakuchangia chochote katika hoja ninazozianzisha. Hana marafiki wengi na hupenda kujitenga kuliko kukaa na mimi," analalamika Miriam.

Tatizo hapa linasababishwa na utofauti wa asili uliopo kati ya Salum na Miriam. Salum anapatikana katika kundi la pili labinadamu (Introvert) na Miriam anapatikana katika kundi la kwanza (Extrovert). Kwa kushindwa kufahamu tofauti iliyopo kati yake na mpenzi wake, Miriam anahisi Salum hampendi. Laiti kama angejua kuwa kuna tofauti kubwa kati yao, angejua namna ya kukabiliana na hali hiyo.

Matatizo kama hayo huwakumba wengi, Cha msingi hapa ni kufahamu tofauti zilizopo na kuwa tayari kuendelea kujifunza. Introvents wana asili ya ukimya na ni wagumu wa kuwasiliana na wengine lakini hiyo haina maanakwamba hawayawezi mapenzi. Ukiweza kufahamu tofauti na kuzichukulia kama changamoto, watu wa kundi hili jhuwa na upendo wa dhati kuliko Extrovert. Wakianzisha uhusiano huwa wanataka udumu kwa kipindi kirefu zaidi.

Karibuni kwa mjadala zaidi.

ZIMEBAKI SIKU 4 MSHINDI KUTANGAZWA, JISAJILI SASA NAFASI NI YAKO USIFE MOYO

$
0
0
Umeshawahi Kufikiria Kupata Gari la Bure bila Kulipa Chochote, Basi hii Kampuni ya Cars From Japan Wanakupa Nafasi Hiyo na ww miliki Gari bure.

Chakufanya ni Kubofya Link hapo chini na Ufate Maelekezo ya Jinsi ya Kuweza Kuwa Mshindi wa Gari hilo, Nirahisi sana wala usihofu

Kisha Jisajili kwa Kuweka Jina na Email Yako... USIWE NA WASIWASI HUDUMA HII NI SALAMA KABISA..

Jinsi ya kujiunga:
Bofya hayo maandishi ya rangi ya blue kisha itafunguka kurasa ambayo itakuwa iko hivi.

Kisha Bofya neno APPLY NOW kisha itafunguka hivi.

Kisha utajaza Form hii kisha utaBofya neno NEXT itafunguka kurasa ingine nayo ufate maelezo yake..

Mwisho wa Kujisajili ni 20 / 3 / 2017

Sababu ya Manji kushindwa kutokea Mahakamani leo

$
0
0


Ile kesi inayomkabili Mwenyekiti wa Yanga, Yusuf Manji ya matumizi ya dawa za kulevya aina ya Heroine, imeshindiindikana kusikilizwa kwenye Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu na kupigwa kalenda hadi Aprili 18, mwaka huu.


Mtuhumiwa, Manji alishindwa kutokea kutokana na kusumbuliwa na maradhi ya moyo ambapo amelazwa katika Hospitali ya Aga Khan jijini Dar es Salaam.


Tuhuma zinazomkabili Manji ni kutumia madawa hayo kinyume na Sheria ya mwaka 2015 ya kuzuia na kupambana na madawa ya kulevya kifungu cha 17 (1) namba 5 ambapo inadaiwa Manji alitumia dawa hizo Februari 6 na 9, mwaka huu. 


Mashabiki mbalimbali wa soka walijitokeza mahakamani hapo kuifuatilia kesi hiyo.


Kesi hiyo ambayo inasikilizwa na Hakimu Mkazi Mfawidhi, Cyprian Mkeha huku upande wa Jamhuri ukiwakilishwa na Wakili Osward Tibaloyekomya huku upande wa Manji ukiongozwa na Wakili Alex Mgongolwa.


Kesi hiyo ilipangwa kusikilizwa jana Alhamisi lakini ilishindikana baada ya pande zote mbili kushindwa kutokea mahakamni hapo.



