Quantcast
Channel: UDAKU SPECIAL
Viewing all 104423 articles
Browse latest View live

KUTANA na Mtabibu Ostadhi Khamisi Kutoka Mombasa Kenya Kwasasa Yupo Tanzania Kwa Ajili yako

0
0
Kutana na ostadhi khamisi kutoka mombasa Kenya kwa sasa yupo Tanzania ni mtabibu na mtafiti Wadawa za asili anatibia kama vile:
Miguu kuuma
Miguu kufagazi
Miguu kuwakamoto
Chango lauzazi kwakina mama
Dawa ya uzazi wakina mama inapatikana
Kusafisha nyota ili uwe namuonekano kwa kila mtu
Kumrudisha mpenzi wako na liekukimbia ndani yasiku 3 bila yapingamizi yoyote
Kumshika mume au mke asitoke nnje ya ndoa
Pata pete ya Bahati inayo endana na nyota yako
Kurudisha mali ilipotea au kudhurumiwa ndani yasiku 3
Pata utajili usiokuwa namashaliti yoyote
Dawa za nguvu za kiume
Dawa ya biashara inapatikana
Dawa ya kuzuia chuma ulete kwenye biashara inapatikana
 Zindiko la nyumba au shamba
 Anatuliza familia zinazogombana DUWA pamoja navisomo vya ufunguzi wa mwili wako njoo ufunguliwe vifungo ulivyo fungwa kutana na ostadhi khamisi utimiziwe ahadi ulizo hadiwa acha kuteseka acha kuhangaika ostadh khamisi yupupo tanzania kwajili yako...

Call +255718746825 +255754765246 kwa what'sapp +255783708487

ALICHOSEMA Askofu Gwajima Baada ya Kuzungumza na Maalim Seif Kuhusu Mgogoro wa CUF

0
0


Mchungaji wa Kanisa la Ufufuo na Uzima Dr Josephat Gwajima amefunguka na kusema Katibu Mkuu wa Chama cha Wananchi (CUF), Maalim Seif Sharif Hamad ni rafiki yake hivyo alitaka kuonana naye ili aweze kujua Professa Ibrahim Lipumba anaharibu vipi chama

Mchungaji Gwajima amesema hayo leo alipokutana na waandishi wa habari baada ya kumaliza mazungumzo na Katibu Mkuu huyo wa CUF na kusema aliamua kukutana na rafiki yake huyo ili ajue hilo baada ya hapo yeye atajua anafanyaje.

‘Mimi huyu ni rafiki yangu kwa hiyo nilitaka kujua Professa Lipumba anafanya nini kuvuruga CUF, hivyo nilitaka kujua Lipumba amepatwa na nini mpaka amevuruga chama chako na kiukweli mimi nilikuwa siufahamu vizuri huu mgogoro ila saizi Seif ameniambia kwa hiyo na mimi nataka nitafakari alichoniambia rafiki yangu ni ‘digest’ baada ya hapo nitajua nafanya nini” alisema Gwajima

Kwa upande wake Maalim Seif Sharif Hamad amesema kuwa amekaa na askofu Gwajima na kuzungumza naye kwa kina juu ya mgogoro huo na kila mmoja amemueleza mwenzake kile anachokifahamu na kusema ameamuchia askofu ili na yeye atafakari juu ya jambo hilo baada ya hapo anaamini huenda askofu akafanya jambo.

“Nimekaa na askofu na kila mmoja akamweleza mwenzake yale ambayo anayajua, kwa hiyo nimemweleza saizi kiundani kwa hiyo yeye ana ‘digest’ halafu askofu yeye ataamua juu ya kile tulichuzungumza” alisema Maalim Seif Sharif Hamad

-EATV

CHARLES Kitwanga Aeleza Serikali Inavyomtumia Bashite Kumhujumu Jimboni Kwake

0
0

Mbunge wa Misungwi kwa tiketi ya Chama cha Mapinduzi (CCM), na aliyewahi kuwa Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi katika serikali ya awamu ya tano, Charles Kitwanga ameijia juu serikali na kusema kuwa inamhujumu ili apoteze jimbo katika uchaguzi ujao kwa kuamua kutokupeleka maji jimboni kwake.

Kitwanga alisema kuwa serikali imeamua kutokupeleka maji jimboni Misungwi kwa sababu wanamuandaa mtu anayeitwa Bashite kwenda kugombea katika uchaguzi mkuu ujao mwaka 2020.

Kitwanga aliyasema hayo jana bungeni mjini Dodoma wakati akichangia hotuba ya bajeti ya Wizara ya Maji na Umwagiliaji ambapo Waziri Mhandisi Gerson Lwenge aliliomba Bunge kuidhinisha TZS bilioni 672.2 kwa ajili ya matumizi ya wizara hiyo kwa mwaka wa fedha 2017/18.

