Quantcast
Channel: UDAKU SPECIAL
Viewing all 104432 articles
Browse latest View live

Kimenukaa..Mengi Aichana Serikali ya Magufuli..Afunguka Mazito Jinsi Mambo Yanavyotakiwa Kuwa...!!!


Jamaa Aliyekufa Miaka 14 Iliyopita Afufuka na Kusimulia Maisha Aliyokutana Nayo Alipokuwa..!!!

0
0

Anaitwa Hassan Mga kijana kutokea Mbeya, anadai mwaka 2003akiwa darasa la tatu alichukuliwa msukule na baada ya kuumwa vikali kichwa na kupelekwa hospitali na mwishowe 'kufa' kimsukule

Anadai uliyechukuliwa msukule huwa anaona yanavyofanyika mazishi yake lakini wao hawaomuoni na hawezi kuongea nao

Alidai walichukuliwa na kwenda kutumikishwa bandarini kupakua makontena mizigo, chakula walichokuwa wakila ilikuwa ni nyama mbichi, pumba na unga uliokorogwa...walikuwa hawanywi maji ila damu

Ila kuna siku alilishwa chakula ambacho hawaruhusiwi kula huko(ubwabwa anadai) ndipo akaibuka dunia hii sehemu ambayo haifahamu na watu kumkimbia na alipata wakati mgumu watukumuelewa...ilaalifanyiwa maombi kanisani ndipo akaweza kuongea na kurudia kawaida

Haya Ndio Maajabu ya Mwenge wa Uhuru kwa Mwaka Huu..!!!!

0
0

Mbio za Mwenge wa Uhuru kwa mwaka 2017 zimezinduliwa rasmi leo katika uwanja wa Kumbukumbu Mjini Mpanda mkoani Katavi na unatarajiwa kuzunguka katika mikoa yote 31, ukipita kwenye halmashauri 195 kwa muda wa siku 195.

Katika sherehe hizo za uzinduzi, kiongozi wa mbio hizo kwa mwaka huu pia ametangazwa rasmi, ambapo atakuwa ni Amour Amad Amour kutoka mkoa wa Kaskazini Unguja visiwani Zanzibar.

Kiongozi huyo atasaidiana na wenzake watano katika kukimbiza mwenge huo ambao ni pamoja na Bahati Mwaniguta Lugodisha (Geita), Bi Fatima Yunus Hassan (Kusini Pemba), Fredrick Joseph (Singida), Salome Obadia Mwakitalima (Katavi) na Shukran Islam Msumi (Mjini Magharibi).

Kauli mbiu ya mbio hizo kwa mwaka huu inasema "SHIRIKI KUKUZA UCHUMI WA VIWANDA KWA MAENDELEO YA NCHI YETU'

Mgeni rasmi katika uzinduzi huo alikuwa ni makamu wa pili wa Rais wa Serikali ya Mapinduzi Zanzibar Balozi Seif Ali Idd kwa niaba ya Rais wa serikali hiyo Dkt. Ali Mohamed Shein, ambapo katika ujumbe wake amesisitiza umuhimu wa watanzania wote kuweka nguvu zao katika kujenga taifa la viwanda

Amesema hadi sasa tangu serikali yake iingie madarakani kwa muhula wa pili tayari viwanda vitatu vya watu binafsi vimekwishajengwa visiwani Zanzibar

Balozi Seif amesema mbali na kaulimbiu ya mwaka huu kusisitiza umuhimu wa viwanda, pia mbio hizo zitakuwa zikieneza ujumbe kuhusu mapambano dhidi ya Malira, UKIMWI, Dawa za Kulevya pamoja na rushwa.

Mbio hizo zimeanzia katika wilaya ya Mpanda, na kilele chake kitakuwa ni Oktoba 14 katika mkoa wa Mjini Magharibi.

Kumbukumbu zinaonesha tukio kama hili la uzinduzi tangu mwaka 2011 lilikuwa kama ifuatavyo

2011 Butiama (Mgani rasmi akiwa Mohamed Ghalib Bilal)
2012 Mbeya (Mgeni rasmi akiwa Mizengo Pinda)
2013 Pemba (Mgeni rasmi akiwa Dkt Ali Mohamed Shein)
2014 Kagera (Mgani rasmi akiwa Mohamed Ghalib Bilal)
2015 Ruvuma (Mgeni rasmi akiwa Dkt Ali Mohamed Shein)
2016 Morogoro (Mgeni rasmi akiwa Samia Suluhu Hassan)

OFM Wamvaa Masogange ‘Kininja’, Siri Nzito Yafichuka Kuhusu Maisha Yake..!!!!

0
0

KUFUATIA madai kuwa, mrembo mwenye figa matata Bongo, Agnes Gerald ‘Masogange’ anaishi na kigogo mmoja kwenye mjengo wa kifahari kule Makongo Juu jijini Dar na yale madai kuwa, anatumia madawa ya kulevya, kikosi kazi cha Operesheni Fichua Maovu cha Global (OFM), kiliamua kumvaa kininja nyumbani kwake.

MADAI KWANZA

Madai ya mwanzo yaliyotua kwenye dawati la IJUMAA yalikuwa ni kwamba, eti modo huyo hufika nyumbani hapo mida ya usiku akiwa na mwanaume huyo ambaye hakuweza kufahamika kama ni yule Dick Sound aliyetajwa kutoka naye awali au ni mwingine. Aidha, kutokana na mrembo huyo kutopatikana kirahisi kwenye simu yake ya mkononi, gazeti hili likiwa na lengo pia la kutaka kuonana naye ana kwa ana kuzungumzia mambo mbalimbali ya kimaisha sambamba na mwenendo wa kesi yake ya madawa ya kulevya, liliamua kumfuata nyumbani kwake.

DAY 1 OFM KAZINI

Jumatatu, Machi 27, majira ya saa 12 jioni, OFM walifika nyumbani kwa Masogange na kugonga geti bila kufunguliwa hivyo wakakaa nje hadi saa 3 usiku lakini hakuonekana mtu yeyote kuingia wala kutoka.

DAY 2 OFM KAZINI

Mapema alfajiri ya siku iliyofuata Machi 28, makachero hao wa OFM walidamkia nyumbani hapo ambapo kuanzia saa 12 mpaka saa 1 usiku hakuna mtu aliyetoka wala kuingia.

OFM WAZAMA NDANI

Baada ya kuona kimya, OFM waliamua kusogea mpaka getini na kugonga lakini kwa muda wa dakika kumi walizogonga, hawakuweza kufunguliwa ndipo walipoamua kuingia ‘kininja’ kupitia kigeti kidogo ambacho hakikuwa kimefungwa.

