Quantcast
Channel: UDAKU SPECIAL
Viewing all 104664 articles
Browse latest View live

Nape "CCM haipo Tayari Kuwabembeleza Walio Susa Bunge Warudi, Waendelee Kukaa Barabarani"

$
0
0
Kamati Kuu ya Chama cha Mapinduzi chini ya Mwenyekiti wake Rais DK JAKAYA KIKWETE ilikutana Dodoma May 5 2014 ili kujadili na kuzungumzia masuala mbalimbali ikiwemo mchakato wa Bunge la Katiba ambalo limesitishwa mpaka mwezi wa nane.
Akitoa mapendekezo ya Kamati Kuu, Katibu wa Itikadi na Uenezi wa CCM Nape Nnauye amesema licha ya kutoa mapendekezo yatakayofanikisha upatikanaji wa katiba mpya, chama hicho kimepinga vitendo vya baadhi ya wabunge kupinga waziwazi kwenye majukwaa juu ya kuendelea kwa bunge Maalum.
Namkariri akisema ‘kamati kuu pia inasikitishwa na juhudi za makusudi za baadhi ya watu au vikundi vya watu kuamua kuendeleza upotoshaji kuhusu mchakato mzima wa mabadiliko ya katiba, wameamua kupotosha kwa kwenda barabarani, kufanya mikutano au kuzungumza na Waandishi wa habari kupotosha baadhi ya mambo’
Kwenye sentensi nyingine Nape amesema chama chake hakipo tayari kuwabembeleza wajumbe waliosusia kuhudhuria vikao kwa kusisitiza ‘hatuna mpango wa kuzungumza nao na tunampango wa kushughulika nao mtaani wanakokwenda, sio sisi na wala hatuna mpango wa kuishawishi Serikali wala viongozi wa kitaifa kuwabembeleza kuwarudisha bungeni, mimi nadhani waendelee kukaa barabarani’

Mwanajeshi Apewa Kichapo Kikali na Askari wa Usalama!

$
0
0

Askari wa Usalama barabarani eneo la Makumbusho, Dar wakimpiga Dereva wa gari ambaye amejitambulisha kama mwanajeshi! Tukio hili limetokea mida ya saa 9 mchana huu. Bado haieleweki chanzo ni nini.

Je, unadhani hivi ndivyo askari wetu wanatakiwa kutekeleza majukumu yao?

Bila Upendeleo, Mabinti Toka Mkoa gani Tanzania Wanaongoza Kuwa na Sura Nzuri?

$
0
0
Bila upendeleo, mabinti toka mkoa gani Tanzania wanaongoza kuwa na sura nzuri? Kama Unajua Andika Mkoa huo kwenye Comment

Wanafunika Nywele Lakini Wanafunua Matiti!

$
0
0
Afrika kama tunavyoifahamu, ilikuwa ni sehemu ya Mila na Tamaduni bora kabisa, sehemu ambayo heshima adabu vilikuwa ni msingi wa jamii yake, hasa kwenye jamii.


Ni sehemu ambayo masikini waliishi kwa mlo mmoja lakini bado waliheshimiana, kuvumiliana na kupendana. Ni sehemu ambayo binti angekutwa akifanya mambo ya aibu basi wazazi wake wangenyooshewa vidole kwa malezi mabaya kwa binti yao. Vivyo hivyo kwa vijana wa kiume. Mambo haya yalipatikana zaidi kwenye nchi nyingi za kiafrika na Tanzania ni mojawapo.

Ila kwa sasa, Waafrika wengi, hasa vijana wamezua mijadala mingi inayotokana na mienendo ya tabia zao zinazopelekea kuvunjika kwa Mila na Tamaduni bara hili…. Kitu kinachozua maswali juu ya nani wakulaumiwa kwa kuvunjika na kuharibika kwa Mila na Tamaduni za Afrika…? Mfano mdogo uko kwenye hiyo picha hapo juu, huyu binti anafunika nywele kwa imani lakini anafunua matiti. Dini, shule, wazazi, walezi na walimu wameshindwa kukisaidia hiki kizazi. Ni nani wa kulaumiwa? Kwangu mimi hiki bado ni kichekesho tu!

