Quantcast
Channel: UDAKU SPECIAL
Viewing all 104667 articles
Browse latest View live

RC PAUL Makonda Aandika Ujumbe Huu Wenye Fumbo Ndani yake

$
0
0

RC wa Dar Ameandika ujumbe wa mafumbo kupitia ukurasa wake wa Instagram, Haijaeleweka na Nani analegwa hapo..Embu jisomee na wewe labda unaweza tegua mtego

By @paulmakonda
"Hakuna kitu kibaya kama kudanganywa na mtu huku ukijua anakudanganya na wakati huo huo anaekudanganya hajui kama unajua anakudanganya. Basi kazi yako inakuwa nikucheka kimoyomoyo"
.
TOA MAONI YAKO HAPA

Hatua 11 Za Kufuata Kumshawishi Mwanamke Mfanye Mapenzi

$
0
0

Najua umechoshwa kumuona yule mwanamke mrembo ambaye unapishana naye kila siku aidha ukiwa nyumbani, kazini, shuleni ama hata katika ule mkahawa maarufu ambao unapenda kutembea kila wikendi bila kuongea na yeye.

Ama labda ni yule mwanamke ambaye umefanya kumuona majuzi na ni mgeni kwako.

Well, haya si matatizo makubwa kwani kama unataka kumtongoza na kumuwini hadi ufanye mapenzi na mwanamke basi unapaswa kuelewa mambo kadhaa yanayofanya kazi, na ujue mbinu za kutumia ili zifanye kazi kwa manufaa yako.
Kama hutaweza kuwa yule mwanaume ambaye anaweza kumshawishi mwanamke kirahisi. basi inaweza kuwa vigumu  wakati wa kujaribu kuteka atenshen yake.

Lakini usiwe na wasiwasi coz hizi hatua ambazo tutakupatia sahizi zitakusaidia pakubwa kuweza kumuwin mwanamke kirahisi.
So inakuwaje?

Kabla tuanze nataka ufahamu kuwa kila mwanamke anakuwa na ladha yake tofauti tofauti ikija kwa kuchagua mwanaume, na ukitumia ujanja wako vyema wa kutotambulika basi unaweza hata kulala naye kwa muda mfupi zaidi bila wewe hata kufikiria.

Hatua 11 za kufanya ufanye mapenzi na yeye


#1 Kuwa karibu na yeye
Kama unamtaka mwanamke basi kitu cha kwanza ni kuwa lazima umjue vizuri. Usijitokeze na ubabe mwingi wa kujiona beberu kwa sababu atakuona kama tishio kwake ama hatakuwa huru kuongea na wewe ama mbaya zaidi ataboeka na wewe.

Fanya kuongea na yeye ili umjue vizuri. Mtumie meseji mara kwa mara na tumia lugha ambazo zitakuwa sahili kwake ili akukubali haraka. Lakini usiwe na pupa ya  kuanza kumtongoza, la. Onyesha tu ule upendo wa kirafiki mara ya kwanza.

#2 Pendezeka
Hii hatua ndio itakayoamua iwapo kama umempendeza ama wampotezea wakati wake. Wakati unapoongea na yeye mara kwa mara jaribu kuangalia ishara zozote kutoka kwake iwapo yuko interested na wewe au la.

Hii hatua unapaswa kumtext na kumtumia jumbe ambazo zitalingana na mambo anayoyapenda. Mfano kama anapenda kuhusu mada za sinema basi pia wewe fanya tafiti kuhusu filamu ambazo anazipenda ili uweze kumpendeza.

Hii hatua pia unapaswa uchunge usiwe mtu wa kuboa kwani ataanza kukutenga polepole mpaka mwisho ujione mjinga. Ukimwona ameanza kujibu meseji zako kuchelewa ama kutokujibu siku nzima basi fahamu ameanza kukutenga. Hivyo basi hakikisha kuwa unakuwa mjanja katika hii hatua. 

#3 Kuwa active usiku wa kiza
Wakati mzuri na ule wa msisimko ni kutumia jumbe usiku wa kiza na kupigiana masimu. Usiku wa kiza ni muhimu kwa kuwa mwanamke ni rahisi kuitikia kile ambacho unataka wewe.

Hakikisha wakati unapoanza kumtumia jumbe anza na nyakati za jioni siku ya kwanza, saa mbili siku ya pili mpaka azoee kuchat na wewe mida hizo za saa nne hadi usiku wa kiza.

Pia hapa uchunge meseji zako zisikuje kwa uzito. Anza kwa kumchokoza polepole hadi ufikie pale ambapo unaweza kumtumia meseji za mapenzi hadi zile za kumpandisha nyege.

#4 Ishi maisha mawili
Hapa ni pale ambapo unahitajika kumchanganya. Kila wakati wa usiku unapomtumia jumbe na kumpigia simu hakikisha kuwa unamsuka, unamtongoza na unamrushia meseji za kimahaba. Lakini ikiwa wakati wa mchana umekutana na yeye usijaribu kuongea kama vile ambavyo unaongea naye usiku unless yeye mwenyewe aanzishe stori kama hizo – ishara ya kuwa amependezwa na wewe.

Halafu muhimu zaidi ni kuwa wakati mnapokuwa na marafiki wengine msiongee kuhusu chat zenu kabisa, yaani ni nyinyi wawili pekee ndio mnaopaswa kuongea mambo kama hayo. Hii itaingia kwa akili yake kuwa mambo mnayoyafanya usiku ni kati ya nyinyi wawili hivyo basi lazima kuna kitu ambacho kinaendelea kati yenu.

#5 Usimuonyeshe kuwa unampenda
Hapa ndipo wanaume wale wa ‘kawaida’ ndio wanapofanya makosa. Wanamwambia mwanamke kuwa wanampenda na kuwa wanahisia na wao. Yeah, ofcourse unampenda. Tayari anajua hilo, si ni kweli? Unamtext kila wakati, unampigia simu kila mara, na lazima atakuwa anahisi hio kemia.

