Quantcast
Channel: UDAKU SPECIAL
Viewing all 104415 articles
Browse latest View live

Point Of Understand..Gigy, Utaacha Lini Ulimbukeni ....!!!?

0
0

Ni jambo zuri na la kheri kumkumbuka mtu unayemfahamu, unayemmiss na hata unayempenda, maana hilo ndilo Mwenyezi Mungu ametufundisha.

Katika barua yangu ya leo, nimemkumbuka mdogo wangu, dada yangu, ambaye amebahatika kujipatia jina mjini baada ya kuonekana kwenye video za wasanii wa Muziki wa Kizazi Kipya, wenyewe wanajiita mavideo queen, Gift Stanford maarufu kama Gigy Money.

Hii ni mara yangu ya kwanza kukuandikia barua, ingawa vioja vyako nimekuwa nikiviona sana kwenye vyombo mbalimbali vya habari, hasa mitandao ya kijamii na magazeti. Nikaanza kuwaza na kuwazua, inakuaje kwa mtindo wa picha za utupu ambazo umekuwa ukizipiga, hivi una wazazi kweli?

Una kaka, dada, shangazi, wajomba, baba wadogo na wakubwa kweli? Pamoja na kwamba huu ni ulimwengu wa digitali, sidhani kama huyu binti anastahili kufanya anavyofanya, maana ni kama vile kichwa chake hakijatulia vizuri. Na inanishangaza pia kama mdogo wangu huyu bosi wake ni mtu wa namna gani, maana hata kama haya ni maisha binafsi, baadhi ya mambo yanaharibu ‘image’ ya kampuni anayoifanyia kazi.

Pengine ni kama vile watu wa masoko wanavyosema, biashara matangazo. Huenda kuna biashara nisiyoijua anaitangaza, lakini naona kuna athari kubwa zaidi ya matangazo yake hayo kuliko faida anayoitaraji. Mimi kama kaka yako, naomba nikupe ushauri huenda ukakusaidia siku zijazo. Wewe mwenyewe unaweza kuona kuwa ni ujanja kupiga hizo picha na kuzitupia kwenye mitandao, kwa sababu hivi sasa wale wanaume wakware watakutafuta na kumalizana, hivi unajua kesho itakuwaje?

Sasa hivi unaweza usione tatizo, lakini amini ninachokuambia, kesho na keshokutwa huwezi kuolewa wewe. Nani atataka kuoa mwanamke wa aina yako, kama leo hii umeshafikisha zaidi ya umri wa miaka 18 unajitandaza mitandaoni, utashindwa kufanya hivyo ukiwa na umri wa kuolewa?

Na heshima ya mwanamke iko kwenye uhifadhi wa mwili wake, sasa kama wewe una heshima gani wakati kila mtu anaujua mwili wako ulivyo? Nahisi unasumbuliwa na ulimbukeni.

Hata hivyo, ulimbukeni siyo ugonjwa ni hali tu ya muda inayomtokea mtu yeyote, hasa anapokutana na vitu ambavyo hakuwahi kuwaza kama atakutana navyo. Pengine hakuwahi kuwaza kuwa siku moja watu watajua kuna Gigy, kama yeye alivyokuwa akiwasikia mastaa wakivuma wakati huo yeye akiwa hajulikani. Na kwa jina alilolipata, anadhani kwamba sasa yupo katika anga nyingine.

Hapana mdogo wangu, wewe bado mchanga sana katika anga za masupastaa, bado unahitaji make-ups za kutosha ili ukae meza kuu. Punguza ulimbukeni, kidogokidogo utakuja kukaa sawa. Jaribu kutafuta, hivi ni staa gani alifanikiwa katika maisha yake kwa sababu ya kupiga picha za utupu hapa Bongo?

Na niwakanye wadogo zangu wengine ambao mna mawazo ya kuja kuwa kama Gigy, heshima kubwa ya mwanamke iko ndani ya mwili wake, kadiri anavyouhifadhi ndivyo thamani yake inavyopanda.

Na kama wewe ni mzuri, utabakia kuwa hivyo hata kama utashinda ndani ya vazi la hijabu. Hata hao wanaume wenye tamaa za mwili hivi sasa, wanakudharau na kukuona kama chombo cha starehe kinachosubiri muda kuekspaya.

Na kwa akili hizi za kujiachia utupu namna hiyo, siamini kama unajua hata kuwekeza ili kufidia maisha ya muda mchache ujao utakapokuwa umekwisha habari yako.

Harmorapa Hana Heshima Kabisa....Amchana Live Master J

0
0
Msanii wa 'hip hop' nchini Harmorapa amemchana mtayarishaji mkongwe wa muziki wa Bongo Master J kwa kusema hamtambui wala hadhani kama kama anaweza kuwa miongoni mwa 'Producer' walioweza ku-hit kwa ngoma kali Bongo.

