Quantcast
Channel: UDAKU SPECIAL
Viewing all 104780 articles
Browse latest View live

Alikiba Kuweka Muziki Wake Wasafi.com ni Sawa na Safari ya Mwezini..!!

$
0
0

Kwa takribani miaka mitatu sasa mafahari wawili wa muziki wa kizazi kipya yaani Bongo Flava Alikiba na Diamond Platinumz wamekuwa katika bifu zito sana, licha ya wao kujaribu kila siku kuukwepa ukweli huo. Hakuna kati yao ambaye amewahi kujitokeza hadharani na kukiri uhasama kati yao lakini ni wazi kuwa watu hawa hawapikiki chungu kimoja.

Mara kwa mara watu wa karibu wa Diamond wakiwemo watu walio kwenye management yake hususan, mameneja Sallam na Ricardo Momo, wamekuwa wakimtupia vijembe Alikiba. “Wao wakipost tembo, sisi tunapost show” na “waambie dada zao Kariakoo waje Ulaya” ni baadhi tu ya mistari ambayo Diamond amewahi kusikika akiimba ikiwa ni kuelekeza mashambulizi upande wa Alikiba na kambi yake.

Hivi karibuni Diamond akiwa kwenye Interview ya kipindi cha 360 cha Clouds FM, alikaririwa akisema kuwa hana tatizo na Alikiba, ni mtu anayeheshimiana naye na hata uongozi wake uko katika mazungumzo na uongozi wa Alikiba ili Kiba aweze kuuza nyimbo zake kwenye mtandao wa wasafidotcom ambao ni mradi mpya wa Diamond.

Baadaye usiku kupitia akaunti yake ya Instagram Alikiba aliandika caption zenye utata zilizotafsiriwa na mashabiki na wadau mbalimbali kuwa zimelenga kujibu maneno hayo ya Diamond Platnumz.

Wamarekani wana sera zao mbili ambazo wanazitumia sana katika kulifanya taifa lao kuendelea kuwa taifa kubwa duniani. Sera ya kwanza; njia pekee ya kumshinda adui ni kumfanya rafiki, ya pili; wamarekani hawahitaji rafiki dhati wala adui kweli, zaidi ni kutimiza interest zao.

Hivyo watakufanya rafiki ili wapate watakacho na utarudi kuwa adui wakishatimiza azma yao. Lakini Waingereza pia wanasema numbers don’t lie. Nimejaribu kufuatilia rekodi za nyuma za Alikiba katika mtandao wa mkito.com nikagundua kuwa Alikiba ni record breaker. Mwana iliweka rekodi, Chekecha Cheketua iliweka rekodi. Hata nyimbo ya Nisamehe aliyoshirikishwa na Barakah Da Prince pamoja na nyimbo ya Kajiandae aliyoshirikishwa na Ommy Dimpoz zimeingia kwenye Top 5 ya ngoma zilizopakuliwa zaidi kwenye mtandao wa Mkito mwaka 2016.

Kwa rekodu hizi ni dhahiri Diamond anahitaji amani na Alikiba kwasababu za kibiashara zaidi. Anatambua fan base aliyonayo Alikiba itabust zaidi mtandao wake, pesa atakayopata ni kubwa, pia number of visitors itaongezeka kwa kasi kwani kila mtu atataka kuamini ni kweli Ali yumo? Haikushangaza kuona editing kwenye mitandao ikionesha kua profile ya Alikiba ipo kwenye wasafidotcom.

Kwa hali ilivyo sioni na sidhani kama management ya Alikiba itaweza kukubali kuuza nyimbo kwenye mtandao wa Diamond. Kwanza wanajiamini sababu wameshauza kabla na kuweza kuweka baadhi ya rekodi kwenye mtandao wa Mkito. Pili kutoka kwa mfululizo wa mashambulizi ya maneno kutoka kwa Dimond na management yake kwenda kwa Alikiba itakuwa ni fedheha kubwa kwa mashabiki wa Ali kama Ali na uongozi wake utakubaliana na suala hili. Na ndio maana nasema sera za kimarekani za Dimond zimedunda kwa Alikiba

Hatarii..Muuguzi Achomwa Moto Hadi Kufa kwa Kumpa Huduma Mbovu Mgonjwa...!!!!

$
0
0

Muuguzi mmoja nchini Israel amefariki baada ya kuchomwa akiwa hai na mgonjwa katika eneo la Holon kusini mwa Tel aviv.

Tova Kararo mwenye umri wa miaka 56 alimwagiwa mafuta na kuchomwa baada ya kujibizana na mgonjwa ambaye alikuwa hajaridhika kulingana na afisa mmoja wa polisi.

Mshukiwa huyo ambaye yuko katika umri wa miaka 70 alitoroka eneo la mkasa huo kwa kutumia gari lakini akakamatwa baadaye.

Vyombo vingi vya habari nchini Israel vimeripoti kwamba mshukiwa huyo alikuwa manusura wa holocaust anayeugua ugonjwa wa akili.

Mkuu wa polisi katika eneo hilo Sigal Bar Tzvi alisema kuwa mtu huyo aliwasili katika kituo hicho cha afya na alidaiwa kwamba hakuridhishwa na matibabu aliyopata.

Fahamu Maajabu ya Nanasi Ambayo Yatakuacha Kinywa Wazi..!!!

$
0
0

BAADHI ya watu wamekuwa wakidai tunda la nanasi kuwa siyo salama kwa akina mama wajawazito, ingawa suala hili bado halijathibitishwa kitaalamu, kwani wapo wanaokula na haijawahi kuripotiwa madhara. Linatumika kama tunda ama juisi na lina faida mbalimbali kwa afya ya mwanadamu.

BAADHI YA FAIDA HIZO NI PAMOJA NA:

Lina vitamini A, B na C, madini ya chuma, calcium, copper na phosphorous ambayo yote ni muhimu sana katika afya ya mwanadamu.Tunda hili husaidia kutengeneza damu, kuimarisha mifupa , meno, neva na misuli (muscles).

Hutibu matatizo ya tumbo, bandama na ini, husaidia kusafisha utumbo mwembamba, hutibu homa, vidonda mdomoni, magonjwa ya koo, hutibu tatizo la kupoteza kumbukumbu, hutibu kikohozi, kutetemeka na uoga (Anxiety). Leo nimeandika tiba ya nanasi kwa sababu ni mjadala mkubwa ulioibuka kuwa tunda hili lina madhara, lakini nikuhakikishie msomaji hakuna madhara ya kukufanya

Usijipe Presha, Kama Unampenda Muamini Kisha Ziba Masikio!

$
0
0

ili uweze kudumu katika uhusiano wako unatakiwa kujenga mazingira ya kumuamini sana mpenzi wako. Nasema hivyo kwa kuwa, mapenzi ni imani. Ni sawa na kuamini Mungu yupo licha ya kwamba hujawahi kumuona.

Vivyo hivyo, amini tu kwamba mpenzi wako anakupenda kwa dhati licha ya kwamba hujaufungua moyo wake na kathibitisha kwamba ndani yake uko wewe peke yako.


Mpende, muamini na weka akilini mwako kwamba, kamwe hawezi kukusaliti licha ya kwamba kinyume chake pia ni sawa. Hiyo itakusaidia wewe kuendelea kuishi maisha ya furaha na amani bila kuwa na presha.

Jiulize, ni wanaume wangapi ambao wake zao wanagawa penzi nje ya ndoa lakini wao wanawaamini kupita maelezo?

