Quantcast
Channel: UDAKU SPECIAL
Viewing all 104789 articles
Browse latest View live

POLISI Wapiga ‘Stop’ Kikao cha Mbunge CUF na Maalim Seif Shariff..!!

$
0
0

JESHI la Polisi Dar es Salaam limezuia kikao cha Mbunge wa Temeke (CUF) Abdallah Mtolea, ambao ulipangwa kufanyika leo kutokana na sababu zisizofahamika.

Jana Mtolea alithibitisha kufanyika kwa kikao hicho ambapo mkutano huo ulitarajiwa kuhudhuliwa na Katibu Mkuu CUF Maalim Seif Sharif Hamad.

Juzi Aprili 22 mwaka huu, watu wanaodaiwa kuwa wafuasi wa Mwenyekiti wa Chama cha Wananchi (CUF), Prof. Ibrahimu Lipumba, walivamia mkutano wa wafuasi wa Katibu Mkuu, Maalim Seif Sharif Hamad na kuwapiga na kuwajeruhi wenzao pamoja na waandishi wa habari.

Lengo la Mkutano huo ni kufanya harambee za kuchangisha fedha kwa ajili ujenzi miundombinu ya ebneo la kilakala hasa wakati wa mvua.

Taarifa alizozipata kutoka polisi zilidai kuwa Mtulia alipanga kuwakusanya wafuasi wa lipumba na kuwashawishi kuhamia kwa maalimu kitu ambachom si cha kweli.

NAPE Amtesa Mwakyembe Katika Sakata la Uvamizi wa Clouds..Habari Vichwa vya Magazeti ya Leo 24/4/2017..!!!

PATA Tiba Asili Kutoka Kwa Shekh Sharifu Rashid

$
0
0

MIUJIZA YA SHEKH SHARIFU RASHID KUTOKA BAGAMOYO PWANI. (RUDISHA MAHUSIANO YAKO NDANI YA MASAA 72 TU) ASANTE KWA KUENDELEA KUMPIGIA SIMU SHEKH SHARIFU RASHID KWA WALE WENYE MATATIZO NA WALE WANAOTOA SHUKRANI: 

SHEKH SHARIFU RASHID ni mtaalamu wa tiba mbalimbali za asili, anatumia kitabu cha quran dawa za asili dawa za kiarabu, na njiwa, Anakuvutia mpenzi alie kuacha au alie mbali, anazo dawa za mapenzi, nguvu za kiume, chango kwa kina mama, ngiri maji na n.k, anakuvutia mali zilizo potea au kudhulumiwa, pia anatoa Pete za bahati zilizoambatanishwa na jini mali, Wenye matatizo ya uzazi, jini mahaba, mapepo ya kichawi, vifungo vya kimaisha, ndoto mbaya za usiku, uelewa mdogo wa ufahamu shuleni kwa watoto wote, pia anauwezo mkubwa wa kumaliza kazi zilizoachwa na wataalamu wengine ndani ya masaa 48 tu, Pia anatibu kwa njia ya simu popote ulipo. WASILIANA NAE KWA WhatsApp na SIMU NO: +255 718-668347 na +255 767-204308 +255 685-224047 Email shekhsharifurashidi@gmail.com.

USHAURI: ni vyema kupiga simu kuliko kutuma sms ili upate huduma kwa haraka.

Gwajima Ajipanga Kununua Treni ya umeme

$
0
0
 Mchungaji wa Kanisa la Ufufuo na Uzima, Josephat Gwajima amesema amedhamiria kununu treni ya umeme  baada ya Rais John Magufuli kuonyesha dhamira ya kujenga reli  ya kisasa(standard gauge).

Gwajima ameyasema hayo leo katika ibada ya Jumapili  huku akimsifu Rais Magufuli kwa kuchukua hatua hiyo.

Alisema licha yeye ni mchungaji wa Taifa na anaamini ipo siku Dar es Salaam yote itakwenda kanisani kwake kusali.


Sababu Tano za Kufa Kwa Bongo Movie

$
0
0
1. MAPENZI NA NGONO:
Ngono ni moja kati ya sababu kubwa za mtu hasa wanawake kuingia kwenye industry.Kama mdada ana makalio makubwa, nyonyo za kueleweka na factors nyingine zenye kuamsha tamaa za mwili basi huyo amefuzu kuwa actress hata kama hana kipaji chochote.Unapotumia ngono kama chujio kwenye interview, unakusanya makapi na wenye vipaji wanachujwa kisa sababu ya mionekano yao.

2. TAMAA NA UBINAFSI:
Unakuta movie moja ambayo mtu mmoja ndiye: Star, director, editor, producer, script writer and so forth. Yaani akili ya mtu mmoja inaongoza positions zaidi ya tano.Siku ikitokea huyo mtu amepatwa na tatizo, karibu kampuni yote inatikisika.Kwanini wasitafute watu tofauti tofauti kwenye positions mbalimbali ili kuingiza akili nyingi na mawazo ya watu wengi kwenye production?

3. UWEZO MDOGO WA KIAKILI:
Kubali au kataa lakini asilimia kubwa ya waigizaji wa bongo movie ni wale wenye uwezo mdogo kiakili, ambao walijishawishi kuwa hawakupewa akili za darasani ila vipaji vya sanaa, wasijue akili ndio mzizi wa kila kitu.Matokeo yake ni kukosa fertile imaginations, creativity, and other mental fore steps zinazotumika kwenye sanaa.Mbadala wake wameishia kukopiana kazi zao, ku-reflect matukio ya kwenye jamii kama vile mauaji ya maalbino na vikongwe, ndoa na uasaliti na mapenzi kwa ujumla.Vitu ambavyo havimsisimui hadhira maana alishavizoea.

4. MADAWA YA KULEVYA:
Madawa ya kulevya ni sababu na ni matokeo ya kufa kwa bongo movie.Ni sababu kwa maana wakishatumia madawa uwezo wa kazi unapungua.Wanakuwa wamesizi kwa muda mrefu zaidi ambao walitakiwa wafanye kazi, pia wanatumia pesa nyingi kununulia unga.Ni matokeo kwa maana wakishafulia kwenye uigizaji wanabakiwa na jina bila pesa.Ili kuendelea ku-keep reputation yao wanakubali kuwa punda wa kubebea unga ili wapate namna ya kuishi mjini.

