Quantcast
Channel: UDAKU SPECIAL
Viewing all 104789 articles
Browse latest View live

Fid Q Afunguka Kuhusu Bifu ya Diamond na Ali Kiba....Amtaka Ali Kiba Wafanye Remix Nyingine

$
0
0
Nyota wa muziki wa hiphop kutoka Mwanza, Fid Q amefunguka namna Diamond alivyomshawishi hadi kumuweka kwenye 'Fresh Remix' ngoma ambayo imepaka upya rangi ya mng'ao Bifu la Ali Kiba na Diamond....

Mkali huyo wa michano amesema Diamond alimuahidi kumshangaza katika verse yake na kukiri wazi kuwa Aliipenda mistari ya CEO huyo wa WCB .

"Alinipigia simu Tale akaniambia Fid eeh nipo na Mond hapa anataka aongee na wewe nikamwambia poa mpe nimsikie, (Diamond) Kaka vipi bhana hii fresh nimeielewa kama vipi tufanye remix mzee halafu mimi nitaku'suprise kwa kuchana humu...Nikamuambia chana halafu unitumie. Akachana ile verse then akanitumia alivyonitumia ile verse niliipenda ukizingatia Diamond ni number 1 Artist in the country (Tz) anafahamika kwa uimbaji halafu akaamua kuchana hii ni baraka kwa muziki wa hiphop na rap kwa ujumla" alisema Fid Q.

Kuhusu ngoma yake kutumika kuchochea bifu la mafahari hao wawili Diamond na Alikiba
Fid Q amesema

"Mimi siamini kama nimetumika kama daraja mimi sio team Diamond wala sio Team Kiba moja ya ndoto zangu ni kukutanisha hawa watu wawili waweze kufanya kazi pamoja tuondoe maswala ya u'team tuweze kutengeneza wakina Diamond na Alikiba wengine! hizo ndio ndoto zangu" .

Katika hatua nyingine star huyo wa 'Fresh' amesema yupo tayari kufanya Fresh Remix nyingine na Alikiba kama msanii huyo akihitaji kufanya .

Waziri Charles Mwijage Awacharukia TRA...Adai Wanataka Kumfukuzisha Kazi

$
0
0
Waziri Charles Mwijage Awacharukia TRA...Adai Wanataka Kumfukuzisha Kazi
Waziri wa Viwanda, Biashara na Uwekezaji, Charles Mwijage ameitaka Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA) kutomfukuzisha kazi kwa uzembe wao uliopelekea nchi kupigwa na kupata hasara kutokana na watu kuingiza cement kutoka nje ya nchi wakidai ni krinka.

Waziri Mwijaga alisema hayo jana kupitia kipindi cha HOTMIX na ambapo alitumia nafasi hiyo kupiga marufuku Shirika la Viwango Tanzania (TBS) kukagua krinka yoyote kutoka nje ya nchi.

"Mtu anatengeneza Krinka anauza Kenya, sasa kama mtu anatengeneza Krinka Tanga anauza Kenya wewe unafuata nini Pakistan? Hakuna krinka inatoka nje ya nchi ile ni Cement iliyokamilika TRA wanashindwa kufanya kazi yao, narudia kusema hakuna krinka inaingia nchini kutoka nje ile ni Cement kamili na anayepinga aje aniambie mimi, na kuanzia leo TBS wasikague krinka yoyote kutoka nje ya nchi waingize ndani ya nchi bila TBS kukagua, TBS ipo chini yangu sasa kama mimi naambiwa sitoshi na wa TBS ajiangalie" alisema Mwijage

Aidha Waziri Mwijage alidai kuwa watu wa Cement walikubaliana na DR Meru kununua hizo Krinka hapa hapa nchini

"Watu wa Cement walikubaliana hapa na Dr. Meru Twiga Cement ananunua Krinka Simba Cement mwingine nani ananunua krinka nyingine kutoka wapi, watu wanaleta cement iliyokamilika wanasema Krinka sasa kuanzia leo TBS hawezi kukagua krinka yoyote kutoka nje ya nchi, mpaka mamlaka iliyopo juu yangu sasa kama TRA walizembea tukapigwa juu yao kwanini wanataka kuharibiana kazi, eti bwana wanataka kuniharibia kazi mimi" alisisitiza Waziri Mwijage

Raif Magufuli Afanya Uteuzi Mwingine wa Kamishina wa Oparesheni ya Kupambana na Madawa ya Kulevya

$
0
0
Raif Magufuli Afanya Uteuzi Mwingine wa Kamishina wa Oparesheni ya Kupambana na Madawa ya Kulevya
Rais Magufuli amteua Luteni Kanali Frederick Felix Milanzi kuwa Kamishna wa Operation wa Mamlaka ya kuzuia na kupambana na dawa za kulevya.

