Quantcast
Channel: UDAKU SPECIAL
Viewing all 104789 articles
Browse latest View live

Baada ya Flora Kumkimbia...Mbasha Adai Hana Hamu na Ndoa Tena

$
0
0
BAADA ya hivi karibuni aliyekuwa mkewe, Flora Mbasha kuolewa na mwanaume mwingine, Mwimbaji wa Injili, Emmanuel Mbasha amefunguka kuwa hana hamu na ndoa hivyo hawezi kuwa na haraka ya kuwa na mke kwa sasa kwani anahofi a kupata mwanamke msaliti tena.

Akipiga stori na Star Mix, Mbasha alisema kutokana na changamoto kubwa aliyoipata kwenye ndoa, kila mwanamke anayemuona anamuogopa kwa kuwa ameshaumizwa kwa hiyo kwa wakati huu ameelekeza nguvu zake kwenye kazi.

“Unajua ukishaumwa na nyoka hata jani likikugusa unaogopa hivyo sina haraka ya kuoa kwa sasa, bado nipo namuomba Mungu akinionyesha nitaoa na kama haijampendeza basi nitabaki hivihivi,” alisema Mbasha.

Kafulila Atema Nyongo Baada ya Prof Muhongo Kutumbuliwa na JPM Sakata la Mchanga

$
0
0
Aliyewahi kuwa Mbunge wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Ndugu David Kafulila ameibuka na kutoa ya moyoni baada ya maamuzi yaliyofanywa na Rais Magufuli baada ya kupokea ripoti ya Kamati Maalum kuhusiana na uchunguzi wa makontena 272 ya makinikia yaliyokuwa  tayari kwa kusafirishwa nje ya nchi .

Kupitia ukurasa wake wa Facebook, Kafulila ameandika yafuatayo,

1 Naipongeza Kamati kwa kazi iliyotukuka iliyojaa majaribu ya rushwa kubwa kwani kampuni nyingi madini, mafuta na gas duniani zina sifa hiyo kama alivyopata kusisitiza Profesa Joseph Stirglitz gwiji la uchumi na utandawazi duniani.

2 Zaidi hatua aliyo chukua Rais kuhusu uharamia huu katika sekta ya madini inapaswa kuungwa mkono na kila mzalendo kwani imekuwa hoja ya upinzani na kila mzalendo kwa miaka mingi iliyoishia kubezwa na kupuuzwa.

3 Rais asiishie kutaka uchunguzi kufanywa dhidi ya watumishi katika sekta ya madini tu, nchi hii imeoza, uchunguzi ufanywe mpaka ndani ya Idara ya Usalama na vyombo kama TAKUKURU kwani mafisadi hawa waliweka mfumo mzima mfukoni kwa kujenga mahusiano na baadhi ya wanausalama na vyombo vingine vyeti kiuchunguzi.

4 Namshauri Rais aboreshe Idara ya Usalama kwa kuwa na kitengo cha ujasusi wa kiuchumi (Economic Intelligency) kitakachoweza kumudu kukabiliana na uharamia ktk utoroshaji utajiri wa nchi (illicits flows) kwani nchi inavuja kwa miaka mingi na mtandao wa uharamia huu uliweka sehemu kubwa ya mfumo mfukoni.

5 Kuna haja yakutazama Katiba yetu upya ili ikibainika hata Rais kama alihusika na ufisadi afikishwe kwenye mkondo wa sheria kwani nchi nyingi za Africa zimeoza kwa ufisadi kuanzia Ofisi Kuu, huko ndio vinatoka VIMEMO kuruhusu uharamia wa namna hii. Ni Ushauri wangu kwa Rais aruhusu mchakato wa Katiba ili pamoja na mambo mengine tuangalie mfumo wa Ofisi Kuu kama moja ya chanzo cha uozo na uharamia huu.

6 Ni vema Mheshimiwa Rais akatambua kwamba kampuni hizi za kimataifa zinaiba duniani kote ikiwemo Ulaya na Marekani, isipokuwa huku kwetu zinaiba zaidi kutokana na sera duni, sheria dhaifu, mifumo ya usimamizi dhaifu na udhaifu wa wanaopewa nafasi kwa ujumla. Kukabili tatizo hili lazima kutazama kwa mapana na kutengeneza mfumo madhubuti.

7 Mwisho nimshauri Rais kwamba pamoja na kuchukua hatua hizi za kisheria za ndani, azifikishe kampuni hizi kwenye Mahakama za Kimataifa (Arbitration court) kama inavyo tamkwa kwenye mikataba ili kuzidai fidia kwa miaka yote ya Mikataba yao.

8 Mitambo na mali zao zishikiliwe mpaka kesi itapomalizika. Na hili lisisomeke kwamba nikukimbiza wawekezaji bali nikukabili uharamia wa utoroshaji rasilimali ambao hata sheria zakimataifa zinapiga vita. Hili ni muhimu sana. Umma una paswa kusimama pamoja dhidi ya uharamia huu!

Mose Iyobo ‘Amchimba biti’ Aunt Ezekiel Kulala Kambi

$
0
0

Ni kawaida kwa wasanii movie kuweka kambi kwa ajili ya maandalizi ya kushoot filamu zao, sasa mpenzi wa malkia wa filamu Aunt Ezekiel,  Mose Iyobo amempiga marufuku mrembo huyo kulala kambini kisa wivu wa kimapenzi.


Mose Iyobo ameimbia show ya XXL kuwa mwanzoni suala hilo lilikuwa linamuumiza kwa sababu walikuwa wanakutana mara chache sana.

“Lakini tulipokubaliana yeye ni Mama na mimi ni Baba vitu vya kambini vikaisha, kama ni kushoot hakikisha unarudi nyumbani sio kulala huko huko. Nyumba ipo ukalale kambini kwa kisingizio gani  na haushoot alfajiri, bali ni mchana kwa nini usilale nyumbani uamke asubuhi ndio uende,  mimi sitaki mambo ya kulala kambini, basi alinielewa tu… ni vivu wa mapenzi na wasiwasi siunajua ndio akili,” ameeleza Mose Iyobo.

Soma Nafasi za Kazi Zilizotangazwa Leo

$
0
0

Inaumiza Sana Kuona Yanayoendelea Mitandaoni Juu ya Zari na Kifo cha Ivan

$
0
0

UKWELI WATANZANIA MITANDAO IMETUPELEKA MBALI NA KUSAHAU HATA UTU WETU NA KUFIKIA HATUA YA KUONA MAISHA YA MTANDAO NDIO KILA KITU.PIA INAWEZEKANA WENGI WETU KWA KUWA MAISHA YANAYOENDELEA WATU HAWAYAJUI NDIO MANA INAKUWA RAHISI KWETU KUWANYOSHEA VIDOLE WALE AMBAO MAISHA YAO YAKO WAZI ILA TUSIJISAHAU HATA KAMA MAISHA YAKO NI YA SIRI MUNGU ANAWEZA KUKUFICHUA.

Najaribu kwa muda kuuvaa u zari nione anapoingia mitandaoni anayokutana nayo anajisikiaje ila naona ni mazito kwake sema hawezi yazungumza.Ila kinachoumiza zaidi ni pale ambapo hata mwili wa marehemu haujazikwa wa Tanzania tushaanza kuitawala mitandao kwa msiba huu kama vile sisi ni waganda au watu wa afrika kusini.Yani mtu sasa hivi anakaa anawaza atunge uongo gani auandike kuhusu @zarithebosslady na familia yake ili page yake ipate uhai mwisho wa siku mtu anaandika vitu ambavyo ukisoma unaweza hisi ni shetani ameandika ujumbe ule na sio binadamu.
Ila eti ukiwauliza watu wanaofanya hivyo utakuta chuki zao zimeanzia pale ambapo @zarithebosslady aliingia kwenye mahusiano na @diamondplatnumz sasa ndio unakuta mtu bado anatumia kumchafua kwenye msiba huu kama njia ya kulipiza.

