Quantcast
Channel: UDAKU SPECIAL
Viewing all 104709 articles
Browse latest View live

Diamond Azindua Perfume yake ya Chibu

$
0
0

Diamond Platnumz leo mchana amezindua rasmi perfume yake ya Chibu Perfume, hatua ambayo ni ya kihistoria. 

Perfume hiyo yenye asili kutokea Dubai itauzwa kiasi cha Tsh 105,000. Diamond alisema “Inaaminika kuwa Dubai ndio sehemu kunakotoka manukato mazuri.

FAHAMU Katuni Zinavyoweza Kutafuna Ubongo wa Mtoto Wako na Kumpa ‘Kifafa’..!!!!

$
0
0
Utamaduni wa kuangalia katuni au vikaragosi kama inavyofahamika kwa nchi jirani, ni utamaduni pendwa, maarufu na uliokubalika kwa wazazi wa watoto wengi kama njia ya kuwasaidia kujifunza na kuburudika. Lakini burudani hii ina hatari kubwa pia.

Kwenye familia nyingi hasa za wenye uwezo wa kuanzia kima cha kati na hata wale wa kima cha chini waliofanikiwa kununua runinga, watoto huanza kuangalia katuni tangu wakiwa na umri wa miezi sita. Wanapofikisha umri wa miaka mitatu kitaalam watoto hao hubadilika na kuwa watazamaji watiifu wa katuni.


Katika umri huo wa miaka mitatu na kuendelea, ni wakati ambapo watoto wanakuwa na uwezo mkubwa wa kuelewa mambo wanayoyatazama. Wanatengeneza ufahamu fulani kuhusu dunia kutokana na kile walichokiangalia kwenye katuni au vipindi vingine wanavyopata nafasi ya kuangalia japo kimakosa.

Hata hivyo, kwa bahati mbaya, katika umri huo, kwenye familia ambazo baba humsikiliza sana mtoto na kutaka afanye kile anachopenda, mtoto hugeuka kuwa na uraibu (addiction) au mfuasi mwaminifu wa katuni. Hivyo, endapo katuni zitakuwa na madhara chanya kwake ikiwa ni pamoja na kujifunza mambo mazuri itamsaidia kwa kiasi chake lakini kama sivyo itamtafuna ubongo na kumsababishia magonjwa, kutokana na madhara ninayoanza kuyataja katika aya inayofuata.

Wataalam wanaeleza kuwa mtoto anayeangalia sana katuni ambazo zinaonesha matukio ya migogoro na mapigano, ana hatari ya kupata matatizo ya kiakili na hisia (mfano kuwa na hasira kupita kiasi), pamoja na ubongo na macho kiasi cha kuongeza hatari zaidi ya matatizo ya kiafya.

Tafiti za taaluma ya saikolojia zimeeleza kuwa katuni za mapigano na migogoro pia zinawafanya watoto kuwa wakorofi na wanaoweza kuchukua hatua kali za vitendo dhidi ya wenzao.

Matatizo mengine pia hushambulia ubongo na macho ya watoto wanaoangalia katuni za aina hiyo. Mwendo kasi wa taswira wanazoangalia kwenye runinga husababisha madhara kwenye macho na ubongo wa mtoto.

Kwa mujibu wa mwandishi na mwanasaikolojia Raymond Villanueva, endapo tabia ya kuangalia katuni za migogoro na mapigano itakithiri, mtoto anaweza kushambuliwa na ugonjwa wa kifafa unaotokana na matatizo yanayogusa utendaji kazi wa ubongo.

Ingawa katuni pia ina faida nyingi hata kwa wazazi ikiwa ni pamoja kuwasaidia kuwafanya watoto wawe na kitu cha kufanya ili wasiwasumbue wanapokuwa bize na majukumu mengine, inawapasa kuchukua tahadhari na kufuatilia kwa makini kitu ambacho watoto hao wanaangalia na muda wanaotumia kuangalia ili kuwanusuru na matatizo haya ya ubongo.

KONA ya Penzi: Jinsi ya Kumjibu Mpenzi Anapouliza ‘Unanipenda Kiasi Gani?..!!!’

$
0
0

Wana jopo, karibuni kwenye jamvi letu jipya lililotandikwa kwenye kona maridhawa ya mapenzi.
Hii ni kona iliyoandaliwa maalum kwa ajili ya kujuzana mambo mawili matatu kuhusu masuala ya mahusiano ya mapenzi ambayo ‘yanafanya dunia izunguke’ bila sisi kujua tunazunguka nayo.

Wapo waliowahi kusema mapenzi ni ‘ukichaa’ kwa sababu kila wakitafakari baadhi ya matukio waliyoyafanya kutokana tu na kupenda wanaamini hawakuwa katika hali ya kawaida kiakili! Lakini wapo wanaoamini hakuna hisia nzuri na zenye busara iliyopitiliza kama hisia za mapenzi ambazo hazifichiki hata akipewa ‘bingwa wa kuficha siri za dunia’.

Anyways, tuweke kando hizo blabla… leo tuangazie swali ambalo karibu kila mmoja aliwahi kuuliza ama kuulizwa na mpenzi wake au hata mtu anayemshawishi kuwa mchumba. “Baby, unanipenda kiasi gani?” ni swali la mtihani ambao ulishavuja karibu kwa kila mtu, lakini hata anayeliuliza huwa hajui majibu.

Hivyo, wa kuliwekea alama hutegemea tu kile anachosikia, hata kama sio sahihi anaweza kuweka alama kubwa ya ‘vema’.

Wakati unajibu swali hili, nakushauri usihangaike hata kidogo kutafuta vipimo unavyovijua wewe hata kama ni kipimo cha ukubwa wa dunia na bahari zote. Picha itakayojengeka kichwani kwa unayemwambia itakuwa ya ‘kusadikika tu’.

Usilijibu swali hili kama unavyojibu maswali mengine ya kawaida anayokuuliza, jaribu kutengeneza kwanza mazingira mazuri ya haraka ya kuishika akili yake. Mvute zaidi umakini uwe kwako. Macho yako na muonekano wako uonekane kweli unataka kujibu swali muhimu la mapenzi sio mtihani wa mwalimu ‘Kabuche’. Lol. Hapo utakuwa umetengeneza mazingira ya ushindi.

Mwite jina zuri mwanzo, mfanye ajisikie anaongea na mpenzi, kama mko wawili mshike mkono taratibu, nyuso zitazamane… macho yako yatakusaidia kuzungumza zaidi kinachoelezwa na mdomo.

Kama wewe ni muongeaji sana, sauti yako ishuke kidogo iwe ‘romantic’. Hii ni kwa sababu moyo wa muuliza swali hupanuka na akili yake hutamani kusikia neno zuri sana kutoka kwako ambalo hata yeye halijui… hivyo inategemea utamwambia nini.

Angalia baadhi ya majibu yanayoweza kufaa, sio lazima uyakopi haya yangu… chukua kama mfano.
Tafadhali sana narudia, usitafute kufananisha nyota, bahari, mchanga na vingine, hii ni dunia ya dijitali na hiyo ilikuwa mifano ya zamani, huenda isimsisimue sana. Ni kama stori ya kunywa maji na kukuona kwenye bilauli!

“Baby, ingawa hakuna kifaa cha kupimia kiasi cha mapenzi, naamini mapenzi hayapimwi kwa maneno bali vitendo. Na hakuna ajuae kipimo cha tendo zaidi ya mtendewa. Kipimo cha mapenzi yangu kwako ni wewe… matendo yangu yanaongea, naomba unipe alama nazostahili. Lakini naamini nakupenda kiasi kisichoelezeka lakini kile kinachougusa moyo wako ni sehemu tu.”

“Baby, nakupenda kiasi kwamba kwamba naamini siwezi kupenda zaidi ya hapa.” Hapa ni kama unasema kuna kipimo na ushafika mwisho wa alama husika.

“Naamini ni neno ‘upendo’ pekee linaloweza kuupima upendo wangu juu yako. Siwezi kusema ni kiasi gani kwa sababu ni vigumu kusimulia kwa uhalisia maumivu ya kidonda, lakini ninaamini hiki ninachokisikia juu yako ndio maana halisi na sahihi kabisa ya neno upendo uliokomaa.”