Ajabu:Mvua ya Samaki Yawapa Neema ya Kitoweo Raia

$
0
0
Afrika Mashariki na sehemu nyingine tumezoa kuwa kama mvua haitakuwa ya maji pekee basi itakuwa mvua ya mawe yanayotokana na barafu, lakini raia wa Sri Lanka wao wana uzoefu wa kukinga mvua ya samaki na kutumia kama kitoweo!
Wakaazi wa kijiji kimoja huko Magharibi mwa Sri Lanka wamekutwa na neema ya aina yake baada ya kunyeshewa mvua ya samaki wadogo wanaofaa kwa kitoweo.

Wakielezea tukio hilo, wanakijiji hao wamesema walisikia kitu kizito kikidondoka waligundua kuwa ni samaki, waliwakinga samaki hao na waliwapata wengi wenye uzani wa kilo hamsini ambao waliweza kuwatumia kama kitoweo.

Kwa mujibu wa BBC, Wanasayansi wameeleza kuwa mvua ya samaki hutokea wakati ambapo upepo mkali unakuwa juu ya maji ya kina kifupi na kusababisha mzunguko wa maji unaovuta karibu kila kitu kilicho ndani ya maji ikiwa ni pamoja na samaki na vyura.

Wameeleza kuwa viumbe hao wa majini wanaweza wakasafirishwa kwa masafa marefu na kushikiliwa na mawingu kwa muda hata baada ya ule mzunguko wa maji kuisha, na baadae wanashuka kama mvua.

Tukio la aina hii liliwahi kutokea Sri Lanka mwaka 2012 ambapo mvua ya samaki aina ya kamba wa baharini ilinyesha kwa mtindo huo.

Mvua hii ikinyesha vijijini huenda wanakijiji wakaomba iwe ya mafuriko ya samaki…anyways, ingekuwa vipi kama mvua inayonyesha sasa hivi Dar es Salaam ingekuwa mvua ya samaki wanaotumika kwa kitoweo?

Kocha wa kwanza mwanamke kufundisha soka kwenye klabu kubwa Ulaya

$
0
0
Ni kawaida kuona makocha wa jinsia ya kiume wakiwa wanafundisha timu za mpira wa miguu za wanawake, lakini ni mara chache sana tumewahi kushuhudia kocha wa kike akiwa anaifundisha timu ya wanaume.
Lakini klabu ya ligi daraja la kwanza ya Ufaransa Clermont imeweka historia mpya kwenye soka la nchi hiyo kwa kumtangaza mwanamama Helena Costa kuwa kocha wao mpya kuanzia msimu ujao, na kumfanya kuwa mwanamke wa kwanza kufundisha soka la hadhi ya juu nchini Ufaransa. 
Costa, 36, alikuwa kocha wa timu ya taifa ya wanawake ya Irani tangu mwaka 2012 lakini sasa amekubali kumrithi Regis Brouard kwenye klabu ya Clermont.
Helena ambaye ni raia wa Ureno, aliwahi kufanya kazi kama kocha mkuu wa kituo cha soka cha klabu ya Benfica na timu kadhaa nyingine nchini Ureno, ambapo aliweza kushinda makombe kadhaa. Pia aliwahi kuifundisha timu ya wanawake  ya taifa ya Qatar.

Lady Jay Dee Aonyesha Zarau kwa Tuzo za Kill, Eti Hajui Kama Zimeshafanyika

$
0
0
Lady Jaydee alishinda tuzo mbili mwaka huu kwenye KTMA lakini kwasababu ambazo hajazisema,hakuwepo mwenyewe kuchukua tuzo hizo, shabiki yake akamuuliza kupitia twitter na Lady Jay Dee Akamjibu Kwani Zimeshafanyika? Akiwa na Maana Hajui kama Tuzo hizo zilishafanyika na Hajui kama Alishinda.....Mweeeeeeh

