Quantcast
Channel: UDAKU SPECIAL
Viewing all 104709 articles
Browse latest View live

TATIZO la Nguvu za Kiume na Suluhisho lake

$
0
0
Ukweli ni kwamba ndoa nyingi za Kikristo zinavunjika kutokana na tatizo hili. Je, hakuna haja ya kuitisha mjadala wa kitaifa? Taifa letu linaangamia kwa kukosa maarifa.

Hivi upungufu wa nguvu za kiume ni nini? Kifupi ni mwanamume kutokuwa na uwezo wa kutoa mbegu bora zenye uwezo wa kutungisha mimba, au kutosimama kwa uume.

Takwimu zilizopo zinaonyesha kuwa asilimia 60 ya wanandoa nchini wanakabiliwa tatizo hili. Kwa hiyo, mabango ya waganga yaliyopo barabarani hayajapunguza kabisa tatizo hilo.

Hawa watu wanatibu watu au majini? Hapo ndipo kiini cha makala haya. Sababu kubwa ya ongezeko la wenye matatizo haya ni kwamba dawa nyingi zinazodaiwa kuponya tatizo hili hazina viwango vya kuitwa dawa, bali ni vichocheo tu kwani kinachopigiwa chapuo huwa ni kumudu tendo kitandani na si nguvu asilia.
Waganga wengi wameelekeza nguvu zao huko na ni hapo ndipo janga hili la kitaifa linapoota mizizi.

Ukweli ni kwamba upungufu wa nguvu za kiume hauondolewi kwa dawa za kuchochea nguvu wakati wa tendo. Hizi zina madhara makubwa na mara kadhaa husababisha vifo kwa wanamume wengi wakiwa ‘guest’ na vimada wao kwani hulipua moyo.

Ni lazima kiini cha tatizo hili kichunguzwe na tiba stahiki ipatikane. Kinyume cha hapo, janga hili linaweza kugeuka na kuwa dubwana kubwa la kutumaliza.
Matatizo ya nguvu za kiume huchangiwa na kuugua kwa muda mrefu, ugonjwa wa kisukari, kuvaa nguo za kubana sana, mionzi ya simu, kompyuta na mengineyo. Pia dawa za kuua wadudu huleta tatizo hili kwani zina viambata sumu viitwavyo ‘estrogen’, matatizo ya kisaikolojia, kupiga punyeto kwa muda mrefu na kutumia vyakula vyenye kemikali.

Utafiti unasema kuna uhusiano mkubwa sana kati ya upungufu wa nguvu za kiume na kuwa na sumu mwilini zinazotokana na vyakula vyenye kemikali tunavyobugia kwa kupenda au kutokupenda.



Kuna aina 9 ya vyakula ambavyo vimefanyiwa utafiti na kubaini kuwa ni moja ya vyakula vinavyosaidia kuongeza nguvu za kiume na havina madhara katika engezeko la nguvu za kiume, katika vyakula hivyo vyenye uwezo wa kuongeza nguvu za kiume kiasili ni:

1. TANGAWIZI

- Tangawizi ni moja ya chakula kinachoweza kurejesha nguvu za kiume, unaweza kuichemsha tangawizi na ukatumia kwa kuinywa kama chai Asubuhi, mchana na jioni pia Tangawizi unaweza ukaitumia katika mchanganyiko wa kiasili kwa kutumia habat soda,asali,kitunguu saumu na tangawizi yenyewe. 

JINSI YA KUTUMIA MCHANGANYIKO HUU: 

Chukua tangawizi na kitunguu saumu vitwange kisha vichanganye na asali pamoja na unga wa habat soda na uwe unakunywa mchanganyiko huu kwa kutumia kijiko cha chai kimoja kutwa mara 3 kwa muda wa wiki moja na utaona mabadiliko.

2. TIKITI MAJI:

Chakula kingine kinachosaidia katika upande wa kuongeza nguvu za kiume ni tunda la Tikiti Maji, unaweza ukachukua tikiti lako ukalikata na kutengeneza juice ya Tikiti kisha unakunywa ila sio lazima utengeneze Juice hata lenyewe tu unaweza ukalila. Ila jitahidi kutumia tunda hili hata kila siku kwani linasaidia sana kwa wenye matatizo ya nguvu za kiume.

3. UGALI WA DONA

Kula ugali wa dona kila siku. Ni mhimu kuachana na mazoea ya kula ugali wa sembe. Ugali wa dona una virutubisho vingi na mhimu kwa ajili ya afya ya mwanaume. Kama ugali wa dona unakukera jaribu kufanya hivi, chukuwa mahindi kilo 10 ongeza ngano kilo 3 na usage kwa pamoja, ugali wake huwa ni mlaini, mzuri na mtamu na unaweza kula na mboga yoyote tofauti na lile dona la mahindi peke yake. 

4. CHUMVI YA MAWE

Chumvi ya mawe ya baharini ile ambayo haijasafishwa au haijapita kiwandani ina mchango mkubwa sana katika kutibu tatizo hili. Tumia chumvi hii kwenye vyakula vyako kila siku.


5. MAJI YA KUNYWA

Kunywa maji ya kutosha kila siku bila kusubiri kiu. Kila mtu anahitaji glasi 8 mpaka 10 za maji kila siku. Maji ni mhimu katika kuongeza damu, kusafisha mwili na kuondoa sumu mwilini.

6. MBEGU ZA MABOGA

Ziloweke katika maji yenye chumvi, zikaushe. Zikaange kidogo bila kuziunguza. Tafuna mbegu 100 kutwa mara 3 kwa muda wa mwezi mmoja. Mbegu hizi sifa yake kubwa ni kuongeza wingi wa mbegu za kiume (manii), kama unatatizo la kuwa unatoa manii machache (low sperm count) basi hii ni mhimu sana kwako. Sasa, hizi usizitumie tu kama dawa, zitumie kama chakula na hivyo ziwepo tu nyumbani muda wote na kila siku uzitafune iwe unaumwa au hauumwi.

7. ASALI NA MDALASINI

Chukuwa lita moja ya asali safi ya asili ambayo haijachakachuliwa, ongeza vijiko vikubwa 4 vya mdalasini ya unga changanya vizuri pamoja. Lamba kijiko kimoja kikubwa cha chakula kila unapoenda kulala. Fanya hivi kwa mwezi mmoja.

