Quantcast
Channel: UDAKU SPECIAL
Viewing all 104795 articles
Browse latest View live

WHO Yamteua Rais wa Zimbabwe Robert Mugabe Kama 'Balozi Mwema

$
0
0
WHO Yamteua Rais wa Zimbabwe Robert Mugabe Kama 'Balozi Mwema
Shirika la Afya duniani WHO limemteuwa rais wa Zimbabwe Robert Mugabe kama 'balozi mwema ' katika kusaidia kukabiliana na magonjwa yaliyosahaulika .

Akifafanua kuhusu uamuzi wa uteuzi huo Mkurugenzi Mkuu mpya wa WHO, Dr Tedros Adha-nom Ghebre-yesus, amesifu namna Zimbabwe inavyozingatia afya kwa umma.
Hata hivyo wakosoaji wanasema katika kipindi cha miaka thelathini na saba ya utawala wa Rais Mugabe, huduma za afya zimekuwa mbaya ambapo wahudumu wa afya wamekuwa hawalipwi mara kwa mara na kumekuwa na ukosefu mkubwa wa dawa muhimu .
Dr .Tedros, ni raia wa Ethiopia ambaye ni Muafrika wa kwanza kuongoza shirika la WHO na alichaguliwa kwa ajili ya kukabiliana na kile kilichoaminiwa kuwa ni kugeuzwa kwa shirika hilo kuwa la kisiasa.


Zitto Kabwe Awapa Makavu Wanachama wa ACT Wazalendo

$
0
0
Zitto Kabwe Awapa Makavu Wanachama wa ACT Wazalendo
Mbunge wa Kigoma Ujiji ambaye pia ni kiongozi wa chama cha ACT- Wazalendo, Zitto Zuberi Kabwe, amewataka wanachama ambao wanaamini chama hicho ni jukwaa la kuitetea serikali, kutoka ACT Wazalendo kwani sio mahali sahihi kwa wao kuwepo.

Zitto Kabwe ameyasema hayo leo alipokuwa akizungumza na waandishiwa habari katika ofisi za chama zilizopo Kijitonyama jijini Dar es salaam, na kusema kwamba kama watu hao wapo ndani ya chama, ni vyema wakaondoka kama walivyofanya wanachama wengine walioondoka ACT-Wazalendo.
“Tunawaasa wote wanaodhani kuwa chama hichi kitakuwa jukwaa la kuisifia chama tawala na serikali, hili sio jukwaa sahihi kwao, wajitathimini ama kuendelea na uanchama au wajivue kama walivyofanya wenzao”, amesema Zitto Kabwe.
Kauli hiyo ya Zitto Kabwe imekuja siku chache tangu aliyekuwa Katibu Mkuu wa Chama hicho Samson Mwigamba, kujiunga na chama cha CCM

'Vempire' Waibuka Afrika

$
0
0
'Vempire' waibuka Afrika
Nchini Malawi kumekua na taarifa za kuwepo kwa watu wanaonyonya damu (vempire) na kuibua hali ya hofu kwa wakazi wa nchi hiyo hasa wanaoishi vijijini, huku kukiwa na vurugu kubwa zinazosababisha mauaji ya watu.

Matukio hayo yaliibuka mwezi Septemba ambapo baadhi ya watu akiwemo mmoja wa wabunge nchini humo, kuthibitisha kuwepo kwa wanyonya damu hao wanaohusishwa na imani za kishirikina, akieleza kwamba watu hao wana vyuma ambavyo watu wakiviangalia hupoteza nguvu.
Rais wa nchi hiyo Peter Mutharika amewataka wananchi kuacha mara moja vitendo vya kujichukulia sheria mkononi na kuua watu, huku akiwaonya wanyonya damu hao kuacha mara moja matendo hayo ya imani za kishirikina, na atapambana nao akisema vimeisikitisha serikali ya nchi hiyo.
Kufuatia vitendo hivyo watu 8 mpaka sasa wameuawa kwa kupigwa na makundi ya watu, wakiwahusisha na vitendo vya unyonyaji damu, huku mmoja wao akichomolewa kwenye kituo cha polisi alikowekwa na kupigwa mawe na wananchi mpaka kufa.
Nao Umoja wa Mataifa umeondoa baadhi ya wafanyakazi wake kwenye maeneo ambayo yana vurugu zaidi, na kuwaamuru kuhamia sehemu salama zaidi.
Matukio ya vitendo vya unyonyaji damu yaliwahi kuibuka mwaka 2002, huku yakihusishwa na ushirikina kutoka nchi jirani ya Msumbiji.

Rais Kenyatta, Jaji Maraga Wakutana kwa Mara ya Kwanza

$
0
0

Rais Kenyatta, Jaji Maraga Wakutana kwa Mara ya Kwanza
Rais Uhuru Kenyatta na Jaji Mkuu David Maraga jana walikuwa kivutio cha aina yake wakati walipokutana kwa mara ya kwanza na kupeana mikono tangu kufutwa kwa matokeo ya uchaguzi wa Agosti 8.Rais Kenyatta amekuwa akimkosoa Jaji Maraga kutokana na uamuzi wake wa kubatilisha matokeo hayo yaliyompa ushindi.
Lakini wawili hao walikaa katika jukwaa moja wakati wa maadhimisho ya Siku ya Mashujaa na kivutio zaidi kilionekana wakati Rais Kenyatta alipoanza kuwasalimia viongozi waliokaa jukwaa kuu na hatimaye kukutana na Maraga.

Walipeana mikono huku kila mmoja wao akionyesha sura ya tabasamu. Tukio hilo liliwavutia wengi huku vyombo vya habari vikionekana kulipa uzito zaidi. Nao viongozi waliokuwa wameketi meza kuu waliwageukia wawili hao wakistaajabu kuona jinsi walivyopeana mikono.

Mara kadhaa Rais Kenyatta amekuwa akisikika akimshambulia waziwazi Jaji Maraga na kudai atashughulika naye baada ya uchaguzi wa marudio uliopangwa kufanyika Oktoba 26 kukamilika.