Ni wanawake wangapi ambao waume zao ni viwembe kwelikweli lakini wanawaamini kupindukia? Unadhani ni kwa nini?

Ni kwa sababu wamejijengea mazingira ya kuwaamini wenzao wao wa kiwango kikubwa na kuziba masikio yao kukwepa wambeya.

Tutambue tu kwamba, katika maisha kuna kitu kuridhika. Unapokuwa na mtu ambaye anakupa kila aina ya furaha maishani mwako bila kuonesha tabia zozote zinazokutia mashaka juu ya penzi lake, huyo mpende, mheshimu na muamini.

Hata kama kuna uwezekano wa yeye kuwa anaficha makucha yake na kuyachomoa pale anapokuwa mbali na wewe, kwa sababu huna uhakika na hujawahi kumuona, chukulia kwamba yeye ni msafi kisha yaache maisha yenu yaendelee kuwepo.

Nasema hivyo kwa sababu, tukianza kuchunguzana hakuna ambaye ni msafi kwa asilimia mia moja. 

Kila mtu anajiamini mwenyewe lakini huwezi kuiamini nafsi ya mwenzako kwa asilimia zote.
Ndiyo maana nikasema, unapoingia katika uhusiano na mtu ambaye umetokea kumpenda sana, ongea na moyo wako. 

Moyo wako ndiyo utakueleza kama mpenzi wako ni muaminifu ama siyo na pindi utakapoona dalili za kwamba ni tapeli wa mapenzi mwenye lengo la kutaka kukuchezea kisha kukuacha solemba, usimng’ang’anie eti tu kwa sababu umeoza kwake, muache!

Tatizo tulilonalo wengi ni kutokuwa tayari kuwakosa wale ambao tumetokea kuwapenda sana bila kujua kwamba unaweza kutokea kumpenda mtu lakini yeye akawa hana mapenzi ya dhati moyoni mwake dhidi yako.

Ifike wakati tukubaliane na uhalisia kwamba, unapoona uliyenaye anakuzingua, yupo mwingine mwenye penzi la dhati kwako ambaye anasubiri umuache huyo uliyenaye ili awekeze penzi lake kwako.

Kwa kumalizia naomba niseme kwamba, mapenzi ya siku hizi usipoangalia yanaweza kukufanya ukawa chizi. 

Hii ndiyo inayosababisha baadhi ya watu kufikia hatua ya kusema kwamba, hawahitaji kuwa na wapenzi katika maisha yao. Kwa nini? Kwa sababu kila uhusiano wanaoingia wanakutana na usanii.

Elewa kwamba, una haki ya kupenda na kupendwa, ukishampata yule unayedhani atayafanya maisha yako kuwa ya furaha, mpende kwa dhati na muamini kwamba hawezi kukusaliti lakini, wakati huo hutakiwi kubweteka, chunguza nyendo zake na kama utabaini kwamba anajiheshimu, ongeza mapenzi kwake lakini kama utabaini kuwa hajatulia, muache.

Hakuna Nishani ya Ndoa, Jipange Kwanza na Epuka Presha za Watu, Wengi Wanalia Moyoni, Ningejua...!!

$
0
0

Nianze kwa kusema ndoa ni kitu chema na inapaswa kuwa sehemu ya amani na sio maradhi wala vita.

Kumekuwa na kitabia kinachokera sana, kila mtu akiona bao hujaoa au kuolewa utasikia unasubiri nini utazeeka, au sijui utaitwa babu au vinginevyo

Ndio sio kitu cha kukimbilia, kitu cha kuiga wala cha kuonyesha watu. usimshangae mtu ukikuta hajaolewa au kuoa kwa muda unaotaka wewe au unaodhani wewe ni sahihi. epuka kumpa mtu presha za ndoa kwa sababu wewe uko huko.

Wengi walio kwenye ndoa wanayajua sana sana waliokurupuka. siri ya wanachokipata wanayo wenyewe. usimshangae mtu akifika miaka 30 hajaoa, ana mipango yake.

Ndoa sio kitu cha kujaribu wa kuiga. ingia kwenye ndoa ukiwa na wito, utayari wa mwili na akili na pia utayariwa uchumi ikiwa kulea matumbo zaidi ya matano mwaka mzima bila kukosa kitu.

Hakuna nishani ya ndoa, kwamba ukikimbilia na kuwahikuoa mapema utapata. ndoa ni kitu cha maelewano ya watu wawili yaani mwanaume na mwanamke ambao wanaona wanaweza kuishi pamoja kwa kusaidia na kuheshimia na kukidhiana tamaa.

Tusipende kuishi kwa mikumbo na pia tusipende kuwalazimisha watu waishi kwa mitizamo yetu au experience zetu. usipende kuwauliza uliza watu kuoa. 

Kama mwanaume yuko kamili hawezi kuuambiwa aoe muda fulani wakati yeye mwenyewe anajielewa.

Pia kwa wadada, ndoa inatakiwa kuwa sehemu ya maelewano na amani, usiolewa sababu ya umri umeenda, kama yupo wako atakuja tu. 

Ukikurupuka kama unakufa kesho utapata jipu uchungu likusumbue mpaka upate kisukaru na mapresha alafu ufe taratibu kwa mateso makali.

Maisha ni jinsi unavyojipanga. Lazima ujipange na kitu cha muhimu kwenye maisha haya ni kifurahia kila siku ukiwa hai.

Usikubali kuishi kwa kunyanyasika sababu ya umri. ishi kwa furaha maana maisha ni mafupi na ukifa hamna maisha tena. Ishi kwa kufurahia kila siku Mungu anayokupa ili uishi vizuri.

Kama Huwezi Kuachana Naye Usijaribu Kuchungulia Mawasiliano Yake....!!!

$
0
0

Kuna siku nilijifanya Mjuaji nikadukua mawasiliano ya mchepuko wangu niliyokutana nayo huko sasa ni hatari tupu, sms ya kwanza kuingia jamaa anampongeza kwa shughuli yao ya jana kuja huku whatsaap shughuli nzito nikajikuta naumwa ghafla pressure inanipanda mara nikaona dunia inazunguka mara nataka kuaga dunia ikabidi majirani zangu wafanye mawasiliano na mchepuko wangu maana walikuwa wanaufahamu ile unakuja home. baby jamani unaumwa nn? aiseeeh nikiuangalia homa inanizidia nikifikiria kuucha siwezi.............kilichoendelea.....................ila mpaka sasa nadunda nao course niliona bora tu nijikaze 

Vijana Tuache tabia ya kudukua mawasiliano ya tunaowapenda wakati jeuri za kuwaacha hatunazo, huo ni ushauri tu kama jasiri endelea kupanga mikakati ya kudukua mawasiliano ya mke au mchumba ako soon tu itabaki story

Jinsi ya Kuishi na Mwanamke Asikuloge au Kukupa Limbwata..!!!

$
0
0

Nipo tena kwa Mara nyingine katika kubadilishana uzoefu juu ya mambo mbalimbali yanayohusu mahusiano,kuna jambo limekuwa likiniumiza kichwa sana ni swala zima la kulogwa au kupewa limbwata na mwanamke.

Nidhahiri kabisa mambo haya katika jamii yetu yanafanyika kwa baadhi ya wanawake huwa wanawafanyia wanaume,na tatizo hilo limezidi kushamiri zaidi kutokana na ongezeko kubwa la waganga wa kienyeji.