Baada ya kuingia ndani na kubisha mlango wa nyumba anayoishi Masogange, alitokea msichana aliyejitambulisha kama mdogo wake na baada ya salamu mazungumzo yalikuwa hivi; OFM: Tuna shida na Masogange, tunataka kuongea naye mambo ya kisanii.

Binti: Mh! Dada hayupo, ila ngoja nizungumze na dada yake halafu nawapa jibu… (anaingia ndani kisha muda mfupi anarudi na kuwakaribisha OFM ndani).

Muda mfupi baada ya OFM kuingia ndani, anakuja mwanadada mrembo mwenye figa kama ya Masogange na kujitambulisha kuwa ni dada yake na kuwauliza OFM walikuwa na shida gani.

OFM: (kwa kuzuga) Sisi ni wasanii, tumekuja hapa kwa ajili ya kazi, tunayo ngoma yetu ambayo tunataka Masogange ashiriki kwenye video.

DADA MTU:  Kwanza nani kawadairekti kuwa Masogange anaishi hapa?

OFM: Sisi ni wakazi wa maeneo haya.

DADA MTU: Oke, sasa ipo hivi Masogange hayupo, lakini pia hashiriki tena kwenye video, kwani nyie mmemuona mara ya mwisho lini? Si muda umepita? Ndiyo hivyo sasa tafuteni mtu mwingine.

OFM: Kwa nini hafanyi muziki?

DADA MTU: Hilo ni suala binafsi siwezi kulijibu, nafikiri tumemaliza, naomba muondoke.

Wakati mazungumzo hayo yakiendelea, OFM walisikia sauti ya watu kutokea chumba kingine, hali iliyowafanya wahisi ni Masogange na mtu mwingine. Hata hivyo, kufuatia dada mtu huyo kuamuru OFM waondoke, zilikuwa zimebainika siri nzito za maisha yake ikiwa ni pamoja na kuishi kifahari kutokana na mandhari ya sebuleni ilivyo.

Pili, mbali na dada yake wapo wadada wawili wa kazi na kubwa zaidi ni kwamba, ule mjumba unaotajwa kuwa kapangishiwa, haishi peke yake bali kuna wapangaji wengine hivyo wale wanaodhani anaishi kwenye bonge la mjumba, mawazo hayo yafutike.

Simba Yaangukia Pua Mbele ya Kagera Sugar...Yanga Yaendelea Kutamba

0
0


SIMBA SC wameshindwa kurejea kileleni mwa Ligi Kuu ya Vodacom Tanzania Bara baada ya kuchapwa mabao 2-1 na wenyeji Kagera Sugar Uwanja wa Kaitaba, Bukoba jioni ya leo.


Ushindi huo unaifanya Simba SC ibaki na pointi zake 55 baada ya kucheza mechi 25 na kuwaacha, mabingwa watetezi Yanga SC wakiendelea kuongoza Ligi Kuu kwa pointi moja zaidi na Kagera Sugar inaendelea kukaa nafasi ya tatu kwa pointi zake za mechi 25.


Katika mchezo huo uliochezeshwa Jimmy Fanuel, aliyesaidiwa na Joseph Masija wa Mwanza na 

Geoffrey Msakila wa Geita,hadi mapumziko Kagera Sugar walikuwa mbele kwa bao 1-0.


Bao hilo lilifungwa na mshambuliaji chipukizi wa kimataifa wa Tanzania, Mbaraka Yussuf Abeid dakika ya 27 kwa shuti kali la umbali wa mita 22 baada ya pasi ya mchezaji mwenzake wa zamani wan Simba B, Edward Christopher.


Simba wakaamua kufunguka baada ya bao hilo na kuanza kupeleka mashambulizi ya moja kwa moja langoni mwa Kagera Sugar.


Na Laudit Mavugo, Said Ndemla na Abdi Banda wote wakapoteza nafasi nzuri za kufunga wakiwa wamebaki na kipa Juma Kaseja.


Nafasi ambayo wataijutia zaidi Simba SC ni ya beki Banda dakika ya 43 ambaye alifanikiwa kuipata pasi nzuri ya beki wa kushoto Mohammed Hussein ‘Tshabalala’ na kuwatoka mabeki wawili wa Kagera Sugar, lakini shuti lake dhaifu likadakwa na Kaseja aliyekuwa hatua mbili tu kutoka kwake.


Kipindi cha pili, kila timu ilifanikiwa kupata bao moja, Kagera Sugar wakianza kupitia kwa Edward Christopher aliyemalizia pasi ya Sulemani Mangoma dakika ya 47 kabla ya Muzamil Yassin kuifungia Simba bao la kufutia machozi dakika ya 67 akimalizia pasi ya Mghana, James Kotei. 


Baada ya hapo, timu hizo zikaanza kushambuliana kwa zamu na sifa zimuendee kipa mzoefu, Juma Kaseja aliyeokoa michomo kadhaa ya hatari ya Simba.


Kikosi cha Kagera Sugar kilikuwa; Juma Kaseja, Godfrey Taita, Mwaita Gereza, Juma Shemvuni, Mohamed Fakhi, George Kavila, Suleiman Mangoma, Ame Ally ‘Zungu’/Ally Ramadhani, Edward Christopher/Themi Felix, Mbaraka Yusuph na Japhet Makalai/Anthony Matogolo.


Simba leo kipo hivi; Simba SC; Daniel Agyei, Muzamil Yassin, Mohammed Hussein ‘Tshabalala’, Abdi Banda, Juuko Murshid, Jonas Mkude, Shiza Kichuya/Mwinyi Kazimoto, Said Ndemla/Juma Luizio, Laudit Mavuo, Ibrahim Hajib/Mohammed Ibrahim na James Kotei.

Fahamu Faida 10 za Kufanya Mapenzi Kipindi cha Ujauzito.

0
0

kuna watu wamekua wakiuliza mara kwa mara kama inaruhusiwa kushiriki tendo la ndoa mpaka umri gani wa mimba au ni sahihi kufanya tendo la ndoa kipindi cha ujauzito? maswali yalikua mengi sana hivyo leo nimeamua nijibu maswali hayo na makala hii.

mwanamke akiwa na mimba anaruhusiwa kushiriki tendo la ndoa hata kama anatarajia kuzaa kesho yake, hakuna tatizo lolote linalomzuia kufanya hivyo, baadhi ya wanawake wamekua wazito sana kufanya hivyo kwa kua na sababu mbalimbali za kujitetea bila kujua kwamba wanazikosa faida hizi ambazo ni muhumu kiafya.faida zenyewe ni kama zifuatazo

husaidia uchungu mzuri na kupona mapema; kufika kileleni wakati wa tendo la ndoa huambatana na kubana kwa misuli ya nyonga hii husaidia kuweka imara misuli ya nyonga ambayo ni muhimu sana wakati wa kusukuma mtoto na baada ya kuzaa kwani misuli hii ikiwa legevu mwanamke huweza kushindwa kuzaa kwa njia ya kawaida na hata baada ya kuzaa huweza kushindwa kuzuia mkojo usitoke wenyewe au kuvuja damu kwa muda mrefu.

