Quantcast
Channel: UDAKU SPECIAL
Viewing all 104709 articles
Browse latest View live

Bashe Afunguka Haya azito Kuhusu Mchanga wa Madini Uliokamatwa na Rais Magufuli..!!!

$
0
0

MBUNGE wa Nzega Mjini, Hussein Bashe(CCM), ameiomba Kamati iliyoundwa na Rais John Magufuli kwa ajili ya kuchunguza makontena ya mchanga katika Bandari ya Dar es Salaam, kurekori kilichomo katika makontena hayo ili yaoneshwe kwenye televisheni kwa lengo la kuwaondoa hofu Watanzania.

Ombi hilo limekuja siku chache baada ya Rais Magufuli kuunda Kamati kwa ajili ya kuchunguza makontena ya mchanga katika Bandari ya Dar es Salaam.

Alitoa ombi hilo bungeni mjini hapa wakati akichangia hotuba ya bajeti ya Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Ofisi yaWaziri Mkuu kwa mwaka 2017/2018.

Alisema wengi wanaamini kwamba yale makontena yaliyokamatwa bandarini yana dhahabu.

“Spika kule kwangu Nzega wanaamini yale makontena yaliyopo bandarini yana dhahabu,tunaomba mrekodi hili tukio la uchunguzi halafu mtuoneshe kwenye TV tuone kilichomo ndani ya zile kontena,” alisema.

Alisema yeye ni miongoni mwa watu ambao wanaamini kwamba uwekezaji wa migodi mikubwa haujasaidia nchi ya Tanzania.

“Mimi ni miongoni mwa watu tunaoamini kwamba uwekezaji wa migodi mikubwa hauijaisaidia nchi yetu,”alisema.

Mbunge wa Gairo, Mohamed Shabiby (CCM), amepongeza hatua ya serikali kupiga marufuku matumizi na biashara ya pombe maarufu kama viroba ambapo alisema kuwa hivi sasa watu wamenenepa kutokana na kuacha kutumia kinywaji hicho.

Aliishauri pia serikali kutafuta namna bora ya kuzuia uwepo wa kinywaji hicho akitaka waanzie kwenye uzalishaji badala ya sokoni kama ambavyo wamefanya wakati wa kutekeleza zoezi hilo hivi karibuni nchini.

Breaking Newss..Nape Moses Nnauye Afyatuka Mazito Kuhusu Sakata la Kufutwa Uwaziri na Magufuli..Ataka Aliyemnyooshea Bastola Akamatwe Lasivo Atafichua Makubwa ya Utawala wa JPM..!!!

$
0
0

Dar es Salaam. Mbunge wa Mtama, Nape Nnauye amezungumza na wapiga kura wake leo katika kijiji cha Chihuta huku akieleza kuwa yeye ndiye aliyemtafutia kura Rais John Magufuli katika kampeni za uchaguzi wa mwaka 2015.

Kadhalika Nape alizungumzia tukio la kutolewa bastola alipotaka kuzungumza na waandishi wa habari hivi karibuni na kuvitaka vyombo vya ulinzi na usalama vichukue hatua.

“Shida niliyonayo wapiga kura wangu huyu jambazi aliyetoa silaha vyombo vya ulinzi nausalama vinafanya nini,” alisema

 Alisema kutokana na tukio lile, alihitaji busara zaidi na kutulia kwani kifua chake kina mambo mengi.

Rasmi..Roma Mkatoliki Apatikana ..Kaka Yake Afunguka Alipokuwa..!!!

$
0
0

Msanii Ibrahim Musa maarufu kama Roma Mkatoliki amepatikana na sasa yupo katika kituo cha Polisi cha Oyesterbay jijini hapa.

Kaka wa Roma,Omar Musa amesema Roma alirudishwa nyumbani saa tisa alfajiri leo, na kwa sasa yupo kituo cha Oyesterbay.

 Hata hivyo Omar hakutaka kueleza kwa kina kuhusu kurejea kwa Roma akisema kuwa hadi familia itakapotoa tamko.

Roma na wenzake wanne, walitekwa wakiwa katika studio za Tongwe, zilizopo Masaki, jijini hapa hivi karibuni.

Ukweli Mchungu...Hii Ndio Sababu za Faru Fausta Kutumia Sh760 kwa Ajili ya Matunzo Tu..!!!!

$
0
0

Hakuna bosi yeyote serikalini anayelipwa zaidi ya Sh17 milioni baada ya Serikali ya Awamu ya Tano kuanza kutekeleza sera zake za kubana matumizi, lakini yupo kiumbe hai mmoja tu ambaye matumizi yake yalifika Sh64 milioni kwa mwezi; na kuna sababu za kuhalalisha gharama hizo.

Kiumbe huyo ni mnyama mwitu aina ya faru aliyepewa jina la Fausta, ambaye sasa anatumia Sh20.4 milioni.

Fausta ndiye faru kikongwe kuliko wote nchini, akiwa na umri wa miaka 54, na anahitaji matunzo mazuri ili aendelee kuvuta watalii na wanasayansi kutoka kila pembe ya dunia.

Fausta anaishi Hifadhi ya Ngorongoro ambako analindwa kwa saa 24 kumuepusha kushambuliwa na wanyama wengine kama fisi na mbwa mwitu kutokana na uzee, lakini gharama za ulinzi zitapungua baada ya kupata makazi salama ndani ya mwitu jengo lake litakapomalizika.

Hiyo ni sehemu tu ya gharama zinazomfanya Fausta kutumia fedha nyingi zaidi ya mfanyakazi mwandamizi wa serikalini.

Kazi ipo kwenye malisho

Imeelezwa kuwa sababu zinazofanya matunzo ya Faru Fausta kutumia jumla ya Sh768 milioni kila mwaka ni pamoja na ulinzi, chakula chake kuagizwa kutoka nje na miwa anayotakiwa kula.

