Quantcast
Channel: UDAKU SPECIAL
Viewing all 104689 articles
Browse latest View live

Nape Aonja Chungu ya Bao la Mkono..Habari Katika Magazti ya Leo 24/3/2017..!!!


Duhh,,Mwanafunzi wa Shule ya Msingi Afanya Ngono na Walimu Watatu..!!!

$
0
0

Mwanafunzi wa Shule ya Msingi Ruwenzera amedai kufanya ngono na walimu wake watatu kwa nyakati tofauti baada ya kuahidiwa kupewa zawadi na fedha.

Akizungumzia sakaa hilo, mwenyekiti wa kamati ya shule hiyo, Masele Omary alisema kuwa Machi 7 uongozi ulikutana na kufikia uamuzi wa kumuomba mkurugenzi mtendaji wa wilaya awaondoe walimu hao baada ya kujiridhisha na maelezo yaliyotolewa na mwanafunzi huyo.

 Kwa mujibu wa mwanafunzi huyo anayesoma darasa la saba, alifanya ngono na walimu hao kwa nyakati tofauti baada ya kumshawishi kumpa Sh10,000 na mwingine kuahidi kumnunulia nguo za ndani.

Alidai mwalimu Gerard Paulo alimuahidi kumnunulia nguo za ndani, huku Osner Yohana na mwingine (jina linahifadhiwa kwa kuwa hakupatikana kuzungumza) alimshawishi kwa kumpa Sh10,000 kila mmoja.

Wakizungumza kwa nyakati tofauti, Paulo na Yohana walikana kumrubuni mwanafunzi huyo wakidai tuhuma hizo zinatokana na wao kuhoji matumizi ya fedha za ukarabati na michango ya chakula.

Baada ya Kutua Clouds Fm na EFM,Gwajima Leo Kusikika Live Kupitia Radio One na ITV...!!!

$
0
0

Askofu wa Kanisa la Ufufuo na Uzima, Bishop Josephat Gwajima amesema kuwa Ijumaa hii atatembelea IPP media kwaajili ya kuwapa pole wana tasnia ya habari kwa yaliyotokea.

Ijumaa iliyopita kituo cha Clouds kilivamiwa na Mkuu wa mkoa wa Dar es Salaam, Paul Makonda akiwa na askari wenye mitutu kitendo kilichopingwa na wadau mbalimbali wa habari.

“Leo  24/03/2017 nitatembelea ofisi za IPP Media ikiwa ni ziara Ya kuwapa pole wanatasnia ya Habari kwa yaliyotokea,” ameandika kupitia akaunti yake ya Instagram.

Alhamisi hii Askofu huyo ametembelea EFM redio na TVE.

Siku Tano za Mwisho za Nape Nnauye Ofisini Zilivyompa Heshima Kubwa kwa Wadau wa Habari Nchini!

$
0
0

NAPE Nnauye, jana ameondolewa kwenye nafasi yake ya Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo, kufuatia mabadiliko madogo yaliyofanywa katika Baraza la Mawaziri na Rais John Pombe Magufuli.

Ingawa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania anayo mamlaka ya kufanya uteuzi wa nafasi yoyote wakati wowote kwa mujibu wa katiba, tukio la kuondolewa kwa Nape, limepokewa kwa mshtuko mkubwa na tasnia ya Habari nchini, hasa kwa kuwa alionekana dhahiri kuwa pamoja nao katika kipindi hiki ambacho wametikiswa.

Nape, mtoto wa kada wa zamani wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) Brigadia Moses Nnauye, aliteuliwa katika Baraza la Mawaziri la Kwanza la Rais John Magufuli Desemba 9, 2015 kushika wadhifa huo. Hadi jana wakati akiondolewa ofisini, Nape anakuwa amehudumu katika uongozi huo kwa siku 467, huku akionekana kama mtu ambaye alitekeleza majukumu yake kwa namna ya kipekee, kwani kwa muda wote huo, aliweza kukutana, kujadili na kutoa maamuzi mazuri kwa watu wote waliohusika na wizara yake.

Ingawa wizara yake ilihusika na wanamichezo, wasanii, wana utamaduni na wanahabari, lakini ni watu wa kundi la mwisho ndilo waliopatwa na mshtuko mkubwa, hasa kwa kuangalia siku zake tano za mwisho akiwa kiongozi, jinsi alivyoshirikiana nao katika tukio kubwa na baya kuwahi kuitokea tasnia ya habari Tanzania.

Ijumaa ya Machi 17, 2017 usiku, chumba cha habari cha televisheni ya Clouds kilivamiwa na askari, wakiongozwa na Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam, Paul Makonda ambaye alikwenda studio na kuwatisha watangazaji, kwa kitendo chao cha kushindwa kurusha habari iliyokosa vigezo, iliyomhusu Askofu wa Kanisa la Ufufuo na Uzima, Josephat Gwajima.

Tukio hilo lilibakia kuwa siri ya kituo hicho hadi video fupi ilipovuja, Jumapili Machi 19, 2017 na kuzua mjadala mkubwa mitaani na kwenye mitandao mbalimbali ya kijamii, kitu kilichomuibua Waziri Nape ambaye kupitia akaunti yake ya mtandao wa Twitter, alisema kama Waziri anayehusika na habari, angekwenda kesho yake, Jumatatu katika ofisi hizo ili kujua kilichotokea. Jumatatu ya Machi 20, 2017 Waziri Nape alikwenda Clouds kama alivyoahidi na huko akakutana na uongozi wa Clouds Media Group, chini ya Mkurugenzi wake Mtendaji, Joseph Kusaga na kufanya mazungumzo.

Pia alikuwepo Mwenyekiti Mtendaji wa kampuni za IPP, Reginald Mengi ambaye ni Mwenyekiti wa chombo cha wamiliki wa vyombo vya habari, MOAT. Akionekana mtu aliyesikitishwa na tukio hilo, Nape aliteua Kamati ya watu watano, ikiongozwa na Mkurugenzi wa Idara ya Habari (Maelezo) Dk.
Hassan Abbas ili kutafuta ukweli wa tukio hilo na kuwapa saa 24 ili wakamilishe ripoti yao. Jumanne, Machi 21 waandishi wa vyombo mbalimbali vya habari walikusanyika Makao Makuu ya Mamlaka ya Mawasiliano nchini (TCRA) barabara ya Sam Nujoma kusikia kilichosemwa na Kamati, lakini hakukuwa na chochote, kiasi kuzua minong’ono kuwa ‘wakubwa’ wamezuia ripoti hiyo, jambo ambalo lilikanushwa na Nape, aliyetaka kuwepo kwa subira, kwani kamati yake ilikuwa bado kazini.

