Quantcast
Channel: UDAKU SPECIAL
Viewing all 104712 articles
Browse latest View live

AAAH!! Bashite Mkuu Hayumo..?Serikali Wasema Sifa Yake ni Kujua Kusoma na Kuandika..Habari Vichwa vya Magazeti ya Leo 29/4/2017..!!!


PICHA 5 za Snura Mushi Akionyesha Bonge la Tako Akifanya Kazi za Kawaida Kama Kulima

$
0
0
Snura Mushi amebarikiwa na makalio na umbo hatari… Mwimbaji huyo amevuma kwa nyimbo za uhuni ambazo zimezua utata kwa jamii.

Snura anapenda sana kuonyesha makalio yake ata anapofanya kazi za kawaida kama kulima, kuokota kitu chini na kazi yoyote ile itakayomfanya ainame.

Tazama picha hizo hapo chini uone vile Snura huonyesha makalio yake afanyapo kazi za kawaida:





SIKU Chache Baada ya Kuonyesha Mtoto Kwenye Mtandao, Ndoa ya Nuh Mziwanda Kukumbwa na Matatizo

$
0
0
Nuh Mziwanda anaonekana mwenye furaha kwenye mitandaoni lakini ndoa yake sio shwari hata kamwe.

sababu moja kuu ni uvutano uliyopo kati ya mke wake na familia yake ambayo haikufurahia Nuh Mzinwanda kiuingia uislamuni ili kumuoa.

Mama yake Nuh ndio aliadhirika ata zaidi kwa sababu yeye anafuata mambo ya kanisa sana.

Stori hii ilibainika wazi wakati Soudy Brown alipata kuzungumza na mke wa Nay katika U heard Cluds FM.

“Nilimwambia mama unachelewa, mwambie aniache. Na anajua kuwa mimi sijaolewa na mwanawe, ila anajua nimezaa tu na mwanawe. Kwenye sherehe ya harusi hakuwepo, alikuwa kwenye msiba. Yule mama ni mzee wa Kanisa, alikuwa anataka niende kanisani nibadili dini ndio niolewe.” Mama Anya alisema.

TRA Yaja na Mikakati 5 Ukusanyaji Kodi...!!!

$
0
0

MAMLAKA ya Mapato Tanzania (TRA) imeweka mikakati mitano ya kuboresha ukusanyaji kodi ya majengo, ikiwamo kutathmini majengo ili kupanga viwango rafiki vya kodi kwa walipakodi.

Mikakati mingine ni kuimarisha usimamizi na ufuatiliaji wa ukusanyaji, kutoa elimu kwa jamii kuhusu ulipaji kodi, kushughulikia pingamizi za kodi kwa wakati na kuboresha orodha ya uthamini ili kuwa na takwimu sahihi.

Ofisa Msaidizi wa Huduma ya Mlipakodi ya TRA, Maya Magimba alisema hayo alipozungumza na waandishi wa habari Dar es Salaam jana kuhusu umuhimu wa kodi.

Alisema kodi ni muhimu kwa Serikali kwa vile inatumika kuendesha shughuli za kijamii, ukiwamo ujenzi wa miundombinu ya barabara, zahanati na madarasa.

“Tutahakikisha nyaraka za usajili zinatunzwa na mlipakodi  kwa  kufuata taratibu ili kuepuka usumbufu,” alisema.

Alisema kodi ya majengo hulipwa kuanzia Januari mosi hadi Machi 31 kila mwaka bila adhabu, na baada ya Aprili mosi hulipwa na adhabu, kodi ya pango la ardhi hulipwa kuanzia Julai mosi hadi Desemba 31 kila mwaka.

Mkuu wa Kitengo  cha Habari na Mawasiliano Serikalini wa  Wizara ya Ardhi, Nyumba na Maendeleo na Makazi, Mboza  Maige alisema  mwananchi au taasisi yenye nyaraka za umiliki wa ardhi ya Serikali anapaswa kulipa kodi hiyo.

Alisema iwapo eneo litakuwa na maendelezo ya jengo la kudumu na linatumika, mtu huyo atalazimika kulipa kodi mbili.

WAKAZI Dar Watahadharishwa Juu ya Mvua Kubwa na Upepo Mkali..!!!

$
0
0

Mamlaka ya Hali ya Hewa (TMA) imetoa tahadhari kwa umma kuhusu vipindi vya mvua kubwa vinavyoambatana na upepo mkali na mawimbi makubwa katika mwambao wa ukanda wa pwani.

Katika taarifa yake ya leo saa 11:15 jioni, TMA imetoa tahadhari kuwa, kuanzia leo hadi keshokutwa kutakuwa na vipindi vifupi vya mvua kubwa inayozidi milimita 50 ndani ya saa 24 vinavyoambatana na upepo mkali unaozidi kilomita 40 kwa saa na mawimbi makubwa yanayozidi mita mbili.

Mamlaka hiyo imesema maeneo yanayotarajiwa kuathirika ni mikoa ya Tanga, Dar es Salaam, Pwani, Lindi na Mtwara. Pia, visiwa vya Unguja na Pemba.

“Hali hii inatokana na kuimarika kwa ukanda wa mvua nchini na kuimarika kwa mgandamizo mkubwa wa hewa katika Bahari ya Hindi eneo la kisiwa cha Madagascar, hivyo kusababisha upepo mkali katika pwani ya Tanzania,” imesema taarifa hiyo.

TMA imewataka wakazi wa maeneo hayo kuchukua tahadhari na hatua stahiki na kwamba, inaendelea kufuatilia hali hiyo na itatoa mrejesho kila itakapobidi.

UCHAGUZI Mwingine wa Eala Kufanyika Mei 10..!!!

$
0
0

Katibu wa Bunge, Thomas Kashililah, amesema uchaguzi wa wabunge wa bunge la Afrika Mashariki(Eala) utafanyika Mei 10 mwaka huu.

Kashilila ameliambia bunge leo kuwa uteuzi wa majina ya watakaogombea uchaguzi huo utafanywa na vyama Mei 3 na uchaguzi ni Mei 10.

Chadema ilishindwa kupata wawakilishi wa wabunge wa Eala baada ya majina waliyoyapeleka, kupigiwa kura ya hapana.

 Chadema kiliwateua Lawrence Masha  na Ezekia Wenje kuwania ujumbe wa bunge hilo la Eala.

HUU Ndio Utajiri wa Kutisha Aliouacha Aliyekuwa Kiongozi wa Freemason Andy Chande Kabla ya Kufa..Inadaiwa Alikuwa Tajiri Zaidi ya Bakhresa na Mo Dewji..!!!