hupunguza kwenda ovyo kukojoa au kujikojolea; wakati wa ujauzito mtoto anapozidi kua mkubwa anazidi kukandamiza kibovu cha mkojo, hii humfanya mama aende chooni kukojoa mara kwa mara na wakati mwingine hata akipiga chafya au kukohoa basi mkojo unaweza kutoka wenyewe. tendo la ndoa huibana misuli ya nyonga na kuzuia hali hii.

huzuia uwezekano wa kupata kifafa cha mimba; tafiti zinaonyesha kwamba aina ya protini inayopatikana kwenye mbegu za mwanaume huongeza kinga ya mwili na kuzuia uwezekano wa kupata kifafa cha mimba ambacho kinaua wanawake wengi sana.

hutibu tatizo la kufika kileleni kwa shida; kipindi cha ujauzito chuchu za mwanamke na kinembe chake huvimba na kuongezeka hisia mara dufu huku kiwango cha homoni za oestrogen kikiwa juu sana, hii humfanya kufika kileleni kirahisi sana kuliko mwanzoni.

huwapa uwezo wa kujiamini; kipindi cha ujauzito mwanamke hua anapata hofu sana na kutojiamini na mwili wake, hua na wasiwasi kwamba mwili wake unaharibika hivyo kitendo cha mwanaume wake kuendelea kushiriki naye tendo la ndoa humpa kujiamini kwamba mwili wake bado uko kwenye hali nzuri na anapendwa.

hupunguza msongo wa mawazo; kipindi cha ujauzito wanawake wengi huwaza sana kuhusu kesho yao...je swala la uchumi litakuaje? mwili wangu utakuaje? je ntapata jinsia nayotegemea? na kadhalika.. tendo la ndoa hutoa homoni ya upendo kwa jina la oxytocin, homoni hii hupunguza mawazo na kumpa amani mjamzito.

huongeza upendo na mshikamano  kati ya wapenzi; katika hali ya kawaida wanandoa wakikwazana wanaweza wakapatana kwa kushiriki tendo la ndoa tu, amani na upendo kipindi hiki ni muhimu sana kwani kuna mtoto anakuja ambaye anatakiwa kuzaliwa huku baba na mama wakiwa wanapatana.

hukuandaa na uchungu; ukishiriki ndoa wakati wa tarehe zilizokadiriwa zimefika unapata homoni moja kutoka kwenye mbegu za  mwanaume kwa jina la prostglandin, homoni hii huivisha mlango wa uzazi na kuanza kufunguka taratibu kujiandaa na uchungu.

hutibu tatizo la kukosa usingizi; wanawake wengi wajawazito hua na dalili mbalimbali za maumivu na kuumwa sehemu tofauti za mwili na msongo wa mawazo, hii huweza kuwakosesha usingizi kabisa..tendo la ndoa huweza kuwapa usingizi mzuri.

hupunguza presha ya damu; kipindi cha tendo la ndoa presha ya damu hushuka kwenye kiwango kizuri sana, hii ni muhimu sana kwa wanawake wenye hatari ya kupata kifafa cha mimba kama wanene sana, wenye kisukari au wenye historia za ugonjwa wa presha kwenye koo zao.

mwisho; hakikisha unatumia staili za tendo la ndoa ambazo hazimuumizi mtoto na mama yaani hakikisha haulilalii tumbo hasa mimba ikiwa kubwa, kuna staili muhimu kipindi hiki kama kuangalia upande mmoja, mwanamke kuja juu, au mwanamke kuinama

Mambo Matano ya Kutisha Yanayotokea Kwenye Uume Kadri Umri Wako Unavyozidi Kuongezeka..!!!

0
0

umri wa binadamu unabadilisha kila kitu mwilini, mifumo yote ya mwili hupungua uwezo wa kufanya kazi pale mtu anapoanza kukaribia miaka hamsini, hii huwafanya watu wa umri kushindwa kujikubali na kupambana sana kurudi ujanani lakini sote tunajua uzee hauzuiliki, wakati ukifika lazima yakutokea yatokee..mfumo wa kuona, moyo, upumuaji, figo, mfumo wa chakula, ngozi na kadhalika vyote huishiwa nguvu.

uume wa mwanaume huanza kazi rasmi anavyofikisha miaka 14, hapo hufanya kazi kwa nguvu zote lakini miaka ya mbele baadae mabadiliko huanza kuonekana kama ifuatavyo.

kupungua ukubwa wa uume moja kwa moja; hali hii husababishwa na kubadilika kwa seli nene ambazo zinapatikana kwenye uume na kubadilishwa nyuzi nyuzi za nyama kitaalama kama collagen fibres ambazo ni nyembamba sana lakini hali hii huchangiwa pia na mafuta yanayoziba uume usipate damu ya kutosha, kupungua kiasi cha hormone ya mwanaume ya testosterone na hali hii hufanywa kua mbaya zaidi na uotaji wa kitambi ambao huficha uume ndani kabisa

kupinda kwa uume; shughuli za kushiriki ngono na mazoezi mbalimbali ambayo huumiza uume bila kujijua huleta makovu mengi ndani kwa ndani kwenye uume ambapo baadae uume ukishakua na makovu mengi hupinda kuelekea chini hata wakati ukiwa umesimama, yaani kama uume wako ujanani ulikua kama mshale sasa utakua kama upinde.

kuishiwa nguvu za kiume; tatizo hili linaathiri zaidi ya wanaume milioni 30 dunia nzima, katika hali ya ukuaji hali hii husababishwa na kupungua kwa kiasi cha damu ambacho kinaingia kwenye uume kila siku ukihitaji kuusimamisha sababu ya kuziba kwa mishipa ya damu na mafuta kama nilivyoeleza hapo juu, usitegemee nguvu zako za kiume ulizokua nazo ukiwa na miaka 18 utakuja kuzipata tena kwenye miaka 40.

saratani za sehemu hizo za siri; saratani mbalimbali kama saratani ya uume hasa kwa watu ambao hawajatailiwa, saratani ya korodani na saratani ya tezi dume. utafiti mpya unaonyesha kutoshiriki ngono kwa wanaume mara kwa mara kunaongeza nafasi ya kupata saratani ya tezi dume.baada ya miaka 30 ni vizuri kupima angalau mara moja kwa mwaka kuangalia kama kuna kansa imeanza.

