Quantcast
Channel: UDAKU SPECIAL
Viewing all 104789 articles
Browse latest View live

MAMBO 10 Yanayomweka JPM Mtegoni Kueleke Uchaguzi Mkuu 2020...Wasomi Wadai Vilio vya Wananchi Vimeongezeka..!!!!

$
0
0

SERIKALI ya Awamu ya Tano imefanya vizuri tangu ilipoingia madarakani, ikifanikiwa pamoja na mambo mengine kurejesha nidhamu ya kazi na kuwajibisha viongozi na watumishi wa umma.

Aidha, imeanza utekelezaji wa miradi mikubwa ya kiuchumi ikiwamo ujenzi wa reli ya kati kwa kiwango cha kisasa, ununuzi wa ndege, kuzuia matumizi yasiyo ya lazima na kufuta maadhimisho ya sherehe mbalilimbali ni baadhi ya mambo yaliyofurahiwa na wengi.

Hata hivyo, wakati Serikali hiyo inayoongozwa na Rais John Magufuli ikikaribia kumaliza mwaka wa pili, baadhi ya wasomi na wanasiasa wametaja mambo 10 yanayotakiwa kufanyiwa kazi kutokana na utekelezaji wake kuathiri kundi kubwa la Watanzania wakisema yanaweza kumweka mtegoni.

Wamesema licha ya kuwa baadhi ya mambo hayo yamefanyika kwa nia njema, utekelezaji wake ulikuwa na kasoro, huku wakikosoa baadhi ya kauli, hatua sambamba na kufanyika mambo waliyosema hayana ulazima kwa sasa.

“Matukio hayo yana maana kubwa sana kwani wananchi wamejawa na hasira hakika wanahifadhi hasira zao kuelekea mwaka 2020,”alisema Zitto Kabwe, Kiongozi wa Chama cha ACT-Wazalendo na Mbunge wa Kigoma Mjini.

Mambo kumi yanayomweka JPM mtegoni

Mikutano ya hadhara

Marufuku ya mikutano ya siasa mpaka wakati wa kampeni za uchaguzi wa mwaka 2020 kama ilivyotangazwa na Rais Magufuli ni moja kati ya uamuzi ulioathiri wanasiasa na vyama, hasa vya upinzani.

Sababu iliyotolewa na Rais Magufuli ni kuwa huu ni muda wa kufanya kazi na siyo siasa. Katika kufafanua kauli yake, Rais alisema wabunge na madiwani tu ndiyo wanaoruhusiwa kufanya mikutano katika maeneo yao na hawaruhusiwi kuleta wageni kutoka nje.

2. Bomoabomoa

Mwanzoni mwa utawala wake liliibuka zoezi la kuondoa watu waliojenga katika maeneo yasiyoruhusiwa.

Bomoabomoa hiyo iliendeshwa na Baraza la Taifa la Usimamizi wa Mazingira (NEMC) katika maeneo mbalimbali ya Jiji la Dar es Salaam na kuathiriwi watu wengi masikini ambao ndiyo waliomchagua pia Rais huyo wa Awamu ya Tano.

Zoezi hilo lililenga nyumba zilizojengwa mabondeni, kwenye fukwe za bahari ya Hindi, kingo za mito na maeneo ya wazi na hivi karibuni wamebomolewa waliojenga pembezoni mwa reli ya kati.

3. Matangazo ya Bunge ‘live’

Kusitishwa kwa urushwaji wa matangazo ya Bunge moja kwa moja nao umewagusa baadhi ya wananchi ambao tangu kutolewa katazo hilo wamekuwa wakilipinga licha ya kuwa baadhi ya televisheni hurekodi na kurusha usiku.

Machi mwaka huu chombo kimoja cha habari kiliandika kuwa Rais Magufuli katika kikao chake cha ndani na wabunge wa CCM mjini Dodoma, aliwaeleza kuwa yeye ndiye aliyeamua kusitisha mikutano ya Bunge kuoneshwa moja kwa moja katika televisheni.

4. Wabunge wa CCM kutowatembelea wa upinzani

Katika kikao hicho pia iliripotiwa jinsi Rais Magufuli alivyoshangazwa na hatua ya baadhi ya wabunge wa CCM waliounda kamati ya kutaka kwenda kumtembea mbunge wa Arusha Mjini (Chadema), Godbless Lema alipokuwa gerezani jambo alilolifananisha na usaliti kwa chama chake.

Lema alikaa gerezani kwa muda wa miezi minne kwa kukosa dhamana kutokana na mashtaka yaliyokuwa yakimkabili. Kauli hiyo ambayo haijakanushwa popote ilizuia taharuki huku wasomi waliotoa maoni katika gazeti hili wakitofautiana mtazamo wao.

5. Utumbuaji majipu

Baada ya kuapishwa Novemba 5, mwaka 2015 Rais Magufuli alianza utekelezaji wa majukumu yake kwa mfumo wa kuwajibisha watendaji wazembe, wala rushwa na wanaolisababishia Taifa hasara kwa njia mbalimbali. Mfumo huo wa utendaji kazi umejipatia umaarufu kuwa ‘utumbuaji majipu’.

Licha ya utumbuaji huo kuungwa mkono, wapo walioukosoa wakitaka watakaotumbuliwa wawe watu waliobainika kuwa na makosa na kasoro mbalimbali, ukiwakumbe hadi watumishi wasiohusika.

Tangu kuanza kwa utumbuaji, zaidi ya watumishi 1,000 wameshatumbuliwa jambo linalowafanya katika maisha yao kutosahau utawala wa Serikali ya Awamu ya Tano.

6. Kufuta safari za nje

Uamuzi wa Rais kubana matumizi, ikiwa ni pamoja na kudhibiti ziara za nje zisizo na tija, safari za mafunzo nje ya nchi, warsha, semina, makongamano na matamasha ulisifiwa na kada mbalimbali nchini lakini kwa kiasi fulani uliacha simanzi kwa watumishi, hasa waliokuwa wakitumia maeneo hayo kujipatia fedha za bure.

7. Pesa kutoweka, kupunguzwa kazi

Wapo wanaofurahia hatua za Serikali kuthibiti na kubana matumizi, lakini uamuzi huo umeathiri sekta nyingi kutokana na fedha kutoweka.

Si hoteli, baa, mashirika ya usafiri, kampuni za huduma za chakula, vyombo vya habari wala viwanda zilizoepuka athari za uamuzi huo wa Serikali.