Lakini ijapokuwa ana fununu ya kuwa unampenda, anahitaji uhakikisho wake kupitia kwa kukusikia wewe umwambie hivyo. Cheza kijanja, usimwambie na mapema. Utakuwa unamsisimua na ataathirika na wewe kihisia. Lakini kumwambia mapema hisia zako zitaua ile haja ya yeye kutakaa kujua zaidi kutoka kwako. Wanipata? [Soma: Jinsi ya kuathiri hisia za mwanamke]

#6 Ingia katika himaya yake ya binafsi
Wakati mko nyinyi wawili pekeenu, kaa karibu na yeye na ujifanye kama hukuona kama umekaa na yeye karibu sana. Umekuwa ukimtongoza mara kwa mara so ni wakati wako sasa wa kuingia katika himaya yake binafsi.

Iguse mikono yake ama vidole vyake wakati ambapo unaongea kitu flani, weka mikono yako kwa kiuno chake wakati unapishana na yeye ama unaenda ule upande mwingine, mguse huku ukimsifia, ama unaweza kumkumbatia sekunde zaidi wakati mnaagana

#7 Jenga tenshen ya kemia
Kufikia sasa, atakuwa anahisi hisia kila wakati ambapo unamgusa kimaksudi au kibahati mbaya. Hii ndio hatua ambayo unapaswa umfanye atamani miguso yako. Kumbuka hapa kuwa lengo letu ni kufanya mapenzi na yeye lakini tunaenda kimpango. Wakati unapokuwa unamgusa, hakikisha kuwa mkono wako unatomasa mgongo wake ama mikono yake. Msogelee karibu zaidi na umwambie maneno kupitia kwa masikio yake. Ongea kwa sauti nzito na iliyo ya kuvutwa wakati unapokuwa naye. Jenga kemia vile inavyohitajika na utamfanya atamani mikono yako ibaki kwake daima

#8 Cheza michezo
Kama umekuwa ukimsuka na umekuwa ukimjaza kila wakati unapokuwa umekaa na yeye, basi utakuwa umemtongoza na ameingiliana na unaweza hata kuenda kulala na yeye.

Lakini kama unataka kuchukua mambo hatua kwa hatua basi unaweza kurudi kule kwa text na uwe unamtumia jumbe za kumsuka na kumchanganya akili mara kwa mara. Hapa utakuwa unamtongoza huku ukienjoy. Tumeelewana hapa?

#9 Mazungumzo machafu
Umekuwa ukimtext, ukimsuka, na kumtongoza kila usiku. Na kama amekuwa akiingiliana na text hizo zako, hapa basi ndipo unaweza kuwa na ile ruhusa ya kuongea uchafu na yeye na kuchukua hatua ya juu zaidi. Tumia simu yako kuanza kwa kumtumia meseji zilizo rahisi ambazo zinaonekana safi hadi ufikie kule kwa kumtumia meseji chafu. Na bila hata kujijua mtajikuta nyote wawili mkisex chat pamoja.

#10 Mwagize mtoke out
Pindi ambapo mtakuwa mshafanya sex chat na mwanamke kupitia kwa simu itakuwa tayari ushafunga mchezo. Sasa kile kilichobakia ni kufanya mapenzi ana kwa ana. Mwambie mtoke out ama mwambie kuwa unataka kukutana na yeye siku moja. Tengeneza plan ya kukutana nyumbani kwake ama aje mkutane kwako. Hakikisha kuwa sehemu ni hizo mbili pekee na wala si kukutana sehemu za umma unless kama bado unajaribu kumtongoza mara nyingine. Na hapa ndipo utaamua kama mahusiano yenu yatakuwa ya mlalano ama yatakuwa ya romance.

#11 Fanya mapenzi na yeye
Na mwisho utakapokutana na yeye – tayari anajua ajenda ya kukutana na wewe – usimrukie papo kwa papo eti kwa kuwa tayari umefanya sex chat na yeye kwa simu.
Unaweza kuharibu mpango mzima ambao umekuwa ukiujenga kwa muda.

ASKOFU Gwajima Amshauri Rais Magufuli Pa kumpeleka Makonda

$
0
0


Gwajima Kuhusu Makonda leo kwenye Ibada ya Ijumapili ya April 9, 2017: "kwanza huwa najiuliza Rais Magufuli akimtoa Leo Makonda, atampeleka wap? Ila ninaushauri mmoja, ampeleke kwenye Balozi zetu nje ya nchi, akimtoa na kumuacha hapa hapa watu watamgawana,


...Akiendelea kumuacha ipo siku atafanya vitu vya kuaibisha na vya ajabu, kwanza  Mimi ningekuwa Makonda ningekuwa nimeshaondoka siku nyingi,


Na hayo Mambo ya Ajabu yatakuja kutokea bado niko hai"

Hata hivyo Gwajima amesisitiza kuwa ataendelea kuzugumzia sakata la vyeti kuhusu Makonda nauacha haya Mengine mengine

Lema, Lissu, Zitto Kumsaka Ben Saanane

$
0
0

MBUNGE wa Jimbo la Arusha Mjini, Godbless Lema, ametangaza kuanza kwa kampeni ya kumsaka Ben Saanane, ambaye ni msaidizi wa Mwenyekiti wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema) Freeman Mbowe, aliyepotea tangu Novemba mwaka jana.

Mbali na Lema, wanasiasa wengine waliotajwa kuanza kampeni hiyo ya kumsaka Saanane akiwa hai au amekufa, ni Mbunge wa Singida Mashariki na Mwanasheria Mkuu wa Chadema, Tundu Lissu na Mbunge wa Kigoma Mjini, Zitto Kabwe (ACT- Wazalendo).

Lema alizungumza hayo mjini hapa jana, ikiwa ni siku moja tangu kupatikana kwa msanii Ibrahimu Mussa, maarufu Roma Mkatoliki, aliyetekwa katika mazingira ya kutatanisha Aprili 5, mwaka huu kabla ya kupatikana juzi huku akimtaja kiongozi mmoja wa Mkoa wa Dar es Salaam kuhusika na vitendo hivyo vya utekaji.

