Quantcast
Channel: UDAKU SPECIAL
Viewing all 104776 articles
Browse latest View live

MSUKUMA Adai Wabunge Walienda kwa Waganga Wakati wa Uchaguzi..!!!

$
0
0

Mbunge wa Geita Vijijini(CCM), Joseph Kasheku 'Msukuma' amesema ni wabunge wawili au watatu ambao tu ndiyo ambao hawakupita kwa waganga wa kienyeji wakati wa uchaguzi.

Msukuma aliyekuwa anauliza swali la nyongeza bungeni, amesema wabunge wamekuwa na tabia ya kuwatetea wasanii waliowasaidia kwenye uchaguzi, lakini ukifika kwa waganga wa kienyeji wanakaa kimya wanapopata matatizo.

Msukuma ambaye Naibu Spika amemtaja kama mwakilishi wa waganga wa jadi, ameuliza kwa nini kisianzishwe chuo cha kuwapatia waganga hao mafunzo.

Akijibu swali hilo, Waziri wa Afya, Ummy Mwalimu amesema waganga hao ni muhimu kwa kuwa asilimia 60 ya Watanzania wanatumia tiba zao mbadala.

Amesema wizara inaendelea kutoa elimu na imewaagiza waganga wakuu wa wilaya kuwa wasajili wa waganga wa jadi.

DK Shein Amponza Kigogo wa ACT - Wazalendo..Asimamishwa Uanachama kwa Kushiriki Uchaguzi wa Marudio na Kukubali Kushindwa na CCM..!!!

$
0
0

CHAMA cha ACT-Wazalendo kimemsimamisha uanachama aliyekuwa Makamu Mwenyekiti wa chama hicho upande wa Zanzibar, Ramadhan Ramadhan kutokana na kukaidi adhabu ya onyo aliyopewa na viongozi wa chama hicho.

Hatua hiyo inatokana na msimamo wa kiongozi huyo kushiriki uchaguzi wa marudio wa Zanzibar uliofanyika Machi 20, mwaka jana pamoja na kumtambua Rais Dk. Ali Mohamed Shein.

Taarifa iliyotolewa jana na Ofisa Habari wa chama hicho, Abdallah Khamis ilieleza, uamuzi wa kusimamishwa uanachama kwa kiongozi huyo umetolewa kwenye kikao cha pili cha Kamati Kuu ya chama hicho kilichofanyika Mei 7, mwaka huu mjini Kahama.

Alisema kutokana na hali hiyo, kikao hicho kilimteua Juma Saanani ambaye alikua Naibu Katibu Mkuu Zanzibar, kuwa Makamu Mwenyekiti wa chama hicho kutoka Zanzibar, hadi suala la Ramadhan litakapoamuliwa na Halmashauri Kuu ya chama hicho.

“Uamuzi wa kusimamisha uanachama Ramadhan ulikuja baada ya kamati kuu ya chama chetu kubaini kuwa aliwahi kukutwa na makosa mbalimbali na Kamati ya chama ya Uadilifu,” alisema Abdallah.

Kutokana na hali hiyo kamati hiyo iliamua kumpa adhabu ya onyo kali na kumtaka kutorudia makosa yake ambayo ni pamoja na kupingana na msimamo rasmi wa chama wa kutoutambua na kutoshiriki kwenye uchaguzi batili wa marudio wa Zanzibar uliofanyika Machi 20, 2016 lakini alikaidi.

Alisema pia, aliwahi kutangaza kwenye vyombo vya habari kuwa chama hicho kinamtambua na kumuunga mkono Rais wa Zanzibar, Dk Ali Mohamed Shein kinyume na matamko rasmi ya Chama.

TETESI za Uwepo wa Al Shabab Nchini..Mwanafunzi wa Chuo cha St Joseph Akamatwa Akiwa na Bastola Yenye Risasi 13..!!!

$
0
0

Mwanafunzi wa Chuo Kikuu cha Mtakatifu Joseph,  Lazaro Mbise (23) anashikiliwa na jeshi la polisi kwa kosa la  kukutwa na bastola pamoja na risasi 13 ambayo alimwibia baba yake.

