Quantcast
Channel: UDAKU SPECIAL
Viewing all 104756 articles
Browse latest View live

"Niliamini Sitamuona Tena Roma"

$
0
0

Nancy Mshana mke wa Roma amefunguka na kusema alikata tamaa juu ya mume wake, ambaye alitekwa na kupotea kwa siku kadhaa bila kufahamika alipokuwa licha ya jitihada zilizokuwa zikifanyika na watu wake wa karibu na vyombo vya usalama bila mafanikio.


Nancy Mshana akimlisha keki mume wake Roma Mkatoliki, katika siku ya kumbukumbu ya kuzaliwa kwake.

Nancy alisema hayo katika siku ya kumbukumbu ya kuzaliwa kwake na kudai hakutegemea tena kama angekuwa na mume wake huyo katika siku hiyo ila anashukuru kwa uwezo wake Mungu ambaye alitenda miujiza na kufanya mume wake kupatikana. 


"Ilifika wakati nilikata tamaa na kuamini kuwa sitakuwa na wewe katika sikukuu ya kumbukumbu yangu ya kuzaliwa ya mwaka huu!! Lakini Mungu Baba wa Mbinguni akasema 'NO'" alisema Nancy 


Mbali na hilo rapa Roma Mkatoliki ambaye sasa anaendelea vyema na hali yake kuzidi kuimarika zaidi kufuatia majeraha aliyopata wakati alipotekwa, anasema ameamua sasa kuendelea na maisha yake ya muziki kama kawaida hivyo mashabiki wasishangae kumuona stejini muda wowote kuanzia sasa.

Soma Nafasi za Kazi Zilizotangazwa Siku ya Leo

$
0
0

#BREAKINGNEWS Basi lililobeba wanafunzi wa Shule ya Lucky Vincent Lapata Ajali na Kuuwa

$
0
0

Basi aina ya Toyota Coaster lililobeba wanafunzi wa Shule ya Lucky Vincent ya Arusha limetumbukia bondeni Karatu.
Zaidi ya watoto 20 na waalimu wanahofiwa kufa.
Walikuwa wakienda tour kwenye hifadhi ya Ngorongoro.
Ni ajali kubwa na mbaya kuwahi kutokea tangu ya miaka 7 iliyopita.
Pole sana kwa ndugu, jamaa na marafiki waliopoteza watu wao katika ajali hii mbaya, Mungu azilaze roho za marehemu peponi

VYETI Vyamuondoa Mhudumu wa Mochwari..!!

$
0
0

Sakata la vyeti fedha limemuondoa kazini mhudumu wa chumba cha kuhifadhia maiti wa hospitali ya Mkoa wa Shinyanga baada ya kukutwa na cheti cha kughushi.

Katibu tawala wa Shinyanga, Albert Msovela amemtaja mtumishi huyo kuwa ni Christopher Lwambo na kusema kuwa ndiye pekee katika hospitali hiyo aliyebainika kuwa na cheti feki.

Msovela amesema hakuna mtumishi mwingine wa umma katika taasisi hiyo aliyenaswa na cheti bandia na kwamba, huduma zinaendelea vizuri.

Wakati mtumishi huyo akiondolewa, Mwenyekiti wa CCM wilayani Chamwino, Charles Ulanga ambaye ni mratibu wa elimu wa Kata ya Buigiri ameandika barua ya kukata rufaa lakini ametakiwa kuipeleka kwa mwajiri wake ambaye ni mkurugenzi mtendaji wa halmashauri.

“Nilishaandika barua, lakini tulielekezwa kuzipeleka kwa waajiri wetu ambao wao ndiyo watazifikisha kwa wahusika. Mimi nimeshafanya hivyo,” amesema Ulanga.

Jina lake lilikuwa miongoni mwa majina yaliyojitokeza katika orodha ya watumishi wanaodaiwa kughushi vyeti.

Hata hivyo, alijitokeza hadharani na kupinga suala hilo akisema alisoma elimu ya msingi na baadaye ualimu bila ya kupitia elimu ya sekondari na kuwa ndivyo vyeti alivyowasilisha.

Wakati Ulanga akikata rufaa, Chama cha Wafanyakazi wa Serikali za Mitaa (Talgwu) mkoani Morogoro kimepokea wafanyakazi zaidi ya kumi wakilalamikia kutotendewa haki.

Katibu wa Talgwu mkoani humo, Lawrence Mdega amesema wafanyakazi hao walifika ofisini kwake wakilalamika kuwa waliajiriwa kwa elimu ya darasa la saba, lakini wanashangaa wameandikwa kuwa walimaliza kidato cha nne.

Mkuu wa kitengo cha utawala na fedha wa Chuo Kikuu cha Sokoine (Sua), Yonica Ndaga amesema watumishi watatu wa chuo hicho wameonyesha nia ya kukata rufaa wakidai kuonewa na uhakiki uliofanyika ambao haukuwatendea haki.

TAHARUKI Kifo cha Hausigeli..Afariki kwa Kuchomwa Visu Ndani ya Nusu Saa..!!!

$
0
0

MSAIDIZI wa kazi za ndani, Christina Mabuga (37), amekutwa amekufa ndani ya chumba chake, mwili ukiwa na majeraha ya kuchomwa kisu tumboni na shingoni dakika 25, tangu aachwe akiwa hai.

Taarifa kutoka eneo la tukio jana zilisema mwanamke huyo huenda alijiua kwa kuwa hadi mashuhuda waliofika kwanza nyumbani hapo walikuta milango ya nyumba hiyo ikiwa imefungwa na kuwalazimu kutumia mlango wa dharura.

Taarifa hizo zinaeleza kwamba tukio hilo lilitokea juzi mchana saa tisa alasiri, eneo la Moshi Bar, Ukonga Mombasa, Manispaa ya Ilala jijini Dar es Salaam.

Akizungumza na Nipashe kwa njia ya simu jana, mwajiri wa binti huyo, Anna Kasanda, alisema akiwa kazini alipokea taarifa majira ya saa tisa alasiri kwamba kuna matatizo yametokea nyumbani kwake.