Nimefanya research kwa baadhi ya waganga wameniambia wateja wao wakubwa ni wanawake na shida kubwa wanayokuwa wanahitaji ni kuolewa au kuwadhibiti wanaume zao.

Nami mekuja kugundua wanaume wengi huwa wanafanyiwa madawa ila wakati mwengine mungu huwalinda hawazuriki bila ya wao kujua na wanaume wengi ambao wapo katika hatari hiyo ni wale wenye kipato kidogo ambacho kinarizisha.

Sasa basi nimejaribu kutafuta prevention za ki psychology, ambanzo hazihusiani na mambo ya kishirikina ambazo zinaweza kukusaidia uepukane na janga hilo nimejaribu kutumia experience yangu ni kama zifuatazo:

Kwanza kabisa kama mwanaume unapoanza mahusiano ya kimapenzi na mwanamke unatakiwa umwambie mwanamke vitu ambavyo huvipendi na moja katika ya vitu ambavyo utamwambia hupendi ni mambo ya kishirikina na unatakiwa umsisitizie kwamba endapo kama wewe utagundua yeye anapenda mambo ya kwenda kwa waganga umwambie siku hiyo ndio itakuwa mwisho wa mapenzi yenu.

Jambo la pili ukiwa unaishi na mwanamke ndani usipende kula chakula peke yako hata kama umechelewa kurudi umerudi labda saa sita usiku mwambie mke wako mle wote chakula cause peke yako hujazoea kula au kama mna mtoto wenu ama ndugu wa mwanamke kula nae chakula.

Kwa kufanya hivyo mwanamke atajua hupendi kula peke yako na unampenda yeye na ndugu zake kumbe unalako moyoni unajilinda na limbwata,jambo la tatu pendelea kufanya ibada ukitaka kula na ukitaka kulala na mshirikishe mkeo katika ibada na wakati mwingine msomee maandiko ya vitabu vya mungu ambayo yanakataza ushirikina na adhabu zake watakazo zipata wanaofanya mambo hayo,mengine mnaweza mkaongezea.

Note:Mwanamke anaweza akawa sio mshirikina lakini akashawishiwa na marafiki zake akufanyie hivyo,kwa hiyo kama mwanaume ni bora ukachukua tahadhari mapema.

Laurence Masha Ajitoa Kugombea Urais TLS, Amuunga Mkono Tundu Lissu

$
0
0
Mgombea Urais wa Chama cha Wanasheria nchini (TLS) Ndg. Laurence Masha amejitoa kwenye kinyang'anyiro hicho kwa hoja kuwa anaamini uwezo wa Lissu katika kuiongoza TLS.

Amewaomba mawakili wote waliopanga kumpigia kura wampigie Tundu Lissu.

Ndoto za Mbwana Samatta Kucheza na Mau United Zawekwa Pending

$
0
0

Ndoto za mshambuliaji wa timu ya KRC Genk ya Ubelgiji Mtanzania Mbwana Samatta za kukanyaga katika dimba la Old Trafford la Manchester United zimesubirishwa baada ya matokeo ya droo ya robo fainali kombe la Europa kwenda kinyume na matamanio yake.

Hamu ya Nahodha huyo wa Taifa Stars ilikuwa ni kuona timu yake ya Genk inapangwa kukutana na Man United katika hatua ya robo fainali ya michuano hiyo, ili atimize ndoto yake mojawapo ya kucheza katika uwanja wa huo maarufu na uliotoa mastaa wengi duniani.

Samatta baada ya mchezo wa kwanza wa hatua ya 16 bora ambao timu yake iliibuka na ushindi wa 5-2 na kutoa nafasi kubwa ya kufuzu robo fainali, alinukuliwa akisema "Moja kati ya ndoto zangu ni kukanyaga katika dimba la Old Trafford, kwahiyo naomba kila siku timu yetu ikivuka, ipangwe na Manchester United"

Hata hivyo, katika droo iliyochezeshwa leo, KRC Genk imepangwa kuanzia nchini Hispania dhidi ya Celta Vigo, na mchezo wa marudiano utapigwa nchini Ubelgiji.

Ili timu hiyo ikutane na Man United msimu huu, inapaswa kwanza kuitoa Celta Vigo, huku ikiomba Man UNited pia ifuzu nusu fainali, halafu droo iwakutanishe.

Kutokana na ukweli kwamba timu ya Man United ndiyo yenye mashabiki wengi zaidi duniani, ingeweza kuwa ni fursa adhimu kwa Samatta kujitangaza zaidi, kwa kuwa watu wengi hawapitwi kutazama mchezo wowote unaoihusu timu hiyo iliyo chii ya kocha Jose Mourinho

Polisi Wadaiwa Kumsaka Mange Kimambi. Latolewa Agizo la Siri Kwa Vituo Akionekana Akamatwe!

$
0
0
Katika hali inayoonesha kuwa taarifa zinavuja kwa kasi na ishara kuwa Mange anakubalika kwa watu wengi hata ndani ya system, Jana Mange amepost waraka anaodai kutumiwa na mtu toka ndani ya system.

Waraka huo ulioandikwa siri unaelekeza baadhi ya maofisa wa mikoani kutoa taarifa haraka iwezekanavyo kwa vyombo husika pindi atakapoonekana maeneo ya mipakani ili akamatwe na kujibu kesi zinazomkabili....

Mange Kimambi amekuwa mstari wa mbele kuikosoa serikali hii na mambo mbali mbali katika jamii....

VIDEO:Magufuli Amdiss Kistaili Wema Sepetu Kuhamia CHADEMA

$
0
0
Magufuli akiwakaribisha wasanii kwenye mkutano wa CCM Dodoma aliwasifu kuwa ni wasanii wazuri na sio kama yule mwingine aliyehamia upande wa pili Tazama Video:

Msemaji wa Jeshi la Polisi Uganda Auawa kwa Kupigwa Risasi..!!!.

$
0
0

Msemaji wa jeshi la polisi nchini Uganda Felix Kaweesi amepigwa risasi na kuuawa na watu wasiojulikana. Taarifa zinasema Bw Kaweesi ameuawa baada ya gari lake kumiminiwa risasi na watu wasiojulikana alipokuwa anaondoka kwake nyumbani Kulambiro, Kisaasi kaskazini mashariki mwa mji mkuu Kampala.

Walinzi wake wawili walioandamana naye pia wameuawa.

Bw Kaweesi aliteuliwa kuwa msemaji wa polisi Agosti mwaka jana.

Taarifa zinasema alikuwa njiani kwenda kuwahutubia wanafunzi katika chuo kikuu cha Uganda Christian University alipokumbana na mauti yake. Wanafunzi walikuwa tayari wamekusanyika ukumbini katika chuo hicho.

Miili ya watatu hao imepelekwa katika chumba cha kuhifadhia maiti cha hospitali ya Mulago.

Yaliyotokea Dodoma ni Ishara Magufuli Amepania Kuisafisha CCM..!!!!

$
0
0


MAJUZI, Chama Cha Mapinduzi (CCM) kilifanya Mkutano wake Mkuu Maalum huko Dodoma, ambao pamoja na mambo mengine ulikuwa na ajenda kuu ya "kujadili na kupitisha marekebisho ya Katiba ya CCM ya mwaka 1977 Toleo la 2012, pamoja na kanuni za chama hicho na jumuiya zake."

Nimeyawekea msisitizo maneno "kujadili na kupitisha" kwa sababu inaonekana kuwa wazi kuwa majadiliano yaliyofanyika hayakupaswa kutoyapitisha marekebisho hayo.

