Quantcast
Channel: UDAKU SPECIAL
Viewing all 104768 articles
Browse latest View live

JB, Wema Wapelekwa Rasmi Nchini China..!!!

$
0
0

WASANII wa Filamu za Kibongo wamepewa fursa ya kuanza kuuza filamu zao nchini China ambao sasa zitakuwa zikitafsiriwa kwa lugha ya nchi hiyo kama ambavyo Rufufu amekuwa akitafsiri za kwao hapa nchini.

Aliyekuwa Waziri wa Habari, Michezo, Sanaa na Utamaduni, Nape Nnauye aliwaombea wasanii hao kwa serikali ya China ambapo maombi hayo yalipokewa kwa mikono miwili.

Rais wa Shirikisho la Filamu Nchini, Simon Mwakifwamba alisema wamepanga kuanza kutengeneza filamu zenye viwango vya juu ili kuweza kukimbizana na soko hilo lenye idadi ya watu zaidi ya bilioni moja.

China imezindua wiki ya filamu zake hapa nchini ambapo kazi hiyo inasimamiwa na kampuni ya ving’amuzi ya Star Times ambapo uzinduzi huo ulifanywa na Nnauye .

Nay wa Mitego - Usalama Wangu Umekuwa Mdogo, Wanapanga Kunipoteza...!!!

$
0
0

Msanii wa muziki wa hip hop ambaye anafanya vizuri na wimbo ‘Wapo’ Nay wa Mitego amedai kuna watu wanataka kumpoteza.

Wiki moja iliyopita rapper huyo alikamatwa na jeshi la polisi kutokana na wimbo wake mpya ‘Wapo’.

Hata hivyo Rais Magufuli alitoa tamko la kuachiwa kwa msanii huyo na kusema wimbo huo hauna matatizo.

Rapper huyo Jumatatu hii amefunguka kwa kudai kuwa kuna watu wanamfuatilia kutaka kumpoteza.

“Usalama wa maisha yangu umekua mdogo kwasasa, Wanapanga kunipoteza ikibidi nisiwepo kabisa kwenye hii dunia.,” aliandika Nay wa Mitego Istagram.

Aliongeza, “Nipo tayari kwa chochote wanacho panga kufanya Coz sijajipanga kupambana nao, Mimi ni mwana muziki si vingine. Kwa chochote kitachotokea familia yangu itakua na chakuongea. Siwezi kuhama nchi wala kukimbia nitafia hapa hapa. Na siko tayari kupindisha chochote.! nyie Ndo mtanilinda. Sina Mlinzi na sitarajii kua na mlinzi. OnlyGod🙏🏿#Wapo,”

Rapper huyo hakuweka wazi ni nani anataka kufanya hivyo.

Zitto Kabwe Afunguka Uteuzi wa Kutila Mkumbo Uliofanywa na Rais Magufuli

$
0
0

KIONGOZI Mkuu wa Chama ACT- Wazalendo Zitto Kabwe aunga mkono uteuzi wa Mshauri wa Chama hicho Professa Kitila Mkumbo uliofanywa na Rais w John Magufuli.

Kwa mujibu wa taarifa aliyoituma kwa vyombo vya habari  mchana huu akiwa Dodoma amesema kuwa Rais Magufuli amekuwa mzalendo kwa kufanya uteuzi bila kujali itikadi ya Professa Mkumbo

 “Leo asubuhi Rais John Pombe Magufuli amemteua Mshauri wa Chama chetu Prof. Kitila Mkumbo kuwa Katibu Mkuu wa Wizara ya Maji na Umwagiliaji. Chama cha ACT Wazalendo kimepokea kw mikono miwili taarifa juu ya uteuzi wa mshauri wa chama chetu Kwa sababu imeonyesha kuwa Rais ameona kuwa hata Watanzania walio kwenye Vyama vya Upinzani wana uwezo, weledi na uzalendo wa kutumikia nchi yetu” ameeleza zitto.

Kwa nafasi hii ya Ukatibu Mkuu wa Wizara, ndugu Kitila hawezi kuendelea kuwa Mshauri wa Chama nafasi ambayo inamfanya kuhudhuria vikao vyote vya Chama ikiwemo Kamati Kuu. Ndugu Mkumbo ameandika barua ya kujiuzulu nafasi yake ya mshauri wa Chama na kubaki kuwa mwanachama wa kawaida tu. Nimeipokea barua yake na kumkubalia Kwa maslahi mapana ya nchi yetu.

ACT Wazalendo tunamshukuru ndugu Kitila Mkumbo kwa mchango wake katika uongozi wa Chama chetu kwa wakati wote ambao alikitumikia Chama chetu kama mshauri wa chama. Msimamo wa chama chetu ni utumishi wa kizalendo kwa Taifa utokanao na kila mwananchi, ndio msingi wa kaulimbiu yetu ya 'Taifa Kwanza, Leo na Kesho', hivyo basi tunamtakia kila la kheri ndugu Kitila katika utumishi wake kwa Taifa letu katika nafasi yake hii mpya. Wizara Hii ni kubwa na muhimu Sana kwa nchi yetu. Maji ni tatizo moja kubwa ambalo wananchi wetu wanakumbana nalo na Kama Taifa hatujaweza kulimaliza. Tunamtakia kila la kheri ndugu Mkumbo katika kuongeza nguvu kumaliza kero ya maji na kuhakikisha tunaimarisha Kilimo cha Umwagiliaji nchi nzima. Tunamsihi aanze na ajenda ya Mfuko wa Maji Vijijini na kuanzishwa Kwa Wakala wa Maji Vijijini utakaosimamia upatikanaji wa Maji Kwa wananchi wetu.

Kwa hatua hii, tunaona Rais ameamua kuunganisha nchi yetu Kwa kufanya kazi na watu wote bila kuwabagua Kwa itikadi zao za vyama. Watanzania ni wamoja na kauli za kuwagawa zinaumiza zaidi Taifa kuliko kuliweka pamoja. Tunaamini kuwa Rais Ana nia njema katika uteuzi huu na sisi tumempa baraka zote Mwanachama wetu mwanzilishi wa Chama kwenda kwenye nafasi ya juu zaidi ya utumishi wa umma. Tunaamini hatamwangusha Rais na muhimu zaidi hatawaangusha Watanzania.

Jakaya Kikwete 'Zamu Yangu Kumuunga Mkono Mke Wangu'

$
0
0

Dkt Kikwete: Zamu yangu kumuunga mkono mke wangu

Rais Mstaafu wa awamu wa nne, Dkt Jakaya Mrisho Kikwete amesema ameshuhudia kiapo cha Mke wake, Mama Salma Kikwete baada ya kuteuliwa hivi karibuni kuwa mbunge wa bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.


Rais huyo mstaafu alifuatana na baadhi ya familia yake na kushuhudia mkewe akila kiapo hicho katika bunge lililoanza leo mjini Dodoma huku akisema kuwa ni zamu yake sasa kumuunga mkono mkewe.

