Quantcast
Channel: UDAKU SPECIAL
Viewing all 104428 articles
Browse latest View live

Yakufahamu Juu ya Urefushaji wa Maumbile ya Wanaume..!!!

0
0

Kwa ufupi
Makala ya juma lililopita ni mojawapo ya makala niliyopokea maelfu ya maswali kutoka kwa wasomaji, naamini kama tutakuwa pamoja mtapata majibu ya maswali yenu katika mfululizo wa makala tatu zijazo.

By Dk Shita Samwel

Juma lililopita tuliona sababu za wanaume kuwa na maumbile madogo ya uume. Leo tunaendelea sehemu ya pili, tutaona dondoo za kitafiti zenye kueleza ukweli wa maumbile ya uume.

Makala ya juma lililopita ni mojawapo ya makala niliyopokea maelfu ya maswali kutoka kwa wasomaji, naamini kama tutakuwa pamoja mtapata majibu ya maswali yenu katika mfululizo wa makala tatu zijazo.

Wanasayansi wengi wa tiba wametoa machapisho mengi ya kitafiti kuhusu urefu na upana wa uume nia na madhumuni ni kujibu swali juu ya wastani wa uume kwa wanaume wengi duniani ni upi.

Baadhi ya wanaume wamekuwa wakiishi kwa hofu na kukosa kujiamini katika uhusiano wao wakihisi kuwa wana uume ambao ni mdogo usioweza kumridhisha mwenza wa kike.

Hofu hiyo inawezekana ni kutokuwa na ufahamu sahihi juu ya maumbile yao yalivyo, wengi wanakosa taarifa sahihi kutoka wataalamu wa afya wenye uelewa wa jambo hili.

Hofu ya wanaume inaongezeka kila siku hasa kutokana na utitiri wa matangazo ya magazeti, mitandaoni, hadithi za vijiweni na matangazo ya waganga wa kienyeji mitaani wanaojitangaza kuwa na dawa na vifaa tiba vya kuongeza urefu na upana wa uume.

Dondoo zifuatazo zinajumuisha ripoti mbalimbali za kitafiti, ikiwamo yale yaliyochapishwa katika majarida makubwa na maarufu duniani ikiwamo ya Science today, Men’s health na British Journal of Urology international.

Asilimia 85 ya wanawake wanaridhika na urefu na upana wa maumbile ya uume wa wenza wao, ingawa wanaume wenyewe hawana uhakika wa jambo hilo, huku asilimia 45 ya wanaume wakiamini kuwa wana maumbile madogo.

Tafiti mbalimbali zilikuja na hitimisho kuwa wastani wa urefu wa uume ukiwa haujasimama, ukiwa katika hali ya ulaini ni kati ya sentimita 7 hadi 10 au inchi 2.8 hadi 3.9, urefu unapimwa kuanzia katika shina la uume mpaka katika kichwa.

Wakati kipimo cha mzunguko wa uume ukiwa haujasimama ni kati ya sentimita 9 hadi 10 au 3.5 hadi 3.9

Urefu wa uume unapokuwa umesimama ni kati ya sentimita 12 hadi 16 au inchi 4.7 hadi 6.3. Urefu wa mzunguko wa uume ukiwa umesimama ni kati ya sentimita 12 au inchi 4.7.

Dondoo nyingine ya tafiti inaonyesha kuwa wanaume wenye unene uliopitiliza na wenye umri mkubwa wengi wao wana “urefu mfupi” wa uume ukiwa umesimama.

Maumbile ya uume yanatofautiana kati ya jamii moja na nyingine, bara moja na jingine. Wanaume wanaotokea Asia wana maumbile madogo ya uume ukilinganisha na wanaume wa bara la Afrika.

Wanawake wengi huwa hawajali urefu na upana wa uume wa wenza wao, pengine ni kutokana na ukweli kuwa kufika kilele cha tendo kwa wanaweka si lazima kumuingilia, wanaweza kufika kileleni hata kwa njia nyingine hata kwa kutomaswa.

Daktari bingwa wa magonjwa ya kina mama Ernst Grafenberg mwenye asili ya Ujerumani, ndiye mgunduzi wa sehemu ya kike ambayo ndio inaelezwa ina msisimko wa kipekee kuliko nyingine yoyote katika sehemu za kike.

Sehemu hiyo ijulikanayo kama G-spot ambayo ipo sentimeta 5.1-7.9 au nchi 2-3 tu kuanzia nje ya uke kuingia ndani.

Inaelezwa kuwa unaweza kuwa na uume mdogo lakini ukamridhisha mwenza wako na kumfikisha kileleni kutokana na sehemu hiyo huweza kusisimuliwa hata na uume mdogo.

Ujue Ugonjwa Hatari wa Homa ya Matumbo (Typhoid fever) na Matibabu Yake..!!!

0
0


TYPHOID FEVER
Homa ya matumbo
Homa ya matumbo husababishwa na bakteria anayeitwa Salmonella Typhoid. Ugonjwa huu huambukizwa kwa mtu kula au kunywa chakula au maji yalio na kinyesi cha mu aliyambukizwa. Bakteria hawa hutoboa na kunyonya chakula kwenye matumbo ya binadamu.

Dalili ya Maradhi:
Homa kali
Kutoka kwa majasho mengi
Kuharisha (bila ya kutoa damu)
Mara nyingine, vitone vyekundu huonekana kwenye mwili.
Kwa kawaida, homa ya matumbo isipotibiwa hugawanyika katika hatua nne, kila hatua ikichukua takriban wiki moja.

Katika wiki ya kwanza:
Joto la mwili huongezeka
Kichwa huuma
Kukohoa
Damu kutoka kwa pua, ingawa tukio hili huwa ni nadra kutokea.
Maumivu ya tumbo pia huweza kutokea

Katika wiki ya pili:
Homa huongezeka
Mgonjwa huanza kupagawa, kama mwenda wazimu
Vitone vyekundu huanza kutokea kwenye kifua
Mgonjwa huharisha, takriban mara sita au nane kwa siku.
Kutapika kwa mgonjwa
Ini la mgonjwa huvimba
Homa ya mgonjwa huongezeka katika wakati wa alasiri kwenye wiki ya kwanza na ya pili.

