Quantcast
Channel: UDAKU SPECIAL
Viewing all 104799 articles
Browse latest View live

Ajiokoa Kwenye Ajali ya Moto juu ya Ghorofa kwa Kuning’inia Dirishani (Video)

$
0
0
Mwanaume mmoja nchini China amejikuta akiokoka kwenye moto mkubwa uliozuka kwenye jengo refu lenye ghorofa 25 kwa kuvunja vioo na kuning’nia dirishani bila kudondoka.

Kwa mujibu wa taarifa kutoka gazeti la Chongqing Daily zimeeleza kuwa moto hupo ulianza kuwaka leo Jumatano Desemba 13, 2017, Mnamo majira ya 05:55 asubuhi ambapo moto huo ulianzia ghorofa namba 24 kuelekea ghorofa namba 25 ambayo yeye ndiye aliyekuwepo.

Kwa muonekano wa video iliyorekodiwa kwa kutumia simu, Mwanaume huyo alionekana akining’inia kwenye madirisha na baadaye kushuka floo ya chini baada ya moto kuongezeka.

Akiwa katika jitihada za kujiokoa alionekana akivunja vioo kwenye ghorofa ya chini ambayo ilikuwa bado haijapatwa na moto huku akidondokewa na vipande vya makaa ya moto kutoka juu.

Hata haikumgharimu muda mrefu kupata mateso hayo kwani baada ya dakika 9 yaani saa 06:04mchana  kikosi hicho cha Moto cha mjini Yuzhong kilifika na kufanikiwa kuuzima moto huo na kuwaokoa watu watatu akiwemo mwanaume huyo.

“Tulifika muda mfupi baada ya kutokea kwa moto, tuliagiza maaskari wetu 71 kuzima moto huo lakini ilitulazimu kwanza kumuokoa mwanaume mmoja aliyekuwa nje ya jengo hilo akihangaika kujinasua na moto. Maaskari wetu walilazimika kuvunja madirisha kwa mashine zetu, lakini tulikuta watu wawili ndani ya jengo hilo wakiwa wameungua vibaya na kuwapeleka hospitali.“imeeleza taarifa ya kikosi cha zima moto cha mjini Yuzhong.

Hata hivyo majina ya majeruhi wote watatu bado hayajulikana kwa sababu za kiusalama nchini humo. Tazama kipande cha video cha tukio hilo


Bongo5

Habari Zilizopo Katika Magazeti yya Leo Alhamisi ya Disemba 14

$
0
0

Habari Zilizopo Katika Magazeti yya Leo Alhamisi ya Disemba 14

Punguza Unene na Kutibu Magonjwa Kwa Kutumia Dawa za Edmark...Bonyeza Hapa

$
0
0
TUNA DAWA AMBAZO NI VIRUTUBISHO NA CHAKULA MBADALA ZIMEHAKIKIWA NA TFDA

Ni uhakika kwa afya yako, kupunguza uzito na Sumu mwilini, Mafuta/Sehemu Mbaya, Kitambi na Nyama Uzembe na kutibu MAGONJWA Mbali mbali yaliyoshindikana

Loose Weight Trainer ni Msaada wako Wasiliana Nasi Kwa WhatsApp 0713 777 470

Upate Suluhisho la Afya yako Bila Madhara pia unaweza kujiunga nami ili ufanye Biashara hii Nicheki


Intagram napatikana kwa jina @looseweight_trainer

Takukuru Singida yamtia Mbaroni Gulamali ( Aliyeshinda kura za Maoni CCM Jimbo la Nyalandu )

$
0
0
Taasisi ya kuzuia na kupambana na rushwa (TAKUKURU) mkoa wa Singida inamshikilia mshindi wa kwanza kura za maoni CCM jimbo la Singida kaskazini, Haider Hussein Ghulamali (46), kwa tuhuma ya kutoa rushwa ya shilingi milioni mbili taslimu kwa afisa usalama wa taifa (jina tunalo).

Lengo la Ghulamali  mfanyabiashara na mmiliki wa kiwanda cha magodoro  mjini Dodoma,ni kwamba afisa usalama huyo amtolee taarifa nzuri Kwenye vikao vya  ngazi za juu, ili aweze kuthibitishwa na vikao hivyo, kuwa mgombea ubunge jimbo la Singida kaskazini.

