Quantcast
Channel: UDAKU SPECIAL
Viewing all 104429 articles
Browse latest View live

SAKATA la Wanafunzi Vyuo Vikuu Kukosa Mikopo Kujirudia Tena Mwakani..Serikali Yawatengea Bajeti Kiduchu..!!!

0
0

BUNGE limeishauri serikali kuongeza bajeti ya Bodi ya Mikopo ya Wanafunzi wa Elimu ya Juu (HESLB) baada ya kubaini wanafunzi wengi watakosa fedha hizo mwakani kutokana na bajeti ndogo iliyotengwa.

Ushauri huo ulitolewa bungeni mjini hapa juzi na Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Huduma na Maendeleo ya Jamii ilipokuwa ikiwasilisha taarifa yake kuhusu utekelezaji wa bajeti ya Wizara ya Elimu, Sayansi, Teknolojia na Ufundi na makadirio ya wizara hiyo kwa mwaka ujao wa fedha.

Akiwasilisha taarifa hiyo, mjumbe wa kamati hiyo, Hussein Bashe, alisema wamebaini wanafunzi wengi watakosa mikopo mwaka ujao wa fedha licha ya kuwa na ufaulu mzuri.

Alisema mwaka huu wa fedha wanafunzi 48,502 walijaza fomu kwa ukamilifu lakini 25,555 tu ndiyo walipata mikopo na hivyo kuacha wengine 22,947 wakiwa hawana mikopo kutokana na bajeti iliyotengwa ya Sh. bilioni 427.5 kutotosheleza mahitaji.

Bashe ambaye pia ni Mbunge wa Nzega Mjini (CCM), alisema mwaka ujao wa fedha HESLB imeombewa Sh. bilioni 427.5 (sawa na bajeti ya mwaka huu) ilhali ufaulu wa wanafunzi waliohitimu kidato cha sita umeongezeka kutoka asilimia 88 mwaka 2012 hadi kufikia asilimia 99 mwaka huu.

"Kamati inaona kwamba, suala la elimu ya juu ni haki ya msingi kwa watu wenye sifa," alisema.

"Kamati inashauri serikali kuongeza bajeti ya HESLB ili wanafunzi wengi zaidi wanaostahili waweze kupata mikopo kwa maendeleo ya taifa letu."

Awali akiwasilisha hutoba kuhusu makadirio ya bajeti ya wizara yake kwa mwaka ujao wa fedha juzi, Waziri wa Elimu, Sayansi, Teknolojia na Ufundi, Prof. Joyce Ndalichako, alisema HESLB itatekeza mambo manne ikiwa ni pamoja na kutoa mikopo na ruzuku kwa wanafunzi wanufaika wa mikopo ambao idadi yake hakuitaja, hata hivyo.

Alisema jambo la pili ni kuboresha vigezo vya utambuzi ili kuwezesha wanafunzi wasio na uwezo wa kiuchumi kupata elimu ya juu kupitia mikopo na ruzuku.

Waziri huyo alisema bodi hiyo pia itapunguza utegemezi wa kifedha kutoka Mfuko Mkuu wa Hazina ya Serikali kwa asilimia 35.

Alisema jambo la nne ni kitambua vyanzo vingine vya kuchangia mfuko HESLB na ufundi kwa ajili ya kukopesha wanufaika wengi.

"Nitumie fursa hii kuwataka wanufaika wote ambao hawajaanza kufanya marejesho kutekeleza wajibu huo mara moja ili kuepusha usumbufu wa kuchukuliwa hatua za kisheria," alisema.

Prof. Ndalichako alisema kuwa, katika mwaka huu wa fedha, HELSB imetoa mikopo kwa wanafunzi 122,374.

Katika mchanganuo wake, waziri huyo alisema wanafunzi 28,785 ni wapya ambao mkopo wao unagharimu Sh. bilioni 104.614 na wanafunzi 93,559 ni wanaoendelea na masomo ambao unagharimu Sh. bilioni 379.18.

BASHE Arusha Dongo Lingine Serikalini..!!!

0
0

BUNGE limeishauri serikali kutoa kibali cha ajira mpya za madkatari na wataalamu 519 na fedha katika Hospitali ya Mafunzo Mlongazila jijini Dar es Salaam ili ianze kutoa huduma.

Ushauri huo ulitolewa bungeni mjini hapa juzi na Kamati ya Kudumu ya Huduma na Maendeleo ya Jamii pamoja na Kambi Rasmi ya Upinzani Bungeni wakati wa mjadala wa makadirio ya bajeti ya Wizara ya Elimu, Sayansi, Teknolojia na Ufundi kwa mwaka ujao wa fedha.

Mjumbe wa kamati hiyo, Hussein Bashe, akiwasilisha taarifa ya kamati, alisema walitembelea mradi Machi 21 na kuridhishwa na hatua iliyofikiwa ya ujenzi wa hospitali, lakini kuna changamoto ya upatikaji wa fedha kutoka serikalini na upungufu wa watumishi.

Alisema wakati wanatembelea mradi huo, ulikuwa umekamilika kwa kiasi kikubwa ikiwamo kuwapo kwa vifaa vya kisasa.

Alisema mradi huu ni moja kati ya miradi mikubwa nchini ukiwa na gharama ya Dola za Marekani 94,540,000 (Sh. bilioni 210.6) ambazo ni mkopo wa riba nafuu wa Dola 76,500,000 na mchango wa serikali ya Tanzania wa Dola 18,040,000.

"Katika mwaka huu wa fedha, chuo kiliomba jumla ya Sh. bilioni 14.549 kwa utaratibu maalum (special arrangement) kwa ajili ya ununuzi wa dawa, vitendanishi na matumizi mengine," Bashe alisema.

"Wakati kamati inatembelea mradi, hakuna fedha iliyokuwa imetolewa. Hata hivyo, waziri aliiahidi kamati kuwa, kufikia Aprili mwaka huu, itakuwa imetoa kiasi cha Sh. bilioni tano kwa ajili ya kuanza kununua vifaa tiba."

Aliongeza kuwa, pamoja na changamoto ya fedha, bado chuo kina upungufu wa rasilimali watu kwa kuwa mahitaji ni watumishi 900 na mpaka kamati inatembelea, waliopatikana ni watumishi 381, sawa na asilimia 42.3 ya mahitaji yote.