Wiki ya tatu:
Matumbo hutoa damu.
Matumbo hutoboka
Wiki ya Matibabu[hariri | hariri chanzo]
tatu ikimalizika, homa huanza`kutilia. Hii huendelea hadi wiki ya nne.

Matibabu kwa dawa za kizungu
Mara nyingi, homa ya matumbo haiuwi binadamu. Dawa kama ampicillin, chloramphenicol, trimethoprim-sulfamethoxazole, Amoxicillin and ciprofloxacin hutumika kutibu wagonjwa katika nchi zilizoendelea.

DAWA YA KUTIBU HOMA YA MATUMBO DAWA YA TIBA ASILIA

FANYA HIVI: Chukuwa Glasi 4 za Maji tia ndani ya jagi la maji changanya na nusu kijiko kidogo cha chumvi ya unga. Kisha tia ndani yake vijiko 6 vidogo vya sukari, kisha koroga vizuri hayo maji.

Matumizi yake: kunywa asubuhi kabla ya kula kitu glasi 1 mchana glasi 1 Jioni Glasi 1na usiku glasi 1 kila siku dawa ikiisha tengeneza dawa ingine utumie hiyo dawa kwa siku 30 utaweza kupona.

Hatua za kuzuia kupata homa hii

Usafi wa mazingara na wa kibinafsi ni hatua bora ya kujikina kutokamana na ugonjwa huu.
Homa ya matumbo haiathiri wanyama kwa hivyo maambukizi ni kutoka kwa binadamu mmoja hadi mwingine.
Homa hii hueza kuenea kwenye mazingara ambayo kinyesi cha binadamu hutangamana na vyakula vyao. Upishi wa makini na uoshaji mikono ni kingo bora zaidi kwa kuzuia maradhi haya kuenea.

Chanjo ni za aina mbili: moja inayotiwa kwa njia ya mdomo iitwayo Ty21a (au Vivotif Berna) na nyingine ya sindano kwa majina Typhim Vi iliyotengenezwa na Sanofi Pasteur au Typherix iliyotengenezwa na GlaxoSmithKline.

Ukitumia Dawa hujapona unaweza kunitafuta nikupe Dawa ya kuweza kukutibu ukapona kwa haraka zaidi.


Ukiwa na Shida yoyote ile
Usipo pona kwa Dawa za Hospitali nitafute mimi nipate kukutibia upate kupona ukihitaji matibabu yangu

Unatatizo la Kuchelewa Kuamka..? Tumia Njia Hizi 10 Zitakazokusaidi Kuwahi Kuamka Kila Siku...!!!

0
0

1.Kuna chakula/tunda unalolipenda zaidi? Jiwekee zawadi, kwamba ukiamka asubuhi tu cha kwanza ni kula chakula hicho/ tunda/ chokleti nk. Hii itakufanya Utoke kitandani pale tu utakaposhtuka!

2.Iwekee Kipaumbele kazi unayopenda kufanya zaidi iwe ya kwanza kutendeka asubuhi. Utajkuta unatamani kuamka mapema zaidi kuwahi kazi hiyo na siku yako itaenda vizuri

3.Andaa mapema nguo ya kuvaa siku inayofuatia, ili kuwahi jumatatu, andaa nguo ya kuvaa jumapili usiku. Utafiti unaonyesha kuwa asilimia 40 (40%) ya watu huchelewa kutoka kitandani kwa kuwa walitumia muda mwingi kupanga watavaa nguo gani.


4. Anza kupunguza dakika 20 kila siku Taratibu; Kama ulikua unaamka saa mbili kamili, amka saa moja na dakika arobaini, baada ya siku mbili punguza tena dakika ishirini mpaka utakaporidhika

5. Jiwekee Lengo na uwaambie watu. Hii itakufanya ufanye kazi kwa bidii kwa kutaka kuwaonyesha watu kwamba umetimiza lengo lako na utajikuta unawahi kuamka asubuhi

6. Tengeneza “appointment” (Miadi) ya kuonana na mtu asubuhi, utajikuta unawahi kuamka kwa kuogopa kumuangusha mtu huyo.

7. Kama una mtu unaishi nae, tengeneza ratiba ya pamoja kama kufanya mazoezi, maombi, kusoma nk! Itakusaidia kukuongeza morali ya Kuwahi kuamka.

8 Weka saa ya kukuamsha (alarm clock) mbali na kitanda ikiwa na sauti kubwa, ni vizuri ukitumia wimbo uupendao.

9. Muombe mpenzi wako akuamshe kila asubuhi, au jenga tabia ya kumpigia mpenzi wako simu asubuhi


10.Ondoa vitu Vinavyokufanya uchelewe Kuamka mfano; pombe, kahawa na kuwahi kulala usiku.

Fahamu Usiyoyajua Kuhusu Ugonjwa wa Malaria..!!!

0
0

Malaria ni nini? Malaria ni ugonjwa wa kuambukizana unaoletwa na chembe chembe zinazoitwa plasmodium.Chembe chembe hizi huingia ndani ya mwili wa binadamu baada ya kuumwa na mbu wa kike kwa jina Anopheles. Mbu mwenye chembe chembe za plasmodium anapomuuma mtu,humuingizia baadhi ya mate yenye viini vya kuambukizana kwenye kidonda hivyo kusabaza Malaria. Viini hivi husafiri hadi kwenye maini ambapo hukaa hadi vifikie ukomavu. Viini hivi baadaye huingia na mtu kama huyu akiumwa na mbu,mbu huyu hubeba chembe chembe hizi na anaweza kumuambukiza mtu atakaye muuma.