Akichangia hotuba hiyo, Kitwanga alieleza hali ngumu ya upatikanaji wa maji wanayopitia wakazi wa kijiji cha Kolomije ambapo ndipo alipozaliwa Bashite.

Kuonyesha kukerwa na serikali kupuuza kupeleka mradi wa maji jimboni humo, Kitwanga alisema kuwa atahamasisha wananchi wa Misungwi kwenda kuzima mitambo ya maji ambayo ipo katika Kijiji cha Ihelele anachodai kuwa kimesahaulika katika miradi ya maji iliyopangwa kwenye bajeti ya 2017/28.

Kitwanga alisema kuwa wakati alipokuwa waziri alikuwa anashindwa kuibana serikali lakini kwa vile sasa ni mbunge tu, basi patachimbika.

Very unfair (si haki), nazungumza kutoka moyoni mwangu, haiwezekani mradi unakwenda Tabora unatumia 600 bilioni alafu watu wangu wanakosa maji hata ya bilioni 10, alisema Kitwanga

WALIMU Mbaroni Kwa Kuvujisha Mtihani Kidato cha Sita

0
0

Jeshi la Polisi Kanda Maalum ya Dar es Salaam, linawashikilia walimu wawili na mwanafunzi wa Shule ya Sekondari Chang’ombe (Mazoezi) kwa tuhuma za kukutwa na mtihani wa Kemia wa kidato cha sita ambayo inaendelea kufanyika nchini.

Kamishna wa Kanda hiyo, Simon Sirro, aliwataja watuhumiwa hao kuwa ni Musa Elius na Innocent Murutu ambao ni walimu wa shule hiyo pamoja na mwanafunzi Ritha Mosha.

Kamishna Sirro alisema wiki iliyopota saa 1:00 usiku Jeshi la Polisi lilipokea taarifa kutoka kwa Ofisa wa Baraza la Mitihani, Aron Mweteni, aliyesema alimkuta kwenye shule hiyo mwalimu Elius na mtahiniwa wakiwa na karatasi yenye maswali na majibu ya somo la vitendo la kemia.

Alisema baasa ya kuwatilia shaka na baadaye kuwatia mbaroni, walifanya ufuatiliaji wa awli kwa baraza la Taifa la Mitihani (NECTA) ambako ilibainika kuwa mtihani huo ni miongoni mwa ile ya kidato cha sita inayofanyika mwaka huu.

“Watuhumiwa wanaendelea kuhojiwa na polisi na upelelezi ukikamilika tutawachukulia hatua za kisheria ikiwa ni pamoja na kuwafikisha mahakamani,”  alisema Kamishna Sirro.

STEVE Nyerere Majanga Tena

0
0
 

Baada ya hivi karibuni nyumba yake kuvamiwa na kunyofolewa madirisha, msanii wa vichekesho Bongo, Steven Mengere ‘Steve Nyerere’ amepata majanga tena kufuatia mwanaye kupotea katika mazingira ya kutatanisha.

Chanzo kilieleza kuwa motto huyo alitoweka nyumbani kwao, Kinondoni Mkwajuni, Dar siku tatu zilizopita na kumsababisha Steve kuwa na wasiwasi mkubwa kwamba huenda ametekwa au la kwani amejaribu kutafuta kila sehemu bila mafanikio.

“Yaani mwaka huu Steve ana majanga makubwa maana hata hajapumzika na tukio la kuibiwa, limetokea tena hili la kupotelewa na mwanaye ambaye ni mwanafunzi yaani ana haha kweli,” kilisema chanzo.

 Baada ya kupata habari hizo, Amani lilimtafuta Steve ambaye alikiri kupotelewa na mwanaye anayejulikana kwa jina la Linda Raymond (17) ambaye ni mwanafunzi wa kidato cha nne kwenye shule moja iliyopo wilayani Moshi, mkoani Kilimanjaro.

“Siku ya tukio ambayo ni Jumapili saa kumi na mbili jioni mwanangu alitoweka nyumbani kwangu Kinondoni Mkwajuni na nimejaribu kumtafuta kila kona lakini sijafanikiwa ambapo tulienda polisi na kufungua kesi kwa jalada OB/RB/697110/17.

