Quantcast
Channel: UDAKU SPECIAL
Viewing all 104789 articles
Browse latest View live

Rapa Chemical Afunguka Kuwa Yeye Ndio Qeen wa Hip Hop Bongo Nzima

$
0
0

Chemical amefunguka kuhusu wimbo wake mpya ‘Queen Of Dar es Salaam’. Rapper huyo mwenye swagga za hatari amesema ameamua kuchanganya verse mbili tofauti ikiwemo ya Profesa Jay na Sugu kwa pamoja kutokana na vitu hivyo waliviimba miaka mingi lakini mpaka leo bado vinatokea.
.
.

@chemical_tz ameongeza kuwa mbali na vyote alivyorap ndani ya wimbo huo lakini pia alitaka kuwafahamisha watu watambue kuwa ndani ya Bongo kuna Queen wa muziki wa hip hop ambaye ni Chemical.

Queen huyo wa Hip Hop Bongo amesisitiza kuwa kwenye wimbo huo hakuna msanii aliyemchana japo baadhi ya watu wameanza kufikiria hivyo.

Wema Sepetu Yamemfika Hapaa! Amtolea Uvivu Harmorapa

$
0
0
Kupitia ukurasa wake wa Instagram Wema Ameamua Kumfungikia Harmorapa Ambae amekuwa akitangaza kuwa anampenda Wema na kupost Picha na Video akimuongelea....Wema Amefunguka Haya:

"Sijawahi kumchukia yeyote anayehangaika kutafuta riziki yake kwa nami pia natafuta. Ila mdogo wangu Harmorappa u are getting too much. Pigana na namna utakavyo kupeleka muziki na jina lako juu but get me out of this. Nakuheshimu kama msanii mwenzangu lakini hili la kunadi kunitaka kimapenzi na kuonyesha utayari wa kufanya mambo kadha wa kadhaa kwangu please waambie wengine unaodhani mnawezana ila mimi sio wa aina hiyo. Usiiharibu image yangu niliyoipigania muda wote, usiniharibie heshima yangu ninayoijenga sasa ktk chama changu CHADEMA, usiniharibie kwenye familia yangu, marafiki zangu na usiniharibie kwa niliye nae. Ni utoto na ujinga kuposti kila uchao picha za wanawake eti wanakutaka au unatoka nao *DO U THINK NAMI NI WA AINA HIYO?* Usidharaulishe. Nadhani kuna busara ya wewe to look for another one but *AM NOT FOR U* and i hope utanipa heshima yangu kama dadaako, msanii mwenzako *LETS STOP THERE" Wema Sepetu
.
TOA MAONI YAKO HAPA

Baada ya Kuteuliwa Jana..Kitila Aweka Historia Hii Nchini..Chadema Watoa Tamko la Kumdhihaki..!!!

$
0
0

MSHAURI wa Chama cha ACT Wazalendo, Profesa Kitila Mkumbo, ametangaza kuachana na siasa na kuwa mtumishi wa umma kwa asilimia 100.

Jana Rais John Magufuli, alitangaza kufanya mabadiliko madogo katika safu ya Makatibu wakuu na kumteua Profesa Mkumbo kushika nafasi iliyoachwa wazi na Mhandisi Mbogo Mfutakamba, aliyekuwa Katibu Mkuu wa wizara ya Maji na Umwagiliaji.

Akizungumza na Nipashe kwa njia ya simu, Profesa Mkumbo alishukuru kwa uteuzi huo na kueleza kuwa unapopewa kazi na Mkuu wa nchi kinachopaswa ni kuwajibika kwa niaba yake.

“Nimeipokea kuwa ukipewa kazi na Mkuu wa nchi unaheshimu kazi, unaheshimu aliyekua kazi yake, unaifanya kwa bidii kadri Mungu alivyokujalia, name nitafanya hivyo,” alisema na kuongeza:

“Mimi ni mtumishi wa umma, kiutumishi rais ana mamlaka ya kuwatumia kwa kadri anavyoona, nadhani ameona nitaweza kutumikia kwenye nafasi hiyo, namshukuru Rais, Namshukuru Mungu, basi nakwenda kuitumikia,” alisema.

Kuacha siasa kwa asilimia 100

Mkumbo alipoulizwa juu ya kuwa na ‘damu’ ya siasa, alisema kuanzia sasa anasimamisha shughuli za kisiasa na kuwa mtumishi wa umma kwa asilimia 100.

“Mambo ya kisiasa kwa sasa itabidi yasimame, nimsaidie Mheshimiwa rais kuhakikisha nchi hii inapata maji  kama anavyotarajia na sera za serikali zilivyo,” alifafanua.

Aprili 17, mwaka jana, Mkumbo alikaririwa na vyombo vya habari kuwa “Huu utaratibu wa kuwateua wasomi tu ambao ni walimu na wanataaluma kutoka vyuo vikuu hasa Chuo Kikuu cha Dar es Salaam (UDSM) si mzuri maana rais haoneshi kuwaandaa wengine kuchukua nafasi zao, tuachwe wasomi tufanye kazi za kitafiti na kitaaluma.”

Alipoulizwa juu ya kuikosoa serikali alisema “Hoja yangu kubwa ilikuwa ni kwamba serikali inapoteuwa ni lazima iajiri, lazima kuwe na ‘replacement’.”

Kitila ambaye amewahi kuwa Mjumbe wa Kamati Kuu ya Chadema Taifa, alipoulizwa tafsiri ya uteuzi huo kwa upinzani, alisema “ni heshima kwamba mtu mmoja ambaye alikuwa mpinzani anateuliwa maana yake kuna wapinzani wenye sifa za kiutumishi.”

“Pia ni kumshukuru rais kuwa ana uwezo wa kuvuka mipaka, amevunja ile miiko kwamba ni lazima utoke chama flani. Mtu kama mimi amenipa mtihani lazima nikaishi kama mtumishi wa umma kama ambavyo taratibu na sheria zinazopaswa kuwa,” alibainisha.

Atakalosimamia

Alisema maji ndilo hitaji namba moja la Watanzania na kwamba atafanya kazi kwa bidii kuhakikisha wananchi wanapata maji kama inavyotakiwa.

Katika kundi la Whatsapp la ACT Habari, wanachama walihoji uongozi wa ACT jinsi walivyopokea uteuzi huo na kama Profesa Kitila ameupokea.

Afisa habari wa ACT wazalendo, Abdallah Khamisi, aliulizwa wameupokeaje uteuzi wa Profesa, alijibu “vuteni subira”

Mnyika: Imedhihirisha alikuwa mamluki

Mjumbe wa kamati Kuu ya Chadema, John Mnyika, alisema uteuzi wa Profesa Kitila kuwa sehemu ya serikali unadhirisha ilikuwa sahihi kufukuzwa Chadema.

“Huo uteuzi umedhihirisha maamuzi yaliyofanywa na kamati Kuu ya Chadema ya kumfukuza uanachama kutokana na usaliti yalikuwa ni sahihi, kwamba alikuwa anatumika na utawala,” alibainisha Mnyika.

Mwaka 2013, Profesa Kitila, aliyekuwa Naibu Katibu Mkuu, Zitto na Samson Mwigamba, walifukuzwa Chadema kwa madai ya kukiuka Katiba, sheria na kanuni za chama hicho.

Credit - Nipashe

Kisa Ujauzito Galatoni Ampiga Chini Linah..!!!

$
0
0

MWANAMUZIKI Ahmed Sadala a.k.a Galatone aliyewahi kutamba katika Tasnia ya Muziki wa Bongo Fleva na Wimbo wa Samaki amefunguka kuwa suala la mwanadada mrembo na Mwanamuziki Esterina Sanga ‘Linah’ kupata ujauzito limemkatisha tamaa kiasi cha kuamua kupiga chini harakati zake za kumnasa.

Akichonga na Uwazi Showbiz, Galatone alisema kuwa Linah alikuwa ni mwanamke wa ndoto zake na alikuwa amepanga kuzianza harakati za kummendea hivi karibuni lakini baada ya kugundua kuwa ni mjamzito imebidi kujiweka pembeni na kumfi kiria mwanamke mwingine atakayempenda kama Linah.

“Najilaumu mwenyewe kwa .uzembe wangu wa kusubiri kujitosa kwake nikiamini muda ulikuwa haujafi ka, lakini sina namna inabidi tu kujiweka pembeni maana tayari wajanja wamemuwahi na si rahisi kunikubalia na kumuacha anayekwenda kuwa baba wa mtoto wake,” alimaliza Galatone

Mambo ya Msingi 9 Chanzo JK Kutikisa Bunge..!!!

$
0
0


SHANGWE, nderemo na vifijo vilitanda kwenye ukumbi wa Bunge mjini Dodoma kwa takribani dakika 10 wakati Rais mstaafu wa awamu ya nne, Jakaya Kikwete alipohudhuria akiwa miongoni mwa wageni huku wabunge wakitaja mambo tisa kuwa chanzo cha kumshangilia sana kiongozi huyo wa zamani wa nchi.

Kikwete, maarufu kama JK, aliingia bungeni asubuhi kushuhudia kiapo cha mkewe, Mama Salima Kikwete, aliyeteuliwa kuwa mbunge na Rais John Magufuli Machi mosi, mwaka huu.