Ni rahisi kutafsiri hatua hiyo kama ya kuminya demokrasia (kwa maana kwamba kujadili pekee hakutoshi bali pia kuwepo uhuru wa kuyakubali au kuyakataa mapendekezo husika) lakini pengine ni rahisi pia kutambua kwanini CCM "ilijihami" mapema.

Mabadiliko hayo ya katiba ya chama hicho yamepelekea kupungua idadi ya wajumbe wa vikao vya ngazi za juu vya chama hicho na kupunguza 'kofia mbili' kwa viongozi wenye vyeo ndani ya chama, serikalini au bungeni.

Kutokana na mabadiliko hayo, mwanachama anatakiwa kushika nafasi moja tu ya uongozi, katika ngazi za Mwenyekiti wa Tawi, Kijiji, Mtaa, Kata, Wadi, Jimbo, Wilaya na Mkoa. Wengine ni Makatibu wa Halmashauri Kuu wa ngazi zote, Diwani na Mbunge/Mwakilishi.

Kwa hiyo ni wazi kuwa mabadiliko hayo yanawaathiri 'vigogo' kadhaa wa chama hicho, na pengine ndio maana ikaamuliwa kuwe na "mjadala na kupitisha mabadiliko hayo" badala ya "mjadala na kupitisha au kutopitisha mabadiliko husika."

Kadhalika, mabadiliko hayo yatapelekea kupungua kwa idadi ya wajumbe wa Kamati Kuu ya chama hicho, kutoka 34 hadi 24.

Vilevile, idadi ya wajumbe wa Halmashauri Kuu ya chama hicho imepungua zaidi ya nusu, kutoka 388 hadi 168.

Miongoni mwa 'vigogo' waliotarajiwa kuathiriwa na mabadiliko hayo kutokana na kushika nyadhifa zaidi ya moja ni pamoja na William Lukuvi, Makame Mbarawa, Dk. Hussein Mwinyi, na Shamsi Vuai Nahodha.

'Kigogo' mwingine ni Mama Salma Kikwete, ambaye licha ya kuwa mjumbe wa NEC wa Mkoa wa Lindi, hivi karibuni aliteuliwa na Rais  Magufuli kuwa Mbunge wa Bunge la Jamhuri.

Wengine ni wenyeviti wa CCM mikoa ambao pia ni wabunge, kama vile Joseph Musukuma, Martha Mlata na Deo Simba, ilhali Godfrey Zambi ni mbunge na mkuu wa mkoa, Adam Kimbisa ni Mjumbe wa Kamati Kuu na Mwenyekiti wa CCM Mkoa wa Dodoma.

Kuna usemi mmoja, kwamba sio kila kitu sahihi ni kizuri, na sio kila kitu kizuri ni sahihi. Uamuzi wa CCM kuwapunguzia wanachama wake kofia zaidi ya moja kwenye uongozi ni sahihi lakini sio mzuri kwa watakaoathiriwa nao.

Jicho la uchambuzi litaelekezwa kwa 'wahanga' hao kadri chama hicho kinavyoingia kwenye mchakato wake wa uchaguzi mkuu baadaye mwaka huu, na kwenye kinyang'anyiro cha urais kupitia CCM katika uchaguzi mkuu ujao, mwaka 2020.

Siku moja kabla ya Mkutano huo Mkuu Maalum, chama hicho tawala kilitangaza adhabu kwa viongozi wake kadhaa, kubwa zaidi ikiwa kuwavua uanachama viongozi 12 akiwemo Sophia Simba, kada mkongwe wa chama hicho na ambaye hadi anapewa adhabu hiyo alikuwa Mwenyekiti wa Taifa wa jumuiya ya wanawake wa CCM (UWT), mjumbe wa Kamati Kuu na Mbunge.

Hatua hizo kali zilizochukuliwa na CCM chini ya uenyekiti wa Rais Magufuli, sambamba na mabadiliko niliyoyaongelea awali, yana tafsiri kuu mbili.

Kwanza, hatua kali za kinidhamu zinapeleka ujumbe kwa wana-CCM wa kada mbalimbali kuwa Rais Magufuli amepania kwa dhati kukisafisha chama hicho tawala.

Pili, mabadiliko kusudiwa, sambamba na hatua kali zilizochukuliwa dhidi ya viongozi kadhaa wa chama hicho, ni mtihani mkubwa, kwa Mwenyekiti Magufuli na CCM kwa ujumla.

Kwa Mwenyekiti Magufuli, hatua hizo zimemwongezea idadi ya maadui zaidi ya wale ambao tayari ni waathirika wa msimamo wake dhidi ya ufisadi na rushwa, ambapo watendaji kadhaa wa serikali wametumbuliwa huku wakwepa kodi wakidhibitiwa, na majangili na 'wauza unga' wakibanwa.

Japo ni mapema mno kufanya tathmini timilifu kwa hatua hizo, ile kuzichukua tu sio tu kwaonyesha dhamira lakini pia ni wazi zimetengeneza maadui wa kutosha dhidi ya Dk. Magufuli.

Katika hili, ni muhimu kutambua kuwa ni bora kuwa na kiongozi atakayechukiwa na kwa kutenda vitu sahihi kuliko atakayependwa kwa kufanya madudu.

Siku moja kabla ya Mkutano huo Mkuu Maalum zilipatikana taarifa za kukamatwa kwa makada watatu wa chama hicho, Msukuma, Hussein Bashe na Adam Malima.

Kilichonisikitisha ni maelezo kuwa "walikamatwa na kuhojiwa na polisi kwa tuhuma za kupanga njama za kuvuruga Mkutano Mkuu Maalum wa CCM."

Katika mazingira ya kawaida, sio rahisi kwa makada hao watatu kupanga kuvuruga mkutano mkubwa kama huo ila yayumkinika kuhisi kuwa kilichofanyika ni kuzuwia kile nilichogusia awali, yaani "sio kujadili na kupitisha tu mabadiliko husika" bali pia "kujadili na kupitisha au kutopitisha mabadiliko hayo."

Hili la kuminya fursa ya upinzani kwa mabadiliko hayo linaweza kuwa na athari kwa chama hicho huko mbeleni. Sauti za manung'uniko ni kitu cha kawaida lakini sauti hizo zikiakisi mtazamo wa watu wengi, zinaweza kuathiri mshikamano wa chama hicho.

Hata hivyo, kwa wanaotarajia kuwa "CCM itakufa kutokana na mabadiliko haya" wanapaswa wazielewe vema siasa za Tanzania yetu.

Si kwamba CCM itatawala milele, lakini kwa mazingira tuliyonayo hivi sasa, hakuna chama mbadala. Huo ndio ukweli mchungu.

CCM wanaweza kukandamiza upinzani dhidi ya mabadiliko ya Katiba yao lakini angalau wameitisha mkutano mkuu, wamejadiliana na kupitisha mabadiliko ya katiba yao, sambamba na wameadhibu waliokiuka taratibu za chama hicho.

Sio kamili, lakini hiyo yaakisi demokrasia kwa kiasi fulani. Kwa takriban vyama vyetu vyote vya upinzani, jaribio la kufanya kilichofanywa na CCM wiki iliyopita linaweza kutishia “kukiuwa” chama husika.