Hata hivyo, majibu kutoka kwa mtu asiyependa kweli yanaweza kumuumbua tu hata akiyasema vyema kwa sababu macho yanayongea zaidi ya mdomo kwenye mapenzi. Chukua hii.

Maneno matamu yaendane na matendo matamu, hapo ndio utaona kweli mapenzi hayana kiwango cha elimu.

Kumbuka kuchagua maneno kutakusaidia kudumisha penzi lako, usiropoke tu majibu kisa umemzoea mwenzio ama unataka kuonekana mjuaji sana, itakugharimu. Katika mapenzi kila alama ni muhimu kuliko hata umuhimu unaoujua, hata kicheko chako tu kinaweza kushusha alama. Beba mapenzi kwa umakini wa hali ya juu zaidi ya kutembea juu ya trey la mayai.

Tunakunja jamvi kwa leo, tukutane tena kwenye kona hii hii ya Dar4, kona ya Penzi unaweza kutupa majibu yako pia mwanajopo, unadhani majibu yapi ni sahihi zaidi kwa swali hili?

UVUMILIVU ni Silaha Katika Kusaka Mafanikio..!!!

$
0
0

Ukiwa mtu wa kuangalia mambo kwa juu juu basi kila kitu kwako kitakuwa kigumu. Kusoma unaweza kuona ni kugumu, kufanya kazi kugumu, hata kusubiri mshahara unaweza kuona ni kugumu.

Urahisi kwako unaweza kuwa katika kutumia pesa, pengine  na kula tu. Ila watu waerevu na wenye uvumilivu kwako kila kitu kinaweza kuwa tofauti na wewe.

Unachoona kigumu kwao wanahisi si ugumu bali ni changamoto za kuzidisha jitihada na umakini tu. Kwenye mapenzi pia hali haiko tofauti sana. Wale wanao achana kila siku si kama ndiyo wanakosewa sana kuliko wale ambao hawaachani, hapana. Suala ni lile lile tu uvumilivu.

Hakuna mapenzi duniani yanayoweza kushamiri bila suala hili. Usipokuwa na moyo wa uvumilivu katika mapenzi basi kila mtu utamuona hafai. Utakuwa mtu wa kuanzisha mahusiano mapya. Hayo si maisha sasa!

Mahusiano yaliyodumu si kwa kuwa wahusika hawakoseani au makosa wanayokoseana ni madogo sana. Hapana. Kila binaadamu ana mapungufu yake. Wote huwa wanakoseana ila tofauti yake na wengine ni kwamba busara na uvumilivu huwa msingi wa mapenzi yao na ndiyo maana tunaona wanadumu mpaka leo.

Ni binaadamu gani unaweza kuishi naye na msikoseane? Ni nani mwenye uwezo wa kukupa unachotaka kila siku? Hakuna binaadamu wa aina hiyo.

Ndiyo, kukosewa kunaumiza sana ila jiulize ni kitu gani kimetokea bila sababu? Kwenye makosa ya mpenzi wako kuna sababu nyuma yake, hebu itafute badala ya kulalamika.

Mapenzi yasiyo kuwa na uvumilivu ndani yake hayana maisha marefu. Kwa sababu binaadamu ni kiumbe mwenye kukosea.

Kuwa mvumilivu. Watu wenye hekima ni wavumilivu. Watu wenye kujielewa ni wavumilivu.
Ukiwa hauna uvumuilivu kila siku utatangaza ndoa. Leo utaachana na Mugambara kwa sababu anaongea sana na wasichana ila, jua huyo unaeenda kuwa naye anapenda sana kitu ambacho hukipendi. Anakunywa pombe je, utawezana naye? Jibu unalo.

Kumbuka, siku zote wanaovumilia ndiyo huwa wanabaki na ushindi.Bila uvumilivu Mandela asingekuja kuwa raisi wa afrika kusini.Uvumilivu ni kila kitu katika maisha.

MAMBO 10 ya Kufanya Kabla Hujafikia Miaka 28..!!!

$
0
0

1. Jifunze kuweka akiba ya fedha

2.Tafuta mpenzi sahihi na tulia nae

3. Acha kuishi na wazazi au kupanga nyumba na washikaji

4. Achana na starehe zisizo na maana

5. Jali sana afya yako

6. Kuwa na marafiki wenye changamoto za maendeleo

7. Anza kununua asset kama vile ardhi, kitanda, vyombo vya nyumbani na n.k

8. Jifunze kuvaa kwa heshima na si tu suala la kupendeza

9. Acha mambo ya kitoto jisikie umekua mkubwa na mambo unayoyafanya yawe ya kiutu uzima

10. Zingatia sana muda wako.

UAMUZI wa Kuoa ni Ujasiri wa Watu Wachache, Wengi Wao ni Waoga...!!!

$
0
0

Vijana siku hizi walio nje ya ndoa huishi maisha ambayo hufananishwa na maisha ya ndoa, kutembea pamoja, kula pamoja, kulala pamoja, kuzaa watoto na kuwaita majina pamoja, kulea pamoja, kucheza pamoja, kulia pamoja, kufurahi pamoja, kusafiri pamoja, kulipia gharama mbalimbali pamoja lakini  bado wanasema hawapo tayari kuoa na kuolewa.

Moja ya sababu ni uoga wa kuingia kwenye ndoa,  watu wengi hawana tafsiri nzuri ya maisha ya ndoa kutokana na waliyaona kwenye maisha ya ndoa ya ndugu, jamaa au marafiki zao ambayo yaliwakatisha tamaa ya kuoa au kuolewa.

Mwisho wa siku ikumbukwe kuwa kila mtu ana maisha yake, ulichopitia wewe sio atachopitia mtu mwingine alichopitia baba yako au mama yako au rafiki yako sio utachopitia wewe, kikubwa ni kufanya maamuzi sahihi kwa wakati sahihi, ni vyema kumjua mwenza wako vizuri kabla hujafanya maamuzi ya kuoa au kuolewa hii itakusaidia kuishi maisha ya furaha, amani na upendo ukiwa kwenye ndoa.

Kijana jifunze ndoa ni Baraka ya mambo yote unayoyafanya, hivyo kama mtu hana utayari wa kufunga ndoa na mototo wa watu basi ni vyema kuchukua maamuzi mapema kuepusha kupotezeana muda na malengo katika maisha usiwe mguu mmoja ndani mwingine nje.

TAKUKURU Yaokoa Mil 74/- Semina Hewa..!!!

$
0
0

TAASISI ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa (Takukuru), Mkoa wa Arusha imefanikiwa kuokoa zaidi ya Sh milioni 74.8 zilizolipwa kwa watumishi na semina hewa. Aidha watumishi wa umma wamesisitizwa kufanya kazi kwa maslahi ya umma, kwa kuzingatia suala zima la uadilifu na kuacha kuwashawishi wananchi kutoa fedha ili wapate huduma.

Hayo yalisemwa  na Kaimu Kamanda wa Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa (Takukuru) mkoani Arusha, Frida Wikessy wakati alipotoa taarifa ya utendaji kazi wa tasisi hiyo katika kipindi cha Julai mwaka jana hadi Machi mwaka huu.

Wikessy alisema fedha hizo zimerejeshwa serikalini baada ya kuziokoa kutokana na watumishi hewa pamoja na semina hewa zilizoandikwa kwa kughushi saini ili watu wajipatie fedha. Alisema fedha hizo zilitokana na watumishi hewa Idara ya afya na elimu ambapo kulikuwa na watumishi wameacha kazi, kufa na wengine kuhama vituo vya kazi, lakini serikali iliendelea kulipa.

Aidha katika kipindi hicho mkoa huo ulipokea jumla ya malalamiko 248 kwa njia mbalimbali na kati ya hayo majalada 24 ya uchunguzi yanaendelea, yapo katika hatua mbalimbali. Frida alisema katika uongozi wa awamu ya tano umekuwa na ongezeko la wananchi kutoa taarifa nyingi tofauti na miaka ya nyuma, hali inayosababisha kupokea malalamiko yalio sahihi na yasio sahihi. Pia alisema katika kipindi hicho mashauri 14 yalisikilizwa na kati ya hayo 10 yalishinda katika kesi za jinsi na uhujumu uchumi

HUKU Wakisema Uchumi Umekuwa..Benki ya Dunia Yainyooshea Kidole Tanzania Kuhusu Madeni..Watoa Kauli Hii kwa Serikali ya JPM..!!!