Katika kile kilichodhihirisha mvutano huo ulikuwa mkubwa Jaji Maraga na watendaji wake walikacha kuhudhuria sherehe ya uzinduzi wa bunge zilizofanywa na Rais Kenyatta.

Sherehe hizo za jana zilihudhuriwa pia na Naibu Jaji Mkuu, Philomena Mwilu. Pia, walikuwemo Makamu wa Rais William Ruto na spika wa bunge Justin Muturi.

Kambi ya Nasa inayoongozwa na Raila Odinga ambaye amesusia uchaguzi wa marudio hawakuhudhuria.


Jeshi la Polisi Linamshikilia Mganga wa Kienyeji Tuhuma ya Kunajisi Wtoto 14

$
0
0
Jeshi la Polisi Linamshikilia Mganga wa Kienyeji Tuhuma ya Kunajisi Wtoto 14
Jeshi la Polisi mkoani Singida linamshikilia mganga wa kienyeji mkazi wa mtaa wa Minga, Daud Idd (74), kwa tuhuma ya kunajisi watoto 14 wenye umri kati ya miaka saba na 12 na kuwasababishia maumivu makali katika sehemu zao za siri.

Mgonga huyo maarufu kama Babu Karatu ameelezwa kuwa alikuwa akishirikiana kutenda vitendo hivyo na mtoto wa mdogo wake aitwaye Abdallah Yahaya (31).

Akizungumza na waandishi wa habari ofisini kwake leo Jumamosi, kaimu kamanda wa polisi mkoani hapa Isaya Mbughi amesema mtuhumiwa anadaiwa kutenda makosa hayo kwa nyakati tofauti kati ya Desemba mwaka jana, hadi Oktoba mwaka huu.

Amesema kuwa mwathirika mmoja mwenye umri wa miaka saba siku ya Oktoba 16 mwaka huu saa 11.45 jioni wakati akiogeshwa na mama yake alilalamika kuwa anasikia maumivu makali katika sehemu yake ya siri.

Amesema baada ya binti kuyo kulalamika kwa mama yake mama huyo aliweza kumchunguza kwenye sehemu zake za siri na kubaini kuwa michubuko inayotokana na kuingiliwa kimwili.

“Mama huyo baada ya kuona michubuko hiyo kwenye sehemu za siri za binti yake alimhoji mtoto wake na mtoto huyo aliweza kumtaja mganga wa kienyeji Karatu. Mwaathirika huyo alienda mbele zaidi na kumweleza mama yake kuwa si yeye pekee hufanyiwa vitendo hivyo, bali wapo watoto wengi wamefanyiwa.”

Kaimu kamanda huyo amesema baada ya hapo mama huyo alitoa taarifa kwa mwenyekiti wa mtaa wa Minga na kisha yeye na mwenyekiti wa mtaa waliweza kuongozana hadi kituo cha kati cha polisi mjini hapa.

“Jeshi la polisi liliweza kuwakamata watuhumiwa hao ambao wanaishi katika nyumba moja, kwa tuhuma ya ubakaji. Uchunguzi wa awali umebaini kuwa watoto waliofanyiwa unyama huo wanasoma katika Shule za Msingi Singidani, Nyerere na Mughanga,” amesema.

Mbughi amesema mbinu iliyokuwa inatumika kuwanasa watoto hao wa ni kuwarubuni na kisha kuwaonyesha video/movie, kwenye kompyuta mpakato.

“Wakati watoto hao wa kike wakiendelea kuangalia video sebuleni, mtuhumiwa huyo alikuwa akichomoa mmoja na kuingia naye chumbani na kumwingilia kimwili. Wachache alikuwa akiwachezea sehemu zao za siri. Baada kuingiliwa kimwili watoto hao walikuwa wakipewa zawadi ya shilingi mia mbili au shilingi 2,000,” amesema.


Hii Hapa Safari ya Music ya Rosa Ree

$
0
0
Hii Hapa Safari ya Music ya Rosa Ree
Staili ya kubinua midomo iliyokolea rangi nyeusi, mitindo ya nywele ya aina yake na vivazi vinavyoacha sehemu kubwa ya mwili wake vinamtambulisha vyema Rosa Ree.

Rapa huyo anayewakilisha kina dada katika gemu alitambulishwa na ngoma yake ya kwanza One Time akiwa tayari ameshaingia mkataba na lebo ya The Industry.

Mwanadada huyo ambaye jina lake halisi ni Rosary Robert Iwole kama wanamuziki wengine naye safari yake imeanzia mbali. Mwenyewe anasema haikuwa rahisi kama tembo kulitafuna bua…ilijaa mabonde na milima.

Mpaka sasa ameachia ngoma tatu ambazo zinakimbiza ambazo ni One Time, One Time remix ambayo alifanya na rapa kutoka Kenya, Khaligraph Jones, Up In The Air na kazi ya Mchaga Mchaga ambayo amewashirikisha mabosi zake kundi la Navy Kenzo.

Dili na The Industry?

“Muziki nilianza muda mrefu, yaani tangu nikiwa shule na tena nilikuwa naimba. Kuna ngoma kadhaa nilitoa ambazo nilikuwa naimba lakini hazikufanya poa,”

“Nilianza kuchana nikakuta watu wanapenda sana nikaamua kukaa humo. Mwaka 2015 nilienda kwa Nahreel kurekodi ngoma alivyonisikia tu alipenda sana. Baadae aliniomba niwe kwenye lebo yake nilifurahi sana kwanza halafu sikuamini lakini ikawa hivyo nikasaini hapo, mpaka sasa napiga mzigo,”

Mishe nyingine?

“Mimi nafanya biashara pia lakini mambo yangu mimi napenda kuyaweka kwa siri hivyo siwezi kusema ni biashara gani mpaka mambo yangu fulani yatimie,” aliongeza.

Nini kinafuata baada

ya Mchaga Mchaga?

