Quantcast
Channel: UDAKU SPECIAL
Viewing all 104698 articles
Browse latest View live

Kimenukaa..Master Jay na P Funk Waingia Katika Bifu Zito Kuhusu Harmorapa..P Funk Amtaka Master Jay Achunge Mdomo Wake..!!!

$
0
0

Mtayarishaji mkongwe wa muziki nchini P Funk Majani amemuonya mkongwe mwenzake katika game, Master J kutomsema vibaya kwa kumsapoti msanii Harmorapa kwa madai kuwa msanii huyo hana kipaji.

P Funk pia amemkumbusha Master J jambo na kumwambia kuwa hata alipoanza kumtengeneza Juma Nature majungu na maneno yalikuwa mengi lakini alitusua na kuwa msanii mkubwa nchini.

Akiongea na eNewz ya EATV, Majani amesema kuwa yeye kama Meneja wa Harmorapa ndiye anajua ni silaha za aina gani amezitengeneza na tayari ameshamtengeneza msanii huyo kwa ajili ya mashambulizi ya kufanya vyema katika soko la muziki hivyo mtu wa nje kama kina Master J wasimuungilie.

"Unajua nilipoanza kumtoa Juma Nature waliniambia siyo msanii ila ni MC cartoon na kwamba hawezi kuwa kama Solo au Prof Jay kwa hiyo nilichekwa sana Nature pia alisemwa sana lakini nachomshukuru Mungu amenipa uwezo wa kumtambua mtu mwenye kipaji na najua huyu ata'hit au la! na kwa Harmorapa nina imani atafika mbali sana kwa hiyo J yeye asizungumze anyamaze tuu". Alisema Majani

Katika hatua nyingine Majani amemuuelezea Harmorapa kama kijana anayestahili kuwapo kwenye sanaa hata kama si mwanamuziki lakini ni mburudishaji ambaye ana kipaji cha kuwafanya watu wafurahi hivyo hatakiwi kuwa nje ya sanaa na kwa sababu yupo tayari kwenye mikono yake anaamini atafika mbali.

"Harmorapa siyo msanii direct, kuna rapa, MC na Entertainer sasa dogo ni Entertainer. Master J kama anakumbuka kuna kipindi alimleta yule Sulukuchu studio anaimba ndugu Sulukuchu, sasa yule msanii gani lakini kuna John Walker (RIP) yule alikuwa mburudishaji kwa style yake ya ulevi kwahiyo Harmorapa anaingia kwa mtu kama Walker, watu wakipenda anachofanya ndiyo burudani yenyewe" Alisisitiza Majani.

Mkongwe huyo amesema yupo tayari kurudi kwenye game na kwa sasa anamalizia kuandaa ujio wake mpya kwa kikundi kipya cha muziki kinachoitwa Bongolos ambao anaamini watafanya vizuri sana kwenye sanaa.

Hatarii..Makachero wa Marekani Waanza Kuingia Korea Kaskazini Tayari kwa Vita..Siri Nzito za Silaha za Nyuklia za Korea Zaifichuliwa...!!!

$
0
0

Hii habari ya majasusi wa USA, majasusi hawa wa America wenye Asili ya korea wamejipenyeza ndani ya korea kaskazi kuanzia December mwaka jana 

Na kwa taarifa zilizovuja Rais wa korea kaskazin ameamuru kusitisha Visa kwa raia wanaotoka nchi za magharibi kutokuingia North Korea kwa muda usiojulikana 

Pia ametoa wito kwa raia wazalendo wa korea kaskazin kutoa taarifa kwa mtu yeyote wanaemshukia hana maadili ya korea kaskazin 

Siku ya jumapili iliyopta wanajeshi watatu wamenyongwa korea kaskazin wakishutumiwa kuvujisha mipango ya jeshi Lao kwa jeshi la USA 

Pia Rais wa korea kaskazin jana alia muru kurushwa kwa kombora kwa siri kubwa ambalo badae lilifeli na mwana jeshi moja wa korea kaskazin anasemekana alituma kila kitu kilichofanyika makao mkuu pentagon 

Ndio maana Leo mkuu wa idara ya jeshi u pande wa peninsula alitangazaa kushindwa kwa kombora lililorushwa la North Korea kufeli vibaya 

Mike pence, makamu Rais wa USA Ambaye yupo njian kuelekea South Korea 
Inasemekana ameambatana na nyambizi zisizoonekana katika peninsula ya korea kaskazin 


Majasusi wa USA wamenasa mawaasiliano kati ya wazir wa mambo ya nje ya urusi, wakiwasiliana na wenzao wa China Pmj na uturuki na North Korea na iran 

Wakat huo huo makao Rais pence anawasiliana na Donald Trump akiwa njian kuelekea South Korea 


Wazir wa mambo ya nje wa uingereza amempigia simu wazir wa mambo ya kigeni wa USA kumhakikishia juu ya North Korea kurusha kombora lililofeli 


Na Inasemekana usiku mzima wa jana Rais Trump alikuwa kwenye mazungumzo mazito na waziri wa ulinzi wa USA pamoja na mkuu wa majeshi 

Wakuu ni baampa to baampa 

Mimi naomba USA asipagane Ase, maana madhara yake yatakuwa ni kwa dunia nzima 

Namwomba Mungu awaongoze washauri wa Trump wasimshauri kuvamia North Korea 

Wamshauri kuiwekea vikwazo tu 

We need peace and not war

Uchambuzi..Hivi Ndivyo Marekani Atakavyofanikiwa Au Kushindwa Kumpiga Korea Kaskazini Katika Vita Inayonukia Huko Korea Kaskazini..!!!

$
0
0

Kukiwa bado tunaendelea na uchambuzi wa kile kinachoendelea eneo la Asia Pacific leo tutakijita kwenye uwezekano wa Russia na China kushiriki vita hvyo kama vikitokea je Russia na China watachagua upande gani ktk vita hvyo?