Picha za Mahabusu Waliovua Nguo Mwanza Hizi Hapa

$
0
0
Mahabusu wawili kati ya sita wanaotuhumiwa kwa kesi za mauaji, wakiwa wameng'ang'ania mlingoti wa Bendera ya Taifa huku mnoja akiwa mtupu mara baada ya kutoroka toka kwenye msafara wa mahabusu waliokuwa wakiingia mahakama ya wilaya ya Nyamagana na kisha mmoja wao kuvua nguo.
 Inspector Henry (shati la bahari) akiwa na Inspector Veda (mwenye koti) wakisikiliza hoja za  Thobiasi Warioba (35), aliyeamua kuvua nguo zote na kubaki mtupu akiwa ameng'ang'ania mlingoti wa Bendera ya Taifa uliopo katika viwanja vya Mahakama ya Hakimu Mfawidhi Wilaya ya Nyamagana mkoa wa Mwanza, ambaye anakabiliwa na kesi ya mauaji Na. 32/2012.
 Inspector Veda (mwenye koti) akichukuwa maelezo ya Thobiasi Warioba (35), aliyeamua kuvua nguo zote na kubaki mtupu akiwa ameng'ang'ania mlingoti wa Bendera ya Taifa uliopo katika viwanja vya Mahakama ya Hakimu Mfawidhi Wilaya ya Nyamagana mkoa wa Mwanza, ambaye anakabiliwa na kesi ya mauaji Na. 32/2012. akiwa na mwenzake Hamis Ramadani (30).
Inspector Henry akiwasihi mahabusu hao wawili wanaotuhumiwa kwa kesi za mauaji, kuachia mlingoti wa Bendera ya Taifa na kurudi kwenye chumba cha mahakama kwaajiri ya taratibu za kesi.

Alazwa Hospitali kwa Miaka 45

$
0
0
Singida. Usiombe yakupate. Abdi Lanjui (75), ametimiza mwaka wa 45 akiwa wodini katika Hospitali ya Mkoa wa Singida alikolazwa tangu mwaka 1971 baada ya kupata ajali ya lori.
Lanjui aliyekuwa dereva wa taasisi aliyoiita “Mamlaka ya Pamba,” alipata ajali hiyo mkoani Mwanza baada ya lori alilokuwa akiendesha kuchomoka gurudumu la mbele na kupinduka.

“Sababu ya mimi kugeuza wodi kuwa makazi yangu ya kudumu ni ajali iliyosababisha kupooza kuanzia kiunoni hadi kwenye nyayo. Kwa kuwa sinyanyuki kitandani, nimepata vidonda kuanzia makalioni hadi miguuni. Kwa sasa naishi maisha magumu mno,” alisema.

Aomba msaada

Kutokana na hali hiyo, ameiomba Serikali na jamii kwa jumla kumsaidia chakula kwa kuwa hana ndugu wa kumsaidia. Lanjui ambaye hawezi kunyanyuka kitandani, alisema kwa miaka mingi uongozi wa hospitali ya mkoa ulikuwa ukimhudumia kwa kumpa chakula lakini baadaye huduma hiyo ilisitishwa, hivyo kumfanya awe ombaomba na maisha yake kuwa ya mlo mmoja kwa siku.

“Kwa vile siwezi kunyanyuka kitandani na sina ndugu yeyote, nimekuwa nikiwaomba msaada manesi na watumishi wengine wa hapa hospitali. Nashukuru sana wamekuwa wakinisaidia bila kuchoka na kuniwezesha kupata walau mlo wa siku moja,” alisema. Lanjui ambaye anazungumza vizuri pia aliomba msaada wa fedha za kwenda Hospitali ya KCMC, Moshi ili apatiwe huduma zaidi ya matibabu.

Mwanza hadi Singida

Lanjui aliyelazwa katika Wodi Namba Nne katika hospitali hiyo tangu Januari Mosi, 1971, awali alilazwa katika Hospitali ya Sekou Toure, Mwanza kuanzia mwaka 1969 mara baada ya kupata ajali.

Alisema akiwa Sekou Toure mwishoni mwa mwaka 1970, hali yake ilibadilika na kuwa mbaya ndipo alipomwomba mwajiri wake amrudishe nyumbani katika Kijiji cha Mhintiri katika Wilaya ya Ikungi mkoani Singida ili ‘akasubiri kifo chake.’

