Quantcast
Channel: UDAKU SPECIAL
Viewing all 104766 articles
Browse latest View live

Gari Mpya Aina ya Toyota Passo Inauzwa...Haijatumika Tanzania

$
0
0

Gari aina ya Toyota Passo Inauzwa ...
Haijatumiwa Tanzania kabisa Imetolewa Bandarini Wiki iliyopita
Namba DKD
Kilometer 90,000
Engine CC 1,000
IPO dar Tegeta Kibo Complex
Inauzwa Million 7.5

Kwa Mawasiliano zaidi Piga simu namba 0714604974


Picha zaidi za gari hizi hapa chini:



Kama Ulimiss Jinsi Ruge Alivyofunguka Kuhusu Paul Makonda Basi Nimekuwekea Video Hapa

$
0
0
Ruge: Niliwambia SHILAWADU siku ya Alhamisi mchana kuwa wasiirushe 'Story' bila kuongea na upande wa pili (wa Gwajima)

Ruge: Niliwambia Vijana wa SHILAWADU kuwa 'Story' kama ndo anayoisubiri RC basi ajue haitaenda hewani hata kwny Social Media

Ruge: Ijumaa niliwasisitiza SHILAWADU kuwa kipindi kile kisirushwe kwakuwa 'Story' haiko balanced

Ruge: Ijumaa saa 5 kasoro usiku nilipigiwa simu kuwa RC Makonda alikuwa kaja ofisini akiwa na maaskari wakiwa na silaha

Ruge: Nilimpigia simu RC Makonda kumhoji kwanini aje ofisini na maaskari wenye silaha? Akauliza kwanini nimezuia kipindi kuruka!?

Ruge: RC Makonda alikata simu, lkn nilipaniki nikiwazia hizo silaha walizokuja nazo ofisini. Makonda alikichukua kipindi kwny flash

Ruge: RC Makonda alisema "Bahati yenu" baada ya kujua kuwa waliokataa vijana wa SHILAWADU sio waliozuia kipindi isipokuwa mimi

Ruge: Nilimwambia Mkurugenzi wa Clouds(Kusaga) kuwa RC alitukosea heshima; kulikuwa na haja gani aje na silaha na ni rafiki yetu?

Ruge: Ukweli hakuna aliyepigwa ila kulijengwa hofu kubwa kwa wafanyakazi wa Clouds Media. Si jambo dogo hili!

Ruge: Tusikwepe ukweli kuwa sisi Clouds Media kama chombo cha habari tuna wajibu wa ku-balance story. Sijawahi kulazimishwa story...

Ruge: Kuacha shughuli za kazi, Makonda amekuwa akija hapa Clouds kama rafiki. Ila kitendo cha kuja na walinzi kiliwashtua walinzi

Ruge: Kama watanzania, hatutaki kuiona bunduki mitaani. Hili limetokea kutufungua macho kujua ma-RC na ma-DC wanavyofanya kazi yao...

Ruge: Sisi tuhukumiwe kama taasisi, wafanyakazi wetu wasitiwe hofu. Mimi sikuwekwa ndani, nilienda Polisi kuripoti suala hili

Ruge: Mtu akikosea kabla hatujaangalia cheo chake, tuangalie makosa yake. Si kudai eti wanaomkosoa wanapingana Vita ya #DawaZaKulevya

Ruge: Mtu kuwa na nafasi ya Uongozi flani si sababu ya 'kuwapanda' watu . All we want is RESPECT!

Ruge: Video clips za CCTV zinazozunguka mtandaoni kweli ni za hapa Clouds Media. Sisi tulidhani Makonda angeomba radhi kwa kadhia hii

Ruge: Siujutii ukaribu wangu na Makonda. Hata akirudi akaomba radhi bado nitamfikiria! Tunataka kuendelea kumpa ushirikiano

Ruge: Niseme, urafiki na BUNDUKI siutaki. Wanaodai Makonda alikuja hapa Clouds akiwa rafiki wanapotosha! Ametumia vibaya madaraka

Ruge: Clouds inalaani kilichotokea, na inaomba Vyombo vya Habari vitoe ushirikiano ktk kukemea hili. Hatutaki kugombana na Serikali

 Tazama Video:


Rukwa: Mwanaume Ajikata Uume kwa Kukosa Mpenzi...!!!

$
0
0

Mkazi wa kijiji cha Kate, wilayani Nkasi, Mkoa wa Rukwa, amejikata uume wake kwa kisu kwa hasira baada ya kuota kuwa anafanya mapenzi na mke wake aliyefariki mwaka mmoja uliopita.

Mwanaume huyo mwenye umri wa miaka 58 alijikata uume wake juzi majira ya saa 4:00 asubuhi akiwa amejifungia chumbani kwake peke yake.

Mwenyekiti wa Kitongoji hicho Richard Mselema, akizungumzia tukio hilo alisema kuwa, mtu huyo alikuwa akitafuta binti wa kumuoa na kuishi nae kwa muda mrefu baada ya mke wake kufariki, lakini wanawake wamekuwa wakimkataa kwa kuwa umri wake ni mkubwa.

Baada ya kufanya tukio hilo akiwa peke yake na kupata maumivu makali, mwanaume huyo alipiga yowe na watu walipofika na kumkuta anavuja damu nyingi sehemu ya uume wake huku kisu kikiwa kimetupwa pembeni, waliamua kumbeba na kumkimbiza katika Zahanati ya Kate Mission.

Kwa mujibu wa daktari wa zamu, Paul Katindi, aliyempatia matibabu katika majeraha aliyoyapata, alisema kuwa hali yake itakuwa nzuri na anaweza kuendelea na mchakato wake wa kumtafuta mwanamke wa kuoa.

“Niliamua kujikata kutokana na kuwa na uume lakini siutumii kwa kuwa sina mke wala mpenzi. Hivyo sikuona umuhimu wala faida ya kuwa nao.” Alisema majeruhi huyo alipoizungumza na mwenyekiti wa Halmashauri ya wilaya ya Nkasi, Zeno Mwanakulya, ambae pia ni jirani yake, alipokwenda kumtembelea na kumpa pole.