Akifafanua madai hayo, Lema alisema katika mazingira ya kawaida haiwezekani kiongozi huyo autangazie umma kwamba Roma angepatikana kabla ya Jumapili na kweli ikawa hivyo.

Alisema kuwa kutokana na kauli hiyo, ni dhahiri kiongozi huyo alikuwa anajua alipo Roma, huku akifananisha tukio hilo na la Ben.

Alisema timu hiyo ya wabunge inaungana kumtaka kiongozi huyo aeleze alipo Ben kwa sababu watu wanaandamana katika mioyo yao huku wakiwa na uchungu na hasira.

“Unakwenda mwezi wa sita Ben Saanane amepotea, siyo chama wala wazazi, ndugu zake wanaojua alipo, suala la kupotea kwake ni suala la kila binadamu mwenye akili timamu, tulitilie mkazo wote na mimi naamini watawala wanajua mahali alipo Ben,” alisema na kuongeza.

“Kama ambavyo kiongozi wa Dar es Salaam alikuwa anajua mahali alipo Roma na wenzake, Kamanda Sirro hawezi kusema alipo Saanane, ila huyo ndiye anaweza kama alivyosema Roma atapatikana lini, tunamtaka Saanane kama amekufa tupeni mifupa yake tukaizike kwa heshima, kama yu hai mleteni akaungane na ndugu zake na akawe huru katika taifa lililopata uhuru tangu 1961.

“Nitahamasisha vijana nchi nzima kuanzia kwenye mitandao tudai haki ya Saanane kwa nguvu zote na viongozi wa dini watusaidie suala hili kwani wakati Kamanda Sirro anasema Roma hashikiliwi katika kituo chochote cha polisi, kiongozi mmoja alisema Roma na wenzake watapatikana kabla ya Jumapili,”

Lema alisema kuwa Jeshi la Polisi ndio wanahusika na masuala ya upelelezi na siyo ofisi ya Mkuu wa Mkoa na kudai kushangazwa na hatua ya mkuu huyo kujihusisha katika suala hilo.

“Ni nani amempa mamlaka kuwa msemaji wa masuala ya polisi kwenye masuala yanayohusu raia na mali zao? Kwanini Ben alipopotea hakuna tamko lolote limeshawahi kutolewa na kiongozi huyo au mwingine yeyote?

“Ukisoma kwenye mitandao mbalimbali ya kijamii, mkuu huyo anahusishwa na kupotea kwa Ben, hajawahi kuita vyombo vya habari kukanusha au kusema atamtafuta, kwa sasa taifa linavyoonekana Waziri wa Mambo ya Ndani hapa nchini ni kiongozi huyo,” alisema.

Lema alidai kwa sasa Waziri wa Mambo ya Ndani nchini  ni yeye kwa kuwa waziri mwenye dhamana hiyo, Mwigulu Nchemba ameshindwa kutekeleza majukumu yake au anaogopa kuyatekeleza kwa kuhofia kutenguliwa kwenye nafasi hiyo kama ilivyotokea kwa aliyekuwa Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo, Nape Nnauye.

 “Inaonekana kama Mwigulu kazi hii ameishindwa au anaogopa akiyaingilia yatampata yaliyompata Nape, siyo Mwigulu peke yake, mawaziri wengi wamekosa ujasiri wa kusema mambo kadhaa yanayohusu nchi, kwani hata juzi niliongea na Mwigulu akasema hana taarifa wakati yeye anahusika na usalama wa raia,” alisema Lema.

Alitolea mfano nchi ya Tunisia kuwa machafuko yalisababishwa na mmachinga mmoja kujilipua moto na kuwa suala la Ben likiendelea linaweza kukuza hasira na watawala wakifikiri bunduki, vifaru na polisi wanaweza kuzuia hasira za wananchi na kuwa taifa lenye watu

wasio na uhakika wa kuishi, siyo kweli.

 “Mimi mwenyewe sina uhakika wa kuishi, ninatembea sijui  kama nitatekwa au sitatekwa kwa sababu mpiga kelele yeyote wa masilahi ya taifa hili anaonekana ni kikwazo yuko katika mkakati wa kutekwa,” alisema Lema.

Noma Sana..Baada ya Gwajima Kudai Diamond ni Freemason na Ataweka Ushahidi..Diamond Aibuka na Kumjibu Haya Makubwa..!!!

Sintofahamu Kuhusu Mkutano wa Roma na Waandishi

$
0
0

Dar es Salaam. Hali ya sintofahamu imeanza kujitokeza tokea leo asubuhi hadi saa 5: 48 baada ya mkutano aliotakiwa kuufanya Roma Mkatoliki na waandishi wa habari kushindwa kufanyika kwa wakati.

Mapema leo kaka yake Roma, Omary Musa amesema mkutano huo ungefanyika saa tano.

Hata hivyo Musa hakuweka wazi eneo la kufanyia mkutano huo kwa kile alichodai bado hawajapata eneo.

"Eneo tulilopata awali mwenyewe anaonekana kuwa na hofu, tunatafuta eneo lingine tutawajulisha kabla ya saa tano ila tunalenga maeneo ya Kinondoni, "amesema

Ilipofika saa tano mwandishi alimtafuta kujua eneo Musa akajibu bado hawajapata na huenda mkutano huo ungesogezwa hadi saa nane.

"Bado tunatafuta kuna watu wamepewa jukumu hilo, hatuwezi kufanyia popote lazima liwe eneo salama, hatujui waliomteka walikuwa na nia gani"


"Nipigie baada ya dakika 45 nitakuwa nimeshajua, muhimu kuweni na subira tutawataarifu," amesema

Jumamosi iliyopita baada ya kupatikana akiwa kituo cha polisi Osterbay Roma aliahidi kuzungumza na waandishi leo kuelezea kilichotokea

Tambwe Asema Simba Ndo Basi Tena, Wasahauuu

$
0
0

Mshambuliaji wa Yanga, Amissi Tambwe, raia wa Burundi, amesema baada ya kikosi hicho kukaa kwenye usukani wa ligi kwa sasa lengo lao lililobakia ni kuhakikisha wanashinda kwenye mechi zao zote ili waweze kuwa mabingwa.