"Kamati inatoa rai kwa serikali kuhakikisha watumishi wote 900 wanapatikana ili kuweza kutoa huduma kwa wagonjwa, kinyume cha hapo ni kutoutendea haki mradi huu mkubwa na mzuri wenye vigezo vya hospitali za kimataifa," alisema.

Mbunge huyo wa Nzega Mjini (CCM) pia alisema kamati yao inaona uwekezaji huo mkubwa ni vyema uende sambamba na utolewaji wa fedha za kutosha ili utoe matunda tarajali.

WABUNGE Walalamika Kuombwa Ombwa Pesa na Wananchi Wao Majimboni..!!!

0
0

MBUNGE wa Ukonga, Mwita Waitara (Chadema), amesema wananchi wamewageuza wabunge wa Tanzania na kuwa kama mashine za kutolea fedha (ATM) na Vyama vya Kuweka na Kukopa (SACCOS).

Kutokana na hali hiyo, amesema kuna haja Serikali kuboresha mafao yao ili yaendane na majukumu wanayokabiliana nayo.

Waitara aliyasema hayo jana mjini hapa wakati wa semina ya wabunge walioko katika mabunge ya nchi Wanachama wa Jumuiya ya Madola (CPA).

“Mshahara wa mbunge kila mwezi unakatwa shilingi milioni 1.2, lakini baada ya kumaliza miaka mitano ya ubunge, mafao yake yanakatwa tena.

“Hivi huo utaratibu mliutoa wapi wakati haupo nchi yoyote duniani? Sisi wabunge tumegeuzwa kama ATM au saccos kwa sababu tutatoa pesa kila mahali.

“Kule Kenya ofisi ya mbunge ni kama taasisi kwa sababu ina mbunge na ina mtafiti anayemsaidia mbunge kila anapotaka kufanya mambo yake.

"Hata kukiwa na harambee, mbunge unaitwa na kutakiwa uchangie fedha nyingi, sasa utachanga kwa fedha zipi wakati mnatulipa kidogo, yaani huu ni mzigo kwetu wabunge.

“Kwa hiyo, tuongezeeni mafao kwa sababu tunalipwa kidogo sana ikilinganishwa na nchi zingine,”alisema Waitara.

Baba amshushia kipigo mke na mtoto kisa ugali

0
0

Polisi jijini Nairobi inamshikilia mwanaume mmoja kwa tuhuma za kumpiga mke wake na mtoto wake wa kiume kwa madai ya matumizi mabaya unga wa ugali. 

Mwanaume huyo ambaye jina lake halijafahamika anadaiwa  kuwapiga wawili hao akiwalalamikia kutumia vibaya fedha anazotoa kwa ajili ya matumizi. 

Mtuhumiwa huyo amedai kuwa fedha hizo kidogo  ambazo anapata shida mkewe na mtoto wamekuwa wakizitumia vibaya kununua unga wa ugali ambao gharama yake imepanda. 

Inadaiwa kuwa baada ya kuwapiga alijisalimisha polisi huku mkewe na mwanae wakikimbizwa hospitalini kwa ajili ya matibabu. 

Aua mke kwa shoka

0
0

Mkazi wa Kijiji cha Msia wilayani Sumbawanga mkoani Rukwa, Patrick Kipesa (39) amejinyonga kwa kutumia kamba ya katani mara baada ya kuumua mkewe kwa kumkata kata na shoka sehemu mbalimbali za mwili wake. 

Kaimu Kamanda  wa Polisi Mkoa wa Rukwa,  Polycarp Urio amesema  kuwa tukio hilo lilitokea jana saa 1:30 asubuhi katika Kijiji cha Msia wilayani Sumbawanga. 

Alimtaja aliyeuawa kuwa ni Theresia Selemani (49) mkazi wa kijiji cha Msia aliuawa kwa kukatwa katwa na shoka maeneo ya kichwani na shingoni na mume wake huyo. 

Amesema baada ya tukio hilo mtuhumiwa naye alijiua kwa kujinyonga kwa kutumia kamba ya katani akiwa sebuleni kwake na kufariki papo hapo. 

Chanzo cha kufanya mauaji hayo na yeye kujiua ni wivu  wa mapenzi baada ya mtuhumiwa kuhisi kuwa mkewe ana mahusiano wa kimapenzi na mwanaume mwingine, ambapo alimvizia marehemu na kumkata na shoka shingoni na kichwani. 

Katika tukio nyingine lililotokea jana, msichana Fatuma Yusuph (22) mkazi wa mtaa wa Shengetela, aliuawa kwa kukatwa na panga kichwani na mzazi mwenzie. 

Inadaiwa kuwa kabla ya mauti kumfika msichana huyo, kulizuka ugomvi baina yake na mwenzi wake ambaye jina linahifadhiwa chanzo kikiwa ni wivu wa kimapenzi ndipo waliposhindwa kuelewana na mwanaume huyo kumjeruhi kwa kumkata na panga kichwani msichana huyo. 

Baada ya tukio hilo marehemu alifika katika kituo cha polisi  kutoa taarifa ya kujeruhiwa akiwa na hali mbaya ambapo alipewa PF3 ili aende akatibiwe na ndipo mauti ilipomkuta akiwa  anapatiwa matibabu katika hospitali ya rufaa ya mkoa wa Rukwa iliyopo mjini hapa. 

Taarifa za kipolisi zinaeleza kwamba baada ya tukio hilo, mtuhumiwa alikimbia na kutoroka na kuelekea kusikojulikana. 

UDSM kuburuzwa mahakamani

0
0

Anadai hakuomba usajili moja kwa kwa moja chuoni hapo bali aliteuliwa kihalali na TCU 

Dar es Salaam. Mwanafunzi aliyefukuzwa Chuo Kikuu cha Dar es Salaam (UDSM), Alphonce Lusako amewasilisha maombi Mahakama Kuu aruhusiwe kukishtaki chuo hicho kwa kumkatisha masomo. 