“Baada ya Mchaga Mchaga kuna ngoma kali inakuja yani hapa nasubiri tu wakati uwadie kitu tukiachie, pia, nafikiria kutowachosha mashabiki zangu sababu nataka kuachia ngoma kali kwa kila kipindi fulani,” alisema.

“Na pia kuhusu video ya Mchaga Mchaga mipango bado ipo inafanyika ili kuja na kitu tofauti kama unavyojua Rosa Ree tangu nitoke kwenye upande wa video nikiri sijawahi kuzingua na hivyo najipanga kuja na jiwe kali sana.” Kolabo na Rapa wa Kenya?

“Aisee hii kolabo nikiri imenipa mafanikio makubwa sana,kwanza imeniongezea sana mashabiki kwa upande wa Afrika Mashariki kwa ujumla na mafanikio mengine ambayo siwezi kuyaweka wazi ila kiukweli nimepata mafanikio niliyotarajia,” Amesema.

Staili yake vipi?

Moja ya jambo kubwa ambalo mara kadhaa amekuwa akikumbana nalo ni watu kadhaa wamekuwa wakimkosoa hasa staili yake ya mavazi wakidai yapo nje ya maadili ya Kitanzania pamoja na matumizi ya maneno katika nyimbo zake ambayo yamejaa matusi sana.

“Mimi sifikirii hata kidogo kubadilika sababu eti kwa maneno ya watu sababu kuwa orijino ndicho kitu cha msingi halafu ukifuata kila kitu watu wanasema ni kazi sana kufanikiwa cha msingi mi sitobadirika bali nitazidi kuwa bora zaidi sababu naamini kuna watu wanapenda ninachokifanya,”

Watu wasichojua

kutoka kwake?

“Kuna vingi wengi hawajui kutoka kwangu, huwa wanaweka vitu vyao kutokana na namna wanavyoniona, lakini kiukweli mimi napenda sana sana watoto na situmii kilevi chochote kuna watu huwa hawaamini lakini ukweli ndio huo,”

Kama si Muziki basi angekuwa anafanya nini?

“Ningekuwa daktari aisee kama sio muziki maana ni kitu ambacho kilikuwa akilini mwangu kwa hiyo kama nisingekuwa nafanya muziki basi ningekuwa nachakarika na wagonjwa Hospitalini,”

Shoo ambayo hatokuja

kusahau.

“Sitokuja kusahau shoo ya “Castle Lite Unlock” ki ukweli shoo nyingi huwa napata shangwe sana ila hiyo shoo nakumbuka nilipafomu wimbo wa Mchaga Mchaga ambao ulikuwa bado haujatoka na watu walikuwa wakiitikia ilinipa sana nguvu asikwambie mtu,”

Vitu ambavyo hapendi

kuja kuvifanya kabisa

“Kitu ambacho sifikiri kabisa kuja kufanya ni siasa,mimi sipendi kabisa siasa na sifikiri kabisa sijui kwa mbele itakuaje ila akili yangu inaniambia hivyo kwamba Rosa Ree siasa wewe kwako haipo,”

Albamu na Mixtapes

(Kanda Mseto) vipi?

“Mipango ipo sema nafikiri bado mashabiki zangu wanahitaji singo zaidi ili kuwatengenezea nafasi ya kuja kufurahia albamu yangu ila mipango ipo na pindi itapowadia watu wataona.”

Watendaji Watano wa Mamlaka ya Vitambulisho vya Taifa (Nida) Wafikishwa Takukuru

$
0
0
Watendaji Watano wa Mamlaka ya Vitambulisho vya Taifa (Nida) Wafikishwa Takukuru
 Katibu Mkuu wa Wizara ya Mambo ya Ndani, Meja Jenerali Projest Rwegasira amewafikisha watendaji watano wa Mamlaka ya Vitambulisho vya Taifa (Nida) kwenye vyombo vya uchunguzi.

Hatua hiyo ni utekelezaji wa agizo alilopewa na Kamati ya Bunge ya Hesabu za Serikali (PAC) iliyomtaka kuwafikisha watendaji hao kwenye Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa (Takukuru), Mkurugenzi wa Upelelezi wa Makosa ya Jinai (DCI) na Mkurugenzi wa Mashtaka (DPP).

Akizungumza na gazeti hili jana ikiwa ni siku ya mwisho ya agizo hilo, Jenerali Rwegasira alisema: “Nimepeleka huko kama nilivyotakiwa, kazi yangu ya kutekeleza maagizo hayo nimefanya.”

Wakati Rwegasira akiwafikisha katika vyombo hivyo vya uchunguzi, ameshauriwa kujiuzulu kufuatia ubadhirifu wa mabilioni ya fedha yaliyofanywa na taasisi anazozisimamia.

Taasisi hizo ambazo Jenerali Rwegasira ni ofisa masurufu ambazo ziliitwa na kamati hiyo kwa ajili ya mahojiano kufuatia ripoti ya Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali (CAG) kubaini madudu hayo ni; Polisi, Idara ya Uhamiaji na Nida.

Jenerali Rwegasira na maofisa wa idara hizo kwa siku tatu mfululizo wamekuwa katika kiti moto mbele ya PAC ambayo inapitia ripoti ya mwaka 2015/16 kwa taasisi hizo.

Ashauriwa kujiuzulu

Akichangia hoja katika kamati hiyo jana Mbunge wa Mtera, Livingstone Lusinde alimshauri Jenerali Rwegasira kuomba kuondolewa kwa kuwa uchafu huo utamharibia sifa aliyoijenga kwa miaka mingi.

Mbunge huyo alisema Jenerali Rwegasira amefanya kazi kubwa kwenye nchi tena ya kutukuka, ni vyema kukabidhi kazi yake kwa Rais kama watu wa taasisi hizo wasipojirekebisha. “Haya madudu matatu ya Nida, Polisi na Uhamiaji yanaweza kukuchafulia sifa yako kwa sababu vitu vinavyofanywa huko nje si rahisi kwa Katibu mkuu kujua.”

