Quantcast
Channel: UDAKU SPECIAL
Viewing all 104709 articles
Browse latest View live

Siri ya Ushindi wa Lissu TLS Yaanikwa..Lowassa Ampa Neno Hili Baada ya Kutangazwa Mshindi..!!!

$
0
0

WAKILI machachari, Tundu Lissu, amechaguliwa kuwa Rais wa Chama cha Wanasheria Tanganyika (TLS) baada ya kupata ushindi wa kishindo katika uchaguzi uliofanyika mkoani hapa jana.

Lissu ambaye pia ni Mwanasheria Mkuu wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), sasa ataiongoza TLS kwa muda wa mwaka mmoja.

Ushindi wa Lissu unatajwa kuchagizwa na mambo mengi, huku makubwa kati ya hayo yakitajwa kuwa ni kauli ya Rais Dk. John Magufuli aliyoitoa Februari 2, mwaka huu akiwa katika maadhimisho ya Siku ya Sheria, Viwanja vya Mnazi Mmoja, Dar es Salaam, pale aliposema TLS imeshakuwa kama chama cha siasa baada ya kupata taarifa ya kuwapo kwa mgombea wa nafasi ya urais ambaye ni mwanasiasa na kutokana na hilo hawezi kuwateua majaji kutoka ndani ya chama hicho.

Kutokana na kauli hiyo, Lissu aliibuka na kusema hiyo ndiyo ilikuwa sababu ya msingi iliyomsukuma kuchukua fomu kuwania nafasi hiyo.

Jambo jingine linalotajwa, ni kauli ya Waziri wa Katiba na Sheria, Dk. Harrison Mwakyembe, aliyoitoa Februari 15, mwaka huu mjini Dodoma, pale aliposema kwamba Serikali haiwezi kuona TLS inajiingiza katika siasa na kama watataka hivyo, hatosita kuifuta Sheria ya TLS sura ya 307 iliyosababisha kuanzishwa kwa chama hicho.

Dk. Mwakyembe alitoa kauli hiyo mjini Dodoma alipozungumza na wanachama wa TLS wakiongozwa na aliyekuwa Rais wao, John Seka, walipomtembelea ofisini kwake.

Alisema kitendo cha kuwaingiza wanachama wanasiasa au viongozi wa vyama vya siasa ni kuruhusu mgongano wa masilahi.

Jambo jingine linalotajwa ni kitendo cha Lissu kukamatwa Februari 6, mwaka huu mjini Dodoma akiwa anahudhuria vikao vya Bunge kwa maagizo ya Polisi Kanda Maalumu ya Dar es Salaam na ilidaiwa alikamatwa ili achelewe kuchukua na kurudisha fomu za kuwania nafasi hiyo.

Kitendo cha mawakili Godfrey Wasonga na Onesmo Mpinzile ambao ni wanachama wa TLS, kufungua kesi Dar es Salaam na Dodoma wakipinga uchaguzi huo, ambazo hata hivyo zilitupwa ni sababu nyingine inayotajwa kuchangia ushindi wa Lissu.

Si hilo tu, pia jambo jingine linalotajwa kusababisha ushindi wake ni kitendo cha Lissu kukamatwa Machi 16, mwaka huu nyumbani kwake mjini Dodoma akiwa anajiandaa kwenda Arusha na kusafirishwa hadi Dar es Salaam kwa kosa la kutotii sheria na juzi kufikishwa Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu alikosomewa mashitaka matano ikiwamo kutoa maneno ya uchochezi yenye hisia za kidini.

Lissu alifikishwa mahakamani hapo, ikiwa ni siku moja kabla ya uchaguzi huo kufanyika jana na kulikuwa na taarifa kwamba pengine asingeweza kushiriki, lakini baadaye taarifa zilisema taratibu na kanuni za TLS zinaruhusu mgombea kuchaguliwa hata kama hatokuwapo katika ukumbi wa kupigia kura.      

Baada ya kuachiwa kwa dhamana Lissu alisafiri kwa ndege ya kukodi na kuwasili Arusha jioni na kwenda moja kwa moja Ukumbi wa Kituo cha Mikutano cha Kimataifa Arusha (AICC) ambako alisababisha wajumbe wa mkutano huo kulipuka kwa shangwe wakimshangilia huku wakimwita ‘jembe’, hali iliyomlazimu Seka kuwatuliza kwa kuwaambia kitendo hicho kitawakatisha tamaa wagombea wengine.



MATOKEO YA UCHAGUZI

Akitangaza matokeo ya uchaguzi huo katika Ukumbi wa Simba uliopo AICC, Mwenyekiti wa Kamati ya Uchaguzi, Dk. Kibuta Omung’wana, alisema idadi ya wajumbe waliojisajili walikuwa 3,556 na kati yao waliohudhuria ni 2,560 huku waliopiga kura ni 1,682 – zaidi ya nusu ya wajumbe waliohudhuria mkutano huo.

Kwa mujibu wa Dk. Omung’wana, nafasi ya urais iligombewa na wajumbe watano ambao ni Victoria Mandari, Godwin Mwaipongo, Fransis Stolla, Lawrence Masha na Lissu.

Licha jina la Masha kujitokeza katika karatasi ya wagombea. lakini wajumbe hawakumpigia kura baada ya kujitoa wakati akiomba kura.

“Naomba nianze kutangaza matokeo nafasi ya rais, Mwapongo amepata kura 23, Mandari amepata kura 176, Stola amepata kura 64 na Lissu amepata kura 1,411.

“Hivyo namtangaza Lissu kuwa ndiye mshindi katika nafasi ya Rais wa TLS,” alisema Dk. Omung’wana.

Pia alisema mshindi wa nafasi ya Makamu wa Rais ni Godwin Ngwilimi aliyepata kuwa Mwanasheria Mkuu wa Tanesco kabla kufukuzwa baada ya yeye mwenyewe kudai kupinga sakata la Akaunti ya Tegeta Escrow. Alipata kura 1,269 na Wakili Mary Mwasongwe kura 414.

Wajumbe waliochaguliwa ni Lambaji Madai, Jeremia Mtobesi, Aisha Sinda, Steven Aweso, Husein Mtobwa, Goodluck Walter na Madeline Kimei.

MWELEKEO MPYA TLS

Akizungumza baada ya kuapishwa, Lissu alisema chini ya uongozi wake itakuwa ni mwisho kwa chombo au mtu yeyote kukitishia chama hicho.

“Ni sisi wenyewe tulioruhusu Serikali ituingilie, iwe ni mwisho. hivyo tuanze mwanzo mpya na turuhusu siku mpya ije.

 “Iwe mwisho sasa kwa chama hiki kutishwa na mtu au chombo chochote, iwe mwisho kwa mawakili kutishwa na kukamatwa ovyo, iwe mwisho kwa mahakimu na majaji kupokea maelekezo.

“Mimi ni mwanachama wa Chadema ni kiongozi, ni mbunge, ni Mnadhimu Mkuu wa Kambi ya Upinzai Bungeni, nawahakikishia sitaileta Chadema ndani ya TLS na sitaipeleka TLS ndani ya Chadema.

“Sijagombea kama mwanachama wa Chadema bali nimegombea kama mwanachama wa TLS aliye ndani ya Chadema,” alisema Lissu ambaye pia ni Mbunge wa Singida Mashariki.

Akizungumzia uchaguzi huo, Wakili James Marenga, alisema umefanyika kwa uhuru, haki, uwazi na kwa kutumia kanuni zote za uchaguzi wa TLS za mwaka 2016.