Manji yupo nje kwa dhamana ya milioni 10 aliyowekewa na Katibu wa Yanga, Charles Mkwasa.

Makonda Ajitetea Kuhusu Wema Sepetu, Gwajima..!!!!

$
0
0

HATIMAYE Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam, Paul Makonda, ametoa ufafanuzi kuhusiana na sababu za kuwatangaza hadharani watu waliohusishwa na dawa za kulevya wakiwamo Askofu Josephat Gwajima na mshindi wa taji la mrembo wa Tanzania mwaka 2006, Wema Sepetu.

Akizungumza katika hafla ya kutimiza mwaka mmoja tangu ateuliwe na Rais Magufuli kuwa Mkuu wa Mkoa huo kwenye viwanja vya Oysterbay jana, Makonda alisema uwazi katika mapambano dhidi ya dawa za kulevya ni miongoni mwa sababu hizo, nyingine zikiwa ni kujiweka kwake mbali na vishawishi vya rushwa na pia kuwadhihirishia wananchi kuwa taarifa wanazotoa kuhusiana na vita hiyo zimekuwa zikifanyiwa kazi bila kusita.

Gwajima ambaye ni Askofu wa Kanisa la Ufufuo na Uzima lililopo jijini Dar es Salaam, pamoja na Wema ambaye pia ni msanii wa filamu, ni miongoni mwa watu maarufu kadhaa waliotajwa na Makonda katika orodha ya awali ya watuhumiwa 65 wa dawa za kulevya.

Wengine katika orodha hiyo ni pamoja na wanasiasa aliyekuwa Mbunge wa Kinondoni kupitia Chama Cha Mapinduzi (CCM), Iddi Azzan; baadhi ya wamiliki wa hoteli na klabu za usiku na pia wasanii wakiwamo Khalid Mohamed ‘TID’ na Chid Benz.

Watuhumiwa hao walitakiwa na Makonda kujisalimisha katika Kituo Kikuu cha Polisi jijini Dar es Salaam kwa mahojiano kabla ya hatua zaidi za kisheria kuchukuliwa kwa baadhi yao.

Magufuli Ashiriki Ujenzi wa Ikulu Mpya Dodoma,Atoa Ahadi Mpya...!!!

$
0
0

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. John Pombe Magufuli leo tarehe 16 Machi, 2017 ametembelea eneo la ujenzi wa Ikulu Chamwino Mkoani Dodoma na kuwahakikishia wananchi kuwa atahamia Dodoma hivi karibuni kama alivyoahidi.

Mhe. Rais Magufuli ambaye ameongozana na Waziri Mkuu Mhe. Kassim Majaliwa Majaliwa, Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu Sera, Bunge, Kazi, Vijana, Ajira na Wenye Ulemavu Mhe. Jenister Joakim Mhagama na Katibu Mkuu Kiongozi Balozi John Kijazi amesema pamoja na majengo ya Ikulu Serikali itajenga miundombinu mingine zikiwemo reli na barabara za lami zitakazounganisha maeneo ya vijiji vinavyozunguka Ikulu na mji wa Serikali.

Pia Mhe. Dkt. Magufuli amewahakikishia wananchi kuwa wote watakaoguswa na shughuli za ujenzi wa miundombinu ya Serikali na wanaostahili kulipwa fidia watalipwa, na ametoa wito kwa wananchi hao kutumia fedha za fidia watakazolipwa kujenga makazi bora na kujipanga kufanya shughuli zenye manufaa kwao.

“Hapa sasa watakuja watu wengi, wafanyakazi na wageni maana tayari Mabalozi wa nchi mbalimbali nao watajenga ofisi zao hapa, sasa na nyinyi mjipange kufanya biashara, mtapata soko la kuuza mazao na bidhaa nyingine, mkipata fedha ziwasaidie kwa manufaa na sio kuzichezea” amesisitiza Mhe. Rais Magufuli.

