Quantcast
Channel: UDAKU SPECIAL
Viewing all 104670 articles
Browse latest View live

ASKOFU Gwajima Amwomba Spika Kuahirisha Bunge kwa Ajili ya Msiba..!!!

$
0
0

Askofu wa Kanisa la Ufufuo na Uzima, Josephath Gwajima amemtaka Spika wa Bunge kuahirisha kikao cha Bunge siku ya kuaga miili ya watoto waliofariki kwa ajali jana.

Amesema kama Rais wa Kenya, Uhuru Kenyatta aliamuru viongozi kusimama kuwakumbuka watoto hao itakuwa ajabu kwa Bunge kuendelea na vikao vya Bunge.

Amesema Spika akiahirisha Bunge kwa siku moja itatoa nafasi kwa wabunge hao kwenda Arusha ili kuomboleza pamoja.

SERIKALI Kugharamia Msiba wa Arusha

$
0
0
Serikali ya Jamhuri wa Muungano wa Tanzania imegharamia Sanda pamoja na majeneza kwa ajili ya Wanafunzi wa Shule ya Lucky Vicent waliopoteza maisha mapema jana kwenye ajali iliyokuwa ikihusisha safari ya kimasomo.

Akitoa taarifa hiyo leo Meya wa Jiji la Arusha , Mh. Calist Lazaro amesema kuwa taarifa za awali zinaonyesha kuwa tayari Serikali imekwishalipia gharama za majeneza na sanda ya kuhifadhia miili ya marehemu ambao kesho wanatarajiwa kufanyiwa ibada katika Uwanja wa mpira wa Sheikh Amri Abeid.

Aidha, Mh. Lazaro amesema kuwa viongozi mbali mbali wakiwemo mawaziri pamoja na wabunge bado wanaendelea kukusanyika katika eneo la shule ya Lucky Vicent  kwa ajili ya kikao na baadae majira ya saa tisa au kumi taarifa rasmi ya serikali itatolewa na Mkuu wa Mkoa wa Arusha.

WAZIRI Atoa Siku Saba Kwa Mbunge Mdaiwa Sugu

$
0
0
Waziri wa ardhi,nyumba na Maendeleo ya makazi Mh. William Lukuvi amemuagiza Mkurugenzi wa Halmashauri ya jiji la Mwanza,Kiomoni kibamba pamoja na watumishi wa idara ya ardhi na mipango miji,kuacha ubabaishaji katika kusimamia zoezi la urasimishaji wa makazi holela,sambamba na kutoa muda wa siku 7 kwa Mbunge wa Jimbo la Kwimba Mh. Shanif mansoor kulipa deni la zaidi ya shilingi milioni 500 la kodi ya ardhi analodaiwa tangu mwaka 2010.


Waziri Lukuvi ametoa agizo hilo jijini Mwanza wakati akisikiliza kero za wananchi wa kata ya Mahina,ambapo amesema Halmashauri hiyo imekuwa ikiwachukulia hatua za kisheria wananchi wenye maeneo madogo ya ardhi,huku ikiwaacha watu wenye maeneo makubwa ambao wameshindwa kulipa kodi kwa miaka zaidi ya kumi,jambo linaloikosesha mapato serikali na kumtaka Mbunge huyo kulipa deni hilo la shilingi milioni 529 linalotokana na kumiliki eneo la ardhi lenye ukubwa wa hekta 39 lililopo kata ya Buhongwa ifikapo Mei 5 mwaka huu.



Wakazi wa Mahina wakatoa ya moyoni kuhusiana na urasimu uliopo katika idara ya ardhi jijini Mwanza, yakiwemo malalamiko ya upotevu wa mafaili.


Mh. Lukuvi ambaye yupo katika ziara ya kukagua utekelezaji wa zoezi la urasimishaji wa makazi holela,katika baadhi ya mikoa ya Kanda ya Ziwa pia amebaini njama za kutaka kupewa taarifa za uongo na baadhi ya maofisa ardhi wa jiji la Mwanza kuhusiana na suala la viwanja vilivyopimwa.

POLISI Wapiga 'Stop' ziara ya Mtatiro Tanga

$
0
0
JESHI la Polisi Mkoani Tanga limezuiya Ziara ya Mwenyekiti wa Kamati ya uongozi wa Chama Cha CUF Juliasi Mtatiro.

Mtatiro  aliwasili jijini Tanga jana jioni kwa lengo la kufanya vikao vya ndani pamoja na kufungua matawi  kazi ambayo ilikuwa aifanye leo na kesho.

Mwenyekiti wa CUF ,Wilaya ya Tanga, Rashid Jumbe amesema licha ya
kwamba hadi jana jioni walikuwa na barua kutoka jeshi la polisi ya
kuwaruhusu kuendelea na ziara ya Mtatiro lakini leo saa 3.00 asubuhi
walizuiwa.


“Tulipopewa taarifa ya kuzuiwa, tuliamua kwenda kwa OCD Tanga.

tukiambatana na mheshimiwa Mtatiro  kupata maelezo ya kwa nini tuzuiwe ndipo tukaambiwa Magdalena Sakaya ametuma barua ya kuzuia mikutano hiyo kwa madai kwamba hana taarifa,”amesema Jumbe.



Mwenyekiti  huyo alieleza kushangazwa kwake na kitendo cha jeshi la
polisi kufanyia kazi maelekezo ya Sakaya huku akisisitiza kwamba CUF
Tanga haimtambui  kwa sababu alishafukuzwa uanachama.

 “Magdalena Sakaya na Profesa Ibrahim Lipumba sisi Tanga hatuwatambui
kwa sababu si wanachama wa CUF, hao ni viongozi wa Msajili wa Vyama
vya Siasa, watambue kwamba njama zao za kuiua CUF hazitafanikiwa
kamwe,” amesema Jumbe.

Amesema Julias Mtatiro alikuwa amepangiwa  kukutana na viongozi wa
kamati ya utendaji ya Wilaya ya Tanga, madiwani, wabunge, kufungua matawi
ya Kata ya Duga, Masiwani Shamba, Masiwani, Mabawa, Magaoni, Mnyanjani, Pongwe na Kwanjeka.

Kamanda wa Polisi wa Mkoa wa Tanga, Benedict Wakulyamba amesema
wamezuia ziara hiyo kufuatia jeshi la polisi kupokea  barua mbili
tofauti zenye kupingana jambo lililoashiria kuwa kusingekuwa na amani

Polisi wapiga 'stop' ziara ya Mtatiro Tanga

$
0
0

JESHI la Polisi Mkoani Tanga limezuiya Ziara ya Mwenyekiti wa Kamati ya uongozi wa Chama Cha CUF Juliasi Mtatiro. 