Marenga alisema uchaguzi huo umeonyesha ni jinsi gani mawakili wanataka kuona mabadiliko ndani ya TLS itakayokuwa na uwezo wa kutoa maoni juu ya utawala wa sheria na masuala ya haki za binadamu.

LOWASSA

 Naye Waziri Mkuu wa zamani na mjumbe wa Kamati Kuu ya Chadema, Edward Lowassa, amempongeza Lissu kwa ushindi mkubwa alioupata.

Lowassa alisema ushindi wa Lissu ni joto la moto mkubwa wa mabadiliko uliotuama ndani ya mioyo ya Watanzania.

 “Uchaguzi ule naweza kusema ulikuwa kama kura ya maoni kwa wanasheria dhidi ya Serikali jinsi inavyoheshimu demokrasia ya umma na utawala wa sheria,’’ alisema Lowassa.

PROFESA MKUMBO

Mhadhiri wa Chuo Kikuu Dar es Salaam (UDSM), Profesa Kitila Mkumbo, akizungumza na MTANZANIA Jumapili kwa simu jana, alimpongeza Lissu kwa kushinda nafasi hiyo na alisisitiza kuwa ushindi wake umechangiwa na Serikali iliyokuwa ikimfanyia kampeni.

 “Ushindi wake ulitarajiwa, ulifanyiwa kampeni na Serikali, tunampongeza na tunawapongeza wanasheria kwa weledi katika kusimamia taaluma na kuonyesha wanaweza kufanya uamuzi wao binafsi bila kujali mashinikizo ya viongozi,” alisema Profesa Mkumbo.

Pia alisema wanasheria wameonyesha utashi wa kitaaluma jambo ambalo ni la kishujaa na endapo  matokeo yangempa ushindi mtu tofauti na Lissu yangeleta  picha mbaya katika jamii.

RIPOTI YA FEDHA

Pia mkutano huo umetishia kuuburuza mahakamani uongozi unaomaliza muda wake kutokana na kunusa harufu ya ufisadi wa Sh milioni 78 za ada na Sh milioni 34 zilizokosa viambatanisho katika taarifa ya fedha ya mwaka 2015/2016.

Kutokana na kuibuka kwa mjadala mzito juu ya fedha hizo kwa zaidi ya saa tatu bila kufikia makubaliano, ndipo waliamua kuunda kamati ya watu watano itakayoshirikiana na uongozi mpya kuchunguza tuhuma za ufisadi huo.

Katika mkutano huo uliokuwa ukiongozwa na Seka, uliwasukuma wajumbe kutoa hoja mbalimbali zilizolenga kujua juu ya fedha zao wanazochanga kupitia ada za uanachama, baada ya taarifa hiyo kuwasilishwa mbele yao huku ikiwa imeonyesha makosa ya kiuhasibu.

Wajumbe watano wa kamati itakayoshughulikia kuchunguza tuhuma hizo ikishirikiana na uongozi mpya inaudwa na Rweikiza Rweikama, Lawrance Masha, Nicholaus Duhia, Magdalena Sylvester na Ana Julia.

Kimenukaaa..Kingunge Aibuka na kuwataja Wasaliti Ndani ya CCM,Amtaja Kikwete na Kinana,Ataka Watimuliwe Haraka...!!!

$
0
0

MWANASIASA mkongwe, Kingunge Ngombale Mwiru, amesema hatua ya Chama Cha Mapinduzi (CCM) kuwaadhibu makada wake hivi karibuni ni mwendelezo wa makosa yaliyoongozwa na kuratibiwa na viongozi wakuu watatu wa chama hicho wakati wa mchakato wa kumpata mgombea urais takribani miaka miwili iliyopita.

Kingunge mmoja wa waasisi wa CCM aliwataja viongozi hao ambao alisema kimsingi ndio wanapaswa kubeba dhamana ya usaliti ndani ya chama hicho kuwa ni Mwenyekiti mstaafu, Jakaya Kikwete, Makamu Mwenyekiti Bara, Philip Mangula na Katibu Mkuu,  Abdulrahman Kinana.

Kingunge aliyasema hayo katika mahojiano maalumu na MTANZANIA Jumapili yaliyofanyika  wiki hii katika makazi yake yaliyoko eneo la Victoria, Dar es Salaam.

Katika mahojiano hayo ambayo yalidumu kwa saa moja na dakika 22,  Kingunge ambaye amepata kufanya kazi na serikali za awamu zote nne, alizungumzia demokrasia, haki, utendaji wa Serikali ya awamu ya tano na hali ya siasa, ikiwamo uamuzi wa hivi karibuni uliochukuliwa na CCM.

Kuhusu yaliyotokea wiki iliyopita ndani ya CCM, ikiwa ni pamoja na kuwaadhibu wanachama wake kwa makosa ya usaliti, Kingunge alisema si mapya bali ni mwendelezo wa makosa yaliyotokea wakati wa mchakato wa kumpata mgombea urais kupitia chama hicho mwaka 2015.

Aliyataja makosa yenyewe kuwa ni yale ya ukiukwaji wa taratibu na kanuni za kumpitisha mgombea wa urais.

Alisema uongozi wa CCM wa wakati huo chini ya uenyekiti wa Kikwete, Makamu Mwenyekiti Bara, Mangula na Katibu Mkuu Kinana, kwa pamoja walifanikiwa kushawishi Kamati Kuu (CC) kuvunja Katiba na kanuni za chama hicho.

Kingunge ambaye hii si mara yake ya kwanza kueleza kile alichokiona ni ukakasi wa mfumo uliotumika na vikao vya juu vya CCM kumpata mgombea wa kiti cha urais, alihoji katika mazingira ya leo ya kuwashuku fulani ni wasaliti wakati unajua kuna watu walikiuka taratibu na kanuni za chama, ni nani anayepaswa kuitwa msaliti?
Kwa muktadha huo, alisema CC ilishindwa kufanya kazi yake kama inavyoelekezwa na katiba na kanuni zake, hivyo ikajikuta imekataa kuwasikiliza, kuwaona na kuwahoji wagombea 38 wa urais, badala yake wakakubaliana na mapendekezo ya majina yaliyotoka kwa Kikwete.

“Huko kwenye NEC baada ya vurumai kubwa ndiko wakapatikana hao wagombea watatu ambao walipelekwa kwenye mkutano mkuu na mwisho wake akapatikana Bwana Magufuli,” alisema.

Kingunge alisema kuwa imekuwa kama alivyosema Mwalimu Nyerere, kwamba ukishakula nyama ya binadamu hutakoma, utaendelea tu.

KUFUKUZA WANACHAMA

Akizungumzia hatua ya CCM kuwafuta uanachama baadhi ya viongozi, kuwapa onyo na kuwasamehe wengine kwa sababu ya kile kinachoitwa usaliti, mwanasiasa huyo alisema anastaajabu adhabu hiyo kuwagusa baadhi wakati msingi wake ni mchakato wa kumpata mgombea urais 2015.

“Kwa hawa waliohukumiwa, wamehukumiwa kwa usaliti wa kuendana na mchakato kumpata mgombea wa urais, sasa swali linakuja, hapo katika mchakato wa kumpata mgombea urais, aliyesalitiwa ni nani? Ni CCM ndiyo iliyosalitiwa ama kuna mgombea fulani maalumu ambaye ndiye aliyesalitiwa?

“Kwa ninavyoijua Katiba ya CCM na kanuni zake, hadi wakati ule wa kumtafuta mgombea, mazingira yalikuwa ya ushindani huria (huru),” alisema.

