Quantcast
Channel: UDAKU SPECIAL
Viewing all 104429 articles
Browse latest View live

LEMUTUZ Amchana Live Mchungaji Msigwa Kwa Kuingiza Siasa Kwenye Msiba wa Watoto Arusha

0
0

By @lemutuz_nation
Mchungaji Msigwa, ustaarabu ni kuwafariji wafiwa kwanza na kusubiri kuwazika marehemu yaani Wanafunzi watoto wadogo 32 waliofariki jana ...halafu ndio huko Chadema muanze kuingiza siasa zenu kuhusu Msiba ..ila kwa sasa wakati kuna Mama aliyepoteza Mume hivi karibuni na jana akapoteza Watoto 3 kwenye hii Ajali ya Taifa kwako wewe Mchungaji wa Kiroho kuandika maneno ya Kejeli kwa Rais na wafiwa ni UKOSEFU WA UTU NA HESHIMA KWA MAREHEMU NA WAFIWA ....Rais hata akimuandikia Mungu at this point and time haiwezi kuwarudisha Marehemu kuwa hai au kuwamalizia uchungu wafiwa ...kutafuta sifa za kisiasa kwa kutumia miili ya marehemu watoto wadogo Malaika wa Mungu ni Dhambi kwa Mchungaji kama wewe ....tunawasoma na kuwashangaa sana baadhi yenu huko Chadema kwa kauli za ajabu ajabu wakati huu wa msiba mzito kwa Taifa ...HEBU MUOGOPENI MUNGU KIDOGO .....KWENYE MSIBA MZITO KAMA HUU SIASA ZINATAKIWA KUFIKA MWISHO...tunatakiwa kunawaombea kwa Mungu awape wepesi wafiwa wote na Taifa zima katika kipindi hiki kigumu sana cha kukubali msiba huu mzito sana kwa Taifa ....hakuna mbaye hatakufa ila sidhani kama wewe ungependa ukifa mwanasiasa atumie kifo chako kutafuta sifa......again tunaomba Mungu afanye wepesi ili kesho Makamu wa Rais Mama Samia aongoze vyema mazishi ya Watoto wetu 32 waliopoteza maisha yao kwenye ajali mbaya Arusha jana ....MUNGU IBARIKI TANZANIA! - le Mutuz...
.
.
TOA MAONI YAKO HAPA

Askofu Mokiwa Aamua Kuanzisha Kanisa lake Nyumbani Kwake

0
0

ALIYEKUWA Askofu wa Kanisa la Anglikana Dayosisi ya Dar es Salaam,  Valentino Mokiwa anadaiwa kufungua  kanisa nyumbani kwake. 

Gazeti hili juzi lilielezwa kuwa  licha ya   Dk. Mokiwa kuvuliwa uaskofu na Askofu Mkuu wa Kanisa la Anglikana Tanzania, Dk. Jacob Chimeledya, bado anaendelea kutoa huduma ya kiroho kama kawaida. 

“Kanisa hilo lipo nyumbani kwake Mtaa wa Kilimani, Mbezi kwa Yusuph… watu wanaendelea kusali kama kawaida,” kilisema chanzo chetu (jina tunalihifadhi). 

Jana, MTANZANIA lilifika eneo hilo na kushuhudia baadhi ya waumini wakiondoka kwenda majumbani kwao baada ya ibada kumalizika. 

Waumini hao  hawakuwa tayari kuzungumza lolote na mwandishi wa gazeti hili wakidai kuwa si wasemaji. 

Juhudi za kuonana na Dk. Mokiwa hazikufanikiwa kwa sababu mwandishi  alizuiwa na walinzi. 

Mahojiano  ya mlinzi na mwandishi  yalikuwa kama ifuatavyo: 

Mlinzi: Ni kweli hapa ni nyumbani kwa Askofu Mokiwa, wewe ni muumini? 

Mwandishi: Ndiyo. 

Mlinzi: Unaishi wapi? 

Mwandishi: Naishi Mbezi Mwisho, nilikuwa na kawaida ya kwenda kusali kule Posta, nimesikia baba yupo hapa  ndiyo nikaja. 

Mlinzi: Pole, ibada imeshamalizika,  njoo Jumapili ijayo mapema. 

Mwandishi: Hakuna ibada  katikati ya wiki? 

Mlinzi: Hakuna, njoo Jumapili. Ibada huwa inaanza saa nne kamili asubuhi. 

Wakati mahojiano hayo yakiendelea, mwandishi alishuhudia viti vingi ambavyo vilikuwa vimepangwa  eneo hilo chini ya hema. 

Kwa kuwa hakufanikiwa kuonana na Dk. Mokiwa, mwandishi alilazimika kuwasiliana naye kwa simu lakini hakuwa tayari kueleza kwa kina kuhusu suala hilo. 

Mahojiano yalivyokuwa: 

Mwandishi: Bwana Asifiwe Baba Askofu 

Dk. Mokiwa: Amen 

Mwandishi: Baba Askofu nilifika   hapo nyumbani kwako  sikuruhusiwa kuingia ndani. Kuna taarifa kwamba umefungua kanisa nyumbani kwako, je ni kweli? 

Dk. Mokiwa: Aliyekuambia nimefungua kanisa ni nani? 

Mwandishi: Nimejulishwa na chifu (Mkuu wangu wa kazi) ofisini. 