Kwa upande wake Waziri Mkuu Mhe. Kassim Majaliwa Majaliwa amesema utekelezaji wa Serikali kuhamia Dodoma unakwenda vizuri ambapo mpaka sasa viongozi wakuu wa wizara zote na wafanyakazi 2,069 wameshahamia Dodoma na wengine wanaendelea kuhamia Dodoma.

Mhe. Majaliwa ameongeza kuwa atasimamia utekelezaji wa maagizo ya Mhe. Rais Magufuli aliyeagiza kujengwa kwa reli itakayounganisha eneo la Bwigili na Dodoma mjini ili kurahisisha usafiri wa watu pamoja na kuharakisha ujenzi wa barabara za kuzunguka mji wa Dodoma na barabara za kuunganisha mji wa Serikali na Dodoma Mjini.

Wakiwa katika eneo hilo, Mhe. Rais Magufuli na Waziri Mkuu Mhe. Majaliwa wameshiriki ufyatuaji wa matofari yatakayotumia katika ujenzi wa majengo ya Ikulu.

Mapema kabla ya kutembelea eneo hilo, Mhe. Rais Magufuli amepokea taarifa ya mapendekezo ya ujenzi wa Mji wa Serikali wa Makao Makuu Dodoma kutoka kwa Mkurugenzi Mkuu wa Mamlaka ya Ustawishaji Makao Makuu Mhandisi Paskasi Muragili na kuagiza ujenzi wa Mji huo uzingatie maslai ya Taifa.

Baada ya Kumtukana Diamond Kupitia Instagram Yake.Harmorapa Ameibuka na Hili Dhidi ya Baba Tiffah..!!!

$
0
0

Harmorapa amemuomba radhi Diamond baada ya akaunti yake ya Instagram kutumika kumtukana hitmaker huyo wa Marry You.

Rapper huyo amepost kipande cha video kwenye mtandao huo akisema kitendo hicho hakufanya yeye bali kuna watu walihack akaunti yake hiyo.

“Followers wangu, mashabiki wangu nasikitika kitu kimoja toka asubuhi leo (jana) nashindwa kuingia katika akaunti yangu,” amesema Harmo kwenye video hiyo.

“Kuna watu wamehack akaunti yangu na kupost vitu ambavyo sio vizuri ni vyaajabu sana. Mimi binafsi siwezi kumtukana Diamond wala kumtukana Alikiba pia na P Funk Majani ambaye nipo naye kwenye mizunguko yangu leo kwa Mx Carter kwa kunisaidia kuirudisha akaunti yangu,” ameongeza.

Simanzi! Maiti ya Mtoto Yafichwa Ndani ya Gari Gereji Dar...!!!

$
0
0

DAR ES SALAAM: Inauma sana jamani! Mtoto Queen Carlos miaka 6 tu aliyekuwa akiishi na mama yake mzazi maaneo ya Vatican Sinza jijini hapa, Machi 13, mwaka huu, maiti yake ilikutwa ndani ya gari bovu lililokuwa gereji kwa matengenezo.

Tukio hilo liliacha simanzi kwa familia, ndugu na majirani baada ya mtoto Queen aliyekuwa akisoma darasa la kwanza katika Shule ya Msingi, Sinza Mihogoni, kubainika amefariki dunia katika mazingira ya kutatanisha.

MAITI ILIVYOKUTWA

Mwili wa marehemu Queen ulikutwa umekuwa umekaa kwenye siti ya nyuma ya gari hilo aina ya Hyundai na kama mtu angemwona kwa mbali, angejua mtoto huyo alikuwa amelala tu na muda wowote angeamka na kurudi nyumbani kwa mama yake!

MADAI ILIVYOKUWA

Mtu mmoja aliliambia Amani kuwa, siku hiyo mmiliki wa gari hilo alikwenda kulichukua gari lake ili kulipeleka sehemu nyingine, hivyo alifuatana na dereva ambaye angekuwa kwenye gari hilo bovu huku mmiliki huyo akiliendesha gari la kuvuta.

