Quantcast
Channel: UDAKU SPECIAL
Viewing all 104775 articles
Browse latest View live

HIZI Hapa Sifa za Mwanamke Mnene Kwenye Malovidavi

$
0
0
Mwanamke mnene ni mtamu sana, ana joto kali sana ndani ya uke, ana nyamanyama ambazo hazimuumizi mwanaume wakati wa kutoa mastyle.

mwanamke mnene akikaa style ya chuma mboga basi lile sponji la nyuma loooote lasababisha maangamizi ya muda mfupi kwa abdalah kichwa wazi.

mwanamke mnene ana degree ya kwenda miondoko ya r ...N b kitandani ambayo huwa so romantic na haitoi jasho.

mwanamke mnene akivua nguo akalala kifudifudi basi mkaka hata kama anaangalia mpira lzm atadata.

mwanamke mnene ana sifa ya kukojoa bila kumwaga maji mengi. happy wanene day vimbaumbau kama nawaona" sifa za mwanamke mnene!!!!


MOJA ya Vigezo vya Kupata Kazi Usalama wa Taifa

$
0
0
Taasisi za Usalama wa taifa ni moja ya taasisi nyeti kwenye taifa lolote duniani ambapo tukiwa nje huwa tunasikia au kuambiwa kwamba wanaofanya kazi humo ni watu wenye mafunzo maalum na huwa hawajionyeshi au kujitangaza kwa watu kuhusu wanachofanya.

Leo millardayo.com na AyoTV zinae Evarist Chahali, Mtanzania anaeishi Ulaya lakini pia anasema aliwahi kufanya kazi kwenye Idara ya usalama wa taifa zamani lakini kwa sasa amestaafu.

Chahali ameandika kitabu kiitwacho SHUSHUSHU ambapo anasema ‘moja ya mahitaji makubwa ya mtu kupata kazi hii ni kutakiwa kuwa na akili ya ziada na sio akili ya kawaida tuliyozoea ambapo upatikanaji wa watu wa aina hii hupitia hatua mbalimbali’

‘Naomba ieleweke kuwa kwenye kitabu hiki sijazungumzia Idara ya usalama wa Taifa Tanzania bali nimezungumzia Idara za usalama wa taifa kote duniani kwani taaluma hii inafanana kama ilivyo Udaktari na taaluma nyingine‘

‘Kitabu kinazungumzia changamoto pia, kimsingi huko nyuma kwenye miaka ya 80 na 90 mwanzoni changamoto kubwa kwenye idara za usalama wa taifa ilikua wenyewe kwa wenyewe, yani idara ya nchi moja dhidi ya idara ya nchi nyingine… kulikua kama kuna kanuni flani zinatakiwa kuheshimiwa japo sio rasmi‘

‘Tishio kubwa kwa sasa kwa Idara za Usalama wa taifa duniani ni ugaidi wa kimataifa unaochangiwa na mwamko wa kidini wa makundi kama AL SHABAAB, ISIS, AL QAEDA na wengine…. hawa pia wanatumia Ushushushu lakini hawafuati kanuni‘

‘Nina malengo makubwa mawili yaliyofanya niandike hiki kitabu, kwanza ni kuondoa dhana potofu kuhusu taaluma hii kwamba kuna watu wanasema hawa ni Wanyonya damu, Wananyonga na kung’oa kucha, kitabu hiki hakizungumzii Idara ya usalama wa taifa Tanzania bali kinazungumzia taaluma hii duniani kwa ujumla’ – Evarist Chahali

Ukitaka kukisoma kitabu hiki unaweza kuingia chahali.com Amazon UK search SHUSHUSHU @chahali au kwa Tanzania unaweza kupiga 0717 331 444.

VIDEO: Florah kuhusu kumualika harusini mume wa zamani na kumzidi umri mume mpya

$
0
0
April 30 2017 Mwimbaji wa nyimbo za Injili Tanzania Madame Flora (zamani Flora Mbasha) alirudi kwenye headlines baada ya kufunga ndoa kwa mara ya pili baada ya kuachana na mume wake wa zamani (Emmanuel Mbasha).

Sasa comment zimekuwa nyingi kwenye mitandao ya kijamii kuhusiana na umri wa mume wake wa sasa aitwae Daudi na wengine wanasema haiwezekani kwa Mkristo kufunga ndoa ya pili, mengine ni kuhusu kumualika Mume wake zamani kwenye harusi, maswali yote kayajibu kwenye hii Exclusive Interview hapa chini. VIDEO:

GABO Afunguka Mahusiano Yake na Wema Sepetu ..!!!!

$
0
0

Gabo Zigamba amefunguka kwa kudai kuwa picha za kimahaba zilizozagaa mitandaoni akiwa na Wema Sepetu ni maandalizi ya kazi yao mpya na siyo mambo mengine

Muigizaji huyo ambaye anafanya vizuri kwa sasa katika tasnia ya filamu, amedai filamu hiyo inayokwenda kwa jina la ‘Heaven Sent’ ni full mahaba ndio maana picha zilizosambaa katika mitandao ya kijamii zinawaonyesha wakawa katika hali isiyo ya kawida.