Dk. Mokiwa: Yeye alijulishwa na nani, huyo chifu wako ana namba za huyo aliyempigia… basi ampigie, amuulize, amwambie zaidi juu ya jambo hilo na mimi nipate jina la huyo mtu na namba zake kwa sababu nataka kuzijua. 

Mwandishi: Lakini Baba Askofu, kimaadili haturuhusiwi kumuandika mtu aliyetupatia taarifa. 

 Dk. Mokiwa: Sasa taarifa za uhakika unazitaka kutoka kwangu mimi au kwa aliyeleta taarifa kwenu. 

  Mwandishi: Tunahitaji uthibitisho kutoka kwako. 

Dk. Mokiwa: Uthibitisho wa nini? Aliyewaletea ndiyo athibitishe, huwezi kuulizwa swali na mtu mwingine halafu unakuja kupata uthibitisho kwangu, hiyo inakwenda sawasawa? 

Mwandishi: Asante Baba Askofu 

Kauli ya kanisa 

MTANZANIA liliwatafuta viongozi wa juu wa kanisa la Anglikana Jimbo la Dar es Salaam  kupata kauli yao juu ya suala hilo. 

Mmoja wa viongozi hao ambaye hakutaka jina lake liandikwe gazetini   alisema hana taarifa rasmi kuhusu suala hilo. 

“Binafsi sina taarifa hizo, ndiyo kwanza nazisikia kwako… siwezi kulizungumzia suala hilo kwa sababu hatuna taarifa rasmi,” alisema. 

MTANZANIA lilitaka kujua iwapo itathibitika kweli ameanzisha kanisa, kanuni, sheria na taratibu za kanisa hilo zinaelekeza vipi na watachukua hatua gani? 

Alisema kwa sasa ni vigumu kufafanua hilo kwa sababu haijajulikana kama kweli Dk Mokiwa ameanzisha kanisa au la. 

“Kwa kuwa hatuna taarifa rasmi, hatuwezi kusema kanuni zinasemaje, hatujui kama kweli kaanzisha kanisa au ni kikundi cha maombi tu kinakutana nyumbani kwake. 

“Kuna tofauti ya kanisa na kikundi cha maombi. Tunahitaji kufanya utafiti tupate habari rasmi ndiyo tuweze kusema kaanzisha kanisa au la. 

“Kanisa lazima liwe na usajili na jina, kwa sasa ni  mapema mno kusema kaanzisha kanisa au la,” alisema. 

Dk. Mokiwa, alivuliwa uaskofu Januari, mwaka huu kwa kile kilichoelezwa kuwa ni utovu wa maadili ya kanisa na kukiuka miiiko ya kanisa. 

Uamuzi huo uliibua mvutano mkubwa ndani ya kanisa hilo na kuzaa makundi mawili hasimu ambako moja linamuunga mkono Dk. Mokiwa na jingine limebaki likimuunga mkono Dk. Chimeledya. 

Hali hiyo ilisababisha mtikisiko mkubwa uliotishia kupasuka kwa kanisa hilo. 

SIMBA Wajibu Mapigo kwa Yanga ..Wamtaja Yondani na Niyonzima Usajili wa Msimu Ujao..!!!

0
0

WEKUNDU wa Msimbazi Simba wamejibu mapigo kwa wapinzani wao wa jadi, Yanga baada ya kumtaja beki wao mahiri, Kelvin Yondani na kiungo Haruna Niyonzima ambao mikataba yao inaelekea ukingoni.

Simba wamefanya hivyo kama sehemu ya kujibu mapigo kwa wapinzani wao hao ambao kila kukicha wamekuwa wakiwataja wachezaji wao mahiri, kiungo Jonas Mkude na mshambuliaji Ibrahim Ajib ambao nao wanamaliza mikataba.

Akizungumza na BINGWA, Makamu wa Rais wa Simba, Geofrey Nyange ‘Kaburu’, alisema wapinzani wao Yanga waache kuwatoa kwenye reli ya ubingwa kwa sasa kwa kutaja nyota wao wanaotaka kuwasajili.

Alisema Yanga wanatakiwa kuwazungumzia nyota wao 14 wanaomaliza mikataba, akiwamo Haruna Niyonzima na Kelvin Yondani akidai kuwa ndio wenye uwezo wa kuichezea Singida United iliyopanda Ligi Kuu msimu huu.

“Kimsingi hata kifikra utaona kuwa si Yanga wala Singida United wenye uwezo wa kuwasajili akina Ajib, Mkude na Said Ndemla kwa kuwa tumeshamalizana nao, lakini pia tambua fika hawa hawawezi kwenda kucheza timu ya porini,” alisema Kaburu.

Alisema ni ngumu kwa nyota hao hivi sasa kuikacha Simba na kwenda kusaini Singida United kama ilivyokuwa ikiandikwa katika vyombo mbalimbali vya habari na kusisitiza kuwa bado wataendelea kukipiga kwa Wekundu hao wa Msimbazi.

Hatua ya nyota hao kutajwa katika usajili wa Singida United inakuja ikiwa ni siku chache tangu timu hiyo ipande Ligi Kuu na kupanga huku wakionekana kuwa na mikakati kabambe ya kutaka kuzinasa saini za wachezaji wengi nyota wa Ligi Kuu Bara, wakiwamo Ajib na Mkude.

Credit - Bingwa

DOGO Janja Afunguka Siri ya Kutupia 'Pamba' Kali..!!!