“Nawaomba Watanzania wanisaidie jamani popote watakapomuona watoe taarifa kituo chochote cha polisi kwani ni mwanafunzi wa kidato cha nne halafu nimejaribu kwenda kuangalia kwenye mtandao wa simu mtu wa mwisho kuwasiliana naye inaonekana ni mwanaume amemtorosha, hatujui ni kwa lengo gani maana sasa hivi hofu kubwa isiwe ametekwa,” alisema Steve.
NA GLADNESS MALLYA

JACK Wolper Nimekoma Mambo ya Mapenzi

0
0


MWIGIZAJI wa sinema za Kibongo, Jacqueline Wolper amefunguka kuwa, kwa sasa amekoma kujihusisha na mambo ya mapenzi hivyo hahitaji kusikia suala hilo.


Akichonga na Showbiz Xtra, Wolper ambaye hivi karibuni aliripotiwa kumpiga chini Harmonize aliweka wazi kuwa, kwa sasa hayupo kwenye uhusiano wa kimapenzi kwa madai kuwa, wanaume wengi aliojihusisha nao hawakuwa wakweli, jambo lililomfanya ajiweke mbali na masuala hayo.


“Sihitaji kabisa kusikia suala linaloitwa mapenzi maana nimekoma, ninahitaji kufanya mambo yangu mengine kabisa hasa biashara na muvi,” alisema Wolper.
NA BONIPHACE NGUMIJE

SOMA Nafasi za Kazi Zilizotangazwa Vodacom na NMB Leo

ZITTO Kabwe Aomba Radhi Baada ya Kusema Kuwa Anajuta Kuzaliwa Tanzania..!!!

0
0

Jana usiku nilikwazika kufuatia matokeo ya uchaguzi wa wawakilishi wa Tanzania kwenye Bunge la Afrika Mashariki ( EALA ). Kufuatia hasira hiyo nikaandika kuwa wakati mwengine unajiuliza Kama unastahili kuwa kwenye nchi ambayo umo Kama raia.

Haikuwa sahihi Kabisa Kwa Kiongozi wa ngazi yangu kujutia uraia wangu kwa sababu tu ya kundi la watu wachache kuamua kuchagua wawakilishi wetu kwenye taasisi za kimataifa bila kujali uwezo, uzoefu na weledi wa wawakilishi husika.

Ninajua hatua ya Sasa ya Mtangamano wa Afrika Mashariki Ni hatua muhimu mno kwani Ni hatua ya kuelekea Umoja wa Fedha ( Monetary Union). Ndio maana Mataifa mengine yamepeleka raia wao mahiri Kabisa. Rwanda wamepeleka Waziri Mkuu mstaafu na Mawaziri 2. Burundi imepeleka Waziri wake Wa Afrika Mashariki. Uganda imepeleka Mawaziri Wastaafu. Kenya imepeleka Wabunge wazoefu na Wafanyabiashara wakubwa. Hata mwanachama mpya Sudani ya Kusini imepeleka Waziri wa zamani, Spika wa Bunge wa zamani na Jenerali wa Jeshi.

Hasira za kuipenda nchi yangu Ndio zilinipelekea kuandika nilivyoandika.

Naomba radhi kwa andiko lile na ninalifuta. Hata hivyo, Wabunge wote wa vyama vyote wajue kuwa wameionea Nchi yetu. Wameweka maslahi ya vyama vyao na mahusiano yao mbele ya maslahi ya nchi yetu. Tanzania imepeleka 'amateurs' huko EALA. Huu ndio ukweli mchungu na lazima usemwe. Itabidi kuwa na program maalumu ya kuwafundisha wawakilishi wetu hawa. Kina Adam Kimbisa lazima wachukue jukumu hili bila kujali usumbufu wake.

Anyways! My country, Right or Wrong.

Zitto Kabwe (MB).

HUYU Ndiye Mrembo Mpya wa Harmorapa? (Picha)

0
0

Kuna uvumi kuwa Harmorapa amepata mrembo mpya ambaye amewaacha wengi wameduwaa kwa muonekano wake.

Harmorapa ambaye anajulikana kupenda kiki hata hivyo hajazungumzia jambo hili kwani kwa sasa anajitahidi kusambaza wimbo wake mpya, Nundu aliyoiwachia jana.

Kulingana na picha ambazo zinasambaa mitandaoni rappa huyu wa Bongo amekuwa akionekana na mrembo huyu kitu ambacho kimewafanya wengi kumfikiria kuwa wanatoka pamoja.

Hata hivyo sio siri kuwa rapa huyu anakimbizwa na wanawake ambao wanatamani maisha yake ya sasa. Angalia picha ya mrembo huyo akiwa na Harmorapa hapa:


MWANAMUZIKI Darassa Aeleza Sababu za ‘Hasara Roho’ Kutofanya Vizuri Kama ‘Muziki’

0
0
Muimbaji Darassa hivi karibuni aliachilia wimbo wake mpya ‘Hasara Roho’ lakini inaonekana kuwa mashabiki wake hawajaupokea kama wengi waliovyotarajia.