“Leo asubuhi nimeshuhudia kiapo cha Mke wangu Mhe. Salma Rashid Kikwete kuwa Mbunge wa Kuteuliwa Bungeni Dodoma.Ni zamu yangu kumuunga mkono,” ameandika Dkt Kikwete kupitia akaunti yake ya Twitter.

Dkt Kikwete aliingia ndani ya bunge akishangiliwa na idadi kubwa ya wabunge wa bunge hilo.

Hataree..Huu Ndio Ujumbe Alioandika Kikwete Baada ya Wabunge Kumshangilia Sana Bungeni Leo..!!!

$
0
0

Baada ya kupokelewa kwa shangwe katika ukumbi wa bunge leo hii, Rais wa awamu ya nne, Jakaya Kikwete amesema ni zamu yake kwa sasa kumuunga mkono mkewe Mama Salma Kikwete.

Kikwete aliyekuwa ameambatana na familia yake, ameshuhudia mkewe akila kiapo cha ubunge katika kikao cha kwanza cha bunge lililoanza leo mjini Dodoma.

Salma Kikwete ambaye ni mwenyekiti wa WAMA, alionekana kuwa mstari wa mbele kumuunga mkono mumewe wakati wa utekelezaji wa majukumu yake ya kulitumikia taifa.

“Leo asubuhi nmeshuhudia kiapo cha mke wangu, mheshimiwa Salma Rashd Kikwete kuwa mbunge wa kuteuliwa bungeni Dodoma. Ni zamu yangu kumuunga mkono,”alinukuliwa Kikwete katika akaunti yake ya twiter.

Kikwete aliingia ndani ya bunge hilo huku akishangiliwa na idadi kubwa ya wabunge wa bunge hilo.

Bei za Dizeli na Mafuta ya Taa Yapanda Juu Mara Dufu..!!!

$
0
0

.Mamlaka ya Udhibiti wa Huduma za Nishati na Maji (Ewura) imetangaza bei mpya za mafuta ya petroli, dizeli na mafuta ya taa zitakazoaanza kutumika kuanzia kesho.

Akitangaza bei hizo leo (Jumanne)Meneja wa Mawasiliano wa Ewura,  Titus Kaguo aliwaambia wanahabari kuwa petroli imeshuka Sh 3 itauzwa Sh 2057 kutoka 2060, dizeli imepanda kwa Sh 12, kutoka Sh 1913 hadi 1925 na mafuta ya taa ni Sh 1958 kutoka 1952.

"Mabadiliko haya bei yametokana na  bei za mafuta katika soko la dunia kubadilika sanjari na mfuko wa bei na gharama za usafirishaji ikilinganishwa na mwezi uliopita,"amesema Kaguo.

Hatimaye The Undertaker Asataaf Kucheza Mieleka,Aaacha Gumzo Dunia Nzima..!!!

$
0
0

Marekani.Mashabiki wa mchezo wa mieleka WWE walitokwa na machozi mwishoni mwa wiki wakati mcheza mieleka mashuhuri The Undertaker alipotangaza kustaafu kucheza mchezo huo baada ya miaka 25.

Katika mchezo wake wa mwisho Undertaker alipigwa na Roman Reigns na kuondoka ulingoni akiwa na rekodi ya kushindi michezo 23 na kupoteza miwili  Wrestlemania.

Wakati akitoka ulingoni Undertaker alifanya kitu ambacho hajawahi kufunga hadharani kwa kwenda kumkumbatia mkewe Michelle McCool baada ya mechi dhidi ya Roman Reigns

Akithibisha kustaafu kwake mchezo huo Undertaker aliacha katikati ya ukumbi koti lake, kofia na glovisi zake na kuamsha shangwe kwa mashabiki wake.

Kimenukaa..Spika Ndugai Afunguka Mazito Baada ya Wabunge Kumshangilia Kupita Kiasi Rais Kikwete Wakati wa Kikao cha Bunge Leo..!!

$
0
0

Spika wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Job Ndugai ameshangazwa na jinsi wabunge walivyomshangilia Rais mstaafu wa awamu ya nne, Dkt Jakaya Mrisho Kikwete na kuelezea kuwa hakuna mgeni aliyewahi kupata shangwe kama hizo.

Rais Mstaafu huyo ameshangiliwa kwa muda mrefu mara baada ya kuingia bungeni leo asubuhi alipoenda kumshuhudia mke wake, Mama Salma akiapishwa tangu ateuliwe kuwa mbunge.

“Waheshimiwa wabunge, binafsi mimi ni kipindi cha nne humu bungeni sijawahi kuona mgeni amepokelewa kwa kiwango hiki,” alisema Spiga Ndugai huku akicheka kwa furaha.

Ikumbukwe kuwa Bunge limeanza leo mjini Dodoma.

Noma Sana..Kitila Mkumbo Amefunguka Haya Makubwa Baada ya Kuteuliwa na Rais Magufuli Kuwa Katibu wa Wizara ya Kilimo..!!

$
0
0

Mhadhiri wa Chuo Kikuu cha Dar es Salaam Prof. Kitila Mkumbo amemshukuru Rais Magufuli kwa kumteua kuwa Katibu Mkuu Wizara ya Maji na Umwagiliaji kwa mujibu wa taarifa iliyotolewa leo akichukua nafasi ya Mhandisi Mbogo Futakamba ambaye amestaafu.

Prof. Mkumbo ambaye pia ni kada na mshauri wa Chama cha ACT Wazalendo kinachoongozwa na Mbunge wa Kigoma Mjini, Zitto Kabwe, amesema Rais amempa heshima kubwa kwa nafasi hiyo, na yeye kama mtumishi wa umma hawezi kuikataa kwa kuwa ni kazi aliyotumwa na mkuu wa nchi.

"Ukishapewa kazi na mkuu wa nchi, unaipokea na unaifanya kwa bidii kama yalivyo matarajio, kwahiyo nimepokea uteuzi, nimekubali, mkuu wa nchi akikupa kazi utaikataa vipi, mkuu wa nchi akikupa kazi unaifanya, kumbuka mimi ni mtumishi wa umma" Amesema Prof Kitila 

EFM yakanusha kurusha habari ya Prof. Kitila Mkumbo Kukataa Uteuzi wa Rais Magufuli

$
0
0
EFM yakanusha kurusha habari ya Prof. Kitila Mkumbo Kukataa Uteuzi wa Rais Magufuli

Harmonize Hawezi Nipiga Chini – Jack Wolper Afunguka

$
0
0
Malkia wa filamu Jacqueline Wolper amefunguka kwa kudai kuwa mpenzi wake wa sasa Harmonaze hana uwezo wa kumuacha kimapenzi pamoja na tetesi ambazo zimekuwa zikisikika kwamba mwanamuziki huyo kuwa ana warembo wengine anaotoka nao kimapenzi.