$
0
0

MTANDAO maarufu wa Wikipedia umedai kwamba hayati Jayantilal Keshavji Chande (Sir Andy Chande) ameacha utajiri wa kiasi cha dola milioni 892; unaomfanya kuwa na utajiri mkubwa kuliko ule wa Said Bakhresa, ingawa watu waliokuwa karibu naye wanakana kuwa na utajiri wa aina hiyo.

Kwa mujibu wa mtandao huo, Bakhresa ana utajiri wa thamani ya dola milioni 560 (shilingi trioni 1.2) akiwa nyuma ya Mohamed Dewji aliyetajwa na jarida la Forbes kuwa na utajiri wa dola bilioni 1.1 (shilingi trilioni 2.2) na Rostam Aziz ambaye Forbes imedai utajiri wake unakadiriwa kufikia kiasi cha dola bilioni moja (shilingi trilioni mbili).

Utajiri wa akina Dewji, Rostam na Bakhresa umekuwa ukifahamika katika jamii ya Watanzania, lakini taarifa hizi mpya kuhusu Chande, aliyefariki dunia mapema mwezi huu, ni mpya katika masikio ya wengi.

Familia ya Chande ndiyo ilikuwa ikitawala biashara ya usagishaji hapa nchini kabla ya ubinafsishaji wa mwaka 1967 na kuwa Shirika la Taifa la Usagishaji (NHC) lililobinafsishwa na kupewa Bakhresa ambaye sasa ndiye mwekezaji mkubwa zaidi mzawa hapa nchini.

Kuna kipindi, katika miaka ya 1970 na 1970, Chande alikuwa mmoja wa wakurugenzi katika bodi takribani 25 za mashirika mbalimbali ya umma hapa nchini – akidaiwa kuaminiwa na Baba wa Taifa, Julius Nyerere, kwa umahiri wake wa masuala ya kibiashara.

Kwa sasa, Chande hakuwa anamiliki biashara yoyote kubwa na maarufu hapa nchini, zaidi ya shughuli za kutoa misaada na nyingine ambazo kwa kawaida hazina uhusiano na utajiri wa namna hiyo ulioelezwa na Wikipedia.

kwamba mke wa Chande ni dada wa familia maarufu ya Madhvani, ambayo ni mojawapo ya familia tajiri za jamii ya kihindi nchini Uganda.

Mmoja wa waliokuwa marafiki wa karibu wa Chande, Hamza Kasongo, ambaye pia ni mwana habari maarufu hapa nchini, alisema haiwezekani kwamba swahiba yake huyo wa zamani anaweza kuwa na utajiri wa namna hiyo.

“ Mimi nimeanza kumfahamu Chande mwaka 1960 wakati akiwa kijana kabisa nami tayari nikiwa mtu mzima. Kwa namna ninavyofahamu, hawezi kuwa na utajiri huo.

“ Labda nikupe mfano. Siku chache kabla hajafariki dunia, nilimpigia simu kupitia namba yake ya simu ya mkononi na aliyeipokea akasema yeye ni fundi simu na alikuwa anaitengeneza.

“ Sasa jiulize, kuna tajiri wa dola milioni 900 ambaye anaweza kupeleka kutengeneza simu yake uswahilini? Basi kama ni kweli ina maana rafiki yangu alikuwa bahili sana. Lakini hapana. Haiwezekani. Hiyo ni ishara ya mtu wa kawaida.

“ Nimekwenda kwa mzee Chande kula chakula mara nyingi tu na nikwambie ukweli kwamba samani za ndani kwake ni zile za muda mrefu. Meza tuliyokuwa tunalia chakula ndiyo ileile iliyokuwepo kwa muda wa miaka 40.

“ Nyumba yake ni ileile na ukiona kuna marekebisho kwa nje ni kwa sababu alikuwa anatembelewa na wageni wengi maarufu na familia yake ikaona ni bora patengenezwe mahali pa kuzungumzia na wageni wake.

“ Hata ofisi yake walimtengenezea shemeji zake wa Madhvani. Baadaye wakaamua kumuwekea hata mahali pa kupumzikia pale ofisini. Hii ni kwa sababu alikuwa anatumia muda mrefu sana kufanya kazi bila kupumzika,” alisema Kasongo.

Kasongo ambaye kwa sasa amestaafu shughuli za utangazaji, alisema Tanzania inapaswa kumuenzi Chande kwa sababu alionyesha uzalendo na utaifa wa aina yake kwa taifa hili.

Alisema ni watu wachache wangeweza kukubali kufanya kazi na serikali ambayo imetaifisha mali zote za familia ya mtu husika, na kuitumikia kwa uaminifu bila kinyongo.

“ Kwa miaka 35, Chande alifanya kazi bila kupumzika kwenye Shirika la Usagishaji na kwingineko alikohitajika bila kinyongo. Ni Watanzania wangapi wanaweza kuwa na moyo wa aina hii. Kwangu, mzee Chande ndiyo alama ya uzalendo,” alisema Kasongo ambaye alikuwa maarufu kwa kipindi chake cha televisheni cha The Hamza Kasongo Hour.

Pamoja na mafanikio yake hayo katika utumishi, katika siku zake za mwisho duniani, Sir Andy alifahamika zaidi kwa uhusiano wake na jamii ya siri ya Freemason na taarifa hii mpya ya Wikipedia imeibua maswali kuhusu utajiri wake huo.

Chande ambaye familia yake ilihamia Tanzania ikitokea India na baadaye Kenya, anatoka katika jamii ya kihindi ambayo japo idadi yake ya watu haifiki asilimia moja ya Watanzania wote, inadaiwa kumiliki asilimia 75 ya uchumi wa nchi.

Kwa mujibu wa ripoti mpya iliyotolewa hivi karibuni na mtafiti-mwana habari, Shamlal Puri, utajiri huo wa sehemu ndogo ya watu wa jamii ya kiasia ni mojawapo ya chanzo cha uhusiano wenye shaka kati yao na wengine.

“ Watu wenye asili ya kiasia ni wachache lakini wanamilia asilimia 75 ya uchumi wa Tanzania. Tabia yao ya kutochanganyika na jamii nyingine na kukaa wenyewe kwenye jamii zao, ni moja ya changamoto kubwa za uhusiano wao na wengine,” ilisema ripoti hiyo iliyopewa jina la Asians in Tanzania: Saboteurs or Saviours (Wahindi nchini Tanzania: Wahujumu Uchumi au Wokozi).

Jayantilal Keshavji Chande alizikwa jijini Dar es Salaam kwa taratibu zote za mazishi kwa mujibu wa imani yake ya Kihindu.