Luteni Kanali Frederick Felix Milanzi anachukua nafasi ya Bw. Mihayo Msikela ambaye amerejeshwa Makao Makuu ya Polisi.

Bill Nasi Aeleza Sababu ya Kutotoa Nyimbo za Mapenzi

$
0
0
Bill Nasi Aeleza Sababu ya Kutotoa Nyimbo za Mapenzi
Msanii wa muziki Bongo, Bill Nass ameleeza sababu ya kutotoa nyimbo zenye maudhui ya mapenzi.

Rapper huyo ambaye anafanya vizuri na ngoma yake mpya ‘Sina Jambo’, ameiambia Live Entertainment ya Azam Tv kuwa anafanya hivyo ili kuleta utofauti katika muziki wake.

“Mimi pia naangalia utofauti huo kwa sababu tukiwa wote 10 tunaimba nyimbo za aina moja au topic moja si rahisi mtu kusikiliza nyimbo zote hatapata choice za hapo hapo” amesema na kuongeza.

“Ninavyoona mimi kuchagua lazima uwe tofauti, wote mkifanana hamuwezi kufika sehemu, mwezio akienda hivi, wewe unaenda hivi unajaibu kutafuta utofauti ili uweze kupata fan base tofauti,” amesisitiza.

Mara ya mwisho Bill Nass kutoa wimbo wa mapenzi ulikuwa ‘Raha’ ambao alimshirikisha Nazizi kutoka nchini Kenya pamoja na TID, pia wimbo huo ndio ulimtoa kimuziki.

Tanzania Yapata Neema Kutoka Serikali ya Uingereza

$
0
0
Tanzania Yapata Neema Kutoka Serikali ya Uingereza
Serikali ya Uingereza kupitia kwa Waziri wa Nchi anayeshughulikia masuala ya Afrika katika Wizara ya Mambo ya Nje ya Uingereza, Mhe. Stewart Rory wamesaidia Tanzania Trilioni moja kwa ajili ya kusaidia miradi ya maendeleo nchini. 
 
Mhe. Stewart Rory amesema kuwa msaada huo utaelekezwa kwenye masuala mbalimbali hasa katika kuboresha ubora wa elimu.
 

Hatimaye Hali ya Mbunge wa Bunda Ester Bulaya Yaendelea Kuhimarika

$
0
0
Hatimaye Hali ya Mbunge wa Bunda Ester Bulaya Yaendelea Kuhimarika
Hali ya Mbunge wa Bunda Ester Bulaya aliyelazwa katika Hospitali ya Taifa Muhimbili (MNH ) inaendelea vizuri baada ya kuanza kupatiwa matibabu jana.

Bulaya ambaye alipata tatizo la kupumua baada ya kuzidiwa akiwa mahabusu ya Kituo cha Kati cha Polisi mjini Tarime, alifikishwa hospitalini hapo juzi usiku na kulazwa katika wodi namba 18 Sewahaji.

Akizungumza Ofisa Uhusiano wa Muhimbili, John Stephen alisema leo Bulaya amepata ahueni kiafya na anaendelea vizuri na matibabu.

"Sasa ameanza kujihudumia mwenyewe, anakula vizuri na bado anaendelea na matibabu," amesema Stephen huku akisisitiza kuwa mgonjwa bado anahitaji utulivu kwa kipindi hiki.

Bulaya amesota rumande tangu akamatwe Ijumaa ya Agosti 18 kwa madai ya kuingia jimbo la Tarime na kufanya shughuli za kisiasa kwa kutoa msaada wa mifuko 50 ya saruji kwa ajili ya ujenzi wa miundombinu katika shule za msingi jimboni humo baada ya kualikwa na mbunge mwenzake Ester Matiko.


Mauno ya Moses Iyobo Yampagawisha Aunty Ezekiel Mpaka Kuikana Ndoa Yake Sunday Demonte

$
0
0
Mapenzi ya Iyobo Yapelekea Aunty Ezekiel Kuikana Ndoa Yake
Siku chache baada ya kuenea kwa madai kuwa mume wa ndoa wa mkali wa sinema za Kibongo, Aunt Ezekiel, Sunday Demonte ameachiwa huru huko Dubai baada ya kutumikia kifungo cha miaka kadhaa huku staa huyo akishi kinyumba na mwanaume mwingine, muigizaji huyo amesema ndoa hiyo haipo tena.

Risasi Mchanganyiko lilimtafuta Aunt ambaye alifunga ndoa na Demonte yapata miaka minne iliyopita, alisema kuwa, anawashangaa watu wanaoikomalia ishu hiyo ambayo kwa upande wake ni ndogo.