Katika kipindi cha utawala wa awamu ya tano, ulioshuhudia fedha kutoweka baadhi ya mashirika na taasisi hasa binafsi zililazimika kupunguza wafanyakazi wake, huku baadhi ya wafanyabiashara wakifunga biashara kutokana na mzunguko wa fedha kuwa hafifu wakilazimika kufanya hivyo ili kwenda sambamba na uzalishaji na kupata faida.

8. Vyeti feki

Uhakiki wa vyeti unaofanywa na Serikali kwa kiasi kikubwa umeacha alama nyingine kwa Watanzania. Baada ya kupokea majina 9,932 kutoka kwa Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais (Utumishi na Umma na Utawala Bora), Rais Magufuli aliagiza wote waliotajwa kughushi vyeti waondoke vituo vya kazi kabla ya Mei 15 na watakaokaidi watafikishwa mahakamani.

Pengine sio ajabu kutajwa kwenye orodha hiyo kwa kuwa ukaguzi haukuacha mtu au cheo, lakini kugundulika kwake kunaibua maswali zaidi katika uhakiki huo ambao tayari uemshaonyesha dosari kama kutaja majina ya baadhi kuwa wana vyeti vya kughushi vya elimu ya sekondari wakati hawakuviwasilisha kwenye uhakiki uliofanyika.

9. Tetemeko la ardhi Kagera

Septemba 11 mwaka jana mikoa ya kanda ya ziwa ilikumbwa na tetemeko la ardhi ambako watu takribani 17 walipoteza maisha, huku zaidi ya nyumba 840 zikibomona na nyingine 1,264 kuharibika.
Wakati akipokea taarifa ya maafa hayo, Rais Magufuli alisema Serikali itarekebisha miundombinu iliyoharibiwa na tetemeko na kuwataka waliobomolewa nyumba, wajipange kuzirekebisha.

Serikali ilizuia watu au taasisi kutoa misaada kwa waathirika, badala yake ikaagiza wapiti Ofisi ya Mkuu wa Mkoa  huku kipaumbele kikiwa ni kukarabati miundombinu jambo ambalo lilipingwa na kulalamikiwa na watu waliotaka fedha hizo ziende moja kwa moja kwa waathirika.

10. Kudhibiti mihimili

Licha ya Seriklai kuwa na wajibu wa kutafuta fedha, kitendo cha Mahakama na Bunge kuwa mihimili inayojitegemea lakini kujikuta ikipangiwa mambo kadha wa kadha na Serikali kumezungumziwa na wachambuzi wa masuala mbalimbali nchini kuwa si utaratibu mzuri.

Mfano ni uamuzi wa Rais kuagiza fedha za sherehe ya kuwapongeza wabunge kutumika kununulia vitanda Hospitali ya Taifa Muhimbili (MNH).

Maoni ya wasomi, wanasiasa

Makamu Mwenyekiti wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), Profesa Abdallah Safari alisema suala la kuzuia mikutano ya hadhara na kutokuonesha Bunge ni moja ya mambo ambayo yanaweza kumnyima Rais Magufuli nafasi ya kutetea kiti chake.

“Rais anasema hakuna siasa na wananchi wafanye kazi lakini anashindwa kuelewa kwamba kuwaminya huko na kuwatengenezea watu hofu ya kushindwa kuzungumza kunawafanya wazidi kuwa majasiri na siku wakipata nafasi ya kufanya maamuzi katika chumba cha kura basi hawatomchagua,”alisema.

“Uhusiano wake na wananchi umedorora kwa kuwa anawafanya wawe kimya na hofu lakini akae akijua kuwa 2020 watu wataikimbia minyororo kwa kuwa anasema analeta maendeleo lakini utekelezaji hakuna na watu wakijaribu kumkosoa wanatishwa na kukamatwa.”

Mhadhiri wa Sayansi ya Siasa Chuo Kikuu Dar es Salaam (UDSM), Richard Mbunda alisema inawezekana Rais akabadilika baadayee kwa kuwa kisiasa bado miaka ni mingi kuelekea Uchaguzi Mkuu.

Mbunda alisema mbali na mambo hayo, suala la ukata kwa wananchi walio wengi ndio limegeuka ajenda huku akitolea mfano jinsi anavyozungumzia hovyo katika mitandao ya kijamii.

“Nadhani demokrasia inawapa nguvu  wananchi kuliko viongozi kwa kuwa wao ndio wanaochagua lakini hapa kwetu viongozi walio wengi huwa wanyenyekevu pindi wanapoomba kura lakini wakishapata madaraka huwasahau wapiga kura wao,”alisema.

“Kuna mambo mengi yanaweza kukwamisha safari yake 2020 mfano suala la kuonekana kutojali wananchi wake ukirejea kauli yake wakati wananchi wakilalamika njaa, chakula hakuna yeye akawaambia Serikali haitoi chakula hiyo maana yake Serikali haijali.”

Mhadhiri mwingine wa chuo hicho, Dk Onesmo Kyauke alikuwa na mtazamo tofauti kuwa mambo hayo hayawezi kuwa sababu ya Rais Magufuli kurudi madarakani lakini akaonya kuwa anapaswa kubadilika ili kurudisha imani ya wananchi waliyokuwa wamejenga kwake.

“Mfano suala la Bunge Live ni haki ya Wananchi karibu nchi zote duniani wanonesha Bunge, ni jambo la hatari kuwanyima watu haki zao za msingi, hata kama Sheria haisemi lioneshwe lakini Sheria hiyo hiyo haikatazi Bunge Live,”Alisema Dk Kyauke.

Mbunge wa zamani wa Kigoma Kusini, David Kafulila alitaja uamuzi wa kufuta mikutako ya hadhara, kubainisha kuwa jambo hilo litampa wakati mgumu Rais Magufuli kwenye uchaguzi mkuu wa 2020.

“Pia kuzuia mikutano ya Bunge ni dosari kubwa kwake, katika utawala wake kuna ukiukwaji wa haki za binadamu, kukandamiza demokrasia na kutunga sheria kandamizi,”alisema Kafulila na kubainisha suala la vyeti feki ni sahihi kufanyika.

MWANDISHI wa Habari wa Mwl Nyerere Afariki Dunia ..!!!

$
0
0

Aliyekuwa Mwandishi wa habari wa Baba wa Taifa,  Mwalimu Julius Nyerere,  Paul Sozigwa amefariki saa 8:30 usiku wa kuamkia jana.

Msemaji wa Taasisi ya Moyo ya Jakaya Kikwete (JKCI) Anna Nkinda amesema kuwa Sozigwa alikuwa anaendelea vizuri lakini akafariki wakati akiendelea na matibabu hayo.