Mke wa Rais na Vibweka Vyake,...!!!

$
0
0

Mke wa Rais alipojua udhaifu wa mume wake, kwamba anampenda sana acha afanye vituko. Nchi ikasimama. Vurugu zote yeye. Nani wa kumzuia na ndiye usingizi wa Mkuu wa Nchi?

Watu waliufahamu ukali wa Rais lakini wakawa wanastaajabu ukimya wake juu ya vitendo vya mkewe. Wengine wakasema Rais ni Bushoke, wapo waliodai Rais huchimbwa mkwara wa kunyimwa unyumba ndiyo maana alikuwa mpole.

Lucy Kibaki, Mungu amrehemu, aliitikisa Kenya miaka 10 ya Urais wa mume wake, Mwai Kibaki, kati ya mwaka 2002 mpaka 2012.

Lucy hakuwa wa mchezo, alivamia chombo cha habari na kushambulia wahariri. Aliwahi kumpa makofi mpiga picha wa gazeti la Nation kwenye kadamnasi. Watu wakashangaa. Mume wake akawa kimya.

Mwaka 2007, katika sherehe ya Siku ya Jamhuri, iliyofanyika Ikulu, MC alimtambulisha Lucy Kibaki kwa majina ya Lucy Wamboi Kibaki badala ya Lucy Muthoni Kibaki, basi MC mbele za watu akachezea makofi.

Kibaki alishuhudia lakini afanye nini? Lucy ndiye usingizi wake. Mama akazidi kutamba, akamtwanga makofi mtumishi wa Ikulu, Matere Keriri. Halafu akatamba: “Nikisema mimi ndiyo sauti ya mwisho.” Usimchezee mama Prezidaa!

Bunge la Kenya likachachamaa na kumsema Kibaki kwa kushindwa kumdhibiti mkewe. Lucy akamwambia mwanasheria Gitobu Imanyara, afungue kesi dhidi ya wabunge. Imanyara aliposema mashitaka yasingekuwa na nguvu, alichezea makofi.

Kibaki alikuwa na kawaida ya kuwaalika marafiki zake na kupata mvinyo kwenye baa ya Ikulu. Lucy akatimua marafiki wa Kibaki halafu akaagiza baa ifungwe.

Kipindi fulani vyombo vya habari viliripoti Kibaki alikuwa na mke mwingine tofauti na Lucy, basi mama akachachamaa, akamwagiza mumewe afanye mkutano na waandishi wa habari ili akanushe. Kibaki alikanusha huku Lucy akimsimamia.

HATA MAREKANI

Rais wa 19 wa Marekani, Warren Harding naye alikuwa mnyonge kwa mkewe, Florence Harding. Wakati huo, mpaka magazeti yaliandika kuwa nchi ilikuwa na inaongozwa na First Lady.

Florence aliagiza intelijensia kufanya kazi, alimwandikia Rais Harding cha kuzungumza kwa waandishi wa habari. Florence ndiye alikuwa kila kitu kwa Serikali ya Marekani. Florence aliwahi kusema yeye ndiye sauti ya Rais. Ni kama mtu mzima Robert Mugabe alivyo mpole kwa Grace.

Unajua jeuri yote ya nini? Ni mke kujua anapendwa. Mke wa Rais asiye na busara akishajua mume wake amependa mpaka ameoza kwake, basi hufanya vituko mpaka kumdhalilisha Rais mwenyewe na nchi yote.



Author: Luqman MALOTO

Ukweli Mchungu...Mange Kimambi Ndiye Mtu Pekee Anayeweza Kumsafisha Makonda..!!!

$
0
0

Ni ukweli usio pingika kwamba asilimia zisizopungua sitini za watanzania wanaamini kila kitu anachokisema Mange Kimambi kiwe kizuri au kibaya wa tanzania watakichukua kama kilivyo na watakiamini kwa 100%

Nina uhakika 100% Mange Kimambi akiamua kuliyumbisha hili tukio la Bashite kwa kuleta information za kumsafisha Bashite ikiwezekana hata kwa kumchafua Gwajima watanzania watamuamini Mange na shutuma zote ambazo alikuwa anahusishwa nazo Bashite zitakwisha haraka kama moto wa nyasi hii yote ni kwa sababu tu Mange ameshika akili watanzania wengi kiasi kwamba wengine hasa wale wapenda ubuyu ni vigumu sana siku ikapita bila kupitia IG kwenda kuona Mange kaposti nini.


Na kwa kuwa ma bloggers wengi source yao kubwa ya habari ni kwa Mange na kwa kuwa watanzania wengi wanategemea habari kutoka kwenye blogs mbalimbali hivyo basi ina maanisha habari itakayosambazwa itaaminika tu bila kuchujwa wala nini 


Na ukitaka kuamini zaidi kwamba Mange ndio kila kitu ,kuna kipindi alitulia kidogo kupost habari za Bashite ,kutulia kwa Mange kulififisha kabisa habari za Bashite watu walikuwa washaanza kumsahau taratibu na alipoenda kufanya ufunguzi wa barabara alishangiliwa kana kwamba hamna chochote kinacho endelea juu yake.


Hivyo basi napenda kumalizia kwa kusema kuwa sakata la Bashite litaisha pale tu Mange atakapoacha kumuongelea watz watalisahau taratibu taratibu hatimaye wataliacha kabisa

Au kama si kuliacha basi aligeuze juu chini chini juu kwa kutafuta taarifa za uongo na kweli za kumsafisha Bashite na nina uhakika atafanikiwa.

Kimenukaa.. Aliyesoma Pamoja na Makonda Chuo cha Ushirika Moshi Aibuka na Haya..Amtaka Ajiuzulu Haraka Kabla Mambo Hayajazidi Kumuharibikia..!!!!