0
0

MSANII wa muziki wa kizazi kipya nchini, Abdulaziz Chande ‘Dogo Janja’, amewaangalia wanamuziki wenzake wote na kubaini hakuna anayemgusa kwa kupiga pamba.

Dogo Janja amesema kwamba, moja ya siri ya mafanikio yake ni kuvaa kwani hali hiyo imekuwa ikumuongezea ushawishi mkubwa kwa jamii inayomzunguka.

Alisema amekuwa akitumia gharama kubwa kujiweka nadhifu na hajutii gharama anazotumia kwa kuwa ameendelea kuwafunika wasanii wenzake kwa upande wa mavazi.

“Unajua moja ya mafanikio niliyonayo kwenye muziki ni pamoja na upigaji wangu wa pamba ambao umekuwa ukinigharimu pesa nyingi, lakini sijawahi kujutia kwa sababu nimewafunika wasanii wenzangu wote,” alisema Dogo Janja.

Aidha, msanii huyo kwa sasa ameingia kwenye ushindani na msanii mwenzake, Juma Jux ambaye ni miongoni mwa wasanii wanaodaiwa kutupia pamba kali zaidi.

INASIKITISHA...Kumbe Mtoto Aliyekufa Kwenye Ajali ya Basi Arusha Alinusurika Kuuawa na Bomu 2013..!!!

0
0

MTOTO aliyejeruhiwa kwa bomu lililorushwa katika Kanisa la Mtakatifu Joseph Mfanyakazi Olasiti miaka minne iliyopita, Arnold Alex amefariki dunia kwa ajali ya basi la Shule ya Awali na Msingi ya Lucky Vincent juzi.

Arnold ambaye wazazi wake wanatoka Jumuiya ya Familia Takatifu katika Parokia ya Utatu Mtakatifu ya kwa Mrombo, ni miongoni mwa wanafunzi 33, walimu wawili na dereva waliofariki katika ajali hiyo.

Aidha, Arnold ni miongoni mwa watoto wanne wa shule hiyo waliofariki katika ajali hiyo, ambao wanatoka wote pia Parokia ya Utatu Mtakatifu hiyo.

Wengine ni Praise Mwaliambi, Hagai Lucas, Gema Gerald na mwingine ambaye jina lake halikuweza kupatikana mara moja.

Ajali hiyo ilitokea eneo la Malera wilayani Karatu, majira ya saa tatu asubuhi wakati mvua ikinyesha, baada ya gari kushindwa kufunga breki, kuserereka na kutumbukia kwenye korongo.

Wanafunzi waliofariki dunia walikuwa kwenye gari aina ya Toyota Coaster lenye namba za usajili T871 BYS, mali ya shule hiyo.

Taarifa zilizoandikwa kwenye kundi la mtandao wa kijamii wa WhatsApp la Shirika la Neno la Mungu, ambazo zilikuwa zikiarifu taarifa ya kifo cha Arnold na wenzake katika parokia hiyo, ilisema alinusurika katika bomu lililorushwa kanisani Mei 5, 2013 lililoua watu watatu na kujeruhi wengine 50.

Kupitia kundi hilo, Paroko wa Parokia ya Utatu Mtakatifu, Castelino Peddey ambaye wakati wa mlipuko wa bomu kanisani alikuwa paroko huko, alisema Arnold ni miongoni mwa waliojeruhiwa katika tukio lile la bomu.

“Kwa masikitiko makubwa tumepoteza vijana wetu, watoto wetu ambao pia ni wahudumu kanisani (alter boys). Tuwaombee wapate pumziko la milele,”

alisema Peddey huku akiwataja kwa majina na kuongeza, "Arnold miaka minne iliyopita alinusurika katika mlipuko wa bomu lililorushwa kanisani Olasiti."

Hivi karibuni, Arnold aliondolewa mwili chuma kilichowekwa mguuni mwake kama sehemu ya tiba, baada ya kujeruhiwa katika tafrani ya bomu lililorushwa kanisani na watu wasiojulikana.

Tukio hilo lilitokea wakati waumini walipoanza misa ya uzinduzi wa kanisa hilo iliyoongozwa na aliyekuwa Balozi wa Vatican nchini, Askofu Mkuu Francisco Montecillo akisaidiwa na Askofu Mkuu wa Jimbo la Kuu la Arusha, Josephat Lebulu.

Watu watatu waliuawa katika tukio hilo lililowaacha karibu watu 50 wakiwa majeruhi huku baadhi yao wakiwa wameumizwa vibaya.

Polisi ilimshikilia dereva mmoja pikipiki aliyetajwa kuwa Victor Ambrose kulisaidia jeshi hilo katika uchunguzi wake.

Mtuhumiwa huyo aliyekuwa na umri wa miaka 20 wakati huo, alifikishwa mahakamani mbele ya Hakimu Mkazi Devotha Kamuzora Mei 13, 2013, akisomewa mashtaka 21 ya kuua na kujaribu kuua.

Mtuhumiwa huyo, hata hivyo, hakutakiwa kujibu lolote mahakamani hapo kwa kuwa mashtaka yaliyokuwa yakimkabili yalipaswa kusikilizwa na Mahakama Kuu.

MWANAE PRAISE
Katika hatua nyingine, Roland Mwaliambi anayeishi Dar es Salaam alisema kwa mara ya kwanza alipata taarifa ya ajali hiyo kupitia WhatsaApp kabla ya watoto wake waliopo jijini hapa kumpigia simu.

