Quantcast
Channel: UDAKU SPECIAL
Viewing all 104789 articles
Browse latest View live

SIMBA Wadhihirisha Kuwa si wa Mchezo Mchezo...Warudi Kileleni

$
0
0

SIMBA SC imetoka nyuma kwa mabao 2-0 na kushinda 3-2 dhidi ya wenyeji, Mbao FC katika mchezo wa Ligi Kuu ya Vodacom Tanzania Bara jioni ya leo Uwanja wa CCM Kirumba, Mwanza.

Sifa zimuendee mshambuliaji Muivory Coast, Frederick Blagnon aliyetokea benchi na kwenda kufunga mabao mawili dakika za lala salama kabla ya kiungo Muzamil Yassin kufunga la ushindi.

Katika mchezo huo uliochezeshwa na refa  Shomari Lawi kutoka Kigoma aliyesaidiwa na Joseph Bulali na Mohammed Mkono wote wa Tanga, dakika 45 za kipindi cha kwanza zilimalizika wenyeji Mbao FC wakiwa mbele kwa mabao 2-0.

George Sangija alianza kuwainua vitini mashabiki wa timu ya nyumbani kwa bao safi dakika ya 21 baada ya kuwatoka mabeki wa Simba na kuingia kwenye boksi la Simba kabla ya kumchambua kipa Peter Manyika. 

Baada ya bao hilo, kocha Mcameroon wa Simba, Joseph Marius Omog alifanya mabadiliko akimpumzisha mshambuliaji Pastory Athanas na kumuingiza kiungo Said Hamisi Ndemla.

Mbao wakaendelea kutawala mchezo baada ya bao hilo na haikuwa ajabu dakika ya 36 walipopata bao la pili kupitia kwa Evarigestus Bernard aliyemalizia pasi ya mfungaji wa bao la kwanza, Sangija.

Baada ya bao hilo, kocha Omog wa Simba akamuinua mshambuliaji Mrundi Laudit Mavugo kwenda kuchukua nafasi ya beki wa kulia, Hamad Juma.

Simba wakafanya mabadiliko ya ndani, Bokungu akienda kucheza beki ya kulia na Mghana James Kotei akirudi kucheza beki ya kati na Mganda Juuko Murshid.

Kipindi cha pili, kocha Omog alikianza na mabadiliko tena akimtoa mshambuliaji Juma Luizio na kumuingiza Blagnon aliyekwenda kufanya kazi kubwa akicheza mechi yake ya kwanza ya Ligi kuu mzunguko wa pili.

Blagnon alifunga bao la kwanza la Simba dakika ya 82 kwa kichwa kuparaza akiwa amelipa mgongo lango la Mbao kufuatia mpira mrefu wa James Kotei.

Bao hilo lilifungwa dakika tano tu baada ya Nahodha wa Mbao, Yussuf Ndikumana kuumia na kukimbizwa hospitali, nafasi yake ikichukuliwa na.

Blagnon tena akawainua vitini mashabiki wa Simba baada ya kufunga katika purukushani kwenye eneo la Mbao kufuatia mpira mrefu wa Bokungu dakika ya 91.

Katika mchezo huo uliodumu kwa dakika 103, kiungo Muzamil Yassin aliifungia Simba bao la ushindi dakika ya 96 akimalizia mpira uliorudi baada ya kuokolewa na mabeki wa Mbao.

Ushindi huo unairejesha Simba kileleni, ikifikisha pointi 58 baada ya kucheza mechi 26, wakati mabingwa watetezi, Yanga wanarudi nafasi ya pili kwa pointi zao 56.

Kikosi cha Mbao FC kilikuwa; Erick Ngwengwe, Asante Kwasi, David Mwasa, Boniphace Maganga, Yussuf Ndikumana, Vincent Philipo, George Sangija, Salmin Hoza, Pius Buswita, Ibrahim Njohole na Everigeston Bernard.

Simba SC; Peter Manyika, Hamad Juma, Mohammed Hussein ‘Tshabalala’,
Juuko Murshid, Janvier Bokungu, James Kotei, Shiza Kichuya, Muzamil Yassin, Juma Luizio, Mo Ibrahim na Pastory Athanas.

Huyu Ndo Mwanamke wa Kuoa, Wala Usimcheleweshe..!!!

$
0
0

Ndo kwanza nimemaliza chuo maisha bado hajasettle kabisa, nahangaika tu na maisha Mara nimeajiriwa huku Mara kule. Huku nikiwa na extended family niliamua kuchukua gheto mitaa flani kwa sababu pia ya hali mbaya ya kuchumi nilichukua tu room moja nikanunua kwa Tv kangu nchi 14, jiko la mafuta na mkaa pia, nilinunua tu godoro dogo la nne kwa nne na kapet la plastic na mito miwili nikaanza kuishi gheto, hiyo nyumba ilikuwa na wapangaji 5 tuna share choo.

Nikiwa kazini dada mmoja sister du kweli akawa amenipenda sana na anataka tuwe karibu maskini nikawa nawaza huyu dada si ataniingiza hasara ambazo mi sikuwa nazihitaji maana mi nilishajizoelea gheto kwangu weekend napika mwenyewe isipokuwa siku nyingine za kati kati ya week.

Akawa analazimisha sana kuja kwangu nikamwambia kwangu sijui kama atapaweza naishi kigogo mazingira yangu nayajua mwenyewe, nikamchania tu ukweli kasema hajali ye anataka tu aje home apafahamu hata siku nikipata shida anifate.

Basi weekend moja nikamwambia njoo akaja dada wa watu.hata kumwelekeza ilikuwa shida maana nlimwambia akifika sehemu flani kuna uzwa mkaa kwa magunia akate kushoto mpaka kwenye kibanda wanachoonesha video baada ya hapo anyooshe mpaka kwa mama muuza mihogo mama Hadija apinde kushoto anyooke mpaka akikuta mtaro wa maji machafu hapo anisubiri nikamchukue yule dada alifanikiwa kweli nikaenda mchukua amechoka na jasho linamtoka make up imetoka maskini.

Nikatembea naye mpaka gheto kumkaribisha hivi namwona yupo fresh tu akajipumzisha chini kwenye godoro apulizwe feni zile za mezani angalau apoe kile chumba changu kina vidirisha vidogo vya kishkaji tu baada kama ya nusu saa salamu na utani akatoa kwenye begi lake khanga akavua suruali yake akaanza kwanza kuosha vyombo vilikuwa vichafu alipomaliza akawasha mkaa akauliza kama kuna mchele au unga vilikuwepo basi yule dada akapika pale na samaki kwa nazi mimi nimetulia tu naangalia tv kipindi cha marudio ya michezo.

Saa saba hivi kila kitu kikawa tayari tukakaa kwenye godoro tukapiga msosi. tukamaliza tukakaa kupiga story za hapa na pale mpaka mida ya saa 10 akasema akaoeshe vyombo akaenda akaosha akarudi tukawa tupo kwenye godoro namuuzia chai tu. Saa 12 akanambia anataka kuondoka nikamsindikiza akapanda daladala ilikuwa imejaa sana alisimama akaenda kwao masaki alifika kwao saa 2 usiku.

Jumatatu tukaonana kazini tukawa tunapiga story tukaenda lunch n.k next week akaomba tena aje kunitembelea sikuamini. Now ni kama miezi minne huyu dada bado huwa anataman aje kunitembelea pamoja na mazingira yangu kutokuwa conducive. 

Nikawa nawaza huyu dada inawezekana vipi akawa interested nami? Na alikuja kipindi flani akaniletea rice cooker, tumeendaenda akaniletea badhi ya vyombo. Maskini nawaza huyu dada mbona angeweza kuwa na mwanaume ambaye ana pesa na vitu vingine vyote lakini kwa nini kaamua kwangu?

Tulishapima hana ugonjwa wowote, yaani hana tatizo na ni mzuri mpaka namwogopa. amekulia mazingira mazuri sana huko kwao kuna siku alinipeleka kwao ni kuzuri hasa ni zile family zinakula chakula cha draft yaani unachukua hapa, unachukua pale unachanganya na kule unapiga msosi ndani kwao ni baridi muda wote na sebule wanazo tatu katika nyumba moja sasa inakuaje anampenda msela kama mimi ambaye sijasettle kabisa?

HIVI WANAWAKE WA NAMNA HII BADO WAPO KWELI? Au anataka roho yangu? nashindwa hata kumwambia kuwa natamani ningemwoa maana daah ndo sasa naanza kujipanga kuhama huku uswahilini nihamie sehemu nyingine ya nyumba self at least vyumba viwili ananambia nibadilishe mazingira kidogo. NATAKA NIOE LAKINI NAWAZA KWA HUYU DADA HARUSI YA KITAJIRI MI NITAIWEZAJE?

Baada ya Utafiti Hizi Ndizo Faida 10 Kubwa za Punyeto..!!!

$
0
0

Kupiga PUNYETO si tu kujihisi au kujisikia vizuri. Pia inaweza kuwa nzuri kwa ajili yenu. Hapa ni kile ambacho maisha ya punyeto kiafya yanaweza kufanya kwa ajili yenu au yako. Soma zaidi ufahamu faida hizi za kushangaza.

1. Husaidia kuweka mfumo wa kinga yako vizuri
"Watu walio imara katika punyeto kuchukua siku nyingi kuwa wagonjwa," anasema Yvonne K. Fulbright, PhD mtaalam wa afya ya ngono.