Kinachonisikitisha zaidi hata yule ambaye wa Tanzania wamemuamini kuwa mtetezi wa haki za watu @mangekimambi_ leo naye anasimama na kuandika vitu vya kupotosha watu tena kipindi hiki cha msiba na at the same time ukiuliza kwanini anafanya hivyo ni muunganiko wa chuki zile zile za diamond kuwa na zari ndio inapelekea mtu kukosa utu.

This is sad very sad kwa wa Tanzania leo @ivandon aliyekuwa na mali nyingi amefariki leo wewe ambaye una hako kasimu kako ka kuingia insta unajisahau na kushadadia misiba kama utaishi milele aisee.

Nadhani ingekuwa busara sana watu wakaacha familia ikamaliza mambo yao mana nahisi pia hizi page zinazozusha ujinga soon baada ya msiba zitadhalilika maana yale wanayopigia kelele kumzalilisha zari yatamalizwa kifamilia.
IFIKE HATUA TUJITAMBUE KUWA SWALA LA MSIBA LINAWEZA KUMPATA KILA MTU NA MATATIZO YA KIFAMILIA YANAMPATA KILA MTU .

HII NI MITANDAO TU ISIKUTOE UFAHAMU SABABU YA USHABIKI MAANDAZI WA TEAM KUMBUKA UTU WAKO.. UJUMBE KUTOKA KWA .

Ben Pol Huo ni Ushamba na Umejidhalilisha! Wabongo si Watu wa Utupu

$
0
0
 


BENARD Paul ndilo jina lake halisi, lakini mashabiki wanamfahamu zaidi kama Ben Pol, yule kijana mweusi, mrefu ambaye nyuma ya kipaza sauti, anafanya vizuri katika Muziki wa Kizazi Kipya, akiwa amejizatiti zaidi katika R&B. Ana sauti nzuri na kwa kweli anaimba vizuri, licha ya baadhi ya nyakati kudaiwa kuwa anakopi na kupesti nyimbo za nje, kitu ambacho naye amekuwa akikanusha mara kadhaa.

Ana nyimbo nyingi, lakini katika ushirika wake na rapa Darassa, ameunogesha kwa kiwango cha kutosha ule Wimbo wa Muziki.

Hawezi kuwa top katika aina hiyo ya muziki, lakini huwezi pia kumshusha kivile, maana anajua nini anafanya. Nikiri, sijawahi kukutana na huyu dogo, lakini ni mfuatiliaji mzuri wa kazi zake na mara kadhaa, nimewahi kuongea naye kuhusu masuala mbalimbali ya kikazi.



Anazungumza vizuri, kitu kinachonifanya nimtabirie kama muungwana. Juzikati nilimsikia Katibu Mtendaji wa Baraza la Sanaa Tanzania (Basata), Godfrey Mngereza akilaani picha za utupu za msanii huyo alizotupia katika akaunti yake Instagram na kusababisha kizaazaa kwa mashabiki, wengi wakimponda na wachache wakimtetea. Mngereza aliwataka wasanii kufanya kazi nzuri ambazo zinaweza kuwaweka sehemu nzuri na siyo kutengeneza mazingira ambayo yanautia dosari muziki wao. Alitumia fursa hiyo kusisitiza umuhimu wa kuzingatia utamaduni wetu, licha ya kusema kabla ya kuchukua hatua, watamuita na kumsikiliza.

Lakini pengine kwa kuzidiwa  na mashambulizi, kijana huyo mwimbaji wa Kibao cha Phone, alijitokeza tena na kutoa ‘clip’ ya video ikimuonyesha akiwa mtupu huku akiimba na kusindikiza na maneno ya kuwaambia watu kuwa wasijaribu kutoa hukumu kwa kitabu ambacho bado hawajasoma.



Ujumbe wake kwa mashabiki ni kuwa walipaswa kujua nini maana ya yeye kuweka picha ile, kwani alikuwa anawawekatayari mashabiki zake kwa ujio wake mpya wa video ya wimbo uitwao Tatu.

Baada ya ufafanuzi huo, kuna baadhi wamekubaliana naye na wengine wameendelea kumponda. Mimi sikubaliani naye na wala simpondi, isipokuwa ninachotaka ni kumpa somo kama mdogo wangu, kama shabiki wa muziki wake mzuri na pia kama mdau. Ben Pol kwa nafasi yake, ni kama balozi wa ndani mwenye wajibu wa kuhakikisha taifa halipotoki kimaadili, hasa vijana wanapohusika.

Ninajua wasanii hivi sasa wako katika vita kubwa ya kujaribu kuwa na ubunifu ili kuweza kutangaza kazi zao zipate kukubalika kitaifa na kimataifa, lakini ni makosa makubwa kufanya ubunifu unaopingana na utamaduni wako.

Wabongo si watu wa uchiuchi, ndiyo maana kila siku tunawapigia kelele wadada wa Bongo Muvi, tunawaambia kuwa kwao nusu utupu hakuwafanyi wauze kazi zao, zaidi kunawadhalilisha, kwani mashabiki wanataka simulizi nzuri, zenye mafunzo kwao na zinazowakilisha utamaduni halisi wa Mtanzania. Hata kama nia yake ilikuwa nzuri kiasi gani, ni jambo la fedheha kijana wa kiume kupiga picha za video ukiwa mtupu.

Ili iweje sasa? Haya tuseme huo wimbo wake wa Tatu, hivi ni kweli mawazo yake yote yaliishia kwenye utupu? Hapana, huu ni ufinyu wa utambuzi wa mambo. Tatizo moja la msingi kwa vijana wetu ni kule kutaka kwao kuleta Umarekani katika kila jambo. Walianza kusuka nywele, wakaja kutoboa pua, wakavalia suruali zao katikati ya makalio na sasa wanataka kuwa uchi kabisa. Tuache ushamba huu, hasa nyinyi ambao mnapaswa kuwa mstari wa mbele katika kutuongoza. Kama tutatukuza utamaduni wa watu, ni lini watu wataufahamu wa kwetu? Au ulitaka kuwaonyesha watu jinsi ulivyobarikiwa umbo zuri lenye mvuto? Hakika umejidhalilisha!

NA OJUKU ABRAHAM,

Wolper Atokwa na Povu Baada ya Kubanwa Kuhusiana na Madai ya Kunuka Mwili

$
0
0
Staa wa filamu ‘grade one,’ ‘Jacqueline Wolper’ ametokwa povu si la nchi hii baada ya kubanwa kuhusiana na madai ya kunuka mwili na kusema hajawahi kunuka maishani mwake na kwamba ingekuwa hivyo asingepapatikiwa na wanaume.

Hivi karibuni Ijumaa lilimfungia kazi msanii huyo nyumbani kwake na katika moja ya maswali aliyobanwa lilikuwa juu ya ishu iliyosambaa kuwa eti anatoa harufu mbaya sehemu za mwili wake.

Katika kuonesha kumaindi ile mbaya kuhusu madaia hayo, mrembo huyo ambaye kiukweli yuko bomba kwa muonekano alifunguka: “Aliyekuambia nanuka nani? Mimi sinuki wala sijawahi kunuka maishani mwangu, kuthibitisha hilo kwanza nisingekuwa napapatikiwa na wanaume kila kukicha sambamba na kuhongwa vitu kibao huku wengine nikiwaacha wakinililia.


Hao wanaosema na kusambaza hayo ni njia tu ya kujipatia followers kwenye mitandao yao kupitia mimi.” Wolper hakuishia hapo aliendelea kumwaga povu kuwa, tangu afungue duka la nguo ambalo amewekeza zaidi ya shilingi milioni 60, watu wengi wamekuwa wakichukizwa na maendeleo hayo. “Wana chuki tu na mimi, tangu nimefungua duka wananichokonoa, wanalishadadia hili jambo kisa tu nimepata mafanikio ya kufungua duka,” alipigilia msumari.