Mtatiro  aliwasili jijini Tanga jana jioni kwa lengo la kufanya vikao vya ndani pamoja na kufungua matawi  kazi ambayo ilikuwa aifanye leo na kesho. 

Mwenyekiti wa CUF ,Wilaya ya Tanga, Rashid Jumbe amesema licha ya 
kwamba hadi jana jioni walikuwa na barua kutoka jeshi la polisi ya 
kuwaruhusu kuendelea na ziara ya Mtatiro lakini leo saa 3.00 asubuhi 
walizuiwa. 

“Tulipopewa taarifa ya kuzuiwa, tuliamua kwenda kwa OCD Tanga. 

tukiambatana na mheshimiwa Mtatiro  kupata maelezo ya kwa nini tuzuiwe ndipo tukaambiwa Magdalena Sakaya ametuma barua ya kuzuia mikutano hiyo kwa madai kwamba hana taarifa,”amesema Jumbe. 



Mwenyekiti  huyo alieleza kushangazwa kwake na kitendo cha jeshi la 
polisi kufanyia kazi maelekezo ya Sakaya huku akisisitiza kwamba CUF 
Tanga haimtambui  kwa sababu alishafukuzwa uanachama. 

 “Magdalena Sakaya na Profesa Ibrahim Lipumba sisi Tanga hatuwatambui 
kwa sababu si wanachama wa CUF, hao ni viongozi wa Msajili wa Vyama 
vya Siasa, watambue kwamba njama zao za kuiua CUF hazitafanikiwa 
kamwe,” amesema Jumbe. 

Amesema Julias Mtatiro alikuwa amepangiwa  kukutana na viongozi wa
kamati ya utendaji ya Wilaya ya Tanga, madiwani, wabunge, kufungua matawi 
ya Kata ya Duga, Masiwani Shamba, Masiwani, Mabawa, Magaoni, Mnyanjani, Pongwe na Kwanjeka. 

Kamanda wa Polisi wa Mkoa wa Tanga, Benedict Wakulyamba amesema 
wamezuia ziara hiyo kufuatia jeshi la polisi kupokea  barua mbili 
tofauti zenye kupingana jambo lililoashiria kuwa kusingekuwa na amani

UKWELI Mchungu...Ajali Lucky Vincent School: Uzembe, Tamaa, Ubadhirifu na Kutokujali Usalama wa Wanafunzi Vimechangia kwa Asilimia 100..!!!

$
0
0

Wazazi poleni kwa msiba huu uliowapata watoto wetu wapendwa wa Lucky Vicent na walimu wao! Hakika ni majonzi makubwa sana! Lakini yafaa tutafakari kwa kina kwanini janga kama hili liwafike watoto hawa, tumaini la maisha yetu! Maswali ni mengi, na kwa kweli yana hitaji majibu ya kina. 

Kwa tunaozunguka kutwa barabarani, mtakubaliana na mimi kuwa, vipo viashiria vingi hatarishi kwa watoto wetu wanapotumia mabasi ya shule zao. Shule nyingi zinatumia mabasi ambayo zamani yalitumika kama daladala, na baada ya kuchoka yakabadilishwa na kuwa mabasi ya shule. Huku madereva wakiendesha kwa mwendo usiostahili kabisa kubeba watoto.

Hatari zaidi, mabasi haya ya shule hubeba idadi kubwa ya wanafunzi kuzidi uwezo halisi wa gari, na kutokuzingatia taratibu zote za kiusalama kama vile kufunga mikanda. Mfano wa hili ni hii ajari ya Lucky Vicent. Wanasema "eti gari lili feli breki" ndo sababu ya ajari! Binafsi sikubaliani nalo. 

Kwa wale ambao wameendesha magari makubwa kwa weledi na kwa kipindi kirefu, watakubaliana na mimi kuwa, kubeba uzito zaidi ya uwezo wa gari pamoja na mwendo kasi husababisha mfumo wa breki za gari kushidwa kuhimili, hivyo kutokukamata pale dereva anapozitumia. 

Sababu nyingine ya kujiuliza, je ni kweli haya mabasi ya shule yanafanyiwa matengenezo na ukaguzi wa mara kwa mara, kwa maana ya motor vehicle service! Hapa inatiashaka! *A motor vehicle service is a series of maintenance procedures carried out at a set time interval or after the vehicle has travelled a certain distance.* Shule ya Lucky Vicent lazima ithibitishe kwa kuonyesha *service na log books* za hilo gari, majibu utayaona, hakuna kumbukumbu ya service.*The completed services are usually recorded in a service book which is rubber stamped by the service centre upon completion of each service.* Mashule mengi yanahuo udhaifu, na hii inatokana na uzembe, tamaa, ubadhirifu wa watendaji wao, kutokujali maisha ya wanafunzi na kutokuwa waangalifu huku wakiweka mbele masilahi yao na kupata faida.

Matengenezo muhimu na ya mara kwa mara kwa gari *motor vehicle service* ni kama ifuatavyo;
-Change the engine oil & oil filter
-Replace the air filter & fuel filter
-Tune the engine
-Check level & refill brake fluid/clutch fluid
-Check Brake Pads/Liners, Brake Discs/Drums, and replace if worn out.
-Check level and refill power steering fluid
-Refill Manual Transmission Fluid,Grease and lubricate components inspect.
-Check condition of the tires
-Check for proper operation of all lights, wipers etc.

Vipuri vingine vyote vinavyo weza kulifanya gari lisiwe salama kwa matumizi ya barabara hukaguliwa na kubadilishwa wakati wa kufany *service* je mashule yetu wanafanya haya! Kama haya hayafanyiki ni wakati sasa wazazi wa watu wote wenye matashi mema kuchukua hatua za kuwawajibisha wahusika wote ili kuokoa maisha ya watoto wasio na hatia.

HIVI Ndivyo Msongo wa Mawazo kwa Mjamzito Unavyoathiri Akili za Mtoto Aliyeko Tumboni..!!!

$
0
0

Uwezo wa kufikiri wa kizazi fulani, unaweza kuathiriwa na hali na changamoto wanazopitia wanawake wajawazito katika hatua za kushiriki uumbaji wa mwana aliye ndani ya tumbo lao kwa muda wa miezi tisa.