Yanga wamejikusanyia pointi 56 baada ya kushuka dimbani mara 25, pointi ambazo zinawafanya wawe juu ya timu zote zinazoshiriki Ligi Kuu Tanzania Bara huku Simba wenyewe wakikamata nafasi ya pili wakiwa na pointi 55.

Mshambuliaji huyo aliyefunga mabao tisa mpaka sasa kwenye ligi, amesema kwamba kwa muda mrefu Simba walijiaminisha kwamba wanachukua ubingwa wakasahau kuhusu wao ambao walikuwa wanazisuka mbinu zao kimyakimya.

“Kilichobakia kwa sasa ni kuhakikisha kwamba tunashinda kwenye mechi zetu tano zilizobakia kwa ajili ya kujiweka kwenye nafasi nzuri zaidi ya kutetea ubingwa wetu ambao tulikuwa tunaupigania kwa nguvu kubwa.

“Niwaambie nafasi hii tuliyonayo kwa sasa ndiyo tumemaliza kila kitu kwani hatutaki kuona tukirejea kwenye nafasi tuliyokuwa awali na nawaomba wenzangu tushirikiane vyema katika kushinda mechi hizi zilizobakia,” alisema Tambwe.

Ukweli Mchungu...Serikali Ikanushe Uongo Huu wa SABC Kumsema Vibaya Rais Wetu Magufuli Kuwa ni Dikteta...!!!!

$
0
0

Uzalendo ni kutokubali na kutonyamaza kimya wakati rais wako anaposemwa vibaya kwa hoja za uongo na media za nchi nyingine, bali ni kwa media zetu kujitokeza, kuukanusha uongo kwa kuusema ukweli na ikibidi serikali yetu sio tuu ikanushe bali pua ihitaji kuombwa radhi!.

Pamoja na matatizo yote na mapungufu yote ya rais wetu Magufuli, kwa sababu na yeye ni binadamu na sio malaika, Watanzania wote wazalendo wa kweli wa nchi yetu, tusikubali rais wetu 
kudhalilishwa kwa kusemwa vibaya, na kusingiziwa uongo na media za nje bila ya media za ndani kukanusha na kumtetea, au kuunyamazia udhalilishaji kama huu ni sawa na kushangilia rais wetu kudhalilishwa.

Wito.

Any bad publicity kumhusu rais wetu ni bad publicity kuhusu nchi yetu, natoa wito kwa wazalendo wote kutanguliza mbele maslahi ya taifa kwa kutokubali au kushabikia bad publicity kuhusu nchi yetu. Think of multiplier effects za bad publicity!. Its not good kwa investment climate, tunapoelekea kwenye Tanzania ya viwanda, its not good for tourism yetu. It's not good for Tanzania in general kwenye international arena, not good at all.

Hivyo natoa wito maalum kwa Waziri wa Habari, Kurugenzi ya Mawasiliano Ikulu au Idara ya Habari Maelezo kuukanusha uongo huu unaoenezwa kumhusu rais wetu, kwa sababu uongo ukisemwa sana na kuachwa bila kukanushwa mwishowe sio utaonekana kama ni ukweli, bali utageuka ukweli.

Jumatatu Njema.

Paskali.

Bashe: Kuna Kikundi Ndani ya TISS Kinahusika na Utekaji. Wabunge 11 Wapo Kwenye Orodha ya Kutekwa.!!!

$
0
0

Mbunge wa Nzega Mjini Hussein Bashe, ameomba mwongozo kuahirishwa kwa Bunge ili kutoa nafasi ya Wabunge wote kujadili matukio ya utekaji watu yanayoendelea.

Akiomba Mwongozo kwa Naibu Spika, Hussein Bashe amedai kuwa amefahamishwa na baadhi ya Mawaziri kuwa ndani ya Idara ya Usalama wa Taifa kuna kikundi ambacho kinahusika na utekaji wa watu. Amedai kuwa kuna Wabunge 11 wapo kwenye orodha ya kutekwa na kuondolewa uhai. Mimi ni kati ya watu 11 tuliopo hatarini kufanyiwa vitu vibaya popote pale nijiangalie

"Kuna watu wamenitumia ujumbe kwamba mimi ni kati ya watu 11 tuliopo hatarini kufanyiwa vitu vibaya popote pale nijiangalie. Hatuwezi kulifumbia macho jambo hili, Watanzania wanatekwa na watu wasiojulikana".

Kwa hapa tulipofika, ni wazi kuwa JPM ajitafakari na baadhi ya watu wanaomzunguka.Kuna hali ya tahayari katika Taifa.

Jana nimeongea na Askofu mmoja wa Kikatoliki, nimeona dalili ya uhusiano wa JPM na Kanisa kudorora kwa namna anavyoendesha mambo ya Nchi.

Hatuwezi kulifumbia macho jambo hili, Watanzania wanatekwa na watu wasiojulikana'

Sumaye Azidi Kuichambua Serikali ya Magufuli Kulinganisha na Zilizopita

$
0
0

WAZIRI Mkuu wa Serikali ya Awamu ya Tatu, Frederick Sumaye, amechambua tofauti ya mazingira ya utawala wa awamu ya tatu, ambao ulikuwa na changamoto ya kukosekana kwa fedha na kinachotokea sasa maarufu kusoma namba.

Akizungumza katika mahojiano maalumu na gazeti hili jana, Sumaye alisema kuna tofauti nyingi lakini akaamua kuzungumzia kubwa zaidi kwa kujikita katika mambo mawili; moja ni uchumi na lingine demokrasia na utawala bora.

Sumaye ambaye ndiye Waziri Mkuu mwenye historia ya kukaa miaka kumi mfululizo katika nafasi hiyo, alisema katika Awamu ya Tatu Serikali iliimarishwa uchumi na kukuza na kuboresha nguzo kuu za uchumi, kwa kujenga mazingira rafiki kwa wafanyabiashara na kuingiza ushindani wa kweli katika biashara.