Mkuu wa TAKUKURU mkoa wa Singida, Joshua Msuya, alisema Ghulamali amekamatwa Desemba 12 mwaka huu saa 8.30 mchana, maeneo ya Rafiki resort wakati akikabidhi rushwa hiyo iliyokuwa imehifadhiwa kwenye bahasha.

 Msuya alisema desemba 11 mwaka huu,ofisi yake ilipata taarifa ya kuwepo kwa vitendo vya rushwa kwa mmoja wa wana CCM anayewania ubunge jimbo la Singida, ambaye ni Ghulamali.

“Baada ya kupokea taarifa hiyo uchunguzi ulianza ikiwa ni pamoja na kuchunguza vitendo rushwa alivyofanya  mtuhumiwa huyo, kabla na baada ya kura za maoni kupigwa desemba 10 mwaka huu huko kijiji cha Ilongero.Kura hizo zilimpitisha Ghulamali aliyepata kura 606 kati ya kura 1009 zilizopigwa,” alisema.

 Mkuu huyo, alisema baada ya zoezi hilo kupita la kura za maoni,mtuhumiwa kwa juhudi zake aliweza kupata namba za simu za afisa wa usalama wa taifa ambaye walikuwa hawafahamiani.

“Baada kupata namba ya simu ya afisa usalama taifa, Ghulamali aliweza kumpigia na akatoa maombi yake ya kusafishiwa taarifa kwenye vikao vya juu.Baada ya maombi hayo,aliweza  kutoa rushwa ya shilingi milioni mbili,na kumkabidhi afisa huyo. Ndipo alipokamatwa na TAKUKURU waliokuwa wameweka mtengo,” alisema Msuya.

Alisema uchunguzi zaidi bado unaendelea kuhusiana na mtuhumiwa Ghulamali  kabla ya uchaguzi na baada ya uchaguzi wa kura za maoni.

Mkuu huyo wa TAKUKURU,ametoa rai kwa wanachama wa vyama vyote vya siasa,wagombea na wananchi kwa ujumla, kuzingatia sheria za uchaguzi ndani ya vyama vyao.Pia kujiepusha na vitendo vya rushwa nyakati za uchaguzi ndani vyama.

“TAKUKURU itamkamata mgombea,mpambe na mwanachama yeyote atakayejihusisha na vitendo ya kuomba na kupokea rushwa,na ikipata ushahidi wa kutosha,itamfikisha mhusika mahakamani,” alisema Msuya

Rais Nkurunziza kufuata nyayo za Kagame, Aja na mpango wa kusalia madarakani hadi 2034

$
0
0
Rais wa Burundi, Pierre Nkurunziza ameanzisha kampeni ya mchakato wa kufanyika kwa kura za maoni kujaribu kubadilisha katiba itakayompa nafasi ya kuongeza mihula mingine miwili baada ya kikomo cha utawala wake  mwaka 2020.

Rais Nkurunziza amesema hayo jana jumanne wakati akihutubia wafuasi wake katika kijiji cha Gitega huku akiwaonya wale wote watakaopinga juhudi zake kwa maneno au kwa vitendo watakuwa wameuvuka mstari mwekundu.

Kampeni hiyo maalumu yenye lengo la kumuweka Nkurunziza hadi mwaka 2017 imeanzishwa baada ya serikali kuzindua juhudi za kuchangisha fedha za maandalizi ya uchaguzi mkuu wa mwaka 2020.

Kwa mujibu wa Shirika la habari la AFP taarifa zimeeleza kuwa mpango huo unahusisha kuidhinishwa kwa rasimu ya katiba mpya ambayo itamuwezesha kuwania urais kwa mihula miwili zaidi ya miaka saba kila muhula baada ya kustaafu kwake mwaka 2020.

Viongozi wa upinzani wanaoishi uhamishoni wanasema kura hiyo ya maoni itakuwa kama mazishi kwa muafaka wa utiaji saini wa mkataba wa amani wa mwaka 2000.

Mkataba huo wa amani ulisaidia kumaliza vita vya wenyewe kwa wenyewe vilivyodumu kwa miaka 13 na kusababisha vifo vya watu 300,000.

Burundi ilitumbukia kwenye mzozo mwingine wa kisiasa mwaka 2015 pale Rais Nkurunziza alipokataa kung’atuka madarakani baada ya kumaliza muhula wake na  kuwania tena urais.

