Quantcast
Channel: UDAKU SPECIAL
Viewing all 104803 articles
Browse latest View live

Serikali Kuchunguza Kumbi za Starehe

$
0
0
Serikali kupitia Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto imewaagiza viongozi wa Mkoa wa Mara na Wilaya ya Musoma kuchunguza tuhuma zinazohusisha kumbi za starehe wilayani humo kuruhusu watoto walio chini ya miaka 18 kuingia na kutumia vilevi ndani ya kumbi hizo.

Naibu Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Dkt. Faustine Ndugulile ametoa agizo hilo alipotembelea Mkoa wa Mara katika ziara ya kikazi ambapo alipokea malalamiko kutoka kwa wananchi kuhusu kuwepo kwa kumbi za starehe zinazowaruhusu watoto walio chini ya umri wa miaka 18 na kutumia pombe wakiwa ndani ya kumbi hizo.

Dkt. Ndugulile amesema kwamba wamiliki wa kumbi hizo wanakiuka sheria ya mtoto, hivyo wanapaswa kuchukuliwa hatua za kisheria mapema iwezekanavyo ili kuwalinda watoto hato chini ya umri wa miaka 18.

Aidha kwa mujibu wa wa kifungu cha 17 cha Sheria ya Mtoto ya mwaka 2009 kinasema mtu ambaye ni mmiliki au anayeendesha au ni msimamizi wa ukumbi wa muziki, 'Bar', au klabu ya usiku hatamruhusu mtoto kuingia katika maeneno yao.

Katika kifungu imeelezwa  kuwa "mtu atakayekiuka kifungu hiki atakuwa ametenda kosa na atakapotiwa hatiani atalipa faini ya kiasi kisichopungua Shilingi millioni moja na kisichozidi Sh millioni tano au kifungo kisichozidi miezi 12 au vyote kwa pamoja".

Baada ya agizo hilo kutoka wizarani, Mkuu wa Mkoa wa Mara, Bw. Adam Malima amesema ataendelea kuwachukulia hatua wale wote wanaofanya vitendo hivyo pamoja na kupambana na vitendo vya ukatili wa kijinsia, ndoa na mimba za Utotoni ambazo zinashamiri katika mkoa huo.

Pata Tiba ya Tatizo la Nguvu Za Kiume, nasaidia Kukufanya Urudie Mara 5 na kuchelewa kwa Dakika 20

$
0
0

TATIZO LA UPUNGUFU WA NGUVU ZA KIUME NA MAUMBILE MADOGO LINATIBIKA.Baada ya utafiti wa mda mrefu juu ya matatizo ya upungufu wa nguvu za kiume na ukosaji wa hamu ya tendo la ndoa ama kushindwa kurudia tendo kwa haraka DR Magise imekuletea tiba ya matatizo hayo kwa kutumia dawa za: 

GUMBA POWER:Ni dawa asili ya vidonge inayotibu tatizo la upungufu au ukosefu wa nguvu za kiume,dawa hii inamchanganyiko wakutosha wenyekuzalisha vichocheo vingi vya Hemone za Gestrogen vikiwemo vitamin B6&B1,vitamini E,pamoja na madini aina ya zinc vitakufanya kuwa na nguvu na mzunguko mzuri wa damu na kuongeza hamu na uwezo wa kufanya tendo la ndoa zaidi ya hatua nne au zaidi,na kuchelewa kufika kileleni zaidi dakka 20-30. 

NTINJE:Inarutubisha maumbile ya uume yani kurefusha na kunenepesha nchi 4-7 upana cm3-4 standard kiafya haijalishi umri wako hata kwa wazee ukiitumia maumbile yako yatabaki kuwa hivyo siku zote,Pia tunatibu Presha,kisukari siku7,ngiri,chango la tumbo tumbo kujaa gesi,kutopata choo vizuri 

 TUPO TZ DAR ES SALAAM   MBAGALA RANGI TATU.HUDUMA HII UTALETEWA POPOTE ULIPO .WASILIANA NAMI 0754741788, 0715741788, 0783741788 

-DR MAGISE

Kumbi za starehe kuanza kuchunguzwa

$
0
0
Serikali kupitia Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto imewaagiza viongozi wa Mkoa wa Mara na Wilaya ya Musoma kuchunguza tuhuma zinazohusisha kumbi za starehe wilayani humo kuruhusu watoto walio chini ya miaka 18 kuingia na kutumia vilevi ndani ya kumbi hizo.

Naibu Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Dkt. Faustine Ndugulile ametoa agizo hilo alipotembelea Mkoa wa Mara katika ziara ya kikazi ambapo alipokea malalamiko kutoka kwa wananchi kuhusu kuwepo kwa kumbi za starehe zinazowaruhusu watoto walio chini ya umri wa miaka 18 na kutumia pombe wakiwa ndani ya kumbi hizo.