Kwa mujibu wa Sumaye ambaye sasa ni kada wa Chadema, Awamu ya Tatu chini ya uongozi wa Rais Benjamin Mkapa,  ndiyo iliyojenga na kubuni vivutio kwa wawekezaji wa ndani na wa nje na kuanzisha ushirikiano wa sekta ya umma na binafsi (PPP) katika uwekezaji.

Sumaye aliendelea kueleza kuwa Awamu ya Tatu, ambayo hali yake ya kukosena kwa fedha ilipewa jina la ‘Ukapa’ ndiyo iliyobuni na kuboresha miundombinu ya uchumi kwa kuunda Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA) na Kituo cha Uwekezaji (TIC) pamoja na kuboresha sheria zilizoendana na uchumi huria na wa kisasa.

Alisema hata maboresho ya miundombinu ya barabara, bandari na maji yalianzia Awamu ya Tatu na katika huduma za jamii hasa elimu, awamu hiyo ndiyo iliyobuni Mpango wa Maendeleo ya Elimu ya Msingi (MMEM), uliopeleka watoto wote wenye umri wa kuanza shule darasani na Mpango wa Maendeleo ya Elimu Sekondari (MMES).

“Awamu hii mengi ya mambo haya ni kinyume kabisa au hayatiliwi mkazo. Kwa mfano Serikali imekwishatamka kuwa kuanzia mwaka huu wa fedha idara za Serikali hazitapewa huduma na sekta binafsi. Hii ni kinyume kabisa na sera ya PPP,” alisema.

Alisema hata sera ya utozaji kodi, inapaswa kujenga uhusiano mwema baina ya mlipakodi na mtozakodi, lakini cha kushangaza hazishabihiani na badala yake wafanyabiashara wengi wamefunga biashara zao. 

Upatikanaji wa fedha

Akizungumzia hali ya upatikanaji fedha iliyopewa jina la ‘Ukapa’, Sumaye alisema Awamu ya Tatu ilipoanza, hali ya uchumi ilikuwa duni na fedha zilikuwa mikononi mwa wenye uchumi usio rasmi au uchumi wa magendo.

Alisema kazi ya kwanza ya Awamu Tatu, ilikuwa kurudisha uchumi katika misingi sahihi na katika kufanya hivyo walikubaliana kuua biashara ya magendo.

Alieleza kuwa kipindi hicho ndiyo watu wengi walipoona ugumu wa fedha kupatikana wakauita 'Ukapa', lakini kipindi hicho hakikudumu muda mrefu, kwani uchumi ulirudi katika misingi bora na kuimarika na watu wakaanza kupata fedha kulingana na jasho lao halali.

Demokrasia

Sumaye alisema Awamu ya Tatu pia ilikuza demokrasia na utawala bora na idadi ya vyama iliendelea kukua na vyama vya siasa vilifanya kazi za kisiasa kwa uhuru bila kuzuiwa au kungiliwa.

Alifafanua kuwa utawala bora wakati wa Awamu ya Tatu, ulikuwa wa 'ukweli na uwazi na uliofuata sheria’ na kutolea mfano wa nguzo tatu za dola ambazo ni Utawala, Bunge na Mahakama kwamba zilifanya kazi kwa uhuru bila nguzo moja kuingilia nyingine.

Waziri Mkuu huyo alisema watu walikuwa huru kutoa maoni yao bila wasiwasi wala kamata kamata au watu kupotea bila maelezo yoyote kutoka vyombo vya dola. 

“Awamu hii ni kinyume kabisa na hivyo. Demokrasia imekandamizwa kiasi kwamba vyama siasa havina uhuru wa kufanya mikutano ya hadhara kama sheria inavyotaka na uhuru wa vyombo vya habari umeminywa kabisa. Mikutano ya Bunge haioneshwi tena mbashara katika luninga kama zamani,” alisema.

Aliongeza kuwa hayo yote yanavunja Katiba ya nchi ibara ya 18 kwa sababu ni haki ya kikatiba wananchi kuwa na uhuru wa kutoa, kupata au kusambaza habari.

Alisema kwa sasa ni jambo la kawaida wapinzani kukumatwa bila sababu za msingi na kukaa rumande muda mrefu kuliko saa 48 zinazoruhusiwa kisheria na hata wengine kufungwa jela.

Kwa mujibu wa Sumaye, hata kupotea kwa watu wenye mawazo tofauti na Serikali au 'kuvamiwa na watu wasiojulikana' kumeanza kuwa jambo la kawaida.

Credit - Jambo leo

Tarime This is Too Much: Kijana Akatwa Mkono kwa Deni la Laki 3..!!!

$
0
0

Mkazi wa Kijiji cha Keisangora, Wilaya ya Tarime Mkoani Mara, Mwita Magige, amekatwa mkono wa kushoto kwa kile kinachodaiwa kushindwa kulipa deni la sh 300,000 baada ya ng’ombe wake wane kukamatwa na mdeni wake.

Tukio hilo lilitokea kijijini hapo baada ya ng’ombe wake waliokuwa wakichungwa na mkewe kukamatwa na mdeni wake ili kumshinikiza amlipe.

Magige alisema, Aprili 5 akiwa safarini alipigiwa simu kuwa mifugo yake imekamatwa na uongozi wa Kijiji na alitakiwa kwenda kuikomboa, baada ya hapo alisitisha safari na kurejea nyumbani, alikwenda kwa Mwenyekiti wa Kijiji, Nuru Magacha alimweleza kuwa mifugo yake ipo na anadaiwa sh 300,000.

Magige alisema muda mfupi baadaye yowe lilipigwa kuashiria hatari na kwamba, akiwa hajui kinachoendelea wananchi walikusanyika na kijana mmoja alimkata mkono wa kushoto kwa panga na kuucha ukining’inia.

Waziri Mwakyembe Aibuka Kwenye Mkutano wa Roma na Waandishi wa Habari

$
0
0

Leo Roma mkatoliki amekutana na waandishi wa habari kuzungumzia tukio lake la kutekwa, Katika mkutano huo Waziri Mwakyembe alikuwa pembeni ya Roma pia alipata nafasi ya kuongea na kuulizwa maswali na waandishi wa habari..