Kumbuka
Unapaswa bado kufanya mambo mengine ili kwamba kufanya mfumo wako wa kinga na uwe imara, kama vile:
Kula vizuri.
kuwa imara / kufanya mazoezii.
Kupata usingizi wa kutosha.
Kuweka au kufanya chanjo kadiri inavyotakiwa.

2. Inaongeza hamu ya kufanya mapenzi zaidi/ boosts libido
"Kwa kupiga puli, hufanya uume/uke kuwa bora na kuboresha hamu yako ya kufanya mapenzi tena na tena ," anasema Lauren Streicher, MD. Yeye ni msaidizi kliniki profesa wa masuala ya uzazi na magonjwa ya wanawake katika Chuo Kikuu cha Northwestern Feinberg katika Shule ya Tiba huko Chicago.


3. huimarisha cha kibofu cha mkojo kwa Wanawake.
Uimara wa nyonga/pelvic ni muhimu kwa ajili ya kuzuia madhaifu hayo, Kitu ambacho huathiri karibu ya wanawake 30% wakati fulani katika maisha yao. punyeto nzuri ni kama kazi ya kuimarisha misuli ya kiuno au nyonga. Wakati una upofika kileleni/mshindo, kwa sababu ukazaji wa misuli yake, hufanya kuimarisha kwa kibofu.


4. Hupunguza shinikizo la damu.
Utafiti unaonyesha uhusiano kati ya punyeto na kupunguza shinikizo la damu, anasema Joseph J. Pinzone, MD. Yeye ni Mkurugenzi Mtendaji na mkurugenzi wa tiba katika chuo cha Amai.
"Kumekuwa na tafiti nyingi," anasema. "Moja ya utafiti wa kihistoria ulibaini kuwa kujichua (Punyeto) hupunguza sytolic shinikizo la damu." na hiyo ndio kipimo cha ya kwanza cha shinikizo la damu.


5. Huhesabika kama moja ya Zoezi
"Punyeto ni aina moja kubwa sana ya zoezi," Pinzone anasema. Japokuwa haiwezi kuchukua nafasi kama ya mashine ya kufanyia mazoezi yale ya kukimbia au kutembea huku upo pale pale (treadmill), lakini huwa inakuwa umefanya kitu fulani.

6. hupunguza hatari ya kupata shambulio la moyo.
Maisha mazuri ya punyeto ni mazuri pia kwa moyo wako. Licha ya kuwa njia nzuri ya kuongeza kiwango cha ufanisi wa moyo wako, punyeto husaidia kuweka estrogen yako na kiwango cha Testosterone katika uwiano sahihi.


7. Hupunguza maumivu ya mwili
Kabla ya kufikiria panadol au aspirin, jaribu kufika kileleni au mshindo kwa kupiga punyeto.
"kilele au mshindo wa punyeto unaweza kuzuia maumivu," anasema Barry R. Komisaruk, PhD, Profesa, Chuo Kikuu cha New Jersey State.

8. Inaweza kupunguza uwezekano wa kupata kansa ya tezi dume / Prostate Cancer

Punyeto inaweza kusaidia kuizuia saratani ya kibofu.
Watu ambao hupiga puli(angalau mara 10 kwa mwezi) huwa wako katika kiwango cha chini cha uwezekano wa kupata kansa ya kibofu wakati wa utafiti moja ulisema, ambayo ulikuwa ukichapishwa katika jarida la American Medical Association.


9. Inaboresha hali ya usingizi
Unaweza kukubali kwa haraka zaidi baada ya kupiga punyeto, na kwa sababu nzuri. "Baada ya kufika kileleni au mshindo, homoni ya prolactin hutolewa, ambayo hujihusisha na hisia ya utulivu na usingizi" baada ya punyeto, anasema Sheenie Ambardar, MD Mtaalamu wa magonjwa ya akili huko West Hollywood, Califonia.

10. HUPUNGUZA MSONGO WA MAWAZO
Kupiga punyeto kunaweza kupunguza mawazo na wasiwasi. 

Zingatia ..Upigaji Uliokithiri wa Punyeto ni Hatari kwa Afya Yako..Hairuhuiwi kwa Watu Walio na Wapenzi..Piga Kistaarabu

Fahamu Hatua 3 Za Kufuata Unapomtongoza Mwanamke..!!!

$
0
0

Kama unataka kumpata mwanamke unayemzimia bila tatizo lolote basi hakikisha unafuata kila kitu ambacho utasoma sahizi. Hii mbinu imeibwa kutoka kwa kitabu cha Jinsi Ya Kumtongoza Mwanamke: Kuanzia Hadharani Hadi Kitandani - ambacho nakipendekeza kwa yeyote yule ambaye yuko tayari kutumia maujanja ya mazungumzo kumnasa mwanamke yeyote.

Inaenda hivi...

Hatua #1: Angalia ishara.  Ufunguo wa kutongoza ni kuzijua na kuzivumbua ishara fiche kwa yale anayofanya na kutenda. Makinika na stori ambazo anaeleza, mambo ambayo anapenda kuongea na kila kitu ambacho kinaamsha hisia zake. Kumbuka hapa unamakinika na mwanamke na wala si wewe. Usijaribu kutoa maoni  yeyote bila kufikiria madhara yake. Unataka kumtongoza - na hautaki maoni yako yaonekane kama kipingamizi.

Hatua #2: Cheza na hisia zake.  Hapa jambo muhimu la kufahamu ni kuwa - kwa kuchagua mambo yafaayo kumwambia mwanamke, unaweza kubadilisha hisia zake hadi vile unavyotaka wewe. Huu uwezo wa 'kubadilisha' hisia za mwanamke ni jambo MUHIMU zaidi ya yote ikija katika maswala ya kumtongoza mwanamke.

Ingiza hisia nyingi iwezekanavyo katika mazungumzo yako kwake. Jibu stori zake na hisia zifaazo na utakuwa umejitenga mbali na wanaume wa kawaida ambao wanamuapproach.

Hatua #3: Mpe uhakikisho. Kila mwanamke (hata kama ni mrembo kiasi gani ama 'amekamilika' mbele ya macho yako) huwa wanakutojiamini ndani yao ambako kunahitajika kupewa uhakikisho kwa njia moja au nyingine. Hivyo hivyo, jambo muhimu la kuzingatia wakati unampa uhakikisho ni pale ambapo utakuwa mkweli wakati ambapo unampa huo uhakikisho.

Kumwambia kuwa ana macho mazuri hakutasaidia - hii ni kwa sababu maneno kama haya yashatumika mara kwa mara, na kila mwanaume anatumia maneno yayo hayo kama anataka kuingia ndani ya chupi ya mwanamke. Kumpongeza na kumpa uhakikisho kwa jambo ambalo hajiamini nalo kutamfanya akuthamini na kukuweka karibu na yeye zaidi. Na kama umefuata hatua hizi mbili za kwanza vizuri basi hautakosa kupata jambo ambalo litampendeza.

Huu uwezo wa kumtongoza mwanamke kwa kutumia maongezi ni advantage ya kikweli ambayo mwanaume anapaswa kuwa nayo. Ni jambo ambalo ni bora kuwa nalo kama unataka kuwa na nafasi nzuri kwa mwanamke yeyote.

Jinsi Ya Kumshawishi Mwanamke Aaamini Kuwa Yeye Ni Mrembo Zaidi ya Wengine..!!

$
0
0

Kila siku huwa tunapenda kuwaambia wanawake ni warembo. Neno hili limewaingia katika akili zao kiasi cha kuwa ile maana msingi ya neno ‘wewe ni mrembo’ imepotea. Hii ni kwa sababu baadhi ya wanaume wasiojua kutongoza wanaishia kulitumia neno hili vibaya kiasi cha kuwa neno hili limepoteza uhalisia.

Ok, tukiachana na hayo, je ulikuwa wajua kuwa wanawake hupenda kusifiwa? Na ulikuwa ukijua kuwa kumsifia mwanamke mara kwa mara ni njia moja wapo ya kutongoza? Well, leo tumekuja na mambo tofauti ambayo unapaswa kutumia ili umshawishi mwanamke kuwa ni mrembo, na wala hataona kama ni maneno unalompakizia ama maneno ambayo ameyazoea kuyaskiliza awali...
Zama nami...

Jambo la #1
Wakati unapotaka kumsifia mwanamke kuwa ni mrembo, usimwambia, “Wewe ni mrembo” mara kwa mara kwa sababu itafikia mahali flani neno hilo litaisha ladha. Badala yake tafuta sehemu muhimu kutoka kwa mwili wake ambayo utaitumia kama kigezo cha kumsifia. Kwa mfano kama umependezwa na pua yake mwambia, “Nimependezwa na pua yako, kila mara nikiiona najiskia na furaha.” Ama kama umependezwa na mashavu yake unaweza kumwambia, “Mashavu yako ndio nuru ya macho yangu, yanapendeza.” Kumwambia mwanamke maneno kama haya yatamfanya atamani kuwa kando yako. Pia ataona kuwa unamwona anapendeza, unamakinika kuuona urembo wake kupitia kwa viungo vyake vya mwili.

Jambo la #2
Kumsifia mwanamke urembo wake hakuhusishi ngozi yake ya nje pekee, bali pia sehemu yake ya ndani, yaani nafsi yake. Wanaume wengi huwa wanamakinika kumsifia mwanamke umbo, sura na shepu yake huku wakisahau kuwa nafsi ya mwanamke ina umuhimu. Kumsifia mwanamke kwa ujasiri wake, ubunifu wake, hikma, na ujanja kutakupa mkono wa mbele zaidi wakati unapomtongoza ama unapomshawishi. Jambo hili tulishawahi kulizungumzia katika moja ya hatua ya kumtongoza mwanamke ambaye hayuko ligi sawa na wewe. Kumshawishi na kumsifia mwanamke nafsi yake kutamfanya ajiunganishe na wewe zaidi kuliko mwanamke yeyote yule, hivyo hatua iko kwako sasa.