“Movie tunayoifanya na Wema iko very tomantic ndio maana hata picha zenyewe lazima ziwe hivo sasa watanzania naona wao washarasimisha kwamba kuna kitu kinaendelea kumbe hakuna pale tupo kazini na niwaahidi mashabiki zangu naanda kitu kikali sana mara mbili za jinsi wanavyonifahamu,” alisema Gabo.

Pamoja na hayo Gabo amewataka mashabiki wa filamu waendelee kuwapatia changamoto za kejeli ikiwa ni pamoja na kusisistiza kazi nzuri ili wasanii wasibweteke isipokuwa kutoa lugha za matusi

HOTUBA ya Sugu Yafutwa Kabla ya Kusomwa Bungeni

$
0
0

Dodoma. Mwenyekiti wa Bunge, Mussa Zungu ameagiza Hotuba ya Kambi ya Upinzani kuhusu Bajeti ya Wizara ya Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo ihaririwe na kufuta maneno yote katika kurasa 17.
Zungu ametoa uamuzi huo leo asubuhi baada ya kipindi cha maswali na majibu, hata kabla ya bajeti yenyewe kuwakilishwa na Waziri Dk Harrison Mwakyembe.
Zungu amesema amezipihitia hotuba zote na kubaini kuwa ile ya upinzani itakayowalishwa na Joseph Mbilinyi 'Sugu' ina masuala yaliyopo mahakamani ambayo yamekwishazuliwa katika bajeti zilizotangulia.
Amesema maneno yenye mwelekeo huo yakisomwa atachukua hatua.
.
TOA MAONI YAKO HAPA

KWA TAARIFA YAKO ..Facebook Ina Watumiaji Zaidi ya Bilioni 2..!!!

$
0
0

Mtandao wa kijamii wa Facebook unakadiriwa kuwa na wateja bilioni 2 duniani kote.

Ndani ya kipindi cha miaka mitatu mtandao huo umeongeza watumiaji kwa kasi kubwa na inakadiriwa kila siku zaidi ya mtu mmoja hujiunga na mtandao.

Kulingana na ripoti iliyotolewa na mtandao huo, kila mwezi idadi ya watu iliongezeka hadi bilioni 1.94, ambao watu bilioni 1.3 huutumia kila siku.Kampuni hiyo ya Kiteknolojia iliyo na makao makuu yake nchini Marekani, iliripoti faida za takriban dola bilioni 3 katika robo ya kwanza ya mwaka, ikiwa ni ongezeko la asilimia 76 kwa mwaka.

Siku ya Jumatano, mkurugenzi mkuu wa kampuni hiyo, Mark Zuckerberg, alitangaza kwamba atawaajiri watu 3000 zaidi kuweka maudhui ya wastani katika mtandao huo. Akizungumza baada ya ripoti hiyo ya matokeo, Zuckerberg alisema kwamba idadi ya watumiaji wake wameipatia Facebook fursa ya kupanua jukumu la mtandao huo, kuanzisha runinga, afya na siasa.

Robo ya idadi ya watu duniani inatumia facebook kila mwezi huku watumiaji wapya wakitoka nje ya bara Ulaya na Marekani Kaskazini. Hata hivyo imeonya kwamba ukuwaji wa mapato ya matangazo huenda ukashuka.

HARMONIZE Ataja Mkwanja Anaoingiza Youtube kwa Mwezi..!!!

$
0
0

Msanii wa Muziki wa Bongo Fleva kutoka lebo ya WCB, Harmonize  ameweka wazi kiasi cha pesa anachoingiza kupitia mtandao wa Youtube kwa Mwezi .

Harmonize amesema watu wanashangaa kuona anatembelea magari ya kifahari ila hawajui tu kuwa muziki unampa Connections nyingi kwani mbali na show pia anaingiza mkwanja mrefu kupitia mtandao wa Youtube ambapo amefunguka kuwa anaingiza kiasi cha Dola za Kimarekani 3,500 kwa mwezi.

“Namshukuru Mwenyezi Mungu Kupitia muziki umenikutanisha na watu wengi,Umenipa Dili napata riziki kwenye njia tofauti tofauti,sio tu kwenye show,licha ya kufanya show nauza nyimbo zangu kwenye Platform,Mimi akaunti yangu ya Youtube kila mwezi nalipwa Dola 3,500“Amesema Harmonize kwenye mahojiano yake na kipindi cha leo tena cha Clouds FM.

Harmonize kwa sasa ambae anafanya vizuri na wimbo wake wa ‘Niambie’ anatarajia kuanza Tour yake ya muziki wikiendi hii mkoani Mtwara.

ZITTO Kabwe Aikosoa Serikali Kwa Kuamua Kujenga Reli ya Kisasa ..!!!!!

$
0
0

Mbunge wa Kigoma mjini kupitia tiketi ya ACT, Zitto Kabwe ameukosoa mpango wa serikali kuanza kujenga reli ya kati baina ya Dar es Salaam na Morogoro na kusema serikali inapaswa kuangalia vipaumbele vya maeneo ambayo shughuli za reli hiyo itasaidia

Zitto amebainisha hayo wakati akichangia hotuba ya Wizara ya Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano katika mkutano wa Bunge Jijini Dodoma kwa kumtaka Waziri Profesa Makame Mbarawa aangalie takwimu ni wapi anapaswa apeleke reli ili aweze kupata pesa ya kujenga reli nyingine.