Hata baada ya mwezi mmoja kuisha bado nakushauri uendelee kuitumia asali hivi maisha yako yote au hakikisha haipiti siku bila kunywa au kula chakula chenye asali ndani yake. Unaweza kuitumia asali kila siku kwenye mkate kama mdabala wa siagi au blueband au ukaitumia kwenye juisi na kwenye chai kama mbadala wa sukari.


8. CHAI YA TANGAWIZI

Tangawizi ni chakula ambacho husisimua sana mfumo wa mzunguko wa damu mwilini, na tangawizi zinajulikana sana kwa kusukuma damu kwenda sehemu za viungo vya uzazi yaani uke na uume. Inaweza kuliwa mbichi, au kupikwa au kuanikwa na kuwa kama unga.

Ulaji wa tangawizi mbichi nusu saa kabla ya tendo la ndoa husaidia katika kuongeza hamu na nguvu ya tendo la ndoa. Unaweza ukanywa chai ya tangawizi tu nusu saa kabla ya kuanza tendo au unaweza ukatafuna kipande cha tangawizi mbichi kwa ukubwa wa dole gumba la mtu mzima nusu saa kabla ya tendo.

Kunywa chai ya tangawizi mbichi kila siku, katika chai hiyo unayopika ndani yake weka tu maji na Tangawizi mbichi uliyosagia ndani yake (usiongeze majani ya chai humo), kumbuka tangawizi inaoshwa tu na maji na uisagie ndani ya sufuria pamoja na ganda lake la nje. Sasa badala ya kutumia sukari wewe tumia asali kwenye hii chai yako ya tangawizi na ukiitumia hivi kila siku hutachelewa kuona faida zake. Tangawizi peke yake ni dawa ya zaidi ya magonjwa 72 mwilini!

9. UNGA WA UDISHE

Unga wa mti wa udishe ni mzuri sana katika kutibu tatizo la nguvu za kiume na pia unasaidia sana kwa wanaume wenye tatizo la nguvu za kiume lililosababishwa na kujichua au kupiga punyeto kwani huimarisha sana mishipa ya uume. Udishe inapatikana pia katika mfumo wa juisi. Pia unaweza kuutumia hata kama unasumbuliwa na tatizo la kisukari pia unao uwezo mkubwa katika kuongeza hamu ya tendo la ndoa hata kwa kina mama.

Udishe pia unatibu magonjwa yafuatayo bila shida yoyote; Pumu, Chango la uzazi, Kupooza mwili, Unaondoa kabisa gesi tumboni na Kuongeza nuru ya macho kuona.
Udishe unao uwezo pia wa kuongeza ukubwa wa uume wako. Labda utauliza kwa namna gani?, kwa sababu moja ya kazi zake mwilini ni kuponya mwili uliokuwa umepooza, mwili unapokuwa umepooza ina maana hata damu yako pia inakuwa haitiririki vizuri kama inavyotakiwa na tuliona hapo juu kwenye somo hili umhimu wa mzunguko wa damu ulio bora katika nguzu za kiume.
Kwa kuwa mwili ulikuwa umepooza, udishe unapokuja kukutibu inakufanya kuwa mtu uliyechangamka na damu yako itaanza kuwa inatiririka kwa mtiririko mzuri zaidi na kama matokeo yake utaanza kuona hata ukubwa wa mheshimiwa unaanza kuongezeka kidogo kidogo. Na hii ni hasa kwa wale ambao walizaliwa na uume wa kawaida lakini sababu ya punyeto, lishe duni au stress walijikuta maumbile yao yanaanza kusinyaa au kupungua badala ya kuongezeka.

Na iwapo utatumia juisi ya udishe basi vitu vingine vyote hapo huhitaji kuvitumia isipokuwa ugali wa dona ambao ni lazima kila mwanaume ale na siyo ugali wa sembe ambao hauna thamani yoyote mwilini.


SERIKALI Yakwama Upelelezi kesi ya Wema Sepetu

$
0
0
Leo April 12, Msanii Wema Sepetu alifika katika Mahakama ya Hakimu mkazi Kisutu Jijini Dar es salaam kusikiliza kesi ya tuhuma za kutumia na kukutwa na Dawa za kulevya, ambapo UPANDE wa Jamhuri umeshindwa kukamilisha upelelezi dhidi ya kesi inayomkabili msanii huyo.

Upande wa Mashtaka uliowakilishwa na wakili wa Serikali Constantine Kakula, ulidai kuwa kesi hiyo imefika kwa ajili ya kutajwa lakini upelelezi haujakamilika hivyo ipangiwe siku nyingine.

Hakimu  Mkazi Mkuu Thomas Simba, ameuhoji upande wa Jamhuri, kutokana na kuchelewesha upelelezi wa kesi hiyo ambapo kila tarehe inayotajwa Serikali inadai kuwa upelelezi haujakamilika.

Kesi hiyo imeahirishwa na itatajwa tena tarehe 2 mwezi Mei mwaka huu.

TUCTA Yajipanga Kuipeleka Serikali Mahakamani

$
0
0
Shirikisho la vyama vya wafanyakazi (Tucta) limeitaka serikali kusitisha makato ya asilimia 15 kama malipo ya mkopo wa elimu ya juu na kurudi kiwango cha awali cha asilimia nane kinyume na hapo wataipeleka mahakamani.

Rais wa Tucta, Tumaini Nyamhokya alisema Baraza kuu la shirikisho hilo limesharidhia uamuzi huo na tayari lipo kwa wanasheria.

"Wanasheria wetu wanalifanyia kazi na kuendelea kukusanya nyaraka zitakazotusaidia,muda wowote kuanzia wiki Idaho tutalifikisha suala hili mahakamani," alisema

Alisema ameendelea kupata malalamiko mengi kutoka kwa wafanyakazi kutokana na makato hayo ikilinganishwa na hali ngumu ya maisha ilivyo sasa.

Rais Magufuli Aelezea Neema za Treni ya Kisasa..!!!

$
0
0

Leo Jumatano Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt John Magufuli amefunguka kwa kuelezea vitu vingi zaidi katika reli mpya ambayo itatumika kupita treni za umeme ambapo awamu ya kwanza itaanza Dar es Salaam mpaka Morogoro.