Mwanamke mjamzito anayekabiliwa na tatizo la msongo wa mawazo kutokana na sababu zozote, huweza kuleta athari ya moja kwa moja kwenye mfumo wa ukuaji wa ubongo wa mwanae.

Hayo yamedhihirika kupitia utafiti uliochapishwa kwenye jarida la Clinical Endocrinology, ambao ulionesha kuwa athari hizo zinaweza kupatikana kwa ujauzito wenye umri wa kuanzia wiki 17.

Utafiti huo ulikuja kama muendelezo wa tafiti za awali kwa binadamu na wanyama ambazo zilionesha kuwa endapo mama mjamzito atakabiliwa na tatizo la msongo wa mawazo, anaweza kusababisha mwanae akawa na uwezo mdogo wa kufikiri (IQ).

Hata hivyo, watafiti hao walieleza kuwa lengo lao sio kuwapa hofu wanawake bali ni kuwatahadharisha kuhakikisha wanakuwa na afya nzuri na kuepuka mambo yanayoweza kusababisha msongo wa mawazo.

Timu ya watafiti ikiongozwa na Professa Vivette Glover wa Chuo cha Imperial cha London (Imperial College London) na wasaidizi wake ambao ni wataalam wabobezi wa afya ya mama na mtoto waliwafanyia utafiti wanawake wajawazito 267 kwa kutumia dawa maalum zinazompa mtu hali sawa na ile ya aliye na msongo wa mawazo.

Profesa Glover aliiambia The Guardian kuwa walitoa dawa hizo kwa kuzingatia hali inayoweza kumpata mtu mwenye msongo wa mawazo wa muda mrefu ambayo ni kuchoka sana na kujisikia mgonjwa.

Hivyo, ni vyema kwa jamii kuhakikisha kuwa ili kuendela kuwa na kizazi chenye uwezo mkubwa wa kufikiria na kuamua mambo, ni vyema tukaanza na kuwajali na kuwapa furaha wanawake wajawazito. Changamoto wanazozipitia katika ngazi za familia zinaweza kuwa chanzo cha kukosa mwana mwenye uwezo wa kuliinua Taifa.

GWAJIMA Amvaa Nabii aliyetabiri Kifo cha Lowassa....Atishia Kuwataja Hadharani Wanaopanga Kumuua

$
0
0
Askofu wa kanisa la Ufufuo na Uzima, Josephat Gwajima leo amemvaa muhibiri maarufu wa Malawi anayefahamika kwa jina la Nabii Bushiri aliyedaiwa kutabiri kuhusu hatma ya uhai waziri mkuu wa zamani, Edward Lowassa.

Katika moja kati ya mahubiri yake, Nabii Bushiri ambaye ni mzaliwa wa Malawi anayefanya kazi zake nchini Afrika Kusini, alidai kuwa ameona hali ya umauti ikimnyemelea Lowassa na kuwataka waumini wake kuomba ili awe na maisha marefu.

Akizungumza leo katika ibada kanisani kwake, Gwajima alilaani utabiri wa Nabii Bushiri, akidai kuwa amekodiwa na watu wenye nia mbaya ili atabiri ubaya kuhusu waziri mkuu wa zamani, Edward Lowassa ili kufanikisha mpango wao wa kufanya tukio baya.

Gwajima alidai kuwa kwa uwezo wa kiroho, amewafahamu watu waliopanga kutekeleza njama dhidi ya Lowassa na viongozi wengine wa Serikali huku wakimtumia nabii huyo kuwaandaa watu kisaikolojia.

“Nataka nimueleze Nabii Bashiri kuwa nafahamu watu waliomkodi kufanya hivyo, na utabiri wake hautawezekana kamwe. Hakuna kiongozi yoyote wa serikali wala wa upinzani atakayekufa kwa utabiri huo. Wote wataishi kwa jila la Yesu,” alisema Gwajima ambaye leo alikuwa akihubiri kwa lugha ya kiingereza na kufasiriwa kwa lugha ya kiswahili.

Hata hivyo, Askofu huyo anayefahamika kwa kauli zake tata alieleza kuwa kwa uwezo wa kiroho amewafahamu watu waliopanga njama hizo na namna walivyoenda Afrika Kusini kukutana na mhubiri huyo kwa lengo la kumkodi atoe utabiri huo.

“Wanaweza kujiuliza nimewafahamu vipi. Roho yangu ilisafiri nao hadi Afrika Kusini, walivyokutana na Nabii Bashiri nilikuwa naye, yote waliyozungumza naye nayafahamu na hata walichompa ninakifahamu,” alisema.

“Ninawafahamu kwa majina na walipo na ninawataka wakome mara moja kuendelea na mpango wao. Wasipositisha mpango wao huo, Jumapili ijayo nitawataja hapa wote kwa majina,” alisikika Gwajima.

Gwajima alidai kuwa hamaanishi kuwa Bushiri sio mtumishi wa Mungu, lakini utabiri wake juu ya viongozi wa Tanzania ni wa kukodiwa.

Nabii Bushiri ambaye amekuwa akizua mijadala na hata kuingia katika mgogoro na baadhi ya nchi za Afrika, pia aliwahi kutabiri kuhusu matokeo ya uchaguzi mkuu Tanzania pamoja na tukio la tetemeko la ardhi nchini.

FAHAMU Siri 5 Kubwa Za Mafanikio Bila Utegemezi..!!!

$
0
0

Kila binadamu ameumbwa na kiu ya kufanikiwa katika kila kitu anachofanya. Mafanikio ndio kilele cha mlima mkubwa wa maisha ambao umejengwa kwa misingi na ngazi za mihangaiko na mitihani ambayo unapaswa kuivuka ili upumzike kwenye kilele hicho.

Kwa bahati mbaya, unaposema ‘mafanikio’ wengi hufikiria kuhusu ‘utajiri’. Lakini ukweli ni kuwa kuna tofauti kati ya kuwa tajiri na kufanikiwa kiuchumi. Unaweza kuwa tajiri lakini ukawa bado hujafanikiwa. Kwa kuwa watu wanawaza utajiri kuwa ndio kigezo cha mafanikio hujikuta wakijiingiza kwenye vitendo vya ajabu kwa lengo la kujizolea mali lakini mwisho huwa wanagundua kuwa hawajafanikiwa japo jamii inahisi wamefanikiwa.

Nanachoamini mimi, kufanikiwa kweli ni kutimiza malengo yako kwa ufanisi na kwa wakati, lakini mafanikio hayo yakupe amani moyoni mwako (peace of mind).