$
0
0

WAKATI ripoti ya hali ya uchumi iliyotolewa na Benki ya Duniani (WB) hivi karibuni ikionyesha uchumi wa Tanzania kukua kwa kasi kuliko nchi nyingi Kusini mwa Jangwa la Sahara, Tanzania inaendelea kuwa moja kati ya nchi zenye madeni makubwa miongoni mwa nchi masikini.

Ripoti iliyozinduliwa na WB jijini Dar es Salaam hivi karibuni, inaonyesha uchumi wa Tanzania ukikua kwa asilimia 6-7, wakati ukuaji wa uchumi kwa nchi nyingine zilizo Kusini mwa Jangwa la Sahara ukikuwa kwa asilia moja na nusu.

Pamoja na ukuaji huu mzuri, ripoti hiyo inaonyesha Tanzania kuwa na madeni makubwa, yakichukua asilimia 20 ya pato la ndani.

Hata hivyo, ripoti hiyo inasema, lengo la Serikali kufikia ukuaji wa asilimia 10 kufikia mwaka 2020/21 linaweza kufikiwa kutokana na nchi kuweka msisitizo kuelekea uchumi wa viwanda, pamoja na uwepo wa rasilimali nyingi.

Ripoti hiyo yenye kurasa 88, inaeleza katika ukurasa wa 14 kuwa pamoja na kuwa Deni la Taifa nchi bado inaweza kulimudu, kuna haja ya kuangaliwa kwa umakini mkubwa, kutokana na deni hilo kuongezeka kwa kasi.

Kwa mujibu wa ripoti hiyo, mlingano kati ta Deni la Taifa na Pato la Ndani (GDP) ulikuwa asilimia 37.7 mwezi Juni 2016,uliongezeka kwa asilimia 2.5 ya GDP ukilinganisha na mwaka 2015.

Ongezeko hilo linaelezewa kusababishwa na ukopaji wa kibiashara kutoka vyanzo vya ndani na nje ya nchi kwa ajili ya kugharamia miradi ya uwekezaji ya Serikali kutokana na kupungua kwa misaada kutoka nje.

“Kufikia mwezi Juni mwaka 2016, deni la kibiashara lilichukua asilimia 23.3 ya jumla ya deni, huku mikopo isiyo ya muda mrefu na yenye riba nafuu (non-concessional loans), ikichukua asilimia 64.4 ya jumla ya deni la kibiashara.

Pamoja na ongezeko hili, Tanzania bado ipo katika nafasi nzuri ya kumudu deni lake. Hata hivyo, Tanzania inahitaji kuwa makini na deni lake kwa sababu kuna mambo kama kupanda na kushuka kwa gharama za kubadilisha fedha za kigeni, ambazo zinaweza kuwa na athari katika deni,” inasomeka sehemu ya ripoti hiyo.

Akiwasilisha matokea ya ripoti hiyo jijini Dar es Salaam hivi karibuni, Abede Adugna Mchumi kutoka WB, alisema ripoti hiyo inaishauri Tanzania kuwa makini katika ukopaji wake.

WAKATI Chadema Wakimchukia Magufuli..Mwasisi wa Chadema Aibuka na Kumshushia Sifa Kedekede..Afungulka Pia Hatma ya Lowassa Ndani ya Chadema...!!!!

$
0
0

MWASISI wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), Edwin Mtei, ameeleza kufurahishwa kwake na mwenendo wa uongozi wa kushtukiza na utekelezaji wa sera za Chadema unaofanywa na Rais John Magufuli. RAI linaripoti.

Tangu alipoingia madarakani Novemba 5, mwaka 2015, Rais Magufuli amekuwa akifanya ziara za kushtukiza katika idara na taasisi mbalimbali za umma, huku baadhi ya wachambuzi wa kisiasa wakidai kuwa anatekeleza Ilani ya Chadema.

Katika mazungumzo yake na RAI, Mzee Mtei ambaye pia alikuwa Gavana wa kwanza wa Benki Kuu ya Tanzania (BoT), alisema Rais Magufuli amewafungulia njia wapinzani, hivyo wanamsubiri kwa hamu katika Uchaguzi Mkuu wa 2020.

“Tena nikuambie kwamba kama kuna jambo ambalo tunajivunia sisi ni pale ambapo serikali inatekeleza sera ya chama changu ambacho nilikianzisha. Hili linanipa furaha, pamoja na udhaifu uliopo ndani ya serikali ya Awamu ya Tano. Ukiangalia elimu, afya, barabara, kufufua reli, viwanda pamoja na mambo kadha wa kadha, najivunia kwamba chama changu ni chama bunifu, kila siku tunabuni mambo mapya kulingana na mabadiliko ya teknolojia.

“Chadema kinasikiliza maoni ya Watanzania, bila kujali ukanda wala kabila. Chadema ni wapenda amani, tutaendelea kumwenzi hayati Baba wa Taifa hili na mwaasisi wetu aliyetukomboa mikononi mwa wakoloni. Alionyesha uzalendo na siyo chama. Hakutaka madaraka, alitanguliza uzalendo wake, tofauti na viongozi wa chama tawala ambao mawazo yao yametawaliwa na uongozi na siyo uzalendo wa kuipenda nchi yao. Hili ni jinamzi linalolitafuna Taifa hili.

“Sasa hivi mimi siwezi kupambana kwenye majukwaa ya siasa, ila nitaendelea kuwaonya viongozi wa chama changu kwa kutumia  mitandao ya kijamii whatAspp na mitandao  mingine, ili waendelee kuyaenzi yale yaliyomema ya kulijenga Taifa hili,” alisema.

HALI YA KISIASA

Akizungumzia hali ya kisiasa nchini, Mzee Mtei alisema hali inabadilika badilika kutokana na mtindo wa Rais Magufuli anaoutumia kuongoza nchi.

“Hivi sasa nchi inaongozwa na Rais ambaye anafanya mambo yake kwa kushtukiza shutukiza na sisi tunamwangalia tu, tuone atafika wapi. Pili nchi haiwezi kuendeshwa kwa mtindo wa namna hii, nchi inatakiwa kuendeshwa kwa kufuata sheria na Katiba.

UJIO WA LOWASSA

Aidha, akizungumzia ujio wa Waziri Mkuu wa zamani Edward Lowassa ndani ya Chadema na kupewa nafasi ya kukiongoza chama hicho katika Uchaguzi Mkuu wa 2015, Mzee Mtei alisema ujio huo ulionyesha ni jinsi gani Watanzania, pamoja makada wa walioko ndani ya CCM walivyochoshwa na mambo ambayo yaendelea ndani ya Serikali.

“Lowassa alikuja kuunga mkono, ili kuleta ukombozi wa Watanzania ambao bado wako kwenye giza nene na hawajui wanakwenda wapi, mbali kuwa nchi yao imesheheni rasilimali nyingi na ardhi zenye rutuba.

“Lowassa pia alikuja ili atusaidie kuchukua nchi, lakini niwaambie kwamba bado tutaendelea kuwa na Lowassa hatutaweza kumtupa. Alileta mabadiliko makubwa sana aliwachangamsha vijana, aliweza kuamsha ari mpya.

SLAA ALINIVUNJIA HESHIMA
Akizungumzia uamuzi wa aliyekuwa Katibu Mkuu wa Chadema, Dk. Wilbrod Slaa kuondoka ndani ya chama hicho katika kipindi cha mwisho cha mchakato wa Uchaguzi Mkuu 2015, Mzee Mtei alisema hilo ni jambo lililomsitikisha sana.

“Kwanza aliondoka kipindi ambacho tuko kwenye mchakato wa Uchaguzi Mkuu. Binafsi Dk. Slaa ni rafiki yangu wa karibu sana, kwa jina lingine namfananisha kama kijana wangu, kabla ya kuondoka kwake nilimsihi sana lakini hakunisikia, nilimwandikia ujumbe mbalimbali kumtaka anieleze juu ya kuachana kwake na siasa, hakunijibu. Nikamwandika barua, hakujibu nikajisikia vibaya sana. Sikutegemea kama angenifanyia hivyo.

“Ukimya wake wa kutonijibu niliona mimi kama rafiki yake msiri wake, tena mtu mzima, moja kwa moja nikaona kama amenivunjia heshima.

