Quantcast
Channel: UDAKU SPECIAL
Viewing all 104756 articles
Browse latest View live

Unajua Hii ...Kuchukua Mkopo Benki na Kujengea Nyumba ni Jambo Jema Lakini Hasara Yake ni kubwa..!!!

$
0
0

Mikopo tunayokopa benki hapa nchini Tanzania zina riba kubwa sana kitu ambacho hufanya watanzania wengi kutofaidika sana na mikopo hiyo. Kwani kuna benki hutoza riba zenye faida ya asilimia 18%-23%.

Watanzania tulio wengi tukishachukua mikopo hiyo hukimbilia kuninua uwanja na kuanza kujenga nyumba, kisha huishi maisha ya shida sana kwa kipindi cha miaka minne mpk mitano. Wapo wengine hukimbilia kununua gari ili waonekane hapa mjini lakini hata uwanja hawana, mikopo hiyo ya benk ina mambo sana.

Wazo la kukimbilia kujenga nyumba kwa kutumia mkopo ni kujitengenezea maisha ya dhiki sana kwani makato huwa makubwa na kufanya kila siku kukimbizana na madeni yasiyoisha. Ushauri wangu na maoni yangu kama unataka kujenga au kununua gari ni bora ujiwekee mkakati binafsi unaweza amua kila mwezi kujiwekea kiasi fulani ambacho unatumia kwaajiri ya ujenzi, utafanya hivyo bila riba wala hasara yeyote.

Mikopo ya benki ni yakuwekeza katika biashara na ili ziongeze kipato na biashara hiyo irudishe mkopo huo yenyewe bila we kuathiri mapato ya kazi yako.

Kuweka pesa kila mwezi au kila sikunkutokana na maingizo yako inawezekana, kikubwa ni uamuzi thabiti na kujiwekea malengo na kuhakikisha unayafikia malengo yako.

Huu ni ushauri na maoni yangu jinsi ninavyoona namna ya kutumia mkopo wa benk kwa faida, lakini hata kama mtu akajenga nyumba ya biashara ni sahihi lakini nyumba ya kuishi ni safi sana lakini kuna hasara kubwa ndani yake.

HIVI Ndivyo Bank Zinavyokunyonya na Kukuletea Umasikini Bila Wewe Kujijua na Kushtukia Mchezo Unavyokuwa..!!!

$
0
0

Hivi kwa nini ma-bank ambayo hayazalishi chochote (isipokuwa kuwapatia wateja wao huduma zisizo za viwango) nimatajiri kuliko taasisi zingine?Angalia Chase nManhattan,Goldman Sacks, Barcklays nk. Na inakuaje kila biashara inakabiliwa na madeni ya bank?

Na inakuaje bank ndizo zenye majengo mazuri mjini tena bila mortgage au mkopo wa aina yeyote,wakati viwanda na watu wengine wanahangaika usiku na mchana ili kuweza kulipa mikopo ya ma-bank waliyopata kwa kuweka dhamana mali zao?

Mtu angedhani watu wa viwanda na Kilimo ambao wanazalisha bidhaa muhimu kwa maisha ya watu,ndio ambao wangekuwa matajiri zaidi ya wenye mabenki ambao kwa asili walikuwa wawekaji tu na watunzaji wa fedha za wateja wao na wenye mabenki wangekuwa watumishi tu,tena wa chini wa wenye viwanda nk,lakini sio. Siri ni nini?

Siri ni kwamba bank zina "leseni"ya kuchapa fedha,fedha ambazo hazitokani na kufanya kazi,au fake money, au money created out of nothing! Wenye viwanda na wateja wengine wamebanwa na ukweli huu mchungu mno.

Jambo la kushangaza ni kwamba hakuna mtu anayetaka kuongelea ukweli huu,ambao unaonekana kama taboo. Wataalam wetu wa uchumi,wana siasa,wana habari, watawala,wanaelekea kutokuwa tayari kuzungumzia swala hili. Vitabu vyote, makala zote, mikataba, majarida, documentaries za TV,vikundi mbali mbali vya majadiliano,vyuo vikuu,taasisi zingine mbali mbali,wote wako kimya kuhusu uonevu huu, kana kwamba haupo.

Rothschild Brothers(London,1863)wamesema,

"Wachache wanaoelewa mfumo huu hawataki kabisa kuuongelea kwa sababu ya faida wanazozipata." 

Njia rahisi ya kuona jinsi bank zinavyofanya kazi ni kufikiria piramidi iliyogeuzwa, upande uliochongoka chini na upande bapa juu. Sehemu iliochongoka inawakilisha fedha halisi za bank,ambazo zamani zilikuwa ni coins za dhahabu na fedha.Juu ya hapo ni viwango mbali mbali vya mikopo kwa wateja wa mabenki.

Mikopo hii sio fedha halisi,kwa kuwa haikupatiiokana kwa kufanya kazi! Hata hivyo wateja waliochukua mikopo hii, inabidi walipe mikopo hiyo na faida kutumia fedha halisi ambazo wamevuja jasho kuzipata!Huu ndio mfumo wa ajabu ambao tunautumikia kwa miaka mingi na mfumo ambao ndio kwa kweli unaofanya thamani ya fedha ipungue.

Ingekuwa busara kama serikali za dunia zingekuwa na vitengo maalum vinayvohusika na uchapaji wa fedha. Kwa namna hiyo serikali zisingehangaika na madeni ya ndani.Ni jambo la ajabu kwamba tumeruhusu bank zichapishe fedha na kubadili riba wanavyotaka.Si ajabu kwa hiyo kwamba tunakuwa na vipindi vya hali nzuri ya uchumi (boom and slumps or financial crises and depressions),vitu ambavyo vinasababishwa na kuongezeka au kupunguza fedha kwenye circulation,hali ambayo imeyapa mabenki mamlaka kubwa mno juu yetu.Hii imeleta hali ya kuwa na watu ndani ya mabank wenye mamlaka kubwa mno.Watu hawa hawawajibiki kwa yeyote isipokuwa kwao wenyewe.Kwa kutumia nguvu ya pesa waliyo nayo wamenunua wana siasa na kuwa na ajenda za ajabu zenye nia ya kuendelea kujilimbikizia mamlaka na madaraka ili wasiguswe.Hatimaye wanaishi maisha ambayo sisi wengine tunayaota tu.