Ndipo alipoanza kujiandaa kutoka ofisini na kurudi nyumbani, alisema.

Nyumbani hapo anaishi na shangazi yake ambaye alijua ya kwamba angeweza kutatua tatizo hilo ambalo hakuwa ameambiwa tayari, kabla ya yeye kufika kutoka kazini.

“Nilipopigiwa simu nilianza kujiandaa kuondoka kazini (muda huo huo) lakini nilifika nyumbani usiku," alisema Anna. "Nilipofika nikakuta baadhi ya majirani na watu wengine wakiwa wamejaa nyumbani."

"Nilipofika ndani nilianza kuona damu zimetapakaa na kuchuruzika kutoka chumbani kwa dada.

“Nilishangaa kwa kuwa nilipotoka asubuhi nilimuacha dada akiwa salama tu, ingawa kwa siku hiyo hakuonekana akiwa na furaha kama siku nyingine.

"Nilipoelezewa na majirani nikaambiwa mwili wa marehemu uliwahishwa kupelekwa Hospitali ya Taifa Muhimbili, hivyo nikaukuta mwili huko.”

Alisema alipotoka nyumbani juzi asubuhi alimuacha binti huyo akiwa na shangazi yake ambaye hushinda nyumbani hapo muda mwingi, na kwamba mtoto wake alikuwa amekwenda shuleni.

Alisema muda wa kutoka shule mtoto wake ulipofika, shangazi alitoka mara moja na kwenda kumchukua mtoto njiapanda ya barabara, akimuacha binti huyo akiwa ndani.

"Shangazi alitumia muda wa dakika 25 hadi kurudi nyumbani na mtoto," alisema.

“Baada ya kurudi, alipofungua mlango wa mbele, ulikuwa haufunguki na alipojaribu kumuita dada kwa nje kwa muda mrefu tu ili amfungulie, hakukuwa na majibu yeyote.

"Ndipo alipoamua kuzunguka nyumba na kuchungulia dirisha la chumba cha binti huyo na kuona akiwa amelala chini na damu zikiwa zimetapakaa.”

Anna alisema baada ya shangazi yake kuona hivyo, alipiga kelele na kuwaita majirani ambao walimsaidia kufungua mlango wa dharura nyuma ya nyumba na kuingia ndani.

“Binti huyu nimekaa naye kwa zaidi ya mwaka mmoja... tumeishi vizuri tu na jana (juzi) wakati naondoka kwenda kazini aliniambia ya kwamba wazazi wake wamempigia wana shida na fedha hivyo nimpatie ili awatumie,nikasema sawa.”

Mwili wa marehemu umehifadhiwa Muhimbili kwa ajili ya uchunguzi zaidi, mwajiri huyo alisema na kwamba baada ya tukio hilo la juzi baadhi ya majirani walitoa maelezo Polisi.

Akizungumza na Nipashe jana, Kamanda wa Polisi Mkoa wa Kipolisi Ilala, Salum Hamdan, alisema yuko safarini hivyo aulizwe kaimu kamanda wa mkoa huo.
Kaimu Kamanda wa mkoa huo, Ernest Matiku, alisema kuna taarifa kuhusu tukio hilo, ingawa yeye si mzungumzaji.

“Sawa, kuna taarifa hizo, ila mimi sio mzungumzaji kwa sasa,” alisema Matiku.

Penzi la Harmonize na Wolper kwishaaa

$
0
0

Msanii wa muziki kutoka WCB, Harmonize Alhamisi hii amethibitisha kuwachana na malkia wa filamu, Jacqueline Wolper. 

Huwenda wawili hao wamezingua siku za karibuni, kwani Machi 16 mwaka huu Harmonize aliachia project yake ya wimbo ‘Niambie’ ambayo ndani yake Wolper alicheza vitendo na pia walishirikiana kwenye ishu ya promotion ya wimbo huo. 

Akiongea katika kipindi cha Leo Tena,  Harmonize amedai alikuwa na mipango mingi na Wolper lakini ameona bora aachane naye ili aupeshe shari. 

“Sipo katika mahusiano, inshort kila mtu ana maisha yake ‘tumeachana'” alisema Harmonize . 

Pia muimbaji huyo alikanusha taarifa za kwenye mitandao kuwa anatoka kimapenzi na msichana wa kizungu. 

Hata hivyo hakuweka wazi sababu maalum ya kuachana na mpenzi wake huyo aliyedumu naye kwa muda mrefu pamoja na kumtambulisha kwao.

POLEPOLE Aaanza Tumbua Tumbua Ndani ya CCM..Afyeka Vigogo Hawa 20 Harakaharaka..!!!

$
0
0

VIONGOZI zaidi ya 20 wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) ngazi ya kata na matawi Jijini Arusha wamesimamishwa uongozi kwa tuhuma za kufuja mali za chama.

Kata ambazo viongozi wake wamesimamishwa kwa tuhuma hizo za ubadhirifu ni Unga Limited, Themi, Sekei, Sombetini na Daraja Mbili. Viongozi hao ni wenyeviti, makatibu, wachumi na makatibu wenezi.

Katika kata ya Unga Limited, mbali ya viongozi wa kata kuchukuliwa hatua pia viongozi wa matawi wa wamesimamishwa kwa madai ya kushindwa kusimamia ipasavyo mali za chama.

Mbali ya tuhuma za kufuja mali za chama, baadhi ya viongozi hao pia wanatuhumiwa kufanya hujuma katika chaguzi zilizopita, ikiwa ni pamoja na kuficha fomu kwa wanachama wanaotaka kuwania uongozi ili wao waweze kuwania tena nafasi hizo na kupita bila ya kupingwa ama kuwa na wagombea dhaifu.

Akizungumza na waandishi wa habari jijini hapa jana, Katibu wa Uenezi na Itikadi wa CCM, Humphrey Pole pole alisema na kutoa salamu kwa watendaji wote wa chama hicho kote nchini kuhakikisha wanatunza mali na kuzitumia kwa uaminifu na uadilifu mkubwa.