Kamishna wa Polisi Kanda Maalum ya Dar es Salaam, Simon Sirro amesema mwanafunzi huyo alipokamatwa alikiri kuiba bastola hiyo pamoja na fedha kiasi cha Sh800, 000.

“Bastola hiyo ni LUGER cz100 mtuhumiwa alikiri aliiba pamoja na risasi kutoka kwa baba yake,” amesema Sirro.

Kamishna Sirro ameagiza mzazi wa mtuhumiwa kukamatwa ili afikishwe mahakamani kwa kosa la kutohifadhi bastola yake vizuri.

TENGA Aula Caf..Ateuliwa kuwa Bosi wa Vilabu Vyote Afrika..!!!

$
0
0

Kikao cha Kamati ya Utendaji cha Shirikisho la Soka Barani Afrika, CAF kimemteua Rais wa heshima wa Shirikisho la Soka Tanzania (TFF), Leodgar Tenga kuwa rais wa kamati ya usimamizi wa mfumo wa leseni kwa vilabu, {Management of club licensing system}

Uteuzi huo umekuja muda mchache baada ya kukaa kikao cha kamati ya Utendaji chini ya uenyekiti wa CAF Rais Ahmad walipokutana hivi karibuni katika Hoteli ya Sheraton Manama, Bahra

Aidha, Tenga atakuwa akisaidiwa na Rais wa Shirikisho la Soka nchini Afrika Kusini, Danny Jordan ambaye ameteuliwa kuwa makamu wa kamati hiyo pamoja na kupewa cheo kingine cha urais katika kamati ya Masoko na Televisheni .


MBUNGE Nchini Australia Apigwa Picha Akimnyonyesha Mwanae Wakati Bunge Likiendelea..!!!

$
0
0

Watu husema hakuna kinachozidi upendo wa mama na wengi wao wamedhihirisha hilo kama ilivyokuwa kwa  Seneta wa Australia, Larissa Waters ambaye aliamua kumnyonyesha mtoto wake wa miezi miwili akiwa bungeni.

Waters ameweka rekodi ya kuwa mwanasiasa wa kwanza kufanya hivyo  nchini humo.

Hata hivyo Bunge la nchi hiyo liliruhusu kunyonyesha lakini tangu lilipotoa ruhusa hiyo hakuna mbunge aliyewahi kufanya hivyo.

Waters  amewatia moyo wanawake kwa kusema kuwa wanataka wanawake wazazi wengi zaidi bungeni kwa sababu hakuna shaka juu ya kunyonyesha mtoto.

Gari Aina ya Toyota Spacio inauzwa Bei Poa

$
0
0

Gari Aina ya Toyota Spacio inauzwa , IPO Dar Masaki...
Kilometer 67,746
Mil 9 Maelewano yapo
Piga simu namba 068 702 1597





BREAKING: Maalim Seif awasili kanisani kwa Askofu Gwajima.

$
0
0

Katibu Mkuu wa Chama cha Wananchi CUF Maalim Seif amewasili jioni hii katika kanisani LA Ufufuo na Uzima lililopo Ubungo DSM, linalomilikiwa na  Askofu Josephati Gwajima. 

Video na Habari zaidi zitakujia Hivi Punde, Unachotakiwa kufanya Ingia YouTube andika Muungwana Tv kisha 'Subscribe' ili uwe Wakwanza kuitazama.

Jux ' Siumizwi Kabisa na Picha Anazopiga Vanessa na Wanaume Wengine'

$
0
0

Jux amewajia juu watu wanaojadili sana kuhusu wanaume wanaopiga picha na mpenzi wake Vanessa Mdee. 

Hitmaker huyo wa ‘Umenikamata’, amesema yeye wala haumizwi na picha hizo kwa kuwa anafahamu kuwa mrembo wake huyo yupo kazini kwani hata yeye anafanya kama hivyo na inaonekana ni kawaida? 