Nchi zote kabla hazijafanya maamuzi magumu ya kuingia vitani jambo la kwanza ni kutafuta waungaji mkono au watakao support ktk uvamizi huo leo US pamoja na uwezo na ubabe wake anakwenda vitani na nchi washirika ikiwamo UK na nchi zingine zinaweza kutoa mchango mwingine sio lazima mchango wa askari au vifaa inawezekana zikawa taarifa za intelligence au kuruhusu kutumika kwa airspace yako au viwanja vyako vya ndege hasa cargo plane za kijeshi kwa ajili ya usambazaji wa vifaa au huduma ndani ya uwanja wa mapambano

Nilisema linapokuja swala la Maslai ya wazungu duniani wanakuwa kitu kimoja mzungu wa SA ,Australia mpaka Canada wanakuwa kitu kimoja so tutegemee ushirikiano mkubwa kutoka Ulaya na nchi zote za wazungu watakuwa nyuma ya USA ktk jamii za wazungu Russia ndio ameamua kujitenga na wenzie na kitendo cha yeye kujitenga kimemfanya kuwa ni threat kwa wenzie(Wazungu) lakini kutokana na uwezo wake kijeshi wameshindwa kumdhibiti baada ya kifanikiwa kuangusha USSR

CHINA amekuwa mashirika mkuu wa US na Ulaya ktk nyanja mbalimbali kuanzia uchumi, biashara na uwekezaji Marekani amewekeza $228 billion ndani ya China wakati China amewekeza $64 billion ndani ya Marekani so ukiangalia Marekani amewekeza sana ndani ya China na kumfanya china kuwa mshirika mkuu ktk eneo lote la Asia lakini mahusiano ya China na Marekani yamekuwa kibiashara lakini kijeshi wamekuwa kila mtu ana mashaka na mwenzie hii imepelekea kuwa kama na bifu la kijeshi na Urafiki wa kibiashara na Uchumi

RUSSIA nchi hii imeshapitia ktk nyakati mbalimbali na US na nyakati vying US ameibuka mshindi kuanzia kuigawa USSR , Vita vya Afghanistan December 1979 to February 1989 mpaka leo NSA wanamsemo "Warusi walikuwa wepesi kuwaona wagumu kuwaua lakini magaidi ni wagumu kuwaona wepesi kuwaua" Russia na Marekani wamekuwa maadui wanaokaa meza moja ya mazungumzo na kunywa lakini ndani ya moyo kila mmoja anawaza mabaya juu ya mwenzie.

NORTH KOREA ni nchi yenye mipaka sehemu 3 mpaka wa kwanza ni mpaka wake na South Korea mpaka huu unafahamika kama DMZ Demilitarized Zone mpaka pekee ambapo US ataitumia kuingia NK kama mpaka wa kuingia kwa miguu mpaka mwingine ni mpaka na China ambao unapatikana kwenye jimbo la Jilin mpaka wenye 1,420 kilometres na unatenganishwa na mito ya Yalu na Tumen

Kaskazini mwa korea kaskazini kuna mpaka mwingine ambao ni mpaka wake na Russia mpaka mwenye 17 kilometres ardhi na 22.1Km ni maji (mto)ndio unawatenganisha sasa wote tunajua eneo la Alaska lilikuwa eneo la Russia then wakauziwa Marekani umbali wa kutoka Alaska mpaka Russia ni 53 miles sawa na 85 km sasa kitendo cha US kuingia North Korea na kuikalia kijeshi inamaana anakua anaichungulia Russia wakiwa wametenganishwa na mto tu inamaana anaweza kwenda Russia kwa kuogelea tu je Russia yuko tayali kuona jambo hilo na Putin yuko tayali kunywa vodka Moscow wakati adui anaweza kuingia Russia kwa kuogelea tu?

China ktk nchi ambazo zinajiandaa kuwa Super Power kiuchumi ni China wanasema mpaka 2050 China atakuwa Super Power kwa Upande wa kiuchumi na Uchumi unaendana na nguvu za kijeshi hili uweze kulinda Maslai yako pale adui anapoingia na ktk kujiandaa na kumpokea kijiti cha Usuper power wa kiuchumi kutoka kwa USA, China hato kuwa na amani endapo USA atakuwa anajua kinachoendelea Beijing hasa ktk maswala ya kijeshi kitendo cha US kuingia North Korea na kuweka military Base kitakuwa ni kitendo cha China kukubali kuwekewa Camera chooni au bafuni sidhani kama kuna Binadamu ambae anaweza kukubali jambo hilo

Njia pekee ya nchi zote ambazo ni Russia na China kuepuka jambo hilo ni kumsaidia North Korea aidha kwa kificho au kwa wazi kwani Silaha zinaweza kutoka Russia kupitia mpaka wao kuingia North Korea na Dunia isijue pia same to China tena China wanaweza kupeleka jeshi kabisa kwani wale so ni ngumu zungu la Texas kujua huyu ni mchina au mkorea ndani ya uwanja wa mapambano 

pia kama nilivyosema Glovbal Navigation Satellite System ( GNSS) ni technologia ya mwaka 1970 watu wanaweza kudanganya na ikaleta taarifa za uongo mfano ni kwenye Project-706 (1974-1983) Pakistan Army Corps of Engineers na Inter-Services Intelligence Pakistan intelligence waliweza kutengeneza Bomu la nuclear na Dunia walishindwa kujua kinachoendelea ndani ya jiji la Islamabad si CIA,MOSSAD AU MI6 walijua kinafanyika nini hata Adui mkubwa na jirani wa Pakistan India hakujua kinachofanyika
Islamabad

Sio kwamba Russia na China wanapenda kumsaidia ila Mazingira ya wao kuwa safe na kunywa vodka Moscow na Xinjiang Black Beer Beijing kwa amani inabidi wamsaidie North Korea kwani kuna msemo unasema "Mazingira yanaweza kuhamasisha kufanyika kwa uharifu"

Trump Aamuru Jeshi la Marekani Kuvamia Somalia na Kuua Alshabab 100..Hii Ni Maanadalizi ya Vita Dhidi ya Korea Kaskazini..!!!