Simulizi..Jinsi Roma Alivyotekwa From A- z..!!!

$
0
0

Kaka wa Roma Mkatoliki, msanii wa muziki wa kizazi kipya aliyetekwa akiwa na wenzake na kurejeshwa juzi, amesema watekaji waliwafunga vitambaa vyeusi usoni, lakini hadi sasa hawawajui wahusika na waliwarejesha na kuwaacha Kituo Kikuu cha Polisi Dar es Salaam.

Pia, kaka huyo, Omari Musa amesema Roma, ambaye alipata umaarufu kwa nyimbo zake za kukosoa ukandamizaji wa vyama vya upinzani hasa katika wimbo wa “Viva Roma”, hakuwa anarekodi wimbo mpya kama inavyodhaniwa.

Licha ya polisi kukana kuwa watu hao hawakuwa wanashikiliwa katika kituo chochote cha polisi, Roma na wenzake walionekana Kituo cha Polisi Oyesterbay, Kinondoni ambako walihojiwa kwa zaidi ya saa sita baadaye kupelekwa Hospitali ya Mwananyamala.

Baada ya kutoka, Roma alizungumza kwa kifupi akiwashukuru Watanzania na kusema atazungumza na wanahabari leo. Lakini, Musa alisema Roma hayupo tayari kuzungumza mambo mengi yaliyompata au alichofanyiwa na watekaji hao.

Live Update..Roma Afunguka A - Z jinsi Tukio Lilivyokuwa,Walipopelekwa na Jinsi Walivyoteswa ba Kutupwa Mtaroni..!!!

$
0
0

Anaeongea kwa sasa ni msanii Roma na anatoa shukrani kwa wote bila kujali itikadi zao, anasema kilichowapata watu wafanye kama case study.

Roma anasema hawana uhakika wa usalama wao hata kidogo, amesema nature ya tukio, studio zilizopo Tongwe records yuko tangu 2007 na ni eneo salama sana. Amesema wana majirani wanaowapa amani sana ikiwemo ujirani na Tibaigana, Waitara na mstaafu mmoja wa Magereza.

Amesema hofu hiyo isiishie kwao kwani inaweza ikarudi kwa yeyote muda wowote, mtu yeyote inaweza kumkuta. Amedai wao ni wachanga mno na hawawezi kupambana na yeyote. Anasema Bin Laden hayuko sawa na anastuka sana mpaka kuwastua watu wote.

Amedai kuna watu wanaamini hakuna kilichotokea kwa kudhani ni kiki na wengine wanasema wanatumika kisiasa labda kuchafua serikali.

ROMA: Tunatafuta ruzuku yetu kupitia mziki, tumelia sana kwa haya maneno tena mengine kutoka kwa watu wa karibu sana ikiwemo wanamuziki, si kweli. Tunaishi familia za kawaida na hatuwezi kurisk maisha yetu kwa ajili ya hela au sababu nyingine yeyote.

Kilichotokea ni kweli, nadhani mnaona mwili wangu(anaonyesha), linatuumiza sana mtu kusema tumepewa dola 5,000. Tumeumia, tumepigwa kiukweli na tumeripoti kwenye vyombo vya dola.

Sheria zetu zinasema jambo likianza uchunguzi ni njema kulielezea kwani wanasema linaharibu upelelezi.

Nilifika Tongwe na kuwakuta wenzangu, haikupita nusu saa wakaja watu na silaha za moto na amri ilikuwa kuingia ndani ya gari, tukiwa tumefungwa usoni na pingu, ilikuwa Jumatano jioni na tumekuja kupata usalama tumekuja kuupata Ijumaa jioni na kulikuwa na mahojiano yanaendelea yakiambatana na vipigo. Maojiano hayo ndo hayo temsharipoti.

Tulifungwa tena na kuachwa eneo ambalo hatulijui tukatupwa kwenye dimbwi la maji, tukajikuta tuko salama na baada ya kutembea sana tukakuta kibao kimeandikwa Mahaba beach na kugundua tulikuwa Ununio.

Swali: Mlingundua mlitupwa beach, mlienda beach Oysterbay police

JIBU: Ilikuwa ni usiku, baada ya muda tulipogundua Ununio, nilikuwa na madoa ya damu. Mpaka mtu ujue mimi ni Roma ilikuwa ngumu, tulifika hadi Kunduchi na kukuta boda sita na kumuomba Moni aite boda, tukaenda hadi nyumbani Mbezi, kuingia ndani hamna mtu, nikawaambia wenzangu tubadili nguo, ilikuwa inaelekea Alfajiri, mtu wa bajaji tukamuomba simu kumpigia bosi wetu.

Tulipofika alikuwa tayari amempigia Ruge Mutahaba, walikuwepo na waliumia sana, wao ndio wakatupa way forward na kusema walifungua hii kesi kituo cha polisi hivyo tukaenda kituo cha polisi Oysterbay.

SWALI: Waliwaachia masharti yoyote

JIBU: Ipo ndani ya upelelezi.

SWALI:Chanzo kilikuwa mziki wako?

JIBU: Siwezi kujua, upelelezi unaweza kuleta majibu.

Dada anaeonekana muongozaji anasema hamna swali jingine na anamkaribisha waziri Mwakyembe.

Mwakyembe: Pale ambapo kuna tatizo na msanii yeyote nitaarifiwe kwanza mimi waziri mwenye dhamana, wasanii wote ukihojiwa na mtu usiemjua wa ajabu nitafute, niliposikia taarifa hii nikajiuliza chombo cha dola kimekiuka tena taarifa yangu? Hili ni swala scientific tuache kupiga ramli, wenzetu wamesema tuwaache wafanye upelelezi, hii sio hali ya kawaida

Inaweza kuwepo wasanii(sio wanamuziki) wachache wanataka kutuvuruga, nawashukuru sana.