"Toka mwaka jana tumelalamika kuhusu jambo hili...Nawashukuru wabunge wemametoa tafsiri mpya ya reli ya kati, reli ya kati tafsiri yake ni Kigoma Dar es salaam au Dar es salaam Kigoma maeneo mengine yote ni matawi ya reli ya kati...... 

"Lakini ujenzi wa  'Standard Gauge' kwa hatua hizo wanazoziita za awali unatoka Dar es salaam kwenda Mwanza....Namuomba Waziri aangalie takwimu ni wapi atapeleka reli ili apate pesa ya kujenga reli nyingine.......

"Takwimu zinaonesha kwamba mizigo ambayo Tanzania inahudumia kwa nchi za maziwa makuu ni tani Milioni tano kwa mwaka kwa mujibu taarifa ya hali ya uchumi mwaka 2015/2016. 

"Katika hizo asilimia 34 ni Zambia, asilimia 34 ni Kongo, asilimia 12 Rwanda, aslimia 6 Burundi, asilimia 2.6 Uganda...

"Unapoanza na 'Standard Gauge' matailion ya fedha ukaipeleka Isaka na Mwanza maana yake ni kwamba unaenda kuhudumia mizigo aslimia 15 ya mizigo yote tunayoipitisha unaacha kwenda kuhudumia mizigo asilimia 40 kwa maana ya Kongo na Burundi ambayo yote inapita Kigoma". Alisema Zitto

Aidha, Zitto amehoji wizara pamoja na serikali kuwa ni njia gani walizozitama mpaka kuamua kupeleka sehemu ambayo wanajua haiwezi kuleta faida kwa taifa.

"Economics' gani ambazo mmetumia katika kuhakikisha kwamba reli inaelekea mahali ambako hakuna mzigo..

"Sipendi kusema kwamba Kigoma inatengwa siyo lugha ambayo  mimi kiongozi napenda kuzungumza lakini hili takwimu zote zinaonesha reli inapaswa kwenda kule ambako kuna faida, hampeleki kule ambako kuna faida ambako kuna faida hii maana yake nini ?...

"Lakini siyo hivyo tu Waziri, kuna fedha za Benki ya Dunia ...kwaajili ya ukarabati wa reli hata hizi Bilioni 200 za ukarabati wa reli ambao upo sahizi na zenyewe mmepeleka kule kule mnapopeleka 'Standard Gauge', mnashindwa hata kutudanganya kwa pipi". Alihoji Zitto


SAKATA la Vyeti Feki: Watusmishi 6 Wafungwa Jela, Zahati 2 Zafungwa kwa Kukosa Watumishi Maana Wote Walifoji Vyeti..!!!

$
0
0

Uamuzi  wa Serikali wa kuwafukuza kazi watumishi wanaodaiwa kughushi vyeti, umezidi kuchukua sura mpya, baada ya watumishi sita wa Halmashauri ya Kilwa mkoani Lindi kufungwa jela mwaka mmoja kila mmoja kwa kosa la kughushi vyeti vya kidato cha nne na kujipatia ajira.

Taarifa nyingine zinasema Katibu Tawala wa Wilaya ya Tandahimba (DAS), Mohamed Azizi naye ameguswa na sakata la vyeti feki baada ya kutajwa katika orodha ya watumishi wenye vyeti feki akiwa namba 5356.

Chanzo cha uhakika kutoka ofisi ya DAS kimesema  kuwa, tayari kiongozi huyo ameshaondoka Mtwara kuelekea Dar es Salaam kupeleka malalamiko yake katika mamlaka za juu kwamba jina lake limeingizwa kimakosa katika orodha hiyo.

Taarifa nyingine kutoka Halmashauri ya Wilaya ya Lindi Vijijini zinasema zahanati mbili zimefungwa baada ya watumishi wote waliokuwapo kukumbwa na sakata la vyeti feki.

Madereva hao, walihukumiwa jana na Mahakama ya Wilaya  ya Kilwa, baada ya kupatikana na hatia ya makosa matatu ya kufoji vyeti vya kidato cha nne.

Hukumu hiyo, imetolewa na Hakimu wa Mahakama hiyo, Gabriel Ngaeje baada ya kuridhishwa na ushahidi uliotolewa na upande wa mashtaka.

Madereva waliohukumiwa ni Juma Sungura, Issa Juma Abdurahamani, Abdull Chubi, Dactuce, Ahamadi Selemani na Abdallah Kilolopera.

Kabla ya kutolewa hukumu hiyo, Hakimu Ngaeje aliwauliza washtakiwa kama wana sababu zitakazoishawishi mahakama isiwape adhabu kali.

Kila mmoja kwa wakati wake, aliomba mahakama iwaonee huruma, kwani wana familia zinazowategemea, hivyo iwapo watapewa adhabu kali kuna hatari ya kukosa matunzo yao.

Naye mwanasheria wa Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa (Takukuru), Emmanuel Camilius aliiomba mahakama kutoa adhabu kali ili iwe fundisho kwa watuhumiwa na watu wengine wenye tabia ya aina hiyo ndani ya Mkoa wa Lindi na Taifa kwa ujumla.