$
0
0

Zaid ya wapiganaji 100 wa Alshabab, ikiwemo makamanda 20 wa Alshabab wanaaminika kuuawa kwenye shambulizi la anga lililotekelezwa na Marekani mapema jana(Jumamosi) katika eneo la El-Adde kusini kwa Somalia.

Wenyeji na maafisa usalama katika eneo hilo ambapo wanajeshi wa Kenya walivamiwa na kuuawa na kundi hilo mwezi januari mwaka jana(2016) walisema kua walisikia ndege za kivita zikiangusha mabomu kwenye maficho ya kundi hilo.

Shambulizi hilo linajiri siku chache baada ya Marekani kusema kuwa itatuma jeshi lake nchini Somalia kutoa mafunzo na vifaa kwa jeshi la Somalia na AMISOM ili kuiwezesha kushinda vita dhidi ya Alshabaab. 

Source: China Xinhua News

Hoja ya Mbowe Waliyoidharau Wabunge wa CCM Imeanza Kupata Majibu..!!!

$
0
0

Juzi Mh Mbowe katoa hoja ya bunge kujadili usalama wa wananchi kutokana na kushamiri kwa matukio ya kihalifu ya mauaji na utekaji.

Wabunge wa CCM wakiongozwa na Jenista Mhagama wakapinga na kusema Tanzania ni salama kuwa bunge lina mambo mengi ya kujadili. Hayajapita hata masaa 12 askali 8 wamevamiwa na kuuawa, bado kina Mhagama wanasema Tanzania ni Salama.

Nataka kuwaambia CCM kuwa endeleeni na dharau zenu, mnayoyataka soon mtayapata na siku yakiwakuta hakutakuwa na mtu wa kuwasemea wala kuwaonea huruma.

Breaking News..Mbunge wa Chadema Alazwa Ghafla Muhimbili..Afanyiwa Upasuaji Kuokoa Maisha Yake..!!!

$
0
0

Wakuu salaam. Natumai tupo wazima. Kama inavyozunguka mitandaoni kuhusu kulazwa katika Hospitali ya Taifa Muhimbili kwa Mhe. John Heche, taarifa hiyo ni ya kweli. 

Mhe. Heche alifika Hospitali ya Taifa Muhimbili siku ya Jumanne wiki hii kwa uchunguzi wa afya yake, baada ya uchunguzi wa awali alishauriana na daktari wake na kukubaliana angerejea Hospitali baada ya wiki mbili kwa matibabu rasmi.

Hata hivyo jana usiku 
Mhe. Heche alipata maumivu makali ya ghafla tumboni na leo asubuhi alikimbizwa Hospitali Muhimbili na kufanyiwa upasuaji (specialised surgery).

Upasuaji umeenda vizuri na hali yake inaendelea vema sana. Mwenyekiti wa Taifa Mhe. Freeman Mbowe amemtembelea kumjulia hali. 

Salum Mwalim
Naibu Katibu Mkuu
CHADEMA 
Jumapili April 17, 2017

Huu Ndio Ukweli..Ma Houseboy ni Hatari Zaidi Kuliko Ma House Girl..!!!

$
0
0

Wasaidizi wanaoogopeka zaidi na wenye sifa mbaya ndani ya majumba yetu ni wale wa kike
Wengi husingiziwa umalaya 
Wengine uchawi na ushirikina 
Wezi wa waume za watu (baba wenye Nyumba)
Wizi wa vitu vya ndani 
Mateso kwa watoto nk 
Kesi zao ni nyingi kuliko za ma house boy...! Lakini kesi zao nyingi ni nyepesi na nyingi kati ya hizo za mauaji ni kama hakuna kabisa, mauaji ya mama wenye nyumba
Tukipindukia upande wa pili wa ma house boy hawa watu ni hatari sana wenye roho mbaya na katili hasa 
Wengi wameshiriki kwenye mauaji ya matajiri wao wa kiume kwa kushawishiwa kwa sehemu kubwa na boss mwanamke, kesi nyingi za namna hii zimetokea sehemu mbalimbali nchini ya karibuni kabisa ikiwa ni ile ya Mabwepande lakini pia bila kusahau ile ya Arusha 
Inashanga sana kuwa kolabo ya baba mwenye nyumba na hg haina ukatili na madhara makubwa kama kolabo ya mama mwenye nyumba na house boy
Ndugu jitafakari tu kama nyumbani umeajiri house boy jijue wazi Kuwa unatembea na kifo mkononi

Zijue Faida 11 za Kulala Uchi au Mtupu Nyakati za Usiku..!!!

$
0
0

UMEZOEA kulala na nguo nyepesi za kulalia? Au unahisi vizuri zaidi ukilala na nguo nzito laini za kulalia? Watu wengi hujifunika mashuka na wengine hujifunika mablenketi kabisa.

Katika makala haya, itakufumbua macho uanze kulala uchi/mtupu kwa kutumia hoja bora zilizochaguliwa kuelezea kwanini kulala uchi ni kuzuri kwako.

Nguo za kulalia zina gharama kubwa

Ni kiasi gani cha fedha ambazo wewe hutumia kununua pea ya nguo za kulalia? Inaweza kuwa kati ya fedha za kitanzania kati ya shilingi 20,000 na 40,000 au zaidi. Ni mara ngapi huzifua hizo nguo? Sasa fikiria ni kiasi gani cha pesa na muda unachoweza kuokoa usipovaa nguo za kulalia.

Hutengeneza uhusiano mzuri ukisaidiwa na kichocheo cha Oxytocin

Natasha Turner, daktari wa tiba asilia aliyeandika kwenye blogu ya Huff Post Canada, alifichua kwamba kulala karibu au mkiwa mmekumbatiana na mwenzi wako mkiwa uchi/watupu hufanya mwili kutoa kichocheo kiitwacho Oxytocin kinachofanya ujisikie vizuri. Hii inatokea pale kunapokuwa na mgusano wa ngozi kwa ngozi, hii inaweza kusaidia kuondoa msongo (Stress) na kushuka moyo (Depression).