Harmorapa anayetamba na wimbo wake wa 'Kiboko ya mabishoo' amefunguka hayo baada ya kutokea maneno makali ya mtayarishaji huyo kuwa Harmorapa hana kipaji cha muziki na kwamba si msanii bali analazimisha.
Kauli hiyo ya Master J ilionekana kuwachukiza baadhi ya wadau wa tasnia hiyo mpaka kupelekea meneja wake ambaye ni P. Funk kuingilia kati jambo hilo.
Harmorapa ambaye leo alikuwa kwenye kipindi cha KIKAANGONI kupitia ukurasa wa facebook wa EATV, ameulizwa kuwa anaichukuliaje kauli ya producer Master J, ambapo katika jibu lake, amesema kauli hiyo haimsumbui kwa kuwa anaamini kuwa ana kipaji, na kwa kuwa yupo kwenye mikono salama ya P Funk, anaamini atafanya makubwa kama walivyofanya wasanii wengine akiwemo Juma Nature.
Amekwenda mbali zaidi na kumpa makavu Master J kuwa si producer wala hamtambui kuwa miongoni mwa ma-producer wakali Bongo maana hakuna kazi yoyote aliyofanya ika-hit kama ilivyo kwa P Funk

"Kwa kaui ya Master J, sikujisikia vibaya kwa sababu najua kuwa mimi ni msanii, na rap kama wanavyorap wasanii wengine, yeye hamjui mtu kwamba baadaye anakuwa nani, ndiyo maana hata Majani ambaye yuko juu yake aliniona akajua mimi nina kitu akaniita akanielekeza.......Huyo Master J anaongea hivyo, hana ishu, hivi ni nani yule, mimi simjui, na sijui kama ni producer, naona hajui chochote na sijui kazi yoyote ambayo ime-hit kupitia mikono yake tofauti na ilivyo kwa P Funk..." Amesema Harmorapa
Akitaja wasanii anaowakubali zaidi Bongo, amesema kwa upande wa hip hop anamkubali zaidi Fid Q na upende wa kuimba anamkubali zaidi Alikiba. Kwa upande wa wasanii wa nje, amesema anamkubali za Lil Wayne, huku akimwagia sifa Diamond Platnumz kwa kuitangaza vyema Tanzania kimataifa

Akizungumzia mafanikio aliyonayo mpaka hivi sasa tangu ajulikane, amesema kubwa kuliko yote ni heshima anayopatiwa na watanzania hata wale ambao hawakuamini kama ni msanii kweli, pia fursa ya kuaminiwa na kushauriana na wasanii wakubwa Bongo kama Juma Nature, Prof Jay n.k.
Pia amesema mafanikio mengine ni fursa ya kufanya kolabo na msanii kutoka nchini Ubelgiji anayefahamika kwa jina la Critical, ambapo amesema Mbelgiji huyo alilazimika kumlipa pesa Harmorapa ili kufanya naye kolabo.
Kwa upande wa vitu, amesema mpaka sasa anamiliki nyumba na gari aina ya Morano yenye thamani ya shilingi milioni 35, ambavyo alipewa kama zawadi na bosi wake.
Ametumia nafasi hiyo pia kueleza jinsi ambavyo P Funk Majani amefanya kazi kubwa ya kubadili mtindo wake wa ku-rap, kutoka mtindo wa kizamani hadi ku-rap kisasa huku akimtia moyo na kuchukua jukumu la kumtengenezea ngoma.

UKIMYA wa Mwanamuziki Naj Watia Mashaka...Je Baraka The Prince Kamnyima Kufanya Muziki? Jibu Lipo Hapa

0
0
Mwanamuziki wa bongo fleva ambaye pia ni mpenzi wa Baraka The Prince, Naj amekanusha kukatazwa kufanya kazi za muziki na mpenzi wake huyo ambaye naye ni mwanamuziki na kudai usimamizi wa biashara za familia ndiyo unaomuweka kuwa 'busy'


Naj ameyasema hayo hivi karibuni baada ya kuulizwa juu ya ukimya wake kwenye sanaa na kama mapenzi ndiyo yanayomnyima kufanya kazi zake.
"Watu hawajui, its not him, mimi mara nyingi kwenye muziki wangu huwa naachaga gap na ni kwa sababu huwa si-focus na muziki pia kama kwa sasa nimeingia mkataba na kina JB wa ku-shoot tamthilia, season 1 tayari kwa sasa tunaendelea na season 2 lakini kitu kingine ni family business ambazo mimi nikiwa huku ndiyo mtu ninayezisimamia nikiondoka ndipo ninapata muda wa kufanya muziki na mambo mengine mengi" alisema Naj
Kwa upande mwingine Naj amesisitiza kuwa Baraka ndiye mtu ambaye anamsisitiza sana kufanya ngoma na katika wimbo mpya anaotarajia kuachia siku za karibuni mpenzi wake huyo anamchango mkubwa

VIDEO: Steve Nyerere Ayasusia Maandamano ya Bongo Movie na Makonda, Aanika Haya!

0
0
KUFUATIA maandamano ya wasanii wa Filamu nchini, Bongo Movie, ambao wameandamana leo katika mtaa wa Aggrey Kariakoo  wakipinga uingizwaji wa filamu za nje na urudufishwaji wa filamu za ndani huku wakiwataka wamachinga wanaouza filamu hizo waache mara moja, msanii wa tasnia hiyo Steve Mengele Nyerere amefunguka kuhusu kutoonekana kwenye tukio hilo.

Akifanya mazungumzo LIVE na Global TV Online, Steve ameeleza kuwa sababu ya yeye kutoungana na wasanii wenzake kuandamana ni kwa kuwa jambo hilo halioni kama lina tija kwake.




“Binafsi ninalipinga hili, wasanii tunataka kutumika ndivyo sivyo, siwezi tu kuambiwa kuwa kuna maandamano nikaenda.


“Tunavyosema filamu za nje zinazuia soko la ndani ni uongo, hizi filamu za nje tangu tunazaliwa zilikuwepo, tumewakuta akina Arnold Schweziniger na Rambo, filamu zao zilikuwa zinauzwa Kariakoo. Tulichukua majority yao tukatengeneza filamu zetu. Tuliwakuta Nigeria tukashindana nao tuaweza, hata za filamu za Kihindi tuliweza kushindana nazo.