JE Dada Unapenda Kuwa Mrembo? Na Kaka Unapenda Kuwa Mtanashati na Kurudisha Heshima ya Ndoa?

$
0
0
JE, DADA UNAPENDA KUWA MREMBO? NA KAKA UNAPENDA KUWA MTANASHATI NA KURUDISHA HESHIMA YA NDOA? Tumia Bidhaa halisi za MARKSON kwa mafanikio ya uhakika na bila madhara. 
Zimetengenezwa kwa mimea na matunda na kuthibitishwa kiafya. 
🍉🌿🍓🍒🎄🍍🍀🍓🍉
Pata hizi 👇👇👇👇👇👇

1. kurefusha nywele na kuzuia kukatika ovyo @120,000/=
2. Kuongeza shepu (hips, makalio na mapaja) kwa (a)BOTCHO MULT-PLUS 10× @200,000/=
(b)Vidonge @180,000/=
3. Kuwa mweupe na softi mwili mzima kwa:- (1)Mafuta @120,000/=
(11)Vidonge @150,000/=
4. Kupunguza unene na manyama uzembe @150,000/=
5. Kuongeza uume pamoja na nguvu za kiume kwa :- 
(a) Gely ya kupaka @130,000/= 
(b) Vidonge kwa ajili ya kuongeza nguvu hata kwa wenye kisukari @130,000/= (c)Handsome up (mashine) original @200,000/=
6. Kuondoa mvi milele zisiludi tena @120,000/=
7. Kuongeza unene wa mwili mzima na uzito pamoja na hamu ya kula @120,000/=
8. Kupunguza tumbo (kitambi) na nyama za pembeni kwa:-
(a) Dawa ya kunywa au kupaka @120,000/= 
(b)Mkanda wa kawaida @100,000/= 
(c)Mkanda wa umeme @200,000/=
9 .Kupunguza maziwa na kuyasimamisha hata kwa walionyonyesha @120,000/=
10.Kushepu miguu na kuwa minene na kuondoa migimbi @120,000/=
11.Kuondoa mipasuko mwilini (michirizi) @100,000/=
12.Kubana uke na kuongeza hamu ya tendo la ndoa kwa mwanamke @120,000/= 

NB: Hakikisha unapata risiti yenye muhuri halisi wa MARKSON CO pamoja na garantii ili kukuhakikishia kufanikiwa kwako. 
Wasiliana nasi :-
(+255) 0767447444 na
0714335378
👉🏻Ili kuona bidhaa zetu na baadhi ya shuhuda za waliotumia bidhaa zetu

Papa Francis Amwambia Trump Kuwa Aache Kula Pizza Nyingi Zinamfanya Awe Kibonge..!!!

$
0
0

BENDERA pekee ya Marekani ilionekana jana ikipepea kwenye lango la kuingilia kwenye kasri la Papa Francis lililoko jijini hapa, wakati Rais wa Taifa hilo kubwa, Donald Trump alipowasili ikiwa ni siku yake ya tatu kutembelea vyanzo vya dini kubwa duniani.

Trump alikutana na Papa Francis katika siku yake ya tano ya ziara yake ya kwanza ya urais, baada ya kutembelea vyanzo vya dini za Uislamu na Uyahudi.

Wakati mazungumzo yao yakibaki siri, Rais huyo alikuwa na ujumbe mfupi kwa ajili ya Francis wakati akiondoka: “Sitasahau ulichokisema.

“Ni heshima kubwa,” alisema wakati akishika mkono wa Papa nao kupiga picha ya pamoja kwenye ghorofa ya pili ya Sala del Tronetto, ambacho ni chumba kidogo cha Utawala.

“Ahsante sana. Hii ni heshima kubwa sana,” Trump alisikika baadaye akisema wakati Francis amekaa upande wa pili wa dawati wakitazamana tayari kuanza mazungumzo yao, kwenye chumba chake cha faragha cha kujisomea.

Francis ambaye ni mtu asiyependa kufichaficha mambo, lakini wakati wote huo alikaa kimya.

Baada ya kutoka kwenye mazungumzo yao, Francis alionekana muda wote akitabasamu kila alipokutana na wana familia hiyo namba moja ya Marekani.

“Unampa chakula gani?” Francis alimhoji Melania Trump kwa Kiitaliano, akimaanisha jinsi Rais alivyo na umbo kubwa. “Pizza nyingi?”  “Pizza!?” Melania aliuliza kwa mshangao huku akicheka.

Papa alibusu Rosari aliyokuwa nayo Melania mkononi, kabla ya kumsalimia Ivanka Trump na mumewe, Jared Kushner, sambamba na Waziri wa Mambo ya Nje, Rex Tillerson na maofisa wengine wa Marekani.

Baada ya mkutano na Papa, Melania alizuru hospitali ya watoto inayomilikiwa na Vatican. Alimwambia Francis: “Nimefarijika sana kutembelea hospitali hii ya watoto wachanga”.

Ziara ya Ivanka ilijumuisha pia kukutana na waathirika wa biashara ya binadamu na kuandaa mijadala mbalimbali na wanachama wa Jumuiya ya Sant’Egidio, kikundi cha kijamii cha kutetea haki cha Kanisa Katoliki.

Familia ya Trump ilikuja na zawadi mbili kwa ajili ya Papa, ikiwa ni pamoja na kasha la toleo la kwanza la vitabu vya Mchungaji Martin Luther King, Jr. “Nadhani utavifurahia,” alisema Trump.

Rais pia alimpa sanamu ya shaba nyeusi yenye maandishi ya ‘Panda Juu’, ikiwa na umbo la yungiyungi lililochanua.

Francis naye alijibu kwa kumpa medali kubwa iliyosanifiwa na msanii wa Kiroma – taswira ya mti wa mzeituni, kama alama ya amani.

“Tunaweza kutumia amani,” Trump alijibu. “Nimeisaini maalumu kwa ajili yako,” Francis alimwambia. “Ooh,” Trump alijibu. “Hiyo nzuri sana.”

Rais pia aliahidi kusoma nakala tatu za Waraka wa Baba Mtakatifu alizopewa na Francis – mojawapo ni ‘Lautado si’ yake, ambayo ni tasnifu inayozungumzia hifadhi ya mazingira. Zingine mbili zinahusu familia na Injili.

Ushauri kwa Tundu Lisu Juu ya Makontena ya ACACIA...!!!

$
0
0

*Ushauri kwa _Tundu Lisu_*

Ukiwa Kama mwanasheria mashuhuri nakuomba ulisaidie Taifa na hawa mapepari na majizi ya rasilimali zetu wanaojiandaa kwenda kulishitaki Taifa letu kwenye Mahakama za kimataifa kisa tu Taifa limechukua hatua kwa namna tunavyoibiwa rasilimali zetu na hao mapepari wanatumia mgongo wa sheria tena walizotunga wao na zinabeba hao hao kuendelea kutunyonya kwa kigezo cha Mahakama za kimataifa. 

Ni kweli kutokana na sheria za kimataifa zilivyokaa ikitokea ACACIA wakaenda mahakamani Taifa litawalipa fidia kubwa sana, pesa ambazo ni kodi za sisi wananchi wa hali za chini. Ifahamike kuwa hawa wawekezaji wanatuibua kwa kutorosha rasilimali zetu wakijua mwisho wa siku kuna sheria za kimataifa zilizotungwa na hao hao zitawatetea tena. Kwa lengo la kizalendo nakuomba Tundu Lisu Ukiwa Kama Rais wa TLS na pia Mtanzania mwenzetu andaa timu yako ya wanasheria mahili (Akina Malya, Mabere Malando, Chenge) na wengine wengi kuhakikisha mnaenda kupambana nao huko kwenye Mahakama zao wanakopanga kwenda kulishitaki Taifa. 

