Quantcast
Channel: UDAKU SPECIAL
Viewing all 104712 articles
Browse latest View live

Jack Wolper Adai Pombe Ndio Imemfanya Akawa Mnene

$
0
0

Kuna usemi unaosema kuwa ‘Wasanii ni kioo cha jamii’ ambapo wamekuwa mstari wa mbele kuhakikisha jamii inafuata maadili, leo April 3, 2017 nimeipata stori hii ya staa wa Bongo movies Jackline Wolper ambaye kupitia ukurasa wake wa Instagram aliwaonya vijana juu ya unywaji pombe.

Wolper alikwenda mbali zaidi na kuwashauri vijana ambao hawatumii pombe wajiepushe nayo, Jackline Wolper anatueleza sababu za kuandika hivyo.

“Niliandika kuhusu pombe kwa sababu naamini pombe labda ndiyo inaweza kuwa ilinifanya nikawa mnene kutokana na mwanzo mimi nilikuwa sinywi pombe kabisa na nilikuwa sijui kitu kinaitwa pombe na hata mtu alikuwa akinywa, mimi namshangaa kabisa. Kwa hiyo ndiyo nikaandika vile pombe siyo nzuri kwa wasichana ambao ndiyo wanaanza kujifunza pombe na wana miili yao mizuri tu. Waache kunywa pombe.” – Jackline Wolper.

Kimenukaa..Kampuni ya The Guardian Inayochapisha Magazeti ya Nipashe Imetoa Tamko Hili Kuhusu Taarifa za Kufilisika..!!!

$
0
0

Kampuni ya uchapishaji magazeti The Guardian Limited ambayo huchapisha magazeti ya The Guardian, Nipashe na Lete Raha, imekanusha taarifa za uzushi zilizosambaa mtandaoni kuwa inaifunga kutokana na ukata.

Hii ni taarifa yake:

Taarifa hiyo ya uzushi ilisema:

Management ya The Guardian Chini ya General Manger, Ndg Srinivas imewatangazia wafanyakazi wa IPP- The Guardian kusudio la kufunga kampuni kutokana na ukata unaoikabili kampuni hiyo. The Guardian ni miongoni mwa kampuni kubwa za Magazeti wachapishaji wa Gazeti la kila siku la The Guardian, Nipashe, Lete Raha.  
Wafanyakazi wa The Guardian wanaishi/Kupita katika kipindi kigumu hawajalipwa mshaara miezi 4 toka January 2017 wafanyakazi hawajalipwa mshahara. Frelencer na correspondence reporter hawajalipwa toka August 2016.  
Media Solution (Wachapishaji wa Gazeti la Kulikoni na ThisDay) ambayo ni kampuni Dada wa The Guardian lilifungwa Rasmi mwezi February 2017. Wafanyakazi zaidi ya 200 wa Media Solution Ajira zao zilisitishwa mwezi uliopita. “Kimsingi hali ni Mbaya,  
kama Mzee Mengi anaisoma number inabidi tujitafakari kama Nchi tunaelekea wap?” Alinukuliwa mfanyakazi mmoja wa The Guardian akilalamika kwa uchungu.
Kufungwa kwa The Guardian kutasababisha wafanyakazi zaidi ya 350 kupoteza kazi.

Serikali Yapokea Msaada wa Bilioni 490 Kutoka Umoja wa Ulaya za Miradi ya Maendeleo..!!!

$
0
0


Serikali kupitia Wizara ya Fedha na Mipango imepokea msaada wa Sh490 bilioni kutoka Umoja wa Ulaya(EU),  kwa ajili ya kufanikisha miradi ya kilimo, afya na viwanda.

Katibu Mkuu wa Wizara hiyo, Doto James amesema maelekezo ya msaada huo ni sehemu ya mpango wa pili wa maendeleo wa serikali.

“Wametoa euro 205 sawa na Sh486.9bilioni na watazitoa katika kipindi cha miaka minne kuanzia msimu huu wa bajeti, wanaanza kutoa Sh120bilioni,"alisema James wakati wa kusaini makubaliano ya upokeaji wa msaada huo.

"Serikali haipokei msaada bila utaratibu,kabla ya kuzipokea Kamati ya kitaifa ya madeni inautazama na kutoa ushauri kwa serikali."alisema

Hizi Hapa Sababu Sita Nzito za Waziri Mwakyembe Kushindwa Kuwapatanisha Diamond na Ali Kiba..!!!

$
0
0

BAADA ya Waziri wa Habari Utamaduni Sanaa na Michezo, Dk. Harrison George Mwakyembe kutamka hadharani kuwa na mipango ya kuwapatanisha wakali wa Muziki wa Bongo Fleva, Nasibu Abdul ‘Diamond Platnumz’ na Ali Saleh Kiba ‘King Kiba’, sababu sita zitakazomfanya waziri huyo kugonga mwamba, zimeelezwa IMEKUJAJE?

Hivi karibuni Waziri Mwakyembe akiwa mkoani Dodoma alizungumza na waandishi wa habari akitoa wito kwa Watanzania kuichangia Timu ya Taifa ya Vijana Chini ya Miaka 17 (Serengeti Boys) huku akitaja listi ya wadau mbalimbali wanaoongoza hamasa hiyo.

Miongoni mwa watu aliowapongeza walikuwa ni Diamond na Kiba na kusema kuwa, amefurahishwa kuwepo kwao katika hamasa hiyo na kuwataka kukutana nao Dodoma mara moja kwani anasikia kuwa hawakai pamoja na kuongeza kwamba, yeye ni kama baba yao hivyo lazima watakaa pamoja (kuelewana).

Kutokana na tamko hilo, vyanzo vya karibu na wakali hao, vimetonya kuwa, jambo hilo haliwezekani huku sababu sita (6) zitakazomfanya Waziri Mwakyembe kugonga mwamba;

SABABU YA KWANZA

Mmoja wa vyanzo vya karibu na wawili hao, alitoa sababu ya kwanza kuwa ni kujitengenezea fedha. Kwamba kuendelea kuwa na bifu kutawafanya kuendelea kuwa na ushindani hivyo ni jambo lililokaa kibiashara hivyo hawapo tayari kupoteza fursa hiyo.

“Hivi karibuni Diamond alifungua tovuti ya Wasafi.com ambayo imekusanya karibu nusu ya wasanii wa muziki wakubwa nchini, wanauza kazi zao huko kwa makubaliano na fedha kidogo zinaingia kwake nyingine kwa wasanii hao. Diamond amekuwa akitamka kuwa anapenda na Kiba ajiunge nao.
“Kiba naye amekuwa mgumu wa kukubali kwa maana ameshaona kuwa kupeleka nyimbo zake Wasafi. com, kwanza kutaliua bifu lao linalomsaidia vitu vingi vya faida na pili atakuwa chini ya Diamond ambapo atakuwa kama anamtengenezea fedha mtu ambaye anashindana naye kwenye biashara ya muziki.

Kutokana na tamko hilo, vyanzo vya karibu na wakali hao, vimetonya kuwa, jambo hilo haliwezekani huku sababu sita (6) zitakazomfanya Waziri Mwakyembe kugonga mwamba;


SABABU YA PILI

Chanzo hicho kilizidi kutiririka kuwa, sababu ya pili itakayomfanya Waziri Mwakyembe kugonga mwamba ni mameneja wa wasanii hao kutoshirikiana kwa ukaribu.

“Tangu nimemfahamu Diamond akiwa chini ya Babu Tale na Sallam SK sijawahi hata siku moja kuwaona kwenye meza moja wakitafuta suluhu na meneja wa Kiba, Seven.

Hawajawahi hata kushirikiana wala kuandaa shoo ya pamoja na inapotokea shoo wakapangiwa pamoja lazima mmojawapo atakataa au kuweka masharti magumu au kufanyiana fitina.

“Ipo mifano mingi inayoonesha wazi hawaivi chungu kimoja. Kama utakumbuka katika Tamasha la Rock lililofanyika Viwanja vya Golf, Mombasa mwaka jana likimshirikisha staa kutoka Marekani, Christopher Maurice ‘Chris Brown’, Kiba naye alikuwa mgeni mwalikwa ambaye alipafomu lakini liligeuka kuwa na sintofahamu baada ya Kiba kupanda na kupafomu nyimbo mbili tu, ikiwemo Mac Muga kisha kuzimiwa kipaza sauti na baada ya kushuka malalamiko aliyaelekeza kwa Meneja wa Diamond, Sallam kuwa amefanya yote hayo,” kilisema chanzo hicho.

SABABU YA TATU

Sababu ya tatu inaelezwa kuwa ni kukwepana wasanii hao kwa muda mrefu pindi wanapoandaliwa matamasha au linapotokea jambo la kuwakutanisha.

“Kwa muda mrefu Kiba na Diamond wamekuwa wakikwepana na ukweli huu upo wazi kwa mashabiki wao. Walishawahi kukwepana mwaka 2015 katika Viwanja vya Leaders jijini Dar katika moja ya shoo iliyoandaliwa na Kampuni ya Mawasiliano ya Tigo ikitambulika kama Tigo Kiboko Yao ambapo Kiba hakutumia mlango maalum wa VIP (aliruka fensi) kuingia ndani kwenye eneo la wasanii wenzake akiwemo Diamond.

