Quantcast
Channel: UDAKU SPECIAL
Viewing all 104756 articles
Browse latest View live

Zitto: Tumejulishwa na NECTA Hakuna Rekodi za Daud Albert Batishe Wala Paul Makonda...!!!!

$
0
0
Tumejulishwa Kwenye Kamati Kuwa Nacte Hawana Rekodi ya Albert Bashite Wala Paul Makonda..Yani Wote Hawapo kwenye Taarifa za NECTA

Makonda: Zitto Amenisaidia Sana Kuelewa Siasa..!!!!

$
0
0

Mkuu wa Mkoa wa Dsm, Paul Makonda akiwa kwenye interview amesema Mbunge wa Kigoma Mjini(ACT) ndiye Mbunge anayemsaidia kuelewa siasa.

Afafanua kuwa, Zitto anajua kujenga hoja za kuiyumbisha serikali hasa kwenye kusimamia mambo mbalimbali yenye maslahi ya kitaifa.

Kutoweka kwa Ben Saanane: Baba Yake Amwambia Godbless Lema Amsaidie Kumtafuta...!!!!

$
0
0

Baba yake na Ben Saanane amwambia Godbless Lema maneno haya;

''Ben ni mwanangu sio mbuzi wangu, nisaidieni kumtafuta mwanangu, moyo wangu unauma''.

Onyo kwa Bunge Dhidi ya Adhabu kwa Makonda...!!!

$
0
0

Ni hakika kwa100% Daud Albert Bashite alimaarufu Paul C. Makonda amekiri tuhuma zote mbele ya Kamati ya Bunge leo,

Kinachosubiriwa ni maoni ya kamati hiyo kwenda kwenye Bunge ambapo taarifa na maoni hayo vitasomwa Bunge linaloanza wiki ijayo 04/04/2017.

Mimi kama raia mwenye haki na wajibu kwa taifa langu, nikitambua haki yangu kwamba Bunge ni chombo changu cha uwakilishi, Natoa onyo kwa Kamati husika na Bunge pia, Ole wenu mje na hadithi ya kwamba MMEMSAMEHE.

Narudia ole wenu, Ole wenu, ole wenu kabisa..... Sisi wananchi tuna kesi nzito sana na huyu mtu nje ya yeye kutudharau na kutudhihaki kupitia bunge letu ambalo nyinyi tumewatuma mtuwakilishe...

Nataka mtambue kila mnachofanya hamfanyi kwaniaba yenu, bali kwaniaba yetu, Hivyo sisi tuliowatuma tayari tulishamhukumu na kufunga file lake.

Ole wenu mbadilishe maamuzi ya umma, Sisi ndio wenye mamlaka ya mwisho katika nchi hii, sio rais, sio jaji, sio spika, bali sisi tukisema na kuamua mbinguni na duniani tumeamua.... Hii ni kwamjibu wa katiba ya 1977 na ile inayopendekezwa ya Warioba na hata ile ya Marehemu Sitta bado hazikutung'anya mamlaka yetu.

Ukisikia kwamba mamlaka yote yanatoka kwa Mungu haimaanishi Mungu wa ulaya au asia, Mungu ni sisi Watanzania..
Sisi tukisema ni Mungu amesema!

Ole wenu wabunge!!!!!

Na Yerico Nyerere

Haya Hapa Maujanja ya Kutengeneza Natural Viagra, Mademu Lazima Wakukome..!!!

$
0
0

Nimeamua kuisaidia kambi yangu ya kiumeni manake wachuchu wanaishambulia sana, mara ooh Sku hizi wachezaji wamekuwa wachovu,
Mara wanasema eti hatufungi magoli ya uhakika na wengine wanafika mbali zaidi wakisema eti hatuwezi kuhimili mchezo kwa dakika 90 Kudadekii..

Sasa nasemajeee wanawake mjiandae...

Mazee miluzi mingi humchanganya mbwa! Sasa mimi ngoja niende straight to the point, Le'go..

JINSI YA KUANDAA MCHANGANYIKO WA NATURAL VIAGRA

Vinavyohitajika

i.¼ Tikikiti maji ( watermelon)
ii.1 Limau (lemon)
iii.1 Komamanga(pomegranate)

Jinsi ya kutengeneza

- Chukua hivyo tikiti likate vipande vidogovidogo( hata ule utando mweupe wa chini pia muhimu sana hivyo hakikisha unalikwangua vizuri), kisha viweke pamoja na hayo matunda mengine kwenye blenda kwaajili ya kusagwa.

- Visage vizuri mpaka viwe juice, kisha chukua juice yako weka kwenye sufuria alafu viweke jikoni vichemke, hakikisha vinachemka mpaka vinatoa mvuke wa kuevaporate,

- Baada ya hapo iepue kisha iache ipoe kwa muda kama wa saa1(lisaa limoja),

- Hapo sasa weka kwenye chupa au chombo chenye mfuniko kisha hifadhi kwenye friji, na hapo utakuwa umeshatengeneza, twende kwenye matumizi sasa tehetehe leo mademu watakoma leooo!

Jinsi ya kutumia

- Kila siku asubuhi kunywa 1/3 ya kikombe au glass, hakikisha unakunywa kabla haujala chochote( empty stomach)

- Fuata utaratibu huo pia kabla ya msosi wa mchana.

NB: Hiyo ni juice ya asili kabisa ambayo itakwenda kurekebisha msukumo wako wa damu mwilini na kukuongezea stamina ya kupafomu shoo ambayo sio ya nchi hii,
Na pia hiyo juice inaweza kutumiwa na mtu yeyote kwasababu haina side effects.