Kupitia kwa wanasiasa hao na kutoa misaada kwa vikundi mbali mbali kama Freemasons,Club of Rome,Council of Foreign Relations,Media na Charities mbalimbali,mabenki yameweza kuwa na maamuzi makubwa kwenye nchi nyisecrengi duniani.Wako nyuma ya uanzishwaji wa tu kama European Union,African Union na jumuiya zingine za kikanda.Hawa pia ndio wanaohusika kwa kiwango kikubwa kuwafanya viongozi wengi wawe wasioeleweka na kusema ukweli.
References:
Google
1.The hidden secrets money.
2.Ancient banking secret.
3.The FED(The Federal Reserve Bank) is a commercial privately owned bank.
4.Federal Reserve Bank ownership. Factcheck.org
5.Google pia "Quotes on Banking and the Federal Reserve system FRAUD"upate ukweli zaidi.Hizi quotes kama zitasomwa zitaleta uelewa mkubwa sana juu ya mada iliyoko mezani.
Naomba nikumbushe kwamba mada hii kwa kawaida hakuna mtu aliyeko tayari kuzungumzia,kwa hiyo haifundishwi darasani!Come with an open mind kwa nia ya kujifunza.Ubishi bila facts hautatusaidia sana.

BAADA ya Tetesi Kuwa Nyingi juu ya Dogo Asley Kutaka Kujieungua na Ya Moto Band..Said Fella Ameibuka na Haya..!!!

$
0
0

Mkurugenzi wa Yamoto Band, Saidi Fella ‘Mkubwa Fella’ amedai kuwa hakuna msanii aliyekatazwa kuondoka ndani kundi hilo.

Aidha amedai kuwa wasanii wa bendi hiyo wanaruhusiwa kufanya project zao binafsi za muziki.

Fella ambaye ni mlezi wa wasanii 106, amesema kuwa kituo chake ni kama shule, yeyote ambae anajiona amekuwa anaweza kuondoka.

“Hakuna msanii ambaye amekatazwa kuondoka Yamoto Band hata Mkubwa na Wanawe ila ukiondoka bila kuaga haufiki sehemu yoyote,” alisema Fella.

Aliongeza, “Mimi nawasaidia kuwaonyesha njia wafike sehemu fulani, mtu akijiona amekuwa kwanini nimzuie?. Hakuna aliyefungwa kwa namna yoyote, sema ni vyema mtu kufuata taratibu hata za makuliano yetu ya mdomo,”

Pia Fella alidai hakuna msanii aliyekatazwa kuachia kazi zake binafsi.

“Aslay hivi karibuni ameachia kazi yake mpya na sisi tunamsupport kwa sababu kabla ya Yamoto Band, Aslay alikuwa msanii ila sisi tulimtumia yeye kuwainua wenzake na kweli tumefanikiwa leo hii vijana wanapata makate wao wa kila siku. Kwa hiyo hata wasanii wenzake wanaweza kufanya hivyo pia lakini kama wanamakubaliano yao binafsi siwezi kuyaingilia,” alisema Fella.

Bendi hiyo kwa sasa inafanya vizuri na wimbo ‘Basi’

HARMORAPA - Sijawahi Kuachwa na Mwanamke..!!!

$
0
0

Msanii wa muziki wa bongo fleva Harmorapa amefunguka na kusema kuwa katika maisha yake hajawahi kabisa kuachwa na mwanamke bali yeye ndiye huwa anawaacha hivyo hajui suala la maumivu ya mapenzi.

Harmorapa alisema hayo alipokuwa kwenye kipindi cha Kikaangoni kinachorushwa kupitia ukurasa wa Facebook wa EATV, na kudai yeye hajui maumivu ya mapenzi kwa kuwa hajawahi kuachwa na mwanamke.

"Hapana mimi sijawahi kutoswa, kuachwa na mwanamke haijawahi kutokea kwangu, mimi ndiyo huwa nawaacha ila si kuachwa" alisema Harmorapa 
 

AT - Mcheezeeni Ali Kiba ,Anayekaa Kimya Hata Akitukanwa Mimi Hamniwezi..!!!

$
0
0

Msanii wa muziki miondoko ya mduara nchini, AT amchana vikali 'dancer' na msanii Msami kwa 
kumwambia kwake siyo mahali pakuchezea kama anavyodhania huku akimtaka aende kwa Alikiba kwakuwa ni mnyonge hata akitukanwa hukaa kimya.

Hayo yameibuka baada ya Msami kumtaka AT aboreshe kazi zake badala ya kulalamika kuwa kuna watu wanaobebwa huku akijitapa kuwa dancers wana maisha mazuri na mafanikio makubwa kumzidi yeye.

“Hawa watoto huku kwangu siyo pakuchezea, mchezeeni Alikiba mnyonge anakaa kimya hata mkimtukana hajibu kitu ila huku kwangu waachane napo siyo kwa kawaida na kama hawataki basi wajaribu zali kama wenzao halafu watapata majibu yao”. Alisema AT

Aidha AT alifika mbali zaidi kwa kusema yeye ni msanii bora kuliko anavyomchukulia kwa kuwa anaweza kucheza na ‘vocal sound’ kwa kuiga sauti  wasanii wakubwa huku akitolea mfano kwa Bi. Kidude, Oliver Mtukuzi pamoja na Chriss Brown

 “Wewe hunijui,  umeenda tu kuruka ruka sehemu umechukuliwa baadae umejiona umeimba chooni ukadhani unajua kuimba. Mimi mwenzio nimeenda chuoni”. Alisisitiza AT

Mbali na hilo AT aliwataka watu ambao wanatafuta majina kupitia yeye wakome kabisa tabia hiyo kwani yeye ni mtu mbaya akisema siku aachie mabomu yake hawataweza kuvumilia kwani watatafutana, hivyo kama wanataka kiki waende kwa Harmorapa lakini si kwake. 