5. KUTUMIKA KISIASA:
Kama nilivyosema, hawa watu uwezo wao kiakili ni mdogo.Wanajiingiza kwenye chama cha siasa kama industry yote bila kujali hadhira wao ni vyama tofauti tofauti na wengine hawana vyama.Hawajui kwamba kama tasnia kujiingiza kwenye chama wanaonekana kama vile ni kitengo cha chama fulani.Ikiwa hadhira ana chuki na chama mlichojiunga nacho, basi ile chuki inasambaa hadi kwenu na mwishowe hakutakuwepo na wa kununua kazi zenu.Baada ya kutapeliwa kwenye kampeni za 2015 na kutengwa na wananchi walio wengi, leo hii hakuna anayewataka, si hadhira wala chama na serikali yake. Wamekufa kibudu kama TBC na sasa wanatumia mabavu kulazimisha watu wanunue kazi zao.

Harmonize Anawekwa Mjini na Demu wa Kizungu, Yadaiwa Ameachana na Jackline Wolper

$
0
0
Kwa story za kunyapia nyapia zinadai kuwa harmonize na wolper gambe washabwagana na kila mtu kachukua 50 zake na kwa ubuyu unaosambaa mjini unadai kuwa Dogo kapata mtt mkaliii wa kitaliano anajulikana kwa jina la sarah na tyari yupo mimba....so mda cyo mrefu harmonize ataitwa baba......demu nasikia anamkwanja wa kutosha ndo anaempa jeuri harmonize apa mjini ndo maana kila siku anabadili dinga tu mara Prado mara Audi.

Hongera sana mmakonde kama izo story ni za kweli.....endelea kuliwakilisha taifa kwa huyo muitaliano.

 SIKILIZA HAPA:

BARCELONA Waichapa Madrid El Clasico..!!!

$
0
0

Miamba ya soka ya Hispania klabu ya Barcelona, wameibuka kidedea katika mchezo wa El Clasico, kwa kuichapa Real Madrid kwa mabao 3-2.

Kiungo wa Kibrazil Carlos Henrique Casemiro, alifunga goli la kuongoza la Real Madrid kisha Lionel Messi, akakomboa bao hilo.

Ivan Rakitic akaiongezea Barca, goli la pili katika dakika ya 73 ya mchezo kabla ya mshambuliaji James Rodriguez wa Real Madrid, kuchomoa goli katika dakika ya 86.

Katika dakika ya 90 Lionel Messi, aliifungia timu yake bao la ushindi na hivyo timu yake inarejea kilele mwa ligi wakiwa na alama 75 huku madrid wakiwa katika nafasi ya pili kwa alama 75, 
wakitofautiana idadi ya magoli na Real wakiwa na mchezo mmoja mkononi.

Madrid walicheza pungufu katika mchezo huu baada ya beki wake kisiki Sergio Ramos, kupewa kadi nyekundu.

KABULA Amchana Live Mr. Chuz

$
0
0

MSANII wa kitambo kwenye anga la sinema Bongo, Miriam Jolwa ‘Jini Kabula’ amemchana live mzazi mwenzie ambaye pia ni msanii mwenzake, Jumanne Kihangala ‘Mr. Chuz’ kwa kumtaka aoe, aache kutangatanga.

Kabula alimpa makavu hayo baba mtoto wake huyo baada ya Chuz kumtumia ujumbe wa kuwa amempata mwanamke ambaye anafanana na yeye hivyo atampelekea amuone ili kama anafaa afunge naye ndoa.

“Unajua Chuz mimi nashangaa umri unaenda sana sasa hivi anatakiwa aoe awe na mke maana kuna kipindi kinafi ka mtu unakua na unaacha kila kitu cha dunia nyuma kwanza halafu unaendelea, sasa Chuz sijui kwa nini hataki kubadilika?” alihoji Kabula. Hata hivyo, alipotafutwa Mr. Chuz hakutaka kuzungumzia suala hilo.

IMEFICHUKA..Amri Hii ya Kikwete Iliitia Nchi Hasara ya Mabilioni ya Pesa..Mbunge Afichua A - Z Jinsi Ilivyokuwa..!!!

$
0
0

AGIZO la Rais wa awamu ya nne, Jakaya Kikwete kujengwa maabara kwa kila shule ya sekondari nchini limebainika kutumika kama mwanya wa watendaji wa serikali kufuja fedha za umma.

Aidha, agizo hilo limebainika kukamilisha miradi mingi ya maendeleo iliyokuwa imepangwa kutekelezwa katika bajeti kwa miaka ya fedha 2013/14 na 2014/15.

Novemba 4, 2012, Kikwete, maarufu JK, aliwaagiza wakuu wa mikoa na wilaya nchini, kujenga maabara kwa kila shule ya sekondari katika kipindi cha miaka miwili kuanzia siku hiyo.

JK alitoa agizo hilo alipohutubia wananchi wa Jimbo la Manyoni Magharibi mkoani Singida, waliohudhuria mkutano wa hadhara uliofanyika katika mji mdogo wa Itigi.

Alisema maabara za sayansi ni muhimu katika maendeleo ya wanafunzi kujifunza kwa nadharia na vitendo. JK alisema kutokana na umuhimu huo, kulikuwa kunahitajika ushirikiano kama ule ulioonyeshwa wakati wa ujenzi wa shule za sekondari za kata ulioanza mwaka 2006.

Hata hivyo, Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Hesabu za Serikali za Mitaa (LAAC) imekosoa utaratibu huo na kufichua ufujaji wa mabilioni ya shilingi uliofanywa na watendaji wa halmashauri na kukwamisha utekelezaji wa miradi mingi ya maendeleo, wakidai pesa zimeelelekezwa kwenye ujenzi wa maabara.

