Quantcast
Channel: UDAKU SPECIAL
Viewing all 104768 articles
Browse latest View live

Rufaa Dhidi Ya Mbunge Wa Bunda Mjini Ester Bulaya Yafika Mahakama Ya Rufaa Jijiji Dares Salaam

$
0
0

Aliyekuwa  kuwa Mbunge wa Jimbo la Bunda Mjini, Steven  Wassira  akiwa katika jengo la Mahakama ya Rufaa jijiji Dares Salaam akizungumza jambo na baadhi ya mawakili kabla ya kusikiliza kwa Rufaa ya kesi yake dhidi ya Mbunge wa Bunda mjini Ester Bulaya.  Katika kesi hiyo jopo la majaji watatu  wa Mahakama ya Rufaa limepanga kuendelea na kesi hiyo Jumatatu ijayo ya Aprili 15, mwaka huu. Uamuzi huo umetolewa  leo  Aprili 11, mwaka huu katika Mahakama hiyo  baada ya  Pande zote mbili  kutoa maelezo  ya sababu za rufaa. 


 Wakili wa Mbunge  wa Jimbo la Bunda Mjini, Tundu Lissu  akizungumza  jambo na mara baada kikao kilichokuwa kinasikiliza ombi la rufaa lilifunguliwa na  wapigakura wanne wa Jimbo la Bunda, kupinga  hukumu ya  Mahakama Kuu Kanda ya  Mwanza, kuhusu ushindi wa mbunge wa jimbo hilo, Ester Bulaya. 


Wakili  Constantine  Mutalemwa  akifafanua  jambo kwa baadhi  ya waandishi  wa habari  mara baada kikao kilichokuwa kinasikiliza ombi la rufaa lilifunguliwa na  wapigakura wanne wa Jimbo la Bunda, kupinga  hukumu ya  Mahakama Kuu Kanda ya  Mwanza, kuhusu ushindi wa mbunge wa jimbo hilo, Ester Bulaya.

TAMBUA Faida Kuu 4 Utakazozipata Kama Ukiacha Kulala na Simu Yako Kuanzia Leo..!!!

$
0
0

Wengi wetu naamini tumekuwa na kajitabia kakulala na karibu na simu usiku kwenye vitanda vyetu pasipo kufahamua madhara ya kijitabia hicho.

Sasa leo ninayo mambo kadhaa yakukwambia msomaji wangu wa www.dkmandai.com kuhusu hii tabia ya kulala na simu usiku.

Zifuatazo ni faida utakazozipata endapo utaacha kulala na simu usiku kitandani kwako.

1.Utalala usinginzi mzuri na wa kutosha.

Inaaminika kuwa mtu ambaye hulala karibu na simu  usiku hulala usingizi wa mang'amng'amu kwa kuwa muda mwingi huwa akihisi huenda kunasimu itaingia. Hivyo endapo kuanzia leo ukiacha kulala na simu usiku itakusaidia kulala usingizi mzuri na wa kutosha usiku.

2. Hautakuwa mtumwa wa msongo wa mawazo tena

Kwa kawaida unapolala na simu unakuwa unamawazo mengi pengine bila wewe mwenyewe kujijua huenda unawaza kwanini fulani haja kupigia usiku huo au atakupigia saa ngapi kukwambia usiku mwema hivyo unajikuta unajipatia msongo wa mawao usio na sababu na hivyo kuathiri afya yako bure. Ili kuondokana na hilo ni vyema kuweka mbali simu yako wakati wa kulala au kuweka silent kabisa.

3. Utafanya kazi / biashara zako vizuri

Kwasababu sasa unapoacha kulala na simu inamaana utapata mda mzuri na wakutosha wa kulala vizuri hivyo hata kazi zako au biashara utazifanya kwa ufanisi zaidi.

4. Utajisikia mwenye afya zaidi 

Kwa sababu utakuwa unalala vya kutosha na watu wenye kulala vizuri huwa ni wenye afya.

KUTANA na Mtabibu Ostadhi Khamisi Kutoka Mombasa Kenya Kwasasa Yupo Tanzania Kwa Ajili yako

$
0
0
Kutana na ostadhi khamisi kutoka mombasa Kenya kwa sasa yupo Tanzania ni mtabibu na mtafiti Wadawa za asili anatibia kama vile:
Miguu kuuma
Miguu kufagazi
Miguu kuwakamoto
Chango lauzazi kwakina mama
Dawa ya uzazi wakina mama inapatikana
Kusafisha nyota ili uwe namuonekano kwa kila mtu
Kumrudisha mpenzi wako na liekukimbia ndani yasiku 3 bila yapingamizi yoyote
Kumshika mume au mke asitoke nnje ya ndoa
Pata pete ya Bahati inayo endana na nyota yako
Kurudisha mali ilipotea au kudhurumiwa ndani yasiku 3
Pata utajili usiokuwa namashaliti yoyote
Dawa za nguvu za kiume
Dawa ya biashara inapatikana
Dawa ya kuzuia chuma ulete kwenye biashara inapatikana
 Zindiko la nyumba au shamba
 Anatuliza familia zinazogombana DUWA pamoja navisomo vya ufunguzi wa mwili wako njoo ufunguliwe vifungo ulivyo fungwa kutana na ostadhi khamisi utimiziwe ahadi ulizo hadiwa acha kuteseka acha kuhangaika ostadh khamisi yupupo tanzania kwajili yako...