SWALI: Bashe amesema vyombo vya usalama vimehusika

JIBU: Umeleta maswala ya kina Bashe, mimi hapa Mwakyembe, mambo hayo yako bungeni.

Swali: Kuna mtu alisema Roma ataonekana kabla ya Jumapili na kweli akaonekana

Moderator: Sasa tuishie hapohapo.

Mwakyembe: Mkiendelea kupiga kelele kama watoto wa shule naondoka hapa, wewe unaamini ni vyombo vya dola? Siwezi kuamini mpaka nione ya recording ya huyo kiongozi.

Nape Nnauye - Najua Wanaoniita shujaa Leo Ipo Siku Watanigeuka..!!!

$
0
0

Mbunge wa Mtama, Nape Nnauye amedai wanaomuita shujaa leo ipo siku wanaweza kumgeuka kwa sababu kama binadamu bado ana safari ndefu na anaweza kujikwaa ndiyo maana hataki kulivaa jina hilo bali anahitaji watanzania waendelee kumuombea.

Akizugumza akiwa Mtama Mh. Nnauye amesema hawezi livaa jina hilo  bali amelipokea kwakuwa wananchi wameamua kumpatia jina hilo kwani hata sababu za kuitwa jina hilo zipo tofauti tofauti.

"Sikatai kuitwa Shujaa kwa sababu wao wenyewe ndiyo wameniita, lakini siyo jambo ambalo nitalivaa.  Hao hao wanaoniita shujaa siku nyingine wanaweza kunigeuka kwa sababu binadamu ukiwa hai unaweza kujikwaa safari bado ni ndefu nachotaka kuwaomba tu wananchi waendelee kuniombea. Hata hivyo sababu za kuitwa shujaa kila mtu ana sababu yake, mwingine atakuambia kwa sababu hujatetereka wengine wanasema umesimamia ukweli, kwa hiyo jina hilo siwezi kulivaa ila siwezi kulikataa". Alisema Nape

Mh. Nnauye jana alipata nafasi ya kuzungumza na wananchi wa Mtama kwa mara ya kwanza baada ya kuvuliwa uwaziri wa Habari, Sanaa, Utamaduni na Michezo Machi 22 mwaka huu

Bashe, Sugu Wataka Bunge Lijalidi Utekwaji wa Watu Nchini..!!!

$
0
0

Wabunge wawili wa CCM na Chadema wametaka Bunge liahirishne shughuli zake mara moja na kutoa nafasi kwa wabunge kujadili suala la utekwaji wa raia nchini.

Wabunge hao ni Hussein Bashe(Nzega Mjini) na Joseph Mbilinyi(Mbeya Mjini)wameomba mwongozo wa Spika kuhusu suala hilo leo asubuhi.

Bashe amesema ni muhimu suala hilo likajadiliwa kwani iko orodha ya wabunge 11 akiwemo yeye mwenyewe wameambiwa wakae chonjo.

Bashe alisimama kwa kutumia kanuni ya 47 vifungu (i,ii,iii) akamtaka Naibu Spika kusimamisha shughuli za bunge kwani jambo lililombele yao ni kubwa na likiachwa linaweza kuwa na madhara makubwa na kuichafua taswira nzima ya serikali.

Hoja ya mbunge huyo iliungwa mkono na Mbilinyi ambaye amesema kuwa Taifa limekuwa gizani kutokana na utamaduni wa utekaji ambao tangu mwanzo haukuwepo na akamtaka Waziri wa Mambo ya Ndani, Mwigulu Nchemba kujihuzulu mara moja nafasi yake ili kulinda heshima.


Zitto ‘Anunua Kesi’..!!!

$
0
0

Kukithiri kwa uvamizi na watu maarufu kutekwa, baadhi kutoweka na wengine kuibuliwa siku chache baadaye, kumesababisha Mbunge wa Kigoma Mjini, Zitto Kabwe (ACT-Wazalendo) kuamua kupeleka suala hilo bungeni.

 Zitto alisema jana kuwa amepata taarifa za kushtua hivyo atalipeleka suala hilo bungeni, huku  mwenzake wa Arusha Mjini, Godbless Lema akimtaka Waziri wa Mambo ya Ndani, Mwigulu Nchemba ajiuzulu.

  Matukio yaliyoibua mjadala huo ni kutekwa na baadaye kuachiwa kwa msanii wa hiphop, Roma Mkatoliki na wenzake wanne, kuvamiwa kwa Mbunge wa Mtama, Nape Nnauye (CCM) na kuvamiwa kwa studio za televisheni za Kampuni ya Clouds Media.

 Pia, matukio hayo yamesababisha kukumbukwa kwa tukio la kutoweka kwa Ben Saanane, ambaye alikuwa msaidizi wa Mwenyekiti wa Chadema, Freeman Mbowe.

 Zitto alisema ana taarifa za kushtua kuhusu kupotea kwa Saanane, taarifa ambazo alisema ni Bunge pekee linaloweza kuzithibitisha, hivyo anaandaa hoja binafsi atakayoiwasilisha ndani ya chombo hicho cha kuisimamia Serikali wakati wowote. Kwa sasa, Bunge linaendelea na vikao vyake vya bajeti mjini Dodoma.

Imefichukaa...Nuh Mziwanda Afumwa na Shilole Zanzibar..Ajitetea Hivi..!!!

$
0
0

Msanii wa bongo fleva Nuh Mziwanda amesema Shilole ni msanii mwenzake na walivyoenda Zanzibar hawakuwa pamoja kila mtu alikuwa ameenda kwa kazi yake.

Akipiga story kupitia eNewz ya EATV Nuh Mziwanda amesema hata kama akiamua kutoka nje ya ndoa siyo lazima atoke na Shilole kwakuwa wanawake ni wengi na anapokuwa  kwenye show huwa anakutana na wanawake wengi hivyo siyo lazima atembee na Shilole..

Hata hivyo Nuh Mziwanda amesema haoni sababu ya kutoka nje ya ndoa yake na mashabiki zake wanapaswa kuelewa kwamba anapokuwa kwenye show moja na Shilole ni kutokana na maslahi hawezi kukataa pesa eti kwa sababu show aliyopata Shilole yupo.