Kwa kawaida, si taarifa zote za mtandao wa Wikipedia ni za kuaminika kwa asilimia 100 –kwa sababu huandikwa na watu binafsi na si taasisi zinazojulikana, mara nyingi huwa na taarifa za kweli.

Kwa mfano, Bakhresa anaaminika kuwa ndiye mtu tajiri zaidi hapa Tanzania; lakini uhalisi wa mali zake haujulikani sana kwa sababu si mtu anayependa kuandikwa kwenye vyombo vya habari kama ilivyo kwa Mo Dewji. Kwenye mtandao wa Wiki, Bakhresa ameelezwa kama mfanyabiashara msiri ambaye taarifa zake hazijulikani wazi.

KUTANA NA Consolata na Maria..Mapacha Walioungana Tumbo..Kila Mmoja Anahisia Zake na Akili Zake Darasani..!!!

$
0
0

MUNGU ana maajabu yake. Mungu ana makusudi yake. Ndivyo unavyoweza kusema ukitafakari uumbaji wa Mungu kwa viumbe vyake wakiwamo binadamu.

Makusudi hayo yanajidhihirisha katika muujiza wa watoto mapacha Consolata na Maria Mwakikuti (26), waliozaliwa wakiwa wameungana kiwiliwili, ambao sasa wana ndoto ya kujiunga chuo kikuu.


Mapacha wengi wanaozaliwa wakiwa wameungana huripotiwa kufariki muda mfupi baada ya kuzaliwa au kufanyiwa upasuaji ili kuwatenganisha japo wapo wengine ambao huishi.

Katika ulimwengu huu wa sayansi na teknolojia, kukua kwa mitandao ya kijamii kuzaliwa kwao kungekuwa gumzo katika vyombo vya habari.

Lakini kwao haikuwa hivyo kutokana na ukweli kwamba teknolojia haikuwa kwa kiwango cha leo lakini pia vyombo ya habari yaani magazeti, televisheni na radio havikunasa tukio la kuzaliwa kwao katika Hospitali ya Misheni ya Ikonda mwaka 1996.

Ulemavu wao ulisababisha wafichwe na kwa wakati huo habari za kuzaliwa kwao hazikuenea sana.

Walianza kujulikana wakati walipojiunga na elimu ya msingi wakati wamisheni walipolazimika kuwahamishia watoto hao kwa mama mlezi wao na kwa wakati huo, walitafutwa walezi wawili.

Wakiwa na miaka mitatu, baba yao Alfred Mwakikuti alifariki dunia na walipofikia darasa la pili mwaka 2002, mama yao pia alifariki dunia hivyo kuwaacha wakiwa yatima.

Mama yao mlezi anasema licha ya kuwa analipwa kiasi kidogo cha mshahara kutoka misheni kwa ajili ya kuwalea, bado maisha yao ni magumu sana na analazimika kulima ili aweze kukidhi mahitaji yao.

Mapacha hao Consolata na Maria wanaoishi Ikonda wilayani Makete, Mkoa wa Njombe, si tu Mungu ameruhusu waendelee kuishi bali pia kuwabariki kuonyesha maajabu yake kwa kuwapa mafanikio na kufanya vizuri kwenye masomo yao.


Mapacha hao walipata elimu yao ya msingi kijijini hapo na kufanikiwa kufaulu vizuri kabla ya mwaka 2011 kuchukuliwa kwa malezi na wamisionari na kupelekwa wilayani Kilolo kwa ajili ya kuwalea zaidi. 

Mapacha hao kwa sasa wamehitimu  kidato cha  sita mwaka huu katika Shule ya Sekondari ya Udzungwa na wanalelewa na kituo cha Nyota ya Asubuhi Kidabaga, wilayani Kilolo Mkoa wa  Iringa.

Wanasema ndoto yao kubwa  pindi watakapomaliza chuo ni kuwa  wataalamu wa kompyuta.

Awali, baada ya kumaliza elimu ya msingi walijiunga na Shule ya Sekondari Nyota ya Asubuhi  baada ya walezi wao kukataa wasijiunge na shule ya sekondari ya Jangwani walikokuwa wamepangiwa baada ya matokeo yao kutoka.


“Siku tuliposikia tumefaulu hatukulala kwa furaha, tuliruka na kumshukuru Mungu kwani hatukuamini kama tungeweza kufaulu kutokana na kusomea katika mazingira magumu.

“Hatukuwa na kiti cha kukalia darasani, siku zote tulikalia kibaiskeli ambacho hakitutoshi na kadri siku zilivyokuwa zikisogea ndivyo kilivyokuwa kikituumiza kwa kuwa ni kidogo na sisi tunakua,” anasema Consolata.

Mabinti hao wanasema wakiwa wanasoma, kila siku asubuhi rafiki zao waliwapitia ili kuwapa msaada wa kusukuma baiskeli yao hadi shuleni. Muda wa mapumziko waliwarejesha nyumbani kwao kwa ajili ya kujisaidia.

Wanasema utaratibu huo ulidumu muda wote wakiwa shuleni ambapo hawasiti kuwashukuru wenzao kwa upendo huo.

Mapacha hao walipata alama zinazolingana kwenye mtihani wao wao mwisho, kila mmoja akipata alama 151, lakini kinachothibitisha kuwa hawakutazamiana wala kusaidiana kwenye mtihani ni tofauti ya alama walizopata kwenye baadhi ya masomo.

Katika somo la maarifa ya jamii, Consolata alipata alama 29 na Maria alipata alama 25, wakati kwenye somo la sayansi Maria amemzidi Consolata kwa kupata alama 31 dhidi ya 29 na hali ni kama hiyo kwenye somo la Kiingereza ambalo Maria amepata alama 36 na kumzidi Consolata aliyepata alama 34.


Consolata na Maria ambao kwa  sasa wamehitimu kidacho cha sita wana shauku ndoto ya kutimiza ndoto zao kielimu kwa kuendelea na masomo ya  chuo kikuu.

Wanasema hawajawahi kufeli masomo na wamekuwa wakipishana  iwapo mmoja atashika namba moja basi mwingine hushika atakuwa wa pili  ambapo pia wamekuwa wakishindana hivyo  hadi wanahitimu kidato cha sita.


Japo wameungana, lakini kila mmoja ana hisia zake. Juhudi zao zinazolingana katika masomo na tabia zao hazikuwafanya watu wa aina moja licha ya kuungana tumbo Kila mmoja ana hisia zake na ana vitu anavyopendelea mfano  Maria ni mcheshi zaidi ya Consolata hachagui chakula lakini Maria akila samaki anasumbuliwa na tumbo.