Dkt. Ndugulile amesema kwamba wamiliki wa kumbi hizo wanakiuka sheria ya mtoto, hivyo wanapaswa kuchukuliwa hatua za kisheria mapema iwezekanavyo ili kuwalinda watoto hato chini ya umri wa miaka 18.

Aidha kwa mujibu wa wa kifungu cha 17 cha Sheria ya Mtoto ya mwaka 2009 kinasema mtu ambaye ni mmiliki au anayeendesha au ni msimamizi wa ukumbi wa muziki, 'Bar', au klabu ya usiku hatamruhusu mtoto kuingia katika maeneno yao.

Katika kifungu imeelezwa  kuwa "mtu atakayekiuka kifungu hiki atakuwa ametenda kosa na atakapotiwa hatiani atalipa faini ya kiasi kisichopungua Shilingi millioni moja na kisichozidi Sh millioni tano au kifungo kisichozidi miezi 12 au vyote kwa pamoja".

Baada ya agizo hilo kutoka wizarani, Mkuu wa Mkoa wa Mara, Bw. Adam Malima amesema ataendelea kuwachukulia hatua wale wote wanaofanya vitendo hivyo pamoja na kupambana na vitendo vya ukatili wa kijinsia, ndoa na mimba za Utotoni ambazo zinashamiri katika mkoa huo.

Kijana: Ukipenda Jimama au Mwanamke Mwenye Pesa Uvumilie Vipigo/Kugombezwa Hadharani

$
0
0
Wale vijana wenzangu mnaopenda majimama (kulelewa) mkubali makofi, makonzi sometimes mitama hadharani, pia hata kufokewa hadharani.

Maana wengi wa hawa majimama wana stress za kutosha lakini usisahau ndo yanayowaweka baadhi ya vijana mjini kwa kila kitu, la muhimu ukishagombezwa we jidai kujichekesha tu ili mambo yaishe.

Pia nawasihi sana baadhi vijana tusiwapende hawa majimama tutafute maisha yetu, tusipende maisha ya bure kwani tunaweza kupata madhara mengi ikiwemo magonjwa UKIMWI na kukosa vijana wa kujenga taifa.

Nawasilisha.

HII Ndiyo DNA ya Kitamaduni Kabisa Yenye Ukweli 90% Kujua Kama Mtoto ni Wako Au Umebambikiziwa

$
0
0
Hapo nyuma nilikuwa nikiambiwa kuwa Wazee ni dawa na hazina hasa katika kutupatia Maarifa sisi Vijana na Wajukuu zao nilikuwa sitaki kuamini na kuna wakati hata nilikuwa nikimwona tu Mtu Mzee au Bibi basi nawapuuza tu nikiamini kwamba hawana jipya tena.

Hali hii ilibadilika taratibu baada ya kuanza sasa kupenda kukaa na Wazee mara kwa mara ili niweze kuchota hekima na busara zao na kwa kweli tokea nianze kurudisha imani yangu kwa Wazee naona nimefaidika mno katika kupata Elimu dunia ambayo wengi wetu hatuna na tumebaki tu kujikita katika Elimu zetu hizi za Kitaaluma tukidhani kuwa pekee ndizo zitatukomboa Kifikra.

Pamewahi kuwa na nadharia kwamba akina Babu na Bibi wao huweza kujua Mtoto mchanga aliyezaliwa leo kama ni Mjukuu wao kweli au labda Mtoto wao amebambikiwa huyo Mtoto na Mama yake kutokana na usaliti wake ndani ya Mahusiano yao.

Niliamua kufanya mazugumzo yangu ya Kiudadisi kabisa na Wazee wa Mikoa mbalimbali ili tu niweze kujua kama kuna njia yoyote mbadala ( ukiachia ile ya kufanya DNA ambayo wengi wetu ndiyo tumeizoea ) ya Kiutamaduni ya kuweza kujua kama Mtoto aliyezaliwa na Mpenzi au Mke wangu ni wangu au nimebambikiwa.

Ndugu zanguni wana JF majibu niliyoyapata kutoka kwa hao Wazee wote yalinifanya nizidi kuamini kuwa kumbe tukiwatumia vizuri hawa Wazee bila kuwadhihaki, kuwadharau na kuwapuuza basi wanaweza kuwa sehemu yetu kubwa sana ya kupata maarifa na hata kutatua changamoto zetu zingine za kimaisha ambazo nyingi zimekuja kutokana na mfumo wetu huu wa Kimaisha ulioratibiwa na utandawazi ambao kimsingi umetuharibu na unaendelea kutuharibu.