Oxytocin pia inaweza kupunguza shinikizo la damu, kuimarisha tumbo na kupunguza uvimbe kwenye utumbo. Pia, utendaji wako wa tendo la ndoa pengine unaweza kuboreka.

Hupelekea usingizi mwanana

Hivi unafahamu baadhi ya matatizo ya kukosa usingizi (Insomnia) yanaambatana kutokana na tatizo la mwili kudhibiti jotoridi? Taasisi ya Usingizi ya Los Angeles inaripoti kwamba hali hii haiathiri tu mzunguko wa usingizi ila pia hukuzuia kupata usingizi mnono. Kulala uchi/mtupu husaidia katika kurekebisha jotoridi la mwili (hivyo mwili hauchemki kupita kiasi, ni vibaya kuamka umelowana jasho.

Hukufanya ubaki kijana

Kama tulivyoona hapo juu kuhusu kudhibiti jotoridi kama unahitaji usingizi mzuri, Natasha Turner anashauri kuweka mwili katika jotoridi chini ya 21°C ukiwa kitandani na njia nzuri kufanta hivyo ni kulala uchi/mtupu. Hii huruhusu vichocheo vinavyozuia uzee na Melatonin ambayo hudhibiti mzunguko wa kusinzia na kuamka kutenda kazi vizuri.

Utajihisi huru, Kulala kitandani kwako, bila kuvaa chochote inakufanya kujisikia huru.

Huhamasisha vichocheo vya furaha (kuponya)

Unapolala na nguo au kulala chini ya blanketi zito unazuia utokaji wa kichocheo cha ukuaji (Growth Hormone/HGH). Hii ina maana hutoweza kupunguza mafuta ukiwa katika usingizi au hautofaidika na ukarabati wa usiku wa mifupa, ngozi na nyama za mwili wako. 

Kulala uchi/mtupu pia huthibiti kiwango cha Cortisol, zinazo dhoofisha kinga ya mwili, kupandisha shinikizo la damu na lehemu (Cholestrol), kuvuruga mpangilio wa usingizi, kupunguza hamu ya tendo la ndoa na kuongeza hamu ya sukari.

Inaimarisha kujipenda

Kama una matatizo ya kutokujiamini basi kulala uchi/mtupu kutakusaidia kujifunza kujipenda. Kwa kuanza, jizoeshe kulala bila nguo kila jioni. Baada ya muda utazoea pia baada ya muda unaweza kuwa umejifunza kuupenda muonekano wako bila nguo.
Inatunza kiafya viungo vya uzazi.

Kina dada, mnafahamu mnaweza kupunguza matatizo ya mabukizi ya fangasi kwa kulala uchi/watupu? Unaweza kupunguza kuzaliana kwa fangasi na uke wako utakushukuru kwa hilo. Vilevile wanaume wanaweza kufaidika kulala uchi/watupu kwa kuwa korodani zinakuwa katika jotoridi la kutosha na uzazi unaongezeka.

Mzunguko wa damu unakuwa bora

Hakuna kitu kibaya kama lastiki inayozuia mzunguko wa damu. Ondoa nguo zenye lastiki na utajipata uko na furaha kwa mtiririko wa damu mzuri ndani mwili wako.

Kuwa na ngozi nzuri

Unapokuwa uchi/mtupu ngozi yako inapata nafasi ya kupumua. Kama una chunusi au vipele mgongoni ni kitu cha thamani kuacha hewa ya Oxygen kufika kwenye maeneo hayo. Ngozi yako inastahili uhuru kidogo na utajisikia vizuri kwa kuiacha ngozi wazi.

Kutokuwa mvivu

Faida nyingine ya kulala uchi/mtupu ni kwamba mara baada ya kuamka unakuwa na ulazima wa kuvaa nguo kwa ajili ya siku hiyo mpya na sio kuamka na nguo zako za kulalia na kutoka nazo nje.

Haya Wanaume Mnaopenda Kuvaa Boxer na Chupi za Kubana Hii Inawahusu..Fahamu Madhara Yanayotokana na Nguo Hizo..!!!

$
0
0

TAFITI za kisayansi zilizofanywa hivi karibuni zimebaini kuwa, nguo za ndani hasa zinazobana kwa wanaume na zile za aina ya nailoni (nylon) zinaathiri uwezo wa mbegu za kiume, hivyo kushindwa kutunga mimba.

Utafiti huo umeofanywa katika nchi za Ufaransa na Uingereza na kuchapishwa katika Gazeti la Daily Mail la nchini Uingereza unabainisha kuwa, wanaume wanaovaa nguo za ndani zinazobana na zile zinazotengezwa kwa malighafi ya nailoni, mbegu zao za kiume (manii) huwa nyepesi na kupoteza uwezo wa kutunga mimba.

Vazi la ndani la wanaume linalojulikana kama boksa na nguo nyingine za ndani za kubana zenye asili ya nailoni, zinakuwa na athari kubwa zaidi hasa zinapovaliwa katika sehemu zenye joto, kama vile jijini Dar es Salaam.

Kutokana na matokeo hayo, wanasayansi wameonya kuwa wanaume wanapaswa kuchukua tahadhari, hasa kutokana na tafiti nyingi za karibuni kuthibitisha kuongezeka kwa matatizo ya mbegu za kukosa uwezo wa kutunga mimbao katika nyumba ya uzazi ya mwanamke

Akizungumzia utafiti huo, Daktari Bingwa wa Magonjwa ya Wanawake na Uzazi katika Hosipitali ya Taifa Muhimbili, Dk Cyril Massawe, amesema kuwa, upo ukweli kutokana na mbegu za kiume kuwa nje ya mwili wa mwanamume tofauti na mwanamke ambaye kizazi chake kipo ndani.