Ingawa wimbo huu hauna tofauti kubwa na Muziki sio wengi wameonyesha kuupenda na pia haujapata mtamzamo mkubwa kupitia YouTube.


Hata hivyo akizungumza kupitia kipindi cha 255 XXL cha Clouds FM, Darassa alisema kuwa mashabiki wake wamezoea Muziki zaidi kwa kuwa alikawia kuwachilia project mpya.

“Kitu ambacho kinatokea ni wimbo wa muziki umewakaa sana na kuusikiliza sana kwa namna moja au nyingine.”
Aliendelea kusema kosa lao ni kumtegemea kuachia wimbo kama Muziki ambacho hangeweza kufanya kwani kila anapoachia nyimbo lazima iwe tofauti.

“Mimi mwenyewe nilikaa sana na huu wimbo na kuupima, nikaona kuwa ni project ambayo inafaa kufuata na ikawatosha. Kwa hiyo kwa watu kukaa na kutegemea kuwa uje wimbo kama “Muziki” hiko ndio kitu kinachorudisha sanaa yetu nyuma.”

WAZIRI Mwakyembe: Msanii Anayetaka Kuzungumzia Siasa, Akagombee Ubunge au Udiwani

0
0
Akijibu hoja ya Profesa Jay kuwa wasanii wakiimba nyimbo za siasa kuhihoji serikali wamekuwa wakinyanyaswa ila wakiimba nyimbo za kuisifia tu wanaachwa Mwakyembe amejibu kuwa wasanii hawatakiwi kuimba nyimbo za siasa na kama wanataka kuzungumzia siasa basi wagombee udiwani au ubunge.

Amesema hakuna mwanamuziki yoyote duniani aliyefanikiwa kwa kuikandia serikali, ametembelea nchi kama Nigeria na wasanii waliofanikiwa kama wakina P Square,Tiwa Savage, Davido ni wasanii wenye mafanikio lakini hawajapata mafanikio hayo kwa kuitukana serikali.

Muziki ni entaritainment industry na sio political Indusrty na hata Afrika Mashariki wasanii kama Chamilione na akina Diamond na Ali Kiba wana mafanikio lakini hawaimbi siasa.

Amemtolea mfano msanii mmoja Fella Ramson Kuti aliyeimba siasa na akaishia pabaya.


 SIKILIZA HAPA:

MANE Atwaa Tuzo ya Mchezaji Bora wa Mwaka wa Liverpool..!!!

0
0

Mshambuliaji kutoka nchini Senegal, Sadio Mane, aliibuka kidedea kwa kutangazwa mshindi mara mbili wa kinyang’anyiro cha kumsaka mchezaji bora wa mwaka wa Liverpool msimu wa 2016/17 katika hafla ilizofanyika Anfield.

Mane ambaye kwa sasa anauguza jeraha la goti, alitangazwa kuwa mshindi wa tuzo ya mchezaji bora wa mwaka wa klabu na mchezaji bora wa mwaka chaguo la mashabiki, akimshinda mshindi wa mwaka jana wa tuzo hiyo Mbrazil, Philippe Coutinho.

Mane ameshinda tuzo hizo baada ya kuwa katika kiwango bora tangu alipotua Liverpool mwezi Agosti mwaka jana akitokea Southampton kwa ada ya Pauni Milioni 32.

Mpaka sasa Mane ndiye mfungaji bora Liverpool akiwa amefunga mabao 13.

Wengine waliochomoka na tuzo ni Trent Alexander-Arnold,18, aliyeshinda tuzo ya mchezaji bora chipukizi. Ben Woodburn ametwaa tuzo ya mchezaji bora wa mwaka wa kituo cha kulea na kukuza vipaji kwa vijana cha Liverpool (Academy).

Emre Can ametwaa tuzo ya bao bora la mwaka, baada ya bao lake la tiki taka alilofunga dhidi ya Watford juma lililopita kuonekana kuwa bora zaidi kuliko mabao yote yaliyofungwa na Liverpool msimu wa 2016/17.

Lucas Leiva amepewa tuzo ya heshima baada ya kufikisha miaka kumi (10) akiwa klabuni Liverpool. Tuzo ya mchezaji bora wa mwaka kwa upande wa wanawake imeenda kwa Sophie Ingle

UKWELI Mchungu ..Msiba na Namna ya Kumsindikiza Marehemu, Utamaduni Uliozoeleka...!!!