Alisema baada ya taarifa hiyo alilazimika kuchukua usafiri wa haraka wa ndege kuwahi Arusha ambako alithibitisha kwamba mwanae Praise ni miongoni mwa waliofariki katika ajali hiyo.

Alisema mwanae ambaye alionyesha kuwa na wito wa upadre alitarajia kujiunga na Seminari ya Maua iliyopo Moshi Januari mwakani na taratibu zilikwishafanyika za kujaza fomu ya maendeleo yake kitaaluma, lakini ndoto yake imezimwa ghafla.

SERIKALI Tupeni Ufafanuzi Kuhusu Shutuma Hizi za Chama cha Rais Uhuru Kenyatta cha JUBILEE..!!!

0
0

Chama cha Jubilee nchini kenya kimeishutumu serikali ya Tanzania kwa kuruhusu muungano wa NASA unaoongozwa na Raila Odinga kufungua kituo mbadala cha kuhesabia kura nchini Tanzania.

Kwa mujibu wa jubilee , NASA baada ya kunyimwa ruhusa ya kuweka kituo hicho nchini kenya, wameoamua kukihamishia Tanzania, kikiwa na malengo ya kufanya ujumuishaji mbadala wa kura, lakini pia kudukua mifumo ya kuhesabu kura ya tume huru ya uchaguzi nchini kenya.



MY TAKE:
Serikali inabidi watoe ufafanuzi kama swla hili ni kweli au la.

Kuingilia uchaguzi na demokrasia ya nchi jirani kwa kuruhusu chama kimoja kutumia nchi yetu kufanya mambo yake ya kiuchaguzi ni kosa kubwa kidemokrasia na kidiplomasia.

lakini pia sisi wenyewe kama nchi hatuamini katika vyama kujijumlishia kura, ndo maana CHADEMA na kile kituo chao tuliwashughulikia, lakini pia Zanzibar uchaguzi ulihairishwa baada ya seif kujijumlishia kura na kutangaza matokeo kabla ya tume

Kama swala hili ni uongo, Jubilee na mwenyekiti wao ambaye ndo Rais wa sasa watuombe msamaha kama nchi kwa kutuingiza katika siasa zao za majitaka

MAAJABU..Aliyekufa Akutwa Akichunga Ng'ombe Mchana Kweupee..!!!

0
0

MFUGAJI mmoja wilayani Kalambo katika mkoa wa Rukwa amegoma kumrejesha kwa ndugu zake kijana ambaye iliaminika amekufa kwa kuliwa na fisi, lakini akakutwa akichunga mifugo; akidai kwanza malipo ya sh. milioni moja alizotoa kwenye msiba wake.

Tukio hilo la kushangaza lilitokea mwishoni mwa wiki baada ya kijana huyo kukutwa akichunga ng'ombe wa Juma Maeka, ambaye aligoma kumrejesha kwa ndugu zake akitaka kwanza kulipwa sh. milioni moja.

Mkazi wa kijiji cha Tunyi kata ya Mabwekoswe wilayani Kalambo mkoani Lukwa, Mtipa Sisunzu (20) alipotea Septemba, mwaka jana katika mazingira ya kutatanisha na ndugu zake waliweka msiba wakiamini alikufa kwa kuliwa na fisi.

Lakini Sisunzu alizua taharuki kijijini hapo wiki iliyopita baada ya kukutwa akichunga ng'ombe wa Maeka, hali iliyopelekea ndugu kushikwa na butwaa.

Diwani wa kata hiyo, Julias Siwale alisema kabla ya kupotea, kijana huyo alikuwa akifanya kazi ya kuchunga ng’ombe wa mfugaji huyo.

Baada ya kupotea kwake na kuwapo kwa msiba nyumbani kwao, alisema Siwale, Maeka alitoa sh. milioni moja kwa ajili ya kusaidia msibani.

Alisema baada ya msiba kumalizika, kila mtu aliamini kuwa kijana huyo alikuwa amefariki dunia.

Lakini wanakijiji walikuja kushangaa baada ya ndugu wa kijana huyo kumkuta akichunga ng’ombe wa mfugaji huyo katika moja ya mbuga zilizopo mbali na kijiji hicho.

Alisema baada ya kumtaka warudi nae nyumbani, Maeka aliwakatalia akitaka kulipwa fedha ambazo alitoa wakati wa msiba na kupelekea kujitokeza kwa malumbano baina yao.

Diwani Siwale alisema baada ya malumbano kuwa makubwa, ikawalazimu kama uongozi wa kata kuingilia kati na kumwamuru mfugaji huyo kumrejesha kijana huyo kwa ndugu zake sambamba na kumpiga faini ya sh. 100,000 kama fidia usumbufu aliowapa ndugu wa kijana huyo.

Mtendaji wa kata hiyo, Oswald Kalindo alisema awali kila mtu aliamini kijana huyo alikuwa amefariki dunia kwa kuliwa na fisi kwani walimtafuta kila kona ya kijiji na maeneo mengine kwa muda mrefu bila mafanikio.

Alisema kupatikana kwa kijana huyo kumeleta faraja kwa wakazi wa kata hiyo kutokana na kwamba kila mmoja alikuwa na shaka juu ya kupotea kwake.

Alisema wanajipanga kuitisha mkutano kuzungumzia suala hilo.