Jumatano, Machi 22, 2017 katika Ukumbi wa Idara ya Habari (Maelezo) Waziri Nape alipokea ripoti ya kamati hiyo, ambayo kabla ya kukabidhiwa, ilisomwa hadharani na Katibu wake, Deodatus Balile. Akiipokea ripoti hiyo, Nape alisema imemsikitisha na akawataka viongozi kuwa na ngozi ngumu, hasa wanapoongoza watu.

Alisema yeye sio mtu wa kutoa uamuzi juu ya suala hilo, isipokuwa ripoti hiyo ataiwasilisha kwa mamlaka ya juu yake, ambao ni Waziri Mkuu, Makamu wa Rais na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, ambao ndiyo wenye mamlaka ya maamuzi.

Jumatano, Machi 23, 2017 taarifa iliyosainiwa na Mkurugenzi wa Mawasiliano Ikulu, Gerson Msigwa ilisema Rais John Magufuli amefanya mabadiliko madogo katika Baraza la Mawaziri, kwa kumteua Dk. Harrison Mwakyembe kuwa mbadala wa Nape, huku nafasi yake yeye (Mwakyembe) ikichukuliwa na Profesa Paramagamba Kabudi. Maisha kweli hayatabiriki, anyway, Karibu Mheshimiwa Harrison Mwakyembe, uanzia pale alipoacha Nape Nnauye!

Diamond, Belle9 Wambeba Saida Kalori...!!!

$
0
0

WASANII wa Muziki wa Bongo Fleva, Nasibu Abdul ‘Diamond’ na Abednego Damian ‘Belle9’ wamembeba msanii mwenzao anayeimba nyimbo za asili, Saida Kalori kwa kushiriki katika albamu yake itakayoitwa Naamka.

Akilonga na Showbiz, Saida aliyewahi kutamba na Wimbo wa Chambua Kama Karanga ‘Maria Salome’ alisema kuwa anamshukuru Mungu amerudi tena kwenye gemu na wasanii hao wamempa nguvu ya kufanya vizuri katika albamu
hiyo.

“Nimeamka tena jamani nashukuru nimebebwa na wasanii wenzangu Diamond na Belle9 ambao nimewashirikisha kwenye nyimbo zangu ambazo zipo kwenye albamu itakayotoka hivi karibuni,” alisema Saida.

Kwa nyakati tofauti Belle9 ameachia Wimbo wa Give It To Me ambapo ndani yake ameweka vionjo vya Wimbo wa Chambua Kama Karanga wakati Diamond naye amefanyia ‘remix’ ya wimbo huo wa Saida kwa kuita jina la Salome

Kimenukaa..Gazeti la Dailymail la Uingereza Waandika Mazito Baada ya Nape Nnauye Kutumbuliwa Uwaziri..!!!

$
0
0

Tanzania's information minister was fired on Thursday after he criticised an ally of President John Magufuli who had stormed into a television station accompanied by armed men.

The sacking comes amid an uproar over the incident at one of Tanzania's main private broadcasters, seen as yet another example of the government riding roughshod over basic freedoms since Magufuli came to power in October last year.

On Friday, Dar es Salaam regional commissioner Paul Makonda stormed into the offices of the Clouds FM Media Group with six armed men to demand the airing of a muckraking video aimed at undermining a popular local pastor with whom Makonda has a dispute.

The station refused to broadcast the video in which a woman claims to have had an illegitimate child with the pastor.

Information Minister Nape Nnauye visited the station in the wake of the intrusion and launched an immediate probe.

"We are used to seeing such incidents during coups d'etat, when armed men enter studios to proclaim they are overthrowing the state," he said.

"If it happens in a state which is not undergoing a coup d'etat, where the president is in place, it gives a very bad image. I will advise my bosses to take punitive measures against the regional commissioner," he said.

Meanwhile, as condemnation poured in from civil society and MPs, Magufuli offered support to his embattled ally.

"I, as president, don't let anyone tell me what to do. I decide who should be where. So you Makonda, do your job and ignore the rest," he said.

On Wednesday Deodatus Balile, chairman of the probe team, revealed his findings, saying Makonda had threatened station staff with blackmail and jail if they didn't air the video.

Then on Thursday, without any explanation, the presidency released a statement announcing the appointment of a new information minister.

Nnauye said he was "just trying to do his job" as he addressed journalists from his car Thursday after police stopped him from holding a press conference in a hotel in the capital.

He said people should not be concerned about him, but about "where Tanzania is headed".

- Bulldozer -

Magufuli, whose nickname "tingatinga" means "bulldozer" in Swahili, swept to power as a no-nonsense, corruption-busting, man of the people shown sweeping the streets while summarily firing officials suspected of ineptitude or corruption.

But critics see a wide authoritarian streak at the core of his populism, as he acts on impulse regardless of due process or political niceties, while being intolerant to any dissent.

Earlier this month he ordered all the passports seized of foreign workers at an Indian company which had failed to complete a water project on time.

Magufuli has also shut down newspapers, banned opposition rallies, switched off live broadcasts of parliamentary sessions and applied a draconian "cyber crimes" law to jail critics.

"Since the inauguration of President Magufuli, attacks on freedom of the press have increased in a worrying manner," said Clea Kahn-Sriber, Africa head at pressure group Reporters Without Borders, known by its French acronym RSF.


Kimenukaa..Mwigulu Nchemba Aingilia Kati Suala la Nape,Atoa Amri kwa IGP..!!!

$
0
0

Mh.Nape Moses Nnauye sio jambazi, ni mtanzania, ni mbunge, mjumbe wa NEC wa CCM, hana record ya uhalifu. Kitendo cha mtu kumtolea Bastola, Sio cha kiasikari, sio cha kitanzania na sio cha ki Mungu, kama mtu ameweza kutoa Bastola mbele ya Kamera nawaza mbali ingekuwa kwenye uchochoro angefanya nini. 
Nahusika na Usalama wa Raia wote wa Tanzania, nimemwelekeza IGP atumie picha kumsaka mtu yule aliyeinua kufanya kitu cha kihalifu kwa kofia ya uaskari. Na kama ni Askari basi sheria zinazoongoza taasisi husika zichukue mkondo wake.

Noma Sana..Mange Kimambi Afunguka Haya Baada ya Mwigulu Nchema Kutaka Askari Aliyemuonyesha Bastola Nape Kukamatwa...!!!

$
0
0

Ahsante Mwigulu., naamini mkuu hatokutumbua sababu alietoa bastola hakuwa Daudi Bashite... Ingekuwa ni Daudi Bashite alietoa Bastola Alafu wewe ukaagiza Hatua zichukuliwe ungeondoka kaka. Haki vile ingekuwa Mtoa Bastola ni Daudi Bashite Alafu ukato agizo hili saaa hivi ningekuwa nachangisha michango ya Farewell party yako!!