Kuna aina 4 za Malaria: P. vivax, P. malariae, P. ovale na P. falciparum. Zimepewa majina kulingana na aina ya plasmodium inayozisababisha. Aina 3 za kwanza sio hatari lakini Falciparumni hatari sana na hata inaweza kusababisha kifo. Hii ni kwa sababu ikishaingia tu mwilini huzaana kwa wingi ndani ya damu.. Hii ni kwa sababu chembe chembe nyekundu za damu(ambazo husambaza oksijeni mwilini)zilizoadhirika huwa nzito na haziwezi kuingia kwenye kapilari. Hii husababisha kufa kwa sehemu ya ubongo,maini,mapafu,figo na matumbo kwa sababu ya ukosefu wa oksijeni. Hali hii inaweza kusababisha kifo kama haita tibiwa haraka.

Malaria hutambulika vipi?

Baridi,kuuma kwa misuli na kichwa zinaweza kuwa dalili za magonjwa mengi mengine. Njia ya pekee unayoweza kudhihirisha kama una Malaria ni kuenda hiospitalini kupimwa damu. Watu wengi wanaotoka sehemu zilizoadhirika na Malaria pindi wanapoona dalili hizi huenda kwenye maduka ya kuuza madawa kununua dawa za kupambana na Malaria. Huu sio ushauri mzuri. Ni muhimu kupimwa damu ili aina ya plasmodium inayosababisha maradhi yako itambulike na upewe matibabu yanayostahili.

Nani yuko kwenye hatari ya kuambukizwa Malaria?

Watoto wachanga,watoto na akina mama waja wazito wako kwenye hatarikubwa ya kushambuliwa hata kufa kutokana na Malaria. Watoto wachanga na watoto wako kwenye hatari kwa sababu wameambukizwa mara chache nahawajajenga 

kinga dhidi ya chembechembe hiziVamizi la Malaria kwa wanawake wajawazito kalikwa sababu kinga yao dhidi ya maradhi huwa chini wakati wa uja uzito. Malaria huongeza tishio kwa mtoto ambaye hajazaliwa kama kuzaliwa kabla ya wakati 

kutimia, uaviaji wa mimba, maambukizi ya sehemu za siri, uzani mdogo wa mtoto anapozaliwa, kupoteza uja uzito na pia ugonjwa huu unaweza kumsababishia mama kifo.


Naweza jilinda vipi dhidi ya Malaria?

Msafiri: Kama unasafiri hadi kwenye eneo linalolotambulika kwa Malaria,mtembelee daktari wako ili akupe dawa mahsusi ya kupambana na Malaria ya eneo unalotembelea.Hakikisha umefuata maelezo vizuri.

Wenyeji wa maeneo yalioadhirika na Malaria: Mbu wa aina ya anopheles hupenda kuuma watu nyakati za macheo na machweo kwa hivyo ni bora kujikinga nyakati hizi.Wakati wa machweo unaweza keti ndani ya nyumba iliyoekewa dawa na usiku unaweza kulala neti iliyotibiwa.

Haribu sehemu mbu wanapozaliana: Kipindi cha mwisho katika ukuaji wa mbu hufanyika majini.Mbu wa aina ya anopheles hupendelea maji yasiyo ya chumvi.Ni muhimu kuharibu ama kunyunyuzia na dawa sehemu zote ambazo mbu wanaweza kutaga mayai.Unafaa kutoa chupa,ndoo ama chochote ambacho kinaweza kusimamisha maji,bacillus thuringiensis(Bti) dawa asili ya kuua wadudu kutoka BioVision inaweza kutumiwa kuua mbu wachanga bila kuharibu maji.

Watoto na mama waja wazito lazima wakingwe na Malaria: Nchini Kenya,wanawake waja wazito wana haki ya kupata matibabu 2 ya bure na neti zilizotibiwa. Chukua moja kutoka katiki kliniki yako.

Neti zilizotibiwa: Kila mtu anapaswa kupata neti iliyotibiwa.Kuna aina mbili ya neti hizi nchini Kenya ambazo zinauwa mbu pindi tu wadudu hawa wanapozigusa.Kuna zile zinazopaswa kutibiwa kila baada ya miezi 6nba PowerTabs na zile zinazodumukwa miaka 3 hadi 5 baada ya kutibiwa

Ni zipi dalili za Malaria?

Dalili za Malaria ni kama zile za Flu; homa, baridi na kuuma kwa misuli na kichwa. Watu wengine hupatwa na kichefuchefu, kutapika na kuharisha. Vipindi vya baridi, homa na kutokwa na jasho hujirudia kila siku moja, mbili au tatu. Watu wenye aina ya P. falciparum wanaweza kupata Malaria ya ubongo ambayo husababisha kuishiwa na fahamu ama kuchanganyikiwa kiakili.

Tiba ya Malaria

Tiba ya Malaria inategemea mambo kadhaa:

Hali ya mgonjwa (mtoto, mama mja mzito, mtu mzima, ni kali ama sio kali)

Nguvu ya dawa dhidi ya ambukizo la viini vya plasmodium.

Eneo la kijiografia ambalo mtu aliambukizwa. Kwa mfano, P.falciparuminayopatikana katika nchi za Mashariki ya kati inaweza kutibiwa na dawa ya chloroquine, lakini inayopatikana Africa, katika nchi zilizo kusini mwa jangwa la Sahara haitibiki kwa chloroquine.

Aina ya plasmodium inayodhuru mgonjwa. Malaria yasiyo makali hutibiwa na dawa za kumeza ilhali wagonjwa wenye P. falciparum kali hulazwa hospitalini na kupewa sindano ya maji.

Kwa bahati mbaya aina fulani za plasmodium zimeleta upinzani dhidi ya dawa ya chloroquine.

Mwalimu atinga kwa DC akiwa chakari

0
0

MKUU wa Wilaya ya Handeni, Godwin Gondwe, ameshangazwa na idara ya elimu msingi ya Halmashauri ya Wilaya hiyo kushindwa kumchukulia hatua aliyekutwa amelewa wakati wa kazi.

Mwalimu huyo, Fikiri Swai wa Shule ya Msingi Kwankonje, anatuhumiwa kufika kazini akiwa amelewa pombe.

Tukio hilo lilitokea juzi shuleni hapo wakati Gondwe alipofika katika mpango wa kusambaza mbegu za mihogo na katika shughuli hiyo, alifika mwalimu huyo na kuanza kusalimia akiwa amelewa chakari.

