Quantcast
Channel: UDAKU SPECIAL
Viewing all 104756 articles
Browse latest View live

FUVU na Mifupa(Skull and Bones) Jamii ya Siri ya Kishetani Inayoongoza Matukio ya Duniani..!!!

$
0
0

Tarehe 10 February mwaka 2017 ilikuwa ni siku ya kutimiza miaka 100 tangu kifo cha Geronimo ambaye alikuwa ni shujaa kutoka Jamii ya Apache( hawa ni mashujaa wa wahindi wekundu au wakazi asilia wa Taifa la marekani maarufu kama Red Indians) Ndugu mmoja katika jamii hii alifungua mashtaka akiwashtaki Skull and bones jamii ya Siri ambayo ilianzia chuo kikuu cha Yale huko marekani kuwa iruhusika na kuiba mabaki ya Geronimo. Miaka kadhaa imekuwa ikipigiwa kelele jamii hii ya Fuvu na Mifupa kuwa imeshikilia mabaki ya Geronimo ikiyatumia kwa shughuli zake za kiimani.

Haryln Geronimo mwenye miaka 61 anasema “ naamini kabisa toka moyoni mwangu kuwa roho ya Geronimo haikuachiliwa” akiwaambia waandishi wa habari waliokusanyika wakifuatilia tukio hili lililohusisha jamii hii ya Skull and Bones. huyu ni kitukuu cha Geronimo .

Inasemekana kuwa Wakongwe Kama Prescott S. Bush ambaye ni baba wa Aliyekuwa Rais George W. Bush na Babu wa George W. Bush . huyu na wenzie wengine wanachama wa Skull and Bones walichimba mabaki ya Geronimo toka kaburini mwaka 1918 WAKAIBA FUVU LA HUYU SHUJAA, NA MIFUPA MIWILI na mavazi ya kivita kutoka katika Kaburi lake huko Fort Sill ( Ujue kuwa hizi imani za kuchimba makaburi na kuiba vitu flan zipo hata kwa wazungu si afrika tu ) na jamii hii ikachukua mabaki haya na kuyaweka Makao yao Makuu ambayo yalikuwa yameanzishwa toka mwaka 1832.

Conspiracy Mbalimbali Kuhusiana na Skull and Bones

Kuna mambo mengi ambayo yamekuwa yakizungumzwa kuhusiana na kundi au jamii hii. Inasemekana hawa ndio waliohusika na utengenezaji wa bomu la nyuklia mpaka kuuawa kwa J.F. Kennedy. Ni kundi ambalo wengi nchi za huku kwetu hawajalifaham lakini kwa Huko kwa wenzetu ni Kundi kubwa na la kutisha sana. Hili ni Kundi lenye viongozi wakubwa sana duniani likihuishwa na miaka ile lilipokuwepo kundi la mafia.. kuwa hili ni kundi la mafia la kimataifa.

Skull and Bones wamehusika na Ku endesha Utajiri wa Carnegie, Rockefeller na Familia ya Ford na pia kujihusisha na CIA, American Psychological association , Baraza la Mahusiano ya Kimataifa na pia Baadhi ya Makampuni makubwa ya Sheria Kimataifa.

Mwaka 2004 wakat wa uchaguzi wa Urais waliokuwa wagombea wa Republic na Democratic walikuwa ni wanachama wa jamii hii. Ingawa haya hayakusemwa sana maana ilikuwa ni siri. Johnn Kerry alipoulizwa jambo hili alijibu kifupi tu kuwa “ni siri na siwezi zungumzia jambo hilo” na Bush W. naye pia alipata kuzungumzia hili kwa hali ya kutotaka liendelee kuwa gumzo hivyo kwa Kiswahili kingine ni kuwa alilipotezea. Uhusika wa watu katika Jamii hii ni wa siri sana.

William Russell alikuwa mwanafunzi wa chuo kikuu cha Yale. Huyu ndiye aliyeanzisha jamii hii ya kishetani yenye nguvu kubwa bada ya kuwa aliwah kukaa Ujeruman akiwa mwanchama wa kundi moja la siri sana duniani likiwepo kundi pia la ILLUMINATI. Rusell alirudi USA akiwa amedhamiria kuanzisha jamii ya siri ya aina yake na akamwambia Alfonso Taft ambaye mtoto wake alikuja kuwa Rais William H. Taft kuwa mmoja ya wanachama wa Kundi hili la Udugu wa Kifo “The Brotherhood of Death” ambalo baadaye ndo likaja kufahamiaka kuwa ni “The order of Skulla and Bones” wanachama walikuwa wakimuabudu Eulogia huyu ni mungu ambaye inasemekana alikuwa na nguvu za kufanya mtu awe na nguvu ya kuongea mbele za watu na kukubalika, kutukuzwa na kuwa mwenye Umiliki wa Dunia.

Fuvu na Mifupa ilianzishwa chuo kikuu cha yale ambacho ni cha Tatu kwa Uzaman Huko Marekani kwa maana ya kuwa ni chuo cha zamani sana katika namba ya vyuo vya zaman usa kinashika namba tatu. Jamii hii imekuwa n ibada zake na mambo mablimbali ambayo yamekuwa ni alama zao I pamoja na nyoka na kutoka sadaka zao kwa mungu wao maybe actually ni shetani ila kwa jina linguine. Wanachama wa kundi hili hupatikana kwa njia ya siri sana na wala huwezi ona matangazo au mtu akijitangaza kuwa yeye ni wmanachama wa kundi hili. Baadaye hupelekwa sehemu ya ibada yao kwa ajili ya kufanyiwa ibada ya kuapishwa kuwa atakuwa mwanachama mwaminifu mpaka kufa.

Wengi wamekuwa wakisikia habari za freemason na illuminati, kundi hili ni kubwa sana na lenye nguvu kubwa sana kiuchumi na kiutawala duniani. Umakini wao umewafanya waendelee kuwa kimya pasipo kujulikana sana kama yalivyo makundi mengine. Na bado limekuwa likihusika sana katika makundi mengine kwa nia ya kujitanua na kujipa nguvu.

Hii dunia tunaishi ila kuna watu wanaiendesha na kupanga matukio mbalimbali. Kuna watu wanaamua nani awe rais na kwa sababu zao wao. Ni mambo machache sana ambayo yanatokea pasipo watu flan kuwa wamepanga yawe.

Wimbo mpya Wa darasa umedhihirisha kuwa ile ngoma ya Muziki alibahatisha

$
0
0
Darasa ametoa ngoma mpya ambayo kwa kweli imedhihirisha kuwa msanii huyu hana kipaji cha kutunga mashairi mazuri. Si hivyo tu ngoma hii imetoa picha kuwa msanii huyu siyo mbunifu kwani ngoma hiyo inaelekea kufanana na ngoma ya muziki

Video kali sana ila audio kuna muda nahisi nasikiliza Muziki....

RAIS Magufuli Atuma Salamu za Rambirambi kwa Wazazi wa Wanafunzi 32 Waliofariki na Ajali ya Basi Leo Arusha..!!!