kuchelewa kufika kileleni; mishipa ya fahamu ambayo inatoa taarifa kutoka kwenye uume kwenda kwenye ubongo huishiwa nguvu umri unavyozidi kwenda na hii humfanya muhanga kuchukua muda mrefu sana kufika kileleni swala ambalo linaweza kua baya au zuri kulingana na muhusika na hata akifika kileleni hutoa mbegu kidogo sana.

suluhisho; kuna mambo unaweza kufanya kuchelewesha au kupunguza kasi ya madhara haya ya ukuaji kwa kumeza vichochoe vya kutengeneza hormone ya testosterone mwilini mara kwa mara ambavyo huongeza nguvu za kiume,stamina, mbegu na kupunguza kasi yaa uume kua mwembamba, 
kufanya mazoezi na kula vizuri kuepusha kitambi na kushiriki mazoezi ya uume ambayo kwa watu wanaozidisha miaka 30 ni muhimu kua sehemu ya maisha yao ili kubaki na uume bora wenye afya

Yafahamu Madhara 10 ya Kutisha Yanayotokana na Ulaji Mkubwa wa Chumvi Kwenye Chakula

0
0

tafiti zilizofanywa na jarida la new england journal of medicine nchini uingereza limegundua kwamba zaidi ya watu milioni moja na laki sita wanauawa na na ulaji wa chumvi kila mwaka, kifo ni hatua ya mwisho ya madhara ya chumvi lakini kuna madhara mengi sana yasababishwao na chumvi kabla ya kifo.

kitaalamu chumvi ni kompaundi au mchanganyiko wa element za sodium chloride, kemikali hii hutumika kuhifadhi chakula na kuleta ladha ya chakula, kemikali hii huweka kiwango cha maji mwilini sawa na kusaidia utumaji wa taarifa kwenye mishipa ya fahamu, husaidia kuhifadhi maji mwilini, ni muhimu kwenye damu ya mwili,kutengeneza tindikali kwa ajili ya mmengenyo wa chakula tumboni, hata dripi za maji tunazopewa mahospitalini hua zina chumvi.

maisha ya kisasa na vyakula viulivyopo vinawafanya watu kula chumvi nyingi sana kuliko zamani, hii husababisha madhara makubwa ambayo hayatibiki kirahisi.

kiafya mtu anatakiwa ale chakula chenye chumvi inayosikika kwa mbali sana na asiongeze chumvi chakula kinapokua mezani, hii ni sawa na gramu 1.5 mpaka 2.3 kwa siku, hii ni sawa na kijiko kimoja cha chakula kwa siku nzima.

ulaji mkubwa wa chumvi kwa wakati mmoja husababisha kuishiwa maji kwa seli, hii huleta kuchanganyikiwa, degedege, kupoteza fahamu na kifo lakini pia uwepo wa chumvi kidogo sana kwenye damu husababisha kuvimba kwa seli, kuchanganyikiwa,kupoteza fahamu na kufa..hii hutokana na unywaji mkubwa wa maji kupitiliza kiasi kwa wakati mmoja.

kimsingi vyakula vingi tunavyokula vina chumvi ya kutosha ambayo inatosha kabisa kuendesha mwili wetu bila kuongeza chumvi nyingine ya ziada, vyakula hivyo ni kama vitunguu,malimao,maji ya kunywa,viazi,ngano,nyanya,maboga,caroti, spinachi, kabechi,mapera, zabibu,epo,karanga,mayai, maziwa na vingine vingi

yafuatayo ni madhara ya ulaji wa chumvi nyingi ambayo yanaweza kua ya muda mrefu au ya muda mfupi.

yafuatayo ni madhara ya muda mrefu wa kula chumvi nyingi kwenye chakula...

presha ya damu; chumvi ina tabia ya kuzuia maji kutoka nje ya mwili kupitia mkojo, lakini pia kuna ushahidi kwamba kupunguza ulaji wa chumvi kwa wagonjwa wa presha hupunguza presha kwa wagonjwa wa presha.

kansa ya tumbo; utafiti umeonyesha kwamba nchi ambazo kuna ulaji mkibwa sana wa chumvi kama japani kuna wagonjwa wengi sana wa kansa ya tumbo la chakula ukilinganisha na nchi ambazo hazina ulaji mkubwa wa chumvi kama uingereza.

ugonjwa wa moyo; chumvi husababisha kuvimba kwa moyo na kuufanya kua mkubwa kitaalamu kama left ventricular hypertrophy, hii husababisha moyo kushindwa kusukuma damu kama unavyotakiwa kufanya kazi.

magonjwa ya figo; kupanda kwa presha ya damu husukuma damu nyingi sana kwenye mishipa ya damu, hii huharibu figo na kuifanya kushindwa kutoa maji mwilini lakini pia viungo muhimu kama macho na mishipa ya damu huharibika.

addiction; ulaji mkubwa wa chumvi humfanya mlaji kuendelea kupenda vyakula vyenye chumvi nyingi sana na kushindwa kabisa kuvumilia kula vyakula vyenye chumvi kidogo...hii hizidi kuathiri mwili na kuusababishia matatizo makubwa zaidi.

kiharusi; huu ni ugonjwa wa kupooza unaosababishwa na kuziba kwa mishipa ya damu ya kwenye ubongo kutokana na mafuta au kuvujia kwa damu, kwa ulaji wa chumvi nyingi huongeza presha ya damu na kupasua mishipa midogo ya kichwa na kuleta kiharusi.

kuongezeka uzito; kama nilivyosema hapo mwanzo kwamba chumvi huzuia maji kutoka nje ya mwili, hii huongeza uzito wa mwili na kumfanya mtu kujisikia amejaa tumbo muda mwingi, kumbuka lita moja ya maji sawasawa na kilo moja ya uzito.

kupungua kwa uwezo wa mishipa ya fahamu; katika watu wenye umri mkubwa chumvi inazidi kupunguza uwezo wao wa kufanya shughuli mbalimbali na kujikuta wakitetemeka na kushindwa kubeba hata kikombe kimoja cha chai.

magonjwa ya mifupa; mwili wa binadamu unapoteza kiwango cha calcium mwilini pale mtu anapozidi kutumia chumvi zaidi, hii huweza kusababisha mifupa kua milaini na kuvunjika kirahisi pale inapoangukua kidogo tu.

mwili kushindwa kutoa mabaki mwilini; chumvi nyingi mwilini huingilia mfumo wa mwili kuondoa mabaki ya uchafu mwilini, moja ya mabaki yanayobaki ndani ya mwili ni uric acid ambayo inaweza kusababishwa ugonjwa wa maumivu makali ya jointi kitaalamu kama gauti.

suluhisho ni nini? punguza sana kiasi cha chumvi kwenye mla wako na baada ya muda utazoea, kwa wagonjwa wa presha ambao wanatakiwa wale chumvi kidogo zaidi kuna chumvi maalumu kwa watu hao ambazo zinapatikana mijini, chumvi hizi zina kiwango kidogo sana cha sodium hivyo presha zao huweza kushuka

Sumaye: Wananchi Wana Haki ya Kumkosoa Rais

0
0
WANANCHI wana haki ya kumsema au kumkosoa Rais na serikali iliyopo madarakani, kwa sababu nafasi walizonazo viongozi hao ni mali ya wananchi wenyewe.