Lakini kama mmoja akijisikia kwenda kulala, basi mwenzake pia atalazimika kulala kwa kuwa wameungana tumboni. Maumbile yao yanawalazimu mapacha hawa wapendane na kusaidiana.


“Maria akiumwa inanibidi niwe mpole, nitulie kwa sababu nikimfanyia fujo nitamuumiza, akitaka kulala tunaenda wote na kama litamuuma tumbo la kuharisha basi tutaenda wote uani, hatujawahi kugombana, tunapendana sana,” anasema Consolata.

Kwa upande wake Maria anasema maisha yao ya shule yalikuwa mazuri kutokana na ukweli kwamba, watu wengi waliwapenda hivyo hawakujiona tofauti.


“Tunahitaji shule ambayo itaweza kutusaidia, kama kuna uwezekano wa kupewa nyumba tutashukuru kwani hali yetu ilivyo ni tofauti na wenzetu,” ansema.

Walimu wao wanashauri, ikiwa Serikali itaamua kuwasomesha, basi ihakikishe kuwa mama yao mlezi anakuwa nao karibu baada ya kuwawezesha kufikia hapo walipo sasa.


Katika maisha yao ya kusoma, kila mmoja alikuwa na madaftari yake na wakati wa kufanya mazoezi au kuandika kazi wanazopewa, mmoja huanza kuandika, akimaliza na mwingine huandika.


“Wala hatupati shida tumezoea, kila mmoja anafanya kazi yake, mimi naandika kwa mkono wa kushoto na Maria anaandika kwa mkono wa kulia,” anasema Consolata, ambaye anaonekana kuwa mchangamfu zaidi.

Kwa upande wake Mkuu wa Wilaya ya Kilolo,  Asia Abdalah na Mbunge wa Viti Maalum Mkoa wa Iringa, Rita Kabati ni miongoni wa viongozi  waliopata kuwatembelea kwa  nyakati tofauti  watoto  hao.

Mkuu huyo wa Wilaya anasema serikali inawathamini na inaendelea kuwapenda hivyo kama mkuu wa wilaya ataendelea kufika kuwasalimia na kuwasaidia. 

“Nimefurahi sana kuwaona mkiwa na furaha kubwa na mnafanya vema katika msomo yenu kwa kufanya vizuri katika masomo yenu ya kidato cha nne na sasa kidato cha sita, hakika mnaonyesha matumaini makubwa ya kwenda chuo kikuu kutokana na jitihada zenu darasani kwa kuwa mnafanya vizuri katika masomo yenu ya kidato cha sita sasa,” anasema Asia. 

Hata hivyo, mapacha hao wanaomba serikali kuendelea kufanya kazi nzuri kwa wananchi wake kwa kasi hiyo laikini pia wanapenda kuona serikali ikiendelea kuboresha elimu mashuleni kwa kutatua changamoto ya vitabu vya sayansi ili kuzalisha wasomi zaidi wa masomo ya Sayansi nchini.

DONALD Trump na Marekani yake Wasalimu Amri Kwa Korea Kaskazini..Wadai Wako Tayari Kwa Mazungumzo

$
0
0
Marekani iko tayari kwa mazungumzo na Korea Kaskazini yenye lengo la kuondoa zana za nuklia kutoka eneo hilo, kwa mjibu wa waziri wa mashauri ya nchi za kigeni wa Marekani Rex Tillerson.
Lakini amesema kuwa Marekani itatumia nguvu za kijeshi ikiwa itahitajika.

Waziri wa mashauri ya nchi za kigeni wa China, mshirika mkubwa wa Korea Kaskazini, anasema makubaliano ya amani ndio njia pekee.

Bwana Tillerson aliliambia baraza la ulinza la Umoja wa Mataifa kuwa tisho la Korea Kaskazini la kushambulia majirani zake na zana za nuklia.

Maelfu ya wanajeshi wa Marekani wako nchi majirani wa Korea Kaskazini ikiwemo Korea Kusini na Japan.

Tillerson amezitaka nchi wachama wa Umoja wa Mataifa kuiwekea Korea Kaskazini vikwazo na kupunguza uhusiano wao wa kidiplomasia na nchi hiyo.

"Kwa miaka kadha Korea Kaskazini imekuwa ikiendesha kwa nguvu mpango huu hatari."
"Ni wakati wetu kuchukua hatua na kudhibiti hali," Tisho la Korea Kaskazini la kufanya shambulizi la nuklia dhidi ya Korea Kusini au Japan ni la kuwezekana, na ni muda tu kabla ya Korea Kaskazini kufanikiwa kupata uwezo wa kushambulia Marekani." alisema Tillerson.

UREMBO: Pendezesha Mwili Wako Kwa Kutumia Bidhaa Toka Kwa Kessy Products..Ngarisha Ngozi na Kuongesha Shape

$
0
0
PENDEZA NA KESSY PTODUCT:-MSIMU MPYA% WA 2017_OFFA YA BIDHA AINA ZOTE KWA UBORA MZURI

PATA DAWA NA MAFUTA YA ASILI ZISIZO NA MADHARA WALA KEMIKALI, NA  MATOKEO NI KWAHARAKA BAADA YA WEEK (1)ADI( 3-4) 🍎🍌🍉🍑🍍🍓🍒🍏🍇