Wawili hao kwa sasa wako karibu zaidi baada ya wiki chache zilizopita kudaiwa wameachana.

Akiongea na mtandao wa Central Filamu wiki hii, Wolper amedai yeye na Harmonize wako vizuri na hawadhani kama wenaweza kutengena hivi karibuni.

“Wengi wanaongea sana kuhusu mpenzi wangu kama anatoka na wanawake wengi pengine inaweza kuwa ndio sababu ya kuniacha mimi hicho hakiwezekana wanaongea kama kuna wasichana wanajipendekeza watachezewa tu,” alisema Wolper.

Muigizaji huyo amedai Harmonaze hana uwezo wa kumwacha kwani yeye ni muhimu kwake.

Soma Nafasi Zingine za Ajira Zilizopostiwa Mitandaoni Jioni Hii

Ukweli Mchungu..Haya Ndiyo Madhara ya Kutisha ya Kufanya Ngono Kinyume na Maumbile

$
0
0

Ngono kinyume na maumbile au wengine husema Ngono kwa nyia ya haja kubwa, ni hali ya kingono ambayo muhusika huingiza uume katika njia ya haja kubwa kwa lengo la kufanya mapenzi kwa njia hiyo ili kujirishiza hisia zake.

Watu ambao wanajishughulisha na kushiriki katika ngono ya nia hii ya kinyume na maumbile wapo katika hatari kubwa ya kiafya, kwa sababu njia ya haja kubwa inazungukwa na mishipa/neva nyingi sana zipo eneo hilo ambalo kazi zake si maalumu kwa tengo la ngono kwa kuingiziwa kitu ambacho hakistahiri eneo hilo.

Ambapo kwa utafiti uliofanyika Nchini Tanzania uliohusisha wasichana na wanawake wa rika kuanzia miakan 15 na kuendelea na iliyohusisha kada tofauti katika jamii kama wanafuzi, wafanyakazi, wahudumu wa baa, wauguzi, makahaba na kina mama wa majumbani katika maeneo tofauti. Watu waliojitokeza ni 903 wakiwemo pia wanaume walihusika katika tafiti hiyo.

Utafiti huo ulisema wanawake 44 kati ya 166 waliohojiwa walisema kuwa wamewahi kufanya tendo la kujamiiana kinyume na maumbile ambao ni sawa na asilimia 27 huku asilimia 73 ya waliohojiwa walidai kufahamu njia hiyo ya kufanya mapenzi kinyume na maumbile, katika Utafiti huo ulifanywa na Irene Mremi kutoka Taasisi ya utafiti wa magonjwa ya binadamu Nchini Tanzania.

Inakadiriwa kuwa asilimia 90% ya wanaume wanaofanya ngono na wanaume wenzao (mashoga) huwa wanajihusisha na ngono kinyume na maumbile.


JE, NGONO KINYUME NA MAUMBILE NI SALAMA?

HAPANA, Ngono kinyume na maumbile si salama kwa sababu ina madhara mengi kiafya kama yafuatavyo;

MOJA, Njia ya haja kubwa haina vilainishi/lubrication asilia kama jinsi Uke ulivyo.

Hivyo wakati wa tendo la ngono husasani wakati wa uingizaji wa uume huwa inasababisha kuchubuka kwa tisu/ngozi laini ndani ya njia ya haja kubwa hiyo, na hivyo kupelekea michubuko ambayo bacteria, virusi na hata vimelea vingine kuweza kupenyea wakati wa majeraha hayo ya michubuko na hivyo kuingia katika mfumo wa damu kupitia majeraha hayo.Hii inaweza kusababisha kuenea kwa magonjwa ya zinaa pamoja na VVU.

Tafiti zinaonyesha ya kuwa Ngono kwa Njia ya haja kubwa ipo katika hatari kubwa ya maambukizi ya virusi vya ukimwi kwa zaidi ya asilimia 30% kuliko watu wanaotumia njia ngono kwa njia ya Uke.

Vile vile mtu anakuwa katika hatari kubwa ya kupata virusi vya human papillomavirus (HPV ) ambavyo huweza kumpelekea mtu anayejihusisha na ngono kinyume na maumbile kupata muwasho katika eneo hilo la haja kubwa na hata kupelekea kupata kansa.

PILI, Tishu ndani ya njia ya haja kubwa, haijakingwa na kulindwa kwa ngozi ngumu kama ilivyo sehemu za nje za mwili. Tishu zote za nje ya miili yetu zina ngozi ambayo ni seli zilizokufa ambazo hutusaidia kutukinga dhidi ya maabukizi ya vimelea na vile vile hutulinda na vitu tofauti katika mazingira.

Hivyo ndani ya njia ya haja kubwa hakujakingwa na ulizi huo wa asili wa seli hizo ili kuweza kuhimili, hivyo kuifanya iwe katika hatari kubwa ya kusuguliwa na hivyo kuchanika ambayo hupekea kusababisha maambukizi kuwa rahisi kutokea.

Pia ngozi ndani ya njia ya haja kubwa iko tofauti na ile ya ukeni ambapo ngozi ya ukeni huweza kuhimili ile misuguano pasipo kuweza kusababisha michumbuko kwa sababu ya vilainishi asili vinavyoatikana ndian ya uke na gozi husika.

TATU, Njia ya haya kubwa ni Maalumu kupitisha Kinyesi tu.

Kwa jinsi ambavyo njia hii imeundwa ama kutengenezwa ni maalumu kwa kuhimili na kupitisha kinyeshi tu na si vinginevyo.

Njia ya haja kubwa imezungukwa na kama misuli mfano wa ringi ama kwa kitaalamu huitwa (Anal sphincter) ambayo kazi yake ni kukaza eneo hilo kabla na baada ya kujisaidia tu.

Kipindi ambapo misuli hiyo (anal sphincter)imekazwa ama kubwa kwa kuingiziwa kitu kingine kigumu huweza kusababisha maumivu makali kwa muhusika.

Panapoendelea kuwa na mrudio wa mara kwa mara wa ufanyaji wa Ngono kwa njia hii ya haja kubwa ama kinyume na maumbile hufanya misuli hiyo ya njia ya haja kubwa kuwa dhaifu ama kulegea na isiwe na uwezo tena wakukaza kama kazi yake inavyotakiwa kufanya. Na hivyo kuwa vigumu kuweza kuzuia kinyesi kuweza kupita mpaka utapokuwa tayari kuweza kukitoa hivyo kusababisha utokaji ovyo wa kinyesi.

NNE, Njia ya haja kubwa imejaa bacteria wengi.

Njia ya haja kubwa imejaa bacteria wengi sana tofauti na Ukeni kulivyo hata kama wapenzi hawana maambukizi yeyote ya zinaa au ugonjwa wowote bacteria huwa wapo tu eneo hilo na hawa ni bacteria wa kawaida (Normal flora).