ONYO: Hiyo juice baada ya maji usiichanganye na kitu chochote kile mfano Sukari, chumvi, Ladha(taste), rangi, au kiungio chochote kile kwa sababu vinaweza kuipunguza nguvu ya utendaji kazi.

Vilevile Wakati unachanganya hayo matunda usitoe mbegu, changanya na mbegu zake...

Mambo ya k\Kufanya Ukifumaniwa...!!!!

$
0
0

1. Tafuta upenyo, utoke nduki (hata kama u mtupu) ndo pona yako.

2. Usifikirie mali zako ulizoacha eneo la tukio (nguo, simu, begi)

3.Hakikisha umekimbilia sehemu ya siri sana, mfano; Mafia, Bagamoyo (upotee kwa muda).

4. Nenda kwa kiongozi wa dini (Sheikh, Askofu, Padiri, Nabii Gwajizo) ukatubu dhambi ya uzinzi

Hizi Hapa Sababu za Wanaume Wengi Kutokuoa Siku Hizi..!!!

$
0
0

Kumekuwa na maswali yasiyo na majibu miongoni mwa jamii kwamba imekuaje vijana wa kiume wamekuwa ni waongo sana hasa linapokuja swala la kuoa? Kwa kadiri siku zinavyozidi kwenda ndivyo ambavyo idadi ya wanaume wanaoogopa kuoa inazidi kuongezeka. Utakuta wapenzi wanaambiana kwamba wanapendana na kuahidiana kuwa wataoana, lakini kitakachotokea baada ya hapo ni mwanaume kuanza kupiga chenga kwa visingizio lukuki.

Kwa nini hali hiyo hutokea? 

Ukweli ni kwamba hakuna jibu la moja kwa moja juu ya tatizo hilo, lakini yapo mambo ambayo yanaweza kutupa angalau tafakuri. Nitajaribu kudadavua baadhi ya sababu zinazowafanya wanaume siku hizi kukwepa kuingia katika taasisi ya ndoa: 

1 Ukosefu wa mtu wa kumchukulia kama mfano:
Hapa nawazungumzia wale watoto wa kiume waliolelewa malezi ya upande mmoja yaani walilelewa na mama peke yao. Sina maana ya kudharau au kutweza malezi ya mama, la hasha, lakini ni vyema mkafahamu kwamba kuwa na baba asiye na malezi mazuri si sawa na kutokuwa na baba. Na ndio maana nikasema ukosefu wa mtu wa kumchukulia kama mfano. Achilia mbali aina ya malezi atakayoyapata kwa familia yawe mazuri au mabaya lakini lazima kutakuwa na tabia za kiume zitakazoakisi malezi ya mtoto wa kiume katika familia husika. Watoto waliolelewa na mama peke yao kuna kitu huwa wanakosa, kwani wanakuwa hawana mtu wa kumchukulia kama mfano kwa upande wa jinsia ya kiume na hapo ndipo hujikuta wakijifunza wenyewe namna ya kuongea na kutenda kama wanaume kwa sababu katika makuzi yao hawakupata fursa ya kuwa karibu na baba zao. Kwa kuwa siku hizi kuna kundi kubwa la kina mama ambao wamejikuta wakiachiwa mzigo wa malezi ya watoto, baada ya aidha kuachwa na waume zao au kuzalishwa na kutelekezwa (Single mothers), na hapo ndipo tunaposhuhudia mtoto wa kiume anapokua kwa umri na kimo huku akiwa hana mtu wa kumuangalia kama mfano wa mume anavyotakiwa kuwa katika familia zaidi ya kujifunza mambo hayo kupitia katika TV, senema au miziki. Wanaume waliopitia malezi ya aina hii huchelewa sana kuoa kwani huyaangalia maisha ya ndoa kwa namna ya kujaribu na ndipo hapo wengi huishia kuishi kinyumba na wanawake kwa ajili ya kutaka kujifunza namna ya maisha ya ndoa yanavyotakiwa kuwa na ndio sababu huchukua muda mrefu kufanya maamuzi. Na mara nyingi huishia kubadilisha wanawake kutokana na kutokuwa na uhakika wa kile wanachokitafuta.

2 Mgogoro wa kiuchumi:
Kuna kundi kubwa la vijana siku hizi hawana ajira au hawana uhakika na kipato. Ukweli ni kwamba hakuna mwanaume atakayependa kujiingiza kwenye ndoa wakati hana kazi au hana uhakika na kipato chake. Na hiyo ni kutokana na wanawake wengi siku hizi kuonekana kujali zaidi wanaume wenye uhakika na kipato. Hii misemo ya wanawake ya kebehi dhidi ya wanaume wasio na ajira au kipato, kama vile “mwanaume suruale” ina mchango mkubwa sana katika kuwafanya wanaume kukwepa kuoa iwapo hawana ajira au hawana uhakika na kipato chao.


3 Wanawake wengi kuwa na kiwango cha elimu ya juu:
Siku hizi wanawake wengi wameibuka katika kutafuta elimu ya juu kwa juhudi kubwa. Idadi ya wanawake wanaojiunga na vyuo vikuu ni wengi tofauti na ilivyokuwa zamani. Na hiyo ni kutokana na wazazi wengi kubadili mtazamo wao juu ya mtoto wa kike. Zamani mtoto wa kike alichukuliwa kama kitega uchumi. Kwa maeneo ya vijijini na katika familia masikini, watoto wa kike walikuwa wanatazamwa kama, ‘biashara ya kesho’ ambapo watauzwa kwa njia ya mahari. Kwa hiyo thamani yao ilikuwa ni kuolewa, ni ile ya kibidhaa na sio kibinadamu. Lakini tofauti na zamani siku hizi hata kule vijijini kumekuwa na mwamko mkubwa sana wa kumsomesha mtoto wa kike hadi elimu ya juu. Kutokana na mwamko huo wanawake wengi wamejikuta wakiona elimu kama kimbilio pekee la kuepukana na mfumo dume. Mwanamke gani atakubali kunyanyaswa na mwanaume akiwa na elimu yake na labda pia akiwa na kazi yake yenye mshahara na marupurupu ya kutosha, naamini watakuwa ni wachache sana ambao hawajiamini au waliathiriwa na malezi. Kwa upande wa wanaume nao, wamejikuta wakiwaogopa wanawake hawa wenye elimu ya juu kwa hofu ya kuzidiwa kipato na labda kukosa sauti kama mwanaume na hiyo inatokana na ego tu.