Leo naweka hapa hadharani jinsi ya Wewe Mwanaume mwenzangu ambaye una Mtoto au hata upo mbioni kumpata Mtoto kuweza kujua kama huyo Mtoto aliyezaliwa ni wako kweli Kibailojia au umebambikiwa tu. Na nitangulize samahani kama kuna ambao nitawakwaza juu ya huu ukweli wa DNA ya Kiutamaduni ila nia yangu ni kuwaokoa tu Wanaume wenzangu juu ya hii kadhia ambayo imesababisha mitafaruku mingi mno katika Mahusiano na Ndoa.

HUU NDIYO UKWELI WA DNA YA KIUTAMADUNI

Ewe Mwanaume mwenzangu uliye na Mtoto hapo ulipo awe bado mdogo au tayari ameshakuwa Mtu mzima chukua mkono wowote uwe wa Kulia au wa Kushoto wa Mtoto unayeamini kabisa kuwa ni wako kisha kwa umakini kabisa huku ukiwa umetulia angalia pale katikati ya mkono ( katika palm ) linganisha ile mistari iliyopo na ya Mwanao kisha ukimaliza linganisha tena mistari iliyopo katika vidole vyake na vya Kwako.

Kwa mujibu wa hawa Mababu na Mabibi ( Wazee ) wanasema kuwa endapo Wewe Baba ukilinganisha hizo alama nilizokuelekeza hapo juu na kuona kuwa hazifanani na zako basi automatically jua ya kwamba huyo Mtoto siyo wako 100% na kwamba Mpenzi wako / Mkeo amekubambikia tu hivyo cha msingi tu ukishajua huu ukweli piga moyo konde, msamehe na maisha yaendelee.

Wamesema kwamba hata iweje Mtoto wako wa damu yako kabisa akizaliwa ni lazima tu alama zilizopo katika Mikono yake zitafanana na Wewe na wala haziongopi. Na ndipo hawa akina Babu na Bibi wakaenda mbele na kusema kuwa hiyo mbinu ndiyo iliweza kuwafanya wao huko nyuma wasiwe wasaliti na wawe wakweli kwani katika Makabila mengi hiyo mbinu ilishasambazwa na iliendelea kutumika. Na ili kulithibitisha hili ndiyo maana Bibi yoyote au Babu akipelekewa Mjukuu akimbeba tu kisirisiri atawahi kuuangalia mkono wa Mjukuu wake na hasa vidole vyake kisha atajua kuwa Mtoto wao kazalisha au kazalishiwa na wenzake.

MWISHO

Andiko langu hili kamwe halina kusudio la kuharibu Mahusiano yoyote yale bali naomba tulitumie tu kama sehemu ya kujipatia maarifa ambayo nina amini wengi wetu ( Vijana na Mabinti ) wa leo tulikuwa hatuna na kama itatokea umekuta umezalishiwa ( umebambikiwa ) basi ninachokuomba tu samehe, piga moyo konde na songa mbele na ule msemo wa Wahenga kuwa siku zote Kitanda hakizai haramu.

Kwa Dada zangu Wapendwa najua huu uzi utawaudhi na kuwauma ila tuvumiliane tu na pengine huu uzi unaweza ukawa msaada mkubwa sana Kwenu hasa katika kuwafanya mbadilike na muache kuwabambikia Wanaume zenu Watoto ambao siyo wao kwani hata Takwimu za mara ya mwisho za Mkemia Mkuu wa Serikali zinasema kuwa 49% ya Wanaume wa Kitanzania wanalea Watoto wasio wao ( wamebambikiwa ) hivyo mtusamehe na mtuonee huruma sisi Wanaume.

Nawasilisha.

BY GENTAMYCINE

OFA!OFA!OFA Je Umepungukiwa Nguvu za Kiume na Umetumia Dawa Bila Mafanikio?

$
0
0

OFA!OFA!OFA je umepungukiwa nguvu za kiume na umetumia dawa bila mafanikio? sasa utapona kwa sh 15000 tu ofa ni kwa watu kumi wakwanza kila siku ofa hii itadumu ndani ya wiki 2 baada ya hapo bei itakuwa nyingine na kama hujapona tunakurudishia hera yako !

Dawa hii ni dawa ya maajabu huwezi kuamini Ila wengi wameiamini, inatibu tatizo la upungufu wa nguvu za kiume na utapewa garantee ya mwezi mmoja dawa hii inapatikana hapo hapo ulipo nyumbani kwako na tutakupatia maelezo ya namna ya kuiandaa wewe mwenyewe na baada ya kuiandaa utakunywa Mara moja tu,na hautatumia dawa yoyote ya nguvu za kiume dawa hii inawafaaa watu kuanzia miaka 18 mpaka miaka 70 zaidi ya miaka hyo haitakusaidia ni dawa ya asilia haina madhara yoyote.