Nkurunziza anakuwa Rais wa Pili Afrika Mashariki kuonesha nia ya kubadili katiba ili apewe muda mwingine wa kuongoza baada ya Rais wa Rwanda, Paul Kagame kufanya hivyo mwaka 2016.

Bongo5

Ufafanuzi Kuhusu Lulu Kusamehewa na Rais Magufuli

$
0
0
Kamishna Jenerali wa Magereza nchini, Juma Malewa amesema katika msamaha uliotolewa na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli siku ya uhuru Desemba 9, 2017 haukumuhusu msaani wa filamu Elizabeth Michael maarufu kama Lulu.

Jenerali Malewa amefafanua kuwa mchakato wa kuanza kuangalia wafungwa wakupunguziwa vifungo na kusamehewa haukumuhusisha Elizabeth Michael kutokana na yeye kuingia gerezani wakati tayari mchakato wa kuangalia wafungwa wa kusamehewa na kupunguziwa vifungo ulikuwa umeshaisha

"Msamaha huu haukumuhusu yeye kwa sababu aliingia magereza wakati tayari zoezi hili lilikuwa limekamilika, kwahiyo labda misamaha ijayo kama itakuwepo lakini katika hii haikumuhusu",amesema Kamishna Malewa.

Kamishna Malewa pia ameeleza  kuwa vipo vigezo vingi vinavyoweza  kumfanya mfungwa asamehewe ama kupunguziwa kifungo kutokana na kosa na muda wa kifungo chake na kwamba misamaha inatofautiana kutokana na kosa kama endapo mfungwa atafata taratibu na kuonekana amerekebishika anaweza kupata msamaha na mengine mengi.

Desemba 9 mwaka huu siku ya uhuru kwa mujibu ya ibara ya 45 ya katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Rais John Pombe Magufuli alitoa msamaha kwa  wafungwa 61 waliohukumiwa kunyongwa hadi kufa na wawili Nguza Viking (Babu Seya ) na Johnson Nguza (Papii Kocha ) waliohukumiwa kifungo cha maisha jela na wengine kupunguziwa vifungo vyao.

Soma Nafasi za Ajira Zilizotangazwa Leo

Miujiza ya Sharifu Seif Mohamed..JE Umeachwa na Mme/Mke au Mpenzi, Umesongwa na Mitihani ya Maisha..Piga Simu Upate Muujiza Wako

$
0
0
SHARIFU SEIF MOHAMED ANAWASHUKURU WALE WOTE WANAOENDELEA KUPIGA SIMU, WENYE MATATIZO NA WALE WANAOTOA  SHUKRANI NA SHUHUDA JINSI TIBA ZAKE ZINAVYO WASAIDIA,

(Rudisha mahusiano yako ndani ya masaa 72 tu)

SHARIFU MOHAMED Ni  mtaalam na mnajimu maarufu wa nyota na kubashiri mambo yanayo watesa binadamu duniani kote na kupata ufumbuzi, Anatumia kitabu cha QUR'AN, Dawa za Asili, Dawa za Kiarabu na majini kwa kumtuliza mke/mme, mchumba au mpenzi ndani ya masaa 72 tu, na kutatua matatizo yote ya kimaisha,

Je Umeachwa na UMPENDAE awe Mme/Mke na bado unampenda? Je Umekimbiwa na Mmeo/ Mkeo n anaishi na mtu mwingine? Je Umejaribu sehemu nyingi bila mafanikio? Mpigie simu SHARIFU SEIF sasa hivi ujionee Muujiza wa Papo kwa Papo, Anauwezo wa hali ya juu wa kusambaratisha mahusiano yao na kumrejesha kwako haraka sana na Kumfanya Atimize Ahadi zote Ndani ya Muda Mfupi Endapo Utafwata Atakacho Kuelekeza

ANAZO DAWA ZA MAPENZI, NGUVU ZA KIUME, CHANGO NGIRI MAJI NA N.K, ZINDIKO LA NYUMBA NA BIASHARA, PETE ZA BAHATI, HUMALIZA KABISA TATIZO LA NGUVU ZA KIUME NA KUREFUSHA UUME KWA SAIZI UNAYOTAKA, HUZUIA CHUMA ULETE KWENYE BIASHARA, HURUDISHA MALI ZILIZOPOTEA, MAGONJWA SUGU, MIGUU KUWAKA MOTO AU KUFA GANZI, HUTIBU BUSHA BILA KUPASUA, ANAO UWEZO WA KUMRUDISHA ALIE MBALI AU ALIECHUKULIWA MSUKULE, KUPANDISHA NYOTA NA KUSHINDA BAHATI NA SIBU, KASAFISHA NYOTA NA KUKUPA MVUTO WA AJABU, KUTOA NUKSI NA VIFUNGO MBALIMBALI,  MAFANIKIO YA MAISHA NA UTAJIRI BILA MASHARI, NA MENGINE MENGI YA SIRI,