Ngoja niulize, hivi jamani mbona watu siyo waelewa? Nani asiyejua kama mimi niko na mtu hivi sasa?

Na ninaamini kabisa hata yeye (Demonte) anajua? Kwa hiyo hata kama ameachiwa huru na akaja, ukweli utabaki kuwa ndiyo huohuo tu, kwamba tayari nina mtu mwingine maana hata yeye asingeweza kusubiri muda wote huo, hivyo ajue tu hana chake,” alisema Aunt.

Staa huyo aliongeza kuwa, kwa hivi sasa ni vigumu kuachana na mzazi mwenziye aliyenaye kwa kuwa tayari wana mtoto ambaye anapenda kuwaona wakiwa pamoja, hivyo hawezi kumtesa mwanaye.

Hebu fikiria, mtoto wangu amezoea kutuona pamoja mimi na baba yake na ni kitu ambacho anakipenda sana, sasa kwa nini nimuumize?” alihoji Aunt.

Risasi Mchanganyiko baada ya kuzungumza na Aunt, lilimtafuta mzazi mwenziye huyo ili azungumzie ujio wa mume wa ndoa wa mpenzi wake, lakini alisema yeye hana cha kuzungumza, isipokuwa mwenye uamuzi wowote ni Aunt.

Unajua kwenye jambo kama hilo mtu anayeweza kuzungumza vizuri ni Aunt mwenyewe na yeye ndiye mwenye uamuzi wote, ninachojua mimi ni baba mtoto na itabaki kuwa hivyo siku zote,” alisema kijana huyo.

Angola Wamchagua Rais Mpya Baada ya Miaka 38

$
0
0
 Angola Wamchagua Rais Mpya Baada ya Miaka 38
Rais Jose Eduardo dos Santos amekuwa madarakani tangu mwaka 1979 na kuwa rais wa pili barani Afrika kuwa madarakani kwa kipindi kirefu zaidi.
Rais Santos hawanii tena uchaguzi huu, ambao waziri wa ulinzi Joao Lourenco anawania kama mgombea kupitia chama tawala cha MPLA.
.
Mpinzani wake mkuu anatarajiwa kuwa Isias Samakuva, kutoka chama cha hasimu wa MPLA, Unita
Wachangazi wanasema kuwa chama cha MPLA ambacho kimekuwa madarakani tangua uhuru wa nchi hiyo mwaka 1975, kinaokana kuwa kitaibuka mshindi.
Santos kujiuzulu kabla ya uchaguzi wa mwaka ujao

Chama cha tatu kwa ukubwa cha Casa-CE, kinaongozwa na Abel Chivukuvuku, ambaye alikuwa afisa wa cheo cha juu wa Unita wakati kilikuwa ni kundi la waasi.
Baada ya vita, Angola ilikuwa moja ya nchi zilizokuwa aa uchumi uliikua kwa haraka zaidi duniani kutona na utajiri wake mkubwa wa mafuta.

Lakini wakati bei ya mafuta ilishuka miaka miwili iliyopita iliadhiri uchumi wote.
Ikiwa asimia kubwa ya watu wako chini ya umri wa maiak 35, watu hao ndio na watakuwa na uamuzi mkubwa.

Maswali 7 Aliyojibu Mkemia Kuhusu Mkojo wa Manji Mahakamani leo

$
0
0
Mkemia kutoka Ofisi ya Mkemia Mkuu wa Serikali, Dominician Dominic leo August 23, 2017 ameieleza Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu matokeo ya uchunguzi wa mkojo wa Mfanyabiashara Yusuph Manji, kuwa yalionesha alikutwa na kemikali aina ya benzodiazepines na morphine.

Akiongozwa na Wakili wa Serikali, Timon Vitalis, Shahidi huyo alidai mbele ya Hakimu Mfawidhi, Cyprian Mkeha kuwa Februari 9, 2017 saa 5 asubuhi alipokea Askari akiwa na watuhumiwa wawili kwa ajili ya kutoa sampuli ili kupima mkojo.

1: Wakili Vitalis: Je, unakumbuka watuhumiwa kwa majina yao na Askari aliyewaleta?

Mkemia: Ndio, watuhumiwa waliofikishwa ofisini hapo ni Mchungaji Gwajima na Manji ambao waliletwa na Koplo Sospeter mwenye namba E 1135.

2: Wakili: Jinsi gani ulianza kufanya uchunguzi?

Mkemia: Kuna maliwato maalum ambayo askari anaingia na mtuhumiwa kutoa sampuli ambapo nilimpatia kontena niliyoipa namba ya maabara 367/2017 ambayo sampuli hii ilikuwa ya Manji.