Amesema kuwa, kwa kawaida mwanamume anayeishi maeneo ya joto anapaswa kuwa makini sana, ili kuhifadhi vizuri manii yake anatakiwa kutumia mavazi yenye kupitisha hewa.

katika nchi za Ufaransa na Uingereza ambako utaiti huo umeafanywa umebaini kuwa, nchini Ufaransa upungufu wa nguvu za kiume kwa wanaume wengi umeanza kutokea tangu mwanzoni mwa 1990 ambapo hapo awali iliaminika kuwa, kupungua kwa uwezo wa mbegu za kiume kulitokana na sababu kama vile mtindo wa maisha, ulaji na matumizi ya dawa kupindukia na matumizi ya vyakula vyenye kemikali nyingi, lakini safari hii utafiti umebaini kuwa matumizi ya nguo za ndani yamekuwa yakiwaathiri wanaume wengi.

Mtafiti wa Uingereza, Profesa Richard Sharpe kutoka Chuo Kikuu cha Edinburgh anasema kuwa, tatizo hilo linaweza kuepukwa ikiwa mhusika atajitahidi kuvaa nguo zinazokubalika na mahala alipo. Hata hivyo, anapendekeza uchunguzi zaidi ufanywe ili kulinda kizazi cha sasa na kijacho.

Mpenzi Wangu Anapenda Ngono tu...!!!!

$
0
0

HABARI anko? Nina mpenzi wangu nimeishi naye miaka miwili simuelewi, anapenda ngono tu. Nimeshachoka kuishi maisha ya kibachela, nimemuomba japo aende kwetu ajulikane anasema ningoje, nifanyeje anko na miaka inasonga?

Jibu: Kwa muda ulioishi naye, huna sababu ya kuwa na hofu kama umeambiwa usubiri labda kama hakuonesha dalili zozote njema tangu mnaanza hadi sasa. Kama hakuonesha na kila siku amekuwa akikuhitaji tu kwa ajili ya ngono na baada ya hapo haongelei maisha wala uhusiano wenu basi una kila sababu ya kujiweka mbali naye.

Yamkini alikuwa kama amekuwa akiendelea kuzungumzia maisha yenu na ukimtazama kweli ana maanisha basi huna budi kumsubiri na kumsaidia kimawazo na kila kitu ili muweze kufi kia malengo yenu. Usiwe na haraka kama unaona ana dhamira ya dhati  na wewe. Mpe muda, mtafi kia kilele cha mafanikio.

na Wewe Unaweza Kuongezea Ushauri wako Hapo chini

Sehemu za Siri za Maiti ya Mama Mjamzito na Matumizi Yake Katika Ulozi..!!

$
0
0

Nikiwa katika kijiji cha kabila wilayani Magu enzi za ujana wangu mwishoni mwa miaka ya tisini, kwa mara ya kwanza nilikwenda nilikwenda kwa mganga nikiwa nimefuatana na shangazi yangu baada ya aliyekuwa mtoto wa shangazi yaani Binamu kufa katika mazingira ya kutatanisha.Baada ya kupigiwa ramli na mganga kupitia kifaa maalum yaani cha kupigia ramli (Shelo) na kifaranga tukagundua ndugu yetu alikufa kwa kuchochewa nafsi ili akajitupe bwawani tuamini amekufa na wachawi wamchukue kirahisi (kusonelwa).

Baada ya ramli mganga akatushauri tufanye zindiko la kumfnya ndugu yetu asibaki msukule ila tummalizie afe kabisa na asiendelee kuteseka huko alikofichwa ktk kijiji jirani cha jinjimili. mganga alitusihi tutafute kuku wa rangi nyekundu yaani (Shingamageji),mafuta ya simba,mchanga wa kaburi la mtu aliyekufa kwa kukujinyonga, mtama na sehemu za siri za mwanamke aliyekufa na ujauzito wake.

Zindiko lilianza mnamo saa moja na nusu usiku ili tuwahi kabla mida ya wachawi hawajafka kisha tuweke kingo za kuwazuia wasisogee eneo la zindiko ambalo lilipaswa kuisha kabla jogoo wa kwanza hajawika ambaye ndo hutumika kama alarm ya wachawi kuondoka na ikitokea jogoo wa pili amewika huyo mchawi amechelewa na lazima atashindwa kurudi na asubuhi ataumbuka.

Tulipofika eneo la zindiko mganga alisimama juu ya kaburi sisi wengine wawili tukakaa upande wa magharibi kwa direction ya kichwa cha kaburi kilipoelekea. Tulimchinja jogoo mwekundu kisha damu yake ikazungushiwa eneo la zindiko kisha tukajichanja na kujiwekea mafuta ya simba kama zindiko ili wachawi wasitusogee japo walikuwa wanatuona sana.mganga alirusha mtama angani kisha kisha ule mchanga wa kaburi la mtu aliyejinyonga akaumwaga juu ya kaburi la ndugu yetu ambapo ndo lilikuwa hasa eneo la zindiko.

Baada ya kuumwaga ule mchanga kwa juu yake tukaziweka sehem za siri za mwanamke aliyekufa akiwa na mimba kisha tukaanza kuziunguza wakati zinaungua mganga aliongea maneno mengi huku akitaja jina la marehemu binamu yangu.cha ajabu zile sehemu za siri hazikuisha na ziliteketea kwa zaidi ya masaa sita.wakati zinateketea mganga alitoa ngozi ya fisi na ndani ya ngozi kilifungwa kifundo cha nyama kubwa kavu ya moyo wa binadamu ambayo tuliipaka dawa kisha mganga akaiweka juu ya zile sehem za siri zilizokuwa zinateketea akatuasa tuwe makini tusishtuke kwani muda si mrefu ile nyama ya moyo ingemezwa na uke unaoteketea halafu baada ya saa moja uke uendelee tena kuungua kisha kuna mlio mkubwa wa kupasuka utoke na hapo ndipo binamu angekufa kabisaa asiendelee kuwa msukule.

Kweli baada ya hilo tukio kutokea nikishuhudia ikiwa ni majira ya saa saba usiku tulikaa kmya mganga akatusihi tuinamishe vichwa na alipotuambia tuinue tukawaona mtoto mmoja na mama mmoja wako uchi wamesimama na kisha walichukua ule uke tulioumaliza kuutumia kwenye zindiko kisha wakaondoka.baada ya tukio hilo mganga akatuambia ile ni misukule ilitumwa na waliomroga ndugu yetu kuja kuchukua hicho kiungo kama ishara ya wao kukubali kuwa binamu yetu amekufa na pia kuashiria amani na mganga maana waganga na wachawi ni mahasimu ambao ni hupatana pia muda mwingine.