Katika kikao hicho cha kwanza cha mkutano wa saba wa Bunge la 11, JK aliingia ukumbini saa 2:50 asubuhi na kutoka saa 3:20 baada ya kile kilichoonekana kuwa ni kuzidi kwa shangwe zilizokuwa zinaelekezwa kwake na wabunge waliokuwa chini ya uongozi wa Spika Job Ndugai. Kwa kiasi kikubwa, hali hiyo ilionekana kuathiri utulivu na ratiba ya kikao hicho.

Udhibiti wa safari za nje unaofanywa na Serikali ya awamu ya tano tangu iingie madarakani na kuathiri pia ziara za mafunzo za wabunge; ukosefu wa kupungua kwa posho za vikao na pia madai ya kuingiliwa kwa kazi za kamati zao ni baadhi ya mambo yaliyotajwa na wabunge kuwa chanzo cha kushangiliwa sana JK, wakidai kukumbukia “neema” kadhaa wanazoamini kuwa sasa hawazipati kwa kiwango sawa na enzi za utawala wake wa awamu ya nne.

Baada ya kutoka ukumbini, JK alitumia dakika takribani tano kupiga picha na wabunge na watu mbalimbali waliokuwapo kwenye viwanja vya Bunge, kisha akaongozana na wasaidizi wake kuanza safari ya kutoka nje ya eneo hilo.

Kabla hajaingia kwenye gari, JK aliombwa kuongea na waandishi wa habari kuhusu kilichotokea bungeni lakini hakuwa tayari akisema: "Mimi si mbunge, siwezi kuzungumza hapa (bungeni)."

ILIVYOKUWA BUNGENI
Dalili za kushangiliwa kwa JK zilianza kuonekana mapema alipoingia ukumbini baada ya baadhi ya wabunge waliomuona kusikika wakisema 'tumekumiss JK' (tumekukumbuka JK).

Baada ya kupigwa kwa wimbo wa taifa na kuapishwa kwa Mama Salma, Spika Ndugai aliuliza kwa Katibu wa Bunge juu ya kinachofuata katika ratiba na kujibiwa kuwa ni kipindi cha maswali.

Hapo, Spika akasema kuwa kabla ya kipindi hicho kuanza, atambulishe kwanza wageni mashuhuri waliopo bungeni na ndipo akamtaja JK na kuamsha shangwe za wabunge zilizodumu takribani dakika 10.

Spika Ndugai alikiri kuwa haijawahi kutokea mgeni kushangiliwa kiasi hicho ndani ya chombo hicho cha kutunga sheria katika kipindi chote cha ubunge wake.

"Waheshimiwa wabunge, mimi binafsi hiki ni kipindi cha nne nikiwa bungeni… sijawahi kuona mgeni akipokelewa kwa kiwango hiki," alisema Ndugai.

Baadhi ya wabunge walisikika wakiomba JK aingizwe kwenye Ukumbi wa Bunge ili awasalimie huku Mbunge wa Kigoma Mjini (ACT - Wazalendo), Zitto Kabwe, akiomba fursa ya kupatiwa nafasi ya kutoa hoja kupitia 'utaratibu' wa Bunge, ambayo hakupatiwa, hata hivyo.

Baada ya kuona Bunge zima linashangilia, Spika Ndugai aliwataka wabunge kumpa heshima zaidi JK kwa kumshangilia wakiwa wamesimama.

"Kwa makofi hayo, sasa naomba mumpe 'standing ovation' (heshima wanayoitoa watu waliokuwa wamekaa kwa kusimama na kumshangilia mtu aliyefanya jambo muhimu)," alisema Ndugai.

WABUNGE WATAJA MAMBO 9
Wakielezea sababu ya kuwapo kwa shangwe hizo ambazo Spika Ndugai alikiri kuwa hajawahi kuzishuhudia hapo kabla, baadhi ya wabunge walitaja mambo tisa kwa nyakati tofauti.

Mosi, ni hali ya wabunge kukumbukia baadhi ya mambo wanayoamini kuwa yalikuwa mazuri enzi za JK lakini sasa hayapo. Mbunge wa Rombo, Joseph Selasini (Chadema), alisema kitendo cha JK kushangiliwa sana bungeni ndicho kinachoashiria jambo hilo.

"Haijawahi kutokea ndani ya Bunge mgeni kushangiliwa kiasi hiki.

Hii si mara ya kwanza marais wastaafu kuingia bungeni. Huu ni ujumbe kwa serikali iliyopo madarakani. Leo (jana) wabunge wamesema kwa vitendo kwa kumshangilia kupita kiasi rais aliyeondoka madarakani," alisema.

Aliongeza: "Kilichonishangaza kuliko vyote ni aina ya ushangiliaji. Wabunge wamepiga makofi, lakini pia wamesimama, na waliosimama ni mpaka Waziri Mkuu na mawaziri wengine.

"Na bado wametamka wazi kuwa wanaisoma namba, na wengine wanamwambia JK kwamba wamemkumbuka.
Ni ujumbe kwa serikali. Inapaswa kujitathimini. Na hawa si watu wa mtaani, ni wabunge,” alisema Selasini.

Pili, zuio la kurushwa moja kwa moja kwa matangazo ya Bunge kupitia vituo vya luninga. Hii ni sababu iliyotajwa pia na Selasini kuwa imesababisha wao kumkumbuka zaidi JK na kujihisi kuwa ‘wame-mmiss”.

" Kufunga Bunge 'live' ni tatizo, wabunge wanataka wanachokifanya bungeni kionekane kwa wananchi wao. Haya ni baadhi ya mambo yaliyofanya wabunge wamshangilie sana JK.

Aidha, Selasini alitaja jambo la tatu kuwa ni kucheleweshewa malipo yao na Serikali, jambo ambalo wakati wa JK lilikuwa nadra kutokea.

“Kuna wakati posho na mishahara inachelewa. Kipindi cha JK hatukuwahi kukosa pesa za uendeshaji wa Bunge," alisema Selasini.

Jambo la nne, kwa mujibu wa Mbunge wa Kigoma Mjini, Zitto Kabwe (ACT), ni hisia za kutokuwapo kwa uhuru wa kutosha wa kuzungumza na demokrasia kulinganisha na ilivyokuwa wakati wa JK.

"Kikwete alitumia muda wake wa uongozi kutoa uhuru kwa watu kusema watakacho, na hata waliokuwa wanamtukana, yeye alikuwa kama mzazi, hakuchukua hatua zozote.

Aliachia vyama vya upinzani vifanye siasa bila shida yoyote. Kwa hiyo, watu wamekumbuka hayo ambayo kwa sasa hayapo. Ndiyo maana wakamshangilia," alisema Zitto.

Jambo la tano, ni kutofuatwa kwa sheria ya bajeti. Mbunge wa Iringa Mjini, Mchungaji Peter Msigwa (Chadema), alidai kusuasua kwa serikali kutekeleza miradi ya maendeleo ndicho kiini cha JK kushangiliwa kwa mbwembwe bungeni.

"Serikali inakiuka sheria za nchi. Bajeti haijatekelezwa na kuna pesa zimetumika bila idhini ya Bunge…hatukuwa na bajeti ya kuhamia Dodoma. Sheria zinakiukwa waziwazi. Wakuu wa wilaya leo wana ving'ora," alisema Msigwa.

Jambo la sita, ambalo ni kwa mujibu wa Mbunge wa Nzega Mjini, Hussein Bashe (CCM), ni mchango ambao JK aliutoa katika kukuza siasa na demokrasia nchini, huku akiwataja baadhi ya wanasiasa walionufaika na hilo kuwa ni pamoja na yeye .

"JK ameshangilia kwa sababu wabunge wengi amewakuza kisiasa. Kina William Lukuvi (Waziri wa Ardhi, Nyumba naa Maendeleo ya Makazi) na hata mimi binafsi. Kipindi cha Kikwete ndiyo nilikua kisiasa.

Amewagusa wabunge wengi. Kama alivyosema Nay wa Mitego -- 'waliommiss' (waliomkumbuka) JK wapo, ndiyo kama wabunge," alisema Bashe.

Jambo la saba, ni udhibiti wa safari za nje. Mbunge wa Ukonga, Mwita Waitara (Chadema), alidai kuzuiwa kwa safari za nje za wabunge ni sababu mojawapo ya kushangiliwa sana JK kwa sababi enzi za utawala wake walipat fursa hizo.

Jambo la nane, ni hisia za baadhi ya wabunge kuwa Serikali ya sasa imekuwa ikiingulia majukumu ya Bunge mara kwa mara, na hasa kwa kuingilia utendaji wa kamati zake kiasi cha baadhi ya viongozi (wa kamati) kuamua kujiweka kando.

"Tumeshuhudia baadhi ya viongozi wa kamati za Bunge wanajiuzulu kutokana na serikali kuingilia majukumu yao…kitu kama hiki hakikuwahi kutokea kwenye uongozi wa JK, " alidai Waitara.

Sababu ya tisa, kwa mujibu wa Waitara, ni miradi iliyopitishwa katika bajeti kutotekelezwa ipasavyo.