“Mwaka jana katika sherehe ya kutimiza miaka 10 ya Chama cha Orange for Democratic Movements (ODM) cha Raila Odinga, Kiba na Diamond walialikwa bila kujuana katika Viwanja vya Mama Ngina, Mombasa kutokana na kutokuelewana kwao. Kilichotokea usiku huo, Diamond alitangazwa kama msanii rasmi atakayetumbuiza akafanya hivyo na baada ya hapo Kiba naye aliingia kama msanii wa sapraizi, jambo lililofanya shangwe kuzidiana na kuonekana kama mmoja amefunikwa,” kilisema chanzo chetu.

SABABU YA NNE

Chanzo kingine cha karibu na wasanii hao kiliongeza kuwa sababu nyingine ambayo ni ngumu kwa waziri huyo kuwapatanisha ni kila mmoja kutaka kuendelea kuwa kileleni. “Diamond ni msanii mkubwa sawa na Kiba, kumekuwa na ushindani sana kila mmoja kuendelea kukaa kileleni kwa kutoa nyimbo kali, ndiyo maana umesikia Kiba amesainiwa na Sony Music Africa na wakati
huohuo Diamond naye ameingia saini na Lebo ya Universal Music Group kusambaza kazi zake na za lebo yake,” kilisema chanzo hicho ambacho ni mchambuzi wa masuala ya burudani na mastaa Bongo.

SABABU YA TANO Ilifahamika kuwa, sababu nyingine kubwa inayoleta ugumu wa wawili hao kupatana ni kuundwa kwa timu (team) ambazo zimekuwa zikigandamizana kimuziki. Kiba ana team yake (Team Kiba) na Diamond (Team Diamond). “Team zote hizi zimekuwa zikilikoleza bifu la Diamond na Kiba na kufanya kuwa ngumu kupatana.

Kama kweli waziri anataka kuwapatanisha, angeanza kudili na makundi haya. Mfano inapotokea Diamond akapata tuzo au akafanya vizuri sehemu f’lan ni wazi timu hizi zitaanza kupondana. Inasemekana kuwa, imefikia hatua hata wawili hao wanapochaguliwa katika tuzo za kimataifa wakiwa kipengele kimoja au mmojawapo akichaguliwa kushiriki basi hizi timu hushirikiana kuuangusha upande wa pili,” kiliendelea chanzo hicho.

SABABU YA SITA Sababu ya sita na ya mwisho iliyotajwa kuleta ugumu wa kuwapatanisha wawili hao ni kutokuwa tayari. Kila mmoja kwa upande wake akihojiwa husema kuwa hana tatizo na mwenzake japokuwa kuna kinyongo wamejiwekea.

“Diamond na Kiba wenyewe hawajawa na utayari wa kupatana. Ukikaa na Kiba atakuambia hana bifu naye na Diamond vivyohivyo. Ujue hawa wana kinyongo tangu wafutiane nyimbo. Diamond alimfuta Kiba katika Wimbo wa Lala Salama na Kiba naye akalipiza kumfuta katika Wimbo wa Single Boy,” kilimaliza chanzo.

MTAZAMO WA DULLY Kuhusu kupatana kwa Diamond na Kiba, staa ambaye ni mkongwe katika Bongo Fleva, Dully Sykes alikaririwa akisema kuwa, kwa sasa wasanii hao kupatana ni jambo gumu mpaka atakapotokea msanii atakayewazidi na kuwa kileleni kwa kila kitu zaidi yao.

Aliyetumbuliwa na Rais Magufuli Dk Mwele Malecela Ateuliwa Kuwa Mkurugenzi Shirika la Afya Duniani (WHO)..!!!

$
0
0

Salamu za pongezi zimeendelea kumiminika kwa aliyekuwa Mkurugenzi wa Taasisi ya Taifa ya Utafiti wa Magonjwa ya Binadamu (Nimr), Dk Mwele Malecela baada ya kuteuliwa kuwa Mkurugenzi wa Vituo vya Kudhibiti na Kuzuia Magonjwa Afrika vya Shirika la Afya Duniani (WHO), Kanda ya Afrika.

Pia, Dk Mwele  aliteuliwa kuwa Mwenyekiti wa Mpango wa Maalumu wa WHO wa kutokomeza magonjwa yasiyopewa kipaumbele (Espen) na sasa atahamia kituo chake cha kazi Congo-Brazaville. 

Mradi wa Espen ulianza kutekelezwa mwaka 2016 hadi 2020, una lengo la kumaliza magonjwa yasiyopewa kipaumbele kwa kutoa vifaa tiba, elimu na dawa. 

Magonjwa yasiyopewa kipaumbele ni pamoja na matende, mabusha, kichocho, minyoo ya tumbo na usubi. 

Miongoni mwa waliomtumia pongezi ni Mkurugenzi wa Taasisi ya Afya ya Sikika, Irenei Kiria ambaye aliandika katika ukurasa wake wa Twitter: “Hongera Mwele kwa kupata nafasi hiyo ina maana ulipangwa kulisaidia Taifa letu ukiwa nje.”

 Mwingine ni Mhadhiri wa Saikolojia wa Chuo Kikuu cha Dar es Salaam, Profesa Kitila Mkumbo aliyeandika katika ukurasa wake wa twitter akisema: “Nina furaha kwa uteuzi wa Dk Mwele kuwa Mkurugenzi wa WHO.Nahisi kusamehewa kwa kuikosoa Serikali baada ya kumuondoa Nimr.” 

Mbunge wa Kigamboni, Dk Faustine Ndugulile yeye aliandika katika ukurasa wake akimpongeza Dk Mwele na kusema, “Nimezidiwa na furaha baada ya kupata taarifa kuwa umepata kazi kubwa katika ogani ya kimataifa. Mlango mmoja ukifungwa mwingine hufunguliwa. Katumikie vyema.” 

Dk Mwele aliondolewa kuwa Mkurugenzi wa Nimr na Rais John Magufuli Desemba 17 mwaka jana. 

Kuondolewa kwake katika nafasi hiyo kulifanyika siku moja baada ya kutoa ripoti ya utafiti wa magonjwa, ndani yake ikiwamo taarifa ya virusi vya ugonjwa wa Zika katika maeneo ya Morogoro, Geita na Magharibi mwa Tanzania. 

Taarifa ya Dk Mwele, ilieleza kuwa kati ya watu 533 waliopimwa, asilimia 15.6 walibainika kuwa na virusi hivyo. 

Siku moja baada ya kutoa takwimu hizo, Waziri wa Afya, Ummy Mwalimu akiwa na Dk Mwele aliitisha mkutano na waandishi wa habari kukanusha taarifa hizo kwamba ugonjwa huo bado haujaingia nchini.

Ile Kesi ya Scorpion Mtoboa Macho Yafikia Hatua Hii..!!!

$
0
0

Mkazi wa Buguruni jijini hapa, Deus Johakim Magosa (45) ambaye ni shahidi wa nane upande wa Jamhuri katika kesi namba 303 ya mwaka 2016 ya kumjeruhi, kumtoboa macho na kumfanyia unyang’anyi wa kutumia silaha, Saidi Mrisho inayomkabili Salum Njwete ‘Scorpion’ katika Mahakama ya Wilaya ya Ilala jijini, leo alinusurika kutupwa lupango baada ya Wakili Mwandamizi wa Serikali, Nassoro Katuga kumtuhumu kutoa ushahidi wa uongo.


Wakili Katuga alimtuhumu shahidi huyo  kutokana na kutoa majibu tofauti wakati akimuongoza kutoa ushahidi wake na maelezo aliyoyatoa awali Kituo cha Polisi cha Buguruni.

Awali shahidi huyo alisema mahakamani hapo kuwa hakuwahi kusikia popote kuwa Scorpion amehusishwa katika tukio la kumshambulia Said, lakini baadaye alipobanwa alisema ni kweli alisikia tetesi hizo kuwa mtuhumiwa huyo ndiye aliyefanya tukio hilo. Pamoja na mambo mengine aliyomhoji na kumbaini kuwa anatoa ushahidi wa uongo wakili Katuga

alipomgeukia hakimu aliyekuwa akisikiliza kesi hiyo, Flora Haule  na kumwambia shahidi anazidi kuidanganya mahakama hiyo na kuitaka mahakama hiyo imchukulie hatua kwa mujibu wa kifungu cha 164 cha ushahidi hapa nchini (Tanzania Evidence Act).

Shahidi huyo alionekana kuwa katika wakati mgumu baada ya wakili huyo kuwaita askari polisi na kuwataka wakae tayari kumchukua shahidi huyo.

Hata hivyo kutokana na ufinyu wa muda hakimu Flora aliahirisha kesi hiyo mpaka Aprili 18 mwaka huu na kumuacha shahidi huyo aondoke na kumtaka kufika tena mahakamani hapo tarehe iliyopangwa bila kukosa ambapo Scorpion naye alirudishwa mahabusu mpaka tarehe hiyo.

Mwandishi wetu alizungumza na mmoja wa wanasheria mahakamani hapo kuhusu ushahidi wa uongo ambapo, mwanasheria huyo alisema unapobainika kutoa ushahidi wa uongo ukiwa ndani ya kiapo unaweza kufungwa jela kati ya miezi sita mpaka mwaka mmoja.