4 Wanaume huwaona wanawake kama tishio wanapokuwa na mafanikio makubwa kifedha:
Inaweza kutokea mwanaume anaweza kuwa na uhusiano na mwanamke ambaye labda tu nisema ni mbangaizaji. Wakati huo anaweza kuahidi kufunga ndoa na mwanamke huyo, lakini iwapo itatokea mwanamke huyo akapata mafanikio kibiashara na kuinuka kifedha. Kama mwanamke asipokuwa makini anaweza kusababisha mwanaume huyo akaingia mitini. Sababu kubwa hapo inaweza kuwa ni hofu ya kuogopa kuongozwa na mwanamke. Kumbuka kwamba mfumo dume bado umetawala vichwani mwa wanaume wengi kutokana na malezi. Mwanaume asiyejiamini ni vigumu sana kwake kuoa mwanamke aliyemzidi kipato. Kwa sababu akifanyiwa jambo dogo tu, inakuwa kama ametoneshwa. Atahisi kutaka kutawaliwa na mwanamke huyo. Jambo ambalo wanawake wanatakiwa kulifahamu ni kwamba kila mwanaume anataka kutambuliwa na kuheshimiwa kama shujaa kabla ya kumfuata msichana. Iwapo utakuwa umesimama iwe ni kifedha au kielimu pale unapotafuta kupata mwenza, inabidi ujishushe sana la sivyo utadoda.


5 Wanaume wengi siku hizi wana hofu ya majukumu, hasa ya kulea watoto:
Kutokana na malezi yao au kile wanachokijua kuhusu watoto, baadhi ya vijana huamini kwamba, kulea watoto ni jambo gumu sana. Lakini wengine wanaamini kwamba, hata mke anapaswa kulelewa kama ilivyo kwa mtoto. Hivyo wanaamua kutafuta kwanza uwezo ambao haupatikani kiurahisi. Kuna wengine, ambao wamefundishwa au kuelekezwa na mila na desturi zao kwamba, kabla hawajaoa, ni lazima wawe na nyumba kwanza, tena kwao. Kwa hiyo, hawa hadi waje wapate uwezo wa fedha wanakuwa wameshachelewa.

6 Kuna baadhi ya wanaume, maisha bila ya ndoa wanayaona kuwa ndiyo bora kuliko yale ya ndoa:
Kuna baadhi ya wanawake hujirahisisha sana kwa wanaume. Siku hizi ni jambo la kawaida sana kukuta mwanaume anaishi na mwanamke bila ndoa, wenyewe wanaita Trial Marriage. Na hapo ndipo unapokuta wanaume hawaoni tena umuhimu wa kuoa. Sasa kama mwanamke anaweza tu kuishi na mwanaume bila ya ndoa na mwanaume huyo akapata huduma zote kutoka kwa mwanamke huyo, unadhani ni kitu gani kitamvuta kufunga ndoa. Jambo lingine ni ile dhana kwamba maana ya ndoa ni tendo la ndoa. Siku hizi wanaume wengi wamejikuta wakiwa hawahitaji tena kuoa kwa sababu tendo hilo linapatikana kiurahisi tofauti na zamani. Siku hizi inawezekana kabisa kumtongoza binti leo na kupata tendo siku hiyo hiyo….. Na hapa siwazungumzii makahaba. Nawazungumzia mabinti zetu ambao wengine ukiwaona ni watu wa kuheshimiwa ukiwaangalia kwa nje lakini kwa ndani hawana lolote, vijana wa siku hizi wenyewe huwaita maharage ya Mbeya.

Kuna sababu nyingi zinazotajwa kusababisha wanaume siku hizi kujivuta sana katika kufanya maamuzi ya kutafuta mwenza. Lakini hizo chache nilizozitaja zina mchango mkubwa.

Kwanini Wanawake Wengi Siku Hizi Hawaolewi? Jibu Mubashara Hili Hapa

$
0
0

*KWA NINI WANAWAKE WENGI SIKU HIZI HAWAOLEWI? WENGI HUPISHANA NA WAUME ZAO*

Mwanamke anapigiwa simu kwa namba ngeni, anauliza namba yangu umeitoa wapi? Usiponiambia aliyekupa usinipigie. _HAPO UMEPISHANA NA MUME_

Mwanamke anaingia ndani ya daladala, amekaa na mwanaume, kwa maringo, anachukua earphone na kuweka masikioni na kuwasha mziki ili asiongeleshwe. _HAPO UMEPISHANA NA MUME._

Mwanamke anasalimiwa njiani, anaitikia, akiongeleshwa tena anachuna. _HAPO UMEPISHANA NA MUME._

Mwanamke unatumiwa meseji inbox, hujibu. _HAPO UMEPISHANA NA MUME._

Mwanamke unapigiwa simu na mwanaume, unaona kabisa anakupigia ila hutaki kupokea tu. _HAPO UMEPISHANA NA MUME._

Mwanamke unakwenda gheto kwa mwanaume, una mkoba wako, ukifika muda wa kuondoka unaomba nauli. _HAPO UMEPISHANA NA MUME._