“Miradi mingi iliyoidhinishwa na Bunge haijatekelezeka, imekwama. Bajeti imekwama halafu serikali inaongeza bajeti,” alisema na kuongeza:

"Kikwete ameshangiliwa kwa mapenzi ya dhati ya watu… kwamba ni mtu ambaye wanamkumbuka."

SABABU ZAIDI
Mbunge wa Welezo, Saada Mkuya Salum (CCM), alisema JK amepata mapokezi makubwa bungeni kutokana na mambo mazuri aliyoyafanya katika miaka 10 ya uongozi wake.

"JK alifanya makubwa sana kwa Tanzania kiuchumi na kuitangaza Tanzania kimataifa. Aliimarisha miundombinu ya barabara na viwanja vya ndege.

Watu wanakubali mchango wake katika taifa hili ni mkubwa na ndiyo maana ukaona wabunge wanamshangilia. Hicho ndicho kiliwatokea wabunge leo (jana)," alisema.

John Heche, Mbunge wa Tarime Vijijini (Chadema), alisema uhuru wa Bunge umeminywa hivi sasa na ndiyo mana JK alishangiliwa sana.

Mbunge wa Sumbawanga Mjini, Aeshi Hilaly (CCM), alisema JK ameshangiliwa na wabunge kwa sababu alikuwa kiongozi wao kwa miaka 10 na hilo ndiyo kubwa.

"Tulikuwa tumemkumbuka kwa sababu muda mwingi hatujawa naye… ni hulka ya binadamu unapoona na mtu ambaye ulikuwa haujamuona kwa kipindi kirefu, unafurahi kwa kiasi kikubwa," alisema Aeshi ambaye pia ni Makamu Mwenyekiti wa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Hesabu za Serikali (PAC) .

Mbunge wa Mbeya Mjini, Joseph Mbilinyi  (Chadema), alidai JK amepata mapokezi makubwa bungeni kutokana na mwenendo wa serikali ya sasa kutowaridhisha baadhi yao.

"Taifa limemkumbuka JK kwa sababu matarajio ya serikali ya awamu ya tano imewakatisha tamaa wananchi. Hakuna Sh. milioni 50 kila kijiji, hakuna mafisadi waliosimama kwenye mahakama ya mafisadi…kilichopo ni kamatakamata tu," alidai Sugu.

Mbunge wa Kilwa Kusini, Suleiman Bungala, maarufu Bwege' (CUF), alisema kushangiliwa kwa shangwe kwa JK bungeni jana kulitokana na kitendo cha Rais Mstaafu huyo kuenzi demokrasia katika uongozi wake.

"JK alikuwa mtu ambaye yuko tayari kukosolewa. Ndiyo kitu ambacho watu wanafurahi. Kwa hiyo hata leo (jana) bungeni wabunge walifurahi kuona mtu aliyeenzi demokrasia tofauti na hali ilivyo kwa sasa. Kikwete alikuwa kiongozi, sasa tuna utawala," alidai Bwege.

Mbunge wa Viti Maalumu Mkoa wa Njombe, Lucia Mlowe (Chadema), alidai wabunge walimshangilia JK kutokana na kuwapa uhuru katika uongozi wake.

Mbunge wa Vwawa, Japhet Hasunga (CCM) alisema JK alishangiliwa sana kwa sababu wananchi walimpenda na aliachia kila sehemu ikawa huru, tofauti na hali ya sasa.

Noma Sana..Baada ya Harmorapa Kuweka Wazi Hisia Zake kwa Wema Sepetu..Hili Ndio Jibu Alilojibiwa na Wema..!!!!

$
0
0

Acha hizo! Vituko vya Mbongo Fleva anayekuja kwa kasi nchini, Athumani Omar ’Harmorapa’ haviishi, juzikati tena, ameandika kwenye ukurasa wake wa Instagram akionesha hisia za mapenzi kwa Miss Tanzania 2006 aliye pia staa wa sinema za Bongo, Wema Sepetu huku Wema sasa akimbeza msanii huyo.

Harmorapa aliandika anavyomzimikia nyota huyo, akaanika urefu wa muda ambao alianza kumpenda kwamba ni kipindi anaingia kwenye ulimbwende na kutwaa taji.

Harmorapa alikwenda mbele zaidi kwa kutoboa siri hata alivyokosa raha pale, Wema alipokatwa jina kwenye kinyang’anyiro cha ubunge wa viti maalum kupitia Chama Cha Mapinduzi (CCM) Mkoa wa Singida, uchaguzi wa mwaka 2015.

Mwishowe, Harmorapa alisema yu tayari kuwa na Wema kimapenzi na ikitokea, atamvisha pete ya uchumba na kuwa wake sanjari na kumtunza kama wake. Soma hii:

“Napenda kusema ukweli ulio moyoni mwangu tangu siku nyingi ninavyosumbuliwa na hisia za kimapenzi kwa Wema Sepetu, tangu naanza kumfahamu na kumwona kwenye tv akigombea u-miss TZ, mwaka 2006, nilitokea kumpenda sana na kupata hisia za kumuoa, basi tu ndo’ vile nilikuwa sina uwezo wa kuonana naye wala kukutana naye kwa sababu ya nafasi niliyokuwa nayo enzi hizo nauza mapochi Mwenge.

“Nakumbuka kipindi kile, Wema wamemkata kwenye uchaguzi wa wabunge wa viti maalum niliumia hadi sikupata usingizi. Niliamka saa 9 usiku gheto na kuelekea Mwenge kuchukua mikoba ya kuiuza. Rafi ki yangu alinipa taarifa kuwa, Wema anaingia Dar kutokea Dodoma.

“Nilisema lazima nikampokee na zawadi nimpe, basi kwenye mikoba kule nilibahatika kupata mmoja mzuri sana, akili ikanijia kuwa ule nimpe zawadi Wema.

“Baadaye nikafunga goli ‘duka la biashara’ mapema, nikaenda kumpokea. Baada ya madam kufi ka nilihangaika sana ili nimfi kie nimpe zawadi ya mkoba, bahati mbaya niligongwa na bodaboda mguu wa kushoto na sikufanikiwa kumpa ila hadi leo mkoba ninao.

“Naombeni mumfi kishie taarifa hizi Wema, mwambieni nampenda sana endapo nitampata hatochukua hata wiki kwangu, n’tamvisha pete na kufunga naye ndoa na kumtunza kwa hali yoyote ile.”

Baada ya ujumbe huo, Uwazi lilimtafuta Wema na kumsomea mwanzo hadi mwisho, akasema: “Jamani! Harmorapa! Ila sasa hapo kwenye pete ya uchumba na kunitunza sina hakika miye.”

Wema alipoulizwa kwa nini hana hakika na eneo hilo tu, alishindwa kufafanua hali iliyotafsirika kuwa, maeneo mengine alikubaliana na msanii huyo kasoro kwenye umalizikiaji wake kwamba, Harmorapa hawezi kumvisha pete wala kumtunza yeye, pengine kwa kipato au ubahili wa msanii huyo kama amewahi kuusikia.

Akyanani..Mashabiki wa Simba Mkisikia Alichokisema Cannavaro ,,Lazima Mlie..!!!

$
0
0

NAHODHA wa Yanga, Nadir Haroub 'Cannavaro' amesema kasi waliyokuwa nayo kwa sasa hakuna timu ya kuwashusha tena kileleni mwa msimamo wa Ligi Kuu Bara.

Cannavaro, alisema watacheza kwa umakini mkubwa michezo yao iliyobaki na kuhakikisha hawapotezi pointi mpaka mwisho ili kutetea ubingwa wao.

"Kwanza tulitaka kukaa kileleni kwa sababu hakuna ubingwa bila kukaa kileleni..., tutahakikisha hatutoki tena kwenye uongozi wa ligi mpaka mechi yetu ya mwisho," alisema Cannavaro.

Aidha, alisema pamoja na kuwa kwa sasa Yanga inaongoza ligi, bado kuna ushindani mkubwa katika kuwania ubingwa msimu huu.

"Vita bado haijaisha…, huu ni mpira na lolote linaweza likatokea hivyo hatupaswi kujisahau," aliongezea kusema Cannavaro.

Aliwataka mashabiki wa timu hiyo kuendelea kuwasapoti na kuwatia moyo wachezaji wao ili kuhakikisha wanatetea ubingwa wao na kupata nafasi nyingine ya kuiwakilisha nchi kwenye mashindano ya kimataifa mwakani.

Yanga inaongoza ligi kwa tofauti ya pointi moja baada ya kufikisha pointi 56 ikifuatiwa na Simba yenye pointi 55.

Mr Ttouch Awajibu Wanaombeza Baada ya Kumsaini Young Dee ‘Subirini Muone Kazi

$
0
0

Mtayarishaji wa muziki wa Touchez Sound, Mr Ttouch amewataka wanaobeza uamuziki wake wa kumsaini rapa Young Dee kusibiri kuona ni nini atakifanya kwa rapa huyo machachari.