Amesema alikuwa akiendelea na matibabu wodi  namba mbili baada ya kutolewa kwenye wodi ya uangalizi maalumu.

"Ni kweli amefariki usiku wa kuamkia jana wodi namba mbili hapa JKCI." amesema Nkinda.

SIMBACHAWENE: Msiwe na Wasiwasi na Ahadi za Magufuli..!!!

$
0
0

WAZIRI wa Nchi, Ofisi ya Rais, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa(Tamisemi), George Simbachawene amewahakikishia wabunge kuwa ahadi zote alizoziahidi Rais John Magufuli wakati wa kampeni za Uchaguzi Mkuu wa mwaka 2015 zitatekelezwa.

Simbachawene alitoa kauli hiyo jana bungeni alipokuwa akijibu swali la nyongeza la Mbunge wa Hai(Chadema), Freemon Mbowe.

Mbowe alitaka kujua ni lini serikali itatoa Sh. bilioni 1.3 kwa ajili ya ujenzi wa kilomita tano za lami ambazo Rais aliahidi wakati wa kampeni.

Akijibu swali hilo, Simbachawene alisema ahadi zote alizotoa Rais wakati wa kampeni zitatekelezwa ndani ya miaka mitano kama alivyoahidi.

Katika swali la msingi, Mbunge wa Viti Maalum (Chadema), Salome Makamba, alitaka kujua ni lini serikali itatekeleza ahadi ya Rais aliyoitoa wakati wa kampeni kwa wananchi wa Jimbo la Kahama Mjini ya kujenga kwa kiwango cha lami kilomita 10 za barabara za mitaa ya mji huo.

Akijibu swali hilo, Naibu Waziri Seleman Jafo alisema hatua ya kwanza ya utekelezaji wa ahadi ya Rais ilikuwa ni kuzitambua barabara zitakazojengwa kwa kiwango cha lami katika Halmashauri ya mji huo ambayo imekamilika.

“Ujenzi huo utahusisha barabara ya Mama Farida yenye urefu wa kilomita 1.305, barabara ya Phantom-Majengo yenye urefu wa kilomita 1.852, barabara ya Nyihogo-Namanga yenye urefu wa kilomita 0.6,”alisema.

Alitaja barabara zingine kuwa ni barabara ya Florida-Stendi ndogo yenye urefu wa kilomita 0.829 na barabara ya Royal ya zamani-Stendi ndogo yenye urefu wa kilomita 0.2.

Alibainisha kuwa ujenzi wa barabara hizo utafanyika kwa awamu ambapo katika mwaka wa fedha 2017/18 na Sh. milioni 603.6 imetengwa kwa ajili ya kujenga barabara yenye urefu wa kilomita moja ya lami.

Aidha, alisema kupitia fedha za mfuko wa barabara zimetengwa Sh. milioni 320 kwa ajili ya kukarabati wa barabara za lami zenye urefu wa mita 800 katika mji wa Kahama.

MAKADA CCM Wamkimbia Lowassa...Habari Vichwa vya Magazeti ya Leo Jumamosi 13/5/2017..!!!!

FUNDI Afa kwa Kuanguka Toka Ghorofa ya 16..!!!

$
0
0

FUNDI ujenzi wa ghorofa la MNF Square lililoko katikati ya jiji la Dar es Salaam, amefariki dunia papo hapo baada ya kuteleza kutoka ghorofa ya 16.

Watu walioshudia tukio hilo wamesema kuwa fundi huyo alianguka jana saa 10:00 alasiri katika ghorofa hilo wakati wakiendelea na kazi ya ujenzi.

Kamanda wa Polisi Mkoa wa Ilala, Salumu Hamduni, alithibitisha kutokea kwa tukio hilo.

NILISIKIA Gwajima Amefariki, Mchungaji Aieleza Mahakama..!!!

$
0
0

MCHUNGAJI wa Kanisa la Ufufuo na Uzima, George Milulu, ameieleza mahakama kuwa alisikia uvumi kwamba Askofu Mkuu wa kanisa hilo, Josephat Gwajima (47) amefariki dunia katika Hospitali ya TMJ jijini Dar es Salaam.

Milulu aliyaeleza hayo juzi mbele ya Hakimu Mkazi Mfawidhi, Cyprian Mkeha wakati akiongozwa na wakili wake, Peter Kibatala kutoa utetezi wake katika kesi ya kushindwa kuhifadhi silaha na risasi inayomkabili Askofu Gwajima.

Alidai kuwa Machi 29, 2015 alikuwa hospitali ya TMJ, ambapo alikwenda baada ya kupata taarifa ya uvumi kwamba Askofu Gwajima amekufa.

Alieleza kuwa alipofika hospitalini alikuta watu ni wengi, lakini muda mfupi baadaye waliamuliwa na polisi wakae eneo moja ikiwamo waliokuwa waumini waliokuwa juu ya ghorofa ambapo waliamriwa washuke chini.

Mchungaji huyo alidai licha ya kutoambiwa sababu ya kutakiwa wakusanyike eneno moja, ilitolewa amri nyingine ya kuwqataka waingie ndani ya gari la polisi aina ya Land cruiser na kupelekwa kituo cha polisi Oysterbay.

Alieleza kuwa walipofika kituoni hapo waliamriwa wavue mikanda, viatu na kuingizwa rumande ambapo wakaanza kutolewa mmoja mmoja na kuhojiwa. Hata hivyo, alikataa kuliona begi ambalo lilikuwa na vitu mbalimbali vya Gwajima ikiwamo bastola.

Naye, shahidi George Mzava alieleza kuwa hajawahi kukutwa na begi lolote katika hospitali ya TMJ kama ilivyoelezwa kwenye hati ya mashtaka. Alidai baada ya kukamatwa na polisi walifikishwa Kituo cha Polisi cha Oysterbay ambapo waliamriwa wavue mikanda na kuanza kuhojiwa mmoja mmoja.

Alipoulizwa na Kibatala kwamba anazijua sababu za kuingizwa mahabusu, alieleza kuwa hawakuambia sababu na walikuwa wakiandika maelezo kwa shinikizo.

Katika kesi hiyo, mbali ya Askofu Gwajima washtakiwa wengine ni George Mzava, Msaidizi wake, Yekonia Bihagaze (39) na Georgey Milulu wao wanakabiliwa na mashtaka mawili ya kukutwa wakimiliki Bastola aina ya Berretta pamoja na risasi 20 kinyume cha sheria.

