Quantcast
Channel: UDAKU SPECIAL
Viewing all 104689 articles
Browse latest View live

Utapeli Magroup ya WhatsApp

$
0
0
Katika kutafuta namna ya kujipatia kipato kwa wakati huu ambapo njia zote za ujanjaujanja zimezibwa na serikali ya awamu ya tano, baadhi ya watu wamebuni mbinu ya kuwatapeli wananchi kupitia makundi ya mitandao ya kijamii hasa WhatsApp.

Kwa mujibu wa mmoja wa watu ambao alijikuta akiingia katika mtego huo kutokana na tamaa yake ya ngono, (jina lake linahifadhiwa) alipata rafiki katika Mtandao wa Kijamii wa Facebook ambaye baadaye alimweleza kuwa ana mtandao wa wasichana mastaa na wasio mastaa wanaojiuza na angeweza kuwapata kirahisi kwa kupewa mawasiliano yao na pia kuona picha na baadhi ya video wakiwa watupu.

Madai yaliyofikia katika dawati la gazeti hili, vijana wengi ambao ndiyo watumiaji wakubwa wa mitandao ya kijamii, wamekuwa wakitapeliwa mara kwa mara kwa kujiunga katika makundi hayo.

Inaelezwa kuwa, mchezo mzima huanzia Mitandao ya Instagram na Facebook ambapo wengi wa matapeli hao huweka picha za wanawake wakali wa Kibongo na kudanganya kuwa wanapatikana kwa njia ya picha na video wakiwa utupu katika makundi yao ya WhatsApp huku wakianika namba za simu watumiwe kiasi cha pesa waunganishwe. Wakishaweka posti hizo katika mitandao hiyo, vijana wengi hukimbilia kujiunga kwa kutumia namba zilizowekwa katika mitandao hiyo kwa kiingilio cha kiasi cha kuanzia shilingi 5,000 hadi 10,000 kwa mmoja lakini wakishajiunga katika makundi hayo hakuna kinachoendelea na hata ukiwatafuta hawapokei simu.

OFM KAZINI Katika siku za hivi karibuni ilibainika kuwa, kuna makundi mengi ya WhatsApp yanayoendesha biashara ya ukahaba. Kikosi kazi cha Operesheni Fichua Maovu (OFM) kikaingia kazini kubaini kama kweli biashara hiyo inaendelea kwa njia ya mtandao ambapo mmoja wa mapaparazi aliomba kuunganishwa na kundi linalojinadi kuwa, ukitaka kahaba wa kila aina unampata.

Kufuatia paparazi kutaka aungwe ili apate huduma, alitakiwa kutuma kiingilio cha shilingi 15, akatuma na kuomba aunganishwe na mmoja wa warembo wakali waliokuwa wamewekwa kwenye group hilo. Heh, imeliwa! Baada ya pesa kutumwa, hakukuwa na mawasilino tena na simu ikawa haipatikani.

Ijumaa linawashauri watumiaji wa mitandao hiyo, kuwa makini na watu wa aina hii kwani kila siku wamekuwa wakiongezeka katika mitandao na kujipatia pesa kwa njia rahisi. Ukishaona unaungwa au unashawishiwa kujiunga na kundi ambalo limekaa ‘kihelahela’, akili kumkichwa.

GPL

Majonzi Kifo cha Mwasisi wa Freemasons Nchini..!!!

$
0
0

NI majonzi! Mfanyabiashara maarufu ambaye pia anatajwa kuwa mmoja wa waasisi wa Freemasons nchini Tanzania, Sir Jayantilal Keshavji (Andy) Chande amefariki dunia akiwa na umri wa miaka 89.

Ndugu wa karibu na familia alithibitisha juu ya taarifa za kifo cha mfanyabiashara huyo jana kupitia simu akiwa Nairobi nchini Kenya, akisema alifariki jana asubuhi wakati akiendelea na matibabu nchini humo.

Alisema familia yake ilikuwa katika harakati za kuusafirisha mwili wa marehemu kutoka Nairobi kuelekea nyumbani kwake jijini Dar es Salaam kwa ajili ya mazishi.

Chande alizaliwa Mei 7, 1928 mjini Mombasa Kenya, alikulia na kusoma katika eneo la Bukene, wakati huo likiitwa Jimbo la Magharibi nchini Tanganyika kabla ya kwenda kusoma katika Chuo Kikuu cha Pune mjini Bombay (sasa Mumbai), India katika miaka ya 1950.

Katika miaka ya 1990 hadi katikati ya mwaka2000, Chande alikuwa kinara wa Freemasons katika ukanda wa Afrika Mashariki na Shelisheli.

Sir Andy Chande amewahi kuandika vitabu mbalimbali, kimojawapo kikijulikana kwa jina la “A Knight in Africa: Jourbey from Bukene”. Ameacha mke na watoto.

Miaka 5 Sasa Bado Tasnia Ya Filamu Inakulilia...!!!

$
0
0

Leo ni siku ya kumbukumbu ya kifo cha aliyekuwa Staa wa Filamu Bongo, Steven Charles Kanumba ambapo ametimiza miaka mitano tangu alipoaga dunia Aprili 7, 2012

Kanumba anakumbukwa zaidi kwa mchango wake katika Tasnia katika kukuza na kuitangaza Bongo Movie ndani na nje ya Afrika Mashariki na Afrika kwa ujumla.

Alikuwa chachu ya mafanikio kwa waigizaji wadogo na kutoa hamasa ya kufanya kazi kwa bidii kwa wasanii wakubwa hapa nchini ili kuweza kutoboa kimataifa na kuweka heshima kubwa hapa nchini

Miongoni mwa filamu zake ni pamoja na, KIJIJI CHA TAMBUA HAKI, MAGIC HOUSE, FAMILY TEARS, MORE THAN PAIN, SATURDAY MORNING, OPRAH, WHITE MARIA, UNFORTUNATE LOVE, YOUNG BILLIONAIRE, NDOA YANGU, THE TWINS, MOSES, FAKE SMILE, RED VALENTINE, OFFSIDE, DANGEROUS DESIRE, BIGDADY, UNCLE pamoja na DAR 2 LAGOS.

Tangu kufikwa kwa mauti yake ni wengi wamekuja huku wengine wakifananishwa naye lakini hakika Kanumba atabaki kuwa Kanumba na kamwe hakuna atayekuja kufanana naye katika kila kitu.
Mungu azidi kuilaza roho yake mahali pema peponi. Amina.