Bodi ya Filamu Yakanusha Kuzuia Filamu za kigeni

$
0
0

Dar es Salaam. Bodi ya Filamu Tanzania, imekanusha taarifa zilizosambaa katika vyombo vya habari na mitandao ya kijamii kuwa Serikali inazuia kwa makusudi uingizaji,usambazaji na uuzwaji wa filamu za kigeni nchini. 

Madai ya taarifa hiyo ni kwamba Serikali ina lengo la kuwalazimisha wananchi kuangalia filamu za ndani (bongo movie). 

Taarifa iliyotolewa kwa vyombo vya habari na bodi hiyo leo zinaeleza kuwa habari hiyo haina ukweli wowote na umma wa Tanzania una tahadhalishwa kuipuuzia . 

“Taarifa hizi zina lengo la kupotosha na kudhoofisha juhudi za Serikali za kuhakikisha kila mtu anafanya biashara ya filamu kwa kufuata sheria na kanuni zilizopo,”imeeleza taarifa hiyo.

BADO Mienendo Yake Huielewi..Fanya Hivii..!!!!

$
0
0

WAKATI mwingine unaweza kujikuta njiapanda muda wa kutaka kuchukua maamuzi. Kila unachotaka kufanya unahisi kama unahitajika muda zaidi au uvumilivu zaidi. Katika maisha vitu vya namna hiyo huwa vinatokea!

Umeshawahi kuwa na mtu na kujikuta kama humuelewi hivi, halafu ukashindwa kujua ni uamuzi wa aina gani unafaa kuuchukua? Mtu ambaye unajitahidi kwa kila hali kumuonesha namna unavyompenda ila wapi! Anakuchukulia kawaida tu.

Wala haoneshi kuthamini wala kuheshimu upendo na mapenzi unayomuonesha. Ulishawahi kuwa naye? Au ndiyo huyo uliye naye? Hapa suala ni moja tu. Mueleze namna unavyojisikia kwa tabia yake.

Katika kumweleza huku unapaswa kutafuta siku ambayo ni tulivu, kwa maana kila mmoja asiwe na kazi kwa muda huo ili maongezi yenu yapate heshima inayostahili.

Tumia nafasi hiyo kuwasilisha yote ya moyoni unayojihisi juu ya tabia yake. Mwambie katika hali isiyokuwa ya kulaumu wala jazba. Eleza namna yote unavyoteswa na tabia yake isiyoonesha kukupenda wala kuuthamini upendo wako.

Baada ya kuhakikisha tayari anajua namna unavyojisikia, sikiliza atakachokisema. Kuwa makini kupima kauli zake na jinsi sura yake inavyomaanisha. Wengine wanaweza kukupa majibu mazuri huku sura yake ikiwa inaonesha dharau na kejeli. Haina maana!

Pima uzito wa maneno uliyomwambia na majibu atakayokupa. Ukiona vina uwiano na ni majibu mazuri, mpe nafasi nyingine hata kama hiyo ni mara ya pili anakukosea. Kuwa mvumilivu – bila uvumilivu hakuna mapenzi ya kweli. Uvumilivu ni mama wa mafanikio.

Baada ya kuwa tayari umemweleza jaribu kusahau makosa yake na ufungue ukurasa mwingine katika maisha yenu. Hapo haitakiwi tena kukumbushia makosa yaliyopita.

Hiyo itamnyima uhuru wa kufurahi kikamilifu na wewe pia kuna uwezekano mkubwa wa kuchochea migogoro isiyo ya lazima katika mapenzi yenu.

Maana unaweza kumkumbusha hili na yeye akakukumbusha lile. Na kila mmoja hapo akataka kumuona mwenzake ndiyo mkosaji zaidi. Mapenzi hayawezi kuwa mazuri kwa staili hiyo.

Baada ya kuwa mmemaliza tofauti zenu anza kuangalia mabadiliko chanya katika matendo yake. Ni kweli kabadilika? Au kilichobadilika ni staili tu ya kukunyima furaha ila balaa ni lile lile?

Kama alikuwa na skendo za vimada sasa huzisikii ila kila siku safari zisizokuwa na sababu na ukijaribu kuuliza anakwambia “kuna mambo naweka sawa”. Mambo gani? Hakwambii! Akirudi ‘break’ ya kwanza bafuni akaoge kwanza ndiyo arudi muongee.

Ikiwa unamfanyia mpenzi wako kila lililojema katika mahusiano na bado haoneshi kubadilika zaidi ya kukusema “we msemaji sana” au anatoa ahadi tu zisizotekelezeka, kuna jambo la kufanya.

Kaa naye kisha mueleze kwa mara ya mwisho juu ya tabia yake na umueleze hatua unayokwenda kuchukua kama asipobadilika. Mapenzi ni raha na amani. Kama mtu hakupi hayo basi hakufai.

Kwa nini kila siku mahusiano yako yawe ya masimango na majuto yasiyokwisha? Kila siku machozi yatoke kwako tu. Kwani wengine hawana wapenzi? Mbona hawalalami wala kuumizwa?

Unapaswa kujua kitu – anayekupenda atakujali na kukuthamini. Hata siku moja hatapenda kuona unahangaika na kulia kwa sababu yake. Ukiona mtu anaona unaumia na kuteseka kwa ajili yake halafu hana habari na wewe jua kuna namna. Siyo bure.

Kama hakuna ulichomkosea wala kumkera basi jua hana mapenzi na wewe. Iweje akupende halafu asijali chozi lako? Kivipi aseme anakuthamini wakati hajali maumivu yako? Kuwa makini. Kuwa makini zaidi!

JINSI Ya Kumsisimua Mwanamke Kabla Ya Kulala Naye..!!!

$
0
0

Wakati umemualika mwanamke sehemu unayoishi ama wakati umetoka deti katika bar, unapaswa kujua ya kuwa kumsisimua mwanamke huanza kabla ya nyinyi wawili kulala pamoja.

Unapaswa kumsisimua kuanzia nafasi ya kwanza ambayo utaipata kutoka kwake. Kufanya hivyo kutamfanya akutake hata zaidi na kumfanya ajiandae na mapema kabla hata kulala naye. Lakini ni mbinu gani inayoweza kutumika kumsisimua mwanamke kabla hamjalala pamoja?