Polepole alisema katika baadhi ya maeneo mali za chama zinatafunwa kama mchwa na viongozi mbalimbali hivyo msako unaendelea kote nchini kuwasaka na bila ya kuonea mtu.

Katibu huyo alisema chama hakiwezi kuwavumilia viongozi wanaofuja mali kwa sasa chini ya uenyekiti wa Rais John Magufuli. "Wote watachukuliwa hatua kali," alisema.

"Kuna baadhi ya maeneo mali za chama zinatumika vizuri sana... kuna baadhi ya maeneo mengine viongozi wanafuja vibaya lakini wameachwa.
"Kwa sasa hilo halipo.

"Heri kuwa na viongozi wachache waaminifu na waadilifu wenye kufuata katiba ya chama kuliko kuwa na utitiri wa viongozi wezi na wasiokuwa waaminfu. Hilo haliko kwa sasa chini ya uongozi wa (Rais) Magufuli."

Wakenya kujipima wenyewe Virusi vya Ukimwi

$
0
0

Kenya imezindua kifaa cha bei nafuu cha kujipimia virusi vinavyosababisha ugonjwa wa Ukimwi, ambacho raia wataweza kukitumia bila usaidizi wa daktari. 

Ili kujipima, mtu anatoa mate, damu au majimaji kutoka mwilini na kisha anajipima binafsi bila ya kusaidiwa na mtu. 

Kifaa hicho kinalenga watu 400,000 ambao hawajafahamu iwapo wana Virusi Vinavyosababisha Ukimwi au la. 

Wataalamu wanasema kwamba, kifaa hicho kinafanikiwa asilimia 80, na kitagharimu kama dola 7 hivi na kitapatikana katika maduka ya kuuzia madawa. 

Martin Sirengo, kiongozi mkuu wa shirika la kukabiliana na Ukimwi Kenya, Nascop, anasema kuwa bado watu watahitajika kwenda hadi katika vituo vya matibabu ili kuthibitisha matokeo. 

Aidha anashauri kuwa, mtu anafaa kujipimia katika sehemu za faragha na mbele ya mtu anayeaminika. 

Rudolf Eggers, mwakilishi wa Shirika la Afya Duniani (WHO) nchini Kenya, anasema kwamba, “lengo kuu la kifaa hicho cha kujipimia virusi vya HIV ni sambamba na njia nyingine zilizopo za kupima HIV.” 

Takriban watu milioni 1.5 wanaishi na virusi vya HIV nchini Kenya, ambapo milioni moja kati yao wanatumia matibabu ya kumeza vidonge vya kupunguza makali ya ugonjwa wa Ukimwi.

Aga Khan yaja na upasuaji kwa WhatsApp

$
0
0

Madaktari wa Hospitali ya Aga Khan na Prince Aly Khan nchini India, wanatarajia kuboresha huduma za upasuaji wa mifupa na majeraha kwa kutumia mtandao wa What’sApp.

Teknolojia hiyo mpya inatarajiwa kuanza kutumika nchini baada ya madaktari bingwa kutoka India kuwasili. Madaktari hao kutoka Hospitali ya Prince Aly Khan waliwasili nchini jana kwa ajili ya kutoa mafunzo kwa wenzao wa Hospitali ya Aga Khan kutumia teknolojia hiyo ya kisasa kufanya upasuaji.

Daktari bingwa wa upasuaji mifupa na majeraha wa Hospitali ya Aga Khan, Harry Matoyo amesema madaktari hao walioanza upasuaji wataondoka Jumatatu na kwamba, wanatarajia wataalamu wa hospitali hiyo watakuwa wamenufaika na uzoefu watakaopata.

“Tumetengeneza group (kundi) la What’sApp ambalo litatumiwa na madaktari bingwa wa upasuaji mifupa kati ya nchi hizi mbili, kwa ajili ya kusaidiana iwapo tutakwama wakati wa upasuaji. Tunaweza kupiga picha na kuuliza kitu kinachotakiwa kufanyika,” alisema Dk Matoyo.

CCM Yaweka Wazi Kupotea kwa Ndg. Kinana..!!!

$
0
0

Katibu wa Itikadi na Uenezi Taifa (CCM), Humphrey Polepole amesema kuwa Katibu mkuu wa chama hicho Abdulrahman Kinana alikuwa akiugulia afya yake pindi yupo kazini hivyo alichukua muda wa kutosha kwenda nje ya nchi kupatiwa matibabu.

Polepole amezungumza na AZAM NEWS ambapo alisema tangu Mzee Kinana akiwa hata kwenye mkutano mkuu wa CCM Dodoma hakuwa sawa kiafya.

“Tangu akiwa kwenye mkutano mkuu maalumu wa CCM Dodoma hakuwa sawa kiafya, alikuwa anafanya yote haya akiugulia afya yake kwahiyo ikakubalika achukue muda wakutosha wa kuitizama afya yake nje ya nchi na anapo rejea mgonjwa akitoka hospitali huwa hakimbii kazini, shambani moja kwa moja inashauriwa kitaalam atumie muda wa kupumzika ili kuimarisha afya yake na nimezungumza nae anaendelea vizuri yuko madhubuti kabisa kuliko jana,” alisema Polepole.

Katibu mkuu wa chama hicho, Abdulrahman Kinana hajaonekana hadharani kwa muda tangu Rais Magufuli aliposema kuwa yuko India.

EVERTON Yaja Kuzifunda Simba, Yanga Julai..!!!

$
0
0

WAZIRI wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo, Harrison Mwakyembe, amesema kikosi cha Everton FC kitatua nchini Julai mwaka huu kukipiga dhidi ya Simba au Yanga katika mechi maalum zilizoandaliwa na serikali ili kutangaza vivutio vya utalii nchini.

Mwakyembe alisema uongozi wa timu hiyo inayoshika nafasi ya saba katika msimamo wa Ligi Kuu ya England (EPL) ikiwa na pointi 58 baada ya mechi 35, umeweka sharti kwamba utacheza dhidi ya timu itakayoibuka mshindi katika mechi maalum ya kirafiki kati ya Simba na Yanga.