Ukiangalia wapinzani wakuu wa CCM, yaani Chadema, sio tu "wamegoma kabisa" kufanya tathmini ya kilichowaangusha katika uchaguzi mkuu uliopita bali pia wametelekeza turufu yao kubwa na iliyowajengea imani kubwa kwa Watanzania, yaani mapambano ya dhati dhidi ya ufisadi, yaliyoibua 'List of Shame,' skandali nzito kama Richmond, EPA, Kiwira, nk.

Cha kusikitisha ni kwamba vyama vyetu vya upinzani sasa vimekuwa kama vinachezeshwa ngoma na CCM. Wafuasi wa vyama hivyo "wapo bize" kujadili matukio yanayoihusu CCM badala ya kuwekeza nguvu kwenye mustakabali wa vyama hivyo.

Jiulize, hivi ajenda kuu ya Chadema, au CUF au ACT- Wazalendo ni ipi muda huu?

Ni katika mazingira hayo, baadhi ya viongozi wa CCM watavumilia mabadiliko yanayoendelea ndani ya chama chao kwa sababu hakuna mbadala wa chama hicho tawala kwa sasa. Tumebaki na miaka mitatu na miezi saba kabla ya uchaguzi mkuu ujao lakini wapinzani wetu wapo bize kuijadili CCM na serikali yake badala ya kujipanga vyema kwa uchaguzi ujao.

Moja kati ya vitu vilivyoiangusha UKAWA katika uchaguzi mkuu uliopita ni "kusubiri makapi ya CCM" badala ya kutangaza mgombea wao mapema na kisha kumnadi kwa nguvu zote, kipindi ambacho CCM ilikuwa na shika-nikushike ya makada wake 40+ waliojitokeza kuwania kuteuliwa kuwa wagombea wa nafasi ya urais kupitia chama hicho tawala.

Nihitimishe makala hii kwa kupigia mstari uwezekano wa aina mbili

Kwanza, CCM kuibuka imara zaidi baada ya Mkutano huo Mkuu Maalum pamoja na hatua za kinidhamu zilizochukuliwa dhidi ya makada kadhaa, kwa sababu nidhamu katika taasisi yoyote ile ni nguzo ya mafanikio, na pia, ili maendeleo yafikiwe shurti kuwepo na mabadiliko, na mabadiliko hukumbana na vikwazo ambavyo vyaweza kurukwa iwapo kuna nidhamu bora.

Japo yaweza kuwa mapema mno kuhitimisha hili, yayumkinika kusema kuwa “mahesabu ya Magufuli yamelipa” kwa maana ya uamuzi wake wa kumteua Mama Salma kuwa Mbunge wa Bunge la Jamhuri hivi karibuni unaweza kuwa umesaidia “kumweka karibu” Rais Mstaafu Jakaya Kikwete ambaye pia ni Mwenyekiti mstaafu wa CCM Taifa, na mwenye ushawishi mkubwa katika chama hicho kuliko Dk. Magufuli mwenyewe.

Pili, mambo mawili – hatua dhidi ya makada walioadhibiwa na mabadiliko yaliyopelekea baadhi ya viongozi kupunguziwa nyadhifa – yanaweza kuzua manung’uniko ndani ya chama hicho. Ni wazi kuwa waliochukuliwa hatua za kinidhamu na walioathirika wa kuvuliwa kofia zaidi ya moja za uongozi hawatofurahishwa na hatua hizo. Hata hivyo, je wana pa kukimbilia? Na hapo ndipo utapobaini kuwa siasa za nchi yetu "zingechangamka sana" laiti tungekuwa na upinzani imara.

Na upinzani imara sio lazima upewe ruhusa na serikali kufanya mikutano/maandamano bali kama ule ulioibua 'List of Shame,' Richmond, EPA, nk…hawakuwa na ruhusa ya kufanya hivyo, na pia wanasiasa kama Dk. Willibrord Slaa na Zitto Kabwe walinusurika kwenda jela kwa ajili ya kuwapigania Watanzania.


Kimenukaa..Polisi Waanza Kamata Kamata kwa Wakazi wa Mabondeni,15 Tayari Wapo Selo..!!!

$
0
0

Watu kumi na tano wamekamatwa na jeshi la polisi kanda maalumu ya Dar es Salamu kwa kosa la kukaidi agizo la serikali lililowataka kuondoka maeneo ya mabondeni.

Kamanda wa polisi kanda maalumu ya Dar es Salaam Saimon Sirro amesema watu hao wamekamatwa na kupelekwa mahakamani kujibu mashtaka ya kukaidi kuhama maeneo hatarishi na kwamba eneo hilo ni mali ya halmashauri ya manispaa ya Ilala.

Hata hivyo kamanda Sirro amesema hali ya usalama katika jiji la Dar es Salaam imetengamaa, ambapo jeshi hilo limefanikiwa kudhibiti vikundi vya kihalifu.

Aidha jeshi hilo limefanikiwa kuwakamata wezi wa magari na uchunguzi bado unaendelea.

Hivi Ndivyo Ahadi ya Rais Magufuli Ilivyotekelezwa kwa Spidi ya Kimondo..!!!

$
0
0

Ahadi ya Rais Dk.John Pombe Magufuli ya kutatua kero ya maji kwa wakazi zaidi ya 12,000 wa mji mdogo wa Kisesa wilaya ya Magu mkoani Mwanza,hatimaye imetekelezeka ndani ya miezi miwili, baada ya mamlaka ya majisafi na usafi wa mazingira jijini Mwanza ( MWAUWASA ) kutumia zaidi ya shilingi milioni 62 kujenga mradi wa maji katika mji huo na hivyo kumaliza kabisa kero ya maji ya muda mrefu.

Ujenzi wa mradi mpya wa maji Kisesa ulianza Januari 29 mwaka huu,siku 18 baada ya Rais john Magufuli, aliyekuwa akipita eneo la Kisesa akitokea Chato kuelekea Bariadi mkoani Simiyu kuombwa na wakazi wa mji huo awasaidie kutatua kero ya maji, ambapo alimuagiza Waziri wa maji na umwagiliaji Mhandisi gerson Lwenge kuhakikisha anashirikiana na mamlaka ya majisafi na usafi wa mazingira jijini mwanza ( MWAUWASA ) kutatua changamoto hiyo iliyokuwa inawakabili wakazi wa kisesa.

Mkuu wa wilaya ya Magu Bi.Hadija Nyembo akizindua mradi huo amekemea tabia ya baadhi ya wananchi kuihujumu MWAUWASA kwa kujiunganishia maji bila kufuata taratibu,sambamba na wanaojihusisha na wizi wa dira za maji na wanaoiba maji baada ya kusitishiwa huduma hiyo kutokana na madeni.

Baadhi ya wakazi wa eneo la Kisesa,wanaeleza jinsi walivyokuwa wakitaabika kwa kukosa majisafi na salama kabla ya mradi huo kukamilika.

Davido: Nampenda Sophia Kinoma!

$
0
0

LICHA ya hivi karibuni kuweka hadharani kuwa anatarajia kupata mtoto wa pili kwa demu wake mpya mwenye asili ya Marekani, Mandy, staa wa muziki kutoka Naija, David Adeleke ‘Davido’ amefunguka ya moyoni kuwa bado anampenda kinoma mzazi mwenzake wa kwanza aitwaye Sophia Momodu aliyezaa naye mtoto mmoja, Imade.

Davido aliyasema hayo alipofanyiwa mahojiano na redio moja nchini Nigeria kuwa, hawezi kumsahau wala kumtupa mzazi mwenzake kwa kuwa amezaa naye.

