Quantcast
Channel: UDAKU SPECIAL
Viewing all 104709 articles
Browse latest View live

Karibu ACT-TANZANIA, wewe ndio mbadala wa CHADEMA na CCM

$
0
0
Chama kilichovunja rekodi kwa kupata usajili wa kudumu miezi michache mara baada ya usajili wa muda; ACT-TANZANIA leo ndio kimekabidhiwa cheti chake cha usajili wa kudumu rasmi na masajili wa vyama vya siasa mara baada ya kumalizika zoezi la usajili lililofanyika katika
mikoa kumi iliyoteuliwa

kilifanikiwa kumaliza zoezi la uhakiki mara baada ya kuruka vihunzi vingi toka kwa wahafidhina na watu wasiopenda siasa za ushindani. Katika zoezi letu tumekumbana na vikwazo vingi ikiwa pamoja na uchomekaji wa wanachama fake waliotumwa kwaajili ya kazi ya kujifanya wako tayari kuhakikiwa lakini kwa lengo la kutojitokeza siku ya kuhakikiwa, jambo ambalo wahafidhina na maadui zetu walikuwa hawajui ni kuwa chama chetu kinapendwa na wananchi hivyo wengi walijitokeza kiasi cha kuziba mapengo ya mamluki ambao kwa makusudi hawajajitokeza siku ya kuhakikiwa. Pamoja na hayo tunatambua wanachama wetu waaminifu waliotaka kujitokeza lakini sababu zilizo nje ya uwezo wao zilipelekea washindwe kujitokeza siku ya kuhakikiwa.

Karibu ACT-TANZANIA, wewe ndio mbadala wa CHADEMA na CCM.

Mungu ibariki Tanzania.

DIAMOND "Behind Every Man's Success There is a Strong Woman, Now These are my Starrings..

$
0
0

Diamondplatnumz
12 hours ago
They say Behind every Man's success there is a strong Woman... Now these are my Starrings...without forgetting my all luvyly and Beautiful, Aunties and sisters 👊👊👊👊 #LuvlyMum #LuvlyBaby (Wanasemaga katika kila Mafanikio ya mwanaume basi kuna mwanamke imara yuko nyuma... Hawa sasa ndio Mastarring wangu, wakishirikiana na ma dada zangu, Aunties, na mawifi pia lol!👊👊👊👊 #LuvlyMum #LuvlyBaby

Team Lemutuz Watupiana Maneno na TeamUkwelinaUwazi Instagram Kisa Ugomvi wa Wema na Kajala

$
0
0

Ilianza Hivi:

Teamukwelinauwazi
3 days ago
Huyu Lemutuzi nae ni mbulula wa kwanza Tanzania kama wewe kweli hawa ni superfriends zako unashindwaje sasa kuwaweka chini ukaongea nao na ukajua chanZo cha ugomvi wao na mwisho ukawasuluhisha !! Nakuona unaegemea upande wa wema ! Kwani alikwambia nani kua ukimsaidia mtu ndio umnyenyekee kama mungu wako hata kama akifanya makosa basi umchekee tu kiiiisa huna sauti eeeeti kwa sababu tu amekusaidia huo ni utumwa!!! Heshima ni kitu cha Bure ndio maana tunaambiwa muheshimu mdogo nae atakuheshimu! Juzi tumeona interview Ya kajala na mwanae kajala kaongea vizuri sana sio kwamba kasahau wema aliotendewa la hasha na kasema hata amlioe mabiliini si kitu !! Yaliyopo nyuma Ya pazia ni mengi ukweli wa chanZo cha ugomvi wao wanaujua wenyewe!! Sasa wewe lemutuz na mtumbo wako peleka huko gym mtu mzima wewe ovyoo sana na hizo system zako !! Kwanza ile Harusi yako uliojigamba haina muchango imeishia wapi ??? Huyo mchumba yuko wapi maana kila siku kupiga picha na bebez Za watu !! Eti ooh bahari baharia utakua wewe meli ikipinduka utahemea wapi kama nakuona utakavyotapatapa ndani Ya Maji .. Ukimkuta kwenye kumbi Za starehe sasa anavyojinadi ooh mi hinijui Mimi ndio lemutuz uliza mjin hapa nafahamika sana !! Nyooo huna haya mwanaume mzima uache kutulia na familia kutwa unakesha kutafuta umbea tutokee hapa na jasho la mchicha pori...