"Wananchi wametuomba viongozi tuitishe mkutano mkuu ili waweze kuzungumzia hali hii wakidai huenda kuna vijana wengi waliodaiwa kufa wakawa hai wakifanyishwa kazi za kuchunga ng'ombe au kulima mashamba," alisema Kalindu.

RAIS Magufuli Atumia Twitter Kusema Machungu Yake Baada ya Kuyaona Kwenye Tv Majeneza ya Watoto Waliofariki Arusha..!!!

0
0

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Joseph Magufuli ametoa neno na kusema amepatwa na uchungu na majonzi baada ya kuona majeneza ya watoto na walezi wao ambao walipata ajali ya basi huko Arusha.

Rais Magufuli amesema hayo kupitia ukurasa wake wa twitter na kuwataka Watanzania kuomboleza msiba huu kwa umoja huku tukiwaombea marehemu hao wapumzike mahali pema peponi.

"Nimepatwa na uchungu na majonzi makubwa ninapoyaona majeneza ya watoto na walezi wao waliopoteza maisha katika ajali ya basi huko Arusha, tumewapoteza mashujaa wetu katika elimu. Tuwaombee na tuendelee kuwa na subira, uvumilivu na ustahimilivu, tunapoomboleza vifo vya wapendwa wetu tuendelee kuwa wamoja. Mungu ibariki Tanzania" alisema Rais Magufuli.

Mbali na hilo miili yote ya marehemu ambayo imeagwa leo katika Uwanja wa Sheikh Amri Abeid jijini Arusha imesafirishwa na kuelekea sehemu mbalimbali za nchi kwa ajili ya ndugu kufanya maziko ya wapendwa wao hao.

WABUNGE Watoa Posho Zao Kuomboleza Vifo vya Wanafunzi..!!!

0
0

Wabunge wametoa posho ya siku moja ya kikao kwa ajili ya rambirambi ya vifo vya wanafunzi, walimu na dereva wa Shule ya Lucky Vincent ya jijini Arusha.

Spika wa Bunge, Job Ndugai amesema amepata ushauri kutoka kambi zote mbili bungeni kutoa posho yao ya siku moja, fedha ambazo zitagawanywa kwa usawa kwa ndugu wa marehemu wa ajali hiyo.

Kutokana na ushauri huo, ameomba wabunge waamue kuhusu suala hilo jambo ambalo lilikubaliwa na wote.

Kabla ya kuanza kwa shughuli za Bunge leo, wabunge walisimama kwa dakika moja kuwakumbuka waliofariki dunia katika ajali hiyo.

Wanafunzi 33, walimu wawili na dereva mmoja walikufa katika ajali iliyotokea Jumamosi iliyopita eneo la Rotya wilayani Karatu wakati wanafunzi wa shule hiyo iliyopo Olasiti jijini Arusha wakienda kufanya mtihani wa ujirani mwema katika Shule ya Tumaini Junior Acadamy.

RAIS Jacob Zuma Kutua Nchini na Wafanyabiashara 80..!!!

0
0

Rais wa Afrika Kusini, Jacob Zuma anatarajiwa kufanya ziara ya siku tatu nchini kuanzia Mei 10 - 12, mwaka huu akiwa ameambatana na mawaziri sita na zaidi ya wafanyabiashara 80.

Katika ziara hiyo, Rais Zuma atakuwa na mazungumzo na mwenyeji wake, Rais John Magufuli na baadaye kufanya mazungumzo ya pamoja kati ya ujumbe wa Afrika Kusini na ujumbe wa Tanzania.

Akizungumzia ziara hiyo leo, Waziri wa Mambo ya Nje, Dk Augustino Mahiga amesema Serikali za Tanzania na Afrika Kusini zitatiliana saini zaidi ya mikataba 10 kwenye sekta za biashara, uwekezaji, miundombinu, utalii, elimu, afya na nishati.

"Kwa kuanzia tutatiliana saini mkataba wa utunzaji wa mazingira (biodiversity), uchukuzi na nishati. Hiyo mingine bado inaandaliwa, itasainiwa baadaye," amesema Dk Mahiga.

Waziri huyo amesema nchi za Afrika Kusini na Tanzania zimeamua kutumia uhusiano wa kihistoria kama fursa ya kuanzisha uhusiano mpya wa kiuchumi kwa kuongeza uwekezaji na biashara.

Amesema uwekezaji wa Afrika Kusini hapa nchini umezidi kuongezeka kutoka Dola za Marekani 803 milioni mpaka kufikia Dola bilioni 2.2 mwaka 2016 na kuifanya nchi hiyo kuwa ya pili kwa kuwa na uwekezaji mkubwa nchini baada ya Uingereza.

"Uwekezaji wa Watanzania nchini Afrika Kusini bado ni duni, zipo fursa nyingi kule lakini hazijatumika vizuri. Hii ni nafasi kwa wafanyabiashara wetu kuzungumza na wenzao wa Afrika Kusini," amesema.

Katika ziara hiyo, Zuma atashiriki mkutano wa wafanyabiashara, atazindua jengo la Ubalozi wa Afrika Kusini na kutembelea Taasisi ya Moyo ya Jakaya Kikwete.

KIMENUKAA..Lema Amchana Live Mkuu wa Mkoa wa Arusha kwa Kumnyima Nafasi ya Kutoa Salamu za Pole Katika Msiba wa Wanafunzi Leo..!!