Watafiti na waganga wameikubali pia hii dawa inawafaa hata wanawake wasiopata hisia za mapenzi pia tunaweza kukutumia dawa popote ulipo lakini c kwa bei ya ofa ukiitumia dawa hii unakuwa na uwezo wa kurudia tendo la ndoa zaidi ya Mara 3 bila hamu kuisha na itakufanya uwe na uwezo wa kufanya tendo la ndoa muda wowote imesaidia watu zaidi yawatu 148 ndani ya mwakammoja tangu igunduliwe Dr kiboko mganga wa tiba za jadi toka kisiwani mafia pia tunatibu magonjwa mbalimbali kurudisha mpenzi aliye kuacha,biashara iliyoyumba, kuondoa mikosi, nyota na nk maelezo zaidi

Wasiliana na Dr kiboko 0679923297

Waliopita Hawakuwa Maninja Sasa Ameingia Ninja – Lugola

$
0
0
Waziri wa mambo ya ndani Kagi Lugola amesema kuwa mawaziri wote wa mambo ya ndani waliopita hawakuwa maninja na sasa ameingia Ninja ambaye ndio yeye.

Maneno hayo ameyaongea katika mkutano na waandishi wa habari Jijini Dar Es Salaam wakati akitoa Tathimini ya ziara zake alizozifanya kuanzia Julai 11 2018 katika miongoni mwa taasisi zilizochini ya wizara yake ya Mambo ya ndani.

Wakari anaongea ameweza kuongea mambo kibao likiwemo la kumuagiza mkurugenzi mkuu wa mamlaka ya Vitambulisho vya taifa (NIDA) Andrew Massawe kufika ofisini kwake katika ofisi zake za Dodoma, afike pamoja na mtambo wa kutengenezea Vitambulisho vya taifa.



Lakini pia Waziri Lugola ameweza kutoa tamko la kumwagiza mkuu wa polisi nchini Saimon Siro kumpeleka Lugumi ofisini kwake Mnamo Julai 31 mwaka huu Jijini Dodoma haraka iwezekanavyo.



Waziri Lugola ameongeza kuwa angependa kuona Lugumi anafika ofisini kwake asubuhi pale anaposikia habari hizi “Ntapenda kuona anafika ofisini kwangu agonge mlango ninaposema karibu nikifungua mlango nimkute ni yeye sio lazima mpaka afuatwe na polisi kwa Lugumi ana  familia na anaishi Tanzania”

By Ally Jei.

Habari Zilizopo Katika Magazeti ya Leo Jumatatu ya July 23

$
0
0

Habari Zilizopo Katika Magazeti ya Leo Jumatatu ya July 23

Waziri Kigwangalla Aagiza Ujenzi Wa Viwanda Vidogo Vya Asali Kwa Wilaya Zote Za Mikoa Ya Tabora Na Katavi

$
0
0
Na Hamza Temba – Tabora
…………………………………………………….
*Ahamasisha kilimo cha Korosho kama zao mbadala la kuinua uchumi na uhifadhi wa mazingira

Waziri wa Maliasili na Utalii, Dk Hamisi Kigwangalla ameuagiza Mfuko wa Ruzuku wa Misitu Tanzania (TAFF) kwa kushirikiana na Wakala wa Huduma za Misitu Tanzania (TFS) kuanzisha mradi wa viwanda vidogo vya kusindika na kufungasha asali katika mikoa ya Tabora na Katavi ili kuongeza uzalishaji wa zao hilo na kujenga uchumi wa viwanda.

Ametoa agizo hilo jana kwenye mkutano wa hadhara katika kijiji cha Mtakuja wilaya ya Skonge mkoani humo ikiwa ni muendelezo wa ziara zake mikoani kwa ajili ya kukagua shughuli za uhifadhi na kutatua changamoto zake.

Alisema kwa kiwango kikubwa wananchi wa mikoa hiyo wamekuwa wategemezi kwenye zao moja tu la tumbaku ambalo sio rafiki kwa mazingira kwakuwa miti mingi hukatwa kwa ajili ya kukausha zao hilo jambo ambalo ni muhimu sasa kuwekeza zaidi kwenye mazao mengine ikiwemo viwanda vya kusindika na kufungasha asali ili kuongeza uzalishaji, ubora na hatimaye kuongeza kipato na faida zaidi.