Vinginevyo, utafanikiwa kwa mrundikano wa fedha huku ukitengeneza tatizo kubwa zaidi la msongo wa mawazo na ukosefu wa amani ya moyo. Hivyo, mafanikio ya njia ya mkato ni mafanikio feki yanayokuja na matatizo mengi mazito zaidi.

Kwa utangulizi huo mrefu, naamini utanielewa zaidi napokupitisha kwenye hizi ‘siri za wazi’ za mafanikio ya kweli katika maisha.

1. Jiamini

Mafanikio ya kweli yanaanza na wewe. Hivyo, kujiamini ni msingi mzuri utakaokufanya utambue uwezo wako katika kufanya jambo fulani. Amini uwezo wa kufanya jambo hilo uko mikononi mwako. Usijishushe, jipime kwa mengi mazuri unayoweza kufanya, ikatae roho ya kujiona huwezi.

2. Thubutu

Neno hili pia ni msingi wa pili mkuu wa mafanikio. Uoga wa kuthubutu ni kikwazo kikuu kinachowarudisha wengi nyuma na kujikuta hata kuanza safari ya mafanikio hawawezi. Jambo lolote zuri na kubwa huwa gumu kufanya na ni rahisi kuhisi haliwezekani. Usikubali kushindwa bila kujaribu. Thubutu kwa dhati na weka nguvu yako na akili yako yote katika uthubutu huo. Hata hivyo, katika uthubutu huu, unapaswa kupima vizuri ili uchukue ‘calculated risk’ na sio ‘just risk’.

3. Panga na tekeleza kwa vitendo

Kumbuka, ukishindwa kupanga ujue umepanga kushindwa. Kuwa na mipango inayopimika na kutekelezeka kwa kiwango cha juu. Usiwe na mipango tu mikubwa ambayo hata utekelezaji wake hauwezekani. Unapopanga fikiria wapi utapata rasilimali na jinsi ya kutelezeka, lakini pia mpango wako ukupe uwezo wa kuutathmini na kujipima mwisho wa kazi hiyo. Hata hivyo, mipango haitakuwa na maana kama hautaitekeleza kwa ufanisi. Ukishindwa kutekeleza mpango wako, rudi angalia ulipoteleza ili urekebishe na sio kuufuta mpango mzima bila sababu za msingi.

4. Tengeneza mtandao na wasiliana

Mtandao ni kama daraja au miundombinu ya kuyafikia mafanikio. Hakikisha haujifungii kwenye dunia yako peke yako. Hakikisha kila unaekutana naye na kupata nafasi ya kumfahamu kama mtu anayeweza kuwa sehemu ya daraja bora kwa namna moja au nyingine, anakuwa sehemu ya mtandao wako.

Lakini kuwa na mtandao wa watu pekee hautoshi kama hautawasiliana nao. Kuwasiliana na mtandao huo ni kuufanya uwe ‘active’ ili isionekane kama unawatafuta wakati ukiwa na shida tu. Aidha, unapaswa kujipima kwa kuangalia watu wangapi wanakufahamu wewe zaidi ya watu wangapi unaowafahamu. Kwa mfano: wewe unamfahamu Mkurugenzi wa kampuni ‘A’, Jiulize, je, yeye anakufahamu? Kama hakufahamu basi yeye sio sehemu ya mtandao wako.

Lakini pia, angalia mawasiliano yako ya siku, wangapi umeongea nao kuhusu wazo la biashara au kazi.

5. Kuwa mweli na Mwaminifu

Hii ni siri kubwa zaidi ya zote, japokuwa nimeiweka mwishoni kati ya hizi tano. Usipokuwa mwaminifu na mkweli huku unaona mambo yako yanaenda vizuri unapaswa kushtuka mapema. Wewe ni kama mtu anaevuka ng’ambo ya pili huku akilivunja daraja. Mwisho wa siku utajikuta unaporomoka kabla hujafika unakotakiwa kufika.

Uaminifu utaimarisha mtandao wako kwa hali ya juu zaidi na utatafutwa kwa kuwa wewe utakuwa sehemu ya sababu ya mafanikio ya watu wengine. Kwa mfano, angalia namba ulizonazo kwenye simu yako ya mkononi. Je, ukitaka kumpigia simu dereva taxi majira usiku au hata muda wa kawaida utatumia vigezo gani? Bila shaka uaminifu na ukweli vitatangulia zaidi.

Kuwa mwaminifu na mkweli kwa kila mtu utakayefanya nae kazi, biashara au hata wakati mnafanya mambo ya kawaida ya kijamii kunakupa nafasi ya kuwa chaguo la kwanza kwa watu wanapohitaji huduma, bidhaa au rasilimali ambayo unayo.

Ukifuata kwa uhakika haya matano huku ukimkumbuka Mungu wako kwa kila jambo utafanikiwa kweli na kubaki na amani ya moyo.

Amini katika kile unachoamini na kifanyie utafiti kujiridhisha kabla haujakubali kuyumbishwa kwa tamaa za haraka haraka ili uwe na sababu za kutosha za kukataa au kukubali jambo lolote.

UMRI Mzuri kwa Mwanamke Kupata Mtoto (Kuzaa) Kitaalamu ni Huu Hapa....!!!

$
0
0

Tamaa ya kutaka kufanikiwa maishani imeenea duniani kote. Hali imebadilika sana, jinsia ya kike inataka kujitosheleza kwa kila kitu. Lakini mabadiliko ya kibaiolojia yanabaki vile vile mfano kuzeeka nk.

Mafanikio wanayowaza wengi ni utajiri wa pesa na elimu kubwa. Hii imesababisha wanawake wengi kusoma sana na kufanya kazi kupita kiasi, hata kupuuzia suala la kuzaa mapema.

Watu wengi wanashtuka wakiona umri wao unafikia au kuwa zaidi ya miaka 30, ndio wanakuwa na tamaa ya kuzaa. Kuchelewa kwao kuzaa kunaweza kuwa kwa taabu ama kuzaa watoto wenye matatizo mengi ya kiafya.

Kwa miaka mingi, wataalamu wengi wa afya ya uzazi bado wanaamini miaka 20-35 ndio umri sahihi kushika mimba na kuzaa.

Utafiti uliochapishwa kwenye jarida la magonjwa ya uzazi (Journal of Obstetrics & Gynacology) uliofanywa na watafiti kutoka Taasisi ya Karolinska ya nchini Sweden umegundua katika nchi tajiri duniani wanawake huzaa wakiwa na umri mkubwa kitu kinachopelekea kuongezeka kwa hatari ya kuzaa watoto njiti (Preterm birth), ukuaji hafifu wa vichanga na kuzaa watoto wafu (Stillbirth).