Waziri huyo aliyasema hayo bungeni mjini hapa jana alipowasilisha hotuba yake kuhusu utekelezaji wa bajeti ya wizara yake kwa mwaka huu wa fedha na makadirio ya mapato na matumizi kwa mwaka ujao wa fedha.

Alisema ili kuimarisha michezo na kuvitangaza vivutio vya utalii vilivyopo nchini, mwaka ujao wa fedha wizara yake kwa kushirikiana na Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, itahakikisha inawasiliana na Balozi zilizopo Uingereza, Ufaransa, Ujerumani, Italia, Uholanzi, Ubelgiji, Urusi, China, Japan, Jamhuri ya Korea, Canada na Marekani kwa lengo la kuzikaribisha klabu kubwa za soka za nchi hizo kuja nchini.

"Tayari tuna uzoefu wa ziara ya wachezaji wa kimataifa wastaafu wa timu ya mpira wa miguu ya Real Madrid ya Hispania ambao walicheza na wachezaji wastaafu wa timu yetu ya Taifa jijini Dar es Salaam mwaka 2014 na kupata fursa ya kutembelea vivutio vyetu vya utalii," alisema.

"Ziara ya timu hiyo ilitangazwa dunia nzima kupitia vyombo mbalimbali vya habari ikiwa ni pamoja na CNN, BBC na Supersport.

Alisema ujumbe wa timu hiyo tayari umeshakuja Tanzania mara mbili ndani ya mwaka huu, mara ya kwanza kujadiliana na wizara na kukagua Uwanja wa Taifa na miundombinu yake na mara ya pili kujiridhisha kuhusu ubora wa nyasi za uwanja huo.

UKWELI Mchungu...Tanzania Ilikua Sahihi Kumtimua Bosi wa UNDP..!!!

$
0
0

Katika Gazeti la RAI toleo la tarehe 4 Mei 2017, kulichapishwa makala yenye kichwa cha maneno : ” Tanzania Ilikuwa Sahihi kumtimua Bosi wa UNDP”. Pamoja na mambo mengine, Mwandishi wa Makala hiyo, Abbas Mwalimu, ameandika kama hivi ifuatavyo:

“APRILI 25 mwaka huu baadhi ya vyombo vya Habari viliripoti taarifa ya kufukuzwa nchini kwa Mwakilishi Mkaazi wa Shirikia la Maendeleo la Umoja wa Mataifa (UNDP) Balozi Awa Dabo, Serikali ya Tanzania ilimpa saa 24 kurejea kwao.

Ikumbukwe kuwa, Balozi Awa Dabo aliinza kazi ya kuiwakilisha UNDP nchini Tanzania mwaka 2015, hivyo kuondolewa kwake kunahitimisha safari yake aliyoianza tangu kipindi hicho ndani ya Tanzania.

Makala hii fupi inakuletea maelezo ya kidiplomasia kuhusu kufukuzwa kwa Balozi huyo lengo likiwa ni kuondoa mkanganyiko uliojitokeza juu ya uamuzi huo wa Serikali.

Kabla ya kwenda mbali, ni vema na haki kuieleza jamii Balozi ninayemzungumzia hapa ni yupi? Kwa mujibu wa Ibara ya kwanza ya Mkataba wa Vienna wa mwaka 1961 ambao ulisainiwa mjini Vienna, Austria, mnamo tarehe 18/4/1961 na kuanza kufanya kazi rasmi tarehe 24/4/1961 Balozi ni Mwakilishi aliyetumwa na nchi (Sending State) au shirika au taasisi ya Kimataifa kwenda katika nchi itakayompokea (Receiving State) kwa lengo la kuiwakilisha nchi hiyo au taasisi hiyo au shirika hilo ndani ya nchi hiyo iliyompokea.

Kuna balozi za aina mbili, balozi za kudumu na balozi za nchi na nchi. Balozi za kudumu ni zile zinazofunguliwa na nchi kwenda shirika au taasisi yoyote ya kimataifa, kwa mfano ubalozi wa Tanzania ndani ya New York ambao unaiwakilisha Tanzania katika Umoja wa Mataifa ni Ubalozi wa Kudumu na Balozi aliyeko kule huitwa Balozi wa Kudumu wa Tanzania ndani ya Umoja wa Mataifa. Vivyo hivyo Tanzania ina Ubalozi wa kudumu kule Geneva Switzerland.

Kuna Balozi za nchi na nchi ambazo hufunguliwa kwa makubaliano ya nchi husika na kwa mujibu wa ibara ya pili ya Mkataba wa Vienna wa mwaka 1961. Ufunguaji huu wa balozi kwa mujibu wa ibara ya pili unahusu pia Balozi za Mashirika na Taasisi za Kimataifa kama vile UN, UNDP, FAO, WHO, ILO n.k. Mabalozi wa mashirika na taasisi za kimataifa wataotumwa na mashirika au taasisi kuwakilisha taasisi hizo au mashirika hayo ndani ya nchi iliyowapokea huitwa Wawakilishi Wakaazi. Ubalozi unaofunguliwa na nchi moja ya Jumuiya ya Madola kwenda nchi nyingine ya Jumuiya hiyo huitwa High Commission wakati ule unaofunguliwa kwenda nchi isiyo ya jumuiya ya madola huitwa Embassy.

Kwa mujibu wa Ibara ya tatu ya Mkataba wa Vienna wa mwaka 1961, kazi za balozi zimeainishwa kama ifuatavyo;

Kuiwakilisha nchi (Sending State) au shirika au taasisi ya kimataifa iliyomtuma ndani ya nchi husika iliyompokea yaani Receiving State.

Kulinda maslahi ya nchi (dola), taasisi au shirika lililomtuma ndani ya nchi iliyompokea pamoja na raia wake, bila ya kuathiri mipaka aliyowekewa kwa mujibu wa sheria za kimataifa.