Waziri Mkuu Mstaafu na Mwenyekiti wa Kanda ya Pwani wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo  (Chadema), Frederick Sumaye, alisema hayo jana alipozungumza kwenye Kongamano la Vijana wa Chadema (Bavicha) lililofanyika mkoani Geita.

Sumaye alisema katika mfumo wa demokrasia, serikali huwekwa madarakani na wapiga kura kwa kutekeleza matakwa yao kwa kufuata katiba, sheria za nchi, taratibu na hata desturi.

“Hao walioiweka serikali madarakani (wananchi) ndio wakubwa na wana haki ya kuiuliza serikali yao, Rais wao na mwingine yeyote mwenye madaraka. Baadhi yao wana haki ya kutofautiana kimawazo na viongozi wao walioko madarakani ikiwa ni pamoja na Rais,” alisema.

Alisema kwa msingi huo kutoa maoni yaliyotofautiana na alichokisema kiongozi wa serikali akiwamo Rais mwenyewe si usaliti, uhaini, uchochezi wala kukosa adabu.

“Kuna watakaomsifia sana, kuna watakaotoa ushauri wa tofauti na kuna watakaopinga na kuwa na msimamo tofauti na Rais na serikali yake, makundi yote matatu ni sahihi, hakuna msaliti wala mchochezi… ni vema yawepo kwa afya ya demokrasia.

“Kama wewe ni kiongozi na hutaki kusikia yale yaliyo kinyume na msimamo wako basi usipende pia kuyasikia na yale yanayokusifia sana.

“Leo  vyama vya siasa vimezuia kufanya mikutano ya hadhara ili viwajulishe watu wavyotaka kuwajulisha. Bunge ambalo ndiyo hufanya kazi kwa niaba ya wananchi shughuli zao huzionyeshwi mubashara kama huko nyuma,” alisema

Kumekuchaaa..Makamu wa Rais wa TLS Akamatwa na Polisi Shinyanga..!!!!

0
0

Makamu wa Rais a chama cha wanasheria Tanganyika (TLS), Wakili Godwin Ngwilimi amekamatwa na polisi huko mkoani Shinyanga na anashikiliwa katika kituo kikuu cha polisi mkoani humo.

Taarifa iliyotolewa na Rais wa TLS Mhe.Tundu Lissu ni kwamba Ngwilimi akiwa katika gari yake alisimamishwa na askari aliyekua kavaa kiraia, akitaka kukagua gari yake.

Ngwilimi alimtaka Askari huyo ajitambulishe kwanza kwa kutoa kitambulisho cha kazi kabla ya upekuzi. Lakini badala ya kujitambulisha alimzuia Ngwilimi na kumuelekeza kituo kikuu cha polisi Shinyanga ambapo anashikiliwa hadi sasa.

Tanzania Kuweka Rekodi ya Dunia kwa Kugundua Dawa ya Kutibu Ugonjwa Tezi Dume...!!!!

0
0

TANZANIA iko kwenye hatua za kuridhisha katika utafiti wa miti maalumu inayoaminika itakuwa chanzo cha dawa maalumu ya kuzuia na kutibu maradhi sugu ya tezi dume pamoja na saratani ya kibofu, matatizo yanayowasibu wanaume wengi duniani.

Taasisi ya Sayansi na Teknolojia ya Nelson Mandela iliyopo eneo la Tengeru wilayani Meru mkoani hapa, inafanyia utafiti mti mwekundu wa asili ujulikanao kama ‘kiburabura,’ unaopatikana katika msitu wa Magamba wilayani Lushoto mkoani Tanga.

Ingawa katika hali ya kawaida utomvu wa mti huo wa kiburabura (unaojulikana kisayansi kama Prunus Africana) unadaiwa kuwa ni sumu, lakini wanasayansi kutoka Chuo Kikuu cha Sayansi na Teknolojia cha Nelson Mandela wanasema hilo hasa ndilo litakuwa chimbuko la tiba ya uhakika kwa matatizo ya tezi dume, saratani ya kibofu na magonjwa mengine ya viungo vya uzazi.

Makamu Mkuu wa Taasisi ya Nelson Mandela, Dk Mussa Chacha alisema mjini hapa kuwa, utafiti huo wa miti hiyo ya asili kwa ajili ya tiba, ulianza miezi sita iliyopita na kwamba upo katika hatua nzuri, ingawa hakusema kuwa watakamilisha lini mradi huo ili kuifanya Tanzania kuingia kwenye historia ya dunia kama wavumbuzi wa tiba ya maradhi hayo yanayowasumbua wanaume wengi duniani na hata kusababisha vifo.

Alikuwa akitoa maelezo ya chuo hicho cha Nelson Mandela kwa Waziri wa Elimu, Sayansi, Teknolojia na Mafunzo ya Ufundi, Profesa Joyce Ndalichako aliyekuwa anazitembelea taasisi kadhaa za sayansi na teknolojia mkoani hapa, kikiwemo Chuo cha Nelson Mandela (NM-AIST) na Tume ya Mionzi (TAEC).

“Kutokana na uharibifu wa mazingira na miti kukatwa hovyo, hivi sasa mti huu wa kiburabura umeanza kutoweka nchini, lakini kuna baadhi ya mimea hii ambayo inapatikana katika msitu wa Magamba wilayani Lushoto na tayari wenyeji wa eneo hilo wanakiri kutumia magamba ya mti huo kwa ajili ya tiba za malaria na matatizo ya viungo vya uzazi,” alisema mkufunzi huyo.

Zaidi ya wanaume 30,000 hufa kila mwaka kutokana na matatizo ya saratani ya kibofu. Ugonjwa huu mara nyingi huwapata watu wazima kuanzia umri wa miaka 45 na kuendelea.

Sasa wasomi wa Tanzania wako mbioni kugundua dawa ya moja kwa moja. Saratani ya tezi dume inashika nafasi ya tatu kwa kusababisha vifo kwa wanaume duniani.

Pia ni chanzo kikuu cha vifo kwa wanaume wenye umri wa miaka 70 na kuendelea.

Tafiti za Chama cha Saratani cha Marekani (ACS) na cha Afrika Kusini (CANSA) zimebaini kuwa, mwanamume mmoja kati ya sita hupata saratani ya tezi dume katika uhai wake.