Mwanamke unakwenda kwa mwanaume, badala ya kusonga ugali, cha kwanza unataka chipsi kuku. _HAPO UMEPISHANA NA MUME._

Mwanamke unaanza uhusiano na mwanaume, siku ya pili tu unamwambia bebi sina hela ya vocha. _HAPO UMEPISHANA NA MWANAUME._

Mwanamke upo na mwanaume, anakwambia agiza chochote, bila kujishtukia unaagiza bia. _HAPO UMEPISHANA NA MUME._

Mwanamke unachati na mwanaume, chatting zako ni K, P, Pw. _HAPO UMEPISHANA NA MUME._

Mwanamke unaweka picha mapaja wazi, kifua umebust. _HAPO UMEPISHANA NA MUME._

Mwanamke unamwambia mwanaume akutumie video za ngono kwenye simu. _HAPO UMEPISHANA NA MUME._

_Usilalamike kwamba kwa nini mpaka sasa hivi hujaolewa. Niambie sasa ni mara ngapi umepishana na mume!_

Dr Lov
@2017

KUTANA na Mtabibu Ostadhi Khamisi Kutoka Mombasa Kenya Kwasasa Yupo Tanzania Kwa Ajili yako

$
0
0



Kutana na ostadhi khamisi kutoka mombasa Kenya kwa sasa yupo Tanzania ni mtabibu na mtafiti Wadawa za asili anatibia kama vile:
Miguu kuuma
Miguu kufagazi
Miguu kuwakamoto
Chango lauzazi kwakina mama
Dawa ya uzazi wakina mama inapatikana
Kusafisha nyota ili uwe namuonekano kwa kila mtu
Kumrudisha mpenzi wako na liekukimbia ndani yasiku 3 bila yapingamizi yoyote
Kumshika mume au mke asitoke nnje ya ndoa
Pata pete ya Bahati inayo endana na nyota yako
Kurudisha mali ilipotea au kudhurumiwa ndani yasiku 3
Pata utajili usiokuwa namashaliti yoyote
Dawa za nguvu za kiume
Dawa ya biashara inapatikana
Dawa ya kuzuia chuma ulete kwenye biashara inapatikana
 Zindiko la nyumba au shamba
 Anatuliza familia zinazogombana DUWA pamoja navisomo vya ufunguzi wa mwili wako njoo ufunguliwe vifungo ulivyo fungwa kutana na ostadhi khamisi utimiziwe ahadi ulizo hadiwa acha kuteseka acha kuhangaika ostadh khamisi yupupo tanzania kwajili yako...

Call +255718746825 +255754765246 kwa what'sapp +255783708487

Hivi Ndivyo Paul Makonda Alivyosulubiwa na Kamati ya Bunge Jana

$
0
0

MKUU wa Mkoa wa Dar es Salaam, Paul Makonda jana alihojiwa kwa saa tatu mfululizo na Kamati ya Haki, Kinga na Madaraka ya Bunge kwa tuhuma za kuingilia haki, uhuru na madaraka ya chombo hicho cha kutunga sheria.


Makonda aliwasili Bungeni Dodoma majira ya saa nne asubuhi kuitikia wito wa Kamati hiyo uliotokana na Azimio la Bunge lililotolewa Februari 8 na kuhojiwa na kamati hiyo kwa muda wa saa tatu kuhusu tuhuma zinazomkabili.


Katika kikao hicho, Bunge liliamua Makonda aitwe kujieleza kwenye Kamati ya Bunge ya Haki, Kinga na Madaraka kwa tuhuma za kukashfu chombo hicho.


Sambamba na uamuzi huo, pia Bunge liliagiza mbunge yeyote ambaye kwa namna yoyote anadhani amekashfiwa na Makonda, awasilishe malalamiko yake kwa Spika ili hatua zaidi zichukuliwe.


Hatua ya kutaka Makonda aitwe mbele ya kamati hiyo, ilitokana na mwongozo uliotolewa na Mbunge wa Mkuranga(CCM), Abdallah Ulega, kwa Mwenyekiti wa Bunge, Andrew Chenge, aliyedai mkuu huyo wa mkoa ameudharau mhimili huo wa dola na wabunge.


Akizungumza mara baada ya kumaliza kazi yao, Mwenyekiti wa Kamati ya Haki, Maadili na Madaraka ya Bunge, George Mkuchika alisema Makonda alidaiwa kutoa kauli kupitia televisheni ya Clouds akidai kwamba wabunge wanasinzia bungeni jambo lililoonekana kwamba ni kudharau mhimili huo wa dola.


“Napenda kutoa taarifa kwamba mheshimiwa Makonda leo amekuja mbele ya Kamati na ametupa ushirikiano mzuri," alisema Mkuchika ambaye ni mbunge wa Newala Mjini (CCM).


"Tumepokea maelezo yake na Kamati imemaliza kazi yake.”


Alisema Kamati yake itakabidhi taarifa yake kwa Spika Job Ndugai kwa mujibu wa kanuni, ambaye ndiye atakayeamua namna ya kutoa taarifa kuhusu kazi ya kamati hiyo.


Katika mwongozo wake kwa Spika, Ulega kwa kutumia Kanuni ya 68 (7), alisema kupitia vyombo vya habari, kuna taarifa kwamba Makonda ametoa kauli ambazo zinaashiria na kuonyesha dharau kwa Bunge.


“Sisi wabunge tuko mstari wa mbele katika kuhakikisha tunapambana na kumsaidia Rais (John Magufuli) kwenye vita dhidi ya dawa za kulevya. Ikumbukwe kwamba sheria inayosimamia vita dhidi ya dawa hizo imeundwa kwenye Bunge hili," alisema Ulega.