Kujadiliana (ku-negotiate) na serikali ya nchi iliyompokea (Katika mambo mbalimbali yenye maslahi baina yao). Hapa tunaona kuwa Balozi anaweza kusaini mkataba na nchi kwa kumuwakilisha Rais wa nchi husika ambaye amemtuma kumwakilisha ama taasisi husika.

Kuenenda na taratibu zote za kisheria katika kufuatilia yanayojitokeza ndani ya nchi iliyompokea na kutolea taarifa yanayojiri kwa nchi iliyomtuma. Hapa tunaona kuwa mabalozi ndiyo macho na masikio ya marais au wakuu wa Taasisi na mashirika husika yaliyowateua kwenda huko waliko lakini wanatakiwa kufanya kazi zao kwa kufuata sheria na mkataba wa Vienna wa mwaka 1961 ambao unawaongoza.

Kuendeleza mahusiano ya kirafiki kati ya shirika au taasisi au nchi iliyomtuma (Sending State) na nchi iliyompokea (Receiving State) sambamba na kuendeleza mahusiano ya kiuchumi, kiutamaduni na kisayansi.

Kimsingi hizo ndizo shughuli anazofanya balozi yeyote kati ya balozi wa kudumu na yule wa nchi na nchi.

JE NCHI ILIYOMPOKEA BALOZI (RECEIVING STATE) INAWEZA KUMSHITAKI BALOZI ALIYETUMWA KATIKA NCHI HIYO?

Kwa mujibu wa Mkataba wa Vienna wa mwaka 1961 mabalozi wana Kinga (Immunities) na Upendeleo maalumu (Privileges). Ibara ya 22 ya mkataba inaeleza kuwa maeneo yote ya ubalozi pamoja na vinavyotumiwa ikiwemo magari hayaruhusiwi kuingiliwa ama kupekuliwa na nchi iliyopokea. Ibara ya 23 inaelezea kuhusu mabalozi kutoguswa na kodi zozote zinazochajiwa na nchi husika isipokuwa kwa wale wasiohusika moja kwa moja na ubalozi husika.

Ibara ya 24 inazungumzia kuhusu nyaraka zote za balozi kuwa na kinga ya kukaguliwa, wakati ibara ya 26 inawapa uhuru wa kutembea maneno ya nchi iliyowapokea kwa mujibu wa sheria na mkabata wa Vienna. Ibara ya 27 yenyewe imejikita katika kuelezea kinga ambazo njia zote za mawasiliano kama vile simu, mabegi, mifuko n.k kuwa haziruhusiwi kuingiliwa na ndiyo maana viwanja vya ndege vyote vina sehemu zimeandikwa “Diplomats” ikiwa na maana kuwa ni maalumu kwa ajili ya mabalozi na wafanyakazi wa ubalozi wanaotambuliwa na mkataba wa Vienna wa mwaka 1961. Mkataba umeendelea kuelezea hivyo mpaka ibara ya 30.

Ibara ya 31 ibara ndogo ya kwanza ya mkataba wa Vienna wa mwaka 1961 inawapa upendeleo mabalozi kutoshitakiwa ama kutohukumiwa na sheria za nchi iliyompokea (Receiving State), isipokuwa;

kwa suala linalohusu mali binafsi isiyohamishika iliyopo ndani ya nchi iliyompokea, isipokuwa labda awe ameishika kwa niaba ya nchi iliyomtuma. Suala lolote au kitu chochote ambacho balozi amekipokea kutoka kwa mtangulizi na ambacho amehusika moja kwa moja kama mtekelezaji ama muongozaji kama mtu binafsi ambacho hakipo kwa niaba ya nchi au taasisi iliyomtuma.

Kama balozi amefanya mambo yanayohusu taaluma ama kibiashara ndani ya nchi iliyompokea nje ya kazi zake za msingi zilizoanishwa kwa mujibu wa mkataba wa Vienna wa mwaka 1961.

Ibara ya 31 ibara ndogo ya pili inawapa upendeleo maalumu mabalozi pia kutotakiwa kutoa maelezo ya ushahidi mahakamani, huku ibara ndogo ya tatu ikifafanua zaidi ibara ndogo ya kwanza (a), (b) na (c).

Kinga na upendeleo anaopewa balozi yeyote unaishia ndani ya nchi alipotumwa tu yaani Receiving State na kinga hizo na upendeleo huo vinaweza kuathiriwa moja kwa moja na nchi ama taasisi iliyomtuma.

Ibara ya 32, Ibara ndogo ya kwanza hapa ndipo penye swali la msingi la swali letu kwamba je nchi iliyompokea balozi inaweza kumshitaki balozi au mwakilishi mkaazi?

Kwa mujibu wa Mkataba wa Vienna wa mwaka 1961 kinga wanayopewa ndani ya nchi inayowapokea (Receiving State) ambayo imeelezwa kwenye ibara ya 37 ya mkataba wa Vienna ikielezea kinga zote na upendeleo kwa wafanyakazi wote wa ubalozi na ule wa watu wanaonufaika na kinga hizo ama kwa kuwa sehemu ya familia ama kuwa wafanyakazi wa ubalozi toka nchi iliyowatuma (Sending State) kuanzia ibara ya 29 mpaka ya 36 inaweza kuondolewa na nchi hiyo iliyowatuma tu yaani Sending State. Kwa msingi huo tunaona kuwa nchi iliyomtuma balozi yaani Sending State ndiyo ina wajibu wa kumshitaki ama kuruhusu balozi kushitakiwa baada ya kumuondolea kinga na nchi, shirika ama taasisi hiyo iliyomtuma kuiwakilisha.

ILICHOKIFANYA TANZANIA KWA MUJIBU WA MKATABA WA VIENNA WA MWAKA 1961 UNAOHUSU MAHUSIANO YA KIDIPLOMASIA KINAITWA PERSONA NON GRATA

Niseme tu wazi, hakika nimefurahishwa na Msemaji wa Wizara ya mambo ya Nje, Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Kikanda na Kimataifa ndugu Mindi Kasiga alipoulizwa kuhusu sababu za kutomuhitaji mwakilishi mkaazi wa UNDP nchini Tanzania Balozi Awa Dabo alipowaambia waandishi wa habari wawaulize UNDP sababu za kutimuliwa kwa huyo balozi, kwa nini nasema hivi?