Kutokana na takwimu za mwaka 2010 za dunia nzima, malaria iliua watu 500,000, kifua kikuu watu milioni 2.1, Ukimwi watu milioni 1.8 na saratani watu milioni 9.9.

Kwa mujibu wa takwimu hizo, idadi ya watu waliofariki dunia kutokana na ugonjwa wa saratani ni kubwa ikilinganishwa na ya magonjwa mengine.

Dk Emmanuel Kandusi ambaye ni miongoni mwa waathirika wa saratani hiyo, na mwanzilishi wa kampeni ya kuangamiza saratani ya tezi dume Tanzania ya ‘50 Plus Campaign’ anasema ugonjwa huo ukitambuliwa mapema huweza kutibika kwa urahisi.

Ameongeza kuwa kutokana na ugonjwa huo kuwa hatari nchini humo, ifikapo mwaka 2020 unatarajiwa kuua watu milioni 20. Matibabu ya ugonjwa huo ni pamoja na kupata dawa pamoja na upasuaji.

Naye Profesa Ndalichako alisifu jitihada za Nelson Mandela katika kufanya tafiti zenye tija na kuongeza kuwa serikali imetenga zaidi ya Sh bilioni 8.3 kwa ajili ya maendeleo ya elimu katika taasisi hiyo ikiwemo vifaa vya maabara na utafiti pamoja na udahili wa wanafunzi.

Fedha hizo zikiwa ni mkopo kutoka Benki ya Maendeleo ya Afrika (AfDB).

Wakati huo huo, utafiti wa Taasisi ya Africa Capacity Building Foundation kwa mwaka huu unaonesha kuwa Tanzania iko katika nafasi ya pili barani Afrika katika matumizi ya sayansi na teknolojia kwa ajili ya kujiletea maendeleo.

Tundu Lissu: Utawala Wangu Utainyosha Serikali ya Magufuli...!!!

0
0

Rais wa wa Chama cha Wanasheria Tanganyika(TLS) Tundu Lissu, amesema utawala wake utahakikisha unainyoosha serikali ya awamu ya 5 ili ifuate misingi ya sheria.

Amesema hivi sasa nchi inakabiliwa na hali mbaya ya uvunjifu wa haki kutokana na baadhi ya viongozi kujiona wapo juu ya Sheria.

Kimenukaa..Chadema Waonyesha Dhahiri Kumchukia Zitto,Watoa Waraka Huu Mzito Kuhusu ACT Wazalendo na Ubunge wa Afrika Mashariki..!!!

0
0

Kwa taarifa za uhakika kutoka Dodoma, kupitia kikao cha Kamati ya Kanuni ya Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Uchaguzi wa Wabunge wa Bunge la Afrika Mashariki utafanyika kama ilivyotangazwa na Spika wa Bunge Mh. Job Ndugai kwa kuzingatia Ibara ya 50 ya Mkataba wa Jumuiya ya Afrika Mashariki na Kanuni za Kudumu za Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.

Katika kikao chake kilichoketi jana hadi majira ya saa nne usiku, taarifa hizo zinathibitisha kuwa ombi la KIONGOZI MKUU wa ACT, kutaka chama hicho kipewe haki na nafasi ya kuweka mgombea uchaguzi wa EALA, limetupiliwa mbali kwa sababu halikuwa na mashiko ya kimantiki wala msingi wa kikanuni.

Kiuhalisia kamati hiyo imeungana na Spika Ndugai na kumpongeza kwa kusimamia kanuni za uchaguzi huo hasa kwa kuzingatia msingi wa Kanuni ya 12 inayosema kuwa Uchaguzi wa EALA utafanyika kwa kuzingatia uwiano wa vyama vyenye uwakilishi bungeni.

Chama kama ACT chenye mbunge mmoja katika Bunge la lenye idadi ya wabunge 393 ni sawa na 0.00% ambayo ni sawasawa na kiti au viti 0. Kwa hiyo taratibu zinakiengua kuwa katika mchakato wa kugombea hata nafasi moja.

Vile vile kanuni ya 5(5) ya Nyongeza ya Tatu ya Kanuni za Bunge inasema "chama chochote cha siasa chenye HAKI ya kusimamisha mgombea wa EALA kinaweza kuweka wagombea watatu katika makundi ya wagombea ubunge."

Mantiki ya hoja kutokana na msingi huo wa kikanuni, inaonesha kuwa vyama vingine tofauti na CHADEMA, CUF na CCM, haviwezi kusimamisha wagombea kwa sababu havikidhi kigezo cha Kanuni ya 12 ya Kanuni za Kudumu za Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.

Kimsingi Spika amesimamia haki iliyokuwa inaporwa au kupokwa katika chaguzi za EALA zilizopita. Kwa uamuzi huo bila shaka sasa uchaguzi utahusisha vyama vitatu ambavyo ni CCM (6), CHADEMA (2) na CUF (1) ambavyo ndivyo vinakidhi vigezo vya kuweka wagombea.

Ibara ya 50 ya Mkataba wa wa EAC, inaelekeza na kutoa mamlaka kwa kila bunge la nchi mshirika kuchagua wawakilishi kwa mujibu wa kanuni za bunge la nchi husika na huo ndio utaratibu uliopo sasa ambao wapeleka maombi wanaujua vyema.

Ni wazi pia uamuzi huo utakuwa umezingatia masuala mengine ambayo yanafanana na suala hilo na tayari yanaweka precedences. Mathalani hata sasa vipo vyama ambavyo pamoja na kuwa na uwakilishi bungeni (mbunge mmoja), ambayo ni sawa na asilimia 0.000 katika bunge la sasa, hata katika baadhi ya maamuzi yanayozingatia kanuni za namna hiyo au zinazofanana na hizo, taratibu za kisheria zilizopo zinawaweka kando katika masuala kadha wa kadha kama ruzuku au kupata wabunge wa viti maalum. Hiyo inadhihirisha kuwa vyama vikafanye kazi ya siasa kuongeza viti bungeni ili vipate au kuongeza nafasi za wagombea wa EALA watakaowakilisha nchi yetu kwenye bunge hilo.

Ni muhimu wakajua kuwa nafasi hizi za EALA kwa utaratibu uliopo sasa hazigawiwi tu kama sandakarawe au jugu ama pipi. Ni matokeo pia ya kazi kubwa iliyofanyika wakati wa kampeni uchaguzi uliopita.

Tusubiri uteuzi kuelekea uchaguzi EALA.

Tumaini Makene

Hatarii...Jaji Mkuu Mstaafu Chande Othmani Aibuka na Kutoa Mazito ya Moyoni,Afunguka Makubwa Kuhusu..!!!!