Katika awamu hiyo ya kwanza reli hiyo inayotarajiwa kukamilika baada ya miezi 30 na itakuwa na urefu wa kilomita 300 ambapo kutakuwa na station sita huku treni ikitarajiwa kutumia muda wa masaa 2 na dakika 15.

Rais Magufuli amesema reli hiyo itakuwa na awamu tatu ambapo itakuwa na urefu wa kilomita 1219 ikiwemo Dar es Salaam hadi Morogoro (Km 300), awamu ya pili ni Morogoro mpaka Makotopola (km 336) itagharimu kiasi cha dola milioni 1.22 ambayo ni sawa na shilingi trilioni 2.8 kwa fedha za Tanzania.

Ameendelea kuwa tayari serikali imeshalipa kiasi cha shilingi bilioni 300 wiki iliyopita ambapo bajeti yake ilitengwa tangu mwezi Julai mwaka jana.

Ameongeza kuwa treni hizo zitakazokuwa na spidi ya 160 zitapita kwenye reli hiyo na zitakuwa na uwezo wa kubeba tani 10,000 (sawa na malori 500 yenye uwezo wa kubeba tani 20 kila moja). Ajira takribani milioni moja zinatarajiwa kupatikana kupitia reli hiyo.

Dkt Magufuli amesisitiza kwa kusema baada ya nchi ya Uturuki kuona katika awamu ya kwanza Tanzania imegharamia ujenzi huo wa reli kwa fedha zake binafsi, imeamua kutoa mkopo wa nafuu kupitia mabenki yake matano katika ujenzi wa reli utakaoanzia Morogoro hadi Makotopola ambapo serikali itaanza nayo mazungumzo. Nayo benki ya dunia imetoa kiasi cha shilingi bilioni 300 kukarabati reli ya zamani ili iendelee kutumika vizuri.

Lema: Jina Langu ni Miongoni Mwa Wanaotaka Kutekwa, Watekaji Hawataona Kaburi Wala Mauti Yangu...!!!

$
0
0

Mbunge wa Jimbo la Arusha Mjini Godbless Lema amesema jina lake ni miongoni mwa wabunge wanaokata kutekwa, aonya watekaji kuwa hawataona kaburi wala mauti yake. 

Ile Kesi ya Gwajima ya Kumtukana Askofu Pengo..Leo Jaji Amechukua Maamuzi Haya Mazito..!!!

$
0
0

Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu imeifuta   kesi ya kutoa lugha chafu inayomkabili Askofu wa Kanisa la Ufufuo na Uzima Josephat Gwajima.

Hakimu Mfawidhi, Cyprian Mkeha aliifuta kesi hiyo leo chini ya kifungu cha 225 cha sheria ya Mwenendo wa Makosa ya  jinai (CPA).

Kesi hiyo imefutwa baada ya Wakili wa Serikali, Joseph Maugo kueleza kuwa hawakuwa na shaidi na kuomba wapewe ahirisho.

Katika uendeshwaji wa kesi hiyo upande wa mashtaka uliita ushahidi mmoja kwa miezi 14.

Katika kesi hii, Gwajima anadaiwa kuwa  kati ya Machi 16 na 25,2015 Tanganyika Packers Kawe alitumia lugha chafu na kumdhihaki  Muhadhama wa Kanisa Katoliki  Askofu Kardinal Polcarp Pengo.

Rasmi..Diamond Kufanya Kolabo Mpya na Chris Brown..Hivi Ndivyo Alivyothibitisha ..!!!

$
0
0

Diamond Platnumz yupo nchini Afrika Kusini ambapo pamoja na mambo mengine, inaonesha ameenda kushoot video ya collabo yake nyingine na staa wa muziki wa R&B na house nchini humo, Donald.

Hii inakuwa mara ya pili wakali hao wanafanya wimbo pamoja. Mwaka 2015 wawili hao waliachia wimbo uitwao Wangu.

Wote wameweka clip ya video Instagram wakielezea kukutana kwao kwa mara nyingine tena.

“Always nice meeting my south African brother @donaldindenial …..!” ameandika Diamond.

Naye Donald ameandika: The Pride of African Music @diamondplatnumz.”

Wakati huo huo, huenda Diamond akawa anatupa habari kimafumbo kuwa kuna uwezekano wa kumweka Chris Brown kwenye mipango yake ya collabo za baadaye. Akiweka picha ya staa huyo, Diamond ameandika: Nifunge bakuli langu….nikojoe nikalale, Mie bado Mudogo sana…..


Manara Awajibu Yanga Baada ya Kupinga Malalamiko ya Simba kwa Mchezaji wa Kagera Sugar..!!!

$
0
0

Baada ya kamati tendaji ya Yanga kupitia kwa mjumbe wake Salum Mkemi kutanganza kupinga malalamiko ya Simba dhidi ya Kagera Sugar kwa kumtumia mchezaji wao Mohamed Fakih kwenye mechi kati ya Kagera Sugar dhidi ya Simba, afisa habari wa Simba Haji Manara ametoa taarifa rasmi akiwataka Yanga kutulia.

Kuna taarifa iliyotolewa na klabu ya Yanga inayoonyesha kuishinikiza Bodi ya ligi kutokutenda haki juu ya rufani yetu dhidi ya klabu ya Kagera Sugar kwa kumchezesha mchezaji Mohammed Fakih aliyecheza dhidi yetu akiwa na kadi tatu za njano ambalo ni kosa kisheria.

Taarifa hiyo ya Yanga iliomnukuu Mjumbe wa kamati ya utendaji ya klabu hiyo Salum Mkemi aliyeoongea mbele ya waandishi huku akiwa na katibu mkuu wa klabu hiyo Charles Boniface Mkwasa iliitaka bodi kutokutoa points kwa Simba eti kwa kuwa hizo points zitawaathiri Yanga kwenye kutetea ubingwa wao ambao kwa sasa upo rehani, pia taarifa hiyo imeonyesha Yanga wanao ushahidi kuwa Fakih ana kadi mbili za njano.