Mwenyekiti wa kamati hiyo, Vedasto Ngombale, ndiye aliyefichua kadhia hiyo katika mahojiano na Nipashe kwenye viwanja vya Bunge mjini hapa.

Alisema kuwa kutokana na tamko hilo la JK, watendaji wa halmashauri walilazimika kuelekeza kwenye ujenzi wa maabara fedha zilizokuwa zimetengwa kwa ajili ya miradi mingine ya maendeleo, huku baadhi yao wakipata mwanya wa kufuja fedha za umma kwa kisingizio kwamba wamezielekeza kwenye utekelezaji wa agizo la Rais.

"Kilichotokea lile lilikuwa tamko, lakini katika maeneo mengi hapakuwa na bajeti kwa ajili ya utekelezaji wa jambo hilo," Ngombale alisema.

"Kama unavyofahamu, ili kutekeleza mradi wowote katika serikali, sharti kwamba mradi huo utajwe kwenye bajeti, lakini Mheshimiwa Kikwete, kwa mamlaka aliyokuwa nayo, akatoa tamko la utekelezaji wa jambo hilo.

"Sasa kilichotokea ni kwamba baada ya tamko lile, watendaji wa halmashauri kwa maana ya wakurugenzi watendaji, walichokifanya ni kuchukua pesa kutoka katika kasma mbalimbali kuhakikisha kwamba wanatengeneza maabara.

"Na matokeo yake, tulipokuja kupitia yale mahesabu baada ya utekelezaji, kukawa kumebainika kuna ufujaji mkubwa wa pesa katika halmashauri nyingi."

Ngombale ambaye pia ni Mbunge wa Kilwa Kaskazini (CUF), alisema licha ya tamko hilo kusababisha kutumika kwa mabilioni ya shilingi yaliyokuwa yametengwa kwa ajili ya miradi ya maendeleo ikiwamo ya maji, mpaka sasa bado kuna halmashauri nyingi hazijakamilisha ujenzi wa maabara, akiitolea mfano halmashauri ya Kilwa anayotoka.

Zipo halmashauri nyingi ambazo bado hazijakamilisha ujenzi wa maabara hali ya kwamba tamko hilo lilitolewa na utekelezaji ulifanyika kwa kuchukua pesa kutoka katika mafungu tofauti tofauti," alisema Ngombale.

Mtoto huyo wa kaka mdogo wa mwanasiasa mkongwe, Kigunge Ngombale Mwiru, alisema agizo hilo la JK lilitolewa bila kuwa na bajeti, hivyo fedha za miradi mingine zilikuwa zinachukuliwa na kuingizwa kwenye ujenzi wa maabara, kinyume cha sheria ya bajeti ya mwaka husika.

"Lakini, katika utekelezaji huo, ndiyo mwanya wa matumizi mabaya ya pesa ulipatikana na sisi tulivyokagua, tumeona ni kiasi gani. Kuna ufisadi mkubwa," alisema.

Credit - Nipashe

KAMBI ya Upinzania Bungeni Yamlima Barua IGP Mangu..Ni Kuhusu Vurugu za Lipumba Cuf..!!!

$
0
0

KAMBI ya Upinzani bungeni imemwandikia barua Mkuu wa Jeshi la Polisi, IGP Ernest Mangu na taasisi za Serikali kuhoji tukio la mkutano wa ndani wa Chama cha Wananchi (CUF) mkoa wa Dar es Salaam kuvamiwa na watu wenye silaha juzi.

Watu wanaodhaniwa kuwa wafuasi wa mwenyekiti wa CUF anayetambuliwa na Msajili wa Vyama vya Siasa, Profesa Ibrahim Lipumba walivamia mkutano wa mwenyekiti wa mkoa na wanahabari wakiwa na bastola, fimbo na mikanda na kutishia maisha, kupiga watu waliokuwa kwenye ukumbi wa hoteli moja jijini na kufanya virugu.

Aidha, upinzani umemtupia lawana Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Mwigulu Nchemba na Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo, Dk. Harrison Mwakyembe kuhusu uvamizi huo kwa kuwa hawakutekeleza majukumu yao.

Kadhalika, umelaani kitendo hicho cha uvamizi wa mkutano pamoja na waandishi wa habari kupigwa kwa kuitaka Serikali kutoa tamko na kuchukua hatua kali dhidi ya waliohusika.

Mnadhimu wa Kambi rasmi ya Upinzani bungeni wa CUF, Ally Saleh akizungumza kwa niaba ya wenzake alisema makundi ya uvamizi yamekuwa tishio katika jamii.

“CUF kimeshamwandikia barua IGP na taasisi zinginezo za Serikali kuonyesha matatizo yaliyotokea jana (juzi) na chanzo cha matatizo hayo," alisema Saleh. "Tunangojea Serikali itasema nini juu ya tukio lile.”

Saleh ambaye pia ni Naibu mnadhimu wa Umoja wa Katiba ya Wananchi (Ukawa) bungeni, alisema kitendo kilichotokea katika mkutano wa CUF cha watu kuvamia na kutoa bastola hadharani hakina utofauti na tukio alilofanyiwa aliyekuwa Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo, Nape Nnauye.

Alisema ukimya wa Waziri Mwigulu na Dk. Mwakyembe juu ya tukio hilo umeonyesha hawajatimiza majukumu yao; hususani Waziri Mwakyembe ambaye alipaswa kuhakikisha waandishi wa habari wanakuwa salama.

“Mambo haya yanavyotokea mawaziri wawili tunataka kuwavisha mnyororo Waziri Mwigulu Nchemba na Mwakyembe," alisema.

"Mwakyembe alipaswa kujitokeza kwa haraka na kutoa tamko dhidi ya kitendo walichofanyiwa waandishi, tunahisi kwamba jukumu a Serikali halijatekelezwa, Mwakyembe anapaswa kuhakikisha usalama wa waandishi unakuwapo. Hivyo Mawaziri hawa wawili wanapaswa kutoa tamko."