0
0

JAJI Mkuu mstaafu, Mohamed Chande Othman amesema mahakama nchini ziko huru, hazipendelei upande wowote wala kushinikizwa na mtu tofauti na baadhi ya watu wanavyofikiri au wakati mwingine kupotosha.

Katika mahojiano ya kwanza tangu astaafu aliyoyafanya  hivi karibuni, Jaji Othman alitoa mfano wa jinsi Mahakama ilivyoshughulikia kwa haraka kesi za uchaguzi wa mwaka 2015 uliokuwa na mvutano mkubwa.

Jaji huyo aliyefanya kazi za sheria nje na ndani ya nchi pamoja na taasisi kadhaa za kimataifa, alieleza kuwa kesi za uchaguzi za ubunge na udiwani zimemalizika bila malalamiko ya upendeleo.

Hata hivyo, anasema bado mahakama ina changamoto nyingi ikiwamo kila mkoa kuwa na Mahakama Kuu, kuongeza idadi ya mahakama za mwanzo na uboreshaji wa miundombinu huku akisikitishwa na baadhi ya mahakama kutokuwa na umeme.

Jaji Othman ambaye alisoma sheria darasa moja na Waziri Mkuu mstaafu, Mizengo Pinda, angependa kuona watendaji wa mahakamani wakipambana ili kuhakikisha wanamaliza kabisa mlundikano wa kesi.

Ukimuliza kitu anachokikumbuka zaidi, Jaji Chande anasema katika utumishi wake mahakamani hatosahau kesi ya mtoto aliyechunwa ngozi mkoani Mbeya iliyofikishwa mbele yake.

Credit - Habari Leo

Imefichukaa..Hivi Ndivyo Mitandao ya Whatspp na Instagram Inavyoaua Watu Wengi Bila Kujijua...!!!!

0
0

Wanasayansi wamethibitisha kuwa mitandao ya kijamii ndicho chanzo cha magonjwa mbalimbali yakiwamo ya akili na kulemaa kwa mishipa ya shingo.

Wanasayansi wanaeleza kuwa mitandao ya kijamii kama vile facebook, twitter, whatsApp na instagram, ujumbe wa simu na michezo ya kwenye intaneti husababisha magonjwa ya akili, uraibu na kujeruhiwa kwa shingo na uti wa mgongo kunakosababishwa na kuinamia simu muda mrefu.

Tovuti ya Neck Institute (London) imeeleza kuwa madhara ya shingo na uti wa mgongo yanayosababishwa na matumizi ya simu kwa muda mrefu hasa kwa kuandika ujumbe mfupi au Text Neck Syndrome, huathiri mamilioni ya watu duniani.

Daktari bingwa wa neva za fahamu (neurologist) wa Hospitali ya Taifa ya Muhimbili, Profesa William Matuja amesema bado hakuna ushahidi wa kisayansi kama matumizi ya simu yanaathiri mishipa ya shingo, lakini namna ya matumizi yake yalivyo yanaathiri misuli.

Profesa Matuja amesema kuinamia simu muda mrefu kunasababisha maumivu ya mgongo, shingo na hata kichwa.

Daktari wa mishipa ya fahamu, wa Florida nchini Marekani, Dean Fishman amesema mishipa ya shingo hasa kwa sehemu ya nyuma huathirika kutokana na kuandika ujumbe mfupi kila mara na kwa muda mrefu, kwa sababu kitendo hicho kinamfanya mtumiaji kuiinamia simu.

Noma Sana..Njemba Yapigwa Risasi Baada ya Kuvamia Ikulu ya Kenya Wakati Kenyatta Alipokuwa Anacheza Golf..!!!!

0
0

Walinzi wa Rauis walimpiga risasi na kumuua mtu aliyeingia kwenye ikulu ya Kenya, Jumapili ya majuzi wakati Rais Uhuru Kenyatta akihudhuria mashindano ya golf huko Muthaiga, kwa mujibu wa gazeti la Sunday Nation.

Katika tukio hilo ambalo limebaki kuwa siri kubwa wakati uchunguzi ukiendelea, mtu huyo asiyefahamika na mwenye umri wa makamo, alidaiwa kuingia bila ruhusa kwenye maeneo yanayolindwa vikali kabla ya saa 11 jioni na alikuwa kwenye eneo la maegesho, si mbali sana na jengo lenyewe na ndipo walinzi walipomuona.

Vyanzo vimeliambia gazeti hilo kuwa maafisa wa usalama wanaamini mtu huyo aliruka uzio wa ikulu hiyo sababu haiwezekani kuingia ndani bila kupita getini ambako nako hadi uruhusiwe.

Hii ni mara ya kwanza mtu yeyote kupigwa risasi na kuuawa ndani ya viwanja vya ikulu, lakini hilo ni tukio la tatu kwa mtu kuingia bila ruhusa tangu Rais Kenyatta ahamie humo mwaka 2013.

Chanzo kimoja kimesema mtu huyo alikuwa na kisu na kingine kudai hakuwa na silaha. Mwili wake ulipelekwa kwenye chumba cha kuhifadhia maiti jijini Nairobi na hadi Ijumaa hakukuwa na mtu aliyeenda kuulizia.

Kimenukaaa..Baada ya Lissu Kudai kuwa Alipigwa Ngumi na Wasira..Wasira Aibuka na Kufichua Haya Makubwa Juu ya Lissu..!!!!

0
0

Waziri wa zamani katika Serikali ya Awamu ya Nne, Stephen Wasira amemshukia Mbunge wa Singida Mashariki Tundu Lissu kwa mambo manne.

Moja ya mambo ambayo Wasira amesema ni kwamba mbunge huyo wa Chadema hana heshima kwa viongozi wakuu wa nchi.

Wasira alisema hayo baada ya Lissu kudai kuwa alinusurika kupigwa na kada huyo wa CCM wakati wa vikao vya Bunge mjini Dodoma, habari ambayo ilichapishwa jana na Mwananchi.

Akijibu tuhuma hizo, Wasira (pichani) alisema Lissu anaongea kama vile hayuko sawasawa kwa sababu yote aliyoyasema ni uongo, hajui yalitokea wapi na hajui sababu zake.

Wasira alisema hakuna mtu mwenye akili timamu anayeweza kumtukana Rais wa Awamu ya Kwanza, Mwalimu Julius Nyerere, lakini alimshangaa Lissu alipothubutu kufanya hivyo wakati wa Bunge Maalumu la Katiba.

Alisema Lissu pia alimtuhumu mambo ya uongo Mwalimu Nyerere kwa kudai alighushi saini ya mwasisi wa Serikali ya Mapinduzi Zanzibar, Abeid Amani Karume kwenye hati ya Muungano. “Hata wapinzani wenzake walimshangaa,” alisema Wasira.