Soma Nafasi Kibao za Kazi Zilizotangazwa Leo Kutoka Makampuni Mbali Mbali

MAITI Yaokotwa Ufukwe wa Ziwa Victoria Ikiwa Imefungwa Kwenye Baiskeli

$
0
0
Tukio la kusikitisha Wakati familia kadhaa za watanzania zikiendelea kupoteza ndugu zao bila kujulikana walipo, leo huko mkoani Mara katika ufukwe wa ziwa Victoria imeokotwa maiti ya mtu mmoja asiyefahamika ikiwa imetupwa ziwani. Mazingira ya kifo chake yanaonesha mtu huyo mwanaume aliuawa, akafungwa kama kifurushi kwenye baiskeli, kisha yeye na baiskeli yake wakatoswa ziwani. Hapa ndipo tulipofika kama taifa.! TAHADHARI: Picha inatisha

TAMASHA la XXL Dodoma lagubikwa na Simanzi, Umati Wamyoshea Mabango Waziri

$
0
0
Katika hali isiyokuwa ya kawaida leo kile kipindi cha XXL kilichokuwa kinaruka moja kwa moja toka Dodoma kimegeuka majonzi baada ya mamia ya vijana kunyoosha mabango yaliyoandika FREE ROMA

Watanganzaji walilazimika kubadili interview na kumwambia naibu waziri habari utamaduni na michezo Antony Mavunde kwamba hawawezi kupuuzia mabango waziri aseme chochote.

Naibu waziri akasema anasikitishwa na kitendo hicho lakini ana taarifa kwamba jeshi la polisi litatoa taarifa punde. Baada ya hapo kwenye segment ya hot 3 at 3 zimepigwa nyimbo mbili za ROMA ambapo umati umepagawa na kupiga mayowe.

Sitosahau Nilipotumia Mafuta ya Korosho Kukuzia Maungo ya Kiume

$
0
0

Maneno ya vijiweni na mtaani yana athari sana kisaikolojia.

Nakumbuka baada ya kuingia advance ndipo nilipoanza kujihusisha na ngono huku nikisikia maneno ya wadada wa mitaani na mitandaoni wanavyopendezwa na large penis ikumbukwe kipindi hicho nilikua nimekanunua katecno kangu ndo nilikua naanza kuingia mitandaoni hasa facebook, blogs mbalimbali n.k hivyo kelele za mitandaoni zili influence hulka ya kuongeza ukubwa wa dushe.

Pasipo kujua kibamia ni kipi na mhogo ni saizi gani ikabidi fikra zinitume moja kwa moja kuna haja ya kuongeza ukubwa wa uume wangu ili kuwaridhisha wadada wa rika tofauti tofauti. Nilianza na dawa za kimasai nakumbuka nilinunua 8000 nilitumia bila mafanikio yoyote. Nikanywa sana maji ya mizizi ya mpapai lakini wapi.

Ila siku moja wazo likanijia kwamba wakati tukiwa watoto tulikua tunatumia mafuta ya korosho kuchorea tatoo na ngonzi ilikua inaumuka na kukaa muda mrefu nikaona ngoja nijaribu inaweza ikafanikisha lengo la kuongeza unene.

Baada ya kujisugua na mafuta ya korosho kimbembe kikaanza baada ya saa moja nikaona ngozi inaumuka na inakua nyeusi seemu yote ya penis, ni kama mtu aliyemwagiwa mafuta ya moto, ngozi yote ikatoka kikabaki kidonda chekundu, hapa nikahisi nilichojaribu nimekipata na kuna uwezekano nikapoteza kila kitu.

Nilitumia dawa ya kukausha vidonda kwa wiki 2 na hatimae kidonda kikaanza kupona na kikapona kabisa, ila nilichomshukuru Mungu iliendelea ku erect kama kawaida maana nilikua naogopa uwezekano wa kuviua vimishipa vinavyohusika na sensitivity.

Nilipona kabisa ila ilibidi nikae muda mrefu bila ku sex coz umbile lilikua na ngozi nyekundu na mabaka mabaka, ikumbukwe yote haya yalifanyika bila mtu yoyote kujua ilikua ni kimya kimya.

Hua nikikumbuka hili tukio hua naishia kucheka tu.

Njia 8 Za Kugundua Iwapo Mwanamke Amepandwa Nyege Akiwa Kando Yako ..!!!

$
0
0

Je unaweza kutambua iwapo mwanamke amepandwa na nyege akiwa kando yako? Well, kama unazifahamu ishara bayana basi inakuwa rahisi kwako.

Ok, tuanze hivi. Hebu chukulia umeketi na marafiki zako wa kiume na wa kike halafu ghafla rafiki yako mmoja akaanza kuonyesha ishara fioa ambazo wewe pekee ndio umezitambua kuwa amepandwa na nyege na anataka ufanye makamuzi ya haraka haraka. Hiki ni kipawa kilioje?

Sasa waonaje kipawa hiki cha kutambua mwanamke kama amepandwa na nyege bila hata kumgusa wala kumchungulia mwili wake wa ndani kiwe unakimiliki? Relax, Nesi Mapenzi iko hapa. Tutakupa ishara zote tuzijuazo hapo chini.

Zama nasi...

#1 Anakuangalia kana kwamba wewe ni nyama iliyotandazwa vyema
Kwa lugha nyingine tunaweza kuita ‘macho ya mahabat’ ama ‘macho ya mlalano’. Kuna mtizamo wa macho ambao mwanamke atakuangalia tofauti na vile ambavyo unamtambua kukuangalia. Hii ni ishara ya kukuambia kuwa amekupa nafasi ya wewe uchukue hatua ya kwanza kwake.

Utamwona kuwa mara kwa mara anataka umwangalie machoni mwake na pindi utakapomwangalia atakuangalia halafu atatabasamu na kuangalia chini. Halafu atakuangalia tena huku akiuuma mdomo wake wa chini. Hapa usiwe mjinga. Amka, anza kumuapproach ili uongee na yeye.

#2 Anakusuka kuliko kikawaida
Ok, katika hali kama hii tutaichukulia kuwa wewe na huyu rafiki yako mumewekeana mipaka flani kati yenu. Kwa kawaida munafanya mambo ya kawaida ambayo marafiki hufanya. Kwa mfano mnakutana sehemu flani mnaspend muda pamoja, mnaongea normal. Lakini siku moja, bila sababu zozote unamwona mwanamke kama huyu anaanza kukusuka kuliko vile ambavyo umezoea. Mfano iwapo mmezoea kuwa mkiwa mmeketi pamoja mnaweka nafasi kati yenu, siku hii unaona kuwa amehakikisha kuwa amekubana kabisa huku akikwambia mambo ambayo ni tofauti na vile ulikuwa ukitarajia.