“Kama haitoshi wabunge bado tunayo kumbukumbu siku alipokuja kipenzi chetu, Rais Dk. John Magufuli na kuhutubia, tulimshangilia sana alipotangaza rasmi kwa nguvu zake zote juu ya vita dhidi ya dawa za kulevya.


"Leo wabunge wameambiwa kwamba hawana jambo isipokuwa wanakuja kufanya kazi ya kulala kwenye Bunge hili.”


KIJANA MZALENDO

Mbunge huyo alisema akiwa kijana mzalendo na Makonda kuwa mdogo wake na rafiki yake pia, ni lazima Bunge kama chombo huru kiendelee kuheshimika.


“Sisi tunadhani ya kwamba mawili... ama kijana mwenzangu huyu hakuwa anajua anachokisema au amefanya dharau ya makusudi.


"Ninaomba kutoa hoja zifuatazo ili unipe mwongozo tuone tunaendaje kutoka hapa tulipo, hasa ukizingatiwa sisi ndio ‘number one’ wa kumsaidia Rais katika vita hii.”


Katika hoja hizo, Ulega aliomba Waziri Mkuu Kassim Majaliwa akiwa kiongozi mkuu wa serikali, achukue hatua za makusudi ili kuwalindia heshima wabunge.


“Au kwa kutumia kanuni za Bunge na sisi tunayo kanuni ya haki, kinga na madaraka ya Bunge, kanuni na sheria basi hatua zichukuliwe kupitia muhimili huu, au atumie tena vyombo vya habari vile vile kusema kwamba amekosea na anaomba radhi, naomba mwongozo,” alisema Ulega.


Mbali na Ulega, Mchungaji Peter Msigwa wa Iringa Mjini (Chadema), alimpongeza Ulega kuomba mwongozo huo wa msingi kwa hadhi ya Bunge.


“Naomba kwenda kwenye kanuni ya 51 ya Bunge ili wabunge tujadili kuhusu tabia ya Mkuu wa Mkoa huyu anayedhalilisha chombo hiki ambacho ni muhimili muhimu ambacho kinaweza ku-‘balance’


(kuweka mambo sawa) ili serikali ifanye kazi," alisema Msigwa.


"Naomba tujadili hadhi ya Bunge iweze kulindwa. Naomba kutoa hoja.”


Akijibu mwongozo huo, Chenge alisema: “Nimepokea ombi la mwongozo wa Ulega na Msigwa ametaka kuchombeza kama hoja ijadiliwe. Mimi nitajielekeza kwenye ombi la muongozo. Nimemuelewa Mheshimiwa Ulega maelezo yake mazuri tu."


Chenge alisema Bunge kama taasisi na wajumbe wake na ni moja ya mihimili mitatu ya dola (ikiwamo serikali na mahakama) lazima liheshimiwe na mtu yeyote.


“Kwa vile tumejiwekea utaratibu wetu kupitia Kamati ya Kinga, Haki na Madaraka ya Bunge, ili sasa ikathibitike kama ameyasema hayo (ya sisi kulala tu ndani ya Bunge) na wapi, lini na kama yanaangukia ndani ya sheria yetu ya kinga, huko ndiko ukweli wote utakapodhihirika.


“Kwa hiyo mimi kwa suala hili naagiza ofisi ya Katibu wa Bunge, kwa taratibu zilizopo, wamtake Makonda atoe maelezo yake na kama kweli amesema au la na watayapokea na kupelekwa kwenye Kamati ya Haki, Kinga na Madaraka ya Bunge.


"Tutakuwa tupo ndani ya taratibu zetu za kikanuni na ndani ya sheria kwa kuwa lazima ithibitike kama inaangukia kwa haki za Bunge zinazopaswa kuheshimika.”

Magari Yaliyokutwa Kwenye Kontena Yawapandisha Kizimbani

$
0
0

WATU wanne wamefikishwa mahakamani katika kesi mbili tofauti za uhujumu uchumi, kwa kuingiza nchini magari sita kwa kuficha na nguo za mitumba, maarufu kama makontena ya Magufuli, na kuisababishia serikali hasara ya kukosa mapato ya Sh. milioni 478.7.


Katika kesi ya kwanza, watu wawili akiwamo raia wa Zambia, Agustino Kalumba (36) wamefikishwa mahakamani wakikabiliwa na mashtaka matatu ya kula njama, uhujumu uchumi na kuisababishia serikali hasara ya kukosa ushuru wa Sh. milioni 287.8.


Mbali na Kalumba mshtakiwa mwingine ni, Sultan Hassan (29) maarufu kama Mwarabu.

Washtakiwa walisomewa mashtaka yao mbele ya Hakimu Mkazi Mkuu, Thomas Simba.


Upande wa Jamhuri uliongozwa na Wakili wa Serikali Mwandamizi, Nassoro Katuga akisaidiana na Wakili wa Serikali Batilda Mushi.


Katuga alidai kati ya Desemba mosi, mwaka jana na Machi mosi washtakiwa wakiwa na wengine ambao hawapo mahakamani walikula njama ya kutenda kosa la kusafirisha mali iliyofichwa.


Katika shtaka la pili, washtakiwa wote kwa pamoja wanadaiwa kuwa kati ya Desemba mosi na 31, mwaka jana katika Bandari ya Dar es Salaam, iliyopo Temeke jijini Dar es Salaam, waliingiza gari tatu aina ya Range Rover Sports za rangi nyeusi, nyeupe na 'daki bluu'.


Upande huo wa Jamhuri ulidai kuwa gari hizo ziliambatana na nguo, mabegi na viatu vya mitumba wakiwa na lengo la kuwadanganya maofisa watoza ushuru.