$
0
0

Rais John Magufuli ametoa salamu za rambirambi kwa Mkuu wa Mkoa wa Arusha, Mrisho Gambo wanafamilia, ndugu, jamaa na marafiki kwa vifo vya wanafunzi, walimu na dereva vilivyotokea leo saa 3.00 asubuhi baada ya gari walilokuwa wakisafiria kupata ajali katika eneo Rhotia Marera, Wilaya ya Karatu Mkoani Arusha.

Rais Magufuli amepokea kwa mshtuko na masikitiko makubwa taarifa ya vifo hivyo  vya wanafunzi 32 wa darasa la saba, walimu 2 na dereva wa gari la shule ya msingi iitwayo Lucky Vicent ya Arusha.

Wanafunzi na walimu hao walikuwa wakitoka shuleni kwao kwenda shule ya msingi iitwayo Tumaini kwa ajili ya kufanya mtihani wa ujirani mwema na walipofika katika eneo la Rhotia Marera basi walilopanda liliacha njia na kisha kutumbukia korongoni ambako limesababisha vifo hivyo na majeruhi watatu.

Kufuatia ajali hiyo, Rais Magufuli amemtumia salamu za rambirambi Gambo na kueleza kuwa ajali hiyo imezima ndoto za watoto waliokuwa wakijiandaa kulitumikia Taifa na imesababisha uchungu, huzuni na masikitiko makubwa kwa familia za marehemu na Taifa kwa ujumla.

“Mkuu wa Mkoa wa Arusha, Mrisho Gambo naomba unifikishie pole nyingi kwa wazazi, ndugu, jamaa na marafiki wote wa wanafunzi, walimu na dereva waliopoteza maisha, hiki ni kipindi kigumu kwetu sote, na uwaambie naungana nao katika majonzi na maombi.

“Muhimu kwa sasa tuwaombee marehemu wote wapumzishwe mahali pema, majeruhi wapone haraka na wote walioguswa na msiba huu wawe na moyo wa subira, ustahimilivu na uvumilivu katika kipindi hiki kigumu,” amesema Rais Magufuli.

LOWASSA na Maalim Seif Wakutana Faragha Kumjadili Lipumba..!!!

$
0
0

Waziri Mkuu Mstaafu, Edward Lowassa amekutana na Katibu Mkuu wa CUF, Maalim Seif Sharif katika ofisi ya Lowassa  iliyopo Mikocheni jijini hapa leo mchana.

 Katika mkutano huo  Lowassa na Maalim  wamejadiliana masuala ya siasa ikiwamo migogoro ya ndani ya CUF na namna ya kuimarisha umoja na mshikamano wa umoja wa vyama vya upinzani.

Maalim Seif, ni Makamu wa Kwanza wa Rais mstaafu wa Zanzibar na Lowassa ni mjumbe wa kamati kuu ya Chadema.

RASMI..Bodi ya Ligi Yainyang;anya Simba Sc Pointi Tatu za Chee Walizopewa Toka kwa Kagera Sugar..!!!

$
0
0

Bodi ya Ligi ya Shirikisho la Soka Tanzania (TFF) imewajibu rasmi Simba SC juu ya sakata lao la kupokwa pointi tatu za mezani walizopewa baada ya rufaa yao dhidi ya Kagera Sugar wakidai kumcheza mchezaji Mohamed Fakhi akiwa na kadi tatu za njano.

Kwa mujibu wa barua kutoka katika Bodi ya Ligi zimesema kuwa Fakhi hakuwa na kadi tatu za njano wakati akicheza mchezo dhidi ya Simba uliofanyikia uwanja wa Kaitaba, Bukoba Aprili 2 mwaka huu.

"TFF ambayo ndiyo yenye dhamana ya usimamizi wa mpira nchini na ambayo ndiyo iliyokaimu madaraka kwa TPLB kuendesha ligi kuu iliitisha kikao cha Kamati ya Sheria na Hadhi za Wachezaji ambayo ilichunguza kwa undani sakata hili na baada ya uchunguzi wao ambao walihoji watu mbalimbali, walituandikia kutujulisha kuwa wamebaini mchezaji Mohamed Fakhi anayelalamikiwa na Simba hakuwa na kadi 3 siku ya mchezo wa Kagera Sugara dhidi ya Simba hivyo alikuwa halali kucheza mchezo huo". Ilisema barua hiyo

UKWELI Mchungu...NIANGALIE Bongo Movie Kweli? Si Ni Bora Niperuzi Zangu Instagram..!!!

$
0
0

ZIPO nyakati ukirudisha kumbukumbu nyuma na kuangalia wapi Tanzania imetoka katika tasnia ya filamu na Muziki unaweza kutikisa kichwa kwa uchungu au kwa furaha. Vyote vinawezekana.

Mwanzoni mwa miaka ya 2000 hakuna ambaye alisikiliza muziki wa Nigeria hakuna msanii wa Nigeria aliyekuwa staa hapa kwetu kumshinda Juma Nature, Profesa Jay, Lady Jide wala Mr Paul.

Zaidi wenye kupenda muziki walisikiliza ngoma kutoka Marekani kwa wakali waliokuwa wakitamba kama Sean Paul, Jay Z, Madonna, Shaggy na R Kelly. Sentensi rahisi Nigeria hawakua na maajabu ya muziki.

Lakini ni wazi katika upande wa pili wa Sanaa kwa maana ya filamu walikuwa wapo mbali sana, hatukuwa daraja moja nao, walituacha maili nyingi na kila kitu walichofanya kilikuwa kigeni kwetu.

Wakati ambao Desmond Elliot, Mama G, Omotola Jalade, Ramsey Noah na Emeka Ike wakiwa wasanii maarufu na kanda za filamu zao zikiuzwa kwa wingi katika maduka yetu Kariakoo, sisi bado tulikuwa bize tukiangaika na tamthilia zetu za saa tatu usiku, Jumamosi, Jumapili na Jumatatu.

Tulikuwa nyuma maili 10 ya walipokuwa wenzetu, haikushangaza pale filamu zao za kichawi zilipotufanya tujenge imani ya kwamba Wanaigeria ni wachawi kuliko watu wote Afrika (inawezekana ikawa kweli ).

Aina ya filamu zao za kichawi ikatufanya hata sisi kuiga stori na staili zao, ushahidi upo katika filamu ya Nsyuka, Safari.

TOA NIGERIA, WEKA BONGO MOVIE

Mapambano ya wasanii wa filamu mwanzoni yalikuwa makubwa, watu waliumiza vichwa kuhakikisha wanatoka kuigiza michezo ya kwenye TV na kuja kuteka na kuzipoteza kabisa filamu za Nigeria.

Tukumbuke kabla ya hapo Muziki wa Bongo Fleva ulishateka rasmi mashabiki, wasanii wao walikuwa mastaa wakubwa ndani na nje ya Nchi, wakasumbua kwenye Media zote.

Wapo waliofanikiwa na kujenga maisha yao, wapo waliopata umaarufu ukawalevya na kujikuta wakidumbukia shimoni, wapo waliomiliki wanawake wazuri, nyumba na magari ya gharama.
Muziki ulikuwa mali kushinda Filamu.

Girlfriend ikawa filamu ya kwanza kufanya mapinduzi ya sanaa ya maigizo nchini, hatimaye taratibu watu wakaanza kujaribu kufanya kile kilichowapa umaarufu akina Genevieve Nnaji nchini kwetu.

