Quantcast
Channel: UDAKU SPECIAL
Viewing all 104689 articles
Browse latest View live

Nimekuwekea Madhara ya Simu Ambayo Wanaouza Simu Hawataki Uyajue ...!!!!

$
0
0

Je, umeshawahi kusoma kilichoandikwa kwenye kitabu cha maelezo juu ya namna ya kutumia simu yako pindi unaponunua mpya? Vitabu vyote vya maelekezo ya namna ya kutumia simu huelekeza watumiaji kusikiliza simu ikiwa mbali kidogo na sikio, lakini ni wangapi wanafuata maelekezo hayo muhimu?

Suala la usalama wa watumiaji wa simu za mkononi limekuwa ni gumzo sehemu mbalimbali duniani. Hata hivyo, kampuni kubwa za simu zimekuwa zikitumia mamilioni ya dola za Marekani kulinda biashara yao kwa kuhakikisha walaji hawapati ukweli wa madhara yanayotokana na simu.

Kwa kipindi kirefu, kumekuwapo madai kutoka kwa wanasayansi pamoja na vyombo vya habari kuwa matumizi makubwa ya simu za mkononi yanasababisha madhara kwa afya ya mtumiaji. Kwa miaka ya hivi karibuni, utumiji wa simu za mkononi umeongezeka mara dufu karibu kila kona ya dunia. Kwa sababu ugonjwa kama satarani unachukua miaka 10 hadi 20  kugundulika, pengine itachukua miaka mingi kwa watafiti kuihakikishia dunia kuwa matumizi ya simu yanasababisha saratani au hapana.

Mashirika ya kimataifa yamekuwa yakifanya utafiti kuhusu suala hili. Shirika la Kimataifa la Utafiti wa Saratani (IARC) ambalo ni sehemu ya Shirika la Afya Duniani (WHO) liliwahi kuwaleta pamoja watengenezaji wa simu za mkononi ili kutoa data zinazohusiana na mionzi inayotokana na simu za mkononi.

Ilielezwa kuwa, simu hutoa mionzi inaitwa Radio Frequency-Electromagnetic Radiation (RF-EMR), ambayo pia hujulikana kama microwave radiation. IARC walisema kuwa mionzi hiyo inaweza kusababisha saratani. Hata hivyo, hakuna utafiti wa kina uliofanyika kuonyesha kama kweli simu za mkononi ni hatari au salama kiasi gani kwa watumiaji.

Kutokana na hilo, IARC ilitengeneza mradi uliokuwa unaitwa Interphone Project ambao ulijaribu kuchunguza madhara yanayotokana na matumizi ya simu za mkononi. Baada ya miaka 10, mradi huo ulimalizika Februari 2012, lakini wanasayansi walisema kuna ushawishi ulioingilia uchunguzi huo na hivyo hawakuweza kutoa uamuzi wa maana.

Katika hatua nyingine, Kituo cha Kuzuia na Kupambana na Magonjwa cha Marekani (CDC) mwaka 2014 kilitoa onyo kwa matumizi ya simu kwa kuwa swali la kuwa simu zinasababisha satarani au hapana bado halijapata jibu la uhakika. Hata hivyo, CDC waliondoa tangazo hilo kutoka kwenye tovuti yake kutokana na msukumo mkubwa kutoka kampuni ya simu. Kwa sasa CDC wanasema utafiti unahitajika kufanyika ili kujua matumizi ya simu yana madhara kiasi gani kwa watumiaji.

 Watafiti wansema nini?

Mwaka 2007 na 2012 wanasayansi wa Uingereza walichapisha taarifa mbili zilizohuhusu madhara ya simu za mkononi na ubongo. Katika taarifa yao hiyo, walisema utafiti ulifanywa kwa mtu mmoja mmoja na kuonyesha madhara kwa watu waliokuwa wakitumia simu za mkononi.

Utafiti mwingine uliofanywa kwa wanyama umeweza kuonyesha uhusiano kati ya matumizi ya simu na madhara ya kiafya. Mwaka 2015 utafiti ulifanyika nchini Ujerumani ulionyesha uhusiano kati ya mionzi ya simu za mkononi na matatizo ya afya ya ubongo ya panya waliomtumia kufanya utafiti huo. Katika utafiti huo, watafiti hao pia waligundua kuwa mionzi inayotokana na simu za mkononi ni moja kati ya visababishi vya saratani. Pamoja na kwamba utafiti huu ulifanyika kwa panya lakini unaonyesha kuwa mionzi ya simu za mkononi inawenza kusababisha matatizo hata kwa binadamu.

Mwezi Mei mwaka 2016 utafiti mwingine wa miaka miwili ulifanyika nchini Marekani juu ya madhara ya mionzi ya simu kwa panya. Utafiti uligundua kwamba, panya waliokuwa kwenye mionzi ya wastani na mikali ya simu waliweza kupata madhara makubwa katika bongo zao. 