Jambo la #3
Unapomsifia mwanamke usitumie maneno yayo kwa hayo. Yaani wewe kila siku ukikutana na yeye unamwambia, “Nakupenda, leo umeangaza nafsi yangu.” Matumizi ya neno moja siku nenda siku rudi kutamfanya mwanamke atilie shaka iwapo unasema maneno hayo ndani ya moyo wako ama unasema kumridhisha tu. Well, mbona usije na misamiati mipya? Ama mbona usije na maneno ambayo angetamani kuyaskia? Ukitumia maneno kama ‘hurulaini’, ‘malkia, leo nimekuja kwa milki yako’, ‘ua langu la waridi’ nk kutamfanya mwanamke akupende zaidi na zaidi. So anza kutafuta maneno ambayo anayapenda. Usiingiwe na uvivu wa kutumia maneno yayo kwa yayo. Kumbuka hapa unataka kuwa mbora zaidi kati ya wanaume wale wengine. Chukua hatua sasa.

Jambo la #4
Wakati ambapo umeamua kumsifia mwanamke kama huyu, hakikisha kuwa unamwangalia machoni. Kama ni mwanamke ambaye ndio unaanza kumfukuzia basi jenga confidence ya kumwangalia machoni. Usimsifie huku ukiangalia pembeni ama kuangalia kando. Kumbuka wewe ni Mwanaume Alpha, na wanaume alpha huwa hawatatiziki kama wanatoa hisia zao kuhusu wanawake wanaowapenda.

Tumemsikia Roma..ila Maswali Bado ni Mengi

$
0
0

TUMEMSIKIA ROMA

Roma au Rhymes Of Magic Attraction wa Mkatoliki, amezungumza. Ameeleza alichonacho kuhusu tukio lao la kutekwa kisha kupatikana Jumamosi, siku moja kabla ya ile ambayo iliahidiwa na Mwenyekiti wa Kamati ya Ulinzi na Usalama Dar.

Kinyume na ahadi ya Mwenyekiti kuwa vyombo vya ulinzi na usalama vipo imara na kwamba vingempata kabla ya Jumapili, wale watekaji wenyewe walimwachia Roma na wenzake watatu. Bila shaka hao watekaji watakuwa waliusikia mkwara Mwenyekiti wakaingia mitini.

Bado una maswali hata baada ya kumsikiliza Roma? Nakwambia Roma alitekwa, wewe ukibisha endelea kukomaa na ubishi wako.

Waliomteka ni akina nani? Je, ni majambazi? Basi hao ni majambazi wa aina yake, ambao wanawachukua watu na kukaa nao siku tatu wakiwafanyia mahojiano kisha wanawaachia baada ya kuwatesa. Nasisitiza, hao ni majambazi wa aina yake.

Waliomteka siyo vyombo vya dola, ndiyo vyombo vya dola havihusiki, ila akina Roma walifungwa pingu, walipewa mkong’oto na kuhojiwa. Nasisitiza, vyombo vya dola havihusiki.

Walitekwa na watekaji wa kukodi? Sawa kama ndivyo hivyo, hao watekaji eti hawakupewa hata picha ya wanayemtafuta. Rejea maelezo ya awali ya CEO wa Tongwe Records, J Murder kuwa watekaji walipofika studio walimuulizia yeye pamoja na Roma ambaye alikuwepo ila hawakumtambua. Nasisitiza, hao ni watekaji wa aina yake.

Wewe unaamini Roma na wenzake walijiteka? Kuamini hivyo ni aina nyingine ya uzezeta wa kufikiri. Kama ni rahisi na wewe jipeleke wakupe kisago, wakuvunjevunje, wakutoe majeraha, wakukate jino moja halafu wakupe Dola 5,000 ugawane na wenzako. Nasisitiza, jaribu wewe uone kama ni rahisi.

Wewe unaamini ni mchongo? Unapoamini hivyo unathibitisha ule utafiti wa kila Watanzania wanne mmoja ni kichaa ambaye ni wewe. Mjinga gani mwenye kupanga soo na watu wanne ili wapige pesa? Kuna siri hapo? Halafu wanne wote wa kazi gani? Kwa nini wasimalizane na Roma peke yake? Nasisitiza, wewe ni mmoja katika wale wanne.

Jiuliza, wale watu waliwaulizia Roma na J Murder ambaye hakuwepo. Je, wangewakamata Roma na J Murder peke yao ingekuwaje? Inawezekana wameachiwa kwa sababu mpango ulifeli baada ya Murder kukosekana.

Hali si shwari

By @luqmanmaloto

Wema Sepetu na Mwigizaji Mafufu Ndani ya Bifu zito

$
0
0

Wema, Mafufu ndani ya bifu zito
NYOTA wa filamu nchini, Wema Sepetu na Jimmy Mafufu, wameingia kwenye bifu kiasi cha kufikia kurushiana maneno kupitia kitandao ya kijamii.

Wema siku chache zilizopita aliandika maneno katika ukurasa wake wa Instagram kuwa kuna baadhi ya wasanii wa Bongo Movie ni wanafki na wanaacha kuposti ishu ya kupotea kwa mwimbaji Roma badala yake wao wako bize kuposti ishu ya kukutana na Mkuu wa Mkoa ili kuongelea ishu za filamu za Wafilipino na Wakorea.

Maneno hayo yalimchoma Mafufu aliyekuwa miongoni mwa walioposti Ishu hiyo ya Wafilipino, ndipo naye akaamua kumchambua Wema katika peji yake kwa maneno ya Dharau na kashfa ambao ugomvi huo ukaingiliwa na mshabiki wa Wema (Team Wema).

Hata Hivyo Mwanaspoti lilimsaka Mafufu kutaka kujua kuliko, ambapo alisema kuwa, amechukizwa na kauli ya Wema kusema kuwa katika Bongo Movie kuna wanafiki wakati, yeye ni mmoja wa wanafki hao na vilevile hataki kupangiwa cha kuposti katika akaunti zake za mitandao ya kijamii.

“Hata kama hao Team Wema wanitukane vipi, sitaacha kusema ukweli, huyo aliyewaita Bongo movie Wanafiki, yeye ndiye kinara wao asitake kuharibu jina la Bongo Movie na asiwapangie watu cha kuposti kwani nani asiyejua kuwa yeye ni mnafiki? Sitaacha kumwambia ukweli acha watu waendelee kunitusi," alisizitiza.

Wema alipotafutwa kutaka ufafanuzi wa kuanzisha bifu hilo na wenzake, siku yake haikupokelewa licha ya kuita kwa muda mrefu.

Jifunze Namna Unavyoweza Kugeuza Makosa Yako Na Kuwa Mafanikio...!!!

$
0
0

Makosa katika safari yoyote ya mafanikio  ni kitu ambacho hakikwepeki. Bila shaka wewe na mimi tumeshawahi kukosea katika maeneo kadhaa ya maisha yetu. Kukosea huko kulitufanya pengine tujute au kuumia kabisa na kujiona kama vile hatufai.

Je, kitu cha kujiuliza hivi ndivyo tulivyotakiwa kuyachukulia makosa haya na kujihukumu vya kutosha. Jibu rahisi hapa ni hapana. Hatukuwa na sababu ya kujihukumu sana kutokana na makosa yetu, zaidi ya kugeuza makosa hayo na kuwa ushindi.

Na ni kwa namna gani tunaweza kugeuza makosa yetu kuwa ushindi?

1. Jifunze kutokana na makosa hayo.

Ili uweze kuwa mshindi na kugeuza makosa yako kuwa ushindi, ni lazima kujifunza kutokana na makosa ambayo unayafanya. Kama hujifunzi, hakuna utachokuwa unafanya, zaidi utaendelea kukosea na kubaki hapo. Wanaojifunza na kuchukua hatua ndio wanaofanikiwa.

Kukosea kwako hakuna shida sana, shida inakuja pale unaposhindwa kujifunza. Ni muhimu kujifunza kutokana na makosa yako na kurekebisha pale ulipokosea. Kwa kadri utakavozidi kujifunza utajikuta makosa yako yanageuka kuwa ngazi ya kukufanikisha badala ya vizuizi.

2. Chukua jukumu la kuwajibika.

Hautaweza kwenda popote wala kupata mafanikio, ikiwa utakuwa ni mtu wa kulaumu wengine kwamba ndio waliosababisha ukakosea. Mtu wa kwanza kuwajibika kwa makosa uliyofanya ni wewe. Acha kulaumu wengine, utakuwa unapoteza wako bure. Wajibika kwanza wewe.

Unapochukua jukumu la kuwajibika elewa wewe ndiye kiongozi wa maisha yako, hivyo kama kuna makosa yamefanyika kwa sehemu una mchngo wa kusababisha makosa hayo kujitokeza. Badala ya kulaumu, tafuta nini kilichokufanya ukakosea, kirekebishe baada ya hapo endelea na safari yko.

3. Jifunze kutokana na uzoefu.

Linaweza likawa ni jambo linalokuuma sana, hasa pale unapokosea. Lakini nina uhakika pamoja na maumivu hayo kuna kitu ambacho unaweza ukajifunza hapo. Kujifunza huko, huo ndio uzoefu ninaotaka uuchukue hapo na kuugeuza kuwa ushindi pengine yanapotokea makosa kama hayo kwa baadae.