Je UMAHANGAIKA KUPATA MTOTO BILA MAFANIKIO? WASILIANA NA MTAALAMU HUYU KWANI YEYE HUFAULU PALE WOTE WALIPOSHINDWA, PIA UMALIZA KAZI ZILIZO SHINDIKANA NA WATAALAM WENGINE NDANI YA MASAA 24 TU,

(NA ANATIBU KWA NJIA YA SIMU UKIWA NCHI YOYOTE AU MKOA WOWOTE ENDAPO UTAFWATA MAELEKEZO YAKE)

Kwa ushauri na mawasiliano  zaidi Piga SIMU No:
Mobile +255 654-836970
WhatsApp +255 756-033670 

Opereshi Saka Makahaba Sasa Kufanyika Nyumba kwa Nyumba

$
0
0
Opereshi Saka Makahaba Sasa Kufanyika Nyumba kwa Nyumba
Muuu wa wilaya ya Bunda mkoani Mara, Bi. Lydia Bupilipili ameliagiza jeshi la polsi wilayani humo kuendesha msako wa watu wanaofanya biashara ya ukahaba nyumba kwa nyumba.

Bi. Bupilipili ametoa agizo hilo katika kijiji cha Kunzugu alipokuwa anazungumza ikiwa ni siku ya maadhimisho ya siku ya Ukimwi wilayani humo, ambayo pia iliadhimishwa kwa kupanda miti.
Mkuu huyo wa wilaya amewataka polisi kupita nyumba kwa nyumba kwenye nyumba za wageni, na kuwasaka wanawake ambao wanadaiwa kukodisha nyumba hizo kwa ajili ya kuendesha biashara za ukahaba.

Baada ya Kumwagana na Mpenzi Wake Kidoa Adaiwa AKurudia Ufuska

$
0
0
Baada ya Kumwagana na Mpenzi Wake Kidoa Adaiwa AKurudia Ufuska
MSANII wa filamu Bongo Asha Salum ‘Kidoa’ ambaye kwa kipindi kirefu alipoa kama maji ya mtungi kutokana na mwandani wake kumpiga ‘stop’ mambo ya kifuska ikiwemo kupiga picha za nusu utupu, amedaiwa kurejea kwenye vitendo hivyo baada ya kumwagana na jamaa huyo.

Kwa mujibu wa chanzo, Kidoa awali alikuwa machachari lakini alivyompata pedeshee ambaye ni kigogo wa serikali
alimpiga ‘stop’ mambo ya kifuska ikiwemo kuuza sura mitandaoni akiwa nusu utupu, pamoja na skendo kwenye vyombo vya habari.

Baada ya kunasa ubuyu huo, mwanahabari wetu alipomtafuta Kidoa, aliangua kicheko na kusema: “Watu wanapenda sana kufuatilia maisha yangu, najua hayo yote yameibuka baada ya kuweka picha Instagram nikiwa na nguo za ndani pekee, mavazi hayo nilikuwa nayapenda kitambo na picha zangu nyingi zilikuwa za hivyo, nikaamua tu nipumzike, si kwamba nimeachwa.”

Zanzibar Nao Waibuka na Hoja ya Miaka Saba ya Urais

$
0
0
Zanzibar Nao Waibua Hoja ya Miaka Saba ya Urais
Hoja ya kuongezwa muda kwa Rais wa Tanzania imeibukia katika Baraza la Wawakilishi Zanzibar ambako mwakilishi ameshauri Rais wa Zanzibar aongezewe miaka miwili ili atawale kwa miaka saba.

Awali, hoja kama hiyo iliibuliwa na mbunge wa Chemba (CCM), Juma Nkamia aliyesema ni vyema yakawepo marekebisho ya Katiba ili kuruhusu Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania atawale kwa miaka saba, hoja ambayo bado hajaipeleka bungeni.