Sakata la Faru huyo kutumia kiasi hicho cha fedha liliibuliwa juzi na Mbunge  wa Babati Mjini (Chadema), Pauline Gekul alipoelezea gharama hizo na Serikali kuthibitisha.

Hata hivyo, Serikali imesema gharama hizo ni za kawaida kulingana na thamani na umuhimu wa mnyama huyo ambaye jamii yake iko hatarini kutoweka.

Meneja wa maendeleo ya tafiti na Ikolojia wa Hifadhi ya Ngorongoro, Asantaeli Merita alisema jana kuwa matunzo yake yalianza kugharimu fedha nyingi baada ya kuanza kutunzwa katika eneo maalumu.

Alisema katika eneo hilo ilibidi kujengwa banda lake la kuishi na uzio wa chuma ambao si rahisi faru huyo kuvunja na kutoka nje. Banda hilo limezungushiwa mbao maalumu.

Merita alisema kutokana na faru huyo kuwa katika eneo hilo, kuna askari 15 maalumu ambao wanamlinda kwa zamu kwa saa 24 na kuna gari ambalo ni la mahitaji mbalimbali, ikiwa ni pamoja na kubeba majani ya lishe kila siku.

Alisema ili kudhibiti maradhi ambayo faru huyo amekuwa akiugua, Hifadhi ya Ngorongoro imekuwa ikigharamia chakula cha virutubisho aina ya luseni ambacho kinapatikana nchini Kenya na amekuwa akipelekewa chakula hicho mara mbili kwa mwezi.

Alisema luseni anayotumia Fausta ni tofauti na luseni ya ng’ombe wa maziwa ambayo inapatikana hapa nchini.

Alisema faru huyo ‘kikongwe’ pia amekuwa akipewa miwa ambayo inapatikana eneo la Dareda mkoani Manyara. Miwa hiyo humsaidia kuboresha afya yake na imekuwa ikipelekwa mara mbili kwa mwezi.

Merita alisema kuna dawa zake ambazo anapaswa kuzitumia kila baada ya wiki mbili.

“Hiyo gharama ya milioni 64 ni ya mwanzo tu baada ya kuanza kuhifadhiwa, lakini baada ya kupatikana eneo la kumuhifadhi na kujengwa itapungua sana,” alisema.

Alisema baada ya kukamilika ujenzi wa banda maalumu la kumuhifadhi kwa sasa wastani wa gharama kwa mwezi zitakuwa Sh20.8 milioni.

Merita alisema kwa maendeleo ya hifadhi ni muhimu kwa Fausta kuendelea kupatiwa matunzo maalumu kwa kuwa  licha ya kuingiza fedha nyingi za kigeni, pia amekuwa akitumika katika tafiti za wataalumu wa hifadhi za asili.

Mamlaka ya Hifadhi ya Ngorongoro imekuwa ikiingiza zaidi ya Sh70 bilioni kwa mwaka kutokana na watalii ambao wanafika kutembelea eneo hilo. Karibu nusu ya watalii wanaokuja nchini, hutembelea Hifadhi ya Ngorongoro.

Katika kipindi cha maswali na majibu bungeni, Gekuji alihoji mpango wa Serikali kwa faru huyo kutokana na gharama kubwa za kumtunza.

“Hifadhi ya Ngorongoro inatumia gharama kubwa, ikiwa ni pamoja na kumtunza na kumlisha Faru Fausta. Kiasi cha Sh64 milioni kinatumika kwa mwezi. Je, Serikali ina mpango gani na huyu Faru Fausta,” alihoji Gekul.

Akijibu swali hilo, Waziri wa Maliasili na Utalii, Profesa Jumanne Maghembe alisema ni kweli mnyama huyo anatunzwa kwa gharama kubwa kwa sababu ni mzee na ananyemelewa na magonjwa mbalimbali.

Waziri alisema wanafanya hivyo kutokana na ukweli kuwa wanyama wa aina hiyo ni wachache katika hifadhi, akasema utafiti unafanyika ili gharama za kumtunza ziwe ndogo kulingana na thamani inayopatikana. Kiwango hicho cha fedha kilisababisha Mbunge wa Tunduma (Chadema), Frank Mwakajoka kuomba mwongozo wa Spika.

”Majibu ya waziri anasema Faru Fausta yupo na anatunzwa kwa Sh64 milioni kwa mwezi. Tafsiri yake ni kwamba anatunzwa kwa Sh768 milioni kwa mwaka. Anatoa sifa eti kwa sababu ni mzee sana, naomba mwongozo wako kuhusu hili kwa sababu mnyama huyu hawezi kuingiza faida yoyote,” alisema Mwakajoka.

Akitoa mwongozo wake Spika Job Ndugai alisema suala hilo anaiachia wizara.

Nimekuwekea Hapa Orodha ya Nchi Zenye Matajiri Wengi Zaidi Duniani..Tanzania Wapo..?

$
0
0
Baada ya Shirika la Fedha duniani ‘IMF’ kutangaza kuongezeka kwa uchumi wa dunia ukilinganisha na mwaka 2016, leo April 8 2017 nakusogezea list ya nchi zenye mabilionea wengi zaidi duniani kwa mwaka 2017, kwa mujibu wa tovuti ya takwimu Statista.

Takwimu hizi zinaonesha China ndiyo nchi yenye mabilionea wengi duniani ambao ni zaidi ya 609 ikifuatiwa na Marekani yenye mabilionea 552. Katika list hii Sweden inakamata nafasi ya mwisho ikiwa na mabilionea 17.



Hataree..Aliyetengeneza Virusi vya Ukimwi Aibuka..Adai Walikuwa na Lengo la Kutaka Kuamaliza Watu Weusi na Mashoga Duniani..Afunguka Haya Makubwa Kuhusu Tiba Yake..!!!

$
0
0

Ameua maelfu na maelfu ya watu, alitengeneza ugonjwa huu mnamo miaka ya 1970, na sasa daktari huyu kwa jina Robert Gallo ametoka adharani na kusema amepata dawa ya kutibu ugonjwa huo.