Manase aliyekuwa akisoma shahada ya kwanza ya sheria alifukuzwa baada ya kufutiwa usajili Januari 26, pamoja na mambo mengine akidaiwa kusajiliwa kwa makosa kwa sababu aliwahi kufukuzwa chuoni hapo. 

Lusako anayewakilishwa na Wakili Jebra Kambole anaiomba Mahakama impe kibali cha kuishtaki UDSM na itoe amri kuzuia uamuzi wa kumfutia usajili. 

Maombi hayo yamefunguliwa chini ya hati ya dharura na yamepangwa kusikilizwa Mei 23 na Jaji Pellagia Khaday. 

Hii ni mara ya pili kwa Lusako kufukuzwa chuoni hapo, mara ya kwanza ni Desemba 13, 2011 akiwa mwaka wa tatu akidaiwa kuchochea mgomo. 

Hata hivyo, anadai alikuwa akipinga ufisadi katika Tume ya Vyuo Vikuu (TCU) kwa kusajili wanafunzi hewa na katika Bodi ya Mikopo ya Wanafunzi wa Elimu ya Juu (HESLB). 

Baada ya kukaa uraiani kwa muda mrefu, aliamua kuomba usajili TCU ili kuanza upya masomo. TCU ilimsajili na kumpanga UDSM kusoma kozi ya sheria. 

Baada ya kusoma muhula mmoja, alipewa barua ya kufutiwa usajili ikieleza alisajili kimakosa chuoni hapo kwa kuwa tayari alishawahi kufutia usajili. 

Katika hati ya kiapo mahakamani, anadai hakuomba usajili moja kwa moja UDSM bali aliteuliwa kihalali na TCU yenye mamlaka ya kutathimini maombi yake na kumpangia chuo. 

Anadai hakupewa haki ya kusikilizwa kwa mujibu wa kanuni za haki asili kabla ya kufutiwa usajili kwa sababu zisizo halali. 

Kabla ya kuwasilisha maombi mahakamani, alidai kwa mara kadhaa aliiomba UDSM imrejeshe chuoni bila mafanikio. 

Lusako alijiunga na UDSM kwa mara ya kwanza mwaka 2009 akiwa amedahiliwa kusoma Shahada ya Biashara katika Uhasibu. 

Mwaka 2011 pamoja na wenzake kadhaa walifukuzwa na kufutwa katika mfumo wa elimu nchini wakidaiwa kuratibu mgomo wa wanafunzi UDSM. 

Katika mgomo huo, walikuwa wakipinga kurudishwa nyumbani wanafunzi wa mwaka wa kwanza waliokuwa wameshawasili vyuo vikuu vya umma kwa hoja kwamba bajeti haitoshi. Walihoji kuwapo mikopo hewa iliyokuwa ikiishia kwa baadhi ya watendaji wasio waaminifu. 

Baada ya kufukuzwa walikakata rufaa Baraza la UDSM wakiomba lirejee uamuzi wa chuo lakini baraza lilikataa maombi yao. 

Agosti 30, 2012 walishinda kesi baada ya Mahakama kutupilia mbali mashtaka dhidi yao na waliporudi chuoni, yeye na wenzake 11 waliokuwa wameshtakiwa, lakini chuo kilikataa kuwarejesha.

KIMENUKA...Chemical Lita 6494 za Kutengeneza Heroine na Cocaine Zakamatwa Dar

0
0

Mamlaka ya kudhibiti na kupambana na Dawa za kulevya nchini inamshikilia mmiliki wa kampuni ya Techno Net Scientific kwa kuingiza kemikali bashirifu nchini zenye ujazo wa lita 6494 kwa kukiuka sheria na taratibu. 

 Imeelezwa kuwa, mmiliki huyo amekiuka sheria ya kudhibiti na kupambana na dawa za kulevya namba 5 ya 2015 na ile usimamizi na udhibiti wa kemikali za viwandani na majumbani, sheria ambayo inasimamiwa na Mkemia mkuu wa Serikali. 

Kamishna Mkuu wa mamlaka ya Kuzuia na Kupambana na dawa za kulevya Rogers Sianga amesema kuwa, Kukamatwa kwa mmiliki wa kampuni hiyo, yenye makazi yake eneo la mwenge kunatokana na taarifa walizopata kutoka kwa raia wema mwezi uliopita waliowataarifu kuwa kampuni hiyo inaagiza kemikali bashirifu, ambazo ni hatari kwa matumizi na zisiporatibiwa zinaweza kutumika vibaya na kuleta madhara. 

Akizungumza na waandishi wa habari ofisini kwake leo, baada ya ziara fupi ya kutembelea maghala mawili ya kampuni  hiyo yanayotumika kuhifhadhia kemikali hizo, Sianga amesema, uchunguzi wao umeonyesha kuwa, kampuni hiyo inaagiza kemikali bila kibali. 

“Tulichogundua ni kwamba kampuni hii ya Tecno Net Scientific yenye makazi yake eneo la mwenge, imeagiza kemikali nyingi ambazo ni bashirifu, kemikali bashirifu ni kemikali muhimu kwa utengenezaji wa kawaida wa dawa za binadamu lakini pia zikichepushwa  zikiwa diverted zinaweza kutengeneza dawa za kulevya za Heroine, Cocaine na nyinginezo ambazo huzalisha kemikali taka zenye sumu ambazo zinaweza kuhatarisha afya za watu na kuchafua mazingira. 

Ameongeza kuwa,wamegundua kuwa kampuni hiyo pia iliagiza kemikali nchini ufaransa kwa kibali cha kughusi na imekua ikiendesha shughukli zake za biashara ya kuuza kemikali bila kibali, licha ya vibali vyake kuisha muda wake tokea mwaka jana. 

 Ameongeza kuwa, mmiliki huyo anaendesha biashara ya kemikali bila ya kuwa na wataalamu kwani yeye binafsi ana elimu cheti cha huku mkurugenzi mtendaji wa kampuni hiyo anaelimu ya darasa la saba na baadae akajiendeleza Veta na kuwa fundi magari wakati kisheria ili uweze kuendesha biashara hiyo unatakiwa uwe na kuanzia diploma ya kemia na kuendelea. 