0
0



Mbunge wa Jimbo la Arusha Mjini kwa tiketi ya CHADEMA Mhe. Godbless Lema ametoa masikitiko yake na kuonyesha kuumizwa na kitendo alichofanyiwa leo wakati wa kuaga miili ya wanafunzi, walimu na dereva waliofariki katika ajali ya basi.

Lema anasema kitendo cha yeye kama Mbunge wa Arusha mjini pamoja na Meya wa jiji kunyimwa nafasi japo ya kutoa pole kwa familia na wafiwa wakati wa kuaga miili hiyo ni ubaguzi mkubwa. 

"Ninamshukuru Makamu wa Rais kuja kutoa pole kwa watu wa Arusha. Leo ni ubaguzi mwingine katika Taifa Mbunge na Meya kwa kunyimwa nafasi ya kutoa pole" alisema Goodbless Lema 

UKWELI Mchungu..Ukishamuoa Mpe Amri, Akibisha Piga... Mbinu Hii Ilidumisha Ndoa za Mababu Zetu...!!!

0
0

Kumekuwa na mijadala isiyokwisha kwamba: kwann ndoa za sasa hazidumu? Jibu ni rahisi tu.."wanaumme mmeacha kutembeza kichapo kwa wake zenu na mmeanza kusikiliza ushauri wao".

Chanzo cha dhambi ya asili ya mwanadamu ni ushauri wa mwanamke. Adam alishauriwa na Eva wale tunda ambalo mungu alikataza. Adam alipokubali akakitumbukiza kizazi chaka chote ktk dhambi. 

Usikubali kushauriwa na mwanamke ewe mwanaume utaangamia. Hata maandiko yanamuamuru mwanaume kuishi na hawa viumbe kwa akili sana. Maana yake tumia akili yako kuishi naye na wala usitegemee ushauri wake. 

Mdhibiti mkeo umfanye mtiifu na msikivu kwako na kamwe usiruhusu masuala ya usawa wa kijinsia ndani ya nyumba yako.

Ndiyo maana imeandikwa mwanamke na AMTII mumewe. Kutii ni kupokea maagizo bila kuhoji. Kama vile jeshini. Sasa unapoanza kushauriana na mkeo lazima ndoa ikushinde. Maana umeenda kinyume na maagizo ya muumba. 

Wazee wetu waliyafanya haya na wake zao walipojaribu kupingana nao walipata vibano vya haja toka kwa mume, jamii na ndugu wa mke. Kila mtu alimuonya mwanamke mkaidi kwa mumewe. Shetani taratibu anajipenyeza eti siku hizi tunaita maonyo haya ni unyanyasaji. Mke anarekebishwa kwa mkong'oto kama mtoto. Si mnakumbuka usemi "mchelea mwana kulia hulia yeye ".

Sasa nawaonya enyi wanaume "mchelea mke vipigo hupigwa yeye ". 

Nyongeza:
Ndiyo sababu ndugu wakisikia mtoto wao wa kiume amepigwa limbwata (amefanywa mtii kwa mkewe) huja juu. Kwa kuwa ni kinyume cha maagizo toka kwa baba muumba.

ASILI ya Mikono Inayojali ni Moyo Unaojali..Kuwa Muangalifu..!!!

0
0

Sherehe ya Harusi ni siku moja tu, na Ndoa ni ya maisha yote.

Mwanaume/Mwanamke aliyezoea kuchepuka kabla ya Ndoa, ataendelea kuchepuka hata baada ya Ndoa.

Upole na ukimya si kiashiria cha tabia njema.

Ukitaka ambacho hakijawahi milikiwa na mtu yeyote, ni lazima ufanye jambo ambalo halijawahi fanywa na mtu yeyote.

Mungu akitaka kukubariki hukuletea mtu, na shetani akitaka kukuangamiza hukuletea mtu.
Bora uishi mwenyewe kuliko kuoa au kuolewa na mtu asiye sahihi.

Kuna iana tatu za wanaume wa kuwaepuka : walevi, wazinzi na wagomvi.

Kuna aina nne za wanawake wa kuwaepuka: wazinzi, wachawi, wagomvi na wasio tii.
Kuolewa na mchekeshaji haitakufanya uwe na ndoa yenye furaha.

Maneno matatu yanayojenga amani katika ndoa: Nakupenda, Samahani, na Asante.

Mafanikio ya ndoa siku zote ni pembe tatu: Mungu mmoja, Mume mmpja na mke mmoja.

Usioe/kuolewa na pesa au mali. Oa/olewa na mtu kwani pesa/mali hufilisika lakini utu hudumu milele.

Uchumba uliovunjika ni bora zaidi kuliko ndoa isiyo na amani.

Usiweke Kipaumbele chako kwa muonekanao mzuri wa mwanamke . Hakuna mwanamke mbaya, bali anahitaji kupendezeshwa.

Ukiwa rafiki mwema, utawavuta marafiki wema. Vivyo hivyo kwa marafiki wabaya.

Asili ya mikono inayo jali ni moyo unaojali.

MAGUFULI Afunguka Kuhusu Mfanyabiashara Aliyeiuza Tanzania Uholanzi, Kufeli kwa Sera Yake ya Sukari..!!