“Nampenda mzazi mwenzangu, haahaa, Sophia sikia hii popote ulipo!” Davido na Mandy walianzisha uhusiano Atlanta, Georgia huko Marekani na hadi sasa demu huyo ameshakanyaga Jiji la Lagos anapoishi Davido mara moja yaani Desemba 2016.

Jipatie Water Dispenser Mpya Kwa Bei Nafuu Upate Maji ya Baridi na Moto

$
0
0
JIPATIE WATER DISPENSER MPYA kwa bei Nafuu sanaa,Kwa matumizi ya OFISINI NA NYUMBANI, Upate Maji baridi na Moto.

Tunakuletea ULIPO Oda yako kwa Wakati na Mikoani tunatuma Oda zenu pia.

Kifaa Hiki tunatoa DHAMANA ya Mwaka 1.

BEI 195,000/= TU HAINA FRIJI.

BEI 270,000/= INA FRIJI CHINI

TUPIGIE SASA NAMBA 0743757575

Ofisa wa TRA Apoteza Funguo za TFF Baada ya Kuzipiga Kufuli

$
0
0


Katika hali isiyokuwa ya kawaida, Ofisi za Shirikisho la Soka Tanzania (TFF) mpaka jana joini zilikuwa bado zimefungwa kutokana na ofisa mmoja wa Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA) kutoziona funguo za ofisi hizo alipoziweka.

Ofisi za TFF zilifungwa Jumatano ya wiki hii kufuatia limbikizo la deni ambalo ni zaidi ya shilingi bilioni moja la tangu mwaka 2010 ikiwa ni deni la kodi la ujio wa timu ya Brazil, kodi ya mshahara wa aliyekuwa kocha wa timu ya taifa, Taifa Stars, Marcio Maximo pamoja na deni la mwaka jana la mechi ya Yanga na TP Mazembe ambao mashabiki waliingia bure.

Ofisa Habari wa TFF, Alfred Lucas amesema kuwa, hadi kufikia jana mchana ofisi hizo hazikuwa zimefunguliwa kutokana na baadhi ya mambo kutokamilika ikiwa ni pamoja na kutoonekana kwa funguo za ofisi hizo.

“Jana (juzi) viongozi wa TFF walikutana na TRA kujadiliana suala hilo na kufikia muafaka ambapo kiasi cha fedha Sh milioni 300 kililipwa ili kuweza kufungua ofisi hizo lakini ilishindikana kutokana na sababu zilizokuwa nje ya uwezo.

“Tumewasiliana nao leo lakini muhusika ambaye anatakiwa kufungua ofisi amesahau alipoziweka funguo,” alisema Lucas.

SOURCE: CHAMPIONI

JPM Anavyozima ‘Kiki’ za Mawaziri..!!!

$
0
0

KAMA kuna waziri au kiongozi yeyote anataka kutoa taarifa yenye kuwagusa wananchi moja kwa moja, ni dhahiri kuwa sasa atalazimika kujiridhisha zaidi.

Aidha, waziri na viongozi wengine wanatakiwa pia kuzingatia dhana ya uongozi wa pamoja kwa kuwahusisha wenzao na pia kupata maoni ya wataalamu katika wizara au taasisi wanazoziongoza kabla ya kulifikisha kwa umma.

Vinginevyo, mawaziri wajiandae kushuhudia maagizo yao yakitenguliwa huku pia wakijiweka katika hatari ya kufikiriwa kuwa wanafanya hivyo kwa minajili ya kutumia matamko yao kama ‘kiki’ za kuwaonyesha kuwa wanafanya kazi vyema na kwa kasi inayosisitizwa na Serikali ya awamu ya tano.

Angalizo hilo limetolewa na baadhi ya wachambuzi wa amsuala ya kisiasa walizoungumza na Nipashe kuelezea mkasa uliomkuta Waziri wa Sheria na Katiba, Dk. Harrison Mwakyembe, ambaye agizo lake la kuzuia ufungishaji ndoa kwa watu wote wasiokuwa na vyeti vya kuzaliwa lilifutwa na Rais John Magufuli kwa kuonekana kuwa litawaathiri mamilioni ya Watanzania wasiokuwa na vyeti hivyo.

Baadhi ya wachambuzi walidai kuwa Mwakyembe siyo waziri au kiongozi wa kwanza kutoa taarifa zilizomlazimu Rais Magufuli kuingilia kati kwa manufaa ya Watanzania na hivyo, wanapaswa kujua kuwa wana wajibu mkubwa kwa taifa na kutakiwa wajiepushe na matamko binafsi yasiyofanyiwa kazi kwa kina kabla ya kutolewa kwa umma.

“Ni vizuri kwa kila waziri au kiongozi yeyote yule kujipa uhakika wa kila tamko na amri wanazotaka kutoa kwa umma…kwa mfano, ni lazima wahakikishe kwamba wanazingatia sheria na pia wanayoyasema ni kwa maslahi ya umma mpana wa Tanzania.

“Vinginevyo, matamko yao yataendelea kuibua maswali na Rais hatakubali wamharibie kwa sababu ameshasema mara kadhaa kuwa daima atakuwa upande wenye maslahi kwa wananchi wake, na hasa wanyonge,” alisema mmoja wa wachambuzi hao.

“Ni vizuri wakaachana na matamko yenye viashiria vya kuwa na kiki za kuonyesha kuwa nao wako vizuri kuendana na kasi ya serikali ya sasa...wasipozingatia hayo kila mara watajikuta wakiwa tofauti,” mwingine aliongeza.

Neno ‘kiki’ ni la mtaani na limejitwalia umaarufu katika siku za hivi karibuni, likitumiwa kumaanisha mbinu zinazoweza kutumiwa na mtu ili kujipatia umaarufu juu ya jambo fulani. Wasanii na wanasiasa huhusishwa zaidi na neno hilo kutokana na asili ya kazi zao ambazo huwakutanisha zaidi na watu.

Awali, katika agizo lake hilo ambalo alilisisitiza pia jana asubuhi wakati akizungumza na kituo kimoja cha redio jijini Dar es Salaam, Mwakyembe alisema wameamua kuzuia ndoa kwa watu wasiokuwa na vyeti vya kuzaliwa kwa nia ya kuondokana na takwimu za sasa zinazoonyesha kuwa Tanzania Bara ni ya mwisho barani kwa utoaji wa vyeti vya kuzaliwa kwa wananchi wake.

Alisema ni asilimia 12 tu ya Watanzania walioko Bara ndiyo wenye vyeti vya kuzaliwa na kuzidiwa hata na Zanzibar yenye wastani wa asilimia 75, hali aliyosema inashangaza kwa sababu bei ya vyeti hivyo ni Sh. 3,500 tu huku gharama za harusi zikiwa kubwa kulinganisha na kiasi hicho.

Hata hivyo, akizungumza na waandishi wa habari muda mfupi kabla ya kuondoka mjini Dodoma na baadaye taarifa yake kusambazwa kwa umma jana, Rais Magufuli alisema anatengua uamuzi huo wa Waziri Mwakyembe kwa sababu utawanyima fursa ya kuoana Watanzania ambao wengi wao hawana vyeti hivyo vya kuzaliwa, hasa wale wa vijijini.

Alisema hadi sasa idadi ya Watanzania walio na vyeti vya kuzaliwa ni chini ya asilimia 20 huku wengi wao wakiwa ni wananchi waishio vijijini ambako ni vigumu kupata vyeti hivyo, na wengine wakiwa ni waliozaliwa kabla ya kuanza kutolewa kwa vyeti vya kuzaliwa nchini mwaka 1961.