Wanadaiwa kuwa Machi 29, 2015 katika Hospitali ya TMJ iliyopo Mikocheni A walikutwa wakimiliki bastola aina ya berretta yenye namba ya siri CAT 5802 bila ya kuwa na kibali toka kwa mamlaka inayohusika na silaha na milipuko.

MVUA Yasababisha Maafa Makubwa Mwanza na Bukoba..Yabomoa Barabara Kuu..!!!

$
0
0

Mvua imesababisha barabara kuu ya Mwanza -Bukoba kukatika eneo la Kemondo, hivyo magari ya abiria na mizigo kuzunguka Kyetema kupitia Katerero kutokea Muleba.

Barabara hiyo imekatika jana (Ijumaa) saa 11:00 alfajiri kutokana na mvua iliyonyesha usiku kucha na kusababisha maji kujaa kwenye karavati.

Kutokana na hali hiyo wananchi na hasa wafanyabiashara wa eneo la Kemondo wameshindwa kuendelea na shughuli zao kwa kukosa mawasiliano.

Naima Issa, mkazi wa Kemondo amesema wanafunzi wamekatisha masomo baada ya kukosa eneo la kupita.

Meneja wa Wakala wa Barabara (Tanroads) Mkoa wa Kagera, Andrew Kasamwa amesema watumiaji wa barabara hiyo wanatumia njia mbadala kwa kupita Katerero mzunguko wa umbali wa takriban kilomita 10.

Amesema jitihada zinafanywa kukarabati eneo hilo ili kurejesha mawasiliano.

MADEE Amtibua Mke wa Roma Mkatoliki..!!!

$
0
0

Mke wa msanii Roma Mkatoliki Nancy Mshana ameonesha kukerwa kwa kitendo cha msanii Madee kutoa kauli iliyojaa udhalilishaji kwa kusema Roma apone na aache kujilegeza.

Hayo yameibuka baada ya Nancy ku-post picha ya pamoja yeye na Roma katika mtandao wa kijamii wa instagram na kuandika maneno yenye kumtia faraja mume wake kwa kusema 'Be a friend encourage someone take time to care. Let your words heal and not wound'

"Apone basi na yeye asijilegeze kha! wanaume wa tanga bana" Ali-comment Madee

Akajibu Nancy...."Nimewaona marafiki na baadhi ya wasanii wakija kumuona, nilitegemea wewe ungekuwa wa kwanza kuja kumuona rafiki yako, ndugu yako, mtani wako lakini huu ni mwezi umekatika sijaona hata ukimpigia simu ! wala kuja kumjulia hali, hakika nimejifunza mengi sana kipindi hiki, ubarikiwe sana shemeji yangu Hamad, msalimie mtoto wetu Saida".

KASEJA Akimbilia Utangazaji wa Radio..!!!!

$
0
0

Mlinda mlango mkongwe hapa nchini ambaye sasa anachezea Kagera Sugar Juma Kaseja amepanga kuwa mtangazaji wa radio au televisheni baada ya kustaafu kucheza soka.

Juma Kaseja amesema hayo alipokuwa akihojiwa na kusema atakapostaafu kucheza soka ataingia rasmi katika kiwanda cha utangazaji, ambapo awali ataanza kwa kutumia kipaji chake lakini kadri siku zinavyozidi kwenda itabidi aingie shule ili kuwa mtangaji mzuri zaidi na bora.

"Kila kitu kinahitaji elimu, ila mimi kwanza nitaanza hivi hivi nilivyo halafu kadri nitakavyozidi kwenda nitakuwa najiendeleza na shule ili niwe mtangazaji mzuri" alisema Juma Kaseja 

Mbali na hilo Juma Kaseja amesisitiza wachezaji wadogo wanaokuja kwenye soka wanapaswa kuwa wavumilivu, wasikivu kwa walimu wao na kuwa na nidhamu kama wanapokuwa kwa wazazi wao.

KUTANA na Mtabibu Ostadhi Khamisi Kutoka Mombasa Kenya Kwasasa Yupo Tanzania Kwa Ajili yako

$
0
0
Kutana na ostadhi khamisi kutoka mombasa Kenya kwa sasa yupo Tanzania ni mtabibu na mtafiti Wadawa za asili anatibia kama vile:
Miguu kuuma
Miguu kufagazi
Miguu kuwakamoto
Chango lauzazi kwakina mama
Dawa ya uzazi wakina mama inapatikana
Kusafisha nyota ili uwe namuonekano kwa kila mtu
Kumrudisha mpenzi wako na liekukimbia ndani yasiku 3 bila yapingamizi yoyote
Kumshika mume au mke asitoke nnje ya ndoa
Pata pete ya Bahati inayo endana na nyota yako
Kurudisha mali ilipotea au kudhurumiwa ndani yasiku 3
Pata utajili usiokuwa namashaliti yoyote
Dawa za nguvu za kiume
Dawa ya biashara inapatikana
Dawa ya kuzuia chuma ulete kwenye biashara inapatikana
 Zindiko la nyumba au shamba
 Anatuliza familia zinazogombana DUWA pamoja navisomo vya ufunguzi wa mwili wako njoo ufunguliwe vifungo ulivyo fungwa kutana na ostadhi khamisi utimiziwe ahadi ulizo hadiwa acha kuteseka acha kuhangaika ostadh khamisi yupupo tanzania kwajili yako...

Call +255718746825 +255754765246 kwa what'sapp +255783708487

EXCLUSIVE: Nape Nnauye Kawajibu Wanaohoji Kwa Nini Anaikosoa Serikali

$
0
0
Mbunge wa Mtama ambaye pia alishawahi kuwa Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo Nape Nnauye alikubali kukaa kwenye exclusive interview na Ayo TV na millardayo.com kuzijibu na kuzitolea ufafanuzi tuhuma za kuikosoa serikali baada ya kuondolewa kwenye nafasi ya Uwaziri.

Hapa nimekuwekea FULL INTERVIEW waweza itazama…

EXCLUSIVE VIDEO: Aliyesali Kwa Sauti ili Gari lisisombwe na Maji Afunguka

$
0
0
Inawezekana Jumapili ya May 8 2017 ulikutana na video kwenye mitandao ya kijamii ikionyesha gari likiwa limezama kwenye maji huku Mmiliki wake akisikika kwenye video hiyo akiwa anasali na kukemea kwa jina la Yesu.