Ray na Kanumba kwa ushirikiano wa Game 1st Quality wakatushtua na filamu kali ya Johari ile hatujakaa sawa wakatuchapa na Sikitiko la Moyo, mwisho filamu zikaiteka Bongo.

Kila mtu akanogewa na filamu zetu za ndani na kuanza kusahau kuhusu ‘movie za kichawi’ za Kinigeria.

Ray, Kanumba, Johari na Mainda wakaiteka Bongo na stori kuhusu Ramsey Noah, Jim Iyke ikaanza kupotea taratibu. 

Bongo movie ikaota mizizi, kwa ubora wa kazi zao ikamea vichwani mwetu.

FILAMU ZIKAICHAPA KO MUZIKI

Pamoja na kwamba muziki ulianza kukiki mapema kabla ya filamu lakini ni wazi baada ya Kanumba na ‘nduguye’ Ray kuamua kuwekeza kwenye filamu walifanikiwa kugeuza vichwa vya mashabiki ambao walianza kununua kazi zao huku wakiwapa utayari ‘tention’ kulinganisha na muziki.

Filamu zikateka kila kona na hata wasanii wake wakapata umaarufu mkubwa kuliko ule waliokuwa nao Bongo fleva.

Nani amesahau namna ambavyo ziara ya Kanumba, Ray, Johari na Irene Uwoya kule Rwanda na DR Congo walipokuwa wakitamba na filamu yao ya Oprah?

Mapokezi waliyoyapata katika ziara hizo yalionesha namna gani filamu inapiga hatua nje ya Nchi, maandamano ya pikipiki, magari na miguu yaliyofanywa na watu wakati walipoenda kuwapokea uwanja wa Ndege yalikuwa mageni kwetu.

Filamu ilitikisa Bongo bwana! Hakuna ambaye hakutaka kumtazama Kanumba, kila mmoja alitamani kusikia Ray angekuja na kali gani, alipotoka JB na swahiba wake Richie Richie kila mtu aliangaika kupata nakala ya CD zao.

Kabla ya kifo cha Kanumba hakuna ambaye aliangaika kusema filamu za Nje zifungiwe mara zizuiwe sijui kodi na lugha nyingine zisizoeleweka, ubora wa kazi ulikuwepo, mashabiki walizitamani filamu za nyumbani.

Ni ukweli mtupu kabla ya kifo cha Uncle JJ Bongo Movie ilitamba kuliko Bongo Fleva, kama ni ngumi muziki ulikuwa umepigwa TKO.

BONGO MOVIE IPO ‘ICU’

Nilicheka kwa dharau niliposikia eti Bongo Movie wanaandama wakiongozwa na ‘fulani’ eti kushinikiza Serikali izuie filamu za nje kuingia nchini eti kwa sababu kodi za movie za nje hazikatwi kama za kwao.

Eti lengo likiwa ni kuwataka Watanzania kusapoti filamu zao na siyo za nje, huku ni kuishiwa kwa mawazo yakinifu kwa watu wanaounda tasnia hiyo.

Hivi hii ndio Bongo Movie ambayo ilipiganiwa na watu zaidi ya miaka 20 nyuma? Bongo Movie ile iliyofanikiwa kuteka filamu za Nigeria kabla ya kuzifurumishia mbali?

Bongo Movie ile ambayo iliwafanya Ray, Uwoya na Kanumba kupata mapokezi ya kifalme Congo, Rwanda na Burundi kuwashinda marais wa Nchi hizo?

Aibu kubwa sana aibu ambayo mwili wa Steven Kanumba uliolala pale Kinondoni unaweza kutikisika.

Yaani kwa uzembe wao wenyewe wameharibu Soko la filamu zao wenyewe na sasa wanataka huruma ya mashabik!

Hivi JB huyu wa sasa ni yule aliyecheza Swahiba na Regina? Stori tamu zinazosisimua zimeenda wapi? Ray bado unajiita The Greatest? Kama jibu ndio tafadhali liondoe hilo jina.

Hakuna ubunifu katika filamu za siku hizi, kila siku mastaa ni wale wale, Dada zetu warembo ndio wanaocheza katika nafasi nzuri kila filamu, nyumba na magari wanayotumia hayabadiliki.

Haishangazi kuona hivi sasa wamekimbilia Muziki na kutoka kimapenzi na Wabongo Fleva, haishangazi siku hizi wanatumika kisiasa, hainishangazi pia kuona siku hizi mashabiki wanapenda kufuatilia Instagram akaunti ya Uwoya, Wolper, Ray kuliko kuuliza filamu zao mpya zinatoka lini.
Aibu yetu aibu yao wenyewe! Hivi Wema Sepetu bado unaigiza?
\
Kwa maoni 0713 153035

UTEJA wa Simu Wamponza Bibi Harusi, Atalakishwa Saa Chache Baada ya Ndoa kwa Kuchat Usiku Mzima..!!!

$
0
0

Matumizi ya simu za mkononi hupelekea mtu unayekuwa karibu naye kimwili kuwa  mbali nawe kiakili na mawazo ambayo ameyaelekeza kwa mtu anayewasiliana naye muda huo. Balaa zaidi ni ‘kuchat’ ambapo mtumiaji wa simu hupelekea hisia zake zote kwenye vidole vinavyoandika huku akimuacha aliyenaye akiwa mpweke.

Hii imemgharimu bibi harusi aliyekesha akipokea salamu za pongezi kwenye simu na kumsahau mumewe. Fuatilia kisa hiki…!

Mwanaume mmoja ameamua kumtalakisha mkewe saa chache baada ya kufunga ndoa, kwasababu mkewe huyo mpya alitumia usiku wao wote wa ‘fungate’ kuchat na rafiki zake.

Kwa mujibu wa gazeti la Al Watan la Saudi Arabia, bibi harusi huyo alikuwa busy akipokea salamu za pongezi kutoka kwa rafiki yake akimsahau mumewe aliyenaye chumbani muda huo.

“Bwana harusi alijaribu kusogea karibu naye na kimahusiano, lakini alishitushwa kuona mkewe anampotezea, hajibu anachoulizwa au hata kuonesha vitendo,” ndugu wa Bwana harusi aliiambia Al Watan.

“Mwanaume alipomuuliza kama rafiki zake ni muhimu kuliko yeye, alimjibu ndio,” walisimulia mkasa walioelezwa na bwana harusi.

Mahakama ya mwanzo katika eneo hilo imejaribu kuwasuluhisha ili waendelee na ndoa yao, lakini mwanaume ameendelea kushikilia msimamo wake wa talaka.

AJABU: Njemba Yafunga Ndoa na ‘Simu Yake’ Kanisani..!!

$
0
0



Dunia ina mambo, na ukiyashangaa haya jiandae kuyastaajabia yajayo..!

Mwanaume mmoja aliyejitambusha kwa jina la Aaron Chervenak mwenye umri wa miaka 34 na mkazi wa Los Angeles nchini Marekani, amefanya tukio la aina yake baada ya kufunga ndoa kanisani na simu yake ya kupapasa (smartphone).