“Siwezi kumsahau kwani alikuwa chachu kwa vyama vya upinzini, alikuwa mwanamapinduzi wa kweli, bila kujali ni nani anapambana nae. Kwenye siasa alikuwa akiisema Serikali bila kuogopa, tena kwa hoja. Alikuwa mtu ambaye aliipenda nchi yake, alikuwa akikisema chama tawala kwa kuwataja mafisadi waliokuwa wanatafuna nchi bila kuwaangalia usoni, tena kwa ushahidi. Pia alikuwa akishirikiana na viongozi wa wake katika kila hali, ni mtu asiyependa kuonewa wala kuwaonea wengine.

“Ila nina imani Dk Slaa bado ni mwanaChadema na ataendelea kuwa mwanamapinduzi, hata ukiangalia siyo yeye pekee yake aliyeondoka, waliondoka wengi wazuri pia, akina Zitto Kabwe na wengine, lakini heshima yake inabaki pale ambapo alibaki bila kujiunga na chama kingine. Huo ndiyo uzalendo wa kweli, hata akija nchini nitamwita, maana najua hatokataa mwito wangu,” alisema.

MWELEKEO WA CHADEMA 2020

Akizungumzia Uchaguzi Mkuu ujao wa 2020, Mzee Mtei alisema hivi sasa chama hicho kimejipanga, kwa kuwa katika Uchaguzi Mkuu wa mwaka 2015, kilishiriki na kufanya vizuri kuanzia ngazi za udiwani, ubunge na urais, lakini CCM kwa uzoefu wao waliiba kura kwa kutumia nguvu ya dola.

“Kwa kuwa Chadema ni chama makini na kinaongozwa na watu ambao ni wasomi, wenye maadili, hatukutaka kwenda kufanya maandamano. Pili, kwa kulinda heshima ya Watanzania waliotuamini, hatukutaka kufanya mikutano ya kupinga matokeo ya urais. Tatu, Watanzania walio wengi, hawakuwa tayari kwa mabadiliko uongozi wa juu kwa kuhofia huenda ingeleta vita endapo mgombea wa Chadema, Edward Lowassa angetangazwa kuwa rais.

“Ila uchaguzi ujao mwaka 2020, Chadema tutashinda kiti cha urais kwa kishindo kwani tumejipanga, hatutaogopa chochote siwezi kuweka wazi mkakati wetu tuliyopanga.

“Kwa sababu tunaona pia kijana wetu Zitto Kabwe amedhamiria kuongeza nguvu, jambo ambalo ni jema na linaonesha jinsi gani vijana wangu niliowalea, wamekomaa kisiasa. Zitto bado ni mwanachadema, kuihama Chadema haimzuii Zitto kuipenda Chadema. Bado ana mapenzi ya dhati, kwani ndiyo chama ambacho kilimleta na kilimpa umaarufu kwenye nyanja za kisiasa ndani na hata nje ya Tanzania.

Naamini muungano wa UKAWA utasaidia kuimarisha upinzani kuingia madarakani mwaka 2020, pia utasaidia kuua nguvu za chama tawala, kwani ndicho kilichokuwa kikiwagharimu na kushindwa kufanikiwa kutokana na mgawanyiko wa upinzani. Umoja ni muhimu sana katika kudai haki na kujenga Taifa, hasa kwa nchi kama Tanzania ambayo haijawahi kutawaliwa na vyama vya upinzani.

Licha ya muungano huo, Mzee Mtei anasema bado hawajaweka mikakati ya kuainisha jina la mgombea urais katika uchaguzi wa 2020.

“Naweza nikasema ni sahihi au la, lakini Lowassa bado ni wa kwetu, siwezi kuiweka wazi mikakati ya chama kwani maamuzi yatakuja wakati ukifika, kwa sasa bado ni mapema mno na kama mnavyojua, Chadema ndiyo chama pekee nchini kilichosheheni vichwa vilivyojaa ubunifu na sera ambazo hazikopiki.

Pili Chadema ni chama ambacho kinasikiliza maoni ya Watanzania na kuyafanyia kazi kulingana na mabadiliko hali ya kisiasa katika nchi kwa wakati husika.

Tatu tutaangalia ni kwa namna gani tutaboresha, ili kuchukua nchi mwaka 2020 kwa kushirikiana na vijana wetu walioko ndani ya chama. Na imani yetu kubwa ni kuchukua nchi mwaka 2020, kwani sasa wananchi wako tayari kwa maamuzi yoyote na kuna kila dalili, hata ukisema uchaguzi ufanyike leo, lazima tuchukue nchi. Watanzania wa leo sio wale wa jana. Ndio maana nasema Tanzania mpya inakuja.



SERIKALI YA AWAMU YA TANO

Aidha, akizungumzia mwenendo wa Serikali ya awamu ya Tano, Mzee Mtei anasema kiujumla Rais Magufuli ni kiongozi mzuri kwa kiasi, ila anadhani Watanzania wataamua kwa kuwa ni mtu wa kufanya mambo kwa kushtukiza.

“Amekuwa akifanya maamuzi yake kwa matukio na siyo kuwasikiliza Watanzania wanasemaje, nini mahitaji ya watu wake, hivyo sisi kama wapinzani tunaangalia tu tuone ataifikisha wapi nchi kwa miaka mitano. Sasa hivi tayari amebakisha miaka mitatu tu,” alisema.

Pamoja na mambo mengine, alisema ni kosa kubwa kumfananisha Mwalimu Nyerere na Magufuli kwa kuwa Nyerere alikuwa analipigania Taifa kutoka kwenye makucha ya wakoloni.

“Huwezi kumfananisha na wanasiasa vijana, tena wanaoliharibu Taifa, Mwalimu Nyerere alikuwa anapigania haki na kuikomboa nchi mikononi mwa wakoloni, leo hii watu kumfananisha na wanasiasa ni jambo la kusikitisha sana,” alisema.

Anasema sera ya kufufua viwanda ni sera ambayo haitekelezeki kwa kuwa jukumu hilo ni jambo linalohitaji maandalizi makubwa.

“Kwanza lazima uwaandae wananchi unaowaongoza, pia kushirikiana na pande zote pili bila kuangalia itikadi ya vyama, kuandaa mazingira ya wawekezaji wa ndani na wa nje, upatikanaji wa malighafi pamoja watalaamu wa masuala kiuchumi na viwanda. Tatu, lazima uandae au kutenga ardhi kwa ajili ya viwanda  kwani hakuna njia rahisi bila kufuata hatua zote.

Aidha, alisema uamuzi wa Rais Magufuli wa kufuta mikutano ya kisiasa hadi 2020, ni jambo ambalo limewafungua macho wapinzani kwa kutumia mitandao ya kijamii kufanya siasa za kimyakimya.

“Ni utashi wa kiongozi aliyeko madarakani na chama chake, na sisi kwetu ni fursa, ametupa mwanga wa kuona mbali zaidi. Pili amevisaidia vyama vya upinzani kuongeza ubunifu, kubadilisha namna ya kufanya siasa na kwamba siyo lazima kufanya siasa kwenye majukwaa.

Ametupa fursa nyingine nzuri ya kufanya siasa badala kutumia gharama kubwa kuandaa mikutano na watu, tunatumia mitandao ya kijamii kuwaeleza Watanzania na tumegundua njia hii ni bora zaidi, kwani tumeweza kuwafika idadi kubwa ya vijana, wamama pamoja na wababa.

“Sasa hivi ukirusha kitu kwenye mitandao ya kijamii baada ya dakika tano tayari unapokea zaidi ya komenti za watu 1000 kutoka mikoa yote Tanzania na hata nje ya nchi, imetusaidia kufanya siasa za kimya kimya, kuliko kuandaa mkutano ya hadhara. Binafsi na namshukuru kwa utashi wake ametufungua macho na ufahamu zaidi. Siasa hazizuiliki kamwe,” alisema. 

Credit - Rai

JAJI Lubuva Atoboa Siri za Uchaguzi Mkuu wa 2015 Ulivyokuwa ..Adai Alitishiwa Kifo Amtangaze... ..!!!

$
0
0

MWENYEKITI Mstaafu wa Tume ya Taifa ya Uchaguzi, Jaji Damian Lubuva amefichua mambo mbalimbali aliyokumbana nayo katika kipindi cha Uchaguzi Mkuu wa mwaka 2015. 