Klabu ya Simba inawaambia viongozi wa Yanga wanayo mambo ya msingi ya kuwashughulisha, ikiwepo kutafuta mishahara ya wachezaji wao iliokwama kwa miezi kadhaa kama inavyoripotiwa mitandaoni na kwenye vyombo vya habari,pia waangalie namna bora ya kuurejeshea hadhi uwanja wake wa mazoezi wa Kaunda ili upate kuchezeka tena na sio ulivyo hivi sasa,ambapo umegeuka kama bwawa la kufugia kambale,,ni kushangazwa kulikochupa mpaka kufuatilia rufani isiyowahusu,Hii ni rufani ya Simba dhidi ya Kagera sio wao Yanga.

Tunaamini bodi haitafanya maamuzi kwa shinikizo la yoyote yule,na hatutarajii kuona porojo walizozisema leo zitaondoa ukweli uliopo mezani kwao ambao klabu yetu imeuwasilisha

Mwisho niwaombe washabiki wetu watulie na waiachie bodi ifanye maamuzi yake ambayo tunaamini yatatoa haki kwa anayestahili.
IMETOLEWA NA.. Haji S Manara
Mkuu wa Habari wa Simba Sc
SIMBA NGUVU MOJA

Huu Ndio Utamu wa Mwanamke Mwenye Mswambwanda wa Maana Wakati wa Kukwichikwichi Kitandani..!!!

$
0
0
0
1.Makalio makubwa hunisaidia kujua kama mwenzi wangu amefika orgasm, mfano ikitokeana hit Doggie basi wakati wa orgasm (most of girls) makalio huwayanatikikisa (twitch, fasciculate ) ambayo huwa inaambatanana miguno ya kimhaba inayo fifia ambayo kabla ya hapo huwa ya sautikubwa... hii unifanya nijue what to next kumzidishia utamu zaidi. Hii kitu inukuwa ngumu kunotice kwa msichana ambaye nimwembamba just have to relay from other signs

2. Makalio makubwa huwa yananifanifanya iwe rahisi kwangu kuyashika (grab) especially wakati wa doggie.ikizingatia gym imekubali na kifua na mabega yametanuka ( shoulder to shouler distance ni kubwa). itaniwia ngumu sana kama msichana an mwili mdogo na makalio yake pia

3. msichana mwenye makalio makubwa obvious atakuwa na nyama nyama kwenye mapaja hii nyama nyama zinakuwa na act kama chock absober na kucushion ile hiting force ,especially when adrenaline na sympathetic flow is at peak and s3x is becoming hardcore, katika situation hiii , kimbau mbau anaweza teguka nyonga. if ur not doing that smoothly.

4. Makalio makubwa yana yanasaidia kutengeneza ile NUMBER 8 ya mwili, mfano ukutane na msichana makalio makubwa na ni mtu wa mazoezi hana na mikunjo ya kunenepa mgongoni na tumboni , and ur hitting doggie, ukitazama her PERFECTARCH from the behind to the the dorsal neck yaani ni full Hamasa.

Kwa kumalizia siwabagui na kuwanyanyapaa wasichana wembamba, kwani kwenye haya mambo siku zote ni combination ya vitu vingi. Wembamba nao wana vitu adimu.. Its just me from what i  have been experiencing....

(+18) ..Hatua kwa Hatua Jifunze Hapa Jinsi ya Kunyonya Uke wa Mpenzi Wako Hadi Akalegea Kabla ya Kuanza Sexy..!!!

$
0
0

Kwanza unatakiwa utambue kuwa baadhi ya wanawake hawako huru kukuachia wewe mwanaume ukodolee macho kwenye uke wake hivyo kama unataka kunyonya uke wa mpenzi wako kwanza kabisa unapaswa kuhakikisha kuwa unamuandaa kwa kusifia uke wake, harufu asilia ya uke wake n.k. Mhakikishie kuwa hakuna kitu kinakufurahisha na kukupa raha kama kuangalia mandharii ya uke wake, mwambie vipi unapenda anyoe nywele zake za huko (mnyoe ukiweza) n.k.

Baada ya kulambana na kukumbatiana anza kwa kubusu na kulamba taratibu sehemu ya kiunoni kuelekea chini, hamia ndani ya mapaja, halafu rudi juu kwenye eneo zima la uke lakini sio mashavuni. 

Ukiona ana-relax au kushika kichwa taratibu endelea ukiona anajibana-bana acha kwani hatokuwa tayari. Jaribu siku nyingine na ongeza zoezi la kusifia mapenzi yako juu ya uke wake).

Baada yakutembelea eneo zima la uke wake huku yeye anajiachia na kujisogeza taratibu au kutoa miguno fulani, hamia taratibu kwenye mashavu na upitishe ulimi wako kuzunguuka hilo eneo, wakati huo kisimi kitakuwa kinaanza kuinuka (sio wote wanawake wote wako hivyo). Ukiona hali hiyo ujue huo ndio wakati muafaka kabisa wa kukinyonya na kuachia mara 3 kwa kutumia midomo yako (lips) na ulimi (kama unanyonya kitu kitamu kidoleni lakini sio kufyonza).

Baada ya hapo sasa ndio unaanza kulamba kisimi kwa kufuata mitindo ifuatayo;

Mzunguko

Kwa kutumia ncha ya ulimi lamba kisimi kwa kukizunguuka kwa muda kisha kinyonye na kuachia alafu endelea na mzunguuko, ongeza kasi kutokana na mpenzi wako anavyo itikia au kufurahia utamu.

Ikiwa utachoka basi unaweza kuupumzisha ulimi wako kwa kulamba eneo na pembe zote za uke kama aiskrimu, halafu rudia kukilamba kisimi kama mwanzo.

Umbo namba 8

Fanya kama nilivyoeleza hapo awali ila unapofika kisimini badala ya kuzunguuka chora namba nane kwenye kisimi kwa kubadilisha mfano unaanza na kulia halafu baadae unaanza na kushoto.

Pembe kwa pembe

Fanya kama nilivyosema mwanzo kabisa lakini unapofika kwenye kisimi unatakiwa kukilamba kwa kutumia ncha ya ulimi wako kama vile unapiga vigeregere ila sio kwa speed ya kigeregere.

Usisahau kukinyonya kisimi kwa kutumia lips na ulimi kwenye kila mtindo ili kupumzika na wakati huohuo kutopoteza utamu unaompatia huyo unaemnyonya.