Kwa hili la rasilimali zetu tuweke uvyama pembeni tuungane kumuunga mkono Mh Raisi kwa hatua alizochukua. Ni kweli kabisa bado Kuna changamoto nyingi kwenye uwekezani wa rasilimali zetu haswa katika upande wa mikataba na sheria mbovu zinazosimamia hiyo mikataba iliyosainiwa na viongozi wetu ambao pia ni Watanzania wenzetu (wengine bado wapo madarakani eg. Akina Chenge kipindi hicho akiwa mwanasheria mkuu wa Serikali) . 

Hivyo basi kwa hatua za awali hawa wanaojiita wawekezaji tukiwashinda kwa hili la mchanga hayo mengine ya mikataba kwa uwezo wa Mwenyezi Mungu siku moja pia tutayafikia tu. 

*UKWELI HUWA UNA ASILI YA KUUMIZA, ILA KWA HILI LA RASILIMALI ZETU TUSIMAME UPANDE WA UKWELI*

Chanzo jf

Mheshimiwa Rais, Umechuma Janga. Gwajima Sio DUDE Ila George H.W. Bush ni DUDE..!!!

$
0
0

Mchuma janga hula na wakwao! Na tutakula wote tu, hamna ujanja.
Sasa kwakuwa umechokoza li dege lililotulia, sasa na wewe utulie tuli usikie sauti yake.

George H.W Bush anahusikaje na Acacia?

Nov.27,2014 Cecilia Jamasmie anaandika ,'African Barrick imebaki historia, imebadili jina kuwa Acacia mining.'
Moja kati ya malengo yake ilikuwa kuendeleza kazi zake North Mara na kuzalisha ounce 450,000 ndani ya miaka mitano kwa gharama ya chini ya dola 750 kwa ounce.

Jan.03,1997 Anton Chaitkin anaandika Inside story juu ya genge la Bush na Barrick Gold Corporation. Anasema;
☆ Barrick Gold ni shirika linalojihusisha na mikakati ya siri katika siasa za George H W Bush.
☆ Shirika hili lenye makao yake Canada ndio biashara pekee ya Bush iliyofahamika wakati huo.
☆ Shirika hili lilianzishwa na marafiki wa kisiasa wa Bush, Wawezeshaji wakubwa wa biashara za madawa ya kulevya, wafanyabiashara haramu wa silaha na watakatishaji wa fedha.
☆ Shirika ni kubwa, liko USA, Canada, South America: Argentina, Chile, Peru, Bolivia na Brazil. Lipo pia Africa.

Majina makubwa kwenye shirika ni ya kina nani?

1. George Herbert Walker Bush 
♨Baba yake alikuwa partner kwenye taasisi binafsi kubwa na yenye nguvu, ya kibenki - Brown Brothers Harriman.
♨Bush alikuwa makamu wa rais na chief kwenye operations za siri katika utawala wa Reagan (1981-89).
♨Bush alikuwa rais wa Marekani (1989-93).
♨Bush alikuwa chief lobbyist wa Barrick, mwanahisa na mshauri mkubwa wa heshima wa bodi ya kimataifa ya washauri wa Barrick.

2. Adnan Khashogi.
♨ Billionea wa saudi na mfanyabiashara haramu ya silaha .
♨Muanzilishi wa Barrick Gold Corp.
♨Maarufu sana kwa biashara yake haramu ya kuiuzia Iran silaha.

3. Peter Munk na 4. Brian Mulroney ; hawa ntawaacha kwa sasa.

Hili ni janga kwasababu kwao Magufuli hatoshi hata kwa breakfast;
Angalia hapa chini!

$ Uwekezaji mkubwa katika shirika ulifanywa na Khashogi na mapartner wake katika biashara haramu ya silaha. Wakati huo wakihangaika na biashara iliyojulikana kama 'guns and cocaine triangle' kati ya Iran - Israeli - na Nicaragua. 1986 biashara hii ilikuja kubumburuka na ikawa maarufu kama 'Iran - contra' scandal.

$ Bush na yeye aliingia kwenye shirika kwa staili yake. Mwaka 1986-87 Barrick Gold Corp ilinunua ardhi, mali ya serikali ya Marekani, yenye thamani ya zaidi ya dola billion 10 kwa dola million 63 tu, kwaajili ya uchimbaji wa dhahabu.
Hapa ni USA ukumbuke, na sio mandazi republic kama hii yakwetu.
Bush alipochaguliwa 1988 akawezesha utaratibu wa kupata hati miliki kwa ajili ya eneo hili.Utaratibu huu ulikuwa special kwaajili ya Barrick tu!

♀Bush alishirikiana bega kwa bega na CIA na FBI katika kujaribu kupindua Serikali ya Fidel Castro katika uvamizi uliopewa jina maarufu kama Bay of Pigs invasion.
Walitumia mgongo wa kampuni ya Zapata Oil Bush akiwa kama rais wa kampuni na baadae Zapata Offshore Bush akiwa kama mmiliki.
Hapa kuna Memo kibao za ushahidi.

Nov.22, 1963 Bush alishiriki katika mauaji ya J.F.Kennedy, rais wa Marekani wakati huo kwasababu tu alikataza ndege za Marekani kutumika kwenye Bay of Pigs invasion. Kennedy pia alistopisha rogue operations zote za CIA na FBI .

Bush amefanya maovu mengi mno! Ana links na shetani wa kila aina;
☞ wa Nazi.
☞ wafanyabiashara ya madawa ya kulevya.
☞ Wafanyabiashara haramu ya silaha.
☞ Wauaji - assassins 
☞ CIA
☞ FBI 
☞ Na taasisi nyingi za kijeshi sehemu mbalimbali ulimwenguni.
Bush hajazaliwa hapo chini ya mfereji kwamba unaweza kumtumbua hata ukiwa grocery!

Kwenye moja ya mkutano mkuu wa umoja wa mataifa, siku moja baada ya Bush kuhutubia, Marehemu Hugo Chavez, Mungu ailaze roho yake mahali pema, Anasema, “ Shetani alikuja hapa jana, na mpaka leo hii, hii meza niliposimama inanuka sulfur.” Kisha Chavez akapiga ishara ya msalaba halafu akaangalia juu akiweka mikono yake kama mtu anayesali kumuomba Mungu.

Mdau unajua kwanini Chavez aliongelea harufu ya sulfur?

Chanzo - Jf

Hivi Ndivyo Mawaziri Wanaohudumu Katika Wizara ya Nishati na Madini Wanavyopukutishwa kwa Uzembe Wao..!!!

$
0
0

KUNG’OLEWEA kwa Waziri wa Nishati na Madini, Prof. Sospter Muhongo, kumeibua upya mjadala juu ya sababu za kutodumu kwa kila anayeteuliwa kuongoza wizara hiyo katika miaka ya hivi karibuni.

Aidha, baadhi ya wabunge na wafuatiliaji wa masuala ya siasa wametaja sababu tano kuwa ndizo chanzo cha kutodumu kwa mawaziri wanaoshika wizara hiyo, ikiwamo ya kuwapo kwa mikataba ya fedha nyingi zaidi kuliko iliyoko katika wizara zingine.

Vyanzo vingine vinavyolinganishwa na zimwi linalowang’oa mawaziri kila uchao katika wizara hiyo vinatajwa kuwa ni changamoto za mianya inayosababishwa na baadhi ya vipengele vya Sheria ya Madini ya mwaka 2010; kukosekana uzalendo kwa baadhi ya watendaji katika wizara ambao mwishowe huwaponza mawaziri husika; kuwapo kwa mikataba iliyojaa utata na uelewa mdogo wa baadhi ya watendaji katika kuwashauri mawaziri husika juu ya masuala mbalimbali ya mikataba ya nishati na madini.