“Tabia ya aina hii si ya kuifumbia macho, kazi wanazozifanya zinahusu usalama wa watu, kugushi vyeti kwa ajili ya kujipatia ajira ni hatari,”alisema Camulius.

Hakimu Ngaeje, akitoa hukumu katika kesi hiyo namba 07/2014, alisema amesikiliza maombi ya pande zote mbili, hivyo akawahukumu kila mmoja kifungo cha nje cha miezi (12) kwa kila kosa na kufanya idadi ya miezi (196).

“Kwa vile adhabu inakwenda pamoja, mtatumikia kifungo cha nje miezi 12,”alisema.

Awali ilidaiwa mahakamani hapo na mwanasheria Camilius, kuwa  watumishi hao wakijua wanachokifanya ni makosa, walifoji vyeti vya kidato cha nne na kujipatia ajira kinyume na sheria ya nchi.

Naye Mbunge wa  Mchinga, Hamidu Bobali (CUF), alisema  zahanati mbili katika Halmashauri ya Wilaya ya Lindi Vijijini mkoani Lindi, zimefungwa baada ya watumishi wake kutajwa katika orodha ya watumishi wa umma wenye vyeti feki.

Bobali alitoa taarifa hiyo bungeni mjini Dodoma  jana, alipokuwa akichangia bajeti ya Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto, kwa mwaka wa fedha 2017/18.

“Mheshimiwa mwenyekiti, hili suala la vyeti feki limeleta shida katika Halmashauri ya Wilaya ya Lindi Vijijini kwa sababu kuna zahanati mbili zimefungwa, baada ya watumishi wake wote kubainika wana vyeti feki.

“Kwa hiyo, namwomba mheshimiwa waziri, achukue hatua haraka,” alisema Bobali wakati alipokuwa akihitimisha mchango wake.

Pamoja na kusema hayo bungeni, nje ya bunge Bobali alisema a zahanati zilizofungwa ziko katika Jimbo la Mtama katika Halmashauri ya Wilaya ya Lindi Vijijini.

“Zahanati zilizofungwa ni za Mkanga 2 na Sudi ambazo zote ziko pembezoni kabisa ya mji, kiasi kwamba kitendo cha kuzifunga, kitaathiri mno wananchi.

“Kwa hiyo, ndiyo maana nilimwomba mheshimiwa waziri afanye kila analoweza kuhakikisha zinafunguliwa haraka ili kunusuru maisha ya wananchi,”alisema Bobali.

Kwa mujibu wa Bobali, zahanati hizo zilikuwa na watumishi watatu watatu kila moja.

Taarifa zaidi kutoka Lindi, zinasema watumishi  236 wa Serikali wamegundulika kutumia vyeti feki.

Katika sakata hilo, halmashauri za wilaya za Nachingwea na Kilwa zinaongoza kwa kuwa na idadi kubwa.

Akizungumza na waandishi wa habari jana, Mkuu wa Mkoa  wa Lindi, Godfrey Zambi alizitaja wilaya na idaidi ya watumishi kwenye mabano, kuwa ni Nachingwea (72), Kilwa (53), Ruangwa (45),Lindi Vijijini (25), Ofisi ya Katibu Tawala (RAS) (23), Manispaa (11) na Liwale (7).

Alisema  katika idadi hiyo, idara za afya na elimu  zinaongoza kwa kuwa na idadi kubwa ya watumishi wa vyeti feki.

SIRI ya Marekani Kufanya Njama za Kutaka Kumuua Rais wa Korea Kaskazini Zavuja

$
0
0

Maajenti wa Marekani na Korea Kusini wanapanga njama ya kumuua kiongozi wa Korea Kaskazini Kim Jong-un, vyombo vya habari nchini humo vimesema. 

Taarifa kutoka wizara ya usalama nchini Korea Kusini imesema mawakala wa kundi la kigaidi linaloungwa mkono na Shirika la Ujasusi la Marekani (CIA) na shirika la ujasusi la Korea Kusini wameingia nchini Korea Kusini wakiwa na silaha hatari ya bio-kemikali. 

Taarifa hiyo imesema Korea Kaskazini itawasaka mawakala hao na kuwaangamiza bila huruma. 

Korea Kaskazini imesema hayo huku wasiwasi ukiendelea kuongezeka katika rasi ya Korea. 
Taarifa hiyo, ambayo imechapishwa na shirika la habari la Korea Kaskazini inasema njama hiyo inahusisha kutumiwa kwa "silaha ya bio-kemikali pamoja na kemikali yenye miali nururishi na sumu". 

Matokeo ya shambulio kama hilo yataanza kubainika baada ya miezi sita hadi 12, taarifa hiyo imesema. 

Vita vya maneno kati ya Marekani na Korea Kaskazini vimezidi wiki za karibuni. 
Korea Kaskazini imetishia kufanya jaribio la sita la silaha za nyuklia. 
Hali ya wasiwasi imekuwa ikiongezeka siku za karibuni, huku Korea Kaskazini na Kusini zikifanya mazoezi ya kijeshi. 