Kwa mtazamo wake, alisema wagombea wote walifuata taratibu za kuchukua fomu hadi kutafuta wadhamini na kuhoji hadi katika hatua hiyo nani ni msaliti na alimsaliti nani?

“Kwa sababu huo ulikuwa ni utaratibu ndani ya CCM… wadhamini waliomuunga mkono mmoja hawakuruhusiwa kwa mwingine. Sasa wadhamini waliomuunga mkono ‘A’ ndio walikuwa wasaliti kwa sababu hawakuwaunga mkono wengine waliobaki?” alihoji Kingunge.

Kwa mujibu wa Kingunge, vikao vya juu vya CCM wajumbe walikuwa na haki ya kujadili sababu za baadhi ya wagombea kuwamo na wengine kutokuwamo.

 “Sophia Simba alimsaliti nani, Madabida alimsaliti nani na katika ngazi gani? Ndiyo maana nasema hili suala lote hili ni mwendelezo wa yaliyotokea 2015, Agosti 10 kule Dodoma, pale ambapo uongozi wa chama, kundi la watu watatu likiongozwa na Kikwete ndilo lilifanya CC na jopo la wazee wastaafu washirikiane na wakubaliane kuvunja katiba na kanuni na wao kuchukua jukumu la kuteua watu watano nje ya utaratibu uliowekwa na chama,” alisema.

Alihoji wanachama waliofukuzwa wamemsaliti nani kwa sababu wakati wa mchakato kila mwanachama alikuwa na mgombea wake anayemuunga mkono.

MAAMUZI YA KAMATI YA MAADILI

MTANZANIA Jumapili lilimkumbusha kwamba majina hayo yalipitishwa katika Kamati ya Maadili ya chama.

Lakini katika maelezo yake Kingunge alifafanua kwamba Kamati ya Maadili wakati wa kipindi hicho ilikuwa ni kitengo ndani ya Ofisi ya Katibu Mkuu, hivyo haitambuliwi ndani ya Katiba ya CCM.

Alisema kwa sasa anaona kuna jitihada za kutaka kuibadili Kamati ya Maadili kiwe kikao rasmi.

“Katika suala la maadili ndani ya chama, mkuu wa maadili ni NEC na katika ngazi zote za chama kuanzia taifa hadi matawi,” alisema.

Kwa mujibu wa Kingunge, kuanzia mwaka 1982 wakati ulipoanzishwa mfumo mpya wa chama, ilikuwapo Tume ya Udhibiti na Nidhamu.

Alisema tume hiyo ilikuwa na hadhi ya idara ya chama, lakini baadaye yakafanyika marekebisho, hivyo suala la maadili halikujumuishwa katika hadhi ya idara ya chama na badala yake likawa ndani ya kitengo ambacho kipo chini ya Ofisi ya Katibu Mkuu.

“Kwa hiyo, Kamati ya Maadili haina majukumu ya kikatiba ya kuwa na kauli juu ya nani awe au asiwe mgombea, lakini inaweza kuishauri CC na NEC na kamati hiyo haiwezi kutoa ushauri wa kuvunja katiba na anayeshauriwa ndiye mwamuzi,” alisema.

MADARAKA YA KIIMLA

Akiendelea kufafanua hoja hiyo, Kingunge alisema madaraka yanatakiwa kujengeka kwa misingi ya hoja na si misingi ya kiimla.

Alisema pamoja na kwamba yeye si mwanachama wa CCM kwa sasa, lakini ana haki za kutoa maoni juu ya uamuzi huo kama raia wa Tanzania.

Kwamba kama raia wa nchi hii, anataka vyama vya siasa vilivyopo vijengeke katika misingi ya demokrasia.

“Hatuwezi kuwa na vyama feki feki tu, kwa hiyo inavyotokea kwamba chama cha siasa hapa nchini kinafanya vitabia ivitakavyo bila kusimamia misingi ya demokrasia, sisi kama raia tuna haki ya kukihoji na kama kimekosea tutawaambia wamekosea na katika hili CCM imekosea,” alisema.

Alisema pamoja na kwamba ameachana na CCM, lakini ana historia na chama hicho. Alitanabaisha kuwa yeye ni miongoni mwa waasisi wa CCM na alikuwa kwenye jopo la watu 20 waliounda kamati ya kuandaa rasimu ya katiba ya chama hicho (1976-1977).

Alisema kuwa ndani ya CCM amehusika na utangulizi na yaliyomo katika katiba ya chama hicho.

“Watu waliomo CCM waelewe, ile katiba ni kitu kikubwa sana na tuliiunda ili ibebe mema yote ya TANU na ASP, ibebe misingi iliyotuongoza kufanya mambo makubwa sana katika TANU na ASP, misingi hiyo ni demokrasia, haki, usawa na utu.

“Sasa wanaodai kwamba wanaongoza CCM wakifanya mambo ambayo hayafanani na ile tuliyoiunda, mimi inanipa tabu na katika hilo siwezi kunyamaza nitasema tu… naweza nikasema nyinyi CCM yenu mliyoiunda ni nyingine, siyo yetu ya akina Kingunge na wenzake,” alisema.

CCM INAINGIA PAGUMU

Kingunge alisema CCM inajiingiza katika hali ngumu, kwa sababu ya baadhi ya viongozi ndani ya chama hicho kujiaminisha kuwa wanajua kila kitu.

“Hii inatokana na jambo moja, lazima niliseme. Binadamu sisi tumepewa vichwa na ndani ya vichwa kuna akili ambayo imepewa kazi ya kufikiri, lakini hakuna binadamu anayejitosheleza katika masuala ya kufikiri, sasa ukifika mahala kwamba baadhi ya binadamu wanajiaminisha kwamba wao wanajua kila kitu, ndio chanzo cha matatizo,” alisema.

CCM HAITAKI MIJADALA

Kingunge alisema kwa yanayofanywa sasa ndani ya CCM, ni wazi inaonekana haitaki mijadala.

 “Mkutano Mkuu wa Taifa ulifanyika kwa saa tatu, mkutano ambao ulikuwa na jukumu la kujadili mabadiliko ya katiba… saa tatu umwekwisha kila kitu… sasa nasema tunalo tatizo katika nchi hii, kwanza mijadala nje ya chama haitakiwi, sasa hawa wenye nchi yao kwahiyo itakuwa ada yao ni kupewa amri tu?

“Wanapewa amri na watawala na ada yao itakuwa ni kutii amri za watawala? Hakuna kuhoji. masuala yanayotokea katika nchi yao, hawa raia hawana haki ya kuyajadili,” alisema.

Akithibitisha kauli yake hiyo, Kingunge alitolea mfano jinsi wale wanaotangaza baa la njaa wanavyopewa adhabu.

NCHI IENDESHWE AU IONGOZWE?

Alisema nchi imefika mahali sio pazuri kwa sababu ya viongozi na alitoa mifano ya njia mbili za kufuatwa.

“Kuna njia mbili, ama nchi iendeshwe au nchi iongozwe, kama mnataka nchi iongozwe maana lazima mkubali wananchi wenyewe watoe maoni yao halafu mnakwenda, lakini mnataka kuiendesha nchi na mnajua matokeo ya nchi kuiendesha,” alisema.

Aliongeza kwa kusema kuwa ni lazima kila Mtanzania, kuanzia viongozi, wote kujitahidi kuondoa munkari na hasira.