“Kwa hiyo ndugu zangu Watanzania msiwe na wasiwasi wowote, endeleeni na utaratibu wenu wa kuoa na kuolewa kama kawaida na kama kuna kifungu chochote cha sheria kinachomlazimisha mtu awe na cheti cha kuzaliwa ndipo aoe ama aolewe nitamuelekeza Waziri wa Katiba na Sheria Mhe. Harrison Mwakyembe apeleke Bungeni kikarekebishwe” alisema Rais Magufuli, huku akitoa wito kwa wanasheria kuziangalia vizuri sheria zinazohusiana na kuzaliwa na kifo na kuoa na kuolewa ili zisilete mkanganyiko kwa wananchi.

JPM ALIVYOZIMA ‘KIKI’
Mbali na tukio la kuzimwa kwa ‘kiki’ ya Waziri Mwkayembe jana, wapo pia mawaziri na viongozi wengine kadhaa wa serikali na taasisi za umma waliokumbana na rungu la Magufuli la kutengua amri au tarifa zao. Hao ni pamoja na Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu, Sera, Bunge, Kazi, Vijana, Ajira na Walemavu, Jenista Mhagama; Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (Tamisemi), George Simbachawene na Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo, Nape Nnauye.

Mhagama alikumbana na mkasa huo Machi 3, 2016 wakati alipotoa taarifa ya kumteua Dk. Carina Wangwe kuwa Kaimu Mkurugenzi wa Shirika la Taifa la Hifadhi ya Jamii (NSSF). Hata hivyo, wakati uamuzi wake ukimpa umaarufu siku hiyo kupitia ‘kiki’ za kwenye mitandao ya kijamii, waziri huyo alilazimika kubatilisha taarifa hiyo kabla Rais Magufuli hajamtangaza Prof. Godius Kahyarara kushika nafasi hiyo NSSF.

Agosti 12 mwaka jana, Simbachwene alisisitiza kuondolewa kwa wamachinga maeneo ya mijini. Hata hivyo, siku chache baadaye, Magufuli alitengua agizo hilo wakati akihutubia jijini Mwanza kwa kutaka wamachinga wasiondolewe kwenye maeneo wanayofanyia biashara hadi pale mamlaka husika zitakapohakikisha kuwa zimewatafutia sehemu za kwenda kufanyia biashara zao.

Waziri mwingine aliyekumbwa na rungu la Magufuli hivi karibuni wakati kauli yake ikiwa imepamba moto na kuibua mijadala kwenye mitandao ya kijamii ni Nape.

Machi Mosi mwaka huu, Nape alielezea umuhimu wa kulinda majina ya wasanii waliotajwa hadharani wakituhumiwa kuhusika na dawa za kulevya, akisema kwamba ni vyema kuzingatia nguvu kubwa walizotumia kujijengea majina hayo na kwamba, ifikiriwe pia ni kwa namna gani watasafishwa ikiwa wataonekana baadaye kuwa hawahusiki na dawa za kulevya.

Nape alizungumza hayo akiwa Dodoma na baadaye kwenye kipindi cha Dakika 45 kinachorushwa na ITV kuelezea hatua iliyochukuliwa na Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam, Paul Makonda, aliyetangaza hadharani majina ya wasanii kadhaa katika orodha yake ya awali ya watuhumiwa 65 wa dawa za kulevya.

Hata hivyo, siku chache baadaye, Magufuli alionekana kupinga maelezo ya Nape kwa kusisitiza kuwa vita dhidi ya dawa za kulevya isiangalie majina ya watu kwa sababu athari zake ni kubwa kwa taifa.

WALICHOSEMA WABUNGE, WASOMI WANENA
Akizungumzia suala la Mwakyembe, Mbunge wa Kibamba, John Mnyika (Chadema), alisema ni ishara kuwa baadhi ya mawaziri na viongozi wengine wamekuwa wakikurupuka kwa kutoa matamko bila kuyafanyia utafiti wa kina na ndiyo maana Magufuli ametengua agizo alilotoa kuhusu amri ya kuzuia ndoa kwa wasiokuwa na vyeti vya kuzaliwa.

Mbunge wa Busega, Dk. Raphael Chegeni (CCM), alisema awali alikuwa haamini na mwishowe akajikuta akisikitika kusikia tamko la Waziri Mwakyembe kuhusu zuio la ndoa kwa wasiokuwa na vyeti vya kuzaliwa kwa sababu agizo lake halikuwa na msingi wa kisheria.

Alisema kupitia mkasa huo wa Mwakyembe, mawaziri wanatakiwa kuwa makini katika kutoa matamko ya aina hiyo na kwamba, kama wana hoja wanatakiwa kupeleka ndani ya Bunge ili ijadiliwe.

“Kama unatoa tamko leo na Rais analipinga ama kulifuta, hiyo inaonyesha kuwa waziri umekurupuka… matamko kama haya yanamgombanisha Rais na wananchi wake. Mawaziri wajiepusha kutoa matamko ambayo hayajapewa ridhaa,” alisema Chegeni.

Mbunge wa Nzega Mjini (CCM), Hussein Bashe, alisema alichokifanya Rais Magufuli kutengua tamko hilo yupo sahihi kwa kuwa suala la ndoa linagusa imani ya mtu na serikali haitakiwi kuingilia, na kwamba kama kuna jambo la kisheria liwasilishwe bungeni ili lifanyiwe kazi.

Mhadhiri wa Chuo Kikuu cha Dar es Salaam (UDSM), Dk. Richard Mbunda, alisema inavyoonekana, huenda tangazo alilitoa Mwakyembe ni binafsi kwa mtazamo wake baada ya kuona kuna udanganyifu mkubwa katika eneo hilo.

Mkurugenzi wa Kituo cha Sheria na Haki za Bindamu (LHRC), Dk. Hellen Kijo-Bisimba alisema agizo la Mwakyembe kuhusu masuala ya ndoa linashangaza kwa sababu halipo kwa mujibu wa sheria

“Katika Sheria ya Ndoa, vitu ambavyo mtu anatakiwa kuwa navyo ili afunge ndoa ama sifa, hiyo ya cheti (cha kuzaliwa) haipo… sijui huyo Waziri ameitoa wapi na pia ingekuwepo kisheria ingepingwa kwa sababu watu wengi hawana vyeti vya kuzaliwa,” alisema Bisimba.

Mhadhiri wa Chuo Kikuu cha Dar es Salaam, Dk. Ally Bashiru, alisema ni vyema Rais Magufuli ameingilia na kutengua agizo la Mwakyembe la kuzuia ndoa kwa asiokuwa na vyeti vya kuzaliwa.


Jinsi Mababu Zetu Walivyotumia Njia ya Kiini Macho Kuongeza Ukubwa na Urefu wa Maumbile ya Kiume..!!!!