1) KUTOA MVI SUGU PIA ZA KUZALIWA NAZO _80,000/
2) KUREFUSH NYWELE  KUZIJAZA NA KUZUIAKUKATIKA _80,000/
3) TENGENEZA SHEPU YAKO FIGA UMBO (8) NA KUJAZA HIPC NA KALIO @ KUPAK _70,000/
@ KUNYWA AU VIDONGE _130,000/  4) KUPUNGUZA NYAMA ZA MIKONO TUMBONI ZILIZOTEPWETA _80,000/
5) PUNGUZA KITAMBI KWA HARAKA KWA DAW HIZI ZA KUNYWA
@) KUNYWAA _10,0000/
@) VIDONGE  _10,0000/
6) PUNGUZA MWILI MZIMA KUANZIA KGM 150 ADI 80 KIASI UNACHOTAK WEWE KWA DAW HIZI
@) DAW YAKUNYWA YA KUCHANGANYA NA MAJI AU JUYC _130,000/
@) VIDONGE VYA HARAKA _130,000/
7) PUNGUZA MAZIWA NA YASIMAME KWA MUDA WA WEEK MOJA _70,000/
8) ONGEZA MAZIWA NA SAIZ UNAYOTAKA WEWE _70,000/
9) ONGEZA MWILI MZIMA NA KUKUPA HAMU YAKULA KWA RIKA LOLOYE _80,000/
10) TOA MICHIRIZI SUGU PIA NA ILE YAKUJIFUNGUA MWILI MZIMA _70,000/
11) TOA MAKOVU, CHUNUSI, WEUSI KATIKATI YA MAPAJA _60,000/
12) TOA NGIRI YA AINA ZOTE _70,000/
13) KUWA MWEUP  NA SOFTI MWILI MZIMA NA KUTOA WEUS MACHON NA VIMISHIPA VIDOGO VIDOGO @ MAFUTA YA KUPAKA _80,000/(@) VIDONGE (WHITE SOLUTION) _120,000/
14) ONDOA  NDEVU NA VINYWELEO MWILINI _80,000/
15/ ONGEZA NGUVU ZA KIUME NA KUIMARISHA MISHIPA ILIYO LEGEA KWA DAW HIZ
@) JEL KUPAKA (MEN GEL) _70,000/
@) VIDONGE (MAXMAN) _80,000/
16) ONGEZA MAUMBIL YA KIUME SAIZI UNAYOITAKA WEWE KWA:
@) (HANDSOME UP) MASHINE _170,000/
@) JELI YAKUPAKA INABORESHA ANZIA NCHI (4 ADI 6 )_100,000/ PIA NA VIDNGE VYAKE VIPO
17) RUDISHA HAMU YA TENDO LA NDOA KWA WALIOPOTEZA KUTOKANA NA NGIRI, KISUKARI NA MAGONJWA MENGINE KWA  _80,000/
18) RUDISHA USICHAN(BIKRA)Na KUTO UCHAFU SEHEMU ZA SIRI _80,000/
19) FANYA USO WAKO KUWA MKAVU NAKUTOA VIJIPELE ILIYOSABABISHWA NA MAFUTS MAKALI _80,000/
20) ONDOA  SUGU KWENYE VIDOLE, MAGOTI, NA SEHEMU ZOTE ZILIZOARIBIWA NA LOSHEN _60,000 (21) TENGENEZ MGUU WAKO NA KUTOA KIGIMBI NA KUWA MZURI NAWAKUPENDEZA _70,000/ 22) MIKANDA YA KUPUNGUZA TUMBO PIA HIPO @ MONALISS _80,000/ @( MICROO)MASHINE WA UMEME _20,0000 @ MKANDA WENYE DAW (NYONGA STAILL) _170,000/

   PIA UDUMA NYINGINE ZIPO

TUNAPATIKAN K/ KOO NA SINZA
 MAPAMBAN, KWA MIKOAN T UTATUMA KWA MABAS YOTE, NA  KWA ZANZBR UNGUJA PIA TUNATUMA  KWA BOT ZOTE

 KWA MAWASILIANO PIGA
                                      
(+255) 0719955528
0756259180
0785371237

@dr_kessy_product


Delivery KWA DAR E SALAAM INAKUFIKIA POPOTE ULIPO, HUDUMA HIZI ZINAPATIKA DUNIAN KOTE  POPOTE ULIPO

RAY Kigosi Awatolea Povu Watanzania, Kisa Unafiki wao

$
0
0
Kupitia ukurasa wake wa Instagram Ray ametoa ujumbe ambao unalenga kutoa uelewa kwa mashabiki hasa wa filamu na muziki nchini ambao wamekuwa wakiponda juhudi za mastaa wa Kitanzania Huku akitolea mfano wa Kanumba na Diamond platnumz

Ray Kigosi ameandika…
1. Kanumba alipoanza kuona mwanga wa kufanikiwa bila kujali juhudi zake kuna watu walimuita Freemanson, Mara anatumia nguvu za Giza. that is to say films zake hazikuwa nzuri but ziliuza sababu ya nguvu za Freemanson na nguvu za giza!!

2. Kanumba alipoenda Big Brother alipondwa Sana na kuitwa bogus kwa Madai hajui kiingereza, Ni watanzania Hawa Hawa walibebea bango hili huku baadhi ya waandishi uchwara wakieneza ujinga huu bila kujali juhudi zake. But Leo wanamsifia hakuna Kama Kanumba!

3. Kuna wakati Kanumba alionekana wazi kuvunjwa moyo na kukatishwa tamaa kwa
kuonekana juhudi zake si kitu. But Alisema maneno machache Kuwa mtanikumbuka kama si Leo basi Ni Kesho.And alichosema kimetimia, wale wale waliokuwa wakisema Ni Freemanson bila hata kujali juhudi zake kwenye game Leo ndio kwa unafiki wanasema hakuna Kama Kanumba !HAO NDIO BINADAMU NA TABIA ZAO Je, Kanumba kaondoka na Bongo Movie yake ya Freemanson ? Kama wengine mnavyodhani industry Ni Mtu sio system !

4. Diamond Platnumz nae baada ya kuona Njia ya mafanikio kuna watanzania, wasanii wenzake na hata baadhi ya wanahabari wanasema Ni Freemanson, wengine
wanaonyesha chuki ya wazi kwake. Wanasema Hana muziki mzuri, Mara Ni Kiki tu ambazo hata Kanumba alikuwa akiripotiwa magazetini na kina Wema.Hawaoni juhudi na thamani ya Diamond sasa ! Hatuombi baya limpate Diamond ili kudhibitisha tabia na unafiki wa binadamu. But HAO NDIO BINADAMU siku zote hawana Jema unafiki ni sehemu ya Maisha.

5. Kila siku Ni kuzua hii na kile, Mara ooh Diamond Ni mchawi, kasema mleteni huyo mganga wangu mkashindwa kumleta, akajitokeza mganga fake sijui na Madai juu Kuwa Diamond atashuka kimuziki kwa sababu ananipuuza niliyempa nyota, Diamond akasema sawa namtegemea Mungu. Miaka 4 sasa tangu yaliyoitwa ya mganga Diamond hashuki ndio anazidi kupaa. HAO NDIO BINADAMU kusema lolote Ni haki Yao.

Kazi za Kanumba sasa zinapewa thamani na ubora uliovuka mipaka na viwango ambao hakupewa kipindi yupo hai ! HAO NDIOBINADAMU na tabia zao. Ni tabia tu ya baadhi ya watu kubebea mabango mabaya ya Mtu au uzushi na kuacha mazuri yake then baadaye wakishikwa Uchawi wanageuza walichoamini Ni nyeusi kiwe nye.