Tashwishi yako itahakikishwa zaidi pale ambapo atakutenganisha na wale waume wengine walioko na wewe. Hii ni obvious kuwa anafanya hivyo ili kuteka atenshen yako yote na amakinike na wewe pekeake. Anakusuka. Ukiona kuwa anajaribu kuteka atenshen yako kama hivi, usizubae. Pia wewe makinika na yeye na uende sambamba ili usipoteze hata dakika moja.

#3 Anakuwa huru kimguso

Ishara nyingine ya kuonyesha kuwa mwanamke kama huyu amejawa na nyege nyingi ni pale ambapo anaipeleka mikono yake sehemu ambazo kikawaida hazijazoeleka. Hapa sasa inaweza kuleta ule mchanganyiko wa kubainisha iwapo ni kusudi ama ni kwa bahati mbaya. Lakini kama tujuavyo ni kuwa katika kamusi ya wanaume hakuna kitu kama ‘miguso ya kibahati mbaya’. Lakini tambua kuwa hii haimaanishi kuwa mwanamke atashika pumbu zako ghafla ili kuonyesha amepandwa na nyege, la. Miguso yake inaweza kuwa fioa huku akitoa ishara kwako pia ufanye vile anavyofanya yeye kama hutomaindi.

Kuna njia kadhaa ambazo mwanamke anaweza kukugusa kuonyesha kuwa amepandwa na nyege nazo ni; kuupeleka uso wake karibu yako, kukukumbatia, kuifungata mikono yake kiunoni mwako ama mkononi, kuipapasa miguu yako na yake, ama wakati mwingine kukunong’onezea karibu na sikioni mwako.

#4 Mazungumzo yenu yanakuwa ya kiundani

Kama unamwona kuwa anaanza kuuliza maswali mengi ya kibinafsi ama anatoa maoni ya kiushawishi katikati ya mazungumzo yenu basi ni ishara ya kuwa amepandwa na nyege. Kutumia maneno ya kutatiza ni njia  ya moja kwa moja kuonyesha kuwa mwanamke kama huyu anatoa ishara kuwa ana hamu ya kitu flani kiasi cha kuwa anasema moja kwa moja.

Anaweza kufanya hivi kwa kueleza mahusiano yake ya awali, staili nzuri kwake za kufanya mapenzi, ama kukuuliza mahusiano yako na mwanamke huwa yakoje, kiufupi atajaribu kukuambia mambo ambayo kwa kawaida mwanamke hawezi kukufungukia. Njia nzuri ya kukabiliana na hili ni kuwa usipanik wala usiwe na pupa. Nenda na spidi yake polepole ili mwisho wa siku unahakikisha kuwa unampandisha mzuka zaidi na zaidi.

#5 Anakusifia vile ulivyopendeza
Katika hali ya kawaida jambo hili la kumsifia mtu huwa tunachukulia ni jambo la kawaida kabisa kwa mwanamke yeyote kufanya. Lakini inaweza kufikia kiwango flani ambacho kinaleta msisimko wa kutaja na kugusia maswala ya moja kwa moja ambayo ni ya kibinafsi. Mambo ambayo mara nyingi yakitamkwa huwa ndani ya akili ya mwanaume huwa na maana tofauti kabisa.

Ok, hebu tuchukulie hivi. Umezoa mwanamke flani kuwa anapenda kusifia mavazi yako, tabasamu lako nk. Lakini pindi ambapo ataanza kukusifia kwa kutaja jinsi ulivyo na mikono iliyoumbika, kifua kilichopanuka, ama jinsi mabega yako yalivyo, ama kwa kukusifia jinsi suruali uliyoivaa imebana vizuri makalio yako ama wakati mwengine anagusia umweleze sehemu ambayo unafanya mazoezi ni ishara tosha kuonyesha kuwa huyu mwanamke ana jambo ambalo linataka kushughulikiwa mara moja. Upo!?

#6 Anakuonyesha ‘mali’ zake

Tushaona mambo kama haya awali. Mwanamke kama huyu anazifungua nywele zake ili zining’inie karibu na shingo yake wakati mnapoongea, anavalia tsheti ya kola ya V pamoja na sidiria ya ‘push up’, kuvalia skin tyt, ama kujiandaa hata kama mnakutana sehemu ya kawaida.

Mwanamke kwa kawaida hufanya haya yote akiwa na lengo moja kuu...kuteka atenshen yake yote kwako. Ishara ya kuwa ana matamanio ambayo anayahitaji kutoka kwako. Usizubae.

#7 Hatulii mbele ya uwepo wako

Wanawake huwa na mbinu tofauti tofauti ambazo hufanyika wakati wanaposisimuliwa ama wanapokuwa na nyege. Hii ni kuanzia kuwa na mpigo wa haraka kwa mioyo yao, kupumua kwa uzito na wakati mwingine kutokuwa na utulivu wakati wanapokuwa wamekaa, hii ndio sababu utamsikia akikwambia yuko ‘HOT’

So hebu tuchukulie umetoka deti na yeye halafu unamwona haangamani sehemu aliyoketi, unamwona anasogea huku na huku ilhali anakuangalia, anacheza na nywele zake, ama anaenda bafuni kujisaidia. Hii ni ishara moja kuwa amebambika na wewe na anataka umpatie full atenshen kwake.

#8 Anakuruhusu umguse
Hii ni kiashirio cha mwisho zaidi kuonyesha kuwa amejiachilia kwako na hakuna kurudi nyuma. Wanawake, hata wale ambao wamezoea kutongozwa, huwa wanakuwa sensitive kwa miguso ambayo haijakaribishwa. Sasa kama wewe ni yule anayependa changamoto, na unataka kujua kama anaitamani, na akakuachilia umguse, basi hakuna la zaidi la kuelezea kwa sababu kile ambacho kinafuata baada ya hapo kinajulikana.

Lakini kuwa makini, anza polepole. Usijaribu kuupitisha mkono wako ndani ya blauzi yake. Balada yake ifanye romantik ili ulete tenshen ya kemia. Anza kwa kuiweka mikono yako kiunoni kwake, hadi kwa mikono yake na ufikie shingo yake. Soma sehemu ambazo anapenda uziguse sana huku akikuelekeza zaidi.

Upo!? Kazi kwako.

Jinsi Ya Kutumia Mbinu Ya Utabiri Kumvunja Nguvu Mwanamke Ili Abaki Na Wewe Milele ..!!!