Akiongea katika kipindi cha eNewz cha EATV Jumanne hii, Mr. T Touchez amedai baada ya kutangaza kuwa amemsaini msanii huyo maneno yamekuwa mengi huku wengi wakimponda kuwa hawezi kufanya maajabu makubwa kwa sababu yeye siyo mtu wa kwanza kufanya kazi na msanii huyo.

“Kwanza ukiachana na mimi kumsaini D yule msanii ana historia kubwa kimuziki. Mimi hata kabla sijakutana alishawahi kuwa na kazi nzuri sana. Hata nilipoamua kufanya naye project nilijua huyu msanii siyo feki kwa hiyo nawaambia watu wa- relax” Alisema Touchez

Aidha Touchez ameongeza kwamba watanzania waendelee kumuamini kwani umebaki muda mfupi wa kuachia wimbo aliomtengenezea msanii huyo ambao ndiyo utakuwa majibu ya kuwafunga midomo watu wote.

Young D ambaye kwa sasa anatamba na ngoma za Furaha pamoja na Young Daddy, amepata usajili kwa Touchez Sound baada ya kutofautiana na meneja wake wa kwanza Max kutoka MDB kwa madai ya msanii huyo kurudi kwenye matumizi ya madawa ya kulevya.

Kunani? Wema Sepetu Nae Ahofia Usalama Wake

$
0
0

DAR ES SALAAM: Miss Tanzania 2016, ambaye pia ni muigizaji nyota, Wema Sepetu, amesema amepunguza matembezi na baadhi ya marafiki kwa sababu ya kuhofia usalama wake, hasa katika kipindi hiki cha mpito.
Uchunguzi uliofanywa na Risasi Mchanganyiko unaonyesha kuwa staa huyo mkubwa, ambaye wiki chache zilizopita alihama kutoka chama chake cha CCM na kujiunga na Chadema, haonekani kwenye matukio mengi ya kistaa katika maeneo mbalimbali ya Jiji la Dar es Salaam kama ilivyokuwa siku za nyuma.

Katika uchunguzi huo, ilibainika kuwa muigizaji huyo haonekani kwenye matukio kama kumbukumbu ya kuzaliwa, send off na hata kwenye kumbi za starehe kama ilivyokuwa, huku baadhi ya watu wake wa karibu wakisema hata simu yake, haipatikani kirahisi. “Kuna kitu naona hakiko sawa kwa Wema, sisi wenyewe tunashangaa maana tunajua yule ni mtu wa kujichanganya na marafiki, lakini pia anapenda kula bata, sasa ghafla tu ametoweka, hapatikani, tukimpigia wakati mwingine hapokei, yaani anatuchanganya kabisa,” alisema mtu wake huyo aliyeomba hifadhi ya jina lake.

Risasi Mchanganyiko lilimpigia staa huyo ili kupata maoni yake, lakini simu yake haikupatikana, jambo lililolifanya gazeti hili kumtembelea nyumbani kwake wiki iliyopita huko Ununio, nje kidogo ya jiji, ambako lilimkuta dada wa kazi, aliyedai kuwa bosi wake alikuwa ametoka na angeweza kupatikana jioni. Katika kujaribu tena simu yake, alipatikana na alipoulizwa kuhusu kupotea kwake, alisema; “Ni kweli, nimejipoteza katika macho ya watu, nahofia usalama wangu kwa sababu hali si nzuri, siyo tu nimepotea, lakini pia nawadelete (kuwafuta) baadhi ya marafiki, siyo unakuwa na marafiki wengi ambao hauna faida nao.

” “Hata katika kutoka, sitokitoki ovyo kama zamani, ni lazima nione kuwa mtoko huo una masilahi kwangu ndiyo natoka, siwezi kwenda sehemu ambayo haina faida na mimi katika wakati kama huu, kwa hiyo naomba uelewe kuwa hiyo ndiyo sababu ya mimi kutoonekana.” Wema Sepetu aliyekuwa miongoni mwa wasanii kutoka Bongo Muvi waliokipigia debe Chama Cha Mapinduzi (CCM), alikihama chama hicho muda mfupi baada ya kupandishwa mahakamani, akituhumiwa kutumia madawa ya kulevya, akiwa ni miongoni mwa wasanii wa kwanza kabisa kutajwa kwenye sakata la madawa ya kulevya na Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam, Paul Makonda.

VIDEO: ‘Sitaki Kushindana na Watoto, Msinishindanishe na Rosa Ree’ Chemical

$
0
0
Ni April 5, 2017 ambapo staa wa kike na Mwanafunzi kutoka UDSM, Chemical alifika kwenye studio za Millardayo na kueleza yale yanayozungumzwa mitandaoni kuhusu yeye na Rosa Ree.

Akizungumza na Millardayo.com & Ayo TV aliyaongea haya:
Unajua lazima watu waongea kama mimi nilikuwa nafanya muziki wa Hip Hop ila pale anapotokea mtu basi utasikia mengi, kwahiyo watu wasitumie nguvu nyingi ya kunifananisha na mtu fulani, sitaki ku battle battle na watoto kila mtu ana ladha ya kile anachokitoa mimi nina ladha zangu na Rosa Ree ana ladha zake’- Chemical

Unaweza ukabonyeza play kumsikiliza Chemical kwa wanaosema Rosa Ree kampoteza kwenye muziki:

Source:Millard Ayo

Prof. Kitila Mkumbo Atoa Neno Kwa Rais Baada ya Kuapishwa...Msikie Hapa

$
0
0
Prof. Kitila amesema katika maisha yake ametumia muda mwingi kuihoji serikali lakini kwa sasa Rais amempa kazi ya kujibu alichokuwa anakihoji serikalini.

''Ukipewa kazi na Mkuu wa Nchi unashukuru Mungu na jukumu langu ni kufanya kazi kwa bidii. Ninaahidi nitakusaidia wewe na Mweshimiwa Waziri wa Wizara ya Maji na Umwagiliaji kuhakikisha kwamba ajenda yako ya kuwafikia Watanzania na kuwaboreshea maisha tunaifanikisha'' Prof. Kitila Alisema.

VIDEO:

Rasmi..Kundi la Vichekesho la Orijino Komedi Lasambaratika..Chanzo Chadaiwa Kuwa ni Mpoki..!!!!

$
0
0

 Hatimaye kundi la vichekesho lililojipatia umaarufu mkubwa nchini la Orijino Komedi, limefikia mwisho kwa kusambaratika, huku chanzo kikidaiwa kuwa ni mmoja wa memba wake mwenye mbwembwe nyingi, Silvery Mujuni, maarufu kama Mpoki a.k.a Mwarabu wa Dubai, Risasi Mchanganyiko limenyetishiwa.

Kwa mujibu wa chanzo kilicho karibu na kundi hilo ambalo halijarusha kazi zake hewani kwa muda mrefu sasa, limeingia katika hatua hiyo, baada ya mmoja wa memba wake, kukiuka makubaliano, kitu kilichosababisha wote waamue kufanya mambo kivyao.

Inadaiwa kuwa hapo awali, kulikuwa na maazimio ya kila mmoja kuleta kundini, makubaliano yoyote ya kazi kibiashara ili mapato yatakayopatikana, wagawane wote.

“Walijua kuwa kazi zao kama kundi ziliwavutia kampuni na mashirika, lakini wakafahamu pia kuwa wakati mwingine siyo rahisi kundi kuingia mikataba, kwamba wapo ambao wangeweza kuvutiwa na mmoja wao, hivyo ikitokea namna hiyo, basi aliyepata dili hilo, alilete kundini, ambako yeye atapewa asilimia kubwa, huku wenzake nao wakipata kidogokidogo,” kilisema chanzo hicho.

Chanzo hicho kikaongeza kuwa, utaratibu ukawa ni huo na kila kitu kikaonekana kwenda vizuri, hadi Mpoki alipokuja ‘kutibua’ baada ya kupata dili kutoka kampuni moja ya simu, lakini kwa mshangao wa wenzake, hakupeleka kundini makubaliano yake.

“Watu walishtukia tu tangazo linaruka hewani, alipoulizwa imekuaje, akawa haeleweki, ndipo wenzake nao wakaamua kila mmoja kufanya kivyake na hapo ndipo kutokuelewana kukatokea,” kilisema chanzo hicho.

Baada ya kupata ubuyu huo, Risasi Mchanganyiko lilimtafuta Mpoki, ambaye kwa sasa ni mtangazaji katika Kituo cha Redio cha EFM, ambapo baada ya kuelezwa kuhusu tuhuma hizo, alihoji;

“Hayo maneno kakuambia nani? Pale kwenye kundi letu tupo wengi au wao ndiyo wamekuambia? Mimi siwezi kujibu hiyo kitu na huwezi kunilazimisha kujibu.”

Risasi Mchanganyiko pia lilijaribu kuwafikia wanakikundi wengine ili kupata ukweli wa habari hizo na safari hii, walimtafuta Lucas Lazaro Mhuvile, anayefahamikazai di kama Joti, ambaye baada ya kuulizwa kuhusu kilichotokea  kwenye kundi lao, mahojiano na mwandishi yalikuwa kama ifuatavyo;

Joti: Lazima uniambie kwanza ni nani aliyekuambia habari hizo.

Mwandishi: Lakini maadili ya kazi yetu hayaruhusu mimi kutaja chanzo changu, nadhani wewe ungejibu tu vile unavyojua juu ya jambo hilo.