Robert Gallo anaelezwa kwamba alihusika na vita vya kibaiolojia kwa lengo la kuwaondosha watu weusi na mashoga duniani katika miaka ya 1970..

Kimenukaa...Askofu Gwajima Afunguka Haya Mazito Baada ya Diamond Kumuimba,,Adai Kesho Lazima Amlipue Kanisani Kwake...!!!

Kimenukaaa..Nape Aaanzisha Vita na Makonda..Afunguka Mazito Jinsi Ilivyokuwa Hadi Akatumbuliwa..Adai Makonda Anamchonganisha Rais na Wananchi .Amtaka Kuchukua Hatua Haraka..!!!!

$
0
0
 Kwanza niseme nawapenda sana, nawashukuru sana kwa mapokezi makubwa mliyonipa, Kilichinitoa machozi ni heshma kubwa mliyonipa kina mama. Mlilala chini, mkataka nipite juu yenu, sio jambo ambalo nilitegemea, nawashukuru sana. Niwaahidi nitafanya kazi kwa nguvu zangu zote, kuwatumikieni, usiku na mchana, ntaikumbuka heshima mliyonipa na hio itanisukumu.

Mmenipa heshima kubwa mpaka ntaenda nayo kaburini, pengine sikustahili, upendo wenu umegusa sana moyo wangu. Ntatumia mpaka senti yangu ya mwisho kuhakikisha jimbo la Mtama lina maisha bora. Niwashukuru Steve Nyerere na kundi lake, waandishi wa habari leo wote wamekuja Mtama.

Nilitaka kuongea Dar es Salaam, ikatokea fujo kidogo, Nimeamua kuja nyumbani na leo nitasema.

Mimi ni mtoto wa Kimakonde na nimefundishwa kusema kweli, nimshukuru Rais ambae nilipigana kufa na kupona kuhakikisha anakuwa Rais, nilipata ajali mabya usiku wa manane wakati natoka kutafuta kura. Watanzania wakatupa dhamana na nikapata heshma ya kuwa kwenye baraza la mawaziri moja kwa moja bila kuwa naibu waziri.

Sina mashaka kuwa nilifanya kazi nzuri kwa akili yangu yote kuhakikisha dhamana niliyopewa nameifanyia haki, kama yupo anadhani sikutenda haki asimame hadaharani. Wakati nateuliwa hakukuwa na majadiliano.

Karatasi ukiisoma haina sababu, yalikuwa ni mabadiliko ya kawaida kulingana na Rais. Wakati mwingine ukiwa na mchezaji mahiri na mkafunga magoli ya kutosha, mnampumzisha akacheze tena kesho.

Siku nne au tano kabla ya mabadiliko nilisema mambo kama hayaendi sawa mimi ntajiuzulu. Nilisema kazi hii ngumu na ikithibitika amevamia kituo cha habari, mimi waziri sitatakiwa kubaki madarakani, watu tunatakiwa kuishi kwenye maneno yetu, mimi no mtoto wa mzee Nnauye, ukifika mahali usiyombishwe na cheo.

Kocha ameamua, hakuna sababu ya kumnunia, mechi ikikamata ntarudishwa uwanjani, mimi ni mchezaji bora.

Kwenye sakata hilo kuna mambo ya kipuuzi, haya nitasema. Nikiwa njiani kurudi kutoka Arusha, kuna watu walisema kwenye mitandao Nape amekamatwa, baada ya kukanusha wakaenda kuwaondoa waandishi wa habari hoteleni.

Nilipofika nikakuta waandishi wa habari wamefukuzwa hotelini kwa ubabe, wakaenda nje na mwenye hoteli abaki na hoteli yake. Wakamwaga vijana wengi, nikisema vijana mnawajua. Mimi ninajua, nimekaa miaka 16 ndani ya CCM na nilijua kilichokua kinaendelea na bahati nzuri wanahabari wakaonyesha lile tukio live.

Nilivyofika nikawaona wale vijana, yule kijana mliemuona mpuuzi, akasogea karibu yangu, nikamnong'oneza tuko moja kwa moja vyombo vinaangalia, nikafikiri wana akili, nilisema kulinda sura ya nchi yangu, vyombo vya Dola na Rais wangu. Nilikuwa nasitiri nchi yangu, mpuuzi haoni, nikamwambia niliyonayo ni kubwa kuliko yako, sema nikaona wote tutakuwa wapuuzi.

Nikaingia ndani ya gari na kutoka juu ili aje, ilihitaji busara na nikiwaambia sina nia mbaya. Sikuwa na haja kuharibu kazi ya mikono yangu mwenyewe.


Hivi nani aliweka mguu, Edward asiende mbele? Wao walikuwa kwenye meza ndefu wanakunywa bia wakati wengine tunatafuta kura ndio maana nilikasirika na naamini mtanisamehe kwa kukasirika kwango, mimi ni banadaamu na nina nyongo, nilikumbuka mengi sana.

Kitenndo kilichofanyika hakikuwa cha kiungwana na namshukuru waziri wa mambo ya ndani kusema sina rekodi ya uhalifu.

Nilisubiri wamtafute, na wanasema sio polisi, leo nyoosha bastola hewani uone kama polisi hawajaondoka na wewe na pale alikuwepo RPC.

Siamini kama alitumwa kuonyesha silaha, mimi ukinitolea silaha naoa kama mic tu. Shida niliyonayo huyu jambazi alietoa silaha, vyombo vya ulinzi na usalama vinafanya nae nini. Kama wameweza kumfanyia Nape, watanzania wangapi watafanyiwa huku mitaani. Vingenevyo wataonewa wengi, naamini wako wengi wametolewa huko, Kijana mmoja wa CHADEMA, Ben Saanane amepotea kwa miezi mingi, watu wamevamia kituo na wameonekana, tusema alieonekana sie yeye, nani alieagiza mtu akiwa na vyombo vya ulinzi na usalama kuvamia studio. Matukio haya yanawafanya watu waishi kwa hofu

Dar imevamiwa studio akiwemo Roma Mkatoliki, sikwenda CCM kwa sababu mzee Nnauye yuko CCM, nilienda CCM kwa sababu ya imani ilikuwa CCM, sema kweli fitna kwangu mwiko.