“Hamuwezi kuwa na nchi viongozi wanaonekana wana hasira tu na raia nao wataonekana kuwa na hasira, tukifika hapo nchi haiendi. Nasema tuwe watulivu sote, wakubwa kwa wadogo ili tuwe wanyenyekevu kwa sababu sisi ni watu tu, ukiwa mkubwa ni mtu, ukiwa mdogo wewe ni mtu.

“Mkubwa mambo yake ya msingi anayoyafanya ni yale yale anayoyafanya mtu mdogo, kwahiyo sisi wote ni watu ndiyo maana Katiba ya CCM inasema binadamu wote ni sawa na kila mtu anastahili heshima ya kutambuliwa utu wake,” alisema.

Aliongeza kwa kusema kama Watanzania wote wanataka kuijenga nchi, wanaweza kuijenga, lakini kama wanataka kuibomoa wataibomoa.

CCM IMECHOKA

Kingunge alikwenda mbali na kusema kwamba CCM si kwamba imeishiwa pumzi tu, bali imechoka.

Alisema mazingira hayo yanakifanya chama hicho kukosa nguvu ya kwenda mbele kwa sababu ndani yake kumekosekana umoja.

“Hakuna suala kubwa katika ‘organization’ (taasisi) yoyote kama umoja, muundo wowote wa watu wanaotaka kufanya jambo kwanza kabisa ni umoja, Mwalimu Nyerere alitufundisha wakati ameanzisha TANU na wenzake 17. Alisema suala la kwanza ni umoja, Waafrika tuungane kumtoa mkoloni.

“Na katika harakati za kujenga umoja kunatokea vitu vingi, zinatokea nguvu nyingine zinazotaka kuwaweka pembeni ili mtengane… uongozi unatakiwa kuelewa masilahi ya chama ni nini… kuna kuelewa masilahi yako na vikija vishawishi vya kujitenganisha na wenzako, unajiuliza kama linafifisha harakati au linaendeleza, hivyo unajirudi na kuendelea na mapambano,” alisema.

WALIFUKUZWA CCM

Katika hatua nyingine, Kingunge aliwatia moyo watu waliovuliwa uanachama wa CCM na wale waliopewa onyo.

Aliwataka wasibabaike kwa sababu kama bado wanaipenda CCM waombe warudishwe.

Lakini akasema: “Dunia si CCM, kwa sababu kabla yake kulikuwa na TANU. Kwani binadamu hawakuishi?”

Elibariki Kingu: Kwa Hili la Makonda, Naomba Niwe wa Kwanza kufukuzwa CCM

$
0
0
Nilisema Nitanyamaza lakini Nimeshindwa. Nimethibitisha bila mashaka Clouds kuvamiwa na Rc akiwa na ulinzi na askari wenye silaha mpaka kwenye matangazo.

Najua hofu mliyonayo watanzania juu ya huyu Rc.

Ikiwa mamlaka zitaendelea kufumbia macho.Mimi Elibariki Immanuel Kingu mbunge wa CCM nitakuwa wa kwanza kufukuzwa CCM kama kupinga matendo maovu ya Rc huyu itaonekana ni usaliti kwa nchi.

Haiwezekani Rais wetu atukanwe kila kona kwa matendo ya mtu huyu.

Wana CCM ukimya wetu kwenye hili halikubaliki.

Magufuli juzi ametuliza Dodoma kwa kuongea kwa hisia.Idara za usalama kweli mmeamua kuacha tutukanwe?

Naomba sasa niweke kumbukumbu sawa najua mnamchafua kila anayempinga RC huyu kwa matendo yake ambayo yanakiuka utawala bora.

Naomba niwe wa kwanza kufukuzwa CCM kwa kumpinga Rc Makonda

Elibariki Immanuel Kingu
Mbunge.

Source:Jamii Forums

Nisha: Sitamtambulisha mpenzi wangu tena

$
0
0

Msanii machachari wa bongo movie Nisha Bebe amesema hatorudia kosa la kumtambulisha mpenzi wake kwa sasa bali atamtambulisha mume wake akiwa tayari.

Akiongea kupitia eNewz ya EATV, Nisha amesema  "Sirudii makosa kwa sasa hivi wasitarajie kumsikia mpenzi wangu wala kumtambulisha kwa jamii mtu nitakaye kuja kumtambulisha ni mume wangu ambaye tayari nishampata ila tunachunguzana tabia kwanza kwa sasa" aliongea Nisha

Hata hivyo Nisha aliendelea kusema kwamba hata kama itamchukua muda mrefu kujuana tabia na mume wake mtarajiwa haijalishi ili mradi waweze kujuana vizuri na
"Watu wasitarajie kuona dalili yeyote ya kumtambulisha mpenzi wangu kabla hatujaoana" Alimalizia Nisha.

Exclusive: Askofu Gwajima atoa cheti chenye matokeo ya kidato cha nne ya Daudi A. Bashite

$
0
0
Askofu Gwajima atoa cheti cha Daudi Albert Bashite (S0546/0016) na kusema kuwa alipata F masomo yote ya Sekondari hadi Bible Knowledge.

Matokeo hayo ni ya Kidato cha nne, Shule ya Sekondari Pamba.

Alama ni kawa ifuatavyo...
Civics - F
History - F
English - F
Geography - F
Biology - F
Kiswahili - F
Mathematics - F
Physics - F
Chemistry - F
Bible Knowledge - F


Source: JF

Viwanja Vinauzwa Bei Rahisi....

$
0
0

Viwanja vinauzwa: Mapinga, Kimele Km 3 Kutoka Bunju Sokoni. Ukubwa 20*20 bei mil 5, ukubwa 20*30 bei mil 7, ukubwa 35*35 bei mil 13. call 0758603077

Yanga Majanga Matupu...Kocha Mpya Lwandamina Aeleza Kinachitesa Yanga

$
0
0
Yanga imetolewa katika mashindano ya Ligi ya Mabingwa Afrika baada ya kulazimishwa suluhu na Zanaco mjini Lusaka jana.

Suluhu hiyo imeifanya Zanaco kunufaika na bao walilopata katika mchezo wa kwanza jijini Dar es Salaam wiki iliyopita walipoilazimisha Yanga sare ya 1-1 kwenye Uwanja wa Taifa, hivyo bao la ugenini kuwapa faida.

Kwa matokeo hayo, Yanga inashuka katika Kombe la Shirikisho Afrika, ikiwa miongoni mwa timu 16 zitakazotoka Ligi ya Mabingwa Afrika na kucheza mchezo mmoja kabla ya kutinga hatua ya makundi ya mashindano hayo.

Lwandamina afunguka

Kocha wa Yanga, George Lwandamina amesema anapata wakati mgumu katika kazi yake kutokana na kutofanya maandalizi ya mwanzo wa msimu na mabingwa hao wa Tanzania.

Lwandamina alisema hali ya majeruhi inayowaandama wachezaji wake pamoja na kushindwa kubadilika kwa aina ya uchezaji kwa nyota wake vimechangia hali waliyonayo sasa ya kushindwa kuwa na kiwango cha uwiano sawa.

Katika kipindi cha hivi karibuni baadhi ya wachezaji nyota wa Yanga kama Donald Ngoma, Amissi Tambwe na Thaban Kamusoko wamekuwa wakisumbuliwa na majeraha, jambo ambalo limeipa timu hiyo wakati mgumu.

Kocha huyo aliyejiunga na Yanga mwishoni mwa mwaka jana, alisema kama wachezaji wanapata maandalizi mazuri mwanzoni mwa msimu, wanaweza kucheza msimu mzima kwa kiwango cha juu lakini kama hawakufanya hivyo ni ngumu kuwabadilisha.