“Pamoja na Kemikali hizi bashirifu kuwa na matumizi halali kama viwandani na hospitali lakini zimewekewa utaratibu wa udhibiti kitaifa kitaifa na kimataifa kuanzia ununuaji, usafirishaji, jinsi ua uhifadhi na utumiaji wake kwakuwa kemikali hizo zikiachwa bila udhibiti watu wenye dhamira mbaya wanaweza kuzitumia kutengeneza dawa za kelevya”, amesema Sianga. 

Ameongeza kuwa mamlaka inachunguza tuhuma dhidi ya kampuni hiyo zikiwezo za kumiliki kemikali ambazo hazijasajiiwa na mamlaka husika kinyume na sheria baada ya usajili wake katika biashara kukoma, kutokuwa na taarifa za mwenendo mzina wa kemikali wanazoingiza  nchini na kuzisambaza kwa wateja, na nyinginezo nyongo. 

Amesema uchunguzi wa tuhuma hizo bado unaendelea na utakapokamilika hatua za kesheria zitachukuliwa na atafikishwa mahakamani.

UVCCM Wajibu Mapigo ya Lowassa..Wadai Anacheza Mchezo wa Tombola..!!!

0
0

Umoja Wa Vijana wa Chama cha Mapinduzi ( Uvccm ) umemtaka aliyekuwa waziri mkuu wa zamani na mjumbe wa kamati kuu ya chadema Edward Lowassa kufuta fikra ya kuwa Chadema itaibwaga CCM hata kama kutakuwa na UKAWA. 

Kauri hiyo imezungumzwa na kaimu katibu mkuu wa umoja wa vijana wa chama cha mapinduzi taifa (UVCCM) Shaka Hamdu Shaka na kusema kuwa.

“Kwa bahati mbaya Lowassa amesukumwa na hasira na kujikuta akijitoa CCM mwaka 2015 kama mtu aliyekuwa anacheza ngoma kwa kwenda upinzani huku akiwa na matumaini ya kuukwaa urais.Alisema kama kuna kosa kubwa ambalo Lowassa amelifanya ni kitendo chake cha kuhama CCM na kwenda upinzani hasa Chadema ,Kwa sababu yeye mwenyewe alishawahi kutamka hadharani akihutubia mkutano wa hadhara mwaka 2006 akilinganisha upinzani ni watoto wanaokimbilia mdundiko”.Lowassa asikubali kucheza tombola katika siasa,Siasa ni hesabu na ina formula zake.Nafikiri amekurupuka kujiondoa CCM ameupanda mkenge kwenda Chadema ajue kuwa si Ukawa wala Udeta wenye ubavu wa kuiondoa CCM madarakani alisema Shaka.

Alimtaka Lowassa kujua kuwa hata viongozi na wanachama wa upinzani hawamwafiki mwanasiasa huyo kwa asilimia kubwa,kwani wapo viongozi aliowakuta ambao wametoa jasho jingi kuvijenga vyama vyao hivyo hawapo tayari kumpisha agombee tena urais.

Pia Kaimu katibu mkuu Shaka alifafanua kuhusu kauri iliyotolewa na Lowassa kwa kusema kuwa Tanzania kuna ukandamizwaji wa demokrasia..Shaka alisema 

“ Haiba ya demokrasia iliyopo Tanzania huwezi kukutana nayo popote Afrika mashariki,Afrika na duniani kwa ujumla,Ila uamuzi wa serikali ya awamu ya tano ni kuwahimiza wananchi kufanya kazina kuzalisha mali viwandani na mashambani.Uhuru wa demokrasia au watu kujitawala bila shibe na maendeleo ya kisekta ni upuuzi.

Alisema kwa msisitizo ndugu Shaka.Pia aliendelea kusema kuwa 



“Tumemaliza kampeni na uchaguzi mkuu kila mmoja sasa afanya kazi, kukusanya watu kwenye makongamano na kuwapa bahashishi ni kuwapumbaza kiakili ikiwa bado ni Maskini" alimaliza kusema ndugu Shaka.. 

KIMENUKAA..Zari Aweka Wazi Mahaba Yake kwa Aliyekuwa Mume Wake wa Zamani Ivan..Ameandika Haya Kuthibitisha Hilo..!!!

0
0

Mama mjengo, Zari amevunja ukimya na kuamua kuweka wazi hisia zake kwa kuguswa na maradhi yanayomsumbua Mzazi mwenzake ‘Ivan Ssemwanga’ kwa kumuombea apate afya njema kama alivyokuwa zamani.

Zari kupitia ukurasa wake wa SnapChat ameandika “Siku mbili kwangu zimekuwa ngumu, nawaomba tumuombee Ivan”.

“Last 2 days have been hard. Let’s pray for IVAN please!“ameandika Mrembo Zari kwenye ukurasa wake wa Snapchat.

Taarifa kutoka mtandao wa Watch Dog wa Uganda umeripoti kuwa Ivan anasumbuliwa na maradhi ya Shambulio la Moyo (Coronary Artery Disease) .

Zari ambaye kwa sasa yupo kwenye mahusiano na Diamond Platnumz, amezaa na Tajiri Ivan Ssemwanga watoto watatu wote wa kiume.

BAADA ya Yanga Kuwa na Nafasi Kubwa ya Ubingwa Msimu Huu..Prof Jay Amefunguka Haya Mapya..!!!

0
0

Rapa mkongwe nchini Tanzania na Mbunge wa Mikumi kupitia tiketi ya CHADEMA, Mh Joseph Haule maarufu kwa jina la ‘Professa Jay’ ameitaka timu yake ya Simba kuweka nguvu zaidi katika fainali ya Kombe la Shirikisho kuliko Ligi Kuu.

Simba ambayo ipo nafasi ya pili kwa pointi 65 wakiwa wametofautiana na Yanga kwa tofauti ya Magoli wote wakiwa na alama sawa huku Wekundu wa Msimbazi wakiwa wamebakiwa na mchezo mmoja na Wanajangwani wakiwa na mechi mbili mkononi.

Profesa Jay licha ya kuiombea timu yake hiyo ichukue ubingwa wa Ligi Kuu, lakini alisema Simba ina nafasi kubwa ya kutwaa ubingwa bila wasiwasi wa Kombe la Shirikisho watakapocheza fainali yao dhidi ya Mbao FC kwenye Uwanja wa Jamhuri mjini Dodoma Mei 28 kuliko ubingwa wa Ligi.