Mwanaume huyo alisafiri hadi Vegas kulisaka kanisa moja ambalo lilimkubalia kufunga ndoa na simu yake na kula kiapo kama ambavyo alipaswa kula kiapo kwa mrembo aliyeyagusa maisha yake na kuamua kumfanya mkewe wa maisha.

Akizungumzia sababu zilizopelekea yeye kufanya tukio hilo, kupitia makala maalum ya ndoa yake hiyo, Aaron alisema kuwa ameamua kufanya hivyo kwa sababu ya ukweli kwamba simu zimekuwa zikichukua nafasi kubwa ya mapenzi na uhusiano na zikifanya jukumu kubwa la kuwatuliza watu katika dunia hii.
“Kama tutakuwa wakweli, tunaunganishwa na simu katika viwango vingi vya hisia. Tunaikimbilia kututuliza, kutulaza usingizi, kuweka unafuu kwenye mawazo yetu. Na kwangu, huo ndio uhusiano nilionao na simu yangu hii,” alisema Aaron.

“Kwa mantiki hiyo, simu yangu hii imekuwa na uhusiano wa muda mrefu na mimi na ndio maana nimeamua kufunga nayo ndoa,” aliongeza.

Kuhusu jinsi alivyokubaliwa kufanya tukio hilo kanisani, alisema kuwa alijaribu kuwasiliana na uongozi wa kanisa hilo kuona kama angeruhusiwa lakini alihakikishiwa kuwa anakaribishwa kwa mikono miwili.

MAMBO 5 ya Maajabu ya ‘Tendo la Ndoa’ Unayopaswa Kuyafahamu 18+..!!

$
0
0

Tendo la ndoa limezungukwa na mambo mengi sana ambayo hata wataalam wa mahusiano na madaktari bingwa wameshindwa kuyamaliza. Tafiti mbalimbali zimekuwa zikija na matokeo mapya na hata kubadili matokeo ya tafiti za awali kutokana na muda husika.

Leo, nimeamua kukueleza kuhusu mambo matano tu kati ya hayo mengi, unayopaswa kuyafahamu kwa ajili ya ufahamu wako tu lakini pia kwa afya yako ili yakusaidie katika maamuzi unayochukuwa unapokuwa eneo la tukio au unapopanga kufanya tukio hilo. Hii imewalenga zaidi watu walio kwenye ndoa na kuwaandaa wanaotaka kuingia kwenye ndoa.

Kumbuka tendo hili ni ‘la ndoa’. Najua hii ngumu kumeza!

Mwanaume hutoa mbegu hadi milioni 300 kwa tendo moja tu la ndoa, lakini mbegu moja pekee hutumika kuzalisha mtoto inapokutana na yai la mwanamke lililotayari.

Kufika kileleni kwa mwanamke ni msaada mkubwa kiafya kwake. Huweza kumsaidia mwanamke kupunguza hatari zaidi ya kupata magonjwa ya moyo, kupooza, kansa ya matiti pamoja na msongo wa mawazo.

 Mwanamke anapokuwa kileleni hukaa takribani sekunde 20 hadi 14, tofauti na wastani wa mwanamme ambaye hukaa kwa wastani wa sekunde 6 tu. Hata hivyo, tofauti na mwanamke, mwanaume anapokuwa kileleni hupitiwa na giza zito katika ubongo wake kwa sekunde takribani tatu (blackout).

4. Tendo la ndoa hupunguza maumivu ya kichwa.

-Utafiti uliofanywa na wa wataalam wa saikolojia na uhusiano kutoka Chuo Kikuu cha Munster chini Ujerumani umebaini kuwa tendo la ndoa husaidia kupunguza maumivu ya kichwa. Utafiti huo uliochapishwa mwaka 2013, ulibaini kuwa mtu mmoja kati ya watano waliofanya mapenzi wakiwa na maumivu ya kichwa, alimaliza akiwa hana maumivu hayo tena.

Kwenda haja ndogo muda mfupi kabla ya tendo la ndoa ni hatari zaidi kwa afya.

-Ingawa wataalam wengi wa afya wamekuwa wakieleza kuwa kwenda haja ndogo kabla na ya tendo kunasaidia kuepuka ugonjwa wa UTI, huu sasa unatajwa kuwa ‘nusu ukweli’.

UTI hutokea pale kibofu cha mkojo kinapopata bakteria wanaoingia kupitia njia ya mkojo. Na tendo la ndoa linaweza kusaidia maambukizi wa bakteria hao kuwatoa kwa mtu mmoja kwenda kwa mtu mwingine.

Kwa mujibu wa Dk. David Kaufman wa New York Marekani, kwenda haja ndogo kabla ya kufanya tendo la ndoa ndio chanzo cha kupata athari kubwa zaidi ya bakteria ikiwa kutakuwa na maambukizi.
Alieleza kuwa kwenda haja ndogo kunasaidia kuweka nafasi kubwa zaidi kwenye kibofu cha mkojo kiasi cha kutunza bila kusumbuliwa, bakteria wengi zaidi.

Hata hivyo, ni salama zaidi kwenda haja ndogo muda mfupi tu baada ya kufanya tendo la ndoa kwasababu inasaidi ku-flash bakteria kwa kiaisi kikubwa waliotokana na tendo la ndoa (sio virusi vya ukimwi).

SEHEMU 4 za Mwili Usizopaswa Kumshika Mkeo Nyakati Hizi 18+..!!!

$
0
0

Ingawa kuna mtazamo uliojengeka katika jamii kuwa ukishamuoa mwanamke na mkawa mwili mmoja basi una kila haki ya kumshika sehemu yoyote uipendayo hasa wakati unahitaji kufanya nae tendo la ndoa.

Lakini utafiti na uzoefu uliokusanywa na wataalam wa mahusiano na ndoa waliofanya mahojiano na wanawake kama kuna sehemu wazisopenda kuguswa na waume zao na nyakati husika, umetoa picha na mtazamo ambao wanaume wanapaswa kuufahamu mapema kabla hawajaingia katika hatari ya kuwa kero au kuwakwaza wake zao.

Kama tunavyofahamu, wanawake ni viumbe wenya mlango mmoja wa ziada wa fahamu kuwapita wanaume. Hii nitaizungumzia siku nyingine. Lakini mlango huu wa ziada ndio huwapa hisia ya ziada pamoja na kuwafanya kujali sana vitu ambavyo mwanaume hasa mwenye haja ya kufanya tendo anaweza asizingatie sana anataka kukidhi haja yake.

Ukifuatilia sehemu hizi za mwili wa mwanamke nitakazozitaja na nyakati zake, utabaini kuwa ni rahisi sana kufahamu kwani mwanamke katika nyakati hizo anaweza kuonesha kusita sana wakati anataka kuguswa.

1. Chuchu wakati miili yao inaendelea na shughuli nyingine za ndani

Idadi kubwa ya wanawake huwa hawapendi kuguswa na wanaume chuchu zao wakati wananyonyesha au wakati wako katika hedhi. Hiki ni kipindi ambacho kama mwanamke ananyonyesha na mwanaume anataka kumgusa sehemu hiyo basi maziwa yanaweza kutoka kwa kasi na kumfanya ajisikie hayuko ‘confortable’ kuendelea na zoezi la kushiriki tendo.