Call +255718746825 +255754765246 kwa what'sapp +255783708487

KAULI ya Mwakyembe Kukataza Wasanii Siasa Yazidi Kupigwa...Afande Sele Amshukia Kwa Mfano wa Bob Marley

$
0
0
Afande Sele amesema hayo baada ya siku moja kupita tangu Dkt. Mwakyembe kutoa kauli yake mbele ya Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kuwataka wasanii wote nchini kuacha kuimba nyimbo zenye tungo za kisiasa ambazo lengo lake ni kuikosoa serikali ama viongozi wa nchi.

"Kama serikali ya Jamaika ingepiga marufuku wasanii wa nchini kwao wasiimbe nyimbo za siasa, basi siku kama ya leo tusingeshuhudia dunia ikiungana kuadhimisha kumbukumbu ya kifo cha kaka yetu mkuu Robert Nesta Marley...Baba Ziggy". Alisema Afande Sele kupitia ukurasa wake wa kijamii instagram

Aidha, Afande Sele aliendelea kusema kuwa

"Heshima na umaarufu wake havikujengwa kwa tungo za mapenzi, kujisifia na blah blah nyingine bali kwa siasa ambayo ndiyo maisha yenyewe.. Nami kwa kumuenzi huyu Nabii wangu siku kama leo natamani kuropoka kwa sauti kuu kwamba 'Ni marufuku kupiga marufuku". Alisisitizia Afande Sele

HAIJAWAHI Tokea..Mvua Sababisha Maporomoko ya Mawe Tanga..Barabara ya Dar Arusha Yafungwa

$
0
0
Jeshi la Polisi mkoani Tanga imefunga barabara ya kutokea Dar es salaam kuelekea Arusha kufuatia eneo la Mombo mkoani Tanga kuangukiwa na maporomoko ya mawe pamoja na matope na kusababisha athari kwa baadhi ya magari

Kamishna Msaidizi Mwandamizi wa Jeshi la Polisi mkoani humo Benedict Wakuyamba  amesema, maporomoko hayo yamesababishwa na mvua kubwa zinazoendelea kunyesha Mkoani humo na maeneo mbalimbali nchini

"Hali ya mvua imeendelea kunyesha na kufukia barabara eneo la Mombo kutokea Dar es salaam kuelekea Arusha ambapo matope na miti vimesombwa na kukwama barabarani hali iliyokwamisha magari makubwa kwa madogo kusafiri kupitia eneo hilo..Niwaombe abiria au wananchi kwa ujumla kama hawana ulazima wa kusafiri kwenda mikoa ya Kaskazini ni vizuri wakatulia kwa siku mbili tuone hali inakwendaje kwa ajili ya usalama wao". Alisema Kamishna Msaidizi Benedict

Kwa upande mwingine Kamishna huyo amesema TANROADS na Jeshi la Polisi mkoani humo wanaendelea kusaidia kuondoa magogo na tope zilizosakama katika barabara ili kunusuru hali ya usafiri

TUHUMA za Mateso Dhidi ya Wafanyakazi wa Ndani Oman, Mtanzania Afunguka Makubwa

$
0
0

Wafanyakazi wa majumbani walioko Oman wanatoka kila mahala duniani. Wafilipino peke yao ni wengi mara nyingi sana kuliko Watanzania na huwasikii ila wachache sana kulalamika. Lakini idadi ya walalamikaji kutoka Tanzania ndiyo iliyo kubwa kabisa ingawa jumla yao ni ndogo sana Oman.

Wapendwa waungwana na wapenda ukweli. Siku hizi za karibuni kumekuwako na upotoshwaji mkubwa wa habari za wafanyakazi wa ndani nchini Oman. Jamani waungwana, Waswahili husema kunya anye kuku akinya bata huambiwa kaharisha. Hizo habari za mayaya Oman ni za fitina na uchochezi uliokithiri na hazitamsaidia mtu yoyote, maana sisi ndio wahitaji zaidi wa hizo ajira nje ya nchi yetu.

Nchi za GCC zimekuwa na utaratibu wa miaka mingi kuajiri wafanyakazi kutoka nchi za Asia. Kwa kuzingatia msemo “mfae nduguyo kwanza” ndipo Waomani wakawa pia na utaratibu wa kuwaajiri wafanyakazi kutoka Afrika Mashariki, kwa kuwa kuna historia ya muda mrefu na ya kidugu baina yao. Sasa imekuwa balaa kila kukicha ni matusi yasiyokuwa na maana ila kutapakaza fitina na chuki kwenye mitandao ya kijamii na hata baadhi ya vyombo vya habari kama vile magazeti na televisheni.

Bora nitangulize kusema kitu kimoja ambacho mtu yeyote mwenye akili zake timamu na kupenda kusikia ukweli hawezi kukikataa, nacho ni kuwa hakuna nchi yoyote duniani ambayo haina watu wema na pia watu waovu. Mambo ni kuzidiana tu. Wala hakuna nchi yenye matajiri wenye kuajiri wafanya kazi pasitokee wenye kudhulumu na wenye kudhulumiwa. Kwa vile nazijua vizuri nchi mbili hizi — Tanzania na Oman — naweza pia kusema kwa uhakika kuwa baina ya Tanzania na Oman, utakuta kuwa dhulma wanazotendewa wafanyakazi wa majumbani Tanzania ni kubwa zaidi ukilinganisha na Oman.

Hapa Tanzania wapo wafanyakazi wanaoteseka kila siku na jamaa zao wenyewe kwa mshahara wa shilingi 20,000 au 40,000 kwa mwezi. Sio hilo tu la mshahara, bali hata siku za mapumziko za Jumamosi na Jumapili au zile sikukuu za kitaifa, hawapewi. Haya ni ya ukweli kabisa na wala sio siri. Ukitaka kumtoa mtu kijiti jichoni mwake, kwanza jiangalie kama jicho lako halina boriti.