“Mwaka huu ule mfuko wa misitu, kwa kiasi kikubwa tuamue tuwekeze ukanda huu wa magharibi  ambapo kuna zaidi ya asilimia 60 ya misitu yote hapa nchini, na tuanze kwa kujenga kiwanda kimoja katika kila wilaya, ikiwemo Nzega, Skonge, Uyui, Tanganyika, Mlele, Mpanda na Kaliua.

“Tuwawezeshe wananchi wajiunge katika vikundi, tuwagawie mizinga ya kisasa, wafuge nyuki kisasa, warine asali kisasa, wakisharina wapeleke kwenye viwanda, ifungashwe kisasa, ipate bei kubwa, na mwisho wa siku wataona faida ya kuwa na misitu.

“Hapo tutakuwa tumewasaidia, watapa kipato mbadala lakini watakua wakali sana kwa watu wanaoharibu misitu na tutatengeneza jeshi kubwa la wananchi la ulinzi wa misitu yetu, hivyo nataka mradi huu uanze mara moja bila kusuasua ili na sisi tuchangie jitihada za Serikali ya awamu ya tano katika ujenzi wa uchumi wa viwanda. ” alisema Dk. Kigwangalla.

Wakati huo huo, Waziri Kigwangalla amewashauri wananchi wa mikoa hiyo kuanzisha kilimo cha korosho kama zao jingine mbadala la kuongeza kipato na kunusuru misitu badala ya kujikita kwenye zao moja la tumbaku ambalo ni chanzo kikubwa cha uharibifu wa misitu ya mikoa hiyo.

Amesema ni muhimu walau kwa kila kaya moja kuanza kwa kupanda ekari moja ya mikorosho ili kuongeza zao jingine mbadala la biashara ambalo lina tija zaidi kiuchumi na kiuhifadhi wa mazingira.

“Kilimo cha tumbaku sio rafiki kwa mazingira tumejaribu kuleta mabani banifu yanayotumia kuni chache,  tumejaribu kuwashawishi wananchi wapande miti lakini tumechemsha, miti mingi imeendelea kukatwa misitu nayo inateketea siku hadi siku, ni lazima tutafute mbinu mbadala ya kukabiliana na changamoto hii, na hii ni kupitia zao hili la korosho” alisema Dk. Kigwangalla.

Amesema tafiti zinaonyesha kuwa zao la korosho katika mikoa hiyo lina uwezo wa kustawi zaidi na kuzalisha mara mbili kuliko mikoa ya kusini ambayo inasifika zaidi kwa uzalishaji huo hapa nchini.

Aidha ameziagiza halmashauri zote za mikoa hiyo kufanya utaratibu wa kupata mbegu na miche ya zao hilo mapema iwezekanavyo kwa ajili ya kuwagawia wananchi kabla ya msimu wa mvua kuanza na wataalamu wa kilimo wawaelimishe wananchi njia bora ya kupanda na kutunza miche hiyo.

Kwa upande wake Mkuu wa Wilaya ya Skonge, Peres Magiri alisema kiwango cha mvua kwa mwaka katika wilaya hiyo kimeshuka na kufikia 600mm kutokana na mabadiliko ya tabia nchi na uharibifu wa mazingira.

Wanandoa Wakabidhiwa Jukumu la Kusoma Taarifa ya Habari Kwenye Luninga Wakiwa Pamoja

$
0
0
Chombo cha habari cha Citizen nchini Kenya kimewatangaza wanandoa maarufu, Rashid Abdalla na mkewe Lulu Hassan kuanza kusoma taarifa ya habari wakiwa pamoja kila ifikao siku ya Jumamosi na Jumapili.

Rashid ambaye ni mume wa mwana dada Lulu alikuwa mtangazaji wa kituo cha NTV kabla ya kujiunga na Citizen ambapo amekabidhiwa majukumu hayo mapya akiwa sanjari na mkewe kwenye kipindi cha Nipashe Wikendi kinachoruka hewani kila Jumamosi na Jumapili kuanzia tarehe 21 mwezi Julai 2018.



Tukio hili la wanandoa kusoma habari wakiwa pamoja ni kwa mara ya kwanza linatokea nchini Kenya. Rashid Abdalla anachukua nafasi ya Kanze Dena ambaye aliajiriwa na Ikulu ya rais kuwa msemaji mnamo mwezi Juni.

Wakenya wengi wakisubiri kuona ikiwa wapenzi hao wataweza kufanya kazi kwenye osifi moja, huku uongozi wa Nipashe Wikendi wakithibitisha wawili hao kuanza kufanya kazi pamoja Julai 22, 2018.

Madereva 11 wa Mabasi ya Abiria Wauawa

$
0
0

Madereva 11 wa mabasi madogo ya abiria nchini Afrika Kusini wameuawa baada ya kushambuliwa na watu wenye silaha.