Ikafuatia Team ya Lemutuz Kutoa Vidonge:

Teamlemutuz
@teamukwelinauwazi naona umeanza kufulia now! Huna mastori ya maana like you used to be, siku hizi @teamukwelinauwazi imegeuka team penny!! Mnakazi ya kutetea tu kinafiki kila kitu kinachifanywa na team penny hata kama wanafanya uozo!! Kajala ni mpumbavu na mnafiki, najua bibie unamtetea kwa kuwa yuko team penny, but the truth be said kajala mjinga hakumbuki alikotoka hajui siku anaweza kupata janga kubwa zaidi and hao alionao wote watamkimbia, marafiki wenyewe wako nae ili tu kumuumiza wema, hawana upendo wowote!!!! Big up @lemutuz kwa kumwambia ukweli si watu wote wenye ujasiri wa kumwambia mtu ukweli pale anapokosea..... waache mburulaazzz waongeee

CUF: Wasiotaka Serikali ya Umoja wafukuzwe

$
0
0
Zanzibar. Chama cha Wananchi (CUF) kimesema wanasiasa wanaojadili suala la kuendelea au kutokuendelea na Serikali ya Umoja wa Kitaifa (SUK), wanastahili kujiuzulu au kufukuzwa ndani ya vyama vyao.

Kauli hiyo imekuja siku moja baada ya Mnadhimu wa Baraza la Wawakilishi Zanzibar (BLW), Salmin Awadh Salmin kusema kuwa Wawakilishi wa CCM wanajiandaa kuwasilisha hoja binafsi kwenye Baraza hilo ili kuwapa nafasi wananchi waulizwe iwapo wanataka kuendelea na Serikali ya Umoja wa Kitaifa au vinginevyo.

Salmin aliyasema hayo juzi kwenye mkutano wa hadhara uliofanyika kwenye Viwanja vya Kibandamaiti, Unguja kwa kuwa wanaona kwamba lengo la kuundwa kwake halina dalili njema kwa siku za usoni.

Jana, Mkurugenzi wa Haki za Binadamu na Mawasiliano ya Umma wa CUF, Salum Abdallah Bimani alisema: “Kimsingi mpango huo unakwenda kinyume na uamuzi wa vyama vya CCM na CUF ambao ulipitishwa na kuridhiwa na vikao vya juu vya vyama hivyo viongozi wanaopinga jambo hilo wanaonyesha kupingana na uamuzi wa vyama vyao.”

Ajenda ya siri

Mkurugenzi huyo wa CUF alikana chama chake kuwa na ajenda ya siri ya kuvunja Muungano au kuyasambaratisha Mapinduzi ya Zanzibar na kusema kinachopiganiwa ni muungano wenye usawa, haki na heshima kila upande wa washirika.

Kuhusu Ukawa kususia Bunge Maalumu la Katiba, Bimani alisema chama chake kimetoa masharti matatu yanayopaswa kuzingatiwa kabla ya kubadilisha msimamo wake. Alitaja masharti hayo kuwa ni kuijadili Rasimu ya Katiba kama iliyowasilishwa na Tume ya Mabadiliko ya Katiba; wajumbe wa CCM kuacha matusi, vijembe na ubaguzi na hilo lithibitishwe kwa maandishi na viongozi wake wa kitaifa.

Jambo la tatu ni kuhakikishiwa kuwa vikao vya Bunge vitumike kujadili rasimu na si sera za vyama vya siasa kwa vile ndiyo mwanzo wa kukaribisha malumbano na kusababisha Bunge kupoteza mwelekeo na kuweka nyufa katika Umoja wa Kitaifa.

Bunge la Bajeti Laanza Leo kwa Posho Mpya

$
0
0
Dodoma. Bunge la Bajeti linaanza leo mjini Dodoma huku wabunge wakitarajiwa kuanza kulipwa viwango vipya vya posho, ambazo ni Sh300,000 kwa siku sawa na kiwango wanacholipwa wajumbe wa Bunge Maalumu la Katiba.