Hapa Tanzania wafanyakazi wana kila mateso lakini wanavumilia tu. Ukifuatilia kwa makini utagundua kuwa haya ya uchochezi uliojaa fitina unatokana na kundi fulani ambalo hawapendelei pawe na masikilizano mema baina ya Waarabu na Waafrika. Na lengo lao hasa hata si Waarabu. Ukipeleleza kwa makini utagundua kuwa wanachokichukia kweli ni dini waliyoileta Waarabu, nayo ni Uislamu.

Katika siku za hivi karibuni kuna sauti zinatumwa na kusambazwa kwenye mitandao ya kijamii, hasa WhatsApp na Instagram, zikidai kuwa kuna wafanyakazi wa majumbani nchini Oman wanateswa vibaya hadi kusema kuwa wanauawa kwa makusudi na wengine wanapangiwa njama za kuuliwa ili wawe mihanga kwa majini ya Kiomani. Mojawapo ni sauti ya mama mtu mzima ambaye dhahiri kabisa inaonekana kuwa alitumwa kusudi kutukana dini ya Kiislamu.

Hilo ndilo lengo lao hasa, maana hakuwa na haja ya kutaja maneno kama vile kuwa watu wanasali sala tano kila siku halafu wanatesa watu. Hiyo haikuhusu kabisa. Ikiwa sala tano zinawaudhi basi wataumia sana. Mimi binafsi nimeishi na Mlokole wa Kanisa la Efatah, (mlokole) ni wale wanaojiita wasafi kwa jina la Yesu, huyo mama kila mwezi au wiki tatu hubadilisha mfanyakazi au wanaacha kazi kwa mateso yake. Sasa jee huyu mlokole anashinda kanisani kusali mpaka ndoa zinavunjika, hivyo tumuweke kundi gani? Mbona hawasemi “wanasali siku nzima na makelele mtaani na ni hao hao wanatesa wafanyakazi!” Jamani tuishi kwa kusema ukweli kuwa fitina za uzushi ni mbaya na haupiti muda huwarudia mwenyewe.

Kuna na mwengine ambaye anasema ni Mkenya anayedai kuwa alitaka kuuliwa na waliomuajiri Oman ili akawe kafara kwa mizimu ya Oman. Naye huyu ni mzushi mkubwa na unauona uzushi wake mara moja ukiwa si mtepetevu wa akili na unaweza kupima anayoyasema. Hebu hapa tutumie akili zetu kuchambua aliyoyasema:

Kwanza, anatuambia anakijua Kiarabu vizuri sana bila ya kututolea ushahidi. Lakini, tumkubalie kwa hili.

Pili, eti amewasikia waajiri wake wakipanga njama za kumuuwa ili kumtoa muhanga na akawasikia vizuri; hivyo kweli waajiri hao wapange njama zao mbele yake naye anawasikia!?

Tatu, eti ameingia chumbani kwake na akafungua ‘air condition’ na kupanga mito kama kuwa yeye amelala na kutoroka asije akauliwa na kutolewa muhanga! Tunajuaje kama huu ni uwongo? Jawabu: Waarabu hawakuwa na mila ya kumtoa binadamu muhanga hata katika siku hizo za ujahiliya kabla ya Uislamu, itakuwa leo!? Hii ni mila yao wenyewe baadhi ya Waafrika na anataka kuipandikiza kwa Waarabu! Tafuteni uzushi mwingine, huu hautafaa.

Nne, eti ametaka ubalozi wa Kenya kumsaidia na hawakumsaidia. Wakatae kumsaidia kwa sababu gani? Anasema haya ili tukitaka kuujua ukweli kutokana na Ubalozi tusiweze kuupata. Kwa nini? Kwa sababu anayoyasema si ya kweli kwani kesi zote zinazofikishwa balozini kokote duniani husajiliwa na hatua huchukuliwa na ubalozi. Huyu mzushi sura zake tumeshaziona, sasa na atuoneshe paspoti yake na mihuri ya kuingia na kutoka Oman na viza yake ya kufanya kazi Oman kama mkweli, tutaifuatilia kesi yake.

Tano, kwa vile waajiri wameshafikwa na mengi kutokana na waajiriwa, kuna walioibiwa dhahabu za kina mama, makarani waliofyeka pesa benki na kadhalika na kadhalika, ndio maana waajiri hao huchukua paspoti na kuziweka wao na kumpa mfanyakazi anapotaka kusafiri kihalali; mfanyakazi huwa na kadi tu. Sasa huyo mzushi, paspoti ya kusafiria aliipata wapi? Tiketi alimlipia nani?

Sita, hapana shaka, hata angelikuwanayo paspoti, hapana shaka ilichukua muda kabla ya kuweza kusafiri, hivyo siku ya pili asubuhi waajiri wake walipokuwa hawamuoni, unafikiri nini wangefanya awali? Si wangelipiga ripoti polisi kuwa mtumishi wao haonekani! Unafikiri polisi hufanya nini? Si hupeleka habari katika kila kituo cha usafiri. Na wakishapiga ripoti na popote atakapotaka kuondokea lazima wangelimzuia na wangelimuhoji na kama ana kesi ya kuwashitaki waajiri wake, basi kesi ingelifunguliwa na waajiri kushtakiwa. Sasa huyu mzushi ameondoka vipi Oman!

Nimekuandikieni haya kwa muhtasari tu. Mkifikiria vizuri mtagundua kuna hoja nyinginezo zinalifanya porojo hili kuwa la ki-paukwa pakawa. Hivyo basi, mkipanga njama zenu wazushi wa fitina tumieni akili, kama mnazo!