0
0

'waache wafu wawazike wafu wenzao' maneno haya ya kwenye maandiko yanamaanisha hatutakiwi kuhangaika sana na wafu au marehemu kwa sababu wameshamaliza muda wao na hakuna kitu kinachoweza kuongeza thamani yake au kupunguza aliyokuwa nayo wala kufanya chochote juu yake kitakacho punguza makosa yake au kuongeza. Akishafariki ni kuzika mara moja.

Zipo tamaduni mbalimbali za kumsindikiza marehemu katika nyumba yake ya milele. 

Waislam huzika siku hiyo hiyo wenda itokee sababu iliyo nje ya uwezo na kusababisha kuzika kesho yake. 

Wakristo hukaa na msiba hadi siku 5 inategemeana tu na sababu nyingi kama uwepo wa ndugu n.k lakini kiufupi hukaa na msiba siku nyingi sana. 

Nimeainisha utaratibu huo katika makundi hayo lakini sidhani kama kuna haja ya kukaa na marehemu kwa muda mrefu sana najua inauma sana lakini ameshakufa ni vizuri kumpumzisha mapema. 

Napenda sana utaratibu wa kiislamu wa namna ya kudeal na msiba. Hawakai nao na huzika haraka lakini kwa namna ya kikristo hukaa na msiba muda mrefu ambapo si vizuri kwanza unaongeza gharama na kuingia gharama kubwa kulisha au kwa namna yoyote kuugharamia hadi muda wa maziko ufike, pili unaongoza uchungu na huzuni kwa waombolezaji na hii yatokana na mawazo yaliyopo juu ya uwepo wa mwili kabla ya kuzika na mwisho, muda wa kushughulika na msiba waweza kupoteza opportunity zingine za kuwaongezea kipato au kupoteza mapato kutokana na kufunga biashara muda mwingine. 

Katika makundi hayo juu, wapo wengine ambao huonesha utamaduni mzuri ambao hawaweki matanga kwa siku nyingi pia hata namna ya kuzika hawakusanyiki wengi wanakuwa wachachekwa ujumla suala la kumpumzisha marehemu huwa rahisi na la muda mfupi na wamalizapo huendelea na shughuli kama kawaida. Mifano ipo mingi lakini twaweza kuangalia desturi kwa white men (western culture). Tunaweza kuwaita wabinafsi na wachoyo kwa kulinganisha namna zetu za kushughulika na misiba lakini naamini yaweza kuwa njia nzuri na rahisi isiyokuwa na gharama kubwa wala ugumu kuikamilisha. 

Nadhani kuna haja ya kubadilisha utamaduni huu ili kuenzi maneno ya wafu kuwazika wafu wenzie. Kufanya sehemu ya msiba sio ya watu kushinda bali kutoa pole na kwenda kuzika then kila mtu kugawanyika. Kwa kufanya hivyo twaweza okoa mambo mengi. 

Waweza kuwa na maoni tofauti ila yangu ni haya. Ni jambo la huzuni na linauma lakini sio lazima likafanyika kutokana na mazoea. Sorry kwa nitakao wakwaza.

AJALI ILIYOUA WATOTO 32: Jalada la Mmiliki wa Shule Kutua kwa DPP..!!!

0
0

MMILIKI wa Shule ya Lucky Vincent iliyokumbwa na msiba wa kuondokewa na wanafunzi 32, walimu wawili na dereva wake katika ajali iliyotikisa taifa mwishoni mwa wiki, Innocent Moshi, anaendelea kushikiliwa na polisi na jalada lake litafikishwa kwa Mkurugenzi wa Mashitaka (DPP) ili kujua hatima yake.

Aidha, wakati Jeshi la Polisi likitoa taarifa hiyo kupitia Kaimu Kamanda wa Polisi Mkoa wa Arusha, Yusuf Ilembo, suala hilo lilinguruma pia bungeni mjini Dodoma jana wakati Mbunge wa Arusha Mjini, Godbless Lema, alipohoji sababu za mmiliki wa shule, Mushi, kushikiliwa huku trafiki katika vizuizi vinne walioruhusu gari lililobeba wanafunzi hao wakiachwa.

Kama hiyo haitoshi, juzi, Serikali kupitia kwa Naibu Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Hamad Yusuf Masauni, ilitangaza kufanyika kwa operesheni kabambe ya kukagua uthabiti wa magari yote yanayobeba wanafunzi nchini.

Ajali hiyo iliyoshitua taifa na kuacha simanzi kubwa ilitokea Jumamosi iliyopita wakati basi lililobeba wanafunzi wa shule hiyo ya awali na msingi lilipoacha njia na kutumbukia kwenye korongo katika eneo la Rhotia Marela, Wilaya ya Karatu, mkoani Arusha.