Kwa mujibu wa polisi nchini Arika Kusini zinasema kwamba madereva hao kutoka jimbo la Gauteng walikuwa wakitoka kwenye shughuli ya maziko ya dereva mwenzao katika Jimbo la Kwa Zulu Natal kuelekea Jijini Johannesburg siku ya Jumamosi usiku na ndipo waliposhambuliwa.

Chanzo cha shambulio hilo hakijajulikana ingawa inadaiwa kwamba kumekuwa na uhasama miongoni mwa makundi yanayoendesha mabasi nchini humo.

Mabasi madogo ya abiria ni maarufu sana miongoni mwa raia wa nchi hiyo wanaofikia milioni 55 sasa.

BBC

Traffic Anusurika Kipigo Kutoka Kwa Wananchi Baada ya Kusababisha Ajali iliyoua Wawili

$
0
0

Traffic Anusurika Kipigo Kutoka Kwa Wananchi Baada ya Kusababisha Ajali iliyoua Wawili

Tazama Video Hapa Chini:

Hatimaye Rich Mavoko Aachiwa Wimbo Mpya Unaoitwa Happy, Usikilize Hapa

$
0
0
Kutoka WCB, Rich Mavoko anakualika kusikiliza wimbo wake mpya ‘Happy’ aliyegonga mdundo wa ngoma hii ni S2Kizzy. Usikilize hapa chini kisha acha maoni yako.

VIDEO

Hii Hapa Dawa Bora ya Nguvu za Kiume na Maumbile Madogo ya Uume

$
0
0
Tatizo hili limekuwa likiwaadhiri watu wengi sana kisaikolojia hasa baada ya kujiona wapo tofauti sana na wengine kwa kawaida mwanaume anatakiwa awe na uume kuanzia nchi 6-8 kwanza upungufu wa vichocheo hivi huchochea ukuaji wa uume chongo ambalo hushambulia nerve ambayo uharibu kabisa ukuaji wa uume, ngiri, punyeto, ambayo huathili misuli ya uume, ngiri huleta maumivu, tumbo kuunguruma na kujaa gesi, korodani moja kuvimba, kutopata choo vizuri, sababu hizi hufanya uume kulegea na kusinyaa na kuwa mfupi na mwembamba na mara nyingi hata nguvu za kiume ( hamu ya tendo la ndoa) hupungua na kwisha kabisa

GEMBE :Ni dawa inayozalisha na kukufanya uume kukua na kuongezeka
NGEMO : Ni dawa bora ya kuongeza nguvu za kiume

Hukutia hamu ya kuludia tendo la ndoa zaidi mara4 nne bila kukinai au kuchoka pia itakufanya uchelewe kufika kileleni zaidi ya dk30-45 kwa mtumiaji pia tunatibu kisukari, bp, ngiri, miguu kuwaka moto KAMA HUNAMDA WA KUFIKA OFISINI KWETU UTALETEWA POPOTE TUPO MBAGALA RANGI TATU

 0753471612/ 0715249530
0623 386 305

DR KUZENZA

Rais Magufuli na Waziri Mkuu wa Korea Watashuhudia Utiaji Saini Ujenzi wa Daraja Jipya la Selander

$
0
0
Rais Magufuli na Waziri Mkuu wa Korea Watashuhudia Utiaji Saini Ujenzi wa Daraja Jipya la Selander
Rais John Pombe Magufuli na Waziri Mkuu wa Jamuhuri ya Korea Lee Nak-yeon kesho watashuhudia utiaji saini wa mkataba wa ujenzi wa daraja jipya la Selander jijini Dar na njia zake

Ngoma Akimbilia kwa TB Joshua Kufanyiwa Maombi

$
0
0
Ngoma Akimbilia kwa TB Joshua Kufanyiwa Maombi
IMEELEZWA kuwa, mshambuliaji mpya wa Azam FC, Donald Ngoma raia wa Zimbabwe, wikiendi iliyopita alienda kufanyiwa maombi maalum na mchungaji maarufu nchini Nigeria, Temitope Balogun Joshua ‘TB Joshua’

Katika maombi hayo ambayo yaliyofanyika kwenye kanisa la mchungaji huyo nchini Nigeria na kurushwa na runinga yake ijulikanayo kwa jina la Emmanuel TV, Ngoma alionekana akiombewa kwa kushikwa goti lake la mguu wa kulia ambalo limekuwa likimsumbua kwa muda mrefu.