Kazi ya msingi ya kikatiba ya serikali, ni kulinda raia na mali zao, ombi langu kwa serikali na Rais aunde tume huru iyachunguze matendo haya ili yasijirudie tena. Mimi nimewasemehe ila haya matendo mengine, yanamjengea chuki yeye(Rais) na wananchi kwa sababu wanadhani ni yeye ndie anaewatuma.

Matendo haya yanachonganisha CCM na wananchi, huko mtaani watu wanasema, namshauri kama mwenyekiti wa chama changu, watu wachche wanaotumia mamlaka waliyopewa kuumiza watu, lazima tume iiundwe.

Ukweli Mchungu.. Hizi Ndio Mbinu Chafu Zinazotumiwa na Maadui wa Rais Magufuli..!!!

$
0
0

Nimekuwa nikisoma "comments" nyingi sana zinazohusu kutekwa kwa Roma Mkatoliki na nyingi kati ya hizo comments zinamlaumu Rais Magufuli na Serikali yake. Hata alipopotea Ben Saanane, watu walikuwa wanaishutumu Serikali ya Rais Magufuli.

Mimi ningependa kuhoji; hivi ninyi mnaoishutumu Serikali mna uhakika gani kuwa Serikali ndiyo inahusika na mambo haya?
Binafsi naamini na ninatambua wazi kuwa hakuna uthibitisho wowote ule unaoonyesha kuwa Serikali ndiyo inahusika.

Serikali yoyote ile duniani huwa na maadui. Hakuna Serikali isiyokuwa na maadui hapa duniani. Hata Serikali yetu inayoongozwa na Rais Magufuli pia ina maadui. Maadui hawa hawapendi kuona Rais wetu Magufuli anaendesha nchi hii kwa amani na mafanikio. Maadui hawa watafanya kila wawezalo ili kumchafua Rais na Serikali yake mbele ya macho ya Watanzania na mbele ya jamii ya kimataifa pia.

Inavyoonekana sasa hivi, maadui hawa wanatumia nafasi iliyojitokeza sasa hivi hapa nchini au mwanya uliojitokeza kufanya uhalifu kwa kisingizio kuwa Serikali ndiyo inahusika. Kuna watu wako tayari hata kutoa roho za wenzao ili mradi tu malengo yao yafanikiwe. 

Mimi nina mashaka sana tena sana na baadhi ya vyama vya upinzani hapa Tanzania. Vyama hivi vikiongozwa na chama fulani hivi, vinaendesha siasa chafu sana hapa nchini ili tu kuhakikisha taswira safi ya Serikali ya Rais Magufuli inachafuliwa kwa gharama yoyote ile.

Kuna baadhi ya waliokuwa viongozi wakubwa tu hapa nchini waliokuwa kwenye madaraka nyeti, sasa hivi wako kwenye upande wa upinzani na viongozi hawa siyo "MALAIKA". Ni watu wenye uchu wa madaraka, ni watu wenye mbinu chafu sana za kutafuta madaraka, ni watu wa kufanya siasa za "matukio" na "maigizo". Watu hawa ni hatari sana kuliko tunavyofikiria, ni hatari sana tena sana.

Nafahamu kuna baadhi yenu mtatukana sana hapa, lakini amini nawaambieni, ukweli utafahamika na mtabaki midomo wazi.

Kila serikali hapa duniani ina namna ya kuwashughulikia watu wenye kuhatarisha uwepo wa serikali husika. Hata Serikali yetu pia ina namna ya kuwashughulikia watu wenye kuhatarisha usalama wa nchi hii, lakini siyo Roma wala siyo Ben saanane. By the way who is Roma Mkatoliki to the government? Roma is no body.

Kama ni kuwashughulikia watu, basi mimi nafikiri Lissu angekuwa wa kwanza, tena siku nyingi sana na siyo Ben Saanane au Roma. Kama ni kuwafunga midomo watu, basi Lema angeshapotezwa siku nyingi sana na siyo Roma. Msijidanganye, kati ya hao niliowataja hakuna mwenye uwezo wa kujificha ama kujilinda iwapo Serikali itaamua kwa dhati kumshughulikia na kumpoteza mazima! Hakuna mwenye uwezo wa kujilinda hata awe nani.

Watanzania kuweni makini sana na mambo yanayofanyika sasa hivi hapa nchini. Msikimbilie kumtukana na kumlaumu Rais Magufuli kumbe chawa anayewatafuna mmembeba wenyewe kwenye nguo zenu.

Serikali inalitambua hili na inajua ni nani anayehusika na mchezo huu mchafu na It's just a matter of time, kila kitu kitajulikana. Serikali ina mkono mrefu sana na mbinu hii inayotumiwa na "MAADUI" imeshajulikana na sasa hivi kuna kazi maalumu "inaendelea". Kazi maalumu ambayo wewe au mimi hatutatangaziwa au kujulishwa ni namna gani inafanyika.

Rais Magufuli, wewe piga kazi na wala usiyumbishwe na mbinu chafu za hawa wahuni wachache wanaotaka kukumaliza. Tuko pamoja na wewe Rais wetu mpendwa.

RAIS WANGU MAGUFULI: Waziri Wako wa VIWANDA Ndio Atakayetuangusha Kwenye Tanzania ya Viwanda..!!!!