Kabla ya kufikia uamuzi wa kupandisha viwango hivyo kwa Sh100,000 zaidi, wabunge walikuwa wakilipwa Sh200,000 kwa siku (yaani Sh70,000 kama posho ya kikao (sitting allowance), Sh80,000 posho ya kujikimu (perdiem) na Sh50,000 ya gharama za usafiri).

Nyongeza hiyo kwa kila mbunge kwa siku, sawa na asilimia 50, italigharimu Bunge la Jamhuri ya Muungano kiasi cha Sh18.5 bilioni kwa siku 52 zilizotengwa kwa ajili ya Bunge la bajeti linalotarajiwa kuhitimishwa Juni 27.

Januari mwaka 2012, Rais Jakaya Kikwete alikataa maombi ya Bunge ya kutaka nyongeza ya posho ipande hadi Sh330,000 na badala yake wabunge hao wakapata nyongeza ya Sh50,000 tu kwa ajili ya usafiri.

Katibu wa Bunge, Dk Thomas Kashililla alipoulizwa kuhusu nyongeza hiyo, hakuthibitisha wala kukanusha, lakini akafafanua kwamba hilo ni suala la uongozi wa Bunge na si la kiutendaji.

Mange Kimambi Afunguka Kuhusu Mpoki Kuzidisha Utani Siku ya Tuzo za Kilimanjaro

$
0
0

Watu Wengi Wamekosoa na wengine kusifia Alichofanya Mpoki siku ya Tuzo za Kilimanjaro Music Kwa Kile Alichokuwa Akifanya Jukwaani kwa Kutania Matani ya Live Live kwa Wahuzuriaji na Wasaniii Siku hiyo ....Mwanamitindo Mange na Yeye Hakukosa cha Kusema :



Ndoa Haina Mwenyewe Bana...Kama Unabisha Angalia Watu Wanao Oa na Kuolewa

$
0
0
Ukitaka Kujua NDOA HAINA mwenyewe angalia watu wanaoolewa na kuoa...Ni wale usiowategemea kabisaaaaaaaa
Ndoa haina Kanuni...Kwamba ukifuata Stage 1,Ukavuka Stage 2 basi unaqualify...WALAAAA
Kuna watu na Bikira zao(kama Mimi) na watu hawana habari nao kabisaaaaa
ILA kuna watu 'wametumika' mpaka Mshale wa Kilomita umeungua,hausomi,lakini kabla ya September mwaka huu, vidole vyao vitakua vinang'aa kwa bati takatifu la dhahabu
Watu wanaloga waolewe...UTASANDA
Wengine wanapretend ili Wawavutie watu flani...UTASUBIRI SANA
Ndoa ni Blessing from God na ni kitu kitakatifu...Ni Mpaka Mungu aaandike,aruhusu...HAINA MBINU
Just BE URSELF mtu akupende na akuoe kama ulivyo,Usimuonyeshe wewe ni Mwekundu ili akupende halafu aje agundue wewe ni wa Pink
UTAKUWA MJANE KIJANA BAADA YA 3YEARS!
By Seth De Jesus

Urembo Kwa Mwanamke Mazoezi ni Muhimu

$
0
0
Mwanamke Ukitaka kuonekana Mrembo na Mwenye Afya Njema Basi Siku Moja Moja Kupiga Mazoezi itakuongezea Muonekana Mzuri Mbele za Watu, Piga Mazoezi Chumbani Mwako sio lazima uende Gim, ila Kama Pesa Inaruhusu basi nenda Gim Kama wakinafulani fulani ....