Watoto 32 waliokuwamo kwenye gari hilo lililokuwa likiwapeleka kufanya mtihani wa kujipima wa ujirani mwema katika Shule ya Msingi Tumaini walifariki dunia, pamoja na walimu wao wawili na dereva wao.

Makamu wa Rais, Mama Samia Suluhu aliongoza maelfu ya wananchi kuaga miili ya marehemu hao kwenye Uwanja wa Sheikh Amri Abeid jijini Arusha Jumatatu huku Jeshi la Polisi likianzisha uchunguzi mkali uliohusisha kukamatwa kwa mmiliki wa shule, Moshi.

JALADA KWA DPP
Akizungumza na Nipashe kwa njia ya simu jana kuhusiana na uchunguzi wa ajali hiyo, Kamanda Ilembo, alisema bado wanaendelea na uchunguzi wao na kwamba, kazi hiyo ikikamilika watalipeleka jalada kwa Mwanasheria Mkuu wa Serikali (AG) ili mwishowe lipitiwe na DPP na kujua kama kuna hoja za kisheria kwa mmiliki wa shule hiyo (Moshi) kufikishwa mahakamani.

SHILOLE Ashindwa Kufika Mahakamani Kutoa Ushahidi..!!!

0
0

Msanii wa muziki wa kizazi wa Bongo Fleva na filamu, nchini Zuwena Mohamed maarufu kama  Shilole ameshindwa kufika mahakamani kutoa ushahidi katika kesi ya matumizi mabaya ya mtandao kwa kuwa anaumwa.

 Jana (Jumatano) Shilole alipaswa kutoa ushahidi katika kesi hiyo inayomkabili mwanafunzi wa Chuo cha Bandari, Thomas Lucas (20) inayosikilizwa mbele ya Hakimu Boniface Lyamwike.

 Katika kesi hiyo, Lucas anakabiliwa na shtaka la mtandao kwa kumkashfu Shilole kupitia kwenye mtandao wa Instagram.

Inadaiwa  kuwa mshtakiwa huyo alifanya hivyo wakati akijiua ni kosa na kinyume na kifungu cha 16 cha sheria ya mtandao namba 14 ya 2016.

 Hata hivyo kesi hiyo imeahirishwa hadi Mei 17,2017 ambapo itaendelea kusikilizwa kwa ushahidi wa mashahidi wa upande wa mashtaka.



SHAHIDI wa Gwajima Adai Kupokwa Sanduku Wodini..!!!

0
0

MUUGUZI wa Hospitali ya TMJ, Devotha Bayona, amedai mahakamani katika kesi ya kushindwa kuhifadhi silaha inayomkabili Askofu Mkuu wa kanisa la Ufufuo na Uzima, Josephat Gwajima (47), askari polisi walichukua sanduku lililokuwa na silaha kwa nguvu kutoka kwake.

Kadhalika, Bayona amedai kuwa sanduku hilo lilikuwa wodini pembeni ya kitanda alichokuwa amelazwa Askofu Gwajima na kwamba mshtakiwa huyo alikataa kulitoa, lakini baada ya kusikia mvutano alimwagiza muuguzi kulitoa na kuwakabidhi askari hao.

Ushahidi huo ulitolewa jana mbele ya Hakimu Mkazi Mkuu, Mfawidhi, Cyprian Mkeha wakati shahidi huyo akiongozwa na Wakili wa utetezi, Peter Kibatala.
Alidai kuwa Machi 29, 2015 aliingia kazini zamu ya usiku kuanzia saa 2:00 hadi saa 2:00 asubuhi.

Alidai kuwa baada ya kuingia kazini eneo lake la kazi lilikuwa wodi ya wagonjwa mahututi (ICU), na mara alisikia mlango unagongwa. Alipofungua, aliendelea kudai, aliwakuta watu watatu, wawili walijitambulisha kwamba ni askari polisi na mwingine ni msaidizi wa Askofu Gwajima.

"Nilipofungua mlango niliona watu watatu, walipojitambulisha, nilirejea ndani kumhoji mgonjwa kuhusu ujio wa askari na msaidizi wake, alikiri kweli Yekonia Bihagaze ni msaidizi wake," alidai shahidi huyo na kueleza zaidi:

"Askari polisi waliniambia wanahitaji sanduku la mgonjwa lililokuwa kando ya kitanda chake pale wodini... nilimjulisha askofu (lakini) alikataa nisitoe sanduku lake kwa sababu lilikuwa na bastola yake ndani."