Nay Anusurika Kutekwa

$
0
0
WAKATI hofu ya kutekwa ikiwa juu, msanii wa Hip Hop Bongo, Emmanuel Elibariki ‘Nay wa Mitego’ amenusurika kutekwa na watu wasiojulikana, Risasi Jumamosi lina habari kamili. Kwa mujibu wa chanzo makini, Nay alipatwa na maswaibu hayo mwishoni mwa wiki iliyopita wakati alipokuwa anatoka kwenye shoo aliyoifanyia Kigamboni jijini Dar.

“Alipiga shoo katika Ukumbi wa G5, akamaliza salama tu, mida kama ya saa 10 alfajiri hivi wakawa wameshamaliza. Wakaanza safari ya kurudi nyumbani kwake Kimara kupitia barabara ya kuzungukia Kibada.

“Kwenye gari Nay alikuwa na jamaa mmoja hivi ambaye ndiye msaidizi wake katika mambo ya mitandao. Nay ndiye aliyekuwa akiendesha mwenyewe.

“Sasa wakiwa hawajafika mbali kutoka ukumbini, walishangaa kuona Noah moja ikionekana kuwafuatilia. Nay alipoona hivyo ikabidi aongeze mwendo,” kilisema chanzo hicho. Kikizidi kumwaga ubuyu huo, chanzo hicho kiliweka wazi kuwa, kuna wakati Nay aliwasha taa kama anataka kukata kushoto, akaona gari ile nayo inawasha taa kama inataka kukata.

Alipoona hivyo, yeye hakukata. Akanyoosha. “Nay alitaka kujiridhisha. Ikabidi aoneshe kama anataka kukata kushoto.

Alipoona ile gari nayo imekata, yeye akanyoosha moja kwa moja kufuata ile barabara ya Kibada. Wakashika barabara kuitafuta ile njia ya Mbagala.

“Wale walipoona gari ya kina Nay haikati imenyoosha, nao wakanyoosha na kuanza kuwafukuzia na hapo ndipo Nay alipojua wale watu waliokuwa kwenye ile Noah hawakuwa wa kawaida, akakanyaga mafuta ya kutosha na bahati nzuri kukatokea gari lingine ambalo liliingia katikati yao, wale jamaa wakapunguza mwendo,” kilisema chanzo hicho na kuongeza:

“Alienda kutoa taarifa Sentro lakini akaambiwa arudi kesho yake (Jumatatu iliyopita) hivyo akarudi zake kupumzika nyumbani.” Baada ya kupata ubuyu huo, Risasi Jumamosi lilizungumza na Nay na kumuuliza kuhusu tukio hilo ambapo alikiri kutokea na kwamba ndiyo anajiandaa kurudi tena polisi kutoa taarifa.

“Ndiyo hivyo bwana mimi kiukweli sasa hivi naishi kwa machale machale hata sielewi wale jamaa walikuwa na lengo gani hasa ila kwa kuwa nakwenda polisi, tuwaachie wao,” alisema Nay.

Hivi karibuni, msanii wa Hip Hop, Ibrahim Mussa ‘R.O.M.A’ na wasanii wenzake watatu walitekwa, wakateswa na watu wasiojulikana walipokuwa Studio za Tongwe Records Masaki jijini Dar.

Baada ya siku tatu, wasanii hao waliachiwa wakiwa katika hali mbaya ambapo jeshi la polisi likaahidi kufuatilia kwa undani sakata hilo ili kuwabaini wahusika.

KIMENUKAA..Rais Magufuli Ayanyooshea Kidole Makampuni ya Simu..Adai Dawa Yao Iko Jikoni Inachemka..!!!

$
0
0

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt John Pombe Magufuli ametahadharisha kuwa, wapo mbioni kuhakikisha mapato ya serikali yanadhibitiwa zaidi ili taifa liweze kujitegemea kikamilifu, huku akionya makampuni ya simu nchini.

Rais Magufuli ameyasema hayo Ijumaa hii, mjini Dodoma wakati akikabidhiwa taarifa ya vyeti feki. Rais ameyaonya makampuni hayo, akisema, dawa ya makampuni hayo bado inatengenezwa.

“Bado kuna maeneo mengi ambayo tunaibiwa fedha. Kwenye haya makampuni ya simu haya, yanafanya transactions nyingi lakini hela haziingii serikalini, dawa yao tunaitengeneza baada ya muda mfupi kidogo itakamilika,” alisema Rais Magufuli huku akishangiliwa.

MSAADA ..Nateswa na Dawa za Kuongeza Uume Nilizopakwa na Babu Yangu!!

$
0
0

Habari za mida tena, kuna story yangu nataka niwashirikishe halafu mnipatie mawazo yenu.

Mimi ni kijana toka pande za kaskazini mwa Tanzania, nikiwa natokea katika kabila la pili linaloongoza kwa umaarufu miongoni mwa makabila yanayopatikana mkoani humo.

Sasa basi kipindi kama cha miongo miwili iliyopita nilibahatika kwenda kwenye mafunzo ya jadi maarufu kama jando, kilichokua kinafanyika kule ni pamoja na mafunzo ya kuihudumia familia yako pamoja na mbinu za kumridhisha mwanamke kimapenzi.

Baada ya wiki sita za mafunzo mbalimbali tulitoka na kufanyiwa sherehe Kubwa, siku ya sherehe Babu alinifuata na kuniambia anataka anifanye mwanaume kamili, mimi sikumuelewa.

Babu aliniambia niende kwake jioni. Nilipoenda jioni hiyo aliniingiza chumbani kwake na kuniambia nitoe uume wangu, baada ya kuutoa uume wangu alinichanja chale na kunipaka mafuta ya uume wa punda akachanganya na dawa nyingine, huku akichanganya na maneno yake anayoyajua yeye mwenyewe.

Baada ya wiki uume ulikuwa mkubwa mpaka leo unanitesa kwani umekuwa mkubwa na mrefu, halafu cha ajabu hata kama ni bao la kwanza ninachelewa mpaka nakua kero kwa mwenzangu, jamani nisaidieni kwani nakosa raha kabisa, Babu amefariki tangu 1998, mpaka sasa nishakimbiwa na wapenzi kadhaa kutokana na maungo yangu kuwa makubwa!!

Ahsanteni wote mtakaochangia matusi na comments za ajabu ajabu sitaki.

Tembelea Tovuti Pendwa ya ASILI ZETU inayohusiana na Masuala ya Tiba Asilia Kama Kusafisha Nyota na Kumvuta Mpenzi

$
0
0
Tembelea Blogu ya Asili zetu upate kufahamu mambo mbalimbali kuhusiana na tiba asilia, utabiri wa nyota, aina za majini, viumbe wabaya wanaowasumbua wanadamu, ilimu ya nyota na masuala ya mahusiano.