Sababu ya msingi ya kufurahishwa nae ni hii; kwa mujibu wa Ibara ya 9 ya Mkataba wa Vienna wa Mwaka 1961 unaohusu mahusiano ya kidiplomasia baina ya nchi na nchi na nchi na mashirika au taasisi za kimataifa inasema hivi:

“Nchi iliyopokea balozi (Receiving State) katika wakati wowote na bila ya kutakiwa kueleza sababu za maamuzi yake, inaweza kuijuza nchi iliyomtuma balozi (Sending State) ama shirika ama taasisi iliyomtuma mwakilishi huyo wa kudumu ndani ya nchi iliyompokea ama mfanyakazi mwingine yeyote aliyeelezwa kwenye mkataba wa Vienna wa 1961 kuwa ni ‘Persona Non Grata’ kwamba mfanyakazi huyo wa ubalozi hakubaliki ndani ya nchi hiyo. 

Neno ‘Persona non grata’ limechukuliwa moja kwa moja kutoka kwenye lugha ya Kilatini ambalo kwa lugha ya Kingereza linaweza kutafsiriwa kama “Person not appreciated” ambapo kwa Kiswahili tunaweza kusema ‘Mtu asiyekubalika ama asiyehitajika’.

Katika hali hiyo nchi au taasisi au shirika lililomtuma balozi linaweza kumrejesha nyumbani ama kuhitimisha shughuli zake za kibalozi. Ifahamike kuwa mtu yeyote aliyeteuliwa kuwa balozi au mfanyakazi wa ubalozi aliyeelezwa kwenye mkataba wa Vienna wa mwaka 1961 kutoka nchi iliyomtuma ama taasisi ama shirika lililomtuma ndani ya nchi hiyo anaweza kutangazwa kuwa ni ‘Persona Non Grata’ au hakubaliki ndani ya nchi hiyo aliyoteuliwa kwenda bila ya hata kufika kwenye nchi hiyo.

Hapa namaanisha kipindi kile cha uteuzi wa balozi, katika hali ya kawaida watu wengi huwa tunahisi uteuzi wa balozi ni kazi rahisi, la hasha. Kuna mambo mengi huwa yanaangaliwa kama vile lugha, mila na desturi za nchi ambayo balozi anaetarajiwa kuteuliwa n.k. Hivyo katika wakati huu ambapo mawasiliano baina ya nchi hufanyika kwa siri mno baina ya wakuu wa nchi ndipo ambapo napo hali ya persona non grata huweza kujitokeza kutokana na vitu kama hivyo nilivyoeleza.

Ibara hiyo hiyo ya 9 ibara ndogo ya pili inaeleza kuwa, “Kama nchi au taasisi au shirika lililomtuma balozi huyo litagoma au kushindwa kutekeleza jukumu la kumtoa ama kumrejesha Persona Non Grata kama ilivyoelezwa kwenye ibara ndogo ya kwanza nchi iliyompokea inaweza kukataa kumtambua muhusika kama mfanyakazi wa ubalozi husika.

Kwa hiyo basi ninapenda kutumia nafasi hii kwa mara nyingine tena kumpongeza msemaji wa Wizara ya mambo ya Nje, Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Kikanda na Kimataifa ndugu Mindi Kasiga kwa weledi alioonesha katika kuliongelea suala hili nyeti kwa nchi na kwa maslahi ya Taifa, pia napenda kuipongeza serikali yetu kwa kufanya kazi kwa weledi wa hali ya juu katika mahusiano ya kimataifa. Mungu ibariki Tanzania, Mungu ibariki Afrika.

MAONI: Kwanza napenda kukubaliana na mwandishi wa makala hii, Abbas Abdul Mwalimu, hasa pale aliposema kuwa Nchi inayopeleka (Sending State) inayo haki kabisa ya kumtimua au kumtangaza Balozi au Mwakilishi yoyote yule kutoka Nchi Inayopokea (Receiving State) kuwa ni ‘Persona Non Grata” au mtu asiyetakiwa nchini hata bila ya kuainisha sababu yoyote ile iliyopelekea kuchukuliwa kwa hatua kama hiyo dhidi ya mhusika. Hii ni haki ya kila nchi yenye mamlaka kamili ya kitaifa kufanya itakavyo kuhusiana na masuala kama haya.

Lakini, kuna jambo moja ambalo lazima lifahamike na kuzingatiwa hapa; nalo ni kuwa ukishamtangaza Balozi au Mwakilishi kutoka nchi au Taasisi iliyoko nje ya nchi kuwa hatakiwi nchini, basi ni vyema, kwa serikali ya nchi inayotimua, ikiwa inataka kufanya hivyo, kutoa sababu inayoingia akilini. Nasema hivi kwa sababu unaposema kuwa Balozi au Mwakilishi kutoka nchi au Shirika fulani amepewa saa 24 kuondoka nchini kwa sababu hana maingiliano mazuri na wafanya kazi walio chini yake, hiyo si sababu nzuri na yenye kuingia akilini; kwasababu mwenye uwezo na mamlaka ya kutathmini utendaji kazi mzima wa Balozi au Mwakilishi anayehusika sio Serikali ya Nchi Inayopokea; hiyo ni kazi ya Serikali au Taasisi ya Nchi Inayopeleka.