Serengeti Boys Wakaza Mbele ya Waghana

$
0
0

Serengeti Boys wamefanikiwa kulinda rekodi yao ya kutopoteza mechi nyumbani na pia kufunga angalau mabao mawili kila mechi ya nyumbani baada ya kutoka sare ya bao mbili kwa mbili dhidi ya Timu ya Vijana ya Ghana...

Fahamu Siri Usiyoijua Kuhusu Ugonjwa wa Kifua Kikuu..!!!!

$
0
0

KIFUA kikuu ambacho ni maarufu kwa kuitwa TB, ni ugonjwa unaosababishwa na kiumbehai. Bakteria wa Mycobacterium Tuberculosis (TB) anaweza kushambulia sehemu yoyote ya mwili, lakini mara nyingi hushambulia mapafu.

Mtu anaweza kuwa na kifua kikuu kikali au tulivu. Kifua kikuu kikali au ugonjwa wa TB inamaanisha kuwa bakteria wanashambulia mwili na mfumo wa kinga unashindwa kuwazuia wasisababishe ugonjwa.

Watu wenye kifua kikuu kikali kwenye mapafu yao wanaweza kuambukiza bakteria mtu mwingine yeyote anayekuwa karibu yake kwani anapokohoa, kupiga chafya au kutema mate, mtu aliye karibu anaweza kuwavuta bakteria wa kifua kikuu wakati wa kupumua na kuambukizwa.

Watu wanaweza kuambukizwa bakteria wa kifua kikuu pia wasiokuwa wakali mwilini mwao. Iwapo mtu ana kifua kikuu tulivu, ina maana kuwa mwili wake umefanikiwa kupambana na bakteria wa kifua kikuu kwa ukamilifu na kuwazuia wasisababishe ugonjwa. Watu wenye kifua kikuu tulivu hawajisikii wagonjwa, hawana dalili, na hawawezi kuwaambukiza kifua kikuu watu wengine.

Kwa baadhi  ya watu, bakteria wa kifua kikuu wanakuwa tulivu maisha yote bila ya kuwa wakali. Lakini kwa watu wengine kifua kikuu tuli kinaweza kuwa kikali iwapo mfumo wa kinga wa mtu unadhoofika- kwa mfano kwa VVU.

Kifua kikuu kinaweza kubainishwa kwa kuingiza kiasi kidogo cha dawa inayoitwa Tuberculin kwenye ngozi ya mkono wa mtu. Iwapo ngozi itavimba ni dalili kwamba pengine mtu huyo ameambukizwa kifua kikuu.

Hata hivyo, njia hii haiaminiki kwa ukamilifu katika kubaini maambukizo ya kifua kikuu miongoni mwa watu walioambukizwa, kwa sababu mfumo wao wa kinga uliodhoofika hauwezi kuleta kinga imara dhidi ya protini alizoingizwa na kusababisha ngozi kuvimba. Kipimo hicho kinabaini kifua kikuu kikali na tulivu, kumaanisha kwamba kipimo hicho si sahihi kubainishia ugonjwa wa kifua kikuu kikali kwa watu wanaoishi katika maeneo ambapo kifua kikuu (na hivyo maambukizo ya kifua kikuu tuli) kimeenea sana.

Ubainishaji wa kifua kikuu kwenye mapafu unaweza kufanywa kwa x-ray au kipimo cha makohozi, ingawa na kipimo hiki hakiwezi kutoa ishara dhahiri ya maambukizo ya kifua kikuu kikali kwa mtu mwenye VVU, kwa sababu mifumo ya kinga haina nguvu ya kusababisha kuvimba dhidi ya bakteria.

Kutokeapo kifua kikuu cha mapafu cha ziada (ambapo ugonjwa unaathiri viungo vingine zaidi ya mapafu), sampuli za majimaji au tishu zinaweza kupimwa. Iwapo kuna shaka kuhusu ubainishaji wa kifua kikuu, kipimo cha ‘kalcha’ cha bakteria wa kifua kikuu kinaweza kupandwa kwenye maabara.

Hata hivyo, njia hii inahitaji vifaa maalumu na ghali na inaweza kuchukua wiki sita hadi nane kuleta matokeo. Iwapo vifaa tiba havipo, ubainishaji wa kifua kikuu mara nyingi hutegemea dalili.

DALILI Dalili za kifua kikuu hutegemea sana ni mahali gani bakteria wa TB wanakuwa. Kwa kawaida bakteria wa kifua kikuu wanakuwa kwenye mapafu na kusababisha kifua kikuu cha mapafu. Kifua kikuu cha mapafu kinaweza kusababisha kifua kikali kinachochukua zaidi ya wiki tatu, maumivu ya kifuani na kukohoa damu au makohozi. Dalili nyingine za ugonjwa wa TB ni pamoja na udhaifu au uchovu, kupungua uzito,   kukosa hamu ya kula, baridi, homa na kutoka jasho usiku.

Kifua kikuu tuli hakina dalili. TIBA Kwa kawaida, mgonjwa wa kifua kikuu anatumia vidonge kila siku wakati wa matibabu yanayosimamiwa. Ugonjwa wa kifua kikuu kikali unaweza kutibiwa kwa mchanganyiko wa antibiotics . Mchanganyiko sahihi wa dawa za kifua kikuu hutoa kinga na tiba.

Tiba inayofaa humwezesha haraka mgonjwa wa kifua kikuu kutoambukiza na kwa hiyo huzuia kuenea zaidi kwa kifua kikuu. Kufanikisha tiba ya TB, huchukua miezi sita hadi minane ya matumizi ya dawa ya kila siku. Dawa za aina mbalimbali zinatakiwa kutibu kifua kikuu kikali. Kutumia dawa mbalimbali kufanya kazi nzuri ya kuua bakteria wote na huenda ikakinga dhidi ya usugu kwa dawa.

Dawa zinazotumika zaidi ni Isoniazid, Rifampin (Rifadin, Rimactane), Ethambutol (Myambutol) na Pyrazinamide. Kuhakikisha matibabu kamili, mara nyingi inapendekezwa kuwa mgonjwa ameze vidonge mbele ya mtu atakayesimamia matibabu. Njia hii inajulikana kuwa DOTS (matibabu yanayofuatiliwa moja kwa moja, muda mfupi).

DOTS hutibu kifua kikuu kwa 95% ya wagonjwa. KINGA Dawa inayoitwa Isoniazid (INH) inaweza kutumiwa kama kinga kwa wale walio hatarini zaidi kuambukizwa kifua kikuu au kwa wale wenye kifua kikuu tulivu. Watu wenye kifua kikuu tulivu ambao si wagonjwa, wanaweza kutumia vidonge vya Isoniazid kwa miezi mingi ili kuwakinga wasipate kifua kikuu kikali.

Shirika la Afya Duniani (WHO) linapendekeza kuwa watu wenye VVU na kifua kikuu tulivu (lakini si kifua kikuu kikali) wapewe kinga ya Isoniazid kama inavyotakiwa. Kifua kikuu chenye usugu wa dawa mbalimbali (MDR-TB) na Kifua kikuu chenye usugu wa dawa uliokithiri (XDR-TB) Iwapo aina fulani ya bakteria wa kifua kikuu ni sugu kwa dawa mwafaka za antibiotic hujulikana kuwa kifua kikuu chenye usugu wa dawa mbalimbali au MDR- TB.

Iwapo kitakuwa sugu kwa dawa za antibiotic tatu au zaidi za kundi la pili, kinajulikana kuwa kifua kikuu chenye usugu wa dawa uliokithiri, au XDR- TB. Usugu wa dawa kwa kawaida hutokea wakati wagonjwa wa kifua kikuu hawatumii na hawataki kutumia dawa walizoandikiwa kama walivyoelekezwa na mabadiliko ya bakteria ambao ni sugu kwa dawa wanaruhusiwa kuzaliana.  MDR- TB ni tatizo kubwa sana na gumu kutibu.

Katika matibabu ya kawaida (wakati mwingine yanaitwa matibabu mwafaka) kwa kifua kikuu, wagonjwa wanatumia vidonge vya isoniazid na rifampicin (dawa jarabati sana zilizopo kwa kifua kikuu) pamoja na dawa nyingine kwa kipindi cha miezi sita hadi minane. Itaendelea wiki ijayo.

Fahamu Maajabu ya Kabichi Katika Kuukinga Mwili Dhidi ya Ugonjwa wa Kansa..!!

$
0
0

Ugonjwa wa saratani (cancer) ni miongoni mwa magonjwa hatari yanayosumbua watu duniani hivi sasa, Tanzania ikiwemo. 

Wagonjwa wanaongezeka kila kukicha katika Hospitali ya Ocean Road jijini Dar es Salaam, ambayo ni maalum kwa ugonjwa huu.

Katika makala ya leo, tutajifunza faida za kabichi katika mapambano dhidi ya ugonjwa huo, licha ya kuchukuliwa kama ni mboga ya kimaskini na ambayo huliwa kwa shida zaidi kuliko kimanufaa ya kiafya. 

Ingawa inaonekana kuwa kabichi ni miongoni mwa mboga za majani zinazolimwa kwa wingi na kusambazwa kwenye masoko mengi nchini, hasa katika miji mikubwa, lakini ni watu wachache sana wanaopenda kula mboga hii.