0
0

Rais Magufuli alipokuwa akiongea na wafanyabiashara nchini juzi alisema serikali sio kwamba haitaki kushirikiana na sekata binafsi na inatambua mchango wa sekta binafsi kwa uchumi wa nchi

Wafanyabiashara kutokuwa waaminifu
Waziriwa ardhi ametaja compexity kwenye umiliki wa ardhi, amesema kuna wafanyabiashara amabao sio waaminifu na lazima wamuone mchungu Ametolea mfano kuna mfanyabiashara aliyenunua ardhi Tanzania hekta 132,000 na kwenda kuombea mkopo mabenki ya Uholanzi mwaka 2015 na ardhi yenyewe haijaifanyia kazi kabisa
Mfanyabiashara huyo alishirikiana na RUBADA taasisi ya serikali akataka kununua nyingine zaidi ya 300,000 maeneo ya Rufiji akafanye tena hivyo

Pia amesema sekta binafsi wamekuwa na tamaa sana akatolea mfano tenda ya kujenga hosteli za UDSM kuwa walikuwa waijenge kwa bilioni hadi 200 lakini TPBA walijenga kwa bilioni 10 tu

Sukari
Pia amezungumzia sakata la sukari kuwawafanyabiashara walikuwa wanaficha na wakiona demand ya sukari pia imekuwa kubwa mfano kipindi cha mfungo wanapandisha kwa makusudi
Na amedai pia aliwapa wenye viwanda vibali vya kuagiza sukari nje kwa kjuwa wao ndio sukari ya nje inaathiri viwanda vyao lakini wenye viwanda wakaviuza tena vibali kwa wafanyabiashara

Wafanyabiashara kuhujumu kilimo

Rais na waziri mkuu pia amezungumzia wapo wafanyabiashara wanaokuwa wanahujumu kilimo kwa kukopa fedha kwenye benki ya kilimo ambazo serikali ndio imekuwa ikiiwezesha lakini wamekuwa wakifanyia fedha hizo mambo mengine kama kununua malori ya usafirishaji makontena

Alimsusia waziri mkuu wa India
Pia amesema alisusia kwenda kuweka jiwe la msingi kwenye plant ya kufua umeme aliyoambaiwa na waziri mkuu wa India alipokuja kwa sababu waziri mkuu huyo alimchomekea tu alipokuja na terms zao wala hazikujulikana na hakutaka kuiweka nchi kwenye IPTL nyingine

Kuibiwa na makampuni ya madini
Pia amesema makampuni ya madini yanapaswa yaweke hisa zao soko kuu la DSM kwa kuwa wamekuwa hawana accounts za kuzishika wala assets zozote mkiingia kwenye dispute na fedha wanazoleta nchini ni za mshahara tu, na wanakuwa wana declare losses kwenye statement zao na kwenye stock exchange London hisa zao zinafanya vizuri

Ila amesema changamoto za wafanayabiashara amezisikia na atazifanyia kazi na wakikwazwa na mtu serikalini basi wasisite kutaarifu mawaziri wake au yeye na sio kusema serikali ni mbaya

RC Gambo Amjibu Lema kwa Nini Hakumpa Nafasi ya Kuongea Jana Kwenye Shughuli ya Kuaga Wanafunzi Waliofariki Arusha..!!!

0
0

Katika page yake ya instagram RC Gambo amewashukuru wanaarusha kwa kujitokeza kwa wingi kuwaaga watoto wetu na pia amekanusha uzushi unaoenezwa na Lema 



VYETI Feki Vyaleta Kilio Sekta ya Afya..!!

0
0

JUMLA ya watumishi wa umma 35 wa Halmashauri ya Bahi mkoani Dodoma wameondolewa kwenye ajira kutokana na kukutwa na vyeti feki katika zoezi la uhakiki huku 26 kati yao wakitoka katika sekta ya Afya.

Akizungumza na waandishi wa habari ofisini kwake jana, Mkurugenzi wa halmashauri hiyo, Rachel Chuwa alisema mbali na afya, sekta nyingine iliyoathirika na hali hiyo ni elimu ambayo ina watumishi nane wenye vyeti feki.

Alisema sekta ya kilimo na mifugo ina mtumishi mmoja.

Hata hivyo, alisema pamoja na watumishi hao 35 kukumbwa katika zoezi hilo hakuna huduma iliyosimama licha ya kuwepo upungufu katika baadhi ya maeneo.

Alisema katika ya watumishi hao wa afya 26 kuna waganga wa vituo, madaktari wasaidizi, matabibu na wauguzi.

MILLARD Ayo Asimulia Alivyonusurika Kwenye Ajali Kama Iliyoua 32 Arusha ..!!!

0
0

Mtangazaji mahiri wa kipindi cha Amplifaya cha Clouds FM, Millard Ayo wakati akitoa salamu zake za rambirambi kufuatia vifo vya wanafunzi 32, walimu 2 pamoja na dereva mmoja, amefunguka kuzungumzia namna alivyonusurika kwenye ajali kama hiyo akiwa mdogo.

Katika ajili hiyo ambayo amedai ilitokea mwaka 1994 mkoni Arusha Ngorongoro, ilisababisha vifo vya wanafunzi wenzake  wanne ambao alikuwa nao kwenye safari hiyo ya kuelekea Serengeti.

Akiongea Jumatatu hii, Millard Ayo amedai katika ajali hiyo alimpoteza rafiki yake ambaye alikaa naye siti moja.