Ijapokuwa, wengi hufikiri matatizo mengi ya uzazi huongezeka baada ya miaka 35 na huwa zaidi baada ya miaka 40.

Kwa wenzi wawili wanaoishi pamoja, kuchelewa kuzaa huathiri pia wenza wa kiume, ambapo mbegu za uzazi za mwanaume hudhorota kila mwaka upitao na watoto wamaotokana na wanaume wazee huwa na hatari zaidi ya kupata matatizo ya akili na matatizo ya chembe za urithi.

Kutoka Arusha: Idadi ya vifo vya wanafunzi imeongezeka

$
0
0

Kutoka kwenye chanzo cha kuaminika Mkoani Arusha, Mwanafunzi aliyekuwa amelazwa katika chumba cha kuhifadhia wagonjwa mahututi (ICU) Doreen Mshana amefariki leo mchana.


Kifo cha Doreen Mshana kimeongeza idadi ya vifo kufikia 36 ambapo wanafunzi ni 33, Walimu wawili na dereva mmoja baada ya ajali iliyotokea jana wilayani Karatu Mkoani Arusha.


Taarifa za kifo cha binti huyo zilianza kusambaa jana kwenye mitandao ya kijamii hali iliyompelekea Kamanda wa Polisi mkoani Arusha, Charles Mkumbo kulitolea ufafanuzi


."Kuna mmoja walimripoti amefariki ndiyo maana wakasema 33 lakini siyo kweli waliofariki ni wanafunzi 32 walimu wawili na dereva mmoja. Hakuna kifo kilichoongezeka, taarifa zilisambaa kuwa yule mwanafunzi  aliyekuwa kapoteza fahamu amefariki lakini siyo kweli. nawataka watoa taarifa wa confirm habari kutoka kwenye vyanzo vya kuaminika.- alisema Mkumbo.

MAMBO Muhimu ya Kuzingatia Katika Malezi Na Makuzi Ya Mtoto..!!!

$
0
0

Malezi ni matendo yote yanayofanywa na wazazi, walezi na jamii kwa lengo la kumlea, kumkuza, kumlinda, kumuendeleza mtoto kimwili, kiakili, kijamii, kihisia na kimaadili ili aweze kuishi, kukua vizuri na kukubalika na jamii.

Ili mtoto aweze kukua katika misingi hiyo muhimu yapo mambo muhimu ambayo wazazi wanapaswa kuyazingatia wakati wote wa malezi na makuzi. Mambo hayo ni pamoja na:

Afya

Ili mtoto awe na afya bora, anahitaji kupatiwa kinga zote dhidi ya maradhi ya kuambukiza kwa njia ya chanjo na kupatiwa tiba mara anapougua. Magonjwa sugu kama Kisukari, Pumu au Saratani  yanaweza kuathiri makuzi na maendeleo ya mtoto.

Mazingira yanayomzunguka mtoto hayana budi kuwa katika hali ya usafi na usalama wakati wote. Mazingira hayo ni pamoja na mahali anapolala, sehemu anazochezea, mavazi na vyombo anavyotumia. Inashauriwa kuwa wazazi, walezi na jamii wahakikishe watoto wadogo ikiwa ni pamoja na wale walio katika mazingira magumu zaidi wanapata chanjo kwa wakati na wanawasaidia kuweka mazingira yao katika hali ya usafi.

Ikiwa mtoto wako ana ugonjwa sugu ni busara kuzungumza na mtaalamu wa afya ili kuweza kufahamu ni jinsi gani ugonjwa huo utaathiri afya ya mtoto wako na namna bora ya kumrinda.

Lishe

Ili mtoto aweze kukua vizuri kimwili na kiakili anahitaji chakula bora au mlo kamili. Chakula bora au mlo kamili unajumuisha vyakula vyenye virutubisho kama protini, wanga, mafuta, vitamini na madini.

Chakula bora hakina budi kianze kwa mama mjamzito, mara baada ya mtoto kuzaliwa apatiwe maziwa ya mama pekee kwa miezi 6 ya kwanza, baada ya miezi hiyo mtoto apatiwe vyakula vya kulizika. Mtoto aendelee kunyonyeshwa maziwa ya mama hadi miezi 24 na kumpatia vyakula vya nyongeza.

Ni muhimu mtoto aliye na umri chini ya miaka mitano apate milo isiyopungua mitano kwa siku na yenye virutubisho vya kutosha. Inashauriwa virutubisho hivyo vitokane na vyakula vinavyozalishwa katika maeneo anayoishi mtoto.

Maandalizi ya vyakula vya mtoto yafanyike kwa makini ili visipoteze viini lishe kwa mfano, ukoboaji wa nafaka mfano mahindi, kuloweka nafaka na upikaji wa mboga za majani kupita kiasi ni sababu zinazochangia uharibifu wa viini lishe na ubora halisi wa chakula. Hali hii husababisha utoaji wa lishe duni kwa mtoto na hivyo kuathiri ukuaji na uchangamshi kwa mtoto.

Wakati wa kutayarisha chakula, kila kundi la chakula liwepo katika mlo kamili. Kimsingi, kuna makundi makuu manne ya vyakula. Kundi la kwanza ni chakula Kikuu mfano nafaka mahindi, 
mtama, mizizi (mihogo). Kundi la pili ni vyakula vyenye Utomwili mfano nyama, samaki, maharage, kunde, mbaazi, Kundi la tatu ni vyakula vyenye vitamini na madini kwa wingi mfano matunda na mboga za majani na kundi la nne ni vyakula vyenye nishati kwa wingi mfano mafuta ya kupikia na sukari.

Uchangamshi

Uchangamshi ni matendo au mwelekeo anaoonyesha mzazi au mlezi kwa mtoto kwa lengo la kuchochea ukuaji na maendeleo ya mtoto kimwili, kiakili, kimaono, kihisia na kimaadili ambapo uchangamshi wa mtoto huanza tangu akiwa tumboni kwa mama na kuendelezwa baada ya kuzaliwa.
Uchangamshi katika kipindi hiki huchangiwa kwa kiwango kikubwa na hali ya afya ya mama. Hivyo malezi na uchangamshi wa awali kwa mtoto unatakiwa uanze mara mimba inapotunga.