Joti: Mimi siyo mwandishi, ninachotaka utuite mimi na yeye aliyekuambia hizi habari, tukae tuambizane vinginevyo siwezi kukujibu kwamba ni kweli au siyo kweli.

Gazeti hili lilimfikia pia mchekeshaji mwingine maarufu wa kundi hilo, Isaya Mwakilasa ‘Wakuvanga’ ambaye baada ya kuelezwa kusudio la kupigiwa simu, alisema hivi; “Unataka nikupe habari hovyohovyo au unataka nikupe kitu kizuri uandike? (Mwandishi alipomweleza kuwa anahitaji kitu kizuri, akamwambia), basi nitafute wakati mwingine kwa sababu hivi sasa nipo katika kazi muhimu.”

Emmanuel Mgaya ‘Masanja Mkandamizaji’ hakupokea simu yake licha ya kupigiwa mara kadhaa na hata ujumbe mfupi wa simu hakujibu, kama ilivyokuwa kwa Mark Regan.

Hata hivyo, kiongozi wa kundi hilo, Sekioni David, maarufu kama Seki, alizungumza na Risasi Mchanganyiko .

“Kundi bado lipo ila kwa sasa liko mapumzikoni. Unajua, shoo ya mwisho tulifanya Septemba 2015, baada ya pale tukaingia katika kampeni, ila kazi ni ngumu na pia tokea tumeanza, hatukuwahi kupumzika, watu wanatakiwa wapumzike ili wapate ubunifu mpya.

“Kifupi ni kuwa tupo likizo tangu ile 2015, nadhani tutaendelea mwishoni mwa mwaka huu, kwa hiyo mwakani kundi linarejea barabarani kama kawaida, hiyo habari kuwa tumesambaratika siyo kweli, hivi sasa watu wako mashambani wanashughulika na kilimo.”

Kaseja Atoa ya Moyoni Baada ya Tetesi za Kutaka Kurudi Simba Kuzidi Kusambaa Mjini..!!!

$
0
0

KIPA namba moja wa Kagera Sugar, Juma Kaseja, ametamka kuwa maisha yake anategemea soka, hivyo hatasita kurejea kuichezea klabu yake ya zamani ya Simba kama ikimhitaji.

Kauli hiyo, aliitoa hivi karibuni mara baada ya kumalizika kwa mechi ya Ligi Kuu Bara dhidi ya Simba iliyopigwa wikiendi iliyopita kwenye Uwanja wa Kaitaba, Kagera, matokeo yaliyomalizika kwa Kagera Sugar kushinda mabao 2-1.

Kipa huyo aliwahi kuichezea Simba na kuipa mataji kadhaa akiwa kama nahodha mkuu wa timu hiyo kabla ya kutimkia Yanga, Mbeya City na hivi sasa Kagera.

Akizungumza na Championi Jumatano, Kaseja alisema umri wake wa kustaafu kucheza soka bado, hivyo basi ataendelea kucheza hadi pale atakapoona ni muda mwafaka kwake kustaafu.

Kaseja alisema anashangazwa na maneno ya mashabiki wa soka wanaodai yeye ni mzee lakini hivi sasa ni tegemeo na mwezi Januari, mwaka huu alichaguliwa kuwa mchezaji bora wa mwezi.

“Bila ya kuwa mvumilivu basi ningepotea kwenye soka muda mrefu kutokana na maneno ya mashabiki, lakini nilijitahidi kuyaweka kando maneno yao na badala yake kupiga kazi ambayo leo hii naonekana kijana.

“Kama unakumbuka niliwahi kuitwa mzee, nauza mechi lakini kama ningekuwa ninauza mechi, basi ningewauzia hao Simba tuliocheza nao katika mechi hiyo ili wapate ushindi, maana si walikuwa wanataka ushindi ili wachukue ubingwa.

“Nikwambie tu, soka halipo hivyo kama wanavyofikiri, mimi maisha yangu ninayaendesha kwa ajili ya soka, na kuhusiana na taarifa za kurudi, mimi sina tatizo, hiyo ndiyo ajira yangu Simba wakinitaka narudi tu,” alisema Kaseja.

Hans Pope Afunguka Haya Kuhusu Kumsajili Kaseja Simba..!!!

$
0
0

Mwenyekiti wa Kamati ya Usajili ya Simba, Zacharia Hans Poppe, amesema kiwango kilichoonyeshwa na aliyekuwa kipa wao, Juma Kaseja ambaye kwa sasa anaichezea Kagera Sugar, ni cha kawaida na kudai kuwa hajaona cha ziada kwake.

Simba ilipoteza mchezo wake wa Jumapili dhidi ya Kagera Sugar na kujikuta ikiwa nafasi ya pili ya msimamo wa ligi kwa kuwa na pointi 55 nyuma ya Yanga yenye pointi 56, huku kipa Kaseja akionekana kuwa kikwazo kutokana na umahiri ambao aliuonyesha uwanjani.

Hans Poppe alifunguka kuwa, kiwango kilichoonyeshwa na Kaseja katika mechi dhidi ya Kagera ni cha kawaida kama alivyokuwa akicheza katika timu yao na kudai kuwa hakuona cha ziada kutoka kwake.

“Ndiyo Kaseja alikuwa mchezaji wetu na aliondoka katika timu yetu miaka kadhaa iliyopita, vilevile amecheza katika timu mbalimbali, kwa upande wangu naona kiwango ambacho amekionyesha katika mechi dhidi ya Kagera ni cha kawaida kama vilevile alivyokuwa akicheza alipokuwa Simba na sijaona cha ziada kutoka kwake, anacheza kama ilivyo kwa makipa wengine.

“Wachezaji wengi wamekuwa wakiondoka na wanaonyesha viwango vya kawaida lakini mwisho wa siku Simba inabakia kuwa ileile,” alisema Hans Poppe.

Nafasi Zingine za Ajira Zilizotangazwa Jioni ya Leo...Zisome Hapa


Siku Chache Baada ya Kukimbia Bastola kwa Nape, Hamorapa Anusa Kifo..!!!!

$
0
0

Chuki! Zikiwa zimepita siku chache baada ya msanii chipukizi wa Bongo Fleva lakini mwenye matukio mengi, Athuman Omary maarufu kama Harmorapa, kukimbia baada ya kushuhudia mtu asiyefahamika akichomoa bastola na kumwelekezea Mbunge wa Mtama, Nape Nnauye katika Viwanja vya Hoteli ya Protea, Oysterbay jijini Dar es Salaam, mwishoni mwa wiki iliyopita alinusurika kifo, baada ya kijana mmoja kumtu pia chupa iliyojaa bia akimlenga kichwani lakini ikamkosa, wakati akifanya shoo kwenye Ukumbi wa Maisha Basement, Kijitonyama.

HALI ILIKUAJE KWANI?

Dayna Nyange , mmoja wa wasanii wanaofanya vizuri katika Bongo Fleva, alikuwa ameandaa shoo yake ndani ya ukumbi huo akiipachika jina la Usiku wa Komela na Harmorapa alikuwa mmoja wa wasanii waalikwa.

Harmorapa ambaye amejipatia jina kubwa ghafla, baada ya kufanana kwa kiasi kikubwa kimuonekano na chipukizi mwingine kutoka Kundi la WCB, Abdulhan Rajab ‘Harmonize’, alikuwa ndiye msanii ‘mwenye jina kubwa’ baada ya Dayna Nyange, wengine wakiwa ni ma-underground.

SAA TISA KAMILI USIKU Kwa kawaida, ndani ya ukumbi huo wa burudani, huwa na matukio mengi ya kiburu
dani na katika shoo kama ya siku hiyo, huanza baada ya saa nane usiku, ambako wasanii wakubwa huanza kutumbuiza. Jumapili, saa tisa usiku, wakati shoo ya Komela, ikiwa imeanza, muda wa Harmorapa kupanda uliwadia, akiwa katika shoo akitumbuiza na wimbo wake unaotamba hivi sasa wa Kiboko ya Mabishoo, tukio la kusikitisha likajitokeza.

HIKI NDICHO KILICHOMPONZA HARMORAPA

Katika kibao hicho cha Kiboko ya Mabishoo, baadhi ya
mashairi yake yanasema… ”Tulikuwa wasafi kabla ya WCB, maneno yao machafu hayanivunjii sivi…,” Maneno hayo yalionekana kumkera kijana mmoja aliyekuwa miongoni mwa mashabiki, ambaye bila kujali athari amba zozingetokea aliinua chupa iliyojaa bia, iliyokuwa  haijafunguliwa na kumlenga msanii huyo, ambaye hata hivyo, akiwa hajui hili wala lile, alishtukia kishindo kikubwa cha mlio wa chupa iliyopasuka.

TAHARUKI UKUMBINI

Kishindo hicho cha chupa kiliibua taharuki kubwa ukumbini, huku muziki ukizimwa kwa muda na Harmorapa, aliyekuwa kama aliyechanganyikiwa kwa kutojua nini kilichoendelea, alichukuliwa haraka ukumbini na kwenda kuwekwa sehemu salama.