Pia Nuh alimalizia kwa kusema "Zanzibar kila mtu alienda kwa kazi zake japo tulijikuta tumeshukia hotel moja, Shilole akiwa ameenda kuzindua Pub lakini mimi nilikuwa nimeitwa na nimepewa pesa zangu kwa ajili ya kufanya show"

Tahadhari..Mvua Kubwa Zaidi Kunyesha Usiku Huu,,Sambaza Ujumbe Huu kwa Jamaa Zako..!!!

$
0
0

Mamlaka ya Hali ya Hewa Tanzania (TMA) imetoa tahadhari  kwa Watanzania  juu ya kuendelea kunyesha kwa mvua kubwa kuanzia leo Jumatatu hadi  Jumatano.

Katika taarifa yake kwa vyombo vya habari iliyoitoa leo (Jumatatu), mamlaka hiyo imesema kutakuwa na vipindi vifupi vya mvua kubwa inayozidi milimita 50 ndani ya saa 24.

Mamlaka hiyo imesema mikoa itakayoathirika ni Dar es Salaam, Pwani, Morogoro, Lindi, Mtwara, Tanga pamoja na visiwa vya Unguja na Pemba.

“Mvua hii yenye wastani wa asilimia 60, inatokana na kuimarika kwa ukanda wa mvua nchini,” imesema taarifa hiyo.

Kutokana na hali hiyo, mamlaka imewataka wakazi mikoa hiyo kuchukua hatua stahiki.

Details: Roma Asimulia Ilivyokuwa Baada ya Kutekwa..!!!

$
0
0

Hatimaye rapper Roma amesimulia mkasa wa kutekwa akiwa na wenzake watatu kuanzia Jumatano iliyopita hadi Ijumaa. Tumekuandikia kile alichosimulia.

Wakati naendelea na shughuli zangu, walifika watu ambao sikuweza kuwafahamu mbaya zaidi walikuwa na silaha za moto na amri yao ya kwanza ilikuwa ni ingia ndani ya gari. Baada ya kuingia tu ndani ya gari, nakumbuka wale watu walitufunga usoni na vitambaa na kutuamuru tuiname chini kwa order ya kwamba inama chini na usiinuke na wakiwa wameshika silaha za moto. Hofu yetu ikatufanya wote tuiname chini na gari ikaanza kuondoka maeneo ya studio na ikaelekea ambako sisi hatukupajua.

Tulipofika hiyo sehemu ambayo hatuijui tukiwa tumefungwa usoni, na walitufunga na pingu. Tukaenda sehemu ambayo hatuijui, kwa kuhisi tu hujui chochote na ndio sehemu ambayo tulikaa kwa siku zote tatu kwasababu ilikuwa ni Jumatano, Alhamis, tunakuja kupata sisi usalama ilikuwa ni Ijumaa usiku kuamkia Jumamosi. Kwahiyo siku zote watu kilichokuwa kinaendelea huko ambako tupo na hatupafahamu, kuna mahojiano yalikuwa yanaendelea baina yetu na wale watu, mahojiano yenyewe ndio hizo details ambazo nasema tumesharipoti katika vyombo vya dola wanaendelea na upelelezi, wakimaliza upelelezi, wao wenyewe wataongea watatoa taarifa.

Lakini mahojiano hayo yaliendana na vipigo ambavyo nimeonesha majereha. Kila mtu alipata majereha, kila mtu alipigwa, kwahiyo mahojiano yalikuwa yanaendelea na hizo torture mpaka siku ya Ijumaa usiku sababu hatukuwa tunaweza kugundua ni saa ngapi. Tulitolewa hapo tulipokuwepo na kuingizwa ndani ya gari na safari ilipoanza hapo tukiwa tumefungwa vilevile lakini safari hiyo tulifungwa na mdomo, tukafungwa na miguu tukiwa ndani ya gari tukaenda umbali ambao hatukuweza kujua ni wapi mpaka kufika eneo ambalo tukatupwa tukiwa katika hali hiyo wote wanne.

Ilikuwa ni usiku sanam hatukuweza kujua ni wapi lakini tulifikiri ni kwenye dimbwi tu la maji tumetupwa. Niliweza kujifungua mimi wa kwanza nikawafungua na wenzangu, hatukujua ni maeneo gani lakini yalikuwa maeneo ya baharini, tulikuwa na maumivu sana. Nilivyoweza kuwafungua wenzangu tukajikuta tuko salama, tukaanza kutembea kwa muda kiasi na baada ya muda tukakutana na kibao fulani kimeandikwa mahaba beach tukagundua kuwa pale ni maeneo ya Ununio. Tulitembea kwa umbali mrefu sana mpaka tulipoweza kupata msaada baada ya hapo tukaenda kuripoti maelezo yote katika kituo cha polisi.

ALIPOFIKA NYUMBANI

Tulipofika Mbezi mimi nagonga mlango, ndani hakuna mtu, nikazunguka mlango wa nyuma nikavunja mlango wa nyumbani kwangu. Kuingia ndani familia hakuna, hilo lilikuwa pigo jingine kwangu sababu sikujua familia yangu nayo imeenda wapi. hiyo ikawa hofu nyingine, kwahiyo tulichokifanya nikawaambia tubadilishe nguo nikachukua nguo nikawa wenzangu, tutokea katika zile nguo za matatizo. Nikawaambia kama familia haipo nadhani hapa si salama, ilikuwa inaelekea alfajiri saa kumi saa kumi na moja ikabidi tutoke tutafute bajaji tukiwa katika mavazi salama ikawa ni nafuu kwetu. Tulipotafuta bajaji tukaomba namba ya simu ya bajaji kumpigia mtu. Na mtu wa kwanza kumpigia ni bosi wetu J-Murder, hakutuamini kwamba ni sisi kwasababu ya kile alichokuwa anajua kinaendelea uraiani.
Viewing all 104667 articles
Browse latest View live




Latest Images