Hata hivyo, tofauti na Nkamia ambaye bado hajawasilisha hoja yake, mwakilishi wa Shaurimoyo, Hamza Hassan Juma yeye ameifikisha barazani akishauri Serikali ya Zanzibar kuwasilisha marekebisho ya Katiba ili Rais wa Zanzibar atawale kwa miaka saba.

Hamza alitoa ushauri huo jana katika mkutano wa Baraza la Wawakilishi unaoendelea Chukwani nje kidogo ya Mji wa Zanzibar wakati akichangia muswada wa sheria ya marekebisho ya Tume ya Uchaguzi ya mwaka 1984.

Alisema kuwa ili kumpa Rais wakati mzuri wa kuwatumikia wananchi ipasavyo, hakuna budi muda wake ukaongezwa kwa miaka miwili zaidi.

Mwakilishi huyo alisema muda wa miaka mitano wa uongozi wa Rais madarakani ni mdogo na Taifa hupoteza fedha nyingi za wananchi kwa kufanya uchaguzi kila miaka mitano, hivyo ni vyema Serikali ikalifanyia kazi suala hilo. Aliongeza kuwa, kwa mujibu wa tathmini yake ya Uchaguzi Mkuu, fedha za walipakodi zinazotumika zinaweza kujenga zaidi ya shule kubwa 20 ambazo zingesaidia jamii kuondokana na upungufu uliopo.

Hamza alisema pamoja na katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na ile ya Zanzibar kuweka muda wa miaka mitano, lakini kuna nafasi ya kuongeza muda kwa Rais wa Zanzibar pindi baraza hilo likiridhia kufanya hivyo kwa masilahi ya wananchi na Taifa kwa ujumla. “Kwa kuwa Katiba ya Zanzibar inajitegemea, hivyo ni wazi kuwa tunaweza kufanya hivyo pasi ya kuathiri lolote katika Katiba ya Tanzania juu ya kuongeza muda wa kiongozi huyo,” alisema mwakilishi.

Akichangia muswada huo, mwakilishi wa Welezi, Hassa Khamis Hafidh alitaka kuongezewa nguvu Tume ya Uchaguzi ili kuepusha baadhi ya watu kujitangaza kabla haijatoa matokeo rasmi.

Akiwasilisha muswada huo, waziri wa Nchi, Ofisi ya Makamu wa Pili wa Rais, Mohamed Aboud Mohamed alisema lengo ni kuifanya sheria hiyo kwenda na wakati uliopo.

Mc Pilipili Avutiwa na Nafasi ya Ben Pol kwa Ebitoke

$
0
0
Mc Pilipili Avutiwa na Nafasi ya Ben Pol kwa Ebitoke
Mchekeshaji Mc Pilipili ameizungumzia style aliyoitumia mchekeshaji mwenzie, Ebitoke hadi kuingia katika mahusiano na Ben Pol.

Mc Pilipili amesema Ebitoke ni mchekeshaji mzuri sana ila style aliyoitumia kumuendea Ben Pol pengine kwa nia ya kutangaza jina lake angeweza kufanya kazi zaidi kama mbadala wake.

“Bado kuna ombwe limeingia Tanzania kwamba inabidi uwe na kiki fulani halafu ndio unaleta kazi zako lakini mimi bado naamini kazi ina nguvu zaidi, hayo mambo tuachie waimbaji” Mc Pili ameiambia Bongo5.

Alipoulizwa iwapo yeye angekuwa Ben Pol angelichukuliaje hilo, alijibu; “(anacheka) ni ngumu, kwanza unajua Ben Pol ni mgogo mwenzangu na nina uhakika walikuwa na mipango yao mizuri na kuna sehemu waliishia, wapo poa”.

Mama wa Diamond Atoa ya Moyoni Kuhusu Diamond na Zari

$
0
0
Mama wa Diamond Atoa ya Moyoni Kuhusu Diamond na Zari
December 13, 2017 kupitia ukurasa wa instagram wa mama yake na muimbaji wa Bongofleva Diamond “Sandrah” ameamua kuandika ya moyoni kuhusiana na kile ambacho huwa anapost kwenye page yake ya instagramna watu kuanza kutoa comment tofauti tofauti huku wengine wakikosoa.

Mama Diamond mara nyingi katika ukurasa wake wa instagra hupost kazi za mwanae za  kisanaa na wakati mwingine anampost mtoto wake Diamond Platnumz na mpenzi wake Zari the Boss Lady, hivyo huwa haishangazi kuona akiwapost wawili hao ila caption ya leo kwenye picha aliyowapost Diamond na Zari imechukua headlines.