Alafu Vipi makosa ya Bashite?? Huyo mbona humgusi?? 😭😭 Nakutania tu , linda kibarua chako mwaya, Huyo Hata ukimuita kwa mahojiano tu kazi huna!!!

Rais John Magufuli: Nikisema Ukweli, Watanzania Wenye Uchungu Mtalia!!!

$
0
0

Rais wetu kipenzi, Mheshimiwa John Pombe Magufuli, jana alifanya yale ambayo huwa anayapatia kweli kweli!! 

Kwa kutumia umahiri mkubwa kabisa, bila shaka aki-apply mbinu za kijeshi alizowahi kujifunza JKT, Mheshimiwa Magufuli aliingia bandarini kwa kushitukiza hali iliyowafanya watu wa pale wapigwe butwaa huku wengine mioyo yao ikipiga mkamba kwa sababu hawakutarajia kutokea Mheshimiwa huyo!!!

Mbinu hizi za kijeshi, na bila shaka zikichanganyika na mbinu za kijasusi; zilimwezesha Mheshimiwa Rais wetu aweze kukamata makontena kadhaa yaliyojaa dhahabu!!! 

Huku akionekana kujawa na uchungu kwa nchi yake, Mheshimiwa Rais John Pombe Magufuli alisema:
Kwa taarifa nilizonazo, nikizisema hapa mnaweza mkalia! Dhahabu iliyopo humu ndani! Kwa Mtanzania yeyote anayeipenda Tanzania... atalia! Kwa mali zilizomo humu...!

Kimenukaa...Familia ya Makonda Yaanika Ukweli Wote Juu ya Jina la Bashite,Wadai ni Lake Kabisa,Wamshangaa Kujiita Paul,Wadai Toka Apate Madaraka Kawasusa Huko Kijijini..!!!!

$
0
0


Mzee Khamesse
Kutokana na kuwepo kwa taarifa za Paul Makonda kulelewa katika familia ya aliyekuwa Meya wa Jiji la Mwanza, Seleman Khamesse, JAMHURI limefika nyumbani kwa Mzee Khamesse, katika eneo la Nyamanoro, jijini Mwanza na kufanya mahojiano;

JAMHURI; Kuna taarifa kuwa Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam, Paul Makonda amewahi kuishi nyumbani kwako. Je, ni kweli?

KHAMESSE; Ni kweli Daudi alikuja kwangu akiwa darasa la tano akitokea kijijini kwao, Koromije na kisha kuishi hapa na familia yangu.

JAMHURI; Mbona unasema uliishi na Daudi wakati nimekuuliza kuhusu Paul Makonda?

KHAMESSE; Ni kweli nimesema Daudi kwa sababu namfahamu kwa jina hilo. Amekuja kwangu akitokea kwa wazazi wake waliokuwa wakiishi Koromije, na jina lake ni Daudi Albert Bashite.

Wakati shangazi yake ambaye ni mke wangu mdogo (Mama Khamesse) anamleta hapa alikuwa akitumia jina hilo na hata alipopelekwa shule alikuwa akitumia jina la Daudi Bashite wakati anasoma Shule ya Msingi Nyanza.

Hata wakati anakwenda kuanza shule Pamba Sekondari alienda kwa jina la Daudi Bashite.

JAMHURI; Una uhusiano gani na Daudi?

KHAMESSE; Daudi ana uhusiano na mke wangu mdogo Bernadeta maarufu kama Mama Khamesse. Mama ndiye aliyemleta hapa kwani ni shangazi yake anaweza kukwambia zaidi kuhusu hilo.

JAMHURI; Tangu alipoteuliwa kuwa Mkuu wa Wilaya ya Kinondoni na kisha Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam mmekuwa mkiwasiliana?

KHAMESSE; Hatuna mawasiliano kwani tangu ateuliwe amewahi kufika nyumbani kwangu hapa tulipo mara mbili tu, tena alikuja usiku.

Mara ya kwanza alikuja saa saba usiku, hakuingia ndani aliishia nje akaongea na vijana wenzie akaondoka. Mwaka jana mwezi wa Ramadhan alikuja saa tano usiku akiwa amesindikizwa na vijana wawili hakuingia ndani aliishia nje akaongea na vijana wenzie, kwa vile nilikuwa sijalala tulisalimiana akanipatia mawasiliano yake kisha akaondoka.

Ukweli ni kwamba hatuna mawasiliano, kutokana na kwamba haoneshi kuhitaji kuwasiliana kwani namba alizonipatia nikipiga hapokei, hata nilipotuma ujumbe hakukuwa na majibu.

Ila wasiliana na shangazi yake anaweza kukueleza zaidi maana mie sikukaa naye sana kutokana na majukumu yangu yaliyokuwa yakinikabiri wakati huo. Pamoja na kwamba alikuwa akiishi nyumbani kwangu.

Ramadhani Khamesse
Ramadhani ni mtoto wa Mzee Khamesse, ambaye alikuwa akisoma shule moja na Paul Makonda, amesema kwamba amesoma na kuishi na Makonda katika kipindi chote alichokuwa nyumbani kwao.

“Tulikuwa naye shule moja ya Nyanza, na jina lake ni Daud Albert Bashite. Dada yangu, mimi, huyu Daudi tulikuwa tunalala naye chumba kimoja hivyo namfahamu. Pia tulikuwa rika moja hivyo hata michezo yetu ilifanana ingawa tulikuwa tunatofautiana baadhi ya tabia,” amesema Ramadhan.

Akimuelezea Makonda amesema anajua kuishi na watu pale anapohitaji jambo lake lifanikiwe kwani alikuwa anajua kunyenyekea kwa walimu ingawa alikuwa na tabia ya kubagua marafiki hasa wale ambao familia zao zilikuwa duni. “Alikuwa ni rafiki wa wenye uwezo,” amesema.

Pia ameeleza kwamba baada ya kujiunga na masomo ya jioni Pamba Sekondari alihamia kwa ndugu yake mwingine anayefahamika kwa jina la Mwana Zakhia.

Kuhusu mawasiliano kati yao, amesema ingawa wamekua pamoja hakuna mawasiliano yoyote kati yao kutokana na Makonda kumpatia namba ambazo hata akipiga simu hazipolewi.

“Alikuja hapa mara mbili usiku tukazungumza mambo mengi ikiwa ni pamoja na kukumbushana maisha tuliyoishi. Zaidi ya hapo hatuna mawasiliano kabisa zaidi ya kumsikia na kumuona kupitia vyombo vya habari na mitandao ya kijamii,” amesema Ramadhani.