Alisema kikundi cha Mungiki siyo kigeni hapa nchini na Serikali inakifahamu lakini hakuna hatua zozote ambazo zimeshachukuliwa hadi sasa.

Kadhalika, alisema Kutokana na tukio lililotokea juzi, mkutano wa ndani wa kikatiba uliotakiwa kufanywa na Katibu Mkuu wa CUF, Maalim Seif Shariff Hamad leo Serikali wameufuta kitendo ambacho siyo sahihi.

Alisema kitendo cha Serikali kuufuta mkutano huo siyo sawa kwa sababu Profesa Lipumba anabebwa na mbereko ya Serikali kwa kufanya mikutano ya ndani kila wakati.

Alisema Serikali inalea Jamhuri ndogo ndani ya Jamhuri, vile vile Serikali imekuwa inalea kambi ndogo ndani ya Buguruni na kwamba wanufaika zaidi wa mgogoro unaoendelea ndani ya CUF ni Chama Cha Mapinduzi (CCM) ambao dhumuni lao ni kuchukua majimbo yanayoongozwa na CUF katika uchaguzi mkuu ujao.

MFANYABIASHARA Achomwa Visu 14 na Kaka’ke..!!!

$
0
0

 Mfanyabiashara wa samaki, Warioba Mtatiro, mkazi wa Kijiji cha Etalo, Musoma Vijijini,
amedaiwa kujeruhiwa vibaya kwa kisu na kaka yake (jina tunalihifadhi).

Tukio hilo la kusikitisha limetokea hivi karibuni katika Mtaa wa Nyamulinda, Kijiji cha Etalo, Musoma Vijijini. Kwa mujibu wa chanzo kilichoshuhudia mtiti huo, Mtatiro alikuwa akicheza kamari maarufu mkoani Mara kwa jina la Magaramka na kaka yake ndiye aliyekuwa akichezesha.

Alisema baada ya ‘kupunwa’, Mtatiro hakuwa na kiasi hicho cha fedha kilichohitajika katika mchezo huo ndipo ugomvi ukaibuka hadi kufikia hatua ya kaka kumchoma visu mdogo wake. “Mtatiro alipunwa shilingi mia tano. Sasa kaka yake akawa anamdai na yeye akawa hana ndipo alipoamua kuchukua kisu na kuanza kumchoma.

“Alimchoma sehemu mbalimbali mwilini, kichwani na mgongoni na kumsababishia majeraha makubwa. Kwani alikuwa anachoma kisha anachomoa na kuchoma sehemu nyingine kama mara 14,” kilisema chanzo hicho.

Chanzo hicho kilieleza kuwa, baada ya watu kuamulia, kaka mtu alikamatwa na kupelekwa Kituo cha Polisi Musoma kwa ajili ya hatua za kisheria huku majeruhi akikimbizwa katika Hospitali ya Mkoa wa Mara.

Majeruhi huyo anafanya biashara ya kuuza samaki katika kontena la samaki lililopo Mtaa wa Nyamulinda, jirani na eneo walilokuwa wakicheza kamari hiyo.

Akizungumza na Risasi Jumamosi kwa shidashida mara baada ya kutokea kwa tukio hilo, Mtatiro alisema kaka yake huyo alimchoma visu hivyo baada ya kushindwa kumlipa shilingi 500 aliyomshinda kwenye kamari.

“Baada ya kunipuna nilimwambia sina lakini yeye hakutaka kunielewa, akaanza kunishambulia kwa visu.

Kanichoma sana visu mgongoni, nashukuru Mungu kama si watu kuniamulia, angeniua
yule,” alisema Mtatiro. Risasi Jumamosi lilimtafuta Kamanda wa Polisi Mkoa wa Mara, ACP Jafari Mohamed kuhusiana na tukio hilo ambapo alipopatikana alisema bado halijamfikia.

“Nashukuru kwa kunipa hizo taarifa, nitazifanyia kazi maana bado hazijafika mezani wangu hivyo nitafuatilia,” alisema Kamanda Mohamed.

Nay Wa Mitego Asalimu Amri Aomba Msamaha

$
0
0

Baada ya kuporomoshewa maneno ya kashfa kwenye mitandao na mzazi mwenzake kwa kushindwa kumtunza mtoto zaidi ya kumuweka tuu kwenye mitandao ya kijamii na kujisifu, Nay wa mitego amekiri kubadilika na kuanza kumuhudumia binti yake.


Nay wa Miteho leo Rapa kupitia ukurasa wake wa Instagram ameamua kuudhihirishia umma kuwa kuanzia sasa atakuwa baba mwema na ataanza kuwahudumia watoto wote kwani yeye ni kama kioo hivyo hana budi kutekeleza hayo.


Nay wa Mitego wiki iliyopita aliandamwa na matusi huku akitolewa maneno ya kashfa na mzazi mwenzake  ambaye ni muigizaji wa filamu bongo, Skyner Ally akimtaka kuwa asishoboke kum-'post' mtoto wao aitwae Munnie kwani yeye hana mchango wowote ule kwa mtoto huyo tena alienda mbali zaidi kwa kusema hajui  hata gharama za nguo za ndani za mtoto huyo.


“Si kwa kichambo kile jamaniiiiii huu...Jamani inatosha basi povu. Nitapeleka matumizi. Nawapenda sana awa watoto wanguu. Wasiopeleka matumizi ya watoto wapo “-ameandika rapa Nay wa Mitego.

HATUA za Kuapproach Wanawake Katika Kikundi..!!

$
0
0

Kuapproach wanawake wakiwa katika kikundi ni jambo gumu sana kwa mtu yeyote kutimiza. Hata kwa wale ambao wanajiamini mbele ya wanawake inafikia wakati flani wanapatwa na changamoto moja au nyingine. Lakini kama kawaida mambo kama haya yanaeleweka kwa kuwa unaaproach wanawake wengi wakati mmoja na pia kunaweza kutokea maswala mengine ambayo yanaweza kujeuka changamoto kwako.