$
0
0

Awali katika machapisho yetu tumeshawahi kuzungumzia swala ya mbinu ya kumkontrol mwanamke kama rimoti kwa kutumia mbinu ya ‘nanga’. Well, leo kama Nesi Mapenzi tumemua kuiweka wazi mbinu ya ‘utabiri’ kama moja wapo ya Sanaa Ya Kutongoza ambazo tumekuwa tukizichapisha hapa.

Ok, hebu tuanze kwa kuuliza maswali. Je ushawahi kuwa na girl friend? Kama huna girlfriend mpaka siku ya leo unangojea nini? 

Na kama umekuwa na girlfriend muda huu wote, je wewe na huyu girlfriend wako mnaishi vipi? Je mnazozana, mnakosana, ama hamuelewani?

Katika mahusiano haswa inapotokea kuwa nyote wawili mnapendana lakini kuna mmoja wenu hajaridhika na mwenzake basi mara nyingi ukifanya uchunguzi utakuja kugundua kuwa mmoja kati ya nyinyi wawili huwa ana mchepuko/ mpango wa kando.

Na mara nyingi inauma sana iwapo huyo ambaye anakuwa na mpango wa kando ni mpenzi wako, na mbaya zaidi ni pale ambapo bado unampenda huyu mpenzi wako.

Kwa kueleza kifupi ni kuwa umegundua kuwa mpenzi wako ana mpenzi wa kando na wewe hujaridhika na hio hatua ya yeye kutaka kukuacha na kumfuata huyo mwingine.

Ikifikia hapa utachukua hatua gani ili asikuache? Hapa ndipo hii mbinu ya ‘utabiri’ inaingia kati.

Hebu tuuchukulie huu mfano. Wakati mteja ameingia katika duka flani anataka kununua bidhaa lakini hajaridhishwa na bidhaa anazoziona na anataka kuenda katika duka la pili huwa mhudumu kwa kawaida hamkatizi tamaa yake ya kuenda katika duka la pili bali humpa mawazo na hutabiri kile ambacho atapatana nacho katika duka la pili. Kwa kawaida atamwambia, “Jiskie huru kuenda katika duka flani na flani , lakini kumbuka kuwa maduka hayo huwa bei zao ziko juu kupita kiasi, ama hutapata bidhaa mahususi unayotafuta, ama utadhulumiwa nk.

So, huyu mhudumu amefanya nini hapa? Rahisi! Kama huyu mteja ameshawishika na kuamua kubaki hapo, atakuwa ameshinda. Kama huyu mteja ameamua kuenda katika duka la pili, na kugundua kuwa kile alichoambiwa ni kweli na kurudi tena, atakuwa pia ameshinda. Na kama ataenda na hatarudi, basi hakutakuwa na utofauti wowote kama vile awali.

Sasa hebu fikiria kidogo jinsi ya kuitumia mbinu hii kwa girlfriend wako ama kwa mpenzi wako. Unaweza kutumia hii mbinu kumvunja nguvu iwapo kuna mwanaume flani yeyote pale ambaye anamtatiza kihisia.

Kwa mfano unaweza kumwambia, “Uko huru kuendelea na yeye, ni kawaida, inakubalika. Lakini najua kufikia hadi sasa umeshagundua kuwa huyo unayemfuata ana tabia ambayo si nzuri kwako, tabia ambayo inakutatiza na kukusumbua... na utapata kugundua tabia nyingine mbaya zaidi kadri ambapo utazidi kuendelea kuwa na yeye.”

Hapa moja kwa moja atajaribu kuvuta taswira za tabia zozote mbaya ambazo ashawahi kuzishuhudia kutoka kwa huyu mwanaume.
NB: Kumbuka utabiri unaoutoa hapa utakuwa hauna uhusiano mmoja kwa moja na huyu mwanaume bali unasema na kubahatisha tu. Lakini kwa mwanamke atadhania kuwa tayari unamjua huyu mwanaume na tabia zake.

So moja kwa moja kama huyu mwanamke kweli ana hisia kwako anaweza kubadili msimamo wake na kukubali kuendelea na wewe.
Upo!?

Hatua kwa Hatua Jifunze Namna ya Kumbusu Au Kumla Denda Mpenzi Wako..!!!

$
0
0

Ili mfurahie busu mnatakiwa kupeana (umbusu-akubusu) .

Jambo muhimu la kuzingatia ni kuto achama au kukusanya midomo yako kama unataka kubusu kwa sauti na badala yake busu kimahaba…..

1.Sogeza midomo yako kama ilivyo (umeifumba lakini iko-relaxed) kwenye midomo ya unaetaka kumbusu…..kisha itulize midomo hiyo juu yake na sasa toa “busu kavu” juu ya midomo yake kisha jitoe alafu rudi tena x3

2.Inua uso wake kwa kutumia kidole (hii ni kwa wanaume) na mbusu moja kwa moja kwa kugusanisha pua kiaina…-Busu kwa kupindisha shingo/kichwa ili kutogusanisha pua zenu…

3)-ukiwa umepindisha kichwa/shingo…mshike mkono au mkumbatie kiasi na busu tena.


Ukiona/hisi anajisogeza au anakupa ishara kuwa uendelee kwa kufungua mdomo kiaina, kukushika mkono/kifua/kitambi/kiuno au kuweka mkono kwenye bega basi endelea na “busu nyevu” kwa kubusu ktk mtindo wa kulamba-kunyonya mdomo(lips) wa chini na tulia hapo kwa sekunde chache kisha pokea ulimi wake kwa ulimi wako (bila kuachama…ni mumo kwa mumo)alafu ukwepe na kisha rudi kwenye midomo ya busu lip ya juu…..


Ongeza ujuzi wako sasa…na kumbuka kupumua kwa kutumia pua sio unampumulia mwenzio mdomoni….(atashiba hewa) au unabada pumzi (Mauti inakukumba). Unaweza kufumba macho au kukodoa....inategema na wakati wenyewe.


Kuna aina tofauti za kubusu ili kutuma ujumbe kwa mpenzi wako lakini busu zote zinahusiaha ulimi na mate.

 Unaweza ukapewa busu wewe ukadhani ni kawaida (kama hujui) lakini mwenzio anakwambia amechoka, anakupenda, anashukuru, amefurahi kukuona, hataki kungonoana siku/wakati huo, hana raha/hujamfurahisha, anataka kuwa peke yake, anamachungu, yuko busy n.k.