Japokuwa matokea ya tafiti ya juu ya madhara ya simu za mkononi kwa ubongo wa binadamu bado hazijatoa taarifa za uhakika sana, lakini watafiti wengi wamekuwa wakionyesha wasi wasi wao juu ya uhusiano wa afya ya ubungo na matumizi ya simu za mkononi.

Kutana na Watoto Wenye Nguvu Zaidi Duniani...!!!

$
0
0

KILA mtoto ana kipaji tofauti na hukionesha kwa njia tofauti. Wakati baadhi wanaweza kuwa wazuri katika uchoraji, wengine hujikita zaidi katika michezo na wachache wengine wakifanya kweli darasani.

Lakini umewahi kusikia au kuona watoto wakifanya yao katika kunyanyua vitu vizito au kujenga mwili kwa mazoezi makali, ambayo watu wazima wasingethubutu kufanya?

Sawa, pengine uko katika mshangao mkubwa au kiasi! Wafuatao  wanahesabika kuwa miongoni mwa watoto wenye nguvu zaidi duniani, ambao watakushtua kwa uwezo na nguvu zao.

1. Giuliano Stroe na Claudiu Stroe

Giuliano Stroe na Claudiu, wenye umri wa miaka tisa na saba bila ubishi ndio watoto wenye nguvu zaidi duniani. Ndugu hawa wawili kutoka  Icoana, kusini mwa Romania, wamekuwa wakinyanyua vitu vizito tangu wakiwa na umri wa miaka miwili na wanaweza kufanya mazoezi ambayo huogopesha hata watu wazima.

Baba yao ni mkufunzi na huwafanya wavulana hao kupitia taratibu zote ikiwamo mlo unaotakiwa na vipindi vya mafunzo kila siku. Giuliano tayari amevunja rekodi ya dunia kwa aina za pushapu.

2. Yang Jinlong

Yang  ana umri wa miaka saba tu na uzito wa 110 lbs sawa na kilo 50, ijapokuwa hafuati utaratibu wa mlo na mazoezi ya kumjenga kama watoto wengine wenye nguvu walioorodheshwa katika makala haya, anastahili kuwamo hapa.

Yang anaweza si tu kumbeba baba yake mwenye uzito wa 200 lbs sawa na kilo 91 mgongoni mwake bali pia anaweza kulivuta gari la familia yao barabarani kwa nguvu yake.  Kwa taarifa 1 lbs ni sawa na kilo 0.453.

Mvulana huyu wa Kichina kwa hakika kwa umri wake huo ni mtoto mwenye nguvu duniani.

3. Richard Sandrak

Akiwa amezaliwa Ukraine, Richard Sandrak ni mtoto mwingine miongoni mwa wale wanaofanya makubwa ambayo watu wazima hawana uthubutu.

Alianza kufanya mazoezi akiwa na umri miaka miwili na alipofikisha miaka sita, alikuwa tayari akinyanyua uzito wa 180 lbs sawa na kilo 81.

Amezama katika mazoezi kila siku kuinama na kuinuka akiwa na vitu vizito mabegani mara 200 na pushapu 600 push-ups zinazomsaidia kuujenga mwili wake. Kwa sasa ana umri wa miaka 23 na mwili uliojengeka mno.

Maryana Naumova

Anahesabiwa kuwa msichana mwenye nguvu zaidi duniani, Maryana Naumova kutoka Urusi amethibitisha kuwa nguvu si sifa kwa wavulana pekee.

Akiwa mnyanyua vitu vizito maarufu, Maryana (16), ni mshindi kwa kila hali. Katika umri wa miaka 15, alishiriki katika onesho la Arnold Classic – mchuano uliopewa jina la mcheza filamu, gavana na mnyanyua vitu vizito wa zamani Arnold Schwarzenegger na kumshangaza kila mmoja wakati aliponyanyua uzito wa 331 lbs sawa na kilo 150!

5. Naomi Kutin



Msichana mwingine mnyanyua vitu vizito na umri wa miaka 13, Naomi Kutin. Msichana huyo wa maajabu alivunja rekodi zote wakati wakati alipoweza kunyanyua uzito wa 215 lbs – ambao ni mara mbili ya uzito wa mwili wake – katika umri mdogo wa miaka 10. Naomi hakuishia kushangaza watu na baada ya miaka kadhaa aliweza kunyanyua mabegani  231 lbs na kuinua uzito wa 249 lbs, akivunja zake za awali. Si ajabu anaitwa “msichana wa aina yake”.

. CJ Senter

CJ Senter ni mtoto wa Kimarekani anayeamini katika ujenzi wa mwili na unyanyuaji wa vitu vizito. CJ amekuwa akifanya mazoezi tangu akiwa na umri wa miaka mitano.

Akiwa na umri wa miaka 10, alijipatia umaarufu , aliponekana katika DVD akionesha umahiri wake wakati akionesha namna watoto wanavyoweza kujitengeneza katika umbo la kuvutia.