Mganga wa Diamond Aibuka na Mapya Baada ya Tuzo Saba

$
0
0
Yule mganga maarufu wa mastaa nchini ambae
aliwahi kutangaza kuwa amekuwa na ukaribu na
mwanamuziki Diamond ameibuka na kusema
kuwa tuzo hizo saba alizozipata zinamaana
kubwa sana kwenye kazi zake anazozifanya.

alisema" Niliongea na Diamond wiki moja kabla
ya shoo nikamueleza kuwa atapokea tuzo nyingi
sana mwaka huu na hizo tuzo ni ishara tosha ya
kudumu kwenye game kwa miaka kama hiyo ya
tuzo zake kwa maana ya miaka saba mbele yote
nyota yake itaendelea kung'ara" Alisema Dokta
Kamdege
Aidha Mganga huyo aliendelea kusema" Unajuwa
haya mambo ya maagano yapo muziki na miti
shamba zinaendana kwani kwenye dunia hii ya
leo maadui ni wengi kuliko marafiki kwani wapo
watakaokuchukia bila sababu za msingi hivyo ni
vyema ukalijua mapema hilo na kujikinga kama
ilivyo kwa Diamond" Alisema mganga huyo
mwenyeji wHa Mkoa wa Tabora
Hata hivyo mganga huyo aliendelea kuto uwito
kwa watanzania popote walipo duniani
waendelee kupata huduma zake kwani hii ni
kama baraka kwa taifa la Tanzania.
Dokta Kamdege amekuwa akitumiwa sana na
vigogo wa Serikali, wasanii na watu mbalimbali
duniani kufanikisha mambo yao kwa kuwapatia
baraka kupitia miti shamba.

Mwanamuzi wa Kenya Jaquar Aanza Maringo Agomea Mwaliko wa Kill Awards..Kisa Hichi Hapa

$
0
0
Post hii ni maalum kwa staa wa muziki wa Kenya anaetajwa kuingia kwenye TOP 5 ya Wasanii matajiri wa muziki wa kizazi kipya Afrika Mashariki huku orodha hiyo ikiwa na watu wengine kama Jose Chameleone.
Imefahamika kwamba Jaguar alikataa kuja kwenye tuzo za Kili 2014 alizokua nominated baada ya waandaaji kushindwa kufikia masharti aliyowapa na badala yake akaamua kwenda kuhudhuria harusi ya producer wa DNA aitwae Refigah.
Jaguar alitaka atumiwe ticket ya ndege ya business class, alitaka achukuliwe chumba kwenye hoteli ya nyota tano, apewe ulinzi popote atakapokwenda na vilevile apewe gari zuri la kifahari la kutembelea.
Kwenye sharti jingine Jaguar alitoa option kwa waandaaji na kuwaambia kama wangeshindwa kumpa ticket ya ndege basi walipaswa kuweka mafuta ili aje na ndege yake ndogo anayomiliki.

Alipohojiwa na ghafla.co.ke Jaguar alisema asingeweza kuhudhuria tukio ambalo asingepewa heshima aliyoitaka kama ambavyo huwa anaipata anapokwenda kwenye nchi nyingine katika matukio kama haya ndio maana ilikua bora ahudhurie harusi na kuongeza kwamba ‘nitahudhuria iwapo wataanza kuwa-treat vizuri wasanii wa Kenya’
Tuzo za KILI 2014 zilihudhuriwa na mastaa wawili wa Kenya ambao ni Wyre na Amani huku Uganda ikiwakilishwa na Jose Chameleone ambae ndio alitangazwa mshindi kwenye kipengele cha Afrika Mashariki.


Source Millard Ayo

Meninah-Mwanamke Mrembo Katika Tasnia ya Bongo Flava

$
0
0

Hakika ni Mrembo wa Haja Anayewakilisha Vyema Wanawake katika Tasnia ya Music wa Bongo Flava....Nani mwingine anakutia uzuri wake kati ya waimbaji wa Kike wa Bongo Flava?

Chungu Anayoipata Waziri Nyalandu Hata Kaa Aisahau

$
0
0
MACHUNGU wanayokutana nayo mawaziri wanaopewa kuiongoza Wizara ya Maliasili na Utalii, siyatofautishi na yale yatajwayo kupatikana jehanamu mahali kunakotajwa kuwa ni kwenye mateso ya watenda dhambi.