Mbinu ya Kuzuia Kufika Kilele Mapema kwa Wanaume Tu..!!!

$
0
0

Sababu ya tatizo hili huweza kuwa ya Kibaiolojia na Kiakili. Kama wewe
pia ni moja yao na unapenda kujua jinsi ya zuia hali hii

Jenga tabia ya kufanya mazoezi ya mwili: Mwili wenye afya nzuri daima hufanya kazi vizuri, kwahiyo kitu rahisi cha kufanya ni kujenga tabia ya kufanya mazoezi ambayo husaidia kukujengea afya njema na kukupa mzunguko mzuri wa damu. Kama una mwili wenye afya basi inaweza kukusaidia kwa namna ya kifikra ambazo huchangia kwenye swala zima la kuwahi kupizi. Hii hutokana na hutokana na kuongeza kujiamini na kujihusudu.

Pumua vizuri na kikamilifu: Kiungo chochote cha mwili huhitaji nguvu kamili ili kufanya kazi na ndivyo ilivyo kwa habari ya viungo vya uzazi! Unapo pumua vizuri na kwa ukamilifu, kiungo hiki hupata nguvu za ziada. Mbinu mbalimbali za kupumua kama pranayama hujajwa kusaidia sana kujifunza jinsi ya kuzuia kupizi mapema. Baada ya kuinza tu (wakati wa tendo), jaribu kupumua kwa ufasaha ili mwili uweze kupata hisia kabla ya kuanza kufanya msuguano.

Mshirikishe mwenzako kikamilifu: Kuridhika kimapenzi ni tukio ambalo wote wawili mnaridhika kikamilifu. Ili kujifunza kujizuia kukojoa haraka, ni vizuri kuwasiliana na mwenzi wako wa kimapenzi. Anaweza akakusaidia kushinda tatizo hili la kiaibu, kila unapohisi unataka kukojoa mapema, sema 'ngoja' na usitishe kwanza shughuli zote kwa muda kidogo.

Pia kabla ya kwenda kuanza tendo kwa mfano upo ofisini na unajua jioni unakwenda kugegeda basi jitahidi usiwaze hayo mambo chukulia kama ni kitu cha kawaida. Hii ni kwasababu kuongeza concentration ya kuwaza ngono inaongeza stimulation kiasi kwamba ukiomgusa mpenzi wako tayari umekwishaachia hata kabla ya kuingiza


Pia angalia angalia style zenye kuchochea kukojoa haraka kwa mfano mbuzi kagoma.... etc hii ni ngumu kujizuia kukojoa hasa kwa bao la kwanza maana panakuwepo na constriction ya hali ya juu very tighten kiasi kwamba ukigusa tu tayari ..so ni vizuri style kama hizi zikafuata baada ya bao la kwanza ili uweze ku-enjoy vizuri zaidi.


Fanya mazoezi ya kukojoa na kubana mkojo mara kwa mara... hii ina maana kuwa unapokojoa mkojo unaachia then unakatiza unaendelea tena alafu unakatiza tena . Fanya mara tatu kila unapokwenda kukojoa. Hii ni muhimu kwa ajili ya kuongeza strength ya misuli ya **** na kupunguza relaxation yake ... njia hii imewasaidia wengi na wamepona kabisa

Mambo Ya Msingi Unapotongoza Mwanamke Katika Kikundi..!!!

$
0
0

Kutongoza ni sanaa ambayo inahitaji mmoja kufanya mazoezi ya mara kwa mara ili aweze kuwa na ustadi ambao unaweza kumnufaisha au kumsaidia mhusika wakati ambapo anakabiliwa na tatizo la kumshawishi mwanamke. Ijapokuwa kuzijua sanaa hizi dhidi ya wanawake haitaonekana kuwa na ustaarabu katika jamii, kila mwanaume ana haki ya kuzijua na kutambua mbinu hizi.

Kitu cha kwanza ambacho unapaswa kujua ni kuwa kutongoza si matumizi ya mistari na miondoko ya mwili pekee bali pia ni subira. Kutongoza mwanamke kutachukua muda mwingi kutoka kwako hivyo unahitajika kuwa na imani. Kwa mfano kabla ya kuchukua hatua ya kuapproach mwanamke lazima upime manufaa na hasara ambazo zitakuja iwapo utaamua kutangamana na mwanamke ambae unakusudia kuwa naye.

Ikija swala la kumtongoza mwanamke katika kikundi cha watu, haya hapa ni baadhi ya mambo ambayo unapaswa kuwa nayo wakati unapokabiliana na windo lako.

#1 Kumsifia
Kama umetoka out hadi kwa klabu na marafiki zako halafu ukamwona mwanamke unayemtamani akiwa katika kikundi, muapproach na umuagizie kinywaji na uwe mkweli na mhakika wakati unapomsifia kuhusu umbo lake na nguo alizovalia. Weka katika akili yako kuwa mwanamke anapenda kusifiwa kwa nguo alizovaa, hairstyle yake, macho yake, ucheshi wake na pia marashi aliyoyapaka. Pia, hakikisha kuwa unaspend muda mwingi zaidi hata kama klabu inaenda kufungwa. Kama umeongea na mwanamke huyu usiku huo, hakikisha kuwa unamwambia kuwa umependezwa na kuspend muda na yeye.

#2 Jiamini
Confidence ni nguzo ya kila mwanaume ambayo anapaswa kuwa nayo wakati wowote ule. Mwanaume anayejiamini anatambulika haraka na wanawake. Hivyo lazima uwe na confidence wakati unapotangamana na wanawake. Hii inamaanisha kuwa lazima uonyeshe confidence mbele ya umati na pia uonyeshe kuwa una interest na yeye hata kama umezungukwa na watu. Confidence ni lazima kama unataka kumtongoza mwanamke. Usifikirie sana kuhusu jinsi utakavyompendeza kwa sasa lakini. Kwa kujionyesha wewe mwenyewe bila kujifanya mtu mwingine kutakusaidia zaidi kuliko kuwa muigo wa mtu mwingine ili uonekane mzuri.