Katika shtaka la tatu, ilidaiwa kuwa kati ya Desemba mosi, mwaka jana na Machi mosi katika bandari hiyo, washtakiwa waliingiza mali wakiwa wameficha na kuisababishia serikali kukosa mapato ya Sh. 287,801,825.19 iliyokuwa kwenye kontena namba MSKU 9914168.

K
Hakimu Simba aliwaeleza washtakiwa hao kwamba kesi inayowakabili ni uhujumu uchumi, hivyo hawatakiwi kujibu chochote kwa sababu mahakama yake haina mamlaka ya kusikiliza kesi hiyo.


Katuga alidai kuwa upelelezi upo katika hatua za mwisho kwa ajili ya kuchanganua kama kesi hiyo itasikiliza na mahakama hiyo au Mahakama Maalumu ya Ufisadi.


Hakimu alisema kesi hiyo itatajwa Aprili 12 na washtakiwa wapelekwe mahabusu.


KESI NYINGINE

Katika kesi nyingine, Hassan na Ramadhani Hamis wamesomewa mashtaka matatu ikiwamo kula njama, uhujumu uchumi na kuisababishia serikali hasara ya Sh. milioni 190.9.


Washtakiwa hao walisomewa mashtaka yao mbele ya Hakimu Mkazi Mkuu, Respicius Mwijage.


Katuga alidai kuwa Kati ya Desemba mosi, mwaka jana na Machi mosi washtakiwa walikula njama ya kutenda kosa la kuingiza mzigo ukiwa umefichwa.


Katika shtaka la pili, ilidaiwa kuwa Januari 24 katika Bandari ya Dar es Salaam, iliyoko Wilaya ya


Temeke, jijini Dar es Salaam, washtakiwa waliingiza magari matatu aina ya Range Rover Sports baada ya kuyaficha pamoja na nguo, viatu na magodoro ya mitumba.


Upande wa Jamhuri ulidai katika shtaka la tatu kuwa kati ya Desemba mosi, mwaka jana na Machi 4, washtakiwa waliingiza nchini magari matatu kwa kuficha na kuisababishia serikali kupata hasara ya sh. 190,923,267.76.


Katuga alidai kuwa upelelezi wa kesi hiyo bado haujakamilika.


Hakimu Mwijage alisema washtakiwa hawatakiwi kujibu chochote kwa sababu mahakama hiyo haina mamlaka ya kusikiliza kesi hiyo.


Alisema washtakiwa wataendelea kukaa mahabusu hadi Aprili 12 kesi yao itakapotajwa.A

Ukweli Kuhusu Taarifa ya Nyasi Bandia za Uwanja wa Simba Kupigwa Mnada leo

$
0
0


Makamu wa Rais wa klabu ya Simba, Geofrey Nyange ‘Kaburu’ amesema kweli suala la taarifa ya nyasi zao bandia kutaka kupigwa mnada, limewashitua sana.



Lakini akawataka mashabiki na wanachama wa Simba kutulia wakati uongozi unapambana katika suala hilo.


“Tokea nyasi hizi zimepita tulifanya juhudi ya kuomba msamaha kwa serikali, unajua nyasi hizi si kwa Simba pekee. Ni kwa kwa jamii yote kwa kuwa tunalenga kuendelea vijana ambao hawatakuwa faida yetu pekee.


“Lakini tumekuwa tukiendelea kupambana kuzitoa, tulishaanza ujenzi wa uwanja na suala la nyasi tu.


“Kuhusiana na taarifa kwamba zinataka kupigwa mnada, kweli linashitua. Unajua kawaida mzigo wako ukikaa bandarini baada ya siku 60, unapewa taarifa ya kupigwa mnada. Tunaendelea kulishughulikia hili,” alisema Kaburu.


Taarifa za Kampuni ya udalali ya Majembe Auction Mart inataka kupiga mnada nyasi bandia za Simba imesambaa kwa kasi leo asubuhi.


Imeelezwa kuwa nyasi hizo zitapigwa mnada leo nyuma ya "The Waterfront Sunset Restaurant and Beach Bar”.

Wale Mashekhe Waliokwenda kwa Gwajima Yawakuta

$
0
0


DAR ES SALAAM: Siku nne tu baada ya watu waliotajwa kama mashehe kuingia na kuhudhuria ibada katika Kanisa la Ufufuo na Uzima linaloongozwa na Askofu Josephat Gwajima, lililopo Ubungo Maji, jijini, Shehe Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam, Alhadi Salum, amewalipua kuwa hawakuwa viongozi wa dini ya Kiislamu, bali ni watu waliovaa vazi la kanzu, ambalo kila mtu anaweza kulivaa.


Akizungumza na Amani jana, kiongozi huyo ambaye pia ni Mjumbe wa Baraza la Amani mkoani Dar, alisema siku zote ndege wamoja hutambuana, kama ilivyo kwa maaskofu na wapiga debe, hivyo wao kama mashehe, hawajaona mtu mwenye hadhi ya kuitwa shehe, zaidi ya kuwaona watu waliovalia kanzu na vibalaghashia.


“Hakuna shehe pale, wale ni watu tu wamevaa kanzu na vibalaghashia, siyo kila mvaa kanzu ni shehe, mtu yeyote anaweza kuvaa, kwani kanzu ni vazi kama vazi jingine na ndiyo maana zinauzwa madukani.


“Siku zote mashehe tunatambuana, hata maaskofu, wapiga debe wanatambuana, wale sisi hatuwatambui kama mashehe. “Na ndiyo maana tulitoa tamko kama Baraza Kuu la Waislamu Tanzania (Bakwata) kuwa wale hawakuwa mashehe kutoka Bakwata na wala hawakuwa na baraka za Bakwata,” alisema shehe mkuu huyo.