Mwishoni nasema kuwa wafanyakazi wa majumbani walioko Oman wanatoka kila mahala duniani. Idadi ya Wafilipino peke yake ni kubwa kwa mara nyingi sana kuliko ya Watanzania na huwasikii ila wachache sana kulalamika. Lakini idadi ya walalamikaji kutoka Tanzania ndiyo iliyo kubwa kabisa ingawa jumla yao ni ndogo sana Oman. Waomani hawana shida ya wafanyakazi. Wala hawatapungukiwa wala kuharibikiwa iwapo wafanyakazi kutoka Tanzania watazuiliwa kwenda kufanya kazi Oman. Sasa kazi kwetu. Kusuka au kunyoa.

MZIKI wa Singeli Wadaiwa Ulikuja Kubeep tu Muda si Mrefu Utakufa...Man Fongo Acharuka na Kudai Haya

$
0
0
Msanii anayefanya poa sana kwenye muziki wa singeli 'Man Fongo' amepinga vikali kauli zinazotolewa ya kwamba muziki wa kisingeli unaweza ukapotea muda wowote na kudai wenye dhamana na muziki huo wameshaubariki hivyo ni vigumu kupotea.

Man Fongo amefunguka hayo kwenye 5 Selekt ya EATV na kusema kuwa kamwe muziki wa singeli hauwezi kupotea kwani asili yake ni uswahilini na kwa kuwa waswahili wameshaushikilia itakuwa ni vigumu hivyo wapenzi wa singeli waendelee kuonyesha sapoti.

"Sisi wasanii wa singeli tunapambana kwa sasa kwa kutengeneza video kali na muziki mzuri. Kwa vile pia tupo wachache lazima tuinuie vipaji vya mitaani lazima na sisi tutadumu kama bongo fleva. Singeli haiwezi kupotea kwa sababu chimbuko lake uswahilini, kabla ya kuvuma tayari ulishakuwa na wapenzi wengi mtaani, na kwa vile wao kwa sasa ndio wameubariki na kushikilia juu basi amini hauwezi kupotea"- Manfongo alifunguka.

Pamoja na hayo manfongo amesisitiza upendo kwa wasanii wenzake na kuwasihii umoja wao ndio utakaowafanya waonekane kwenye ramani ya muziki hapa nchini.

WANAOSHANGAA Tanzania Kuomba Afrika Kusini Msaada Huenda Wakawa Hawajui Haya

$
0
0


Sasa mnashangaa nini Tanzania kuomba Afrika ya Kusini.
Hivi mmesahau jinsi tulivyowasaidia hawa tena buree.
Tuliwapa ofisi.

Tulwalipa mishahara.

Tukatoa jeshi letu kuwafundisha mapigano.

Tuliwapa silaha za kivita , magari ,vifaru.

Walikula ng'ombe wetu na kuku wetu.

Wakaoa na kuzaa na dada zetu.

Kiufupi Uhuru wao tumeutengeneza sisi Tanzania.

Tulitoa fedha za Watanzania kwa ajili ya ukombozi wa ndugu zao wa Afrika ya Kusini.

Leo isiwe nongwa , acheni watulipe fadhila kwa wema tuliowatendea.
Mahusiano na yadumu. 

Afrika ni moja na itabakia kua moja .


By Chiwinga A.

DR Mashinji Kwa Haya Hufai Kuwa Katibu Mkuu CHADEMA

$
0
0
Samahani kama nitakukosea ila ukweli lazima ni useme. Naomba nieleweke mimi siyo mfuasi wa chama chochote bali ni.mfuasi wa kiongizi bora toka chama chochote.

Nimejikita katika vipengele vifuatavyo:-

1. HOJA
Mimi binafsi nimefuatilia uongozi wako toka mwanzo, kwa sasa nimeridhika kabisa bila shaka kuwa hufai kuwa Katibu mkuu wa chama kinacho itafuta dola. CHAMA kimekosa ubunifu. CHADEMA imekosa hoja za msingi kupambana na serikali. Serikali imekuwa ikionekana njema licha ya maovu kukithiri. Hoja za msingi zimebaki kwa T. Lissu pekee huku akiatarisha maisha yake. Wekezeni katika kutafuta Scandal mbalimbali za CCM au serikali ili muwe Popular. Chama ni uwekezaji. Wafundisheni wabunge wenu jinsi ya kujenga hoja. Pia wapatieni HINTS zenye ushahidi tosha mf CAG REPORTS.

2. NIDHAMU NDANI YA CHAMA

Nidhahiri ndani ya chama kuna kutokuelewana au mpasuko mkubwa sana. Chama ni mali wa watu na si taasisi. Mf. Saed Kubenea kupitia Magazeti yake ya MAWIO/MWANAHALISI aliwahi kuandika kuwa Ben Saanane ameonekana mitaani na atafuta kiki tu wala hajatekwa, hii ni ishara mbaya sana ndani ya chama. Mimi binafsi natambua na nakiri mchango mkubwa sana wa SAED KUBENEA kuichamba CCM na kuineza CHADEMA toka miaka ya 2000 hadi kufikia kumwagiwa Tindikali. kusameana ni jambo la mhimu sana.

Kuna vijana kama MALISA GJ na timu yake wamekuwa wakiposti hoja au vitu vya hovyo hovyo Fb na mitandao mbalimbali dhidi ya Wabunge (hasa Saed Kubenea) au wanachama wenzao. Hujawahi kuwa kemea ndio maana wanaendelea. Hii ni dhahiri umeshindwa kudhibiti nidhamu ndani ya chama. Jenga chama kama taasisi na si SACCOS ya watu. Vijana wadogo kama Malisa na wengine wote wadhibitiwe mapema.

