Quantcast
Channel: UDAKU SPECIAL
Viewing all 104689 articles
Browse latest View live

Huyu Hapa Muuza Madawa ya Kulevya Aliyependwa na Wananchi Mpaka Kupewa Jina la Yesu na Mlinzi wa Amani

$
0
0

TAJIRI WA UNGA AKAWA MWEMA MPAKA AKAITWA YESU

Christopher Coke a.k.a Dudus, ni tajiri wa dawa za kulevya, akiongoza genge la Shower Posse.

Genge hilo na mtandao mzima wa unga, Dudus au President alirithi kutoka kwa baba yake, Lester Coke a.k.a Jim Brown au Ba-Bye aliyeuawa gerezani mwaka 1992.

Shower Posse makao makuu yake yapo Tivoli Gardens, Kingston, Jamaica.

Dudu alikuwa mtu mwema. Alisaidia fedha familia maskini, alilipia ada wanafunzi ambao wazazi wao hawakuwa na uwezo, zaidi alitengeneza ajira nyingi kwa vijana.

Hayo yalisababisha apendwe sana. Dudus aliitwa Rais wa Tivoli Gardens, alilindwa na kila mwananchi. Serikali ya Jamaica pia ilimlinda, maana alikuwa mfadhili wa viongozi.

Marekani ilitaka Dudus akamatwe lakini Serikali ya Jamaica haikutekeleza.

Dudus alipokamatwa na Marekani mwaka 2010, kwananchi wa Jamaica, hususan wakazi wa Tivoli Gardens, waliingia mitaani na kuandamana, wakitaka Dudus aachiwe huru.

Wananchi walikuwa na mabango yaliyoandikwa kuwa Dudus ni mlinzi wa amani ndani ya Tivoli Gardens, hivyo aachiwe. Wapo waliokwenda mbali zaidi na kuandika kwamba kumkamata Dudus ni sawa na alivyokamatwa Yesu kwa sababu ni mtu safi.

Wananchi wa Jamaica, hasa wa wakazi wa Tivoli Gardens, walikuwa hawaambiwi kitu kuhusu Dudus. Tuhuma zote za kuhusika na dawa za kulevya, waliona ni uzushi.

Ijumaa ya Juni 15, 2012, Mahakama ya Kuu ya New York, ilimhukumu Dudus kifungo cha miaka 23 jela. Miaka 20 ikiwa kwa kosa la kupanga njama na kufanya biashara haramu na miaka mitatu kwa kosa la kuuza bunduki Marekani bila utaratibu.

Sheria ya Marekani ni kufilisi mali zote za wauza dawa za kulevya pindi wanapokutwa na hatia, lakini imekuwa vigumu kumfilisi Dudus, maana uwekezaji wake wote ameufanya Jamaica ambako Serikali inamlinda.

Hata sasa, genge la Shower Posse linaendelea na kazi ya usafirishaji wa bangi, cocaine na silaha kwenda Marekani, japokuwa bosi wao yupo jela.

Ipo hofu kuwa hata baada ya Dudus kumaliza kifungo jela, huenda Serikali ya Marekani isimwachie huru kwa sababu ya hofu kwamba atarudi kazini kwake na kuzidi kuwaangamiza Wamarekani kwa kuwauzia dawa za kulevya na silaha haramu.

Huyo ndiye Dudus wa Tivoli
By @luqmanmaloto

Tanesco - Watanzania Anzeni Kusahau Mgao wa Umeme..!!!

$
0
0

SERIKALI kupitia TANESCO imefanya uwekezaji mkubwa katika Sekta ya umeme Nchini ambao haujawahi kutokea Katika Historia ya uwekezaji katika Sekta ya Umeme. 

Miongoni mwa Miradi mikubwa ya umeme inayotekelezwa ni pamoja na upanuzi wa Kinyerezi I, ujenzi wa Kinyerezi II, Kinyerezi III, Kinyerezi IV, Malagarasi Mkoani Kigoma, Lusumo Falls Mkoani Kagera, Kikonge Mkoani Luvuma, Mkoani Mtwara na mingine mingi.

Kwa upande wa miradi ya ufuaji umeme, Sekta binafsi nayo haikuachwa nyuma katika harakati za ufuaji na usafirishaji umeme Nchini, Kwa kuzingatia kuwa azma ya Serikali ni kufikia ufuaji wa umeme wa Megawati 5,000 ifikapo 2020 na Megawati 10,000 ifikapo 2025. Kwa kuzingatia hilo Serikali ilianzisha mkakati maalum wa kuongeza uwekezaji katika miradi ya kuzalisha umeme ambayo inatekelezwa kwa kushirikiana na Sekta binafsi kutoka ndani na nje ya Nchi.

Sekta binafsi imeshirikishwa katika miradi midogo ya Nishati Jadidifu (Renewable Energy) yenye MW 16.29, imetekelezwa na Sekta binafsi, nayo ni Miradi midogo ya kuzalisha umeme wa maji (Min Hydropower) ambayo ni Uwemba- MW 0.84, Mwenga MW 4, na Yori MW 0.95, na Miradi midogo ya kuzalisha umeme kwa kutumia tungamo taka (Biomass) ni Tanwat MW 1.5 na TPC MW 9.0.

Aidha, Katika kuhakikisha kwamba Taifa linapata umeme wa uhakika, Serikali imeendelea kufanya jitihada mbali mbali za kuongeza na kuimarisha mtandao wa usafirishaji na usambazaji umeme, (National Grid) unaounganisha Nchi nzima kwa kutekeleza miradi mikubwa ya ujenzi wa njia za kusafirisha umeme kwa ajili ya kuhakikisha upatikanaji wa umeme wa uhakika katika maeneo mengi ya nchi yetu.