Huo ndio ukawa mwanzo wangu wa kujua mengi sana niyajuayo sasa kuhusu uchawi katika ardhi ya Usukuma

Askofu Aitaja Rushwa Kanisani..!!!!

$
0
0

Msaidizi wa Askofu wa Kanisa la Kiinjili la Kilutheri (KKKT), Dayosisi ya Mashariki na Pwani, Mchungaji Chediel Lwiza amesema wala rushwa ni sawa na wauaji.

Akihubiri jana wakati wa sikukuu ya Pasaka kwenye Kanisa la Azania Front, Lwiza alisema rushwa ni adui wa haki na inaweza kusababisha hadi vifo.

Alisema licha ya rushwa kuwepo tangu enzi za kifo cha Yesu Kristolakini madhara yake yamekuwa makubwa katika jamii hadi sasa.

Alisema baada ya Yesu Kristo kufufuka katika kaburi, walinzi walipewa rushwa ili wasiseme ukweli kuwa amefufuka bali waseme amechukuliwa na wanafunzi wake.

“Kwa hiyo viongozi waliwapa rushwa walinzi ili wasiseme ukweli na hivyo wakatoa taarifa za uongo, rushwa inapofusha macho,” alisema. 

Baada ya Kula Ujana Vyakutosha..Aunty Lulu Sasa Kuimba Gospo...!!

$
0
0

BAADA ya maisha ya ujana yenye kila aina ya uchafu hatimaye msanii na Mtangazaji Lulu Semagongo maarufu kama Aunty Lulu, amesema anajiandaa kuimba nyimbo za Injili zitakazozungumzia maisha yake ili watu wengine wajifunze.

Aunty Lulu alisema nyimbo zake zitabadilisha maisha ya watu wengi kwani ujumbe utakaokuwemo ndani yake utazungumzia mambo mengi ambayo amepitia katika maisha yake.

“Najiandaa kuimba nyimbo za Injili na wimbo wangu wa kwanza utaitwa Unikumbuke Mungu, ambapo ndani yake nitaeleza mambo yote niliyopitia kwenye maisha yangu ikiwemo kubadilisha wanaume tofauti, starehe za kila aina, kuvuta sigara na mengine mengi na nimeamua kufanya hivi ili kupitia historia ya maisha yangu vijana wengi wabadilike,” alisema.


Wabunge wa CCM Wamkaba Koo Waziri wa Magufuli...Waunga na na Upinzani Kudai Katiba Mpya...!!!

$
0
0

Waziri wa Katiba na Sheria, Profesa Palamagamba Kabudi amebanwa na wabunge kuhusu mchakato wa Katiba Mpya.

Jana ilikuwa mara ya kwanza kwa Profesa Kabudi kufika mbele ya Kamati ya Katiba na Sheria ya Bunge, akiwa katika nafasi ya uwaziri baada ya kuteuliwa hivi karibuni na Rais John Magufuli kushika wadhifa huo, baada ya Dk Harrison Mwakyembe kuhamishiwa Wizara ya Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo.

Profesa Kabudi alisema hajakutana na viongozi wake kuzungumzia suala la Katiba Mpya, ingawa anajua mambo mengine kuhusu mchakato huo ambao wakati wa maandalizi yake, alikuwa mjumbe wa Tume ya Mabadiliko ya Katiba.

Wabunge wa CCM walikuwa wa kwanza kuibua hoja hiyo jana wakisema Katiba Mpya ni sehemu ya ilani ya uchaguzi ya chama chao.

Mbunge wa Bahi (CCM), Omari Badwel alimtaka waziri huyo aseme ni lini hasa mchakato huo utaendelea na Watanzania watarajie kuipata lini Katiba hiyo.

Mbunge huyo alisema mapendekezo ya bajeti ya mwaka wa fedha 2017/18 hayaonyeshi ni mahali gani na kifungu kipi kitakachotumika kwa ajili ya kusaidia mchakato wa katiba ikiwamo upigaji wa kura ya maoni.

“Hata humu sijaona kama kuna fedha zilizotengwa kwa ajili ya kuendeleza mchakato wa Katiba Mpya, najiuliza ina maana si kipaumbele au mmesahau kuwa hata ilani ya uchaguzi ya CCM imetaja suala hilo?” alihoji Badwel.

Mbunge wa Malindi (CUF), Ali Saleh alisisitiza kutozimwa kwa suala hilo kwa kuwa ni muhimu sasa na akahoji kwa nini linachukua muda mrefu kukamilika.

Saleh alisema inashangaza kuona mchakato huo ukipelekwa kwa mwendo wa kusuasua licha ya kuwa fedha nyingi za walipakodi zilishatumika.

Mbunge huyo ambaye alikuwa miongoni mwa wajumbe wa iliyokuwa Tume ya Mabadiliko ya Katiba, alilalamika kuwa suala la Katiba Mpya limezimwa, akataka Serikali kusoma alama za nyakati kuwa huu ndiyo wakati wake.

Hata hivyo, Profesa Kabudi alisema ana muda mfupi katika wizara hiyo na kwamba, hajapata muda wa kukutana na mabosi wake akiwamo Waziri Mkuu, ili wazungumzie suala la Katiba Mpya.

“Najua nia yenu njema, ninalichukua jambo hili na nitahakikisha nalifikisha kwa wakuu wangu yaani Waziri Mkuu, Makamu wa Rais na kulifikisha kwenye Baraza la Mawaziri,” alisema Profesa Kabudi.

Alisema mchakato huo unahitaji umakini mkubwa hivyo atafanya kazi kulingana na utaratibu wa kisheria ili liwe na mwanzo na mwisho mzuri.

Achana na Tukio la ROMA na Wenzake…. Mwinjilisti Dar Atekwa, Auwawa...!!!!