Mtu anapokuwa naingiza uume ndani ya njia ya haja kuwa anakuwa anaingiza vimelea vingine vya bacteria katika eneo hilo na wanapokutana na wale bacteria wengine waliopo katika eneo hilo husababisha madhara.

Pia pale unapohamisha uume toka katika njia ya haja kubwa na kupeleka katika Njia ya Uke badi bacteria hao utawapeleka katika eneo Uke ambapo Njia ya haja kubwa inakuwa na bacteria wengi na hivyo kupelekea maambukizi ukeni na pia maambukizi katika njia mkojo.

Ngono kwa njia ya haja kubwa inaweza kusababisha madhara mengine kwa afya ya watu wanaojihusisha na Njia hii ya ngono na wanaweza kupata madhaara kama haya yafuatayo,
Pale mdomo unapogusana na njia ya haja kubwa au kugusa uume uliotoka kwenye njia ya haja kuwa kwa mdomo kunaweza kupelekea kupata kwa wote mtu na mpenzi wake kuwa katika hatari ya kupataa magonjwa ya HEPATITIS C, HERPES/ malengelenge, kupata virusi vya human papillomavirus (HPV) na maambukizo mengine.

Hata hivyo, majeraha makubwa wakati wa ngono kwa njia ya haja kubwa mara nyingine ingawa sio kila mara hali hii kutokea inaweza kupelekea Damu kuvuja kwa ndani (hemorrhoids) baada ya tendo hilo kufanyika ambalo inaweza kusababisha au kupasuka ama kuchanika kwa misuli/nyama ndani ya njia ya haya kubwa kwa sababu ya msuguano mkali na muda mwingine hupelekea kuweza kutoboka kwa utumbo mpana(colon) hii huweza kwa ni tukio la hatari zaidi ambalo huhitaji msaada wa kitabibu haraka kwa matibabu na hata kufanyiwa upasuaji zaidi na hata kupoteza maisha kunaweza kutokea.

TANO, pia kwa wanawake wengi wanaofanya ngono kinyume na maumbile wamekuwa wakipata shida wakati wa kujifungua kwa misuli yao kushindwa kuhimili kukaza kwakati wa kusukuma mtoto na hivyo inaweza kupelekea utokaji wa kinyesi wakati wa kusukuma mtoto. jambo ambalo huleta tabu kwa wahudumu wa afya kwa kutumia muda mwigi kuwahudumia.

Njia pekee ya kuepuka kabisa hatari hizo za ngono kinyume na maumbile ni kuacha kabisa ngono kwa njia hiyo ya haja kubwa.

shiriki katika ngono kwa njia ya kawaida na ikibidi kwa kutumia kondomu ili kujilinda dhidi ya kuenea kwa maambukizi ya magonjwa ya zinaa.

Kuepuka kuingiza uume ndani ya uke na kisha mdomoni ikiwa uume ulikuwa umeingizwa katika njia ya haja kubwa.

Ikiwa umepata michubuko na kutoka damu baada ya ngono ama vidonda karibia na njia ya haja kubwa na hata katika maeneo ya uke basi onana na daktari wako haraka iwezekanavyo ili upatiwe tiba hii iakusaidi kuzuia maambukizi ya vimelea katika eneo la jeraha.

MADHARA ANAYOWEZA KUYAPATA MWANAUME ANAYEPENDA KUJIHUSISHA NA MCHEZO HUU WA NGONO NI KAMA IFUATAVYO;

KWANZA, Kunauwezekano wa Njia ya haja ndogo kuziba kiasi au kuziba kabisa kwa sababu ya vimelea kuingia na kuziba ama kuingia kwa kinyesi katika njia ya haja ndogo hivyo kukuweka katika wakati mgumu utapohitaji kujisaidia haja ndogo.

PILI, unaweza kupata magonjwa ya saratani(kansa) ya tezi tezi Prostate gland.

TATU, Maambukizi ya Virusi vya ukimwi kwa sababu kuna uwezekano mkubwa sana wa kupata maabukizi tofauti na kwenye njia ya Uke hii ni kutokana na kuwa na uwezekano mkubwa wa kupata michubuko kiurahisi.

NNE, Kuathirika kisaikolojia hivyo mhusika kuandamwa na msongo wa mawazo kila wakati kujutia tendo hili baya.

Nina imanai ndugu msomaji wa makala hii umeweza kuona madhara mabaya sana ya tabia hii mbaya. Inawezekana umezoea mchezo huo wa kuwaingilia wenzako ama kuingiliwa kwa namna hiyo na kuona raha lakini umeziona hasara zake, amabazo kwa hakika kama wewe ni mmoja wao, unatakiwa kuacha mara moja kwa vile mwisho wake ni majuto na mateso.

Jiepushe kuiga mambo bila kujua hasara zake, pia usimtie mwenzako majaribu kwa kumlazimisha kufanya kitendo hiki na wanaume kwa kigezo cha kuachwa kwa lengo la kuwaingilia kinyume na maumbile kwa kuwatishia kuwaacha kama watakataa.

Kipi bora kuharibiwa ama kuachwa? Jibu unalo mhusika!!

Kumbuka baada ya kuharibiwa thamani yako inashuka mbele ya jamii. Kasha kupelekea kuingia katika msongo wa mawazo na mateso ya ugonjwa ama magonjwa utakayoyapata baada ya kukubali kuingiliwa kinyume na maumbile.

UKWELI MCHEZO HUU UMEWAATHIRI SANA WANAWAKE NA WANAUME AMBAO WENGI WANAUJUTIA.
JIEPUSHE NA NGONO KINYUME NA MAUMBILE!!!!!

Haihitaji Ushauri wa Daktari..Zingatia Mambo Haya Saba Tu Ili Kuwa na Afya Bora..!!!

$
0
0

Ni wakati wa matazimio mapya. Miongoni mwa maazimio(resolutions) zinazoongoza ni pamoja na ile ya kuishi maisha yaliyo na afya bora zaidi na 

furaha. Afya na furaha ni mambo mawili makubwa sana katika maisha yetu.Ukichunguza sana takribani kila kitu tunachokifanya ni katika mpambano wa kimaisha wa kuwa na afya bora zaidi na kuwa na furaha.

 Sote tunakubaliana kwamba afya bora ndio kila kitu.Ukiwa tajiri kupindukia halafu ukawa na afya mgogoro,ni wazi kwamba huwezi kuzifurahia hizo hela zako.

Yafuatayo ni baadhi ya mambo unayoweza kuyafanya ili kuwa na afya bora katika maisha,
.Lakini kabla sijaendelea mbele sana,naomba niweke wazi kwamba afya bora haihusu kula vizuri na mazoezi peke yake bali pia fikra chanya(positive 

attitude). Kuna umuhimu wa kuhakikisha kwamba siku zote unakuwa na mawazo chanya na pia kuwa karibu zaidi na watu wenye mawazo chanya.
1.Kunywa Maji kwa wingi-

Bila shaka unakumbuka msemo “Maji ni Uhai”.Hiyo ni kweli kabisa.Maji ni uhai sio tu kwa mazingira yetu na dunia kwa ujumla bali pia kwa afya au 

miili yetu.Maji ni kitu muhimu sana kwa afya zetu.Asilimia 60% ya miili yetu imetengenezwa au imesheheni maji. Maji yanahitajika kwa ajili ya kuondoa takataka au vitu visivyofaa kutoka mwilini.Maji ndio hubeba virutubisho na oxygen.
  