#3 Kujieleza
Wakati unapomtongoza mwanamke katika umati, ni bora zaidi kuweka toni ya sauti yako chini na ambayo itavutia kadri uwezavyo. Hii haimaanishi kuwa unapaswa kumnong’onezea, la. Kile unachopaswa ni kuweka wazi sauti yako aisikie vizuri na mara kwa mara umuonyeshe tabasamu ambalo utalichanganya na mvutio wa macho yako. Pia wakati unapoongea onyesha ujuba na maneno unayoyatamka. Hii itamfanya akuone kuwa wewe una interest kwake na unataka kuendeleza aproach yako zaidi.

Wakati utakapokuwa umeuchukua muda wako kuongea na mwanamke na kumuonyesha kuwa uko interested na yeye, jaribu kutafuta ishara ambazo zinaonyesha kuwa pia yeye amevutiwa ama anahisi kama vile unahisi wewe. Ishara hizi utaziangalia kupitia miondoko ya mwili wake. Je anapinda mwili wake upande wako? Je kifua chake amekienua ili uone ukubwa wa matiti yake? Je anacheka mizaha yako hata kama haichekeshi? Kama umeona kuwa amevutiwa na wewe kupitia ishara hizi, basi rudi nyuma na umngojee yeye aanze kuchukua hatua. Hii ni njia hakika ya kumfanya amaintain interest na wewe.

Lifahamu Tatizo la Kukosa Usingizi na Jinsi la Kulitatua Haraka..!!!

$
0
0

tafiti zinaonyesha kwamba asilimia 9 mpaka 15 ya binadamu duniani wanasumbuliwa na matatizo ya kukosa usingizi, tatizo hili ni moja ya matatizo mabaya sana ambayo huweza kumfanya mtu ashindwe kutambua anaishi ulimwengu wa aina gani kwani muda mwingi anakua ni mchovu na hawezi kufanya kitu chochote kwa umakini.

ugonjwa wa kukosa usingizi huwasumbua zaidi watu wazima kwanzia miaka 40 kwenda mbele hasa wanawake kuliko wanaume japokua unaweza pia kuwashambulia vijana wadogo kulingana na matatizo mbalimbali lakini watu wazima sana ndio waathirika wakuu wa shida hii.

kuna aina tatu za matatizo ya kukosa usingizi

kukosa usingizi kunaweza kuja kwa aina tatu yaani kukosa usingizi ghafla, kukosa usingizi mara moja moja au kukosa usingizi kwa muda mrefu sana.

hali hii ya kukosa usingizi husababisha matatizo mbalimbali kama kunenepa,kupoteza kumbukumbu, kushindwa kufaulu darasani, kushindwa kua makini na kazi, kuchoka sana,wasiwasi, mgandamizo wa mawazo, na hatari ya kupata magonjwa yasiyotibika kama ugonjwa wa presha na kisukari.

nini husababisha kukosa usingizi?

watu sababu mbalimbali huweza kukosa usingizi kama ifuatavyo

mabadiliko ya mfumo wa maisha; hii inaweza kusababishwa na kazi unayofanya kama kuanza kufanya kazi usiku...kazi za ulinzi, kazi za uuguzi, na kadhalika lakini pia kuishi sehemu yenye kelele sana,kusoma sana usiku, baridi sana au joto sana.

matatizo ya kisaikolojia; watu wenye msongo wa mawazo unaosababishwa na matatizo mbalimbali kama kukosa ajira, matatizo ya kiuchumi, kuvunjika kwa mahusiano, magonjwa ya akili, kua na wasiwasi sana wa mambo yanayokuja, wasiwasi wa kuibiwa mali zako ukiwa ndani umelala hasa wamiliki wa magari na mali zinazolala nje.

magonjwa mbalimbali; kuugua magonjwa fulani fulani huweza kumfanya muhusika kukosa usingizi kabisa wakati wa kulala mfano pumu au asthma, magonjwa ya moyo, maumivu makali ya sehumu ya mwili,kiharusi, madonda ya tumbo, maumivu ya jino, na kansa mbalimbali.

mabadiliko ya kiwango cha homoni; hii hutokea wakati wa kipindi cha hedhi ambapo kunakua na mabadiliko madogo ya homoni za uzazi, kipindi cha ujauzito na ugonjwa wowote unaobadilisha kiwango hicho.

teknolojia; kulala na simu na kuendelea kuchati, tv au komputa chumba cha kulala,michezo ya gemu na kadhalika..hii imeathiri sana watu wengi kwani siku hizi kabla ya kulala utamkuta kila mtu anachezea simu angalau saa moja.

dawa mbalimbali; kuna dawa nyingi sana ambazo zimetajwa kunyima watu usingizi kama ifuatavyo
dawa za presha mfano propanolol,metoprol,losartan,atenolol,metoprol, captopril,enapril na solatol,lisinopril

dawa za msongo wa mawazo mfano fluoxetine na paroxetine

dawa za kushusha kiwango cha lehemu mwilini mfano simvastatin,rosuvastatin,lovastatin.

dawa za kupunguza maumivu ya mifupa mfano chrondotin na glucosamine

dawa za kutibu aleji mfano cetrizine

sababu zingine mfano kulala sehemu yenye kelele nyingi, kulala na mtu anayekoroma usiku, kulala sehemu yenye wadudu kama mbu na chawa

watu gani hasa wanasumbuliwa na shida hii?


  • watu wanaosafiri sana
  • watu wanaofanya kazi za usiku
  • wazee sana
  • wanaotumia dawa mbalimbali
  • vijana wadogo ambao mahusiano na ajira ni tatizo kubwa kwao.
  • wanawake waliofika mwisho kuona siku zao za hatari
  • watu wenye magonjwa ya akili


dalili za kukosa usingizi ni kama ifuatavyo..