$
0
0

niseme tu ukweli kuwa viwanda havijengwi siku moja pengine hata mwaka mmoja!

mwanzoni wananchi waliaminishwa kuwa serikali ndo itajenga viwanda lakin baadae mambo yalibadilika tukaambiwa wawekezaji ndo watakuja kujenga viwanda!

wazungu na wachna wanatucheka sana kwa kuwa hatujui tunatoka wap tunaelekea wapi!


mwijage kamuangusha rais kwa kuwa hakuja na mpango wa kweli wa kujenga viwanda! huwezi kutuambia kuna kiwanda cha matrekta kinajengwa wakat hakuna hata malighafi moja ya trekta inayotengenezwa nchini, Hiyo ni ASSEMBLY kwa maana hata goroli au taa ya trekta inatengenezwa nje huko! na kiwanda kitaishia kuleta ajira ya watu 50 tu
hv mfano kwa kuwatumia hata SUMA JKT tungeanza na kujenga kiwanda kama cha SAMAKI, tukanunua meli zetu hata mbili kubwa za maana zenye crane ya kukamata samaki wakubwa kabisa! kwanza kiwanda kingekuwa pure and 100% tanzanian! 

kiwanda hchohcho cha samaki kingetoa BYPRODUCTS ambazo tungetengeneza hata chakula cha kuku, mafuta ya samaki na mbolea ya asili pia! hapohapo tungetengeneza ajira kibao ukianzia baharini ajira, kiwandani ajira, wasambazaji ajira, wauzaji ajira, yan mji ajira ajira ajira! huo ni mfano tu wa kiwanda kimoja ambacho hata gharama yake ingekuwa ndogo na soko lake la uhakika wa 100% hata kama tungeuzia jesh tu kiwanda kingepata mabilioni kila kukicha!

halafu tungekuwa tunauziana samaki hata elfu 4 kwa kilo

swali langu kwa mwijage je hata kiwanda hcho cha mfano kinahtaji uwekezaji kutoka nje au waziri na wewe upo kwenye mpango wa kumuangusha raisi wetu!??? 

swali la pili, je kwa kutumia mfano huo wa kiwanda cha samaki je ingeshndikana kujenga viwanda vingi vya kutumia malighafi zetu wenyewe ambavyo ving vingetokana na mazao ambayo yangewapa ajira kubwa watanzania? jaman mwijage hata kiwanda cha karatasi ambacho miti ipo iringa? hujaona hlo mpaka ulete kiwanda cha ku ASSEMBLE mavitu yaliyokwisha tengenezwa nje? hapa panatia shaka !

najua wapo watakaonizodoa na kusema sina maana lakin ukweli utabakia ukweli, huwezi kushndana na wazungu eti kutengeneza magari wakati wao walishajiimarisha kwa miaka zaid ya 200!

I wish ningekuwa mie ndo waziri wa viwanda! haki ya mungu leo hii tayari ningeshajenga viwanda na ela ya magufuli ningekuwa nimesharudisha na faida kibao mpaka sasa rais angekuwa anafurahia matunda ya kuhubiri viwanda huko na huko wakat wa kampeni! napata uchungu wa kutaman hata kukata kichwa cha mtu kumuweka alama tu ajue alikosea!

lazima kufanya uthubutu sio kutegemea wawekezaji hadi kiwanda cha kugharimu bilioni 5 unaleta mwekezaji ni aibu!



mwijage ana maneno mengi sana mdomoni mpaka anakera! umemdanganya raisi eti kuna viwanda elfu 52 khaaaa! yan hata mtu akiwa na cherehani mbili za kushona nguo basi imekuwa kiwanda khaaaa:confused::(:rolleyes:

tupishe bwana mwijage muda unaenda na unaweka kiwingu sie tunataka viwanda vya watanzania sio wahindi na wachna!

uwezo tunao na nia tunayo tukiamua tutatoka hapa tulipo

Imevujaaa... Mkuu wa Freemason Duniani Kutua Tanzania na Mafreemason 300 Kushuhudia Live Tukio la Kuuchoma Moto Mwili wa Aliyekuwa Mkuu wa Freemason Tanzania ...!!!!

$
0
0

Mazishi ya mkuu Sir Andy chande (88 years) aliyefariki huko Nairobi Kenya yanatarajiwa kufanyika Jumanne ijayo kwa mwili wake kuchomwa moto mpaka kuteketea wote (cremation.)

Wageni zaidi ya 300 kutoka nje ya nchi wakiongozwa na Freemason mkuu watahudhuria mazishi yatayofanyika hapa Dar. Booking za guest watazofikia wageni mashughuli wa freemason zinaendelea kufanyika kwa kasi ya ajabu hapa jiji zina la dsm.

Kumbuka Sir Andy chande alikuwa kiongozi wa Freemason, mmiliki wa shule ya shaaban Robert, Ashawahi kuwa mkuu wa makumbusho ya Taifa (mkabala na IFM).

Askofu Gwajima Aposti Ujumbe Huu Tata ..!!!

$
0
0

Mtu akichukua mateka atachukuliwa mateka, mtu akiua kwa upanga, atauawa kwa upanga, hapa ndipo penye subira na imani ya watakatifu 
Ufunuo 13:10 

NA HILI NDILO NENO LA MUNGU.

Duh..Tazama Hapa Video ya Nape Nnauye Akipita Juu ya Migongo ya Wanawake Waliolala Chini Wakati Wakimpokea Kama Mfalme Leo Jimboni Kwake..!!!

Kimenukaaa..Baada ya Gwajima Kudai Kesho Atamgeuza Diamond Kuwa Maji..Diamond Aibuka na Kuandika Haya Kumjibu Askofu Gwajima..!!!