Wakati hayo yakitokea, walinzi wa ukumbi huo nao walimuwahi kijana huyo ambaye jina lake halikupatikana mara moja na kumpeleka eneo salama zaidi kwao, akiwa chini ya ulinzi lakini hata hivyo, mashabiki waliojawa na hasira, walishindwa kuvumilia na kuamua kumpa kipigo kikali, kilichomuacha na majeraha kadhaa, hasa mdomoni.

Kuona hivyo, walinzi wa ukumbi huo walimchukua kijana huyo na kumpakiza kwenye gari na kumkimbiza katika Kituo cha Polisi cha Kijitonyama, maarufu kama Mabatini, ambako baadaye, Harmorapa na meneja wake, Irene Sabuka pia walikwenda kutoa ushahidi.

MSIKILIZE MENEJA WA HARMORAPA

Irene akizungumza wakati akiwa kituoni hapo, aliliambia Risasi Mchanganyiko, kuwa amesikitishwa na kitendo hicho kwani hajui kwa nini watu wanaumizwa na harakati za kijana huyo mdogo, anayejitafutia maisha kama wao walivyoanza kutoka kimuziki.

“Ninachokiona hapa ni chuki tu ambazo hazina maana, watu wanaonekana wanakereka sana kumuona huyu kijana akifanya vizuri, wangemuacha tu na yeye ajitafutie maisha yake kwa sababu kila mmoja alianza hivihivi.”

Kwa upande wake, Harmorapa alisema kitendo hicho kilimuumiza sana, lakini hajavunjika moyo, atakaza buti kuliko zamani hadi kieleweke.

“Kitendo kile kilinishtua, sikutegemea kama kingetokea, kilinitoa katika mudi kabisa, hata hivyo hakiwezi kunifanya nikate tamaa maana bado niko ‘strong’ na kama hawajui basi ni kuwa wananiongezea ari ya kupambana zaidi,” alisema.

Duh,,Noma Sana..Nuh Mziwanda Afunguka Jinsi Alivyobadili Dini Kisa Mwanamke..!!!

$
0
0

MUZIKI wa Bongo Fleva, umekuwa ukipanda kwa kasi ya hali ya juu sana kwa siku za hivi karibuni. Kila msanii amekuwa akifanya ubunifu wake ili kuhakikisha anakwenda juu na kujikusanyia mashabiki wengi kadiri siku zinavyozidi kusonga. Umaarufu wa msanii yeyote yule unakuja kutokana na kazi bora ambazo amekuwa akifanya kwa ubunifu wa hali ya juu.

Pamoja na Tanzania kuwa na wasanii wengi, lakini kuna msanii anaitwa Nuh Mziwanda ambaye nyimbo zake za hivi karibuni zimekuwa zikiteka masikio ya watu wengi kwa kasi ya hali ya juu.

Pamoja na kutanua na wimbo wa Jike Shupa, ambao ulifanya vizuri sana mwishoni mwa mwaka jana na mwanzoni mwa mwaka huu, sasa Nuh amerejea na wimbo mwingine unaoitwa Anameremeta.

Huu ni wimbo ambao watu wengi wamekuwa wakiufurahia kwa jinsi midundo yake ilivyo na aina ya ubunifu uliotumika.

Championi limefanya mahojiano na Nuh, ambapo msanii huyo amefunguka mambo mengi ikiwemo uhusiano wake na Ali Kiba, mke wake, maisha ya ndoa na mwenendo mzima wa muziki wa kisasa.

“Watu wengi wamekuwa wakishindwa kunielewa vyema, lakini mimi sikuanza kama mwanamuziki, nilikuwa prodyuza wa nyimbo za Kwaya.

“Huko ndiko nilipoanzia na kupatia umaarufu, wanakwaya, vikundi na hata viongozi wa makanisa wengi wakanifahamu kutokana na kazi hii.

“Nimelelewa kwenye dini kali sana ya Kikristo, baba yangu alikuwa anapiga kinanda kwenye Kanisa la Kiinjili la Kilutheri, Usharika wa Kariakoo, mama yangu ni mwimba kwaya kwenye kanisa hilohilo, hapa utaona ni jinsi gani kwetu dini imetawala.

“Nimefanya kazi huko kwa muda mrefu sana, baadaye nikahamia Sinza, nakumbuka ofisi ilikuwa Sinza Palestina, lakini baadaye nikawaomba wazazi wangu niingie kwenye kuimba mwenyewe.

“Walijua labda nataka kuimba gospo, lakini nilipowaeleza ni Bongo Fleva waligoma, nikawaomba sana baadaye wakakubali, wimbo wangu wa kwanza ulikuwa wa rapu ambao uliitwa Bwege Mtozeni, huu haukufanya vizuri hata kidogo.

Nikaachana na kurapu na kutoa wimbo mwingine uliojulikana kwa jina la Filling Love, nao haukufanya vizuri pia,” anasema Nuh huku akicheka.

Mwanamuziki huyo ambaye anaishi kwenye jumba la ghorofa eneo la Ubungo External, anasema baada ya hapo alimtafuta rafi ki yake wa muda mrefu, Ali Kiba na kufanya naye kolabo ya wimbo wake unaoitwa Mniache.

“Unajua watu wengi wanafi kiri kuwa mimi na Ali tumejuana kwenye Jike Shupa, hapana hata kidogo, mimi nimekuwa na Ali kama mtu na kaka yake, nilianza kuimba naye tukiwa chini sana na nimekuwa nikimheshimu naye ananisheshimu.

“Wimbo wangu wa tatu unaoitwa Mniache, niliimba naye na hata leo nikitaka kuimba na Ali wala situmii nguvu kubwa, namwambia tu naomba nikushirikishe kwenye wimbo wangu, najua hawezi kukataa, hapo biashara inaisha.

“Nikipata shida hapa nampigia Ali namwambia nimepata shida f’lani na baada ya dakika tano unamuona mlangoni, huyu mimi ni kaka yangu siyo kwamba tumejua leo wala jana.

“Hata wimbo wa Jike Shupa, yeye ndiye aliupa jina, nilikuwa nimeupa jina lingine kabisa, lakini tulipokwenda studio wakati anaweka sauti akaniambia huu wimbo uitwe Jike Shupa, sikubisha.”

Nuh ambaye mke wake amejifungua hivi karibuni, anaendelea kuzungumza kwa kusema halikuwa jambo rahisi kwake kuoa kwani alipita kwenye wakati mgumu sana.

“Kila mtu alifi kiri kuwa nitamuoa Shilole kutokana na ukaribu wetu, ni kweli tulipendana na mwenzangu alikuwa tayari kubadili dini ili tufunge ndoa ya Kikristo, lakini ndiyo hivyo Mungu hakupenda, nikamuoa Nawal.

“Kumuoa huyu binti, dah! (anacheka) ilikuwa kazi ngumu sana, lakini mimi nitumike kama njia ya kuwashauri vijana wenzangu kuwa siyo kila mwanamke unaweza kumchezea chezea, wengine utalazimika kumuona tu.

“Tazama, mimi ni Mkristo safi  kama nilivyosema hapo awali, baba mpiga kinanda, mama mwimba kwaya, lakini nimebadilisha dini kwa sasa mimi ni Muislam kwa ajili ya mke wangu (anacheka tena).

“Huyu bibie katika uhusiano wetu alipata mimba kabla ya ndoa, sasa nilikula mikwara sana, wazazi wake ni Waarabu, baba yake alijua kuwa mimi ni mwanamuziki, ukweli ni kwamba alinitisha, ndugu zake wakanitisha hata mambo mengine siwezi kuyasema sasa, mpaka wazazi wangu wakanionea huruma na kuniruhusu kumuoa Kiislamu, nilibadilishwa jina nikaitwa Nurdin,” anasema staa huyo na kuendelea.

“Lakini maisha ya sasa najua mwenyewe, kama nakwenda msikitini au kanisani kwa kuwa hakuna anayenifuatilia ingawa nina mke wangu ndani na maisha yetu yanakwenda vizuri sana kama unavyoona nimemtuma dogo pampers kwa ajili ya mwanangu mwenye wiki mbili sasa.”

Kuhusu Shilole mara kwa mara kudaiwa kuwa na uhusiano naye wakati tayari ana ndoa yake, Nuh anakanusha hilo na kusema kuwa yeye na msanii huyo wanafanya kazi tu kwa sasa, lakini mapenzi hakuna.

“Unajua hata mke wangu mwanzoni alikuwa akifi kiri kuwa naweza kuwa na uhusiano na Shilole hadi akawa anakuja kwenye kila shoo ninayofanya, lakini baadaye alielewa kuwa ni uhusiano wa muziki tu.

“Waandaaji wengi wa shoo wanaamini kuwa wakiniweka na Shilole wanapata watu wengi, sasa nami nataka mkwanja siwezi kugoma kwenda sehemu alipo, lakini tukishamaliza shoo kila mtu na hamsini zake, hakuna uhusiano wa kimapenzi tena, ile ilikuwa zamani,” anasema Nuh anayemiliki studio ya Last Bon Records.

Imefichuka..Hii Ndio Sababu Kuu ya Kwanini Mtu Anakuwa na Kitambi..!!!