$
0
0

Hapa sikutaka kumzungumzia kabisa Makonda hata nilipokuwa Dodoma kwenye mkutano baadhi ya marafiki tuliosoma nae ushirika tulijadili na kuona chama kinamlea vibaya sana.

Leo nimeona video ikimuonyesha akivamia ofisi za clouds Tv hili jambo ni gumu sana sana Mhe. Rais aliangalie kwa kina sana la sivyo linaendelea kutuchafua sana, ukitazama mitandao ya kijamii utaona tunavyotukanywa na mtu anayeonekana mbaya ni Rais wangu.

Nemeona mandiko baadhi ya makada wenzangu wabunge na hata mawaziri wakishanga jambo hili, mimi binafsi nimeshindwa kuvumilia namuomba Rais wangu na mwenyekiti wangu wa ccm amuondoe Poul Makonda kwenye nafasi hii ya mkuu wa mkoa kuendelea kumwacha ni kukichafua chama chetu.

Makonda Ondoka Mwanyewe kaka yangu na rafiki yangu ondoka mwenyewe kuendelea kubaki ni kuifanya ofisi ya Rais inapoteza dira yake na mwelekeo.

ni mimi

Meijo Laizer 
Mjumbe wa NEC TAIFA
Wilaya ya Siha

Alichosema Rais Magufuli Kuhusu Paul Makonda Leo

$
0
0

Tofauti na kile ambacho watanzania wengi leo walikuwa wakitarajia kuona Rais wa Jamhuri wa Muungano wa Tanzania, Dkt John Magufuli akichukua uamuzi mgumu dhidi ya mkuu wa mkoa wa Dar es Salaam, Paul Makonda, mkuu huyo wa nchi amemuelezea Makonda kuchapa kazi.

Makonda anakabiliwa na kashfa lukuki ikiwemo ile ya kudaiwa kughushi vyeti na kwamba jina lake halisi ni Daudi Bashite, kutumia vibaya madaraka yake ikiwemo tukio la juzi la kuvamia studio za Clouds Media Group akiwa na wanajeshi wenye silaha akilamizimisha kurushwa kwa kipindi na zingine. Tukio hilo limelaaniwa vikali.

Akizungumza Jumatatu hii kwenye uwekaji jiwe la msingi katika mradi wa barabara za juu (Flyovers) Ubungo, Dar, Rais Magufuli amesema, “Mimi ndio najua mwenyewe nani anatakiwa kuwa wapi akae wapi, ni mimi ninayepanga. Ninajua wamenielewa. Kwahiyo Makonda wewe chapakazi, nasema chapa kazi.”

“Suala la kuandikwa kwenye mitandao sio tija kwangu, hata mimi ninaandikwa kwenye mitandao kwahiyo nijiuzulu urais? Chapa kazi, hapa kazi tu.”

Rais amesema Watanzania wanapoteza muda mwingi kwa mambo yasiyo ya msingi.

“Tumepoteza direction tumeanza kujadili personalities,” aliongeza.

Kimenukaa..Nape Nnauye Atoa Saa 24 Makonda Ahojiwe Juu ya Kuvamia Clouds Media na Kikosi cha Askari Wenye Silaha za Kivita..!!!

$
0
0

Waziri Habari, Utamaduni, Vijana, Sanaa na Michezo, Nape Nnauye, ameunda kamati Maalum ya watu watano kuchunguza kitendo kilichofanywa na Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam, Paul Makonda cha kuvamia Ofisi za Clouds Media Group, kwa lengo la kushinikiza habari yake irushwe katika kipindi cha Da’ Weekend Chat Show maarufu kama (Shilawadu).

Waziri Nape amesema hayo leo wakati akizungumza na waandishi, baada ya Mkurugenzi wa vipindi na uandaaji, Rude Mutahaba kuthibitisha tukio hilo. Nape amesema kamati hiyo itafanya kazi kwa muda wa saa 24 na baada ya hapo, itatoa ripoti kwa waandishi wa habari na kila kitu kitaanikwa hadharani.

“Matukio kama haya hutokea pindi nchi inapotaka kupinduliwa, lakini kama Rais yupo na nchi haijapinduliwa basi kuingia ndani ya chombo cha habari na silaha, huku ni sawa na kunajisi uhuru wa habari katika nchi yetu,” alisema Nape

Aidha Nape amesema jambo lililotokea lisiwavunje moyo Clouds Media na wana habari kwa ujumla huku akisema kuwa serikali ipo kulinda haki za wanahabari bila kushinikizwa na lolote lililotokea.

Mbwana Samatta Atoa ya Moyoni Baada ya Makonda Kuvamia Clouds Usiku Usiku Akiwa na Kikosi cha Askari..!!!

$
0
0

BAADA ya kuvamiwa kwa Kituo cha Redio cha Clouds Fm, imeibuka mijadala mingi, Watanzania wakaijadili kila kona ya nchi. Katika mijadala hiyo, wapo wanasiasa, watumishi wa umma, waumini wa dini na wanamichezo ambapo mchezaji wa Taifa Stars anayekipiga nchini Ubelgiji katika Klabu ya Genk, Mbwana Samatta amefunguka kuwa wanasiasa wanakosa maadili.

“Ndiyo maana siasa imekuwa cheap maana viongozi wenyewe wana-hang out na akina Amber Lulu na Gigy Money” aliandika Samatta.

Credit  -Globalpublisher

Imevuja Shilole na Nuh Hawawezi Kuachana,Waonekana Hotelini Wakipeana Malove kwa Siri...!!!!

$
0
0

Wanaubuyu wanakuambia kuwa kuendelea kuwasiliana mambo ya malavidavi na ‘eksi’ wako ni sawa na kutembelea muwa kama fi mbo kwani ipo siku utautafuna! Hicho ndicho kinachodaiwa kuendelea kati ya mastaa wawili Bongo, Zuwena Mohammed ‘Shilole’ na Naftal Mlawa ‘Nuh Mziwanda’.