Alipoteuliwa Waziri Lazaro Nyalandu kuongoza wizara hiyo niliyoibatiza jina baya, nilistaajabu kumuona akiwa mwenye furaha kana kwamba aendako kulikuwa ni mahali pema. Jehanamu ni jehanamu tu, nia aliyoiita njema ya kuwaondoa vigogo wa wanyamapori, Mkurugenzi Alexander Songorwa na msaidizi wake Jaffer Kidegesho kama njia ya kutekeleza azimio la bunge na kusafisha ufisadi, duru ziligeuzwa na kuwa ubaya.

Kelele zikasikika kuwa, kitendo cha kuwasimamisha watumishi hao ilikuwa ni njia ya kujisafishia ulaji rahisi, kwamba amewatoa wachapakazi ili iwe rahisi kwake kujisevia maliasili.

Kwa kuwa chemichemi ya maji machungu haiwezi kutoa maji matamu, Katibu mkuu wa wizara hiyo Maimuna Tarishi aliibuka, sijui kwa kutumwa na nani, akawarejesha vigogo waliofukuzwa na Nyalandu, huku Katibu Mkuu Kiongozi Ombeni Sefue akimfedhehesha waziri huyo kwa kumwambia hakufuata sheria, kanuni na taratibu za kumfukuza mtu kazi.

Swali langu; kama Nyalandu hajui hata sheria ndogo kama hizo alikuwa na sifa gani za ziada kuteuliwa kuongoza wizara hiyo nyeti? Narudi kulekule nikowahi kusema, mfumo wetu wa utawala una walakini!
Waziri Nyalandu anakuwa waziri wa 11 kupwaya kwenye wizara hiyo ndani ya miaka michache.

Najipongeza kwa jina kwamba maliasili ni wizara yenye sifa za jehanamu kwani hakuna waziri aliyewahi kuiongoza kwa mafanikio na furaha, kila aliyekuja alinusa kwa miaka miwili na kuondoka zake kwa aibu, kidogo Zakhia Meghji ambaye alikaa kwa miaka saba na kisha kisa cha uuzwaji wa Hoteli ya Kilimanjaro, kikamuondoa.

Mwaka 1988-1990, Waziri Arcado Ntagazwa aliongoza wizara ya maliasili, viatu vikampwaya, akalaumiwa sana kwa ufisadi kwamba alibinafsisha hoteli za kitalii kiholela ikiwemo Lake Manyara, Ngorongoro, Seronera na Lobo.

Ntagazwa alipotimuliwa ‘jehanamu,’ akaingia Abubakari Mgumia, 1990-1993, akaambiwa ameshindwa kudhibiti uharibifu mkubwa wa misitu kutokana na kushamiri kwa biashara ya mbao.
Alipotokomezwa Mgumia, akaingia Juma Hamad Omar, huyu akakumbwa na kashfa nzito kupata kutokea ya kuliuza Pori la Loliondo, akafukuzwa kwa aibu kubwa.

Baadaye 1995-1997, ‘jehanamu’ ikamwita Juma Ngasongwa, naye hakufaa, biashara ya uuzaji wa minofu ya samaki nje ya nchi bila kibali ikamwondoa na nafasi yake kushikwa na Meghji 1997-2005.
Awamu ya Nne ya Rais Jakaya Kikwete ikaanza na Anthony Diallo, akadumu kwa miaka miwili, mvutano kati yake na watendaji wa wizara na kashfa ya uuzwaji wa vitalu, vikamng’oa na nafasi yake kuchukuliwa na Profesa Jumanne Maghembe, ambaye maji yalizidi unga akatolewa ndani ya mwaka mmoja tu, 2007-2008, kwa kushindwa kusimamia vema uuzwaji wa vitalu na uvunaji miti.

Uteuzi ukamfuata Shamsa Mwangunga, 2008-2010, mambo yakamshinda akatolewa kwa kashfa ya kuongeza muda wa umiliki wa vitalu bila kufuata sheria, nafasi yake ikachukuliwa na Ezekiel Maige, waziri kijana ambaye alidumu kwa miaka miwili kabla ya kuingia kwenye skendo ya kuuza wanyamapori hai kiholela.