Jaji mstaafu  Lubuva, aliteuliwa kushika wadhifa huo mwaka 2011 na kustaafu Disemba mwaka jana na nafasi yake kuchukuliwa na aliyekuwa Jaji wa Mahakama ya Rufaa, Semistocles Kaijage, amebainisha kuwa uchaguzi huo wa mwaka 2015 hatousahau kutokana na kuwapo kwa ushindani mkubwa.

Akizungumza  nyumbani kwake Oysterbay jijini Dar es Salaam, alisema mazingira ya ushindani wa kivyama katika uchaguzi huo yalimsababishia hata baadhi ya ndugu zake kumnunia.

Alisema tangu mfumo wa vyama vingi uanze mwaka 1992, uchaguzi wa 2015 ulikuwa na ushindani mkubwa kuliko chaguzi zote zilizofanyika nchini.

“Uchaguzi Mkuu wa mwaka 1995, Agustino Mrema alileta changamoto kama mtu binafsi si chama, mwaka 2015, hali ilikuwa ni nzito kwa kuwa ushindani ulikuwa wa vyama zaidi. Hata hivyo nashukuru Mungu tulimaliza kwa amani, hata watazamaji waliona uchaguzi uliisha kwa amani na baadhi yao nilikuwa nashirikiana nao. Nakumbuka walipokuwa wanaona kampeni walinieleza kuwa ushindani utakuwa mkubwa, najivunia kumaliza uchaguzi ule kwa amani.

“Wakati naingia NEC tulianzisha uandikishaji wapiga kura kwa kutumia mfumo mpya wa BVR. Mfumo huo ulikuwa na changamoto zake mojawapo ikiwa ni ucheleweshwaji wa vifaa kwa kuwa vilichukua muda kufika nchini huku Oktoba ilikuwa inakaribia, hata hivyo tulijitahidi kuandikisha kwa kutumia mashine  zilizofika kwa kuhamisha hamisha. Hata wadau wetu walishangaa tumefanikiwa vipi kuandikisha watu milioni 23 kwa muda mfupi ule,” alisema.

 KUNUNIWA NA NDUGU

Alisema kutokana na ushindani huo wa kivyama, baada ya matokeo baadhi ya ndugu zake walimnunia kwa kudhani kuwa haki hakutendeka jambo ambalo halikuwa na ukweli.

“Hata watu wengine ambao ni ndugu zangu walinuna, waliona hawakutendewa haki, lakini ndio kura kwani kwa mujibu wa kura Magufuli ndio kashinda.

“Katika uchaguzi wowote kuna mawili kushinda na kushindwa, anayeshindwa mara nyingi hawezi kuzungumza vizuri juu ya uchaguzi. Ila niseme uchaguzi ule uliendeshwa kwa taratibu na kanuni za uchaguzi, si kweli kwamba kura ziliibwa, kwa sababu tuliendesha uchaguzi kwa uwazi. Kwa mara ya kwanza kura za rais ziliwekwa wazi kwani vituo vyote vilibandika matokeo, hivyo mpiga kura anajua mgombea wake amepata nini ndipo tunaletewa huku Dar es Salaam tunajumlisha na kutangaza.

“Pia mawakala wao wanakuwapo na wanajua mgombea wao amepata kiasi fulani, hivyo niseme kuwa hakuna sehemu jimbo wala wilaya kwamba kura za mgombea urais ambazo zilitangazwa makao makuu hapa Dar es Salaam  ambazo zilikuwa batili. Hivyo unaposema kura zimeibiwa ushahidi upo wapi? Ndio hicho ninachozungumza wakati wote kuwa kadiri matokeo yanapokuja ndivyo nilivyokuwa nayasoma,” alisema.

KUTISHIWA MAISHA

Aidha, Jaji Lubuva alisema licha ya kuwapo baadhi ya kundi la vijana waliomtishia kumuua iwapo kungetokea matokeo wasiyoyataka, anamshukuru Mungu uchaguzi huo ulifanyika kwa amani bila vurugu na kamwe hakuwa na hofu.

“Sikuwa na hofu, tunajua baadhi ya vyama walikuwa na sehemu zao wanaita Ngome, walikuwa wamejiandaa sana kwamba labda kufanya fujo ila nilikuwa nimejiandaa vizuri kwani hata hivi vyama vya upinzani kwa ujumla walishirikiana na chama tawala baada ya matokeo. Kama kweli wangedhamiria kufanya fujo basi wangewachochea vijana wao, na kwa sababu sikufanya lolote baya ndani ya utendaji wangu hapakuwapo na uvunjifu wa amani. Kuna baadhi ya vijana walikuwa wanatishia kuniua iwapo ningetangaza matokeo tofauti na walivyokuwa wakitaka lakini bahati nzuri hapakuwapo na lolote uchaguzi uliisha kwa amani,” alisema.

Licha ya baadhi ya Watanzania kudai kuwa NEC si huru, Jaji Lubuva alisisitiza kuwa Tume hiyo ni huru kwani hata katika kipindi cha uongozi wake hapakuwahi kutokea wito wa Rais kuwataka viongozi hao wafike Ikulu.

 “Nimelizungumza sana tangu nimeingia pale, kwamba yapo madai kwamba Tume si huru, nimesema kwamba hizi ni hisia kwamba Jaji Lubuva ni mteule wa rais na mkurugenzi na makamishna ni wateule wa rais, pia wakati rais huyohuyo ni mwenyekiti wa chama. Lakini siku zote nilisema tume inafanya kazi zake kwa uhuru, hakuna siku yoyote tumeingiliwa na rais na hata sasa nimeicha NEC ikiwa huru. “Kwa sababu tumekuwa tukishirikiana na tume za nchi za EAC na SADC baadhi yao wanajiita tume huru, ila sisi hatukujiita jina hilo ila niwahakikishie kuwa tume yetu ni huru kabisa.

 “Kama mtakumbuka Tume ilikwenda kwa Jaji Warioba kipindi cha kuandaa rasimu ya Katiba, tukawasisitizia kuwa tunafanya kazi kwa uhuru ila kuondoa hayo maono ni vyema kuangalia namna ya kubadilisha kidogo vifungu vya sheria. Kwa sababu pamoja na rais kuteua makamishna, mkurugenzi na hata Jaji mkuu hapakuwapo kabisa na mwingiliano wowote, tangu niwapo pale hata siku moja hatukuwahi kuitwa na rais Ikulu,” alisema

LEMA Afichua Jinsi TRA Wanavyowafanyia Ukatili Wafanyabiashara wa Arusha..!!!

$
0
0

MBUNGE wa Arusha Mjini, Godbless Lema amesema   Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA), imekuwa ikiwatesa na kuwasumbua wafanyabishara hasa katika miji mikubwa ya Dar es Salaam, Arusha na Mbeya.

Lema alitoa kauli hiyo bungeni jana wakati akiuliza swali la papo kwa papo kwa Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa.

“Mheshimiwa Waziri Mkuu, tunafahamu jitihada za serikali ya awamu hii ya kupigania sera ya viwanda ambalo ni jambo jema.

“Kila mwenye akili timamu analipongeza ili suala la viwanda liwe na ukweli ni lazima wawekezaji na wafanyabiashara wawe na mazingira bora.

“TRA wamekuwa wakitesa na kusumbua wafanyabishara hasa katika miji mikubwa ya Dar es Salaam, Arusha na Mbeya hasa katika  mkoa ninakotoka, TRA wanatumia polisi, Takukuru na usalama wa taifa kuwatishia katika masuala ya kodi.

“Ili waweze kufanya biashara zao kwa uhakika nini kauli ya serikali juu ya mfumo wa TRA?”alihoji Lema.

Akijibu swali hilo, Majaliwa alisema ni kweli kipo chombo kinachowajibika kukusanya kodi kutoka kwa walipa kodi wakiwamo wafanyabishara.

“Ni kweli wanatambau ulipaji kodi ni wadaiwa sugu, TRA kupitia chombo chake Task Force makao makuu, ilikuwa na mkakati wa kuwapitia wadaiwa sugu. polisi, Takukuru walienda kule kuona hakuna utoaji rushwa.

“Na katika msafara huo kama Arusha, polisi walikuwa wanatumia silaha na utaratibu kama fedha zinaweza kulipwa papo kwa papo na nimshukuru RC wa Arusha kwa kuwaita wafanyabishara na kuwaeleza wale polisi walikuwapo kwa ajili ya kulinda tu na alirudisha amani.