Nguli huyo wa Hip Hop  amesema ubingwa wa Ligi Kuu kwa Simba utatagemeana na mechi za Yanga kama watashinda mechi moja kati ya mbili zilizosalia basi Simba hawatakuwa na chao hata wakishinda mchezo wao wa mwisho hivyo ni vyema zaidi kujipanga kwa fainali ya FA.

“Furaha yangu ni kuona Simba inachukua ubingwa wa Ligi Kuu  Tanzania bara na ubingwa wa Shirikisho kutokana na ubora wa kikosi cha timu yetu hivyo tutashinda mechi zilizobaki na kutwaa ubingwa japo imani yangu kubwa zaidi ipo kwenye Kombe la Shirikisho“,Alisema Professor Jay.

Akizungumzia fainali ya Kombe la Shirikisho itakayochezwa kwa mara ya kwanza kwenye Uwanja wa Jamhuri mjini Dodoma msanii huyo alilipongeza Shirikisho la Soka nchini {TFF} kwa kuipeleka fainali hiyo Makao makuu ya nchi kwani hata yeye na wabunge wengine watapata uhondo wa kushuhudia fainali hiyo.

Chanzo:Mwanaspoti

JPM Avunja CDA, Wafanyakazi Kupangiwa Kazi Ofisi Nyingine za Serikali..!!!

0
0

Rais John Magufuli amevunja Mamlaka ya Ustawishaji Makao Makuu Dodoma (CDA) na kuagiza mali na shughuli zote zilizokuwa zikifanywa na mamlaka hiyo zihamishiwe halmashauri ya manispaa ya Dodoma.

Rais Magufuli pia amevunja bodi ya CDA hivyo  aliyekuwa mkurugenzi  mkuu wa bodi hiyo, Paskasi Muragili atapangiwa kazi nyingine na ameagiza wafanyakazi wote wa mamlaka hiyo wahamishiwe Halmashauri ya Manispaa ya Dodoma na ofisi nyingine za Serikali kadri inavyofaa.

Rais Magufuli amevunja CDA kwa kutia saini hati ya amri ya Rais ya kuivunja mamlaka hiyo.

Amesema ameamua kuivunja mamlaka hiyo na kuhamishia majukumu yake katika Halmashauri ya Manispaa ya Dodoma ili kuondoa mkanganyiko wa utoaji huduma kwa wananchi uliokuwa ukisababishwa ma mgongano kati ya vyombo hivyo viwili.

Pia amesema ni kwa ajili ya kuendana na mahitaji ya sasa ambayo yamedhihirishwa kuwa hakuna haja ya kuwepo kwa CDA.

RAHA ya Kufanya Mapenzi Sehemu Hatarishi zisizo Sahihi..

0
0
Wimbi la Watu Kufanya Mapenzi kwenye Magari hapa Mjini mchana kweupe limeongezeka kwa kasi...Hapa namaanisha kufanya mapenzi katika maeneo hatarishi na siyo mapenzi hatarishi,yan kufanyia mapenzi maeneo ambayo hayakupi utulivu wa asilimia mia,na maeneo hayo ni kama vile kufanyia mapenzi ofisini au choo cha ofisi, Beach disco,kwenye siti ya nyuma ya bus la public,vichochoroni, Kwenye Gari  nk,hivi wapendwa huwa ujasili unatoka wapi?
Na je kufanya mapenzi sehemu hizi kuna raha zaidi ya kufanya kwenye chumba?
Tupe Maoni yako

GODBLESS Lema: Kuwa Mpinzani Tanzania inahitaji Uvumilivu

0
0
Mbunge Godbless Lema amedai kuwa mpinzani wa siasa za bongo ni kazi ngumu sana, Mh Lema amesema hayo baada ya baaadhi ya watu kumdhihaki alipotoa shukrani zake kwa Mbunge Lazaro Nyalandu kufuatia kuwasaidia majeruhi wa ajali ya basi la Lucky Vicent.

Jana baada ya Mbunge Godbless Lema kumshukuru Mbunge wa Singida Kaskazini (CCM) Lazaro Nyalandu kuna kundi la watu liliibuka na kuanza kutoa maneno ya dhihaka kwa Lema huku wengine wakipongeza na kusema ni jambo la kheri kwa mbunge huyo kutambua kazi iliyofanywa na Nyalandu, lakini baada ya mijadala hiyo kuzidi kuwa mikuba aliibuka Mh. Lema na kutoa kauli hii kumjibu mtu mmoja ambaye alikuwa akimdhihaki.

"Kuwa mpinzani wa siasa Tanzania ni kazi ngumu sana, ila hatukati tamaa kwa sababu upendo wetu ni mkuu kuliko dhihaka. Mungu akubariki" aliandika Godbless Lema

ADAM Malima Atibuana na Polisi, Wafyatua Risasi Hewani

0
0
TAHARUKI imeibuka mchana huu maeneo ya  Masaki karibu na Double Tree Hotel baada ya askari polisi mmoja kufyatua risasi hewani kutokana na kile kilichoonekana kuwepo kwa mzozo kati ya polisi na mbunge wa zamani wa Mkuranga, Pwani, Adam Kighoma Ali Malim.

Taarifa zimeeleza kuwa chanzo cha tukio hilo yalikuwa ni majibizano kati ya Majembe Auction Mart waliokuwa wameambatana na polisi walipojaribu kukamata gari lililokuwa limeegeshwa barabarani.


Inasemekana gari lilikuwa la mwanaye Kighoma Malima aliyekuwa eneo hilo kwa shughuli zake binafsi ambapo ofisa wa Majembe alivamia gari hilo na alipodaiwa kuonyesha vitambulisho aligoma kutoa ndipo wananchi walipolizingira gari wakitaka kumpiga wakizania ni jambazi.

Polisi aliingilia kati na katika majibizano ya maneno na Malima, ndipo askari mmoja akafyatua risasi kadhaa hewani hali iliyozua taharuki kubwa eneo hilo.

Mtandao wa Global Publishers umefanya jitihada za kumtafuta Malima kwa njia ya simu lakini simu zake zimeita bila kupokelewa.