Mama mjamzito anahitaji matunzo kimwili, kijamii na kisaikolojia ili mtoto aliyeko tumboni aweze kukua katika mazingira salama. Ili kuhakikisha kuwa mtoto anapata malezi changamshi akiwa tumboni wazazi au walezi hawana budi kuzingatia mambo kama mjamzito kupata mahitaji ya lazima, asifanye kazi nzito na ngumu, apewe upendo, apate muda wa kupumzika, mahali pazuri pa kulala, 
ahudhurie kliniki pamoja na kupata matibabu na ushauri wa kitaalamu.

Inashauriwa mama mjamzito kutojihusisha na ulevi wa pombe, madawa ya kulevya, uvutaji wa sigara na vile vile kujiepusha na magonjwa ya kuambukiza.

Uangalizi

Uangalizi unajumuisha vitendo vitakavyowezesha kuhakikisha kuwa mtoto yuko katika hali ya usalama ili kulinda uhai na maendeleo ya mtoto. Vitendo hivyo vinajumuisha kumpatia mtoto mahitaji muhimu kama vile chakula chenye virutubisho vyote, chanjo dhidi ya magonjwa na tiba mara anapougua, ulinzi na usalama, kumpakata, kuzungumza naye na kucheza nae.

Hivyo inashauriwa kuwa ni vyema mtoto apewe uangalizi wa kutosha ili kumwepusha na ajali na mazingira hatarishi yatakayopelekea kuathiri afya yake, kupata ajali au kufanyiwa vitendo viovu kwa mfano kubakwa.

Ujirani na Jamii inayozunguka

Majirani na jamii inayokuzunguka vina mchango katika malezi na makuzi ya mtoto wako. Ukuaji na maendeleo mazuri ya mtoto yanachagizwa na mahusiano mazuri na watoto wenzake, walimu wake na watu wengine wanaomzunguka.

Lakini vitu kama ufinyu wa makazi, matunzo mabaya ya mtoto au sehemu isiyo salama kwa mtoto kuchezea au kukaa vinazorotesha ukuaji na maendeleo ya mtoto.

MAMBO 10 Muhimu Ya Kuufanya Uume Kuwa Na Afya..!!!

$
0
0

Uume (Penis) ni kiungo chenye hisia na muhimu katika jinsi ya kiume kutokana na nafasi yake katika mwili.

Wanaume wengi wamekuwa wakitumia kiungo hicho pasipo kuzingatia utunzaji wake nakuifanya sehemu hiyo nyeti kuwa chafu na hata pengine kutoa harufu mbaya kwa kutoifanyia usafi sawasawa hasa baada ya kushiriki tendo la ndoa na kusisahidia haja ndogo.

Leo kati safu hii ya afya nikakufahamisha jinsi 10 muhimu za kutunza uume wako:

Usafi kwa asiyefanyiwa Tohara

Watu wengi usahau hata kushindwa kusafisha ngozi ya juu ya Uume wakati wa kuoga na baada ya tendo la ndoa na hasa wale ambao bado wana Ngozi ya juu ya uume (govi) na kusahau kusafisha eneo la chini yake. Kama una ngozi ya mbele katika uume (govi), unapaswa kuvuta kwa chini kwa upole ngozi hiyo na kufua eneo la chini yake na maji moto. Kama utashindwa kufanya hivyo utasababisha eneo hilo kuwa na harufu mbaya na kusababisha kuzaliana kwa bakteria.

Kunawa mikono

Ni lazima kuwa na tabia ya kusafisha uume wako si tu baada ya kutoka chooni lakini pia kabla. Osha mikono yako wakati wowote kabla ya kugusa uume wako. Hii ni kutokana kushika vitu vingi ambapo kunakuwa na uwezekano mkubwa wa kutunza kemikali. Pia ni muhimu kama umekuwa katika kuwasiliana na watu hivyo uweza kubaki na chembechembe ambazo zinaweza kusababisha muwasho kwa kushika pilipili hivyo utajikuna na kusababisha michubuko katika uume.

Uchunguzi wa Mara kwa Mara

Si tu kama wanawake wenyewe ndio wanashauriwa kujitegemea kwa kufanyiwa uchunguzi wa saratani ya matiti na kizazi, Lakini pia wanaume wanapaswa kuwa na utaratibu wa kuangalia sehemu zao za siri kama wana uvimbe wowote na pia kwa ishara ya magonjwa ya zinaa. Kuchunguza pia shahawa yako kutambua mabadiliko yoyote katika muonekano au uwepo wa damu katika uume.

Epuka Majeraha

Uume wako unahitaji ulinzi, upendo na huduma kutoka kwako sambamba na kuepuka hali ambazo zinaweza kusababisha majeraha katika uume. Hii inaweza kutokea kwenye ngono isiyo salama au punyeto bila kurainisha ngozi. Pia kuhakikisha unaepuka kuvaa nguo ya ndani (chupi) ambayo haibani sana. Ni vyema ukapata muda wa kukaa bila nguo ya ndani (chupi) ili kuweka wazi uume na kuepusha msuguano utakaoweza kuleta madhara.

Kuwa na mwanamke mmoja

Kuwa na mpenzi zaidi ya mmoja uua uwezo wako kingono lakini pia kuwa na mwanamke mmoja kutakusaidia kuwa mwenye tabia njema na kuwa na nguvu na uwezo mzuri wakati wa kufanya tendo la ndoa na hasa kabisa kujikinga na magonjwa ya zinaa.

Kupata muda wa Mapumziko

Hii ni nzuri kwa afya yako kwa ujumla lakini nzuri hasa kwa uume wako kuwa na afya. Kila wakati kila unapokuwa umepumzika kwa usingizi mzito, uume wako utakuwa na uimara kutokana na kuupumzisha. Hii ni muhimu kwa sababu husaidia kurejesha sura yake na pia kuongeza muda wa utendaji kazi wa damu yenye oksijeni.

Kunywa maji

Kuwa na tabia ya kunywa angalau glasi nane za maji safi. Maji huvuta sumu nje ya mwili wako na kuruhusu damu kufanya kazi na kuongeza kukusisimua wakati wa tendo la ndoa.

Uchaguzi wa sabuni ya Kuogea na mafuta

Ni vizuri na muhimu kufanya usafi wa sehemu za uzazi. Na hata hivyo haipaswi kwenda kuosha na kuskrabu sehemu za siri kwani ngozi ya uume ni raini na nyeti. Matumizi ya sabuni ambazo uondoa vidonda si nzuri kwa kutumia katika uume na kwa kutumia kama njia ya kurainisha uume wakati wa tendo la ndoa lakini pia ni kivutio cha maambukizi. Vizuri kuosha mara mbili kwa siku na maji ya joto kwa kutumia sabuni za kawaida.