“Katika soka hakuna msingi mkubwa kama maandalizi ya mwanzo wa msimu. Wakati huu ndiyo mchezaji anajengewa uwezo wa kucheza kwa kiwango bora kwa msimu mzima,” alisema kocha huyo wa zamani wa Zesco United ya hapa Zambia.

“Mchezaji akifanya mazoezi kwa wiki sita kabla ya msimu kuanza ndipo anaongeza kasi ya mishipa kusambaza damu mwilini. Utimamu wa mwili wake pamoja na uvumilivu mchezo, tofauti na hapo ni ngumu kusonga mbele,” alisema kocha huyo.

Lwandamina alisema kutokana na kubanwa na mechi nyingi za mashindano, ameshindwa kuingiza falsafa yake moja kwa moja klabuni hapo kwani muda mwingi anautumia katika kuangalia wachezaji wanapumzika vipi na wanawezaje kupata utimamu wa kucheza mechi inayofuata.

“Ratiba imebana, kuna wakati ninatamani kuwafundisha vitu vipya lakini hivi navyo vinahitaji muda.

“Tumekuwa na mechi mfululizo msimu huu, mara nyingi ninatazama namna ya kuwasaidia wachezaji kurejesha viwango vyao kwanza.

“Ni vigumu kufundisha katika mazingira hayo hasa unapotaka kuleta vitu vipya. Ni lazima utazame wachezaji ulio nao kama wana uwezo wa kubadilika, vinginevyo inakuwa tatizo,” alisema kocha huyo.

Mchezo ulivyokuwa

Yanga ilishuka uwanjani ikiwa na mabadiliko kadhaa katika kikosi chake tofauti na kile kilichocheza mchezo wa Dar es Salaam. Nahodha Nadir Haroub ‘Cannavaro’ alianzia benchi huku Vincent Bossou na Kelvin Yondani kuanza katika nafasi ya ulinzi wa kati.

Kipindi cha kwanza Yanga ilitawala mchezo kwa kiasi kikubwa na mara nyingi ilitengeneza mashambulizi yake kutokea katikati kwa Thaban Kamusoko.

Kurejea kwa Haruna Niyonzima katika kikosi kuliongeza umiliki wa mpira na Zanaco walilazimika kutumia muda mwingi kujilinda na kushambulizi kwa kushtukiza.

Nafasi ya wazi zaidi kwa Yanga katika kipindi cha kwanza ilipatikana dakika ya 30, wakati Kamusoko alipopokea mpira akiwa ndani ya eneo la hatari, lakini alishindwa kufanya uamuzi na kutoa pasi fyongo.

Mashambulizi mengine makubwa ya Yanga yalitokea dakika ya 14 na 17, kwa Obrey Chirwa na Geofrey Mwashiuya lakini hata hivyo hawakuwa makini na lango.

Live Video: Askofu Gwajima akijibu tuhuma kuwa amezaa na muumini wake

$
0
0
Siku za hivi karibuni kumekuwa na makanda wa video unaosambazwa kwenye mitandao ya kijamii ambao anaonekana mwanamke mmoja akihojiwa akidai kuwa amezaa mtoto na Kiongozi wa Kanisa la Ufufuo na Uzima, Askofu Josephat Gwajima.

Katika video hiyo anaonekana mtangazaji wa Clouds Fm/Tv, Soudy Brown akimhoji mama huyo ambaye alisema kuwa amezaa mtoto na Askofu Gwajima. Mwanamke huyo anaeleza kuwa kazi yake yeye alikuwa akifanya usafi katika kanisa hilo kipindi likiwa Kawe kabla ya kuhamia Ubungo.

Kufuatia Tuhuma hizo, kiongozi huyo amesema kuwa leo atatolea ufafanuzi suala hilo huku akidai kuwa ni watu wamejipanga kumchafua. Hapa chini ni video ya Askofu Gwajima akihubiri Kanisani kwake. VIDEO:

Erick Shigongo...Paul Makonda Hafai Kuwa Kiongozi Kwa Anachodaiwa Kufanya Clouds FM

$
0
0

From @ericshigongo - Wiki Chache zilizopita nilimsifia Paul Makonda hapa, lakini kwa anachodaiwa kukifanya Clouds usiku, nafuta sifa nilizompa! Hafai kuwa kiongozi. Kwa Mahali tulipo kama taifa hatuhitaji kiongozi wa aina hii hata kidogo.

Nampenda sana Rais John Pombe Magufuli, sipo tayari kuona rais wangu anatukanishwa na iasi hiki na matendo yanayofanywa na Mkuu wa Mkoa.

NITAMPINGA MAKONDA KILA ANAPOFANYA YASIYOSTAHILI NA NITAMTETEA RAIS WANGU ANAPOTUKANISHWA!

E.J Shigongo

Mengi Naye Ashindwa Kujizuia Kwa Haya ya Leo..Asema Haya kuhusu Washauri wa JPM

$
0
0

Mengi Naye Ashindwa Kujizuia Kwa Haya ya Leo..Asema Haya kuhusu Washauri wa JPM

Tundu Lissu Afunguka..Amshauri Rais Atengue Uteuzi wa Mkuu wa Mkoa wa Dar..

$
0
0

Kwa heshma na taadhima naomba nikupinge Mh. Rais: His name is Daudi Bashite not Paul Makonda. I hope hutonilaza ndani kwa kukupinga Mh. Rais Lissu....
Waheshimiwa wananchi wa Tanzania. Nimesikia taarifa za kuvamiwa kwa kituo cha habari cha Clouds Media.

Mkuu wa Mkoa katika nchi yetu sio kamanda wa kikosi chochote cha jeshi lolote lililoanzishwa kwa mujibu wa sheria.
Mamlaka aliyo nayo kwa mujibu wa sheria za nchi yetu hayajumuishi kuamrisha askari jeshi au polisi au usalama wa taifa kuvamia makazi au sehemu za biashara za watu.
Mkuu huyu wa mkoa hastahili kuendelea kwenye madaraka hayo kwa siku moja zaidi. Hana tena sifa wala maadili wala sababu za kuendelea kuwa kiongozi wa umma.
Namshauri Rais Magufuli atengue uteuzi wake haraka iwezekanavyo kabla hajachafua zaidi taswira ya serikali na ya Rais Magufuli mwenyewe.
Aidha, namshauri Rais Magufuli amchukulie hatua stahiki kamanda au mkuu wa kikosi chochote cha Jeshi lolote aliyeruhusu askari wake kutumiwa na Paul Makonda kwa namna iliyoripotiwa.
Tundu Antiphas Lissu, Rais, Chama cha Mawakili wa Tanganyika.

Man U Yamchapa Mtu 3-1, Yapanda Nafasi ya 5

$
0
0


Marouane Fellaini (kushoto) akishangilia na Jesse Lingard (kulia) baada ya wote kufunga katika ushindi wa Manchester United wa 3-1 dhidi ya wenyeji Middlesbrough leo kwenye mchezo wa Ligi Kuu ya England Uwanja wa Riverside. Fellaini alifunga la kwanza dakika ya 30, Lingard la pili dakika ya 62 na la tatu lilifungwa na Antonio Valencia dakika ya 90 na ushei, wakati la kufutia machozi la Boro lilifungwa na Rudy Gestede dakika ya 77.