Acha kuishia kuumia na kulalamika na ukabaki hivyo, utakuwa hufanyi kitu. Utumie uzoefu kukusaidia kufika kwenye kilele cha mafanikio. Mara nyingi kwenye kipindi cha kukosea unaweza ukakiona ni cha mateso na maumivu. Lakini , kumbuka siku zote uzoefu ni mwalimu mzuri w mafanikio yako.

4. Badili tabia zako.

Inawezekana ukawa unashindwa na unaendelea kufanya makosa kwa sababu ya tabia ulizonazo. Ili uweze kutoka hapo na kuepuka makosa huna namna nyingine zaidi ya wewe kuweza kubadili tabia zako mara moja. Ukiweza kubadili tabia zako hizo zinazokurudisha nyuma, basi yapo makosa ambayo unayarudia kuyafanya utayaepuka moja kwa moja na kuwa mshindi.

Hivi ndivyo unavyoweza kugeuza kushindwa kwako na kuwa ushindi wa mafanikio. Acha kuhuzunika na kusononeka sana. Fanyia kazi mambo hayo yatakuwa msaada mkubwa kwako sana.

Ukweli Mchungu...Hali ya Uchumi si Shwari...Bidhaa Zapanda Bei..Makampuni Yapunguza Wafanyakazi..!!!

$
0
0

Hali si nzuri katika sekta mbalimbali baada ya baadhi ya biashara kufungwa, kampuni kupunguza wafanyakazi na bidhaa kupanda bei, imeelezwa.

Hali hiyo inaashiria kudorora kwa uchumi huku baadhi wakiihusisha na uwapo wa sera zisizo rafiki kwa ukuaji wa uchumi.

Uchunguzi uliofanywa na gazeti hili kwenye baadhi ya masoko hapa nchini umebaini kuwa bidhaa mbalimbali zimepanda bei yakiwamo maharage ambayo yamepanda kutoka Sh1, 800 hadi kati ya Sh2, 700 na 3,000 kwa kilo.

Pia, sukari imepanda kutoka bei elekezi iliyotolewa na Serikali ya Sh1, 800 hadi Sh2,500, mchele kutoka Sh1,200 hadi 2,600 kwa kilo.

Unga wa sembe nao umepanda kutoka Sh1, 200 hadi Sh 2,000. Bidhaa nyingine zilizopanda ni mboga za majani ambapo fungu la mchicha, chainizi, tembele limepanda kutoka Sh200 hadi Sh400 na Sh500.

Hali hiyo inasadifiwa na ripoti za Ofisi ya Takwimu ya Taifa (NBS) zinazobainisha kuwa kasi ya mfumuko wa bei imekuwa ikiongezeka mwezi hadi mwezi kutoka asilimia 4.8 Novemba mwaka jana hadi asilimia 6.4 kwa mwaka unaoishia Machi mwaka huu.

Mkurugenzi Mtendaji wa Mwananchi Communications Limited (MCL), Francis Nanai amesema kampuni hiyo imepunguza wafanyakazi kwa asilimia nane na kusimamisha ajira zote zilizokuwa zimeidhinishwa mwaka 2016/2017.

TDL ambayo ni kampuni tanzu ya Tanzania Breweries Limited (TBL) nayo mapema Machi 27 mwaka huu ilitangaza kupunguza wafanyakazi wake wasiozidi 50 ili kukabiliana na hali ya kiuchumi.

Ukubali Ukatae...Harmorapa, Bahati Haiji Mara Mbili. Ukomedi Unakufaa,,!!!!

$
0
0

ATHUMANI Omary ambaye Sasa ni gumzo kubwa kwenye mitandao ya kijamii na magazeti kama Harmorapa, ni msanii ambaye amekuja na bahati ambayo wengi wameshindwa kuipata, hata baada ya miaka kadhaa ya kuhangaikia jina kwenye Muziki wa Kizazi Kipya.

Wapo wanaoamini katika bahati na wengine wanajaribu kumhusisha meneja wake, Irene kuwa ndiye aliye nyuma ya matukio yote yanayoendelea kumhusisha msanii huyo ambaye ana nyimbo mbili tu kwenye gemu, Kiboko ya Mabishoo ukiwa ndiyo wenye kupigwa zaidi, kutokana na kumshirikisha mkongwe Juma Kassim ‘Nature’. Kijana huyu mdogo kiumri, anaonyesha wazi kuwa amekuja mjini kutafuta, kwani hana aibu na wala hajisikii vibaya.

Yupo tayari wakati wowote kusimama mbele ya kamera na kujibu chochote anachoulizwa, ingawa ukimsikiliza kwa makini, unagundua kuwa siyo mjuzi wa mambo mengi anayoyazungumzia.

Tofauti na wasanii wenzake ambao walianza kujulikana kidogokidogo kutokana na kazi zao kupata mashiko masikioni mwa mashabiki, kijana huyu kutoka Kusini mwa nchi yetu ameibuka tu ghafla akiwa hana kazi yoyote ‘mezani’.

Kilichomuibua, ni kule kufanana kusiko kawaida na chipukizi mwenzake, Abdulhan Rajab ‘Harmonize’. Na ndiyo maana nikasema pale mwanzo kuwa kijana huyu ana bahati, kwa sababu kama kufanana na mtu ni tiketi ya kupata jina na umaarufu, wamewahi kutokea watu kibao waliofananishwa na mastaa.

Kuna jamaa alifanana ‘mbaya’ na Ngwair, lakini hajawahi kupata kiki kupitia ufanano huo. Wapo pia waliowahi kufananishwa na akina Ray C, Wema Sepetu na wengineo kibao. Na utakubaliana na mimi kuwa hii ni bahati ya mtende kwa Harmorapa, mwangalie Harmonize mwenyewe, siyo msanii mkubwa kivile, ni dogo tu mmoja hivi aliyepata jina kwa sababu ya Diamond, ingawa anajitahidi kufanya kazi.

Kinachonisikitisha, ni hii tabia ambayo inaonekana wale walio nyuma ya Harmorapa wanadhani itamsaidia kumfanya aendelee kuwa ‘talk of the town’. Amekuwa mtu wa matukio na maigizo zaidi, badala ya kufanya kazi anayoipenda.

Angekuwa makini, hiki kilikuwa ni kipindi kizuri kwake, cha kukaa muda mwingi studio na kufanya kazi nzuri, kwa sababu tayari ana watu wanasubiri kusikia anaimba nini. Lakini yeye amebakia kuwa mtu wa vichekesho, anayeendeshwa na matukio.

Leo ataonekana huku akifanya hivi, kesho yake yupo kule akiwa na flani, ili mradi tu watu wacheke. Angalia, mara tu baada ya kusikika kwa taarifa ya kifo cha kiongozi wa Freemasons Bongo, Andy Chande, watu wanadai kijana huyo mwenyeji wa Masasi alikuwa njiani kwenda kuwafariji wafi wa! Hii maana yake ni kebehi, watu hawamuoni kama mwanamuziki, bali mtu wa vituko.

Na siamini kama ana washauri, maana kama ushauri wenyewe ndiyo ule wa kumfanya ageuke kituko, basi hawajui. Wangemshauri awe comedian, aachane na muziki. Na muda unakimbia, kama ana watu nyuma yake wana matumaini ya kuja ‘kula kuku’ kupitia muziki wake, wamshauri achague moja, muziki au vichekesho.

Na akichagua, afanye hima kabla wakati haujamuacha, maana kwa staili ya maisha aliyoichagua, baada ya kejeli anazochukua hivi sasa, mashabiki wataanza kumdharau na huo ndiyo utakuwa mwisho wake.

Harmorapa anaweza kuwa msanii wa vichekesho na mkono ukaenda kinywani kama wanavyofanya wenzake akina Steve Nyerere, MC Pilipili, Idris Sultan, King Majuto na wengine wa aina hiyo, kwa sababu jina ameshapata na kipaji cha kuvunja watu mbavu kwa vituko anacho, lakini kama ni muziki, kwa staili hii, asahau kutoboa!

Zaidi ya Habari...Vitisho Vyazidi… Mama Aikimbia Nyumba, Amwambia Nay Aache Muziki

$
0
0

WAKATI msanii wa Bongo Fleva, Emmanuel Elibariki ‘Nay wa Mitego’, akiende­lea kusaka faraja ya moyo kutokana na kudai kuwa amekuwa akikabiliana na vitisho, mama yake mzazi ameamua kuondoka ny­umbani kwake akihofia ku­uawa.

Nay aliingia kwenye mgogoro na serikali kutokana na wimbo wake wa Wapo uliosababisha ashikiliwe na jeshi la polisi pamoja na wimbo huo ku­fungiwa na Baraza la Sanaa Tanzania (Basata) lakini al­iokolewa na kwa amri ya Rais John Magufuli.

Akizungumza na Championi Ijumaa, Nay amesema pamoja na tamko la Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo, Harrison Mwakyembe, kutoka kwa rais, kuruhusu wimbo wake uchezwe kote, ameende­lea kuwa na vitisho kila kukicha kutoka kwa watu asiowafamu.

“Ninaishi kwa mashaka makubwa, tangu nilipoachia wimbo huu, maana kumekuwa na mfululizo wa kupigiwa simu na meseji za watu wakinitishia maisha jambo ambalo limepelekea hadi mama yangu kuamua kuhama ny­umbani kwangu na kurudi kwake.