Taarifa Mpya ya Wizara ya Habari na Sanaa Kuhusu Roma Kutoweka

$
0
0


Taarifa za kupotea kwa Msanii Roma Mkatoliki na wenzake wawili baada ya kutekwa na kuchukuliwa na Watu wasiojulikana kwenye studio za TONGWE Dar es salaam, zilianza kusambaa kuanzia juzi usiku (April 5 2017)

Leo April 7 2017 Wizara ya Sanaa, Utamaduni na michezo ambayo iko chini ya Dr. Mwakyembe imetoa taarifa ifuatayo >> “kwa dhamana yake katika tasnia ya Sanaa Wizara imepokea kwa mshtuko taarifa za kutoweka kwa Mwanamuziki Ibrahim Mussa kwa jina la kisanii “Roma Mkatoliki””

Wizara imefuatilia kwa karibu suala hili kwa kuwa lina muelekeo wa jinai. Hata hivyo taarifa kutoka vyombo vya dola zinathibitisha kuwa Roma Mkatoliki hashikiliwi katika kituo chochote cha polisi.

Kutokana na hali hiyo, Wizara inawaomba wadau mbalimbali na wananchi kwa ujumla kushirikiana na Jeshi la Polisi kwa kutoa taarifa zozote zitakazo saidia kujua alipo msanii huyo.

Ukweli Mchungu..Uangaliaji Wa Filamu Za Ngono Huharibu Akili Yako ..!!!

$
0
0

Katika pitapita zangu katika mitandao na baadhi ya kazi zangu mtandaoni, nilikumbana na hili chapisho ambalo niliingiwa na hamu ya kuliweka hapa ili kuwajulisha umuhimu wa kufanya mapenzi na mpenzi wako. Chapisho lenyewe hili hapa:

"Tendo La Ngono Litakufanya Uwe Mjanja, Utafiti Waonyesha

Kuna watu watatetea kuwa tendo la ngono ni kama baraka kutoka kwa Mungu, ni dawa ambayo haijawahi kutokea kamwe. Inasemekana kuwa ngono hupunguza mawazo(stress), depression, husaidia kuchoma kaloria mwilini na pia huwa ni furaha kwa wawili wanaopendana. Kuongezea mambo haya yote imebainika kuwa ngono inafanya mtu kuwa mjanja/mwerevu.

Utafiti huu ulifanywa katika familia ya panya na imeibuka kuwa ngono imewafanya kuwa wajanja, na kwa sababu tuna uhusiano wa karibu na familia ya panya, utafiti huo pia unafanya kazi kwa binadamu.

Kulingana na utafiti uliofanywa na wanasayansi tofauti kutoka chuo kikuu cha Maryland na Konkuk, Seoul nchini N. Korea, imeonekana kuwa panya hao wameongezeka kipawa cha kufikiria na pia jambo hilo limeongeza 'neurogenesis' (ongezeko la neurons kwa ubongo)

Utafiti umeonyesha kuwa sehemu inayofaidi zaidi kwa tendo la ngono ni sehemu iitwayo 'hippocampus', sehemu inayoweka matukio ya zamani ya kiumbe. Sehemu hii hukuwa na kunawiri.
Kiufupi tunaweza kusema kuwa matendo ya ngono unayoyafurahia ukiwa miaka ya 30 na 40 itasaidia kuongezea mawazo ya matendo ya ngono uliyoyachukia wakati wa miaka ya 20.

Lakini katika utafiti huo kuna mambo ambayo hayakuwa sawa, kuna sehemu fulani ya ubongo ambayo ukuaji wake ulikuwa duni, nayo ni 'ngono ya uongo'. Ngono ya uongo ni kama kuangalia ilamu za pornography kupindukia. Utafiti unaendelea kusema kuwa matukio yote yaliyowekwa kwa kufanya tendo la ngono yatafutika baada ya kuangalia filamu za ngono mno.

Huu ni utafiti sahihi kwani kuna ule msemo kuwa kuangalia filamu za ngono kuna haribu akili, kunakufanya usahau mengi. Kwa hivyo kuangalia porno nyingi kunakufanya uwe na mawazo duni." -FoxNews

Hebu sasa turudi kwenye mada kidogo. Ok hivi wewe mara ya mwisho ulifanya mapenzi lini? Na ni lini mwisho uliangalia filamu za ngono?

Ni mara ngapi ulifanya mapenzi na ni mara ngapi ulishaangalia filamu za ngono? Iwapo kuangalia filamu za ngono imepita ile ya kufanya mapenzi basi uko katika tatizo kubwa, tatizo la kupoteza uwezo wako wa kukumbuka mambo siku zako za usoni.

Na kwa kutatua hili tatizo unachukua mkondo upi? Je unachagua kutulia kuacha kuangalia filamu za ngono ama utaamua kuongeza kufanya mapenzi ili kuongeza ushapu wako kimaisha?

Na kama umeamua kufanya mapenzi kwa wingi, je una  mpenzi wa hakika ama ni mpenzi wa kuotea, kesho anakupa kesho kutwa anakunyima?

Ok, kwa kutatua na kukusaidia kukupa mawazo...

Kwa wale ambao tayari wako na wapenzi thabiti (Wanaume Alpha) na wako tayari kufanya mapenzi kila siku ili kukuza bongo zao bila kuchoka wala kuboeka ingieni hapa.

Kuna wale ambao wana wapenzi wa kuotea, wale ambao hawana wapenzi kabisaaa, na kila wakijaribu kutongoza wanashindwa, wanabakiwa kuenda majumbani mwao na kujifungia chumbani huku wakiangalia filamu za ngono na wakipiga punyeto. Kama unaamini kuwa wewe hauko miongoni mwa hili kundi ingia hapa.

Ok. Kazi kwako. Ni wewe wa kuchagua iwapo utaamua kuendelea kuharibu akili yako ama kuikuza akili yako ili upate ujuzi wa kijasiriamali maishani.

Kimenukaaa...Bunge, Maalim Seif Wambana Msajili Kuhusu Mgogoro wa CUF..!!!

$
0
0

Wakati katibu mkuu wa CUF, Maalim Seif akisema kuwa Msajili wa Vyama vya Siasa, Jaji Francis Mutungi anakivuruga chama chao, Kamati ya Bunge ya Sheria na Katiba imemtaka kuhakikisha anamaliza mgogoro wa chama hicho kuepusha kutia dosari Muungano.

Kauli hizo zimekuja siku moja baada ya Bunge kumtambua naibu katibu mkuu wa CUF-Bara, Magdalena Sakaya kuwa kaimu katibu wa chama hicho kwa maelezo kuwa Maalim Seif anashindwa kutekeleza majukumu yake.