Mradi wa kuunganisha Nchi za Tanzania – Uganda (Mwanza – Masaka 220 KV) ambao utaboresha hali ya umeme kwa Kanda ya Ziwa, Ujenzi wa njia kuu ya kusafirisha umeme ya msongo wa Kilovolti 400 kutoka Mkoani Iringa hadi Shinyanga, Mradi wa ujenzi wa njia kubwa ya umeme ya 400KV kutoka Singida - Arusha – Namanga, mradi huu utawezesha kuboresha kwa kiasi kikubwa upatikanaji wa umeme wa uhakika kwa Mikoa ya Kaskazini.

Miradi mingine ni Mradi wa ujenzi wa njia ya 220 KV (Western spur.) utakaoanzia Tunduma, Sumbawanga, Kigoma mpaka Kyaka, mradi huu utaunganisha katika Gridi ya Taifa, Mikoa ya Songwe, Rukwa, Kigoma mpaka Kagera na hivyo kuboresha hali ya umeme katika kanda ya Magharibi, Mradi wa Chalinze hadi Arusha, Kanda ya Kaskazini (North West Grid), Mradi wa Njombe, Songea na Mbinga (South west Grid), mingine ni ya uzalishaji umeme ya Kinyerezi (Megawati 240), Luhudji (Megawati 400) na mingineyo, Uboreshaji umeme jijini Dar es Salaam, City Centre-Dar es Salaam na Electricity V.

kutokana na uwekezaji huo mkubwa,na uboreshaji wa Miundombinu unaofanywa na TANESCO, hakutakuwa na upungufu wa umeme Nchini, Mwaka 2015 Nchi ilikuwa na upungufu wa umeme wa jumla ya Megawati 300, na maeneo mengine yalikuwa na hali mbaya hususan Mwanza, Arusha na Kilimanjaro lakini kwa sasa hali ya umeme katika Mikoa yote na mingine ni nzuri na hakuna upungufu wa umeme na kama ikitokea umeme umekatika ni matatizo ya kiufundi katika eneo dogo na kwa muda mfupi.

Sambamba na uwekezaji unaoendelea, TANESCO imeongeza juhudi za kusambaza umeme kwa Watanzania wengi zaidi kote Nchini, maeneo ya Mijini na Vijijini. Aidha, katika Takwimu mpya za kiwango cha utumiaji wa umeme Nchini zilizotangazwa na Waziri wa Nishati na Madini Prof. Sospeter Muhongo ambazo zilizotayarishwa na Wakala wa Taifa wa Takwimu (NBS) kwa kushirikiana na REA, TANESCO na Wizara ya Nishati na Madini zinaonesha hadi kufikia Desemba 2016: (i) Watu wenye fursa ya kutumia umeme Nchini (Overall National Access Level) ni 67.5% (2007: ilikuwa 10%) ambapo Vijijini ni 49.5% (2007: ilikuwa 2%) na Mijini ni 97.3%.

Serikali kupitia TANESCO pia inaendelea kuhimiza Wananchi kuunganisha Huduma ya umeme katika maeneo yao ya Vijijini hii ni baada ya utekelezaji wa Miradi Kabambe ya REA kufanikiwa kwa kiasi kikubwa ikilinganishwa na kasi ya Wananchi ya kuunganisha Huduma ya umeme.

Mradi Kabambe wa Kusambaza Umeme Vijijini Awamu ya Tatu (REA TURNKEY PHASE III) ambao umeshaanza kutekelezwa. Mradi huu utatekelezwa kwa kipindi cha miaka 5 katika Vijiji 7,873 vya Wilaya zote za Tanzania Bara. Takribani Vijiji 7,697 vitapelekewa umeme wa Gridi ya Taifa na Vijiji 176 umeme wa nje ya Gridi (Off-grid).

Mpango huu utaongeza wigo wa usambazaji umeme katika maeneo ambayo hayakufikiwa na Mradi wa REA II (Turnkey Phase II)

Breaking News..Mchepuko Wafia Gest Siku ya Pasaka...

$
0
0

Mtu mmoja amefia nyumba ya wageni "Lodge" hapa Magomeni Kagera eneo maarufu kama "Friends Corner "Lodge ya Jumba la Dhahabu ,Haijafahamika mpaka sasa kama ni Mwanaume au Mwanamke, ILA kwa tetesi za watu wanadai ni mwanamke na Polisi hawakuweza kuzungumzia swala hili wala kuonesha mwili

Pichaaa..Hivi Ndivyo Watu wa Koromije Walivyojisosomola kwa Pilau la Pasaka..!!!

Picha Mpya za Vanessa Mdee Akiwa Beach..Zinazozungumziwa Mitandaoni

Kilichokuwa Kinasubiriwa na Dunia Nzima Sasa Kimetimia..

$
0
0

Nijambo la kushukuru Mungu, kwa tukio la kuhadhimisha skukuu ya Pasaka limemalizika salama !....Tuwaombee kwa wale waliopata matatizo ya hapa na pale bila kusahau wagonjwa wote...

Mambo Si Mambo..Kuelekea Vita na Korea Kaskazini..Marekani Waamua Kutumia Helment Hizi Ghali Zaidi Duniani..Moja Inauzwa Milioni 900..!!!

$
0
0

Marubani wanaotumia ndege za kivita za Marekani F-35 stealth fighter watakuwa wakitumia helmet ghali zani duniani. 