$
0
0

Suala la udogo wa  maumbile  ya  kiume lipo tangu  enzi  za  mababu  zetu. Enzi  za  mababu  zetu, suala  la  udogo  wa maumbile  ya  kiume  lilikuwa  linatibiwa  kwa  kutumia  njia  kuu  mbili.  Njia  hizo ni  kama  ifuatavyo :

1.   KUCHANJIWA AMA  KUNYWESHWA  DAWA  YENYE  KUONGEZA  UKUBWA WA  MAUMBILE

 Hapa  mwanaume  mwenye  tatizo  la kuwa  na  maumbile  madogo  ya  kiume  alichanjiwa  au  kunyweshwa  dawa  ya  asili  yenye  uwezo  wa kurefusha  na   kuongeza  urefu na  ukubwa  wa  maumbile  ye  kiume.  Kama  iligundulika  kuwa, tatizo  la  mwanaume  husika  lilitokana  na  mkono  wa  mtu ( kurogwa ), basi  zoezi  la  kumchanja  au  kumnywesha  dawa  mwanaume  huyo lilienda  pamoja  na  tambiko  maalumu  la  kuua  nguvu  ya  uchawi  ulio  tumika  kufunga  ukuaji  wa  maumbile  ya  kiume  ya  mwanaume  huyo

Sababu  zilizo  wafanya  watu  wawafunge  watoto  wa  kiume  au  wanaume  maumbile  yao  yawe  madogo  ni  pamoja  na ; Kwenye  ndoa  za  mitaala, mke  anawafunga  watoto  wa  kiume  wa  mke  mwenzake  ili  waishie  kuwa  na  maisha    yenye  mateso  na  mahangiko ( SIKU NYINGINE  NITAELEZEA  JINSI   WATOTO  WA  KIUME  NA WANAUME  WANAVYO  FUNGWA   KUWA  NA  MAUMBILE  MADOGO  YALIYO SINYAA  )

Mwanamke  anamfunga  mwanaume  aliye mkataa  nakadhalika. Sababu  ni  nyingi  sana.

Kwa  bahati nzuri, nimeshaelezea  jinsi  na  namna  ya  kuongeza  na  kurefusha  ukubwa  wa  maumbile  ya  kiume  kwa  njia  ya  kuchanjia  au  kunywa  dawa.

Leo  nitaelezea  kuhusu  njia  ya  pili, ambayo  ni  KUONGEZA  UREFU  NA  UKUBWA  WA  MAUMBILE  YA  KIUME  KWA  NJIA  YA  KIINI  MACHO.  Njia  hii  haijulikani  na  watu  wengi.

Tiba  hii  hutumiwa na  mtu  ambaye  amethibitika  kuwa  suala  la  udogo  ama  ufupi  wa  maumbile  yake  ya  kiume, unatokana  na  maumbile  ya  asili. Yaani  amerithi  vinasaba  vya  maumbile  yake  kutoka  kwa  wazazi  wake na  wala  hajarogwa   na  mtu  yoyote.

Njia  hii  hutumiwa  na  magwiji  wa  tiba  za  jadi  tangu  enzi za  mabibi  na  mababu  wa  mababu, leo  nitaielezea  kwa  ufupi.

JINSI  YA  KUONGEZA  UKUBWA  NA  UREFU WA  MAUMBILE  YA  KIUME  KWA  NJIA YA  KIINI  MACHO

Kiini  macho  ni  uchawi  unao tumika  kufunga  na  kuyamiliki macho  ya  mtu  pamoja  na  kuyaelekeza  ama  kuyaamuru  yaone  na  kuamini  kile  ambacho  wewe  unataka   yakione  na  kukiamini.

  Katika  tiba  hii, mwanaume  anachanjiwa  dawa  kwenye  uume  wake  pamoja na  sehemu  nyinginezo za  mwilini mwake  kwa  lengo  la  kuyafunga, na kuyaamuru  macho  na  akili  ya  mwanamke  atakae  kutana  nae  faragha  kumuona  kama  mwanaume  mwenye maumbile makubwa  ya  kiume.

Kabla  ya  mwanaume  kuchanjiwa  dawa  hii, kwanza  unaandaliwa  huo  uchawi  wa  kiini  macho.

JINSI  UCHAWI  WA  KIINI  MACHO  UNAVYO TENGENEZWA.

Anachukuliwa  paka  mweusi  aliye  asi  nyumbani (  Paka  wa  aina  hii  katika  ulimwengu  wa  wachawi  huwa  wanajulikana kama  “  KIMBURU” ,    paka  huyo  anapelekwa  njia  panda  saa  sita za usiku, kisha  anatobolewa  macho, halafu  kwenye  macho  yake  zinawekwa  mbegu  za  mti  wa   mnyonyo.

Baada  ya  hapo, litachimbwa  shimo , kisha  paka  huyo  atazikwa  humo.

Huyo paka  akisha  zikwa , litaanza  zoezi  la   kumwagilizia  sehemu  aliyo  zikwa  paka  huyo.  Eneo  hilo  litakuwa linamwagiliziwa  mara  saba  kwa  siku, asubuhi  mara  tatu, mchana  mara  mbili  na  usiku  mara  tatu.

Eneo  hilo  litamwagiliziwa  hadi  uote  mti  wa  mnyonyo na  kukomaa.

Mti  wa  mnyonyo  ukishaota  na  kukomaa , itachukuliwa  ile  mizizi  ya  huo  mnyonyo  na  kupondwa  pondwa   pamoja  na  dawa  ya  asili  inaitwa  nkwesi.

Zoezi  la  kuponda  ponda  hiyo  mizizi  ya  mnyonyo  pamoja  na  hizo nkwesi likikamilika,   mhusika    ataenda  kwenye  eneo  lenye  mkutano  au  onyesho  lolote  kisha  atachukua  uchafu au takataka  za  eneo  hilo  wakati  watu  hao wakiwa  bize  wanasikiliza  mkutano, atazichoma  hadi  ziwe  unga unga.

Baada  ya  hapo  atachanganya  dawa  hizo  nilizo  zitaja  mwanzo,yaani mizizi  ya  mnyonyo  na  nkwesi  pamoja  na  madawa  mengine  ya  asili.

Zoezi  la  kuchanganya  mizizi  ya  mnyonyo  iliyo  sagwa  pamoja  na  kwesi , takataka  & uchafu  uliochukuliwa kwenye  mkutano  na  kuchomwa  pamoja  na  dawa  nyingine  za  porini, litafuata  zoezi  la kuchinja  punda.

Watachukuliwa  punda  saba  (YOTE  MADUME  YALIYO KOMAA ), Punda  hawa  watachinjwa  kwa  tambiko  rasmi.  Punda  hawa  watachinjwa  kwa  muda  wa  siku saba  mfululizo, kila  punda  mmoja  atachinjwa  kwa  siku  moja.

Kila  punda  atakae  chinjwa, itachukuliwa  DHAKARI  yake  ama  uume  wake kwa  wale  wasio elewa  dhakari  maana yake  nini, dhakari  za  hawa  punda zitaunganishwa  zote  kwa  pamoja, zitachanganywa  na  majivu  ya  kondoo  mweusi  aliye  pita  duniani  bila  kuonekana, utukakanga  wa  baharini  au  wa  porini  pamoja  na  dawa  nyingine  za  porini..  Baadae   litafanyika  tambiko  rasmi  la  kuchanganya  dawa ama  vizimba  vyote  nilivyo  vitaja  hapo  hapo  juu.

Dawa  hii  watapewa  wanaume  wenye  tatizo la  maumbile  mafupi  na  madogo  ya  kiume,  watajichanja  wenyewe   katika maeneo  Fulani  Fulani  mwilini  huku  wakitamka  maneno  Fulani 

Basi  kila  mwanamke  atakae  kutana  na  mwanaume  huyu ataenda  kusimulia,  kwa  wenzake  kuwa amekutana  na  mwanaume  wa  ukweli  na  anae  ijua  kazi  ambayo  iliwaleta  wanaume  duniani.

Viewing all 104780 articles
Browse latest View live




Latest Images