Muhongo aliyekuwa akiiongoza Wizara ya Nishati na Madini kwa mara ya pili baada ya kuteuliwa na Rais John Magufuli katika Baraza la Mawaziri la Serikali ya awamu ya tano, aliondoshwa katika nafasi hiyo juzi kutokana na ripoti ya kamati teule ya Rais iliyochunguza usafirishaji wa mchanga wa dhahabu (makinikia) kwenda ughaibuni kubaini upotevu mkubwa wa mapato ya Serikali, hali inayotokana na kuwasilishwa kwa taarifa potofu juu ya kila kilichomo kwenye makontena 277 ya mchanga huo yanayoshikiliwa kwenye Bandari ya Dar es Salaam.

Kabla ya Muhongo, wengine waliowahi kuongoza wizara hiyo katika kipindi cha kuanzia Serikali ya awamu ya nne ni Dk. Ibrahim Msabaha, Nazir Karamagi, William Ngeleja, Muhongo, George Simbachawene na Muhongo aliyeongoza kwa mara ya pili, kuanzia mwaka 2016 hadi juzi.

KILICHOTOKEA KWA WALIONG’OKA
Wakati akipokea ripoti ya mchanga wa madini na kutangaza kumng’oa Muhongo juzi, Rais Magufuli alisema kutokana na kile kilichobainika, hana namna nyingine isipokuwa na kumwondoa licha ya kumpenda sana, tena ni rafiki yake.

“Ninampenda sana Profesa Muhongo, pia ni rafiki yangu… lakini kwenye hili ajifikirie, aji-asses (ajitathmini) na bila kuchelewa nilitaka aachie madaraka,” alisema kabla ya uamuzi kamili wa kutenguliwa nafasi yake kutolewa baadaye.

Pia nakala ya barua ya Muhongo kuachia ngazi ilionekana kwenye mitandao ya kijamii, ikimnukuu akisema ameamua kujiuzulu kutokana na ripoti ya Kamati Teule ya Rais kuhusu usafirishaji mchanga wa dhahabu.

Aliyeanza kuongoza wizara hiyo katika awamu ya nne ya Rais Jakaya Kikwete kuanzia mwaka 2005 ni Dk. Msabaha. Hakudumu sana baada ya kuondolewa Oktoba, 2006 na kuhamishiwa katika Wizara ya Ushirikiano wa Afrika Mashariki.

Aliyefuatia baada ya Msabaha ni Nazir Karamagi. Naye hakudumu baada ya hatima yake kufika Februari 6, 2008 alipojiuzulu kutokana na matokeo ya ripoti ya Kamati ya Bunge iliyochunguza kashfa ya mkataba wenye utata wa Serikali kupitia Shirika la Umeme (Tanesco) na kampuni ya Richmond kwa ajili ya kufua umeme wa dharura.

Ripoti ya Bunge iliyomng’oa Karamagi na Msabaha pia ilisababisha Baraza la Mawaziri kuundwa upya baada ya aliyekuwa Waziri Mkuu, Edward Lowassa, kujiuzulu kutokana na ilibaini kuwa mchakato ulioipa Richmond zabuni ulighubikwa na vitendo vya ukiukwaji taratibu, kanuni na sheria za nchi.

Ngeleja akatwaa kijiti cha kuongoza wizara hiyo baada ya kuteuliwa na Rais Kikwete katika baraza jipya la mawaziri lililoundwa baada ya mtikisiko wa kashfa ya Richmond.

Ngeleja naye aling’olewa Mei 2012 baada ya Rais Kikwete kufanya mabadiliko makubwa ya baraza lake la mawaziri yaliyotokana na kishindo cha Ripoti ya Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali (CAG), iliyofichua madudu mengi yaliyofanywa na wizara hiyo chini ya uongozi wake.

Ni hapo ndipo Rais Kikwete alipomteua Prof. Muhongo kuongoza wizara hiyo kwa mara ya kwanza.

Hata hivyo, zimwi linalong’oa mawaziri katika wizara hiyo halikumwacha Muhongo adumu. Rais Kikwete alilazimika kukubali kuondoka kwa waziri huyo baada ya wabunge kumhusisha katika kashfa ya uchotwaji wa mabilioni ya fedha kwenye akaunti ya Tegeta Escrow.

Baada ya Muhongo kung’oka, Rais Kikwete alimteua George Simbachawene kushika nafasi hiyo, ambaye aliitumikia vyema hadi serikali ya awamu ya nne ilipomaliza muda wake wa kuwa madarakani mwaka 2015.

Kwa mara nyingine, Muhongo alirejea kuiongoza wizara hiyo baada ya Rais Magufuli kumteua katika baraza lake la mawaziri la Serikali ya awamu ya tano.

Hata hivyo, Muhongo alijikuta akikumbwa tena na mikasa ya kung’olewa mapema kwa mawaziri katika wizara hiyo juzi kutokana na kashfa ya mchanga wa dhahabu, ikiwa ni mara ya pili kwake kukutwa na masahibu hayo.

Credit - Nipashe,

Bosi wa ACACIA Atoboa Siri, ya Mikataba ya Madini Waliosaini na Serikali ..Ni Baada ya Ripoti ya Mchanga Kutua kwa JPM..!!!

$
0
0

Mnamo tarehe 12 mwezi Machi mwaka huu, Mwandishi Jon Yeomans wa gazeti la telegraph la nchini Uingereza alifanya mahojiano na Mtendaji Mkuu wa Kampuni ya Uchimbaji Madini ya ACACIA, Brad Gordon.

Pamoja na mambo mengine, Mtendaji Mkuu huyo wa ACACIA alisema kwa kukiri kuwa mikataba/makubaliano kuhusu uchimbaji wa madini pamoja na kuwa ya kisheria lakini hayakuwa ya usawa.

Majeruhi Wawili ya Lucky Vincent Waruhusiwa Kutoka Hospitali

$
0
0

Dar es Salaam. Watoto wawili majeruhi wa ajali ya gari la Shule ya Lucky Vincent wameruhusiwa kutoka hopitalini.

Mbunge wa Singida Kaskazini, Lazaro Nyalandu ameandika katika ukurasa wake wa Facebook kuwa watoto hao, Sadia Ismael na Wilson Tarimo waliokuwa wamelazwa katika hospitali ya Mercy ya Marekani wameruhusiwa na sasa wapo katika makazi mapya.

“Watoto Sadia na Wilson waruhusiwa rasmi kutoka hospitali ya Mercy  na wanaelekea kwenye makazi yao mapya mjini Sioux City IA. Mungu azidi kuwaangazia nuru ya uso wake. Amani iwe nawe na Nesi wetu mpendwa kwa huduma kubwa mmefanya kwa watoto hawa na Tanzania,”ameandika Nyalandu.

Jana Nyalandu aliandika kuwa mtoto Doreen ataendelea kuwepo hospitali katika wodi ya watoto akiendelea kupata huduma za karibu hadi itakapoamuliwa vinginevyo.

Simba Wakanusha Taarifa ya Wao Kukubali Ushindi wa Pili Inayozunguka Mitandaoni

$
0
0
Siku moja baada ya tuzo za Ligi Kuu ya Vodacom Tanzania bara kufanyika na kutoa zawadi kwa wahusika huku timu ya Simba ambayo ni mshindi wa pili kutokuwepo wala kutuma muhusika katika eneo la tukio ikihisiwa kuwa ni muendelezo wa kugomea zawadi ya mshindi wa pili.



Leo May 25 2017 ziliripotiwa habari za uongo katika mitandao ya kijamii kuwa wekundu wa Msimbazi Simba kupitia kwa Rais wao Evans Aveva wamekubali nafasi ya mshindi wa pili na kufuta malalamiko yao FIFA kuhusiana na TFF kuituhumu kutotenda haki.