Waziri Nape: Nakwenda Clouds Media kuona kilichotokea, Ni kuhusu Ishu ya RC Makonda

$
0
0

Waziri Nape: Nakwenda Clouds Media kuona kilichotokea, Ni kuhusu Ishu ya RC Makonda
Kufuatia kusambaa kwa video mitandaoni ikiaminika ni mkuu wa mkoa wa Dar es salaam, Paul Makonda akiingia Clouds Media akiwa na askari, Waziri wa habari, utamaduni, sanaa na michezo, Nape Nnauye kupitia account yake ya twitter ameyaandika haya……

Zanzibar Yasalimu Amri..Yailipa Tanesco Kiasi Hichi

$
0
0

Zanzibar yapunguza deni, yalipa Tanesco Sh 10 bilioni

Dar es Salaam. Waziri wa Nishati na Madini, Profesa Sospeter Muhongo amesema kuwa Serikali ya Mapinduzi Zanzibar(SMZ) imeanza kulipa deni lake inalodaiwa na Shirika la Umeme Tanzania(Tanesco).

Taarifa iliyotolewa leo na Mkurugenzi wa Mawasiliano ya Rais, Ikulu, Gerson Msigwa imesema kuwa Profesa Muhongo amesema SMZ imelipa kiasi cha Sh10 bilioni na itaendelea kulipa deni hilo hadi litakapomalizika.

Njia 5 za Kudumisha Mahusiano ya Kimapenzi..!!!

$
0
0

Japo inasemwa kuwa mapenzi hayana njia moja ya kufuatwa lakini kuna vitu ambavyo vinajulikana kuchangia katika kuboresha mahusiano baina ya wapenzi.

Mahusiano ya mapenzi yenye kudumu ni sharti yapandwe katika udongo wenye rutuba kama ulivyo mmea,yatahitaji maji ya kumwagilia na mbolea ya kukuzia.  Na zaidi ya yote yanahitaji muda wa kukua kabla matunda kuonekana.

Uaminifu

Kumwamini mwenza wako ni jambo la msingi sana katika kudumisha mahusiano. Usimshuku mpenzi wako kuwa si muaminifu bila ushahidi wowote.

Kushukiwa kukosa uaminifu pasipo ukweli inasononesha sana na kumkosesha raha mpenzi wako.
Imesemwa na wanafalsafa wa mawazo ya binadamu kuwa “Unachofikiri na kuamini kinatokea” hivyo unashauriwa kutofikiri vibaya juu ya mpenzi wako kwani haileti afya katika mahusiano.

Hali kadhalika na wewe uwe mwaminifu na mwenye kusema kweli mara zote. Ongeeni juu ya mipango na mawazo yenu bila kufichana.

Watambulishe kwa mpenzi wako ndugu ,jamaa na marafiki wakaribu ili kumpa mwenza wako amani.

Weka muda kwajili ya Mwenza wako.

Mahusiano mazuri kati ya wapenzi yanahitaji muda wa wapenzi hao kukaa pamoja. Wapenzi wasio na muda wa kukaa wana hatari ya kupoteza mvuto wa mahusiano yao na hivyo kuhatarisha uhai wa mapenzi kati yao.
Kama wapenzi wapo mbali mbali basi wanahitaji kuweka muda wa kuongea kila inapowezekana.
Tafuta muda wa kutoka pamoja,hata kama mtaenda mkahawani kunywa chai au juisi tu,inatosha sana na inawaweka karibu zaidi.

Mawasiliano

Mawasiliano ni muhimu sana baina ya wapenzi.

Hata kama umebanwa na kazi pata dakika chache za kuongea na mpezi wako na kumtaka hali. Andika hata ujumbe wa maneno au barua pepe. Mwambie mpenzi wako ulipo kila mara inapobidi ili kumjengea imani na wewe na kumpa amani moyoni. Tuma ramani ya mahali ulipo kama unatumia simu ya “Smart” (Tuma location kwenye whatsapp)

Mawasiliano ni ufunguo wa kudumisha upendo.

Wakati kuwasiliana na mpendwa wako, kumbuka kwamba upendo ni muhimu. Ongea toka moyoni na si kwa ajili ya kutimiza wajibu tu,kwani mpezi wako atajua tu kama hakuna mahaba katika mawasiliano yenu hivyo kutoleta faida ile inayotegemewa.

Mawasiliano mengine ni yale ya kuelezana yaliyo moyoni. Mweleze mwenza wako linalokusibu ili kupata ufumbuzi wa pamoja. Wapenzi wanaoongea kwa utulivu siku zote watakuwa pamoja.

Zawadi

Tafuta kitu cha kumpa mpenzi wako. Si lazima kiwe na thamani kubwa.Inaweza ikawa pipi au matunda tu.
Mnunulie zawadi kila inapowezekana hasa unaposafiri au katika siku yake ya kuzaliwa.

Onyesha Upendo wako

Kila mtu anajinsi yake tofauti ya kuonyesha upendo, lakini vyovyote itavyokuwa ni jambo la muhimu sana kuonyesha hisia zako kwa mpenzi wako.

Mara nyingi wapenzi wa muda mrefu wanasahau juu ya hili.

Maneno kama “Nakupenda”au majina ya mahaba kama “Mpenzi” au ”La-azizi” yanachangia sana kuonyesha mapenzi na kumfanya mwenza wako kujisikia vizuri.

Maneno haya yanaposemwa kwa hisia halisi na toka moyoni yana mchango mkubwa katika kuboresha mahusiano.

Mambo ya Kufanya Wakati Unapogundua Uke Umekauka Ute Wakati wa Kufanya Mapenzi..!!!

$
0
0

Swala la kukauka kwa uke mara baada ya mwanake kufika kileleni ni la kwaida kwa wanawake wengi na huwa na sababu mbali mbali ambazo mimi nitakutajia kwa kifupi tu kamaifuatavyo:-

1-Mwanamke huitaji kunyegeshwa tena baada ya bao la lake la kwanza, inategemea lilipopatikana kama kwenye Kipele G, Kwenye Kisimi, Mwisho wa Uke au kuta za uke. Ikiwa amepata bao "via" kisimi hapo lazima atahiji muda kidogo wa kupumzika kama dakika kumi 5 kisha wewe mpenzi wake ni wajibu wako kumnyegesha tena kwa kucheza na sehemu nyngine za mwili wake mbali na Kisimi. Inaweza kuwa kum-busu, kumla denda huku unamshika-mshika na kadhalika.

2-Mwanamke kuwa na uwezo mdogo wa kungonoana (low sex drive/libido) ni wazi kuwa hamjuani hivyo yawezekana yeye yuko hivyo na mara baada ya wewe kupiga bao la kwanza ksiha kurudi na "kumpigisha" yeye bao lake ndio ilikuwa mwisho wa "game" mpaka kesho au labda wiki ijayo kama sio mwezi mwezi ujao. Kama ulihitaji tena kwenda basi ulitakiwa kumfaya aendelee kuwa "interested" kiakili nakimazingira zaidi ya kimwili na pia ungepaswa kutumia kilainisho kwa ajili ya Condom au hata K-Y Jel.

3-Mwanamke kutokuvutiwa na ufanyaji wako, kama ulivyosema kuwa ilikubidi uache nje-ndani, swala l a kungonoana ni pana na sio kusimamisha kisha kupiga nje-ndani mwanzo mpaka mwisho >>( Kuna wanawake kibao baada ya kibaruti cha kwanza inabidi uanze upya kuwatuliza a.k.a kuwa NYEGELESHA. Dawa yake kwa wengi usikazanie NJe ndani Nje ndani sana kama ushambarutisha tayari. 