Tatizo hilo la goti limemfanya Ngoma akae nje ya uwanja kwa muda mrefu na sasa anatarajiwa kurudi uwanjani mwezi ujao na kukosa baadhi ya mechi za mwanzo za msimu ujao wa Ligi Kuu Bara.

Ikumbukwe kuwa, Ngoma aliyejiunga na Azam hivi karibuni akitokea Yanga baada ya mkataba wake kuvunjwa kutokana na matatizo hayo ya goti, alipelekwa Afrika Kusini kufanyiwa matibabu ya kina na hivi karibuni anatarajiwa kurudi uwanjani.

Trump Aionya Iran 'Isiijaribu Marekani', Ajibizana na Hassan Rouhani

$
0
0
Trump aionya Iran 'isiijaribu Marekani', ajibizana na Hassan Rouhani
Rais wa Marekani Donald Trump na mwenzake wa Iran Hassan Rouhani wamejibizana vikali na kutoa vitisho huku uhasama baina ya mataifa hayo mawili ukizidi.

Bw Trump ameandika kwenye Twitter, kwa herufi kubwa, kwamba "Iran itapata madhara ambayo ni wachache sana wamewahi kukumbana nayo katika historia" iwapo itaitishia Marekani.

Bw Rouhani awali alikuwa amesema kwmaba vita na Iran vitakuwa "vita zaidi ya vita vingine vyote".

Mwezi Mei, Marekani ilijitoa kutoka kwa mkataba wa nyuklia na Iran ambao ulikuwa umehusisha Iran kusitisa shughuli zake za nyuklia ili iondolewe vikwazo vya kimataifa.

Marekani sasa imeanza kuiwekea tena Iran vikwazo licha ya pingamizi kutoka kwa Uingereza, Ufaransa, China, Urusi na Ujerumani wote ambao walikuwa wadau katika mkataba huo wa mwaka 2015.

Kesi Aishtukia Yanga Asema Hawatampata

$
0
0
Kesi Aishtukia Yanga Asema Hawatampata
BEKI wa pembeni wa Yanga, Hassan Kessy ameshtukia mtego unaofanywa na viongozi wa timu hiyo na kutamka kuwa kamwe hawatampata baada ya kuwashtukia.

Kessy ni kati ya wachezaji waliomaliza mikataba ya kuendelea kuichezea timu hiyo mwishoni mwa msimu huu na kuanza mazungumzo ya kuichezea timu hiyo.



Beki huyo hivi karibuni ilielezwa kutimkia Klabu ya Nkana FC ya nchini Zambia katika msimu ujao baada ya kutakiwa na timu hiyo.

Akizungumza na Championi Jumatatu, Kessy alisema ujanja wanaotaka kuufanya viongozi wa timu hiyo ni kutaka kumfanyia usajili dakika za mwisho kabla ya dirisha kufungwa ikiwa ni kwa dau dogo wakiamini hatakuwa na sehemu ya kwenda.



“Ujanja wanaotaka kuufanya viongozi nimeshaushtukia wa kutaka kunikurupusha kusaini ikiwa ni siku chache baada ya usajili kufungwa kwa dau wanalolitaka wao.

“Mimi nitasaini Yanga kwa dau ninalolitaka ambalo tayari nimewapatia kama hawatakuwa tayari kunipa hiyo hela basi, nitaondoka zangu kwingine ikiwezekana hata kurudi Mtibwa Sugar,” alisema Kessy.

Gabo Amefanikiwa Kuziba Pengo La Kanumba- Mama Kanumba

$
0
0
Gabo Amefanikiwa Kuziba Pengo La Kanumba- Mama Kanumba
Mama mzazi wa aliyekuwa staa wa Bongo movie Steven Kanumba, Flora Mtegoa maarufu kama Mama Kanumba amemtaja msanii ambaye anaamini ameziba pengo la Kanumba Kwenye tasnia ya Bongo movie.

Mama Kanumba ambaye naye aliingia Kwenye Bongo Movie mara baada ya mwanaye kufa amemtaja Gabo Zigamba kama Msanii ambaye ameziba pengo la Kanumba.

Kwenye mahojiano  na Wasafi TV, Mama Kanumba amemtaja Muigizaji wa Kiume Gabo Zigamba kama ndiye msanii pekee mwenye uwezo sawa na Kanumba kwa sasa.

Gabo anajitahidi kwa kweli, nilichogundua kwanza anajua kuuvaa uhusika kwenye filamu zake, akiwa kama mlinzi anakuwa mlinzi kweli, akiwa kichaa anakuwa kichaa kweli. Namwambia asikate tamaa kuna watu watamkatisha tamaa kila atapokaribia kuyafikia mafanikio zaidi.”