“Si kweli mimi nilimind, sababu kama kupiga picha za namna hizo Vanessa anapiga na watu wengi sana picha za namna ile. Naomba nirudi nyuma kusema hili tena wasichana kwenye tasnia yetu sisi wavulana ndiyo tunatakiwa kuwasupport sana kwa sababu wapo wachache,” amesema Jux. 

Muimbaji huyo ameongeza, “Mimi hata nikipiga picha na wanawake 10 hapa, watu watajua tu Jux anafanya video ila Vanessa akipiga picha hizo watu watasema huyu mwanamke mhuni.”

Sina beef na Adam Juma, nilisema ukweli Kuwa Hanscana ni Zaidi yake– Rama Dee

$
0
0

Msanii wa muziki, Rama Dee amedai kauli yake “Hanscana ni muongozaji mkali wa video kuliko Adam Juma” siyo kama alimkosea heshima muongozajii huyo mkongwe wa video za muziki.

Muimbaji huyo amedai alitaka kumwambia ukweli muongozaji huyo ili kama anaweza kubadilka abadilike.

“Sikujenga beef na Adam Juma, nilisema kitu ambacho nakiona,” Rama Dee alimjibu mmoja  kati ya mashabiki wake ndani ya Kikaangoni EATV.  “Kwanini nimwambie kwa siri, hakuna cha siri, mtu akizungua unamwambia moja kwa moja,”

Aliongeza, “Mimi sina beef na mtu, mimi nafikiri mtu akiambiwa ukweli anatakiwa kutulia siyo na wewe unanza kutafuta namna ya kujitetea,”

Muimbaji huyo amedai hataki kuzungumzia zaidi mahusiano yake na Adam Juma kwa kuwa tayari ameshamalizana naye.

Hata hivyo kauli hiyo ya ‘Hanscana ni mkali kuliko Adam Juma’, ilipingwa na wadau mbalimbali katika mitandao ya kijamii wakidai muimbaji huyo amemkosea heshima Adam Juma.

SERIKALI Yaifungia Benki Hii Nchini kwa Kuhusishwa na Ughaidi..!!!

$
0
0

Moja kati ya benki kubwa nchini Tanzania, FBME, imenyang’anywa leseni na kufungiwa huduma kutokana na kuhusishwa na kusaidia kutoa fedha kwa taasisi ya kigaidi ya Hezbollah.

Benki ya FBME, zamani Federal Bank of The Middle East, ilikua na makao makuu yake nchini Cyprus kabla ya kuhamisha rasmi nchini Tanzania mwaka 2003.

Tanzania imelazimika kufuta leseni ya uendeshaji wa benki hiyo kufuatia ripoti za kiinteligensia kutoka kwa serikali ya Marekani, ambayo ilikua ikiendesha uchunguzi dhidi ya benki hiyo tangu mwaka 2014.

FBME inasadikiwa kuwa miongoni mwa benki kubwa nchini Tanzania yenye mtaji wa zaidi ya dola bilioni 4.

TRUMP Amtumbua Jipu Bosi wa FBI..Ni Baada ya FBI Kuchunguza Mahusiano ya Trump na Rais Putin wa Urusi..!!!

$
0
0

Rais Donald Trump amemfuta kazi Mkurugenzi wa Shirika la Ujasusi (FBI), James Comey kutokana na namna alivyoshughulikia barua pepe za aliyekuwa mgombea wa urais kupitia chama cha Democratic, Hillary Clinton.

Hata hivyo, wanachama wa Democratic wamesema kuwa Comey alifukuzwa kazi kwa sababu FBI ilikuwa inachunguza madai ya uhusiano kati ya Trump na Urusi.

Hatua hiyo imekuja baada ya kubainika kwamba Comey alitoa habari za uongo kuhusu barua pepe za Clinton kwa Bunge la Congress wiki iliopita.

Rais Trump alimwandikia barua Comey kumwambia kuwa alikubaliana na mapendekezo ya mwanasheria mkuu Jeff Sessions kwamba ameshindwa kuliongoza vizuri shirika hilo.

Sessions alisema kuwa Wizara ya Sheria ina nidhamu ya hali ya juu, uadilifu wa sheria na mwanzo mpya unahitajika.