Cheza sindimba au msondongoma katika mduara bila kuvuta filimbi nje wakati unaASALISHA mambo mengine!Baada yamuda kadhaa wakati unahisi au unasikia pumzi fulani ndio endeleza pupa kama navyohisi unafanya.Hii hasa kama unacheza mkao wa kimishenari ).<<

4-Mwanamke kutokuwa na mapenzi pia inaweza kuwa sababu ya Uke wake kuwa mkavu mara baada ya zile nyege mshindo kumalizika/kumtoka (baada ya yeye kufikia Mshindo), mwanamke kama hana mapenzi huishiwa hamu ya kuendelea kungonoka haraka sana mara tu baada ya bao lake la kwanza.

5-Kuchoka au Uvivu, mwanamke kama kachoka au mvivu hali hiyo ya ukavu ukeni hujitokeza kwa vile akili yake inakuwa haipo/haizingatii kilekinachofanyika bali saa ngapi atapata nafasi ya kwenda kulala/pumzika.

Condom huwa hazisababishi Uke kukauka tena japokuwa inashauriwa kubadili au kutumia kilainisho kilichotengenezwa kwa ajili hiyo. Makampuni mengi ya bidhaa hzi yanatoa mafuta maalum kabisa kwa ajili ya kukuongezea ile hali ya ulaini amabo unakulinda wewe kwa kuzuia Condom kupasuka/chanikakutokana na ukavu wa Uke na vilevile kumuongezea mwanamke raha ya tendo.

Condoms hazimsababishii mwanamke maumivu bali ile hali ya wewe kumfanya mwanamke mwenye uke mkavu kwa muda mrefu ndio inasababisha maumivu.Ili ufurahie Ngono basi ni vema ukatafuta mwanamke mmoja umpendae na yeye akupende na mfanye tendo kwa ushirikiana na kumbuka ku-focus kwenye kufurahia tendo zaidi kuliko kupiga mabao na mambo yatakuwa bomba kabisa.

Fahamu Sehemu Kuu Muhimu Zinazompa Utamu Mwanamke Pindi Mnapokuwa 6x6 ...!!!!

$
0
0

Kwa bahati nzuri wanawake wana maeneo 5 ambayo huwawezesha kusikia utamu wa kufanya ngono tofauti na wanaume. Sehemu maarufu ni kisimi na G spot lakini kuna eneo lingine linaitwa AFE ambalo liko mwishoni kabisa mwa uke na vile vile kuta za uke bila kusahau mwanzo wa uke. 

Mwanamke huweza kupata utamu wa tendo hili takatifu kwenye maeneo yote hayo ikiwa mpenzi wake anajua kuwajibika, sio kufanya mapenzi kwa muda mrefu tu bali pia kujua kucheza na uume wake. Pamoja na utundu wake pia wewe mwanamke unatakiwa kuwa wazi na huru kumuelekeza ikiwa kagusa kusiko au kapatia kunako utamu. Utamu wa maeneo yote hayo ni tofauti na unazidiana kati ya mwanamke mmoja na mwingine. 

Hebu sasa tutazame hizo sehemu tofauti za utamu wa ngono kwa wanawake. 

Kisimi Wanawake hupata utamu wa kisimini kwa njia ya kusuguliwa, kushikwa, kuchezewa kwa ulimi, kidole au kichwa cha uume. Utamu wa mahali hapa hupatikana haraka na hufanya usitamani tena tendo hilo kwa muda fulani (Kuanzia dakika 3 – 15) na kikiguswa tena huweza kumpa mwanamke maumivu fulani hivi. Baadhi ya wanawake huwa hawawezi kuendelea 
tena na tendo mara baada ya kuchezewa 

kisimi. G-spot Utamu wa mahali hapa ni wa nguvu sana na wanawake wengi huishiwa nguvukwa muda wanapoguswa eneo hili. Nguvu hizo huchukua muda wa dakika 20 – 45 kurejea, na zikirejea hamu haiishi. Hivyo wakati wewe umezimia mpenzi wako anaweza kuendelea na mchezo na nguvu zikirudi basi na wewe unaendelea kutafuta goli lingine. 

Mwanzo wa uke Utamu wa mahali hapa haumpotezei mwanamke hamu, kwani hafiki kileleni bali anasikia utamu fulani hivi. Ili mwanamke aweze kufika kileleni,mwanaume anatakiwa aingize uume ndani zaidi ili aweze kugusa eneo la G- Spot na kuta za uke. 

Kuta za uke Utamu wa eneo hili unapatikana toka mwanzo uume ulipoingizwa, na kadri mnavyoendelea kufanyana ndivyo utamu unavyozidi kuongezeka na hatimaye mwanamke hujikuta akifika kileleni. Mwisho wa uke (karibu na njia ya uzazi) Utamu wa eneo hili hupatikana endapo uume wa mpenzi wako utagusa mwisho wa uke. Kwa kawaida mwanamke husikia maumivu flani anapoguswa eneo hili lakini wakati huo huo badoanapenaendelee na wakati mwingine anaweza kumuomba mpenzi wake afanye kwa nguvu.

 Pia mwanamke anaweza kutokwa na damu endapo ataguswa eneo hilo. Ewe mwanamke,hakikisha unamruhusu mpenzi wako kufika huko ikiwa mnaaminiana, mko kwenye uhusiano wa kudumu, msafi kiafya na uko tayari kuwa mama endapo mpenzi wako atateleza na kuachia kidogo kwani eneo hili lipo mlangoni kabisa mwa njia ya uzazi.

Unaumia Wakati wa Tendo la Ndoa? Soma Hapa!

$
0
0

HII ni hali ambayo mwanamke anakuwa na hamu ya kufanya tendo  la ndoa lakini anapata ugumu kutokana na maumivu makali anayopata.

Hali hii inatokana na kubana au kukaza kwa misuli ya uke lakini pia  inaweza kusababishwa na matatizo ukeni.

Mfano endapo kuna michubuko au vidonda au kasoro yoyote ya uke,  aidha uke ni mdogo au maumbile ya uke hayana uwiano na uume. Tatizo hili huwapata wanawake wa rika zote ilimradi tayari yupo katika  umri wa kuzaa.

TATIZO LINAVYOGAWANYIKA

Tatizo hili la maumivu wakati wa tendo la ndoa limegawanyika katika maeneo makuu mawili. Kwanza ni Primary Dyspareunia .

Hapa  mwanamke anakuwa hana historia ya maumivu wala  hana historia ya kuwahi kufanya tendo hilo ndiyo, kwanza anaanza. Kitaalamu hali hii ya maumivu huitwa Honey moon Dypareunia au maumivu ya fungate na hutokea mara tu anapoanza kujamiiana kwa mara ya kwanza. Katika hali hii misuli ya uke inaweza kubana kutokana na michubuko au kuchanika ubikira au hata kuchanika upande wa chini wa uke na wakati mwingine  michubuko hutokea katika tundu ya mkojo.Hali ya michubuko inaweza kuwa mbaya na ikajitokeza hata kwa kugusa tu upande wa nje wa uke.

Maumivu yakiendelea au yakizidi husababisha mgonjwa apate matatizo ya kisaikolojia kiasi kwamba huanza kuogopa tendo lenyewe na kuhisi endapo atalifanya ataumia. Tatizo hili likileta michubuko kwenye njia ya mkojo husababisha maambukizi sugu ya kibofu cha mkojo kutokana na michubuko ya mara kwa mara ya tundu ya mkojo.