2. Kwapani wanapokuwa wanatoka jasho kabla ya kuoga

Wanaume wengine huwa na hisia za matamanio zaidi wanapoyaona makwapa ya wake zao. Hii ni hali ya kisaikolojia inayojengeka kwa baadhi japo sio wengi. Kuna wanaume wakiona kwapa la mwanamke basi matamanio yao huongezeka mara dufu. Lakini wanawake wengi wameeleza wazi kuwa hujisikia vibaya na kukosa amani pale wanaume zao wanajaribu kuwashika kwapani wakati ambapo wametokwa jasho.

3. Sehemu za siri kabla ya kuoga

Hili ni eneo ambalo wanawake wengi wameonesha kulalamikia waume zao. Kwa mazoea wanaume wengi huwa kama wanawabaka wake zao bila kufahamu, hasa pale wanapotoka safari zao wakiwa na matamanio. Lakini wanawake wengi wameeleza wazi kuwa hupoteza hali ya kuwa ‘comfortable’ pale wanapoguswa na wanaume zao sehemu za siri wakati bado hawajaoga.

Wanaume wengi hujikuta wakishiriki tendo la ndoa na wake zao ghafla baada ya kukamilisha kazi kadhaa za ndani wakati wanawaangalia. Wanaume wanaweza kuwa wanafurahia zaidi tendo hilo lakini wanawake pamoja na kwamba hufurahia pia lakini mlango wao wa ziada wa fahamu huwafanya kukosa amani kwa kiasi fulani wakati wa tendo ukilinganisha na nyakati ambazo wanajiamini ni wasafi.

4. Nywele zao dakika chache baada ya kutoka saloon kujiremba

Ingawa unaamini kuwa mkeo alienda saloon kujiremba kwa ajili ya kukuvutia wewe, usithubutu kutaka kuzivuruga nywele zake dakika chache baada ya kutoka kwa mtaalam wa kutengeneza nywele, hata kama pesa aliyotumia ulimpa wewe.

Hiki ni kama kituko hivi, lakini ndio ukweli. Wanawake hutumia muda mrefu sana kwenye vibanda au saloon za gharama kwa ajili ya kujiremba ili waongeze mvuto. Lakini, hugeuka kuwa walinzi wa vichwa vyao angalau kwa saa kadhaa. Msifie uwezavyo, lakini nywele zake usizivuruge mapema mtaharibiana ‘mood’.

Haya ni kati ya mambo machache ambayo wanaume huyaona madogo sana na kufuatilia yale wanayoamini ni makubwa zaidi. Lakini mambo haya ni kati ya machache yanayokwangua taratibu kuta za hisia za mwanamke kwa mmewe.

FAIDA ya Kuvaa Socks Miguuni Wakati wa Tendo la Ndoa..!!!

$
0
0

Utafiti uliofanywa na jopo la watafiti wenye utaalam wa masuala ya uhusiano na saikolojia wa Chuo kikuu cha Wageningen nchini Uholanzi umebaini faida za kushiriki tendo la ndoa ukiwa umevaa socks miguuni.

Bila shaka utakuwa umewahi kuona picha za watu wanaotengeneza taswira ya wanandoa wakiwa kitandani na socks miguuni. Huenda waliuamini utafiti huu na baada ya kujaribu wakaona unazaa matunda wayatakayo.

Katika utafiti huo, waligundua kuwa uvaaji wa socks miguuni kwa wanaume na wanawake kunaongeza ari zaidi na uwezekano wa kufika kileleni kwa haraka na mshindo wa nguvu zaidi kutoka 50% (kabla ya kuvaa socks) na 80% (baada ya kuvaa socksi).

Utafiti huo ulizaliwa kutoka kwenye ule wa awali ulifanywa mwaka 2011 na Chuo Kikuu cha Johns Hopkins. Watafiti wa Johns Hopikins walikuwa wakijaribu kuusoma ubongo wa binadamu wakati akishiriki tendo la ndoa, kujua madhara ya kisaikolojia na kimwili anayoyapata wakati anapofika kileleni.

Wakati wakiendelea na na zoezi hilo, watu waliokuwa wanatumika kama sampuli wakifanya mapenzi, walilalamikia hali ya ubaridi ndani ya chumba chenye ‘scanner’ ya ubongo. Ndipo watafiti hao walipoamua kuwavalisha socks miguuni. Ghafla uwezo wao katika tendo hilo ulipanda kutoka 50% hadi 80% za kukifikia kilele kwa kishindo zaidi.

Nao watafiti wa Chuo Kikuu cha Wageningen wamebaini kuwa kuiweka miguu pekee kwenye hali ya joto kupitia socks, kunaongeza kwa asilimia za za ziada 30.

HALI Mbaya ya Uchumi Yapelekea Benki Tatu Kubwa Nchini Kuwa Hatarini Kufungwa..!!!

$
0
0

Hali ya mtikisiko wa uchumi uliozikumba taasisi nyingi, hasa za fedha sasa unazinyemelea benki tatu ambazo zinaweza kuwekwa chini ya uangalizi maalumu wa Benki Kuu ya Tanzania (BoT) kama ilivyokuwa kwa Twiga Bancorp.

Twiga Bancorp, ambayo kwa sehemu kubwa inamilikiwa na Serikali, imewekwa chini ya uangalizi wa BoT baada ya madeni yasiyolipwa (NPL) kuzidi kiwango kinachotakiwa kisheria.

Hali hiyo inazinyemelea taasisi nyingine tatu za fedh; Benki ya Wanawake (TWB), ambayo pia inamilikiwa na Serikali, Ecobank Tanzania na Efatha Bank, ambayo inahusishwa na taasisi ya kidini ya Efatha, kwa mujibu wa uchambuzi wa The Citizen ambalo ni gazeti dada la Mwananchi.

Benki hizo tatu zimelimbikiza kiwango cha NPL kinachozidi asilimia 50 ya jumla ya mikopo iliyotolewa, huku kiwango cha Efatha kikifikia asilimia 63.

Wataalamu wa benki wanaamini kuwa kiwango cha NPL kinachozidi asilimia 15 ya jumla ya mikopo yote ya beki za biashara, kinaashiria uwezekano wa kuanguka.

Katika toleo la tisa la Hali ya Kiuchumi Tanzania, Benki ya Dunia ilitahadharisha kuhusu kukua kupita kiasi kwa kiwango cha NPL, ambacho kilifikia asilimia 9.5 mwaka 2016 kutoka asilimia 6.4 mwaka 2015.

Ripoti hiyo iliitaja TIB Development Bank ambayo kiwango chake cha NPL kilikuwa asilimia 38 katika robo ya kwanza ya mwaka 2017.

Hata hivyo, taarifa za fedha za benki za biashara za robo ya kwanza mwaka 2017 zinaonyesha hali ni mbaya zaidi kwa Efatha, TWB na Ecobank Tanzania.

Lissu, Nchemba, Zitto waguswa na msiba Arusha

$
0
0

Baadhi ya wanasiasa nchini wametuma salamu za rambirambi kwa wanafamilia, ndugu, jamaa na marafiki katika mitandao mbalimbali ya kijamii kutokana na ajali iliyotokea Arusha na kugharimu maisha ya wanafunzi, walimu na dereva.