Katika miji mikubwa, kabichi inatumika zadi kwa walaji wa chips. Hata hivyo hawaitumia ipasavyo kwa sababu huwa inapikwa na kukaangwa kwa mafuta kwa muda mrefu na hivyo kupoteza baadhi ya virutubisho vyake muhimu.

 KINGA DHIDI YA SARATANI
Miongoni mwa faida nyingi zinazopatikana kwa kula kabichi (nyeupe na nyekundu), inayoongoza ni ile ya kutoa kinga dhidi ya ugonjwa hatari wa saratani. 

Inaelezwa kuwa zaidi ya tafiti 475 zimefanyika kuhusu virutubisho vinavyopatikana kwenye kabichi na kuthibitisha kuwa vina uwezo wa kuzuia ugonjwa wa saratani na wakati mwingine kutibu.

Kabichi imeonekana kuwa na uwezo wa kipekee katika kupambana na ugonjwa huu kutokana na kuwa na kiasi kikubwa cha aina tatu muhimu za virutubisho; 
‘Antioxidant’, ‘Anti-inflammatory’ na ‘Glucosinolates,’ ambazo zina uwezo wa kudhibiti magonjwa nyemelezi kadhaa ambayo husababisha saratani za aina mbalimbali mwilini.

Kwa kuzingatia madhara na mateso yatokanayo na ugonjwa wa saratani, na kwa kuzingatia upatikanaji wa kabichi usiokuwa na gharama, huna sababu ya kupuuzia ulaji wake. Laiti kama watu wote tungejua sawasawa faida za kabichi, bila shaka mboga hii ingekuwa ghali kuliko hata samaki.

AHUENI YA VIDONDA VYA TUMBO
Mbali ya kuwa na uwezo wa kutoa kinga dhidi ya ugonjwa wa saratani, juisi ya kabichi inaelezwa kuwa na faida nyingi tumboni, hasa kwa wale wenye matatizo ya vidonda vya tumbo (peptic ulcers). Ikitumika mara kwa mara huwa kama tiba kwao. Hali kadhalika mfumo wa usagaji chakula tumboni, huwa imara.

HUIMARISHA MFUMO WA MOYO
Utafiti mwingine uliofanyika kuhusu kabichi umeonesha kuwa mboga hii huimarisha mfumo mzima wa moyo kwa kudhibiti utengenezwaji wa lehemu (cholesterol) mbaya mwilini ambayo inapozidi mwilini, husababisha matatizo ya moyo.

VITAMINI ZINAZOPATIKANA KWENYE KABICHI
Ndani ya kabichi, kuna kiwango cha kutosha cha aina mbalimbali za vitamin, hususan Vitamin K, Vitamin B1, Vitamin B2, Vitamin A na Vitamin C. Aidha, kabichi ina kiasi kingi cha kambalishe (fiber) Manganizi (Manganese), Potashiamu (Potassium) na Fatty-3 acids. Vyote hivi ni kinga ya mwili dhidi ya magonjwa nyemelezi.

Ili kupata faida za kabichi na kujenga kinga imara dhidi ya magonjwa ya saratani, weka mazoea ya kula kabichi mara kwa mara, angalau mara tatu kwa wiki, kwa namna ambayo utaona mwenyewe inafaa, iwe kama mboga au kachumbari.

Nafasi Zingine za Ajira Zilizotangazwa Siku ya Leo

Wanaume Wenye Mkono wa Kupiga, Hii Inawahusu..!!!!

$
0
0

KUNA baadhi ya wanaume au makabila fulani huwa wanaamini bila mwanamke kupigwa, mambo hayaendi. Wengine wanaenda mbali na kusema kupiga ndiyo tamu ya penzi lenyewe. Ili mwanamke ajisikie vizuri, lazima apigwe kidogo na mumewe ili penzi liende sawa.

Wapo wanawake ambao nao wanafurahia. Wanajisikia vizuri kuona wamepigwa. Wakikaa muda mrefu bila ya kudundwa kidogo, wanaona kuna kitu kimepungua. Wanaanzisha chokochoko ya aina yoyote ili waweze kupewa kipigo.

Mke akiwa ana muda mrefu hajapata kipigo, anakuwa kama anaumwa. Mazungumzo yake utayagundua tu, akiwa na mumewe. Anamchokoza ilimradi tu. Akipigwa, baadaye atabembelezwa, atasamehe na maisha yanaendelea.

Na hii niseme, wale wenye tabia hii ni rahisi sana kuwajua. Huwa wanajaribu kuvimbisha. Wanajaribu kutunisha misuli ili kuona wanaume wao watafanya nini huku wakijua kitakachotokea.

Anamjibu mumewe anavyotaka. Kama hiyo haitoshi, anajaribu kumshinikiza ajaribu kumpiga ‘kama yeye ni mwanaume kweli’. Kauli hiyo huwa inachochea moto sana kwa wanaume. Mwanaume huwa anajitathmini, anajiuliza mara mbilimbili kwamba ‘sijakamilika au vipi.’

Anajiamini yeye ni mwanaume, tena rijali ambaye anajua vizuri kumshughulikia mkewe iweje mke ahoji uhalali wa uanaume wake? Jibu la haraka hapo huwa linakuwa kumuonesha huo uanaume wake kwa kumtandika angalau kofi moja.

Baada ya kofi hilo mara nyingi huwa linakuwa ni la utangulizi. Anapima kama atajibu tena ili amuongezee dozi. Akijibu anamuongeza zaidi, baada ya hapo inakuwa ni kipigo cha hasira na madhara yake yanaweza kuwa makubwa zaidi.

Kawaida ya wanaume huwa hawapendi kudharauliwa. Huwa hawapendi kuonekana wadhaifu. Hakuna kitu ambacho kinaweza kumkasirisha kwa kiwango cha juu mwanaume kama kuhoji au kuutilia shaka uanaume wake.

Anajisikia vibaya. Hakubali. Kinachofuata baada ya kuambiwa hivyo huwa ni kuutetea uanaume wake. Kuonesha kwamba yeye si dhaifu na baada ya hapo moyo wake unakuwa umetulia kwatu.

Ukiwahoji wanaume wengi kabla hawajafanya

tukio hilo, wengi wao watakuambia ni tukio baya, hawalipendi hata kidogo. Mara nyingi huwa linatokea ghafla na bahati mbaya kulingana na mazingira. Utasikia sikupanga kumpiga na wala haikuwa dhamira yangu ila basi tu, imetokea!

Amechochewa na maneno ya mkewe. Amekasirishwa na kudharauriwa. Kukejeliwa au kuhojiwa uanaume wake. Hasira inapanda, anapiga!

SOMO KWA WANAWAKE

Ni vyema kuwa makini. Kuepuka kuleta uchochezi kwa mwenzi wako. Hata kama amekukosea, tumia lugha rafiki kumuelewesha kuliko kuonesha dalili za dharau. Kuhoji uhalali wa uanaume wake, kumuonesha kwamba na wewe ni mwamba.

Kwamba unajimudu, unaweza kujibu mashambulizi hata kama kweli unaweza, jifanye tu hauwezi.

KAULI ZENYE HEKIMA

Mwanamke unapaswa kuzungumza na mumeo kwa staha. Tumia hekima, busara na unyenyekevu. Unamuonesha ubabe mumeo ili iweje? Unabishana naye kwa lugha za ukali unategemea nini? Kuna sababu gani wewe kujifanya mbabe mbele ya mumeo?

Anaweza kunyamaza, akakuacha na kuondoka zake je utashangilia ushindi wa kumdhibiti mumeo? Halafu ukisha kuwa mshindi, itakusaidia nini? Mwanamke jishushe kwa mumeo maana kwa namna nyingine ni mpango wa Mungu.

Unaposema mwanaume ni kichwa cha familia, isiishie kwenye kuleta matumizi, kulipia ada watoto na mahitaji mengine bali umpe heshima yake kama kichwa cha familia na kamwe hamuwezi kugombana. Mtaishi vizuri.

KWA WANAUME

Ukishaona mwanamke hakuheshimu, mara kwa mara anapenda kuhoji uhalali wa uanaume wako hakuna sababu ya kumpiga. Mfanye akuheshimu kwa njia ya mazungumzo. Muoneshe kwamba wewe ni mwanaume kweli kwa njia ya mazungumzo.

Epuka kumpiga. Ikiwezekana, ukiona anakujibu, anakupandisha munkari, kwanza jua tu ni haiba ya kike. Si kwamba anaweza kujibu mashambulizi pindi utakaponyanyua mkono kumpiga. Yeye huwa anakujibu tu halafu ukianza kumdunda, anainama kusikilizia kipigo.

MADHARA YAKE

Unaweza ukampiga sehemu mbaya, ukampoteza kabisa. Utapata kesi, ukishampoteza ni suala lingine. Kesi ya Jamhuri itakuwa inakuhusu.

Kama unaona kuna jambo linakukwaza, muache. Tafuta muda mzuri, zungumza naye kwa kutumia lugha rafiki na hakika atakuelewa.

LISIMAMIENI MAPEMA

Ni vyema wote wawili mkachunguzana mapema kabla uhusiano haujakua. Mkafundishana mapema kabla tatizo halijawa kubwa. Mkiona mnashindwana kurekebishana katika lugha rafiki ni vyema mkasitisha safari ili msije kupata kazi kubwa huko muendako!