     Kiasi cha maji anachohitaji mtu kinategemea na mambo kadhaa kama vile unyevu(humidity) wa mahali ulipo,shughuli zinazohusisha mwili anazozifanya mtu na 

pia uzito wa mwili.Pamoja na hayo,kwa wastani miili yetu inahitaji lita 2 na nusu mpaka 3 za maji.Vyakula tunavyokula 

huchangia kama asimilia 20% za maji katika miili yetu.Kwa hiyo tunahitaji kunywa maji kiasi cha lita 2 mpaka lita 2.4 au glasi 8-9 za maji kwa siku.

    Njia rahisi ya kujua kama mwili wako una maji ya kutosha ni katika kuangalia mkojo. Mkojo wako unatakiwa kutokuwa na rangi(colorless) au 

kuwa wa njano kidogo.Kinyume cha hapo ni ishara kwamba hauna maji ya kutosha mwilini.Njia nyingine kutambua ni pamoja na kukaukwa na midomo(lips) na hata ulimi na pia kupata kiasi kiduchu cha mkojo.


2.Pata Usingizi wa Kutosha:

Unakumbuka tulipokuwa wadogo wazazi wetu walisisitiza sana kwamba twende tukalale mapema ili tukue? Bila shaka walikuwa wanajua kwamba usingizi ni sehemu muhimu sana katika afya. 

Ukiachilia mbali faida za usingizi kwa ajili ya afya za akili/ubongo wetu,usingizi au mapumziko ya kutosha ni muhimu kwa miili.Afya njema huenda sambamba na mapumziko.Ni wakati wa kuupa mwili nafasi ya kujijenga,kujiongezea nguvu na muhimu zaidi kuhakikisha kwamba tunakuwa na akili timamu. Pia ukosefu wa usingizi ni chanzo cha kuzeeka mapema.

3.Fanya Mazoezi-

Hili linaweza kupita bila maelezo ya ziada.Mazoezi ni muhimu sana kwa afya bora. Fanya mazoezi angalau mara tatu katika wiki.Jipatie muda wa kutembea japo kwa dakika 30. Kama inawezekana nenda Gym.Badala ya kupanda lifti pale kazini kwako au mitaani,tumia ngazi za kawaida.Egesha gari lako mbali kidogo na unapokwenda ili upate nafasi ya kutembea nk. Muhimu zaidi ni kuchagua aina ya mazoezi unayoipendelea. Mazoezi hayatakiwi kuwa adhabu.

    Faida za mazoezi ni pamoja na kujiepusha na magonjwa mbalimbali,kupunguza unene(bila shaka unajua kwamba unene kupindukia sio afya bali ni ugonjwa na sababu kubwa ya maradhi mengine)

4.Kula Matunda Kwa Wingi

-Matunda ni chanzo kizuri sana cha madini na vitamins ambazo miili yetu inahitaji sana kwa ajili ya afya bora. Unajua kwamba machungwa,kwa mfano, yana faida kubwa zaidi kiafya kuliko vidonge vya Vitamin C unavyobugia kila leo? Aina mbalimbali za matunda ambayo yana virutubishi vingi zaidi kiafya ni Parachichi(Avocado),apple,matikitimaji(cantaloupe),Zabibu(Grapefruit),Kiwi,Guava,mapapai,machungwa, strawberries nk.

5.Kula mboga za majani

 Kama ilivyo kwa matunda,mboga za majani(vegetables) ni muhimu sana kwa afya zetu. Wataalamu wa afya wanashauri kwamba tule aina 5 mpaka 9 za mboga za majani na matunda.Jitahidi kupata angalau zaidi ya aina 5 za mboga za majani na matunda.


6.Punguza Kula Vyakula vya Makopo

 Kutokana na jinsi dunia inavyozidi kwenda mbio,watu wengi huwa tunakosa muda wa kupika.Matokeo yake tunakimbilia kwenye vyakula vya kwenye makopo ambavyo ndivyo vimejaa katika maduka na ma-supermarket. Jitahidi kuviepuka vyakula hivyo kwa kadri unavyoweza.Mara nyingi vyakula vya 

makopo huwa na ingredients ambazo hazifai kwa afya zetu.Kwa mfano,vingi miongoni mwa vyakula hivyo huwa na chumvi nyingi kitu ambacho ni chanzo 

cha High Blood Pressure na maradhi ya moyo. Unaposhindwa kabisa kujizuia kununua vyakula hivyo vya makopo jaribu kuangalia ambavyo havina sukari au chumvi.

7.Jipende

 Kama nilivyodokeza hapo mwanzo,afya bora huenda sambamba na afya ya akili/ubongo.Njia mojawapo ya kupata afya hiyo ni pamoja na 

kujipenda.Pengine unajiuliza,kuna mtu ambaye hajipendi? Ukweli ni kwamba pengine ni kweli kwamba hakuna mtu ambaye hajipendi.Tofauti inakuja pale mtu anapofanya vitu ambavyo ni kinyume kabisa na mapenzi ya mwili.
     
Mfano,uvutaji sigara,unywaji pombe kupindukia,kutojisafisha mwili wako kwa mfano kuoga,kupiga mswaki na pia kupumzika nk.Hizo zote ni tabia 

ambazo zinaweza kuonyesha jinsi ambavyo hujipendi au huupendi mwili wako.Kama unaupenda utautumia vibaya au kuuharibu?

Ukwepaji Kodi: TRA wawashusha Serengeti Boys njiani walipokuwa wakielekea kwa Makamu wa Rais

$
0
0
Mamlaka ya Mapato Tanzania Wamewashusha Njiani Timu ya vijana chini ya miaka 17 TRA wakilitaka Basi lililokua limewabeba vijana hao ili kulipiga mnada waweze kulipa deni la kodi.

Ni hatua nzuri kama unashindwa kulipa madeni maana yake umefilisika na kama umefilisika Mali zako zitauzwa na Cha kwanza Kulipwa huwa Kodi kama unadaiwa na Wadai wengine

Hii ni Hatua nzuri na fundisho kwa Taasisi zingine zinazokwepa kulipa kodi na Alarm hii inaonesha kuwa Nchi hii si yawapiga dili tena.

Maalum kwa Kina Dada: Tumia Njia Hizi 5 za Kumridhisha Mwanaume Wako Kisawasa..!!!