Endelea kufuatilia taarifa zetu tutakujuza zaidi kadri tutakavyozipata.

JE, Hujaona Siku Zako (Hedhi) na Huna Mimba? Majibu ya Hali Hiyo Yapo Hapa..!!!

0
0

Kuna baadhi ya wanawake wamekuwa wakikosa la kufanya pale wanapoona siku zao za mzunguko (hedhi) zimefika halafu bado hawajaona siku hizo.

Hali hiyo huwapelekea wengi wao kuwa na maswali mengi, huku wengi wao wakianza kufikiri kuhusu ujauzito, lakini wanapopima ujauzito kwa bahati mbaya hukuta hakuna kitu hapo ndipo huzidi kuchanganyikiwa zaidi.

Sasa leo napenda tufahamishane hizi sababu ambazo huweza kuchangia siku zako kuchelewa kuonekana:-

1. Mabadiliko ya shughuli zako za kila siku
Huenda umeajiri sehemu mpya ambayo inakulazimu kubadili mfumo wako mzima wa maisha ya kila siku ikiwa ni pamoja na muda wa kuamka au umesafiri kutoka sehemu moja kwenda sehemu nyingine, hali hiyo na mengine huweza kuwa chanzo cha mabadiliko ya mzunguko wako ikiwa ni pamoja na kuchelewa.

2. Msongo wa mawazo 'stress'
Msongo wa mawazo ni mojawapo ya sababu ambazo huweza kuchangia kuvuruga mzunguko wako wa hedhi na kuchangia siku zako kuchelewa pia.

3. Magonjwa
Pale mwili unapopatwa na mabadiliko yakiwemo ya kuumwa nayo huweza kuwa sababu ya kubadili mzunguko wako wa hedhi na kuchangia pia kuchelewa kuona siku zako, kwahiyo ukiona hali hiyo unaweza kurudisha nyuma kumbukumbu zako na kukumbuka endapo wiki moja au mbili nyuma kama ulikuwa unaumwa au ulikuwa sawa.

4. Mabadiliko ya uzito.
Kuongezeka au kupungua kwa uzito huweza pia kuwa chanzo cha tatizo hili, hii ni kwasababu watu wenye uzito mkubwa au wenye uzito mdogo kunawakati huweza kujikuta wakiingia kwenye tatizo kama hili la kuchelewa kuona siku.

WASTARA Adaiwa Kushindwa Kulipa Kodi ya Nyumba!

0
0
Ubuyu wa mjini unamgusa staa wa sinema za Kibongo, Wastara Juma ambaye baada ya kutua Bongo akitokea nchini Sweden alikokuwa kikazi, anadaiwa kufulia na kushindwa kulipa kodi ya ile nyumba aliyodai kuinunua huko Ukonga, Dar.

ADAIWA KUJIPANGA KURUDI TABATA

Ubuyu mzito umeshushwa kwenye Wikienda kuwa, kwa sasa Wastara anajipanga kurudi kuishi kwa dada yake, Tabata, Dar alikokuwa akiishi zamani.

Mtoa ubuyu wetu alinyetisha kuwa, si kweli kwamba, nyumba hiyo aliyokuwa akiishi Wastara kabla ya kutimkia Sweden aliinunua kama alivyodai badala yake alipanga na sasa ameiacha kwa sababu hali yake kiuchumi ni tete.



TUJIUNGE NA MTOA UBUYU

“Hivi mnajua kuwa ile nyumba ambayo Wastara alikuwa anasema ameinunua si kweli, alikuwa amepanga? Sasa imebidi arudi kwa dada yake, Tabata kwa sababu maisha ya kupanga yamemshinda,” alitonya mtoa ubuyu huyo kwa ombi maalum la kutotajwa gazetini.

WIKIENDA HALILAZI DAMU

Kama kawa, Wikienda huwa halilazi damu hivyo lilianza kuichimba habari hiyo ili kupata ubuyu mtamu ambapo lilimsaka Wastara na kufanya naye mahojiano juu ya ishu hiyo ambapo mambo yalikuwa hivi;

Wikienda: Mambo vipi Wastara? Tumepata ubuyu kuwa umerudi Bongo kutoka Sweden lakini inasemekana mambo si mambo. Hapa kuna ubuyu kuwa ile nyumba uliyosema umeinunua na kuimiliki maeneo ya Ukonga si yako. Pia kuna madai kuwa imekushinda kwa sababu umeshindwa kuilipia kodi, je, hili likoje?

Wastara: Dah! Jamani nimeamini watu ni wambeya sana. Mbona mimi nipo Ukonga? Ila ni kweli nina mpango wa kuhama, lakini ‘pliiz’ si mambo ya kodi. Huku (Ukonga) nilihamia kwa sababu ya mtoto wangu. Sasa amemaliza masomo hivyo nahama, lakini siyo kwamba nimekosa kodi. Siwezi kukosa ninyi wenyewe mnajua.



Wikienda: Vipi kuhusu suala la kuinunua nyumba hiyo?

Je, ni kweli kwamba hukuinunua maana suala hilo linaleta utata?

Wastara: Wewe elewa nilichokueleza, kuhusu nyumba, mimi nina nyumba tatu, nikiamua nikae ipi ni mimi ndiye ninaamua. Hakuna wa kunipangia.

Wikienda: Wastara mbona unakuwa mkali? Pia kuna habari kuwa kwa sasa unatembelea Bajaj na kwamba gari lako lipo juu ya mawe. Unalizungumziaje hilo?

Wastara: Mimi najua anayeeneza mambo yote hayo yote ya uongouongo ni kijana wangu wa kazi ambaye nimemfukuza juzikati kwa sababu ameniibia. Nimekuwa nikitendwa sana na vijana ninaowasaidia kazi kwa hiyo mimi sishangai, najua yatasemwa mengi juu yangu.

NENO LA MHARIRI

Kama kweli Wastara anasingiziwa tunampa pole na kumtaka kuwa makini na vijana wake wa kazi ambao amekuwa akiwalalamikia mara kwa mara kuwa huwa wanamfanyia mambo ya kihuni kisha kumwacha akiugulia maumivu.