7. Varvara Akulova



Mzaliwa huyu wa Ukraine Varvara Akulova, yu ndani ya kitabu cha rekodi za dunia cha Guinness akihesabiwa kama msichana mwenye nguvu zaidi duniani. Alianza kunyanyua vizito akiwa na umri wa miaka minne na kufikia umri wa miaka 10, tayari alikuwa na rekodi ya unyanyuzi wa vitu vizito kwa kunyanyua 220 lbs.

Miaka minne badaye alivunja rekodi yake mwenyewe kwa kuinua 660 lbs! akiwa amejaliwa na nguvu za ajabu akiwa ametokea kwa wazazi ambao walifanya kazi katika kikundi cha sarakasi, mwili wake ni mwepesi na hauonekani kuwa na nguvu alizo nazo sasa kwa kunyanyua vizito vya mno.

Jake Schellenschlager

Kwa kuingia katika mazoezi na ujenzi wa mwili katika umri wa miaka 12, mnyanyua vitu vizito Jake Schellenschlager (sasa 15) ni mmoja wa watoto wenye nguvu zaidi duniani. Akiwa na uzito wa 119 lbs katika umri wa miaka 14, Jake alimshangaza kila mmoja kwa kunyanyua 225 lbs katika mchuano huko Pennsylvania. Kana kwamba hilo halitoshi, alienda kunyanyua 300 lbs i.e. uzito wa mara mbili ya ule wa mwili wake. Mvulie kofia mvulana huyu.

Lissu Kidume..Aishinda Urais wa TLS kwa Kishindo...!!!

$
0
0

Mwanasheria Mkuu wa Chadema na Mbunge wa Singida Mashariki,Tundu Lissu Mapema Hii Leo ameweza kuibuka na ushindi wa kishindo cha Chama cha Wanasheria Tanganyika TLS kwa Kujizolea Asilimia 88 ya Kura Zote.


Tanzania Yaisaidia Kenya Madaktari 500 ...!!!

$
0
0

Rais Magufuli akubali ombi la kuipatia Kenya madaktari 500 kusaidia utoaji tiba baada ya kutokea kwa mgomo wa madaktari nchini humo Ikulu yathibitisha.

Rais Magufuli amekubalina na ombi hilo leo tarehe 18 March 2017 baada ya kufanya mazungumzo na ujumbe wa viongozi wa Wizara ya Afya ya Kenya uliotumwa na Rais wa nchi hiyo Mhe. Uhuru Kenyatta.

Hivi Ndivyo Tundu Lissu Alivyoandika Historia Mpya Tanzania..!!!

$
0
0

Mwanasheria Mkuu Chadema Tundu Lissu achaguliwa kuwa Rais wa Chama cha Wanasheria Tanganyika (TLS) kwa jumla ya kura 1,411 kati ya 1,682 zilizopigwa.

Mwanasiasa Julius Mtatiro ambaye kwa sasa yupo jijini Arusha amethibitisha ushindi huo wa Tundu Lissu 

"Wakili msomi Mhe.Tundu Lissu ameshinda Urais wa Chama cha wanasheria nchini (TLS) kwa kupata kura 1,411 kati ya kura 1,682 zilizopigwa, sawa na ushindi wa 84% ya kura zote." Ameandika Julius Mtatiro 

New Video: Barakah The Prince – Acha Niende..!!!

$
0
0

Muimbaji mwenye sauti ya pekee kutoka ndani ya label ROCKSTAR4000, Barakah The Prince baada ya kufanya vizuri na wimbo Nisamehe akiwa amemshirikisha Alikiba, ameachia video ya wimbo wake mpya Acha Niende. Audio ya wimbo huu imeandaliwa na producer Maneck kutoka AM Records na video imeongozwa na kampuni ya Head Master Production.

New Video: Professor Jay – Kibabe..!!!!

$
0
0

Mbunge wa jimbo la Mikumi na msanii mkongwe wa Bongo fleva Joseph Haule a.k.a Professor Jay ameachia video yake mpya wimbo unaitwa “Kibabe”. Video imeongozwa na Hanscana.

Hiki Hapa Kikosi cha Kwanza cha Yanga Dhidi ya Zanaco Leo..!!!

$
0
0

Leo timu ya Yanga inatupa karata yake katika mchezo unaopigwa Zambia katika mechi ya marudiano dhidi ya Zanaco FC. Mchezo huo unatarajiwa kuanza majira ya saa 10: 00 ya jioni.

Yanga wametangaza wachezaji wake ambao leo watakuwa kibaruani kuitafutia timu hiyo ushindi dhidi ya Zanaco FC. Huku Nadir Haroub Cannavaro pamoja na Vicent Andrew Dante watashindwa kuichezea timu hiyo kutokana na kuwa na majeraha. 