Katika akaunti yake ya Twitter, Mbunge wa Singida Mashariki Tundu Lissu ameandika, “Nimesikitishwa na vifo zaidi ya 31 vilivyosababishwa na ajali mbaya iliyotokea Karatu. Mungu azilaze roho za marehemu mahali pema.”

Waziri wa Mambo ya Ndani Mwigulu Nchemba, ameandika katika ukaunti yake ya Twitter, “Natoa pole kwa familia, ndugu, jamaa na shule ya Lucky Vincent kwa msiba huu mzito uliopata Taifa letu uliotokana na ajali mbaya pale Karatu. Tumepoteza watoto wetu ambao wazazi wao, ndugu zao na Taifa kwa ujumla liliwategema. Kwa kuwa Mungu wetu anaishi na kumiliki tuendelee kuziombea familia zilizoguswa na msiba huu, watoto wetu wapumzike kwa amani.”

Naye Mbunge wa Kigoma Mjini, Zitto Kabwe, “Moyo wangu umesinyaa baada ya kusikia taarifa za ajali ya watoto wetu huko Karatu. Natoa salamu zangu za rambirambi kwa wazazi wa wanafunzi wa shule ya St Lucky kwa ndugu na familia za walimu na wafanyakazi wa shule waliopoteza maisha.Huu ni msiba mkubwa sana. Huzuni haielezeki. Nawaombea kwa Mola awape wazazi na ndugu wote moyo wa subira katika mtihani huu. Ni msiba wa Taifa zima.”

Simulizi ya mzee wa miaka 127..Anadai Aliiona Vita Vyote vya Dunia na Majimaji Vikipigwa

$
0
0

WAKATI Dunia ikiwa imeaminishwa kuwa binadamu aliyeishi miaka mingi alikuwa anatoka nchini Italia na amefariki hivi karibuni, ameibuka mzee mmoja mkazi wa Kijiji cha Majengo, Kata ya Ihanda Wilaya ya Mbozi mkoani Mbeya ambaye ana miaka 127.

Mzee Ambilikile Mwanyaluke Panja, anaishi kitongoji cha Izyiga takribani kilomita mbili kutoka Kituo cha Mabasi cha Ihanda upande wa Magharibi, na hajiwezi kwa lolote kutokana na kuwa na umri mkubwa.

Kutokana na umri wake kuwa mkubwa ambao umemfanya kushindwa kutembea, familia yake inatumia kiti cha magurudumu kumsukuma wakati wa kumtoa nje na kumrudisha ndani.

Anasema Kabila lake ni Mndali na ni mzaliwa wa Kijiji cha Kapelekesi kilichopo katika Kata ya Kafule wilayani Ileje na kwa mujibu wa maelezo yake alihamia Mbozi baada ya vita ya kwanza ya dunia.

Baadhi ya matukio ambayo mzee Panja anayakumbuka ni pamoja na Vita ya Majimaji ya mwaka 1905 hadi 1907 ambayo anadai ilikuwa inapiganwa wakati yeye ana umri mkubwa na anachunga ng’ombe kijijini kwao Kapelekezi.

Mzee Panja anasema siri kubwa ya yeye kuishi miaka mingi ni aina ya vyakula alivyokuwa anakula tangu akiwa mtoto mpaka hivyo karibuni alipoanza kubadilishiwa.

Anasema alikuwa anakula zaidi ugali wa dona na wa Ulezi, ndizi aina ya Matoki huku mboga kuu ikiwa maziwa ya ng’ombe, maharage, Karanga na Njugu mawe.

Aidha anasema kipindi hicho kulikuwa hakuna chumvi za kisasa na badala yake walikuwa wanatumia chumvi za asili kwa kuchoma baadhi ya majani na kutumia majivu yake kwenye mboga (Chipembekwa).

MAALIM Seif Afunguka Jinsi Anavyoogopa Kuchukua Pensheni Yake ya Umakamu wa Urais..Adai Huwa Anajikimu kwa Pesa Zake za Mfukoni..!!!

$
0
0

KATIBU Mkuu wa Chama cha Wananchi (CUF), Maalim Seif Shariff Hamad amesema kamwe hatumii fedha za serikali katika shughuli zake zozote ziwe binafsi au za kichama.

Alikwenda mbali zaidi kwa kudai kuwa pia hatumii fedha yoyote ya Serikali kwenye matibabu yake.

Maalim Seif ameyasema hayo alipokuwa kwenye mahojiano ndani ya kipindi cha 360 kinachorushwa na kituo cha runinga cha Couds Tv.

Maalim ambaye aliwahi kuwa Makamu wa Kwanza wa Rais wa Serikali ya Umoja wa Kitaifa, Zanzibar, alilazimika kutoa ufafanuzi huo baada ya kuulizwa kama amekuwa akitumia fedha za Serikali katika shughuli zake mbalimbali.

Alisema Rais Dk. John Magufuli alipotoshwa kuwa Rais wa SMZ, Dk. Ali Mohamed Shein aliidhinisha fedha za matibabu za Maalimu Seif licha ya kukataa kumpa mkono.

Rais Magufuli alifanya ziara visiwani Zanzibar Septemba mwaka jana, ambapo alionesha kushangazwa na hatua ya Rais wa Zanzibar, kuidhinisha fedha za matibabu ya mpinzani wake wa kisiasa, Maalim Seif na kuongeza kuwa angelikuwa yeye kamwe asingeidhinisha.

Tukio hilo la Maalim Seif kukataa kumpa mkono Dk. Shein lilijitokeza Agosti mwaka jana wakati wa maziko ya Rais wa pili wa Zanzibar, Aboud Jumbe Mwinyi yaliyofanyika makaburi ya Migombani.

Katika mazungumzo yake jana Maalim Seif alisema, alifanya makusudi kutompa mkono Dk. Shein ili kudhihirisha kuwa ndiye aliyempora haki yake.

“Kwanza Magufuli alipotoshwa kabisakabisa… tangu niache nafasi ya Makamu wa Kwanza wa Rais, nimekuwa nikijihudumia mwenyewe kwenye kila kitu,  si hela ya Makamu wa Rais ambayo nina haki ya kisheria kuipata. Lakini kwa sababu nawajua hawa ukiwaomba watakupa ila watakushambulia, watasema anachukua pesa zetu na hatutambui, kwa kweli najibana kwa njia yoyote ili kujihudumia. Kwa hiyo Magufuli alipotoshwa hakuambiwa ukweli, mimi hawanijui hawa,” alisema.

Alisema baada ya chama chao kutopatiwa ruzuku wameandaa utaratibu maalumu wa kupata fedha ambapo kila kiongozi wa ngazi ya kitaifa huchangia Sh 10,000 kwa mwezi, kiongozi wa ngazi ya wilaya Sh 3,000, Jimbo Sh 2,000 na mwanachama wa kawaida Sh 1,000 kwa mwezi.