Akifafanua zaidi, shahidi alidai kuwa aliwajulisha wale askari pamoja na msaidizi wa askofu kwamba utaratibu wa kuchukua hilo sanduku wanatakiwa kuandika maelezo ya kuchukua mali hiyo kutoka kwa mgonjwa.

Hata hivyo, askari walimjibu kwamba watapeleka maelezo hayo kesho yake.

"Askofu aliniita akanieleza amesikia mvutano kuhusu hilo sanduku nichukue nimpe msaidizi wake awakabidhi askari," alisema Bayona.

"Nilifanya kama mgonjwa alivyoniagiza, niliwakabidhi askari baada ya kung'ang'ania kutaka kuingia kwa nguvu wodini kuchukua sanduku hilo."

Alidai baada ya kukabidhi hakujua kilichoendelea kwa sababu alianza kumhudumia mgonjwa ambaye alipata msongo wa mawazo (stress) kutokana na tukio lile kubwa.

Mbali na Askofu Gwajimba na Bihagaze, washtakiwa wengine katika kesi hiyo ni George Mzava na Georgey Milulu. Wote wanakabiliwa na mashtaka mawili ya kukutwa wakimiliki bastola aina ya Berretta pamoja na risasi 20 kinyume cha sheria.

Wanadaiwa kuwa Machi 29, 2015 katika Hospitali ya TMJ iliyopo Mikocheni A walikutwa wakimiliki bastola aina ya Berretta yenye namba ya siri CAT 5802 bila ya kuwa na kibali toka kwa mamlaka inayohusika na silaha na milipuko.

Iliendelea kudaiwa kuwa washtakiwa hao walifanya kosa hilo kinyume na kifungu cha 32 (1) na cha 34 (1)(2) na(3) cha sheria ya silaha na milipuko sura ya 223 iliyofanyiwa marekebisho mwaka 2010.

Pia, inadaiwa kuwa siku hiyo ya tukio washtakiwa hao pia walikutwa wakimiliki isivyo halali risasi tatu za bastola na risasi 17 za bunduki aina ya shotgun.

Akitoa ushahidi wake mahakamani hapo juzi, mshtakiwa wa nne na mchungaji wa Kanisa la Ufufuo na Uzima, Milulu alidai hakuwa anajua kama Askofu Gwajima anamiliki bastola hadi siku aliposikia ushahidi wa Jamhuri dhidi yake.

Aidha, Mzava pia juzi aliieleza mahakama kuwa hajawahi kukutwa na begi lolote katika hospitali ya TMJ kama ilivyoelezwa kwenye hati ya mashtaka na kwamba bastola na risasi anavyoshitakiwa navyo aliviona kwa mara ya kwanza mahakamani.

MAMBO ya Kumfanyia Msichana Uweze Kumteka Asikuache Hata Kama Hujamtongoza

0
0

1. KILA siku usisahau kumsifia kwa kumwambia ni kiasi gani alivyo mzuri. Kumbuka kila msichana anapenda kusifiwa hivyo unapomuambia yeye ni mzuri anaona una mthamini kuliko msichana yeyote awaye.


2. Wakati wowote ukipata nafasi muandikie barua au msg kwenye simu mueleze hisia zako kiasi gani unampenda. Kumbuka wasichana hupenda kusikia zaidi kutoka kwa wapenzi wao ni kiasi gani wanapendwa. Haitakiwi iwe tu katika kipindi cha siku ya wapendanao ndio umuoneshe kuwa unampenda. Muoneshe msichana ni kiasi gani yeye ni muhimu sana kwako.


3. Busu la ghafla na kumshika mkono wakati mkitembea pamoja itamfanya yeye kujisikia raha zaidi. Na wakati mwingine msuprise kwa kumtembelea mara kwa mara hi humfanya akuone wewe ni mtu muhimu pale usipokuwa naye karibu na kumfanya kukuhitaji zaidi ukiwa naye mbali.


4. Tambua mahitaji yake. Uwe msaada kwake kipindi ambacho mpenzi wako amekasirika kuwa pale kwa ajili yake na ukimpooza kwa sauti ya upole na mahaba. Utashangazwa sana na kiasi gani msaada huo umeleta mabadiliko kwake. Hakikisha unamsaidia katika shida zake hapa ndipo kuna tatizo kwa wavulana wengi. Mapenzi si pesa lakini kuna kipindi ambacho pesa huitajika kulinda penzi lako. Si msichana anapokuomba pesa ina maana ana nia ya kukuchuna au amekupendea pesa kuna shida nyingine inabidi akuombe wewe tena kwa kukupima kama utakuwa tayari kumsaidia.