NI TABIA YA BAADHI YA MASTAA

Hata hivyo, baadhi ya mastaa wamekuwa na tabia ya kudanganya juu ya misha yao halisi. Wamekuwa wakidanganya kuwa wanamiliki vitu vya thamani, lakini tunapozama kusaka ukweli huwa wanaumbuka na mfano mzuri ni nyumba aliyokuwa akiishi Wema Sepetu, Mtaa wa Bwawani, Kijitonyama jijini Dar ambayo mwanzoni alidanganya kuinunua ilihali alikuwa amepanga.

NJIA 3 Rahisi Ambazo Zikizingatiwa Huweza Kurejesha Nguvu za Kiume..!!!

0
0

Huenda umekuwa ukisumbuliwa na tatizo la ukosefu wa upungufu wa nguvu za kiume na umeshindwa kujua nini ufanye ili kutatua tatizo hilo.

Yafuatayo ni mambo ambayo ukizingatia wewe mwanaume mwenye tatizo hilo unaweza kupata ahueni:-

Epuka matumizi ya pombe.

Matumizi ya pombe huweza kukushawishi kufanya tendo la ndoa lakini pia pombe hiyo hiyo huweza kumnyima mhusika uwezo wa kushiriki tendo la ndoa. Hivyo kama unapenda kuepuka tatizo hilo jitahidi kuepukana na matumizi ya pombe.

Jitahidi kushiriki kufanya mazoezi

Watu wengi hujikuta wakisongwa na magonjwa mbalimbali kutokana na kutofanya mazoezi, lakini pia ni vyema ikafahamika kuwa mazoezi husaidia hata kufanya mzunguko wa damu kuwa mzuri ndani ya mwili jambo ambalo pia husaidia kwenye masuala ya tendo ya ndoa.

Jitahidi kupata muda wa kutosha wa kulala, punguza mawazo (stress) kula vizuri na upate muda wa kufurahi na marafiki na ndugu

HII Hapa Faida Ya Kufikiri Kama Tajiri Hata Kama Huna Kitu Mfukoni...!!!

0
0

Kuna wakati unakuwa unashangaa kwa nini watu wengine ni matajiri sana na wakati wengine ni maskini. Najua umekuwa na mawazo mengi juu ya hili na kufikiri pengine hawa ni watu wenye bahati sana, wamezaliwa kwenye familia tajiri au pengine watu hawa wana kazi nzuri na wamezaliwa kwenye nchi zenye mafanikio.

Ni ukweli, yote haya yanaweza kuwa majibu kwa namna fulani, lakini hata hivyo kipo kitu kimoja muhimu sana ambacho kinafanya watu wengine kuwa matajiri na wengine kuendelea kubaki kwenye umaskini. Kitu hiki ambacho kinaleta tofauti zote hizo si kingine bali ni mawazo yako.

Badala ya kuendelea kulalamika kwa nini upo kwenye hali ngumu, kwa nini maisha yako yako magumu, kwa nini hufanikishi malengo yako fulani ambayo unayatamani sana karibu kila siku, kitu cha kwanza ambacho unatakiwa kukiangalia, angalia sana mawazo yako hasa linapokuja suala la pesa.

Mawazo yetu mara nyingi sana yana nguvu ya kutupa kitu chocho ambacho tunakihitaji katika maisha yetu. Mawazo yetu yamepewa uwezo wa kuumba fursa na kila hali ambayo tunaitaka ijitokeze kwetu. Kinachotakiwa kufanyika ni kuamua kutumia  mawazo haya kwa ufasaha hadi kuweza kutufanikisha.

Kwa hiyo mpaka hapo unaelewa kabisa faida kubwa ya kufikiri kama tajiri hata kama huna kitu mfukoni inakusaidaia wewe kuweza kupata kile unachokihitaji kwa hatua. Ni suala la kuujaza ubongo na akili yako taarifa za kitajiri, taarifa za mafanikio na hapo utatengeneza mazingira mazuri ya kufanikiwa.

Epuka sana kuwa na mawazo mgando, mawazo ambayo kila wakati  yanalenga kukukwamisha. Ukiwa na mawazo hayo utateseka sana kwenye dimbwi la umaskini na hautaweza kutoka hapo. Kikubwa endelea kuwa chanya mpaka kuhakikisha ndoto zako zinatumia na kuwa kweli.

HAYA Ndiyo Matokeo Sita ya Kushangaza Utakayoyapata Kama Utajiwekea Ratiba ya Kula Ndizi Kila Siku..!!!

0
0

Ndizi zina virutubisho vingi kama vile vitamini, nyuzinyuzi, protini, wanga, madini ya chuma na virutubisho vya sukari kama ‘Sucrose’ na ‘Fructose’. Wataalam wa lishe wanasema kula ndizi mbili kwa siku kwa muda wa mwezi tu, afya yako itaimalika.

Kuondokana na tatizo la Kiungulia

Ndizi kiasili sio tunda lenye asidi kwa wingi, ikumbukwe kuwa kiungulia husababishwa na uwepo wa asidi nyingi mwilini. Hivyo ndizi ni tiba kwa wote ambao wanasumbuliwa na kiungulia. Kula japo ndizi moja kwa siku basi itatuliza haraka na kuondoa dalili zote za kiungulia.

Kuondoa Presha

Ndizi pia zina wingi wa madini ya ‘Sodiam’ na ‘Potassium’ ambayo huweka sawa presha ya damu na kuimarisha afya ya moyo. Madini hayo pia husaidia kutanua misuli ya moyo ili kufanya kazi zake kwa urahisi.

 Kuongeza Nguvu

Endapo utakula ndizi mbili kabla ya kazi yoyote hakika nguvu zako zitaongezeka. Kama ilivyoelezwa awali ndizi zina vitamini, madini, wanga, na ‘Glycemic’ (kiwango cha sukari yenye kutia nguvu mwilini) ambavyo vyote hivyo ni vyanzo vizuri vya kutia nguvu mwilini kwa haraka.
Kuondokana naugonjwa wa Vidonda vya tumbo

Ndizi zina mchanganyiko wa vilainishi na nyuzinyuzi ambazo hulainisha tumbo na kupelekea kuzuia mikwaruzo kwenye utumbo hivyo kuzuia vidonda vya tumbo.