3. UCHAGUZI EALA

Uchaguzi huu ni dhahiri wewe kweli ni Daktari wa binadamu siyo wa siasa. CCM ni mabingwa wa hujuma, wanafiki, nk lakini hilo ulijidai hulijui!! (Hawa wanacheka na wewe dk1; dk inayo fuata wana kucheka-mpuuzi yule.

Binafsi kwa mtizamo wangu ungepeleka majina 3 tu.
1. EZEKIAH WENJE
2. LAWRENCE KEGO MASHA
3. JOSEPHINE L.

Namuondoa Pamela coz hafai na hana sifa kuwa Mbunge EALA. Alipaswa asubiri hadi 2020 awanie viti maalum Tz au awanie Jimboni. Uwezo wake bado ni mdogo na English hajui ikumbukwe lugha katika EALA ni English. Hapa nahisi kuna mahusiano yapo nyuma ya huyu binti. Pia kuna kampeni kubwa sana ilipigwa ndani ya chama kumpitisha. Kwa style hii vijana wazuri watazidi kujiondoa na kurudi CCM. Yaani mnawakatisha tamaa.

Nitumie nafasi hii kuishauri CHADEMA kuwa Makini sana na Dr. Mashinji. Huyu na JPM ni kanda moja, kamwe hawezi kumtupa. Itakula kwenu endeleeni kusinzia usingizi wa Nyangumi mtashituka 2020 hii hapa mnapigwa KO.

Mungu ibariki Tz.

Written by Enzymes/JF

JE, Dada Unapenda Kuwa Mrembo? Na Kaka Kuwa Mtanashati na Kurudisha Heshima ya Ndoa?

$
0
0

JE, DADA UNAPENDA KUWA MREMBO? NA KAKA UNAPENDA KUWA MTANASHATI NA KURUDISHA HESHIMA YA NDOA?

Tumia Bidhaa halisi za MARKSON kwa mafanikio ya uhakika na bila madhara.
Zimetengenezwa kwa mimea na matunda na kuthibitishwa kiafya.
🍉🌿🍓🍒🎄🍍🍀🍓🍉
Pata hizi 👇👇👇👇👇👇

1. kurefusha nywele na kuzuia kukatika ovyo @120,000/=
2. Kuongeza shepu (hips, makalio na mapaja) kwa (a)BOTCHO MULT-PLUS 10× @200,000/=
(b)Vidonge @180,000/=
3. Kuwa mweupe na softi mwili mzima kwa:- (1)Mafuta @120,000/=
(11)Vidonge @150,000/=
4. Kupunguza unene na manyama uzembe @150,000/=
5. Kuongeza uume pamoja na nguvu za kiume kwa:-
(a) Gely ya kupaka @130,000/=
(b) Vidonge kwa ajili ya kuongeza nguvu hata kwa wenye kisukari @130,000/= (c)Handsome up original @200,000/=
6. Kuondoa mvi milele zisiludi tena @120,000/=
7. Kuongeza unene wa mwili mzima na uzito pamoja na hamu ya kula @120,000/=
8. Kupunguza tumbo (kitambi) na nyama za pembeni kwa:-
(a) Dawa ya kunywa au kupaka @120,000/=
(b) Mkanda wa kawaida @100,000/=
(c) micro-computer belt unaovaibret @250,000/=
9 .Kupunguza maziwa na kuyasimamisha @120,000/=
10. Kushepu miguu na kuwa minene na kuondoa migimbi @120,000/=
11. Kuondoa mipasuko mwilini (michirizi) @100,000/=
12. kubana uke na kuongeza hamu ya tendo la ndoa kwa mwanamke @120,000/=

NB: Hakikisha unapata risiti yenye muhuri halisi wa MARKSON CO pamoja na garantii ili kukuhakikishia kufanikiwa kwako.


Wasiliana nasi :-
(+255) 0767447444 na
0714335378


Follow us on instagram @Markson_beauty_pr
@Markson_beauty_pr

MAJERUHI wa Ajali iliyouawa Wanafunzi 32 Wapelekwa Marekani

$
0
0

Mbunge wa Singida Kaskazini, Lazaro Nyalandu amesema wamekamilisha  safari ya kuwapeleka Marekani majeruhi watatu wa ajali iliyoua wanafunzi 32, walimu wawili na dereva wa Shule ya Lucky Vincent ya Arusha.

Akizungumza leo (Alhamisi) katika ofisi ya mganga mkuu wa Hospitali ya Mkoa wa Arusha ya Mount Meru, Nyalandu amesema ndege maalumu ya kuwabeba majeruhi hao  imetolewa na Shirika la Samaritan Fund la nchini Marekani ambayo itawasili kesho.

Nyalandu amesema rubani anatarajiwa kuwasili jijini Arusha leo akitokea Nairobi nchini Kenya na iwapo kila kitu kitakamilika safari itakuwa Jumamosi.

"Watakaoondoka ni abiria wanane, ambao ni majeruhi na wazazi wao, muuguzi mmoja na daktari mmoja. Hati za kusafiria ziko tayari, kinachosubiriwa ni viza," amesema Nyalandu.

IMEBAINIKA..Kumbe Robert Mugabe Huwa Halali Bali Hupumzisha Macho tuu

$
0
0
Msemaji wa Rais wa Zimbabwe Robert Mugabe amesema kiongozi huyo huwa anapumzisha macho tu na si kulala wakati wa mikutano kama wanavyoamini watu wengi.Kiongozi huyo amekuwa akionekana kusinzia katika mikutano mingi."Rais huwa anasumbuliwa na mwanga mkali," George

Charamba amenukuliwa akisema na gazeti la serikali la Herald.Rais huyo kwa sasa yupo nchini Singapore akipokea matibabu maalum kwenye macho yake.Bw Mugabe, 93, anapanga kuwania tena urais katika uchaguzi mkuu mwaka ujao.
"Huwa najihisi kama mtu ambaye amekosa kutekeleza kazi yake vyema ninaposoma (kwenye vyombo vya habari na mtandaoni) kwamba rais alikuwa anasinzia katika makongamano - la hasha," Bw Charamba amesema.Alilinganisha tatizo la Bw Mugabe na matatizo ya macho ambayo yalikuwa yanamsibu Rais wa zamani wa Afrika Kusini Nelson Mandela.