Mwishoni mwa wiki, Rais Marekani Donald Trump alisema angependa kukutana na kiongozi wa Korea Kaskazini Kim Jong-un, iwapo kungekuwa na mazingira mahsusi. 

Amesema ingekuwa "heshima kuu kwake"."Kungelikuwa na hali mahsusi kwangu kukutana naye, ningekutana naye - bila shaka. Ingekuwa heshima kuu kwangu kufanya hivyo," Bw Trump aliambia shirika la habari la Bloomberg Jumatano. 

Jumapili, alikuwa amemwelezea Bw Kim kama "kijana mwerevu". 
Lakini Ikulu ya White House baadaye ilitoa taarifa kufafanua matamshi ya Bw Trump na kusema Korea Kaskazini ingehitaji kutimisha masharti mengi kabla ya mkutano kati ya viongozi hao wawili kufanyika. 
Marekani imetuma meli za kivita na nyambizi eneo hilo na pia imeweka mtambo wa kutungua makombora ya adui Korea Kusini, mtambo ambao maafisa wanasema umeanza kufanya kazi. 
Jumapili, makala katika shirika la habari la serikali ya Korea Kusini KCNA ilitoa wito kwa Marekani kutafakari kuhusu "madhara makubwa ambayo yanaweza kusababisha na uchokozi wake wa kipumbavu wa kijeshi." 

Korea Kaskazini imekuwa ikifanya majaribio ya makombora mara kwa mara miezi ya karibu na imekuwa ikitishia kufanya jaribio la silaha za nyuklia kwa mara ya sita.Rais Trump aliambia CBS kuwa Marekani "haitakuwa na furaha sana" iwapo majaribio zaidi yatatekelezwa na Korea Kaskazini. 
Alipoulizwa iwapo hili litasababisha hatua ya kijeshi kutoka kwa Marekani, alijibu: "Sijui mimi. Naam, tusubiri tuone." 

Pyongyang kwa muda mrefu imeamini kwamba inahitaji silaha za nyuklia ili kujilinda, na imekuwa tayari kukabiliana na vitisho na adhabu kutoka kwa jamii ya kimataifa. 

Kim Jong Un ameonyesha kujitolea kwake, kinyume na babake na babu yake, kupuuza msimamo na maoni na mshirika pekee mkuu wa Korea Kaskazini, China. 

Kiongozi wa mashauriano wa zamani wa Marekani Chris Hill anasema Kim Jong il (babake Kim Jong-un) alijali sana yale ambayo wengine walifikiria, na hasa Wachina. Lakini mwanawe Kim Jung Un hajali wasemayo watu. 

MOURINHO: Nitawaweka Benchi Baadhi ya Wachezaji Kwenye Mechi Dhidi ya Arsenal..!!!

$
0
0

Mkufunzi wa klabu ya Manchester United Jose Mourinho anasema kuwa atawapumzisha baadhi ya wachezaji wake katika mechi ya siku ya Jumapili dhidi ya Arsenal.

Ushindi mwembamba wa 1-0 dhidi ya klabu ya Uhispania Celta Vigo siku ya Alhamisi ulikuwa wa 10 tangu mwezi Aprili.

Huku kikosi hicho cha Mourinho kikiwa katika nafasi ya tano katika Msimamo wa ligi ya Uingereza, ligi ya kombe la Europa inaweza kuwapatia fursa ya kushiriki katika kombe la vilabu bingwa Ulaya msimu ujao.

”Wachezaji ambao wameshiriki katika mechi nyingi hatawachezeshwa wikendi”, alisema Mourinho.

Mpira wa adhabu wa Marcus Rashford uliipatia United ushindi katika mchezo wakwanza  na nchini Uhispania huku mcezo wa marudiano ukitarajiwa kupigwa siku ya Alhamisi ijayo katika uwanja wa Old Trafford.

Maumivu Wakati Wa Kufanya Mapenzi Kwa Wanawake

$
0
0

Maumivu wakati wa kufanya mapenzi ni hali inayojitokeza hasa kwa wanawake. Hujulikana kwa kitaalamu kama.

dyspareunia. Maumivu haya yanaweza kutokea wakati wa kufanya mapenzi au baada ya kufanya mapenzi. Sababu kuu za maumivu haya mara nyingi ni magonjwa ya zinaa na kupungua kwa majimaji ukeni wakati wa ngono.

Maumivu Wakati Wa Kufanya Mapenzi
Unaweza kuwa unapata maumivu wakati tendo la ngono linaendelea. Mara nyingi maumivu haya huwa kwenye kuta za uke, shingo ya uzazi au chini ya kitovu. Sababu za maumivu haya ni;

Kuchubuka ukeni kutokana na maji ya uke kupungua. Inawezekana kutokana na kutoandaliwa vizuri wakati wa mapenzi au uke kutotoa majimaji ya kutosha.Magonjwa ya zinaa kama kisonono, klamidia, vaginitis.Maambukizi ya shingo ya uzazi (cervicitis)Maambukizi kwenye mirija ya uzazi. Mara nyingi amumivu hutokea chini ya kitovu au kiuononi.Maumivu Baada ya Kufanya Mapenzi
Baada ya kukutana na mwenzi wako kingono, unaweza kuanza kupata maumivu dakika chache mpaka siku kadhaa toka mlipokutana. Maumivu ya kawaida huwa ni kwenye uke kutokana na kuchubuka wakati wa kufanya mapenzi. Unaweza kuyahisi vizuri hasa pale unapojisafisha kwa maji au wakati wa kukojoa ikiwa njia ya mkojo imechubuliwa.