1.Deo Munishi Dida 
2.Hassan Hamisi 
3.Haji Mwinyi 
4.Kelvin Yondani
5.Vicent Bossue 
6.Justine Zulu 
7.Saimon Msuva 
8.Thaban Kamusoko 
9.Obrey Chirwa 
10.Haruna Niyonzima 
11.Godfrey Mwashiuya

SUB 

-Alli Mustafa Bathez 
-Juma Abdul 
- Andrew Chikupe
-Oscar Joshua 
-Said Juma Makapu 
-Juma Mahadhi 
-Emmanuel Martin

Jike Shupa Afungua Mdomo Baada ya Picha zake Kusagana Akidendeka na Mwanamke Mwenzake Mrembo Nai

$
0
0

Video Queen ambaye alishiriki katika video ya Nuh Mziwanda 'Jike Shupa' na kujipatia jina la Jike Shupa amefunguka na kusema yeye si msagaji ila pombe ndiyo zilipelekea yeye kum kiss video quen Nai na kusema kitendo hicho kinamfanya ajisikie vibaya


Jike Shupa aliyasema hayo jana kwenye kipindi cha Friday Night Live na kuwaomba msahama Watanzani wamsamehe kwa kitendo kile alichokifanya kwa mdada mwenzake.

Makubwa...Hiki Ndicho Alichokifanya Nuh Mziwanda Baada ya Mke Wake Kujifungua Mtoto wa Kike...!!!

$
0
0

BAADA ya mkewe, Nawal kujifungua mtoto wa kike, Mwanamuziki wa Bongo Fleva, Naftal Mlawa ‘Nuh Mziwanda’ ameamua kumzawadia wimbo ikiwa ni njia ya kumshukuru kwa kuwa ni mwanamke wa kipekee kwake kuliko aliowahi kutoka nao kabla hajaingia kwenye ndoa.

Akichezesha taya na Mikito Nusunusu, Nuh alisema anajivunia kupata mtoto wa kike aliyempa jina la Anyagile japokuwa alitamani angepata wa kiume lakini hana budi kumpokea kwa furaha ndiyo maana ameamua kumzawadia mkewe wimbo unaokwenda kwa jina la Anameremeta.

“Namshukuru Mungu kwa kunipa mtoto Jumatatu iliyopita, siku iliyofuata nikatoa wimbo huo ambao ni zawadi kwa mke wangu kwani ni mwanamke wa tofauti kwangu kwani kanizalia mtoto mzuri ambaye ndiye wa kwanza kwangu, nina furaha sana kwa kweli,” alisema Nuh Mziwanda.

Video:Kimenukaa..Mwanamke Aibuka na Kudai Amepewa Ujauzito na Gwajima Kisha Akatelekezwa,Adai Mtoto Aliyemzaa Anatabia Kama za Askofu Gwajima..!!!

Yanga Mdebwedo Yatolewa Ligi ya Mabigwa..ila Kushiriki Mashindano Haya

$
0
0


YANGA SC imeangukia Kombe la Shirikisho Afrika baada ya kutolewa katika michuano ya Ligi ya Mabingwa baada ya sare ya 0-0 na wenyeji, Zanaco jioni ya leo Uwanja wa Taifa wa Mashujaa, Lusaka nchini Zambia.

Matokeo hayo yanamaanisha Yanga inatolewa kwa mabao ya ugenini, baada ya kulazimishwa sare ya 1-1 kwenye mchezo wa kwanza wiki iliyopita Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam.

Yanga wataumia zaidi kwa kutolewa na Zanaco, kwani bao la kusawazisha la Wazambia hao Dar es Salaam lililopatikana dakika ya 78  kupitia kwa mshambuliaji wake Mghana, Attram Kwame lilikuwa la kuotea.

Na pamoja na hayo, wachezaji wa Yanga walikuwa wamezubaa kusubiri wapinzani wao watoe nje mpira kiungwana (Fair Play) baada ya mchezaji mwenzao, Obrey Chirwa kuangushwa.

Siku hiyo, Yanbga ilitangulia kwa bao la winga Simon Happygod Msuva dakika ya 39 baada ya kuwachambua mabeki wa Zanaco kufuatia pasi nzuri ya kiungo Mzambia, Justin Zulu.

Na ushindi huu unaifanya Zanaco iendeleze rekodi ya kuitupa nje Yanga kwenye michuano ya Afrika, baada ya mwaka 2006 pia kuwatoa katika hatua kama hii ya Ligi ya Mabingwa kwa jumla ya mabao 3-2, wakishinda 2-0 Lusaka baada ya kufungwa 2-1 Dar es Salaam.

Yanga sasa itamenyana na timu iliyofuzu hatua ya 32 Bora ya Kombe la Shirikisho kuwania tikeit ya kucheza hatua ya makundi ya michuano hiyo, wakati Zanaci inakwenda moja kwa moja hatua ya makundi ya Ligi ya Mabingwa.