Jinsi ya Kujua Kama Umemfikisha Kweli au Anakuibia na Kukushika Masikio kwa Kelele za Kimahaba...!!!

$
0
0

Mimi sio mwigizaji, zaidi ya hapo nilikuwa mtu wa mwisho kwenye maigizo kipindi cha shule ya msingi, ila nina uwezo mkubwa wa kusema "Oooh, hapo hapo.. unanifikishaaa!", mpaka mwanaume akahisi kweli amenifikisha, hata hivyo siko peke yangu wanawake wengi tu wanaigiza wakati wapo wanafanya mapenzi.
Utafiti wa kitaifa wa ngono uliofanywa na chuo cha indiana, ulionyesha asilimia 85% ya wanaume wakisema mara ya mwisho kufanya ngono waliwafikisha kileleni wenza wao, hata hivyo asilimia 64% tu ya wanawake walisema walifika kileleni mara ya mwisho walipofanya ngono, hii inamaanisha ni hesabu ya ajabu hata mtoto wa darasa la pili anajua imekosewa, na inamaanisha asilimia 21% ya wanaume walidanganywa na milio ya kimahaba ya wenza wao na wakaamini kuwa waliwafikisha.
Iwapo tukichukulia na wewe utaki kuwa mmoja wa hao waliodanganywa na mbaya zaidi hawakua na ufahamu wowote kuwa wamedanganywa, waulize wanaume wamekuandalia dalili zinazoonyesha na zitakazokuwa zinakuonyesha iwapo unadanganywa.

        #1; Unamwelewa

Tuweke hivi, "Ooooh, hapo hapo usiitoe... ooh, naisikia mpaka kichwani!", mwanamke huwa anasema hivi akiwa anakandwa miguu yake na maji ya moto baada ya safari ya miguu ya mwendo mrefu, "OH... USI...., JAMA... UNA.... NDIO...., HAPO HA...", hivi ndomwanamke anavyosema ukiwa unashughurika vizuri kitandani, akiweza kuunganisha sentensi nzima na ikaeleweka ujue anakuzuga, maana akifikia mshindo akili yote inakua kama haifanyi kazi vizuri na ikitokea akiwa analia kama kwenye video za ngono wanavyolia, ujue anakusubiri umalize mambo yako aanze kukuelezea shida zake alizonazo, wale wa kwenye video za ngono huwa wana igiza, mwanamke wa kihalisia wa kawaida huwa hawafiki kileleni iwapo mwanaume anatumia nguvu ovyo ovyo bila ya mpangilio na msuguano wowote unaohusisha kinembe.

         #2; Anakubusu bila kuacha

Kwa mwanamke ili afike mshindo, inabidi awe na umakini mkubwa na kuweka hisia zake zote kwenye msuguano na msisimko anaoupata mwilini mwake ili afike mshindo, kubusu na kutekenya hawezi kuvifanya kwa wakati huo ambao anaweka mawazo yote mahala hapo, ukiona unataka kumpiga denda akageukia pembeni ujue mambo ndo yamemkolea vizuri na sio vinginevyo.

        #3; Uso wake unakuwa mzuri

Ulishawahi kujiangalia kwenye kioo wakati uume wako unagombana na mikono yako, najua ulishawahi kujisugua, nani ambae hajawai..., hakuna!, na unaelekea yale mambo kumwagika, unajua usowako unakuwaje?, uso wako unakuwa kama vile unataka kutolewa maisha au kama unataka kulia vile, binadamu wote wako sawa upande wa kihisia, hata wanawake pia!, akiwa na sura nzuri wakati ndo anafika mshindo ujue hapo hakuna!, anatakiwa kuwa na sura ambayo haina mvuto kama anataka kulia na sio awe bado anapendeza kama ndo anaingia harusini.

     #4; Unafanya mapenzi na mpenzi wako kwa stairi ya kimbwa mbwa

Mwanamke kufika kileleni kwa stairi ya kutoka kwa nyuma ni sawa na wewe kufika mshindo huku mwanamke akiwa anakuchzea kwa mikono.
Sijasema haiwezekani, ila inahitaji ufundi mkubwa na dereva inabidi awe anaijua kwa umakini mkubwa njia yake anayopita, ili manbo hayo yaweze kutokea, kwa hio nitakua na wasiwasi kama mwanamke akisema kafika kileleni kwa kutumia hio stairi, mwanamke anauwezo mkubwa wa kufika kileleni iwapo anafanya mapenzi ila yeye ndo yuko juu ya mwanaume kashika msukani, au kwa stairi ya missionary inayoitwa Coital Alignment Technique kwa kifupi The Cat, najua huijui... i gugo(google) na utaiona.

     #5; Ngozi yake inakuwa nyororo na kavu

Mwanamke akiwa amefika kileleni, moyo, presha ya damu na mdundo vyote vinakuja juu ambavyo inamaanisha lazima jasho limtoke kwa aina yeyote ile na mwili unakua na majimaji kwenye ngozi, hii ni moja ya dalili amekwea mlima na kufika kileleni kwa furaha 

Acha Kusingiziwa singiziwa Mimba..Fahamu Jinsi ya Kutambua Siku za Hatari za Mpenzi za Kubeba Ujauzito..!!!

$
0
0

Moja ya makala zilizopita niliwahi kuongelea namna ya kupata mtoto wa kiume na jinsi ya kujua siku za mwanamke za hatari za kubeba mimba ni zipi lakini watu wengi wamekua wakinipigia simu kwamba hawakuelewa.

Siku za hatari za mwanamke ni zipi?
Hizi ni siku ambazo mwanamke akishiriki ngono bila kutumia kinga anapata ujauzito bila wasiwasi wowote labda kama ana matatizo yanayomfanya asibebe mimba au mwanaume wake ana matatizo.

Utazijuaje siku hizo?
Kwanza kabisa ili ujue siku zako za hatari lazima ujue idadi ya siku za mzunguko wako. Kuna aina tatu za mzunguko.. mzunguko mrefu ambao unachukua siku 35, mzunguko mfupi unaochukua siku 25 na ule wa kawaida unaochukua siku 28 na ndio mzunguko ambao watu wengi wanao. 

Unajuaje mzunguko wako?
Hesabu siku tangu siku ile ya kwanza uliyoona siku zako za hedhi mpaka siku moja kabla ya kuona siku zako za hedhi zinazofuata. Unashauriwa uchukue miezi mitatu mpaka  sita ukihesabu ili ue na uhakika kwamba mzunguko wa tarehe zako haubadiliki, kama umeshahesabu siku za nyuma kabla ya kusoma makala hii ni vizuri pia. Mfano umeanza kuona siku zako tarehe moja mwezi wa nne alafu ziko zako zingine ukaziona tarehe 29 mwezi wa nne, chukua 29 toa 1 utapata 28.. maana yake wewe unamzunguko wa siku 28.

Je siku za hatari ni zipi? 
siku ya hatari ni siku ya 14 kabla ya kuona hedhi inayofuata na sio siku ya 14 baada ya kuona hedhi iliyopita na hapa ndio watu wengi wanachanganya na kupata mimba. 

Mfano kama mzunguko wako ni siku wa kawaida siku  28, chukua 28 toa 14 utapata 14. Hivyo siku yako ya hatari ni siku ya 14, lakini kwa kua mbegu ya kiume inaweza kuishi mpaka siku tano na yai la kike linaweza kuishi mpaka masaa 24 ndani ya mfuko wa uzazi basi siku nne kabla na siku moja baada ya siku ya 14 ni hatari hivyo siku za hatari ni ni siku ya 10,11,12,13,14 na 15.

Kama mzunguko wako ni mrefu labda  siku 36 basi chukua 36 toa 14 utapata 22. Hivyo siku ya 22 ni hatari na zingine ni 18,19,20,21,22 na 23.

Kama mzunguko wako ni mfupi, mfano mzunguko wa siku 21, sasa ukichukua 21 ukatoa 14 unapata 7 yaani siku ya saba ni siku yai linashuka hivyo ni hatari kwa huyu mtu.hivyo siku zingine za hatari ni 3,4,5,6,7[mtoto wa kiume] na 8.

kama mzunguko wako ni  wa kawaida yaani siku 28 sasa chukua 28 toa 14 unapata 14 yaani siku ya 14 ndio hatari zingine ni siku ya 10,11,12,13,14,15


Dalili kwamba uko kwenye siku za hatari ni zipi?

Kuongezeka kwa joto kidogo, tumbo kuuma kidogo, na ute mweupe kutoka sehemu za siri..

mwisho: maelezo hayo hapo juu yanaweza kusaidia kupanga uzazi, kuchagua jinsia ya mtoto au kutafuta mtoto. Lakini pia tarehe zote nilizoweka mabano ambazo ndio tarehe yai linashuka  ndio za mtoto wa kiume zingine zote zilizobaki ni za watoto wa kike. kwa lugha ya kingereza soma hapa

Utata Waibuka Mchanga wa Dhahabu..Yadaiwa Kama Madai ya Magufuli Yakiwa ni Kweli ..Tanzania Itavunja Rekodi ya Dunia..!!!

$
0
0

WAKATI Rais John Magufuli akiunda ya kuchunguza taarifa za makinika ya dhahabu kutoka migodini kama una asilimia 90 ya madini hayo, wataalamu wamebainisha kwamba kiwango hicho kikithibitishwa, Tanzania itakuwa imevunja rekodi ya kuzalisha tani 4,000 kwa mwaka, kiasi ambacho hakijawahi kutokea tangu dunia iumbwe.