Ubuyu unadai kuwa, Shilole au Shishi na Nuh wanaendeleza libeneke la kukwichikwichi na kwamba hawawezi kuachana, licha ya Nuh kufunga ndoa na Nawal na kujaliwa mtoto wa kike hivi karibuni.

Chanzo makini kilinyetisha kuwa, tangu Shishi na Nuh wamwagane umepita muda mrefu, lakini kuna ubuyu wa kunyapianyapia kwamba wamekuwa wakimtesa Nawal kwani anaweza kukata hata mwezi mzima bila kumtia machoni mumewe huyo.

CHANZO CHATHIBITISHA

Chanzo hicho ambacho ni rafi ki wa karibu wa ‘kapo’ hiyo kilidai kuwa kina uthibitisho usiokuwa na shaka kwamba Shishi na Nuh wamekuwa wakikutana kwenye hoteli moja iliyopo Sinza, Dar (jina tunalo) ambapo wanadaiwa kuitumia kula bata na kumbonji mara kwa mara

WALALA HOTELINI

“Hivi mna ubuyu kuwa Shishi Trump na Nuh hawajawahi kuachana? Kwa taarifa yenu huwa wanatoka ‘out’ na kulala pamoja pale…(kinataja jina la hoteli hiyo).

“Kiukweli hawa watu hawawezi kuachana na naionea huruma sana ndoa ya huyo Nawal kwani siyo siri inaelekea pabaya maana Shishi naye si mtu wa mchezomchezo linapokuja suala la malavidavi anapokuwa kwenye kumi na nane,” kilisema chanzo.

Chanzo hicho kiliendelea kufunguka kuwa, shosti wake, Shishi ana imani ipo siku Nuh atamwagana na Nawal kisha ataolewa yeye maana anampenda jamaa huyo kinoma na hakuna anayeweza kuwaachanisha.

WIKIENDA LACHIMBA

Baada ya ubuyu huo kutua kwenye meza ya Wikienda, wanahabari wetu walianza kuichimba ambapo walikutana na Shishi uso kwa uso ili azungumzie ishu hiyo ambapo mahojiano yalikuwa hivi; Wikienda: Kwanza Shilole unazungumziaje Nuh kupata mtoto wa kike?

Shilole: Nimefurahi sana…tumepata mtoto… hahahaaa…

Wikienda: Kwani mtoto wa Nuh ni wako pia?

Shilole: Si aliwahi kuwa hivyo? Nuh akipata mtoto mimi nafurahi kama mtoto wangu.

Wikienda: Je, hutamani nafasi hiyo ingekuwa yako? Shilole: Hapana.

Ningetaka kuzaa na Nuh ningezaa naye na si mtoto mmoja hata watatu, lakini haikuwa hivyo.

Wikienda: Hata hivyo, kilichotuleta kwako si mambo ya mtoto bali ni ubuyu tuliofi kishiwa kuwa huwezi kumuacha Nuh na mmekuwa mkijifungia hotelini Sinza kisha mnafanya yenu, je, hili likoje?

Shilole: Hahahaaa…mbona mnapenda kuniuliza swali hilo? Niseme mara ngapi? Nuh ana familia yake jamani! Kama ndivyo itafi kia time (wakati) nitaacha kuongea kuhusu ishu hiyo.

Wikienda: Wewe unachotakiwa kujibu ni kweli au si kweli kwani watu wakiachana kurudiana inawezekana hata ndani ya siku mbili tu.

Shilole: Kiukweli siwezi kuliongelea suala hilo, kama mmesikia basi lifanyieni kazi, kama mambo yapo yataonekana tu lakini ninachojua Nuh ana mkewe na wamepata mtoto hivyo wana furaha sasa.

HUYU HAPA NUH.

Nuh alipoulizwa aliendelea kusisitiza kuwa, yeye na Shilole ni washkaji tu na anamheshimu mkewe. “Mimi na mke wangu tunapendana, huyo Shilole atabaki kuwa zilipendwa tu, mimi sina uhusiano naye kwa sasa,” alisema Nuh.

KUTOKA KWA MHARIRI.

Kama kweli lisemwalo lipo, Shilole atakuwa anamkosea Nawal na kwa upande wa Nuh anapaswa kuheshimu ndoa yake.

Breaking Newss..Wabunge wa CCM Dalaly Kafumu na Vicky Kamata Wajiuzulu,Waandika Barua Zenye Ujumbe Mzito Kuhusu Serikali ya Magufuli...!!!

$
0
0

Mwenyekiti Kamati ya Kudumu ya Bunge, Viwanda na Biashara, Dkt. Dalaly Peter Kafumu, makamu mwenyekiti wa Kamati hiyo, Vicky Kamata wamejiuzulu nyadhifa zao hizo leo Machi 20, 2017.

Wabunge hao wamesema wamefanya uamuzi huo ili waweze kupata muda wa kutosha kuwatumikia wananchi majimboni mwao.

Aidha viongozi hao wameeleza sababu za kuchukua hatua hiyo kuwa ni serikali kuingilia majukumu yao katika utendaji kazi na hivyo wakaeleza kuwa hawaoni sababu za kuendelea na majukumu hayo.
Kafumu ni Mbunge wa Jimbo la Igunga (CCM) ambapo Vicky Kamata ni Mbunge wa Viti Maalum (CCM) akiwakilisha wanawake wa Mkoa wa Geita.

Wamekabidhi barua za kujiuzulu kwenye ofisi ya spika wa bunge jana.

Kudadadeki..Makonda Azidi Kupigwa Kila Kona..Machangudoa Waungana Kuanzisha Mtandao Huu Hatari Ili Kumkabili...!!!!

$
0
0

BAADA ya Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam, Paul Makonda kuelezea mafanikio aliyoyapata, changamoto alizokutana nazo na mipango inayofuata ya mwaka wake wa pili aliouanza, wanawake wanaofanya biashara ya ‘uchuuzi wa mwili’ (machangudoa), wameibuka na mbinu mpya ya kumdhibiti kiongozi huyo ili asiwabughudhi.