“Kabla sijatoa wimbo huu nilikuwa naishi na mama nyumbani kwangu, lakini ameamua kuondoka kufuatia kutishiwa maisha kila kukicha, lakini baya zaidi vitisho hivyo vimenifanya mimi na mama kupishana mawazo am­bapo ameniambia niachane na wimbo huo, tena ikiwezekana niachane na muziki ili nifanye biashara zingine jambo ambalo sijam­kubalia.

“Nafikiri kutomkubalia kwangu dhahiri nahisi itakuwa ndicho kisa cha kuamua kuondoka na kurudi nyumbani kwake, napata tabu sana na wimbo huu, lakini naamini mimi ni mtu wa mi­simamao hivyo si­wezi kuachana na muziki kisa vitisho.

“Katika maisha hakuna jam­bo rahisi hasa kama wewe ni mpambanaji, vitisho kama hivi sitaki kuvipatia nafasi ya ku­niharibia maisha kwani mimi ninachokifanya ni kuwakilisha mawazo ya wazalendo wengi ambao imekuwa ni ngumu kila mmoja kufikisha maoni yake kwa jamii.

“Kuna watu wanadhani nilipoitwa na Mwakyembe nilienda kushikiwa akili ili ni­badili muziki wangu lakini ukweli ni kwamba, kule alikuwa akinipa ush­auri wa kawaida tu, hivyo hakuna jambo ambalo amenibadili­sha kwenye muziki wangu na nitaen­delea kupigania ninachokiamini ili nitimize ndoto yangu.

“Kifo kipo tu lakini wengi t u m e k u w a waoga wa ku­tangulia hasa ukifikilia jamii inayokuzunguka, Wapo imenikutan­isha na watu nisio­wafahamu, maana nakumbuka siku mbili nyuma zilizo­pita nilipigiwa simu na mtu nisiyemjua akidai anahitaji ku­fanya biashara na mimi hivyo nikaenda kuonana nae Ubungo.

“Huwezi kuamini ningekua muoga basi nisingemsikiliza maana baada ya kukutana alinitoa chemba na kuanza kunihusia juu ya kuachana na wimbo huo akidai watu wameji­fanya kunichunia lakini hakuna anayefurahishwa, hivyo kama nataka amani iendelee basi niuache na kingine akaniamia niwe makini kwani kuna watu wana nia mbaya na mimi.

“Kusema kweli nimeshatishwa sana lakini watu wanacho­takiwa kujua kama kifo kipo basi nitakufa kwa kuwatetea mamilioni ya mashabiki zangu, ila suala la kushikiwa akili au kubadilishwa gia yangu hapa halina nafasi,” anasema Nay.

Ikumbukwe kwamba mwishoni mwa wiki iliyopita Nay baada ya kutoka Dodoma, alikoenda kui­tikia wito wa waziri Mwakyem­be, alisema amefarijika kwa namna moja au nyingine hasa baada ya kukutana, kwani wali­pata muda wa kuketi na kuzun­gumza mambo mengi juu ya sanaa ya muziki.

Huku akimtaka kuwa makini na tunzi zake kwani zimekuwa na mfululizo wa maneno ya kuwa­gusa watu moja kwa moja hivyo awe makini kwani kuna wen­gine huwa si wavumilivu kwani asipojiahadhali wanaweza kuja kumdhuru kwa namna moja au nyingine.

Kuhusiana na Tetesi Kuwa Amelipwa Dola 5000 Ili Kusema Tofauti na Ukweli..Roma Kafunguka Haya Huku Akilia..!!!

$
0
0

Msanii wa Muziki wa kizazi kipya, Roma Mkatoliki amezungumza kwa hisia juu ya wasanii wenzake na watu wengine ambao wanahusisha kutekwa kwao na mchezo wa kiini macho.

“Watu wanasema tunatumika kisiasa tunataka kuichafua Serikali, wapo wanaosema tunatafuta kiki na kuna wengine wamekwenda mbali zaidi na kudai tumelipwa Dola 5,000 ili tutengeneze habari hii.

“Tunaumizwa sana na kauli hizo, nguvu za watu walizotumia kupaza sauti zao halafu watu wanasema tunacheza mchezo, hatuwezi kuhatarisha maisha yetu kwa sababu ya fedha sisi ni watu wa kawaida sana familia zetu ni masikini, lakini hatuwezi kukubali kuumizwa hivi kwa ajili ya fedha.”

Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo Dk Harrison Mwakyembe amesema anataka kupata majibu ya tukio la utekaji wa Roma Mkatoliki kabla ya kuwasilisha bajeti yake bungeni.

“Mimi nitakuwa kwa wapelelezi, nataka kujua suala hili nipate majibu kabla sijawasilisha bajeti yangu bungeni ili bajeti yangu ipite bila makelele mengi,” amesema.


Hivi Ndivyo Naibu Spika Alivyokataa Kata Kata Kuruhusu Bunge Kujadili Suala la Utekaji wa Kina Roma..Akidai Jambo Hilo Halina Maslahi kwa Nchi...!!!

$
0
0

MBUNGE wa Nzega Mjini, Hussein Bashe (CCM), amedai kupewa taarifa na mawaziri kuwa muda wowote anaweza kuuawa na kikundi maalumu kinachoendesha utekaji nchini.

Aidha, Bashe amedai kuwa mbali na yeye kuwa katika hatari hiyo, pia ameambiwa na mawaziri hao wa serikali kuwa kuna wabunge wengine 10 ambao wanawindwa na kikundi hicho na wametahadharishwa 'kuwa makini barabarani'.

Bashe (41), aliyasema hayo bungeni mjini hapa jana asubuhi aliposimama na kukiomba Kiti cha Spika kuahirisha shughuli za Bunge ili kujadili hoja ya dharura akitumia Kanuni ya 47(1),(2)na (3) vya Kanuni za Kudumu za Bunge toleo la Januari 2016.

Huku akiungwa mkono na Mbunge wa Mbeya Mjini, Joseph Mbilinyi (Chadema) na kushangiliwa na baadhi ya wabunge, Bashe alisema kumekuwa kukitokea matukio ya sintofahamu yanayowahusu wabunge na raia wa kawaida yanayoendeshwa na kikundi hicho ambacho alidai kinatoka idara nyeti serikalini.

Katika kujenga hoja yake, Bashe alisema Mbunge wa Geita, Joseph Kasheku (CCM), mbunge wa zamani Mkuranga mkoani Pwani, Adam Malima (CCM), msanii Roma Mkatoliki na yeye mwenyewe ni miongoni mwa watu waliowahi kutekwa huku akikumbushia pia madai ya kupotea kwa Ben Saanane ambaye ni msaidizi wa Mwenyekiti wa Chadema, Freeman Mbowe.

Aliliomba shughuli za Bunge ziahirishwe ili wabunge wajadili jambo la dharura ambalo limekuwa likitokea kwa muda mrefu katika nchini.

"Miongoni mwa watu waliowahi kutekwa ni Mheshimiwa Musukuma (Joseph Kasheku), Mheshimiwa Bashe kwenye mkutano mkuu wa CCM, ndugu Malima, Ben Saanane amepotea... (makofi), juzi amepotea Roma Mkatoliki," alisema Bashe huku akishangiliwa na baadhi ya wabunge kwa kugonga meza.

Alisema zaidi: "Nasema ni jambo la dharura kwa sababu hawa ni wale ambao wanafahamika. Hatujui Watanzania wangapi hawafahamiki katika ngazi za chini.

"Na zipo taarifa ambazo binafsi nimezipokea kutoka kwa baadhi ya mawaziri, wakinitahadharisha mimi binafsi kwamba 'Bashe kuwa makini, wewe ni mmoja kati ya wabunge 11 ambao wamewekwa katika 'list' (orodha). Mkikaa barabarani vibaya, mnaweza kupoteza maisha yenu'.

"Nasema jambo hili ni dharura kwa sababu kikundi hiki kilichomo ndani ya idara ya ... (alitaja idara nyeti), ambacho kimeamua kuchukua mamlaka haya ya kuteka watu, kinaharibu heshima ya serikali yetu, kinaharibu heshima ya chama changu ambacho mimi na wabunge wenzangu wa CCM, tuliomba ridhaa ya kutaka kuwaongoza Watanzania na siyo kuwahatarishia maisha yao."

Bashe alimuomba Naibu Spika wa Bunge, Dk. Tulia Ackson, kuruhusu jambo hilo lijadiliwe na wabunge na ikiwezekana chombo hicho cha kutunga sheria kiunde kamati maalumu ya kuchunguza jambo hilo.

Bashe pia alimuomba Naibu Spika kutumia mamlaka yake kuiagiza Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Usalama na Mambo ya Nje kufanya kazi changamoto hiyo na kulipatia Bunge taarifa kwa ajili ya usalama wa nchi.

"Hali ya nchi siyo salama, Watanzania wana taharuki, Watanzania wanajadili mambo haya katika mitandao na 'there is no statement' (hakuna kauli) toka serikali.

Waziri wa Mambo ya Ndani..." Bashe alisema huku akikatishwa na Naibu Spika ambaye alimtaka aketi ili Kiti cha Spika kiangalie Kanuni ya 47 inaeleza nini kuhusu madai yake.

Kabla ya kutoa uamuzi wa Kiti kuhusu madai ya Bashe, Naibu Spika alitoa nafasi kwa Sugu kueleza hoja yake bungeni baada ya mbunge huyo kusimama na kuomba kupewa nafasi ya kuwasilisha hoja ya dharura bungeni.