3: Wakili: Je, kuna chochote kiliwasilishwa kwako na nani aliwasilisha fomu namba 001?

Mkemia: Sampuli iliwasilishwa na fomu maalum kwa mujibu wa sheria ya dawa za kulevya ambayo Koplo Sospeter ndiye aliyeiwasilisha.

4: Wakili: Je, ukiiona fomu hiyo utaweza kuitambua? Pia uieleze Mahakama baada ya kuchukua sampuli ya mkojo ulifanya nini?

Mkemia: Fomu hiyo naweza kuitambua kwa kuwa ina saini yangu na jina la Mtuhumiwa aliyeletwa kwa ajili ya uchunguzi.

“Nilifanya uchunguzi wa awali kwa kutumika kifaa kinachoitwa Diaquicky multpanel urine test na matokeo yalionesha kuwa mkojo ulikuwa na kemikali inayoitwa benzodiazepines.

Kuwepo kwa dawa hizi wakati mwingine hutumika kupunguza maumivu na matumizi mengine kulingana na daktari anavyosema.”

5: Wakili: Baada ya hatua ya kwanza ulifanya nini kwa hatua ya pili kuthibitisha dawa hizo?

Mkemia: Kemikali hizi zipo za aina nyingi lakini ili kupata majibu kama kweli anatumia dawa za kulevya nilichukua kemikali hiyo na kuunganisha na dawa za kulevya kulinganisha. Katika sampuli hii niligundua kwamba mkojo una kemikali aina ya morphine.

Alidai kemikali hiyo ya Morpine ilikuwa ndani yake na chembechembe ya dawa za kulevya aina ya heroin. Dawa hii pia hutumika hata wakati wa upasuaji mahospitalini.

6: Akiulizwa maswali na Wakili wa utetezi Ndusyepo alihoji shahidi kueleza kama mkojo ni wa Manji au Polisi?

Mkemia: Sijui kama Mkojo ni wa Manji au Polisi kwa sababu sikwenda nao maliwato wakati wa kutoa sampuli ila nililetewa sampuli na Polisi, nilikuwa nje.

7: Wakili Ndusyepo; ulitumia sampuli kiasi gani kufanya uchunguzi hatua ya pili?

Mkemia; Sampuli inayohitajika ni ujazo wa milimita 10.

Simba Waliamsha Dude Mbele ya Yanga....Waichapa Mabao na Kuchukua Ngao ya Jamii

$
0
0
Timu ya Simba imeibuka mshindi kwenye mchezo wa kufungua michuano ya Ligi Kuu Tanzania Bara (Ngao ya Jamii) baada ya kuifunga Yanga SC kwa penati 5-4.

Mchezo huo uliokuwa mkali na wa kusisimua huku kukiwa na upinzani mkubwa baina ya mahasimu hao wa jadi, ulimalizia kwa sare ya bila kufunga ndipo timu zote zikaenda matuta.

Donald Trump Jeuri..Atoa Kauli Ngumu Kuhusu Ukuta wa Mexico......

$
0
0
Trump jeuri…

RAIS Trump amewalaumu vikali wapinzani wa chama cha Democratic kuwa wanakwamisha ujenzi wa ukuta utakaotenganisha Marekani na Mexico.

Amelitaka bunge la Congress kupitisha bajeti ya ujenzi wa ukuta huo ili kuzuia wahamiaji haramu ambao wamekuwa wakiingia Marekani.

Katika hotuba yake Trump alisema Democratic wanahatarisha usalama wa raia wa Marekani kwa kukataa hoja ya ujenzi wa ukuta.

Pia alisema kuwa endapo hoja yake haitaungwa mkono, yuko tayari kusimamisha shughuli zote za serikali. Hii itatokea pale mswada kuhusu ujenzi huo utakapojadiliwa bungeni Oktoba 1 mwaka huu.

Wapinzani wa Democratic wanataka tusijenge ukuta. Lakini nawaambia niko tayari kufunga shughuli zote za serikali ili kujenga ukuta wa Mexico,” alisema Trump, kisha akaongeza, “Wananchi wa Marekani walinipigia kura ili nirekebishe sera za uhamiaji.”

Baada ya kumalizika kwa hotuba yake, polisi walikabiliana na waandamanaji ambao walipinga kauli hizo za Trump.

Mbunge wa Arusha Mjini, Godbless Lema Amekamatwa na Polisi Kwa Madai ya Kuzidisha Muda wa Mkutano‬

$
0
0
Mbunge wa Arusha mjini Mhe.Godbles Lema amekamatwa na jeshi la polisi mkoani humo kwa madai ya kuzidisha muda katika mkutano wake kwa dakika saba (07).