Kutokana na hali hiyo, Gondwe alitaka kufahamu kama ni mwalimu wa shule hiyo na ndipo alipojibiwa kuwa ndiyo na kuelezwa kuwa
hiyo ni tabia yake ya muda mrefu. Pia ilielezwa kuwa ameshachukuliwa hatua za kinidhamu ikiwamo kusimamishwa kazi.

Baada ya majibu hayo, Gondwe alisema mtumishi wa umma kufika kazini akiwa amelewa au kufanya hivyo muda wa kazi na kwamba kitendo cha mwalimu huyo ni kosa na ameonyesha dharau mbele ya viongozi wa ngazi ya juu ndani ya wilaya.

"Kumbe mmeshamsimamisha sasa kwa nini anakuja shuleni tena akiwa amelewa muda wa kazi? Hamuoni inaleta taswira mbaya kwa wanafunzi kuona hili ni jambo la kawaida? Kwa kweli  sijafurahishwa na hili kabisa," alisema Gondwe.

Alipoulizwa sababu ya kulewa pombe muda wa kazi, Mwalimu Swai alisema hali hiyo inatokana na kusimamishwa kazi kwa muda mrefu hivyo kumfanya aingie kwenye ulevi na hali hiyo imetokana na uamuzi wake wa kuomba kupandishwa daraja na ndipo ulipoibuka ugomvi kati yake na viongozi.

Swai aliongeza kuwa anashangazwa na kusimamishwa kufundisha huku akitakiwa kuripoti shuleni na kutia  saini kila siku na kuchukua mshahara kila mwezi.

Alisema tangu  mwaka 2013 alisimamishwa kazi na mshahara wake anachukua kama kawaida ila hakuna hatua nyingine za kinidhamu zinazoendelea dhidi yake.

Mratibu wa Elimu Kata,  Nuru Faraji, alisema ni kweli mwalimu huyo amekuwa na tabia ya kulewa muda wa kazi na alishawahi kufanya hivyo hata kwenye kikao kimoja na viongozi wa elimu wa wilaya, hali ambayo ilibidi kutolewa kwenye kikao na kupewa adhabu.

Naye Ofisa Elimu ya Msingi wa Halmashauri ya Wilaya ya Handeni, Selemani Mtinda, alisema wanafahamu tatizo la mwalimu huyo na kueleza kuwa kesi yake iko mamlaka inayoshuhulika na walimu, ambayo ndiyo yenye mamlaka na jambo hilo.

Moi kuwatimua 45 waliokutwa na vyeti feki

0
0

Kaimu Mkurugenzi Mtendaji wa Kitengo cha Tiba na Mifupa (Moi), Dk Othman Kiloloma amesema kipo katika mchakato wa kupunguza wafanyakazi 45 waliokutwa na vyeti feki.

Akizungumza mbele ya Kamati ya Bunge ya Huduma za Jamii iliyofika hospitali hapo jana, Dk Kiloloma alisema pia taasisi hiyo ina upungufu wa fedha kutokana na Serikali kushindwa kutoa zuruku ya Sh4.8 bilioni zilikuwa zitolewe kwa mwaka wa 2016/17.

Alisema kutokana na tatizo hilo imekuwa vigumu kwao kujiendesha kwani kitengo kinatumia Sh20.6 bilioni kwa mwaka kwa ajili ya kununulia vifaa vya tiba pekee, wakati huo asilimia 70 ya wagonjwa wakitibiwa kwa msamaha.

Mkurugenzi Mtendaji wa Hospitali ya Taifa Muhimbili, Profesa Lawrence Museru alisema MNH iliidhinishwa kupewa Sh4 bilioni kwa ajili ya utekelezaji wa majukumu mbalimbali lakini mpaka sasa haijapokea fedha hizo.

Wapo Wapi Jakaya, Mkapa na Mwinyi...?

0
0

Haya yanayotokea, marais wetu wastaafu, Jakaya Kikwete, Benjamin Mkapa na Alhaj Ali Hassan Mwinyi, hawayaoni?

Baba wa Taifa, Mwalimu Julius Nyerere, enzi zake baada ya kustaafu, hakupoteza macho ya kuona wala masikio ya kusikia. Alipoona mambo hayapo sawa, alitokeza na kuzungumza.

Faida ya kuwa na wazee ni kupata busara zao katika vipindi tofauti. Hii hali na wasiwasi mkubwa uliopo, je, wao hawaoni? Mbona hawatoki na kusema chochote?

Je, hii hali iliyopo inawafurahisha wazee wetu? Siyo vibaya, watokeze hata wasifie tujue kuwa wazee wetu wanaunga mkono kinachofanywa na Rais wetu mpendwa, Dk John Magufuli.

Hali ilivyo, wananchi wamegawanyika makundi mawili, wapo wanaosema Rais anapatia, wengine wanaona anakosea. Mbona sasa wazee hawatokezi na kusema chochote?

Je, wazee wanampinga Rais Magufuli? Watoke na waseme kuwa kinachofanywa na Rais hakipo sawa. Je, ukimya huu maana yake nao wanaogopa kusema?

Kwa nini wazee wetu wanatufanya tutamani Mwalimu Nyerere afufuke? Kwa nini mnakaa kimya kama vile hamuoni hali iliyopo?

Wazee Joseph Warioba, John Malecela, Salim Ahmed Salim, Cleopa Msuya na wengine, tokezeni mseme. Hata kama ni kusifia, sifieni tu ili tujue wazee wetu wanasimamia wapi.

Je, wazee wetu wamepoteza ujasiri? Nakumbuka akina Butiku na Warioba walivyokuwa wajenzi wa hoja kinzani dhidi ya Serikali wakati wa JK, ujasiri huo umekwenda wapi?
JK upo wapi mkuu? Mkapa hutokezi baba! Mwinyi umejichimbia wapi mzee?

Mwalimu Nyerere hakuwahi kutuacha kama ambavyo ninyi mnatuacha. Ni kama baada ya kumaliza utawala wenu mmeamua kunawa mikono, hapana! Bado mnayo kazi ya kufanya. Kushauri, kukosoa, kusahihisha au kusifia.