Uchunguzi uliofanywa na Risasi Jumamosi umebaini kwamba, baada ya kuchoshwa na kukimbizwa na kukamatwa na polisi chini ya Kamanda wa Polisi Kanda Maalum ya Dar es Salaam, CP Simon Sirro wanapojiuza barabarani kwa amri ya Makonda, sasa wameanzisha mtandao wa kujiuza ambao unaelezwa ni hatari zaidi.

“Unaambiwa sasa hivi mambo ni kidijitali na ni vigumu kuwakamata kwani huwezi kumtambua mwanamke anayejiuza kirahisi kwa sababu mchongo mzima unachongwa mtandaoni kupitia Mitandao ya Kijamii ya Instagram na WhatsApp na siyo kusimama barabarani kama zamani.

“Wenyewe wanasema wamempiga tobo Makonda kwa kubuni njia mpya ya kuwaingizia kipato, tena bila kujidhalilisha kama zamani,” alitonya mtoa taarifa wetu hivyo kutoa ‘asainmenti’ kwa Oparesheni Fichua Maovu (OFM) ya Global Publishers.

OFM KAZINI Ikiwa kazini, OFM ilitonywa kuwa kwa sasa kuna mbinu mpya ambayo machangu wanatumia kwa sasa hasa wa maeneo ya Sinza ambao wametoweka katika vijiwe vyao kisha kujituliza magetoni kwao kusubiria oda kutoka kwa wanaume hivyo kuwataka Mamlaka ya Mawasiliano Tanzania (TCRA) na polisi kuingilia kati kukomesha ishu hiyo.

“Hivi mnajua kuwa machangu siku hizi hawaonekani kwenye maeneo yao ya usiku? Unajua kuna kipindi walizidi mno lakini kufuatia udhibiti wa polisi chini ya Makonda wa kuwapitia na kufunga maeneo, sasa wameunda magrupu tofautitofauti mitandaoni na kuwavuta wateja wao kirahisi. WANAFANYAJE? ”

Ishu nzima ipo hivi, wanajitangaza kwa kuanika picha zao za utupu na nusu utupu pamoja na vipande vya video kwenye Instagram kisha wanakuwekea namba zao za simu na kukutangazia, ukitaka kujiunga kuwaona live unatuma kiasi cha kati ya shilingi 5,000 hadi 10,000 na ukiingia humo unawakuta kibao hivyo TCRA na polisi kazi wanayo.

“Wapo wanaotoa huduma ya kukuunganisha tena kwa utakayemtaka kwa gharama ya shilingi 10,000 kisha ushindwe mwenyewe tu kwani wapo tu magetoni wanasubiri uingie kwenye kumi na nane zao,” alisema Abdi, mkazi wa Afrika Sana, Dar.

OFM YACHIMBA Baada ya kujua mbinu hiyo, OFM ilijipanga na kumtuma mmojawao ambapo aliingia katika Mtandao wa Instagram na kukutana na makundi mengi ambayo yamewekwa majina ya kukuonesha kuwa huduma hiyo ipo kisha akawatumia kiasi hicho cha fedha na punde akaunganishwa na kushuhudia video na picha za utupu.

MMOJA AINGIA MTEGONI Baada ya kuunganishwa kama yalivyo masharti yao, aliomba apatiwe mmojawao ambapo aliambiwa atoe tena kiasi kingine cha shilingi 10,000 na baada ya kufanya malipo hayo aliunganishwa na mrembo aliyetambulika kwa jina moja la Irene tayari kwa kwenda kujinoma naye.

OFM aliahidiana na Irene kukutana sehemu kwa ajili ya huduma hiyo na kukubali kufika lakini baada ya kuketi katika maongezi, OFM akiwa katika harakati za kuchomoa simu apige picha kadhaa, Irene alishtuka na kuwa mkali kama pilipili ambapo alitaka kumkusanyia watu hivyo OFM kupata wakati mgumu kabla ya mrembo huyo kutimua kwa kumnyeshea mvua ya matusi.

OFM ARUDI TENA KUNDINI Licha ya Irene kushtuka kama anataka kupigwa picha, OFM ilirudi tena katika kundi hilo kwa lengo la kumpata mwingine kwa kuwa alikuwa bado mmoja wa memba hivyo ikawa rahisi kuchukua na namba ya mwingine lakini kila alipokuwa akipigiwa alipokea na kudanganya maeneo alipo.

WASIKIE TCRA Baada ya kujiridhisha kuwepo kwa mbinu hiyo mbadala OFM iliwasiliana na Meneja Mawasiliano wa TCRA, Innocent Mungy ambaye alisema kuwa, ishu hapo ni kuwe na mtu wa kwenda kulala kwenye Kitengo cha Uhalifu wa Kimtandao cha Polisi (Cyber Crime Unity) ambao hao ndiyo wenye idhini ya kumkamata mtu.

KITENGO CHA CYBER Kuhusu ishu hiyo, kamanda wa kitengo hicho, Mwangasa Joshua aliliambia gazeti hili kuwa baada ya kupokea malalamiko juu ya biashara hiyo, jopo lake la uchunguzi litakaa na kuyabaini ‘magrupu’ hayo ili kuyachukulia hatua kwani Sheria ya Makosa ya Mtandao ipo na inafanya kazi.

TUJIKUMBUSHE Juni mwaka jana, Makonda alitangaza vita na makakapoa (mashoga) na madadapoa (machangu) walioko jijini Dar kuwa ataendesha msako mkali wa kuwaondoa, jambo lililofanikiwa kwa kiasi kikubwa.

Credit - Global Publishers

Zitto Awashauri Wanahabari Kugomea Kutoa Habari za Serikali

$
0
0

Zitto afunguka haya hapa chini baada ya kauli ya Magufuli leo


Mdau una Maoni Gani?

Alichokisema Wema Sepetu Baada ya Rais Magufuli Kumtetea Makonda Leo....