Naye Mbunge wa Iramba Mashariki, Allan Kiula alisema Katibu mkuu amefanya kazi iliyotukuka kuna mambo hayaendi vizuri na kwamba si yeye anayesababisha lakini baadhi ya watendaji wa chini yake ni tatizo.

Hata hivyo, Mwenyekiti wa PAC, Naghenjwa Kaboyoka alisema majibu yaliyotolewa kwenye hoja za ukaguzi wa fungu hilo ni hafifu.

“Fedha inayozungumziwa ni mabilioni yametumika vibaya na kwa uzembe, inaonyesha Polisi kumekuwa na uzembe wa hali ya juu kuna watu wamejiwekea wigo… hawa waliostaafu si ajabu wameacha mizizi ambayo ndiyo inayotufikisha hapa,” alisema.

Kwa upande wake Jenerali Rwegasira alisema wameona kuna upungufu mkubwa na katika kujibu hoja wameonekana hawakidhi kiu ya wajumbe.

“Tunakwenda kuyafanyia kazi haya na maelekezo yaliyotolewa hapa ukweli unaonekana, tutakwenda kuelezana ukweli na kutekeleza maagizo haya na tutachukua hatua kadri tulivyoona,” alisema.


Korea Kaskazini: Silaha za nyuklia ni 'Maisha Yetu'

$
0
0
Korea Kaskazini: Silaha za nyuklia ni 'maisha yetu'
Mjumbe wa Korea Kaskazini amesema kuwa silaha za kinyuklia za taifa hilo haziwezi kujadiliwa.
Choe Son Hui amesema kuwa Marekani inafaa kujiandaa kuishi na Korea Kaskazini yenye silaha za kinyuklia.
Amesema kuwa ndio njia pekee ya kuwa na amani ya kudumu kati rasi ya Korea.
Mkurugenzi wa shirika la kijasusi nchini Marekani Mike Pompeo awali alikuwa ameonya kwamba Korea Kaskazini inaweza kuishambulia Marekani na kombora la kinyuklia katika kipindi cha miezi michache ijayo.
Korea Kaskazini imesema kuwa tayari ina uwezo huo.
Bwana Pompeo amesisitiza kuwa Washington bado inataka kutatua swala hilo kidiplomasia na vikwazo lakini ikasema inaweza kulazimika kutumia nguvu.
Akizungumza katika kongamano la kuzuia kuenea kwa silaha za kinyuklia mjini Moscow, bi Choe alisisitiza matamshi yaliotolewa awali na maafisa wa Korea Kaskazini kwamba silaha za kinyuklia ni swala la ''maisha na kifo'' kwa taifa hilo.
Mapema mwaka huu, aliripotiwa akisema kuwa taifa hilo liko tayari kufanya majadiliano na Marekani iwapo mazingira yataruhusu.
Lakini siku ya Ijumaa bi Choe alisema kuwa Korea Kaskazini itaangazia utekelezwaji wa maamuzi ya vikwazo vya Umoja wa mataifa akivitaja kuwa ni hatua ya uchokozi na vita.
Tangu Korea Kaskazini ilipoanza kufanyia majaribio makombora yake mwaka huu, vikwazo dhidi ya taifa hilo vimeongezeka.
Serikali ya Australia ilisema siku ya Ijumaa kwamba ilipokea barua kutoka Korea Kaskazini ambayo pia ilikuwa imetumwa kwa mataifa mengine ikiitaka Australia kutoshirikiana na Marekani.
Siku ya Alhamisi bwana Pompeo alionya kuwa makombora ya Pyongyang yalikuwa yanapiga hatua kwa kasi hivyobasi kuwa vigumu kwa majasusi wa Marekani kuwa na hakika kuhusu ufanisi wake, lakini akasema watagundua hivi karibuni

Sikiliza na Pakua Upo Hapo ya Mwana FA, AY na FID Q Kupitia Mkito APP Upate Punguzo la 50%

$
0
0
Ngoma kali ya wakali na legends wa Bongo Fleva nchini Tanzania ambao pia wanatamba nje ya Tanzania, Hamis Mwinjuma, Ambwene Yessaya na Fareed Kubanda inayokwenda kwa jina la “UPO HAPO” inapatikana exclusively kupitia Mkito App ambayo imezinduliwa rasmi hiyo jana na inapatikana kwenye Playstore http://bit.ly/-Mkito-Android-App

Mkito App inakuwezesha kusikiliza na kupakua nyimbo za wasanii wa ndani ya Tanzania na wa Kimataifa BILA KIKOMO katika ladha tofauti kama Afrobeat, Genge, Bongo Flava, Swahili Rap, Fusion, Jazz, Singeli, Taarab, Zouk, Soul, Reggae, muziki wa jadi, Beats, Mashairi na maudhui mengine ya sauti - popote ulipo.


Katika jambo ambalo Mkito wamefanya poa sana ni kuiwezesha App hiyo kucheza nyimbo ambazo umezitunza kwenye simu yako au au kadi ya kumbukumbu na kuhakikisha kuwa mzuka unaendelea popote unapoenda! Ipakue leo ufurahie kile ambacho umekuwa ukikosa.

Jinsi ya kupata Punguzo kupitia Coupon
1. Pakua Mkito App kwenye simu yako
2. Jisajili kwa kupitia barua pepe au akaunti ya mtandao wa kijamii
3. Ongeza salio kwenye akaunti yako ya Mkito (MPesa/Tigo Pesa/Paypal)
4. Jiunge na kifurushi (Ingiza code “UPOHAPO” unapojiunga upate punguzo la 50%)
5. Furahia muziki bila kikomo popote ulipo

Haya ni baadhi ya matukio katika uzinduzi wa video hiyo ya UPO HAPO uliofanyika Tips Bar Mikocheni.




Kutana na The Great Maalim Hussein Aweze Kutatua Matatizo yako Kwa Tiba za Asili, Dua na Nyota..