$
0
0

Huku tukio la msanii wa Hip Hop, Ibrahim Mussa ‘Roma Mkatoliki’ na wasanii wenzake watatu kutekwa studio likiwa bado halijapoa, mwinjilisti aliyefahamika kwa jina la Onoratus Mwinuka (51), mkazi wa Mabwepande jijini Dar, amedaiwa kutekwa na kuuawa kisha mwili wake kufukiwa ardhini huko Mabwepande, Risasi Jumamosi linakudadavulia.

HABARI KAMILI Kwa mujibu wa dada wa marehemu aliyejitambulisha kwa jina la Veronica Mwinuka, taarifa za kupotea kwa kaka yeka alizipata Machi 14, mwaka huu kutoka kwa watoto wa marehemu ambapo walisema tangu baba yao alipoondoka alfajiri ya Machi 13, mwaka huu hakuwa amerejea tena nyumbani.

Veronica aliendelea kusema watoto hao walimwambia pia katika alfajiri hiyo ya saa kumi, marehemu aliondoka na mfanyakazi wake wa kiume aitwaye Ayubu aliyekuwa na kawaida ya kumsindikiza kila mara kutafuta usafi ri ili apeleke maziwa ya ng’ombe mjini kisha akishapata usafi ri yeye hurudi nyumbani.

Inadaiwa kuwa, siku hiyo, walipofi ka kituoni, lilitokea gari aina ya Toyota Noah, wakamuuliza marehemu kama anakwenda, akakubali na kupanda, gari likaondoka.

“Baada ya hao watoto kunipa taarifa hizo sikuweza kushituka mara moja maana nilifahamu pengine kaka alikuwa amepitia kwenye shughuli zake nyingine za kiuinjilisti maana alikuwa ni muinjilisti lakini baada ya kupita siku hiyo aliyopotea, siku iliyofuata kuna wizi ulitokea nyumbani kwake ndipo nikashituka,” alisimulia Veronica.

WIZI WATOKEA NYUMBANI KWA MAREHEMU

Veronica aliendelea kusema kuwa, wizi huo uliofanyika ulifanywa na mmoja wa wafanyakazi wa marehemu ambaye aliiba fedha zinazokadiriwa kufi ka shilingi milioni 30 ambazo marehemu alikuwa amezitoa benki siku moja kabla ya kupotea kwake kwa ajili ya kununua gari ndogo (pick up) ya mizigo na kuwalipia wanaye ada ya shule.

“Kiukweli niliona si hali ya kawaida hasa nilipounganisha matukio ya kuibiwa nyumbani na kupotea kwake.

“Lakini mbaya zaidi kaka nyumbani alikuwa amebaki mwenyewe. Mkewe alikuwa nyumbani kwao kwa ajili ya kumuuguza mdogo wake, kwa hiyo niliamua kuwataarifu ndugu zangu wengine, akiwemo shangazi yetu ambapo akatutaka tutoe taarifa kwenye vyombo vya usalama.”

ATAFUTWA MPAKA MOCHWARI

“Mkewe pia alirudi, tukaenda kwenye ofisi za serikali ya mtaa kisha kwenye Kituo cha Polisi Mabwepande ambako tulitoa taarifa na kupewa RB ili kumtafuta yeye pamoja na mfanyakazi yule aliyeiba.

Kazi ya kumtafuta sehemu mbalimbali ikaanza ikiwemo mahospitalini, mochwari na sehemu nyingine mbalimbali lakini hatukuweza kumpata kaka kwa zaidi ya siku ishirini baadaye,” alisema Veronica.
AZIDI KUSIMIULIA

Dada huyo wa marehemu aliendelea kusema kuwa, ilifi ka hatua ndugu wakakata tamaa kwamba hawezi kupatikana tena, lakini hivi karibuni mdogo wao mwingine wa mwisho aitwaye Alphonsia Mwinuka alifi ka kutoka Mbozi, Mbeya kwa ajili ya kazi hiyo ya kumtafuta kaka yao.

Baada ya kufi ka akishirikiana na kijana wa kazi (Ayubu) aliyekuwa na marehemu siku ya mwisho kuonekana pamoja na watoto wa marehemu, walianza msako upya katika misitu inayozunguka nyumba ya marehemu.

SIKU YA MWILI KUONEKANA

“Kiukweli siku hiyo tulimtafuta kwa muda mrefu bila mafanikio. Giza lilipoanza kuingia mimi nilikuwa tayari nimechoka, nikamwambia Ayubu pamoja na mtoto wa marehemu aitwaye Daniel mwenye miaka kama saba kwamba, waende upande mwingine kumtafuta mimi nikarudi nyumbani.”

DALILI ZA KUONEKANA MWILI WA MAREHEMU

“Baada ya muda walirudi na kuniambia kuna sehemu porini ilichimbwa, pia ilikuwa na ufa jambo lililoashiria kwamba kuna kitu kilizikwa.

Ayubu alisema alipatilia shaka hivyo kupapiga picha kwa kutumia simu yake ya kisasa (smart phone). “Baada ya kunionesha na mimi zile picha niliitilia shaka ile sehemu.

Lakini sikuongea jambo lolote mpaka siku iliyofuata, tulitoa taarifa kwenye vyombo vya usalama na kwenda kwenye eneo lile tukiambatana na wananchi wa mtaa ule, lengo ni kuangalia pale mahali palizikwa nini,” alisema Alphonsia.

ENEO LA TUKIO

Alphonsia alisema, walipofi ka jirani na eneo hilo aliloliona kwenye picha mnato za simu, cha kushangaza, yule kijana akaanza kuwazungusha, lakini baada ya kumbana aliweza kuwaonesha na baada ya kuchimba waliukuta mwili wa marehemu ukiwa umeharibika sana.

“Kiukweli ilitusikitisha mnomno, hatukuweza kuamini kuwa mwili tuliokuwa tunauona ulikuwa ni wa ndugu yetu, hasa baada ya mkewe kuyatambua mavazi. Kutokana na tukio lenyewe ilionesha ndugu yetu alitekwa na watu waliomuua kisha wakamzika pale.