Ikulu ya Whitehouse imesema mrithi wake atapatikana haraka.

Pamoja na hayo yote, kiongozi wa chama cha Democratic katika Bunge la Seneti, Chuck Schumer amesema kuwa ni wakati mwafaka sasa kumteua kiongozi maalumu wa mashtaka kusimamia uchunguzi huo juu ya uhusiano na Urusi.

MSAADA..Nimedata na Manjonjo ya Huyu Changudoa Hadi Nafikiria Kumuacha Mke Wangu..!!!

$
0
0

Nikiwa katika pitapita zangu, nilimuona mtoto Mmoja mrembo Sana akiwa ameket kibarazani(Kama mita 500 kutoka ninapoishi)

Nilishangaa kuona navutiwa naye Sana kiasi cha kutotaka atoke machoni kwang, nilisogea Na kumpa hi, Aliitikia kwa sauti ya uchovu Sana (kimahaba)

Nilipiga naye story za hapa Na pale nikijidai natafuta chumba cha kupanga mitaa Ile, nikafanikiwa kupata namba yake ya simu..!

Mara kwa Mara nimekuwa nikicjat naye mida ya mchana maana alidai ameolewa, pia Na mm nna mke..!

Niliendelea kumchimba Ili kujua Maisha yake kiundani, ndipo nilipogundua kuwa anaish mjin kwa kuuza uchi wake...( Kuna meng Sana ya kuandika kuhusu suala hili ila ngoja niishie hapo kwani sio lengo)

Siku zilizid songa huku tukiendelea kuchati.Alianza kunitext usiku, nilichat naye huku nukiavoid hali hiyo maana mke akijua n tatizo, 

Ilifikia kpnd akawa anantumia picha zake za nusu uchi,akiwa na chupi,bikini na wakat mwngne alijiselfisha akiwa kifua wazi,( nilidata na maumbile ya huyu changudoa, chuchu zake zilisimama barabara)

Kidume nilikosa cha kufanya maana huyu dada alikuwa ananipeleka mbali Sana kihisia.., baada ya kuhakikisha mazingira ya kiusalama wa kiafya ya huyu dada ilinibidi nifanyenaye mapenziTu hakukuwa na namna..!

Kilichonileta hum Ni suala moja Tu, huyu dada anajua mapenz balaa kumzid wife maana nnakoelekea sifurahii penz la mke wangu, sasa najiuliza haya maujuzi mke wangu atayajuaje Ili niweze kufrah naye, na kunavitu nikisema nimuelekeze Ili nienjoy atastukia na kujiuliza nimeyajuaje..!

Niko njia panda wakuu, naomben ushaur maana mke Wang nampenda lakini huyu changudoa ananteka na maujuzi yakee..

Nifanyeje???!!!!

MWAKYEMBE Awashauri Wasanii Waache Kuimba Nyimbo za Siasa.......Asema Anayetaka Siasa Aache Mziki Akagombee Udiwani..!!!

$
0
0

Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo, Dkt Mwakyembe amewasihi watanzania kuacha kutumiwa na viongozi mbalimbali kwa kuimba nyimbo za masuala ya kisiasa na badala yake wafanye kazi ambazo zitawasaidia kupata mafanikio.

Waziri Mwakyembe aliyasema hayo bungeni wakati akijibu hoja mbalimbali zilizotolewa na wabunge wakati wa kujadili hotuba ya bajeti ya wizara yake.

"Tembea dunia kote huko, nimekwenda Nigeria na kuona wasanii wakubwa kama Tiwa Savage, Don Jazz, Akon, P Square wale hawaimbi kuhusu viongozi wao wa kisiasa.

"Hivyo niwasihi wasanii wangu, muache kuimba kuhusu siasa sababu hii ni ‘entertainment industry’ (sekta ya burudani) na sio ya masuala ya kisiasa, "alisema Waziri Mwakyembe.

Aidha, waziri alisema kama kuna msanii yeyote anayetaka kuwa mwanasiasa aache muziki akagombee udiwani kwani wasanii waliotaka kuchanganya siasa na muziki walipotea kabisa.