Nchi bado inawategemea mno kwa busara na uzoefu wenu. Mwalimu Nyerere alijua kuwa Tanzania ilimhitaji ndiyo maana hata baada ya kung'atuka alibaki nasi, akawa anatokeza na kuzungumza kwa kuyajenga kuhusu nchi yetu.

JK, Mkapa na Mwinyi, kila mmoja ameongoza nchi miaka 10. Rais Magufuli ndiyo yupo mwaka wa pili. Tokezeni mseme jambo la kumshauri. Au kama huwa mnamshauri kimyakimya afanye anayofanya, basi tokezeni msifie utekelezaji wake.

Ndimi Luqman MALOTO

Tukubaliane, Sio Kila Anachosema Huyu "Binti wa Insta" ni Ukweli, Hata Hili la Kinana Anapotosha...!!!

0
0

Sipo huko "instagram" lakini nimekuwa nikipata "update" za huko kupitia hapa au hata kuona baadhi ya "screenshot" zenye maandishi na picha ya kinachoendelea huko.Nasikia huko umaarufu unatokana na mtu kuwa na idadi kubwa ya wanaokufuatilia.Idadi hiyo inaongezeka kutokana na habari unazo-post.


Huyu mtoto (maana wengine tulikuwa washirika wa baba yake kikazi) amekuwa anatuma habari nyingi sana za ndani ya kapeti.Kwa kweli nyingine ukiziona zina ukweli wake japo nyingine hazina ukweli.Lakini kwa sbb tayari ana wafuasi wengi na kwa vile anayewaongelea wamekuwa kwa sasa hawapendwi au wamepoteza umaarufu,basi chochote ukisema mwingine kinyume na huyo binti,basi tegemea matusi sana toka kwa "wafuasi watiifu" wa huyo binti.


Bahati mbaya au nzuri na yeye amewajenga "wafuasi" wake katika muktadha wa kujibu hoja jumlisha tusi.Yaani anaweza kuwa na hoja nzuri tu,lakini lazima isindikizwe na matusi ya maana tu.Anaweza kuwa na hoja nzuri tu kuhusu Bashite,lakini lazima hoja hiyo iambatane na matusi ya nguoni,anaweza kuwa na hoja nzuri tu kuhusu aina ya uongozi wa JPM,lakini hoja hiyo lazima iambatane na tusi.Hii si sawasawa...Hii si sawa


Na kwa sasa amekuwa kama "Authority".Sikatai,lakini pia watu wawe makini na aina nyingine ya habari.Sio zote anazokuwa anatoa zinaweza kuwa za kweli.Na wale walioumia sana wakati ule akimtukana braza Eddo,maumivu ya matusi yale ndio wanayapata hawa wanaotukanwa kwa sasa.Tukiwa jamii inayotengeneza watu wa ustaarabu wa mijadala,tukubaliane na habari anazotulisha,ila tutafotiane na aina ya "matusi" yanayoambatana na habari anazozirusha.


Kwa mfano ile ya gari la kwenye kontena bandarini,ukiangalia gari ya kwenye kontena haina namba,lakini gari anayoisambaza yeye kuwa ndiyo ilikuwa kwenye kontena ina namba zenye usajili wa Zanzibar.Mimi mpaka sasa sijajua hoja kuu hasa ni nini?Inawezekana kweli ile ilikuwa "kick" ya JPM kupoteza habari ya Napelembe Moses Nnauye,lakini kuna haja ya kupotosha kwa kuweka gari isiyokuwepo ktk kontena?Yaani ye huyu binti kwanini aweke gari ambayo siyo yenyewe?

Lakini kwa sasa inabidi usihoji,unaweza kumuuliza hata mkeo akakwambia "Mang**** kasema",ukimuuliza kwani akisema huyo ndio ukweli usio na shaka?Atakwambia yule anajua kila kitu,hata wewe akipewa jina lako anakuchimbua mpaka kwa vimada wako...Asalaleeeee!!!Mwakubwa haya.

Toka kauli ya Rais kuhusu Kinana na India ilivyotoka.Tayari binti katengeneza story na kupata "wafuasi" lukuki.Kwamba Kamaradi Kinana kafungiwa,mara katumiwa usalama ili akae ndani bila kuongea na maneno kibaoooo.Hii kitu imeshasambaa na kuaminika kwa 95%.

Lakini ukweli ni kuwa Kinana yupo nje ya nchi,kama ni India au China hiyo si habari kubwa sana.Kwamba Mzee anasema "amemtuma kutibiwa India",siyo jambo la ajabu sana.Kama tumemvumilia Rais anaposema "ngombe" badala ya "Ng'ombe","ngangania" badala ya "ng'ang'ania" na "broken" nyingi tu katika Kiswahili,basi hata hili lisitusombe,muhimu ni kweli kuwa Kinana yupo India?

Kamaradi Kinana aliondoka kwenda ng'ambo,alikwea ndege ya Emirates,flight # EK726 aina ya B773 kupitia Dubai,siku aliyoondoka Kamaradi Kinana ndio siku aliyoondoka Mstaafu wa Bagamoyo,yeye aliondoka na Ethiopia,flight # ET804 aina ya B738 kupitia Bole Addis Ababa.Hawa wawili waliondoka siku moja kwa mashirika tofauti.

Kwamba kaenda kutibiwa,hilo si jambo la kulisemea,kwamba yupo nje ya nchi...hilo ni kweli.Sasa kwa sbb kashasema "binti" basi,na kwasababu wanaosemwa ndio wale waliopoteza mvuto,basi lolote wanalosemwa itakuwa ni kweli tena ukweli mtupu.

Tuko katika ulimwengu wa "Post-Truth Politics",yaani ukweli huja baadae sana baada ya uwongo kutawala.Kipindi ambacho uongo hushika hatamu zaidi ya ukweli.Zama ambazo uongo wa kidijitali unasambaa kuliko ukweli wa kianalojia.Ni wakati wa kuchagua,kuchuja na kuamua.