  • kushindwa kulala kabisa
  • kuamka usiku sana na kukosa usingizi
  • kuamka mapema sana kuliko kawaida
  • kusikia usingizi baada ya kuamka asubuhi
  • kuchoka sana mchana wakati wa kazi
  • mgandamizo wa mawazo na kua na wasiwasi sana
  • kukosa umakini wakati wa kazi
  • kupata ajari za wakati wa kutumia vyombo vya usafiri.
  • kuumwa kichwa sana
  • kuharisha, kichefuchefu na kukosa hamu ya chakula
  • kushindwa kuongeza na watu


vipimo vinavyofanyika

daktari humuuliza mgonjwa mbalimbali kuhusu tatizo lake la kukosa usingizi, vipimo mbalimbali pia huweza kuchukuliwa pia kutafuta magonjwa ambayo yanaweza kumkosesha mtu usingizi.
kwa mtu kugunduliwa na tatizo hili lazima awe amemaliza mwezi mmoja bila kupata usingizi unaoeleweka

vipimo vya kisasa zaidi kama polysmonography huweza kutumika kwa mgonjwa aliyelazwa kupima usingizi wake wakati wa usiku

matibabu;

mara nyingi matatizo ya kukosa usingizi hua yanaaisha pale chanzo cha tatizo kinapotibiwa kwa mgonjwa husika, hivyo mara nyingi matibabu yanalenga kuondoa chanzo cha tatizo hili.

matibbu yamegawanyika katika matibabu yasiyohusu dawa yaani non pharmacological treatment na matibabu yanayohusu dawa yaani pharmacological treatment kama ifuatavyo

matibabu yasiyohusu dawa[ non pharmacological treatment]

ongeza nidhamu ya usingizi; epuka kulala sana au kidogo sana, epuka kulala na njaa, epuka kunywa kahawa na kuvuta sigara wakati wa kulala, hakikisha ratiba yako ya kulala haibadiliki, hakikisha unalala kwenye mazingira rafiki ya usingizi yaani bila kelele au usumbufu wowote.

muone mtalaamu wa ushauri; unaweza kuonana na mshauri akakusaidia kutatua tatizo lako la kisaikolojia linalokusumbua, huduma hiyo tunatoa pia.

epuka vitu mambo ya teknolojia yanayozuia usingizi; tabia ya kua na tv chumba cha kulala, laptop kitandani au kutumia simu usiku kabla ya kulala huweza kukunyima usingizi.

epuka kulala mchana; tabia ya kulala mchana huweza kukunyima kabisa usingizi wakati wa usiku, hivyo kaa mbali kabisa na kitanda wakati wa mchana.

pata matibabu ya tatizo lolote la kiafya linalokusumbua; kama kuna ugonjwa wowote unakusumbua hakikisha unatibiwa, kama ni ugonjwa usiotibika basi hakikisha unafuata matibabu ya kupunguza makali yake.

pata suluhisho la tatizo la kisaikolojia;kama una msongo wa mawazo sababu ya kuachwa kwenye mahusiano huwezi kulala kabisa, kama una matatizo ya kiuchumi, umefiwa, au msongo wowote wa mawazo basi hakikisha unapata suluhisho lake.

matibabu ya dawa[pharmacological treatment]

wakati mwingine chanzo cha kukosa usingizi kinaweza kua nje ya uwezo wa muhusika yaani hawezi kutatua tatizo linalomsumbua hivyo anahitaji matibabu ya dawa ambazo angalau zitampa usingizi alale kama ifuatavyo :-

ant depressant; mfano fluoxetine na paroxetine ,anthistamine
ramelteon ,melatonin

Rais Magufuli Ampigia Simu MwanaFA na Kumwambia Anapenda Kazi Zake Hasa Wimbo wa Dume Suruali..!!!!!

$
0
0

Rais wa Tanzania Dkt John Pombe Magufuli, jana amempigia simu Msanii wa Muziki wa kufokafoka aka Hip Hop ndugu Hamis Mwinjuma aka MwanaFalsafa aka MwanaFA aka Binamu, na kusema yeye ni mpenzi wa kazi zake haswa Wimbo wake unaotamba anga za Miziki wa #DumeSuruali ambao alimshirikisha Vanessa Mdee. Moja ya ya Msitari anaoupenda ni "Utoe hela kwani ina TV ndani?"

"Nimefurahi kupokea simu ya Mheshimiwa Rais Magufuli kunisalimia na kuniambia yeye ni mpenzi wa kazi zangu,haswa #DumeSuruali" amesema MwanaFA kwenye Ukurasa wake wa Twitter

Kikosi Kilichomuua Osama Chajiadaa Kumwondoa Dikteta Kim Jong wa Korea kaskazini..!!!

$
0
0

Kikosi maalumu cha Kijeshi cha jeshi la Marekani kijulikanancho kama "Navy Seal Team Six" Kinadaiwa kujiandaa katika kumwondoa Kim Jong un wa Korea Kaskazini toka madarakani.
Navy Seal Team six ikishirikiana na wanajeshi wengine WATAALAAM wa vikosi vingine wamekuwa wakifanya Mazoezi kujitayarisha pindi watakapohitajika wakati wowote.

Kikosi hicho cha Navy Seal Team six ndicho kilichoweza kumuua Osama bin Laden baada ya kuingia nchini Pakistani usiku wa manane. Kikamuua yeye na walinzi wake na kuubeba mwili wake na kuutupa baharini.

habari kutoka gazeti la Australia na the Sun la Uingereza likinukuu habari za gazeti lingine la Korea Kusini Joog Ang newspaper likisema matayarisho ya kumwondoa Kim yako mbioni.

Hii inakuja wakati Marekani inafanya mazoezi makubwa ya WANAJESHI ZAIDI YA 17,000 wa ardhini
Angani
Maji 
na 
Nchi kavu 
pamoja na jeshi la Korea Kusini.
Maafisa wa serikali walipohojiwa walikanusha wakisema mazoezi hayo si ya kumwondoa Kim Jong Un.
Japokuwa well placeD sources zinasema mpango huo uko na waweza kutekelezwa wakati wowote ili kumzuia Dikteta huyo kumiliki zana hatari za Kinyukilia ambazo Marekani inadai Korea ya Kaskazini imo mbioni kutaka kuwa nazo.ili ziweze kuipiga Marekani. 

Nayo Marekani imesema haitairuhusu Korea ya Kaskazini kumiliki zana hizo. Ni juzi juzi tu wa kati rais Trump wa Marekani aliposema Anaweza kuchukuwa HATUA YEYE MWENYEWE bila msaada wa mtu mwingine.

Meya wa Jiji la Dar Amnanga Rais Magufuli..!!!

$
0
0

"Sijawahi Kupanda Lori,sio usafiri wangu kwa kuwa mimi sio mizigo".

" Dereva tuheshimiane"

mayor Jacob.