Mama Khamesse
JAMHURI lilifika nyumbani kwa Mama Khamesse Lumara na kufanya mahojiano;

JAMHURI: Una uhusiano gani na Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam?

MAMA KHAMESSE: Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam ni ndugu yangu kwani baba yake, Mzee Albert Bashite ni binamu yangu. Kwa hiyo Daudi ananiita mimi shangazi.

JAMHURI: Unaweza kunisaidia jila lake ni Daudi au Paul Makonda?

MAMA KHAMESSE: Mimi ninamfahamu kwa jina la Daudi Albert Bashite. Na hata wakati nampeleka kuanza shule katika shule ya mshingi Nyanza aliandikishwa kwa jina la Daudi Bashite.

JAMHURI: Ilikuwaje ukaanza kuishi naye?

MAMA KHAMESSE: Mama yake alikuja kuniomba mtoto wake aje kuishi na kusomea kwangu. Ukweli sikuona sababu za kumkatalia. Nilimkubaliana na kumpokea kisha ‘kumfanyia mpango wa kujiunga’ na shule ya Nyanza ambapo aliingia darasa la tano mpaka alipomaliza darasa la saba.

JAMHURI: Alipomaliza darasa la saba matokeo yake yalikuwaje?

MAMA KHAMESSE: Ukweli ni kwamba hakubahatika kufaulu ili kujiunga na kidato cha kwanza hivyo alilazimika kuanza kusoma masomo ya jioni katika shule ya sekondari ya Pamba.

Lakini hakuweza kukaa nyumbani kwangu kwa kipindi kirefu baada ya kuanza kusoma Pamba kutokana na sababu ambazo siwezi kukuelezea, kwani nilimuita mama yake tukazungumza kisha akamchukua na kumuhamishia kwa ndugu mwingine ambaye ni baba yake mdogo na Daudi.

Hata hivyo, wakati shangazi yake akigoma kutaja chanzo cha Makonda kuondoka kwa Mzee Khamesse, habari za uhakika ambazo familia ya Khamesse haikuthibitisha wala kukanusha zinasema Makonda alikuwa anachezea bunduki ya Mzee Khamesse risasi ikafyatuka na kupasua paa.

“Mzee Khamesse alisema huyu mtoto andoke haraka. Alisema kama amechezea bunduki yake kuna hatari anaweza akaua watoto wake kwa risasi kupitia michezo yake isiyokubalika,” kinasema chanzo chetu.

Mtu aliyeko karibu na Makonda amekiri lilitokea tukio hilo, ila akasema: “Hiyo ilikuwa michezo ya watoto. Mbona wengi tumemwaga uji wa mgonjwa? Ni hawa watu wa dawa za kulevya tu wanaochochea hata hayo mambo madogo.”

JAMHURI: Je, alimaliza masomo yake ya sekondari na kuhitimu?

MAMA KHAMESSE: Mh! Hapo kwenye kumaliza sekondari siwezi kukueleza lolote maana ni kautata kidogo kwani sikumbuki kitu kama hicho.

Ila ninachofahamu ni kwamba alianza kufanya kazi ya ukondakta wa daladala kwenye mabasi ya baba yake mdogo ambaye kwa sasa ni marehemu anayefahamika kwa jina la Mabina.

Baada ya muda kupita nilisikia kuwa amejiunga na Chuo cha Uvuvi Nyegezi, jijini Mwanza, na baadaye nikasikia yuko chuo huko Mbegani, Bagamoyo anasoma.

Lakini muda haukupita sana ndipo nikasikia kuwa amekuwa muhubiri hivyo alikuwa akihubiri injili na alikuwa akisafiri sana.

JAMHURI: Katika kipindi chote hicho uliwahi kusikia kuwa amebadili jina na kuitwa Paul?

MAMA KHAMESSE: Hapana nilikuwa sijawahi kusikia akiitwa jina zaidi ya tunalolifahamu wanafamilia la Daud Bashite. Na siku zote namfahamu kwa jina hilo hilo ingawa nilikuja kushangaa kuona kwenye luninga wakati yuko Umoja wa Vijana wa CCM (UVCCM) alipotambulishwa kwa jina la Paul Makonda.

Nilishangaa jina nikadhani wamekosea, lakini kila siku zinavyokwenda niliendelea kumuona kwenye luninga akitambulishwa kwa jina la Paul Makonda huku akiwa ni Daud Bashite ninayemfahamu.

JAMHURI: Hili jina la Makonda unadhani amelitoa wapi?

MAMA KHAMESSE: Jina hili la Makonda ni jina ambalo lipo katika ukoo, upande wa babu na bibi zake, hivyo sio jina jipya katika ukoo. Lakini suala la yeye kuanza kuitwa hivyo labda yeye binafsi au wazazi wake wanaweza kulisema hilo.

Ndugu

Mmoja wa ndugu zake wa karibu (jina linahifadhiwa) amesema kwamba Daudi alishindwa kuendelea kuishi nyumbani kwa shangazi yake (Mama Khamesse) kutokana na tabia ya kupenda kuwa karibu na marafiki wenye uwezo mkubwa jambo lililokuwa linamnyima uhuru kwani alikuwa na tabia ya kuhamia huko na kutorudi nyumbani.

“Daudi alikuwa anaweza kutoka nyumbani kwao Nyamanoro akahamia nyumbani kwa rafiki zake baada ya siku kadhaa akarudi nyumbani tena kwa shangazi yake. Tabia hii ilimkera Mama Khamesse ikamlazimu kuwasiliana na wazazi wake ambao walimuondoa hapo na kumpeleka kwa ndugu mwingine,” amesema.

Amesema Mzee Albert Bashite alibahatika kuzaa watoto wawili tu ambao ni Daudi na mdogo wake wa kike ambaye hata hivyo alifariki akiwa mdogo, hivyo Daudi ni mtoto wa pekee wa Mzee Daudi Bashite na Susan Daud Malagila. Jina la Daudi alilithi kutoka kwa babu yake mzaa mama.

Shule ya Msingi Nyanza
JAMHURI lilifika Shule ya Msingi Nyanza na kukutana na Mwalimu Mkuu ambaye alikataa kujitambulisha kwa jina kwa madai kuwa hawezi kuzungumza chchote mpaka atakapopata kibali kutoka kwa wakubwa wake.

JAMHURI: Mimi ni Mwandishi wa Habari kutoka Gazeti la JAMHURI. Nimefika kwako kupata ufafanuzi kuhusiana na taarifa za Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam kusoma katika shule yako ya Nyanza.