$
0
0

“Yala! Yala! Jamani Mwenzenu nimeyatimba😟….. lakini mi nafkiri watu wanatakiwa waiskilize hii nyimbo kwa umakini sana tena sana na wataelewa nini ilikuwa maana yangu haswa… Hususani kama kipengele nilichomtaja mzee wangu @Bishopgwajima nilisema: “mara nasikia vya aibu Konda na Gwajima eti ugomvi umekolea….ila kuchunguza kwa karibu ni kuna binti mmoja tu ndio kwa mitandao anachochea…”
Point yangu ni kwamba licha ya kweli kuna yaliyojiri nyuma, lakini kwa busara zao ninazoamini wamejaaliwa na Mwenyez Mungu muda si mref wangekaa chini na kumaliza…nawote kufurahi kwa pamoja, lakini kwakuwa kuna dada mwingine alikua anachochea hawa ndugu zetu wazidi kufarakana…ikapelekea hadi kufikia hapa…asa hapo kosa langu mie liko wapi?😭
Chonde chonde mzee wangu @Bishopgwajima usinigeuze maji kesho 👐, mana nakujua ukimuamulia mtu…. naweza jumapili ya kesho nikaiona chungu Mwaka mzima😁😆😅,” aliandika Diamond Instagram.

Fahamu Maswali 40 Ya Msingi Ya Kumuuliza Mwanamke Mnapokuwa Faraghani..!!!

$
0
0

Ushawahi kutoka deti na mwanamke halafu ukafikia mahali katika chat yenu unaishiwa na maneno ya kuongea?

Ama umeagana na mwanamke mtoke deti siku ya pili halafu umekuwa ukikesha siku nzima ukiwaza ni maneno ama ni usemi gani utakaoongea siku ya pili wakati ambapo mtakutana?

Well, usiogope. Hapa umefika kwa zahanati ambayo itakutibu matatizo yako.

Hapa tumekuandalia maswali 40 ambayo utayatumia kumuuliza mwanamke na kuyafanya maongezi yenu yavutie na kumfanya mwanamke apendezeke na wewe hadi mwisho.

Well. Kabla ya kuorodhesha maswali haya kuna mambo ambayo unapaswa kufahamu:

Anza kwa kumsifia ama kumpendezea kwa mambo anayofanya mfano unaweza kumsifia vile alivyovalia, kazi yake, umbo lake nk.
Wakati utakapokuwa unamuuliza mwanamke haya maswali, hakikisha ya kuwa unatoa nafasi ya angalau sekunde 30 kabla ya kumuuliza swali la pili, yaani usimmiminie maswali yote wakati mmoja.
Hakikisha kuwa haulazimishi maswali yako, mwanamke akikataa kujibu swali lako jipe shughli kiasi kv unaweza kucheza na vidole vyako ama jambo jingine kabla kumuuliza swali lingine.
Baadhi ya mambo ambayo pia unapaswa kuzingatia katika rodha ya maswali haya ni kuwa:

Unapaswa kuyachanganya maswali yako. Maswali tuliyoyaorodesha hapa ni maswali yaliyowazi, yaani yanaweza kupanuliwa yakazua mada nyingine. Anza na maswali sahili kuangalia iwapo mwanamke unayezungumza naye anapenda kuongea au la. Pia muulize maswali yaliyo wazi ili kuongeza hoja yako.

Usimakinike na orodha ya haya maswali. Tumia maswali machache ambayo unayaona unaweza kuyatumia halafu ujeuza mada yako uanze kuongea maswala yako. Ukimakinika kutaka kutumia maswali haya yote basi unaweza kumfanya akuone hauvutii na anaweza kuboeka na wewe haraka sana.

Usihifadhi maswali haya. Hili ndilo jambo baya zaidi la kufanya. Ukikaa na deti wako huku ukirudia swali la kwanza hadi jingine unaweza kumfanya mwanamke aone kwamba unamfanyia mahojiano ya kazi. Unachohitajika ni kusoma baadhi ya maswali haya, yahifadhi kwa simu yako halafu yatumie wakati ambapo maongezi yako yanafifia.


Maswali yenyewe ni kama ya fuatayo...

1. Unaipenda hii sehemu?

2. Huwa unapenda kunywa kinywaji gani?

3. Mapochopocho unayoyapenda ni yapi?

4. Ushawahi kuja hii sehemu awali?

5. Siku yako ilikuwaje?

6. Unafanya kazi wapi?

7. Huwa unapenda nyimbo aina gani?

8. Unapenda salad aina gani?

9. Ni mkahawa gani unaoupenda zaidi?

10. Ni movie aina gani unapenda kuangalia zaidi?

11. Ni mambo gani unapenda kufanya baada ya kutoka kazini?

12. Unafanya mambo gani ili kujifurahisha?

13. Ulisomea wapi?

14. Sehemu gani unaipenda sana zaidi kwa likizo zako?

15. Ni kitu gani unapendekezea ili kuinjoy siku yako?

16. Je wewe ni mtu wa kufuga mnyama gani? Paka ama mbwa?

17. Kama ungetawala dunia, ungetaka kubadilisha kitu gani?

18. Mapenzi mazuri ni yapi kulingana na mtizamo wako?

19. Mzazi gani yuko karibu na wewe?

20. Ni kitu gani kinachokuboa kwa mwanaume?

21. Unapenda kuvalia kikazi ama kimtaa?

22. Unawachukuliaje wanawake ambao wanapenda maringo?

23. Hivi ni kweli kuwa wewe unakuwa mrembo hivi?

24. Je wewe ni mtu wa kusoma ama wapenda kucheza games?

25. Ni mtu gani katika maisha yako ambaye unampenda zaidi?

26. Unapenda mambo ya ghafla ghalfa ama mpangilio?

27. Ni nani huwa unaongea naye kama unapata changamoto katika mapenzi?

28. Je una kumbukumbu yeyote ya utotoni mwako ambayo inakufanya utabasamu unapoifikiria?

29. Ukisafiri katika hii dunia, ungetamani usikose nchi ngapi tano?

30. Ni kitu gani kinakufurahisha maishani mwako?

31. Je, wewe uko karibu na familia yako?

32. Ni kitu gani unachochukia zaidi kuona wakati unapokutana na deti wako mara ya kwanza?

33. Je wewe ni mtu wa kurauka mapema ama kuchelewa usiku zaidi?

Haya yafuatayo ni baadhi ya maswali ambayo unaweza kumuuliza deti wako iwapo ameingiliana na mazungumzo yako. Maswali haya yanaweza kuwa ya ucheshi, mengine yanaweza kuchangia kuongeza mazungumzo na baadhi yanaweza kubashiri vile ambavyo deti yako itakuwa mbeleni na huyu mwanamke.