Aidha, wamesema ili kujenga kiwanda cha kuchenjua dhahabu nchini takriban megawati 500 za umeme wa uhakika zinahitajika kwa kiwanda kimoja jambo Tanzania haiwezi kulifanikisha kwa nishati iliyopo.

Kauli hiyo imekuja siku chache baada ya Rais kuunda tume hiyo kuchunguza mchanga kwenye kontena 282 alizobaini alipotembelea bandari ya Dar es Salaam hivi karibuni zikiwa katika mchakato wa kusafirishwa.

Akizungumza katika kipindi cha Mizani ya Wiki kinachorushwa na kituo cha Televisheni cha Azam,  Meneja Mkuu wa Uhusiano wa Serikali wa kampuni ya Accacia, Assah Mwaipopo alisema Serikali ina haki ya kuhakiki, lakini haiwezi kutokea yanayosemwa yakawa kweli.

Mwaipopo alisema katika historia, inaonesha kuwa nchi inayozalisha dhahabu kwa wingi duniani ni Afrika Kusini ambayo inazalisha tani 600 hadi 400 na kiwango cha dunia kwa takwimu za mwaka 2015 ni tani 2,500 tu hadi sasa.

Alisema wanaosema kuwa mchanga huo una dhahabu asilimia 90 wanatoa tafsiri potofu na kubainisha kuwa hata miche ambayo wanavuna katika hatua ya kwanza dhahabu si asilimia 90.

Meneja huyo alisema ni vigumu kutorosha dhahabu hasa kampuni ya Accacia ambayo imesajiliwa katika Soko la Hisa la London, Uingereza na kusisitiza kuwa taarifa hiyo itaondoa utata.

“Mfano ukisema kontena moja lina asilimia 90 ya dhahabu ni kwamba kuna tani 18 za dhahabu katika kontena la tani 20; ni vigumu kwani kwa kontena 260 zilizo bandarini  unataka kuiambia dunia bandari ya Dar es Salaam ina tani 4,000, ni taarifa ya kushitua dunia,

“Haijatokea kwa mwaka mmoja dunia ikavuna tani 3,000, kwani nyingi sana ni 2,500 hivyo taarifa zinazosemwa si sahihi ila ngoja Serikali ijiridhishe,” alisema.

Mchakato

Mwaipopo alisema mchakato wa kuchimba dhahabu una hatua muhimu ambazo zinahitajika ili kupatikana dhahabu ambapo katika hatua ya kwanza dhahabu huwa kubwa.

Alisema katika hatua ya pili kemikali zinazovuta dhahabu hutumika ili madini hayo kutenganishwa.

Alisema uchenjuaji unahusu tani moja ya makinikia ili kupata gramu mbili, hivyo haiwezi kuwa kama inavyosemwa kwamba asilimia 90 ya mchanga huo ni dhahabu.

Mwaipopo alisema pia hutumia kemikali ya carbon kupata dhahabu kabla ya kufikia makapi ila kama ingewezekana wangeishia kwenye makinikia.

Alisema kemikali ya synite ni aghali na baada ya matumizi inapaswa kuharibiwa hivyo ni ngumu kuiingiza nchini.

“Katika kuchenjua tunapata gramu 0.02 ambayo inatoka kwenye tani moja kwani yale ni makapi tunayaita dhahabu athari,” alisema.

Alisema kibiashara ingekuwa heri mchakato wa dhahabu kuishia kwenye makinikia ila gramu 150 kwa tani na ukiibadilisha tani iwe gramu utapata gramu 0.02 kwenye wastani wa tani moja.

Mhandisi huyo alisema katika mgodi wa Buzwagi wanapata tani 18 za shaba ambapo kwa gharama ya soko haina tija kubwa.

Kuhusu gharama za kusafirishia, alisema si kubwa sana kwani kontena moja linasafirishwa kwa dola 2,000 za Marekani na kuchenjua haizidi dola 1,000 hivyo tani 3.6 itakayopatikana itarejesha gharama na faida.

Mahitaji

Akifafanua kuhusu kiwanda cha kuchenjua dhahabu nchini alisema kiuhalisia kiwanda hicho kinahitaji uwekezaji wa muda mrefu ambao utazingatia ukweli kuhusu makinikia yaliyopo.

Alisema uwezo wa migodi iliyopo nchini ni kuzalisha makinikia tani zaidi 50,000 na kuwa ili kiwanda kifanye kazi yanahitajika makinikia tani 150,000 kwa mwaka.

Mwaipopo alisema pia kiwanda kimoja kitahitaji umeme wa megawati 500 hivyo kwa Tanzania ni vigumu kupata umeme huo kwani uliopo ni wa megawati 2,000.

“Kama yupo mwekezaji anayetaka kuwekeza anakaribishwa, lakini ni vema akahakikishiwa uendelevu wa uwekezaji wake kwani kiwanda kinachofanya kazi hiyo ya kuchenjua makinikia kina thamani ya zaidi ya dola milioni 500,” alisema.

Alisema mgodi wa Buzwagi umeanza kwisha hivyo utakaobaki ni Bulyanhulu jambo ambalo linaweka bayana kuwa makinikia yatakuwa tani 30,000 kwa siku zijazo.

Mtaalamu  

Dk Elisante Mshiu alisema dhahabu ni dhahabu wakati unatumia ila kijiolojia inapatikana kwenye ukanda wa miamba.

Alisema Tanzania ina kanda sita ila kanda ya Ziwa Victoria zipo kanda nane mbili zikiwa Kenya.

Mshiu alisema nchini kanda maarufu ya dhahabu ni Sukuma Land   ambayo inahusu Buzwagi, Bulyanhulu na Geita.

Dk Mshiu alisema hoja ya Serikali kutaka mtambo wa kujengwa nchini ni lazima wataalamu washirikishwe ili kuuhakikishia umma kuwa makinikia yatakuwapo ya kutosha.

Kuhusu kontena za tani 20 bandarini kuwa na dhahabu asilimia 90 alisema ni kitu ambacho hakiwezekani kwani kwa uzito wa dhahabu hiyo magari yasingetembea.

“Yote yanayofanywa yanafaa kupewa nafasi ila kiuhalisia haiwezekani kontena la tani 20 likawa na asilimia 90 kwa uzito wa dhahabu gari haliwezi kutembea,” alisema.

Kamati iliyoundwa na Rais inaongozwa na Profesa Abdulkarim Mruma na wengine ni Profesa Justinian Rwezaura,  Profesa Joseph Buchweishaija, Dk Yusuf Ngenya, Dk Joseph Yoweza, Dk Ambrose Itika, Mohamed Makongoro na Hery Gombela.

Aidha, Bunge kupitia Spika Job Ndugai litaunda tume ya kibunge kuchunguza sakata hilo la mchanga wa dhahabu.

Breaking News..Maalim Seif Atoa Tamko Zito Kuhusu Prof Lipumba,...!!!

$
0
0

Jana  Katibu mkuu wa chama cha wananchi CUF Maalim Seif alifanya mahojiano na kituo cha Television cha Azam two na kusema hamtambui mwenyekiti wa chama hicho Pro. Ibrahim Lipumba pamoja na uwamuzi aliochukuwa wakumuweka kando na nafasi yake kukaimiwa na Magdalena Sakaya.

Malim Seif alisema  hawezi kwenda ofisi za Buguruni kwa kuwa makao makuu ya chama hicho yapo Zanzibar na sio Dar es Salaam

Hii Hapa ..Ratiba ya Mkutano wa Saba wa Bunge Linaloanza Leo Jumanne April 4

$
0
0

Waziri wa Fedha na Uchumi Dkt Philip Mpango anatarajiwa kusoma Bajeti ya serikali kwa mwaka wa fedha 2017/18 siku ya Alhamisi, Juni 15 mwaka huu.

Tarehe hiyo ni kwa mujibu wa ratiba ya Mkutano wa Saba wa Bunge unaoanza leo  Jumanne (Aprili 4) katika ukumbi wa Bunge mjini Dodoma, mkutano ambao ni maalum kwa ajili ya bajeti.

Ratiba hiyo inaonesha shughuli ya kwanza kuwa ni uchaguzi wa wabunge wa Bunge la Afrika Mashariki siku ya Jumanne, na Bajeti ya Ofisi ya Waziri Mkuu itasomwa siku ya Alhamisi, Aprili 6 na kujadiliwa kwa siku nne, ikifuatiwa na bajeti ya Rais (siku 4) na Bajeti ya Ofisi ya Makamu wa Rais (Siku 1) kabla ya bajeti ya Wizara ya Sheria na Katiba Aprili 25.

Mbali na bajeti za wizara, mkutano huo pia utajadili na kupitisha miswada kadhaa ya sheria ukiwemo Muswada wa Sheria ya Marekebisho ya Sheria Mbalimbali wa Mwaka, 2017

JPM awateua Kitila Mkumbo na Semakafu

$
0
0

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. John Pombe Magufuli leo tarehe 04 Aprili, 2017 amefanya mabadiliko madogo katika safu ya Makatibu Wakuu.