“Walipofika, walifunga kamba ya kuvutia, dereva akaingia kwenye gari la kuvutwa lakini alibaini kuwa, anasikia harufu mbaya. Mmiliki akamwambia lazima kuwa na harufu mbaya kwa sababu gari lilikaa muda mrefu pale gereji. Gari lilipotoka nje ya gereji ikaonekana haliwezi kutembea kwenye lami kwa sababu matairi yote hayakuwa na upepo.

“Sasa katika kuangalia nini wafanye kuhusu upepo ndipo yule dereva akaona mwili wa marehemu umekaa siti ya nyuma, akapiga kelele na watu wakafika,” alisema mtu huyo akiomba asitaje jina lake.

MANENO YA MAJIRANI

Kwa mujibu wa mmoja wa majirani aliyejitambulisha kwa jina la Bahati Salum, Queen alitoweka nyumbani kwao Jumapili ya Machi 12, mwaka huu ambapo mama yake mzazi aliyefahamika kwa jina moja la Lilian, akishirikiana na majirani walifanya juhudi za kumtafuta lakini bila mafanikio.

“Queen alitoweka hapa nyumbani Machi 12, mwaka huu. Nakumbuka ilikuwa majira ya saa 4 asubuhi, tulimtafuta sana hatukumpata, tulitoa taarifa Serikali za Mtaa, tukatangaza msikitini lakini hatukumpata.”

TAARIFA YAFIKA POLISI “Mwishowe, tuliamua kwenda kutoa taarifa katika Kituo cha Polisi cha UrafikiUbungo na kupewa RB Na. UPR/RB/2091/2017

TAARIFA.

“Kesho yake kwenye majira ya jioni,  tulimkuta akiwa ndani ya gari bovu ambalo lilikuwa linahamishwa kutoka gereji iliyopo hapa jirani na mwenye gari alishtuka alipomuona mtoto huyu nyuma ya siti akiwa amefariki dunia huku damu zikimtoka puani na usoni. Pia alikuwa  na jeraha kwenye paji la uso kama alipondwa na kitu kizito,” alisema jirani huyo.

MASWALI YA NDUGU NA MAJIRANI

“Inauma sana! Sijui nini kilimpata mtoto huyu? Ila kinachotushangaza sisi ni kuwa  na jeraha kwenye paji lake la uso. Hata kama alifariki dunia kwa kukosa hewa, damu ilitoka wapi sasa? Au inawezekana Queen aliuawa sehemu nyingine na maiti yake kufichwa pale  kwenye gari? “Baada ya kuuona mwili tulikwenda kumtaarifu mwenyekiti wa mtaa ambaye aliwasiliana na Polisi wa Urafiki na kupewa RB Na.  UPR/RB/2100/2017
KIFO CHA MASHAKA.

“Polisi walikuja na kuuchukua mwili wa marehemu na kuupeleka katika Hospitali ya Mwananyamala (jijini Dar kwa ajili ya uchunguzi zaidi ili kujua kichomuua. Lakini pia, mwili wake uliharibika,” alisema jirani mwingine.

MAMA MTU APAGAWA

Kwa upande wa mama mzazi wa mtoto Queen, Lilian alipoona mwili wa mtoto wake, alijikuta akiishiwa nguvu na kupoteza fahamu ambapo, baadhi ya watu walisema ilimchukua karibu saa mbili kuzinduka. Alipokutwa na waandishi wetu, muda mwingi alikuwa akilia huku akisema anamtaka mwanaye.

“Mimi namtaka mwanangu Queen, namtaka mwanangu! Yuko wapi mwanangu Queen”

Lilian alilia kwa uchungu na kuwafanya waandishi wetu pia kutokwa machozi. Mwenyekiti wa Serikali ya Mtaa wa Sinza ‘D’,  Muumin Herezi alikiri kutokea kwa tukio hilo pamoja na maiti ya mtoto huyo kukutwa ndani ya gari gerejini hapo ambapo ametoa ushauri kwa wazazi kuwa makini na malezi ya watoto wao.