Polisi wanadai Lema amemaliza mkutano saa 12:7 jioni badala ya saa 12:00 kamili kama ilivyo utaratibu.

Polisi "wamemblock" Lema katika "keepleft" cha mnara wa saa kwa kusimamisha gari mbili (moja mbele na nyingine nyuma), kisha kuingia katika gari ya Lema na kumuelekeza kituo kikuu cha polisi (central).

Hali hii imesababisha foleni kubwa kwenye barabara zinazoingia katikati ya mji.

By Malisa Godlisten

Wanawake: Mumeo Akikukera Usilale Mpaka Pakuche Hamjasameheana.....

$
0
0
Usiku kama mumeo kakukera usilale mpaka pakuche hamjasameheana, hata malaika baraka hawawezi shuka kwenu. Huyo ulionae amezaliwa kwao kaja na tabia zake na wewe umezaliwa kwenu una tabia zako.

Sasa ukitaka kila kitu kiwe wewe unavyotaka atakuwa mwanao tena huyo sio mumeo samehaneni kwa kila mnalofanyiana.

Usiweke vinyongo tena ukajua unamkomoa mana unavyonuna ndo mchepuko unavopata chance ya kuwasiliana na si kila mwanaume anamchepuko wengine washkaji tu sasa ukijitia umenuna kisa umemuona kachat, sijui umekuta meseji sijui nini utakonda uzikwe na presha na unavyotiwa kaburini tu huku wenzio wanamtext pole kazi ya Mungu mpenzi.

Gangamala mtoto wa kike sio kidogo kununa kama unga wa ngano ulokosa amira. Tabasamu njia nzuri na sahihi ya kumuua mtu akikosea ukatabasamu ataanza kutafuta mchawi kumbe mchawi mwenyewe, ataanza kutoka kujua kwanini hujakasirika atatulia tu akiamini anakuvizia kumbe anajivizia.

Jipange Dada Usidhani Ndoa ni Kama Kupiga Picha Huku Umejibinua Makalio

$
0
0
Umepata bwana, umempenda kweli kweli na umemlalamikia sana eti kwanini hakupeleki kwa wazazi wake kukutambulisha, jamaa akagoma sana mwishowe akaona isiwe kesi akakupeleka.

Wewe badala hata utake hiyo advantage umefika tu siku ya kwanza umeshinda unachati, siku ya pili umeshinda unachati tena ndio unajisifia kwenye groups upo ukweni kumbe wao wanakutazama tu na kukupimia wala hawakwambii kitu.

Siku ya tatu wanakwambia leo ni zamu yako kupika, unaingia jikoni unaona kila kitu kigeni vya huku unaweka kule, vya kule unaweka huku (yaani hujui kupika chochote)

Sufuria unashika kama umeshika power bank, unapika na lipstick, mdomo mwekundu utafikiri mtoto wa jini katoka kufundishwa kunyonya damu tena huku umevaa saa, umevaa culture zimejaa nusu ya mkono, umevaa mini skirt kama wafanyakazi wa Emirates.

Msosi wa wakwe huwezi kupika. Ukiambiwa hufai kuolewa unavuta mdomo utafikiri umenyimwa USB cable ubust smartphone yako.

Unaanza kulalamika wakwe hawakupendi, unalalamika wee, unashindwa kuelewa kuwa wewe ndo tatizo.

Usitake kuolewa ukidhani mumeo atakula chips na wewe utakuwa utakula pizza kila siku, jifunze hata kuchemsha chai basi au unadhani google wataleta app ambayo unaweka USB kwenye simu yako alafu unaielekezea kwenye sahani inaproduce msosi.

#Jipange dada usidhani ndoa ni kama kupiga picha huku umejibinua makalio

Kutana na Mtabibu wa Asili Allan Shariffu Musa Mtabibu wa Nyota za Binadamu na Dawa za Asili

$
0
0


Kutana na Mtabibu Mwenye KUBRI kutoka kwa ALLAH shariffu musa Mtabibu wa Nyota za Binadamu na Dawa za Asili ya Africa Mwenye UWEZO Kubaini tatizo lako Pindi tu Utakapo Fanya Mawasilino Kupitia Wasaa Husika..JE UNASUMBULIWA NA Mapenzi? (Umeachwa na Umpendae,Awe Mume,Mke na Bado unampenda?Na Umejaribu Sehemu nyingi Bila Mafanikio?Wasilina na shariffu musa Ujione muujiza wa Papo kwa Papo.. anauwezo WA KURUDISHA MAHUSIANO NA KUIMARISHA NDOA YAKO NDANI YA SAA 12 TU. Umekimbiwa na Mumeo,mkeo au Mpenzi na anaishi na mtu mwingine? Muone akutatulie Anauwezo wa Hali ya Juu wa Kusambalatisha Mahusiano yao Endapo utafata Atakacho kuelekeza.
Atamfanya Atimize Ahadi zote kwa Muda Mfupi.