Taarifa iliyotolewa na Katibu Mkuu Kiongozi Balozi John Kijazi imeeleza kuwa Mhe. Rais Magufuli amemteua Prof. Kitila Alexander Mkumbo kuwa Katibu Mkuu wa Wizara ya Maji na Umwagiliaji.

Prof. Kitila Alexander Mkumbo anachukua nafasi ya Mhandisi Mbogo Futakamba ambaye amestaafu. 

Kabla ya Uteuzi huu Prof. Kitila Alexander Mkumbo alikuwa Mhadhiri wa Chuo Kikuu cha Dar es Salaam (UDSM).

Mhe. Rais Magufuli amemteua Dkt. Leonard Akwilapo kuwa Katibu Mkuu wa Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia.
Kabla ya Uteuzi huo Dkt. Leonard Akwilapo alikuwa Naibu Katibu Mkuu wa Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia.

Kufuatia uteuzi huo aliyekuwa Katibu Mkuu wa Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia Bi. Maimuna Tarishi amehamishwa na kuwa Katibu Mkuu Ofisi ya Waziri Mkuu (Bunge).

Bi. Maimuna Tarishi anachukua nafasi iliyoachwa na Mussa Uledi ambaye uteuzi wake ulitenguliwa.

Mhe. Rais Magufuli amemteua Dkt. Ave Maria Semakafu kuwa Naibu Katibu Mkuu wa Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia ambako anajaza nafasi iliyoachwa na Dkt. Leonard Akwilapo ambaye ameteuliwa kuwa Katibu Mkuu wa Wizara hiyo.

Kabla ya Uteuzi huo Dkt. Ave Maria Semakafu alikuwa Mhadhiri wa Chuo Kikuu cha Afya na Sayansi Shirikishi Muhimbili (MUHAS).

Wateule hao wataapishwa kesho tarehe 05 Aprili, 2017 saa 3:00 Ikulu Jijini Dar es Salaam.

Kimenukaa..Wabunge wa CCM Wamng'ang'ania Dauni Bashite Bungeni..Waungana Pamoja Kutaka Atumbuliwe...!!!!

$
0
0

Wabunge wa CCM wameitaka Serikali kutoa majibu sahihi bungeni kuhusu utambulisho wa mtu aitwaye Daudi Bashite.

Sakata hilo liliibuka juzi katika kikao cha wabunge wa CCM kilichoongozwa na Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa mjini hapa.

Wabunge tofauti waliozungumza na Mwananchi walisema kuwa, suala hilo lilihojiwa kwenye kikao hicho cha ndani ambacho hufanyika kabla ya mkutano wa Bunge kwa ajili ya kuwekana sawa.

Kwa mujibu wa chanzo chetu, wabunge hao walidai kuwa Serikali imeendesha na inaendelea kuhakiki vyeti vya elimu na baadhi ya watumishi wameshakumbwa na adhabu au kufukuzwa kazi kwa tatizo la vyeti feki.

Mpashaji mwingine aliiambia Mwananchi kuwa, Waziri Mkuu alijibu kuwa Serikali imepokea hoja hiyo bila kutoa ufafanuzi zaidi.

 Pamoja na kelele za watu tofauti kueleza uwezekano wa kughushi vyetu, si Baraza la Mitihani (Necta), Polisi wala Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa (Takukuru) iliyojitokeza kuzungumzia suala hilo au kuchukua hatua.

 Credit - Mwananchi

Noma Sana..Kambi ya Upinzani Waapa Kuitikisa Serikali Bungeni..Waja na Hoja Hizi Nzito..!!

$
0
0

IKIWA imebaki siku moja kabla ya kuanza kwa Bunge la Bajeti mjini Dodoma, Kambi Rasmi ya Upinzani Bungeni imefunguka jinsi itakavyoibana serikali kwa kuwasilisha bajeti ‘hewa’ kwa mwaka huu wa fedha unaomalizika.

Aidha, kambi hiyo imesema itakutana na kujadili mapendekezo ya serikali kuhusu ukomo wa bajeti ya mwaka ujao wa fedha wa 2017/18 ambayo imebaini kwa kiasi kikubwa hayaakisi uhalisia.

Kiongozi wa Kambi Rasmi ya Upinzani Bungeni, Freeman Mbowe, aliiambia Nipashe jana kuwa wamesikitika kuona bajeti iliyoidhinishwa na Bunge kwa mwaka huu wa fedha imetekelezwa kwa kiwango kidogo.

Hata hivyo, uongozi wa wabunge wa Chama Cha Mapinduzi (CCM), umesema wabunge wa chama hicho tawala watajadili utekelezaji wa bajeti ya mwaka huu na kupitisha bajeti ya mwaka ujao bila kujali lawama zinazoelekezwa na upinzani kwa serikali.

Nipashe ilitaka kujua kutoka kwa Mbowe mambo ambayo Kambi Rasmi ya Upinzani Bungeni unakwenda kuyasimamia wakati wa vikao vya Bunge la Bajeti na vipaumbele vya kambi hiyo katika bajeti ya mwaka ujao wa fedha.

Mbowe alisema kambi hiyo inaendelea vikao vyake vya kujadili bajeti hizo ya mwaka huu na ujao kwa kina kabla ya kuwasilisha mapendekezo yake na kuibana serikali bungeni.

Alisema kwa sasa wanafanya uchambuzi wa bajeti inayoelekea ukingoni kujua imetekelezwa kwa kiasi gani na maeneo yepi hayajatekelezwa na serikali, sababu za kushindwa kutekelezwa kwa bajeti na funzo inatoa lake kuelekea bajeti mpya ambayo itakuwa ya pili kuidhinisha na Bunge chini ya uongozi wa Rais wa tano, John Magufuli.

“Tunasikitishwa kwamba bajeti tuliyopitisha bungeni na inayotekelezwa ni vitu tofauti sana," Mbowe alisema.

"Taarifa ya Waziri wa Fedha na Mipango (Dk. Philip Mpango) wiki iliyopita (Machi 28) ilionyesha dhahiri kwamba fedha za maendeleo ambazo zingesaidia kunyanyua sekta nyingi zilipatikana kidogo sana na baadhi ya sekta hazikupata fedha kutokana na uwezo mdogo wa kiserikali.

“Wakati hali ikiwa hivyo, serikali inasema imeongeza mapato na inakusanya kwa wingi wakati hali hiyo siyo kweli.
“Bajeti ya mwaka 2015/16 ilikuwa ni Sh. trilioni 23 na bajeti ya kwanza ya Rais Magufuli (2016/17) ilikuwa Sh. trilioni 29.5.

Alikuja na mipango mingi, akapandisha bajeti hadi trilioni 29, tulihoji sana wakati wa mjadala wa bajeti mwaka jana kuwa haiko sawa na serikali haina uwezo wa kuongeza mapato ya kukidhi vigezo vya bajeti.

"Matokeo yake tukajipangia mipango mingi, tukapanga shughuli za maendeleo, matokeo yake tukagundua serikali haina fedha na imekopa sana. Hii inazidi kuongeza mzigo kwa mkulima na Deni la Taifa.”

Mbowe ambaye pia ni Mwenyekiti wa Chama Cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), alisema wakati ikijua utekelezaji wa bajeti ya mwaka huu umekuwa wa kusuasua, serikali imekuja na bajeti kubwa zaidi ya Sh. trilioni 31.69 kwa ajili ya mwaka ujao wa fedha.

“Tunaendelea kuwadanganya wananchi katika mambo ambayo tunajua hatutatekeleza au serikali ije na mpango wa kukopa zaidi. Kukopa siyo jambo jema la kujisifia kuwa kila siku mnakopa bila mpango,” alisema.

Mbunge huyo wa Hai mkoani Kilimanjaro, alibainisha kuwa utekelezaji wa bajeti ya maendeleo kwa mwaka huu wa fedha bado haujafika hata asilimia 40 ya bajeti iliyotengwa hivyo haoni sababu za serikali kuja na bajeti kubwa zaidi ya Sh. trilioni 32.

“Baada ya kumaliza uchambuzi wetu, tutatoa msimamo wetu wa kibajeti na mwelekeo wa kisera wa namna gani tunafikiri ni sahihi uchumi wetu uelekezwe,” alisema Mbowe.

KIPAUMBELE CHA UPINZANI
Mbowe alisema upinzani unakwenda kwenye Bunge la Bajeti ukiwa na kipaumbele cha uchumi wa vijijini na uchumi wa kilimo.

“Hili (kilimo) ni eneo ambalo safari hii kambi ya upinzani tutalipa kipaumbele katika kila bajeti tutakazowasilisha. Tunaona eneo hili serikali ya Magufuli imelisahau kabisa, hazungumzii kilimo mahali popote bali reli, ndege mambo ya usafirishaji tu,” alisema.

Mbowe alisema kambi ya upinzani imeona kuwa kilimo kinagusa asilimia 70 ya wananchi na kitendo cha serikali kutokipa kipaumbele wanakiona ndiyo sababu kubwa ya kutopungua kwa umaskini nchini.

"Katika mwaka wa fedha uliopita kilimo kilikuwa asilimia 3.4 ya Pato la Taifa, lakini lilikuwa anguko la asilimia mbili ikionyesha kuwa kinashuka zaidi wakati kinahudumia wananchi wengi zaidi,” alibainisha.