“Hatujawahi kumzuia Yemi Alade afanye muziki hapa nchini ijapokuwa tuna wanamuziki wetu akina Diamond na Ali Kiba.


“Nachoweza kusema ni kwamba turudi tuangalie ni wapi tumeharibu, tuache kuingiza visingizio ambavyo havina mantiki. Wafanyabiashara Kariakoo wanauza filamu zinazouza na siyo uzalendo.


“Watanzania tumezoea kukaa mezzani na siyo maandamano. Utazuia Dar, je vipi kuhusu Arusha, Dodoma, Mwanza nk… hili janga sio la Dar es Salaam pekee ni la Tanzania nzima.


“Mpaka sasa msambazaji ni mmoja, kaelemewa mzigo, serikali iruhusu wasamazaji wengine waingine kwenye biashara hii.”


“Tumeshindwa kutengeneza radha ya Watanzania, tusiwaadhibu wafanyabiashara, tujiadhibu sisi wenyewe kwa kutengeneza filamu zisizouza.” Alisema Steve Nyerere.

Spika Ndugai Ahoji Jina la Bashite Bungeni..Habari Vichwa vya Magazeti ya Leo 20/4/2017..!!!

Barca, Dortmund Zatupwa Nje Mabingwa Ulaya..!!!!

0
0

BARCELONA na Borussia Dortmund zimetupwa nje ya michuano ya Ligi ya Mabingwa Ulaya baada ya kushindwa kupenya kwenye mechi za robo fainali ilizocheza dhidi ya Juventus na AS Monaco. 

Barcelona iliyocheza na Juventus ilitupwa nje kwa jumla ya mabao 3-0 baada ya sare ya 0-0 kwenye mechi ya jana Jumatano huko Nou Camp, huku Borussia Dortmund wao wakitupwa nje kwa jumla ya mabao 6-3 baada ya kuchapwa 3-1 usiku huo wa jana. Katika mechi za kwanza za hatua hiyo ya robo fainali, Barca ilichapwa 3-0 Turin, Italia wiki iliyopita wakati Dortmund wao walichapwa 3-2 kwao Ujerumani.

Rais Magufuli, Makomandoo Kupamba Sherehe Za Miaka 53 ya Muungano Dodoma

0
0

Maonesho ya ukakamavu na mbinu za medani katika kupambana na adui hasa kulinda amani ya nchi yetu kutoka Kikosi Maalum cha Makomandoo wa Jeshi la Wananchi Tanzania (JWTZ), itakuwa ni sehemu ya shamrasha zitakazopamba maadhimisho ya miaka 53 ya Muungano yatakayofanyika kwa mara ya kwanza mjini Dodoma Aprili 26 mwaka huu.

Kwa mujibu wa taarifa iliyotolewa na Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu Sera, Bunge, Ajira, Kazi, Vijana na Watu Wenye Ulemavu, Jenista Mhagama maadhimisho hayo yanatarajiwa kuhudhuriwa na Rais Dkt. John Pombe Magufuli, pia yatapambwa na burudani nyingine kutoka vikundi mbalimbali.

Taarifa ya Waziri Mhagama ametaja shughuli nyingine zinazotarajiwa kufanyika siku ya Muungano kuwa ni gwaride la heshima lililoandaliwa na vikosi vya ulinzi na usalama (JWTZ,JKT, Polisi na Magereza) na onesho la mbwa na farasi waliofunzwa.

Aidha, Waziri Mhagama aliongeza kuwa mambo mengine yatakayofanyika ni gwaride la uzalendo la wanafunzi wa shule za sekondari za Dodoma, burudani za vikundi vya ngoma za asili kutoka Dodoma na Zanzibar, Yamoto Band, vikundi vya muziki wa kizazi kipya kutoka kwa wasanii Mchungaji Zayumba, Jacob Beats, Mwenge Jazz Band na Mgosi Maturumbeta.

“Kauli mbiu ya sherehe za kutimiza miaka 53 ya Muungano wa Tanganyika na Zanzibar ni Miaka 53 ya Muungano; Tuulinde na Kuumarisha, Tupige Vita Dawa za Kulevya na Kufanya Kazi kwa Bidii,” alifafanua Waziri Jenista Mhagama.

Ametoa wito kwa wananchi wote nchini kusherehekea siku hiyo muhimu kwa kudumisha amani, upendo, umoja na mshikamano kwa maendeleo ya nchi.

“Ninaomba kuchukua nafasi ya pekee kuwaomba wananchi wote waliopo Dodoma kujitokeza kwa wingi uwanja wa Jamhuri siku hiyo ya Jumatano tarehe 26 Aprili 2017 kuanzia saa 12:00 asubuhi ili kusherehekea kwa pamoja maadhimisho hayo muhimu kwa nchi yetu,” alisema Jenista Mhagama.

Maadhimisho ya Muungano yanafanyika kwa mara ya kwanza Dodoma ikiwa ni siku kadhaa tangu Serikali ya Awamu ya Tano ianze kutumiza azma ya kuhamia katika makao makuu hayo mapya

Sakata la Mzazi Kuibiwa Mtoto Hospitali ya Temeke Lachukua Sura Mpya..Aliyempima Azua Utata Mpya..!!!