$
0
0

Mtaalam wa mapenzi, Bi. Layla Quinn, anasema wamaume ni viumbe rahisi sana kuridhishwa tunapokuja katika suala la unyumba. Mwanzoni, kitu kinachomhamasisha mwanaume kujamiiana ni muonekano wako (mwanamke) tu wakimahaba, lakini kadri siku zinavyokwenda ndani ya mahusiano, inakuwa ngumu kupandisha munkari wake, hata kama wewe ni mwanamke mrembo barabara!

Bi. Layla anaendelea kusema kuwa, kumridhisha mwanaume wako kitandani inaweza ikawa rahisi kama tu utakumbuka kuweka mambo katika hali ya mvuto ( Remember to keep things intereting!). Tafuta namna ya kuleta hamasa, iliyokuwepo siku za mwanzo mwanzo, na kwa hakika utakamata usukani. Sasa swali linakuja…..Nini unatakiwa kufanya, ili kumridhisha mwanaume wako kitandani? Kujibu swali hilo, Bi. Layla amekuja na sheria 10 zifuatazo, ambazo kama zitazingatiwa kwa makini, basi mwanamke hatokuwa na shida ya kumridhisha mwanaume wake kitandani na nyanja nyingine muhimu za mahaba.

# 1 Vaa vizuri. Utamu wa kujamiiana unaweza ukawa kwenye tendo lenyewe, lakini matamanio ya kufanya tendo hilo, yanategemeana na mambo mengine mengi. Vaa vizuri wakati wa kulala wakati wote, na sio tu wakati wa usiku, ambao unataka kufanya mapenzi. Vaa nguo nyororo, yenye mtelezo unaomwagika mwilini. Kwa vazi hili na mtembeo wa kimahaba chumbani, mwanaume wako hatotaka kutoa mikono yake mwilini mwako.

#2 Usiwe mtu wa aibu aibu linapokuja suala la kujamiiana. Mwaume anaweza akakupenda kwa mapozi yako na aibu kwanza (lugha iliyotumika hapa ni “innocence”), lakini hamna mwanaume atakaye endelea kuvumilia mwanamke, ambaye anastushwa kirahisi na kila kitu (mitindo ya kujamiiana), isipokuwa mtindo wa kifudi fudi, maarufu kama “Kifo cha Mende”. Wanaume wanapenda wanawake, ambao ni wataalam kitandani. Wanaume wanapenda wanawake, ambao wanajiamini na wanabuni manjonjo mbalimbali wakati wa shughuli. Kama unataka kumridhisha mwanaume wako kitandani, basi soma mbinu mbalimbali, ambazo zinatumiwa na wapenzi mbalimbali.

#3 Fanya mazoezi na onekana Bomba. Wanaume ni watu wakujali sana muonekano wa mwanamke. Kwahiyo, sio lazima kuonekana kama walimbwende wa vichupi, lakini mtazamo wa karibu na hapo, utakuongezea mvuto zaidi kitandani. Ndio, mwanaume wako “anakupenda kama ulivyo” na tila lila nyingiiiii…..lakini lazima tuukabili ukweli kwamba watu wenye kufanya mazoezi wanaonekana na mvuto zaidi, hakuna kupinga hilo. Hata kwetu Bongo katika nyakati hizi za utandawazi, wakina kaka wengi wanawaona wanawake kama wakina Naomi Campbell na Jennifer Lopez, ambao wanatamani kuwa nao. Lakini hauhitaji kuwa kama wakina Naomi na Jennifer kumridhisha mwanaume wako, bali hakikisha tu upo katika umbo zuri la kumpelekesha kirahisi kitandani, Basi!

#4 Kuwa Mchokozi. Hapa haimaanishi ule uchokozi wa kuleta ugomvi, lahasha! Bali, ni ule uchokozi, ambao kwa lugha ya kingereza unafahamika kama “Tease”, kwa maana hiyo basi tunasema “Tease him”. Cheza nae michezo mbalimbali na burudika nae ipasavyo, na michezo isiwe ya kitandani tu, kama karata na kadhalika, bali michezo ya hata nje ya kitanda kama kukimbia na kucheza kidali po! Kama unataka kuwa mjuzi kitandani, basi unatakiwa umfanye mwanaume wako akutake wakati wote na popote pia. Kujamiiana sio kitasa ambazo unawasha na kuzima mnapokuwa chumbani tu. Mchokoze chokoze wakati mnasakata muziki jukwaani, na mchokoze chokoze (katika mitindo ya kimahaba, bila kuvuka mipaka) wakati yupo na marafiki zake.

#5 Jiamini na Jipende. Ndio, utaonekana vizuri zaidi ukipunguza maunene, lakini hiyo haimaanishi kwamba haupo bomba. Hakuna kinacho kera wanaume, kama mwanamke, ambae anauonea aibu mwili wake mwenyewe wakati anafanya mapenzi. Jiamini kuhusu mwili wako wakati upo mtupu, na jaribu mambo mbalimbali na mwanaume wako.

Ohh..Bado Unateseka kwa Kukosa Nguvu za Kiume..?Bado Unamawazo Kuwa Haumfikishi Kileleni Mpenzi Wako..Usiwaze Tumia Njia Hii Kujitibu Wewe Mwenyewe..!!!

$
0
0

Mahaba pamoja na matatizo mengine kutajwa kuchangia upungufu wa nguvu za kiume na kushuka kwa msisimko wa tendo miongoni mwa wanandoa, uchunguzi umeonesha kuwa utumiaji holela wa vyakula hasa vyenye mafuta ni moja kati ya sababu zinazochangia kwa kasi tatizo hili. Kwa kuzingatia hilo, watafiti wa masuala ya uhusiano wa kimapenzi wamebaini aina kumi ya vyakula ambavyo vina uwezo wa kumuongezea mtu nguvu ya kufanya tendo la ndoa. Vyakula hivyo ni hivi vifuatavyo:

PILIPILI

Pilipili zilizocheshwa zimetajwa kuwa na uwezo wa kusaidia msukumo wa usambazaji damu mwilini, ambao kwa kiasi kikubwa ndiyo unaoweza kumfanya mtu akawa na hisia kali za kimapenzi. Kwa msingi huo, ni vema kwa wale wanaokabiliwa tatizo la uwezo wa kufanya mapenzi wakatumia pilipili si kwa wingi bali kwa kiwango stahili, ili waamshe hisia zao.

PARACHICHI
Aina nyingine ya chakula ambacho husaidia kuongeza uwezo wa mtu kufanya tendo la ndoa ni Parachichi. Tunda hili linauwezo mkubwa wa kuzalisha vitamini E ambayo husaidia katika uzalishaji wa homoni. Inatajwa kuwa watu wanaotumia 

tunda hili kwa wingi huwana msisimko mkali wa kimapenzi na kwa upande wa wanawake husaidia kuongeza majimaji yenye utelezi sehemu za siri na hivyo kuzuia uwezekano wa kuchubuka wakati wa kujamiiana.