Ujumbe wa mama Diamond katika post yake ya instagram haujaweka wazi ni nini kimemfanya aandike maneno kama hayo katika picha aliyowapost Diamond na Zari lakini baadhi ya watu wanautafsiri ujumbe huo kama onyo kwa mtu, au shabiki anayecomment vitu visivyompendeza baada ya kupost Diamond na zari

a kuwapost Diamond na Zari.

Kupitia picha hiyo aliyoipost leo December 13,2017 katika ukurasa wake instagram ameandika caption inayosomeka

“Mapenzi niliyonayo kwa wanangu hawa hayana mfano…Ninapompost mkwe wangu @zarithebosslady au mwanangu @diamondplatnumz sifanyi kwa ajili ya kuwaridhisha WASIOTUPENDA….Nawapost kwa mapenzi makubwa kwao na wajukuu zangu @princess_tiffah @princenillan Imani yangu si kumkwaza mtu au kumkebehi mtu bali Nawapendaaa sana…Akaunti hii ni MALI yangu hivyo asitokee MTU kunipangia cha kupost au kujifanya Mama/Baba ushauri… Maisha ni kuchagua na si kuchaguliwa #StrongFamily#TusipangianeChaKupost#NajitambuaKulikoMjuavyo#ABoyFromTanda“

Hamisa Mobetto Amtolea Mtu Povu ” Yani Naskia Bila Mimi Huwezi Kabisa Mrs Fudenge”

$
0
0
Hamisa Mobetto Amtolea Mtu Povu ” Yani Naskia Bila Mimi Huwezi Kabisa Mrs Fudenge”
Mwanamitindo Hamisa Mobetto ambaye pia ni mzazi mwenzake Diamond Platnumz amezichukua tena headlines baada ya kupost picha katika ukurasa wake wa Instagram na kuandika caption zilizoleta gumzo kwa mashabiki lakini haijajulikana zimemlenga nani.

Hamisa Mobetto kupitia ukurasa wake wa instagram amepost picha zake mbili katika post mbili tofauti na kuandika “Yani naskia bila Mimi huwezi kabisa….🙆🏽‍♀️🙆🏽‍♀️ yani upo nyang’anyang’a #mrsfudenge @mobettostyles 👑”


 Post nyingine ya Hamisa Mobetto alipost picha yake akiwa katika gari na kuandika maneno haya “Ety …. Naskia ukiona picha yangu Moyo wako unapiga paaah 🙆🏽‍♀️💘💖 #MrsNaniliuwh…🧜🏽‍♀️ @mobettostyles @mobettostyles”

Israel Yaendeleza Mashambulizi Dhidi ya Hamas Kujibu Mashambulizi Kutoka Gaza

$
0
0
Israel Yaendeleza Mashambulizi Dhidi ya Hamas Kujibu Mashambulizi Kutoka Gaza
Jeshi la Israel limesema mashambulizi yake roket yanazilenga ngome tatu za kijeshi za wapiganaji wa kundi la Hamas,ikiwa ni hatua ya kujibu shambulizi dhidi yao la kutoka ukanda wa Gaza.
Israel pia imeamuru kufungwa kwa mpaka kati yake na Gaza,baada ya shambulizi la nne maroketi yanayodaiwa kurushwa na kundi la HAMAS.
'Mtego wa kundi la Hamas' wanasa wanajeshi wa Israel
Israel yashambulia ngome ya Syria
Hali hii ya mapigano ya kundi la Hamas inadaiwa kuwa ni kutokana na hasira kufuatia hatua ya rais Trump kuutambua mji wa Jesrusalem kama makao makuu ya Israel.
Hata hivyo jeshi la Israel linasema kuwa makombora kati ya yaliyorushwa,walifanikiwa kuyazuia,ambapo moja lilianguka eneo la wazi kusini mwa Israel na jingine lilipoteza uelekeo

Ajinyonga Kisa Kukataliwa na Mpenziwe

$
0
0
Ajinyonga Kisa Kukataliwa na Mpenziwe
MKAZI wa kitongoji cha Ndondobya katika kijiji cha Fubu, Kyela mkoani Mbeya, Labson George (22), amejiua kwa kujinyonga na mtandio kwa madai kuwa mwanamke aliyekuwa mpenzi wake wa muda mrefu kukataa kuoana naye.