0
0

Sakata la Asma Juma (29) anayedai kuibiwa pacha wake, limechukua sura mpya baada ya uongozi wa hospitali binafsi ya Huruma kusisitiza kuwa mtaalamu aliyechukua vipimo vya utrasound amekuwa akifanya kazi hiyo hata kwa mwajiri wake ambaye ni Serikali.

Kauli hiyo inapingana na iliyotolewa na Mganga Mkuu wa Hopsitali ya Temeke, Amani Malima kwamba daktari aliyemfanyia Asma vipimo hivyo hana utaalamu huo na kwamba yeye kazi yake ni kupiga picha za x-ray na amekuwa akifanya vipimo vya ultrasound kama njia ya kumweka mjini.

Hospitali ya Temeke ndiyo inadaiwa na Asma kwamba imehusika na wizi wa mtoto wake mmoja baada ya ujauzito wake kuonyesha alikuwa na mapacha.

Lakini, jana Mganga Msimamizi wa Zahanati ya Huruma, Dk Erasmo Kuwendwa akiwa ameambatana na daktari aliyemfanyia mama huyo vipimo hivyo, alisema wana uhakika na vipimo vyao.

Dk Kuwendwa alisema kuwa mama huyo alifika katika zahanati hiyo na kufanya vipimo hivyo mara mbili na kwamba mara zote hizo alibainika ana mapacha na kwamba wote walikuwa na afya njema.

“Mara ya kwanza alifika hapa Februari 17 mwaka huu, alifanyiwa kipimo cha ultrasound na majibu yaliyoonekana ni kwamba ana mapacha ambao wote walikuwa salama na walikuwa na umri wa wiki 33.” alisema Dk Kuwendwa na kuongeza:

“Lakini pia Asma Juma alifika tena hapa Machi 7, mwaka huu, pia alifanyiwa kipimo hicho hicho na mtaalam wetu na kilichoonekana ni kwamba ana mapacha wenye umri wa wiki 36.”

Dk Kuwendwa alisema taarifa hizo ndizo zilizoko kwenye kumbukumbu zao na kwamba baada ya kufanyiwa vipimo hivyo mtaalam wao huwa anaandika ripoti na kisha anabandika na picha (image) za vipimo vya kile alichokiona.

Kuhusu taarifa za daktari aliyefanya vipimo hivyo kutokuwa na utaalam, Dk Kuwendwa alisema:

“Ninachojua mimi ni kwamba huyu mtaalam wetu aliyefanya hivyo vipimo ni mwajiriwa wa Serikali, ndani ya Manispaa ya Temeke, anafanya kazi Hospitali ya Mbagala Rangi Tatu, na huko anafanya x-ray, anafanya ultrasound na ni muda mrefu.”

Alisisitiza kuwa anaamini kuwa mtaalam huyo ana uzoefu na anajua kwamba ameajiriwa na Serikali kufanya kazi hizo hizo.

Alisema anashangaa kuwa picha za ‘ultrasound’ zimepotea na kusema kuwa hizo ndizo zingeleta majibu.

Wakati mkanganyiko huo ukitokea kamati iliyoundwa kuchunguza sakata hilo imemaliza kazi na kukabidhi ripoti kwa Mganga Mkuu wa Serikali, Mohamed Kambi.

Mganga Mkuu wa Hopsitali ya Temeke, Amani Malima jana alisema: “Tunasubiri tu majibu ya ripoti toka kwa waziri mwenye dhamana ila ripoti tayari imekabidhiwa kwa Mganga Mkuu wa Serikali ambaye pia ataipeleka kwa waziri kwa ajili ya hatua stahiki,” alisema Dk Malima.

Alisema kamati hiyo iliundwa na Mganga Mkuu wa Serikali kwa agizo la Naibu Waziri wa Afya Maendeleo ya Jamii Jinsia Wazee na Watoto, Dk Hamis Kigwangalla baada ya kupata malalamiko kutoka kwa mwanamke huyo.

Alisema kamati ilifanya uchunguzi kwa muda wa wiki moja imekabidhi ripoti Ijumaa ya wiki iliyopita.

Hata hivyo, juhudi za kumpata Dk Kingwangala hazikufanikiwa baada ya simu yake kutopokelewa kwa siku nzima ya jana.

Asma ambaye alijifungua kwa njia ya upasuaji kwenye Hospitali ya Temeke Machi 17 na kuambiwa alikuwa na mtoto mmoja, alidai vipimo alivyofanyiwa kwenye Zahanati ya Huruma pia madaktari wawili wa Temeke walivithibitisha kwamba ujauzito wake ni wa watoto mapacha.

Alidai licha ya madaktari hao wawili kujiridhisha, lakini baada ya kufanyiwa upasuaji, alipewa mtoto mmoja.

Asma na mumewe Aboubakar Pazi walisema wamewasilisha madai yao kwa uongozi wa hospitali na uchunguzi unafanywa.     

Raia wa Kigeni Nchini Wapewa Siku 90..!!!

0
0

Idara ya Uhamiaji nchini Tanzania imetoa siku 90 kwa wageni kufanya uhakiki wa vibali vya ukaazi ili kuimarisha udhibiti wa wageni wanaoishi nchini pamoja na kuzuia mianya ya upotevu wa maduhuli ya serikali.

Akizungumza jijini Dar es Salaam Kamishna Jenerali wa Uhamiaji Dkt. Anna Makakala baada ya uzinduzi wa mfumo wa uhakiki kwa kutumia njia ya kielekroniki amesema mfumo huo ni rahisi na unatoa fursa kwa waajiri na wageni wote wenye vibali vya ukaazi kuhakiki kumbukumbu za vibali vyao ili kujua kama vimetolewa na mamlaka husika.