34. Ni sehemu gani ya mwili wako huwa inatekerenyeka zaidi ikiguswa?

35. Ulikuwa miaka mingapi mara ya kwanza ulipohisi kupenda mtu flani?

36. Ni kitu gani kinachofanyika kawaida unapokuwa na marafiki zako wa kike mkiwa mnapokula bata?

 37. Kimtizamo wako, maana ya mahusiano ni nini?

38. Hivi, mahusiano yako ya awali yalichukua muda gani?

39. Deti yetu ya leo umeiona vipi kabla tumeet tena wakati mwingine?

40. Sahizi unafikiria nini?

Jifunze Jinsi Ya Kumzuzua Mwanamke Mpaka Akupende

$
0
0

Kila mwanaume anapenda kutaka kujua jinsi ya kumzuzua mwanamke mpaka ampende. Lakini wengi hushindwa kutimiza azma hii kwa kuwa hawajui mambo muhimu ya kufanya ili aweze kumzuzua mwanamke.

Je, uko tayari kuzijua mbinu TANO kuu za kumfanya mwanamke azuzulike kwako?

Najua labda ushawahi kuwaona mwanamke fulani wakiweza kuzuzuliwa na mwanaume, na mwanamke kama huyu anacheka mara kwa mara huku akikiri kuwa mwanaume flani anajua kuzuzua. Well, waonaje kama ni wewe sasa hivi unapewa sifa kama hii?

Kupewa sifa ya kuwa mzuzuaji na mwanamke ni sifa kubwa zaidi kwa mwanaume kutoka kwa mwanamke. Na si kwa ajili ya sura, shepu wala ujanja wako. Yote itategemea na kipawa chako na tajriba yako wa kuzuzua.

So, utamzuzua vipi mwanamke?

Kumzuzua mwanamke kutategemea uwezo wako wa kuwasiliana na yeye na kumfanya ajihisi kuwa na furaha wakati wote. Tumia mbinu tano ambazo tumezihakikisha utendaji wake.

#1 Ongea na yeye mambo ambayo anataka
Unaweza kuona kuwa haina umuhimu wowote, sababu wanaume wengi hufanya hivi. Wanaume wengi hubaki wakijiuliza kuna haja gani  kwao kuongea mambo ambayo mwanamke anataka kuongea. Mbona wanawake hawawezi kuongea mambo ambayo mwanaume pia anataka?

Bila shaka, wanawake wanaweza. Wanawake pia wanakuwa active kutaka kujua aina ya mwanaume ambao wanajihusisha nao. Lakini wakati mwingine, haswa unapotaka kumfurahisha na kuteka atenshen yake kwako, ni vizuri kujua mambo ambayo yanagonga ndani ya kichwa cha mwanamke. Na kumakinika kuteka atenshen yake haimaanishi kuwa mwanaume anapaswa kuongea kuhusu mambo ya vipodozi na urembo na mwanamke, La. Daraja kati ya mwanaume na mwanamke imepungua siku hizi. Ni rahisi kuongea na mwanamke mambo ambayo anapenda bila hata kutatizika. Bora tu uhakikishe kuwa utaweka kando maswala ya mipira, elekroniki na hesabu katika mazungumzo yenu.

#2 Msuke
Wakati unapozungumza na mwanamke, ni rahisi kumfanya aweze kuongea na wewe. Lakini hio haitoshi. Kama unataka kumzuzua mwanamke basi unahitajika kumfanya ajihisi huru, na pia umuonyeshe kuwa uko interested na yeye.

Marafiki hawawezi kuzuzuana hadi wavuane chupi. So kama utaongea na yeye kama rafiki yako basi atakuona tu kama mwanaume anayevutia. Lakini hatakuona kama mwanaume anayezuzua. Kutaka kuonekana kama mwanaume mweye uwezo wa kuzuzua machoni mwa mwanamke, basi unahitajika kumfanya akuone wewe kama mwanaume ambaye anaweza kutoka naye deti. Na kufanya hivyo lazima umsuke.

Na unapochukua hatua ya kumsuka hakikisha kuwa hautumii maneno kama ‘unapendeza’, ‘leo umerembeka’, ama kutumia mstari wowote ambao unaendana na hii. Inaboesha na haionekani kuwa na uhalisia wowote. Badala yake tumia maneno ambayo yanamlenga yeye moja kwa moja. Umemuona amepaka wanja kwa macho? Mwambie “Leo nauona utofauti kwa sura yako, kwani umejipaka nini?” akijibu hajui, ama akikwambia ni wanja mtamkie, “Basi unapendeza kupindukia, hata nashindwa kuacha kukuangalia.” Haya ni baadhi ya maneno ambayo unaweza kumsifia yeye binafsi na moja kwa moja.

Kwa kumsuka utakuwa umefanya mambo matatu wakati mmoja. Kwanza ni kuwa umemchangamsha kwa kumfanya atabasamu. Pili umemfanya atambue kuwa wewe umemuona anapendeza. Na tatu ni kuwa umemuonyesha kuwa umevutiwa na yeye. Yote haya ni ya kufanya ili akutizame kama mwanaume ambaye anaweza kutoka deti na yeye.

#3 Kuwa mcheshi
Kufikia sasa kwa kuwa tayari ushamfanya kuwa na tabasamu kwa kumsuka, ni wakati wa kuingia katika himaya yake binafsi. Kila mtu huwa na himaya yake binafsi na kawaida hatujihisi huru iwapo mtu mwingine ataingia katika himaya zetu unless mtu huyu ni mtu ambaye tunajihisi comfortable naye. Ok, kwa kueleza juu juu ni kuwa mfano hauwezi kumuaproach mwanamke usiyemjua halafu uende ukakae na yeye sako kwa bako na uongee na yeye kana kwamba ni mtu unayemjua na kufahamiana naye tangu kitambo bila kufuata taratibu zake.