Lakini pia Mama Kanumba amelinganisha uwezo wa Kanumba na Gabo:

Ni kweli Gabo ‘anashika kijiti cha Kanumba’ anajitahidi, anauthubutu, anajaribu, anajituma na anaweza”.

NEC: Wagombea 30 wa CCM Wamepita Bila Kupingwa

$
0
0
NEC: Wagombea 30 wa CCM Wamepita Bila Kupingwa
Wagombea 30 wa Udiwani katika uchaguzi Mdogo wa kata 77 utakaofanyika Agosti 12 mwaka huu, wamepita bila kupingwa.

Akizungumza Jijini Dar es Salaam Mkurugenzi wa Uchaguzi wa Tume ya Taifa ya Uchaguzi (NEC), Dkt. Athumani Kihamia amesema kuwa wagombea hao wamepita bila kupingwa baada ya Tume kukutana, kujadili na kuyatolea maamuzi mapingamizi mbalimbali yaliyoweka na wagombea wa udiwani.

 Amesema Madiwani wote waliopita bila kupingwa wanatoka Chama cha Mapindizi (CCM) na kuongeza kuwa rufaa zilipokelewa na kujadiliwa kwa kuzingatia matakwa ya kifungu cha 44(5) cha Sheria ya Uchaguzi ya Serikali za Mitaa, Sura ya 292, kikisomwa pamoja na Kanuni ya 28(1)(2) ya Kanuni za Uchaguzi wa Serikali za Mitaa (Uchaguzi wa Madiwani) za mwaka 2015.

“Tume, ilipokea, ilijadili na kufanya maamuzi ya Rufaa 25 ambapo jumla ya wagombea kumi (10) walifanikiwa na hivyo kuendelea na uchaguzi na wagombea 15 rufaa zao hazikufanikiwa na hivyo kutoendelea kuwa wagombea,” amesema Dkt. Kihamia.

Ameongeza kuwa katika kata sabini na saba (77) wanachama 254 kutoka vyama kumi na moja (11) vya siasa walichukua fomu za uteuzi na kwamba jumla ya wanachama 186 sawa na asilimia 73.2 ya waliochukua fomu za uteuzi walizirejesha na kuteuliwa kuwa wagombea ambapo kati yao wagombea 179 sawa na asilimia 96.2 ni wanaume na wagombea 7 sawa na asilimia 3.8  ni wanawake.

“Hadi muda wa mwisho wa uteuzi ulipofika (saa 10.00 jioni siku ya uteuzi)  wanachama 68 sawa na asilimia 26.8 ya waliochukua fomu hawakuteuliwa kutokana na sababu mbalimbali zikiwemo kutorudisha fomu, kurudisha fomu nje ya muda unaokubalika kisheria na fomu kutojazwa ipasavyo,” amesema.

Dkt. Kihamia amefafanua kuwa katika uchaguzi huu mdogo wa madiwani utakaofanyika Agosti 12 mwaka huu jumla ya vyama kumi na moja (11) vimesimamisha wagombea.

Amewataja Wagombea hao katika Kata kwa kila Chama kuwa ni ACT-Wazalendo Wagombea 17 (sawa na asilimia 22), ADC Wagombea 3 (sawa na asilimia 3.9), CCM Wagombea 77 (sawa na asilimia 100) CHADEMA Wagombea 54 (sawa na asilimia 70), CHAUMMA Wagombea 2 (sawa na asilimia 2.6), CUF Wagombea 17 (sawa na asilimia 22), Demokrasia Makini Wagombea 4 (sawa na asilimia 5.2), NCCR-MAGEUZI Wagombea 6 (sawa na asilimia 8), NRA Wagombea 3 (sawa na asilimia 3.9), SAU Mgombea 1 (sawa na asilimia 1) na UPDP Wagombea 2 (sawa na asilimia 2.6).

Wakati huohuo, Dkt. Kihamia amesema kwamba katika jimbo la Buyungu jumla ya wanachama kumi (10) kutoka vyama kumi (10) vya siasa vya AAFP, ACT-Wazalendo, CCM, CHADEMA, CUF, DP, Demokrasia Makini, NRA, UMD na UPDP walichukua fomu za uteuzi.

 “Wanachama wote kutoka vyama hivyo walirejesha fomu na kuteuliwa kuwa wagombea wa Ubunge katika Jimbo hilo, kati yao wanaume ni tisa (9) na mwanamke mmoja (1),” amesema Dkt. Kihamia.

Amevitaka vyama vya siasa na wagombea wao kuzingatia maadili ya uchaguzi wa Rais, Wabunge na Madiwani ya Mwaka 2015, wakati wote wa kampeni na siku ya uchaguzi.
Viewing all 104803 articles
Browse latest View live


Latest Images