Dkt. Makakala amezitaka taasisi na mashirika binafsi baada ya kuhakiki vibali vya wageni wao watatakiwa kuwasilisha taarifa za vibali hivyo katika ofisi za Idara ya Uhamiaji za mikoa zilizopo karibu na ofisi hizo ambapo amesema baada ya muda huo kuisha wale wote ambao hawajahakiki hatua za kisheria zitachukuliwa dhidi yao.

Bandeji Inayotumia Teknolojia ya 5G Yatengenezwa..Inauwezo wa Kutuma Taarifa za Maendeleo ya Kidonda Kwenye Simu..!!

0
0

Bandeji ambazo zinaweza kutambua jinsi kidonda kinavyopona na kutuma ujumbe kwa daktari itafanyiwa majaribio katika kipindi cha miezi 12 ijayo.

Bandeji hizo zitatumia teknolojia ya 5G kufuatilia na kutambua ni matibabu ya aina gani yanahitajika kwa mgonjwa.

Majaribio hayo yanafanywa na taasisi ya Sayansi ya chuo cha Swansea huko Wales nchini Uingereza.

Bandeji hii inatumia teknolojia inayofahamika kama nano, kutambua hali ya kidonda cha mgonjwa wakati wote.

Kisha itaunganisha kidonda na mfumo wa 5G kupitia kwa simu ya mkononi na kuonyesha vitu kadhaa kuhusu mgonjwa, kama eneo alipo na hali yake.

Wakati taarifa hiyo yote inakuja pamoja, teknolojia hiyo kisha itatambua aina ya matibabu mgonjwa ambayo anahitaji kuyapata.

MAKUBWA! Baby Madaha na Isabela Wahisiwa Wanasagana

0
0
Kioja! Mastaa wawili wasioishiwa vituko wanaounda Kundi la Muziki la Scorpion Girls, Baby Madaha na Isabela Mpanda, wikiendi iliyopita waliwaacha watu midomo wazi baada ya kujiachia kimahaba kama mtu na mpenziwe.

Baby Madaha na Isabela walilishana keki kwa staili ya njiwa ‘kugusanisha midomo’ ikiwa ni kwenye sherehe ya bethidei ya Isabela iliyofanyika katika Hoteli ya Belinda iliyopo Mbezi Beach jijini Dar.


Akizungumza katika ishu hiyo, mmoja wa wahudhuriaji ambaye hakutaka jina lake litajwe gazetini, alisema tukio hilo ni la kushangaza kwani linaashiria kuna kitu kingine nyuma ya pazia kwa wasanii hao marafiki wa muda mrefu.

“Kiukweli Isabela na Baby wamenishangaza sana, maana kulishana huko keki kama mtu na mpenzi wake inaashiria kuna kitu nyuma ya pazia, inawezekana wenzetu ni wapenzi wa jinsia moja (wasagaji), maana siyo kwa ukaribu huo tena hadharani, hawaogopi hata watu tuliopo hapa jamani, kweli dunia imevaa koti,” alisema mmoja wa wahudhuriaji.


Alipoulizwa Isabela kulikoni kulishana keki na Baby kama wapenzi, alisema jambo hilo ni la kawaida tu kwa kuwa ni marafiki na hakuna kitu kingine chochote kinachoendelea kati yao. “Sisi ni marafiki na tumeshakuwa kama ndugu hivyo kulishana keki hivi kwa mdomo ni upendo tu na hakuna mambo ya usagaji kama wengi wanavyohisi wala nini,” alisema Isabela.

Na GLADNESS MALLYA/GPL

UREMBO: Pendezesha Mwili Wako Kwa Kutumia Bidhaa Toka Kwa Kessy Products..Ngarisha Ngozi na Kuongesha Shape

0
0
PENDEZA NA KESSY PTODUCT:-MSIMU MPYA% WA 2017_OFFA YA BIDHA AINA ZOTE KWA UBORA MZURI

PATA DAWA NA MAFUTA YA ASILI ZISIZO NA MADHARA WALA KEMIKALI, NA  MATOKEO NI KWAHARAKA BAADA YA WEEK (1)ADI( 3-4) 🍎🍌🍉🍑🍍🍓🍒🍏🍇