Mwalimu Mkuu: Siwezi kuzungumzia suala lolote linalohusu jambo hilo. Unatakiwa kuwa na kibali kutoka Ofisi ya Mkoa, nenda kwa RAS (Katibu Tawala wa Mkoa), RAS akishatoa kibali kitatakiwa kuthibitishwa na DAS (Katibu Tawala wa Wilaya), kisha utakipeleka kwa Afisa Elimu Wilaya, ambaye naye atakithibitisha na kukuelekeza kwa Mkurugenzi wa Wilaya ambaye atakupatia kibali cha kuja nacho hapa shuleni niweze kukujibu maswali yako.

Hapa unataka data (takwimu), na taratibu za kupata data unazifahamu. Hivyo siwezi kabisa kukusaidia chochote. Karibu tena.

JAMHURI limefanya mahojiano na mmoja wa walimu shuleni hapo (jina linahifadhiwa) ambaye amethibitisha Daudi Bashite kusoma katika shule ya Nyanza.

“Nashangaa hili jambo kukuzwa kiasi hiki! Hili suala lipo wazi kabisa, Daudi au Makonda kama anavyoitwa alisoma hapa na huyo Mwalimu Mkuu wa Nyanza, Jovenary anaweza kuwa anafahamiana naye kama hakumtangulia darasa kwani naye alisoma hapa hapa. Picha unayoiona kwenye mitandao Daudi aliipigia palee kwenye ngazi,” amesema Mwalimu huyo. 

Source: Jamhuri.

Alichokiandika Zitto Kabwe Baada ya Kumtembelea Nape Nyumbani Kwake...!!!

$
0
0

Nimetoka nyumbani Kwa Mbunge wa Mtama ndg Nape Nnauye kumpa Salam zangu za mshikamano na kumtia moyo katika majukumu yake ya kuhudumia watu wa Mtama Lindi na Tanzania Kwa ujumla. 

Amenieleza kuwa anakwenda jimboni kwake ndani ya siku chache zijazo. Nataraji watu wa Lindi, bila kujali itikadi za vyama vyetu vya siasa, watampa mapokezi anayostahili

Exclusive..Hivi Ndivyo Biashara ya Madawa ya Kulevya Inavyofanywa na Masharti Yake Kwa Muuzaji,...!!!!

$
0
0

NAUPENDA wimbo wa Ten Crack Commandments ulioimbwa na Christopher Wallace ‘Notorious BIG’. Kwa Kiswahili chepesi, wimbo huo unaweza kuuita Amri 10 za Dawa za Kulevya.

Sababu ya kuupenda wimbo huo ni kuwa amri zote 10 kama ambavyo BIG a.k.a Big Small aliziorodhesha katika shairi lake kisha kuimba kwenye mdundo mzuri wa Hip Hop, zinajenga picha wauza unga ni watu wa namna gani.

BIG kwa kutambua kuwa wangeweza kutokea watu wakambishia katika hizo amri zake 10, anaanza kwa kutamba kuwa hakuna mtu wa kumwambia kitu kwenye biashara ya dawa za kulevya. Anasema aliifanya biashara hiyo kwa miaka kadhaa na ilimfanya awe mnyama.

Chukua mstari huo; biashara ya dawa za kulevya ilimfanya BIG awe mnyama. Maana yake ukiwa muuza dawa za kulevya unakuwa mnyama. Yaani unapoteza roho ya utu.

Amri zote nazikubali, lakini huvutiwa zaidi na amri ya nne; Never get high on your own supply.

Kiswahili: Kamwe usitumie unachouza.

Kwamba unapokuwa muuza unga unajua kuwa hicho ni kilevi cha maangamizi, kwa hiyo BIG anakufahamisha kuwa usijaribu kutumia, maana utaangamia.

Amri ya tano ni muhimu; never sell no crack where you rest at. I don't care if they want a ounce, tell 'em "bounce!"

Kiswahili: Usiuze dawa kwenye maeneo yako ya kujidai. Sijali kama watataka japo cha ukucha, waambie imegonga mwamba.

Ufafanuzi ni kuwa unga ni maangamizi, kwa hiyo unatakiwa kuuza mbali, siyo kwenye maeneo unayoishi, maana utawaangamiza watu wanaokuzunguka.

Ipo amri ya saba ambayo BIG anasema; “tenganisha biashara na familia yako”, kwamba haitakiwi hata kidogo watu wa familia yako wahusike na uharamia wako ili ukipata msala ujikute matatizoni peke yako.

Amri ya nane pia anaelekeza “usijibebeshe mzigo mwenyewe”, kwamba ukiwa muuza unga unafahamu kuwa ni kimeo, kwahiyo wabebeshe wengine ili wakikamatwa uwe msala wao.

Alichokiimba BIG, ndicho hasa wauza dawa za kulevya wakubwa huzungumza. Muunza unga hufahamu kwamba dawa za kulevya ni kifo, kwa hiyo huhakikisha anauza mbali ili ‘aue’ watu baki.

Curtis Jackson ‘50 Cent’ ambaye alipata mafanikio makubwa katika biashara ya dawa za kulevya akiwa na umri wa miaka 12 tu kabla ya kuacha baadaye kujikita kwenye muziki wa Hip Hop na filamu, anasema kuwa muuza unga wa kweli hatumii.

50 Cent anakiri kuwa alikuwa ‘mnyama’ wa kuuza unga, anasema: “Ngoja niwaambieni, ukiona mtu anatumia ujue si muuzaji. Na kama ni muuzaji ujue hiyo kazi haiwezi. Muuzaji anayeijua kazi yake huwa hatumii.”

Uzoefu wake na mafanikio aliyoyapata kupitia biashara ya dawa za kulevya, 50 Cent ameeleza kwenye documentary inayoitwa How to Make Money Selling Drug, iliyotengenezwa Hollywood, Marekani.

SERA YA WAUZA UNGA

Afghanistan wakati wa utawala wa Taliban chini ya Mullah Omar, walikuwa wastawishaji wakubwa wa cocaine. Hata hivyo, sera yao ilikuwa na kanuni mbili.

Kanuni ya kwanza; cocaine yote iliyokuwa inastawishwa kutouzwa nchini humo. Yaani ni lazima isafirishwe yote kwenda nje. Hawakutaka ibaki Afghanistan kisha raia wa nchi hiyo watumie na kuangamia.

Kanuni ya pili; wasafirishaji lazima wathibitishe kuwa cocaine yote wataipeleka Marekani na Ulaya. Shabaha yao ilikuwa kuhakikisha vijana wengi wa Marekani na Ulaya hasa Uingereza, wanatumia dawa za kulevya ili kudhoofisha kizazi cha mataifa hasimu.