Maalim Hussein Anatumia Jina la Muhusika au Picha Kumaliza Tatizo lako..
Anatibu kwa Kutumia Vitabu vya QUR-AN Dawa za Asili za Africa,Dawa za Kiarabu na Majini.Anatafsiri Ndoto. Kushinda BAHATI NASIBU, KUSAFISHA NYOTA. Mvuto wa Mwili na BIASHARA, Kinga ya Mwili,ZINDIKO za Nyumba.MIGUU Kufa GANZI.Kufungua KIZAZI kwa wale walio fungwa kwa njia za KISHIRIKINA. Anakupa Jini la Mali kwa yule anaehitaji Utajiri BILA MASHARTI. Nguvu za KIUME, Humaliza Kesi zilishindika ndani ya siku 14 tu..na mengi zaidi

+255 629793352 au watsap
+255 679119679

NB: TIBA KWA DINI ZOTE NA IMANI ZOTE.

TFF Yaongeza Idadi ya Timu Zinazoshiriki Ligi Kuu Tanzania....

$
0
0
Kamati ya Utendaji ya Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF) litapandisha idadi ya timu zinazoshiriki Ligi Kuu msimu ujao wa 2018/19 kutoka 16 za sasa hadi 20, imefahamika.

Uamuzi huo umefanyika Jumanne Agosti 22, 2017 wakati Kamati ya Utendaji inafanya marekebisho ya Kanuni za Ligi Daraja la Kwanza inayotarajiwa kuanza Septemba 16, mwaka huu.

Kwa marekebisho hayo, timu zitakazoshuka daraja msimu ujao kutoka Ligi Kuu ya Vodacom ya sasa ni mbili hivyo kubaki 14. Na ili kufikia timu 20, timu sita (6) za Ligi Daraja la Kwanza zitapanda daraja.

Kwa mujibu wa utaratibu wa Ligi Daraja la Kwanza, timu, ina maana kwamba msimu huu timu mbili zitapanda kutoka katika kila kundi katika ligi hiyo ambayo inatarajiwa kuanza Septemba 16, mwaka huu.

Makundi ya Daraja, kundi ‘A’ lina timu za African Lyon, Ashanti United, Friends Rangers za Dar es Salaam, JKT Ruvu na Kiluvya United za Pwani, Mgambo JKT ya Tanga, Mvuvumwa ya Kigoma na Polisi Moro ya Morogoro.

Kundi ‘B’ ziko za Coastal Union ya Tanga; JKT Mlale ya Ruvuma; KMC ya Dar es Salam, Mawezi Market ya Morogoro, Mbeya Kwanza ya Mbeya, Mufundi United ya Iringa, Mshikamano na Polisi Dar za Dar es Salaam.

Kundi ‘C’ lina timu za Alliance School, Pamba na Toto

African za Mwanza, Rihno Rangers ya Tabora, Polisi Mara ya Mara, Polisi Dodoma ya Dodoma, Transit Camp ya Shinyanga na JKT Oljoro ya Arusha.

IMETOLEWA NA SHIRIKISHO LA MPIRA WA MIGUU TANZANIA

Mambo Matatu Unayotakiwa Kuyazingatia ili Ustaafu Mapema na Kuachana na Ajira ya Kuajiriwa

$
0
0

Watu wengi sana wanatamani kuwa na uwezo na uhakika wa kustaafu mapema, lakini ni wachache sana wanachukua hatua mahususi kuhakikisha wanalitimiza jambo hilo.
Ili uweze kustaafu mapema, mambo matatu yanahitajika: kipato cha uhakika, kuweka akiba na kuwekeza akiba yako.
Jambo la kuzingatia ili utimize lengo hili ni kufanya mambo hayo matatu yawe ndio kipaumbele chako maishani.
wekeza
Vijana wanajulikana kwa kuwa na tabia ya kutopenda kufata sheria, na linapokuja swala la matumizi ya pesa zao wanazozipata kwa jasho lao – wengi zaidi huwa hawataki hata ushauri kabisa.

Lakini uwezekano wa kustaafu mapema unaweza kuwafanya wengi washawishike kuachana na ubishi wao na kufikiria uhakika wa maisha yao ya uzeeni na kuanza kuchukua hatua za uhakika kuyanyoosha wangali bado vijana na wenye nguvu za kufanya kazi.