1) KUTOA MVI SUGU PIA ZA KUZALIWA NAZO _80,000/
2) KUREFUSH NYWELE  KUZIJAZA NA KUZUIAKUKATIKA _80,000/
3) TENGENEZA SHEPU YAKO FIGA UMBO (8) NA KUJAZA HIPC NA KALIO @ KUPAK _70,000/
@ KUNYWA AU VIDONGE _130,000/  4) KUPUNGUZA NYAMA ZA MIKONO TUMBONI ZILIZOTEPWETA _80,000/
5) PUNGUZA KITAMBI KWA HARAKA KWA DAW HIZI ZA KUNYWA
@) KUNYWAA _10,0000/
@) VIDONGE  _10,0000/
6) PUNGUZA MWILI MZIMA KUANZIA KGM 150 ADI 80 KIASI UNACHOTAK WEWE KWA DAW HIZI
@) DAW YAKUNYWA YA KUCHANGANYA NA MAJI AU JUYC _130,000/
@) VIDONGE VYA HARAKA _130,000/
7) PUNGUZA MAZIWA NA YASIMAME KWA MUDA WA WEEK MOJA _70,000/
8) ONGEZA MAZIWA NA SAIZ UNAYOTAKA WEWE _70,000/
9) ONGEZA MWILI MZIMA NA KUKUPA HAMU YAKULA KWA RIKA LOLOYE _80,000/
10) TOA MICHIRIZI SUGU PIA NA ILE YAKUJIFUNGUA MWILI MZIMA _70,000/
11) TOA MAKOVU, CHUNUSI, WEUSI KATIKATI YA MAPAJA _60,000/
12) TOA NGIRI YA AINA ZOTE _70,000/
13) KUWA MWEUP  NA SOFTI MWILI MZIMA NA KUTOA WEUS MACHON NA VIMISHIPA VIDOGO VIDOGO @ MAFUTA YA KUPAKA _80,000/(@) VIDONGE (WHITE SOLUTION) _120,000/
14) ONDOA  NDEVU NA VINYWELEO MWILINI _80,000/
15/ ONGEZA NGUVU ZA KIUME NA KUIMARISHA MISHIPA ILIYO LEGEA KWA DAW HIZ
@) JEL KUPAKA (MEN GEL) _70,000/
@) VIDONGE (MAXMAN) _80,000/
16) ONGEZA MAUMBIL YA KIUME SAIZI UNAYOITAKA WEWE KWA:
@) (HANDSOME UP) MASHINE _170,000/
@) JELI YAKUPAKA INABORESHA ANZIA NCHI (4 ADI 6 )_100,000/ PIA NA VIDNGE VYAKE VIPO
17) RUDISHA HAMU YA TENDO LA NDOA KWA WALIOPOTEZA KUTOKANA NA NGIRI, KISUKARI NA MAGONJWA MENGINE KWA  _80,000/
18) RUDISHA USICHAN(BIKRA)Na KUTO UCHAFU SEHEMU ZA SIRI _80,000/
19) FANYA USO WAKO KUWA MKAVU NAKUTOA VIJIPELE ILIYOSABABISHWA NA MAFUTS MAKALI _80,000/
20) ONDOA  SUGU KWENYE VIDOLE, MAGOTI, NA SEHEMU ZOTE ZILIZOARIBIWA NA LOSHEN _60,000 (21) TENGENEZ MGUU WAKO NA KUTOA KIGIMBI NA KUWA MZURI NAWAKUPENDEZA _70,000/ 22) MIKANDA YA KUPUNGUZA TUMBO PIA HIPO @ MONALISS _80,000/ @( MICROO)MASHINE WA UMEME _20,0000 @ MKANDA WENYE DAW (NYONGA STAILL) _170,000/

   PIA UDUMA NYINGINE ZIPO

TUNAPATIKAN K/ KOO NA SINZA
 MAPAMBAN, KWA MIKOAN T UTATUMA KWA MABAS YOTE, NA  KWA ZANZBR UNGUJA PIA TUNATUMA  KWA BOT ZOTE

 KWA MAWASILIANO PIGA
                                      
(+255) 0719955528
0756259180
0785371237

@dr_kessy_product


Delivery KWA DAR E SALAAM INAKUFIKIA POPOTE ULIPO, HUDUMA HIZI ZINAPATIKA DUNIAN KOTE  POPOTE ULIPO

IKULU: Rais Magufuli Apokea Ujumbe Kutoka kwa Kagame. Akubali Kupeleka Rwanda Walimu wa Kiswahili..!!!

0
0

Rais Magufuli leo amepokea ugeni kutoka kwa Rais Kagame wa Rwanda na kuzungumza nao Ikulu, Dar es Salaam.

Rais wa Tanzania Dkt. John Magufuli amepokea barua yenye ujumbe wa Rais wa Jamhuri wa Rwanda Mhe. Paul Kagame iliyowasilishwa kwake na Mjumbe Maalum ambaye ni Waziri wa Elimu wa Rwanda Dkt. Musafiri Papias Malimba.

Pamoja na kupokea barua hiyo, Mhe. Rais Magufuli na Dkt. Musafiri Papias Malimba wamezungumzia masuala mbalimbali ya ushirikiano kati ya Tanzania na Rwanda ikiwemo katika sekta ya elimu hususani maendeleo ya sayansi na teknolojia.

Aidha, Mhe. Rais Magufuli ameipongeza Rwanda kwa kuamua lugha ya Kiswahili ianze kufundishwa katika shule zake na ameahidi kuwa Tanzania ipo tayari kutoa walimu wa kwenda kufundisha lugha hiyo.

WAZIRI Mkuu Abariki Utaratibu wa TRA Kusaka Wadaiwa Sugu wa Kodi kwa Kutumia Mtutu wa Bunduki..!!!

0
0

Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa ameibariki Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA) kuendelea kuwatumia TAKUKURU pamoja na Jeshi la Polisi wenye silaha za moto wakati wanapokwenda kukusanya mapato pamoja na kodi kwa wafanyabiashara ambao ni wanadaiwa sugu.

Akijibu swali la Mbunge wa jimbo la Arusha Mjini Godbless Lema katika kipindi cha maswali kwa Waziri Mkuu Bungeni Mjini Dodoma, amesema ni sahihi kwa kikosi kazi hicho (task force) kutumika kwa kuwa wapo baadhi ya wafanyabiashara sugu wenye lengo baya la kutotaka kulipa madeni na badala yake hutoa rushwa.