Imefichuka..Sumaye Alikuwa Analipwa Zaidi ya Milioni 55 Kama Posho ya Vikao Tu Kwenye Bodi ya CRDB..!!!

$
0
0

Waziri Mkuu mstaafu, Frederick Sumaye si wa kwanza kustaafu ukurugenzi wa bodi ya Benki ya CRDB. Ni utaratibu uliopo ndani ya taasisi hiyo ya fedha, kuchiana vijiti licha ya malipo manono yanayoambatana na nafasi hiyo.

Sumaye alitangaza kujiondoa kwenye bodi ya wakurugenzi wa benki hiyo kwenye mkutano mkuu wa 22 uliofanyika jijini Arusha wiki iliyopita, jambo lililozusha mjadala miongoni mwa wadau wengi wa biashara hasa sekta ya fedha.

Kujiuzulu kwa Sumaye aliyedumu kwenye bodi hiyo tangu mwaka 2011, kulitoa nafasi ya kuchaguliwa kwa Mhadhiri Mwandamizi wa Chuo Kikuu cha Dar es Salaam, Dk Neema Munisi.

Sumaye na mrithi wake, wamo kwenye kundi la wenye chini ya asilimia moja ya hisa zote za kampuni ambao wanatakiwa kuwa na mkurugenzi mmoja miongoni mwa 13 wanaotakiwa.

Kwenye mkutano huo, Dk Neema aliwashinda wenzake baada ya kupata asilimia 50 ya kura zote zilizopigwa. Wanahisa zaidi ya milioni 527 walipiga kura kwenye uchaguzi huo.

Kuepusha mgongano wa maslahi, benki inawataka wakurugenzi wake kueleza bayana kama wanazo biashara zenye ushindani na CRDB. Ni sharti mkurugenzi kutokuwa na biashara au ajira ya kudumu yenye mgongano wa maslahi na benki hiyo.

Siasa zimemuondoa Sumaye, ambaye anasema atalazimika kutumia muda mwingi kuitumikia Chadema katika kujipanga na uchguzi mkuu ujao au wowote utakaojitokeza kabla ya mwaka 2020.

“Mambo yangu mengi yanafuatiliwa. Hata mashamba ya wanangu yamechukuliwa. Sitaki kuiingiza benki hii yenye maelfu ya wanahisa kwenye matatizo kwa ajili yangu,” anasema Sumaye.

Sumaye mwenye zaidi ya hisa milioni 7.448, amejiondoa kwenye bodi hiyo licha ya mamilioni ya shilingi aliyokuwa akilipwa kutokana majukumu aliyokuwa akitekeleza. Kumbukumbu za benki hiyo zinabainisha; mwaka jana alilipwa Sh58 milioni kati ya Sh616 milioni, wakati mwaka 2015 alipokea Sh53 milioni kati ya Sh553 milioni zilizotengwa kwa ajili ya malipo ya wajumbe wa bodi. Malipo hayo yalifanywa baada ya Sumaye kuhudhuria vikao saba kati ya vinane vilivyopangwa na kufanyika mwaka 2016.

Mwanasiasa huyo amejiondoa wakati bajeti ikiwa kwa ajili ya posho za wakurugenzi ikiwa imeongezeka. Zaidi ya Sh700 milioni zinatarajiwa kutumika kwa ajili hiyo mwaka huu.

“Hata baada ya uamuzi huu rafiki zangu wa Mtaa wa Lumumba hawafurahi. Nilitarajia wataridhika kwa kuona nitakosa posho hizi zinazolipwa kwa wajumbe,” anatania.

Waliiojiuzulu

Bodi ya wakurugenzi ndiyo mamlaka ya juu inayosimamia utawala ambayo inazo kamati zinazoshughulikia vihatarishi vya mikopo, ukaguzi, utawala na rasilimali watu ili kuongeza umadhubuti wa biashara na fedha.

Kwenye mkutano mkuu uliopita, wajumbe watatu; Boniface Muhegi, Ally Laay na Adam Mayingu walistaafu. Mayingu hakutaka kurudi tena, lakini Laay aligombea na kuchaguliwa kuwa mwenyekiti baada ya kustaafu kwa Martin Mmari. Muhegi bado yupo kwenye bodi hiyo baada ya kuchaguliwa tena.

Bodi ya wakurugenzi wa CRDB ina wakurugenzi 13, miongoni mwao 12 siyo watendaji akiwamo mwenyekiti isipokuwa mkurugenzi mtendaji. Mwenyekiti huchaguliwa kila mwaka kuiongoza bodi hiyo.

Kila mwenye asilimia 10 ya hisa za benki huruhusiwa kuchagua mkurugenzi wa benki. Wenye kati ya asilimia moja mpaka 10 huruhusiwa kuchagua mkurugenzi kwa kila asilimia 10, wale ambao hawafikishi asilimia 10 kwa ujumla hawaruhusiwi kuchagua mkurugenzi.

Kwenye mkutano mkuu uliofanyika mwaka 2015, wanahisa walikubaliana kuwaruhusu International Finance Co-operation (IFC), Africa Capitalizationa Fund (AFCap) na Kampuni ya CDC (Commonwealth Development Corporation) Group kuteua mkurugenzi mmoja iwapo hisa zao zitafika asilimia tano.

Wanahisa wanaomiliki chini ya asilimia moja ya hisa zote, wanaruhusiwa kuchagua mkurugenzi mmoja na wanahisa wote kwa pamoja wanaweza kuchagua mkurugenzi huru.

Kwa mujibu wa katiba ya benki, wajumbe wa bodi wanapaswa kustaafu ingawa wanaweza kuchaguliwa tena baada ya muda wao wa miaka mitatu kumalizika iwapo wanakidhi vigezo.

Itakumbukwa, aliyekuwa Mwenyekiti wa bodi, Martin Mmari aliteuliwa na Mfuko wa Pensheni wa PPF na alistaafu tangu Julai 2016 na nafasi yake kujazwa na Hosea Kashimba.

Profesa Mohammed Warsame alichaguliwa kuwakilisha kundi la wenye hisa kati ya asilimia moja mpaka 10, wakati Madren Oluoch-Olunya alichaguliwa kuwa mjumbe huru akichukua nafasi iliyoachwa wazi na Lawrence Mafuru.

Bodi ina jukumu la kusimamia na kupitisha malengo na mikakati ya benki na kampuni zake tanzu na kufuatilia utekelezaji, kusimamia utekelezaji wa mfumo wa utawala kuhakikisha unaendana na mabadiliko yoyote kama vile ukubwa, mtandao wa shughuli, mkakati wa biashara, masoko na udhibiti.

Vilevile, hushirikiana na menejimenti kuangalia vihatarishi na sheria za udhibiti zilizopo na maslahi ya muda mrefu ya kampuni kwa ufanisi.

Mhadhiri Mwandamizi wa Chuo Kikuu cha Ardhi, Dk Mlenge Fanuel anasema kuondoka kwenye bodi ya wakurugenzi siyo kitu cha ajabu kwa wajumbe wa taasisi nyingi.

“Kitu muhimu ni ufanisi wa taasisi husika. Kama huduma zake zinakidhi matarajio ya wateja, hakuna tatizo lolote. Ni kawaida kwa wajumbe kupishana. Waikuwapo wengi CRDB ambao waiondoka,” anasema Dk Fanuel.

Credit - Mwananchi

Serikali Yashusha Neema ya Ajira Nchini..Yatangaza Nafasi 291 kwa Wizara ya Ardhi..!!!

$
0
0

SERIKALI imezidi kutangaza neema ya ajira kwa Watanzania baada ya kubainisha kuwa katika mwaka ujao wa fedha watumishi wapya 291 wataajiriwa katika Wizara ya Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi.

Waziri wa wizara hiyo, William Lukuvi, aliyasema hayo bungeni mjini hapa jana alipokuwa akiwasilisha hotuba yake kuhusu utekelezaji wa bajeti ya wizara hiyo kwa mwaka huu wa fedha na makadirio ya mapato na matumizi yake kwa mwaka ujao wa fedha.