Pia kwa wale wanaosumbuliwa na ndoto mbaya, wanaohitaji kusafisha nyota, mvuto wa biashara, kupandishwa cheo, kufata kesi mahakamani, kumvuta umpendae, dawa za nguvu za kiume na waliodhulumiwa mali zao.

Tembelea Asilizetu.wordpress.com

Kama Umeshawahi Kutoa Mimba Fanya Haya Mambo Matatu

$
0
0

Makala iliyopita niliongelea madhara sita ya kutoa mimba, kutokana na jamii yetu kukumbwa sana na janga hili la utoaji wa mimba hasa kwa mabinti wadogo ambao wengi wao wapo vyuoni na mashuleni.

Kutokana na maswali mengi niliyoulizwa nini cha kufanya kwa ambao tayari wameshatoa mimba nimeamua niandike makala hii. Mambo yenyewe ni haya…

Nenda hospitali uonane na daktari; ukitoa mimba kuna madhara mengi yanayofuatia ikiwemo ugumba, na kuharibika viungo vya uzazi.. nenda ukapige picha ya ultrasound kuangalia hali ya viungo vya uzazi, na kama vinaumwa vianze kutibiwa mapema iwezekanavyo kabla mambo hayajaharibika. Pia pima magonjwa mengine ya kuambukizwa ikiwemo ukimwi, kaswende na gono kwani ni magonjwa yanayo ambatana na ngono zembe. usiogope hakuna daktari wa kukupeleka polisi kwa kutoa mimba..

Obama na mtaalamu wa ushauri: kama una mawazo mengi kwanini umetoa mimba na unajutia maamuzi yako au moyoni unahisi umefanya kosa kubwa kwa binadamu au mungu wako nenda unana na mshauri na atakusaidia kurudi katika hali yako ya kawaida.


Chagua njia ya uzazi wa mpango: kuna watu wameshatoa mimba mpaka tano sasa hivi, mimi naona huo ni uzembe kwani kuna njia nyingi sana za kuzuia ujauzito. Kama huwezi kondomu njia ya kijiti ni nzuri kuliko zote kwani siku ukitaka mtoto unakitoa kijiti na kunasa mimba haraka. njia ya kalenda ni nzuri pia ila wengi hawaiwezi na inataka umakini sana hivyo achana nayo..Acha kusikiliza kelele za watu eti njia hizo zina madhara kwani hizo ni imani potofu na ukipuuzia utaendelea kutoa mimba zaidi kitu ambacho ni hatari kiafya. tumia virutubisho vya uzazi; mara nyingi kutoa mimba huharibu mfumo wa homoni za uzazi wa wanawake na  maumbile ya uzazi.hali hii ni hatari na ndio hufanya wanawake wengi kushindwa kubeba mimba siku za usoni. tumia virutubisho vya multmaca ambavyo vimesaidia sana kurudisha hali ya homoni katika kawaida yake na kusaidia kubeba mimba kwa wanaozitafuta. 

Simba Yaingia Fainali, Yaiadhibu Azam 1 - 0 Kombe la Shirikisho

$
0
0

SIMBA SC imefanikiwa kwenda Fainali ya Kombe la Shirikisho la Soka Tanzania (TFF), linalojulikana kama Azam Sports federation Cup baada ya ushindi wa 1-0 dhidi ya Azam FC jioni ya leo Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam. 

Sifa zimuendee mfungaji wa bao hilo pekee dakika ya 48, Mohammed ‘Mo’ Ibrahim ambaye hata hivyo hakumaliza mchezo baada ya kutolewa kwa kadi nyekundu baadaye. 

Kwa ushindi huo, Simba itasubiri kukutana na mshindi kati ya wenyeji Mbao FC na Yanga SC zinazomenyaa kesho Uwanja wa CCM Kirumba mjini Mwanza. 

Katika mchezo huo uliochezeshwa na refa Mathew Akrama wa Mwanza, Azam FC ilipata pigo dakika ya 15 baada ya kiungo wake mchezeshaji, Salum Abunakar ‘Sure Boy’ kutolewa kwa kadi nyekundu ya moja kwa moja baada ya kumchezea rafu mshambuliaji wa Simba, Ibrahim Hajib.

Ilionekana kama wachezaji hao wamegongana kwa kawaida mno, lakini kwa namna Hajib alivyojirusha huku akipiga yowe la kuugulia maumivu Akrama aliingia kwenye mtego wa kumtoa kwa kadi nyekundu Sure Boy. 

Tukio hilo lilileta kizaazaa kidogo uwanjani baada ya wachezaji wa Azam kumfuata refa na kuanza kumlalamikia kwa maamuzi yake. Walinzi wa Uwanja wa Taifa walimfuata Sure Boy na kujaribu kumtoa kwa nguvu, jambo ambalo liliwafanya wavutane na Meneja wa Azam, Philipo Alando. 

Mchezo uliendelea baada ya tukio hilo, huku timu zikiendelea kushambuliana kwa zamu na kabla ya Akrama kupuliza kipyenga cha kumaliza ngwe ya kwanza kukiwa hakuna bao. 

Kipindi cha pili, Simba walikianza vizuri na kufanikiwa kupata bao baada ya dakika tatu tu, kiungo Mohammed ‘Mo’ Ibrahim akimtungua vizuri kipa Aishi Salum Manula kwa shuti la mguu wa kulia kufuatia ya krosi ya mshambuliaji Mrundi, Laudit Mavugo. 

Simba wakaanza kucheza kwa tahadhari kwa kujihami zaidi baada ya bao hilo, huku Azam FC wakionekana kusaka bao la kusawazisha kwa nguvu zao zote. 

Mo Ibrahim akaonyeshwa kadi ya pili ya njano na kutolewa kwa kadi nyekundu dakika ya 77 baada ya kumchezea rafu beki wa Azam FC, Shomary Kapombe. 

Beki Mkongo, Janvier Besala Bokungu akaizuia Azam FC kusawazisha baada ya kuokoa mpira uliopigwa kwa kichwa na Nahodha wa timu hiyo, John Raphael Bocco uliokuwa unaelekea nyavuni dakika ya 84. 

Kikosi cha Simba kilikuwa; Daniel Agyei, Janvier Bokungu, Mohammed Hussein ‘Tshabalala’, Juuko Murshid, James Kotei/Said Ndemla dk88, Jonas Mkude, Shizza Kichuya, Muzamil Yassin, Laudit Mavugo/Mwinyi Kazimoto dk86, Ibrahim Hajib na Mohammed Ibrahim. 