AyoTV na millardayo.com zimempata Mmiliki huyu na kuelezea tukio zima na sala ilivyosaidia, bonyeza play kwenye hii video hapa chini utafahamu kila kitu..

Tazama Video Mpya ya Mwimbaji Rayvanny Kutoka WCB ‘Zezeta’

$
0
0
Mwimbaji kutoka WCB Rayvanny amerudi kwenye TV na hii video mpya inaitwa ‘zezeta’ ambayo video yake haijafanyika hapa Tanzania… ukishaitazama hapa chini usisahau kutoa comment yako umeipokeaje.


JE, Dada Unapenda Kuwa Mrembo? Na Kaka Kuwa Mtanashati na Kurudisha Heshima ya Ndoa?

$
0
0

JE, DADA UNAPENDA KUWA MREMBO? NA KAKA UNAPENDA KUWA MTANASHATI NA KURUDISHA HESHIMA YA NDOA?

Tumia Bidhaa halisi za MARKSON kwa mafanikio ya uhakika na bila madhara.
Zimetengenezwa kwa mimea na matunda na kuthibitishwa kiafya.
🍉🌿🍓🍒🎄🍍🍀🍓🍉
Pata hizi 👇👇👇👇👇👇

1. kurefusha nywele na kuzuia kukatika ovyo @120,000/=
2. Kuongeza shepu (hips, makalio na mapaja) kwa (a)BOTCHO MULT-PLUS 10× @200,000/=
(b)Vidonge @180,000/=
3. Kuwa mweupe na softi mwili mzima kwa:- (1)Mafuta @120,000/=
(11)Vidonge @150,000/=
4. Kupunguza unene na manyama uzembe @150,000/=
5. Kuongeza uume pamoja na nguvu za kiume kwa:-
(a) Gely ya kupaka @130,000/=
(b) Vidonge kwa ajili ya kuongeza nguvu hata kwa wenye kisukari @130,000/= (c)Handsome up original @200,000/=
6. Kuondoa mvi milele zisiludi tena @120,000/=
7. Kuongeza unene wa mwili mzima na uzito pamoja na hamu ya kula @120,000/=
8. Kupunguza tumbo (kitambi) na nyama za pembeni kwa:-
(a) Dawa ya kunywa au kupaka @120,000/=
(b) Mkanda wa kawaida @100,000/=
(c) micro-computer belt unaovaibret @250,000/=
9 .Kupunguza maziwa na kuyasimamisha @120,000/=
10. Kushepu miguu na kuwa minene na kuondoa migimbi @120,000/=
11. Kuondoa mipasuko mwilini (michirizi) @100,000/=
12. kubana uke na kuongeza hamu ya tendo la ndoa kwa mwanamke @120,000/=

NB: Hakikisha unapata risiti yenye muhuri halisi wa MARKSON CO pamoja na garantii ili kukuhakikishia kufanikiwa kwako.


Wasiliana nasi :-
(+255) 0767447444 na
0714335378


Follow us on instagram @Markson_beauty_pr
@Markson_beauty_pr

AJALI:Treni ya Abiria Yapata Ajali Mbaya Mkoani Morogoro

$
0
0
Treni ya abiria iliyokuwa inakwenda Bara imepata ajali usiku wa kumakia leo majira ya saa 5:25 katika eneo la Stesheni ya Mazimbu mkoani Morogoro. Katika hajali hiyo ilihusisha mabehewa saba ambapo manne yakiwa yameegama na matatu yameacha reli.

Abiria mmoja, Ashura Mrisho aliyekuwa anasafiri kwenda Tabora amepata maumivu baada ya kuangukiwa na mizigo ilikuwamo ndani ya behewa moja.

Mabehewa 13 yamerejeshwa Morogoro kuwapangia usafiri mbadala abiria wa treni hiyo.
Shirika la Reli Tanzania (TRL) linafanya utaratibu wa kuwasafirisha abiria wa bara kwa mabasi hadi Kijiji cha Lukobe Manispaa ya Morogoro ambapo watapanda treni kwenda bara. Kuhusu wale wa treni ya kuja Dar es Salaam kutoka bara ambayo itasimama Lukobe, watasafirishwa kwa mabasi kurudi Morogoro kuendelea na safari.

Taarifa zaidi zitafuata wakati uongozi wa TRL, mafundi na wahandisi wakishughulikia ajali hiyo.



Shamsa Adaiwa Kumfirisi Mumewe

$
0
0
DAR ES SALAAM: Ikiwa ni miezi nane tu imepita tangu aingie kwenye ndoa, staa wa filamu za Kibongo, Shamsa Ford anadaiwa kumfilisi mumewe, Rashid Said ‘Chid Mapenzi’, Risasi Jumamosi lina mkanda kamili.

Chanzo makini ambacho ni ndugu wa mume wa Shamsa kililiambia Risasi Jumamosi kuwa mwanamama huyo tangu aolewe, maisha ya Chid Mapenzi yamebadilika kwani hata biashara zake haziendi vizuri jambo ambalo linaonekana kuwa mwanamke huyo amempa gundu.

“Kiukweli Shamsa ni kama amempa gundu mumewe kwani tangu waoane mambo siyo mazuri, amekuwa akimkataza kuwa hata na marafiki zake jambo linalowachukiza sana ndugu maana anamrudisha nyuma ndugu yao.


“Angalia mpaka duka walilokuwa nalo pale Mwananyamala-Komakoma wamelifunga na vitu vimerudishwa nyumbani hivyo wanauzia nguo na viatu nyumbani.

“Kilichosababisha wakafunga pale ni kwamba kwanza Shamsa anaringa sana pia kodi iliwashinda kwani walitaka kutoa ya miezi mitatu baada ya kodi waliyolipia kuisha hivyo mwenye nyumba akakataa kwani alitaka ya mwaka mzima ndiyo wakaamua kurudisha kwanza nyumbani wakiendelea kutafuta sehemu nyingine,” kilisema chanzo hicho.

Baada ya kujiridhisha, Risasi Jumamosi lilimtafuta Shamsa aliyekiri kuwa ni kweli duka wamefunga lakini wanampango wa kuhamia sehemu nyingine siyo kwamba mumewe amefilisika.

“Nilijua watasema mengi tu lakini ukweli ni kwamba baada ya kuona kodi ni kubwa na biashara ni ngumu nilimshauri mume wangu tuhamie sehemu nyingine na mimi kama mke nina jukumu la kumshauri mume wangu kwa jambo lolote na tumeshapata sehemu nyingine hapohapo Mwananyamala ndiyo tunapafanyia matengenezo tutahamia hivi karibuni tu,” alisema Shamsa.