“Huyu mtu amethubutu kuwatukana maraisi waliopita, kamtukana (Benjamin) Mkapa, kamtukana (Jakaya) Kikwete ambaye alimkaribisha Ikulu na kunywa juisi huku amejikunyata, sasa anamtukana Rais (John) Magufuli. Mimi si msemaji wa Magufuli, lakini huyu Lissu amekuwa anamtukana,” alisema Wasira huku akisisitiza kuwa Lissu hana heshima na maadili.

Wasira alisema kutokana na vitendo hivyo inaonekana Lissu ana matatizo kwa kuwa mtu aliye kamili hawezi kufanya vituko vya aina hiyo.

Pia, alimshangaa Lissu kuwa mstari wa mbele kumsafisha kwa maelezo mazuri Waziri Mkuu wa zamani, Edward Lowassa, wakati alikuwa wa kwanza kumtuhumu kwa kumuita fisadi kiongozi huyo alipokuwa CCM, akisema huo ni uhalisia wa mtu ambaye mara zote amekuwa hasemi kweli.

“Nashangaa leo ndiye amekuwa mstari wa mbele kumsafisha kwa brashi ya chuma baada ya Lowassa kujiunga nao,” alisema huku akibainisha kwamba hizo ndiyo dalili za mtu asiyesema kweli.

Alisema Lissu kumsafisha Lowassa inaonyesha kabisa kuwa kuna tatizo la ukamilifu kwa mwanasheria huyo mkuu wa Chadema.

“Suala la mwisho Lissu hana maadili…kama atabisha nitatoa ushahidi…” alidai Wasira ambaye amekuwa waziri katika awamu nne za serikali.

Ingawa jana, Lissu hakupatikana, lakini alipozunguma na Mwananchi wiki iliyopita alisema huwa haogopi kusema ukweli.     

Credit - Mwananchi

Wenger: Sijiuzulu Ng'oo, Wanaojiuzulu Huishia Kufa Tu..!!!

0
0

Arsene Wenger ametoa mpya na safari hii amesema haondoki kwani wanaostaafu mara nyingi hufa kwa wenye umri kama wake.

Wenger, 67, amekuwa akishutumiwa na mashabiki wa Arsenal kwa kushindwa kuipa ubingwa na sasa iko nafasi ya sita katika msimamo wa Ligi Kuu ya England baada ya kufungwa mechi nne kati ya tano ilizocheza.

Kipigo cha mabao 10-2 kutoka kwa Bayern Munich katika Ligi ya Mabingwa Ulaya, ndicho kilichochochea hasira za mashabiki kutaka aondoke.

Hata hivyo, Wenger ameonyesha hajali na akasema: “Sifikirii kustaafu. Wanaojiuzulu ni makocha vijana.” Pamoja na kwamba, mkataba wa Wenger unamalizika mwishoni mwa msimu, lakini Bodi ya Arsenal inampa jeuri kocha huyo kwani imemwongezea mkataba wa miaka mwili. Alisema pia kuwa atatangaza hatma yake karibuni.

“Kwa wazee kama mimi, ukistaafu, utakufa,” aliongeza Wenger, muda mfupi kabla ya mpambano wa jana dhidi ya Manchester City. Wenger anafundisha Arsenal mwaka wa 21 sasa lakini katika miaka hiyo, hajawahi kuipa ubingwa katika miaka 13.

“Of course hata mimi inaniuma kukosa mataji,” alisema. “Nikiangalia miaka 20 kwa kweli inaumiza kuona hakuna mafanikio.

“Lakini ukiangalia klabu ya wakati huo na sasa, wakati nilipofika, wanachama walikuwa saba, lakini sasa kuna watu 700, mambo yanabadilika.”

Alisema: “Ninachukia kufungwa. Ninaelewa kuwa mashabiki wanachukia kila Arsenal inapofungwa lakini kikubwa ni kushikamana na kila mmoja na kila shabiki kuangalia timu yetu hadi mwisho wa msimu, hicho ndio cha kufanya.”     

Mbarawa Amaliza Mgomo wa Mabasi..!!!

0
0

Mkurugenzi Mkuu wa Mamlaka ya usafiri majini na nchi na kavu (SUMATRA) Gilliard Ngewe amesema huduma za usafirishaji wa abiria na mizigo nchini zitaendelea kama kawaida hapo kesho  baada ya wamiliki wa  vyombo vya usafiri nchini kuzungumza na Waziri wa Uchukuzi na Mawasiliano,  Profesa Makame Mbarawa.

Makubaliano hayo yalifikiwa mapema leo baada ya wamiliki wa mabasi (TABOA), wamiliki wa Daladala Dar es Salaam (UWADAR) pamoja na wamiliki wamalori(Tatoa) kuzungumza na Profesa Mbarawa na kukubaliana kubadili kanuni na kuzitafsiri kwa lugha ya Kiswahili.

Walikubaliana kuzifanyia marekebisho kanuni hizo ndani ya siku 14 na zipelekwe kwa wadau, pia zitenganishe makosa ya madereva na makosa ya wamiliki.

The Guardian Limited Yakanusha Uzushi wa Kuifunga Kampuni Kutokana na Ukata

0
0

Kampuni ya uchapishaji magazeti The Guardian Limited ambayo huchapisha magazeti ya The Guardian, Nipashe na Lete Raha, imekanusha taarifa za uzushi zilizosambaa mtandaoni kuwa inaifunga kutokana na ukata.

Taarifa hiyo ya uzushi ilisema:

Management ya The Guardian Chini ya General Manger, Ndg Srinivas imewatangazia wafanyakazi wa IPP- The Guardian kusudio la kufunga kampuni kutokana na ukata unaoikabili kampuni hiyo. The Guardian ni miongoni mwa kampuni kubwa za Magazeti wachapishaji wa Gazeti la kila siku la The Guardian, Nipashe, Lete Raha.

Wafanyakazi wa The Guardian wanaishi/Kupita katika kipindi kigumu hawajalipwa mshaara miezi 4 toka January 2017 wafanyakazi hawajalipwa mshahara. Frelencer na correspondence reporter hawajalipwa toka August 2016.

Media Solution (Wachapishaji wa Gazeti la Kulikoni na ThisDay) ambayo ni kampuni Dada wa The Guardian lilifungwa Rasmi mwezi February 2017. Wafanyakazi zaidi ya 200 wa Media Solution Ajira zao zilisitishwa mwezi uliopita. “Kimsingi hali ni Mbaya, kama Mzee Mengi anaisoma number inabidi tujitafakari kama Nchi tunaelekea wap?” Alinukuliwa mfanyakazi mmoja wa The Guardian akilalamika kwa uchungu.

Kufungwa kwa The Guardian kutasababisha wafanyakazi zaidi ya 350 kupoteza kazi.
Viewing all 104432 articles
Browse latest View live




Latest Images