“Pole sana kwa familia za Arusha najua ni kiasi gani sasa hivi watu wana huzuni sana, watu 32 kwa wakati mmoja ni kitu kikubwa sana,” alisema Millard.

“Na mimi hii ajali nilipoisikia tu ni wanafunzi imenikumbusha mbali sana kwa sababu hata mimi mwenyewe niliwahi kupata ajali kama hiyo mwaka 1994 tulikuwa Ngorongoro sehemu moja maarufu inaitwa Malanja Cross. Tulikuwa na gari la jeshi wanafunzi wa shule ya msingi, Patandi Primary Schools Tengeru Arusha tukielekea Serengeti kuangalia wanyama lakini bahati mbaya gari ikafeli breki ikaingia bonde la ufa, wakafa wanafunzi wenzangu wanne akiwemo rafiki yangu ambaye nilikaa naye siti moja,” aliongeza Millard.

Mtangazaji huyo amedai yeye wakati basi hilo likibiringika, alikuwa amebanwa na chuma kichwani hivyo hakuweza kutoka mpaka watu walivyokuja kumwokoa.

Pia amesema aliumia vibaya katika mguu wake wa kushoto.

Credit - Bongo 5

MAMA Samia - Waliondoka ni Malaika Ambao Hawana Hatia..!!!

0
0

Makamu wa Rais Mama Samia Hassan Suluhu amesema wanafunzi wa shule Lucky Vicent waliofariki kwa ajili juzi ni malaika ambao hawana hatia, na kuwataka madereva kuwa makini barabarani

Akizungumza katika uwanja wa Sheik Amri Abeid, Arusha jana, Mama Samia amesema ajali na msiba ulitokea ni wa aina ya pekee kwa kuwa umegusa nyoyo za watanzania wote.

‘Wamendoka kwa matendo yasiyo ya kwao, ni watoto waliokuwa wanaenda kujifunza lakini Mungu amewachukua katikati, msiba huu kwa kweli umetupa majonzi mengi na wakati ni huu mgumu, hatuna la kusema ila tuwaombe Mungu awapokee salama,” alisema.

Pia alichukua nafasi hiyo kuitaka serikali na jamii kwa ujumla kutufumbua macho katika kufanya marekebisho ya mambo mengi ambayo yanakosoro na kuleta maafa kama haya.

“Naomba nichukue nafasi hii kupaza sauti yangu kuwaomba sana ndugu zangu madereva kuwa waadilifu na kuwa makini wanapokuwa barabarani, serikali yetu inapiga vita utumiaji wa vilevi wakati unapoendesha, tunapiga vita utumiaji wa dawa za kulevya kwa sababu tunajua ni moja ya sababu inayoleta hasara ya namna hii.

“Madereva wanapochukua abiria wahakikishe magari yanachukua abiria kwa uwezo yalitengenezewa, watanzania hatuhimili na haipendezi kila siku kusikia kuna ajali na kupata misiba,” alisema.

Aliongeza kuwa waombolezaji katika kipindi hiki hawapo pekee yao bali taifa lipo pamoja nao na watanzania wote wanasimama kwa maombi na sala.

“Huzuni hii si yenu, bali ya ni ya taifa na Afrika Mashariki kwa ujumla, kwa kuwa kazi ya Mungu haina makosa tunaamini aliwapenda sana watoto wetu,” alisema na kuongeza.

“Nitoe wito kwa Wizara ya elimu, jeshi la polisi, wazazi na walezi kuwa makini kuhakisha sheria za usalama barabarani zinazingatiwa kwa kuchukua hatua za kulinda watoto wetu na watanzania kwa ujumla wao ,” alisema.

KINANA Aibuka Msibani Arusha ..Ateta na Lowassa na Mbowe..Habari Vichwa vya Magazeti ya Leo 9/5/2017..!!!

MANGE Kimambi Akipa Tano Kituo cha Radio Clouds FM Msiba wa Wanafunzi Arusha

0
0

Mange Kimambi Akipa Tano Kituo cha Radio Clouds FM Msiba wa Wanafunzi Arusha

Ameandika haya hapa chini:
.
#Regrann from #mangekimambi_ - Sijui nyinyi, Ila mimi nimeona hawa watu walichangia mnoooo kufanya siku ya jana kuwa na hisia za kipekee au kuiongezea umuhimu siku Hiyo.... Kwanza jeshi la Wananchi, kusema kweli waliji organize vizuri, shughuli ikawa na uzito. Seriously jeshi letu jana lilitufanya tukajivua kuwa watanzania....
.
.
Clouds huwa wana matatizo yao sometimes ila kwa jana kwa kweli walikuwa the people's station for real! Yani Clouds waliivalia njuga shughuli na kuipa uzito wa aina yake..
.
.
Huyu Kijana @engine kusema kweli nyimbo yake Jana iliongeza hisia za uchungu. Tena ukiwaza alitunga nyimbo ile ndani ya Sasa 24. Yani nyimbo yake ilikuwa on repeat. Ilikuwa inapigwa na kurudiwa over and over. Yani ndo ilikuwa official song ya shughuli ile....Yani Dah nyimbo iliendana na Shughuli. So Na yeye tumpe nafasi kubwa kwenye tukio la Jana. @engine I hope kuna mtu ataona kipaji chako akunyanyue na wewe utoke. Watanzania watakusapoti sana maana umekuwa unaimba nyimbo za kuwagusa hisia zao.
Viewing all 104429 articles
Browse latest View live




Latest Images