Kupitia helmet hii, rubani ataona kila kitu cha dunia kinachoonwa na camera za ndege.

Bei ya helmet moja ni dola za Marekani 400,000 sawasawa na milioni 900 za Kitanzania.

Usidharau..Kabla ya Kufunga Ndoa au Kusexy KavuKavu na Mpenzi Wako Hakikisha Mmepima Haya Magonjwa 4 ya Kuambukizwa...!!!

$
0
0

1. Ugonjwa wa kaswende.
Kitaalamu kama syphilis, huu ni ugonjwa hatari sana ambao umeharibu maisha ya watu wengi bila wao kujifahamu. Ugonjwa huu ambao huambukizwa kwa njia ya kujamiana huanza kidogo na kidonda ambacho hakiumi sehemu ambapo wadudu wamepita mfano mdomoni au sehemu za siri. 

Kidonda hicho hupona, upele usiowasha hutokea na baadae vyote hivyo hupotea. Ugonjwa huu baadae huingia ndani ya mwili na kuuanza kuharibu viungo vya ndani. Mwisho kabisa ugonjwa huu huahamia kwenye ubongo na kumfanya mtu kua kichaa.
  
2. Ugonjwa wa hepatitis B.
Ugonjwa huu ni hatari na unaua haraka kuliko ukimwi, virusi vya ugonjwa huu huambukizwa kwa njia ya kujamiana na kugusana kwa damu au majimaji ya mwili kama ukimwi lakini ni rahisi zaidi kuambukizwa ugonjwa huu kuliko kupata ukimwi. 

Ugonjwa huu hushambulia maini na kuacha makovu, Mgonjwa hupata macho ya njano, homa, maumivu ya kichwa na kadhalika. Ugonjwa hii mwishoni hupelekea kansa ya ini ambayo inaua ndani ya miezi sita.

3. Ugonjwa wa ukimwi.
Huu ni ugonjwa unaofahamika kwani unatangazwa sana hasa kwenye vituo vya Radio, Tv, Magazeti na sehemu mbalimbali.

Ugonjwa huu uligundulika karne ya 20 na mpaka sasa umeshaua watu wengi sana na zaidi ya 95% ya wagonjwa waliambukizwa kwa kushiriki ngono bila kinga. 

4. Ugonjwa wa gonorea.
Huu ni ugonjwa wa zinaa ambao unashambulia jinsia zote yaani Wanaume na Wanawake, mara nyingi Mwanaume hawezi kujificha na ugonjwa huu kwani dalili za ugonjwa huo kama kutoka na usaa kwenye njia ya kukojolea zitamuumbua lakini kwa wananwake ugonjwa huu huweza kukaa kimya na mwana mke hujikuta akisambaza ugonjwa huo bila kujua. Mwishoni ugonjwa huu hushambulia kizazi na kusababisha ugumba.

Snura Ajipanga Kumuanika Laazizi Wake

$
0
0
DAR ES SALAAM: Staa wa mduara Bongo, Snura Mushi ‘Snusexy’ amefunguka kuwa, baada ya ukimya wa muda mrefu na kuzushiwa kila mwanaume, sasa anajipanga kumuanika laazizi wake ili watu wamtambue kwani usumbufu umekuwa ‘too much’.

Snura aliliambia Wikienda kuwa, ishu ya kuambiwa mara anatoka na mtu fulani, mara na Mwarabu ni suala linalomsababishia usumbufu hivyo mashabiki wake wakae mkao wa kula kwani kuna kitu kikubwa anataka kukifanya katika kumtambulisha mwanaume anayetoka naye.

“Soon nitawatambulisha shemeji yao maana naona ni miaka miwili sasa nasingiziwa mambo mengi, mara yule mara huyu lakini wasiwe na wasi kwani kuna kitu kikubwa kinakuja,”  alisema Snura.

Hii Hapa Fiada ya Kumnyonya Mpenzi Wako Uume Kabla ya Tendo.

$
0
0

Utafiti uliofanywa na jopo la madakitari kutoka Hospitali ya Chuo kikuu cha Hopkins (JHU) wakiongozwa na Dr. Carl Walker toka Chuo Kikuu cha madakitari cha Yenepoya Medical College, Canada 🇨🇦, kimeeleza kuwa wanaume wanaonyonywa nyeti zao (uume) wana nafasi nzuri ya kupata watoto wenye afya njema na uwezo mkubwa wa kinga dhidi ya magonjwa (immune response capability).

Utafiti huwa unabainisha pia kuwa, kitendo hicho cha mwanaume kunyonywa humfanya mwenye furaha zaidi, na hivyo uchamgamfu wake huzifanya pia mbegu kutoka /kumwagika zikiwa zimechangamka, hivyo kuwa na uwezekano mkubwa wa kupata mtoto mwenye akili na afya njema.

Zaidi ya hayo, utafiti huo umeeleza kuwa mbegu za mwanaume aliyenyonywa kabla au wakati wa tendo la ndoa pia ni kinga ya magonjwa kwa mwanamke anayekojolewa mbegu hizo ukeni, kwani huwa zina protein Za kutosha na hulainisha ngozi na kumfanya mwanamke awe na uso mwang’avu.

Utafiti huu unatokana na kuonekana wanawake wengi wanaotumia kondom au kutoruhusu kukojolewa ukeni kupata magonjwa zaidi ikiwemo fibrosis zaidi ya wanawake wenye kunyonya uume na kujiachia. Vilevile imebainika kuwa wanaume wenye kunyonywa wana nafasi kubwa ya kuendelea na urijali zaidi ya wale wasionyonywa!