Maumivu ndani ya uke kabisa, kiunoni au chini ya kitovu baada ya kufanya mapenzi mara nyingi huonesha dalili za
Maambukizi ya shingo ya uzaziMaambukizi ya mirija ya uzaziSaratani ya shingo ya kizazi
Dalili hii inaweza kuambatana na hali ya homa, kutokwa damu ukeni baada ya ngono, kutoa uchafu ukeni, kutapika na kichefuchefu.

Matibabu
Unapopata hali hii jichunguze vizuri. Kama maumivu hayajatokana na michubuko wakati wa mapenzi, basi onana na daktari haraka iwezekanavyo. Maambukizi ya shingo ya uzazi na mirija ya uzazi (Pelvic Inflammatory Disease – PID) huchangia kwa kiasi kikubwa hali hii. Matibabu ya haraka ni muhimu ili kupunguza madhara ya magonjwa haya.

Michubuko kutokana na kufanya mapenzi hupona yenyewe polepole. Jioshe vizuri kwa maji safi. Usipake dawa zozote mpaka uambiwe na daktari wako.

Mauaji mengine yatokea Rufiji

$
0
0

Rufiji.Mtu mmoja Aitwae Amri Chanjale (55), mkazi wa kitongji cha Makaravati katika Kijiji cha Umwe Kusini wilayani Rufiji ameuawa kwa kupigwa risasi akiwa nyumbani kwake.

Tukio hilo limetokea jana saa 1.30 usiku baada ya watu wasiojulikana kufika kwake na kutekeleza shambulio hilo. 

Marehemu huyo ambaye pia ni mwanachama wa CCM ameuawa ikiwa ni baada ya siku tano kuuawa kwa  Mohammed Malinda ambaye nae alikuwa ni mwanachama wa chama hicho. 

Katibu wa Siasa na Uenezi wa CCM wilayani Rufiji, Musa Nyeresa amethibitisha kuuawa kwa mwanachama huyo kwa kupigwa risasi.

Machangudoa Wajilipua Kwa Rais Magufuli

$
0
0

DAR ES SALAAM: Kama mbwai na iwe mbwai! Ndivyo wanavyosema baadhi ya wasichana wanaojihusisha na biashara haramu ya kujiuza (machangudoa) sehemu mbalimbali jijini Dar wakimaanisha liwalo na liwe baada ya kuamua kujilipua kwa Serikali ya Rais Dk. John Pombe Magufuli ‘JPM’ na kurejea barabarani kuendelea kujiuza kama zamani. 

Uchunguzi wa gazeti hili wikiendi iliyopita maeneo ya Kinondoni, Buguruni, Temeke, Manzese na mitaa mbalimbali ya Sinza jijini Dar ulibaini kuwa, machangudoa hao wamerejea upya barabarani baada ya kujificha kwa miezi kadhaa tangu walipopigwa marufuku kuifanya biashara hiyo. 

Kikosi cha Oparesheni Fichua Maovu (OFM) cha Global Publishers kiliwashuhudia wanawake hao na kufanya nao mahojiano juu ya kurejea barabarani ambapo walikuwa na maoni mbalimbali. Baadhi ya wanawake hao walifunguka kwa OFM kuwa, licha ya kupewa kashikashi na Jeshi la Polisi kwa kukamatwa na kupelekwa mahakamani, lakini hawawezi kuiacha ‘kazi’ hiyo kutokana na ugumu wa maisha. 

Kwa mujibu wa baadhi ya wanawake walionaswa na OFM maeneo ya Sinza-Mori, Dar, walisema biashara hiyo ndiyo maisha yao lakini Magufuli amewanyoosha kwa sababu hata hivyo, dili hizo kwa sasa hazina pesa. 

“Hatupendi kujiuza lakini tutafanyaje kwa sababu Magufuli ndiyo hivyo amebana, kama ni kutukamata acha tu tukamatwe hatuna jinsi. “Nani asiyependa kulala usiku na familia yake? Ukituona barabarani ujue hali ni mbaya, Magufuli alegeze kidogo basi,” alisema mmoja wa madadapoa hao. 

“Kwa hali hii ya Magufuli, kama ni ambushi tupo tayari potelea mbali maana maisha yenyewe ndiyo hayahaya, kama vipi waturudishe vijijini maana hatuwezi kufa njaa, bila kujiuza tutakula nini? “Potelea mbali acha tu watukamate tukale ugali wa bure jela,” alisema mwingine kwa kujiamini. 

Ijumaa lilimtafuta Kamanda wa Polisi Kanda Maalum ya Dar es Salaam, CP Simon Sirro ili kumuuliza kama jeshi hilo limesitisha oparesheni za kuwaondoa machangudoa jijini Dar lakini simu yake iliita bila kupokelewa. Gazeti hili linalishauri Jeshi la Polisi jijini Dar kurejesha zile oparesheni ambazo lilikuwa likizifanya kwani kwa namna moja ama nyingine kasi ya biashara hiyo ilipungua.