WAZIRI wa Katiba na Sheria Waziri wa Katiba na Sheria Prof. Palamagamba Atajwa Kwenye Orodha ya Watumishi Wenye Vyeti Feki..!!!!

$
0
0

Sakata la watumishi wa umma waliofanyiwa uhakiki wa vyeti limezidi kuchukua sura mpya kila iitwapo leo ambapo awamu hii, Waziri wa serikali ya awamu ya tano amebainika kuwa miongoni mwa watumishi ambao vyeti vyao vina utata.

Waziri wa Katiba na Sheria, Prof. Palamagamba John Aidan Mwaluko Kabudi ametajwa katika orodha ya watumishi ambao vyeti vyao vina matatizo ambapo uhakiki wake ulifanyika wakati akiwa mkufunzi katika Chuo Kikuu cha Dar es Salaam (UDSM), kabla ya kuteuliwa kuwa mbunge na kisha waziri.

Waziri Prof. Kabuni ambaye amebobea katika sheria, pamoja na waafanyakazi wengine wa UDSM wametajwa katika orodha ya watumishi wa umma ambao vyeti vyao havijakamilika.

Katika orodha aliokabidhiwa Rais Dkt Magufuli na Waziri wa Nchi, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Angellah Kairuki, jumla ya watumishi 9,932 walikutwa na vyeti vya kughushi, huku wengine zaidi ya 1,500 wakiwa na vyeti vyenye utata na wengine walikuwa wamepeleka vyeti pungufu kwenye uhakiki.

Akizungumza suala hilo, Makamu Mkuu wa Chuo Kikuu cha Dar es Salaam, Prof. Mukandala alisema kwa Prof. Kabudi ametajwa katika orodha hiyo kwa sababu cheti chake cja kidato cha nne hakikuonekana wakati wa uhakiki. Aidha, Prof. Mukandala alisema kuwa tayari Prof. Kabudi ameshawasilisha cheti hicho na kwamba watakipeleka Baraza la Mitihani la Taifa (NECTA) kwa ajili ya uhakiki.

Wakati Rais Magufuli akikabidhiwa ripoti ya uhakiki wa watumishi wenye vyeti feki alisema kuwa, kwa wale ambao wanavyeti pungufu, wanaendelee kubaki kazini lakini uhakiki ufanyike vizuri kwa sababu si kila mtu alipita kidato cha sita kiweza kufika chuo. Hivyo kama hakupita kidato cha sita alafu ukamwambia akuletee cheti, hatokuwa nacho.

Hotuba ya Prof. Jay Bungeni Yamkuna Darassa

$
0
0

Rapa Darasaa CMG amempongeza Mbunge wa Mikumi Joseph Haule ‘Prof Jay’ kwa kuendelea kupaza sauti Bungeni kudai maslaHi ya wasanii na sanaa yao.

 

Mbunge huyo wa Mikumi (Prof Jay) alitumia zaidi ya dakika nane Bungeni kuchangia katika bajeti ya Wizara ya Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo, alichokizungumza hiki hapa chini, kisha pongezi za Darassa.


Prof Jay akiwa na Mbunge wa Mbeya Mjini, Joseph Mbilinyi ‘Mr Two Sugu’ bungeni

Mh Spika kabla sijaanza kuchangia na declare interest mimi ni mwanamuziki  bora wa Hipo Hop Afrika Mashariki na Kati  na kusini mwa jangwa la sahara, kwa hii wizara inanihusu sana. Mh. Spika

historia ya nchi yetu inaonyesha tangu wa wahasisi wa nchi walipokuwa wanafanya harati kadha wakadha walikuwa wanatumia  sana sanaa, nakumbuka Mwl Nyerere  alikuwa akitumia wasanii mbali mbali kama Mzee Mwinamila,  Mzee Moresi Nyunyusa ambao hadi leo midundo yao inatumika katika taarifa za habari huko TBC  wakati wanafanya harakati za kupromote vijiji vya ujamaa.