Matumizi ya Bangi Kuidhinishwa Kenya

$
0
0
ZAIDI ya Wakenya 1,400 wanaunga mkono ombi la kutaka kuidhinishwa kwa matumizi ya mmea wa bangi baada anayewasilisha hoja hiyo kuwawasilisha ombi lake mbele ya bunge la seneti.

Iwapo ombi hilo la mtafiti Gwada Ogot litaidhinishwa haitakuwa haramu kupanda ama hata kuuza bangi nchini Kenya.

Gwada Ogot anasema kwamba matumizi ya kiafya pamoja na utumizi wa mmea huo viwandani unaojulikana kwa jina la sayansi kama Cannabis sativa una faida nyingi.

Anasema kuwa matumizi ya mmea huo yataimarisha hali ya uchumi.

Sheria ya Kenya inapiga marufuku utumizi wowote wa bangi na kwamba mtu yeyote atakayepatikana akitumia dawa hiyo atashtakiwa kwa uhalifu.

Ogot anaomba bangi kuondolewa miongoni mwa orodha ya vitu haramu na kutaka sheria mpya kuanzishwa ili kuweka bodi simamizi ya utumizi wa mmea huo.

Ukweli Ndio Huu..Wanawake Ndio Hufaidi Tendo la Ndoa..Ila Wengi Ndio Huishia Kudhulumiwa..!!!

$
0
0

Somo langu la leo ni juu ya wanawake  kuenjoy zaidi tendo la ndoa. Nikwambie tu kuwa kati ya mwanamke na mwanaume linapokuja swala la kufaidi na kufurahia sex basi ni mwanamke ndio anafaidi zaidi.

Lakini cha kusikitisha ni kuwa wanawake wengi hudhulumiwa raha hii na wengi wao; sababu kubwa ikiwa wanaume wengi hawajui jinsi ya kuwapa raha wanawake lakini pia kwa wanawake wao wenyewe kutokuwa wazi na kujieleza vema kwa wenzi wao.

Mwanaume kwake sex ni sex haina mashiko yoyote ndio maana ni rahisi wao kukojoa hata kwa punyeto , kulala na kichaaa , wasaidizi nyumbani , yaani hoe hae. Akishakojoa basi akili inabadirika kwenda kwenye mambo mengine. Wao huendeshwa na kutamani zaidi.

Mwanamke kwake sex ni hisia – Mwanamke hawezi fanya sex na mtu kama hana feelings nae na kama ikimlazim afanye kwa maslai mengine basi atafanya tu kumridhisha huyo mtu na yeye apate anachotaka ila sio kwa ajili ya kufurahia tendo la ndoa. Kwa mwanamke sex is LOVE and FEELINGS

Wanaume wanakuwa wao ndio wa kwanza kujiona wanapenda sex ila ukweli ni kuwa wanawake wanapenda sex zaidi ya wanaume ila kutokana na mazingira na malezi wanawake huficha hisia zao ila huzifungua wanapopata partner muelewa na kupelekea wao kuenjoy tendo.

Hapa sina cha kukwambia nini ufanye maana wa kufundishwa ni mwanaume. Ila usijali sana nitakuja na waraka mwingine wenye maelezo ya nini cha kufanya kuweza kusaidiana na mwenzako

Hivi Wajua Mav*zi na Ndevu ni Urembo Muhimu Kwako..Soma Hapa Ujue kwa Kina

$
0
0

Je wajua kuwa nywele za chini aka mavuzi na ndevu ni urembo wa kimahaba?

Mwenyezi Mungu alituumba na kutuwekea hivyo akiwa na maana kabisa ila sasa binadamu wa leo wamestaarabika kiasi waonaona ndevu au mavuzi ni uchafu tena uchafu sana. Mwanaume akiwa na ndevu anaonekana mchafu sana, Au ikiwa ni mwanamke wa mwanaume na uvuzi mwingi basi mchafu.

Ntakupa mifano michache kwa wanyama

Hivi wajua kule porini kama ni SIMBA dume na halina minywele ya kutosha Simba jike hasisimki na hivyo hali mzigo

Hivi wajua hata ndege pori DUME huwa na minyoya ya kutosha na ile humpendezesha kushawishi majike

Hivi wajua hata samaki – Kama unafuga samaki hata wale wa urembo je wajua dume lazima liwe na matezi mengi mengi

Hivi wajua hata Mbwa wetu hawa akiwa siku za kupata mimba yakaja madume mengi atachagua lile lenye manywele mengi

Kwa mifano hiyo utakuwa umenisoma kiduchu.

Mwanamke kikawaida hana ndevu ila vuzi lipo… Linatakiwa lipendeze ila sio kusafisha kiwanja kinakuwa cheupeeee basi tukupe dawa zisiote tena maana huzitaki na hujui kazi yake.

Mwanamke uwe wazinyoa kwaa style ile ya kupunguza tu na ndio maana mwezi wako anatakiwa kukusaidia. Au kama kuna salon za kunyoa huko basi sio waxing bali kuzipunguza kifashion….

Kwanza ukiwa unapunguza tu hautakaa upate taizo la in-grow hair na kufanya pussy iwe na mapeleeee mabalaa duniani. Mipele inafanya pussy inakuwaa na vidoti vyeusi.

Mwanaume anatakiwa kuwa na ndevu ile ziwe ninakwatwa kwa uzuri ili kupendezesha asiache kama Alshabab – Na hata kule chini anatakiwa kupungusa kwa sehemu za kende ndio amalize ile juu ya dyudyu ndio anaacha kiasi tena ikibidi kwa style mahususi aipendayo malkia wake.