$
0
0

MIONGONI mwa maswali ya wasomaji wetu ni juu ya watu ambao wametumia njia mbalimbali ili kuondoa uzito au unene kupita kiasi bila mafanikio. Leo tutajadili hilo.

Unene kupita kiasi ni nini? Haya ni mafuta yaliyozidi kuzunguka eneo la tumbo na sehemu nyingine za mwili. Unaweza kutokea kwa watoto, vijana na watu wazima hata wazee wa jinsia zote. Mwili wa binadamu una seli bilioni 50-200 za mafuta zilizogawanyika kwenye mwili wa binadamu.

Kwa wanawake zipo sana maeneo ya matiti, nyonga (hips), kiuno na kwenye makalio. Kwa wanaume seli zipo sana kwenye kifua, tumboni na kwenye makalio. Mafuta ya tumbo yanayofanya kitambi hukusanywa kwa njia kuu mbili, ya kwanza ni mafuta kutoka kwenye tishu zilizo chini ya ngozi na ya pili ni kutoka kwenye ogani za ndani kama moyo na kongosho.

Sababu kubwa ya unene ni kukosekana ulingano wa nguvu (kalori) kama vile mtu kula vyakula vinavyotia nguvu sana kuliko jinsi anavyoweza kutumia na kutoa kama taka mwili.

Sababu zingine ni kuwa na chembe za urithi za unene kutoka kwa wazazi. Kuna sababu za kimazingira na nyingine zisizojulikana. Vitu kama kukosa usingizi na sababu nyingine zinachangia kuendelea kuwepo kwa unene au kitambi ambacho kinaweza kuashiria maradhi ya moyo, kisukari na baadhi ya magonjwa ya saratani.

Mchanganuo wa sababu 10 zinazofanya mtu kuendelea kuwa mnene au kitambi: 1.Kadiri unavyozeeka, mwili wako unabadili jinsi unavyo ongezeka na kupunguza uzito. Jinsi zote; za kike na kiume, hupatwa na kupungua kwa utendaji wa kimetaboliki, kutia ndani kiasi cha kalori zinazohitajika kwa mwili kufanya kazi kwa ukawaida.

Zaidi ya hayo wanawake hupatwa na kukoma kwa hedhi, ikiwa wanawake wataongezeka uzito, mara nyingi uzito huo huwa kwenye matumbo yao.

Wakati wa kukoma kwa hedhi, uzalishaji wa homoni za Istrojeni na Projesteroni hupungua. Wakati huo huo homoni ya Testosteroni huanza kupungua kidogo kidogo.

Mabadiliko ya homoni hufanya wanawake wengi kuendelea kubeba uzito mwingi kwenye matumbo yao. 2. Kutofanya mazoezi kwa usahihi. Mazoezi ya kulala chali na kuinua mwili kuanzia kiuno hadi kichwa Crunches siyo mazoezi yatakayokusaidia kuondoa unene au kitambi. Badala yake fanya mazoezi ya stamina yatakayo kufanya utumie nyama Muscles za tumbo, mgongo, nyonga na
sehemu zingine za mwili.

Kufanya mazoezi ya namna hii kutasaidia kuunguza/ kutumia kalori nyingi mwilini na hivyo kufanya mafuta yaliyo maeneo ya tumbo kutumika pia. Mazoezi ya kukaa kwa muda jinsi fulani kama unapiga pushapu kitaalamu hujulikana kama Plunk , ndiyo mazoezi yanayofaa kwa kuwa huhusisha matumizi ya nyama za mikono, miguu na makalio.

Kukimbia kila siku ni mazoezi bora kwa mwili na moyo wako ingawa mazoezi kwa ajili ya moyo wenye afya peke yake hayawezi kusaidia maeneo ya kiunoni na kutoa kitambi.

Umuhimu wa Kufika Kieleleni Wakati wa Kumega Tunda..!!!

$
0
0

KUNA kitu kimoja tu ambacho Susan* anatamani maishani mwake. Sio pesa, sio gari wala si vipondozi, bali ni kupata burudani tosha la mapenzi.

Anasema maishani mwake, hajawahi kufikia kilele cha tendo ndoa hata mara moja.

 “Sijawahi kufikia kilele cha tendo la ndoa. Kwangu shughuli ni shughuli tu. Ninavumilia tu kwa sababu nampenda mpenzi wangu kwa dhati,” asema Bi Susan na kuongeza kuwa wakati mwingine anachukia tendo hili ili asiache kwenye njia panda.

Ili kuhakikisha kwamba kamwe havujiki moyo wakati wa shughuli, wataalamu wanasema Susan anaweza kutumia mbinu za kisasa za kufanya mapenzi.

Wanasema imegunduliwa kwamba kwa kubadilisha staili za kula uroda wachumba wanaweza kuridhishana kikamilifu na kufikia kilele cha shughuli hii muhimu.

“Kwa kutumia staili tofauti za kulishana uroda wachumba huridhishana kikamilifu,” asema mwanasaikolojia Kathy David.

Wataalamu wengi wa mapenzi wanakubaliana kwamba wachumba wanapotumia mbinu tofauti za kuburudishana kitandani, wanaridhishana na wanawake wanafikia kilele cha tendo la ndoa.
Kulingana na mwanasaikolojia Bi David aliye pia mwandishi wa vitabu vya mapenzi wachumba wanaotumia ubunifu wakati wa burudani kitandani wanaridhishana vilivyo.

Bi David asema sio siri kwamba wanaume wengi wamekuwa wakiwapoteza wachumba wao kwa kukosa kuwaridhisha kitandani.

“ Ni kweli watu wengi na hasa wanaume  wamekuwa wakiwapoteza wachumba wao wa kukosa kuwapagawisha wakati wa tendo la ndoa.

 Hata hivyo wanaotumia ubunifu na kutumia staili tofauti huwa hawana tatizo lolote,” asema na kuongeza kuwa  utaalamu wa kurushana roho  ndio msingi wa ndoa na uchumba wowote ule.
Bi David asema wachumba wanapasa kuwa wakibadilisha mbinu ili kufanya penzi kunoga na kupatiana  shibe la burudani.

Anasema ubunifu na staili  tofauti za kurushana roho huongeza ladha tendo la ndoa.

“Unaweza kutia nakshi burudani faraghani kwa kutumia mitindo mbalimbali ya kula uroda inayoendelea kuvumbuliwa  kila siku,”asema na kuongeza kuwa kizazi  cha wakati huu hakiridhishwi  na mitindo ya zamani wanayosema imepitwa na wakati.

“Hizi sio nyakati ambazo mwanamke alikuwa akilala chali na kusubiri mwanaume apande juu  yake. Kila mmoja ana wajibu wa kuchangia kufanikisha  tendo la ndoa,” asema.

Kulingana na Bi David mwanamke anaweza kumfanya mwanaume alipuke kwa raha kwa kuwa juu yake na kumwongoza  akiwa nahodha  wa mechi kitandani.

“Mwanamke anaweza kuchukua usukani  na kuwa nahodha wa mechi na kumfanya mchumba wake kuridima kwa raha  ya ajabu. Na kwa sababu nahodha uelewa na kufahamu mechi vilivyo, ushindi lazima upatikane,” asema.

Anaeleza kwamba wanawake  wanaojua kuwaelekeza  mwanamume  wanapocheza rumba kitandani  huwapagawisha  kimapenzi.

 “Muulize mchumba wako kinachomtia kichaa mnapolishana  asali. Mwelekeze ipasavyo huku ukiwasiliana na hisia zako mnapoelea katika bahari ya mahaba ,” asema.

Wataalamu wa mahaba wanasema watu wengi hukosa kuwafikisha  wachumba wao katika kilele cha mapenzi kwa kutojiwachilia wakati wa tendo la ndoa tatizo  ambalo baadhi ya mitindo ya kisasa inalenga kutatua.

 Kulingana na Bi Libby Keatinge mwanasailokojia  mwenye uzoefu mkubwa wa maswala ya mapenzi, ni muhimu kujiwachilia ili kupata matokeo bora ya raha wakati wa kulishana tunda.
Anasema ulaji uroda hufanikiwa ipasavyo ikiwa kuna  mawasiliano ya mwili na akili. Bi keatinge asema baadhi ya staili za kisasa za kufanya mapenzi zimenuiwa kuimarisha hali hiyo.

“Unaweza kubadilisha maisha yako ya mapenzi kwa  kuchagua baadhi ya mbinu ambazo wataalamu wamevumbua ili kupamba burudani na mchumba wako.”asema.

Kwenye kitabu Discovering Erotic Sex,  Bi Keatinge anaorodhesha  baadhi ya mitindo iliyothibitishwa kukata kiu cha penzi cha wanaoitumia.

Anasema mitindo hiyo humpatia mwanamke  fursa ya kutawala wakati wa kucheza goma kitandani na mpenzi wake.  Hata hivyo mtaalamu huyu asema sio staili zote za kisasa  zinawafanya  vidosho  kuwa rubani wa ndege ya mapenzi.