Bw Mandela alikuwa anatatizwa na mwanga mkali na wapiga picha hawakuruhusiwa kutumia mwanga wa kamera wakati wanapiga picha katika hafla zake.Matatizo ya Bw Mandela yalitokana na kufanya kazi kwa muda mrefu katika timbo na pia kufungwa jela muda mrefu Robben Island.

miliki ya pichaAFPImage captionMacho ya Robert Mugabe hutatizwa na mwanga, msemaji wake amesema. Hapa Mugabe anaonekana akiwa Bamako Januari 13, 2017.Safari za Bw Mugabe za mara kwa mara nje ya nchi zimekuwa zikishutumiwa sana na wakosoaji wake.Sekta ya afya nchini Zimbabwe imedorora na wahudumu wa afya hulalamika kwamba huwa hawalipwi vyema.

PERFUME za Diamond Platnumz Zamzindua ALI Kiba Usingizini.....

$
0
0
Msanii wa muziki Alikiba ametangaza ujio wa bidhaa mbalimbali kutoka katika brand yake ‘AK’ pamoja na ‘King Kiba’.


Muimbaji huyo wa Aje, amesema kuwa hiyo ni mipango mizito na hatarajii kuifanya kiholela kwani hata mwanzo alitoa baadhi ya bidhaa kama promotion.

“AK ni  brand ya Alikiba nashukuru imekuwa kubwa watu wanavaa lakini pia ipo na ya King Kiba nayo ni brand yangu na zipo official kabisa na kazi zitakapoanza watapata product zote,” Alikiba alikiambia kipindi cha XXL cha Clouds FM.

Aliongeza,
 “Kuna malengo makubwa sana tumeyaweka lakini siwezi kusema sasa hivi ila kuna jeans, viatu na glasses tayari zishatoka soon wataziona maana hizi zitakuwa za kwanza sababu tayari zishatoka na kuna energy drink”

Wiki mbili zilizopita muimbaji mwingine Diamond Platnumz alikuzindua perfume yake iitwayo, Chibu Perfume.        

Nafasi za Kazi Zilizotangazwa Leo

$
0
0

MREMBO Aliyeuawa na EX Wake Kwa Kuchomwa Moto Afrika Kusini

$
0
0
Karabo Mokoena, binti wa Afrika Kusini ambaye takribani wiki mbili zilizopita, habari zake zilienea mitandaoni kuwa anatafutwa kutokana na kupotea kwake tangu April 28, amekutwa amefariki dunia.



Kwa mujibu wa baba yake Karabo, Tshepo Mokoena kupitia mtandao wa Facebook ameripoti kuwa mwanaye amekutwa amekufa huku mwili wake ukiwa umechomwa moto. Habari zinasema kwamba, aliyekuwa mpenzi wa mrembo huyo ndiye anayetuhumiwa kuhusika na tukio hilo.



“The boyfriend has confesses, He killed and burned my daughter,” ameandika Tshepo kwenye mtandao huo. Hata hivyo muuaji wa tukio hilo bado anasakwa na polisi.

Mapema wiki hii rafiki wa karibu wa marehemu, Stephy Leong kupitia mtandao wa Instagram atoa taarifa za kupotea kwa rafiki yake huyo kwa kuandika, “If anyone has seen my friend Karabo from around April 28th, please let me know. She’s been missing since, it’s urgent ☹️🙏🏽.”

WEMA Sepetu Akosa Ladha yake ya Zamani...Mwenyewe Adai Siasa Amemfanya Asing'ae

$
0
0
Kwa mujibu wa Wema Sepetu, zamani alikuwa anabipu lakini baada ya kubadili upepo na kuhama Chama Cha Mapinduzi (CCM) na kuhamia Chama cha Demokrasia na Maendele (Chadema) amejikuta ‘akifi chwa’ na kushindwa kuwika hivyo kuhisiwa kuwa ufalme wake unataka kupotea kutokana na staili ya maisha ya upande huo ambayo hayataki mbwembwe nyingi.

Nyendo za Wema tangu siku ya kwanza alipotangaza mabadiliko yake ya maisha ya kisiasa na kuhamia rasmi Chadema ambapo limebaini kuwa kwa kiasi fulani baadhi ya ndugu na mashabiki wake wamekosa ladha yake ile ya zamani.

Wamekosa ile ladha yake ya kujichanganya kila kona na kusababisha matukio yaliyokuwa yakimfanya kutokaukiwa na vituko na vijimambo, jambo ambalo kwa sasa ni nadra sana kujitokeza.

Akizungumzia na Ijumaa juu ya kufi chwa kwake, Wema anasema kwamba, siku zote unapoamua kuanza maisha mengine lazima ukubali kubadilika kwa kila jambo hivyo kwa kipindi hiki ambacho ameamua kuanza maisha mapya ya siasa, ili aweze kufi kia malengo na dhamira yake, hana budi kuchagua namna nyingine ya maisha japokuwa kuna wale ambao hawatakubaliana naye wala kuridhika na maisha aliyoyachagua kwani wapo ambapo staili yake hiyo itawagharimu.