Kuapproach wanawake wakiwa kwa kikundi si sawa na kubadilisha gemu ya kutongoza mwanamke mmoja bali ni mbinu tofauti kabisa ambayo inahitajika kutumika. Mbinu ambayo lazima uijue na kuielewa.

Kwa nini unahitajika kujua kutongoza wanawake katika kikundi

Jambo muhimu ambalo unapaswa kujua wakati unapoapproach wanawake kwa kikundi ni kuwa unaaproach kundi zima, na wala si mwanamke mmoja ambaye unataka kuongea naye. Kama unaaproach kwa kikundi, ni vyema uende pekeako. Mkiapproach kama kikundi mnaweza kuonekana kuogopesha na wanyemelevu, hivyo ni vizuri zaidi kama marafiki zako watangojea kwa dakika, ili uweze kuwatambulisha vyema kwa kikundi hicho cha wanawake.

Wasalimie wanawake wote wakati mmoja

Ikija na swala la kusalimia wanawake katika kikundi, ni vizuri kuwasalimia wote wakati mmoja. Vile ambayo utawasalimia wanawake katika kikundi ni kama vile utakavyomsalimia mwanamke mmoja; unatoa matamshi ya mizaha na ucheshi, halafu inafuatiliwa na tabasabu halafu sasa unaanza kufunguka zaidi kwa kuongea zaidi na wale wana kikundi ambao wanapenda kuongea. Ni bora kuwasalimia wanawake wote kwa wakati  mmoja hata kama kuna mwanamke kikundini ambaye ulitaka kumvizia ama kuongea naye. Hii haitaonyesha ya kuwa unakimbilia kukutana na mwanamke mrembo pekee, bali unajionyesha ya kuwa umekuja hapo kujumuika na watu na kuinjoy muda wako ipasavyo.

Ipunguze makini yako

Pindi unapoendelea kuongea na wanawake wote, halafu rafiki au marafiki zako wakatokezea, inakubalika kupunguza umakini wako hadi kwa mwanamke mmoja au wawili. Labda bado unataka kuongea na mwanamke ambaye ulimpangia kuongea naye, ama umepata mwanamke mpya kutoka kwa kikundi hicho, unaweza kuyapendua maongezi yako zaidi. Unaweza kuanza na maneno rahisi kama "nimependezwa nawe" ama "unaonekana uko sawa." Hapa unapaswa kumsifu mwanamke kando na umbo lake, halafu baadaye uanzishe gumzo la "nataka kukujua zaidi"

Jaribu kuwa na kisaidizi

Kuwa na kisaidizi wakati unaaproach wanawake katika kundi kubwa inakuwa rahisi sana. Kwa mara, wanaweza kuchat na wanawake wale wengine huku wewe ukimakinika na mwanamke mmoja ambaye ulikuwa umeazimia kukutana naye. Zaidi ni kuwa wanaweza kutoa presha ambayo inakuja wakati unapotaka kuapproach, hii inasaidia kwa kuwa inakupa ujiaminifu kama mwanaume wakati unapoapproach wanawake katika kikundi.  Sababu ni kuwa unajua kuwa usaidizi hauko mbali na wewe na muda wowote wanaweza kutokezea ili kuondoa presha zozote ambazo zinaweza kujijenga.

Mtenge mmoja kutoka kwa kikundi

Kama kuna mwanamke ambaye umeonyesha interest kwake, jaribu kutafuta wakati muwe pekeenu. Hii haimaanishi ya kuwa ni lazima mujitenge katika sehemu moja ya hio klabu ama baa bali pia inaweza kumaanisha ya kuwa unaweza kuamua kutoka ziara hadi katika mkahaha ama sehemu nyingine ya kuvutia ambayo itawaruhusu nyinyi wawili kupata nafasi ya kuongea moja kwa moja ili mjuane vyema zaidi

Ujumbe Huu wa Shilole ni Pigo Kwa Wanaume Wanaopendwa Kulelewa

$
0
0

From @shilolekiuno_badgirlshishi
Yan nilipe hotel mimi
Ninunue chakula na nguo mimi
Bado nikupe na pesa mimi
Hivi mpk hapo nani mwanaume kati yangu na wewe?

Kwanini ukileta ujinga usile tu vibao yani.
Mwanaume majukumu ukiona yamekushinda kubali tu yote...kupigwa, watu kukusaidia kazi na vinginevyo.

Hii Imejipost jamani #hatutoikiki
.
UONGO AU KWELI????

JINSI Ya Kuwa 'Classy Man' Utongoze Wanawake

$
0
0

Kwa muda nimekuwa nikiushabikia huu wimbo wa Jidenna wa 'Classic Man' kwa kuwa unavutia kwa sauti na maneno ambayo yanatamkwa katika nyimbo hio. Cha kushangaza ni kuwa wimbo huu umependwa sana na wanaume kuliko wanawake. Ok, kwa kuupitia wimbo hii kijuu juu ni kuwa Jidenna anajaribu kujieleza ya kuwa yeye ni mwanaume 'classy', yani mwanaume ambaye ana taasubi za watu wa zamani kimaisha, wanaume wale ambao waliyatambua na kuyaenzi maisha yao kiusafi, kifasheni, kuwa na taasubi za kiume nk.

So kwa kutumia kigezo cha kuwa 'classy', hapa Nesi Mapenzi tumeamua kuandika chapisho spesheli kuhusiana na kigezo cha mwanaume 'classy' kwa kuwa imeonekana kuwa tabia ya mwanaume aina hii inaenziwa mpaka karne ya sasa.

So unataka kuwavutia wanawake?

Kuna wanaume wengine mpaka sasa hawajasahau wala kutupa tabia hii ya kuwa 'classy'. Mwanzo wanawake huvutiwa automatic na wanaume ambao wana tabia aina hii katika maisha yao. Lakini pia kuwa 'classy' pekee hakutakusaidia kuweza kuvuta na kunasa mwanamke yeyote, lazima uwe na ujiaminifu wa kiwango cha juu. (Machapisho yetu ya awali yanafafanua zaidi).

Hizi hapa ni hatua ambazo zitakusaidia kuwa na tabia za uclassy.