Ukichukua sera hiyo kuwa hakuna kuuza unga nyumbani na sharti ni kuwauzia maadui, unaungana na amri ya tano ya Big Small kuwa ‘ngada’ haiuzwi maeneo ya kujidai. Kuuza nyumbani ni uharibifu wa kizazi.

Muuza unga akimkuta mwanaye anatumia atalia kisha atamtafuta mtu ambaye anamuuzia na akimkamata vita yake haitakuwa ndogo. Maana anajua kazi ambayo anaifanya kwa watoto wa wenzake.

Ni kwamba muuza unga hutaka utajiri kupitia kuharibu watoto wa wenzake lakini huwalinda wa kwake na matumizi ya ‘madubwasha’ hayo.

KICHEKO CHA MUUZA UNGA

Unapomuona teja ameharibikiwa na matumizi ya dawa za kulevya, maana yake muuza unga anakenua vizuri kabisa, kwani anakuwa ameshafanya biashara na kuingiza fedha nyingi.

Muuza unga hana tofauti na mtu ambaye anamtoa kafara mtu mwingine ili apate utajiri. Muuza unga ni sawa na mchawi anayemiliki misukule.

Kijana na nguvu zake anaanza kutumia unga kisha anakuwa mtumwa wa kilevi hicho cha maangamizi. Jinsi anavyoendelea kutumia ndivyo anavyoteketea.

Muuza unga hawezi kumhurumia teja anayeangamia na unga kwa sababu kadiri teja anavyoangamia ndivyo inavyomaanisha yeye kuzidi kuingiza fedha na kutajirika.

Ukiona kijana alikuwa na mwili mzuri, afya bora kabisa, ghafla anaanza kudhoofika na kupukutika. Hapo piga mahesabu kwamba kuna wauza unga wamejenga majumba, kununua magari na kufanya kufuru nyingi za starehe kupitia afya ya kijana huyo na fedha zake.

Hivyo, kwa kila mtu mwenye moyo wa kibinadamu, anayeumizwa na vijana wengi kutopea kwenye mihadarati, anapaswa kila akimuona teja anateseka, aanze kusikitika.

Tofauti yako na muuza unga lazima ionekane pale nyote mnapomtazama mtumia dawa za kulevya. Muuza unga achekelee kwa sababu ananufaika kwa kuingiza fedha kupitia mabadiliko ya kiafya ya teja. Wewe unapaswa kuumia maana nguvu kazi inapotea.

Inapotokea wewe unamcheka teja kama ilivyo kwa muuza unga, maana yake hapo tofauti yenu haionekani. Nyote mpo sawa! Je, wewe unakuwa umeingiza nini kwa mabadiliko ya kiafya ya teja zaidi ya kushuhudia nguvu kazi inapotea?

Vijana wengi ambao walikuwa na nguvu zao, walikuwa wakifanya kazi na kuingiza vipato halali, mara wakajikuta kwenye vishawishi na kuanza kutumia. Walipoanza wakashindwa kutoka, mwisho wameteketea.

Je, huoni kama taifa tunakuwa tunapoteza mzunguko wa wachapakazi? Na hiyo ni hasara kubwa mno katika nchi.

MITEGO YA MUUZA UNGA

Kwa taarifa hizo kwa ukamilifu wake, jawabu ni kuwa mitego ya kunasa wauza unga huwekwa mbali. Mara nyingi wapelelezi hufanya makosa kwa kuwachunguza wauza unga kwenye maeneo wanayoishi.

Wauza unga kwa utaratibu wao wa kibiashara, huwa hawafanyi mgawanyo wa bidhaa zao kwenye maeneo wanayoishi. Kumfuata nyumbani na kumpekua ni kujisumbua tu. Wauza unga wengi hukwepa familia zao kujua kuhusu biashara zao.

Muuza unga huchunguzwa hatua kwa hatua. Kwa kuanzia watu anaokutana nao, halafu nao wanafuatiliwa mpaka mwisho wa mzunguko. Kutaka kufupisha mzunguko wa upelelezi ni sababu ya wauza unga wengi kuendelea kutamba mitaani kuwa hawahusiki.

Kutokana na teknolojia ya kukwepa simu kufuatiliwa au kuingiliwa, inakuwa vigumu kunasa ushahidi wa muuza unga kwenye mawasiliano yao, hivyo njia isiyo na shaka ni kutengeneza mnyororo.

Mtu anayehisiwa anauza dawa za kulevya, hufuatiliwa kwa kumchunguza mmoja baada ya mwingine katika mzunguko wa watu ambao huwasiliana nao au kukutana nao. Kila mmoja hufuatiliwa kwa mzunguko wake.

Baada ya mtu kwenye mtandao kunaswa, hutumika kunasa wengine wote mpaka yule mhusika mkuu. Mtindo unaotumika ni kumkamata mmoja na kuwachia huru kwa masharti ili asaidie kupata wengi.

Mataifa makubwa, askari wake wakishamkamata mtu mdogo yeye hupewa ahadi ya kuachiwa huru lakini mpaka asaidie mtandao wake wote ukamatwe. Ni hapo ndipo kazi hufanyika kwa ufanisi zaidi mpaka wale mapapa kabisa kukamatwa.

Hivyo, ni kosa kufupisha mzunguko wa upelelezi kwa kutegemea kumkamata muuza unga na kumpata akiwa na vidhibiti nyumbani kwake au kwenye maeneo anayoishi. Wauzaji hasa hupiga mishale ya mbali kisha kukusanya mabilioni yao bila presha.

Ukweli Mchungu...Ugumu wa Magufuli Kumtumbua Makonda Uko Hapa..

$
0
0

Kama Mtanzania niishie Dar es Salaam kuna mambo hupaswi yakupite. Wengi walikuwa wakitegemea mheshimiwa Rais kumtupilia mbali Makonda/Bashite ila haijawa kama mategemezi ya wengi kuwa hivyo.

Hii inatokana na sababu mbalimbali kama zifuatazo

i) Vita ya Dawa za Kulevya. Wengi tunajua vita hii ilivyo ngumu na hii ndo iliomfanya mpaka siri zake zikafichuka na raisi mwenyewe akaisapport hiyo vita na kutaka iendelee. Sasa leo hii akimtumbua kwa visa vilivyoibuka kutokana na madawa ya kulevya itakuwa ni usaliti na kutokuwa na maana.

ii) Kuna watu wanaopinga kila kitu afanyacho Rais, hapa nasemea Instagram pamoja sana sana pamoja na wanasiasa wanaopinga kila kitu kinachofanywa. Imagine mtu anapinga hadi kuletwa kwa ndege au flyover zinajengwa mtu anapinga   (watanzania hatuko serious)

Kuna hadi wengine wanataka ufisadi urudi ili maisha yapungue ugumu. Wengine wakawa wanasema ni mpango wa ikulu kumtuma afanye hivyo ili wamtoe wafunike skendo na udhaifu wa serikali.