Zama nami...

Kutumia maneno

Maneno yanaweza kumsisimua mwanamke asilimia mia. Mwanzo wanawake husisimuliwa na vitu wanavyosikia zaidi kuliko wanavyoona. Hii ndio tofauti kuu kati ya jinsi ya kumsisimua mwanaume na mwanamke. Hauhitaji kuonekana mchafu wakati ambapo unamsisimua mwanamke kwa kutumia maneno. Mwanzo anaweza kusisimulika na jinsi ambavyo anakusisimua wewe.

 Unaweza kumwambia maneno kama "Siwezi kungojea ile siku ambayo nitakuwa pekeangu na wewe", "Nimeanza kuingiwa na mawazo nikifikiria hio nguo uliyovaa inaficha nini" ama maneno mfanano na haya.

Lakini kando na kuwa maneno yanamsisimua mwanamke, kutategemea pia na vile ambavyo unamshika na miguso yako.

Kutumia miguso

Hapa ndipo utaleta utofauti wa yote. Miguso ni mbinu nzito na ya nguvu kama unaazimia kumfanya akutamani, kabla hata nguo za yeyote kuvuliwa, kabla ya nyinyi wawili kuanza kubusiana ama kufanya chochote. Baadhi ya mifano ya kufuata ya kumsisimua mwanamke kwa miguso ili aweze kukutamani kabla ya nyinyi wawili kulala pamoja ni kama ifuatayo

Kuzivuta nywele zake kiulaini: Usizivute nywele zake hadi ukazing'oa kichwani mwake. Lakini usiogope kuzishika baadhi ya nywele zake na kuzichezea kimvuto.

Miguso ya kukawia: Wakati ambapo unamgusa kikawaida - kwa mfano, wakati mikono yako iko katika mabega yake, mgongo au mkono - usiogope kuuzuia mkono wako ukawie sehemu hizo kwa dakika moja.

Karibu kumla dende: Hii ni siri kubwa ambayo inahakikisha gemu yako kuwa ya juu. Usikimbilie kumbusu. Jiweke katika hali ambayo nyinyi wawili mko "karibu" kubusiana. Hii itamfanya aingiwe na wazimu wa kutaka kuibusu midomo yako haraka kuliko ulivyokuwa ukitarajia.

Kumkwaruza kiulaini: Unapomgusa, usiogope kuzipitisha kucha zako kwa mgongo wake, nyuma ya shingo yake na sehemu mfanano na hizi. Hii unaweza kuitumia wakati ambapo mshajenga uhusiano wa ndani kati yenu.

Mtizamo wa macho: Kumuangalia mwanamke kwa macho pekee kunaweza kumfanya apandwe na mzuka. Mwangalie machoni, zaidi kuliko yeye. Kufanya hivyo kunaashiria ujiaminifu. Ijapokuwa mbinu hii haitumii miguso, inaweza kufanya kazi sawa na kama vile matumizi ya miguso kabla nyinyi wawili kulala pamoja.

Ok hizi ni baadhi ya mbinu za kumfanya mwanamke asisimke kabla kulala na yeye. Unaweza hata pia kuamua kumpandisha nyege bila kutumia miguso yeyote.

MAMBO 3 Yanayofelisha Maisha..!!!

$
0
0

1. Kulalamika katika kila kitu
2. kulaumu watu wengine kwa shida zako na matatizo yako
3. Kutokuwa mtu wa shukrani

UTAFITI: Kuangalia TV Kupita Kiasi Hupunguza Uwezo wa Kuzalisha Mbegu za Kiume..!!!

$
0
0

Kuangalia TV ni sehemu ya maisha ya asilimia kubwa ya watu duniani hivi sasa, lakini utafiti umeonesha kuwa wanaume wako kwenye hatari ya kupungua uwezo wa kuzalisha mbegu za kiume pale wanapotumia muda mwingi kuangalia TV.

Kabla hujaanza kubisha, soma kwa makini utafiti huu. Wenzetu husema ‘no research no right to speak’.

Utafiti huo ulifanywa hivi karibuni na wataalam kutoka Chuo Kikuu cha Copenhagen, umeonesha matokeo hayo baada ya kutumia sampuli ya vijana wa kiume 1,200.

Utafiti huo uliochapishwa kwenye Jarida la Marekani la ‘Epidemiology’ ulionesha kuwa wanaume wanaopenda kuangalia TV (kwa saa tano na zaidi) walitoa wastani wa mbegu za kiume (sperm counts) milioni 37 kwa mililita moja, huku wale ambao hawakuwa na tabia ya kuangalia TV kabisa walitoa wastani wa mbegu za kiume milioni 52 kwa mililita moja.

Mwanaume huwa katika hali ya kawaida pale anapokuwa na wastani wa mbegu milioni 40 kwa mililita moja hadi milioni 300 kwa mililita moja. Lakini kuwa na kiwango cha mbegu chini ya milioni 10 kwa mililita moja huchukuliwa kama kiwango duni cha uzalishaji wa mbegu za kiume.

Katika sababu zilizotolewa kufikia matokeo hayo, wataalam hao wameeleza kuwa huenda hilo hutokana na ukweli kuwa wanaume wanaotumia zaidi ya saa 5 kuangalia TV hukosa muda mzuri wa kufanya mazoezi na kula kiafya, mambo ambayo ni muhimu kwa afya ya uzazi wa mwanaume.

POLISI Wafanikiwa Kuua Majambazi Matatu Yalioua Askari Nane Mkoani Pwani..!!

$
0
0

Utata umezuka baada ya kuwepo kwa taarifa za polisi kuua watu sita wanaodaiwa kuwa majambazi wilayani Kibiti.

 Kamanda wa Polisi mkoa wa Pwani, Onesmo Lyanga alisema anafuatilia ukweli wa tukio hilo.

 Mkuu wa Operesheni wa Jeshi la Polisi, Nsatu Marijani, alisema kama taarifa hizo zingekuwa za ukweli basi jeshi hilo lingetoa taarifa.