Hata hivyo, alisema uongozi wa Mamlaka ya Pamba ulikataa kumpeleka kijijini kwake, badala yake ulimkabidhi katika Hospitali ya Mkoa wa Singida mwaka 1971.

Alisema wakati anapata ajali na kulazwa hospitalini, wazazi na ndugu yake wa pekee, walikuwa wamekwishafariki dunia.

Kaimu Mganga Mkuu wa hospitali hiyo, Mussa Kamala alisema hivi sasa mgonjwa huyo anahudumiwa na hospitali kama watu wengine wenye ulemavu ambao hawatozwi gharama yoyote.

Upinzani Watoa Masharti Magumu Kushiriki Uchaguzi Mkuu 2015

$
0
0
Serikali imetakiwa kuandaa taratibu za mpito za kushughulikia Uchaguzi Mkuu ujao ili kunusuru nchi kuingia katika mtanziko unaoweza kuwa chanzo cha machafuko ya kisiasa, endapo utafanyika bila kupatikana kwa Katiba Mpya la sivyo Kambi Rasmi ya haitashiriki.
Hayo yalielezwa jana na Kiongozi wa Kambi Rasmi ya Upinzani Bungeni, Freeman Mbowe alipokuwa akitoa hotuba ya kambi hiyo bungeni kuhusu Makadirio ya Ofisi ya Waziri Mkuu.

“Hatuwezi kuingia uchaguzi wa vitongoji, vijiji na mitaa kwa utaratibu uliopo leo, hatuwezi kwenda kwenye Uchaguzi Mkuu mwakani na Tume ya Uchaguzi kama ilivyo leo, hatuwezi tena kwenda kwenye Uchaguzi Mkuu mwakani wakati matokeo ya uchaguzi wa Rais hayawezi kuhojiwa mahakamani.”

Aliongeza: “Hatuwezi kuingia kabla na hoja ya mgombea huru haijapatiwa majibu, tukiwa na daftari la wapigakura lililopo leo na hatuwezi kulikubali daftari jipya litakalotengenezwa kama wadau wote hatutashirikishwa kikamilifu.”

Kauli hiyo ya Mbowe imekuja siku moja tu baada ya Waziri Mkuu, Mizengo Pinda kuwasilisha bungeni, Bajeti ya ofisi yake ambayo imetenga Sh5 bilioni kwa ajili ya uchaguzi wa Serikali za Mitaa uliopangwa kufanyika baadaye mwaka huu.

Mbowe alisema kama ilivyo kawaida, Serikali na CCM inaweza kupuuza tahadhari hizo na kulazimisha kwenda katika chaguzi hizo katika mazingira ambayo hayana mwafaka kama inavyoonekana sasa katika Mchakato wa Katiba Mpya.

Matokeo ya Mechi Kati ya Man City na Aston Villa Haya Hapa

$
0
0

Ni game full time ni Manchester City 4 magoli ambayo yamefungwa na Dzeko kwenye dakika 64′+ 72′+ Jovetic 89′ + Yaya Toure kwenye 90 +3) – 0 Aston Villa. Kwa Mtonyo huo Kwa sasa Man City Inaongoza Ligi kwa Point 83 , Liverpool Ana Point 81 ....

Ufisadi:Magari Mapya 11 Yaliyonunuliwa na Serekali Hayajulikani Yalipo

$
0
0
Ofisi ya Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali CAG imeamplfy kwamba kitendo cha Serikali kukosa nyaraka za mali zake kumechangia baadhi ya watendaji wasio waaminifu kutumia mwanya huo kujisogezea mali za umma.
Katika ripoti yake ya Ukaguzi kwa mwaka 2013 CAG Ludovick Utouh amesema ofisi yake imebaini upotevu wa magari 11 yaliyonunuliwa kwa ajili ya matumizi na mamlaka ya maendeleo na biashara Tanzania (TanTrade) ambayo hadi sasa hayafahamiki yalipo.
Ofisi yake inalifanyia uchunguzi suala hilo na tayari imegundua hayo magari yalisajiliwa kwa namba binafsi badala ya namba za serikali huku akisema ‘wizara ya viwanda na biashara ilinunua magari kwa ajili ya bodi ya biashara  na tunaomba kusema magari hayo tumejaribu kuyafatilia lakini hayaonekani na hayajulikani yalipo na ni magari mapya yalinunuliwa kwa ajili ya TanTrade lakini TanTrade wenyewe wanasema hawajayapokea na Wizara inasema haijui yako wapi’

Snura Aingilia Kati Beef la Wema Sepetu na Kajala

$
0
0
  MSANII wa filamu na muziki, Snura Mushi ameingilia kati ugomvi wa wasanii wenzake, Wema Sepetu na Kajala Masanja na kuwaagiza wamalize tofauti zao.