$
0
0

Wema Sepetu Kupitia moja ya Account zake za kijamii ameandika ujumbe ambao dhahiri shari kuwa unamuelekea Rc Makonda kwa njia ya mafumbo

ameandika hivi

Ukiona twiga anaringa mbugani basi ujue simba bae wake,,,,

Ukweli Mchungu..Hii Ndiyo Sababu ya Rais Magufuli Kutomtumbua Rc Makonda Hadi Sasa...!!

$
0
0

Naamini wengi wenu humu ndani leo mlitegemea mkuu wa mkoa wa Dar kutumbuliwa na mheshimiwa mtukufu rais wa JMT.

Imani hiyo naamini iliongezwa na utolewaji wa video ya usalama ya kituo cha habari na burudani cha Clouds ambapo mkuu wa mkoa alionekana akiingia na askari wenye bunduki kwenye ofisi za kituo hicho majira ya usiku.

Hilo la kutumbuliwa halijatokea na kusema ukweli mimi sikuwa nategemea litokee hapo Ubungo mbele ya kadamnasi [ingawa Magu na huyo Makonda wake wameshawahi kumtumbua mtu hadharani]. Sikutegema wao kwa wao watumbuane hadharani.

Kwa jinsi rais Magufuli alivyo na kwa jinsi suala zima la vita dhidi ya Makonda linavyoendeshwa hivi sasa [kiudaku udaku hususan huku mitandaoni] mimi sitegemei kuona wala kusikia kuwa Makonda atatumbuliwa hivi karibuni. Uwezekano wa kutumbuliwa upo ila uelekeo wake mimi siuoni.

Kwa nini nasema hivyo? Nasema hivyo kwa sababu nadhani Magufuli akifanya hivyo atakuwa kama kasalimu amri ya shinikizo linalotoka huku kwenye mitandao na sidhani yuko tayari aonekane kasalimu amri.

Naamini kabisa Magufuli naye anayaona makosa ya Makonda. Ila sidhani kama 'ego' yake itamruhusu kufanya vile ambavyo wengi, hususan huku kwenye mitandao, wanataka afanye. Akifanya hivyo itakuwa ni kama kawapa ushindi wapinzani wake.

Baada ya muda suala hili la Makonda litapoa tu. Sina hakika itachukua muda gani lakini naamini litapoa tu.

Likishapoa ni imani yangu pia kuwa hapo ndo utakuwa mwanya wa Magufuli 'kumpangia' Makonda shughuli nyingine.

Lakini kwa sasa jinsi mazingira yalivyo [mipasho madhabahuni, matusi mitandaoni, drama magazetini, n.k.] sidhani kama yanampa rais nafasi nzuri ya kufanya kile ambacho wapinzani wake wanamtaka afanye.

Naona labda hataki kuweka precedent ya kuyumbishwa na kelele za watu. Tena watu wanaomtukana hadi matusi ya nguoni. Watu wanaomzushia kila aina ya uzushi. Watu wamefikia hadi hatua ya kudokeza kwamba Makonda na Magufuli ni wapenzi....seriously?

Mtu mnamtukana hivyo halafu bado mnategemea afanye jambo la kuwasuuza nyonyo zenu? Acheni masikhara bana.

Ila muda utatuonyesha tu....tusubiri tuone.

Zitto Kabwe Atoa Kauli Tata Baada ya Magufuli Kushindwa Kumtumbua Makonda Leo...!!!

Jenerali Ulimwengu Ashauri Makonda Ashitakiwe kwa Kuvamia Kituo cha Clouds...!!!

$
0
0

Akihijowa na DW mchana huu Jenerali Ulimwengu ameshauri Makonda ashitakiwe...

Amesema ni tukio linaloweza kufanywa na viongozi ambao wanajiona hawana mipaka katika utawala wao. 

Amesema mkuu wa mkoa amelewa madaraka na kwa kufanya tukio hilo ameonyesha kwamba hana kitu chochote kinachoweza kumzuia. Amewaomba wananchi kupata sauti zao katika kutetea haki zao.

Amesema suala la Makonda kuwajibishwa linategemea na mtu aliyemchagua ambaye ndiye kiongozi wa nchi kwa hiyo Raisi akiona kwamba kuna haja ya Makonda kuwajibishwa basi amuwajibishe ili iwe fundisho na kwa viongozi wengine.

Rais Wangu Magufuli: Makonda Ulimtengeneza Alengwe - Wape Ushindi Wao...

$
0
0

Na. M. M. Mwanakijiji 

Ninalirudia hili mara nyingi siku hizi za hivi karibuni - tunatumia muda mwingi kujadili mambo ambayo yalitakiwa yawe ya kujadilika siku moja yakaisha. Inasikitisha, inaudhi, inakera na inakatisha tamaa kuona karibu taifa zima tunazungumzia suala ambalo kama kungekuwa na hekima, busara na weledi lingeisha mapema sana na wala lisingezaa mambo mengine. 

Suala la cheti cha Makonda au kubadili jina lake wala halikuwa jambo ambalo halitatuliki kwa haraka. Naamini lingeweza kuzungumzwa, kutolewa uamuzi na watu wangesonga mbele; hata kama ni kuendelea na Makonda watu wangeendelea kama ingetolewa kauli ya kwanini watu wanaendelea. Ambao wangetaka kuendeleza ligi wangeendeleza tu. 

Bahati mbaya sasa limefika mahali kwamba linahoji siyo tu hekima, bali uthubutu, busara, umakini, heshima na tunu nyingine mbalimbali za Rais na viongozi wenzake wa juu. 

Niseme tu kuwa, Makonda angeweza kuendelea kuwa mkuu wa Wilaya au hata na utumishi ndani ya chama akiendelea kujengwa na hata kushughulikia mambo mengine. Niliandika wakati anateuliwa ukuu wa wilaya kuwa ilikuwa ni jambo la ajabu kidogo. Na sikutaka kuendelea kuandika muda wote baada ya hapo. Sababu kubwa ni kwamba, ni kiongozi kijana ambaye anahitaji muda wa kujifunza na kufunzwa. Sijui kama ameshajifunza lakini nina uhakika matukio ya hivi karibuni yatakuwa yamemfunza mambo mengi tu. 