Mbali na ajira hizo mpya, alisema wizara yake itatoa mafunzo kwa watumishi 70 na kuboresha ofisi zake ili kuwezesha watumishi wengi zaidi kuhamia Dodoma.

CHANGAMOTO TANO

Lukuvi alisema wizara hiyo inakabiliwa na changamoto tano ambazo ni pamoja na uratibu wa sekta ya ardhi kusimamiwa na mamlaka zaidi ya moja na upungufu wa wataalamu na vitendea kazi vinavyohitajika ili kukidhi utoaji wa huduma katika sekta ya ardhi.

Alizitaja changamoto nyingine kuwa ni kasi ya ongezeko la watu na mifugo kulinganishwa na upatikanaji wa ardhi iliyopangwa na kupimwa, ucheleweshaji wa ulipaji wa fidia stahiki kwa ardhi iliyotwaliwa kwa ajili ya matumizi ya maendeleo na uelewa mdogo wa wananchi kuhusu sera na sheria za nchi.

Ili kutekeleza majukumu yake katika mwaka ujao wa fedha, Lukuvi aliliomba Bunge kuidhinisha bajeti ya jumla ya Sh. bilioni 70.77. Kati yake, Sh. bilioni 25.4 ni kwa ajili ya miradi ya maendeleo.

Kwa mujibu wa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Ardhi, Maliasili na Utalii, wizara hiyo iliidhinishiwa Sh. bilioni 61.873 kwa ajili ya bajeti yake ya mwaka huu wa fedha. Kati yake, Sh. bilioni 20 zilikuwa za maendeleo.

Akiwasilisha maoni ya Kambi Rasmi ya Upinzani Bungeni kuhusu makadirio ya wizara hiyo, Waziri Kivuli wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi, Wilfred Lwakatare, aliishauri serikali kumaliza changamoto ya migogoro ya ardhi nchini, kuitaka Mamlaka ya Mapato (TRA) kuongeza kasi ya makusanyo ya kodi ya majengo na kuhamisha ajira za sekta ya ardhi kutoka serikali za mitaa kwenda serikali kuu.

Lwakatare ambaye pia ni Mbunge wa Bukoba Mjini (Chadema), aliishauri serikali kuunda mamlaka ya kusimamia sekta ya miliki hasa za majengo makubwa, kuwafidia wananchi waliobomolewa nyumba kupisha miradi ya serikali, kutathmini gharama za nyumba zinazojengwa na Shirika la Nyumba (NHC) na kuwaagiza wakuu wa mikoa na wilaya kutoingilia majukumu ya mabaraza ya ardhi.

Tetemeko la Ardhi la Sekunde 10 Laua na Kujeruhi Watu Mwanza..!!!

$
0
0

ASKARI polisi mmoja alifariki dunia na mwingine mmoja, mtuhumiwa mmoja kupoteza fahamu jana kufuatia tetemeko la ardhi lililopiga kwa sekude 10 katika maeneo machache ya mkoa wa Mwanza. Tetemeko hilo lililotokea jana saa 6:55 mchana.


Akithibitisha kutokea kwa kifo hicho, Kamanda wa Polisi mkoani hapa, Ahmed Msangi alimtaja marehemu kuwa ni askari wa kike mwenye namba WP 4674, koplo Joyce Mwalingo.

Kamanda Msangi alisema WP Joyce alifariki akiwa katika eneo lake la kazi, akifanya mahojiano na mtuhumiwa katika kituo cha Polisi Misungwi kilichopo wilaya ya Misungwi mkoani hapa.

“WP Joyce alifariki dunia baada ya tetemeko lililotokea majira ya saa 6:55 mchana, wakati akifanya mahojiano huku akiwa na askari mwenziye WP 11954, Stela ambaye alipata mshtuko baada ya kupata taarifa ya kifo cha mwenzake," alisema Kamanda Msangi.

Alisema WP Stela alipelekwa hospitalini kwa matibabu kutokana na hali yake kuwa mbaya pamoja na mahabusu Mathias Saimon ambaye alizimia kwa mshtuko wa janga hilo.

Kamanda huyo hakuweza kutaja kipimo cha tetemeko hilo, lakini halikuwa na ukubwa wa janga la Septemba 10, mwaka jana lililokumba mkoa wa Kagera lililokuwa na nguvu ya 5.7 katika vipimo vya Richter, na kwa mujibu wa mtandao wa kompyuta wa earthquaketrack.com ndilo kubwa zaidi katika historia kutokea nchini.

Tetemeko hilo lilisababisha vifo vya watu 18, majeruhi 190 na uharibifu mkubwa wa mali na miundombinu.

Aidha, Kamanda Msangi alisema tetemeko hilo lilitikisa maeneo kadhaa ya wilaya za Kwimba, Misungwi na Nyamagana na kuzua hofu kwa watu kutokujua nini wafanye.

Alitaka wananchi, hususani waliojenga katika maeneo ya milimani, pembezoni mwa mawe, kuchukua tahadhari ya kutoka nje mapema pindi waonapo hali ya tofauti.

Meneja wa kampuni ya bima ya Jubilee Insurance, Jared Awando ambaye ni shuhuda wa tetemeko hilo alisema jengo ambalo ofisi yake ipo lilitikisika, hivyo yeye na wafanyakazi wote walitoka nje kwa kukimbia na kuungana na wananchi wengine ambao walionekana kuhangaika bila kujua cha kufanya.

Jackline Timo na Bahati John walisema wao walikuwa ndani ya nyumba wakifanya shughuli zao na pindi wakaona jengo linatetemeka ndipo wakachukua maamuzi ya kutoka nje haraka.

Tetemeko hutokeaje?

Mtaalamu wa masuala ya miamba, George John anasema ardhi ya dunia imegawanyika katika sehemu kuu tatu ambazo ni tabaka la juu, la kati na la chini.

Anasema katika tabaka la kati mara nyingi kunatokea msuguano ama msukumo wa volcano ambao kila upande unavuta upande wake.

Anasema wakati kitendo hicho kinatokea ndipo mgongano unagonga katika tabaka la juu la uso wa dunia na kutokea tetemeko la ardhi.

“Ni mvutano ambao hautabiriki utatokea lini, hata utabiri wa hali ya hewa hawajui, ni kitendo ambacho hutokea chini ya ardhi ya dunia,” alisema John.

John anasema hata ziwa Victoria na Tanganyika yote yametokea kutokana na mvutano huo miaka bilioni 3.5 iliyopita.

Anasema maeneo kama Manyara, Kagera, Mwanza na Mara yapo katika bonde la ufa, hata nchi za Kenya, Rwanda na Uganda.

Anasema tetemeko lililotokea katika mikoa ya Mwanza na Kagera lilisababishwa na msuguano wa volkano, lakini ni tofauti na tetemeko lililotokea nchini Japan hivi karibuni ambalo lilisababishwa na msuguano wa miamba.

Kwa Watasha Tu..Pitia Nukuu Hii Inakuhusu Moja kwa Moja..!!!

$
0
0

Mimi ninachoamini tu ni kwamba kwenye dunia hii wewe fanya wema tu hata ukifanyiwa uhuni basi ila utakuwa huru na mwenye furaha wakati wote. Mafanikio kwenye maisha ni kuwa na utu, kudhaminiwa na kuwadhamini wengine.Udhaifu wa mtu mwingine usikufanye nawe kuwa dhaifu.Unatakiwa kuwa imara na usifanye makosa kwa kuwa wengine wanafanya makosa.Fanya jambo ambalo linakuweka huru na kukupa furaha na hata kuwa na sababu ya kuendelea kuishi.

Umewahi Kukaa Sehemu Ukawa Unapiga Story na Mungu? Fanya Hivyo kwa Njia Hii...!!!