Ndevu – kidogo zatumika kukuna mgongo wa mwanamke – Imagine akiwa anakupumulia kwa nyuma alafu anakukuna na kidevu sehemu za shingo hahahha bye……

Ugomvi wa Gwajima na Makonda Wamfikia Askofu Mkuu wa KKKT..Ajiingiza na Kuibuka na Hoja Hizi Kuntu..!!!

$
0
0

Sakata la Gwajima na jina la Daudi Bashite limeendelea kutikisa maeneo mbalimbali hapa nchini ambapo Askofu  (mstaafu)  wa kanisa la  kiinjili la  Kilutheri  Tanzania (KKKT)  dayosisi ya  Iringa Dkt. Owdenburg Mdegella amefunguka  na kuwataka wananchi kujikita katika shughuli za  kiuchumi badala ya kupoteza muda  mwingi  kujadili  mambo  ya  Daud Bashite.

Askofu Mdegella alisema hayo wakati  akitoa  salama  za Pasaka  jana katika  usharika  wa kanisa kuu, ambapo alidai kuwa watanzania wanapoteza  muda  mwingi kwa jambo hilo badala ya  kushughulika na mambo ya msingi yenye  tija kwa  Taifa .

Alisema kwa wiki tatu watu wanajadili Bashite na Gwajima badala ya kufanya kazi kwa kuwa Gwajima na Bashite wote wametoka Mwanza hivyo wanajuana vizuri.
Alisistiza kama kuna mtu  amedandia  vyeti  atakamatwa  kwa  utaratibu   na kuwataka watu wengine kujikita katika kufanya kazi.


CAG: Mkataba wa Mlimani City na Chuo Kikuu cha UDSM ni Wizi Mtupu..!!!

$
0
0

RIPOTI ya Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali (CAG), imeanika madudu ya mkataba wa Chuo Kikuu cha Dar es Salaam (UDSM) kwenye mradi wa Mlimani City.

Madudu hayo yanaonyesha namna chuo hicho kinavyopoteza mamilioni ambako amependekeza mkataba huo ufanyiwe marekebisho.

Kwa mujibu wa ripoti hiyo iliyowasilishwa bungeni hivi karibuni, ujenzi wa mradi wa Mlimani City ulianza Oktoba Mosi mwaka 2004, ukikadiriwa kukamilika Septemba Mosi mwaka 2016.

Hata hivyo, CAG ameshauri yafanyike marekebisho katika baadhi ya vifungu vya mkataba huo.

Ripoti hiyo inaonyesha kwamba moja ya sababu ya kukiukwa maeneo ya mkataba wa wabia hao wawili ni uzembe wa menejimenti ya chuo.

Ripoti inasema: “Tulibaini kwamba mradi mdogo wa hoteli ya nyota tatu (ambayo ina vyumba 100 kikiwemo chumba cha mikutano kinachochukua watu 1,000) na uboreshaji wa bustani ya botania, ikiwa ni sehemu ya mradi wa Mlimani City, haujakamilika kwa kipindi cha miaka 10 tangu tarehe ya makubaliano ya kumaliza mradi.

“Mtazamo wangu ni kuwa hakuna ufuatiliaji wa karibu, usimamizi na tathmini ya mkataba huo kwa uongozi wa Chuo Kikuu cha Dar es Salaam.

“Kwa sababu hiyo kuna uwezekano wa kushidwa kumalizia kazi iliyobaki kwa sababu ya ongezeko kubwa ya gharama ya kumalizia mradi tangu kipindi kilichopangwa kupita.

“Menejimenti ya Chuo Kikuu inashauriwa kuuangalia upya mkataba iliouingia na Mlimani City Holding, kuharakisha umaliziaji wa miradi,” ilieleza ripoti hiyo ya CAG.

Ripoti hiyo pia inaainisha ukiukwaji wa ulipaji wa ada ambayo mwekezaji anatakiwa kuitoa kwa Chuo Kikuu cha Dar es Salaam.

Kwa mujibu wa kifungu cha 1.1(j) cha mkataba pamoja na kifungu 10.1 cha hati ya ukodishaji wa uwanja, Chuo Kikuu cha Dar es Salaam kinapaswa kipate asilimia 10 ya mapato ya kodi ghafi.

“Kinyume na kufungu tajwa hapo juu, Mlimani Holding Limited (MHL), hufanya hesabu za gawio la kodi ya Chuo Kikuu kwa kuzingatia asilimia 10 ya mapato ya kodi baada ya kutoa gharama za uendeshaji badala ya kujumuisha gharama za uendeshaji.

“Ukiukwaji huu unakifanya Chuo Kikuu cha Dar es Salaam kuwa katika hatari ya kupoteza kiasi kikubwa cha mapato kutoka katika mradi wa Mlimani City,” inasema ripoti hiyo.

CAG anaishauri menejimenti ya chuo hicho ifanye upya hesabu za gawio lake la asilimia 10 kutokana na mkataba na kuomba kulipwa na mpangaji kiasi kilichokuwa kimekosewa.

Pia alishauri kuwasiliana na mpangaji na kufikiria kubadilisha mkataba kuweka vifungu ambavyo vitaruhusu idara ya ukaguzi ya ndani ya chuo kuangalia mapato na gharama za uendeshaji za mradi.

Ripoti hiyo pia imeainisha udhaifu wa ufuatiliaji na usimamizi wa mapato kutoka kwa wapangaji wadogo kwenye mradi huo.