Wasanii hao ambao wameingia kwenye bifu la kufa mtu kufikia hatua ya kuanikana kwenye vyombo vya habari huku chanzo kikubwa kikitajwa ni shilingi milioni 13 ambazo Wema alimlipia Kajala kama faini ya kesi ya kuuza nyumba iliyokuwa imewekwa rehani kisheria iliyokuwa ikimkabili mahakamani.

Nyumba hiyo iliwekwa rehani kutokana na mume wa Kajala, Faraja Agustino kushitakiwa kwa kosa la kutakatisha fedha haramu.

Snura amewataka Wema na Kajala kutoangalia nani ana makosa, wamalize tofauti zao.
“Nawashauri wenzangu wasigombane na kuwekeana vinyongo hiyo ni kama wanawapa watu faida,

nawaomba wamalize kwani haipendezi kabisa kwa jinsi walivyokuwa wameshibana. Kama mmoja anaona amemkosea mwenzake ajishushe na kuomba msamaha,” alisema Snura.
By Na Chande Abdallah na Mayasa Mariwata GPL

Jokate Ataja Sifa za Mume Wake Mtarajiwa..Wanaume Kazi Kwenu

$
0
0
MTOTO mzuri kunako anga la watangazaji Bongo, Jokate Mwegelo ameibuka na kuanika sifa za mwanaume ambaye anafaa kuwa mume wake

Akipia stori na paparazi wetu juzi jijini Dar, Jokate alisema anapenda mwanaume ambaye atajua kutafuta fedha kwa nguvu zote, awe anajua kubembeleza na awe na nidhamu kwa wazazi wake.

“Sifa ya mume ninayemtaka, anapaswa kuwa mtafutaji wa fedha, sipendi mwanaume asiyependa kutafuta, awe anajituma kwa kazi zake na kwa mpenzi au familia yake na pia ajue kunibembeleza,’’ alisema Jokate.

Baby Madaha Aumbuka...Aonekana ni Muongo wa Kutupwa

$
0
0
STAA wa muziki na filamu Bongo, Baby Joseph Madaha ambaye aliwahi kutangaza kuacha fani ya maigizo na muziki amejikuta akiumbuka kwa mashabiki wake kutokana na kuendelea kukomaa katika gemu kwa kuachia kazi mpya na kuandaa matamasha mbali mbali.
Msanii huyo alitoa uamuzi huo kwa madai kuwa alichoshwa na skendo za kila kukicha ambazo wakati mwingine zimekuwa zikimshushia hadhi katika jamii, ikiwemo skendo ya kunaswa kwenye mtego wa kujiuza ilioandliwa na Oparesheni Fichua Maovu ‘OFM’ ya Global.

Akizungumza na paparazi wetu hivi karibuni, Baby Madaha alisema hawezi kupinga kama alizungumza hayo isipokuwa tangu atoe kauli hiyo amejikuta akizidi kupata mafanikio makubwa katika muziki.

“Naweza kusema nimeumbuka kwa kile nilichoongea, maana nimejikuta nashindwa kutekeleza nilichowaambia mashabiki wangu sababu dili zinakuja, siwezi kuziacha,” alisema Baby.