Aliposhindwa Maige, akaingia Balozi Khamis Kagasheki, waziri mchapakazi aliyeaminika na kila mtu, akafanyiwa mizengwe kwa kuhusishwa na Oparesheni Tokomeza, ikamlazimu ajivue gamba na kumwachia msaidizi wake Nyalandu ambaye leo anatajwa kuwa hajui hata sheria za uajiri. Pole Nyalandu ‘jehanamu’  hakuna furaha. Nachochea tu!

Huyu Mwanamke Kanishangaza Sana..Haridhiki !!

$
0
0

Nina mpenzi wangu anayefanya kazi Morogoro, mwezi march alikuja kunitembelea sababu alikuwa likizo na alikaa kwangu wiki 2 na siku 3 tangu afike. Alishikwa na malaria kali ikabidi niombe ruhusa kazini ili nimuuguze.

Kiukweli nilimpa kila kitu anachotakiwa kupewa mgonjwa including dawa,vyakula vilivyopendekezwa na daktari na vyakula alivyopenda mgonjwa, pamoja na gari kumpeleka hospitali au sehemu yoyote aliyopenda ili kumliwaza mgonjwa. Mungu akasaidia akapona na amerudi morogoro.

Lakini cha ajabu juzi ananiambia sikumjali alipokuwa anaumwa sababu sikuwahi kumletea kadi ya get well soon pamoja na Mauwa kama wenzake wakiumwa wanavyofanyiwa. Ebu nisaidieni kadi na maua tu ndio mtu akujali?

Napenda Mwanamke Mwenye Matiti Makubwa ila Wenzangu Wanaponda

$
0
0
Wadau naomba kuuliza!Mwanzoni wakati naanza mahusiano ya kimapenzi nilikuwa napenda sana wasichana wenye chuchu ndogo,

but as time went on nikajikuta napenda wenye matiti makubwa Kinachonichanganya zaidi ni pale washikaji zangu wanavyowadis wenye mtindi!

Nini maoni yenu wadau katika hili? 

I mean,ninyi wenzangu mnawachukuliaje wenye matiti makubwa!?

Duh! Achana na Azam kwa Mambo ya Fedha

$
0
0
AZAM Tv imefanya kufuru kwa kutoa udhamini wa Sh 361.6 milioni kwa ajili ya kurusha ‘live’ mashindano ya mpira wa kikapu ya Miji Mikuu ya Afrika Mashariki na Kati, ambayo yanaanza leo Jumanne Uwanja wa Ndani wa Taifa, jijini Dar es Salaam.

Mashindano hayo yatafanyika kwa siku sita kuanzia leo Jumanne mpaka Jumapili, Azam itakuwa inarusha mechi zote kuanzia saa 2 asubuhi mpaka saa 2 usiku mechi hizo zinapomalizika kwa mujibu wa ratiba ya mashindano hayo.

Kurusha mechi moja kwa saa moja ni Dola 3,000 (Sh 4.8 milioni) ambapo kwa saa 12 itakuwa ni Sh57.6 milioni na hivyo kwa siku sita ni sawa na Sh345.6 milioni. Imeelezwa kuwa Azam wameahidi kusaidia bajeti ya Sh16 milioni ambayo waandaji walipeleka hivyo kufika kiwango cha Sh 361.6 milioni.

Mwenyekiti wa Kamati ya Mashindano, Mwenze Kabinda, alisema; “Bajeti yetu ilikuwa ni Sh16 milioni ndiyo tuliyopeleka kuomba kusaidiwa, lakini Azam wamechukua jukumu la kutudhamini kurusha mechi zetu zote na kusaidia fedha tulizoomba. Sisi tusingeweza kufanya hivyo kwani kiasi tulichoomba kilikuwa ni kwa ajili ya maandalizi mpaka tutakapomaliza.”

Katika ufunguzi wa mashindano hayo timu ya jiji la Dar es Salaam ambao ni wenyeji itaanza kampeni yake ya kusaka ubingwa huo kwa kucheza na Mombasa katika mechi ya ufunguzi, Mbeya na Kigali, Tanga na Adiss Ababa wakati upande wa wanawake, Dar es Salaam watacheza na Kampala mechi hizo zitachezwa kabla ya ufunguzi rasmi wa michuano hiyo.