Inasema kifungu cha 11.2(l) cha hati ya makubaliano, mpangaji (MHL) anapaswa kutopangisha mtu yeyote ambaye hajathibitishwa na Mpangishaji (Chuu Kikuu cha Dar es Salaam), ikiwa ni njia ya kudhibiti mapato yake.

Kinyume na makubaliano ya hayo, ukaguzi wa CAG umebaini kwamba MHL amepangisha majengo kwa wapangaji wengine bila kupata kibali cha Chuo Kikuu cha Dar es Salaam.

“Kuna upungufu wa utekelezaji wa vipengele vya mkataba kwa upande wa Chuo Kikuu cha Dar es Salaam hivyo kusababisha Chuo kushindwa kujua kwa usahihi mapato ya kodi kutoka kwa wapangaji wote.

“Menejimenti ya Chuo Kikuu cha Dar-es-salaam inashauriwa kutekeleza vifungu na vipengele vyote vya hati ya makubalian ya upangaji kikiwamo kifungu 11.2 (l) cha hati ya makubaliano ambacho kinakitaka Chuo Kikuu cha Dar es Salaam kuwathibitisha wapangaji wadogo wadogo,” anashauri CAG.

Ripoti hiyo pia inaonyesha mapitio ya mkataba wa upangishaji wa ardhi kati ya Chuo Kikuu cha Dar es Salaam na Mlimani Holding Limited yamegundua kwamba mkataba haumpi mmiliki wa ardhi haki ya kukagua kazi zinazofanywa na mpangaji.

“Katika hali hii, mpangishaji, ambaye ni Chuo Kikuu cha Dar es Salaam hawezi kujua endapo mpangaji, Mlimani Holding Limited, anakiuka mkataba katika uendeshaji au kuna baadhi ya wapangaji wa nyumba hawawekwi wazi na mpangaji huyu,” inasema ripoti.

CAG anashauri Chuo Kikuu cha Dar es Salaam kuwasiliana na Mlimani Holding Limited kupata haki ya kukagua shughuli za miradi kwa manufaa ya pande zote mbili.

Ripoti hiyo inasema pia kwamba mapitio ya mkataba yamegundua mkataba huo hauelezei hali halisi ya ugawanaji mali mkataba utakapoisha (miaka 50 au 85 kutokana na makubaliano ya pande mbili).

“Hakuna makubaliano yoyote yanayoelezea mgawanyo wa mali na miondombinu itakayokuwapo wakati mkataba unaisha.

“Kwa hali hii, kuna uwezekano wa kutokea mvutano wa sheria mwisho wa mkataba. Hali hii ikitokea, Chuo Kikuu kitakosa msaada wa sheria.

“Uongozi wa Chuo Kikuu cha Dar es Salaam, unashauriwa kuingia katika mazungumzo na Mlimani Holding Limited kuweka vifungu vitakavyoonyesha haki ya kila upande wakati wa mkataba utakapoisha,” anaeleza CAG.

Ripoti hiyo pia inasema Chuo Kikuu cha Dar es Salaam ( kiliingia katika makubaliano na kampuni ya Ernest and Young kufanya ukaguzi maalumu kujua kiasi cha mapato ambacho kinaidai kampuni ya Mlimani Holding Limited katika kipindi cha Mei Mosi mwaka 2006 mpaka Juni 30 mwaka 2014 na kubaini kutolipwa dola za Marekani 57,607.

“Wakati wa ukaguzi niligundua kuwa kiasi cha Dola za Marekani 309,458 kilitakiwa kipokelewe na Chuo kutoka MHL, lakini usuluhisho wa hesabu ulionyesha MHL ililipa Dola za Marekani 213,850 kupitia uhamisho wa benki kwa njia ya eletroniki na kubakisha Dola za Marekani 57,607.

“Kuna ufuatiliaji duni kwa upande wa menejimenti ya Chuo Kikuu cha Dar es Salaam katika kukusanya deni hilo. Menejimenti ya Chuo Kikuu cha Dar es Salaam inashauriwa kuongeza nguvu katika kufuatilia na kukusanya deni wanalolidai MHL,” inasema ripoti hiyo.

CCM Yatoa Onyo kwa makada wake Wanaolalamika Baada ya Kutumbuliwa na Rais...!!!

$
0
0

Chama cha Mapinduzi (CCM) kimeibuka na kukemea vikali kauli zinazotolewa na viongozi au makada wa chama hicho wambao wametenguliwa na Rais Dkt John Pombe Magufuli katika nafasi zao mbalimbali walizokuwa wakishikilia.

Katibu wa Halmashauri Kuu ya CCM (NEC), Siasa na Uhusiano wa Kimataifa, Kanali Mstaafu Ngemela Lubinga aliyasema hayo juzi akizungumza Mjini Iringa katika mkutano na wanafunzi wa vyuo vikuu vilivyomo mkoani humo ambao ni wananchama na pia viongozi wa chama hicho katika ngazi ya matawi na kata.

Lubinga aliwataka makada hao walioteuliwa na kisha kutemwa na Rais Dkt Mwagufuli ambaye pia ni Mwenyeketi wa CCM Taifa, kuacha kulalamika na kupiga kelele badala yake wakubiliane na mabadiliko hayo kwa nia ya kuheshimu maamuzi ya Ikulu kwa uamuzi uliochukuliwa dhidi yao.