Mhe. Lema alitaka kusikia kauli ya serikali juu ya mfumo unaotumiwa TRA wa kusumbua na kuwatisha wafanyabiashara katika shughuli zao za kila siku huku ikiwa inadaiwa kuwa mamlaka hiyo hutumia Jeshi la Polisi, Usalama wa Taifa na TAKUKURU katika miji mikubwa ikiwemo Dar es Salaam, Mwanza , Arusha na Mbeya.

“Ni kweli kwamba tunacho chombo ambacho kinachowajibika katika ukusanyaji wa mapato na kodi kutoka kwa walipa kodi wetu wafanyabiashara wakiwemo, lakini TRA kutumia ‘task force’ haina maana ya kuwatishia amani wafanyabiashara ila lengo lake ni kufuatilia wadaiwa sugu japokuwa siyo wote ila wachache hawataki kabisa kulipa pamoja na kwamba wanajua wao ni wadaiwa sugu..... Tunatumia TAKUKURU kwa sababu kuna wengine hutumia fursa hiyo kutaka kuwahonga maafisa wa TRA ili wafutiwe madeni yao”. Alisema Majaliwa

Vile vile Majaliwa amesema ‘task force’ imeundwa na TRA wenyewe ili kuona wanapokwenda kukusanya madeni yao hakutumiki vitendo ambavyo havikubariki kama vile utoaji wa rushwa ili madeni hayo yasilipwe au namna nyingine yoyote ambayo mfanyabiashara anaweza kuona si sahihi kwake

RAIS Magufuli Akutana na Viongozi wa TUCTA..!!!!

0
0
 Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akiwa katika kikao na Viongozi wa Shirikisho la Vyama vya Wafanyakazi nchini (Trade Union Congress of Tanzania -TUCTA) Ikulu jijini Dar es Salaam April 20, 20

17

JB Aungana na Yusuph Mlela Kumporomoshea Lundo la Maneno Nay wa Mitego..Huu Hapa Ujumbe Aliouandika Leo..!!!!

0
0

Ikiwa ni siku moja toka biashara ya filamu ‘feki’ za nje zipigwe marufuku mpaka pale wafanyabiashara wa filamu hizo watakapokamilisha taratibu za ulipaji wa kodi, mengi yameendelea kuibuka, ikiwa ni pamoja na wasanii ambao walihusika kwenye kampeni hiyo kuambiwa wanatumika kisisasa.

Wasanii hao wakiongozwa na JB, Jumatano hii waliungana na ofisi ya Mkoa wa Dar es salaam kufanya opesheni hiyo ndani ya soko la Kariakoo kwa madai filamu hizo zinawanyonya wasanii wa filamu wa ndani kwa kuwa zinauzwa bila kulipiwa kodi wakati wao filamu zao zinalipiwa kodi.

JB amedai amesikitishwa kuona baadhi ya watu wanalihusisha tukio hilo na siasa.

“Ndugu zangu kuna jambo naomba niongee na nyinyi, hivi mnajua tunayoyalilia ni maisha yetu, kwa nini kila kitu mnahusisha na siasa? Hivi ni haki mimi nitozwe 30% ya pato langu mwingine asitozwe?,” aliandika JB Instagram.

“Kwenye shida mimi sitajali nani ananisaidia ilimradi anagusa maslahi yangu, ugali wangu, ninakiri sinema zetu zina mapungufu mengi lakini hiyo siyo sababu za kuacha kudai haki zetu. Ni kama mgonjwa akiumwa leo anapelekwa kwa mganga kesho anapelekwa kuombewa anatetea roho yake. Nawaomba sana hatukatai mkitusema kuwa movie zetu zina matatizo lakini ngoja tumalize hili, tusichanganye, na pia hakuna aliye sema zifungiwe hapana zifate utaratibu kama sisi tunavyo fata. Hizo hizo movie zetu mbovu ndio zinatuwezesha kuishi,” aliongeza.

“Lakini pia lazima mfahamu biashara hii ni kubwa kuliko mnavyodhania, movie 2 zinanitosha kuishi kwa mwaka mzima, ushawaza ni kiasi gani mimi pamoja na kushiriki mapambano haya ni kama nimemaliza muda wangu kwenye kazi hii nimebakiza movie 1 tu. Je udhani mwanao au ndugu yako naye anaweza kuingia huku?. Tukiiponda tasnia huniharibii mimi tu, unaharibu maisha ya watu wengi wajao ambao watafanya vizuri zaidi yetu,” alifafanua zaidi.

Sakata hili limewagawa wasanii wa filamu nchini mara mbili. Wapo ambao wanaamini njia hiyo itasaidia kukuza tasnia ya filamu huku wengine wakipinga njia hiyo kwa madai kua siyo sahihi kwani filamu za nje zilikuwa nchini toka zamani.

ABDI Banda Sasa Huru Kuitumikia Simba..!!!

0
0

Beki wa Simba Abdi Banda hivi sasa yupo huru kuitumikia klabu yake ya Simba baada ya leo adhabu yake kutangazwa  kumaliza kutumikia adhabu yake . Mchezaji huyo alifungiwa na Bodi ya Ligi baada ya kumpiga ngumi mchezaji wa Kagera Sugar,  George Kavila

Kamati ya nidhamu ilikaa siku ya jana na wakati inakaa tayari mchezaji huyo alikuwa amekosa mechi mbili hivyo kamati ilipitia  na kusikiliza pande zote mbili na kufanya maamuzi kuwa zile mechi mbili ambazo mchezaji huyo alizikosa ndiyo adhabu yake tosha kwa kosa alilofanya.