$
0
0

THE GREAT MAALIM HUSSEIN
Wasiliana na Mtaalam Huyu Kwani yeye hufaulu Pale wote waliko Shindwa na Pia Humaliza kazi zilizo Shindikana ama Zilizo Achwa ndani ya Siku Moja 1.
Maalim Hussein ANAWASHUKURU WALE WOTE WANAOPIGA SIMU ZA SHUKRANI NA KUTOA SHUHUDA JINSI TIBA ZAKE ZINAVYO SAIDIA(Rudisha Mahusiano yako Ndani ya Saa 12 tu)

MAALIM HUSSEIN ni Mtabibu wa Nyota za Binadamu na Dawa za Asili Mwenye Uwezo wa Kubaini Tatizo lako tu Pindi Utakapo Fanya Mawasiliano Kupitia Wasaa Husika.
(NA ANATIBU KWA NJIA YA SIMU UKIWA NCHI YOYOTE MKOA WOWOTE ENDAPO UTAFATA MAELEKEZO YAKE..)

Je Unasumbuliwa na Mapenzi..?
Umeachwa na UMPENDAE Awe Mume/Mke na Bado Unampenda
Je Umejaribu Sehemu Nyingi Bila Mafanikio?
Mpigie Simu sasa Hivi Ujionee Muujiza wa Papo kwa Papo..
Anauwezo wa Kurudisha Mahusiano yako na Kuimarisha NDOA Ndani ya saa 12 tu.
Je Umekimbiwa na Mumeo/Mkeo au Mpenzi na Anaishi na Mtu Mwingine..?
Muone akutatulie Anauwezo wa Hali ya Juu wa Kusambalatisha Mahusiano yao (Mfarakano/Kimavi) Endapo Utafata Atakacho Kuelekeza.
Je Una Mpenzi wako ana Pesa na unataka Kumkamata? Muone Maalim Hussein Atamfanya Atimize Ahadi zote Ndani ya Muda Mfupi..
Maalim Hussein Anatumia Jina La Muhusika au Picha Kumaliza Tatizo..
Anatibu Kutumia QUR_AN DAWA ZA ASILI YA AFRICA, Dawa za KIARABU NA MAJINI..
ANATAFSIRI NDOTO. ANAPANDIKIZA NYOTA YA KUSHINDA BAHATI NASIBU, KUSAFISHA NYOTA NA KUKUPA MVUTO WA AJABU, KUTOA NUSKI NA VIFUNGO MBALIMBALI.

ZINDIKO ZA NYUMBA NA BIASHARA.. PETE ZA BAHATI.. HUMALIZA KABISA TATIZO LA NGUVU ZA KIUME NA KUREFUSHA UUME KWA SAIZI UNAYOTAKA. HUZUIA CHUMA ULETE KWENYE BIASHARA. HURUDISHA MALI ZILIZOPOTEA..
MAGONJWA SUGU, MIGUU KUWAKA MOTO AU KUFA GANZI, HUTIBU BUSHA BILA KUPASUA..ANAO UWEZO WA KUMRUDISHA  ALIE MBALI AU ALIECHUKULIWA MSUKULE..

Humaliza Kesi ya Aina Yoyote Ndani ya Siku 7 tu..

Hutoa Jini la MALI kwa wale Wanao Hitaji Utajiri Bila Masharti..
+255 674 835 107

Nicki Minaj atajwa kweye kesi ya kaka yake

$
0
0
 Nicki Minaj ametajwa kuwa shahidi katika kesi ya ubakaji inayo mkabili kaka yake Jelani Maraj.

Kwa mujibu wa Page Six, wakili wa Jelani ‘David Schwartz’ amesema kesi hii ni njama za kupata fidia ya dola milioni 25 kutoka kwa familia ya Nicki Minaj.

Mama wa mtoto anayelalamika kubakwa Jacqueline Robinson, alimwambia Nicki kuwa anaweza kufuta kesi kama watalipwa dola milioni 25.

Ndani ya siku chache tu baada ya Jacquelin kufunga ndoa na Jelani ndipo mtoto wake wa miaka 11 alianza kusema baba yake amembaka mara nne kila wiki.

Biti huyo alikuwa na miaka 8 alivyoanz kufanyiwa hivyo vitendo, DNA ya kaka yake Nicki Minaj ilikutwa kwenye nguo za kulala za mtoto huyo huku wakili wa Jelani akidai kuwa iliwekwa hapo na mama yake mzazi ili kupata pesa kutoka kwa Nicki Minaj.

Kaka yake Nicki amekataa mashtaka yote haya toka alivyokamatwa December 2015.

Polisi wapambana na vijana

$
0
0
 Polisi juzi ni kama walikuwa wanacheza mchezo wa kujificha na kuibuka ili kupambana na vijana wenye hasira waliovamia nyumba ya mbunge wa Jinja Mashariki, Nathan Igeme Nabeta kwa lengo la kutaka kuichoma moto.

Vijana hao wanamshutumu mbunge wao kwa kupuuza matakwa yao badala yake mbunge huyo amekwenda kuunga mkono mswada tata wenye lengo, pamoja na mambo mengine kuondoa ukomo wa umri wa rais kwenye Katiba ya Uganda.

“Tunamuona mbunge wetu kila siku kwenye TV akizunguka kufanya mashauriano na umma juu ya kampeni ya kuondoa ukomo wa umri wa rais, lakini mbunge huyu hajatenga muda kuja kwetu azungume nasi kuhusu mada hiyo,” alisema Paul Onyango, mmoja wa vijana hao.

Tayari vijana hao walikwisha kufika kwenye nyumba ya mbunge huyo na kuanza kuchoma matairi kwenye lango la kuingilia kabla polisi hawajafika na kuwatawanya. Polisi hao ndio walianza kufanya kazi ya kuzima moto huo.

Naibu kamanda wa polisi wa mkoa wa Kiira Onesimus Mwesigwa alithibitisha kutokea kwa tukio hilo juzi na kwamba mtuhumiwa mmoja amekamatwa na wengine wanasakwa.