Mtu kama huyu utafata atakachokushauri na ina maana ukifata umempa kiburi aonekane yeye ndo yeye na atakaloamua nchi nzima inafata, liwe baya au zuri. Na mwenendo kama huo ungefanya serikali iwe dhaifu kupita kiasi

So ndo maaana Magufuli akaita hiyo call

Rais Magufuli azidi kuiandama mitandao ya Kijamii..

$
0
0

Akiongea leo wakati anaapisha wateule wapya Ikulu. Amesema mitandao yetu ni ya ovyoovyo na inaandika mambo ya ajabu ajabu.

"Jana nimesoma kwenye mitandao ya kijamii kuwa eti Mwakyembe hawezi kuja kuapishwa, na mimi nilikuwa nasubiri asifike nione. ''Sasa si huyu hapa amefika"

Ameongeza kuwa..... "Jana kuna mwingine kapost Kinana kuongea na waandishi wa habari kesho, wakati ukweli Kinana nimemtuma India Kwa siku kumi na mbili"

Amewaonya wamiliki wa vyombo vya habari kwa kuzipa nafasi habari mbaya mbaya tu, "mfano kuna tv habari za migogoro ya wafugaji ndio wanaipa nafasi kubwa zaidi, amesema hayupo tayari kuvumilia hayo mambo.

Ameshangaa magazeti ya leo kujaza mbele picha ya mtu mmoja, na hata kurasa za ndani kujaza habari hiyo hiyo.

Amemwambia Mwakyembe akasimamie kwa umakini hasa tasnia ya habari, amesema hayupo tayari kuona nchi ikichezewa..l

Ameshangaa kutangaza kutoandika habari za mtu, wakati huo huo wanaandika mbaya tu.... "Kama hamtaki kumwandika si masiandike yote mazuri na mabaya"

Young Killer Aeleza Nia Yake ya Kuja Kuwa Mbunge au Diwani 2025

$
0
0

Rapper kutoka Rock City Mwanza Young Killer Msodoki ameitaja sababu ya yeye kutaja taja Mwanza kwenye ngoma zake kama njia moja wapo ya kutengeneza njia hapo baadaye.

Kupitia kipindi cha Zero Planet ya Ice Fm Msodoki aliulizwa endapo ashapata nafasi ya kuongea au kuitwa na viongozi wa mkoa wa Mwanza kutokana na anavyopeperusha bendera ya jiji hilo kwa mifano ya huko kwa wenzetu Drake alipewa tuzo ya heshima huko Toronto, Fetty Wap pia ashapewa Tuzo hiyo kwa kuitangaza miji yao na Ma-Mea wa miji.

“Siitangazi Mwanza kwasababu ya kuonekana ila nafanya kwa mapenzi yangu mwenyewe familia yangu yote ipo kule na mpaka sasa na wakilisha kule ndiko nimejifunza vitu vingi zaidi pia tutegemee kitu chochote kwenye 2025 huko huwezi jua ishu nzima ya Ubunge au udiwani ndio kitu ambacho….” amefunguka Killer

Kazi Immeanza Rasmi..Waziri Mpya wa Habari Aaanza na Sakata la Makonda Kuvamia Clouds,Ametoa Kauli Hii...!!!!

$
0
0

Waziri mpya wa Habari, Sanaa, Utamaduni na Michezo amejibu swali la waandishi kadhaa wa habari waliomhoji mapema leo baada ya kuapishwa katika viunga vya Ikulu Jijini Dar es Salaam.

Waziri Mwakyembe amenukuliwa akisema maneno yafuatayo juu ya sakata hilo lililotikisha vichwa vya habari nchini kwa juma moja sasa.

"Ninachokijua kuhusu tukio la Clouds Media kinatokana na vyombo vya habari, sidhani kama taarifa hizo zinatosha mimi kutoa uamuzi"-Waziri Mwakyembe

Hatareee..Kajala Masanja Atema Cheche Sakata la Makonda,Amefunguka Haya...!!!

$
0
0

MASTAA wengi Bongo wamekuwa wagumu kuzungumza chochote kuhusu yanayomkuta Mkuu wa Mkoa wa Dar, Paul Makonda, mmoja wao akiwa ni Kajala Masanja ambapo yeye alipoulizwa alisema, aachwe kwani mambo ya kiongozi huyo hayamhusu.

Staa huyo aliyewahi kupata ushirikiano mkubwa katika shughuli zake za kisanii kutoka kwa Makonda alipotakiwa kuzungumzia mapito ya kiongozi huyo na kipi angeweza kumshauri alijibu kwa kifupi:

”Hayanihusu jamani.”

Ijumaa: Hayakuhusu vipi wakati alikuwa swahiba wako na amekupa sana sapoti kisanii?

Kajala: Akuuu!

Ukweli Mtupu..Chid Ukirudi Ulikotoka, Tutashangaa sana!

$
0
0

HI…chi…chii Chid Benz! Inakuwa vigumu sana kuacha kuandika kuhusu huyo mkali wa Hip Hop Bongo.

Unamtazama akiwa bado kinda anapovamia jukwaa la vijana wenye majina katika Bongo Fleva, unamuona anavyopenya na kung’ara katikati yao, lakini ghafla, unamuona akijimaliza kikatili! Nimewahi kuandika mara kadhaa katika safu hii kuhusu Rashid Makwiro na mara moja kati ya hizo, niliwahi kupata simu kutoka kwake na tukazungumza kwa muda mrefu, akinilalamikia kwamba nilikuwa na uwezo wa kumtafuta na kumkalisha chini kama mdogo wangu, nikamweleza mwenendo wake na tukaelewana, kuliko kumuandika, kwani anayo familia inayoumia kwa kuandikwa kwake.

Nilimuelewa, nikamuomba radhi kwa kumuumiza na kuahidi kuwa nitajitahidi mara nyingine nimtafute endapo atateleza na tuzungumze. Lakini Chid Benz wa kwenye simu si Chid unayekutana naye mtaani. Ni watu wawili tofauti na njia pekee ya kumfi kia kwa ufasaha ni kuendelea kuandika.

Na nina muandika siyo kwa sababu nina wivu naye, ila kwa sababu ninaumia kuona kipaji chake kikipotea bure na hasa ukizingatia kuwa siioni kazi ambayo Chid anaweza kuifanya na kuendesha maisha yake na familia zaidi ya muziki.