“TRA inao utaratibu, wale ambao wanadhani haiwatendei haki kusikiliza kero watumie madawati hayo kupeleka malalamiko hayo.

“Serikali inawaheshimu wafanyabishara na inatambua umuhimu wao wa kulipa kodi na kila mmoja  atambue wajibu wetu na waendelee kutoa ushirikiano na haiwapelekei hofu,”alisema Majaliwa.

Simba Wataka Kufanya Maandamano ya Amani, Wamechoshwa na TFF

$
0
0

KUFUATIA sakata la kamati ya katiba, hadhi na wachezaji kuliweka tena mezani suala la Klabu ya Simba kupewa pointi 3 dhidi ya Kagera baada ya kumchezesha Mohamed Fakhi akiwa na kadi tatu za njano, wekundu hao wa Msimbazi wametuma barua kwa Kamanda kwa kanda maalum Mkoa wa Dar es salaam, Kamishna Simon Sirro kuomba maandamano ya amani. 

Maandamano hayo amb kwa mujibu wa barua hiyo ya leo yanatarajiwa kufanyika siku ya Jumanne kuanzia majira ya saa 4 asubuhi mpaka saa 7 mchana yakianzia Makao Makuu ya klabu hiyo kuelekea  Ofisi ya Wizara ya Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo.

Dhumuni kuu la barua hiyo ni kupinga namna Shirikisho la Mpira wa Miguu Nchini TFF kufanya vitendo na maamuzi ya uonevu kwa Klabu ya Simba huku malalamiko mengi ya msingi wanayopeleka maombi yakiwa hayasikilizwi kwa wakati. 

Mbali na hilo ni pamoja na leo, Shirikisho hilo kuamua kumpeleka Msemaji wa klabu hiyo Hajji Manara mbele ya kamati ya maadili ikiwa wanaonyesha nia ya kutaka kumfungia na kumziba mdomo ili asioongelee uonevu unaofanywa dhidi yao. 

Barua ya kuomba maandamano hayo ya amani imendikwa na Rais wa klabu hiyo, Evance Aveva na kutuma nakala kwa Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo pamoja na Katibu Mkuu Shirikisho la Mpira wa Miguu Nchini (TFF) na maandamanio hayo yatapitia katika barabara za Msimbazi, Nyerere na Chang'ombe. 

PATA Tiba ya Asili Kutoka Kwa Mtabibu wa Nyota Maalim Hussein...Una Shida na Mapenzi Au Pesa Hazikai?

$
0
0

Kutana  na Mtabibu Mwenye KUBRI kutoka kwa ALLAH Maalim HUSSEIN Mtabibu wa Nyota za Binadamu na Dawa za Asili ya Africa Mwenye UWEZO Kubaini tatizo lako Pindi tu Utakapo Fanya Mawasilino Kupitia Wasaa Husika..

JE UNASUMBULIWA NA Mapenzi? (Umeachwa na Umpendae,Awe Mume,Mke na Bado unampenda?Na  Umejaribu Sehemu nyingi Bila Mafanikio?Wasilina na Maalim Hussein Ujione muujiza wa Papo kwa Papo.. 

Anauwezo WA KURUDISHA MAHUSIANO NA KUIMARISHA NDOA YAKO NDANI YA SAA 12 TU. 

Umekimbiwa na Mumeo,mkeo au Mpenzi na anaishi na mtu mwingine? Muone akutatulie Anauwezo wa Hali ya Juu wa Kusambalatisha Mahusiano yao Endapo utafata Atakacho kuelekeza, Atamfanya Atimize Ahadi zote kwa Muda Mfupi.

Maalim Hussein Anatumia Jina la Muhusika au Picha Kumaliza Tatizo lako..

Anatibu kwa Kutumia  Vitabu vya QUR-AN Dawa za Asili za Africa,Dawa za Kiarabu na Majini.Anatafsiri Ndoto. Kushinda BAHATI NASIBU, KUSAFISHA NYOTA. Mvuto wa Mwili na BIASHARA, Kinga ya Mwili,ZINDIKO za Nyumba, MIGUU Kufa GANZI, Kufungua KIZAZI kwa wale walio fungwa kwa njia za KISHIRIKINA, Anakupa Jini la Mali kwa yule anaehitaji Utajiri BILA MASHARTI, Nguvu za KIUME, Humaliza Kesi zilishindika ndani ya siku 14 tu..na mengi 

ZaidiWhatsapp +255 674 835107  Au Piga +255746757102

NB: TIBA KWA DINI ZOTE NA IMANI ZOTE...

Dah, Kuna Kila Dalili Huyu Binti wa Kitanga Kashaniloga

$
0
0
Ni miaka mitatu toka niache haya mambo ya kua kwenye serious relationship(whatever that means) na mtu, hii ni baada ya kuja kijamaa chenye pesa na kumchukua mwanamke niliyodumu nae kwa miaka miwili,mwanamke ambaye nilihisi sitokaa kuja kumsahau, just like that, she got saved up by some dude,got married, had kids, got thick...(at least like a soccer mom).. Eway let's save that for some other time

Nikaingia rasmi kwenye chama la ma bachelor, kwa kweli hili chama nakatokea kulipenda sana na nikaapa sitakuja kulisaliti mapema, nikapokelewa rasmi na Mshkaj wangu kwenye hili chama, showed me a trick or two, maisha yanasonga

Maisha ya u bachelor raha sana, come friday night, there is nothing more than having a good shave(yeah I mean on em pr#vate parts) and go out hunting!!! Huyu Mshkaj wangu aliniyenikaribisha kwenye chama akanambia Sheria la chama ni kua ukienda mawindoni lazima urudi na nyama, man gotta eat right?? Haya ndo yakawa maisha, full kukichafua, si instragram, si viwanja, si wapi, any place u can get a nice piece of a,,,ss!! Nimeenjoy sana haya maisha until kama miezi miwili iliyopita

Huyu mtoto wa tanga, anafanya kazi kwenye supermarket moja karibu na nlipohamia, nikawa nikitoka kutafuta mkate wa kila siku napitia hapo supermarket and get some supplies, tukazoena baada ya muda( maybe because of the tips?) Well whatever!!! Tukabadilishana namba, haichukua muda she was already inside my trap, akaanza kuja kulala kwangu weekends tu(anaishi na Dada yake ambaye kila weekend anaenda Moro kwa mchumba wake) so ndo anaweza kutoroka and the sort

Tatizo ni kwamba ex wangu alikua the typo with extremely good looks rating kama ya (9/10), huyu mtoto wa tanga ni wa kawaida tu let's say (6.5/10), nilipoanza kua nae I was all in for s..ex tu na wala si kingine, sikua na feelings nae kivile hata, balaa likaanza hapa, her s..ex game is A+, been fooling around with all types of ch..icks but huyu mtoto bana,her s..ex game is A+(mind you I've never rated anyone that much before)

Ikawa weekend mi sitoki wala nini, just In with her, no more hunting games, mpaka Mshkaj wangu akawa ananishangaa, nikawa sio mtu wa kutoka tena, ila nikawa naona poa tu, after a long hauling week na hii kasi ya maguboy, who wouldnt settle in for some good s..ex?

Plan yangu ya kupiga na kusepa ikawa inaharibika kila siku zinavyozidi kwenda, she is a cool lady, keeps her head down and the sort, and yeah she run all the home errands(cooking,cleaning and the sort, ma ex su..cked at this)

Kilichonifanya nilete huu Uzi ni kwamba weekend hii ameenda kwao tanga, and am like, yay, back to the hunting game... Nampigia mshkaj namwambia am back chamani, today we hunting vile haijawahi tokea, mida ya jioni natoka mishe huyu mtoto ananipigia simu kaniomba sana nisimsaliti, ghafla mawazo yote ya kutoka yakapotea, jamaa nikampigia nikampa visababu vya kuunga unga, alafu huyu mtoto akanambia kua simu yake haina chaj blah blah+some electric problems huko kwao, analala mapema eti, kanitext na goodnight tiari, wakuu for the first time napata wivu yani, napata mawazo anaweza kua na mtu mwingine, funny thing is am feeling this for someone i never gave two shits about

Hii hapo last text aliyonitumia



Seriously this girl has thrown a monkey wrench into my plan, I was supposed to be hunting, yet here I am f*ck!ng with the internet and drinking alone on a ****!ng Friday night!