Husaidia wagonjwa wa Anaemia

Anaemia kitaalamu ni ugonjwa unaosababishwa na upungufu wa madini ya chuma mwilini, madini hayo husaidia kwenye uzalishaji wa chembechembe za damu nyekukundu ambazo huhitajika kwa wingi mwilini.

Ndizi zina madini ya chuma ambayo huwasaidia wagonjwa wa Anaemia kwa sababu madini ya chuma husukuma uzalishaji wa ‘Haemoglobin’. Hivyo huongeza chembechembe nyekundu za damu na kuongeza mzunguko wa damu mwilini.

Haemoglobin ni protini inayopatikana kwenye chembechembe nyekundu za damu ambazo husafirisha hewa ya Oksijeni kutoka kwenye mapafu na kwenda sehem mbalimbali za mwili, Aidha huchukua pia hewa ya Kabondayoksaidi kutoka kwenye viungo vya mwili na kurudisha kwenye mapafu.

Wakati mwengine ugonjwa wa Anaemia hujulikana kama Upungufu/Ukosefu wa damu mwilini.

Huondoa mgandamizo wa mawazo

Ndizi zina muunganiko wa pekee ambao kitaalam huitwa ‘Tryptophan’ hii ni asidi inayopatikana kwenye protini, ambayo husaidia kwa kutotokea mgandamizo wa mawazo. Virutubisho hivi vikiingia mwilini vinabadirika na kuwa ‘Serotonin’ ambayo hupatikana moja kwa moja kwenye ubongo, huweka misuli sawa na husaidia mtu ajisikie furaha na kuondokana na mawazo.

FAHAMU Mambo 14 Ya Kuzingatia Pale Unapoanzisha Biashara Yako....!!!

0
0

Njia pekee itakuyokusaidia kuingiza kipato cha ziada na kukupeleka kwenye uhuru wa kifedha ni kwa wewe kuamua kuanzisha biashara yako na utakayoamua kuisimamia kikamilifu hadi ikuletee mafanikio.

Ili kuanzisha biashara na ikafika mahali ukaanza kuona matunda ya biashara yako, kwa kawaida huwa ipo misingi au mambo ambayo unatakiwa uzingatie sana ili biashara yako iweze kudumu na kutoa faida uitakayo.

Yafuatayo Ni Mambo Ya Kuzingatia Pale Unapoanzisha Biashara.

 1. Elewa wateja wako wa mwanzo wanataka nini na hapo utapata picha ya jinsi utavyoiendesha biashara na uzingativu juu ya kazi. Ukijua wateja wako wanataka kitu gani, itakusaidia sana kuweza kuwapa huduma hiyo.

2. Kuwa mbunifu,  hilo ndilo jambo kubwa zaidi, biashara ni zilezile ila kinachofanya wateja wakimbilie biashara  yako ni ubunifu wako. Kama usipokuwa mbunifu na ukataka kufanikiwa kibiashara uwe na uhakika utakwama.

3. Lugha nzuri kwa wateja na ukarimu, huweza kumasisha kuongezeka wa wateja wengi katika biashara yako. hakua biashara ambayo italeta mafanikio makubwa kama wewe mwenyewe una lugha mbovu na wateja wako.

4. Epuka kutoa pesa ya mtaji kwa mahitaji binafsi utaua biashara. Hakikisha mahitaji ya biashara na mahitaji yako binafsi unatenga kabisa. ni sumu kubwa sana katika biashara kama eti huwezi kutofautisha matumizi binafsi  na biashara yako. 

5. Jenga utaratibu wa  kufanya tathimi ya biashara yako wapi ulipotokana wapi ulipo na wap unaelekea,? Je, unasonga mbele au unarudi nyuma, ukiona unarudi nyuma jiangalie upya, kujitathimini na ushituke mapema kabla jahazi halijazama.

6. Hifadhi kumbukumbu, hasa matumizi pamoja na mapato hata ya shilingi moja ya sehem ya biashara. Jambo ambalo watu wengi hasa sisi weusi ni ngumu kwetu, na hii ni kila siku unatakiwa kufanya. Huwezi kuendesha biashara na  ikakua bila ‘documentation’. Hutajua ulikotoka, ulipo na unako enda kibiashara.

7. Kujifunza kutoka kwa watu mbalimbali wanaofanya biashara kama yako na kufanikiwa pia usiwapuuze walioshindwa kwani nao wanacho cha kukufundisha. Jifunze kwao kila siku hadi uweze kufanikiwa.

8. Kuhakikisha biashara/duka haliishiwi bidhaa na kama likiishiwa bidhaa maana yake uliowakopesha hawajarudisha, pia jitahidi kuweka mambo, mazingira ya kuvutia wateja. Ukiweka mazingira hayo ujue ni lazima utaweza kufanikiwa kwa kiasi kikubwa.

9. Kujitahidi kuweka aina ya bidhaa ambazo wateja wako watapata kwa urahisi na jamii itakayo kuzunguka. Mteja anapenda sana duka ambalo kila akienda hakosi bidhaa ambayo anaihitaji. Hapo ndipo mahali pake.

10. Jitahidi na jifunze kukubali challenges/changamoto  katika biashara yako na kutafuta njia madhubuti ya kuzimaliza au kuzishughulikia. Ukiwa mtu wa kulia na hutaki changamoto uwe na uhakika hutafika popote.

11. Jitahidi kuangalia mbele kadri unavyona faida inaongezeka, jitahidi kuongeza mtaji na kuzid kupanua biashara, hata kwa kufungua matawi zaidi pengine na kuongeza ubora na ufanisi.

 12. Usafi, ukarimu, kusoma nyakati, utafiti na ubunifu na ni moja pia ya mambo ya kuzingatia. Eneo lako la biashara likiwa safi na ukaongeza na ukarimu ni lazima utawavuta wateja wako katika biashara kwa sehemu kubwa.

Kama unataka kuanzisha biashara na ikakupa faida, hayo ndiyo mambo ya msingi sana unatakiwa kuyazingatia na kuyatilia maanani kwa kiasi kikubwa ili kupata mafanikio makubwa katika biashara yako.
Viewing all 104429 articles
Browse latest View live




Latest Images