1. Usingojee uthibitisho kutoka kwa wengine

James Bond ni mfano mzuri tunaoweza kuufikiria wa mwanaume ambaye ni classy. Ni jambo gani linalomfanya kuwa hivyo? Hangojei wala kutaka uthibitisho kutoka kwa wengine. Mvuto-ushawishi wake si kuwa anavalia tuxedo za kuzuzua, bali ni kwa sababu ni mwanaume ambaye hahitaji kuambiwa na yeyote yule kuwa yuko SAWA - tayari anajua. Kama kuna watu ambao watakubali na kujiunga naye, ni vizuri. Kama hawataki, hakuna tatizo pia

2. Valia ipasavyo

Kuna watu wanajidanganya ya kwamba kuwa mwanaume classy lazima uwe umevalia suti ya three piece kila mahali ambapo utaenda. Ok ukweli ni huu...kuwa classy kunaangaliwa zaidi na vile unavalia nguo zinazokufaa zaidi kuliko kuvalia nguo ambazo zitakuanika kama mwana fasheni. Classy ni kuvalia nguo ambazo zina hadhi ya juu kuwaliko wengine lakini pia unavalia kulingana na hulka yako.

Mwisho wa siku ni kuwa wewe mwenyewe ndio utajifahamu iwapo ni wewe halisia ama ni mwigo. Kama unashindwa na kutafuta nguo ambazo zitakuweka classy unaweza kuenda katika duka la nguo karibu na wewe ukajigeze

3. Gonga ndipo

Kwa blog tumekuwa tukiligusia hili swala kwa kina na mfano mzuri tukauweka kwa Leonardo Di Caprio. Jambo ambalo yeye hufanya kwa  kuwasiliana kiujiaminifu na uvuto ni kuwa anaongea moja kwa moja. Hii kwa kawaida ni kuonyesha tabia ya uclassy, kwa sababu unaonyesha uadilifu kwa kitu ambacho unaazimia kutaka ama kufuatilia. Hakuna makosa yeyote kusimama na kumuapproach mwanamke katika klabu ama baa na kumwambia "Nimekuona ukisimama katika ile sehemu na nimetaka kuongea na wewe." Maneno haya najua hayafai kuishia hapa, lakini umemwendea direct na kugonga ndipo kuhusu ajenda yako, jambo ambalo huonekana kuwa classy

4. Chukua namba yake kama mwanaume classy

Jambo ambalo linakuwa changamoto kwa wanaume wengi hadi sasa ni kuona wakitatizika kupata namba kutoka kwa mwanamke. Hapa tumekuandikia mbinu ya kuomba namba kiclassy (tofauti na mbinu tulizozipendekeza awali)

i) Mwombe namba yake wakati ambapo maongezi yenu yamefikia kileleni, si ule wakati ambapo uko karibu kumaliza maongezi.

ii) Usiweke lionekane kama swali. Badala yake, unamwambia kuwa unataka namba yake ili uweze kukutana na kuongea naye wakati mwingine.

iii) Weka simu yako tayari kupokea namba yake ya simu.

iv) Mpatie simu yako kwa kuiweka sehemu yake anayoichukulia binafsi.

v) Wakati anapoandika namba yake kwa simu yako, gusia kuhusu maswala ya deti ukilenga gumzo ambalo mumekuwa mkiongea awali.

vi) Mtumie jumbe papo hapo wakati amekurudishia simu yako ili aweze kupata namba yako. Mtumie jumbe nyepesi na ya ucheshi. Mfano "Ni P.p.T, yule mwanaume mwenye tabasamu la kuua. :-D"

AKIMBIZWA Hospitali Baada ya Kukaa ‘Airport’ Siku 10 Akimsubiri Mpenzi Aliyempata Mtandaoni..!!!

$
0
0

Mwanaume mmoja raia wa Uholanzi amejikuta akilazwa hospitalini baada  ya kukaa katika Uwanja wa Ndege kwa siku 10 nchini China alipoenda kwa lengo la kukutana na mrembo aliyekuwa akiwasiliana naye mtandaoni, ambaye hakutokea.

Mwanaume huyo aliyetajwa kwa jina la Alexander Peter Cirk mwenye umri wa miaka 41, alisafiri kutoka Uholanzi na kutua katika Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Changsha Huanghua kukutana na mrembo aliyemfahamu kwa jina la Zhang.

Hunan TV imeripoti kuwa Cirk alikataa kuondoka katika uwanja huo wa ndege, lakini hali yake ya afya ilizorota kwa kukosa maji ya kutosha na chakula, hivyo maafisa walilazimika kumkimbiza hospitalini.

Baada ya tukio hilo kuripotiwa kwenye vyombo vya habari, mrembo huyo alijitokeza na kufanya mahojiano na Hunan TV wakati mwanaume huyo alikuwa tayari amesharushwa nchini kwao.

Mrembo huyo alieleza kuwa alidhani mwanaume huyo anatania pale alipomwambia anaenda nchini China kwa ajili yake. Aliongeza kuwa wakati wote huo yeye alienda kufanya upasuaji (plastic surgery), hivyo simu yake ilikuwa imezima.

“Siku moja alinitumia picha ya tiketi za ndege ghafla na nilidhani alikuwa anatania. Hakuwahi kuwasiliana na mimi tena baadae,” alisema mrembo huyo.

Hata hivyo, mwanaume huyo alipoulizwa wakati anarudishwa Uholanzi baada ya kutibiwa, alieleza kuwa anaamini atakaporudi nchini kwao wataendelea na uhusiano wao wa mapenzi mtandaoni.

BAADHI ya Haya Yatakufanya Ushinde Usahili..!!!!

$
0
0

Baadhi ya mambo mengi ambayo wadada wakiwa wanaenda kwenye usahili (interviews) wa kazi cha kwanza atazingatia muonekano.

Ndani ya jambo la muonekano ni mengi ambayo unaweza kuwa bado hujayajua kuwa ndio kikwazo cha kufeli katika usahili wako japo ulijibu kwa ufasaha katika maswali uliyo ulizwa.