“Ni vigumu kufahamu sababu hasa ilikuwa nini lakini ni jambo lililoibua maswali mengi yasiyokuwa na majibu. “Baadaye polisi walipokuja, walimchukua Ayubu kwa ajili ya kwenda kusaidia upelelezi na mwili wa marehemu ulipelekwa katika Hospitali ya Taifa ya Muhimbili kwa ajili ya taratibu zingine za kipolisi,” alisema Alphonsia.

TAMKO LA SERIKALI YA MTAA

Naye mwenyekiti wa mtaa huo, Abdallah Omar alithibitisha kutokea kwa tukio hilo ambapo alilaani vikali matukio ya utekaji nyara yanayoendelea nchini na kusema ni kinyume na haki za binadamu. Mwili wa marehemu ulizikwa juzi Alhamisi kwenye Makaburi ya Mabwepande. Ameacha mke na watoto wanne.

KUMBUKUMBU MUHIMU

Matukio ya utekaji yanazidi kushamiri nchini, hadi sasa rekodi inaonesha, waliowahi kutekwa ni Msaidizi wa Mwenyekiti wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), Ben Saanane (hajapatikana), aliyekuwa Mhariri Mtendaji wa Kampuni ya Free Media, Absolom Kibanda (alijeruhiwa), Mwenyekiti wa Chama cha Madaktari, Dk. Steven Ulimboka (alijeruhiwa) na Roma Mkatoliki (alijeruhiwa) na wenzake watatu.


Hata hivyo, baadhi ya matukio hayo yamekuwa yakihusishwa kufanywa na wabaya wa waathirika hao ambapo baadhi ya wabunge, akiwemo Mbunge wa Kigoma Mjini (ACT-Wazalendo), Zitto Kabwe, hivi karibuni alitoa hoja ya kuundwa kwa kamati teule ya bunge kuchunguzaa matukio hayo.

Waziri wa Mambo ya Ndani, Mwigulu Nchemba, kwa upande wake alisema serikali inachunguza matukio hayo ili kuwabaini wanaofanya vitendo hivyo.

Baada ya Kumsimamia Roma..Mwakyembe Adai Maisha Yake Yapo Hatarini..Habari Vichwa vya Magazeti ya Leo 17/4/2017..!!!

Kudadeki..Mbwana Samatta Anunua Gari Hili Kama la Ronaldo wa Real Madrid..!!!

$
0
0

Mtanzania Mbwana Samatta anayeichezea KRC Genk ya Ubelgiji leo April 15 2017 amepost tofauti tofauti zikimuonesha akiwa na gari aina ya Mercedes Benz, Samatta ambaye kwa sasa anaishi Ubelgiji kutokana na kufanya kazi na KRC Genk nchini humo amepost picha gari hiyo bila maelezo mengi.

Inawezekana ikawa ni gari lake jipya ameamua kuliweka hadharani kupitia ukurasa wake wa instagram


.

Jamaa Afanya Mauaji Huku Akionyesha Live Marafiki zake Kupitia Facebook

$
0
0

Polisi katika jimbo la Ohio nchini Marekani wanamtafuta mtu anayedaiwa kufanya mauaji,huku akionyesha moja kwa moja mauaji hayo kupitia mtandao wa Facebook.
Maofisa katika mji wa Cleveland wamesema kuwa Steve Stephens anaonekana akionyesha moja kwa moja mauaji wakati akimpiga risasi mwanaume mmoja mtu mzima kupitia Facebook.

Mkuu wa Polisi mjini Cleveland Calvin Williams amemtaka Stephens ajisalimishe mwenyewe. Williams alisema kuwa mtu huyo ni hatari kuendelea kuwa mafichoni kwake.

Polisi wanasema hawajapata ushahidi madai ya Stephen kuwa amewauwa watu kumi na mmoja.

#BBC

Mbwana Samatta Aonyesha Mapenzi Kwa Yanga Kwa Kufanya Hili Jambo

$
0
0

Mchezaji Samatta akiwa amevalia uzi wa Yanga ambao ni zawadi aliyopewa na mchezaji wa klabu hiyo, Simon Happygod Msuva.⁠⁠⁠⁠

Machi 30, mwaka huu pia Mbawana samatta alimzawadia Msuva jezi yake ya Klabu ya Genk, ambapo Msuva alionekana ameivaa na kuandika jumbe huu..."#Hellow my Brother @samagoal77 I appreciate Thanks for the Gift #Popa77"

Baada Yakupokea Kipigo cha Goli 4-0,Yanga Waamua Maamuzi Haya Mazito..!!!

$
0
0

BAADA ya Yanga kuondolewa katika mashindano ya kimataifa ya Kombe la Shirikisho Barani Afrika, mabingwa hao watetezi wa Ligi Kuu Tanzania Bara wanatarajia kumaliza hasira zao kwenye michuano ya ndani.

Kabla ya kipigo hicho cha aibu, Yanga walipata ushindi wa bao 1-0 wakiwa nyumbani na hivyo kuhitajika kupata ushindi au sare ya aina yoyote ili kusonga mbele.

Mbali na mechi za ligi, Yanga wanarejea nchini huku wakihitaji pia kutetea kombe lao linaloandaliwa na Shirikisho la Soka la Tanzania (TFF) maarufu Azam Sports Federation Cup ambalo tayari Azam FC, Simba  na Mbao FC wameingia hatua ya nusu fainali.

Katika mashindano hayo, Yanga wanatarajia kukutana na Tanzania Prisons Mei 6, mwaka huu katika Uwanja wa Taifa jijini Dar es Salaam.

Meneja wa Yanga, Hafidh Saleh, alisema timu hiyo imerejea jijini kwa mafungu ambapo kundi la kwanza liliwasili jana usiku na jingine leo mchana wakitokea Algeria.

“Tunashukuru Mungu tumemaliza salama ingawa matokeo hayakuwa mazuri, tumewasili jana usiku na wengine watawasili leo mchana baada ya jana kulala Dubai,” alisema Hafidh.
Viewing all 104698 articles
Browse latest View live




Latest Images