5. Mchukue mpenzi wako out mara nyingine itamfanya ajisikie furaha sana kwa sababu wasichana hupenda enjoyment na boyfriend zao. Hii haitamfanya mpenzi wako tu kuwa na furaha bali itawafanya nyie kwa pamoja kujuana na kufahamiana zaidi.


6. Kuwa muwazi kwake usimfiche jambo linalokuhusu. Msichana hupenda kutoa ushauri kwa mtu ampendaye hivyo unapokuwa muwazi atajisikia kuthaminiwa nawe na kukuona umemuamini.


7. Ukijiona upo busy sana usithubutu kuacha japo kumpigia simu mara mbili kwa siku hata kama ukishindwa kumpigia wakati upo ofisini darasani au kwingineko hakikisha unapopata nafasi japo ujumbe mfupi wa kumwambia unampenda.


8. Mkumbatie mara kwa mara katika tukio la kumbatizi kuna jambo kubwa sana hutokea. Si kwake tu hata kwako mvulana. Hali ya joto lenu huwaweka pamoja kifikra hata pale msipokuwa pamoja.


9. Epuka maugomvi na hasira za mara kwa mara ukiwa nae. Mwanamke hupenda ustaarabu kwa mtu ambaye yupo serious naye hivyo ukionesha hasira kabla hata hujamtongoza unaweza ukamkosa msichana hivihivi wasichana huwaogopa wavulana wenye hasira na wagomvi kwa sababu hupenda kubembelezwa.


10. Mdekeze. Msichana anapenda kudeka anaenda kudeka sana na kubembelezwa sana hivyo mvulana ukidekewa usikasirike eti huyu msichana kazidi wewe ndio wakati wako wa kumuonesha msuchana wako unampenda mdekeze mpaka aone aibu kudeka siku nyingine. Wasichana wameumbwa kwa jili ya wavulana ndio maana hudeka hii ndiyo silaha pekee na ya mwisho kumpata msichana hata kamasi wako ni wa rafiki yako unaweza ukatumia silaha hii kumpora msichana huyo kwa mwenzio usipojua kudekeza utaachwa pia.

NAPE: CCM Ikiendelea Hivi Wananchi Hawatairudisha Madarakani..!!!!

0
0

Nape Nnauye amesema serikali ilipoingia madarakani iliongeza mapato, kupunguza matumizi yasiayo ya lazima na tunaambiwa uchumi unakua kwa asilimia 7.2 lakini haya hayatakua na maana kama hayatatafsiriwa kwenye kuboresha huduma za jamii hasa maji 

Amesema tunatakiwa tuone matokeo ya hatua hizi kwenye maboresho ya huduma za kijamii hasa maji la sivyo hazina maana

Amesema bajeti iliyopita imetengwa bilioni 900 na bajeti hii bilioni 600 hapo watanzania hawawezi kuilewa na ukuaji wa uchumi hauwezi kubaki kwenye makaratasi

Amesema ilani ya CCM ndio mkataba kati ya CCM na wananchi na wasiposhughulikia kama walivyoahidi basi wananchi hawatawarudisha

JIBU Alilotoa Ray C Kuhusu Kuwa na Uhusiano wa Kimapenzi na Mbunge

0
0

Kuna uvumi nyingi kuhusu Ray C, mwimbaji huyo amesemwa mara mingi kwasababu amehushishwa na kashafa kadhaa wa kadhaa.

Hivi karibu kumekuwa na ubuyu kuwa mrembo huyo alijiingiza katika uhusiano wa kimapenzi na mbunge ambaye ameoa.

Ray C hata hivyo amekana uvumi huo, amedai kuwa hajawai kujihusisha katika uhusiano wa kimapenzi na mheshimiwa yeyota licha ya kufahamiana na wabunge mbalimbali.

“Kwanza kwa sasa mambo ya mapenzi nimeyaweka kando, niko bize na muziki wangu, akili na hisia zangu zote nimezielekezea kwenye kazi. Muziki ndiyo kila kitu kwangu,” alisema Ray C.

MUONEKANO Mpya wa Idris Sultan Baada ya Kupaka Ndevu zake Rangi (Picha)

0
0
Idris Sultan amebadilisha muonekano wake wa sura, muigizaji huyo sasa amepaka ndevu zake rangi ya hudurungi.

Hapo awali Idris hakuwa na mashurubu, alikua anakaa kijana chipukizi bila kuwa na nyweli kwenye mashavu.

Kwa sasa Idris ameamua kupaka ndevu zake rangi, anadai kuwa aliamua kubadilisha muonekano wake wa sura kwasababu alitaka kufanana na Lionel Messi – mshambuliaji wa timu ya Barcelona.



Viewing all 104423 articles
Browse latest View live




Latest Images