Zifahamua Hatua Tatu Muhimu Anazopitia Mtu Mgonjwa Ili Kukifikia Kifo...!!!

$
0
0

wataalamu husema kifo huwa na hatua tatu

hatua ya kwanza ni kukikataa kifo,yaani hapa sasa mtu anahangaika kuhakikisha anaokoa uhai wake kwa kila namna


hatua ya pili ni makubaliano au mapatano, (wazungu husema kubargain) yaani hapa ndio anahangaika kweli mara mumkute katulia kama kafa mara yuko macho

hatua ya tatu ni kukikubali kifo (hapa sasa ndio mtu yuko tayari kufa nyie mnamuona kama amegive up) mtu huwa tayari kabisa kakubali matokeo kuwa ndio anaondoka. 

Arsenal Yahitaji Maombi ya Gwajima...Yachapwa 3-1

$
0
0

Craig Dawson akiwa hewani juu ya Nahodha wa Arsenal, Laurent Koscielny kuifungia West Bromwich Albion bao la kwanza dakika ya 12 katika ushindi wa 3-1 dhidi ya timu ya kocha Mfaransa, Arsene Wenger katika mchezo wa Ligi Kuu ya England jioni ya leo Uwanja wa The Hawthorns. Dawson alifunga mabao mawili na la tatu dakika ya 75, huku la pili la West Bromwich likifungwa na Hal Robson-Kanu dakika ya 55 na la kufutia machozi la Washika Bunduki wa London, likifungwa na Alexis Sanchez dakika ya 15

VIDEO: Tundu Lissu Alivyohutubia Kwa Mara ya Kwanza Baada ya Kuchaguliwa Kuongoza TLS

$
0
0
Mwanasheria Tundu Lissu ameibuka na ushindi wa kishindo katika uchaguzi wa Rais wa chama cha wanasheria Tanganyika ‘TLS’.
Katika uchaguzi huo uliofanyika katika ukumbi wa kimataofa wa mikutano wa Arusha ‘AICC’ Lissu alitangazwa mshindi kwa kupata kura 1,411 kati ya kura 1,682 zilizopigwa.


VIDEO: Mama Wema Atambulishwa Rasmi Chadema, Aitolea Povu CCM

$
0
0
Mama wa Malkia wa filamu Bongo, Wema Sepetu, Mariam Sepetu maarufu kwa jina la Mama Wema, leo Machi 18, 2017 amekaribishwa na kutambulishwa kwa uongozi wa CHADEMA jimbo la Kinondoni na kisha kupewa fursa ya kuzungumza machache, itazame video mpaka mwisho kujione tukio zima.

Tazama Video:

Miujiza ya Shekh Sharifu Rashid Je? Unapata Pesa Haika? Kusafisha Nyota na Kurudisha Mke/Mume Aliekuacha

$
0
0

MIUJIZA YA SHEKH SHARIFU RASHID KUTOKA BAGAMOYO PWANI. (RUDISHA MAHUSIANO YAKO NDANI YA MASAA 72 TU) ASANTE KWA KUENDELEA KUMPIGIA SIMU SHEKH SHARIFU RASHID KWA WALE WENYE MATATIZO NA WALE WANAOTOA SHUKRANI: SHEKH SHARIFU RASHID ni mtaalamu wa tiba mbalimbali za asili, anatumia kitabu cha quran dawa za asili dawa za kiarabu, na njiwa, Anakuvutia mpenzi alie kuacha au alie mbali, anazo dawa za mapenzi, nguvu za kiume, chango kwa kina mama, ngiri maji na n.k, anakuvutia mali zilizo potea au kudhulumiwa, pia anatoa Pete za bahati zilizoambatanishwa na jini mali, Wenye matatizo ya uzazi, jini mahaba, mapepo ya kichawi, vifungo vya kimaisha, ndoto mbaya za usiku, uelewa mdogo wa ufahamu shuleni kwa watoto wote, pia anauwezo mkubwa wa kumaliza kazi zilizoachwa na wataalamu wengine ndani ya masaa 48 tu, Pia anatibu kwa njia ya simu popote ulipo. WASILIANA NAE KWA WhatsApp na SIMU NO: +255 718-668347 na +255 767-204308 +255 685-224047 Email shekhsharifurashidi@gmail.com.

USHAURI: ni vyema kupiga simu kuliko kutuma sms ili upate huduma kwa haraka.

David Kafulila: Rais wetu Magufuli Una Nini na Makonda?

$
0
0
Moja ya kauli nzito ambayo Rais wetu amekuwa akiirudia na kuongea kwa uzito na msisitizo ni ile ya kwamba dhamira yake ni kuchukua hatua kwa uozo wowote kwa maslahi ya Umma hata kama ungemuhusu mke wake Janneth.