Mjini Mbale, Polisi walimtia ndani katibu mkuu wa Forum for Democratic Change (FDC), Nathan Nandala Mafabi kwa madai ya kuchochea vurugu baada ya kuongoza maandamano kupinga Marekebisho ya Katiba yenye lengo la kufuta ukomo wa umri wa rais.

Nandala alikamatwa Ijumaa, mita chache kutoka kampasi ya Chuo Kikuu cha Kiislamu cha Mbale alipokuwa anaelekea kwenye jimbo lake akiwa amefuatana na kikundi cha wafuasi wake.

Hadi jioni Nandala bado alikuwa anashikiliwa katika kituo cha polisi cha Mbale pamoja na wenzake wawili waliotambuliwa kuwa ni Emmanuel Masaba na Abdulah Magambo.

Nandala ambaye ni mbunge wa Budadiri Magharibi wilaya ya Sironko alitarajiwa kufanya mkutano wa mashauriano jana Jumamosi.

Msanii bongo Movie amuomba Rais Magufuli

$
0
0
Muigizaji wa filamu bongo Shamsa Ford amemuangukia Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli, na kumtaka alegeze kidogo kamba ili hali ya maisha ikae sawa kiuchumi.

Kwenye ukurasa wake wa instagram Shamsa ameandika ujumbe akisema hali siku hizi imekuwa ngumu kiasi cha watu kushindwa kufanya yale waliyoyazoea kwenye maisha yao ya kila siku, hata biashara imekuwa ngumu zaidi, na kama kunyooka ilipofikia imetosha.

"Mr President tunaomba ulegeze kidogo hali mbaya baba, tumeshashika adabu sasa hivi na tunaheshimu pesa .Buku sasa hivi tunaiita elfu moja, yaani sijapata hata mialiko ya birthday kubwa kubwa kama ambavyo wanafanyaga. Mbwembwe hakuna tunaishia kupostiana instagram tu.

Baba naomba usikie kilio changu hali mbaya sitaki kurudi iringa kulima mjini patamu jamani. Biashara imekuwa ngumu sana wateja hakuna jamani ...Baba Tuonee huruma jamani tumepauka kweli yaani mpaka ukimuona mwenzio unakimbia", ameandika SHamsa Ford.

Shamsa Ford ambaye kwa sasa ameolewa na mfanya biashara maarufu hapa mjini, amekuwa kimya kwenye sanaa kwa kutotoa kazi mpya kama ambavyo alizoeleka, hali inayozidi kuibua sintofahamu kama inasababishwa na ukata ama la.

TAKUKURU yalalamikiwa Kagera

$
0
0
Mkazi mmoja  wa kijiji cha Nyambale wilaya ya Biharamulo mkoani Kagera ameilalamikia Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa TAKUKURU kwa kushindwa kumkamata Mkuu wa Kituo cha Polisi Lusahunga anayedaiwa kuomba rushwa ya shilingi Milioni moja ili

aweze kuziachia ng'ombe 20 alizozikamata wakati zikipelekwa mnadani kwa madai kuwa hazikuwa na vibali vya kusafirishwa.

Akibainisha hayo mbele ya kamera za ITV Bi Bilatwa Mabuga katika kijiji cha Kibale na kusema kuwa tukio hilo limetokea wakati akisafirisha mifugo yake kutoka wilaya ya Kasulu mkoani Kigoma kwenda kwenye mnada wa katoke wilaya ya Biharamulo mkoani Kagera.

Kwa upande wake Mwenyekiti wa kitongoji cha Kabumbilo Bw.  Paul Mussa aliyehusika kuwadhamini watuhumiwa amethibitisha kutokea kwa tukio hilo huku Katibu wa Chama cha Mapinduzi wilaya ya Biharamulo Bi. Joyce Massi amelaani vikali unyanyasaji uliotokea.

Akijibu malalamiko hayo kwa masharti ya kutopigwa picha Mkuu wa TAKUKURU wilaya ya Biharamulo Bw.Hassan Mossi amekiri kupokea malalamiko ya mfugaji huyo

Birdman kutua Tanzania

$
0
0
Mmiliki wa lebo ya Cash Money, Birdman amethibitisha mpango wake wa  kutua nchini mapema mwakani ikiwa ni sehemu ya ziara kwenye nchi tano za Afrika.

Rapa huyo wa  Marekani, mapema wiki hii ameandika katika akaunti yake ya Instagram kuwa atafanya ziara licha ya kutoeleza ni kwa ajili ya muziki au la!

Mkongwe huyo wa Hip Hop amesifu upendo na mapokezi makubwa wanayopata kutoka nchi za Afrika ikiwamo Tanzania.

Mbali na Tanzania amezitaja nchi nne ikiwamo Nigeria, Gambia, Ghana na Kenya na kuandika “Nitatembelea kwenye nchi hizi kuanzia Februari.

Birdman ameingia katika mzozo na rapa, Lil Wayne ambaye amekuwa akimtuhumu bosi huyo kuchelewesha kutoa albamu yake “Tha Carter V”.

Bifu hilo limeendelea kuwa kubwa huku baadhi ya mastaa akiwamo Rick Ross kumtaka Birdman amlipe fedha Lil Wayne licha ya meneja huyo kuwa mbogo.

Mbali na Weezy, lebo hiyo iliyojipatia umaarufu kutokana na kuzalisha mastaa wakubwa akiwamo Drake, Nicki Minaj na Tyga.

Ufafanuzi Watolewa Kuhusu Gari Alilotumia Makonda Akiwa Zanzibar

$
0
0

Mkuu wa Mkoa wa Mjini Magharibi, Ayoub Mahmoud ameeleza kusikitishwa kwake na taarifa zisizo za kweli zinazosambazwa kwenye mitandao ya kijamii na baadhi ya vyombo vya habari kuhusu gari alilolitumia Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam, Paul Makonda alipokuwa ziarani mkoa humo.

Mahmoud ameyasema hayo kupitia ukurasa wake wa Instagram, baada ya kuwepo kwa taarifa mbalimbali kuhusu gari aina ya Range Rover ambayo ilikuwa na namba za usajili zinazoonyesha kuwa ni la RC Dar es Salaam.