Lakini Mh. Spika pia wanakina Mzee Mkapa walikuwa wanawatumia wanamashairi kama wakina Mzee Tambalizeni na watu wengine kama hao,  inaonesha ni jinsi gani sana ni kitu cha muhimu na ni nyenzo muhimu sana katika taifa  kuonyesha utamaduni, mila, lakini pia kufikisha ujumbe.

Tunajua kwamba sanaa inatumia sana mafundisho  lakini pia inakanya, inaonya  na inasifia inapobidi lakini kwa sasa kwa siku za usoni imeonekana wasanii kadhaa wakadha wamekuwa wakibanwa kutoa yale mawazo yao kama ilivyotokea kwa msanii  Roma ambaye ametekwa na akaja kuachiwa katika mazingira ya kutatanisha. Lakini pia msanii Nay wa Mitego ambaye alishikwa na baadae akaja kutolewa  kwa msamaha wa Rais, hii inawapa hofu wasanii kutoa kile ambacho walikuwa wanakifikiria kwa sababu tunaamini msanii yuko huru  na anatakiwa kutoa mawazo huru kulisaidia taifa letu.

Hata sisi tulikuwa tukifanya muziki tunaimba nyimbo kama ‘Ndio Mzee’ na vitu vingine wengi mnazijua, Mh. Waziri (Mwakyembe) wewe ulisema ni shabiki wangu  mkubwa kwa hiyo tunaamini kabisa mlikuwa mnajua jinsi tumetumia sanaa hii kufundisha kukanya , kuonya na kuburudisha pia.

Lakini Mh. Spika wasanii wa Tanzania tumekuwa tukiwatumia katika kampeni mbalimbali  kama Maleria,  na hata katika uchaguzi uliopita  mmeona jinsi wasanii walivyokuwa wakitumika,  na baadae mmewatumia kama makarai na kuwaweka uvunguni, makarani yanatumika katika kujenga korofa  lakini nyumba ikishakamilika yanaweka uvunguni hayatakiwa hata kuonekana mbele za wageni.

Wasanii wa Tanzania wamekuwa wakitumika kwa stahili hiyo na wengi wamekuwa masikini sana  na hali yao ya uchumi imekuwa ngumu kwa sababu wamekuwa hawathaminiwi tena.

Katika nchi zilizondelea kama Marekani, Uingereza mataifa hayo yanapata mapato makubwa sana kupitia sanaa zao. Takwimu iliyofanywa hapa Tanzania na Lulu Art Promotion inaonyesha kwamba muziki pekee yakee inachangia zaidi ya asilimia moja katika pato la taifa. Naamni wizara ikitumia umakini na ikamamu kuwekeza wasanii wa Tanzania wataweza kuchangia pato kubwa sana katika pato la taifa, lakini pia imesaidia katika kutoa ajira, wasanii wameweza kujiajiri na kuajiri vijana wengi sana.

Mh. Spika katika bajeti ya mwaka 2016/7 serikali ilitenga pesa kidogo sana ambayo ni sh.  bilioni 3 na katika hali ya kustahajabisha ni sh. bilioni 1. 9 ndio ilienda katika wizara hii, na sasa hivi tunaweza kuona imetengwa fedha kidogo ambayo tunaona kama utani. Imetengwa sh. Bilioni 6 katika sekta nzima ya Habari, Utamaduni Sanaa na Michezo. Sanaa inatoa ajira kwa vijanaa wengi wa kitanzania tulitakiwa tuweke pesa nyingi na hiyo pesa kufika katika maeneo yanayohusika.

Mh. Spika hivi karibuni kumekuwa na malalamiko ya wasanii wa filamu ambao juzi wameandamana na wakiwa wanapaza sauiti zao wakitaka haki zao za msingi, tunaamini movement yoyote inayofanyika katika kutetea haki inahitaji muungano wa watu wengi. Kama mngetaka kufanikiwa katika hili jambo mngemtumia kama Waziri wa Habari kama alivyofanya press conference yake na Roma tuliona vyombo vyote vikionyesha mshikamano na umoja wao, tunafamu sanaa ya filamu inatoa ajira na sisi tunaitetea.