Zifuatazo ni njia hizo na jinsi ya kufanya:

1. Tengeneza chanzo imara cha mapato

Kama huna chanzo cha mapato, hutakuwa na nafasi hata ya kuanza kujenga utajiri. Hatua ya kwanza kabisa ya kuhakikisha unapata uhuru wa kipato ni kuwa na chanzo cha uhakika cha kipato ili uwe na uhakika kwamba kutokana na kipato hicho, unaweza kuweka akiba pamoja na kuwekeza kwa ajili ya maisha ya baadaye.

Kwa baadhi ya watu, hii yaweza kumaanisha ufanye kazi kwa ufanisi kwenye ajira yako ya sasa ili uweze kutimiza lengo hili. Ukiwa na chanzo cha uhakika cha mapato, hata ikiwa ni kutokana na kazi za mkataba au tenda za kulipwa kwa siku, bado unaweza kuweka mipango ya baadaye na kuanza kuitekeleza, japo kidogo kidogo.

2. Weka akiba sehemu kubwa ya kipato hicho

Ukishakuwa na kipato cha uhakika, jambo muhimu ni kuhakikisha kuwa hutumii pesa yote unayopata. Kujifunza jinsi ya kuishi maisha ya gharama nafuu chini ya kipato chako ni muhimu ili uweze kubaki na pesa (hasa ukianzia ujanani mwako) na uweze kujiwekea akiba itakayokusaidia kwa maisha yako yote yaliyobaki.

kwanza, miongoni mwa njia rahisi zaidi za kuhakikisha utakuwa na fedha uzeeni mwako ni kujiunga na mfuko wa hifadhi za kijamii. Mifuko hii itakusaidia kutoa michango yako kila mwisho wa mwezi au kwa muda maalum na kuja kuipata utakapotimiza umri wako wa kustaafu. Kwa waajiriwa, michango hii huwa inakatwa moja kwa moja kutoka kwenye mshahara wako – kwahiyo huna haja ya kuwa na wasiwasi kuhusu hilo – lakini kwa ambao hawajaajiriwa, unaweza kujiunga kwenye mifuko hii kama mtu binafsi, kwakuwa inaruhusiwa kufanya hivyo pia. Michango unayoiweka ni kiasi kidogo sana cha pesa kwa mwezi, lakini faida yake uzeeni ni kubwa.

Pia, unaweza kupunguza matumizi yako ya pesa kwa kupunguza gharama za nyumba (kama umepanga) ili kodi yako kwa mwezi isizidi asilimia 30 ya kipato chako.

3. Wekeza akiba yako kwenye vitega uchumi vitakavyoongezeka au kutopungua thamani

Kuwa na pesa nyingi kwenye akiba yako ni jambo zuri, lakini unapoiwekeza pesa hiyo yaweza kusababisha tofauti kubwa sana kwenye safari yako ya kustaafu mapema.

Kuna wanaoamua kuwekeza kwenye sekta ya majumba, na inaweza ukunufaisha kwakuwa una uwezekano wa kuingiza kipato cha kila mwezi kutokana na kodi za pango.

Kwa wale wasiovutiwa na biashara ya majumba, unaweza kujifunza na kuwekeza kwa kununua hisa za makampuni mbalimbali ambayo yana rekodi nzuri ya ukuaji.

Mwanzo wa safari ya mafanikio ya kuwa na uhuru wa kipato unaanza kwa uamuzi wako kwamba kufanya hivyo ni muhimu sana kwako. Kisha ukiwa unazingatia malengo yako, basi unaweza kutimiza kila unachokitaka bila wasiwasi.

Ugomvi wa Diamond, Alikiba na Ommy Dimpoz Wavuka Mipaka

$
0
0
Ugomvi wa Diamond na Alikiba na Ommy Dimapoz unaweza ukawa umevuka mipaka baada ya mama mzazi wa Diamond kuingizwa katika mgogoro huo, kwa namna inayoonekana ni kumkosea heshima.

Baadhi ya watu wamemkosoa Ommy Dimpoz kwa kuweka picha yake akiwa na mama Diamond katika ukurasa wake wa Instagram huku akitoa maelezo yanayoonyesha kwamba yeye ndio baba mzazi wa Diamond.