Kwa lugha nyingine, Nchi Inayopokea inapaswa kujikita zaidi katika kutathmini na kufuatilia kwa karibu maslahi mapana yanayohusiana na mahusiano na mashirikiano ya kisiasa, kiuchumi na kimaendeleo baina ya Taasisi au Serikali ya Nchi Inayopeleka na Nchi Inayopokea. Na katika hali kama hiyo, Nchi Inayopokea ikiona kuwa vitendo vinavyofanywa na Balozi au Mwakilishi kutoka katika Taasisi au Nchi Inayopeleka vinahatarisha usalama au mahusiano na maingiliano mazuri baina ya pande mbili zinazohusika, basi ni kawaida kabisa kwa Serikali inayohusika kumtaka Balozi au Mwakilishi huyo kuondoka nchini kutokana na vitendo vyake hivyo ambavyo kwa lugha ya kidiplomasia hujuulikana kama “Activities unbecoming or incompatible with his/her diplomatic status”; yaani vitendo vinavyokwenda kinyume kabisa na majukumu yake ya kibalozi.

Ningelipenda kusisitiza hapa jambo moja, nalo ni kuwa bila ya sababu yenye kuingia akilini na kukubalika, si vyema kumfukuza Balozi au Mwakilishi kutoka nchi au taasisi za nje kwa sababu ya kutaka kufukuza au kutimua tu; kwani kufanya hivyo, kunaweza kuleta athari mbaya itakayosababisha Taasisi au Serikali ya Nchi iliyofukuziwa Mwakilishi au Balozi wake nayo kulipiza kisasi kwa kumtimuwa au kumfukuza Balozi au Mwakilishi wa Nchi iliyotimua. Utamaduni huu wa kulipizana kisasi unakubalika kabisa katika ulimwengu wa kidiplomasia na ulikuwa ukifanyika sana wakati wa Vita Baridi baina ya Marekani na Urusi katika miaka ya 60 hadi 80 mpaka pale Ukuta wa Berlin ulipoanguka mnamo mwaka 1989.

La mwisho ambalo ningelipenda kuligusia ni kuwa Mwakilishi wa UNDP, Awa Dabo, hakuwa na cheo cha Ubalozi, na kwa hivyo haikuwa sahihi kumbatiza au kumuita Balozi; kwani vyeo hivi viwili ni tofauti kabisa katika kuzingatia, kulinganisha na kupima darja, hadhi na nyadhifa za kibalozi katika ulimwengu wa kidiplomasia. Kama si zaidi, Awa Dabo alikuwa ni Mwakilishi Mkaazi wa UNDP na sio Balozi.

LISSU: Rais Alipowaambia Waandishi 'Hamna Uhuru Kiasi Hicho' Alishauriwa na Nani..!!!

$
0
0

Tundu Lissu akichangia bajeti habari, sanaa na michezo amesema katiba yetu imeondoa mipaka ya uhuru wa habari na kipindi kuanzia mwaka 2015 uhuru wa habari unakabiliwa na hatari kuliko kipindi chochote,

Amemuuliza waziri wa katiba na sheria kuwa rais aliposema hadharani kuwa waandishi wa habari hawana uhuru kiasi hicho kwa kutangaza habari za migogoro ya wakulima na wafugaji alikuwa ameshauriwa na mtu au ni yeye mwenyewe?

Amesema kuna mambo mabaya yanafanyika lakini wabunge wanayazuia yasihojiwe bungeni ila baada ya muda na wao wataanza kushughulikiwa na hakutakuwa na kelele 

Steve Nyerere: Kuna wasanii wanajifanya wao ni ‘Mungu watu

$
0
0
Muigizaji huyo amedai hakuna mtu wa nje ambaye ataweza kuja kuikomboa tasnia yao ya filamu isipokuwa wao wenyewe.

“Leo hatupo katika umoja, kwanza ili tuweze kufanikiwa mafanikio hayapo ya mmoja mmoja, mafanikio yote duniani yalipita kwa watu ndiyo wewe ukafanikiwa kwa hiyo lazima tukubaliane, tupendane na nyoyo zetu ziwe zimefunguka kwa kufanya vitu vizuri,” Steve alikiambia kipindi cha Enewz cha EATV.

Aliongeza,

“Kuna ma-director wazuri zaidi lakini leo wote hawapo, wanachokikosa ni ushirikiano, tunao ma-director wazuri tu, wanaweza wakafanya kitu kizuri tu ‘site’ lakini ushirikiano hawana, kuna watu wanakuwa Mungu watu haiwezekani, haiwezekani kuwa Mungu mtu jamani Mungu ni mmoja tu,”

Muigizaji huyo amekuwa akipingana na wasanii wenzake wa filamu walioandamana mwezi mmoja uliopita wakiishinikiza serikali kuzifungia filamu za nje ambazo hazilipi kodi kwa madai zinawaharibia soko lao la filamu za ndani.

PATA Tiba ya Asili Kutoka Kwa Mtabibu wa Nyota Maalim Hussein...Una Shida na Mapenzi Au Pesa Hazikai?

$
0
0

Kutana  na Mtabibu Mwenye KUBRI kutoka kwa ALLAH Maalim HUSSEIN Mtabibu wa Nyota za Binadamu na Dawa za Asili ya Africa Mwenye UWEZO Kubaini tatizo lako Pindi tu Utakapo Fanya Mawasilino Kupitia Wasaa Husika..

JE UNASUMBULIWA NA Mapenzi? (Umeachwa na Umpendae,Awe Mume,Mke na Bado unampenda?Na  Umejaribu Sehemu nyingi Bila Mafanikio?Wasilina na Maalim Hussein Ujione muujiza wa Papo kwa Papo.. 

Anauwezo WA KURUDISHA MAHUSIANO NA KUIMARISHA NDOA YAKO NDANI YA SAA 12 TU. 

Umekimbiwa na Mumeo,mkeo au Mpenzi na anaishi na mtu mwingine? Muone akutatulie Anauwezo wa Hali ya Juu wa Kusambalatisha Mahusiano yao Endapo utafata Atakacho kuelekeza, Atamfanya Atimize Ahadi zote kwa Muda Mfupi.

Maalim Hussein Anatumia Jina la Muhusika au Picha Kumaliza Tatizo lako..