Arsene Wenger Asingedumu Hispania Kama Angekuwa Kocha kwenye Ligi Hiyo

$
0
0
KOCHA Mkuu wa West Brom, Pepe Mel amesema kocha Arsene Wenger kushindwa kutwaa mataji kwa muda mrefu huku akiwa na kikosi imara kama cha Arsenal ana bahati sana kwa sababu kazi yake anafanya England na kama angekuwa Hispania angefukuzwa kazi siku nyingi.

Arsenal haijatwaa taji lolote la maana tangu mwaka 2005 ilipotwaa Kombe la FA na msimu huu wanaweza kumaliza ukame huo kama wataifunga Hull City kwenye fainali ya Kombe la FA itakayofanyika Mei 17 uwanjani Wembley, London.

Mel anasapoti falsafa za kocha huyo Mfaransa, lakini anashangaa ni vipi anakinoa  kikosi chenye wachezaji makini kama cha Arsenal na kushindwa kunyakua mataji.

Wakati Gerardo Martino akijiandaa kuondoka Barcelona mwisho wa msimu, Wenger anapewa nafasi ya kurithi mikoba, lakini Mel anamtaka aendelee tu kubaki England kwa sababu kama atakwenda Hispania hatadumu kwa muda mrefu kwa kuwa na timu isiyotwaa mataji.

“Sidhani kama Arsene angeweza kudumu na kibarua chake nchini Hispania,” alisema Mel, 51.

“Carlo Ancelotti ni mfano mzuri pale Real Madrid. Miezi mitatu iliyopita alikuwa kwenye presha kubwa sana kabla ya sasa kupoa kwa sababu ameifikisha timu fainali ya Ligi ya Mabingwa Ulaya. Hispania kocha anaishi kutokana na matokeo.”

Mbeya City: Simba Imekula Kwenu

$
0
0
MBEYA City imewaambia Simba kwamba wamebugi kwa wanachokifanya kwa straika wao, Saad Kipanga na kwamba wao hawamuachii kwani wana mkataba naye.

Mchezaji huyo alizungumza na Mwanaspoti na kuihakikishia kwamba amezungumza kwa kina na matajiri wa Simba, lakini hajataka kuliweka bayana suala hilo kwa uongozi wa Mbeya City.

Mwanaspoti linajua kwamba Simba inafanya mambo yake kimyakimya na imejidhatiti kwamba lazima kijana huyo avae jezi nyekundu msimu ujao.

Mbeya City imefura na kumtaja Kipanga kwamba bado ana mkataba wa mwaka mmoja na nusu na kama Simba amewaeleza vinginevyo wamechemka. Katibu Mkuu wa Mbeya City, Emmanuel Kimbe, alisema kuwa uongozi wao bado haujapanga kuwauza wachezaji ingawa suala hilo linawezekana endapo pande zote mbili zitakutana na kukubaliana na si vinginevyo.

“Tumesikia, mchezaji tumemuuliza amekataa kuzungumza na viongozi wa Simba, ila ukweli anaujua yeye kikubwa ni kwamba hakuna mchezaji ambaye tumepanga kumuuza,” alisema Kimbe.

“Kipanga ana mkataba na sisi tena wa muda mrefu, hivyo kama Simba wanafanya mazungumzo na mchezaji huyo ni kosa, wanatakiwa kuja kuzungumza na viongozi ili wasikie sisi tunasemaje, huko ni kuwarubuni wachezaji.”

Alisema kuwa Simba wanafahamu kanuni zote za usajili ambazo wanatakiwa kuzifuata huku akisisitiza kuwa endapo Kipanga angebakiza mkataba wa miezi sita ilikuwa ni ruhusu kufanya naye mazungumzo.

“Sheria zipo wazi ambazo kila kiongozi wa soka anazifahamu, Kipanga tulimsajili wakati wa usajili wa dirisha dogo, wakiamua kuja ndipo tutajua cha kuwajibu zaidi na watajua mkataba wa mchezaji huyo umebaki wa muda gani, ila napo wanaweza kumkosa kwani hatuna mpango wa kumuuza kwa sasa,” alisema Kimbe.