Ujumbe uliowekwa na Ommy Dimpoz unasomeka;

BARUA YA WAZI KWA BINTI YANGU MALKIA WA NGUVU

Salam zako nimezipata mwanangu Hivi kweli ww wa kukosa Adabu na kuamua kunichamba mimi Baba yako? Sasa kosa langu mimi nini?😭😭😭 Kwani kuna Ubaya kumtandikia Kitanda Baby wako King?
#UnanioneaKwaKuaSijuiKurap😭#SijuiNaMimiNimkatae🤔🤔#KamaYeyeAlivyomkataaWaMobeto #YaniUnamkataaMjukuuWangu😭#UnakubaliKuleaWatotoWa5SioWako#UmerogwaWWSioBureMwanangu #NilikuwaNajuaNimezaaSIMBA #NilikuwaNajuaNimezaaSIMBA#NilikuwaNajuaNimezaaSIMBA#KumbeNimezaaKIMBA#DavidoNaeAnalalamiKuhusuENEKA#UmeletaJanjaJanjaKwenyeFallOnU
#NnaedhalilikaMimiBabaYaKo😭😭#UtakujaKuniuaKwaPreshaJomoniiii😭#HayaNendaKatungeVesiNyingine😜
#RahaYaVitaUsichagueSilaha #BABAMALKIA

Baadhi ya watu waliokwetwa na ujumbe huo ni pamoja na aliyekuwa Meneja wa Ommy Dimpoza, Mubenga ambapo ameandika akimtaka msanii huyo kuacha kuwaheshimu wazazi na kama ameshindwa mziki basi akae pembeni.

Omary mdogo wangu maandiko yanasema waheshimu wazazi upate heri na Miaka mingi duniani na mzazi sio mpaka akuzae ata mzazi wa mwenzio pia ni mzazi wako why unamuingiza mama naseb kwenye mambo yenu? Uko ni kukosa adabu wew si unajifanyaga innocent kwa watu kumbe una pretend? Wew sindio uliyeimba nani kama mama imekuwaje leo una watusi wa kina mama? Au ndio stress za Mziki? Watu wanataka video ya cheche na sio kutusi wazazi wa watu usituaribie muziki wetu kama game imekushinda please kaa pembeni pia naomba vyama vyenye dhamana ya muziki vichukue atua kali zidi ya matusi ya omary kwa mama wa diamond ili iwe fundisho kwa wengine ya kwangu ni hayo tu!

Mbali na Mubenga watumiaji wengine wa mitandao ya kijamii wamekerwa na kitendo hicho cha Ommy Dimpoza huku wakimtaka kutoingiza wazazi kwenye ugomvi wao binafsi.

Kutokuelewana huko kati ya Diamond na wasanii wenzake wawili Ommy Dimpoz na Alikiba kumetokana na wao kuwaimba vibaya katika wimbo wa Fresh Remix.

Sababu 5 Zinazoweza Kuchangia Hedhi yako Kuchelewa Kuiona

$
0
0
Wasichana wengi huanza kutawaliwa na hofu kila wanapoona wakati wa kuonda siku zao (hedhi) umefika halafu hawaoni hali ikijitokeza.

Wengi wanapoona hali hiyo mawazo yao yote hueleka kuwa wameshashika ujauzito, lakini kumbe hali hiyo huweza kutokea kutokana na sababu mbalimbali zikiwemo hizi hapa 5 chini;-

1. Huweza kuwa ni mabadiliko ya homoni mwilini

2. Mabadiliko ya uzito wa mwili

3. Msongo wa mawazo

4. Mpangilio au mabadiliko ya mlo

5. Maambukizi kwenye via vya uzazi

Inasikitisha Ajali ya Treni na Daladala, Yaua Wanafunzi Mkoani Morogoro

$
0
0
Inasikitisha Ajal yai Treni na Daladala, Yaua Wanafunzi Mkoani Morogoro
Watu ambao idadi yake haijaweza kufahamika mara moja, wamefariki dunia na wengine kujeruhiwa, baada ya daladala waliyokuwa wakisafiria kugonga treni mkoani Morogoro.

Akithibitisha kutokea kwa ajali hiyo Kamanda wa Polisi Mkoa wa Morogoro Urich Matei, amesema ajali hiyo imetokea leo asubuhi na imehusisha gari aina ya daladala yenye amba za usajili T 438 ADR iliyokuwa inakwenda Mvumi kwenye njia panda inayoingilia treni ndipo ikagonga treni hiyo, na kuburuzwa takribani mita 200.

Kamanda Matei amesema chanzo cha ajali hiyo ni daladala kuingia kwenye njia ya treni bila kusimama ili kuangalia kama kuna treni inakuja, ndipo treni hiyo ikaburuza gari hiyo kwa umbali mrefu na kusababisha maafa hayo.

Idadi rasmi ya majeruhi bado haijafahamika rasmi mpaka sasa na majeruhi wamepelekwa hospitali ya mkoa wa Morogoro
Viewing all 104789 articles
Browse latest View live




Latest Images