“Unaweza ukasikitishwa sana pale unapoona chombo kinacho aminiwa kwenye maswala ya habari kuwa ni chanzo cha upotoshaji!. No research no right to speak !.”

RC Mahmoud aliendelea kueleza kuwa, “Hii sio gari ya serekali au ya ndugu yangu Paul Makonda! Kilichokuwepo ni nini? In fact hakuna asojua kuwa ndugu yetu Paul yuko Zanzibar na Mimi nikiwa kama mwenyeji wake ndani ya mkoa wangu!.”

RC Mahmoud alisema kwamba, kinachosumbua watu kuhusu gari hilo, ni watu kutokufahamu taratibu zinazo wahusu viongozi hao.

“Hii ni gari ya mtu binafsi imetumika kwa mdaa wakati ule wote wa Mkuu wa mkoa wa dar es Salaam kuwa zanzibar katika kilele cha mbio za mwenge na maadhimisho ya kifo cha Baba wa taifa pamoja na ziara yake katika mkoa wa mjini magharibi!.”

Kwa upande wake RC Makonda alisema kwamba, sio kwamba watu wanaozusha habari hizo hawajui ukweli, bali wanakerwa na upendo ambao ameonyeshwa na kiongozi huyo akiwa ziara Mjini Magharibi.

“Mhe Rc na Kaka yangu mpendwa @ayoubmahmoud_ . Hawa Watu wanajua wanachokifanya na wanaelewa kabisa kwamba nilikuwa Zanzibar. Wanachoumia ni upendo na ukarimu wako na watu wako wa unguja kwangu. Tuchape kazi maneno niya

Nkamia ampongeza Rais Magufuli kuhusu majadiliano na Barrick Gold

$
0
0
Mbunge wa Chemba (CCM), Juma Nkamia amesema Serikali inastahili pongezi kwa majadiliano yake na kampuni ya Barrick Gold yanayohusu uwekezaji kwenye madini.

Alhamisi iliyopita, Rais John Magufuli alipokea ripoti ya mazungumzo kati ya Serikali na kampuni mama ya Acacia, Barrick Gold iliyoeleza makubaliano yaliyoafikiwa ili kuendelea na uchimbaji wa dhahabu nchini, ikiwamo kulipa Dola 300 milioni za Marekani (zaidi ya Sh660 bilioni).

Lakini siku moja baada ya taarifa hiyo, ofisa mwandamizi wa fedha wa Acacia, Andrew Wray alisema kampuni hiyo haina uwezo wa kulipa kiasi hicho.

Kwa mujibu wa taarifa zilizoripotiwa na vyombo tofauti vya habari vya kimataifa, uongozi wa Acacia umesema hauna uwezo wa kulipa kiasi hicho cha fedha.

“Hatuna huo uwezo kuilipa Tanzania ili tumalizane kwenye mgogoro wa kodi uliopo,” alikaririwa ofisa mkuu wa fedha wa kampuni hiyo, Wray.

Pamoja na changamoto zilizopo, Nkamia alisema hatua hiyo bila kujali tofauti ya itikadi kutokana na vyama vilivyopo, Watanzania wanapaswa kumpongeza Rais Magufuli.

“Serikali imefanya kazi nzuri. Hata kama humpendi mtu, mpongeze akifanya vizuri,” alisema Nkamia.

Miongoni mwa makubaliano ya Serikali na Barrick Gold ni kwamba sasa pande hizo mbili zitakuwa zikigawana faida asilimia 50 kwa 50.

Mwananchi:

Kenya: Mabaki ya ndege aina ya helikopta iliyoanguka haijapatikana

$
0
0
Majina ya watu waliokuwemo kwenye Ndege moja aina ya Helikopta ambayo ilihusika katika ajali Jumamosi asubuhi katika Ziwa Nakuru nchini Kenya, yametolewa. Kwa mjibu wa kanmshena wa kaunti ya Nakuru, Joshua Nkanatha, ndege hiyo ya Helikopta ilikuwa njiani kuelekea maeneo ya Narok ambapo Rais Uhuru Kenyatta alikuwa ahutubie mkutano wa kisiasa, siku chache kabla ya kufanyika uchaguzi mkuu wa Urais Oktoba 26, ajali hiyo ilipotokea.

Majina ya wahasiriwa ambao bado hawajapatikana ni Bwana Sam Gitau, John Mapozi, Anthony Kipyegon na mwanamke aliyetambuliwa tu kama Veronicah, pamoja na rubani wa ndege hiyo Bwana Apollo Malowa. Hadi sasa watano hao hawajulikani waliko.

Ndege hiyo pia ilikuwa imepangiwa kuwabeba waandishi wa vyombo kadhaa vya habari nchini Kenya.

Taarifa ambazo bado hazijathibitishwa na wakuu nchini Kenya, zinasema kuwa abiria wa ndege hiyo pamoja na rubani walikuwa walevi- Kwani walikesha usiku kucha wakinywa vileo katika maeneo kadhaa ya burudani mjini Nakuru.

Ndege hiyo ya helikopta aina ya 5Y-NMJ ilianguka katika ziwa Nakuru nchini Kenya muda mfupi baada ya kuondoka katika hoteli moja mjini humo.

Afisa mkuu wa Polisi mjini Nakuru Joshua Omukata amethibitisha kutokea kwa ajali hiyo huku akikanusha taarifa kuwa ndege hiyo inamilikiwa na Rais Uhuru Kenyatta. Ndege hiyo inadaiwa kumilikiwa na kampuni ya Flex Air Charters, na kusimamiwa na Kapteni Bootsy Mutiso.

Aidha, amesema kuwa shughuli za kutafuta mabaki ya ndege hiyo na miili ya wahasiriwa zinaendelea.

Ripoti zinasema kuwa kulikuwa na watu watano katika ndege hiyo.