Kwa nini unapaswa kunyoa

Mwanaume unaweza kutoona umuhimu wa kunyoa kama ilivyo kwa mwanamke lakini ukweli ni kwamba hata wewe unapaswa kunyoa na kutumia nyia nyepesi za kunyoa ili kuweka eneo lako la uzazi laini na safi. hivyo kama kunyoa mwenyewe kutakuwa na kisingizio mnaweza kufanya hivyo pamoja kama wanandoa hivyo mwenza wako akakuweka katika hali ya usafi.

SHULE Ambayo Wanafunzi Wake Wamefariki kwa Ajali ya Basi Arusha Yafungwa kwa Wiki Moja..!!!

$
0
0

Shule ya Lucky Vicent imefungwa kwa siku saba kufuatia vifo vya wanafunzi wake 32 vilivyotokea kwenye ajali ya gari jana Karatu.

Kutokana na ajali hiyo Mbunge wa Arusha Mjini, Godbless Lema na wabunge wengine wa Chadema wamefika shuleni hapo kutoa pole.

Lema kwa niaba wabunge ameeleza kusikitishwa na msiba huu na amewapa pole wafiwa lakini akatoa angalizo kusiingizwe siasa katika msiba huu mkubwa.

Meya wa jiji la Arusha Kalist Lazaro ameeleza kuwa Waziri wa Afya, Ummy Mwalimu, Waziri wa Tamisemi, George Simbachawene na Waziri wa Elimu, Profesa Joyce Ndalichako watafika jioni kuzungumza na wafiwa.

Leo Makamu wa Rais Samia Suluhu kwa niaba ya Rais John Magufuli ataongoza kazi kuaga miili ya wanafunzi hao Uwanja wa Sheikh Amri Abeid.

Mkuu wa shule hiyo, Ephraem Jackson amesema  hadi sasa vifo ni 36 na wanafunzi wawili bado wamelazwa Hospitali ya Mkoa ya Mount Meru. Wanafunzi hao ni Sadiely Ismail na Wilson Tarimo.

KINANA Aibuka na Sakata la Ajali ya Bus Iliyoua Wanafunzi 32..Afunguka Haya ya Moyoni..!!!

$
0
0

Kufuatia ajali iliyotokea jana Mkoani Arusha na kuua watu zaidi ya 30, Chama Cha Mapinduzi kimetuma salamu zake za rambirambi na pole na kuongeza kuwa msiba huo wameupokea kwa masikitiko makubwa sana

Salamu hizo zimetolewa leo na Katibu wa Itikadi na Uenezi, Ndg, Humphrey Polepole na kusema kuwa Chama Chama Mapinduzi kimepokea taarifa za ajali na vifo hiovyo kwa masikitiko makubwa kwa kuwa wanafunzi hao walikuwa katika safari ya kujiimarisha kiitaluma ili kutimiza malengo yao na

"Taifa limepoteza raia wema na nguvu kazi ya sasa na baadae. Chama kinatambua kuwa safari hiyo waliyokuwemo watoto hawa ilikuwa sehemu ya kuwaimarisha kitaaluma ili kutimiza ndoto zao maishani"-  Humphrey Polepole

Aidha Katibu Mkuu wa Chama hicho Comrade Abrahman Kinana ameungana na Watanzania wote kupitia msiba huo na kusema kwamba

"Licha ya kwamba wapendwa wetu wametangulia mbele za haki , wataendelea kubaki katika kumbukumbu zetu daima na tunamuomba Mungu aziweke roho za marehemu mahali pema peponi, Amina. Tunawaombea Kupona haraka majeruhi wote waliotokana na ajali hiyo"- Abrahman Kinana.

Ajali hiyo imetokea jana Mkoani Arusha, Wilayani Karatu baada ya basi walilokuwa wamepanda wanafunzi wa shule ya Lucky Vicent jijini Arusha walipokuwa wakienda kufanya mtihani wa ujirani mwema katika shule ya Tumaini kuacha njia na kutumbukia kwenye korongo eneo la Rhotia Marera, ambapo limeua zaidi ya watu 30 wakiwepo wanafunzi, waalimu na dereva wa basi hilo.

SERIKALI Yagharamia Msiba wa wa Wanafunzi 32 Waliofariki Arusha..!!

$
0
0

Serikali ya Jamhuri wa Muungano wa Tanzania imegharamia Sanda pamoja na majeneza kwa ajili ya Wanafunzi wa Shule ya Lucky Vicent waliopoteza maisha mapema jana kwenye ajali iliyokuwa ikihusisha safari ya kimasomo.

Akitoa taarifa hiyo leo Meya wa Jiji la Arusha , Mh. Calist Lazaro amesema kuwa taarifa za awali zinaonyesha kuwa tayari Serikali imekwishalipia gharama za majeneza na sanda ya kuhifadhia miili ya marehemu ambao kesho wanatarajiwa kufanyiwa ibada katika Uwanja wa mpira wa Sheikh Amri Abeid.

BASHE Awalilia Wanafunzi 32 Waliofariki Katika Ajali..!!!

$
0
0

Mbunge wa Nzega Mjini (CCM), Hussein Bashe ametoa pole kwa familia zilizopatwa na msiba kufuatia ajali iliyotokea jana Jijini Arusha na kusababisha vifo zaidi ya 30.

Mbunge huyo kupitia ukurasa wake wa Instagram amesema kwa niaba ya wananchi wa jimbo la Nzega amewatia moyo wanafamilia wote na Taifa kwa ujumla kufuatia msiba huu na kuwataka watanzania wote kuwa tayari kwa safari hii.

"Kwa niaba ya wananchi wa Jimbo la Nzega niwape pole familia za watoto hawa waulim na madereva ambao mwenyezi Mungu amewaita mbele ya haki" - Hussein Bashe.

"Kila nafsi itaonja mauti na mwenyezi Mungu amewaita hawa binadaam wenzetu katika umri mdogo wakati wazazi wao, familia zao na Taifa likiwa na matarajio makubwa na matumaini makubwa, ila Allah hutupima imani zetu kwa majaribu makubwa kama haya, tumshukuru kwa kila jambo na sisi tujiandae kwa safari hii ya asili na kimaumbile" - aliongeza Bashe.