Ni bahati mbaya sana. tena sana. kwamba namna Rais anavovuta miguu kuhusu tuhuma dhidi ya RC wake huyu, zimepoteza kabisa imank ya kama kweli Rais wetu ni mkweli na anasimamia dhamira hiyo aliyotuaminisha.

RC ametuhumiwa vyeti, kashindwa kujibu kwa kutoa vyeti. imekuwa mjadala nchi nzima miezi sasa. mamlaka za Serikali zipo kimya. pengine zinaogopa mapenzi yako kwa RC huyu. na wewe tofauti na kawaida yako tumeona kwa RC huyu unavuta miguu tuuu. unashindwa japo kuzitaka mamlaka zithibitishe au zikanushe mzozo umalizike

Hilo halijaisha, zimefuata tuhuma za uhusiano kati ya RC na wanaosadikiwa kuwa wathhumiwa wa biashara za madawa. nchi nzima inasoma. zimewekwa mpaka kadi za magari na nyaraka za TRA. mtuhumiwa yupo kimya na mamlaka husika hazikanushi wala kuthibitisha.

Sasa leo kuna tuhuma za RC wako kuvamia kituo cha Clouds akitumia askari wako. na kwamba lengo ikiwa kushinikiza matakwa yake katika vita yake na Gwajima kuhusu vyeti, vita ambayo kwa maoni yangu imekuwa ya Gwajima vs Makonda sababu yako wewe Rais kutochukua hatua kwani inahusu uadilifu na agenda yako ya vyeti feki kwa maslahi ya taifa.

Mhe Rais binafsi sina chuki na wewe, nakwambia ukweli kama washauri wako hawakwambii, nikwamba namna ulivoshindwa katika suala la Makonda umethibitisha kwamba wewe sio mpenda haki na usawa kama ambavyo ulipenda tukuone siku zote. tuhuma na video inayosambaa kumwonesha RC wako anavamia Radio Clouds ni mfano mbaya kabisa unaopatikana kwenye nchi zenye tawala za hovyo kabisa kama Burundi na sio nchi kama Tanzania yenye historia kubwa Afrika.

Mhe Rais suala hili limechefua kila mzalendo nchi hii. na tunahoji uzalendo wako upo wapi sasa? Haya mambo anayofanya msaidizi wako ni kiburi na ushamba mkubwa ambao usingevumilika kwenye nchi yenye mfumo imara wa utawala! Imefika mahala hata ukichukua hatua baadae tayari umekwishakuondoa imani ya watu kwamba wewe ni Rais usiepepesa macho inapokuja suala la kuchukua hatua hata kwa mtu anaekuhusu! Imani ya Umma ndio mtaji kwa Kiongozi. ukiwa na imani ya Umma ni wazi hutaongoza kwa amri kwani kila kauli yako itapata ufuasi mkubwa. lakini ukipoteza imani ya Umma utahitaji dola kutawala.

Source:Jamii Forums

Diamond Afungua Mwaka na Deal Hii Kubwa ya Ubalozi...!!!

$
0
0


Msanii wa muziki Nassib Abdul maarufu, Diamond Platnumz ameteuliwa rasmi na kampuni ya GSM kuwa balozi wa kutangaza bidhaa mbalimbali za taasisi hiyo.

Akizungumza Jijini Dar es Salaam Afisa Masoko wa kampuni hiyo, Lauma Mohamed ameeleza kuwa Diamond
Platnumz ni msanii mkubwa sana ndani na nje ya Afrika, hivyo wanaimani atakuwa balozi mzuri kwa bidhaa zao
bora kwa watanzania.

Kwa upande wake Diamond Platnumz ameeleza kuwa anafarijika sana kuona wasanii watanzania wanapata nafasi
ya kuwa mabalozi, kwani wasanii ni wengi lakini yeye amepata heshima hiyo hivyo ana imani ni jambo jema kwa tasnia ya muziki.

Ameongeza kuwa hapo mwanzo bidhaa nyingi kwa mfano samani za ndani zilikuwa zinaagizwa nje ya nchi lakini kwa
sasa itakuwa rahisi kwani GSM kwenye duaka lao la ‘The New Home’ wanauza samani hizo halkadhalika nguo za watoto.

Licha ya kumtambulisha msanii huyo kama balozi mpya wa GSM wamezindua matangazo mapya mawili yaliyoigizwa na msanii
huyo pamoja na familia yake akiwemo Zari the Boss Lady na mtoto wao Tiffa, huku tangazo moja likiwa la nguo na lingine la samani za ndani.

Ahadi Tisa za Makonda 2016 Alizoshindwa Kuzitekeleza....!!!!

$
0
0

Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam, Paul Makonda ametekeleza mambo manane mapya ambayo hayakuwamo kwenye orodha ya ahadi zake za mwaka jana wakati alipoingia madarakani.

Siku chache baada ya kuapishwa, Makonda alikutana na wenyeviti wa Serikali za mtaa na kuwaeleza mikakati tisa aliyopania kuifanya katika kulibadilisha Jiji la Dar es Salaam.