“Staili za kisasa  zimebuniwa ili kuleta usawa na kuhakikisha kila mmoja ametawala uwanja kwa awamu tofauti. Itatengemea aina ya mtindo na eneo la kusakatia goma,” asema.
Kusimama

Wataalamu wanakubaliana kwamba mawasiliano ya kihisi, kimwili na kiakili ndio msingi wa kufanikisha  tendo la ndoa.

“Mnaweza kufanya mapenzi mkisimama, mkiinama mkichuchumaa, kwenye bafu,sakafuni kwenye zulia, mezani  kwenye kochi na hata ndani  ya gari. Hizi zote ni staili na maeneo ya kufanyia mapenzi. Hata hivyo cha muhimu ni mawasiliano kati ya mwili, akili na hisia zako  zitakazokupeleka katika kilele cha tendo lenyewe,” asema.

Bi David asema mazingira ya kusakatia mechi pia huchangia  kufanikiwa kwa staili yoyote ya kufanya mapenzi. “ Ikiwa unatumia mbinu yoyote ya  kufanya mapenzi katika mazingira yasiyofaa  ni vigumu kufikia kilele cha mlima wa ashiki,” asema katika makala yake kwa jina 5 things men think about sex.

Kulingana na  Bi Keatinge wachumba wanaweza kufufua maisha yao ya gono  na kujenga upya tajiriba ya  kutifua vumbi kitandani kwa kutafuta na kutumia staili zinazowafaa.
Hata hivyo anasema ni hatari kumlazimisha mchumba wako kutumia staili isiyompendeza akisema ni kama kusukuma gari ya moshi mlimani.

Bi Keatinge asema kumshinikiza mrembo kutumia staili asiyoitamani ni kumwongezea mateso na anaweza kukuchukia maisha yake yote.

“Wachumba wanafaa kukubaliana  staili zinazowafaa kuburudishana. Ni makosa kumlazimisha kiosha roho wako kutumia staili asiyoitamani kwa sababu itamwongezea mateso,” asema jambo ambalo watu wengi wanakubaliana nalo.

Anasema wachumba hawafai kukubali chochote kiwe kikwazo katika juhudi za kusaka shibe la uroda. “ Kila mmoja anapasa kumhusisha  mchumba wake katika kila hatua hadi amfikishe katika kilele cha mlima wa mahaba,” asema.

Jinsi ya Kutumia Kondom za Kiume na za Kike Kiufasaha..!!!

$
0
0

NUSU ya watu wanaotumia kondomu kwa ajili ya kujikinga na mimba ama magonjwa ya zinaa, hawajui namna ya kuitumia mipira hiyo

Tumia kondom mpya kila mara unapofanya mapenzi.
Jitahidi kutokugusa sehemu za siri ya mpenzi wako (au osha mikono yako) kabla ya kugusa sehemu zako za siri.

1. Usiguse sehemu za siri za mpenzi wako kabla ya kuvaa kondom. Angalia kwa makini paketi za kondom kabla ya kuifungua.
Hakikisha haijaharibika au kupasuka. 


Angalia tarehe ya mwisho ya matumizi ya kondom hii, ambayo itakuwa imechapishwa sehemu ya nje ya paketi ya kondom kuhakikisha tarehe haijafika. Kama tarehe imeishafika na kupita, tumia kondom nyingine. 

2. Fungua paketi kwa uangalifu kwenye sehemu iliyo na makucha makucha kama msumeno, ili kuhakikisha hauharibu kondom.
Usitumie makucha au meno kufungua paketi, kwa sababu kondom inaweza kuchanika.

Upapogusa kondom, iwe na utelezi kidogo. Kama kondom haina utelezi, imeharibika, kwa hiyo usiitumie. Sehemu ya nje ya kondom huwa na majimaji yanayorahisisha kufanya mapenzi. Kabla ya kuvaa kondom kwenye uume, hakikisha unafahamu sehemu gani inakaa nje unapoikunjua.

Tumia kondom mpya kila mara unapofanya mapenzi.
Usitumie tena kondom iliyokwisha tumika.

3. Weka kondom kwenye uume uliyosimama tu. Minya chuchu iliopo sehemu ya juu ya kondom kuhakikisha hamna hewa ndani yake. Hii ni kuhakikisha kuna nafasi ya kutosha katika kondom wakati mwanaume anamwaga shahawa.

4. Endelea kuminya chuchu na kunjua kondom kwa uangalifu hadi unapofika sehemu ya chini ya uume. Kuminya chuchu kunahakikisha kuna nafasi ya kutosha kupokea shahawa itakayomwagika.
Kama unaweka kondom juu ya uume na unaanza kuikunjua vibaya, usiitumie tena, kwa sababu ukiigeuza kuna uwezekano kuna tone chache za shahawa zilizokaa nje ya kondom.

Usitumie Vaseline, losheni au aina nyingine yeyote ya mafuta kuongeza utelezi wa kondom zaidi. Mafuta ya aina hii huongeza uwezekano wa kondom kupasuka. Kama unahitaji utelezi zaidi, tumia mate au majimaji maalum yaitwayo KY-Jelly, yanayopatikana katika duka ya madawa.

5. Anza kufanya mapenzi

6. Mara tu baada ya kufikia mshindo, toa uume ukeni wakati unaendelea kushikilia kondom kwenye sehemu ya chini ya uume karibu na mapumbu. Kila mara ondoa uume kabla haujalegea kuhakikisha kondom haiachii na kubaki ndani ya uke.

7. Kwa uangalifu, vua kondom kutoka kwenye uume.

8. Funga kondom kwa fundo kwenye sehemu ile ya wazi kuzuia shahawa kumwagika.

9. Funga kondom kwenye karatasi au kwenye paketi yake ya mwanzo.

10. Tupa kondom kwenye choo cha shimo, au ichome moto. Nawa mikono yako na maji na sabuni.

TUMIA KONDOM MPYA KILA UNAPOFANYA MAPENZI.



JINSI YA KUTUMIA KONDOM YA KIKE:
Tumia kondom mpya kila mara unapofanya mapenzi. Kondom ya kike inaweza kuwekwa ndani ya uke mara tu kabla ya kufanya mapenzi, au hadi masaa 6 kabla ya kufanya mapenzi.

Jitahidi kutokugusa sehemu za siri za mpenzi wako (au osha mikono yako) kabla ya kugusa sehemu zako za siri.

1. Tazama paketi ya kondom ambayo bado haijafunguliwa.
Hakikisha haijaharibika au kupasuka.

Angalia tarehe ya mwisho ya matumizi ya kondom hii, ambayo itakuwa imechapishwa sehemu ya nje ya paketi ya kondom kuhakikisha tarehe haijafika. Kama tarehe imeishafika na kupita, tumia kondom nyingine.

2. Fikicha kwa upole paketi ili kuhakikisha majimaji yaliyomo yanasambaa kote kwenye kondom.
Fungua paketi kwa uangalifu kwenye sehemu yenye makucha kama msumeno, ili kuhakikisha kondom haiharibiki.
Usitumie makucha au meno kufungua paketi kwa sababu yanaweza kuchana kondom.

Unapogusa kondom, iwe na utelezi kidogo. Kama kondom haina utelezi, imeharibika, kwa hiyo usiitumie. Sehemu ya nje ya kondom huwa na majimaji yanayo-rahisisha kufanya mapenzi.

3. Ni rahisi zaidi kuingiza kondom ukeni kama unachuchumaa, kupandisha mguu mmoja juu ya kiti, au kulala kitandani ukiwa umekunja magoti wakati umepanua miguu yako wazi kabisa. 

4. Minya kondom kwa nje, ukiminya sehemu mbili za mviringo mdogo wa ndani kwa pamoja kama ilivyooneshwa kwenye picha. Muundo huu hurahisisha kuingiza kondom ukeni.

5. Wakati umeendelea kushikilia sehemu ya nje ya kondom namna hii, pole pole ingiza mduara mdogo wa ndani ukeni ukitumia kidole cha shahada.

7. Hakikisha mduara wa nje wa kondom unaishia kwenye mlango wa uke: usiingie ndani ya uke. Mduara wa nje utafunika mlango wa uke wakati wa kufanya mapenzi. 

8. Usitumie Vaseline, losheni au aina nyingine yeyote ya mafuta kuongeza utelezi wa kondom zaidi. Mafuta ya aina hii huongeza uwezekano wa kondom kupasuka. Kama unahitaji utelezi zaidi, tumia mate au majimaji maalum yaitwayo KY-Jelly, yanayopatikana katika duka ya madawa.

Fanya mapenzi ndani ya muda wa masaa 6 baada ya kuvaa kondom.
Tumia mikono yako kuongoza uume ndani ya kondom, ili kuhakikisha kuwa uume unaingia ndani ya kondom na siyo kando.

9. Baada ya kufanya mapenzi, viringisha mduara wa nje wa kondom mara moja ili kuzuia shahawa kumwagika.
Kisha toa kondom ukeni polepole. 

10. Funga kondom kwenye karatasi au kwenye paketi yake ya mwanzo. 

11. Tupa kondom kwenye choo cha shimo, au ichome moto.
Nawa mikono yako na maji na sabuni.


TUMIA KONDOM MPYA KILA UNAPOFANYA MAPENZI

Viewing all 104789 articles
Browse latest View live




Latest Images