“CUF msifanye mchezo nayo, tumewaambia wanachama kuwa huko nyuma hatukua na ruzuku, wakasema lazima tuchangie, na tumeweka utaratibu wa kuchangia. Tunajua hatuna wanachama matajiri kwa sababu  matajiri wanaogopa kuja CUF maana wakijulikana TRA watawatia adabu.” alisema

Alisema CUF kwa upande wa Zanzibar ina wanachama zaidi ya 200,000  kati ya wanzanzibar milioni 1.3 wakati Bara kinawachama milioni 1.5.

Aidha, alisema licha ya kwamba analipa kodi lakini haridhiki na serikali  iliyopo madarakani kwa namna inavyofanya kazi.

“Nalipa kodi shingo upande, lakini si kwamba naitambua serikali. Hata mkono sikumpa kwenye Msiba wa Abood Jumbe, nilifanya makusudi, kwani huyu ndiye aliepora haki yangu, ningempa wananchi wanione namchekea wananchi watanielewa vipi? nilikataa kumpa mkono makusudi ili ajue kuwa sikuridhika,” alisema.

KUTANA NA Mariam Nabatanzi..Mama Mwenye Watoto 38 Akiwa na Watoto 37 Toka kwa Baba Mmoja Tu..!!!

$
0
0

WAKATI unapozungumzia ‘mama wa mataifa yote’, mtu aliye hai anayeweza kuendana na wasifu huo, atakuwa Mariam Nabatanzi Babirye mwenye umri wa miaka 37.

Katika umri huo, Mariam amejizolea umaarufu kwa sababu ya idadi kubwa ya watoto aliozaa mwenyewe bila msaada wa mtu.

Si hivyo tu, idadi hiyo ya watoto 38, unaweza kujiwa na fikira gani kwa haraka? Aliwazaaje wote hao wakiwa wameuzidi umri wake, jambo ambalo si la kawaida?

Fikra za haraka zitakazokujia ni kwamba kila mwaka alizaa mtoto mmoja tangu akiwa na umri wa mwaka mmoja huku mwingine mmoja akizaliwa mwaka mmoja kabla ya yeye mwenyewe hajazaliwa.

Inawezekana? Hapana! Ukweli ni kwamba watoto hao 38 kwa sehemu kubwa amewazaa kama mapacha, mapacha watatu, wanne na wote walizaliwa nyumbani kwa njia ya kawaida isipokuwa wa mwisho aliyezaliwa hospitali.

Mwanamke huyo, aishiye katika Kijiji cha Kambiri, Wilaya Mukono nchini Uganda, aliozwa bila ridhaa yake tena bila kujua wakati akiwa na umri wa miaka 12 kwa mwanamume mwenye umri wa miaka 40.

Hiyo ilikuwa mwaka 1993, mwaka uliofuata wakati akiwa na umri wa miaka 14, alipata seti yake ya kwanza ya watoto wawili mapacha, kisha miaka miwili baadaye wakafuata mapacha watatu kabla ya mwaka mmoja na miezi saba baadaye kuongeza seti ya mapacha wanne.

Kwa ujumla, katika watoto wa Mariam kuna seti sita za mapacha wawili, nne za mapacha watatu na seti tatu za mapacha wanne na watoto waliozaliwa mmoja mmoja. Kati ya watoto wake wote wasichana ni 10, wavulana wakiwa 28.

Mkubwa ana umri wa miaka 23 huku mdogo akiwa na umri wa miezi minne.

Mariam anafichua kuwa alinusurika kifo mwaka 1993 na muda mfupi baadaye aliozwa kwa mume mwenye wake na watoto wengi, na ambaye ni katili.

 “Sikujua kama nimeozwa. Watu walikuja nyumbani na kuleta vitu kwa baba yangu. Wakati muda ulipofika ugeni kuondoka, nilidhani nilikuwa namsindikiza shangazi yangu, kumbe nilipofika mbele alinikabidhi kwa mwanamume huyo.

Wakati Mariam alipoanza kuzaa seti za watoto, hakuona kama ni ajabu kwa vile baba yake alikuwa na watoto 45 kutoka wanawake tofauti na wote hao walizaliwa kama mapacha watano, wanne, watatu na wawili.

Ilipofika mimba ya sita, Mariam alikuwa tayari na watoto 18 na alitaka kusitisha kizazi, hivyo alienda hospitali, ambako madaktari walimwambia hawawezi kumsaidia kwa vile ana kiwango kikubwa cha mayai, ambacho kingemuua iwapo angeacha kuzaa.

Alijaribu tena kusitisha uzazi alipofikisha watoto 23 lakini alipewa onyo kama hilo kuwa atakufa akijaribu kuacha kuzaa.

“Nilishauriwa kuendelea kuzaa kwa sababu bila kufanya hivyo ni kumaanisha kifo. Nilijaribu kutumia kifaa kijulikanacho kama Inter Uterine Device (IUD) lakini niliugua na kutapika na kukaribia kufa. Nilipoteza fahamu kwa mwezi mmoja,” anakumbuka.

Ni baada tu ya kufikisha mtoto wake wa 38, ndipo madaktari walipoweza kumuondolea kizazi. Na ni uzazi huo pekee ambao alijifungulia hospitali tangu alipoanza kuzaa miaka 24 iliyopita.

“Nilimuomba daktari asitishe kizazi ili nisizae zaidi, akaniambia ameshaondoa kizazi. Hii ilikuwa njia pekee niliyozaa kwa upasuaji kwa sababu nilikuwa bado dhaifu kutokana na ugonjwa niliougua wakati nilipojaribu kutumia IUD," anasema.

Mmoja wa watoto wake mapacha wa kwanza ana cheti cha uuguzi na mwingine ujenzi ijapokuwa bado hawajapata kazi.

Watoto wake wengine wako kuanzia chekechea hadi madarasa ya juu ya elimu ya msingi.

Kuhusu kulisha watoto wake, anasema: “Kila kitu kinatoka mfukoni mwangu mwenyewe, nanunua kilo 10 za unga wa mahindi kwa siku, kilo nne za sukari kwa siku na miche mitatu ya sabuni.

“Nahitaji kuwa na Sh 100, 000 za Uganda (sawa na Sh 62,000 za Tanzania) kwa siku kutosheleza familia. Mungu amekuwa mwema kwangu, kwa sababu watoto hawajawahi kulala na njaa."

Mariam hupata fedha kutokana na kuuza dawa za kienyeji za kutibu maradhi mbalimbali, shughuli ambayo ameifanya tangu alipokuwa msichana mdogo.

Pia hufanya vibarua kama vile kusuka nywele, mapambo na kupamba maharusi. Kwa sasa yuko katika mchakato wa kukusanya fedha kuunganisha bomba la maji ili afanye biashara kwa vile eneo lao lina uhaba wa maji na dumu moja la maji huuzwa kwa Sh 800 za Uganda.

“Sidharau kazi yoyote inayoniletea fedha. Ninachojisikitikia ni kuacha shule ila namshukuru Mungu kwa zawadi ya hawa watoto."

Miaka 25 ya ndoa kwa Nabatanzi pia imekumbwa na maumivu na mateso.

“Nimeteswa mara nyingi na mume wangu; hunipiga wakati ninapojaribu kujadiliana naye masuala muhimu ya kifamilia, hasa anapokuja nyumbani akiwa amelewa.