Kiongozi Simba aonya

Mweka Hazina Msaidizi wa zamani wa Simba Humprey Laban, ameuonya uongozi wa klabu hiyo kwamba usithubutu kusajili wachezaji waliowahi kukipiga timu hiyo kisha kuhamia Yanga kwani endapo utafanya hivyo utakuwa unakaribisha hujuma.

Simba iko kwenye mazungumzo na kipa Ally Mustapha ‘Barthez’ aliyemaliza mkataba na Yanga. Laban alisema kwa uzoefu wake wachezaji waliowahi kuhama kutoka Simba kwenda Yanga kisha kurudi tena ndio wamekuwa wakihusika katika kufanya hujuma.

“Simba chonde chonde wachezaji waliohamia Yanga kutoka kwetu tusiwarudishe tena wengi wao ndio ambao wamekuwa wakihusika katika kutuhujumu, tatizo ni kwamba wachezaji wa namna hii wanakuwa na marafiki kutoka pande zote hivyo inakuwa rahisi sana wao kutumika kwenye michezo michafu naomba waachane nao kabisa,” alisema.

Ray C Hoi Kitandani, Adaiwa Kuugua Ugonjwa Mpya

$
0
0
Nimepata Habari kuwa Mwanamuziki Ray C yupo hoi Kitandani Akiugua Ugonjwa Mpya Unaojulikana kama Homa ya Denge...Inasemekana Baada ya kutoa tuzo ya Kill  Siku ya Jumamosi Kesho yake alianza kuumwa Kichwa na Baadae alipelekwa Hospitalini Mwananyamala Akidhani ana Malaria, Alipopimwa ikagundulika unaumwa huo ugonjwa wa Denge......Ugonjwa huo inasemekana unaambikizwa kwa kung'atwa na Mbu
Get Well Soon

Fid Q "Nilistahili Kushinda Tuzo ya Kill, Kila Mtu Amefurahi Baada ya Kunibania kwa Muda Mrefu"

$
0
0

Msanii Fid Q amehabarisha kuwa kila mtu amefurahi kwa yeye kushinda Tuzo ya Mwana Hip Hop Bora wa Mwaka , Amesema hiyo inajidhihirisha hata kwenye Social Media kila mtu anasifia na kukubali ishindi wake ..Amasema Amebaniwa Miaka Mingi hiyo tuzo na Hatimae ameipata....


Swali:
  • Je huko Nyuma ni Kweli watu walikuwa wanabaniwa Tuzo ?
  • Je Utaratibu Mpya wa Kill Awards kupata washindi ni wa Uwazi zaidi ?

Dr Mwakyembe"Madereva wa Malori ya Kwenda Nje ya Nchi Wanatutia Aibu wa Tanzania"

$
0
0
Dr Mwakyembe Akiwa njiani kwenda Congo Kufungua Kituo cha Bandari ya Tanzania ambacho kitasaidia Malipo kwa Wafanya Biashara wa Wanaopitishia Mizigo ya Bandari ya Dar es salaam aliweza kuona hali halisi waliyonayo Madereva wa Magari Makubwa ya Mizigo Kutoka Tanzania kwenda nchi zingine, Amehabarisha kuwa Madereva wa Tanzania ni wachafu na wananjaa Sana Kiasi wanatembea na Masufuria na vikombe kwenye Malori yao kwa vile hawana uwezo wa Kununua chakula Mahotelini wakiwa njiani ni Bora wafike mahali Wapike...Amesema hii inatia Aibu Taifa kwani ukikutana na Malori Mengine kutoka nchi zingine ni wasafi na wanaonekana Wamewezeshwa vya kutosha, amesema Madereva wa Tanzania Wamesema wanapewa Hela kidogo ya Kujikimu njiani , Boss anakupa laki tatu hiyo uitumie mwezi mzima ukiwa njiani ni haki Kweli ? Mwakyembe amehaidi kulishughulikia hilo swala 
Viewing all 104709 articles
Browse latest View live




Latest Images