BABU WA MAREHEMU AZUNGUMZA NA AMANI

Babu wa marehemu Queen, Frank Moshi aliliambia gazeti hili kuwa, amesikitishwa sana na kifo cha mjukuu wake na kudai familia inafanya mikakati ya mwili wa marehemu kuzikwa katika Makaburi ya Sinza.

RPC KINONDONI AZUNGUMZA Kwa upande wa Kamanda wa Polisi Mkoa wa Kinondoni, ACP Suzana Kaganda alikiri kupata taarifa ya tukio hilo ila kwa muda huo alikuwa kwenye kikao na hakujua nini kilikuwa kinaendelea

Msala...Irene Uwoya Asakwa Kwa Kifo cha Bodaboda...!!!

$
0
0

Ni msala? Nyota wa sinema za Bongo, Irene Uwoya anadaiwa kusakwa na Jeshi la Polisi Mkoa wa Kinondoni ili kutoa maelezo yake kwa kina kufuatia kifo cha kijana Fahari Colos katika ajali ya gari iliyotokea Masaki jijini hapa.

Kwa mujibu wa chanzo kimoja, Uwoya anatakiwa kituoni hapo kwa vile, kifo cha Fahari kina utata wa simulizi kutoka kwa ndugu na kwa askari polisi waliokuwepo kwenye eneo la ajali.

Fahari alifariki dunia Machi 12, mwaka huu kwenye Hospitali ya Taifa Muhimbili kufuatia ajali hiyo mbaya aliyoipata siku hiyohiyo. “Kama umesoma mitandaoni utakuwa umeona kuhusu ajali ya yule dereva wa bodaboda, sasa Irene Uwoya ana sehemu kubwa ya maelezo kutokana na ajali mpaka kifo cha yule kijana.

“Tumekuwa tukimtafuta kuanzia siku ya tukio lengo letu aje kituoni atoe maelezo maana na yeye ana sehemu ya maelezo muhimu. Lakini kama amezima simu au sijui ameiseti kiaina,” alisema afande mmoja na kutaka kusitiriwa kwa jina lake.

Amani juzi lilimtafuta Uwoya mwenyewe na kumuuliza kuhusu madai ya kutafutwa na polisi ambapo alisema:

“Mimi niko tayari kwenda kutoa meleozo yangu polisi, tena nitayatoa kwa uzuri sana. Kama wananitafuta safi sana.”

Kuhusu simulizi ya tukio hilo, Uwoya alisema:

“Machi 12, usiku nikiwa naelekea Masaki, kufika Colosseum Hoteli nilikuta ajali mbaya sana. Nilimkuta mkaka mmoja kagongwa na gari, yeye alikuwa na pikipiki.

“Nikasimama pale nikakuta polisi wapo na gari lao na ndiyo kwanza wanapiga stori tu, hawana habari watu wanaomba msaada.

“Niliwauliza polisi kwa nini mtu anakufa wanamuangalia tu? Wakajibu wao wafanyaje wakati hakuna gari la kumbeba! Nikawaambia gari lenu si hilo hapo? Wakasema haliwezi kumbeba, basi nikawaambia watu wampakie kwenye gari langu ili nimkimbize hospitali.

“Ile nataka kuondoka tu, wakaniambia nikachukue PF3 kwanza halafu niende hospitali, nikawaambia mtu anakufa nyie mnasema nikafuate PF3? Mimi sifuati PF 3, wakaniambia watapiga simu hospitali wasimpokee.

“Tukaenda na baadhi ya watu mpaka Hospitali ya Mwananyamala, kufika akapokelewa na tulikuta watu wa ajali wawili wamekaa karibu saa nzima.

“Niliumia sana! Tukaandikiwa vitu vya kununua kwa ajili ya majeruhi, kwenda nje hakukuwa na dawa, tukapata baadhi ya vifaa wakaanza kumhudumia! Baada ya muda difenda ikaja ikamchukua dereva wangu eti alikuwa anapiga kelele na kutukana wakati tulikuwa tunapiga kelele wamhudumie mgonjwa.