NDIZI
Wakati unafikiria uwezo wa kufanya vema tendo la ndoa unatakiwa kuwaza juu ya uimara wa misuli ya mwili ambayo inatajwa kuwa ni sehemu kuu na yenye muhimu katika kujamiiana. Kwa msingi huo ulaji wa ndizi mbivu unatajwa kusaidia kujenga misuli mwilini na kumfanya mtu aweze kuwa hodari katika tendo la ndoa.

CHOKOLETI
Ulaji wa Chokoleti huongeza uchangamfu mwilini na hivyo kumuwezesha mtu anayeshiriki tendo la ndoa kuwa na mguso sahihi kwenye fikra zake, jambo litakalomuwezes ha kupokea hisia za mapenzi kwa urahisi zaidi ya mtu ambaye anakwenda kwenye uwanja wa sita kwa sita akiwa mchovu wa mawazo.

CHAZA NA PWEZA
Aina hizi za samaki zinazovuliwa baharini huwa na madini ya zink na chumvi ambayo yanatajwa kusaidia uzalisha wa vichocheo vinavyohamasisha msisimko wa mwili wakati wa tendo la ndoa.

POMEGRANATE
Ni aina fulani ya matunda mekundu yanayofananana na apple. Haya yatajwa kusaidia kuamsha mishipa ya fahamu na kuweka mawasiliano sahihi ya mwili na hivyo kumuongezea mtu uwezo kwa kufanya tendo la ndoa kwa hamasa kubwa.

MVINYO MWEKUNDU
Mvivyo mwenyekundu unatajwa kuwa na uwezo wa kuuchangamsha mwili na kuongeza msukumo wa damu, kiasi cha kumuondolea mtu uchovu kabla na baada ya tendo la ndoa, hivyo ni muhimu kunywewa hasa na wale ambao wanasumbuliwa na tatizo la kushindwa kurudia tendo.

MBEGU ZA MATUNDA
Mchangayiko wa mbegu mbalimbali za matunda, mfano tikiti, maboga husaidia kuondoa ACID mwilini na kumfanya mtu ajione ni mwenye afya njema.

VANILLA
Vanila husaidia kuamasha hamasa mwili.Mwisho wa aina hizi za vyakula ni TIKITI MAJI ambalo linatajwa kuwa na virutubisho vingi vyenye uwezo wa kuusaidia mwili kuwa na nguvu za kutosha kufanya tendo la ndoa.

Siri ya Wanawake Kupenda Wanaume Warefu Hii Hapa...!!

$
0
0

Utafiti uliofanyika na kutolewa miezi kadhaa iliyopita na Vyuo Vikuu Vya Rice na North Texas, umegundua mambo kadhaa muhimu linapokuja suala la wanawake kupendelea zaidi kutoka na wanaume warefu. Watafiti hao walifanya utafiti katika sehemu mbili. Sehemu ya kwanza, waliangalia vipaumbele vya wanawake na wanaume katika suala zima la kudeti (Dating Prefences) kwa kutumia matanganzo ya mapenzi 925 (personal dating ads) yaliyowekwa Yahoo!.

Sehemu ya pili ya utafiti ilihusisha wanaume 54 na wanawake 131 kutoka chuo fulani Marekani, ambapo majibu yao kwa maswali waliyoulizwa yalidhibitisha tafiti zilizowahi kufanyika siku za nyuma. Katika majibu yao, zaidi ya nusu ya wanawake (asilimia 55 ya wanawake) walisema wanapendelea zaidi kudeti wanaume warefu, wakati asilimia 37 ya wanaume walisema wanapendelea kudeti wanawake wafupi.

Embu tuchambue kidogo…hii ina maana gani? Ina maana kwamba mambo hayapo sawia hapa (no balance), kwani wakati asilimia 55 ya wanawake wanataka wanaume warefu, ni asilimia 37 tu ya wanaume wanaotaka wanawake wafupi, angalau kwa mujibu wa utafiti huu. Kwa maana hiyo basi wanaume pia wanapendelea wanawake warefu? Tukumbuke pia idadi ya wanaume (55) waliolizwa ilikuwa ni ndogo ukilinganisha na wanawake walioulizwa (131). Poa tuendelee basi, ili tuone utafiti huu ulibaini lipi la ziada…

Kati ya wale watu 925 waliolizwa, 455 walikuwa ni wanaume wenye wastani wa umri wa miaka 36 na urefu wa futi 5 na inchi 8 (177 cm) na wanawake walikuwa 470 wenye wastani wa umri wa miaka 35 na urefu wa futi 5 na inchi 4 (165 cm). Matokeo ni kwamba, wanaume asilimia 14 tu ndio walisema wanapendelea kudeti wanawake wafupi. Hapa pia wanaume wachache sana wameonyesha kupendelea wanawake wafupi, na tukumbuke kwamba katika kundi hili idadi ya waliolizwa ilikuwa inakaribiana sana, yaani wanaume 455 na wanawake 470.

Ilipokuja kwa wanawake wale 470 walioulizwa, karibia nusu au asilimia 49 walisema kwamba wanataka kudeti wanaume warefu kuliko wao tu! Na baadhi yao walinukuliwa wakisema yafuatayo:

“Kama mwanamke, najisikia na amani zaidi (secure) [anapokuwa na mwanaume mrefu]. Nahisi kama kuna kitu akipo sawa nikifikiria kumuangalia mwanaume wangu kwa chini!” alisema mmoja wa washiriki hao. Na mwingine nae akasema..

“Kuna pia suala zima la kuvaa viatu vya mchuchumio (high heels) na wakati huohuo bado kuendelea kuwa mfupi mbele ya mwanaume wako. Na pia nataka kumkumbatia huku mikono yangu ikimzunguka shingoni”. Nafikri unapata picha jinsi jamaa alivyo mrefu kwake au sio?

Hayo ni baadhi tu ya maoni ya wale walioulizwa kwanini wanapendelea wanaume warefu, bila shaka unaweza ukafanya utafiti wako mwenyewe kwa kuuliza wanawake wachache unaowafahamu kwanini wanapendelea wanaume warefu. Sababu nyingi huwa zinajirudia (kama hii sababu ya kujihisi na amani a.k.a “secure”), lakini si ajabu unaweza ukajikuta unaibua sababu nyingine mpya lukuki!

Ile Kesi ya Kumuua Mvungi Yafikia Hatua Hii..!!!

$
0
0

WAKAZI sita wa Dar es Salaam wanaotuhumiwa kumuua kwa makusudi aliyekuwa mjumbe wa Tume ya Mabadiliko ya Katiba, Dk Sengondo Mvungi, leo wanatarajiwa kusomewa maelezo ya mashahidi katika Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu, baada ya upelelezi wa kesi hiyo kukamilika.

Washitakiwa hao ni John Mayunga (56), Juma Kangungu (29), Longishu  Losingo (29), Paulo Mdonondo (30), Mianda Mlewa (40) na Msungwa Matonya (30).