Sugu Amvaa 'Bashite' Bungeni

$
0
0

MBUNGE wa Mbeya Mjini, Joseph Mbilinyi ‘Sugu’ amemshambulia Bashite huku akisema kuwa mtu huyo alipaswa awe mahakamani na sio ofisini kwa madai kuwa amefoji vyeti vya elimu ya sekondari jambo ambalo ni kosa kisheria.


Hayo ameyasema leo Bungeni Mjini Dodoma wakati akichangia hoja kuhusu Wizara ya Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo.


Aidha Sugu amemtaka Rapa ROMA Mkatoliki ajitokeze hadharani aeleze wazi kuhusu alivyotekwa na nani alihusika ili jamii ielewe na mamlaka husika iweze kuchukua hatua ikiwemo kuwabaini waliyotekeleza tukio hilo ambalo si la kibinadamu.


Sugu aliwageukia wasanii wa Filamu Bongo ambao hivi karibuni waliandama wakipinga uingizwaji holela wa filamu za nje ambazo wanadai zinaporomosha soko la filamu za ndani. Sugu amewataka wasanii hao waache kutumika kisiasa na badala yake wafate misingi ya kazi zao.

‘Hakuna Mwanaume Anaependa Kuwa na Mwanamke Mmoja’ -Kipanya

$
0
0

Mtangazaji na Mchoraji katuni maarufu nchini Tanzania,Masoud Kipanya amewaaacha watanzania midomo wazi kwa kuweka wazi maoni yake kuwa mwanaume hawezi kuridhika na mwanamke mmoja.


Masoud amesema tangia zamani wanaume ni Watu mwenye tamaa hivyo hakuna mwanaume ambae anapenda kuwa na mwanamke mmoja ila ni vitu vidogo vidogo tu vinavyozuia kama dini ya Kikristo na masuala mengine ya kiuchumi.


“Hakuna mwanaume anaependa kuwa na mwanamke mmoja,na hiyo ndiyo huruka ya uanaume,tunajizuia tu kwa sababu!! hivyo kwa mfano kwa wenzangu wakristo utaratibu unawazuia lakini angalia vidumu vilivyo nje unaona eeehh??“Amesema Masoud Kipanya kwenye Mahojiano yake na Kwanza TV.


Hata hivyo Masoud alizungumzia suala la idadi ya kuzaa watoto kwenye familia na kusema kuwa kwa upande wake  yeye hana kikomo kwenye kuzaa kwani anaamini watoto hawarishwi na yeye bali wanarishwa na mwenyezi Mungu.


Masoud Kipanya kwa mujibu wa Takwimu za mwaka jana zilizofanywa na kituo cha Clouds FM kupitia kipindi cha XXl ni moja ya watu watatu maarufu nchini Tanzania wanaoendesha magari ya kifahari akiwa anamiliki gari aina ya Hummer H3.

Zitto Kabwe Aikosoa Serikali Kwa Kuamua Kujenga Reli ya Kati Toka Dar Hadi Moro

$
0
0

Mbunge wa Kigoma mjini kupitia tiketi ya ACT, Zitto Kabwe ameukosoa mpango wa serikali kuanza kujenga reli ya kati baina ya Dar es Salaam na Morogoro na kusema serikali inapaswa kuangalia vipaumbele vya maeneo ambayo shughuli za reli hiyo itasaidia


Zitto amebainisha hayo wakati akichangia hotuba ya Wizara ya Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano katika mkutano wa Bunge Jijini Dodoma kwa kumtaka Waziri Profesa Makame Mbarawa aangalie takwimu ni wapi anapaswa apeleke reli ili aweze kupata pesa ya kujenga reli nyingine.


"Toka mwaka jana tumelalamika kuhusu jambo hili...Nawashukuru wabunge wemametoa tafsiri mpya ya reli ya kati, reli ya kati tafsiri yake ni Kigoma Dar es salaam au Dar es salaam Kigoma maeneo mengine yote ni matawi ya reli ya kati...... 


"Lakini ujenzi wa  'Standard Gauge' kwa hatua hizo wanazoziita za awali unatoka Dar es salaam kwenda Mwanza....Namuomba Waziri aangalie takwimu ni wapi atapeleka reli ili apate pesa ya kujenga reli nyingine.......


"Takwimu zinaonesha kwamba mizigo ambayo Tanzania inahudumia kwa nchi za maziwa makuu ni tani Milioni tano kwa mwaka kwa mujibu taarifa ya hali ya uchumi mwaka 2015/2016. 


"Katika hizo asilimia 34 ni Zambia, asilimia 34 ni Kongo, asilimia 12 Rwanda, aslimia 6 Burundi, asilimia 2.6 Uganda...