Jumatano iliyopita, Makonda aliadhimisha mwaka wake mmoja tangu ateuliwe kushika wadhifa huo akielezea mambo 10 aliyoyafanya katika kipindi hicho na mengine 10 atakayoyafanya katika mwaka wake wa pili.

Wachambuzi wa masuala ya sayansi ya siasa wamempongeza kiongozi huyo na kusema hata kama hajatimiza baadhi ya ahadi, lakini amekuwa mbunifu kwa kujifanyia tathmini ukilinganisha na viongozi wengine.

Mipango aliyotekeleza

Mambo aliyotekeleza ambayo hayakuwamo kwenye orodha ya mikakati yake ni kampeni ya mti wangu, ujenzi wa wodi ya wagonjwa, vita ya dawa za kulevya, ujenzi wa ofisi ya Bakwata, kampeni ya uchangiaji wa damu, marufuku ya shisha na migogoro ya ardhi.


Ahadi tisa za 2016

Wakati alipoingia madarakani na kuzungumza na wenyeviti wa Serikali za mtaa, Makonda aliahidi usafi wa jiji, ofisi za Serikali kutokuwa za chama, kutenga maeneo ya biashara, sensa ya nyumba kwa nyumba, usalama wa raia na mali zao, watumishi hewa, kurudisha hadhi ya watendaji wa Serikali za mitaa, elimu na barabara.

Kwenye suala la usafi, Makonda aliahidi zawadi ya gari la Sh20 milioni au fedha taslimu kwa mwenyekiti ambaye mtaa wake utaongoza kwa usafi na Sh5 milioni kwa kila mjumbe wa mtaa husika. Pia, alisema zawadi hiyo itakayokuwa ikitolewa kila baada ya miezi mitatu na kwamba ingeanza Aprili Mosi, 2016.

Licha ya kusema kuwa amefanikiwa kufanya mambo kumi, Makonda ameshindwa kutekeleza ahadi tisa za mwaka jana alizoahidi mwaka jana.

Kuhusu usalama

Mwaka jana, Makonda aliahidi kutoa pikipiki 30 kwa Kanda Maalumu ya Polisi Dar es Salaam ili kuwawezesha askari kuwafuatilia watu watakaotupa taka ovyo barabarani.

Kwenye suala la usalama wa raia na mali zao, kiongozi huyo alisema kila mwenyekiti wa mtaa anapaswa kuhakikisha wananchi wake wanakuwa salama na hilo litafanikiwa endapo atakuwa na utaratibu wa kujua nani anafanya nini.

Ofisi za Serikali

Suala la ofisi za Serikali kuwa za chama, mkuu huyo wa mkoa alisema ofisi za Serikali ni kwa ajili ya kazi na siyo sehemu ya kufanyia siasa akisema katika uongozi wake haangalii chama, bali kusikiliza matatizo ya kila mtu.

Kutenga maeneo ya biashara

Katika kutenga maeneo ya biashara, Makonda alisema matamanio yake ni kuiona Dar es Salaam ya kisasa ambayo itakuwa na maeneo maalumu kwa ajili ya biashara ya vileo, magari, gereji na vifaa vya ujenzi.

Aliwaagiza wakurugenzi wa manispaa ifikapo Mei Mosi wawe wameainisha maeneo maalumu kwa ajili ya biashara hizo.

Barabara za biashara

Makonda aliahidi kuzungumza na wakurugenzi wa manispaa ili kuangalia namna ya kuandaa utaratibu wa kutenga barabara moja kwa kila kata kwa siku moja ili watu wafanye biashara.

Sensa ya wakazi wa Dar

Katika suala la sensa nyumba kwa nyumba aliwataka wenyeviti wa mitaa kupita kila nyumba katika mitaa yao kuorodhesha idadi ya watu wanaoishi na shughuli zao.

Alisema hiyo itasaidia pia kujua watu wasiokuwa na ajira hivyo kujipanga namna ya kuwasaidia.

Ahadi kwa polisi

Aliahidi kutoa Sh1 milioni kwa polisi atakayepambana na majambazi, huku milioni moja nyingine ikienda kwa mtu atakayesalimisha bunduki au bastola kituo cha polisi.

Watumishi hewa

Akizungumzia watumishi hewa, alitoa agizo: “Nitakapoagiza orodha ya watumishi hewa ije kamili, kinyume na hapo ofisa utumishi atalazimika kulipa hata madeni yaliyopita maana anaonekana ana nia ya dhati ya kufuga uozo huo.”

Ofisi za watendaji wa mitaa

Makonda pia aliwaahidi kuwajengea ofisi wenyeviti wote wa Serikali za mitaa na kuachana na habari za kupanga na kwamba, ifikapo Aprili Mosi atawakopesha pikipiki 1,000 ili ziwasaidie katika utendaji wao wa kazi na kuwasaidia kujikimu kimaisha.