Wema anasema kuwa, anajitahidi kuendelea kumfanya mtu ampendaye asione mabadiliko ya maisha yake, lakini pia lazima kila mmoja atambue kuwa siku na umri havisubiri. Hivyo ni lazima aanze mapema kuchagua vitu vya msingi vya kujihusisha navyo.


Wema anasema:
“Kweli kuna watu wengi wanasema nimepotea japo sijajua wa
namaaninisha nimepotea wapi, maana nilichoamua kukifanya kwa sasa ni kuangalia mambo ya muhimu na hasa kwenye siasa ambayo ndiyo sehemu niliyoichagua kuwekeza asilimia kubwa ya maisha yangu.

NAPE na Kitwanga , Wawekwa Kitimoto

$
0
0
Wabunge wawili waliokuwa mawaziri katika Serikali ya Awamu ya Tano, Nape Nnauye (Mtama) na Charles Kitwanga (Misungwi) jana waligeuziwa kibao, wakidaiwa kukiuka maadili ya uongozi baada ya kuzungumza kwa hisia dhidi ya bajeti ya Wizara ya Maji na Umwagiliaji.

Nape alikuwa Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo kabla ya kuachwa katika mabadiliko madogo ya Baraza la Mawaziri, wakati uteuzi wa Kitwanga ulitenguliwa baada ya kuingia bungeni akiwa amelewa.

Wawili hao juzi walizungumza kwa hisia kuhusu kiwango kidogo cha fedha kilichowekwa wakisema hakiwezi kutatua tatizo la maji katika maeneo yao; Kitwanga akisema yuko tayari kuhamasisha wananchi wake 10,000 kwenda kufunga bomba la maji linalopita eneo lake.

Nape , ambaye pia alionekana kuwa na hisia kali, alisema sera ya Tanzania ya viwanda haitawezekana kama suala la maji halitapewa kipaumbele na kutengewa fedha za kutosha.

Jana, mbunge wa Geita Vijijini (CCM), Joseph Kasheku, maarufu kwa jina la Msukuma, alisema wakati akichangia hoja ya bajeti hiyo kuwa kauli za wawili hao zinaonyesha kuwa kuna haja ya kazi ya uhakiki kufanyika pia kwa mawaziri.

“Kazi zilizoahidiwa katika Ilani ni nyingi si moja. Hizi hela ni nyingi tuunge mkono na wala tusiwasumbue kwa kuzikataa. Tuwape nafasi ili wakafanye kazi,” alisema Msukuma.

“Lakini suala langu, nataka kuwazungumzia wana-CCM wenzangu ambao jana nilisikiliza mchango wa mmoja, Kitwanga analalamika anasema atawamobilize (atawashawishi) wananchi 10,000 wakazime mashine ya maji Iherere.

“Nataka niwaulize nyinyi mawaziri wa Magufuli hivi vile viapo mnavyokula mnajua maana yake? Kama hamvijui basi sina hakika kama mko sawasawa na kama hamko sawasawa, (Waziri wa Elimu, Joyce) Ndalichako hebu pitisha operesheni ya vyeti feki, huenda hapa penyewe kuna feki za kutosha.”

Alihoji sababu za mtu aliyekuwa waziri kusimama bungeni na kusema kuwa alivyokuwa waziri alibanwa kuzungumza.

“Kwahiyo sisi mambo (ambayo) hatuzungumzi kwa kuwasaidia nyinyi tumebanwa na nani? Mnasimama mnasema sasa nazungumza na nakwenda kuwahamsisha wananchi 10,000 wakazime mtambo?” alihoji.

“Hebu ngoja niwakumbushe tukio la mwaka 2014. Wakati Mheshimiwa Kitwanga akiwa Naibu Waziri wa Nishati na Madini, alikuja Geita . Mimi kama mwenyekiti wa CCM wa mkoa nikawaambia wananchi wasitoke mpaka walipwe na mzungu, yeye akaja akamwambia mkuu wa mkoa hata kama kuna mwenyekiti wapigwe mabomu na kweli kesho yake tulipigwa mabomu.

“Kwa hiyo nataka nimwambie Waziri wa Mambo ya Ndani siku akienda kuunganisha wananchi palepale Misungwi naye apigwe mabomu aonje joto ya jiwe. Haiwezekani waziri uliyekula kiapo, ukitimuliwa unakuja humu kutuchanganya, wakati hatujui mambo mliyokuwa mnazungumza kwenye cabinet (baraza la mawaziri).”

Baadaye alimgeukia Nape.

“Nape ambaye alikuwa mwenezi wangu wa (CCM) Taifa, jana (juzi) alizungumza mambo mazuri lakini kuna moja alisema ‘tusipowatekelezea suala la maji wananchi hawataturudisha tena madarakani’.”

Alisema hilo haliwezekani kwa sababu wananchi wanawategemea kwa mambo mengi na si maji pekee yake na wamewafanyia vizuri.

Alisema ilani hazijaanza kuandikwa katika Serikali ya Awamu ya Tano na suala si kumaliza ahadi zote.

Awali alimpongeza Rais John Magufuli na wizara hiyo kwa kazi aliyoiita kuwa nzuri, akisema ameona mabadiliko makubwa. “Mimi niko tofauti kidogo na wabunge wenzangu wanaosema tusipitishe bajeti kwa sababu hela ni ndogo. Binafsi naona hizi hela ni nyingi sana, tatizo ni zitoke zote tofauti na bajeti

VIDEO:Wabongo Walivyovaa Kizamani Kwenye Party ya Sallam

$
0
0
Meneja wa WCB Sallam amesherehekea birthday yake Dar es salaam kwa kuangusha party ambayo ili uruhusiwe kuingia lazima uwe umevaa nguo ambazo ndio zilikua zinatamba kwenye fashion ya miaka ya 90…..