Mwenyekiti wa Kijiji hicho, Abdul Mwamafupa, alisema kijana huyo alikuwa na uhusiano wa muda mrefu na Violet Joseph na inadaiwa kuwa alipomfuata na kupanga kumweleza kuwa waoane, alikataa.

Kutokana na hatua hiyo, alisema George alimnyang’anya mtandio na kutokomea kusikojulikana hadi alipokutwa saa 10:00 jioni pembezoni mwa Mto Mbaka akining’inia juu ya mti akiwa amejinyonga.

Baada ya tukio hilo, alisema serikali ya kijiji ilitoa taarifa polisi ambao walifika wakiwa na daktari na kumtoa kwenye mti aliokuwa amejinyonga.

Mwamafupa alisema kumekuwapo na uvumi mitaani kuwa chanzo cha kijana huyo kujiua ni kutokana na kumfumania mpenzi wake akifanya ngono na mwanamume mwingine vichakani.

Hata hivyo, alisema habari hizo si za kweli bali alijinyonga baada ya mpenzi huyo kukataa kuoana naye akimhisi kijana ana michepuko mingi.

“Kijana huyu kabla umauti haujamkuta aliandika meseji kwa dada yake anayeishi Iringa kuwa ‘Dada yule mwanamke Violet niliyepanga kuoana naye amenikataa ghafla, naamua kujiua ili nisiwepo tena duniani maana amekula pesa zangu nyingi, nahisi amepata wengine’’, alisema.

Alisema baada ya kumtoa kwenye mti walikagua mfukoni na kukuta barua ikiwa na ujumbe kuwa ameamua kujiua kwa sababu mwanamke amekataa kuolewa naye wakati amekula pesa zake nyingi, hivyo hakuona sababu ya kuendelea kuishi duniani kuendelea kuwa na machungu.

Akizungumzia tukio hilo, Violet aliyekuwa mpenzi wa Joseph, alisema chanzo cha kukataa kuoana naye ni kwamba alikuwa na wanawake wengi kutokana na umaarufu alio nao wa kucheza mpira wa mchangani, hivyo alihofia kupata magonjwa  na kufa na kumuacha mama yake ambaye ni mlemavu bila msaada.

Joseph Mwambunga, baba mzazi wa msichana huyo, alimweleza mwandishi wa habari hii kwamba kijana huyo alikuwa na uhusiano wa muda mrefu na binti yake na aliwahi kumfuata na kumweleza kuwa amuoe aache kumchezea na baada ya hapo akashangaa siku iliyofuata amejinyonga.

Kamanda wa Polisi Mkoa wa Mbeya, Mohammed Mpinga, licha ya kukiri kuwapo  tukio hilo, alitoa rai kwa wananchi kuacha kuchukua uamuzi mgumu wa aina hiyo na kusema kama mtu mpenzi amemkataa, anapaswa kuvuta subira na kutafuta namna ya kumbembeleza, lakini si kujiua.

Mwili wa kijana huyo ulizikwa jana kijijini hapo baada ya vipimo vya kitabibu na uchunguzi wa kipolisi kukamilika hivyo kubainika kuwa alijinyonga kwa mtandio.


Waziri Mkuu Aongoza Waombolezaji Kuaga Miili ya Askari 14 wa JWTZ Waliouwawa na Waasi DRC

$
0
0
Waziri Mkuu Aongoza Waombolezaji Kuaga Miili ya Askari 14 wa JWTZ Waliouwawa na Waasi Kongo
WAZIRI Mkuu, Kassim Majaliwa ameongoza waombolezaji kuaga miili ya askari 14 waliouawa na waasi wa ADF nchini Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo (DRC) ambapo shughuli ya kuaga miili ya askari hao imefanyika leo Alhamisi, Desemba 14, 2017 katika viwanja vya Wizara ya Ulinzi na Jeshi la Kujenga Taifa, Upanga jijini Dar es Salaam.
Viongozi wengine waliohudhuria katika kuaga miili hiyo ni Rais Mstaafu wa Awamu ya Nne, Dkt. Jakaya Mrisho Kikwete, Mkuu wa Majeshi ya Ulinzi Jenerali Venance Mabeyo, wakuu komandi za anga, maji, nchi kavu na Jeshi la Kujenga Taifa (JKT), viongozi wa Umoja wa Mataifa, na wakuu wa vyombo vya ulinzi na usalama, askari na wananchi.
Baada kukamilika shughuli ya kuaga miili hiyo itasafirishwa kwao mazishi.