Hata hivyo, Makonda amejikuta kwenye hali ngumu ya mengi si kwa sababu ya yeye mwenyewe tu bali kwa sababu ya Rais wangu Magufuli mwenyewe. Alimteua kuwa Mkuu wa Mkoa na kumbakisha Dar-es-Salaam kama namna ya kuwakata ngebe watu waliokuwa wanamsemasema sana akiwa Mkuu wa wilaya. Alimpa Dar kama alama ya "wakome" waliokuwa wanamsema. Ni yeye alimfanya Makonda awe mlengwa wa kisiasa (political target). Katika siasa kama vile ilivyo katika mapenzi na vita - yote yanaruhusiwa (all is fair in politics just as they are fair in love and war). Kama alitaka kumtumia Makonda kama mjeledi wake wa kisiasa katika Jiji la Dar basi alipaswa kujua kuwa na wenzake wanaweza kumtumia huyo huyo Makonda kumfanya awe mjeledi wao. 

Lakini pia pamoja na hayo kitabia, na weledi wa kiuongozi Makonda mwenyewe pia amejitengeneza kuwa mlengwa. Tangu sakata lake lianze na mashambulizi yaanze dhidi yake ni wachache wameonesha kujali kumuonea huruma. Hii imenishangaza kidogo lakini nimeelewa. Kama hawawezi kumgusa mfalme, kwanini wasimguse mtoto wa Mfalme? Tuliliona hili kwa Kikwete sana; pale ambapo watu waliona ni ngumu kumgusa Kikwete wakaamua kumgusa Ridhiwani - kwa ukweli au la. Bahati mbaya Makonda amechukuliwa na wengi na jinsi alivyojengwa kama vile ni mtoto wa Magufuli mwenyewe na hivyo kama watu hawawezi kumgusa Magufuli basi watamgusa "mwanaye mpendwa aliyependezwa naye". 

Lakini, ukiondoa tuhuma za vyeti - ambazo kama nilivyoelezwa jana kwenye ZamaMpya - kwa kiasi kubwa zile zilikuwa ni siasa zaidi. Kulikuwepo na hoja lakini haikuwa hoja kubwa kivile bahati mbaya ni hoja inayomhusu mpendwa wake na hivyo imekuwa hoja kubwa. Kama ingewezakana kumuangusha Makonda kwa suala la cheti wangeweza lakini naamini lile lilikuwa linapita na nilitarajia lipite kwa maelezo machache tu. Ikulu ingeweza kulizima lile hata kwa hadaa za kisiasa (serikali inafuatilia tuhuma mbalimbali dhidi ya Makonda lakini hadi hivi sasa Rais ana imani naye - kauli ingesema). Watu wangekasirika na kulalamika lakini lingepita. 

Nina uhakika lingepita kwa sababu hata waliotoa tuhuma zile za vyeti wanajua kabisa kuwa kipimo hicho kikiendelea kutumiwa kwamba hata mtu aliyesoma baada ya kubadilishwa jina lake na wazazi wake akiwa darasa la saba au kidato cha nne basi wengi watakwenda na maji. Wengi walikuwa na ukali zaidi kwa mtu aliyefoji cheti cha taaluma kuliko aliyetumia jina jingine kwenda kusoma na kupata taaluma ya ukweli. Kuna tofauti ya John Juma kusema ana shahada ya uhandishi na kuonesha cheti wakati hana elimu hiyo bali cheti kanunua mtaani na mtu ambaye anaitwa Juma John ambaye jina lake la asili ni Fredy Ramadhani. Juma John akaenda akasoma, akafaulu, akaenda chuo kikuu akapasi vizuri akiwa na jina hilo jingine na akawa na elimu ya uhandisi na kazi yake ikaonekana ana tofauti sana na John Juma mwenye cheti feki! Sidhani kama kuna mtu ambaye ama shule ya msingi au sekondari ambaye hakuwa kukutana au kusoma na kina Juma John na akawaheshimu. 

Kuwafukuza kina Juma John kazi baada ya kuwekeza kote katika elimu yao ni dalili ya kutokuwa na hekima na kukosa ubunifu wa kusahihisha na kuadhibu makosa ya wa zazi wao lakini bila kuwapoteza hawa hasa kama ni watu wenye weledi na waadilifu. Bora unipe Juma John kuliko mtu ambaye ana jina lake la asili na amesome kote lakini hajaelimika, hana weledi na ni janga katika mahali pa kazi. Kuna faida gani ya kuwa mtu mwenye jina halisi lakini hana a wala be ya utendaji? Ndio maana nasema suala la cheti halikuwa kubwa isipokuwa limekuwa kubwa kwa sababu ni la mpendwa wa Rais. 

NI kwa sababu hiyo basi naamini, tuhuma hizi mbili kubwa za wiki iliyopita ni kubwa mno kiasi kwamba wanaotaka Makonda aondolewe - hata kwa kuwa demoted - wanafanya hivyo kwa haki na ni ushindi ambao wameushinda. 

Katika mapambano kuna kushindwa baadhi ya mapigano; si lazima ukubali umeshindwa vita. Magufuli raia wangu kwenye hili la Makonda umeshindwa pigano hili, na kwa vile wewe pia ni mwanasiasa unajua ni wakati gani wa kukubali kushindwa na kuamua kujipanga upya. Na njia mojawapo ya kujipanga ni kuhakikisha watendaji wako huwafanyi wawe walengwa wa kuangushwa na mojawapo ni kuhakikisha wanasimamiwa vizuri katika utumishi. 