Mashehe wanaozungumzwa ni wale ambao walienda kanisani katika siku ambayo pia wasanii wa vichekesho, Stanley Yusuph ‘Stan Bakora’ na Musa Kitale, ‘Mkude Simba’ walihudhuria ibada kwenye kanisa hilo.


Tukio hilo lilitokea Machi 26, mwaka huu na kuzua mshangao hata kwa waumini wa kanisa hilo ambao walishindwa kujizuia na kulipuka kwa kelele za ushindi, zilizoambatana na shangwe, miluzi na vifijo.

Kimenukaa..Tundu Lissu Aaanza Kulegeza Kamba kwa Rais Magufuli..Kwa Mara ya Kwanza Amsifia na Kumpongeza..!!!

$
0
0

Mwanasheria wa Chadema na rais wa TLS akiwa anahojiwa na radio Times FM akijibu ni jambo gani ambalo wanaweza kumpongeza rais Magufuli amedai yapo na TLS wameomba mwaliko wa rais ili wakampongeze.

Tundu Lissu amedai rais ametenda mengi na mengine ni mazuri na pia anastahili pole kwa kuwa kazi ya urais ni kazi ngumu, akisema alimuona jana alikuwa amechoka

Pia amewaambia wananchi kuwa wasiipe TLS nguvu kubwa kwakuwa TLS haisimamii mahakama wala haiteui majaji na hivyo sio wategemee kuwa kesi za uonevu , au kucheleweshwa kwa kesi ni jambo ambalo linaweza kutatuliwa na TLS pekee

Imefichuka..Wabunge wa CCM Wapangwa Kumtetea Makonda Bungeni..Mchezo Mzima Utakuwa Hivi..!!!!

$
0
0

Baada ya taarifa ya Kamati ya Maadili, Haki na Madaraka ya Bunge chini ya mtani na kaka yangu Kepteni Mstaafu George Huruma Mkuchika kukabidhiwa kwa Spika, Spika ataiweka taarifa hiyo katika ratiba za shughuli za Bunge ili iwasilishwe na kujadiliwa. Tayari Mkuchika na Kamati yake wameshakamilisha taarifa yao tayari kuikabidhi kwa Spika, Ndugu Job Justino Ndugai.

Taarifa hiyo inatarajiwa kuwasilishwa na kujadiliwa kati ya leo au kesho. Taarifa ya Kamati ya Mkuchika itabeba kilichopatika katika mahojiano na Makonda; maoni na mapendekezo ya Kamati. Makonda (Daudi Albert Bashite) aliitwa kuhojiwa na Bunge kupitia Kamati hiyo kwa kulidharau Bunge kupitia kauli zake za kejeli na kiburi alizozitoa juu ya Bunge na Wabunge.

Katika hali ya 'kudhibiti' kauli na mwenendo wa Wabunge wa CCM kuhusu taarifa hiyo, viongozi wa Wabunge wa CCM wameanza kuwapanga Wabunge wa CCM. Kuwapanga huko kunaratibiwa na Katibu wa Wabunge wa CCM, Ndugu Jason Rweikiza. Rweikiza, kwa mujibu wa taarifa toka Dodoma, anawataka Wabunge kupongeza hatua ya Makonda ya kuomba msamaha kwa barua.

Imeelekezwa kuwa kama Rweikiza na timu yake watakwama kuwapanga Wabunge wa CCM kuhusu taarifa hiyo, basi kutalazimu kuwepo kwa Kikao cha Wabunge wote wa CCM almaarufu kama Party Caucus ili Wabunge waandaliwe na utaratibu wa kuwamulika mjadala utakapoanza uwekwe. Maandalizi ya haraka ya Caucus yatafanyika.


Jacob Steven (JB): Sijabarikiwa Kupata Mtoto Mpaka Sasa, Sijawahi Kuwa na Mchepuko..!!!

$
0
0

Mwigizaji wa bongo movie Jacob Steven JB akihojiwa kwenye kipindi cha kikaangoni amefunguka kuhusu maisha yake na kusema ameoa lakini mpaka sasa hajabarikiwa kupata mtoto lakini ana furaha tele.

Amedai pia ameokoka na hana mchepuko katika maisha yake kwa kuwa anaamini kuwa na wanawake wengi kunakuletea mabalaa katika maisha

Hatarii..Maadui wa Paul Makonda Watofautiana..!!!

$
0
0

Suala LA mkuu Wa mkoa Wa Dar es salaam Paul Makonda limezua sura Mpya baada ya maadui zake wakubwa kutofautiana has a kuhusu uhalali Wa vyeti vyake vya kidato cha NNE. Wiki chache zilizopita adui yke namba moja Mange kimambi aliibuka na kusema Mkuu wa mkoa wa Dar anatmia jina na cheti cha mtu anayejulikana kwa jina la Paul Christian Kagenzi na kuwa alinunua jina hilo baada ya kufeli mtihan Wa kidato cha nne..adui huyo alizidi kusisitiza na kuuaminisha umma kuwa jina halali LA mkuu huyo wa mkoa ni Daud Albert Bashite na ndo jina lake halali alilopewa na wazaz wake ikiwa ni pamoja na kulitumia katika kuitafta elim kabla ya kufel kidato cha NNE. Kutaka kuuaminisha umma Mange alieleza kuwa hilo jina linatumiwa na mtangazaji wa kituo kimojawapo cha redio mjini mkoan Tabora. 

Adui mamba mbili Mchungaji Gwajima ,huyu namuita adui namba mbili ,huyu adui Juma takriban nne zilipita alitumia mathabahu take vibaya kwa kueneza chuki na uongo Wa waumin wake ..adui huyu amekaririwa Mara kadhaa akisema mkuu wa mkoa wa Dsm amefoji vyeti na vyeti anavyotumia pamoja na jina ni la mtu aitwaye Paul kagezi Muyenje na kuzidi kukusitiza kuwa yeye anaitwa Daudi Albert Bashite. Bila kujali kuwa alikuwa anatenda dhambi akaendelea kusema kuwa hata namba ya Dada yake na hyo Paul anayo ikiwa ni pamoja na vyeti vya Bashite..