Licha ya kuwa kiongozi huyo hakutaja majina ya viongozi aliowataka kuheshimu maamuzi ya Ikulu, lakini ni dhahiri kuwa miongoni mwa waliolengwa ni Mbunge wa Mtama (CCM), Nape Moses Nnauye ambaye alitenguliwa katika nafasi yake aliyokuwa ya Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo nafasi aliyoitumikia kwa kipindi cha miezi 15.

Nape alitenguliwa katika nafasi hiyo ikiwa ni saa chache tu tangu alipopokea ripoti ya kuvamiwa kwa kituo cha Clouds Media Group ambapo ripoti hiyo ilithibitisha kuwa Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam ndiye aliyehusika katika tukio hilo.

Nafasi ya Nape ilichukuliwa na aliyekuwa Waziri wa Katiba na Sheria, Dkt. Harrison George Mwakyembe ambaye naye nafasi yake ikajazwa na Mbunge wa kuteuliwa na Rais, Prof. Palamagamba Aidan John Kabudi ambaye ni mbobezi katika taaluma ya sheria.

Mwingine ambaye licha ya kuwa hakuenguliwa na Rais moja kwa moja lakini alionyesha kutoridhishwa na mchakato wa kuenguliwa kwake ndani ya CCM ni aliyekuwa Mbunge wa Bunge la Afrika Mashariki, Shyrose Bhanji. Yeye alienguliwa alipotaka kugombea kwa mara ya pili, na tangu hapo amekuwa akilalamika kwa madai  kuwa njia zilizotumika hazikuwa za haki.

Hizi Hapa Sababu 15 za Kwanini Chai ya Tangawizi ni Muhimu Kwako Kila Siku..!!!

$
0
0

Hakuna ambacho kinaongeza joto katika mwili wa binadamu wakati wa baridi kama chai ya tangawizi.

Kutokana na kiwango chake cha juu cha Vitamin C, magnesiamu na madini mengine, tangawizi ni ya manufaa sana kwa afya ya bianadamu.

Tangawizi ni mmea ambao hutumika kama kiungo na pia hujulikana kwa sifa yake ya kutumika kama tiba.

Inaweza kutumika kama unga,kama mafuta, juisi au chai.

Tangawizi inafahamika sana kwa sifa yake ya ajabu ya kutibu magonjwa.

Tangawizi ni nzuri kutumiwa kama chai, tangawizi ni chanzo kizuri cha vitamini na madini kama vile vitamini C na magnesiam.

Kuna faida nyingi utakazozipata kwa kunywa chai ya tangawizi:

1. Huzuia Magonjwa ya Mtingishiko
Chai ya Tangawiziinawezakuzuiakutapika na kumaliza maumivu ya kichwa.

Pia inazuia kichefuchefu kinachotokana na mitingishiko ya safari za gari,meli au ndege.

Hivyo kunywa kikombe kimoja cha tangawizi kitaweza kusaidia kuepuka kichefuchefu na kutapika.

2. Inazuia Mchafuko wa Tumbo
Chai ya Tangawizi inasaidia mmengenyo wa chakula tumboni hivyo kuongeza kunyonywa kwa chakula tumboni na kuzuia maumivu ya tumbo yanayotokana na kula chakula kingi.

Pia huongeza hamu ya kula.


3. Hupunguza Uvimbe

Tangawizi chai inaweza kupunguza uvimbe wa viungo unaojulikana kama rheumatoid arthritis.


4. Hupambana na Magonjwa ya Kupumua.

Unashauriwa kunywa tangawizi kama unasumbuliwa na magonjwa ya kupumua kama vile mafua na kikohozi.


5. Huchochea Mzunguko wa Damu 

Kunywa kikombe cha chai ya tangawizi kunaweza kukusaidia kuboresha mtiririko wa damu, kama vile kusaidia kuzuia mafua na homa.


6. Huongeza Kinga za Mwili

Chai ya Tangawizi ina chemikali za antioxidants zinazosaidia kuboresha mfumo wa kinga.

Kunywa kikombe cha chai ya tangawizi kila siku kunaweza pia kusaidia kuondokana na hatari ya kiharusi kwa kuzuia mafuta katika kuta za mishipa ya damu

Tangawizi pia imeonyesha mafanikio katika kupunguza viwango vya rehani (Chorestrol) na kuzuia kansa.


7. Hutuliza Msongo wa Mawazo

Tangawizi ina uwezo mkubwa wa kupunguza msongo wa mawazo kwa harufu yake nzuri ya kuvutia.


8. Inapunguza Matatizo ya Tumbo:

Inachochea kasi ya mmengenyo wa chakula kwa kuchangia kutolewa kwa asidi katika tumbo. Tangawizi inaweza kutumika kushughulikia tatizo la kukosa choo.


9. Husaidia Katika Kupunguza Maumivu:

Tangawizi chai inaweza kupunguza maumivu ya mwili na misuli.

Kunywa kikombe chachai ya tangawizi kila siku kunaweza kusaidia kuzuia maumivu yamisuli pia kusaidia kupunguza uchovu wa mwili.


10. Husaidia kwa Kuondoa Ugonjwa wa Asubuhi

Husaidia kupungua kichefuchefu kwa akinamama wajawazito kunakotokakna na ugonjwa wa asubuhi kwa kizungu “Morning Sickness”


11. Huboresha Nguvu za Uzazi kwa Wanaume

Tangawizi inasaidia kuboresha mbegu za kiume na nguvu za uzazi kwa wanaume kama ikitumiwa mara kwa mara. Pia inasaidia kutibu upungufu wa nguvu za kiume.