Barabara

Kuhusu kero ya barabara, aliahidi kuzishughulikia, huku akiwashangaa wahandisi kwa kukaa ofisini.

Mafanikio 10 aliyotaja

Baada ya mwaka mmoja, mkuu huyo wa mkoa alibainisha mambo aliyoyafanya ndani ya mwaka huo mmoja.

Aliyataja mambo hayo kuwa ni kuendesha kampeni ya mti wangu inayohamasisha upandaji miti, ujenzi wa wodi za wagonjwa, vita dhidi ya dawa za kulevya na kutatua migogoro ya ardhi kwa wananchi.

Mambo mengine aliyoyafanya ni ujenzi wa Makao Makuu ya Baraza Kuu la Waislamu Tanzania (Bakwata), kampeni ya kuchangia damu, utengenezaji wa madawati kwa ajili ya shule za umma, uhakiki wa silaha, usafi wa jiji na kupiga marufuku matumizi ya shisha.

Ahadi mpya 10 alizotoa

Makonda alibainisha pia mambo mengine 10 atakayoyafanya katika mwaka wake wa pili wa uongozi akianza na kusimamia watumishi wa umma kutekeleza wajibu wao katika ngazi ya Serikali za mitaa mpaka ya mkoa.

“Nitapita kuanzia ngazi ya Serikali za mtaa na kila mtendaji atanieleza namna anavyowahudumia wananchi. Wananchi wanakuja mpaka ofisi ya mkuu wa mkoa kuleta kero zao wakati zinaweza kutatuliwa kwenye mitaa yao, hatuwezi kwenda namna hiyo,” alisema.

Makonda ambaye amejipatia umaarufu zaidi kutokana na vita dhidi ya dawa za kulevya, alisema atahakikisha kwamba anawahudumia waathirika wa dawa hizo kwa kuwapatia tiba ya uraibu wao.

Kuhusu wakazi wa mabondeni, alisema atahakikisha wote wanaoishi katika maeneo hayo wanahama na tayari ameagiza nyumba zao kubomolewa kwa ajili ya kulinda usalama wao.

Alisema wakazi waliopewa viwanja katika maeneo hayo ambao wana hati za viwanja hivyo, atawapatia ardhi sehemu nyingine kwa sababu ni uzembe wa watendaji wa Serikali na kusisitiza kwamba watakaobainika kuhusika na uzembe huo watawajibishwa.

Asifiwa wa wasomi

Mhadhiri wa Chuo Kikuu cha Dar es Salaam (UDSM), Dk Benson Bana alisema hadi hapo Makonda ameonyesha ushujaa kwa kuwa mkuu wa mkoa wa kwanza kuelezea utekelezaji wa ahadi zake. “Ingekuwa ni kugawa medali kijana huyu angepata licha ya makandokando yanayomzunguka, amefanya kazi nzuri, amethubutu na ni mbunifu,” alisema.

Alisema kwenye utendaji wa kazi jijini Dar es Salaam, kiongozi huyo wa mkoa anasikika zaidi katika uchapaji wa kazi kuliko viongozi wa kuchaguliwa wakiwamo wabunge na mameya.

Hata hivyo alisema ni wakati wa viongozi wengine kujitathmini na kuelezea yale waliyoyafanya.

Kuhusu ahadi ambazo hajazitekeleza, Dk Bana alisema muda bado na kwamba, ikiwa atadumu kwenye nafasi hiyo huenda utekelezaji wa ahadi zake ungekuwa juu zaidi.

Mhadhiri wa Chuo Kikuu cha Iringa (UoI), Jimson Sanga alisema mara nyingi viongozi huwa wanatekeleza mipango ambayo haikuwepo kwenye ratiba zao kutokana na kuibuka ghafla au umuhimu wake.

Alisema ni afadhali Makonda kwa kuwa ameonyesha kwa vitendo hata kama hakutimiza ahadi zake za awamu iliyopita kuliko, kukaa kimya bila kujifanyia tathmini ulikofanikiwa na kushindwa.

“Hatua ya kujifanyia tathmini naweza kusema ni ya kishujaa, wakuu wa mikoa wengine wanaweza kuiga hii itawafanya watimize yale wanayoyapanga na hivyo kuwaletea wananchi maendeleo,”alisema.

Mchambuzi wa uchumi mkoani Arusha, Dk Godwin Maimu alisema hatua ya kiongozi huyo kujitathmini ni nzuri japo anapaswa, kutekeleza ahadi zake kwa wananchi licha ya kuwa si kiongozi wa kuchaguliwa.

“Bado jiji la Dar es Salaam linakabiliwa na tatizo la wamachinga kutengewa maeneo kwa ajili ya biashara, amejitahidi lakini lazima awe na vipaumbele kwa masuala ya msingi anayodhani atayatekeleza,” alisema.
Viewing all 104689 articles
Browse latest View live




Latest Images