“Baada ya muda ndugu zake majeruhi wakajitokeza, mgonjwa akahamishiwa Muhimbili. Mimi nikamfuata dereva wangu. Kabla Sijafika kituoni akanipigia simu kwamba wamemuachia.

“Jana asubuhi (Machi 13) napiga simu kwa ndugu wa mgonjwa naaambiwa amefariki dunia. Niliumia sana kwa kweli. Sasa kama wanasema wananitafuta askari ili wanihoji sawa tu mimi nipo sana, nimejaa tele.”

Juzi, Amani lilimpigia simu Kamanda wa Polisi Mkoa wa Kinondoni, ACP Suzana Kaganda ili kumsikia anasemaje kuhusu kuwepo kwa madai hayo, lakini simu iliita kwa muda mrefu bila kupokelewa

Penzi la Lulu, Majizzo Chalii..!!!

$
0
0

Lile penzi mubashara kati ya staa wa filamu nchini, Lulu Michael na Mkurugenzi wa E-fm maarufu kama Majizo, linadaiwa kuingia kidudu mtu.

Za kunyapia nyapia zinadai eti bibie huyo anatuhumiwa kujihusisha na imani za kishirikina. Hata hivyo chanzo kamili cha wawili hao kuwa katika hali ya sintofahamu bado hakijajulikana ila wawili hao sasa hivi hawakai zizi moja kama zamani.

Je Ni Kweli Wanawake Wakipenda Huwa Wanakuwa Wanapenda Kweli...!!!!?

$
0
0

KARIBUNI wasomaji wangu katika safu hii ya mahusiano ambayo huwajia kila siku ikilenga kufahamishana hili au lile kuhusiana na mambo ya mapenzi au ukipenda unaweza kuita mahaba.

Awali ya yote, niwashukuru wale wote ambao wamekuwa wakitumia muda na fedha zao kutuma ujumbe wenye lengo la kupongeza mada zinazotolewa katika safu hii, huku wengine wakichangia pale walipoona inafaa kufanya hivyo. Nasema asanteni sana.

Baada ya salamu hizo, tugeukie mada ya leo. Katika mada zilizopita kuhusiana na suala zima la kupenda, wasomaji wangu wamekuwa wakichangia kwa mitazamo tofauti, huku wengi wakionekana kutofautiana kwa misingi ya kijinsia.

Mathalani, katika mada zilizohusisha suala zima la usaliti katika mapenzi na dhana nzima ya kupenda, kumetokea mabishano makali kuwa kati ya wanawake na wanaume, wanawake ndio ambao wamekuwa wakiwapenda wenzao wao kwa dhati kuliko ilivyo kwa wanaume.

Lakini pia, wapo wanaume waliokuwa wakisisitiza kuwa wanawake ndio vigeugeu katika suala zima la mapenzi kwani wengi wao si waaminifu hasa pale wanapokutana na vishawishi vya fedha, magari na nyumba za kifahari, kazi nzuri na mengineyo kama hayo.

Hao wanadai kuwa hata mwanamke umwonyeshe upendo kiasi gani, akikutana na mwanamume mwenye fedha chafu atakayemhakikishia kuishi katika nyumba ya kifahari, kutembelea gari la kifahari na mengine kama hayo, lazima atamsaliti mume au mpenzi wake.

Lakini kwa wanaume, imedaiwa kuwa wao hawatabiriki, wanaweza kuonyeshwa kila aina ya upendo na wake au wapenzi wao, lakini bado wakaendelea kujihusisha kimapenzi na wasichana wengineo, hasa wale wenye mvuto wa kisura na kimaumbile.

Kwa kifupi, wanaume wamelalamikiwa na wanawake kwa tabia zao za kutoridhika na walivyonavyo, wakitamani kila wakionacho mbele yao yaani kila mwanamke anayepita mbele yao hutamani ‘kumvua nguo’.