Bunge lilifikia uamuzi wa kutambua pande zote zinazopingana kwenye mgogoro huo baada ya Msajili kumwandikia Profesa Ibrahim Lipumba kumweleza kuwa amekubali ombi lake la kutaka Sakaya atambuliwe kama kaimu katibu mkuu, jambo ambalo linaonekana kuzidi kukigawa chama hicho.

Profesa Lipumba aliingia kwenye mgogoro na chama chake baada ya kuandika barua ya kujivua uenyekiti na kukaa nje kwa takriban mwaka mmoja kabla ya kurejea nchini na kuandika barua ya kufuta uamuzi wa kujiuzulu uenyekiti, jambo ambalo mkutano mkuu wa CUF ulilikataa na kuridhia kujiuzulu kwake.

Mgogoro huo umefanya kuwa na pande mbili; wa kwanza ukikubaliana na uamuzi wa mkutano mkuu wa kuridhia kujiuzulu kwa Lipumba, na wa pili ukikubaliana na kujirejesha madarakani kwa msomi huyo.

Upande wa kwanza unaendesha shughuli zake kutoka makao makuu ya CUF yaliyopo kisiwani Unguja na wa pili ukiwa ofisi kuu zilizopo Buguruni jijini Dar es Salaam.

Jana, kamati ya Bunge ya Katiba na Sheria ilimtaka Jaji Mutungi kuchukua jitihada za kuumaliza mgogoro wa CUF ili kuepusha athari kubwa zinazoweza kujitokeza katika Muungano.

Akisoma maoni ya kamati hiyo kuhusu utekelezaji wa Bajeti ya Ofisi ya Waziri Mkuu ya mwaka wa 2016/17 na ile ya 2017/18, mjumbe wa kamati hiyo, Joseph Mhagama alisema mgogoro huo unaweza kusababisha athari za Muungano.

“Katika mgogoro unaoendelea ndani ya CUF, Kamati inashauri Ofisi ya Msajili wa Vyama vya Siasa kuchukua jitihada za kutosha kusuluhisha mgogoro huo ili kuepusha athari kubwa zinazoweza kujitokeza katika Muungano,” alisema.

Mhagama alisema kamati hiyo inaiagiza Ofisi ya Msajili wa Vyama vya Siasa kuzingatia sheria, kanuni, taratibu na weledi katika kusimamia na utoaji wa ruzuku kwa vyama vya siasa na kuhakikisha kwamba taratibu hizo zinafuatwa katika utoaji ruzuku kwa vyama vya siasa.

Wakati wa uchaguzi mdogo wa Jimbo la Dimani na madiwani, Msajili alitoa ruzuku ya zaidi ya Sh300 milioni ambazo zilichukuliwa na upande wa Profesa Lipumba ambao ulibadilisha majina ya watia saini wa akaunti iliyokuwa wilayani Temeke.

Oktoba mwaka jana, Bodi ya Wadhamini ya CUF ilifungua kesi Mahakama Kuu dhidi ya Msajili, Profesa Lipumba na wanachama 12 waliosimamishwa. Pamoja na mambo mengine, bodi hiyo inataka Msajili.

Katika kesi hiyo, bodi inaiomba mahakama ibatilishe barua ya Msajili ya Septem,ba 23 mwaka jana iliyotengua uamuzi wa Mkutano Mkuu wa kukubali kujiuzulu kwa Profesa Lipumba, imzuie Msajili asiendelee kufuatilia suala la kufutwa kwa uanachama wa Profesa Lipumba na pia azuiwe kuingilia mambo ya CUF.

Jana akizungumza na gazeti hili kuhusu uamuzi wa Msajili kumtambua rasmi Sakaya kukaimu nafasi yake, Maalim Seif aalisema Jaji Mutungi ndiye chanzo cha matatizo ya chama hicho.

Alisema Profesa Lipumba si mwanachama wa CUF na pia si mwenyekiti wao kama anavyotambuliwa na Msajili.

“Tangu mwanzo Msajili aliamua kuchukua upande na kuwa pamoja na Lipumba na ndiye mshauri wake. Wanashauriana kwa kila hali, lakini bado ukweli unabaki pale pale kwamba Lipumba si mwanachama kwa mujibu wa katiba ya CUF,” alisema Maalim Seif.

Maalim Seif alisema hata kama Profesa Lipumba angekuwa ni mwenyekiti, hana uwezo kumuengua katibu mkuu wa CUF.

“Chombo ambacho kina uwezo wa kuwashughulikia na kumsimamisha mwenyekiti, makamu mwenyekiti au katibu mkuu ni Baraza Kuu la Uongozi la Taifa. Halafu kama kuna kesi wanapeleka mkutano mkuu ambao unafanya maamuzi,” alisema Maalim Seif.

“Hata huyo Magdalena Sakaya mwenyewe naye kasimamishwa uanachama, si mwanachama. Mutungi ndiye anaendelea kulivuruga suala hili kwa mapenzi yake kwa Lipumba au sijui anapata instruction (maelekezo), sijui. Lakini Lipumba si mwenyekiti wetu, si mwanachama wa CUF.”

Alisema uchaguzi wa wabunge wa Eala umeharibika kwa sababu ya Msajili kukubali waliowapendekezwa na Lipumba ambao si wanachama.

Katika uchaguzi huo uliofanyika Jumanne, Maalim Seif alipeleka jina la mgombea mmoja, wakati upande wa Lipumba ulipeleka majina matatu na ofisi ya Bunge ikayapokea yote, ikiyaweka majina hayo chini ya CUF “A” na CUF “B” kwa kuzingatia maelekezo ya Msajili.

Maalim Seif alisema Habib Mnyaa, ambaye alichaguliwa kuwa mbunge wa Eala baada ya jina lake kuwasilishwa na Sakaya, alifukuzwa uanachama na tawi lake na katiba yao inasema hawezi kurudi uanachama hadi miaka miwili ipite.

“Yote haya Mutungi ndiyo kayachukua yeye ndiyo anavuruga na anaendelea kuvuruga,” alisema.

Jana, Jaji Mutungi alisema hatazungumzia suala hilo tena na vyombo vya habari, ma kumtaka Maalim Seif asubiri uamuzi wa mahakama.

“Waandishi wa habari acheni kuendesha debate (mjadala) kuhusu suala hili kwa sababu liko mahakamani,” alisema Jaji Mutungi.

Jaji Mutungi ametoa onyo hilo wakati ameshtakiwa mahakamani lakini ofisi yake ikimwandikia barua Profesa Lipumba kukubali uteuzi wake wa Sakaya kuwa kaimu katibu mkuu.