Adui namba tatu Balile (jamhuhuri) huyu nampa hiyo namba kwa kuwa katika gazeti lake la tarehe 21/22 march alieleza zaid ya kurasa Nana kuhusu habari ya Bashite lakin cha kushangaza alitofautiana na maadui wengine kwa kufika Pamba Sekondari na kutokuta jina la Daud Albert Bashite tofuti na adui wa Pili alivyokuwa ametuaminisha kwa kuja na matokeo feki kutoka Pamba.
Lakini pia adui huyu alipomhoji Paul christian alikiri kuwa hana dada na yey alipata division three ya point 25 kama tulivyokuwa tumeaminishwa na mchingaji Gwajima.

Adui wa NNE Mh. Nyepesi huyu namuita adui maana naye amelivalia njuga suala la bashite ikiwa ni pamoja na kutumia mda mwingi kufuatilia suala hilo kuliko suala la wapiga kura wake walikatiwa maji toka juzi. Huyu naye kaenda Nectar hakukuta jina la Bashite wa Paul Makonda.
Tumuamin nan??nawasilisha

Ripoti: Tanzania Yaongoza Afrika kwa Kupokea Wageni Wengi Zaidi kwa Njia ya Anga..!!!

$
0
0

Tanzania imechangia asilimia 19.3 ya jumla ya wageni wa kimataifa kupitia anga (international air arrivals) ukilinganisha na asilimia 18.2 ya Kenya, asilimia 17.2 Misri na asilimia 12.1 ya Afrika Kusini katika kipindi cha kuanzia September 2016 hadi January 2017.

Takwimu hizi ni kwa mujibu wa ripoti mpya ya shirika la ufuatiliaji wa masuala usafiri wa ndege, ForwardKeys ambayo hulinganisha ukataji tiketi za ndege zaidi ya milioni 16 kila siku ili kuiweka Afrika kwenye ramani ya utalii duniani.

Kwa jumla, Afrika Mashariki ina asimilia 16.4 ya ufikaji wa wageni kwa njia ya anga. Na kwa ujumla pia, kuna ongezeko la asilimia 10.3 ya ufikaji wageni Afrika

Kimenukaa Clouds Media..Mfanyakazi Asimamishwa Clouds kwa Kutangaza Habari ya Paul Makonda, TEF Yaitaka Mitandao Iunge Mkono..!!!

$
0
0

Bodi ya Jukwaa la Wahariri Tanzania (TEF) imekutana jijini Dar es Salaam leo Machi 30, 2017. Pamoja na mambo mengine imejadili mwenendo wa vyombo vya habari ndani ya wiki moja tangu tulipotoa msimamo wa kutotangaza habari za Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam, Paul Makonda.

Bodi imepitia habari za Mkuu wa Mkoa zilizochapishwa tangu ulipotolewa msimamo wa kumfungia. Bodi inapenda kawapongeza wahariri wote waliotekeleza kwa usahihi msimamo wa kutochapisha habari za Mkuu wa Mkoa kwa wiki nzima.

Bodi inapenda kusisitiza kuwa wahariri katika vyombo vya habari; magazeti, radio na televisheni waendelee na msimamo wa kususia habari za Mkuu wa Mkoa, Paul Makonda, hadi atakapotimiza takwa la kuomba radhi kwa tukio la kuvamia kituo cha Clouds.

Bodi inatoa wito kwa viongozi wa mitandao ya kijamii kuunga msimamo huu. Bodi inapenda kufafanua kuwa Mhe. Makonda amewekewa vikwazo Maalum (Smart Sanction) kwa mikutano atakayoiandaa au matukio atakayoyaongoza habari zake hatutazichapisha.

Bodi inakipongeza Kituo cha Clouds kwa kumsimamisha kazi mtangazaji aliyekiuka msimamo wa kutotangaza habari za Makonda. Bodi pia imewasiliana na Uongozi wa UTPC na kukubaliana kwamba msimamo huu uendelee.

Theophil Makunga,
Mwenyekiti TEF
Imetolewa Leo,
Machi 30, 2017

Hivi Hapa...Vituko vya Maiti Zikiwa Mochwari..!!!

$
0
0

Jamani jamani jamani pale mahali paoneni hivi hivi, pana vibweka pale mwanzo mwisho, na Kama kuna viumbe wana visa vibaya marehemu wanaongoza
Kama mtu alikuwa malaya kwenye uhai wake hata akifa maiti yake huwa na pozi zile zile.

Mtu katili hufa na ukatili wake na hata pale mochwari maiti yake huwa na dalili zote.... Wabishi matapeli wachawi nk hubaki na hizi tabia hata pale ndani
Huwezi amini maiti uliyokuwa umeiweka vizuri tu ukaikuta imechanua miguu.

  ,ama maiti nyingine kuikuta tu imegeuka yenyewe ...! Unakaa na kujiuliza na mshangao mkubwa hii imegeuka saa ngapi? Ama imegeuzwa ?   na nani? 

Mbaya zaidi ni zile zenye tabia ya kukonyeza.... Yani live kabisa ukiangalia unaona marehemu anakukonyeza.... Walevi mateja mabosi nk wote wapo kwenye kile chumba.

Na kuna wakati mochwari attendant hujua kabisa kwamba Leo mochwari patafurika ama mzigo utakuwa mdogo.... Ni uzoefu tu wa kazi.
Viewing all 104756 articles
Browse latest View live




Latest Images