Seneta wa Nakuru Susan Kihika amesema kuwa watatu kati ya wale waliokuwa wameabiri ndege hiyo, walikuwa wanachama wa kitengo chake cha mawasiliano.

Kwa mjibu wa kanishena wa kaunti ya Nakuru, Joshua Nkanatha, ndege hiyo ya Helikopta ilikuwa njiani kuelekea maeneo ya Narok ambapo Rais Uhuru Kenyatta alikuwa ahutubie mkutano wa kisiasa, siku chache kabla ya kufanyika uchaguzi mkuu wa Urais Oktoba 26, ajali hiyo ilipotokea.

Ndege hiyo iliondoka katika hoteli ya Jarika County Lodge na duru zinasema kuwa ilikuwa ikipaa chini chini kabla ya kuanguka.

Ndege hiyo ilitarajiwa kusafrisha waandishi wa habari katika mkutano wa kampeni za Rais Uhuru Kenyatta.

Waokoaji walilazimika kusubiri boti kusafirishwa kutoka Ziwa Naivasha.

Mkurugenzi wa Idara ya kitaifa ya kukabiliana na majanga Pius Masai amesema kuwa ndege ya polisi imetumwa katika eneo hilo kusaidia katika uokoaji.

Kutana na Bi Khadija na Kamgambile ni Watabibu wa Tiba za Asili na Kusafisha Nyota

$
0
0

KUTANA NA BI KHADIJA NA KAMGAMBILE NIWATIBABABU WATIBA ZA ASILI KUSAFISHA NYOTA PETE YA MALI

BI KHADIJA NA KAMGAMBILE WANAO UWEZO MKUBWA WAKUJUWA JAMBOLAKO NA KUKU SAIDIA

BI KHADIJA NA KAMGAMBILE WANA TIBU MARADHI KAMA HAYA MIGUU KUUMA NAKUEAKA MOTO

PRESHA KISUKARI VIDONDA VYA TUMBO PUMU TEZI NA UVIMBE TUMBONI ANA UWEZO WAKURUDISHA MTU ALIEPOTEA KIMAZINGIRA

(MSUKURE)  KUMFANYA MKE MUME MPENZI ASIKUSALITI DAWA YA LIMBWATA KUMTAWALA MPENZI WAKO UNAVYOTAKA

KUMUONA MBAYA WAKO LIVE KWASABABU MAALUM  ANOTOA PETE YA BAHATI ITAKAYO KUKETEA PESA BILA YAMASHARITI

NA KUMILIKI MALI UNAZO TAKA DAWA YA KUONGEZA UUME SAIZI UIPENDAYO DAWA YA NGUVU ZAKIUME PIA ANAYO

DAWA YA KUONGEZA HIPSI SHEPU KUWA NA UMBO BOMBA KAMA UMEIBIWA AMA KU DHULUMIWA

UTARUDISHIWA MALIYAKO NDANI YA MASAA (24) ANAFUNGA KESI NAKUPATA HAKIYAKO

DAWA YA MVUTO WA BIASHARA KUUZA MALIYAKO KWA HARAKA KUZUIYA CHUMA ULETE KUSAFISHA NYOTA NA KUTOWA MIKOSI KARIBU

CALLING +255719866726/

KWA WHATSAPP IMO +255768455841/

Serikali Kuvunja Nyumba Zilizojengwa Bila Kibali

$
0
0
Serikali imewaagiza Wakurugenzi wa Halmashauri, Maafisa Ardhi, Maafisa Ujenzi na Maafisa Mipangomiji kuweka alama za X na kuvunja majengo yote yanayojengwa katika miji yao bila kibali na yale yanayojengwa katika viwanja vya watu wengine walio na hati

Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi Mhe. William Lukuvi.
Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi Mhe. William Lukuvi ameyasema hayo alipofanya ziara wilayani Sumbawanga mkoani Rukwa alpoenda kutatua mgogoro wa ardhi ambapo ameagiza eneo ya lililokuwa shamba la mifugo la Malonje wilayani Sumbawanga mkoani Rukwa lenye ukubwa wa ekari 12,750, lirejeshwe serikalini kwa vile utaratibu wa kuligawa umekiukwa kwa kiwango kikubwa, na masharti ya uendeshaji hayajazingatiwa kabisa.

Waziri Lukuvi amesema tatizo la ujenzi holela lianaanza pale ambapo Wakurugenzi wa Halmashauri, Maafisa Ardhi, Maafisa Ujenzi na Maafisa Mipangomiji wanaacha majengo yanaibuka katika miji yao bila kujua ujenzi huo una kibali au unajengwa katika kiwanja chenye hati na muhusika wa hati hiyo ndio anayejenga.

“Hatuwezi kuendelea na zoezi la kufanya urasimishaji wa makazi kila siku wakati chanzo cha tatizo hilo kinajulikana, kwa hiyo naagiza Wakurugenzi, Maafisa Ardhi, Maafisa Ujenzi na Maafisa Mipangomiji kuweka x katika majengo yote yanayojengwa bila vibali na ujenzi unaofanywa kwenye viwanja vya watu masikini kwa dhuruma” amesema Lukuvi.

Lukuvi amesema atapambana na viongozi hao pale ambapo atakuta majengo yamekithiri katika miji yao na hayana vibali vya ujenzi na baya zaidi majengo hayo yamejengwa katika maeneo ambayo hayaruhusiwi kujenga au yamejengwa katika kiwanja cha mtu mwingine na viongozi hao wameshindwa kufuatilia kwa kuyavunja au kuyaweka alama ya x majengo hayo, kwa kuwa huu ni uzembe unaotokea nchi nzima.

Mkuu wa Mkoa wa Rukwa Kamishna Mstaafu Zelote Stephen amemhakikishia Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi Mhe. William Lukuvi kuwa atayafanyia kazi mapendekezo yake kikamilifu na kwa haraka ili kuondoa migogoro na kero zinazoukabili mkoa wake katika masuala yote ya ardhi.
Viewing all 104795 articles
Browse latest View live




Latest Images