 Hata hivyo, chanzo kimoja cha habari kutoka wilayani humo kililiambia Mwananchi kuwa polisi imewaua watu sita.

 Pia chanzo hicho kilieleza kuwa milio ya  mabomu na risasi ilisikika katika maeneo kadhaa ya kijiji cha Jaribu , Mpakani, wilayani humo.

Mama kuwa makini House Girl Yaweza Kuwa Mke Mwenzio

$
0
0

Ivi ni vibaya House girl kuolewa na baba mwenye nyumba? 

Ndugu msomaji wa Muungwana Blog, karibu kwenye makala hii maalumu, nimeamua kuandika habari hii ili kujaribu kupunguza mifarakano kwenye familia zetu especially familia zenye wafanyakazi wa ndani wanaojulikana kama house girl. 

Katika mada hii nimekuwa nikikutana na maswali mengi sana ambayo mda mwingine yalikuwa yakituchanganya hata sisi wenyewe katika kuwajibu wahusika, maswali haya malanyingi yalikuwa yakiulizwa na akina mama. 

Na kwa upande wa akina baba maswali yao sio mengi ukilinganisha na akina mama, sasa napenda nianze kwa kusema mambo yafuatayo ili wote twende sawa. 

WAJIBU WA MWANAUME KATIKA FAMILIA:  
Mwanaume anawajibu wa kutimiza mahitaji yote ya msingi katika familia yake, moja ya majukumu hayo ni pamoja na kutoa pesa za matunzo ya familia yake kadri ipasavyo, kuonyesha upendo wa dhati kwa mama pamoja na watoto wake, na mambo mengineyo nk. 

WAJIBU WA MWANAMKE KATIKA FAMILIA:  
Mwanamke ndiye mtendaji mkuu wa familia kwa upande wa nyumbani ukiachilia mbali ya kwamba baba ndiye kichwa cha familia, mwanamke anamajukumu mengi kwa upande wa nyumbani moja ya majukumu yake ni pamoja na kupika chakula cha familia, kufua nguo za mumewe pamoja na nguo za watoto, kuakikisha nyumba pamoja na eneo linaloizunguka nyumba ni safi, kuonyesha upendo wa dhati kwa mumewe pamoja na watoto wake, nk. 

Ndugu msomaji wa makala hii, nadhani mpaka hapo tayari umeisha anza kupata mwanga kuhusu jibu la swali la makala yetu, sasa twende kuona wajibu wa mfanya kazi wa ndani kama house girl. 

House girl wajibu wake ni kuakikisha anafanya usafi wa kuizunguka eneo la  nyumba kwa nje na kufanya usafi huo kwa upande wa ndani kwa baadhi tu ya maeneo ya nyumba hiyo pamoja na kuwaogesha watoto, kufua nguo za watoto, na kufanya kazi ndogo ndogo za nyumbani. 

House girl hatakiwi kufanya usafi chumbani kwa mume wa mama mwenye nyumba, house girl hatakiwi kufua au kupiga pasi nguo za mume wa mama mwenye nyumba, house girl hatakiwi kumuandalia chakula au chai mume wa mama mwenye nyumba, nk. 

Sasa ukiona house girl anafanya kazi zote nilizosema kuwa hatakiwi kuzifanya pindi awapo nyumbani kwako, ukiwa kama mama mwenye akili timamu jua kabisa tayari umeamua kumuletea mumeo mke mdogo na pia usipige kelele wala kulaumu maana jitihada zote za kumuandaa mke mwenzio umezifanya wewe mwenyewe. 

Ushauri wangu kwenu akina mama na akina dada nikwamba, hatukatai kuwa wafanyakazi wa ndani hawafai, ila jitaidi mfanyakazi wako awe na mipaka ya kazi, mwanaume anaamua kumuoa house girl kwa sababu yeye amechukua majukumu yote ya mama mwenye nyumba, sasa wewe mama usianze kumtupia maneno mtoto wa watu pamoja na mumeo maana yote hayo umeyataka wewe mwenyewe. 

Julius Mtatiro afunguka Baada ya CUF Kuvamiwa na Watu Wasiojulikana

$
0
0

KUFUATIA Kundi la watu wasiofahamika waliokuwa wamevalia kininja wakiwa na MAPANGA na BASTOLA moja kuvamia mkutano wa Chama Cha Wananchi (CUF) na kudaiwa kuwapiga viongozi na wanahabari. 

Katika Mkutano huo, Mwenyekiti wa CUF wilaya ya Kinondoni na Mjumbe wa Baraza Kuu Mhe. Juma Mkumbi alikuwa anazungumza na Vyombo vya Habari katika Hoteli ya Vina iliyoko kata ya Mabibo, Dar ambapo baada ya tukio hilo la kutisha, wananchi na wafuasi wa CUF waliokuwa eneo la tukio walitaharuki. 

KUHUSU KUNDI LA LIPUMBA KUVAMIA VIONGOZI WA CHAMA… Wengi mmeniuliza kuhusu viongozi wa CUF kuvamiwa, ni kweli. Leo Mwenyekiti wa CUF wilaya ya Kinondoni na Mjumbe wa Baraza Kuu Mhe. Juma Mkumbi alikuwa anazungumza na Vyombo vya Habari katika Hoteli ya Vina iliyoko kata ya Mabibo, Dar. 

Ghafla mkutano wake ukavamiwa na kundi la Lipumba liitwalo MUNGIKI. Wavamizi hao walivalia kininja wakiwa na MAPANGA na BASTOLA moja. Wavamizi wakaanza kuwapiga viongozi na wanahabari wakiwatuhumu kuwa kwa nini hawamuungi mkono Lipumba.Waandishi Na kadhaa na viongozi kadhaa wamejeruhiwa, kuporwa simu zao, kamera, vitendea kazi, fedha n.k. Wananchi wa Mabibo waliposikia mayowe na kelele za kuomba msaada walipandisha ghorofani (kwenye PRESS) ili kutoa msaada. 