GPL

Namna ya Kujua Kama Umemridhisha Mpenzi Wako Kitandani

$
0
0
Raha ya kuwa katika mahusiano ya kimapenzi baina ya wapenzi wawili ni kila mmoja kuwa na furaha na kuridhika kwa yale anayofanyiwa na mwenzake. Siku zote kila mmoja hujitahidi kufanya mambo ambayo anahisi yatamridhisha na kumfurahisha mwenza wake ili kuendelea kuyastawisha mapenzi baina yao.

Watu wengi wamekuwa wakifanya mambo kama vile kununuliana zawadi, kwenda kutembea pamoja, kuukaapamoja na mengine mengi kwa lengo la kuwafurahisha wenza wao.

Vilevile katika mahusiano kufanya mapenzi ni njia moja wapo muhimu ya kuonyesha kuwa unampenda na kumjali mwenza wako.

Wapenzi wengi wanapofanya mapenzi, kila mmoja hutamani kumridhisha mwenzake na kuhakikisha kuwa amelifurahia tendo. Japo wapo wengi hasa wanaume wanaodhani kuwa wamewaridhisha wapenzi wao lakini ukweli ni kuwa wenza wao hawakuridhika.

Wanawake wameumbwa na hisia tofauti kwa kila mmoja, na wana namna tofauti ya kuridhishwa katika kujamiiana.

Idadi kubwa ya wanawake walioko katika mahusiano hawakuwahi kufika kileleni ama wamefikishwa mara chache sana katika muda wote ambao wamefanya mapenzi.

Wako wachache wenye ujasiri wa kuwaeleza wapenzi wao kuwa hawajafika kileleni, lakini wengi wao hubaki wakiugulia tu moyoni jambo ambalo hupelekea wao kutafuta wanaume wengine ili wajaribu kama watafikishwa kileleni.

Kwa wanaume wengi hudhani kuwa wapenzi wao wamefika kileleni, kumbe hudanganywa na wanawake ili tu wamalize na wasiendelee kuwpotezea muda pasipo mafanikio.

Hizi hapa ni njia chache ambazo kupitia hizo unaweza kutambua kama mwenza wako amefika kileleni ama anakudanganya ili umalize haja yako na kuondoka.

Kukukumbatia kwa nguvu au kukufinya

mwanamke anapokuwa anakaribia au anapofika kileleni, huwa na tabia ya kujikaza na kufanya vitendo kama vile kufinya shuka, kukukumbatia kwa nguvu au hata kung’ata meno. ukiona mwanamke amefikia hatua ya kufanya vitendo hivyo basi huenda anakaribia kufika au ndiyo anafika kileleni.

Kutokwa na jasho ndani ya sekunde chache
Ukiona mwanamke anatokwa na jasho ndani ya sekunde chache na katika hali isiyo ya kawaida basi jua kua utendaji wako ni mzuri na unamridhisha.

Uhisi misuli ya uke ikikaza na kuachia

Mwanamke anapokaribia kutaka kufika kileleni utasikia misuli kuzunguka uke kama inakaza na kuachia hivyo hivyo kwa sekunde kadhaa na utahisi wazi uume ukibanwa na kuachiwa hivi. Na wakati huu mwanaume hatakiwi afike kileleni kwani atamwacha mwenza wake pabaya sana. Kadri mwanamke anavyokaribia kufika kileleni ndivyo na kasi ya kukaza na kuachia kwa misuli ya uke itakavyokuwa inaongezeka. Kitendo hiki cha uke kuubana na kuuachia uume kitaendelea kwa kujirudia rudia mpaka mwanamke atakapofika kileleni.

Lugha ya mwili

Hapa mwanamke anaweza kuwa anahema haraka haraka kwa sababu ogani zake za ndani na mishipa yake vitakuwa vinahitaji oksijeni zaidi ili aweze kufika kileleni salama. Hivyo hivyo atazidisha kujikunjakunja, kujinyonganyonga au kujisogeza kwako. Kama atakuwa ametulia tu ujue bado hivyo ongeza bidii.

Jack Wolper Aongoza Mastaa Kwa Kuhongwa!

$
0
0
CONFESSION! Staa mwenye umbo na muonekano wa ‘kokoro’, Jacqueline Wolper Massawe ‘Gambe’ amekiri kuwa hakuna msanii wa kike anayeongoza kwa kuhongwa vitu vya thamani na gharama kubwa zaidi yake, Ijumaa tunakutiririshia aya zake.

Jumatatu ya wiki hii, ‘mbayuwayu’ wetu walipiga hodi na kuweka kambi ya muda nyumbani kwake, Kinondoni, Mkwajuni jijini Dar na ‘kumbananisha ukutani’ kwa maswali magumu ambapo pamoja na mambo mengine, alikiri kuhongwa vitu mbalimbali na vigogo, wakiwemo viongozi wa ngazi za juu serikalini pamoja na wafanyabiashara. Wolper amesema japo kuna wasanii wengi wanaohongwa vizuri, lakini yeye amekuwa wa tofauti, kufuatia aina ya vitu anavyopewa ambavyo ni mijengo ya maana na magari ya kifahari.

ALISEMA;
“Naweza kuwa kinara wa mastaa wa Bongo kuhongwa mali na fedha nyingi kuliko msanii mwingine yeyote,  kama nyumba, magari lakini kwenye duka hili hakuna mkono wa mwanaume isipokuwa ni jitihada binafsi. “Kama mtakuwa na kumbukumbu nzuri, mtakuwa mnajua habari ya lile gari la kifahari, Toyota Prado nililowahi kuhongwa na mmoja wa wanaume niliyewahi kutoka naye kimapenzi, thamani yangu ni kubwa, mwanaume akitaka kunitokea na kunihonga lazima aje kwa kujitosheleza kikubwa zaidi na ajipange kiume kwelikweli.

” Pia Wolper aliweka wazi kuwa, kwa sasa amebadili mfumo mzima wa maisha yake, ambapo ameachana na utegemezi wa kuhongwa na wanaume ndiyo maana ameamua kujiingiza kwenye ujasiriamali ili atumie jasho lake halisi.