Lakini kwa mujibu wa tafiti mbalimbali, inadaiwa kuwa wanawake ndio wenye mapenzi ya kweli kiasi kwamba wanapowapenda wanaume, huwapenda kweli kweli.

Lakini pia, wapo wanaosisitiza kuwa wanaume ndio wenye mapenzi ya dhati kiasi kwamba wanapopenda hupenda kweli na si maigizo kama ilivyo kwa wanawake.

Naamini mada ya leo itakuwa imewagusa wengi hivyo nitoe nafasi kwenu wasomaji wangu kutoa maoni yenu kabla ya kuwaletea ukweli juu ya mada hii kutokana na tafiti mbalimbali zilizofanywa na wataalamu wa mambo ya mahusiano. Maoni yenu nitayatoa katika toleo la Jumamosi hii.

Lakini hebu niwape kibwagizo cha mada ya leo kutoka kwake Michael Bolton, mmoja wa waimbaji mahiri wa nyimbo za kimapenzi wa Marekani aliyejizolea sifa na tuzo kede kede.

Bolton, katika wimbo wake wa When A Man Loves A Woman, anaelezea jinsi inavyokuwa pale mwanamume anapompenda mwanamke. Pata uhondo wa kibao hicho matata.

U-Heard-: Mapovu ya Lulu Kuhusu Kunyang’anywa Bwana na Hamisa Mobetto...!!!

$
0
0

Moja kati ya story kubwa sana ambazo zimekiki week hii ni pamoja na hii ya muigizaji Elizabeth Michael (Lulu) kusemekana kupigwa kibuti na aliyekuwa mpenzi wake.

Mpenzi ambaye hapo awali alikuwa akitoka kimapenzi na mwanamitindo Hamisa Mobetto na taarifa zinasema walifanikiwa kupata mtoto.

Kuna sauti ambayo inasambaa katika mitandao ya kijamii ikielezea ubuyu mzima kuhusu Lulu kuachwa na mwanaume huyo na kusemekana kwamba mwanaume huyo amerudi kwa mwanamke wake wa zamani ambaye ni Hamisa Mobetto. Kama hujaisanukia bonyeza play kwqenye video hii hapa chini kusikiliza mwanzo hadi mwisho.
Soudy Brow aliamua kumvutia waya Lulu na kumtaka alizungumzie suala hilo, ndipo Soudy Brown alipokutana na mapovu mazito kutoka kwa mrembo huyo. Uhondo kamili nimekuwekea kwenye video hii unaweza kuitazama kwa kubonyeza play hapa chini.


Mapenzi Haya Khaa....! Nimeenda Kwetu Kujifungua Kurudi Namkuta na Mwanamke Mwingine..!!!

$
0
0

Naomba ushauri, 

Nina mume nipo naye mwaka wa nne na tumepata mtoto mmoja wa kiume, lakini cha kushangaza nilipojifungua nimeenda kwetu kurudi nakuta anamwanamke mwingine na bila kujua kumbe kabla yangu anamtoto mwingine. 

Nilipomuuliza alisema walishindwana kisa dini, baada ya hapo ndo kanipata mimi lakini baada ya kurudi nyumbani naona anamwanamke mwingine tena kamzidi umri, nikimuuliza ananipiga, kumbe yule mwanamke anamimba na ninavyoongea sasahivi ameshajifungua mtoto.

Nilipojua inauma sana na kumpeleka kwa ndugu zake akatubu kweli mtoto wake akasema alipitiwa lakini cha ajabu bado anaendelea na huyo mwanamke
ukimuuliza anasema mtoto anaumwa nilienda kumwona.

Huwa ananiaga anaenda kanisani kumbe anaenda kwa huyo mwanamke alafu anataka mtoto akikuwa aniletee mimi wote nyumbani. Jamani naumia sana na sijawahi kumsaliti na natimiza kazi zangu zote kama mke.

Naombeni ushauri jamani maana hali tete.
Viewing all 104694 articles
Browse latest View live




Latest Images