Kweli mapenzi hayana formula, i have entirely shaped my attention kwa hawa average ladies!!!

Je Inawezekana Nimelogwa na Huyu mtoto wa Kitanga au ni kawaida ?

By Hainaga ushemeji/JF

VIDEO: Msikilize Mwakyembe Akiongelea Sakata la Richmond, huku Akimtuhumu Nassari Kuingia na Konyagi Bungeni

$
0
0
Juzi Waziri wa Habari, utamaduni, sanaa na michezo Dr. Harrison Mwakyembe alimtuhumu Mbunge wa Arumeru Mashariki Joshua Nassari kwa  kuingia bungeni akiwa amekunywa pombe  aina ya konyagi, huku akijibu tuhusa za sakata la Richmond

==>Msikilize hapo chini



Sakata la Lugumi Bado Halijachacha...

$
0
0

Sakata la mkataba baina ya Kampuni ya Lugumi Enterprises na Jeshi la Polisi, halijafa; ripoti ya Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali (CAG) imeliibua ikionyesha madoa lukuki.

Sakata hilo lilikuwa kama limezikwa baada ya kamati iliyoundwa na Bunge kulichunguza na baadaye kukabidhi ripoti ofisi ya Spika ambayo ilisema ingeishauri Serikali cha kufanya.

Juni 30 mwaka jana, Naibu Spika Tulia Ackson alilieleza Bunge kuwa ametumia kanuni ya 117(17) kuikabidhi Serikali matokeo ya uhakiki uliofanywa na kamati ndogo iliyoundwa na Kamati ya Bunge ya Hesabu za Serikali (PAC).

Alisema matokeo ya ripoti hiyo yana maoni, ushauri, mapendekezo ya namna ya kutatua changamoto zilizoainishwa na taarifa ya kamati ya PAC na hivyo kuzuia wabunge kujadili suala hilo.

Lakini, ripoti ya CAG iliyotolewa wiki iliyopita imeibua upya sakata hilo, ambalo linahusu utekelezwaji mbovu wa mkataba wa uwekaji mashine za kielektroniki za kuchukua alama za vidole (Automated Fingerprint Identification System-Afis).

Ripoti ya CAG inaonyesha kuwa Lugumi Enterprises kufunga mashine katika vituo 36 kati ya 152, hii ikiwa ni tofauti na ukaguzi wa awali ulioonyesha kuwa kampuni hiyo ilikuwa imefunga mashine hizo katika vituo 14 tu kati ya 108 ilivyotakiwa kufunga na kulipwa asilimia 99 ya malipo kwa mujibu wa mkataba.

Ripoti mpya ya CAG pia inaonyesha kuwa mamlaka husika zilisababisha mradi huo kutumia Sh41 bilioni badala ya Sh37 bilioni kama ilivyoonekana katika ukaguzi wa awali uliofanywa katika kipindi kilichoishia Juni 30, 2014.

Msemaji wa Jeshi la Polisi, Advera Bulimba aliomba muda wa kufuatilia taarifa hiyo alipoulizwa na Mwananchi kuhusu ripoti hiyo mpya ya CAG.

“Subiri nifuatilie niione halafu tutawasiliana,” alisema Advera.

Sakata hilo la mkataba wa Kampuni ya Lugumi Enterprises na Jeshi la Polisi liliibuliwa mwanzoni mwa mwaka jana baada ya Kamati ya Bunge ya Hesabu za Serikali (PAC) kubaini ufisadi katika utekelezaji wake.

Katika mkataba huo ilibainika kwamba kampuni hiyo ililipwa Sh34 bilioni sawa na asilimia 99 ya fedha zote za mradi ambazo zilikuwa Sh37 bilioni. Ilifunga mashine katika vituo 14 vya polisi mkoani Dar es Salaam.

Wabunge walimtaka aliyekuwa Waziri wa Mambo ya Ndani, Charles Kitwanga kuwajibika kwa madai kuwa alikuwa mmoja wa wanahisa wa kampuni ya Infosys iliyoshiriki katika mradi huo.

Wakati sakata hilo likikolea Rais John Magufuli alitengua uteuzi wa Kitwanga, akieleza kuwa aliingia bungeni kujibu maswali ya wizara yake akiwa amelewa.

Ripoti mpya ya CAG ya kipindi cha 2015/16 inaeleza kuwa uchunguzi uliofanywa Wizara ya Mambo ya Ndani katika ununuzi wa teknolojia ya mfumo wa kielektroniki wa uhamiaji (E- immigration System) kwa ajili ya Idara ya Uhamiaji, Lugumi Enterprises ilibabaisha katika uwasilishaji wa makabrasha ya zabuni.

Ripoti inasema kuwa Lugumi iliwasilisha makabrasha mawili tofauti ya zabuni yenye bei tofauti ya Sh37.1 bilioni na 39.5 bilioni, jambo lililoathiri uthibitisho wa kabrasha sahihi.

Pia kamati ya tathmini ilishindwa kubaini makosa yaliyowasilishwa na Lugumi, hali iliyosababisha bodi ya zabuni kuidhinisha bei ambayo haikuwa halisi hivyo kusababisha mabadiliko ya gharama za mkataba kutoka Sh37 bilioni kwenda Sh41 bilioni.

Ripoti hiyo inaeleza kwamba, wajumbe wawili wa kamati ya tathmini hawakutia saini ripoti ya tathmini wala kujaza fomu za agano kinyume na Kifungu cha 37(6) cha Sheria ya Ununuzi wa Umma (PPRA) ya mwaka 2011.

Maeneo mengine yaliyotajwa ni pamoja na mkataba wa Lugumi na wizara kuonekana kuwa na baadhi ya vitu vyenye mchanganuo sawa, lakini bei zake zikiwa tofauti, hali iliyosababisha hasara ya Sh656.7 milioni.

Pia, kuna Sh1 bilioni zilizolipwa kama gharama ya mafunzo, lakini mafunzo hayo hayakufanyika wakati Sh3 bilioni zililipwa kwa ajili ya matengenezo lakini pia hayakufanyika.

Pia Lugumi imeonekana kutolipa kodi.
“Hapakuwa na uthibitisho kuwa mzabuni alilipa kodi kwa TRA yenye thamani ya Sh2.2 bilioni kati ya Sh5.7bilioni zilizopaswa kulipwa licha ya mzabuni kupata msamaha wa kodi wa Sh3.5 bilioni katika mkataba wa Sh37 bilioni,” inasema ripoti hiyo.

Pia inaonyesha kuwa baadhi ya gharama za vifaa katika mkataba zilikuwa juu kulinganisha na bei ya soko na hivyo kusababisha hasara ya Sh5.9 bilioni.

Kwa mujibu wa ripoti hiyo, Bodi ya Wakurugenzi wa Mamlaka ya Udhibiti wa Ununuzi wa Umma (PPRA) ililiagiza Jeshi la Polisi kwa kushirikiana na Wakala wa Tehama (e-GA) wa Serikali kufanya tathmini ya kina ya mfumo huu ili kutoa mapendekezo ya hatua madhubuti zinazopaswa kuchukuliwa dhidi ya vifaa vilivyofungwa.

Pia iliagiza Mamlaka ya Mapato (TRA) ifanye tathmini ya kina kama mzabuni alilipa kodi zote zinazostahili katika mkataba, mamlaka za nidhamu zichukue hatua kwa mkuu wa idara ya ununuzi kwa kuidhinisha makabrasha ya zabuni yasiyokuwa sahihi, wajumbe wa kamati ya tathmini kwa kushindwa kubaini makosa katika zabuni.

Pia ilishauri kuchukuliwa hatua kwa maofisa waliohusika katika mapokezi ya vifaa kwa kukubali kuvipokea wakati havikidhi masharti ya mkataba.

Wengine wanaostahili kuchukuliwa hatua ni wajumbe wa Bodi ya Zabuni waliohusika kuidhinisha zabuni kwa Lugumi wakati wakijua hakustahili.

Akizungumzia sakata hilo na ripoti ya CAG, mkurugenzi wa shirika lisilo la kiserikali la Fordia, Bubelwa Kaiza alisema ripoti hiyo imeweka wazi ukweli wote, hivyo sheria ichukue mkondo wake.

Pia, alishauri PPRA kwa kutumia mamlaka yake ifute zabuni ya Afis kwa kampuni hiyo ya Lugumi.