Azam FC; Aishi Manula, Shomary Kapombe, Gardiel Michael, Aggrey Morris, Daniel Amoah, Himid Mao, Stephan Kingue/Joseph Mahundi dk58, Shaaban Iddi/Frank Domayo dk46, Salum Abubakar ‘Sure Boy’ na Ramadhani Singano ‘Messi’/Mudathir Yahya dk82.

Chidi Benz Arudi Uraiani...Amfungikia Kalapina

$
0
0

Msanii wa muziki wa hip hop, Chidi Benz amedai amejifunza vitu vingi kwa kipindi cha miezi mitatu alichokaa rehab mkoani Tanga na Iringa kwa ajili ya kusaidiwa kuacha matumizi ya dawa za kulevya. 

Akiongea katika kipindi cha Clouds E cha Clouds TV, Chid Benz amedai kukaa rehab kwa miezi mitatu bila tatizo ni mafanikio mapya katika maisha yake. 

“Nimejifunza vitu na ninaendelea kujifunza vitu,” alisema Chidi. “Nimekaa muda mrefu zaidi maana sijawahi kukaa rehab miezi mitatu na ndio maana unaona nimetulia mpaka sasa hivi. Nina miezi miwili toka nimetoka niko poa niko freshi,” 

Katika hatua nyingine rapa huyo amemtaka mwanaharakati wa kupambana na dawa za kulevya, Kalapina, kujifunza mbinu mpya ili aweze kuwasaidia vijana wa aina mbalimbali ambao wanakumbwa na tatizo hilo.

HARUFU ya Asili ya Mwanamke ni Very Romantic Kuliko ya Kujipulizia Pafyumu..!!!!

$
0
0

Kwa kweli wanawake hii kitu ngoja niwaambie ,,,,zile harufu zenu ambazo huwa mnatoa kabla hamjajipulizia pafyumu huwa zinaleta hamasa kubwa sana ya mapenzi kuliko hayo mapafyumu ya gharama mnayojipulizia

Kwa kifupi nikikaa na demu ambaye hajajipulizia pafyumu kile kiharufu chake kinachotoka huwa kinanivutia sana yani kuliko nikikaa na demu anayenukia pafyumu.

Hii siri nimewamegea usiipuuze izingatie sana.

SMS Za Nguvu Za Kutumia Baada Ya Kupewa Namba Na Mwanamke

$
0
0

Tangu tuweke chapisho ambalo linagusia swala la mbinu tofauti tofauti za kuomba namba ya simu ya mwanamke, tumekabiliwa na janga jingine ambalo baadhi wa readers humu ndani wamekuwa wakituandama katika inbox na maswali ya kurudia rudia ya 'Jinsi ya kuufunga mchezo baada ya kupewa namba na mwanamke'

Tumekuwa tukiwajibu baadhi ya readers wetu na tumeamua kuweka wazi mbinu rahisi ambayo itamfunga mwanamke ili uweze kukutana naye mara ya pili, ya tatu, ya nne...

Na kufanikisha hivi, tumekuja na mbinu ambayo kwa kawaida imekuwa ikitumiwa na guru wengi ambao wamebobea katika sekta ya kudeti wanawake.

Zama nami...

Ok. Umefuata mbinu ya moja kwa moja ukamfanya mwanamke akakupatia namba yake ya simu.

Uliongea naye na uliona anavutia kupindukia...

Ulikuwa ama alikuwa na haraka hivyo hukupata nafasi ya kuongea naye kwa muda mrefu bali ulichukua namba yake ya simu.

Sahizi umeachwa hujui ufanye nini!

Je umpigie simu ama umtumie ujumbe mfupi?

Utasema ama utamwambia nini baada ya kuwasiliana naye?

Je, utamuuliza kama atoke deti na wewe au la?

Ok bila kupanic, mbinu ya kufanikisha maswali haya ni rahisi...

Mwanzo ni rahisi kama kusema A...B...C...

SMS za nguvu za kumtumia mwanamke siku ya leo baada ya kukupatia namba

1. Funga deti na yeye 
Jambo la kwanza kabisa ambalo unafaa kufanya wakati ambapo atakuachia namba yake ya simu ni uhakikishe ya kuwa unamwomba atoke deti na wewe. Na meseji unayohitajika kumtumia ni kama ifuatayo...

"Hi. nlikuwa nahakikisha kama umefika nyumbani salama. Nimefurahia sana kukutana na wewe. Ningependa tukutane wakati mwingine. Jumamosi nitakuwa free. Nije nikuchukue wakati gani?"

SMS hii huwa inafanya kazi kwa mambo mawili: Jambo na kwanza ni kuwa inamfanya ajihisi yuko salama, yani kujiona ya kuwa kuna mtu anadhamini maslahi yake, jambo ambalo wanawake wengi wanatamani kuwa nalo.

Pili ni kuwa unamlazimisha kujiazima. Aidha akubali kutoka deti na wewe ama kukukataa papo hapo. Kivyovyote vile utaujua msimamo wake.

Kama atakubaliana na wewe na kujibu sms yako,  turuke katika hatua ya pili.

2. Mfunge kwa kumpigia simu
Kabla kutoka deti na yeye lazima ufahamu mambo angalau kidogo kumhusu. Kujua mambo kadhaa kumhusu kutakupa wewe nafasi ya rahisi kuifanya deti yako na yeye kuvutia, bila kuboesha. Pia kumpigia simu kunajenga ile hisia ya mapenzi ambayo hujitokeza katika mazungumzo ya simu.

Pia unataka kumjulisha ya kuwa uko interested na yeye, lakini usiivuke mipaka yako hapa. Meseji ya pili inafaa ienda hivi:

"Poa. Natumai kukutana na wewe hio siku. Nitakupigia simu wakati flani kukujulisha vile tutavyoendelea. Kesho inaweza kuwa siku nzuri kwako?"

 Kutumia meseji hii ina nguvu zifuatazo:  Unaufunga mchezo wako wa simu. Unamwambia ya kuwa deti yenu itafanikiwa. Pia unamwambia ya kuwa unapanga sehemu ambayo unapania kukutana kwa deti. Kiukweli ni kuwa utajua vitu ambayo anapenda wakati ambapo utampigia simu, na hii itakuwa kama msingi wenu wa kwanza katika deti.

Halafu sasa itambidi akujibu. Na hapa ndipo maongezi yenu yataanza kupanda kwa kasi. Haswa kama amependezwa na wewe.

Mwanzo meseji ambazo atakuwa akituma baada ya hizi mbili kutaashiria kwako kuweza kutoka deti na yeye mara kwa mara...na hata kufanya kufikia level ya texts za kimapenzi.

Viewing all 104712 articles
Browse latest View live




Latest Images