Maelezo hayo yanatarajiwa kusomwa na Wakili wa Serikali, Patrick Mwita mbele ya Hakimu Mkazi Mkuu, Thomas Simba wa Mahakama hiyo, ambapo washitakiwa hao waliposomewa mashitaka ya mauaji walikana kuhusika.

Baada ya kusomewa maelezo yao, jalada la kesi hiyo litapelekwa Mahakama Kuu ya Tanzania Kanda ya Dar es Salaam ili kesi ianze kusikilizwa, kwa sababu Mahakama ya Kisutu kisheria haina mamlaka ya kusikiliza kesi hiyo.

Awali, Mwita aliieleza Mahakama kuwa hawawezi kuwasomea maelezo hayo, kwa sababu bado wanashughulikia taratibu za kuliondoa jina la Chibago Magozi kwenye jalada ambalo lipo Mahakama Kuu, kwa sababu bado hawajapata cheti cha kifo licha ya kuandika barua kwa mamlaka husika.

Awali, washitakiwa walikuwa 11 mmoja akafariki dunia na kubaki 10, na kati yao Mkurugenzi wa Mashitaka nchini (DPP), Biswalo Mganga aliwasilisha mahakamani nia ya kutoendelea kuwashitaki wanne kwa hiyo wakabaki sita.

Washitakiwa walioachwa huru baada ya kusota rumande kwa miaka minne ni Ahmed Kitabu (30), Zacharia Msese (33), Masunga Makenza (40) na Msungwa.

Inadaiwa kuwa washitakiwa hao Novemba 3, 2013, wakiwa   Msakuzi Kiswegere, Kinondoni, kwa pamoja walimuua Dk Mvungi.

A - Z ya Binti Aliyejitupa Bahari Juzi Wakati Akirudishwa Kwao Zanzibar...!!!!

$
0
0

KISA cha binti mwenye umri wa miaka 16 (jina linahifadhiwa kutokana na miaka yake) kujitupa baharini akiwa katika boti ya Kilimanjaro V akitoka Dar es Salaam kwenda Zanzibar juzi, kinaanzia kwenye mawasiliano yake na mvulana mmoja, kwenye mtandao wa kijamii wa Facebook, imefahamika.

Msichana huyo alikuwa akiwasiliana na mvulana huyo ambaye walifahamiana kupitia Facebook, kwa kutumia simu ya mkononi.

Nipashe ilifika Kikwajuni, nyumbani kwa msichana huyo ambaye ni mwanafunzi wa kidato cha tatu (shule inahifadhiwa) na kuikuta familia yake ikiwa na majonzi, huku wakiwa hawaamini kilichotokea na binti huyo akiwa bado hai.

Akizungumza kwa huzuni, mama mdogo wa msichana huyo, Asha Saleh Mandhi, alisema palitokea mzozo baina yake na binti huyo baada ya kumkuta na simu ya mkononi wakati wazazi wake hawajamnunulia.

Alisema Jumatano iliyopita majira ya jioni akiwa nyumbani hapo na baada ya kupata taarifa kuwa mtoto wake wa kumlea anamiliki simu, alimwita na kumtaka aeleze amepewa na nani la sivyo atampeleka polisi akajieleze.

Alisema siku ya pili yake asubuhi, msichana huyo alitoroka nyumbani na ndipo alipotoa taarifa kituo cha polisi Madema kuwa amepotelewa na mtoto.

“Mimi ndiye ninayemlea huyu mtoto. Kwa kweli sijui amefikwa na mtihani gani kwa sababu hatujampa simu, lakini nashangaa tumemkuta na simu na hakutaka kumtaja aliyempa," Asha alisema.

"Kitendo cha kumuuliza ndicho kilichomfanya kukimbia na kwenda kusikojulikana.”

Mama mdogo huyo alisema baada ya kuwa ametoroka, aliichukua simu hiyo na kuangalia mawasiliano yake na ndipo alipofanikiwa kupata jina la kijana mmoja wa kiume ambaye alikuwa anawasiliana naye mara kwa mara. Hakumtaja.

Alisema baada ya kumpata kijana huyo kwa njia ya simu, aliulizwa anamfahamu vipi binti yao na kujibu kuwa wamejuana kupitia Fecbook, lakini hawajawahi kuonana kwa sababu yeye anaishi Dar es Salaam na binti anaishi Zanzibar.

Alisema alimpa taarifa kijana huyo kuwa binti yao ametoroka na haijulikani alikokwenda, hivyo kumwomba kusaidiana kuhakikisha wanampata akiwa salama.

“Kwa kweli huyo kijana alikubali kutoa ushirikiano na akawa anawasiliana na binti yetu na kumueleza kuwa yuko Dar es Salaam na amehifadhiwa na dereva teksi baada ya kukosa msaada wa eneo analotaka kwenda ambako ni kwa bibi yake anayeishi Mburahati, Dar es Salaam,” alisema.

Alisema aliwasiliana na dereva huyo ambaye alimueleza kuwa amesharipoti katika serikali ya mtaa katika eneo analoishi kuwa amemwokota binti huyo bandarini, Dar es Salaam baada ya kukaa kwa muda mrefu bila kupata msaada.

Mama mdogo huyo alisema mama mzazi wa binti huyo anaishi Muscat, Oman na kwamba amemlea tangu akiwa mdogo.

Alisema walipata mshtuko baada ya kupata taarifa kuwa binti yao amejitupa baharini wakati akitokea Dar es Salaam baada ya kusakwa kwa siku kadhaa na hatimaye kupatikana.

MFANYAKAZI WA NDANI
Mmoja wa mashuhuda na mfanyakazi wa ndani katika nyumba anayoishi manusura huyo alisema wakati akiwa katika boti wakitokea Dar es Salaam juzi, walipata taarifa kuwa kuna mtu amejitupa baada ya kufika Chumbe, lakini hakujua kuwa aliyejitupa anamfamu.

“Baada ya kupata taarifa kuwa kuna mtu kajitupa baharini, tukaanza kupiga kelele na nilimwona akielea baharini, lakini nilijua ni mtoto wa kizungu bila kufahamu kuwa nilikuwa namfahamu,” alisema Hiyari Miraji Othman.

Alisema alikuja kufahamu kuwa anamfahamu manusura baada ya saa nne na kwamba hakutegemea angeweza kufanya kitendo hicho.

Alimwelezea msichana huyo kuwa ni mpole na mwenye nidhamu kwa kuwa amekuwa akimuona hivyo nyumbani kwao Kikwajuni kwa muda mrefu.

“Hapa kwao nakuja kila siku kwa sababu ndipo penye kibarua changu," alisema.


"Hapa huwa tunapika vyakula kwa ajili ya biashara na huwa namwona tabia zake ni mtoto mzuri anayejielewa.”

Credit - Nipashe
Viewing all 104768 articles
Browse latest View live




Latest Images