Kwa sababu sasa hivi ukiangalia kinachohojiwa siyo tena Makonda bali ni wewe mwenyewe. Kama ulimuondoa Kitwanga kwa kuhutubia Bunge akiwa amelewa na alikuwa ni Waziri na inadaiwa alikuwa ni rafiki yako wa karibu ni kitu gani kimefanya mtu mwenye tuhuma kama za Makonda kuendelea kuwepo hata kwa siku nyingine moja? Maana hata Mlevi anaweza kusema kweli akiwa amelewa na akawa sahihi! 

Rais wangu Magufuli wape wapinzani wako ushindi huu kwani wamekushinda katika hili; halafu twende kwenhye mambo mengine ya kitaifa na ya kulijenga taifa, siyo ya kutafuta kujibu mashambulizi, kukomoa na visasi. Acha kazi yao na utendaji wako useme wenyewe. Waache Watanzania waangalie jinsi unavyotekeleza kazi zako na unavyowasimamia watendaji wako. Usiwape mianya isiyo ya lazima. 

Lakini ukiwapa mianya hiyo, usishtuke, usikasirike wala kukwazika wao nao wakaaitumua kukugonga na wewe mumo kwa mumo. 

Ndio siasa hiyo. Kuna magoli unaweza kuyapinga lakini mengine inabidi ukubali tu umefungwa. Huitaji kamera kukuonesha goli limeingia kweli kweli.

Nape Nnauye : Hili Likinishinda Hakika Nitajiuzulu

$
0
0

Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo Mhe. Nape Nnauye amesema endapo atashindwa kusimamia uhuru wa habari na vyombo vya habari nchini atakuwa hafai kubaki kwenye nafasi hiyo kwa kuwa atakuwa ameshindwa majukumu yake katika nchi huru

Nape ametoa kauli hiyo leo wakati akizungumzia na kulaani kitendo kinachodaiwa kufanywa na Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam, Paul Makonda, cha kuvamia chombo cha habari cha Clouds, akiwa na askari wenye silaha na kukifananisha kitendo hicho na kuinajisi taaluma ya habari.

Waziri huyo amesema amezoea kuona matukio kama hayo yanatokea kwenye nchi ambazo zimepinduliwa kwa bunduki lakini kwa nchi yetu si jambo jema kwenda kwenye vyombo vya habari na mabunduki mkononi.

"Tumezoea kuona matukio haya yanatokea kwenye nchi ambazo zimepinduliwa kwenda kwenye vyombo vya habari na mabunduki si sawa, kwa jambo hili tunataka kutenda haki tumsikilize Mkuu wa Mkoa ili tujue kwanini amefanya jambo hili". Alisema Nape

Kufuatia tukio hilo Waziri Nape ameunda tume yenye wajumbe takribani watano itakayoenda kumhoji Makonda na kutoa mrejesho wa kazi hiyo ndani ya masaa 24 ikiwa imeeleza sababu maalum kutokea kwa tatizo hilo.

Pamoja na hayo Mwenyekiti wa Chama cha Wamiliki wa Vyombo vya Habari (MOAT), Dkt. Reginald Mengi amesema hawezi kutoa lawama kwa mtu yoyote mpaka pale ukweli utakapofahamika japokuwa ameonekana kukerekwa.

"Kwetu sisi hili ni jambo ni la hatari sana, linatuogopesha na linatishia maisha ya waandishi wa habari". Alisema Dkt. Mengi

Kwa upande mwingine Mengi amewasihi waandishi wa habari kutokuwa waoga kwa jambo lolote wanalopambana nalo ila wanachopaswa ni kufanya kazi kwa kufuata misingi iliyowekwa.

Nahitaji Ushauri, Mke Amebadilika Sana Tangu Mimi Niondoke..

$
0
0

Wadau hamjambo,

Naomba msaada, niko South Africa since last week, niliondoka Tz mpaka South Africa baada ya kupata mchongo kwa rafiki yangu ambaye alinitafutia mchongo wa kazi.

Namshukuru Mungu nilifika salama na maisha yanaendelea vyema kabisa.
suala kubwa lililopo ni kuhusu wife wangu, kipindi naondoka nilimshirikisha lakini alionekana kuwa na hasira sana juu ya uamuzi wangu wakuja South,

Nilijaribu sana kumsihi yakuwa nakuja kuangalia namna mambo au upepo ulivyo kisha nitageuza lakini alishindwa kunielewepa kabisa na kuwa mtu mwenye hasira kiasi ambacho hata unyumba alininyima.

Nikafikiri sana namna gani yakufanya, sikuona namna, maana nilikuwa tayari nishakatiwa ticket ya kuja na kurudi(Go and Return) yaani kama mambo yakiwa mabaya niko huru kurudi. Basi kiukweli nilichukua uamuzi mgumu nikafwatilia kila kitu na safari ikaiva yakuja South, nikaondoka na kufika salama.

Lakini kabla sijaondoka wife alinitumia sms na kuniambia nisimshirikishe lolote wala kumpigia wala kuhangaika na yeye.

Sasa tangu nimefika nimejaribu kumtumia sms, kutaka kujua hali ya maendeleo na nilimwomba hata akaunt ya bank ili nimtumie pesa kwa ajili ya matumizi, lakini wadau huyu mwanamke alinitukana na kunitumia sms za ajabu sana, oooh, wewe mwanaume gani, tena kwa taarifa yako nimeshapata baba wa mtoto na maneno mengine mengi ya ajabu.

Kweli najisikia vibaya sana na majuto kuwa na mwanamke mwenye hasira na asiye na kipimo cha maneno kwangu kwa heshima. Japo alinitukana vya kutosha lakini sijaacha kumtumia sms za kutaka kujua hali yake na mtoto, ila cha ajabu hajibu chochote.

Niko njiapanda, nishaurini nifanye nini, kwa wadau naombeni ushauri wenye hekima ili niuchukue maana niko mbali na ninahisi kuumia sana.

Please ushauri sio kejeli.

Thanks wadau.

Nawasilisha
Viewing all 104766 articles
Browse latest View live




Latest Images