Kumfanya ajihisi huru na wewe, lazima uwe na muda  mrefu na yeye ili akuzoee. Akikuzoea hapo sasa unaweza kutumia ucheshi ambao unaweza kuutumia kwa manufaa yako. (machapisho ya awali tuliongea kuhusu jinsi ya kuwa mcheshi)

Hapa hakikisha kuwa wakati unapomchekesha mwanamke usitumia wala usijilazimishe kutumia hekaya ama stori za kuchekesha ulizozisikia mahali ama kusoma kitabuni. Kinachohitajika kwako ni kuwa mhalisia tu, mwanamke akipendezwa atacheka tu.

#4 Mtongoze
Wanaume huwatongoza wanawake kila wakati, lakini wakati mwingine wanawake wanahisi kuwa wanaume wanaowatongoza ni mafala. So usivuke mipaka yako wakati unapomtongoza sababu anaweza kukubeza. Mbinu rahisi ya kuanza kutongoza ni kwa kuanza kwa wepesi. Muulize wikendi atakuwa wapi baada ya shughli zake za wiki, muulize kuhusiana na sehemu anayopenda kubarizi na pia mkahawaha anaoupenda, na kitu chochote kile kinaweza kuhusiana na yeye moja kwa moja. Atajua kuwa unajaribu kumtongoza kwa sababu hakuna mtu anaweza kuuliza maswali haya bila lengo madhumuni.

Halafu mrushie hili swali.

“Enhe, hii inaweza kuwa personal, hivi wewe una boyfriend? Kama uko naye, basi moyo wangu naona unaweza kuyayuka wakati wowote kuanzia sasa!”

Hii inaweza kuoneka nzito lakini hufanya kazi wakati wote.

Atacheka, lakini mstari huu utakuwa umepitisha lengo lako kwako, na atajua kuwa uko interested na yeye. Lakini usifanye mambo yaende segemnege kwa kunyamaza kwa muda baada ya kukupa jibu lake. Endelea na stori nyingine ujifanye kana kwamba swali hilo halikuwa na umuhimu wowote kwako. Lengo lako umeliweka wazi lakini hutaki ajihisi kuwa hayuko huru mbele yako.

#5 Mguse
Hii ni sehemu hatari, lakini unahitaji muda kujifundisha. Unataka kujua jinsi ya kumzuza mwanamke, sawa? Basi kumgusa wakati ufaao inakupa point tano muhimu ambazo unahitaji kujua ili umzuzue mwanamke. Kama umepata kila kitu sawa, basi utakuwa umefanikiwa kwa kila kitu.

Lakini tena kumgusa mwanamke ni sawa na kucheza na moto. Ukiwa na haraka ya kuuguza hautahisi lile joto. Na ukikaa muda mrefu ukiugusa, utachomeka. Unaona venye hatari iliopo hapa?

Unaweza kutuma msisimko hadi kwa uti wake wa mgongo kwa kumgusa kiulaini kama tayari umemchangamsha awali. Lakini kumbuka hili, mguse wakati ambao unataka kumgusa pekee, kama vile kugusa sikio lake wakati unapomsifia kuhusu vipuli alivyofaa, kupapasa nywele zake wakati kuna upepo mkali, ama kuuwekeza mkono wako nyuma yake wakati mnavuka barabara. Mguso ni njia ya kuingia katika hulka ya mwanamke, so unahitajika kuwa makini zaidi na umsome vile ambavyo atareact kabla umguse kwa mara ya pili.

Upo?

Hizi Hapa Meseji Tatu Kali za Kimapenzi Maalum Kwa Mpenzi Wako Usiku wa Leo..!!!

$
0
0

Kuna miezi 12 katika mwaka…siku 30 katika mwezi…siku 7 katika wiki, masaa 24 katika siku…dakika 60 katika saa……lakini wewe ni mmoja tu maishani mwangu.
****
I asked God for a rose and He gave me a garden. I asked God for a drop of water and He gave me an ocean. I asked God for an angel and He gave me you!
****
Kuna vitu viwili zinavyoniamsha asubuhi na mapema: Alamu ya saa yangu na wewe

Fahamu Maajabu Sita ya Limao Ambayo Yatakushangaza..!!!

$
0
0

Limao ni moja ya tunda ambalo linafahamika sana, ni tunda ambalo mara nyingi hutumika zaidi jikoni kwa ajili ya kukata shombo fulani fulani ya baadhi ya mboga mfano samaki.

Kwa kawaida limao huwa na ladha ya uchachu, lakini pamoja na kuwa na ladha hiyo tunda hili limekuwa na faida pia za kiafya.

Yafuatayo ni miongoni mwa matatizo 6 ambayo huweza kudhibitiwa na limao:-

1. Husaidia kuimarisha mfumo wa umeng'enyaji wa chakula

2. Husaidia kupunguza sumu mwilini

3. Hutumika kama njia ya kupunguza uzito

4. Husaidia kupunguza hatari ya mawe kwenye figo

5. Husaidia kuimarisha afya ya ngozi

6. Hupunguza maumivu ya viungo vya mwili hasa joint

Tazama Katuni 5 Bora za Leo

MADARAKA Nyerere: Picha ya Mwl. Nyerere iondolewe Kwenye Wimbo wa Diamond

$
0
0
Baada ya malalamiko mengi toka kwa watanzania hasa watumiaji wa mtandao wa twitter kuwa Diamond ametumia isivyo picha ya mwalimu katika cover la wimbo wake mpya, mzee madaraka ameibuka na kusihi picha hiyo iondolewe katika wimbo huo.

Itakumbukwa kuwa Mwalimu hakuwa mtu wa kukaa kimya hasa maovu yanapozidi, alikuwa akikemea.

Viewing all 104709 articles
Browse latest View live


Latest Images