Aliongeza:
“ Hao watu wanaozusha maneno kwamba biashara yangu nimehongwa, huko  ni kutafuta kiki na cheap popularity (umaarufu wa bei nafuu) kupitia mgongo wangu, biashara hii imenichukua zaidi ya miaka miwili kuifanikisha, watu waache maneno na badala yake wafanye kazi.
” TUGEUZE SHINGO KIDOGO

Kumbukumbu zinaonesha kuwa, kipindi cha nyuma msanii huyo aliwahi kuhongwa gari aina ya Toyota Prado na aliyewahi kuwa mpenzi wake, Dallas ikiwemo kuishi kwa mbwembwe za kuonesha jeuri ya fedha.

GPL

Mwalimu Atiwa Mbaroni Baada ya Kuiba Mtoto Mchanga Hospitalini

$
0
0

JESHI la Polisi mkoani Songwe linamshikilia Mwalimu wa Shule ya Msingi Majengo, mkazi wa Songa katika Halmashauri ya mji wa Tunduma, (jina linahifadhiwa) kwa tuhuma za kuiba mtoto mchanga wa siku moja.

Mtoto huyo aliibwa katika wodi ya wazazi kwenye Hospitali ya Wilaya Mbozi mjini Vwawa.

Roida Salimu, ambaye ni shuhuda wa tukio hilo, alisema mwanamke huyo aliingia wodi hiyo  kwa njia ya kificho muda usiojulikana akiwa amejifunga nguo tumboni kama mjamzito anayetarajia kujifungua na pia hakuwa na kadi ya kliniki.

Alisema baada ya kumwiba mtoto huyo alimficha chooni nyuma ya mlango akiwa amemviringisha nguo wakati akitafuta njia
ya kutokomea naye.

Alisema mama mzazi wa mtoto huyo ambaye alijifungua watoto mapacha wote wakiume, alishtuka kuwa mtoto mmoja hayupo kitandani muda wa saa
10:00 alfariji Mei 11 mwaka huu na kutoa taarifa kwa muuguzi wa zamu ndipo jitihada za kumtafuta zilianza.

Mganga Mkuu Wilaya ya Mbozi, Janeth Makoye, alikiri kukamatwa kwa mama huyo katika hospitari hiyo na kuwa mama mwenye mtoto ni mama wa
miaka 17, mkazi wa Kamsamba wilayani Momba .

Alisema baada ya kujifungua  Mei 10 mwaka huu, alikuwa akisubiri kuruhusiwa na watoto wake mapacha wote wakiwa wakiume wakiwa na umri wa siku moja.

Alisema ni utaratibu mama mjamzito akijifungua lazima awe kwenye uangalizi wa saa 24 ili kufuatilia afya ya mama na mtoto kama wako salama kabla ya kuwaruhusu.

Aidha, alisema kuwa elimu kwa  jamii inatakiwa kutolewa hasa kwa wale wasio kuwa na uwezo wa kuzaa ama kutungisha mimba ili kufika katika
vituo vya afya na kupima kwani wanawake wamekuwa wakinyanyaswa bila kujua kati ya mama au baba nani ana tatizo.

Atupele Gabriel, alisema tukio hilo liwe fundisho na hatua madhubuti za kuimarisha ulinzi hospitalini hapo zichukuliwe kwa kujenga uzio wa
ukuta badala ya uzio wa senyenge uliopo ambao unatoa nafasi mharifu kupenya.

Kaimu Kamanda wa Jeshi la Polisi, mkoani hapa Ambwene Mwanyasi, alisema kuwa mwanamke huyo alikamatwa Mei
11 mwaka huu saa 11 alfajiri akijaribu kutoroka na mtoto huyo wa jinsia ya kiume.

Mwanyasi aliongeza kuwa mama huyo alijifunga nguo tumboni ili aonekane ana ujauzito na kwenda wodini bila kupitia mapokezi.

Kamanda alisema mahojiano yalionyesha kuwa chanzo cha tukio hilo mwanamke huyo kunyanyaswa na mume wake kwa kutozaa ndipo alipoamua kufanya tukio hilo ili kunusuru ndoa yake.

Huu Ndio Ukweli Kuhusu Ndege iliyovutwa Kwa Trekta

$
0
0
NI kioja. Tangu lini ndege ndogo inayoonekana kuwa ya kubeba abiria ikatembea kwenye barabara za magari mitaani kwa kukokotwa na trekta?

Hivyo ndivyo wananchi wengi wa maeneo ya Dodoma mjini, hasa kutoka Uwanja wa Ndege hadi Area C, ambako walikuwa wakijiuliza kutokana na kujiri kwa tukio hilo la aina yake.

Na ndivyo ilivyokuwa pia katika maeneo mengine nchini, hususan kwa wale waliobahatika kuiona picha iliyosambazwa sana kwenye mitandao ya kijamii juzi, ikionyesha ndege ndogo yenye mwonekano wa kuvutia pichani ikiburutwa na trekta barabarani.

Ni tukio lililotokea kutoka Airport kwenda Area D, kupitia barabara ya Maili Mbili, ambako ndege hiyo ilikuwa ikikatiza polepole kwa kukokotwa na trekta kiasi cha kuwashangaza mamia ya watu waliobahatika kushuhudia jambo hilo ‘live’.

Kwingineko nchini, uvumi mwingi ukasambaa, ukiwamo ule uliokanushwa na Jeshi la Polisi kwamba ndege hiyo ilikuwa ikikokotwa baada ya kuanguka.

Kutokana na yote hayo, ambayo mwishowe yaliibuwa mijadala ya aina yake kwenye mitandao ya kijamii, ndipo Nipashe ilipofuatilia kwa kina zaidi jana na kumpata mmiliki wake, ambaye alisema kuwa amefurahi kutimiza ndoto yake ya kuipata ndege hiyo ambayo haikuanguka, bali aliinunua kwa bei poa isiyotosha hata kununulia gari kama Toyota Noah.

Kwa sharti la kutotajwa jina lake wazi, akihofia baadhi ya ndugu zake kudhani kwamba sasa amekuwa bilionea mkubwa kiasi cha kununua ndege ilhali ukweli ni kwamba ameipata kwa bei ya chini, mmiliki wa ndege hiyo, ambaye pia anamiliki hoteli ya African Dreams iliyoko Area D, alisema aliipata ndege hiyo iliyokuwa ya Serikali (ikidaiwa kuwahi kuwa ya JWTZ) baada ya kuibuka kinara katika mnada wa wazi uliofanyika Julai, mwaka jana, na kuwashirikisha watu wengine kadhaa.

“Hii ndege niliinunua tangu mwezi wa saba (Julai), mwaka jana. Lakini tatizo lilikuwa ni je, tutaitoaje kama ilivyo kuifikisha hapa hotelini bila usumbufu kama vile wa kukata miti ovyo?” alisema mmiliki huyo alipohojiwa na Nipashe jana.