Anatibu kwa Kutumia  Vitabu vya QUR-AN Dawa za Asili za Africa,Dawa za Kiarabu na Majini.Anatafsiri Ndoto. Kushinda BAHATI NASIBU, KUSAFISHA NYOTA. Mvuto wa Mwili na BIASHARA, Kinga ya Mwili,ZINDIKO za Nyumba, MIGUU Kufa GANZI, Kufungua KIZAZI kwa wale walio fungwa kwa njia za KISHIRIKINA, Anakupa Jini la Mali kwa yule anaehitaji Utajiri BILA MASHARTI, Nguvu za KIUME, Humaliza Kesi zilishindika ndani ya siku 14 tu..na mengi 

ZaidiWhatsapp +255 674 835107  Au Piga +255746757102

NB: TIBA KWA DINI ZOTE NA IMANI ZOTE...

Kanye West ashangaza mashabiki wake, baada ya kafuta akaunti zake zote

$
0
0
Boss wa kampuni inayotengeneza mavazi ya Yeezy ,ameushangaza ulimwengu kwa kufuta akaunti zake za mitandao ya kijamii.

Kanye ameamua kufuta akaunti yake ya Instagram pamoja na ile ya Twitter. Kufutwa kwa akaunti za rapa huyo kulianza kujulikana siku ya jana baada ya mashabiki zake kushangaa kutomuona kila walipokuwa wakimtafuta kwenye mitandao hiyo.

Mr. West ameamua kujiweka katika maisha ya kawaida hasa kwa upande wa kuonyesha kila anachofanya kupitia mitandao tangu alipotoka hospital mnnamo mwaka jana baada ya kupata stress za kupindukia na kushindwa hata kufanya shows.

Kwa sasa Kanye na Kim wameamua kubadilisha mfumo wa maisha kwa kutopendelea kuonyesha mali zao kwa kuzinadi katika mitandao ya kijamii.

Lowassa Alizwa na Wanafunzi, Maiti 32 zapelekwa Mochwari

$
0
0
Arusha. Waziri Mkuu Mstaafu, Edward Lowassa ametuma salamu za rambi rambi kutokana na tukio la watu 32 kufariki dunia katika ajali ya basi.

Waliofariki katika ajali hiyo iliyotokea leo asubuhi Karatu, ni wanafunzi 29, walimu wawili, pamoja na dereva  wa gari hilo.

“Nimepokea kwa masikitiko taarifa ya ajali hiyo, ni ajali mbaya ambayo inaifanya siku hii kuwa mbaya katika historia ya nchi yetu,”alisema

Miongoni mwa wanafunzi waliofariki ni pamoja na wanaume 11 na wasichana 18.

Kadhalika maiti 32 zikiwamo za walimu wawili, dereva mmoja na wanafunzi 29 zimepokelewa sasa hivi katika Hospitali ya Lutheran Karatu.

Tutaendelea kuwapa habari zaidi kuhusu tukio hili.

Hivi ndivyo Idris alivyoamua kumtania Linah kuhusu ujauzito wake

$
0
0
Baada ya msanii Linah Sanga kuachia picha mtandaoni zinazoonyesha ujauzito wake, mchekeshaji Idris Sultan ameamua kutia neno katika moja ya picha hizo.

Kupitia instagram Idriss ameandika haya machache “best celebrity pregnancy photos Tanzania nzima, shoutout to the baby it is photogenic.

“Ila swali ni moja kama unakaa unatushauri raha tujipe wenyewe alafu unatuacha kwenye mataa hii mimba jinsi ulivyoipata kumbe uliteleza ukadondokea virutubisho eee @officiallinah alafu @director_ghost njoo uone hii picha ya msanii ni kali nilitaka tu uione wala hauhusiki,” aliandika Idriss.


Picha za utupu za mgombea urais Rwanda zavuja mtandaoni

$
0
0
Baada ya siku chache Mrembo Diane Shima Rwigara kutoka Rwanda kutangaza kugombea urais nchini humo,hatimae akutwa na skendo ya kuvujisha picha zake za utupu mtandaoni.

Mrembo Diane 35, ambae ni msomi wa Uchumi na mtoto wa aliyekuwa tajiri maarufu nchini Rwanda Asinapol Rwigara, picha zake za utupu zilianza kusambaa mapema jana nchini Rwanda hususani kwenye mitandao ya kijamii kama WhatsApp na Facebook na baadae kutapakaa Duniani kote.

Kwa mujibu wa mtandao wa Habari Pevu umeeleza kuwa picha hizo zilitumwa awali kwa njia ya E-mail na mtu aliyejiita ni Muandishi wa habari aliyejulikana kwa jina la Twahirwa Emmy huku akishinikiza kuwa mrembo huyo hafai kuchaguliwa kuwa Rais kwa vitendo vyake  vichafu vya kupiga picha za utupu.


Hata hivyo Jitihada za kumpata mrembo huyo kuzungumzia picha hizo zilizovuja ziligonga mwamba baada ya waandishi wa habari nchini Rwanda kumsaka bila mafanikio.

Uchaguzi mkuu wa Rais nchini Rwanda unatarajiwa kufanyika mwaka huu mwezi wa Augosti, na mpaka sasa kuna wagombea watatu tuu ambao ni Mpayimana Philippe ambae ni mgombea binafsi na Franck Habineza kutoka chama cha Green pamoja na Diane Rwagira wote wakitarajiwa kuleta upinzani mzito kwa Rais Paul Kagame .

Wanafunzi 31 wathibitishwa kufariki katika ajali Arusha

$
0
0
Arusha. Kamanda wa Polisi, mkoa wa Arusha, Charles Mkumbo amesema wanafunzi 31 na walimu wao wamefariki katika ajali iliyotokea wilayani Karatu, ulipo mto Mlera.

Mkumbo ambaye yupo njiani akielekea wilayani Karatu amesema wanafunzi waliopoteza maisha katika ajali hiyo ni wa shule ya mchepuo wa Kiingereza, iitwayo LackVicent ya mjini Arusha.

Taarifa zaidi kuhusu tukuio hili zitaendelea kuwekwa hapa katika chumba cha habari cha kidijitali, MCL.
Viewing all 104756 articles
Browse latest View live




Latest Images