Profesa Kitila Mkumbo: Kuna Nini Kati ya Magufuli na Makonda?..!!!!

0
0

Mwanasiasa kutoka chama cha ACT wazalendo anaonekana kushangazwa na Magufuli alivyomkingia kifua Makonda mkuu wa mkoa wa Dar na amehoji kuna nini hadi Magufuli asimuengue Makonda?

Amesema Magufuli amekuwa akitengua watu madarakani haraka hata kwa makosa ambayo yanakuwa hayahitaji mtu kuenguliwa lakini kwa hili la Makonda Magufuli amekuwa akimng'ang'ania kitu amabacho kina zua maswali mengi kwa wadau wengi

Wasaidizi wa Rais, Please Msaidieni Rais Wetu Kwenye Public . Msimuachie Kila Kitu Peke Yake!...!!!

0
0

Nimeangalia kipindi cha Jicho Letu Ndani ya Habari kinacharushwa Live na Star TV kila Jumamosi asubuhi. Namshauri Dialo atafute muda kipindi hiki kirudiwe jioni wakati wa prime time ili wengi waone.

Kipindi cha leo kusema ukweli muongozaji Dotto Bulendu na Ansbert Ngurumo wameitendea haki tasnia ya Habari dhidi ya vitisho vilivyotolewa jana na rais Magufuli.

Naomba nisiingie ndani sana kuhumu Ngurumo na Bulendu walisema nini kuhusu rais kutaka kuipangia media nini cha kuandika, mimi najikita kwa watu ambao ni wasaidizi wa rais wanajukumu la kumsaidia.
Haya chini ni yangu.

Tanzania ni nchi yetu sote na sio nchi ya mtu mmoja, japa Tanzania ya sasa ni Tanzania ya Magufuli kama ilivyo Darisalamu ya Makonda.

Rais Magufuli ni kiongozi wetu, ni rais wetu, kutokana na kuwa yeye ndiye rais, taasisi ya urais ndiyo ni mamlaka kuu kiutawala kuliko mamlaka nyingine zote, ila pia Magufuli ni binadamu, sio malaika, hawezi kufanya kila kitu yeye peke yake ndio maana amewekewa wasaidizi mbalimbali wakiwemo washauri.

Kunawakati rais kama rais anatoa matamko tata au maamuzi tata yanayoashiria kuwa rais hakupewa ushauri sahihi kabla, kisha waziri wake anakuja kuibuka baadae na kuirekebisha kauli ya rais kwa kuifuta na kuweka mambo sawa.

Mfano mzuri ni siku ile rais alipotoa tangazo hili
Rais Kusitisha Uzazi wa Mpango Kwa"Fyatueni Watoto wa Kutosha",Ni ...
kisha waziri wake akaja kuibatilisha kauli hii kwa kusema rais alikuwa anatania tuu watani zake. Rais anapozungumza kwenye hotuba inayotangazwa moja kwa moja kwa taifa zima na akatangaza jambo fulani, hii maana yake ni kulitangazia taifa. Sijadhani kama Watanzania walichagua rais Msukuma ili atoe maagizo kwa watani wake Wazaramo kwenye matangazo ya moja moja mubashara ya kulitangazia taifa zima. Kauli yoyote ya rais ni sheria.

Rais kama binadamu na kama Msukuma ana haki ya kutaniana na watani zake Wazaramo vyovyote vile ataona inafaa, lakini utani huo ama autolee kwa Wazaramo wwnyewe na sio mubashara kwa taifa zima, na utani kama huu ukitolewa kwenye matangazo mubashara ya moja kwa moja kwa taifa zima, then rais akiishatoa utani kama huo amalizie kwa kusisitiza ni utani tuu au kwa Wazaramo tuu.

Kuna vitu rais wetu anasema au anafanya vinavyoashiria amekosa ushauri sahihi.

Mfano mzuri ni issue ya Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam Mhe. Paul Makonda, hii issue imekuwa too much mishandled hadi kumchafulia rais na kumjengea chuki ndio maana kwenye mitandao ya kijamii watu wamekasirika sana hadi kumkosea heshima na kutoa lugha za machukizo.

Japo mimi sio mtu wa serikali, bali naamini Wakuu wa Utumishi wa Umma wote popote walipo ni wasaidizi wa rais. Wasaidizi wa rais wanaoaswa kuwa pro active kumsaidia rais wakali wote na sio kusubiri hadi waulizwe rasmi ndipo wasaidie.

Kadhia ya Paul Makonda kutumia vyeti ya kughushi na kufanya udanganyifu ilipoibuka tuu, kabla haijafikia stage ya kumchafulia rais, wasaidizi wa rais wanaohusika walipaswa kujitokeza wao na kumweleza rais ukweli kuwa ni kweli Paul Makonda ndie Daud Albert Bashite na yote yanayosemwa kumhusu mtu huyu ni ukweli kabisa hivyo wangemshauri the right thing to do, hili jambo lingekuwa limekwisha, lakini kumfukuza Waziri Nape kwa hasira na kuendelea kunyamaza as if nothing has happened, hukuwezi kusaidia kitu kuondoa hizo negative perception. Solution ya kudumu ni kuja na ukweli tuu. He has to tell the truth and the truth will set him free. Nikimaanisha baada ya ukweli kujulikana kuwa Daud Albert Bashite ndiye Paul Christian Makonda, then kwa wanaoujua ukweli huu kuwa Daud Albert Bashite ndiye Paul Christian Makonda, kwao he will always be Daud Albert Bashite, and never will he be Paul Christian Makonda, na huyu Paul Makonda he is an imposter!. Na kwa wale wote wanaomfahamu Paul Christian Makonda as Paul Christian Makonda, wataendelea kumfahamu kama Paul Makonda but with much skepticism and reasonable doubt kuwa could he be the real one or ni imposter hadi tuhuma zile zikanushwe rasmi kuwa ni uongo na uzushi!.