Kuona wananchi wanakuja kwa wingi, kundi la MUNGIKI likaanza kushuka mbio kuelekea kwenye magari mawili waliyokuja nayo. Baadhi ya Mungiki hawakuyafikia magari na wakazidiwa nguvu na wananchi. 

Huyu aliyeko pichani ni Mungiki mmojawapo aliyedhibitiwa na wananchi wenye hasira kali, baada ya kumkimbiza na kumkamatia mitaanu ambapo inasemekana amevunjwa kisigino na mfupa umetokea nje (So sorry and sad). Huyu wa pichani pia ni mmoja wa walinzi wa Lipumba na mara nyingi huwa pamoja na Lipumba. Bahati nzuri, vyombo vya habari vimemhoji mbele ya wananchi na amekiri kuwa UVAMIZI walioufanya umetokana na maagizo ya LIPUMBA. 

Chama chetu kimekwishatoa taarifa rasmi kwenye vyombo vya habari (unaweza kuisoma kwenye ukurasa wangu wa FB). Tumestushwa na kusikitishwa sana na tukio hili baya na la aibu kabisa. 

Chama chetu kimetoa pole kwa waandishi wa habari na viongozi wa majukwaa ya waandishi na kimelitaka jeshi la Polisi lichukue hatua za haraka dhidi ya LIPUMBA na genge lake lijiitalo MUNGIKI. 

#Mtatiro J 


annayesayaDuuu inasikitisha hapo lipumba hayupo wewe unavunjwa kiuno nyie vijana acheni siasa chafu on a sasa umepata chai ya kutoshajr.huseniNae process uchwara ama kweli kisicho riziki hakilikimmahmoudjabirMasikini roho yake

WAKATI Sekeseke la Watu Kupotea Likizidi Kushamiri..Mwingine Akutwa Amekatwakatwa Mapanga na Kutelekezwa Msituni..!!

$
0
0

MKAZI wa kijiji cha Tingeni wilayani hapa Mkoani Tanga, Philipo Fred Elias (45) ameuawa kinyama kwa kuchinjwa na watu wasiojulikana kwa kutumia panga wakati akirejea nyumbani kwake akitokea kijiji cha Kerenge kwenye shughuli zake.


Kamanda wa Polisi mkoa wa Tanga, Benedckt Wakulyamba, alisema kuwa mtu huyo alifikwa na mauti hayo juzi wakati akirejea nyumbani kwake katika kijiji cha Kerenge saa 2:00 usiku akitokea kijiji cha Tingeni.

Alisema mtu huyo akiwa njia kurejea kijijini kwake akiwa na pikipiki ghafla alikutana na watu ambao idadi yao haijulikani walimsimaisha na kuamkamata na kuanza kumchinja kwa kutumia panga hadi kufariki.

Kamanda Wakulyamba alisema mauaji hayo yalifanyika katikati ya pori linalounganisha kijiji cha Tingeni na Kerenge ambapo vijana waliofanya tukio hilo walikimbia kusikojulikana.

Aliongeza kuwa mwili wa marehemu uligundulika na wapiti njia ukiwa pembeni mwa barabara na pikipiki yake ikiwa imetelekezwa ndipo zilifanyika jitihada za kutoa taarifa kwa viongozi wa kijiji ambao nao waliwataarifu polisi.

Hata hivyo, alisema kuwa marehemu alikuwa akituhumiwa kwa vitendo vya ujambazi na unyang’anyi wa kutumia nguvu na tayari enzi ya uhai wake ameshakamatwa mara kadhaa kwa matukio hayo na kufikishwa katika kituo cha polisi kwa tuhuma za ujambazi.

Kufuatia tukio hilo, jeshi la Polisi linafanya msako wa kuwasaka na kuwakamata waliohusika na mauaji hayo ya kinyama ili sheria iweze kuchukua mkondo wake na mwili wa marehemu umehifadhiwa katika Hospitali Teule Wilaya ya Muheza.

Kamanda Wakulyamba ametoa wito kwa wananchi kuacha vitendo vya kujichukulia sheria mikononi kwa kuwa kufanya hivyo ni kosa kubwa la jinai kama mtu wanamtuhumu anavitendo vya ujambazi wamkamate wampeleke polisi.

Wanajeshi wa Kenya Wawaua Wapiganaji 50 wa al-Shabab

$
0
0

Wanajeshi wa Kenya wamewaua takriban wapiganaji 50 wa kundi la al-Shabab nchini Somalia 

Jeshi la Kenya linasema kuwa limewaua zaidi ya wapiganaji 50 wa Al-Shaabab katika oparesheni iliyofanywa Kusini mwa Somalia. 

Jeshi hilo lilisema lilinasa shehena ya silaha na risasi na kuharibu kabisa kambi ya wapiganaji hao katika eneo la Badhaadhe katika Lower Juba. 

Hadi sasa Al Shaabab hawajasema lolote. 

Maelfu ya wanajeshi wa Kenya wanahudumia nchini Somalia chini ya mwavuli wa Muungano wa Afrika. 

Al Shaabab hufanya mashambulizi ya mara kwa mara kwenye mpaka na Kenya na pia kwenye kambi za wanajeshi wa Kenya walioko Somalia.

Quick Rocka akana kutoka kimapenzi na Kajala Licha ya Kunaswa Wakidendeka

$
0
0

Quick Rocka amejitokeza na kudai kuwa hatoki kimapenzi na malkia wa filamu, Kajala Masanja na kusema hizo ni stori za uongo.


Quick Rocka aliwahi kupost video mtandaoni akidendeka na mrembo huyo.

Akiongea katika kipindi cha FNL cha EATV, akitambulisha video yake mpya ya wimbo ‘Down’, Quick Rocka amesema hajawahi kutoka na mrembo huyo wa Bongo Movie.

“Stori kuwa nilikuwa natoka na Kajala ilikuwa ya uongo, usitake nitafutia matatizo” alisema Quick Rocka huku akiwa anacheka.

Kwa sasa, imeonekana wawili hao hawana ukaribu kama ilivyokua zamani.

Hivi Ni Bongo Movies au Bongo Lala..!!!?