Awali, Kamanda wa Polisi Mkoa wa Dodoma, Lazaro Mambosasa, pia aliithibitishia Nipashe jana kuwa taarifa nyingi zilizosambazwa mitandaoni hazikuwa za kweli, ikiwamo madai kuwa ni ndege iliyoanguka.

Bali, kilichotokea ni kwa mmiliki wa ndege hiyo chakavu kulazimika kuiondoa kutoka kwenye Uwanja wa Ndege wa Dodoma ilikokuwa imeegeshwa kwa muda mrefu na kuipeleka kwenye hoteli yake ikiwa kama ilivyo – jambo lililozingatia taratibu zote za kisheria ikiwamo masuala ya usalama barabarani.

“Kuna taarifa zinasema kuwa imeanguka si kweli. Hii ndege ni chakavu na ilishauzwa kwa mtu binafsi ambaye ni mmiliki wa hoteli ya Africa Dreams… sasa alikuwa akiivuta kwa trekta kuiondoa kwenye uwanja wa ndege na kuipeleka kwenye eneo lake la hoteli,” alisema Kamanda Mambosasa.

MMILIKI AFUNGUKA ZAIDI
Akielezea zaidi, mmiliki wa ndege hiyo alisema licha ya kushinda katika mnada wa mauzo ya ndege hiyo tangu Julai na kukwama kuiondoa kwa kutojua aisafirishe vipi bila kuathiri pia mwonekano wake, juzi alilazimika kutumia trekta kutimiza ndoto ya kuifkisha hotelini kwake, baada ya kuamriwa kuitoa kwenye eneo ilikokuwa ili kupisha ukarabati mkubwa wa uwanja huo.

“Awali nilitaka kuibeba kwa lori. Lakini lengo langu si kuiharibu hata kidogo. Nataka ifike kama ilivyo, hivyo nilishindwa kuitoa. Njia pekee ambayo ilionekana inawezekana ni hii ya kukokota taratibu kwa trekta,” alisema.

Alisema vibali vya kuihamisha kwa kuipitisha kwenye barabara ya magari alivipata kwa mamlaka zote husika zikiwamo Manispaa ya Dodoma, Wakala wa Barabara (Tanroads), uongozi wa Uwanja wa Ndege, Jeshi la Polisi na Jeshi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ).

Alisema lengo la kununua ndege hiyo ni kuongeza wigo wa biashara yake ya hoteli kwa kuifanya kama sehemu ya kivutio ambayo watu wataitumia kupigia picha mbalimbali za matukio kama ya sherehe za kuzaliwa, kipaimara, harusi na wanafunzi kupata fursa ya kujifunza pindi wakihitaji kufanya hivyo.

“Hapa hotelini nina eneo kubwa ambalo nitaiweka hii ndege na kuitengenezea mandhari kama ya ‘Airport’ (uwanja wa ndege) na itakuwa kama sehemu ya makumbusho ambako watu mbalimbali, wakiwamo watoto, watapata fursa ya kupigia picha kwa kulipia,” alisema na kuongeza:

“Ndani mle hamna viti (hivi sasa). Nitaanza kwa kuviweka, nitafunga kiyoyozi, nitatengeneza ndani ili iwe kama na kimgahawa au kioski kwa ajili ya vinywaji. Nitaiboresha zaidi ili itumike kupigia picha za harusi, birthday na kujifunzia pia.”

Akizungumzia chanzo cha ujio wa wazo lake hilo kibiashara, mmiliki huyo alisema ni kupingana kwake na wazo walilokuwa nalo washindani wake kwenye mnada wa mauzo ya ndege hiyo, ambao karibuni wote walipania kuibomoa ili wanufaike nayo kwa matumizi mengine kama chuma chakavu. Yeye akafikiria vinginevyo, akiamini kwamba ndege hiyo inaweza kumnufaisha zaidi kwa kuifanya sehemu ya kivutio hotelini kwake.

“Ndiyo maana hata kuitoa pale imekuwa ngumu ni kwa sababu nataka ifike hotelini kama ilivyo. Unajua hii ni rahisi mtu kuja hapa kuona na kujifunza. Wengine hawajawahi kuisogelea hata ndege… lakini hapa wataifikia, kupiga picha, wataingia ndani na kujifunza (zaidi) pia,” alisema.

Alisema changamoto mojawapo kwake ni hisia za baadhi ya watu wake wa karibu wanaoweza kudhani kuwa sasa ni tajiri sana kiasi cha kumiliki ndege, jambo ambalo si la kweli kwa sababu hiyo siyo mpya bali ni chakavu.

Aidha, alisema kumekuwapo pia na woga wa baadhi ya watu kuwa ndege inaweza kumilikiwa na taasisi za serikali au wazungu tu, jambo ambalo pia si sahihi kwa sababu kuna uwezekano wa Watanzania kumiliki ndege pia, kama yeye ambaye sasa anayo hiyo hata kama hairuki, lakini itamfaa kwa matumizi mengine ya kibiashara.

YAFIKIA AREA C
Hadi kufikia jana, ndege hiyo ilikuwa katika eneo maarufu la Wajenzi lililoko Area C, ikibaki hapo barabarani kwa muda wakati mchakato wa kuisafirisha hadi kwenye makazi ya kudumu hotelini, African Dreams ukiendelea.

Akizungumzia mahali ilipoweka kituo kwa muda sasa, mmiliki huyo alisema anashirikiana na wataalamu kuona namna ya kuipitisha salama bila kuharibu miti iliyoko pembezoni mwa eneo itakapopita hadi kufika hotelini na njia mojawapo ni kuifungua mabawa yake na kuyarudishia pindi safari yake hiyo itakapokamilika.

Alisema sababu nyingine ya kuiacha kwa muda eneo hilo hadi kufikia jana jioni ni kutoa fursa kwa wananchi kuiona ili wapunguze kiu, hivyo kupunguza idadi ya wale wanaoifuata kwa karibu kuishangaa safari ya kuipeleka hotelini itakapoanza tena.

“Kuna mtaalamu jioni ya leo (jana) tutakutana naye aangalie namna tutakavyoipitisha bila kusababisha uharibifu katika barabara ya Wajenzi hadi Area D. Kama ataona upana unaweza kuharibu miti, tutafungua mabawa yake halafu ikishaingia hotelini tutayafunga kama yalivyokuwa awali,” alisema mmiliki huyo.
Viewing all 104789 articles
Browse latest View live




Latest Images