Kwa mfano mdogo, kabla ya kufanya filamu inabidi utoe sh. 500,000 katika bodi ya filamu kwa ajili ya kupeleka script yako, alafu inabidi utoa tena sh 300,000 kwa ajili ya kupewa kibali cha kushoot, ukishamaliza kushoot, unaipeleka tena kukagulia ambapo unatoa sh. 1,000 kwa kila dakika katika filamu, ukionda kufunguliawa faili Cosota unalipa tena zaidi ya sh. 40,000, baada ya hapo unapeleka TRA wanakupa stika ambayo ni sh. 8 ndani, sh. 8 nje (sh 16. Kwa kila copy), ukimaliza hapo unaenda kunegotiate   na yule distributor ambaye mkishakubalia bei anakata asilimia 30 kwa ajili ya kupeleka kwenye kodi ya Tanzania.

Unaweza kuona jinsi wasanii wa filamu wanavyoumia, lakini njia waliyoitumia kutetea haki zao wametumia mlango mwingine wa kutokea. Kwa hiyo ni muombe waziri huu ni muda wa kukaa na wasanii kuunganisha nguvu zote, tunamuhitaji waziri wa mambo ya ndani, Cosota, Basata ili kujua shida za wasanii  lakini pia tatizo la hati miliki, Mh Spika katika hati miliki namba saba ya mwaka 1999 imeipitwa sana na wakati, wasanii wanaibia kazi zao, uaramia umekuwa mkubwa lakini tukikamata wezi hamnza adhabu kali wanayopata.

Lakini hata juzi msanii Darassa alienda Arusha TRA wakavamia show yake wakasema hayo mapato inabiki wagawane asilimia 18, watu wameituba from nowhere, Darassa amenda Arusha kwa gharama zake, amenda kufanya matangazo, amelipa ukumbi,wameenda wamefunga mageti saa 12 wanamwambia lazima tukate asilimia 18, matokeo yake wamekuja kufungua mageti saa sita usiku, kijana wa watu aliyejiajiri kupitia mzuiki amepata hasara, amepata watu 200/300  TRA wakakata fedha zao.

TRA kama mnataka mapato kaendi chini na wasanii tutengeneze mfumo mzuri ambao utawasaidia wasanii wa Tanzania wanapowekeza kupitia kitu kama hiki

Sasa baada ya hotuba hiyo Rapa Darassa naye akachukua nafasi yake, kupitia mtandao ya instagram Darassa ameandika hivi, “asante sana Mh. Professor Jay kwa kuendelea kupigania sanaa yetu ikae kwenye msingi mzuri japo unajua wewe sio mfanyaji kwa kiasi kikubwa! I can see unataka kue na future nzuri kwa kizazi cha baadae, God bless you brother,”.


Je Diva Anamjibu Dkt. Mwakyembe Kuhusu Kupinga Wasanii Wasiimbe Nyimbo za Kisiasa?

$
0
0
Ni muda mchache baada ya Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo, Dkt. Harrison Mwakyembe kusema wasanii waachane na tabia ya kuimba nyimbo za kisiasa kwani hakuna msanii aliyewahi kufikia mafanikio makubwa kwa kufanya hivyo.


Mtangazaji Diva the Bawse kupitia mtandao wake wa twitter ameandika ujumbe ambao unasadikika pengine amejibu kauli ya waziri huyo.

Video: Chid Benz Afunguka Kwa Mara ya Kwanza Baada ya Kutoka Rehab ‘Stay Away From Drugs’

$
0
0
Rapa Chid Benz amefunguka kwa mara ya kwanza tangia atoke Rehab alikokuwa akipata matibabu ya kuachana na matumizi ya madawa ya kulevya na amewaasa vijana watu,iaji wa Tanzania kuacha kabisa mchezo huo.

Chid Benz ambaye anaonekana mwenye afya na uso wenye furaha, amesema madawa ya kulevya sio ya kuyazungumzia. Amesema kama mtu hataki kujutia maisha yake yote basi aachane na mchezo huo mara moja.