Akitumia Kanuni ya 47, Sugu aliunga mkono hoja ya Bashe kwamba Bunge liahirishe shughuli zake za jana na kujadili hoja ya dharura ya kadhia ya utekaji na kupotea kitatanishi kwa watu nchini.

"Taifa limekuwa gizani kwa utamaduni mpya uliozuka wa kuteka watu, utamaduni ambao si wa kwetu, ni utamaduni wa kimafia, utamaduni ambao kwa mara ya mwisho kwenye mipaka ya Bara na visiwani, tuliusikia alipotekwa Mzee Kassim Hanga kule Zanzibar miaka hiyo," Sugu alisema.

"Lakini tangu kipindi hicho haujakuwapo tena. Toka operesheni hii ya kuteka watu nyara ianze, kila anayehusika na usalama likiwamo Jeshi la Polisi, 'always' (mara kwa mara) wanasema 'hatujui, hatujawaona kwenye vituo vyote'.

Nchi inabaki kwenye tahayari, kapotea Ben Saanane, mara miili sita, saba imeopolewa kwenye Mto Ruvu ikaenda kuzikwa bila kufanyiwa 'post-mortem' (uchunguzi) kwa amri ya ambaye hatujui ni nani.

"Bashe alitekwa, Nape (Nnauye) alitekwa, akaokolewa na Maulid Kitenge, vinginevyo pengine angekuwa ametekwa, hakuna mtu aliyezungumza kitu."

Kutokana na changamoto hiyo mpya nchini, Sugu alimshauri Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Mwigulu Nchemba, kuachia ngazi ili kulinda heshima yake kama kweli bado ana matumaini ya kuwa Rais wa Tanzania.

"Waziri wa Mambo ya Ndani yuko kimya mpaka najiuliza kama anabanwa kiasi hicho, huyu ni mtu 'potential' (muhimu) ambaye alifikia hatua ya kugombea urais na bado ana 'future'," Sugu alisema.

"Kwanini asijiuzulu, akalinda heshima yake kuliko kukaa kwenye 'mess' (aibu)? Alihoji Sugu. "Kujiuzulu ni utamaduni mzuri.

Mzee (Alhaji Ali Hassan) Mwinyi alikuwa Waziri wa Mambo ya Ndani miaka hiyo, mwaka '76, ikatokea messy (kuboronga), 'aka-bounce back' (akarejea), miaka ya '80 akaja kuwa Rais wa nchi hii.

"Ndugu yangu Mwigulu, nikushauri kama hushirikishwi, mambo yanafanyika, hamna mtu anakuja na majibu.
"Lakini juzi baada ya kutekwa Roma Mkatoliki, tumepata mwanga. Yupo mtu Dar es Salaam alituambia anajua Roma aliko na angerudi kabla ya Jumapili.

"Kama Waziri Kivuli (wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo), nikatoka Jumamosi na 'ku-demand' (kuagiza) kwamba aachiwe siku ileile na akaachiwa, nashukuru Mungu. Sasa basi, hatujui nani 'next' (anayefuata) atatekwa. Yawezekana Sugu ingawa mimi 'I don't care much' (sijali) kwa sababu Mbeya wataziba nafasi yangu.

"Lakini Naibu Spika 'it could be you' (yaweza kuwa wewe). 'It is the war' (ni vita), 'no body is safe' (hakuna aliye salama. Kwanini Bunge hili lisijadili na hatimaye limlazimishe Bashite kama alivyojua kwamba Roma Mkatoliki yuko wapi na angemrudisha Jumapili, tumlazimishe sasa Bunge hili tujadili na baadaye tumlazimishe Bashite atutajie aliko Ben Saanane na atutajie kwamba ili miili iliyotupwa Ruvu na kuzikwa haraka haraka bila kufanyiwa 'post-mortem' ni ya kina nani kwa sababu huyu anaonekana anajua undani wa mambo haya."

KULIPATIA UFUMBUZI
Akijibu maombi ya wabunge hao, Naibu Spika alikataa kuruhusu jambo hilo kujadiliwa bungeni kwa kupitia utaratibu wa hoja ya dharura kwa kuwa vyombo vya sheria vinaweza kulipatia ufumbuzi.

Dk. Acskon alisema jambo la dharura linaloweza kusababisha kuahirishwa kwa shughuli za Bunge kulijadili ni lile lenye maslahi kwa umma na iwapo utatuzi wake unategemea zaidi ya utekelezaji wa kawaida wa sheria.

"Waheshimiwa Bashe na Sugu wameeleza kwa kirefu kuhusu jambo ambalo limetokea hapa na pale, lakini pia tumeliona kwenye vyombo vya habari na tumelisoma," Dk. Ackson alisema.

"Maelezo yao kwa ujumla yanahusu mambo ambayo yanawapata wananchi ambayo watu kadhaa wametajwa kama mifano kwamba wamekuwa wakitekwa ama wamekuwa wakikamatwa.

"Sasa, nadhani wote tunafahamu matakwa ya Kanuni ya 47, hili jambo la hawa watu kukamatwa ama kutekwa kwa sababu sasa hata wale waliokamatwa, na wao wamewekwa kwenye kundi la kutekwa. Sasa sijui kama tunaweza kuyatenganisha haya mambo mawili; nani amekamatwa na nani ametekwa?

"Lakini maelekezo yaliyotolewa kwa kirefu ni kwamba wakati mwingine mtu akiwa haonekani, polisi ndiyo sehemu ya kwanza ambayo inaulizwa na yapo mazingira polisi haijatoa maelezo kwamba hawa watu wako wapi na mifano imekwishatajwa.

"Mheshimiwa Bashe amekwenda mbali zaidi akisema kwamba kipo kikundi ambacho kinafanya kazi hiyo.

Na Mheshimiwa Joseph Mbilinyi na yeye ameeleza kwamba hili jambo sasa limekuwa kama utamaduni kwa maana ya kwamba linatokea kila wakati na akaenda mbele zaidi na kumshauri Mheshimiwa Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi (Nchemba) kwamba aweze kujiuzulu akiona inafaa.

"Kanuni ya 47 huwa ni lazima isomwe pamoja na (Kanuni ya) 48 kwa sababu 48 ndiyo inayoweka masharti ya matumizi ya Kanuni ya 47.

Sasa kwa kuwa Kanuni ya 48(4) nitaisoma, inasema hivi 'jambo lolote litahesabiwa kuwa ni lenye maslahi kwa umma iwapo utatuzi wake unategemea kuwa zaidi kuliko zile za utekelezaji wa kawaida wa sheria peke yake.

"Masuala haya yaliyoulizwa na Mheshimiwa Bashe na pia yaliyoulizwa na Mheshimiwa Mbilinyi yako chini ya utaratibu wa kisheria na Bunge hili litashughulika na mambo ambayo ni yenye maslahi ambayo sheria haina uwezo wa kuyatolea majibu.

Kwa sababu hiyo, sitalihesabu hili jambo kwa mujibu wa Kanuni ya 47(4) kwamba ni jambo la dharura lakini ni jambo ambalo utaratibu wa kawaida wa kisheria unaweza ukafanya kazi. Hayo ndiyo majibu yangu kuhusu matumizi ya Kanuni ya 47.

Matukio ya kupotea, kutekwa na kuuawa kwa wanasiasa nchini ni nadra, ingawa Juni 12, mwaka jana, chama cha ACt-Wazalendo kilidai kiongozi wake mkuu, Zitto Kabwe, alikuwa hajulikani alipo kwa zaidi ya saa 12 huku akiwa anasakwa na Jeshi la Polisi.

TATIZO la Mwanamke Kukosa Hamu ya Tendo la Ndoa...Sababu na Suluhisho

$
0
0

Tatizo la kukosa hamu ya kufanya mapenzi huwatokea zaidi wanawake kuliko wanaume lakini ni wanaume wanaokerwa zaidi na tatizo hili kulio wanawake. Wakati ambapo ni asilimia 15 hadi 16 ya wanaume wenye tatizo hili, idadi ya wanawake ni mara mbili ya hii ya wanaume. Lakini wakati ni asilimia 23 ya wanaume wanaonyesha kuridhika kuishi na tatizo hili, asilimia 46 ya wanawake wapo radhi kabisa kuendelea kuishi na tatizo hili.

Si lazima kuendelea kuishi na tatizo la kukosa hamu ya kufanya tendo la ndoa kwa sababu kuna mambo mengi unayoweza kuyafanya ili kuondokana na hili tatizo.

Hali ya kupenda kufanya mapenzi au tendo la ndoa kwa mwanamke inabadilikabadilika sana ikipanda na kushuka kulingana na matukio mbalibali yanayomtokea katika maisha yake. Baadhi ya matukio yanayoathiri hamu ya mwanamke kufanya mapenzi ni pamoja na kuanza na kwisha kwa mahusiano ya kimapenzi na mwanamme, kupata ujauzito, na magonjwa. Kama wewe mwanamke umepatwa na ha hii unaweza kukabiliana nayo kwa kubalisha jinsi unavyoishi, kufanya mambo kadhaa yatakayo badilisha hali hii au kutumia baadhi ya dawa zinazosaidia kuondoa tatizo hili.

Jee, Utajuaje kama Una Tatizo?