Wazoefu na Wajuzi mbali mbali ambao wamekwishapitia katika mambo hayo wanatoa ushauri wa kuzingatia pindi unapokuwa umeitwa kwenye usahili. Hapa chini baadhi ya mambo ya kufanya au kuepuka wakati wa usahili. Kumbuka vazi kubwa kabisa ni ujasiri.

1. Wakati ukiwa unazingatia suala la muonekano hakikisha unaepuka mapambo yaliyo pita kiasi (make up) kwenye uso wako iki ni pamoja na urembo uliopitiliza,

2. Chagua mtindo wa kitaaluma na weledi wa nywele zako . Mtindo wa nywele utakusaidi kuwa makini kusikiliza na siyo kuhangaika kuzitengeneza zikae vizuri wakati unajibu maswali.  kama nywele ni fupi ni vizuri ukazichana ili zionekane nadhifu.

3. Tafuta kijifaili kizuri au pochi ajili ya kuweka  vyeti vyako au nyaraka mbali mbali (muhimu) kama zitahitajika wakati huo

4. Tafuta viatu  ambavyo unaweza kutembea navyo vizuri kwa kujiamini wengine hupendelea viatu virefu lakini ni vyema ukava vyenye soli fupi kutokana na mazingira kwa kuwa utakua mgeni katika maeneo hayo huwezi jua miundombinu ilivyo.

5. Epuka nguo fupi sana inayokufanya usikae kwa amani ukabaki tu kuishikilia, Inategemea na aina ya kazi lakini ni vyema uka vaa  nguo ambayo itakuonesha upo nadhifu na siyo tena ikufanye uabike mble za watu.

UNAVYOPASWA Kujibu Unapotakiwa Kuelezea Udhaifu Wako Kwenye Usaili Wa Kazi..!!!

$
0
0

Kwa kawaida watu wengi wanapoenda kwenye usaili wa kazi hufikiria zaidi katika kujitetea kwa uwezo mzuri walionao katika kuifanya kazi iliyotangazwa huku wakisahau kuhusu upande wa pili wa swali hilo.

Kumbuka kuwa muajiri anaamini kuwa wewe ni binadamu wa kawaida na sio ‘robot’. Hivyo, mbali na kufahamu uwezo wako wa kufanya kazi angependa kufahamu upande wa pili wa maisha yako ya kawaida. Kwa kuwa hakufahamu, anaweza kukupa nafasi ya kujielezea mwenyewe mapungufu au udhaifu wako kama binadamu.

Uzoefu unaonesha kuwa karibia asilimia 90 ya waajiri/waasili huuliza swali hili katika usaili wa kazi. Nitakueleza sababu mwishoni mwa makala hii.

Unapaswa kuwa mkweli kiasi, eleza mapungufu hayo katika mtazamo chanya zaidi ili kujiweka katika nafasi nzuri zaidi. Kumbuka, kila unachoongea kwenye usaili lazima kiwe na lengo la kujiuza zaidi kwa mwajiri na sio vinginevyo.

Kwanza kabisa unapaswa kuzingatia aina ya kazi ili majibu yako yawe na mantiki wakati wote.

Kwa mfano, kama unatafuta kazi ya kuwa ‘meneja wa maudhui ya mitandao ya kampuni fulani’ (online content manager), unaweza kuutaja udhaifu wako wa kwanza kuwa ni uteja wa kukaa mtandaoni (online addict). Unaweza kueleza kuwa unafahamu uteja wa aina yoyote hautakiwi kabisa katika kazi hivyo huu ni udhaifu. Lakini uteja huu unaweza kuonekana kama faida kwa muajiri wa/kwa aina fulani.

Lakini, utakuwa umejiondolea sifa zote kama utatumia jibu hilo hilo katika usaili wa kumtafuta mtu anaetakiwa kuwafundisha watoto kuogelea.

Unaweza kufirikia nini kitatokea kama utakuwa unaperuzi mitandao muda wote wakati watoto wanaogelea.

Hata hivyo, yapo baadhi ya majibu ambayo unaweza kuyatoa kwa swali hilo katika usaili wa kazi yoyote. Nitatoa mifano ya majibu ya udhaifu wako katika mtazamo ulio chanya.

Cha muhimu, usijielezee sana wakati unataja udhaifu huu, na usionekane kama unajitetea sana badala ya kujibu ulichoulizwa.

Kwa mfano; siamini kabisa katika kushindwa. Naamini kushindwa ni uzembe na kukata tamaa. Lakini katika uhalisia, binadamu ana kikomo cha utendaji kwa hiyo nina udhaifu wa kushindana na uhalisia huo pale ninapotaka kutekeleza majukumu yangu. Kwa hiyo huwa nafsi yangu inashindana na uhalisia kuwa ‘kuna kushinda na kushindwa’.

Pili, sina Kiasi katika kazi. Kuna wakati nafanya kazi zaidi ya muda unaoshauriwa hata na wataalam wa masuala ya afya.

Tatu, ni msumbufu, huwa nageuka kuwa msumbufu pale ambapo ninapotaka kufahamu kitu fulani ambacho naamini kitanisaidia kukamilisha vizuri majukumu yangu. Ninapofahamu kuwa mtu fulani ndiye anayeweza kuwa msaada wa kunielewesha vizuri, humfuata kadri niwezavyo ili nipate maarifa ya kutosha kutoka kwake. Kwa wengine hii hugeuka kuwa usumbufu kutokana na kuwa na ratiba zao.

Ni mkamilifu kupitiliza, napenda kuona kazi yangu inafanyika kwa ukamilifu uliotukuka, hii hupelekea mara nyingi kutumia muda mwingi sana kuhakikisha nakamilisha jukumu langu kwa ubora uliotukuka. Hii hugeuka kuwa changamoto wakati mwingine kwa kazi ambazo zina ‘deadline’ ya kushitukiza.