Mbowe aliongeza: “Kama kilimo kinashindwa kuchangia kwenye Pato la Taifa, maana yake wakulima wako hoi, na kama serikali haikupeleka fedha kwa wakulima, umaskini hautaisha nchini.”

KAULI YA CCM
Katibu wa Wabunge wa CCM, Jasson Rweikiza, akizungumza  jana, alisema wabunge wa chama chake watajadili na kupitisha bajeti ya serikali kwa mwaka 2017/18.
Rweikiza alisema wabunge wa CCM wanatarajia kuona fedha zitakazopatikana zinaelekezwa kwenye miradi inayowagusa wananchi moja kwa moja.

Mbunge huyo wa Bukoba Vijijini mkoani Kagera alisema: “Tungependa fedha zipatikane, ziende kutekeleza miradi ya wananchi kwenye sekta ya maji, elimu, afya na mingine. Utekelezaji wa miradi ya maendeleo uwaguse moja kwa moja wananchi wa kawaida.”

Alisema miradi ya maendeleo itatekelezwa ikiwa serikali itaendelea kupunguza matumizi yasiyo ya lazima.

Kuhusu utekelezaji wa bajeti ya mwaka 2016/17 ambao Waziri Mpango ameshakiri umekuwa wa kusuasua, Rweikiza alisema wabunge wanaijua nchi na uchumi ulivyo.

“Tunapopitisha bajeti, siyo kwamba kuna kapu fulani tutaenda kutoa na kutumia, bali tunaweka bajeti kwamba tutumie kiasi fulani kilichoidhinishwa kulingana na upatikanaji wa fedha,” Rweikiza alisema.

“Zikipatikana hiyo kazi inafanyika, kama haijafanyika tunajua ukaguzi ukifanywa na CAG (Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali), tutajua ilipatikana kiasi gani na ilitumika kiasi gani na kama haikupatikana, huwezi kumlaumu mtu.”

Machi 28, Dk. Mpango aliwasilisha bungeni bajeti elekezi ya Sh. trilioni 31.69 kwa mwaka ujao wa fedha huku akibainisha changamoto tano zilizokwamisha utekelezaji wa bajeti ya mwaka huu.

Waziri huyo alisema serikali ilipanga kutumia Sh. trilioni 11.82 kwa ajili ya bajeti ya maendeleo. Kati yake, Sh. trilioni 8.702 zilikuwa za ndani na Sh. trilioni 3.117 ni fedha za nje.

Hata hivyo, Dk. Mpango alibainisha kuwa hadi kufikia Februari mwaka huu, fedha zilizokuwa zimetolewa ni Sh. trilioni 3.975 ikijumuisha fedha zilizotolewa kwa Halmashauri, sawa na asilimia 34 ya bajeti yote ya maendeleo.

“Kati ya kiasi hicho, fedha za ndani zilikuwa Sh. trilioni 3.103 na fedha za nje Sh. bilioni 871.8,” Dk. Mpango alisema.

Waziri huyo alisema kutotekelezwa kwa bajeti hiyo ni pamoja na kuelekeza sehemu ya fedha kulipia madeni ya miradi ya maendeleo, na kuchelewa kupatikana kwa misaada na mikopo kutokana na majadiliano na washirika wa maendeleo kuchukua muda mrefu.

Nyingine ni kupanda kwa riba ya mikopo ya kibiashara katika soko la fedha kimataifa, matayarisho hafifu ya miradi na mwamko mdogo wa kulipa kodi hususan uzingatia matumizi ya mashine za kielektroniki (EFDs).

BAJETI ‘HEWA’
Kwa mujibu wa Dk. Mpango, katika kipindi cha Julai 2016 hadi Februari mwaka huu, jumla ya Sh. trilioni 16.152 zilitolewa kwa wizara, idara zinazojitegemea, sekretarieti za mikoa na mamlaka za serikali za mitaa, sawa na asilimia 54.68 ya bajeti yote iliyoidhinishwa na Bunge.

Kati ya hizo, Dk. Mpango alisema Sh. trilioni 12.177 (sawa na asilimia 41.22 ya bajeti yote) zilizotolewa kwa ajili ya matumizi ya kawaida, ikijumuisha makusanyo ya Halmashauri Sh. bilioni 126.3.

VIPAUMBELE VYA SERIKALI
Kwa mujibu wa Dk. Mpango maeneo ya kipaumbele kwa mwaka ujao wa fedha ni ujenzi wa reli, ukamilishaji malipo ya ununuaji ndege tatu za serikali, mradi wa chuma Liganga, makaa ya mawe Mchuchuma, uanzishwaji wa kanda maalumu za kiuchumi ambazo ni Tanga, Bagamoyo, Kigoma, Ruvuma na Mtwara, miradi ya gesi asilia, shamba la kilimo na uzalishaji sukari Mkulazi.

Serikali pia inapanga kuendelea na miradi mingine ya kipaumbele ambayo ni ujenzi wa msingi wa uchumi wa viwanda ikiwa ni pamoja na uendelezaji wa eneo la viwanda Tamco, Kiwanda cha General Tyre mkoani Arusha, mradi wa magadi Soda, kuimarisha mfumo wa taifa wa maendeleo ya wajasiriamali, na uendelezaji wa viwanda vidogo na ujenzi wa ofisi za Sido.

Mingine ni kufungamanisha uchumi na maendeleo ya watu, mazingira wezeshi kwa uendeshaji biashara, kuimarisha mitaji na kutumia benki za ndani za maendeleo TIB na TADB, na kuhamishia shughuli za Serikali Kuu makao makuu Dodoma ambapo tayari wizara zimeelekezwa kutenga fedha.

VIBANO
Katika mkutano ujao wa Bunge, serikali inatarajiwa kubanwa kutoa maelezo kuhusu kutotekelezwa kwa mpango wa kutoa Sh. milioni 50 kwa kila kijiji/ mtaa. Ofisi ya Waziri Mkuu iliidhinishiwa na Bunge Sh. bilioni 59 mwaka huu kwa ajili ya kuanza kutekeleza ahadi hiyo ya Rais Magufuli.

Serikali pia inatarajiwa kubanwa na Bunge kutokana na kutotoa ajira kwa wananchi na pia kutolipa malimbikizo ya madeni ya watumishi wa umma. Wizara ya Nchi, Ofisi ya Rais, Utumishi wa Umma na Utawala Bora iliahidi kutoa ajira 71,496.

Kibano kingine ni kwenye miradi ya maji, ujenzi wa meli mpya Ziwa Victoria na ukarabati wa meli zilizopo kwenye maziwa makuu, uhaba wa dawa, vifo cya uzazi na utapiamlo, ongezeko la watu nchini, ahadi ya zahanati kila kijiji na kituo cha afya kila kata, ufufuaji wa Kiwanda cha General Tyre na kuifanya Tanzania kuwa nchi ya viwanda.

Serikali pia inatarajiwa kubanwa ili kutoa maelezo ya kina kuhusu kitendo cha wizara sita kuweka ofisi kwenye Chuo Kikuu cha Dodoma (Udom), utekelezaji wa ununuzi na ugawaji wa pikipiki kwa Waratibu Elimu Kata wa mikoa 18 na kuchangia mafuta kwa ajili ya magari na pikipiki hizo.

Kibano kingine kwa serikali kinatarajiwa kuwa faida ya mradi wa mabasi yaendayo haraka, ujenzi wa nyumba za walimu na watumishi wengine wa umma na uzingatiaji wa sheria ya manunuzi ya umma katika ununuzi wa ndege mpya za serikali.

Kudadeki..Umesikia Hii Kuhusu Yanga...?

$
0
0

KOCHA msaidizi wa Yanga, Juma Mwambusi, amesema kuongezeka kwa majeruhi katika kikosi chao ni pigo na wataivaa kiugumu MC Alger ya Algeria katika mchezo wa Kombe la barani Afrika utakaochezwa wiki hii kwenye Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam.

Kikosi cha Yanga kinakabiliwa na majeruhi wengi baada ya Mzambia Justine Zullu kuumia katika mchezo wa Ligi Kuu Tanzania Bara dhidi ya Azam uliochezwa juzi, Uwanja wa Taifa na wao kushinda bao 1-0.

Wachezaji wengine majeruhi ni  washambuliaji Amis Tambwe, Donald Ngoma, kiungo Thabani Kamusoko na  beki Pato Ngonyani.

Akizungumza  juzi, Mwambusi alisema majeruhi walionao wamezidi kupunguza idadi ya wachezaji muhimu wa kikosi chao cha  kwanza.

Mwambusi alisema hali hiyo imekuwa ikiwagharimu mara nyingi ukizingatia wameanza vibaya katika michuano ya Ligi ya Mabingwa Afrika na kutolewa mapema.

“Inasikitisha sana kuongezeka kwa majeruhi katika kikosi chetu, tunazidi kuwapunguza watu na tunakwenda kwenye michuano muhimu ambayo lengo letu ni kufanya vizuri baada ya kuanza vibaya,” alisema Mwambusi.

Mwambusi alisema malengo yao ni kutaka kufika mbali katika michuano hiyo, lakini wamekuwa wakiandamwa na majeraha na ni pigo.

Alisema wachezaji watano majeruhi ambao wanacheza kikosi cha kwanza, hivyo wanahitaji kufanya kazi kubwa  kurudi katika hali ya kawaida.
Viewing all 104712 articles
Browse latest View live




Latest Images