Akizungumzia ripoti ya CAG, Mbunge wa Arusha Mjini, Godbless Lema alisema hotuba ya maoni ya kambi ya upinzani imejaa taarifa nyingi zaidi kuhusu zabuni na mkataba huo na madudu mengine.

Alisema tayari anazo taarifa za kutosha zenye ushahidi kuhusu sakata hilo kwa kuwa anataka kumsaidia Rais Magufuli kufahamu asiyoyafahamu na kuchukua hatua.

“Hotuba yangu itakuwa na ukali wenye lengo la kuibua udhaifu huo. Itakuwa imeainisha wazi zaidi sakata hilo, itakuwa ya tofauti na nisingependa kueleza kwa kina kuhusu hotuba ila kwa ufupi hakuna jiwe litakalobakia juu ya jiwe safari hii,” alisema Lema.    

Lowassa Amchapa Mwakyembe..Habari Vichwa vya Magazeti ya Leo 22/4/2017..!!!

TEMBO Wavamia Kijiji na Kuharibuharibu Mashamba ..!!!

$
0
0

Tembo zaidi ya 20 wamevamia vijiji vya Wenje mpakani mwa Tanzania na Msumbiji wakitokea nchini Msumbiji ambapo tembo wawili wameuawa na wananchi na kuondolewa meno mawili na kugawana nyama yao huku tembo wengine zaidi ya 30 wakivamia kijiji cha jakika wakitokea Pori la Akiba la Selou na kuharibu zaidi ya ekari 50 za mazao mbalimbali.

Hayo yameelezwa na Kaimu Afisa wanyamapori wa wilaya ya Tunduru Bw.Limbega Hassan aliyeongoza kikosi cha askari  wanyamapori waliokuwa wakiangalia usalama wa tembo na wananchi ambapo wananchi wamemng’oa meno mawili tembo mmoja na kuondoka nayo  huku meno mawili ya tembo mwingine yakisalimishwa kituo cha polisi cha Tunduru.

Kaimu Afisa wanyamapori  huyo wa wilaya ya Tunduru anasema kuwa wamewakamata watu watano wanaodaiwa kuhusika na kuwaua tembo wawili na kutoweka na meno huku wekiwatafuta wengine wawili  wawachukulie hatua na pia mikakati ikiwekwa  kuwadhibiti tembo katika vijiji vitano vinavyosumbuliwa na tembo.

Hata hivyo pamoja na makundi makubwa ya  tembo kuingia kwenye vijiji na kuleta taharuki  mkuu wa wilaya Tunduru Bw. Juma Homera amesema kuwa hali ya usalama  iko shwari  askari wanyamapori wamefanikiwa kuwadhibiti tembo hao na hakuna  mwananchi aliyedhurika.

HII Hapa Taarifa Mpya Kuhusu Hali ya Umeme Nchini Kutoka Tanesco..!!

$
0
0

Shirika la umeme Tanzania TANESCO limesema kuwa utunzaji wa vyanzo vya maji vya mto ruaha mkuu ambavyo vinapatikana wilaya za Wanging’ombe na Makete mkoani Njombe unasaidia kuongeza Maji yanayohitajika katika ufuaji wa umeme kwenye mabwawa ya Mtera na Kidatu.

 Kaimu mkurugenzio mtendaji wa TANESCO Dr Tito  Mwinuka akiwa katika ziara ya kikosi kazi maalumu kilicho undwa Hivi karibuni na makamu wa raisi Samia Suluhu Hassani akiwa  mkoani Iringa kwaajili ya kutunza ikolojia ya mto Ruaha mkuu amesema kuwa Asilimia 41 ya umeme unaozalishwa hapa nchini unategemea maji na huwa ni bei nafuu.

Mwenyekiti wa kikosi hicho  kilichopangiawa kuzulu vyanzo vya maji vya mto Ruaha mkuu katika mkoa wa Njombe Katibu Tawala wa mkoa wa Njombe Jackson Ole Saitabau amesema lengo la kikosi hicho kuundwa ni kurudisha hali ya utiririshaji wa maji  katika mto ruaha mkuu.

Baadhi ya wananchi wilayani Wangingombe wanaotunza vyanzo mto Ruaha mkuu vya Mbukwa na Mtitafu vilivyoko katika vijiji vya Nyumbanitu, Igima na Mlevela wameeleza changamoto zinazowakabili katika kuhifandhi vyanzo hivyo pamoja na kutoa mapendekezo kwa serikali kusimamia sheria.

UKWELI Mchungu...Perfume ya Diamond na Niliyoyawaza,,!!!

$
0
0

Nilikuwa napata elimu kidogo ya kibiashara sehemu, na jambo kubwa lilikuwa namna ambayo Diamond kaja nayo juu ya Perfume yake, nimemfikiria Diamond kwa sababu ni staa kama wanavyoweza kuwa mastaa wa michezo pia wakaanzisha biashara zao.

Swali kubwa lilikuwa bei lakini pia Chapa (brand) aliyoingia nayo sokoni.

1. Bei ya Perfume ya Diamond ni 105000, yaani laki moja na elfu tano. Hii ina maana kuwa wenye uwezo wa kununua hii ni kwa kiasi kikubwa nusu ya wale walioweza kulipa Elfu Hamsini kuingia kwenye show yake Mlimani City. Nasema hivi kwa sababu kwa bei hii kuna brand kubwa Ulaya zenye bei jirani na hiyo ambazo watu wataendelea kuzinunua.

2. Washabiki Wengi wa Diamond ni watanzania. Kipato cha siku cha Mtanzania wa kawaida ninaambiwa hakizidi elfu 70 kwa siku kama tukiamua kukadiria juu sana, lakini wengi wanaishi chini ya Dola 5, yaani elfu 12 hivi. Hii ni changamoto.

3. Biashara ya msanii au staa yoyote ni nadra kuhusishanishwa na kazi yake. Kwa mfano Rihanna viatu vya Fenty vipo chinii ya kampuni kubwa za Puma, sio kwamba hawezi kuanzisha kampuni yake. Air Jordan zipo chini ya Nike, sio kwa sababu hakuweza kuanzisha kampuni, Ronaldo na Pestana Hotels aliingia ubia na wafanyabiashara wakubwa. Msingi wa hili ni kuondoa fikra za watu wanaonuua kuendana na mziki au kipaji chako, ili siku ukishuka ubaki katika soko.

Mikataba ya ushirikiano hii uweka mlinganyo wa kudumu zaidi. Hapa Diamond angeweza kuja chini ya nembo ya kampuni yoyote kubwa, na Fragrance zake zikaitwa hata Armani Chibu, na hii ingefanya Giorigio Arman wafungue kampuni yake nchini.

4. Lakini pia huwa namkubali Diamond kwenye promotion. Sidhani katika hii chibu kama alifanya maandalizi sahihi. Ile amusement na excitement (kufurahia na kuitamani) bidhaa hajaiweka kipindi hiki. Hata yeye mwenyewe hajaonekana katika promo hata kujaribu kuonyesha ina harufu gani, inafaa chumbani kwa namna gani, mtu atafeel vipi akiwa nayo ofisini na mambo mengine ambayo yangevuta wateja wake.

5. Mwisho, bado naamini Diamond ni mpiganaji, kijana wa kipekee na ambaye anajaribu kuleta utofauti wa kufikiri katika kila jambo na kuweka misingi ya fikra za ujasiriamali. Lakini nahisi hili hapa lilichangiwa kwa kiasi kikubwa kuamini katika jina lake kabla ya kufanya utafiti wa walaji wake. Hii ingeambatana na Deodorant na Spray ambazo zingekuwa bei rahisi, angewachota wa Masaki na kwa bibi yangu Magu pale Mwanza.

Mwisho wa siku, bado anahitaji kupongezwa, ni uthubutu wa kipekee huu. Akili yake nimeshindwa kuifananisha na staa yoyote wa Tanzania kwa sasa, katika sekta zote. Hawapo jirani yake, lakini alipoelekea sasa, Menejimenti yake inatakiwa kuwa makini. Uwekezaji huu sio wa muziki sasa, misingi ya uchumi, biashara izingatiwe. Sio kipaji tu huku, ni mahesabu kwelikweli.

Ni mimi mpendasoka Nicasius Agwanda (Coutinho). Nimeandika baada ya kupewa elimu pia.
Viewing all 104709 articles
Browse latest View live




Latest Images