12. Kupunguza Uzito wa Mwili:

Tangawizi inasaidia sana katika kupunguza uzito wa mwili. Inasaidia kuunguza mafuta ya ziada katika mwili.


13. Kuongeza hamu ya Kula

Tangawizi inasaidia kuongeza hamu ya kula kwa kuchochea kutengenezwa kwa asidi za kumengenya chakula katika tumbo.

14. Husaidia kutoa Gesi.
Tangawizi inasaidia kutoa gesi chafu tumboni kwa njia ya asili.


15. Inasaidia Kupumua Vizuri.

Tangawizi inasaidia kufungua njia ya hewa na kukufanya upumue vizuri. Unaweza kuitumia baada ya kula kama kiburudisho pia.

Wanawake wajawazito na wale wenye tatizo la kutokwa na damu kirahisi wanashauriwa kupata ushauri wa Daktari kwanza kabla ya kutumia  chai ya Tangawi

Siku Kadhaa Baada ya Kuteuliwa Mbunge..Mchungaji Rwakatare Amefanya Haya Makubwa Kanisani Kwake..!!!

$
0
0

Mchungaji  Kiongozi wa Kanisa la Mlima wa Moto  lililopo Mikocheni B,  Assembles of God, Dk. Getrude Rwakatale, amemshukuru Rais Dk. John Magufuli kwa kumkumbuka na kumteua katika nafasi ya ubunge wa Viti Maalumu.

Dk, Rwakatale alitoa shukrani  hizo Dar es Salaam jana wakati alipozungumza katika kanisa hilo wakati wa ibada ya Sikukuu ya Pasaka.

“Leo (jana) tunasherehekea kumbukumbu ya kufufuka kwa mwokozi wetu Yesu  ambaye alitufia pale msalabani,… Pasaka ya mwaka huu ni yangu, Mungu ameniona.

“Nina furaha ya mwili na roho kwa sababu Yesu amefufuka na pia Mungu amenirudisha bungeni, Mungu amejibu maombi yetu, tulifunga siku tatu na ile ya mwisho akajibu,”  alisema Mchungaji Rwakatale.

Alisema ana kila sababu ya kumshukuru Rais Dk. Magufuli kwa sababu  wapo wanawake wengi ambao angeweza kuwachagua na kuwapa nafasi hiyo.

“Nakishukuru pia Chama Cha Mapinduzi (CCM) kwa kunikumbuka, wapo wanawake wangapi lakini leo mlima wa moto katikati ya maombi, Mungu ametenda,” alisema.

Dk. Rwakatale alitumia ibada hiyo kuwaomba msamaha watu aliowakosea huku akiwasihi waungane naye kumshukuru Mungu katika maombi.

“Katika Luka 24:1-9 tunasoma habari kuhusu ufufuko wa Yesu, tumezoea makaburini huwa kuna habari mbaya lakini kwa Yesu ilikuwa tofauti, ilikuja habari njema.

“Alitangaza msamaha hata alipokuwa msalabani basi naomba mnisamehe nilipokosea maana na mimi ni mwanadamu,”  alisema.

Aprili 14, mwaka huu Tume ya Taifa ya Uchaguzi (NEC),  kupitia kwa Mkurugenzi wa tume hiyo, Ramadhan Kailima ilitangaza jina la Mchungaji Rwakatale kuwa mbunge baada ya Chama cha Mapinduzi (CCM) kupeleka jina lake.

 Tume ilipitia  fomu zake na kuridhika kuwa mteule huyo ana sifa za kuwa mbunge akichukua nafasi ya Sophia Simba ambaye alivuliwa uanachama na chama chake.

Machi 11, mwaka huu, Sophia Simba ambaye alikuwa Mwenyekiti wa Umoja wa Wanawake wa CCM (UWT) alivuliwa uanachama kwa madai ya ukiukwaji wa maadili ya chama hicho na hivyo kumfanya kukosa sifa ya kuendelea kuwa mbunge kwa mujibu wa Katiba ya Tanzania.

Mavoko: Nimeamua Kuja na Mtindo wa Kuimba Utakaokuwa Wangu Peke Yangu

$
0
0
Rich Mavoko amesema anaendelea kutengeneza mtindo wa kuimba utakaomfanya asifanane na msanii yeyote.

Ameiambia Bongo5 kuwa mtindo huo aliuanzisha kama majaribio kwenye Kokoro na baada ya kuona watu wameuelewa, ameuboresha zaidi kwenye wimbo mpya aliofanya na Harmonize, Show Me.

“Nilikuwa natamani nipate style ambayo haifanywi na watu wengine Bongo, kama nilivyofanya kwenye Kokoro na kwenye verse ya Show Me,” Mavoko ameiambia Bongo5. “Soko pia linahitaji ubunifu, hata ninachokifanya ni sehemu ya ubunifu sababu nimejaribu kubadilika,” ameongeza muimbaji huyo huku akielezea kuwa ngoma zijazo zitadhihirisha zaidi anachokisema.

Kuhusu wimbo Show Me, Mavoko amesema yeye alianza kuwa na wazo na kisha kumshirikisha Harmonize aliyetengeneza msingi.

“Sababu mimi ndiye nilikuwa nina wazo, picha nzima nilikuwa naijua Harmonize alivyoanza verse ya kwanza alinifungua baadhi ya vitu kwamba mimi ntafanya hivi, na wewe utafanya vile.”

Aliyemtolea Nape Bastola Yamfika Hapa..Habari Vichwa vya Magazeti ya leo 18/4/2017..!!!

Viewing all 104689 articles
Browse latest View live




Latest Images