$
0
0

KATIKA moja ya ngoma zake, mwanamuziki wa Hip Hop Bongo kutoka Kundi la Weusi, John Simon ‘Joh Makini’ aliwahi kudokeza kuwa hivi sinema zetu ni Bongo Movies au Bongo lala? Hapa ndipo hoja yangu ilipo. Nina neno juu ya maandamano ya baadhi ya waigizaji wa sinema za Kibongo jijini Dar kwenye Mitaa ya Kariakoo, katikati ya wiki hii kupinga wizi wa kazi zao na uingizwaji holela wa sinema za nje hasa zile series za Kikorea unaofanywa na maharamia wa kazi za sanaa. Ambazo hutengenezwa kimagumashi na kuuzwa kwa shilingi elfu moja.

Tofauti na sinema zao ambazo huuzwa shilingi elfu nne kwa nakala. Naamini huu ndiyo muda muafaka wa kujadili Bongo Movies maana wameingia wenyewe kwenye kumi na nane. Ieleweke kwamba, sipingi maandamano hayo kwa sababu siku hizi kila anayepinga jambo anaambiwa si mzalendo. Pia sipingi kwamba kuna wizi wa kazi za sanaa. Hapana! Ila nina neno kwao! Inawezekana kabisa wasanii hao wako sahihi lakini haukuwa muda mwafaka au mbinu ya maandamano inaweza isiwe suluhisho sahihi.

Nitaeleza. Mara kadhaa nimekosoa mambo ambayo kama hayatarekebishwa, hata wakiandamana kutoka Dar hadi Kigoma kwa miguu kupinga sinema za kutoka nje ya nchi bado hawatapata suluhu wala Bongo Movies hazitaweza kufunika Prison Break, Empire, Fast And Furious, Into The Badlands, Pirates of Caribbean, Power, The Blacklist, Crisis, 24, 3 Days, Revolution, Arrow, Tyrant, Scandal, Revenge na nyingine nyingi kutoka nje ya nchi. Wakati mwingine tuseme ukweli tu, huwezi kulinganisha sinema au series hizi na Bongo Movies.

Ukifanya hivyo, dunia itakushangaa kwa sababu Bongo Movies zimeshindwa kukidhi viwango kwani hazijafikia hata nusu au robo ya zile za nje! Tukubaliane kuwa kuna mambo yanayohitaji elimu, umakini (seriousness), teknolojia na mengine. Ifahamike pia kwamba kutokana na ukosefu wa mambo hayo, ni kwenye Bongo Movies pekee ambako
jambazi anavua viatu anapovamia nyumbani kwa mtu na lazima avae koti jeusi, refu na miwani nyeusi. Mtu anapigwa risasi mguuni anatoka damu mdomoni. Mtu anatoka kulala huku amepaka make ups. Mlinzi wa geti lazima awe amepoteza f’lani (hamnazo).

Pia ni kwenye Bongo Movies pekee ambako inachukua dakika 20 kwa mtu kuwasha gari na kuondoka nyumbani. Mtu anashuka kwenye gari amevaa shati la njano akifika ndani utamuona ana shati la drafti. Mhusika (mfano Ray) anakumbuka maisha yake ya miaka kumi iliyopita halafu anaonekana mweupe na ameweka nywele waves. Pia mtu anapigwa risasi kwenye part one halafu anakufa part two! Katika hali kama hii, maandamano hayawezi kuleta tija badala yake kuna mambo ya kufanywa kwa umakini ambayo mengi ni ya kitaalam. Ni wakati mwafaka kwa madairekta kuzingatia uhalisia wa mambo na mazingira.

Mazingira katika sinema au series ni ishu kubwa mno kama kweli tunataka kupanua soko letu lifikie duniani kote. Tanzania ni tajiri wa mali asili, lakini mazingira yetu ya asili hayaonekani kwenye sinema zetu. Waigizaji ‘uchwara’ wameng’ang’ania kuonekana mabosi kwenye majumba ya kifahari. Wamesahau kabisa kwamba tuna vijiji, mapori na mbuga zenye mvuto wa aina yake ambazo lazima zitamvutia mtazamaji wa sinema husika.

Basi, hata kama tuking’ang’ania mijini basi vitu kama magari yaonekane ni matoleo ya kisasa na siyo yale ya miaka ya 2,000. Tunajipa aibu isiyokuwa ya lazima. Hivi waigizaji wetu wanajua mtu mweusi ana asili ya mavazi yake hata kama hatuna vazi la taifa? Sasa utofauti uko wapi kati ya sinema ya nje ambayo mhusika anapiga suti na Bongo Movies nako anapiga suti au mwanamke mzuri anavaa kimini hadi inakuwa aibu kutazama sinema na watu wa rika tofauti? Narudia tena, Bongo Movies mmejileta wenyewe kwenye kumi na nane hivyo vumilieni kuchomwa sindano. Kuna tatizo kubwa kwenye eneo la uhalisia wa kiugizaji.

Hapa unakuta msanii anaigiza hadi anaigiza anachoigiza! Ni kama mtu kukimbia spidi hadi unapitiliza nyumbani kwenu au kwako. Tukiacha mambo ya kitaalam ndani ya sinema na hasa matumizi ya vifaa vya kisasa (HD-High Definition), pia kuna maisha binafsi ya baadhi ya wasanii wetu nje ya uigizaji. Huko ndiko kuna balaa kwa sababu msanii anataka kufanya mambo ambayo ni nje ya kamera yaonekane kama ni ndani ya kamera. Wanashindwa kutofautisha. Wanaigiza hadi maisha halisi ya kila siku.

Huko kwenye mitandao ya kijamii ndiyo balaa kubwa kwani hakuna wanachokifanya cha kuwajenga kwenye tasnia hii zaidi ya maonesho ya picha za utupu na mambo ya aibu yasiyo na tija. Mwisho kwa leo, maana nitaendelea kukosoa, wasanii wetu ni lazima wajue, tupo kwenye dunia ya kidijitali. Ukiandamana kupinga sinema za nje kuuzwa kiholela Kariakoo, ujue watu watazifuata kwenye mitandao. Huko ni kuwa na bando lako tu, unajiachia utakavyo. Ubora utakaotokana na mambo niliyoyaeleza, unatosha kulikamata soko la Tanzania, Afrika na dunia bila maandamano au kokoro na mtu. Swali la kutafakari; Je, ni kwa nini enzi za uhai wa Steven Kanumba, Bongo Movies ilikuwa juu? Kwani hakukuwa na sinema na series za nje? Tafakari chukua hatua!