Barua hiyo ya Machi 21 imesainiwa na Sisty Nyahoza wa ofisi ya Msajili na inamweleza Profesa Lipumba kuwa itampa ushirikiano Sakaya katika majukumu yake ya kukaimu nafasi ya katibu mkuu.

Kimenukaaa..Ofisi ya Mwakyembe Yakana Tetesi za Roma Kushikiliwa Polisi

$
0
0

Serikali kupitia Wizara ya Habari, Utamaduni, sanaa na Michezo imesema imepokea kwa mshtuko taarifa za kutoweka kwa Mwanamuziki Ibrahim Mussa kwa jina la kisanii “Roma Mkatoliki”  tangu tarehe 5 Aprili 2017.

Katika taarifa yake iliyotolewa jioni ya jana na kusainiwa na Kaimu Mkuu wa Kitengo cha Mawasiliano Serikalini wa wizara Zawadi Msalla, amesema kuwa wizara hiyo kwa dhamana yake katika tasnia ya sanaa, imefuatilia kwa karibu suala hilo kwa kuwa lina muelekeo wa jinai na kwamba hashikiliwi katika kituo chochote cha polisi.

"Hata hivyo taarifa kutoka vyombo vya dola zinathibitisha kuwa Roma Mkatoliki hashikiliwi katika kituo chochote cha polisi".Amesema Zawadi.

Amesema kutokana na hali hiyo, wizara imewaomba wadau mbalimbali na wananchi kwa ujumla kwa kushirikiana na Jeshi la Polisi kwa kutoa taarifa zozote zitakazo saidia kujua alipo msanii huyo.

Hata hivyo, mapema jana baadhi ya wasanii wa muziki na filamu nchini wamezungumza na wanahabari kuhusiana na hilo, na kutoa taarifa kuwa wamezunguka katika vituo karibu vyote vya polisi jijini dar es Salaam lakini hawajaweza kupata taarifa zozote kumuhusu Roma, huku wakidai kuwa Kamanda wa Polisi Simon Sirro ameahidi kulitolea ufafanuzi siku ya kesho Jumamosi.

Noma Sana..Husein Bashe Ashindwa Kuvuimilia..Afunguka Haya Mazito Kuhusu Sakata la Roma..!!!

$
0
0

Jana usiku taarifa za kukamatwa kwa msanii wa hip hop Roma Mkatolikia zilianza kuenea katika mitandao ya kijamii kwa kuripotiwa kuwa Roma Mkatoliki na Moni wakiwa studio za Tongwe Records walikuja kukamatwa na watu wasiojulikana na kuwapeleka kusikojulikana.

Watu mbalimbali ikiwemo wasanii mbalimbali wamekuwa wakionesha hisia zao juu ya tukio hilo kwa kutumia kurasa zao za mitandao ya kijamii kuoneshwa kuguswa na tukio hilo, mbunge wa Nzega Hussein Bashe ni miongoni mwa watu waliyotumia kuraza zao za instagram kuandika anachowaza kuhusu Roma.

"Who is behind all this? Ni genge ambalo limejipa mamlaka ya kupandikiza woga na chuki miongoni mwa jamii na kuharibu Taswira ya CCM. Tunawajibu wa kukataa woga ,Tunawajibu wa kutoruhusu Misuse ya vyombo vya Ulinzi na usalama, Tunawajibu wa kulinda Taifa letu

“Tunawajibu wa kupigania Values zilizopiganiwa na waasisi wa Taifa letu kama Mzee Karume na Mwl Nyerere, Tunawajibu wa kukataa ukandamizaji tukikaa kimya kwa kufikiri kuwa hayanihusu mimi yanamhusu yule yatakapokufika wewe hatakuepo mtu wa kukutetea na halitakuepo Taifa la Tanzania

“Sote tusimame tuseme hapana kwa mfumo huu unaoanza kuota mizizi kama mtu Ana makosa ufuatwe utaratibu wa kisheria kumkamata na sio utekaji tunakabiliwa na vita kubwa ya kupambana na Umasikini na kujenga Taifa huru la kiuchumi . 

"Umasikini ni hatari kwa usalama wa taifa sio nyimbo
#FreeRoma"

Noa Sana Aisee..Zitto Kabwe na Waitara Walilia Fedha Bungeni..Wadai Wabunge Hawapati Posho Kama Zamani..!!!

$
0
0

Mbunge wa Kigoma Mjini (ACT –Wazalendo), Zitto Kabwe amesema tangu Serikali ya Awamu ya Tano iingie madarakani, taasisi za uwajibikaji ikiwamo Bunge zinashindwa kufanya kazi kutokana na kutopewa fedha za kutosha.

“Mdhibiti na Mkaguzi wa Hesabu za Serikali (CAG) amenyimwa fedha. Hii inaonyesha kuwa Serikali haina dhamira ya kweli ya kuwezesha Bunge kufanya kazi yake kinyume kabisa na hotuba ya Rais John Magufuli wakati akifungua Bunge Novembea 2015,” amesema Zitto ambaye ni kiongozi wa chama hicho.

Zitto alikuwa akizungumzia taarifa kwamba, chombo hicho cha kutunga sheria kimekumbwa na ukata, kiasi kwamba kina fedha za muda mfupi ujao.

Mbuge wa Ukonga (Chadema), Mwita Waitara ameunga mkono kauli ya mbunge wa Mtwara vijijini, Hawa Ghasia akisema shughuli za Bunge zimedorora.

“Ni kweli kama alivyosema Ghasia kuwa Serikali imeshindwa kutoa fedha za miradi ya maendeleo kwa wizara mbalimbali. Hata kwenye Bunge imeathiri utendaji,” amesema Waitara.

“Kwa mfano katika kamati wabunge wanakwenda kwenye ziara, lakini hawalipwi posho. Wabunge wanakwenda kwenye ziara hawalipwi posho, mwisho kazi zinashindikana kufanyika.

‘Kamati za Bunge zilitakiwa kukaa kwa wiki tatu, lakini zimeishia kukaa wiki moja kwa sababu ya ukata. Wabunge wanashinda mchana kutwa bila kula. Tumemuuliza Spika akasema hakuna hela.”

Juzi, Ghasia ambaye ni mwenyekiti wa Kamati ya Bunge ya Bajeti, alisema wakati ikiwasilisha maoni kuhusu bajeti ya ofisi ya Waziri Mkuu kuwa kumeonekana changamoto kubwa ya Bunge kupewa fedha kwa wakati na hivyo kuathiri utekelezaji wa baadhi ya majukumu.