Daily Mail Kumlipa Melanie Trump $2.9m Kufuatia Kuandika Habari ya Kumchafua..!!!

$
0
0

Gazeti maarufu la Uingereza, The Daily Mail limemuomba radhi mke wa Rais wa Marekani, Donald Trump, Melania Trump na kukubali kumlipa fidia kumaliza kesi iliyofunguliwa baada ya kuandika habari ya uongo kuhusu kazi yake kama mlimbwende.

Trump atalipwa dola milioni 2.9 kama fidia kutokana na madhara yaliyotokea.

“We accept that these allegations about Mrs. Trump are not true and we retract and withdraw them. We apologize to Mrs. Trump for any distress that our publication caused her,” Daily Mail na Mail Online wamesema kwenye maelezo yao.

Trump alifungua kesi dhidi ya Mail Online September mwaka jana akiwatuhumu kuandika habari ya kumchafua. Kwenye mashtaka yake alitaka alipwe dola milioni 150.

The Daily Mail ni gazeti la udaku nchini Uingereza lakini website yake inasomwa sana Marekani.

Stamina: Treni ya Umeme Dar Mpaka Moro Ikikamilika,Narudi Kuishi Zangu Moro..!!

$
0
0

Leo April 12 Rais Dkt John Pombe Magufuli amezindua awamu ya kwanza ya ujenzi wa reli ambayo itakayorahisisha usafiri wa Dar es Salaam hadi Morogoro kwa njia ya treni.

Inawezekana mtu akawa anaishi Morogoro na kufanya kazi zake Da es Salaam kwani usafiri utakuwa wa uhakika na haraka zaidi. Rapper Stamina ambaye ni mzaliwa na Morogoro anayefanya mishe zake Dar, amehaidi kurudi kuishi Moro na wakati huo huo akiendelea kufanya mishe zake Dar endapo njia hiyo ya usafiri itaanza kufanya kazi.

“Ikikamilika hiyo Rais, naenda kuishi zangu Morogoro tu,” ameahidi Stamina wakati akipiga story na Prince Ramalove kupitia Kings Fm Leo.

Harmorapa Afunguka Kuhusu Utajiri Alionao na Suala la Yeye Kumiliki Bastola..!!!

$
0
0

Harmorapa amefunguka kuhusu kumiliki bastola yake binafsi.Rapper huyo machachari ambaye kila kukicha huteka vichwa vya habari kutokana na vituko vyake, amekiambia kipindi cha Dj Show cha Radio One,japo ana mali nyingi kwa sasa lakini hafikirii kuwa na bastola kwakuwa ana ulinzi wa kutosha.

“Sasa hivi nina pesa nyingi, nina gari nini. Lakini sijawaza au kufikiri siku nije kumiliki bastola kwa sababu eti nina pesa sijawaza kwa muda huu ila sijajua huko mbeleni iatkuwaje,” amesema Harmo.

“Nikisema kwaajili ya kujilinda unajua sasa hivi mimi nina bodyguard wangu ameshiba na ameenda hewani. Hata ninapokaa kwenyewe nina ulinzi mpaka umfikie Harmorapa kuna kazi kubwa sana na unaweza usionane naye,” ameongeza.

Nape Noma Sana..Afanya Tukio la Karne Jimboni Mwake..Awaswalisha Waislamu Kanisani...!!!

$
0
0

Katika hali isiyo ya kawaida,wananchi wa Kijiji cha Majengo, kilichopo kwenye Jimbo la Mtama, mkoani Lindi ambao ni Waislamu, wiki iliyopita waliangusha dua ndani ya Kanisa Katoliki Parokia ya Nyangao, ili kumtakia afya njema Mbunge wao, Nape Nnauye katika kazi zake za ubunge.

Nape, akiwa ameambatana na baadhi ya waigizaji wa filamu na wachekeshaji, alikuwa amekwenda jimboni kwake Mtama, kuzungumza na wapiga kura wake, ikiwa ni mara ya kwanza tangu nafasi yake ya Uwaziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo itenguliwe na Rais Dk. John Pombe Magufuli, mwezi uliopita.

Ndani ya kanisa hilo, ambamo pia walikuwepo waumini wa Kikristo, bila kujali tofauti zao, Waislamu hao walisoma dua kwa ajili ya kumtia nguvu ya kuwatumikia wananchi wake na kumtaka kutokata tamaa katika utendaji wa kazi zake za kibunge, kwani kilichotokea ni kitu cha kawaida kwa wanasiasa. Katika tukio hilo, pia wakristo nao walifanya ibada ya kumuombea mbunge huyo.

Nape alisema aliamua kuwakutanisha pamoja waumini wa dini hizo ili kuonyesha umoja na mshikamano miongoni mwa wapiga kura wake.

Kabla ya tukio hilo la aina yake lilijiri  Jumapili iliyopita, Jumamosi yake, katika Kijiji cha Kiwalala, wasanii walioambatana na kiongozi huyo, Steven Mengere ‘Steve Nyerere,’ Mike Sangu, Chopa Mchopanga, Blandina Chagula ‘Johari’, Mark Reagan na wengineo, walipanda jukwaani kuonesha kumuunga mkono kiongozi huyo kijana mwenye historia ya upambanaji ndani ya Chama Cha Mapinduzi (CCM). Steve akiwa jukwaani aliwapandisha wasanii wenzake ambao baada ya kuwasalimia wananchi, walimuelezea mbunge huyo kuwa mtu muhimu katika chama na serikali.

Wasanii hao walielezea jinsi Nape alivyohangaika kwa hali na mali usiku na mchana ili kuhakikisha CCM inabaki madarakani na kusema wakati huo wengine wanaotamba sasa walikuwa hawajulikani walipo.

Wakati wasanii hao wakisema hayo umati uliofurika kwenye mkutano huo ulilipuka kwa mayowe ya furaha na kuchagiza;

“Ndiyooo… ndiyooo…. Kweli kabisaaa”.

Mapokezi makubwa aliyopata mbunge huyo, alijikuta akitoa machozi ya kutoamini alichokiona, hasa baada ya kinamama  wa  kijiji cha Kiwalala  kulala chini na kumruhusu kutembea kwa kuwakanyaga migongoni
Viewing all 104709 articles
Browse latest View live


Latest Images