Kuna vitu vingi ukiviona vinakutokea, ujue una tatizo hili la kukosa hamu ya kufanya mapenzi.Tulivijadili viashiria hivi kwa kina tulipozungumzia tatizo hili la kukosa hamu ya kufanya tendo la ndoa kwa wanaume. Unaweza kusoma tulivyojadili kwa kusoma ukurasa huu “Mwanamme Kukosa Hamu Ya Kufanya Tendo La Ndoa

Sababu Za Kukosa Hamu Ya Kufanya Tendo La Ndoa

Sababu zinazoweza kupelekea mwanamke kukosa hamu ya kufanya tendo la ndoa ni nyingi lakini kwa ujumla karibu zote tunaweza kuzigawanya katika makundi manne:

1. Mahusiano Baina Ya Mwanamke Na Mwanamme Kwa wanawake walio wengi ukaribu wa kihisia ndicho kitu cha kwanza katika kujenga mapenzi kati yake na mwanamme. Hivyo, mahusiano mabovu yaweza kuwa ndicho chanzo cha kukosa hamu ya kufanya tendo la ndoa kwa mwanamke. Mwanamke atakosa hamu ya kufanya mapenzi endapo hakutokuwa na mawasiliano baina yake na mumewe, kutakuwa na migogoro kati yake na mumewe isiyokwisha, kutakuwa na ukosefu wa mawasiliano kuhusu mahitaji yake ya kufanya mapenzi na jinsi ambavyo yeye angependa kufanyiwa kimapenzi na kama atahisi kuna ukosefu wa uaminifu katika ndoa au mahusiano yao.

2. Matatizo Katika Maisha Yako Matatizo mbalimbali katika maisha ya mwanamke humsababishia kukosa hamu ya kufanya mapenzi. Baadhi ya matatizo ambayo huweza kusababisha mwanamke kukosa hamu ya kufanya mapenzi ni pamoja na magonjwa, mabadiliko katika mwili wake na hata matumizi ya baadhi ya madawa:

Matatizo Katika Kufanya Tendo La ndoa. Kama mwanamke anapata maumivu wakati wa kufanya tendo la ndoa au kama mwanamke anakosa kufika kileleni, hali hii inaweza kusababisha akakosa kabisa hamu ya kufanya mapenzi.

Matatizo ya afya. Magonjwa mengi husababisha mwanamke akose hamu ya kufanya tendo la ndoa. Baadhi ya magonjwa ni maumivu ya viungo vya mifupa (arthritis), kansa, ugonjwa wa kisukari, high blood pressure, matatizo katika mishipa ya damu ya arteri na matatizo ya akili.

Matumizi ya madawa. Baadhi ya madawa yakitumiwa, huondoa kabisa hamu ya kufanya mapenzi kwa mwanamke. Mfano wa dawa hizo ni madawa ya kukabiliana na msongo wa mawazo.

Mtindo wa maisha. Matumizi ya pombe kuzidi kiwango, uvutaji wa sigara na madawa ya kulenvya huathiri hamu ya kufanya mapenzi.

Upasuaji. Upasuaji uliofanyika katika maeneo ya maziwa au katika maeneno ya viungo vya uzazi humbadilishia mwanamke mwonekano wake, huathiri ufanyaji kazi wa viungo hivyo na mwisho kuathiri hamu yake ya kufanya mapenzi.

Uchovu. Uchovu unaotokana na kulea watoto wadogo au vikongwe kuweza kuathri hamu ya mwanamke ya kufanya mapenzi.

3. Mabadiliko Katika Mfumo Wa Homoni. Kukoma Hedhi.Mabadilko ya viwango vya homoni katika mwili wa mwanamke yanaweza kusababisha kukosa hamu ya kufanya mapenzi kwa mwanamke. Kupungua kwa Estrogen katika mwili wa mwanamke katika kipindi cha kuelekea kukoma hedhi kunaweza kusababisha ukosefu wa hamu ya kufanya mapenzi. Upungufu wa homoni hiyo husababisha uyabisi wa wa viungo vya sehemu nyeti na kusababisha maumivu wakati wa kufanya tendo la ndoa.

Mwanamke pia huweza kuwa na upungufu wa homoni ya testosterone, homoni ambayo husaidia kuongeza hamu ya kufanya mapenzi kwa wanaume na wanawake, hivyo mwanamke huyo akapungukiwa na hamu ya kufanya mapenzi.

Pamoja na kuwa wanawake wengi huendelea kupata hamu ya kufanya mapenzi baada ya kukoma hedhi, baadhi kupungukiwa na hamu hiyo baada ya mabadiliko haya ya viwango vya homoni katika miili yao.

Ujauzito na kunyonyesha. Mabadiliko katika mfumo wa homoni wakati wa ujauzito, baada ya kujifungua na wakati wa kunyonyesha huweza kusababisha mwanamke kukos hamu ya kufanya tendo la ndoa.

4. Matatizo Ya Kisaikolojia 
Matatizo ya kisaikolojia yana mchango katika kumfanya mwanamke akose hamu ya kufanya tendo la ndoa. Baadhi ya mtatatizo hayo ni:

Waswasi na kuwa na msongo wa mawazo
Kuwa na mawazo mengi kuhusu matatizo ya kifedha au kikazi
Kuhisi kutothaminiwa katika jamii
Kuwa na historia ya kunyanyaswa kimwili au kijinsia kama kupigwa au kubakwa
Kuwa na historia mbaya ya kimapenzi

Njia Za Kuondoa Tatizo La Kukosa Hamu Ya kufanya Tendo La Ndoa

Hakuna dawa ya moja kwa moja toka hospitalini kwa sasa hivi kwa ajili ya kuondoa tatizo hili, hata hivyo wanawake wengi wanaweza kurudi kwenye hali zao za kawaida kwa kushirikiana na waume zao waelewa. Jaribu kufanya mambo tuliyoyadokeza katika mada yetu ya “Mwanamme Kukosa hamu Ya Kufanya tendoLa Ndoa” ukisaidiana na mumeo. Unahitaji kuchunguza taratibu na kwa kina chanzo cha tatizo lako, na taratibu lifanyie kazi kwa msaada wa mume wako.

Aeshi Hilaly (Mb-CCM): Nilitishwa na Makonda Hadi Sasa Naogopa Kwenda Dar kwa Usalama Wangu..!!!

$
0
0

Mimi Leo nilikuwa sitaki kusema, lakini ngoja tu niseme, nimetishwa na mkuu wa mkoa wa Dar es Salaam, aliniambia nyie wabunge ni wanafiki na nitawashughulikia na nitaanza na wewe, mimi leo Dar naiogopa.

Niko tayari kuhojiwa hapa nimelisema hapa kwa usalama wangu. Alinitisha mbele ya Mkuu wa Wilaya ya Kinondoni pale Colosseum Hotel.

JE Umewahi Kusikia Kuwa Kinywaji Cha Redbull Kina Madhara Makubwa Mwilini...Ukweli Huu Hapa

$
0
0

RED BULL Huuzwa katika maduka makubwa (Supermarkets) na madogo (Retail Shops) katika nchi ya Tanzania, watu wazima na watoto wengi wana mazoea ya kunywa kinywaji hiki ambacho kinaweza kusababisha kifo. Kemikali zinazopatikana katika kinywaji cha RED BULL zilitengenezwa maalum katika maabara za kijeshi za Marekani kwa ajili ya kutuliza mzuka wa maaskari wao wakati wakitekeleza mauaji ya kikatili sana dhidi ya wananchi wa Vietnam miaka ya sitini na sabini. Kemikali hizo zilitumika pia kama dawa ya kuwazindua watu waliozirai (“stress coma”).

Hazikukusudiwa kutumiwa kama kinywaji au kilevi cha kawaida! Duniani kinywaji hiki
(RED BULL) huuzwa kama kitu cha kuleta msismko (Energizer Drink) na matangazo
yake yanataja sifa zake kama ifwatavyo. “Ni kinywaji kinachompa mtu nguvu ya kustahimili na umakini. Humpa mtu kasi ya vitendo” na kadhalika.

RED BULL imesambaa katika nchi 100 kwa mpigo (nchi masikini!). Na matangazo yake huwalenga vijana na watoto, hasa wanamichezo. Hawa ni rahisi kushabikia kinywaji hiki kibaya na kudhurika kiafya baadaye. Katika hali yake ya matumizi ya sasa kinywaji hiki kiligunduliwa na Mjerumani Dietrich Mateschitz ambaye alikikuta huko Hong Kong kikiwa ni mojawapo ya madawa yaliyotumika katika kutengeneza dawa ya mswaki wa meno.

Dawa hiyo ilitengenezwa kwa kemikali ambazo zina kafeni na taurini (“caffeine and “taurine).

Mjerumani huyo aliona vijana wajinga wa huko wakishabikia unywaji wake akaona mwanya wa kufanya biashara na akafanikiwa kukileta ulaya. ATHARI ZA KUNYWA RED BULL Kinywaji kinachotengenezwa na kusambazwa leo hii kina kemikali mbaya iitwayo “Glucuronolactone”, kemikali hatari ambayo ilitengenezwa na idara ya jeshi la Marekani wakati wa vita na Vietnam kwa ajili ya kutuliza mvurugiko wa mawazo wa maaskari wake uliotokana na mauaji ya kinyama waliokuwa wanafanya huko Vietnam.

Kwa sababu ya madhara makubwa ya kinywaji hiki nchi za FRANCE na DENMARK zimepiga marufuku kinywaji hiki na kibatiza jina la “MKOROGO WA UMAUTI”. Katika nchi hizi, utafiti uligundua kuwa maaskari wa Marekani waliotumia kinywaji chenye
kemikali ya “GLUCURONOLACTONE” waliishia kupata madhara ya maumivu makali ya kichwa, uvimbe wa ubongo na hata ugonjwa wa ini (Migraines, Cerebral tumours and liver diseases).