$
0
0

Je umewah kukaa sehemu ukawa unapiga story na Mungu mnacheka,mnagonga na kushauriana?
wakati mwingine dhambi zetu zinatutenga na Mungu tunaanza kuwa waoga na wenye kujishtukia, wenye chuki kwa Mungu na moja kwa moja tunajitenga naye. lakini kama Tungejua vile ambavyo yeye alipenda tuwe wala tusingekuwa tunamchukulia jinsi tunavyomchukulia. Mungu alipenda sana tuish naye kwa maisha ya amani na upendo. 

sasa chukua muda wako vizuri nenda chumbani kwako katika mazingira mazuri na tulivu. kama utakaa kwenye kochi au kitandani au hata chini yeye Mungu hampi shida ongea naye. anasikiliza. na unaweza ukawa unaongea na Mungu kiasi kwamba sometime unajikuta unacheka au unapata furaha flan ambayo katika mazingira ya kawaida huwez ipata. Unapoongea na Mungu Ukamzoea utajikuta ukiwa unapiga naye story moyoni unajisikia utulivu sana. kichwani kunakuwa hakuna makelele tena hata kama humo ndani kuna makelele. 

unasikia harufu nzuri yenye utulivu na mwili mwako unalegea kwa maana ya kuwa una relax sana. ukimya wake unakuwa kana kwamba hata mapigo ya moyo huyasikii. hapo unaweza jikuta unatulia sana. una furaha sana, una amani sana. utaongea na Mungu. 

give thanks and praise. Acha lawama na majungu unapokuwa unapiga story na Mungu
Usiongee na Mungu kwa Kumlaumu. nani anapenda lawama? hamna. na ni unaweza anzisha naye mazungumzo kwa lawama? nenda kwa boss wako anayekupenda na kukujali. mwambie " boss unajua wewe unatunyonya sana?hutujali, kazi nyingi mshahara kidogo, tunateseka na kazi zako wewe tu ndo unafaidika" halafu angalia uhusino wenu utakuaje.


Mpe sifa Mungu. maana Mungu huketi mahali penye sifa na Mungu anapenda sifa. anapenda sana sifa. msifu na mshukuru kwa kila ulicho nacho na sasa hapo u(chomekee na mahitaji mengine) tuache kumlaumu Mungu. hili ni kosa kubwa tunafanya. lawama kwa Mungu. tunasahau kuwa tunapolalamika kuwa mimi sijala na familia yangu. kuna mwingine chakula anapata lakini hawezi kula. au analishwa kwa mirija hata ladha ya chakula hapati. au akila chote kinatoka. 
Ukiwa unapiga Story na Mungu acha Majungu, fitna ,Umbea na Uchonganishi. usimpe hizo story.
acha majungu na umbea... "ooo Mungu mbona flan umemsaidia, mbona flan anakula bata, mbona flan anatutesa hapa mtaani" hayo ni majungu. wewe omba au piga story zako achana za kuwafitinisha watu na Mungu. hiyo ni kazi ya shetani asilimia 100. kama unataka kupiga story za watu wengine kwa Mungu basi ziwe njema kuwa unamsifu kwa kuwa amemtumia flan kuwasaidia watu flan.lakini siyo kumwaribia mwenzio kuwa anapata utajiri wakati ye mlevi mzinzi au si mwema kama wewe...hizo siyo issues za kupiga story na Mungu. acha majungu fanya yako.

tumshukuru Mungu huyu baba yetu na sisi wana wake kwa sifa na utukufu. watu wanashangaa mtu akisema yeye ni mwana wa Mungu. kwa nini?kama shetani ana watoto wake na kwa nini Mungu asiwe na watoto wake? 

Unaweza mshawishi Mungu akufanyie jambo mpaka akakubali kulifanya.
unapokaa na Mungu kupiga story hebu jifunze kumshawishi. mshawishi afanye jambo lako ikiwa ni jema. yeaah yu can do that. sometime Mungu anakuwa hakukuweka kwenye ratiba flan. lakini kama utamshawishi anaweza akakufanyia Upendeleo. na Mungu anatoa Upendelea kutokana na Ushawishi wako na Kazi zako.Si kweli kuwa Mungu hana Upendeleo. anao. kwa nini unadhani si wote wamelazwa muda huu? unadhani kwa nini wewe umekula?kwa nini wewe mzima? unadhani ni sababu wewe ni mwema sana au unastahili kuliko aliyepata ajali jana na juzi au mgonjwa wa kusubiri kufa?

well..upendeleo wake hauhusian na mali au uzuri wa nje. kila jambo Mungu hufanya kwa kusudi au huruhusu litokee kwa makusudi

Mungu anapenda sana Sifa hasa akiwa anapiga story na Shetani
Usidhani Mungu na Shetani hawaongei. wanaongea. tena huwa sometime wanatambiana sana. Mungu anatamba kwa shetani kwa watu wake wema wanaotenda mema. rejea habari ya Ayubu katika kitabu cha Ayubu 1:7 Shetani akiwa katika mizunguko yake ya kila siku ya kutafuta watu wa kuwapoteza akapita sehemu Mungu akamwona akamwuuliza "unatoka wapi?" naye akajibu kuwa anatoka katika kuzunguka zunguka huko na kule. Kwa majidai kabisa Mungu akamwuliza Shetani "unamwona mtumishi wangu Ayubu? maana hakuna aliye mkamilifu kama yeye....."

Mungu anajivunia Ayubu. unadhan wewe ikitokea Shetani amekutana na Mungu nani atajivuna kwa mwenzie?anyway, wadau msisite ku kaa na kupiga story na Mungu na ukiwa katika story usipige story za hovyo hovyo. jiheshimu na umheshimu. muombe kwa unyenyekevu na kujishusha na pia uwe na subira usiforce mambo.ndo hapo unasema Mapenzi yako yatimizwe.

Jifunze kudeka kwa Mungu. anapenda sana kudekeza aisee...tena utaenjoy sana.
sometime unaweza hata deka kwa Mungu. unajua anapenda sana kudekeza. hivi umewah kuwaangalia ndege wa angani? walivyo wazuri na wenye kupendeza. hivi uliona wapi mashamba wanayolima? uliona wapi wakifuma nguo au manyoya wanayotumia? anyway. wewe ni bora kuliko wale ndege. wewe una thaman kuliko wale ndege. MUNGU NI BABA YAKO. Issues nyingine mweleze tu reality a juhudi zako then mwambie umemwachia yeye. unataka mke...mwambie wewe umeshajipanga na upo tayari sasa naye akupige tafu maana wewe huwezi jichagulia mke. mke mwema anatoka kwa Mungu.basi akupe mtoto mkali mwema anayekufaa. basi. unaachana na hiyo issue unasubiri. kama una vifungu vya kumkamatia kwenye biblia hebu mtajie. mkumbushe mwoneshe unajua unachoomba. sometime wewe dai mambo yako kupitia tu maandiko yake then mwachie. au kama kuna mazuri unatenda mkumbushe wala si dhambi

Haya, njooni, tusemezane, asema Bwana.Dhambi zenu zijapokuwa nyekundu sana, zitakuwa nyeupe kama theluji, zijapokuwa nyekundu kama bendera, zitakuwa kama sufu.

Kama mkikubali na kutii mtakula mema ya nchi, kama mkikataa na kuasi mtaangamizwa kwa upanga;maana kinywa cha Bwana kimenena haya
(Isaya 1: 18-19)

Mungu ni Rafiki, Mungu hataki aogopewe, Mungu anapenda wana wake... Sisi ni wana wa Mungu na kama sisi ni wana wa Mungu basi sisi ni Miungu. "ninyi ni miungu" katika Zaburi 82: 6 na Yohana 10:34?"
Viewing all 104789 articles
Browse latest View live




Latest Images