Wanaume Mliohamishiwa Dodoma Mmetuachia Wake zenu Makazini Wanatusumbua Sana

$
0
0

Ni wamama wawili sasa nimeona wamebadilika sana hapa kazini. Kila mtu kwa nafasi yake analalamika kuwa sasa ana hard time mahitaji ya kimwili hapati na mumewe yupo dodoma.

Ushawishi wao ni mkubwa. Huyu mmoja amefikia hatua kabisa ananambia " leo am so h.orny yaani ukinigusa tu wazungu haoo" akija ofisini kwangu ananitega sana kila wakati anataka tuzungumzie mambo ya mapenzi penzi tu

Na jimama lingine nalo linanambia linekuwa likiniangalia sana na kuona nipo serious so linapenda sana tupeane kampani hasa kipind hiki ni mpweke mumewe kaenda dodoma.
Ananambia anajua nimeoa name ndo maana anataka atulie nami tukapime tuwe tunakamuana tu kishkaji ye hataki hata shilingi yangu moja.

Nashauri waume mliohamia dodoma chukueni wake zenu, Wanatusumbua sana huku makazini na mitaani. Na wao wanaamini nanyi dodoma mnafanya hivyo hivyo.

By Gudume

KIGWANGALLA Amjibu Haya Mange Kimambi ..Baada ya Mange Kupost Hali Mbaya za Hospitali Nchini..!!!

$
0
0

Hamis kigwangalla leo ameamua kufunguka kwa mwanaharakati Mange Kimambi huko Instagram baada ya mwanadada huyo kupost picha na maombi kibao kutoka kwa wananchi wakimwomba awasaidie kufikisha vilio vyao serikalini.

Majibu hayo yamekuja siku chache baada ya mwanadada Mange kufululiza kupost picha na post mbali mbali zikionyesha hali mbaya ya huduma za afya kwenye baadhi ya hospitali zetu.

Nyingi ya post zinaonyesha jinsi wanawake kwenye baadhi ya hospitali kubwa ( including MUHIMBILI ) wakiwa wamelala chini sakafuni na watoto wao baada ya kutoka kujifungua, na baadhi ya post nyingine ni message anazotumiwa na watu mbalimbali wakilalamika jinsi wanavyopata tabu kupata huduma za afya mahospitalini .


FAHAMU Mita za LUKU Zinazofungwa Majumbani..!!!

$
0
0

Wateja wetu wengi wamekuwa wakijiuliza iwapo wamefungiwa mita sahihi kutokana na matumizi yao ya umeme? Ama mita ambazo wamefungiwa ni za Viwandani na kulalamika wanatumia umeme mwingi zaidi tofauti na matumizi wanayotumia

Mita za LUKU zinazofungwa majumbani ni sahihi kwa matumizi ya nyumbani, ufungaji wa mita za majumbani hutegemea sana upimwaji wa matumizi /mahitaji ya umeme katika nyumba husika.

Mteja anafanyiwa tadhimini kabla ya kuunganishiwa umeme, wakati wa uunganishaji wa umeme inaangaliwa maombi kama Mteja ameomba kufungiwa njia moja (single phase) ama njia tatu (three phase) na haiwezekani Mteja aombe njia moja ya umeme afungiwe njia tatu.

Iwapo matumizi ya umeme ya Mteja yakiongezeka kufika unit 7500 hapo atalazimika kutumia mita za njia tatu (three phase) zenye uwezo wa Volts 400 kutoka mita ya njia moja yenye Volts 220 -250. 

Wateja wengi hawafahamu hasa anapo tumia umeme ukafikia units 300 anadhani TANESCO ilikosea kumfungia umeme/mita. Sio kweli, kinachotakiwa ni Mteja kuwa na matumizi mazuri ya umeme ili kupunguza gharama.

Aidha, mita za LUKU za njia tatu kwa baadhi ya Wateja wenye mahitaji makubwa ya umeme wamefungiwa majumbani mwao hasa ambao tangu tathmini inafanyika ilionekana mahitaji ya umeme yatafika units 7500 maeneo mengine ni ya Kibiashara na ambako matumizi ya umeme wa njia moja hautofaa huwa wanafungiwa huo wa njia tatu. 

Kwa wastani wa units 10 usiku na 6 mchana maana yake Mteja ana zaidi ya units 300 kwa mwezi yaani 16x30 utapata units mia nne (400) hayo si matumizi madogo, pia yapo mambo mengi ya kuyaangalia linapokuja suala la matumizi ya umeme, cha kwanza hiyo mita iko sahihi? TANESCO huwa inapima mita kulingana na maombi ya Mteja, ikiwa itagundulika kuwa mita ni mbovu Mita hiyo huondolewa eneo la Mteja, na Mteja atasahihishiwa account zake kulingana na kile kipindi mita haikusoma ipasavyo,

Jambo la pili ni Mteja anatakiwa kukagua mfumo wa umeme wa nyumba yake na kuhakikisha hakuna hitilafu (leakage) yoyote inayo pelekea umeme kuvuja na kumuongezea matumizi Mteja (Wiring system) na pia Mteja kuhakikisha earth load iwe shaba halisi.

Tatu ni vifaa anavyo tumia Mteja vina uwezo gani wa kutumia umeme? Nirahisi ku hesabu umeme tunaotumia na kutoa malalamiko kwa TANESCO, na Shirika litafanya ukaguzi ili kubaini matumizi hayo pengine ni sahihi, kila kifaa kina kiasi cha umeme kinachotumia kwa dakika ama masaa kadhaa. Inashauriwa Mteja kutumia vifaa vinavyotumia umeme mdogo (Energy Server), pia inashauriwa kuepuka vifaa vya mitumba sababu vingi vinatumia umeme mwingi.
Viewing all 104756 articles
Browse latest View live




Latest Images