"Unapoanza na 'Standard Gauge' matailion ya fedha ukaipeleka Isaka na Mwanza maana yake ni kwamba unaenda kuhudumia mizigo aslimia 15 ya mizigo yote tunayoipitisha unaacha kwenda kuhudumia mizigo asilimia 40 kwa maana ya Kongo na Burundi ambayo yote inapita Kigoma". Alisema Zitto


Aidha, Zitto amehoji wizara pamoja na serikali kuwa ni njia gani walizozitama mpaka kuamua kupeleka sehemu ambayo wanajua haiwezi kuleta faida kwa taifa.


"Economics' gani ambazo mmetumia katika kuhakikisha kwamba reli inaelekea mahali ambako hakuna mzigo..


"Sipendi kusema kwamba Kigoma inatengwa siyo lugha ambayo  mimi kiongozi napenda kuzungumza lakini hili takwimu zote zinaonesha reli inapaswa kwenda kule ambako kuna faida, hampeleki kule ambako kuna faida ambako kuna faida hii maana yake nini ?...


"Lakini siyo hivyo tu Waziri, kuna fedha za Benki ya Dunia ...kwaajili ya ukarabati wa reli hata hizi Bilioni 200 za ukarabati wa reli ambao upo sahizi na zenyewe mmepeleka kule kule mnapopeleka 'Standard Gauge', mnashindwa hata kutudanganya kwa pipi". Alihoji Zitto

Kwa Nini Uchumba ni "Mtamu" Zaidi Kuliko Ndoa Kwa Walio Wengi?

$
0
0

1. Wapendwa wanaJF, kwa wale waliowahi kupitia hatua ya uchumba hadi kufikia ndoa au hata wale ambao hawajawahi kupitia hatua hizo, lakini wameona mifano kadhaa kwenye jamii, watakubaliana na mimi kwamba ndoa nyingi "zinaumwa" na zinahitaji kutafutiwa "chanjo" au "tiba!"

 2. Naamini kwamba kabla ya kufikia ndoa wachumba huwa wanavumiliana na kupendana mno, kila mmoja anamwona mwenzake ni bora kuliko yeye! In fact kama hawajaonana siku inakuwa haijaenda sawa!


3. Lakini baada ya kuingia kwenye ndoa mambo hubadilika taratibu na kuanza kuleta kero, malumbano yasiyoisha, huzuni zisizoisha, ngumi, mateke, n.k. Kuna baadhi ya wachungaji huwa wanatumia usemi huu ufuatao wakati wanafungisha ndoa: "Wengi wa walio ndani (ya ndoa) wanaka watoke na walio nje (ya ndoa) wanataka kuingia!" Kwa maana hiyo ndoa ni taasisi ya ajabu sana!


4. Swali langu ni kwamba kwa nini uvumilivu, upendo, huruma, kujaliana, (ambao mimi nimeuita "utamu") nk ambako kunaonekana kwenye uchumba usiendelee hata wakati wa ndoa?


5. Lengo la mada hii ni kujaribu kuwasaidia wenzetu ambao wanataka kuingia kwenye ndoa pamoja na wale walioko kwenye ndoa ili waweze ku-"think twice" na kutengeneza mahusiano yao ili maisha yao yawe na ushuhuda mbele ya jamii na watoto (kama wamefanikiwa kuwapata).


6. Kwa kuanza kutoa maoni, kwa

 upande wangu naona kwamba (a) wengi wanaingia kwenye mahusiano kwa sababu ya "tamaa za mwili" kiasi kwamba wanaangalia uzuri wa nje zaidi kuliko wa ndani! Uzuri wa nje ukishaanza kuchuja upendo nao unaanza kuchuja vile vile! (b) Kingine ni kwamba baadhi ya watu (hapa nafikiri ni wengi zaidi) huwa wanaingia kwenye mahusiano kwa sababu ya kuangalia vipato zaidi kuliko upendo wa dhati, uchumi ukianza kuyumba, ndoa nako inaanza kuyumba na hatimaye kuvunjika!


USHAURI: Upendo wa kweli usiathiriwe na mazingira: uzuri, kipato na kadhalika! Hii ni sumu mbaya katika ndoa! Naomba maoni yenu zaidi.

Makosa Wanayofanya Wanaume Walio Kwenye Ndoa

$
0
0

1- Kuja na vimada mpk home na kumuacha ndani ya gari


2-Kuingia ndani na viatu vya matope wakati

kumeshadekiwa


3-Kuvurugua nguo au vitu wakati wa kutafuta kitu kabla ya kuuliza kilipo.


4-Kumtambulisha mtoto wako kwa kimada wako.


5-Kumleta rafiki yake kuja kula bila kutoa

taarifa.


6-Kumsifia rafiki au ndugu wa mke wa kike

kuwa anavutia bila hofu.


7-Kukosoa muonekano wa mke bila kujali

atajisikiaje.


8-Kutosema chochote mke akipendeza mpaka aulize.


9- Kujifutia taulo na kuliacha ovyo bila kulianika


10- Kutotandika bed mke asafiripo na kugeuza bed kama kiota cha ndege


11-Kutofua boxer na socks zake hadi wife

awepo na kama kasafiri zitasubiri arudi

BASHITE Amkanganya Waziri wa Magufuli Bungeni..Habari Vichwa vya Magazeti vya Leo Jumamoi ya Tarehe 6/5/2017..!!!

Viewing all 104775 articles
Browse latest View live




Latest Images