Kama kuna marapa ambao nchi yetu imewahi kuwapata, huyu ni mmoja wao. Alikuwa anapokea kijiti kutoka kwa kaka zake kina Profesa Jay, Sugu, Solo Thang na wenzao na yeye alikuwa na muda mwingi wa kukikimbiza. Lakini bahati mbaya sana, Chid ameingia kwenye mtego mgumu kujinasua, japo inawezekana kabisa.

Mara ya mwisho picha za msanii huyu zilizoonekana, zilimtisha kila mmoja anayemfahamu, akionekana kama mtu ambaye siku zake za kuishi zilielekea ukingoni. Mungu siyo Athumani, haijulikani msamaria mwema huyu aliibuka kutoka wapi, lakini akamkimbiza Chid Benzino mjini, akampeleka Iringa, huko Mafi nga ambako aliweza kusaidiwa na kuurejesha mwili wake katika hali yake ya kawaida.

Wiki mbili zilizopita, ilikuwa ni vigumu kidogo kuamini kama picha unayoitazama ni ya King Kong, maana ilikuwa na mabadiliko ya asilimia 100 na hapo awali. Bwana Ametenda! Hili siyo jaribio la kwanza kwa watu kutaka kumweka Chid katika mstari salama.

Wamefanya hivyo watu wake wengi wa karibu na wameshindwa. Huyu wa sasa amekaribia kwenye ukweli. Nina uzoefu na wabwia unga, nimeishi nao na wengine ni rafi ki zangu.

Baadhi wamepoteza maisha. Ukitaka ukaribu na rafi ki yako mla unga upotee, mkanye kuhusu kubwia. Hatapenda kuwa karibu yako na kila ukikutana naye, atakuambia ameacha, hata kama unamuona ‘anabembea’.

Kwa Chid, uamuzi anao mwenyewe moyoni mwake. Anapenda aendelee kuishi au hataki ni juu yake kuchagua. Yeye hawezi kuwa wa kwanza kuacha, wako wengi.

Yupo msanii mkongwe wa Bongo Fleva, Terry Fanani. Hawa ndiyo watu wa kwanza kwanza kwenye game kuanza kula ngada. Ninamfahamu Fanani na ninajua kwa kiasi gani anapambana kwa zaidi ya miaka kumi sasa kuachana na jambo hili.

Yupo Msafi ri Diouf, yule rapa mkali katika Muziki wa Dansi, aliyekuwa Twanga Pepeta. Ilifi kia wakati Diouf alikuwa akibwia na kupoteza fahamu, akilala popote bila kuchagua wala kujali. Leo hii ameachana nayo, na sasa yupo zake Uingereza, akifanya shughuli zake za kumuingizia kipato. Q Chillah ‘alikula sembe’ hivi sasa ameacha.

Rai yangu kwa Chid Benz, usirudi kule ulikotoka, ukirudi nitakushangaa sana. Mimi ni shabiki namba moja wa ile sauti yako nene, yenye mamlaka, inayokwaruza, ambayo ni moja ya silaha kubwa katika muziki wako. Hivi sasa Chid alipaswa kuwa tajiri mwenye utitiri wa mali badala yake ameshindwa kupiga hatua kwa sababu ya ‘sembe’.

RPC Kinondoni Akana Kuhusika na Zuio la Mkutano wa Nape Nnauye,Afunguka Juu ya Askari Kuonyesha Bastola..!!!

$
0
0

Kamanda wa Polisi Mkoa wa Kipolisi Kinondoni Susan Kaganda, amesema kuwa yeye hakutoa maelekezo ya kuzuia mkutano wa aliyekuwa Waziri wa Habari, Sanaa, Utamaduni na Michezo Nape Nnauye pamoja na Waandishi wa Habari Jana Protea Hotel.

Akifafanua kupitia kipindi cha Maisha Mseto cha Times Fm mapema Leo asubuhi, Susan amedai yeye kama Kamanda hana mamlaka ya kuingilia biashara binafsi (Protea Hotel), na alikwenda pale kuhakikisha Usalama unaimarika zaidi na si vinginevyo.

“Protea ni private Hotel sio Mali ya Serikali, ile ni Biashara huru kamanda hawezi kuzuia, lakini nilikuta Waandishi wengi pale na alipata fursa ya kuongea nao.

” Mimi kazi yangu ni kusimamia Usalama wa Raia na Mali zao, mkutano unanihusu ukiwa wa Hadhara” alisema RPC Susan.

Alipoulizwa kuhusiana na kipande cha ‘Picha Jongefu’ (video) inayomuonyesha mtu anayedhaniwa kuwa Askari akimtolea silaha Nape Nnauye, amesema hawezi kuliongelea swala hilo kwa sasa mpaka uchunguzi utakapokamilika kwa maana kipande hicho hakionyeshi Sura ya mtu Huyo.

“Jeshi la Polisi tunawafundisha Askari wetu kutumia nguvu kwa namna wanavyokutana na mazingira, sikuwepo sikuona nilielezwa na ndio maana nilikwenda nikamuuliza Mh uko sawa akanijibu yuko salama,”

“Lakini kama kuna Silaha imetumika kama ambavyo nimeona kwenye vyombo vya Habari tunalifanyia Uchunguzi, sikuwepo eneo la tukio picha ile inaonyesha KISOGO, kuwa mtulivu tunachunguza” alifafanua.

Tiba kwa Mpenzi Anayekojoa Kitandani...!!!

$
0
0

Ni matumaini yangu mpo salama,
Naamini kuna watu humu wamewahi kuachwa au kuachika kisa kuwa na tabia ya kujikojolea kitandani wakati wa usiku,

Baadhi ya wanandoa wanapitia kero hii sana sema huhifadhiana siri kwa sababu walisha kula kiapo cha pingu zamaisha,
Baadhi yao uzalendo huwashinda pale chumba kinapoanza kunukia kibeberu beberu na kuamua kuvunnja ndoa zao,

Usifadhaike ,

Kama una mpenzi, ndugu, jirani au mtoto mwenye tatizo la kukojoa kitandani leo ninamwaga tiba yake hapa ili mkapate kuwasaidia,

TIBA,
Ufuta mbichi (ambao hauja kaangwa),
Unapatikana sokoni, 
Baada ya kuununua upepete ili kuondoa mchanga na vumbi,
Baada ya hapo tafuna vijiko vinne vya ufuta kutwa mara tatu, tumia kuanzia siku tatu na kuendelea,
Utapona kabisa na itabaki kuwa historia,
Hii imewasaidia wengi sana,

Kwa leo naishia hapa,
Viewing all 104689 articles
Browse latest View live


Latest Images