Matatizo yote Yanayokusibu Sasa Basi! Suluhisho Ndio Hili

$
0
0
Matatizo yote yanayokusibu sasa basi! Doct Shkh Omari bin Mshamu ndio suruhisho la matatzo yako..Ni Doct aliyebobea mambo ya sayansi inayohusika na mfumo wa mwili wa binadamu na maisha yake, na ni mtaalamu wa mambo ya tiba za jadi..Anayejulkana zaid ya nchi nne zinazoizunguka Tanzania.
Ni mtaalamu wa matatizo haya;
A.Saratan ya ini(Kansa)
B.Kisukari
C.Kifua kikuu na pumu
D.Miguu kuwaka moto
E.Kichaa na taila(mtindio wa ubongo)
F.Moyo mkubwa(bila kupeleshen)
G.Uzazi kwa wale wenye matatzo ya kuzaa(mgumba)
H.Kupata watoto mapacha
I.Kuua virus vya ukimwi(itokanayo na mbuyu)
J.Nguvu za kiume(gori 4 mpaka 7)
K.Bonge tumboni(bila kupeleshen)
L.Kuvimba mapumbu(bila kupeleshen)
M.Kushepua body, kuongeza hips, kukausha maji maji ukeni, kuondoa harufu mbaya ukeni na kusmamisha matiti
N.Kifaa cha kurefusha na kenenepesha uume saizi uitakayo kutoka UK,kiitwacho Handsome pamp, knapatkana kwa sh.100000 badala ya sh.150000 kama knavyouzwa clinic zingne.

Mafuta yatakayokufanya ushinde mtihani kwa lever yoyote ile ema shindano lolote lile utakaloshiriki na pia kupandishwa cheo kazini pindi ukipakaa.
Dawa hizi zitokanazo na mimie zimethibitisha na kualalishwa na wizara ya afya na ustawi wa jamii Tanzania, kuwa hazna madhara yoyote kwa mtumiaji.
PIA
1.Pete za bahati
2.Pete itakayokufanya uendapo kununua kitu cha laki 1 na kutoka na kitu cha laki 2
3.Pete za mvuto wa biashara
4.Pete za mvuto wa kimapenzi
5.Kitambaa chekundu cha kumrudisha mpenzi au rafiki aliyepote(kukusaliti)
6.Limbwata kwa mume au mke
7.Tego la kuganda kwa mume au mke(kwa wale walio ndani ya ndoa tu)
8.Uchawi wa chuma ulete
9.Uchawi wa radi
Hivi pia vyote vnapatikana na utamiliki mwenyewe kama utaitaji.
Kumbuka kuwa tiba na vitu hvi hazina masharti,kafara wala c za miujiza ya aina yoyote ile.

Pia tuna mahabara ya kisasa, inayotoa huduma ya vipimo vya aina yote katka mwili wa binadamu,,vipimo ni bure kwa wewe mgonjwa ambae unaitaji kutibiwa, utalipia gharama za matibabu tu.
Na wewe mteja wa mbali uswaze wapi kwa kufiki endapo kama unataka kuja clinic kwetu,,Tuna nyumba kubwa zenye vyumba vya kutosha na vyenye hadhi ya kulala watu wa kada za aina yote na sehemu kubwa ya kupumzika wagonjwa na wauguzi wao iloambatana na clinic yetu.
Epuka matapeli kumbuka kuwa hatuna tawi lolote nchini.
Fika kwenye clinic yetu, Tupo Liwale mjini jirani na msikiti mkuu.
Kwa wateja wa mbali wasliana nasi kwa namba +255788476047 Masaa24.
Kumbuka kuwa dawa itakufikia popote ulipo kwa uharaka zaidi bila ya usumbufu wa aina yeyote endapo
kama utaitaji utumiwe.

Master Jay "Uchawi Bongo Flava Upo Nimewahi Kuona Msanii Anatokwa na Panzi Kooni"

$
0
0
Producer mkongwe wa muziki na mmliki wa MJ Records, Master J, amesema uchawi upo kwenye muziki na ameshawahi kushuhudia msanii wa bendi akitolewa panzi kooni iliyoingia kimazingara ili ashindwe kuimba.
Akiongea na kipindi cha The Cruise cha East Africa Radio jana, Master J amesema wapo baadhi ya wanamuziki wanaojihusisha na masuala ya ushirikina.