Awali mchezaji huyo baada ya kufanya tukio hilo ambalo mwamuzi hakuliona, alisimamishwa kucheza ligi kuu kusubiri maamuzi, na akakosa michezo dhidi ya Mbao FC na Toto Africans.

Mchezaji huyo wa Simba ataungana na wachezaji wengine wa klabu hiyo ambao wataingia kambini siku ya Jumapili kujiweka sawa dhidi ya mechi zilizobaki kwenye Ligi Kuu Bara ambazo zinaendelea nchini. 

Almasi Mzambele atoa sababu zilizomtoa WCB

0
0

Licha ya kuamua kukaa kimya tangu aondoke WCB, Meneja Biashara wa Baraka the Prince na Bana Music Records, Almas Mzambele ameamua kuzungumzia hilo akisema hakufukuzwa bali aliamua kuondoka mwenyewe. 

Akijibu baada ya kuulizwa na mtangazaji Adam Mchonvu, Almas alisema mambo matatu aliyoyataja Lord Eyes yaani ubinafsi, wivu na utengano ndio yamesababisha kuondoka kwake WCB. 

”Any way, sikufukuzwa nimetoka, ila kuna mengi japo sijapenda tuzungumzie huko sana. Hapo kwenye ubinafsi ndio point yenyewe, ila tukaushe kwenye hilo.” – Almasi Mzambele.

Mange Kimambi Amshukia Jack Wolper, Ampa za USO Live Bila Chenga

0
0


Mange Kimambi Amshukia Jack Wolper, Ampa za USO Live Bila Chenga ni baada ya Majibizano ya Wolper na Mwigizaji Mwenzake
.
.
#Regrann from @mangekimambi_ - Huyu Wolper nae needs to take Several 💺 💺 .... .
.
Ndo maana bongo movie inakufa, wamejaa mazero brain huko! Kumbe mtu kalipwa 2 million akafanye kazi Alafu anamchamba mtu as if alitoa msaada🤣🤣. Yani anahisi yeye ndo aliemsaidia mwenzie wakati Huyo M2 ndo aliemsaidia yeye kwa kumlipa 2 Million... Huyu dada akili zake ni wereva kwa kweli....🤣🤣
.
.
Alafu kama anajiamini si awachambe Kina Nay na steve Nyerere waliowaita mataahira? Mbona kamfata Huyu mpoleee Tena ambae aliongea kistaarabu Na kwa unyenyekevu mkubwaaaaa, Yani @m2wulfat aliongea kistaarabu kidogo nisiposti video zake Alafu Eti Wolper ndo kaona Huyo ndo wakumchamba. Kama yeye mwanamke kweli amchambe @naywamitego 🙈
.
.
Alafu Eti Sasa hivi anachamba watu Eti waendeleee kuongea Maana ndo wanazidi kusambaza meseji yao.. Hawa bongo movie wanachekesha, hapo hapo wanalia njaaaa wanafosi tununue kazi zao hapo hapo wanatuchamba.... So stupid yani

HIZI Haa Faida Tano za Kiafya za Kulala Bila Kuvaa Nguo(Uchi)..!!!

0
0

1. Utapata usingizi mzuri na mororo.
Kuvaa manguo mengi na kujifunika ma blanket kunaweza sababishia mwili wako joto hivyo uchelewe kupata usingizi mwili unahitaji mazingira cool ili upate kulala.

2. Unaupa mwili wako nafasi ya kupumua.
Kwa sababu muda wote wa mchana tunakua tumevaa nguo, inapofika muda wa usiku ni vyema tukauacha mwili upumue. Hasa kwa wanawake, kuvaa nguo za ndani muda wa kulala kuna sababisha vi bacteria na fungas kuwa traped. Watu wanaolala uchi wapo katika hatari ndogo ya kupata fangas sehemu za siri kuliko wale wanaolala wakiwa wamevaa nguo.

3. Kulala uchi pembeni ya mpenzi wako kunapunguza stress.
kwa wale wana ndoa, kulala uchi kunasababisha miili yenu igusane ngozi kwa ngozi kitu ambacho kinafanya miili yenu isiwe na stress. Pia hupunguza presha ya damu na kufanya muwe relaxed. Bila ya kusahau kulala uchi pembeni ya mtu unaempenda kunakufanya uwe mwenye furaha, hivyo kuwa na afya njema.

4. Utajisikia una ukaribu sana na mwenza wako.
Utafiti uliofanya huko Marekani unaonesha kuwa wanandoa wanaolala uchi huwa wanajisikia wapo karibu sana na wenza wao. Asilimia 57% ya wanandoa wanao lala uchi wame ripoti kuridhika na ndoa zao, huku asimilia 48% ya wanaolala na pajama wame ripoti kuridhishwa na ndoa zao. Kulala uchi kunakufanya ujisikie upo karibu na mwenza wako na pia bond nae zaidi.

5. Kulala uchi kunasaidia katika kupunguza unene (uzito).
Usingizi mbovu husababisha homoni za stress kuongezeka mwilini, na kuongezeka kwa homoni za stress katika mwili kunasababisha mtu uwe unakula vyakula ovyo hasa vile "junk food" ambavyo husababisha watu kuongezeka kilo na unene.


Tahadhari: Kabla hujaanza kulala uchi hakikisha mazingira uliyopo ni salama na yanakuruhusu wewe kufanya hivyo. Kwa mfano wale ambao wanaishi na roommates au ambao wapo hostel si vyema kulala uchi. Hakikisha upo mazingira salama ndio ulale uchi.
Viewing all 104415 articles
Browse latest View live




Latest Images