Tukija kwenye tukio la uvamizi wa Clouds Radio, Msaidizi wake Nape did the right thing kwa ku come forward na kusema wazi ule ni unajis wa mtu binafsi na sio serikali. Japo kuunda tume wasn't the right approach Nape kama Msaidizi wa rais ambaye ni Waziri, Makonda ni bwana mdogo sana kwake, angemkabili kuupata ukweli yeye and go straight kwa rais kumpa first hand information na kumwachia rais kufikia uamuzi.

Rais angekuwa ameshauriwa vuzuri na wasaidizi wake wanaoujua damage control, wangemshauri rais kuwa dogo ame mess, hivyo ili kulipa millage ya kutosha tukio la rais wa Benki ya Dunia, rais hakupaswa kusema chochote kumhusu huyo dogo. Tukio la uvamizi wa RC kwenye Chumba cha Habari ni tukio kubwa kuliko hata Benki ya Dunia ingehamishia strong room yake pale ikulu kutokana na proximity na impact ya news ya uvamizi.

Juzi asubuhi rais anafanya uteuzi mpya kwa hasira bila kutengua uteuzi wa zamani, kisha akaenda bandarini kwenye ziara ya kushtukiza. Huku nyuma akatokea kichaa mmoja kumtishia bastola waziri wake aliyetumbuliwa. Kihabari yaani ki newsworthyness, tukio la waziri kutishiwa bastola na kichaa fulani ni bigger news kuliko rais kutembelea bandarini.

Kwa vile rais hakufurahishwa jinsi media haikutoa umuhimu stahiki kwa matukio ya msingi yenye umuhimu mkubwa sana kwa taifa, na yeye pale ikulu anayo kurugenzi yake ya habari, lilikuwa ni jambo dogo tuu hata kuteta na Msigwa kwa kumuuliza hivi hii inakuwaje, Msigwa angemweleza tuu ukweli what was news kuliko rais kuonyesha hasira kwa media.

Wasaidizi wa rais wa kila eneo wana wajibu wa kumsaidia rais wetu kwa kumshauri kufanya uamuzi sahihi na kumwachia rais kufanya uamuzi wowote ila sisi kama Watanzania tuna shauku ya kumuona kila wakali rais wetu akifanya na kutenda the right thing at the right time and doing it right. Handling ya Makonda-Bashite-Nape Thing was a wrong thing, done at at a wrong time and done wrongly!.

Washauri wa rais mko wapi na kumuona rais wetu anasema na kutenda as if hana washauri?! .
Sisi jf tutaendelea kushauri kwa lengo la kujenga.

Tanzania ni yetu sote na rais Magufuli ni rais wetu wote.
Mungu Ibariki Tanzania.
Jumamosi njema.
Paskali

Kudadeki..Hivi Ndivyo Diamond Akusanya Kijiji Kwenye Show ya Muscat(Pichazz)..!!

0
0

Usiku wa Ijumaa hii Diamond alifanya show kubwa ambayo ilihudhuriwa na umati mkubwa wa watu waliojitokeza kutoka sehemu mbalimbali katika mji wa Muscat nchini Oman. Hizi ni baadhi ya picha za show hiyo.


Mo Dewji Kuikabidhi Simba Mikononi Mwa Juventus ya Italia..!!!

0
0

Mohammed Dewji amepanga kuiunganisha Simba kwa Juventus ya Italia.

Tajiri huyo namba moja kwa sasa hapa nchini alitua Italia katika klabu hiyo mapema wiki hii na kufanya nao mazungumzo juu ya kuinua soka la Tanzania. Akiongea na mtandao wa Salehjembe, Dewji amesema, “Wiki hii nilifanya kikao na Juventus FC. Wanayo nia ya kuendeleza soka kwa vijana wa Tanzania. Ninatazamia kuitambulisha timu hiyo ya Italia kwa uongozi wa Simba SC ili waanze majadiliano ya jambo hilo.”

Juventus imekuwa ikishirikiana na baadhi ya nchi za Afrika katika kuendeleza mchezo huo ikiwemo Libya (wakati ikiwa tulivu), Tunisia, Morocco na Misri.

Ni Mlipuko..Huu Ndio Mchezo Atakao Ufanya Gwajima Kesho Jumapili Kuhusu Makonda na Vyeti Vyake vya Elimu...!!!

0
0

Baada ya jumapili iliyopita kuweka wazi cheti cha matokeo ya Makonda na hujuma zake za kumtumia dada kupotosha umma,Dr.Gwajima pamoja na mahubiri,kesho ataendelea kuwafunulia watanzania. Kesho ataweka wazi cheti cha Paul Christian mwenyewe ambacho ni cheti alichokitumia Makonda kupatia elimu ya chuo

Harmorapa Bwana..Eti Ametaja Sababu ya Kutimua Mbio Baada ya Nape Kuonyeshwa Bastola Juzi..!!!

0
0

Msanii asiyekaukiwa 'kiki' katika ulingo wa sanaa ya Bongo, Harmorapa amesimulia kilichomkuta alipokwenda kumuona aliyekuwa Waziri wa habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo Nape Nnauye kiasi cha kutoka mbio za aina yake, baada ya kuona bastola.

Harmorapa ambaye kwa sasa anatamba na ngoma yake inayokwenda kwa jina la 'Kiboko ya Mabishoo' aliyomshirikisha Juma Nature, amesema kilichomfanya aende katika mkutano ule mara baada ya Nape kuondolewa kwenye nafasi yake ya uwaziri, ni kumpa pole na kumshukuru Nape kwa kuwa ndiye aliyekuwa mlezi wa tasnia ya sanaa nchini.

Akizungumzia tukio alilolishuhudia la Nape kutishiwa bastola mbele yake, Harmorapa aliyekuwa akizungumza na eNewz ya EATV, amekiri kuwa ni kweli hajawahi kuiona kwa ukaribu ule, hivyo alipoona inachomolewa aliogopa na kujikuta akitoka mbio, huku akikanusha utani ulioenea mitandani kuwa alikimbia hadi Mtwara.

Noma Sana .. Steve Nyerere Afunguka ya Moyoni Baada ya Nape Kutumbuliwa,Amtaka Afanye Hivi..!!!