“Hatoi fedha wala mahitaji yoyote ya kifamilia; watoto hawamfahamu vyema kwa vile hukaa hadi mwaka bila kuja nyumbani na watoto wanapozaliwa huwapa majina kwa njia ya simu.”

Charles Musisi (23), mwanae mkubwa anasema baba yao ametoweka na wamelelewa kwa mapenzi ya mama pekee.

“Naweza kukuambia wadogo zangu hawamjui baba jinsi alivyo. Mara ya mwisho nilimuona wakati nikiwa na umri wa miaka 13 tena muda mfupi usiku na hatujui furaha ya baba ikoje,”anasema mtoto huyo.

Kwa mujibu wa Nabatanzi mumewe anapokuja nyumbani huvizia usiku mwingi na kutokomea mapema asubuhi.

Kuendelea kwake katika ndoa hiyo kunatokana na ushauri wa shangazi yake kuwa asijaribu kuzaa na wanaume tofauti tofauti.

HOFU Yatanda Kinana Kufichwa..Habari Vichwa vya Magazeti ya Leo Juapili ya 7/5/2017..!!!

HUMPHFREY Pole Pole Amchokonoa Mange Kimambi Issue ya Kinana...Mange Amtolea Uvivu

$
0
0
Mange na Hamphfrey Pole pole wapeana na USO...
.

Baada ya Pole pole kuandika hiyo post hapo juu ikiwa imemtaja Mange Kimambi, Mange akaamua kumtolea  uvivu kama ifuatavyo :
.
#Regrann from #mangekimambi_ - :

"PolePole Tokea uwe katibu uenezi wa CCM ile brain ya kuongea mapoint mazito mazito imetoweka kabisa Yani. Hivi PolePole unakumbuka ulivyokuwaga unawa-inspire watanzania kwa jinsi ulivyokuwaga unaongea mapoint mazitoooooo. Siku hizi unaongea kama Bashite. Huna point, unajibu vitu bila busara, unajibu mambo kiwepesi wepesi...
.
.
Hivi Kweli Polepole kweli kati ya yote niliyosema point kubwaaaaa uliyoiona wewe ni Mimi kusema Kinana ameacha kufanya kazi za Chama???? And it's 100% true kinana amegoma kufanya mambo ya chama mpaka Baba Bashite A.k.a mwenyekiti wa CCM akamueleze why alimuitia TISS. Kinana alishikiliwa Na TISS nyumbani kwake for over 2 weeks...
.
Kwa issue ya Kinana alivyokaaa vibaya kwa Sasa ilibidi nyinyi kama chama muwatoe hofu wana CCM Na watz kwa ujumla kwa kuweka wazi data kuwa siku ile Rais anasema kamtuma kinana india kwa matibabu Ni kweli alikuwa india mtaje na hospitali aliyokuwa amelazwa, aliondoka TZ tarehe ngapi kwa ndege gani Na alirudi lini after that itakuwa easy watu kuhakiki habari hizo..
.
.
Polepole naomba uongeeee hadharani kuwa Kinana hakuita mkutano na waandishi siku ile Na kwamba Hakuzuiliwa Na TISS nyumbani kwake na kwamba hakutolewa silaha na Tiss. Na kwamba hakuwahi kuwa under house arrest chini ya TISS.Hiyo ndo response Watanzania wanayoitaka Na sio unatoa Majibu mepesi mepesi yasiyo Na point like je nikokuonyesha picha za kinana akifabya kazi za chama utanipa nini? Yani umejibu ka mtoto wa miaka mitano. That's a shallow answer to such a deep issue? Tena kutoka kwa mtu uliekuwaga unachambua mambo kwa kina, ukituonyesha picha za zamani ukasema ni za recent tutajua vipi? Ndo maana nakwambia umetoa majibu shallow. Na kama alifanya lazma kulikuwa na media tuonyeshe link tukaangalie sio picha zako wewe za kuchomoa chini ya godoro, tunataka picha zilizokuwa released Na media. Ukinionyesha hizo ntakupa hii account iwe account ya CCM.
.
.
Kama wewe kweli unajiamini jibu mambo ya TISS. Najua you can't do that sababu ni ukweli Na unaogopa siku Kinana au Nape wakiamua kufunguka utaaibika so huwezi shubutu kusema Tiss hawajawahi kumzuia kinana..CCM jibuni issue ya TISS kumshikilia Kinana, sio mnakuja namajibu ya KiBashite."Mange Kimambi

RAIS Magufuli Aamuru TRA, TFDA, TBS na TPA Wawe Wanafanya Kazi Saa 24 Bandarini Kuanzia Jumatatu

$
0
0
Ili kukamilisha kazi ya kutoa mzigo bandarini kwa muda mfupi, mamlaka hizo hizo zimeamriwa kufanya kazi masaa 24 kwa shift, kwa kuwa bandarini ni sehemu sensitive.

Waziri Mkuu amesema anataka kupata taarifa Jumatatu kuwa utekelezaji huo umefanyika,.

Amesema bandari ya Mombasa inatoa mzigo ndani ya siku 9 huku ya Dar ikichukua siku 14.

CHANZO Cha Vifo Vingi: Ajari ya Wanafunzi wa Arusha

$
0
0
Wakuu,
Kabla ya yote, natoa pole kwa familia, Ndugu na marafiki waliofikwa na msiba huu katika ajari ya Bus.

Lakini pia nitoe pongezi kwa watanzania wenzangu ambao kwa namna moja au nyingine wameshiki katika kuwatia moyo na kuwapa pole wafiwa.

Ni kweli tujuavyo kwamba ajari haiepukiki lakini kutokana na maendeleo ya sayansi na teknolojia kuna baadhi ya ajari zinaepukika.

Kwa utafiti mdogo niliyo ufanya nimegundua baadhi ya mambo ambayo yamepelekea kutokea kwa vifo vingi vya wanafunzi hawa.

1. SEAT BELT
Kuna kila dalili Bus haikuwa na seat belts, na hata kama ilikuwepo wanafunzi hawakufunga ile mikanda. Ukiangalia mwonekano wa Bus, sehemu kubwa iliyopondeka ni sehemu ya Mbele na karibia robotatu ya Bus halijapondeka Sana. Sasa kama kila mwanafunzi angekuwa kafunga mkanda wanafunzi waliokaa siti za nyuma wengi wangepona.

Kwa sababu hakukuwa na seat belt ilipelekea wanafunzi na walimu wao wote kulushwa mbele ya gari baada ya gari kukita kwenye kolongo.

2.UZEMBE WA DEREVA
Kuna kila dalili palikuwa na uzembe. Dereva alikuwa speed kubwa na gari likamshinda kwenye kona ukizingatia na ubichi wa barabara kutokana na mvua zinazoendelea.

OMBI LANGU:
wazazi/Waalimu tuwe makini muda wote na hawa watoto wetu hasa kwenye hizi School Bus, kuna ka tabia ka kulundika watoto, unakuta seat ya watu wawili watoto wamewekwa wanne. Inapelekea watoto kushindwa kufunga mikanda.

Mungu atusaidie!

By The Tomorrow People/JF

Viewing all 104756 articles
Browse latest View live




Latest Images