Kila kitu kipo hapa chini kwenye hii video:

NAHISI Hili Jamaa Linachukua Msichana Wangu

$
0
0
Kuna huyu mwanadada ambae sasa ninafikisha miezi kadhaa tangu tuanze mahusiano, kiasi flani nimeridhika na tabia zake, tunaenda vizuri, yupo serikalini, amepanga upande wa nyumba ambayo wana share na jamaa mmoja hivi ambae pia ni work mate wake, mwenye hiyo nyumba ni bosi wao kazini, huko nyuma aliwahi kutangaza kazini kuwa ana nyumba ya kupangisha lakini ni ya ku share sababu ilikua designed for a single United family, ndipo akajitokeza msichana wangu na huyo jamaa kuihitaji hiyo nyumba, wamegawana vyumba ila sebule na jiko wana share.

Tatizo lenyewe ni hili;

Kitendo cha watu wa jinsia mbili tofauti kuishi mazingira kama hayo kimeni irritate mimi hivyo kusababisha magomvi ya kila mara kati yangu na msichana wangu, kwa sababu, wakati mwingine nikifika pale nawakuta wamekaa sebuleni wakitazama filamu huku lile jitu likiwa na boxer tu huku msichana wangu akiwa na night dress ingawa anakua kajifunga na kanga pia, halafu wakati wote msichana wangu ndie mpishi kwenye hiyo nyumba, hilo pumbavu limekaa kwenye sofa kusubiri chakula kama mme vile, huwa nikikuta hali hiyo naingiwa na hasira kali mno na tukiingia chumbani namuanzishia vagi msichana wangu.

Msichana huyu nilikua nimepanga kumuoa maana mimi pia umri wangu umesogea kidogo na wazee wamekua wakinisukuma sana kuhusu kuoa, ila mimi nilipanga nioe nikishajenga nyumba yangu jambo ambalo nilishalikamilisha mwaka Jana, nimekua nikimsihi huyu binti aondoke kwenye hiyo nyumba aje tuishi wote lakini hataki anasema hadi ndoa, jambo ambalo linanikasirisha maana mtu yupo tayari kuishi nyumba moja na hilo jitu lakini hataki kuishi na mimi Mchumba wake, hiyo ni haki kweli wadau?

Sasa inanilazimu mimi kwenda pale hata usiku wa manane kwenda kuchungulia tu hata madirishani bila wao kujua ili kuona kama usiku huwa wanajuana, wakati mwingine nalazimika kwenda kulala pale bila kupenda katika mazingira ya hofu,
lakini yote hayo ni tisa, kumi, lile jitu huwa halinipendi, nikifika pale linaondoka, likiniona mimi nimefika pale, hata kama lilikua limevaa nguo litaenda kuvua linakua linapitapita hapo na boxer tu huku nyeti zake zikionekana wazi ku swing kwenye boxer, haliongei na mimi wala story tu za udugu kama watanzania tulivyozoeana,
i mara zote nikianzisha mada hii msichana wangu hunitoa wasi wasi kuwa hamna chochote kinachoendelea kati yao, na kwamba ni wasi wasi wangu tu, na kwamba anamheshimu tu kama kaka yake na ndio maana humpikia na kumfulia wakati mwingine, mimi siamini.

Ngoja niishie hapa, kwa kweli nina hasira sana, hivi kwa jinsi nilivyowaeleza mnadhani kuna chochote kinaendelea kati ya msichana wangu na hili jitu behind my back?

Tusaidiane wadau

HANS Poppe: Yanga Musishangilie Ngoma Bado ipo Uwanjani

$
0
0
Hans Poppe amewaambia Yanga wasijiamini na kuona kuwa tayari wameshauchukua ubingwa wa Ligi Kuu Bara msimu huu, kwa sababu tu bado wana mechi nyingi mkononi, tofauti na Simba.

Yanga ipo kileleni ikiwa na pointi 62, sawa na Simba lakini ikiwa na uwiano mzuri wa mabao ya kufunga na kufungwa, huku ikiwa na mchezo mmoja mkononi.

Hans Poppe amesema kuwa mchezo wa soka haupo hivyo kama wanavyofikiria kwani lolote linaweza kutokea mbele yao.
Alisema kutokana na hali hiyo, wamejipanga vilivyo kuhakikisha Simba inashinda mechi zake zote zilizobakia ili iweze kujitengenezea mazingira mazuri ya kunyakua kombe hilo.
 “Waache tu waendelee kushangilia lakini maajabu yanaweza kutokea na kuwaacha midomo wazi, kwa sababu mchezo wa soka una maajabu yake.

“Kwa upande wetu sisi tutaendelea kupambana kwa uwezo wetu wote ili kuhakikisha tunashinda michezo yote iliyobakia kwani kwa jinsi ligi ilivyo na ushindani mkubwa, Yanga bado hana uhakika wa kunyakua ubingwa huo licha ya kuwa na mechi nyingi ambazo hawajacheza tofauti na sisi.

“Mpaka aweze kupata uhakika huo, atatakiwa kushinda mechi zote zilizobakia jambo ambalo bado ni mtihani mkubwa kwake, hivyo mpaka sasa bado hawana uhakika wa kuwa mabingwa na hapaswi kuanza kushangilia kwa sasa,” alisema Poppe.


Mpaka sasa Yanga imecheza mechi 27 na imebakiza tatu ili kuhitimisha kivumbi cha ligi kuu msimu huu wakati Simba yenyewe mpaka sasa imecheza 28 na imebakiza mechi mbili
Viewing all 104768 articles
Browse latest View live




Latest Images