0
0

Muigizaji maarufu wa vichekesho  Steve Nyerere amemshauri Mh.Nape Nauye kumshukuru Mungu na kumuomba kwa kutenguliwa uwaziri kwa kuwa hajui ameepushwa na jambo gani.

Akiongea na eNewz Steve Nyerere ameendelea kusema kwamba Mh. Nape nje ya uwaziri alikuwa ni msanii pia na alikuwa anaithamini thamani ya msanii na kuilinda pia alikuwa akipenda maendeleo ya wasanii na maendeleo yake na alikuwa na uwezo wa kupiga simu hata usiku kufuatilia masuala ya sanaa.

Amemshauri Nape aendelee kuwa karibu na wasanii na kuwashauri kwa ajili ya kusukuma mbele maendeleo ya sanaa nchini.

"Nape kama waziri aliyekuwepo, ajue kuwa ana jukumu la kuwashauri wasanii kupiga hatua, kuondoka kwake siyo kuwakimbia wasanii, abaki kuwa mshauri wa wasanii kupiga hatua na kusonga mbele.. Nape ana uwezo mkubwa sana, ana ushawishi mkubwa sana" Amesema Steve

Hata hivyo Steve alimalizia kwa kumshauri Nape kukaa na familia yake na kusali kwa kuwa Mungu ndiye alipanga apewe madaraka ya kuwasimamia wasanii lakini pia amshukuru kwa kuchukua cheo hicho kwa kuwa hajui Mungu kamuepusha na nini na asiogopeshwe na miguno ya wananchi"

Steve pia amemsihi Dkt. Mwakyembe kukabiliana na changamoto lukuki zinazoikabili sanaa

Kimenukaa..Mchungaji Peter Msigwa wa Chadema Amchana Magufuli Kuhusu Hotuba Yake ya Jana...!!!!

0
0

Nadhani Mhe.Rais hajui maana ya uzalendo. Na pengine anadhani kwa kuwa Rais basi yeye ni Mzalendo kuliko wote. Ni mtazamo potofu. Kuwa Rais wa nchi au ngazi yoyote ya UONGOZI na madaraka katika taifa letu, sio kigezo cha uzalendo , japo inategemewa hivyo,
1. Kuvunja katiba ya nchi kwa kuzuia vyama vya siasa visifanye mikutano ya hadhara , huo sio uzalendo.

2. Kutisha vyombo vya habari visitangaze askari anyetoa bastola hadharani kinyume na taalume na maadili yake , huo sio uzalendo.

3. Kukemea na kufokea wahanga wa tetemeko la ardhi kwa kudai setikali haikuleta Tetemeko huo sio uzalendo.

4. Kutumia vyeti amabavyo sio vyako , huo sio uzalendo.

5. Kuvamia vituo vya Tv za watu kwa maslahi yako binafsi , huo sio uzalendo,

Msigwa the MP For iringa urban 24/3/2017

Msukuma - Sioni Tatizo kwa Mhe Nape Kuonyeshwa Bastola,Mbona Mimi Nilionyeshwa SMG Nane na Sikulalamika,Pia Aaache Kulilia kwa Kutenguliwa Kila Mtu Anauhitaji Uwaziri..!!!!

0
0

Akihojiwa Jana, Msukuma alidai kwa walichokifanya watu wanaodaiwa ni askari kumuonyesha bastola mhe Nape ni sahihi kwani kitambulisho cha askari yeyote ni bastola au bunduki hivyo Nape hakupaswa kuwa na shaka maana walikuwa wanamlinda. Msukuma alienda mbali zaidi na kusema hata yeye alionyeshwa SMG nane lakini hakuwa na shaka maana wale ni askari.

Aidha Msukuma Alisema Kuwa Mhe Nape Alipaswa Kutulia kwanza hata kwa miezi mitatau ndipo angezungumza aliyotaka kuzungumza.

Pia Amemsihi Mhe Nape Kuacha Hasira  mara baada ya kutenguliwa kuwa Waziri kwani wakati anaomba kura katika jimbo lake la Mtama aliomba hakuomba na uwaziri ,hivyo asilie kuenguliwa katika wazifa huo kwani bunge lina wabunge 360 na kila mbunge angependa kuwa waziri,hivyo kuenguliwa kwake katika nafasi hiyo inawapa nafasi wabunge wengine nao kuwa mawaziri siku moja na hata yeye anatamani kuwa waziri  

Tuweni Makini Wakati wa Kuwapa Watoto Majina...!!!

0
0

Hili limekuwa tatizo sasa, wazazi mnawapa watoto wenu mizigo bila kujua. Majina yana tabia ya ku-reflect tabia ya mhusika... Mfano mtu anaitwa mashaka, tabu, shida, mawazo,hatia,majuto.
Matokeo yake mtoto akiwa mbaya mnaanza kumlaumu kumbe shida ni nyie. 

Mfano mtu anaitwa kilevi... Alafu unategemea awe na busara kweli.. Matokeo yake ndo haya mnakuja kuwapa watu shida buree.
Kuweni makini.

Breaking News,,Baada ya Jana Kuawaapisha Mawaziri,Rais Magufuli Afanya Uteuzi Mwingine Mpya Leo..!!!

0
0

Rais Dkt Magufuli JP amteua Bw. Charles Edward Kichere kuwa Kamishna Mkuu Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA)

Mbowe :Rais Magufuli Ndiye Rais wa Pekee Tanzania Atakaekaa Madarakani kwa Kipindi Kimoja..!!!

0
0

Mhe Rais Magufuli ndiye rais wa pekee Tanzania atakaekaa madarakani kwa kipindi kimoja cha utawala wake kutokana na kuendesha nchi kibabe bila kufuata sheria, uonevu, upendeleo na hali ngumu ya maisha inayawakabili wananchi tofauti na kipindi kilichopita.Mbowe ametoa kauli hiyo wakati akizindua tawi jipya la Chadema katika kijiji cha Mpakani Kata ya Kwakifua Wilaya ya Muheza mkoani Tanga leo Jumamosi

Freeman Mbowe

M/kiti Chadema-Taifa.
Viewing all 104428 articles
Browse latest View live




Latest Images