"Poleni wanafamilia, poleni walimu, poleni watanzania wote"- Hussein Bashe.

LEMA Aanika Meseji ya Mwisho ya Ben Saanane Bungeni..!!!

$
0
0

MBUNGE wa Arusha Mjini, Godbless Lema (Chadema), ameeleza bungeni kile alichokiita ujumbe wa mwisho wa Ben Saanane, Msaidizi wa Kiongozi wa Kambi Rasmi ya Upinzani Bungeni, Freeman Mbowe

Akichangia mjadala wa makadirio ya Wizara ya Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo, Lema alisema: “Kama itanyesha mvua ya radi basi itaambatana na mwanga na cheche zitazowamulika walaghai, watesaji na watetezi wa haki watapata mwanga katikati ya giza totoro la unyanyasaji.”

Mbunge huyo alisema maneno hayo ni ujumbe wa mwisho ya Ben Saanane ambaye hajui kama ni marehemu ama yupo hai.

“Lakini hata kumjadili humu haturuhusiwi. Nje mikutano ya hadhara hatufanyi. Kama kijana wa miaka 16 katika Taifa ambalo halina uhuru wa vyombo vya habari, halina chama cha siasa aliandika maneno machache tu “Assad must go, Assad will be next, leo Syria haina amani,”alisema.

“Uhuru wa habari ni altenative (mbadala) ya amani, si kikwazo cha amani. Watu wanapoongea wanatema nyongo, ‘wanarealise tension’. Leo tunapotaka kujadili mambo ya msingi, mnatumia nguvu na uwezo mlio nao, mtashinda,” alisema Lema.

Alisema kila jambo wanalotaka kulipitisha kwa wingi wao watashinda.

“Katika mchango wangu uliopita, nilisema  Mungu hadhihakiwi, apandacho mtu ndicho avunacho,”alisema

Alifunguka kuwa alipokuwa gerezani, vijana waliokamatwa kwa makosa ya mtandaoni ni wengi na walikamatwa kimya kimya.

“Wanapelekwa mahakamani wanasomewa mashitaka bila ndugu zao kuwapo. Vijana wamejaa magerezani kwa sababu ya ukosoaji,” alisema na kuongeza kuwa haiwezekani kuwa na taifa lenye amani bila kuwa na uhuru wa habari.

“Msifikiri mnatunga sheria kutukomoa sisi. Mna watoto wanakua, wajukuu wanakua…Tunapopigania uhuru wa habari hatupiganii Chadema, CCM tunapigania taifa bora na huru,” alisema.

“Leo ndani ya bunge hatusemi, kwenye mitandao hawaongei, vyombo vya habari havitasema huko mitaani mikutano ya hadhara imezuiwa. Iko siku watu wataingia mitaani kudai uhuru mnaowanyima.

Alisema watu hao watakuwa hawajatumwa na Chadema wala CUF na siku hiyo kila mtu atatafuta nyumba ya kujificha.

“Unapozuia haki, unapozuia uhuru, unapozuia kweli unatengeneza balaa katika taifa hili. Tunalalamika kwa sababu familia zetu zinaishi hapa, tungekuwa na mpango wa kuondoka tungeenda kulalamikia Marekani.

“Tukisema miongozo ni mingi na sijui hata hotuba yangu itakuwaje. Kama hotuba ya Waziri wa habari na michezo mmeifanya hivi, hotuba ya waziri wa mambo ya ndani na uzoefu wa Lijualikani alipokuwa magereza na uzoefu wangu nilipokuwa magereza mtaanza kuizuia kwenye salamu.

“Wabunge mko wengi tusaidieni, mawaziri tusaidieni tukishamalizwa sisi, msumeno utakaouata utakuwa kwenu. Ni nini mnakipigania waheshimiwa wabunge, kita kitu kinakuwa hovyo. Ni fedha?,” alihoji.

Lema alisema utu wa mtu haupimwi kwa ghorofa, cheo, bali unapimwa kwa kazi na wajibu alioufanya duniani.

“Mimi nilikamatwa nje hapo getini nikapelekwa Kondoa nikaweka ‘lock up’ (rumande) saa 4:00 hadi saa 8 usiku nikapelekwa Arusha nikatengwa chumba peke yangu, nikakaa jela nikatoka baada ya miezi minne. Mnaweza kufanya hivi leo,” alisema.

Lema aliongeza kuwa: “Mimi mkitaka kuniua niueni leo, kesho ni mbali. Mkitaka kumuua yeyote hapa muueni leo, kesho ni mbali. Haya mambo mnayotuzuia kuyasema mnafikiri tunasema tunapenda uwanaharakati.”

Alieleza kuwa ana mtoto wa kwanza ana miaka 11 na wa mwisho ana miaka minne na angependa kuona ndoa na harusi na elimu  za watoto wake kwa macho yake.

“Lakini ikibidi nisione hiyo harusi kwa sababu ya kupigania ya ninachokipigania watakumbuka maisha yetu bungeni kupigania property (mali). Yalipigania haki na msingi wa taifa hili ambayo mmeishindwa,” alisema.

Alisema ni muhimu wanaokalia Kiti cha Spika wakaacha faraja, baraka na kuacha kutumia wingi wa wabunge wa CCM.

“Hapo alikaa Mzee Sitta leo ni marehemu, kila mtu atapita kwa wakati wake. Ni muhimu mkapita mkaacha faraja nyuma, baraka acheni kutumia wingi wenu vibaya. Simbachawene wewe una historia. Ulikuwa kondakta Mungu amekuweka mpaka umekuwa hapo, tulitarajia kukuona wewe unapigania nchi hii.

“Leo unaishi utafikiri umezaliwa katika familia ya  Warren Bafet. Mtu akisimama kuongea ukweli unapinga.

Breaking News: Ajali ingine yatokea Tanga, Costa imeigonga Lori

$
0
0

Ajali mbaya imetokea usiku huu eneo la Lusanga, Muheza. Basi aina ya Coaster likitokea Tanga kuelekea Korogwe limegonga Lori kwa nyuma na kusababisha vifo vya watu wengi (karibu gari zima) 


Updates zinakuja zaidi.. 


Mbwana Samatta Afanya Kweli Tena na Kuendeleza Record ya Magoli

$
0
0

Mbwana Samatta afanya kweli Atupia goli la ushindi katika mechi iliyochezwa usiku wa Jana - Genk inashinda 2-1 mbele ya Eupen
Viewing all 104670 articles
Browse latest View live




Latest Images