Kamanda Siro Kumsaka Roma na wenzake

$
0
0
JESHI la Polisi kanda maalum ya Dar es Salaam limeazimia kumtafuta msanii wa muziki wa Bongo Hip Hop Ibrahim Mussa, (Roma) wa wenzake.

Roma , Monii (msanii),(Bin Raden mtayarisha muziki wa studio hiyo) na emmanuel  walitekwa na watu wasiojulikana siku ya tarehe 5 Aprili mwaka huu usiku wa kuamkia alhamis kwenye kwenye makoa ya studio hizo.

Akizungumza na Waandishi wa Habari Kamshna wa Polisi Kanda Maalumu ya Dar es salaam Simon Sirro ,amesema kuwa tayari Jeshi la Polisi linamsaka Roma na wenzake pamoja na kuunda timu maalamu.

Kamanda Sirro amesema kuwa amesema kuwa jeshi hilo linaendelea na Upelelezi na kwamba tayari jarada wa uchunguzi wa tukio hilo tayari umeshaundwa.

Amewasisitiza wananchi kuliamini jeahi hilo na kuwa wavumilivu jeshi hilo likiwa linafanya uchunguzi.

Hata hivyo jeshi hilo  limewataka wananchi kuwa na imani na jeshi hilo



 

Thomas Ulimwengu kuanza kuonja utamu wa ligi kuu Sweden leo

$
0
0

Baada ya kupoteza mechi iliyopita, timu ya Mtanzania Thomas Ulimwengu leo Jumamosi itakuwa kwenye uwanja wake wa nyumbani wa Tunavallen kucheza na Oerebro katika muendelezo wa Ligi Kuu ya Sweden.

Katika mchezo uliopita, Eskilstuna ilifungwa mabao 3-1 na GIF Sundsvall hali iliyowafanya kushika nafasi ya 14 katika msimamo wa timu 16 za ligi hiyo. Hata hivyo hii ni mechi ya pili ya ligi hiyo.

Kocha wa Eskilstuna, Pelle Olsson leo atakuwa na chaguo la kumtumia Ulimwengu au la baada ya mshambuliaji huyo kupona majeraha ya kifundo cha mguu yaliyokuwa yakimuanda kwa muda mrefu.

Hata hivyo, itategemea na ripoti ya daktari na jinsi Ulimwengu alivyo tayari kulingana na mazoezi aliyofanya mapema wiki hii na kikosi cha kwanza baada ya kupona.

Kama mambo yataenda vizuri, straika huyo atakuwa ameianza safari yake ya kuitumikia timu yake hiyo aliyojiunga nayo hivi karibuni baada ya kumaliza mkataba na TP Mazembe ya DR Congo.

Meneja wa Ulimwengu, Jamal Kisongo hivi karibuni alisema Ulimwengu kwa sasa yupo tayari kwa mapambano baada ya kupatiwa matibabu maaalum kutibu majeraha yake.

“Nimewasiliana na Ulimwengu ameniambia ameshapona na yupo tayari kwa mapambano kuhakikisha anapata nafasi kwenye kikosi cha kwanza,” alisema Kisongo.

Sakata la Kina Roma ni Jambo la Kawaida Sana - Sirro..!!!

$
0
0

Kamanda wa Polisi Kanda Maalum ya Dar es salaam, Kamishina Simon Sirro amesema kupotea (kutekwa) kwa msanii Roma Mkatoliki na wenzake ni jambo la kawaida huku akisitiza kuwa hayajaanza kutokea leo kwani ni tukio kama matukio mengine.

Kamanda Sirro amesema hayo baada ya kelele za watu kwenye mitandao ya kijamii ndani ya siku tatu, huku wasanii, wanasiasa pamoja na wadau mbalimbali wa muziki kuja juu juu ya suala la kupotea vijana hao katika mazingira ya kutatanisha huku wengine wakihusisha tukio hilo na masuala ya kisiasa yanayoendelea nchini.

“Matukio ya utekaji hayajaanza leo, hili la kina Roma na wenzake ni tukio kama matukio mengine yaliyokuwa ya ujambazi kwa hiyo tupeni muda tupeleleze, tukifika mahali pazuri tutawaita tuwape taarifa lakini nimeona mitandao mingi inazungumza, jana nikaona wasanii wamekutana lakini nikajiuliza hivi yangekuwa haya matukio yanatokea ya uhalifu yanapotokea watu wanakutana ingekuwaje ?,Jamani kazi hii tumepewa kwa mujibu wa Katiba na ni lazima tutimize wajibu wetu kwa hiyo tupeni muda tutakuwa na majibu mazuri katika hili”. Alisema Kamishna Sirro pindi alipokuwa anazungumza na waandishi wa habari ofisni kwake Jijini Dar es Salaam

Aidha Kamanda huyo amesema mpaka sasa wameshaunda timu ya uchunguzi na inaendelea vizuri katika upelelezi huku akiwataka wananchi kuwa na subra kwa kuwa upelelezi ndiyo utasema kila kitu.

Kwa upande mwingine amewataka watu waache tabia ya kujifanya wao ndiyo ‘Kamishna Sirro’ na kutaka kuzungumzia habari za upelelezi hivyo amewataka watu kuliamini jeshi la Polisi kwa kuwa hawapendi vitendo hivyo viwepo na viendelee kutokea.  

Tesisi:Roma apatikana, yupo kituo cha Polisi Oysterbay

$
0
0

Msanii Roma Mkatoliki anadaiwa kupatikana na yupo Kituo cha Polisi Oysterbay jijini Dar.

Habari ya akina Roma kupatikana imethibitishwa na Mkurugenzi wa Tongwe Records J. Mada.

Bado hakuna maelezo ya kutosha kuhusiana na wapi walipokuwa na nani waliokuwa wamewashikilia. Kwa sasa wanadaiwa kuwepo kituoni hapo kwa taratibu za kipolisi kwa kuwa jalada la kupotea kwao lilifunguliwa hapo.

Kupatikana kwao kumefuatia wito mkubwa uliokuwa ukipaishwa na wasanii wenzake na mashabiki kuhusu kuachiliwa huru, ndani na nje ya mitandao ya kijamii.

Awali, Kamanda wa Polisi Kanda Maalum ya Dar es salaam, Kamishina Simon Sirro alisema bado walikuwa wakiendelea na upelelezi wa tukio la kupotea (kutekwa) kwa msanii Roma Mkatoliki na wenzake.


Taarifa zaidi zinafuata..
Viewing all 104689 articles
Browse latest View live




Latest Images