“Hivi ni vitu vya kawaida, huu ni utamaduni wetu,mimi sishangai wala sioni kitu chochote cha ajabu. Mimi nilianza kwa kurekodi muziki wa rap tu, lakini baadaye nikaanza kurekodi band, Taarab na mchiriku ndio maana nishasemaga nimeshawahi kuona kwenye band mtu anatoa panzi kabisa kutoka kooni, akafanyiwa maujanja ndo akaweza kuimba. Kusikia wasanii wa Bongo Flava wanajihusisha sio kitu cha ajabu kwani wao si ni Watanzania na Tanzania taka usitake utamaduni wetu ni uchawi, uchawi upo,kwahiyo mimi sishangai,” alisema.

Exclusive: Dr Cheni alazwa hospitali kutokana na ugojwa wa Dengue

$
0
0
Msanii wa filamu nchini, Dr Cheni amelezwa toka jana katika hospitali ya Buruhani jijini Dar es Salaam kutokana na ugonjwa wa Dengue.

Akizungumza na Bongo5 leo Dr Cheni amesema kuwa bado hali yake sio nzuri kutokana na kuishiwa damu na mwili kupoteza nguvu.

“Bado ni nipo hospitali ya Buruhani naumwa hili gonjwa jipya,sijui unaitwa Dengue,” amesema. “Bado hali yangu sio nzuri kabisa,yaani naumwa,napungukiwa damu,mwili unauma,kwahiyo yanai bado ninaumwa,hii homa ilinianzia wiki iliyopita sema nilikuwa bado hawajaigundua ila jana ndio wameingundua,” ameongeza.

Dr Cheni amesema kuwa anawaomba Watanzania wamuombee kwani bado hali yake sio mzuri.

Diamond Platnumz Aendelea Kuwagalagaza Wasanii wa Afrika Kwenye Nominations za Kora

$
0
0
Pamoja na kwamba tuzo za Kora hazina tena ‘kiki’ kama zamani, Diamond Platnumz ameendelea kuwagalaza wasanii wa Afrika kwakuwa jina lake ndilo limekuwa likitajwa zaidi na mashabiki kwenye akaunti ya Facebook ya tuzo hizo...Click <HAPA>Kuona Page hiyo

Katika wiki ya ya 17 tangu watu waanze kutaja majina ya wasanii wa Afrika, Diamond ameendelea kuongoza na kuwaacha mbali wasanii wakubwa wakiwemo Koffie Olomide, Sarkodie, Fally Ipupa, Werason na wengine.

Imebainika:Serikali ilifanya Siri Ugonjwa wa Dengue

$
0
0
Ugonjwa wa homa ya dengue ambao umezidi kusambaa mkoani Dar es Salaam na kuathiri wilaya zake tatu za Temeke, Ilala na Kinondoni umezua hofu na taharuki kubwa kwa wananchi. Takwimu za Kitengo cha Utafiti wa Magonjwa cha Ifakara (IHI), kimeweka kambi katika Hospitali ya Mwananyamala hapa jijini kutafiti aina za homa zinaonyesha kuwa, kwa miezi miwili ya Machi na Aprili pekee, wagonjwa 85 walibainika kuwa na ugonjwa huo
Waziri wa Afya na Ustawi wa Jamii, Dk Seif Rashid.

Sisi tunadhani Serikali inastahili lawama kwa kutochukua hatua stahiki mapema kupambana na ugonjwa huo, ambao uliingia Dar es Salaam kwa mara ya kwanza mwaka 2010 na kuua wanafunzi kadhaa wa Chuo cha Usimamizi wa Fedha (IFM). Juni mwaka jana, Wizara ya Afya ilithibitisha kuwapo kwa ugonjwa huo na Machi 26 mwaka huu, ilitoa taarifa kwa umma, ikisema wagonjwa 70 walikuwa wamebainika, 58 kati yao wakiwa Kinondoni, saba Temeke na watano Ilala.

Hata hivyo, wizara hiyo haikupaswa kuishia katika kutoa taarifa tu pasipo kuwaelimisha na kuwahamasisha wananchi nchi nzima kuhusu ugonjwa huo, namna ya kujikinga na nini cha kufanya iwapo wataambukizwa. Ulihitajika uwazi badala ya usiri, vinginevyo ugonjwa huo usingeenea kwa kasi tunayoishuhudia hivi sasa.
Viewing all 104664 articles
Browse latest View live




Latest Images