Maumivu ukeni hutokana pia na maandalizi mabovu kabla ya tendo ambapo uke unakuwa haujalainika kwa kutofanya romance ya kutosha,  kutofanya tendo hilo kwa ustaarabu, yaani kutumia nguvu au endapo mwanamke atakuwa na maambukizi ukeni mfano fangasi ambayo huambatana na kutokwa na uchafu ukeni na muwasho, magonjwa ya uke kama kuvimba kwa tezi za uke, kuvimba kwa mashavu ya uke au hali yoyote inayomwondolea amani mwanamke pale ukeni inaweza kumfanya kisaikolojia aathirike na kuhisi maumivu wakati wa tendo.

Michubuko ukeni au kuhisi moto ukeni wakati wa tendo la ndoa kunaweza kusababishwa na matumizi ya vilainishi visivyofaa  au kuumwa kutokana na uwepo wa vinyweleo virefu ukeni na endapo havikupunguzwa vitaingia ukeni wakati wa tendo na kukuchubua.  Kasoro katika ubikira pia husababisha mwanamke ahisi maumivu wakati wa tendo.

Maumivu haya huwa hayahusiani na yale ya awali ya fungate na wakati mwingine huanza baada ya kipindi kirefu cha miaka mingi tangu uanze tendo la ndoa na wengine huwa na tatizo hili tayari wana watoto. Chanzo cha tatizo hili ni ukavu ukeni, umri mkubwa wa mwanamke na kusinyaa kwa misuli ya uke.

Matatizo haya isipokuwa la umri mkubwa  hutokea katika umri wa kati na tayari mwanamke  anayo historia ya kuwa katika mahusiano na hata tayari ana watoto. Umri mkubwa tunaouzungumzia ni zaidi ya miaka hamsini. Kubana misuli ya ukeni hutokana na makovu baada ya kushonwa msamba au kuongezewa njia wakati wa kujifungua au upasuaji wa kurekebisha fistula pia husababisha tatizo hili.

Vyanzo vingine vya maumivu haya ya tendo la ndoa ni kushuka kwa kizazi ambapo mwanamke atahisi kitu kama gololi ukeni wakati  akijisafi sha au kuhisi kizazi kinasukumwa wakati wa tendo, kugeuka kwa kizazi, matatizo katika tabaka la ndani la kizazi, maambukizi sugu ukeni ambapo uchafu na muwasho ukeni hujirudiarudia, matatizo katika njia ya mkojo na maambukizi katika viungo vya uzazi ’PID’  husababisha maumivu wakati wa tendo la ndoa.

Matitizo ya kisaikolojia husababisha maumivu wakati wa tendo la ndoa pale ambapo misuli ya ukeni itakaza na mwanamke anapochunguzwa huwa hana tatizo au kasoro yoyote ukeni. Matatizo katika mishipa ya fahamu ya ukeni, kuogopa tendo lenyewe kuhisi utapata maumivu au kama kuna historia ya kuingiliwa kwa nguvu na ukaumia, kutokuwa na taarifa sahihi kuhusu tendo la kujamiiana, yote haya na mengine mengi humharibu mwanamke kisaikolojia na kujikuta anaanza kuhisi maumivu hata kabla ya tendo lenyewe kwa kuingiwa na hofu.

Hali nyingine inayoweza kumfanya mwanamke aathirike kisaikolojia na asiwe tayari kwa tendo na hata akilifanya apate maumivu ni kuogopa kupata ujauzito wakati hayupo tayari kwa hilo, kuogopa kupata maambukizi, kulazimishwa penzi endapo haupo tayari na mwanaume uliye naye na kuhisi kuna tofauti ya maumbile na mume uliyenaye.

Endapo mwanaume anakukwaza kutokana na kutokwa na jasho jingi sana wakati wa tendo, kutoa harufu mbaya ya pua, kinywani, makwapani au sehemu zake za siri, huwa na magonjwa ya ngozi au hata mwilini mwake, matatizo haya huweza kumwathiri mwanamke kisaikolojia na asifurahie tendo na kutotoa ushirikiano wakati wa tendo na kupata maumivu.

UCHUNGUZI Tatizo hili ni pana sana, unaweza kuhisi una kasoro au maambukizi kumbe tofauti. Kwa hiyo basi ni vizuri uchunguzwe kwa umakini katika kliniki za madaktari wa akina mama katika hospitali za mikoa ili kujua chanzo halisi cha tatizo.

Afariki Dunia kwa Kuzidiwa Utamu wa Mapenzi...!!!

$
0
0

Kijana mmoja nchini Malawi Fletcher Jere (26) amefariki dunia kutokana na kuzidiwa utamu wakati akifanya ngono na kahaba mmoja mjini Blantyre.

Gazeti la Daily Times nchini Malawi limeripoti kuwa kijana huyo alinunua kahaba huyo maeneo ya Ndirabe katikati ya jiji la Blantyre.

Afisa wa Polisi mjini Blantyre Bi.Edina Ligowe amesema Jerre alikufa kutokana na kuwa na hisia za juu sana pamoja na kuhisi utamu uliopitiliza wakati akifanya ngono na kahaba huyo (sexual excitement and sweetness).

Aidha Afisa huyo amesema kuwa kahaba huyo hatafunguliwa mashtaka yoyote kwa sababu hakuna kosa alilofanya kwa yeye kuwa mtamu kupitiliza. "She committed no crime by being too sweet to the man"

Nape Nnauye: Kitendo Kilichofanywa na Mkuu wa Mkoa kimenajisi Tasnia ya Habari

$
0
0
Waziri Nape: Kabla ya kuchukua hatua zozote, sisi kama Serikali tunataka kusikia kutoka kwa Mkuu wa Mkoa wa Dar, Paul Makonda

Waziri Nape: Tumeunda timu ya watu 5 kufanya kazi katika saa 24 ili wapate maelezo ya RC Makonda na ripoti hiyo itasomwa wazi

Waziri Nape: Kitendo kilichofanywa na RC Makonda kinanajisi Uhuru wa Vyombo vya Habari katika Nchi Huru. Mamlaka zitajua cha kufanya

Kusaga: Kama RC Makonda ataomba radhi hatuna shida naye, ataendelea kuwa rafiki!

Reginald Mengi: Tuna Rais anayependa Vyombo vya Habari, lakini mapenzi haya ayaonyeshe kwa Vitendo!

Nape Nnauye(Waziri wa Habari): Wanahabari tutulie na tusubiri kusikia kutoka pande zote mbili kabla ya kuchukua uamuzi

Nape: Natoa pole kwa Clouds Media na kwakuwa tumejiridhisha kuwa jambo hili limetokea basi tutalishughulikia

Nape Nnauye: Ripoti itakayoletwa na Kamati ya Uchunguzi pamoja na hatua zitakazochukuliwa vitatangazwa hadharani baada ya saa 24\


Habari zaidi....

Waziri Waziri wa Habari,Utamaduni,Sanaa na Michezo Mh Nape Nnauye amesema kuwa Tukio la Uvamizi wa Kituo cha Habari cha Clouds unaodaiwa kufanywa na Mkuu wa mkoa wa Dar es salaam Mh Paul makonda akiwa na askari kadhaa ni tukio la kupingwa huku akidai kuwa matukio kama hayo hutokea pindi nchi inapotaka kupinduliwa lakini kama Rais yupo, nchi haijapinduliwa.

Aidha amesema kuwa Vitendo hivyo ni kunajisi uhuru wa habari na kama akishindwa kusimamia hilo na yeye hafai kuwa katika nafasi aliyopo.

Chanzo : Mwananchi
Viewing all 104709 articles
Browse latest View live




Latest Images