Na kwa sababu hiyo wamarekani waliacha kuwapa maaskari wao hicho kinywaji katika miaka ya sitini na sabini. Jambo la kushangaza ni kuwa lebo ya RED BULL inaonyesha wazi kuwa kinwaji hiki kimetengenezwa kwa kemikali hatari ya “GLUCURONOLACTONE”! Ni kwa sababu hiyo serikali za Denmark na Ufaransa nazo zikapiga marufuku unywaji wa RED BULL. Pamoja na wauzaji wa RED BULL kuweka bayana kuwa ndani mwake mna hiyo kemikali hatari ya “GLUCURONOLACTONE” lebo ya RED BULL hailezi madhara makubwa yanayoletwa na kemikali hiyo.

Madhara ambayo hayakuwekwa bayana kwa mnywaji ni kama yafuatayo:

1. Ni hatari kwa mtu ambaye hafanyi kazi au mazoezi mazito sana kukitumia kwani kina tabia ya kuongeza msukumo wa damu na kasi ya mapigo ya moyo kiasi kwamba mtumiaji anaweza kupatwa na ugonjwa wa moyo.

2. Mtumiaji anaweza kupatwa na ugonjwa wa damu kuvuja ubongoni kwani RED BULL ina kemikali zinazoifanya damu iwe nyembamba ili moyo upate kusukuma damu nyingi bila kutumia nguvu nyingi.

3. Ni hatari kuchanganya RED BULL na pombe ya aina yoyote kwani mchanganyiko wake huwa ni sumu (“Deadly Bomb”) inayoathiri musuli za ini la mtumiaji na kuiacha katika hali ambayo haitapona kamwe.

4. RED BULL Ina vitamini B12 kwa wingi, vitamini ambayo hutumiwa kama dawa ya kuwazindua wagonjwa mahututi. Matumizi ya vitamini hii katika watu wazima ina athari za kuleta shinikizo la damu na humfanya mtu ajisikie kama mlevi.

5. Unywaji wa RED BULL mara kwa mara huvuruga mfumo ya neva za fahamu na husababisha maradhi mithili ya mfadhaiko wa akili usioponyeka.

HITIMISHO:
RED BULL ni kinywaji HATARI SANA ambacho hapana budi kipigwe marufuku katika nchi zote zinazoendelea kwani ni dhahiri kimetengenezwa na kusambazwa ili kiathiri afya za wananchi wasiojiweza wa nchi hizi masikini. Kwa kuwa wengi katika nchi hizi hutumia pombe za kila aina ni wazi kuwa kinywaji hiki kinalenga kuwamaliza watu watu wetu– kana kwamba ukimwi uliobuniwa na hao wabaya wetu hautoshi!

Bashe: CCM Acheni Unafiki, Mimi Nimeshakamatwa na Watu wa Usalama. Nipo Tayari Mniondoe Kwenye Chama Chenu..!!!

$
0
0

Mbunge HusseinBashe awataka wabunge CCM kuacha unafiki, akisema yupo tayari kufukuzwa ila kweli alikamatwa na maafisa wa usalama wa taifa.

'CCM acheni unafiki mimi nimeshakamatwa na watu wa usalama mnasema hawakamati, kwa hili nipo tayari mniondoe kwenye chama.

Huu ni muendelezo wa alichokizungumza jana Bungeni kuhusu usalama wa Taifa kuhusika na utekaji

Zitto Kabwe: Niko Tayari Kuthibitisha Waliovamia Ofisi za Clauds ni Usalama wa Taifa...!!!

$
0
0

Mbunge wa Kigoma Mjini.Zitto Kabwe Ametanabaisha kuwa yupo tayari kutoa Ushahidi wake bungeni kuwa waliovamia Studio la Clouds Tv na Kumtishia Makonda Bastola ni maafisa Usalama wa Taifa.

Hivi Karibuni wabunge wa Upinzan na CCM Wamekuwa wakilaani vitendo vinavyoendelea nchini vya kutekwa kwa watu huku wakidai kuwa vimekuwa vikifanywa na maafisa usalama wa taifa kwa Agizo la Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam Mhe Paul Makonda.

Bungeni Dodoma: Nukuu Tata za Wabunge wa CCM Bungeni Leo..!!!

$
0
0

Namini kwa kinachoedelea Bungeni kama mtu unajua kuchekecha mambo kamwe hautampuuza Roma Mkatoliki na kwamba ati "alijiteka".

Nukuu za Wabunge leo:

"Nipo tayari kuthibitisha kwamba waliovamia Clouds Tv ni Usalama wa Taifa kutoka kikosi cha Ulinzi wa Rais, Nipo tayari pia kuthibitisha aliyemtoloea bastola Nape ni Usalama wa Taifa" Zitto Kabwe (ACT-Wazalendo)

"Hivi Waziri wa Habari alikwenda kufanya nini katika Press ya Roma, mkiambiwa mlimteka mtakataa? Bora kusema ukweli kuliko kukaa kimya, najua mtasema kwa kuwa nilikosa uwaziri No!" Juma Nkamia (CCM)

"Mimi nimekamatwa na kuteswa na Usalama wa Taifa. Nimenyanyaswa sana nchi hii. Ikibidi mnifukuze CCM (machozi)". Hussein Bashe (CCM)

Hakuna sababu ya Mwigulu kuendelea kukaa kimya wakati wananchi wanaishi kwa wasiwasi juu ya usalama wao. Kutoa kauli kunasaidia kutoa hofu" Ridhiwani Kikwete (CCM)

Mimi ni miongoni mwa wabunge niliotishwa na Mkuu wa mkoa wa Dar, na mpaka sasa mimi sikanyagi Dar licha ya kuimisi sana" Hillary Aeshi (CCM)

Tafakari, Chukua hatua

Ukweli Mubashara..Roma Kaumia na Anateseka, Sahau Blah Blah za Mtandaoni...!!!

$
0
0
Ni kama naota kwa hiki nachokisikia na kinachendelea mitandaoni kwa sasa. Siku chache zimepita tuliona ujumbe ulienea katika mitandao ya kijamii ukisomeka “WAKO WAPI WAKINA ROMA?” huku vilio na dua nyingi kutoka kwa mashabiki, wadau, viongozi wa dini na wa kisiasa pamoja na watu wengine walikuwa wakiwaomba zikisikika.

Mungu ni mwema na huwa hachoki kumpa na kumjibu yule amuombaye. Hatimaye Jumamosi asubuhi kupitia mitandao hiyo hiyo zilienea taarifa za kupatikana kwa Roma Mkatoliki, Moni Centralzone, Bin Laden na Imma ambao walitekwa usiku wa Jumatano ya wiki iliyopita na kupelekwa sehemu isiyojulikana.

Baada ya huzuni kugeuka furaha kwa siku moja hatimaye sasa furaha hiyo imegeuka kuwa matusi na kejeli kutoka kwa baadhi ya watu maarufu na wengine ambao wanadai tukio hilo halina ukweli wowote na kulifananisha na kiki kwa watu hao waliotekwa.

Baadhi ya redio mbao zinadai kuwa Roma na wenzake waliotekwa walilipwa kiasi cha dola 5000 kuikamilisha filamu hiyo. Lakini kwa hili nililoliona jana kwa Roma na wenzake waliotekwa, zaidi kwa Roma ambaye ni rapper mpambanaji kutokana na majeraha aliyonayo imewainamisha kwa sura za aibu wale wote waliokuwa mstari wa mbele katika kusambaza ‘upuuzi’ huo ambao ndani yake haukuwa na utafiti wa kutosha tena mbaya zaidi ni watu maarufu ndio wameonekana kufanya kitu hicho.

Fikiri kabla ya kutenda, unatakiwa kujiuliza kutokana na kile kilichoonekana kwa Roma, je thamani ya dola 5000 ambazo wanadai kulilipwa kwa ajili ya kutengeneza hiyo sinema inalingana na zile alama za damu zilizoonekana kwenye mwili wake ambapo imetenganisha rangi ya ngozi ya mwili wake na alama alizozipata? Na lile jino Je? Vipi kuhusu mguu wake na mkono wake wa kushoto?

Ukimuona mtu mzima analia ujue kuna jambo, nimemshuhudia Roma akikohoa kwa shida huku akikutana na maumivu makali anayoyapata. Sauti ya Roma inashindwa kusikika kama vile tulivyomzoea, hata kuongea muda mrefu hawezi kutokana na maumivu anayoyapata kutokana na mateso ambayo wameyapata huko walikopelekwa.

Tusiwafanye wenzetu waliopatwa na majanga hayo kuzidi kuwaweka katika wakati mgumu wakati tayari wametoka katika chupa ndogo iliyofungwa na mfuniko ambapo walikaa humo kwa siku tatu huku wakipata mateso, hakika hakuna anayeweza kuvumilia hilo.

Hakuna anayeijua kesho yake, “Usimtukane mamba kabla haujavuka mto” angalia lisije likakutokea wewe ukashindwa wa kumtazama wala kuzungumza naye kutokana na maneno yanayokufanya yakutoke kwa ajili ya kufurahisha baraza la mitandaoni huku ukiuweka utu pembeni.

Napenda kutanguliza pole kwa Roma, Moni, Imma na Bin Laden ambao wamepatwa na mkasa huo.
Viewing all 104789 articles
Browse latest View live




Latest Images