“Stay away from Drugs,wakae mbali sana na madawa ya kulevya kitu kibaya sana sitaki kuongelea sana lakini wajitahidi (Watanzania) kadri wanavyoweza wakae mbali na madawa ya kulevya ni kitu kibaya sana kinaweza kukufanya ujutie maisha yako yote“Alisema Chid Benz kwenye mahojiano yake na Muungwana TV.

Tazama hapa chini mahojiano yake yote.




Chid Benz alishawahi kuathirika na madawa ya kulevya na kupelekwa Rehab mara tatu kabla ya Afya yake kutengamaa.

TAMBUA Faida Kuu 4 Utakazozipata Kama Ukiacha Kulala na Simu Yako Kuanzia Leo..!!!

$
0
0

Wengi wetu naamini tumekuwa na kajitabia kakulala na karibu na simu usiku kwenye vitanda vyetu pasipo kufahamua madhara ya kijitabia hicho.

Sasa leo ninayo mambo kadhaa yakukwambia msomaji wangu wa www.dkmandai.com kuhusu hii tabia ya kulala na simu usiku.

Zifuatazo ni faida utakazozipata endapo utaacha kulala na simu usiku kitandani kwako.

1.Utalala usinginzi mzuri na wa kutosha.

Inaaminika kuwa mtu ambaye hulala karibu na simu  usiku hulala usingizi wa mang'amng'amu kwa kuwa muda mwingi huwa akihisi huenda kunasimu itaingia. Hivyo endapo kuanzia leo ukiacha kulala na simu usiku itakusaidia kulala usingizi mzuri na wa kutosha usiku.

2. Hautakuwa mtumwa wa msongo wa mawazo tena

Kwa kawaida unapolala na simu unakuwa unamawazo mengi pengine bila wewe mwenyewe kujijua huenda unawaza kwanini fulani haja kupigia usiku huo au atakupigia saa ngapi kukwambia usiku mwema hivyo unajikuta unajipatia msongo wa mawao usio na sababu na hivyo kuathiri afya yako bure. Ili kuondokana na hilo ni vyema kuweka mbali simu yako wakati wa kulala au kuweka silent kabisa.

3. Utafanya kazi / biashara zako vizuri

Kwasababu sasa unapoacha kulala na simu inamaana utapata mda mzuri na wakutosha wa kulala vizuri hivyo hata kazi zako au biashara utazifanya kwa ufanisi zaidi.

4. Utajisikia mwenye afya zaidi 

Kwa sababu utakuwa unalala vya kutosha na watu wenye kulala vizuri huwa ni wenye afya.

MAMBO Manne Ambayo Hupaswi Kuyafanya Wakati wa Kulala..!!!

$
0
0

Wataalam wa afya wamekuwa wakieleza kuwa kulala ni moja ya mambo muhimu kwa afya ya binadam.

Licha wengi kutozingatia umuhimu wa  kulala hasa yale masaa 8 ambayo hupendekezwa na wataalam kutokana na mambo mbalimbali ikiwa ni pamoja na kazi za kila siku.

Sasa leo naomba msomaji wangu nikueleze mambo kadhaa ambayo unaambiwa si mazuri kufanyika wakati unapokuwa kitandani tayari kwa kulala.

1. Hutakiwi kuangalia Tv wakati unapokuwa kitandani tayari kwa ajili ya kulala.

2. Kuchezea simu au kuchat kwenye mitandao mbalimbali wakati unapokuwa kitandani kwa ajili ya kulala.

3. Kula au kunywa wakati upo tayari kitandani nayo si tabia nzuri vinginevyo labda iwe unaumwa na hauna jinsi.

4. Kufanya mazungumzo hasa yale ya hasira wakati unapokuwa kitandani pia si vizuri

Gwajima " Nilikuwa Sijui Vizuri Mgogoro wa CUF ila Sasa Nimejua..Ninatafakari Kuliamsha Dude"

$
0
0

Nilikuwa siufahamu vizuri mgogoro wa CUF ila sasa Seif ameniambia. Natafakari alichoniambia ni 'digest' halafu nitajua nafanya nini- Gwajima
Viewing all 104776 articles
Browse latest View live




Latest Images