Kwa mifano hiyo naamini umeelewa vizuri njia sahihi ya kujibu swali hili ambalo huulizwa mara kwa mara na wasaili. Ingawa wapo wakosoaji wanaodai kuwa hii ni njia mtambuka ya kujibu swali hilo, bado majibu yanabaki kuwa muhimu kwa swali hilo.

Ni muhimu kutoa ufafanuzi wa jinsi gani utajiboresha ili kuweka sawa hicho ulichokitaja kama udhaifu katika kila unachokitaja. Elezea pia jinsi gani umeanza kuyafanyia kazi mapungufu hayo kwa kujifunza kila wakati.

Mambo ya kuzingatia wakati unachagua udhaifu wa kutaja

Usichague udhaifu wa kutaja kwa sababu tu ni mzuri kutamkika na kueleza jinsi utakavyoutatua, inabidi ufikirie zaidi. Usichague udhaifu ambao unaendana na vigezo vilivyowekwa na muajiri (required skills/ desired qualities).

Zingatia sana udhaifu unaoutoa, hakikisha unataja udhaifu ambao ni rahisi kuurekebisha kwa hali ya kawaida.

Kwa mfano, ni vyema ukasema kuwa, “Hujisikia uoga ninapokuwa naongea mbele ya umati mkubwa.” Huo mfano ni bora zaidi ya kusema, “Hujisikia aibu na kupata shida napoongea kwenye kikao.” Na usitaje kabisa udhaifu kama ‘kukosa umakini’.

Ni rahisi kuelezea jinsi ambavyo utauondoa uoga huo kuliko jinsi ambavyo utaiondoa aibu ya kuongea hata kwenye kundi dogo la watu kwenye kikao.

Kama unakumbuka mwanzo wa makala hii nilikuahidi kuwa nitakwambia sababu za kuulizwa swali hili. Unadhani kwa nini waajili au wasaili huendelea kuuliza swali hili wakati wanajua kabisa huenda majibu unayotoa sio ‘ukweli mtupu’?

Ukweli ni kwamba waajiri wataendelea kuuliza swali hili hata kama wanajua hutawaeleza ukweli mtupu kwa kuwa wanafahamu majibu yako yatawaeleza kitu cha ziada kuhusu wewe. Muajiri anaweza kusoma katikati ya mistari ya maelezo yako hayo.

Nini kitatokea endapo utashindwa kueleza udhaifu wako?

Muajiri anaweza kudhani unaudhaifu wa kutisha kiasi cha kushindwa kuutaja hadharani.

Muajiri anaweza kuhisi kuwa unadhani wewe ni mkamilifu kwa kuwa hauitambui nafsi yako.

Anaweza kufikiri pia kuwa unadhani wewe ni mkamilifu kwa sababu uelewa wako ni mdogo.

Kwa mifano hiyo michache, naamini unaweza kupata picha nzuri ya kujibu swali hili na kuonekana kuwa wewe ndiye chaguo bora zaidi kwa nafasi ya kazi iliyotangazwa baada ya kujibu maswali mengine vizuri.

NI Vigumu Kuelewa Kuwa Mapenzi ni Pamoja na Kipigo – Waziri wa Katiba na Sheria Prof. Palamagamba..!!!

$
0
0

Waziri wa Katiba na Sheria Prof. Palamagamba Kabudi ameeleza  Bungeni mjini Dodoma kuwa imekuwa vigumu watu kutambua kuwa mapenzi yamekuwa yakiendana na kipigo kwa wapendanao hivyo kuhatarisha maisha.

Prof. Palamagamba ameeleza hayo wakati akijibu swali la Mbunge wa Ukonga, Mwita Waitara (Chadema) kuhusu mkakati wa serikali kupambana na tatizo la ukeketaji wa watoto wa kike na unyanyasaji wa wananwake jambo ambalo ni kinyume cha sheria ya nchi.

NOMA Sana..JB Amtolea Povu Wema Sepetu na Wenzake Ambao Hawakuandamana na Makonda Kupinga Uuzaji wa CD Feki na Za Nnje..!!!!

$
0
0

Muigizaji mkongwe nchini Jacob Stephen 'JB amefunguka na kudai hawakufanya maandamano ya kuzuia movie za nje ya nchi kuuzwa nchini bali waliandamana kuzitaka zilipiwe kodi au serikali itoe msamaha kwenye filamu za ndani.

JB amezungumza hayo alipokuwa akifanya mahojiano na wanahabari wakati wa uzinduzi wa filamu ya Tunu na kudai kuwa watu wengi wamehusisha maandamano yao na siasa kitu ambacho hakina ukweli na kuongeza kuwa tasnia ya filamu kwa sasa inahitaji watu watakaowasaidia kumaliza kilio chao.

"Sisi hatupingi movie za nje kuingia nchini, mimi mwenyewe nazipenda na ninaziangalia. Hapa ugomvi uliopo ni wao watozwe kodi au na sisi tuondolewe hizo kodi, wakifanya hivyo hakuna mtu ambaye atapiga kelele tena. Sasa hivi nakatwa asilimia 30 lakini bado natakiwa nitoe asilimia tano na wakati huo huo, nikitaka kutoa movie mpaka nikaombe kibali kama ni wewe ungekubali? Na jambo hili lisihusishwe na siasa kwani sisi mtu yoyote ambaye ataweza kutusaidia kutusemea tutamsikiliza hata akiwa wa upinzani hatuna shida" Alisema Jb

Aidha msanii huyo ameongeza kuwa wasanii wenzao wanaowakejeli kwa kuandamana wengi wao hawategemei movie kuwaingizia kipato na ndio maana wanaongea maneno ya ajabu huko nje.

"Msanii yoyote ambaye filamu ndiyo chakula chake hawezi kuwa nje ya hili kwa sababu hataweza kuishi. Mimi niseme tu siwezi kuishi bila filamu ndiyo maana tunapiga kelele. Sitaki kuwataja majina lakini angalia tu wewe mwenyewe huyo mtu ambaye hataki kupiga kelele anaishi bila filamu?" JB alimaliza
Viewing all 104789 articles
Browse latest View live




Latest Images