Huyu Hapa Bingwa wa Magonjwa Sugu Kama Vile Pumu, Vidonda vya Tumbo, Busha, Kisukari na Nguvu za Kiume

$
0
0

BABU MADUHU NI BINGWA WA MAGONJWA YOTE SUGU YANAYOSUMBUA KAMA VILE PUMU, VIDONDA VYA TUMBO, BUSHA, NGUVU ZA KIUME, KISUKARI, MIVUTO YOTE, KUSAFISHA NYOTA, KURUDISHA MALI, NK.

Tatizo la upungufu ukosefu wa nguvu za kiume, maumbile madogo ya uume limekuwa kubwa kwa lika zote hapa duniani

Matatizo hayo sio mageni kigeni ni ile tiba sahihi yakutibu na kuponya haya.chanzo cha hayo matatizo ni:KISUKARI, NGIRI,CHANGO, TUMBO KUUNGURUMA NA KUJAA GESI, KIUNO KUUMA, MAUMIVU YA MGONGO,MAGONJWA YA ZINAA, KORODANI KUVIMBANAKUUMA,VIDONDA VYA TUMBO, NK.

Tiba sahihi nabora ya tatizo la nguvu zakiume ni NYASOSE MIX, Nidawa ya vidonge asilia vilivyotengenezwa kwa kiwango bora na salama kwa ajili yakutibu mojakwamoja tatizo la nguvu za kiume maradufu

1,Hutibu nguvu za kiume mda mfupi sana kati ya umri wa miaka 18-85 naitakufanya uchelewe kufika kileleni kwa mda wa    dk 20 hadi 40 tendo lakwanza bila kuchoka naitakufanya uwe nahamu yakuendelea na tendo la ndoa zaidi ya mara 5 bila hamu kuisha.

MHESHA POWER Nidawa yakuboresha maumbile ya kiume kwa kunenepesha na kurefusha kwa saizi uipendayo inchi 6,7 hadi 8 kwa mda mfupi sana.dawa hizi huanza kufanya kazi kwa mda wa dk 67 ukisha tumia guarantee miaka 55 ikishakutibu.

Pia tunatibu,KISUKARI, PRESHA, UZAZI, NGIRI, PUMU,MALARIA SUGU, VIDONDA VYA TUMBO, CHANGO AINA ZOTE, BP, BUSHA BILA UPASUAJI NK.

ITINYA,Nidawa ya mvuto wa biashara,kazi,hupandisha cheo humfanya mfanyakazi apendwe na mwajiri wake,humvuta mme,mke,hawara,mchumba,unaemhitaji au hakutaki hatimizi ahadi zako kwa dhati utampata kwa mda wa dk 45 tu naatatulia milele nakumfunga asitoke inje ya ndoa.

SUPER POWER,Nidawa ya yakupunguza matiti,unene tumbo,kitambi kwa akina baba,hutoa mafuta mabaya mwilini,makovu sehemu mbalimbali mwilini,chunusi sugu,minyama uzembe,michirizi mwilini,nakuongeza makalio hips,mguu wa bia nk.

BABU MADUHU ANAPATIKANA MAGOMENI MOROCCO HOTEL/KANISANI
SIMU NO 0652 102 152/0755 684 297/0788 330 105.

HUDUMA HII UNAWEZA KUIPATA/KULETEWA MAHALI POPOTE NCHINI

 

Kutana na Mtabibu wa Asili Allan Shariffu Musa Mtabibu wa Nyota za Binadamu na Dawa za Asili

$
0
0
 
Kutana na Mtabibu Mwenye KUBRI kutoka kwa ALLAH shariffu musa Mtabibu wa Nyota za Binadamu na Dawa za Asili ya Africa Mwenye UWEZO Kubaini tatizo lako Pindi tu Utakapo Fanya Mawasilino Kupitia Wasaa Husika..JE UNASUMBULIWA NA Mapenzi? (Umeachwa na Umpendae,Awe Mume,Mke na Bado unampenda?Na Umejaribu Sehemu nyingi Bila Mafanikio?Wasilina na shariffu musa Ujione muujiza wa Papo kwa Papo.. anauwezo WA KURUDISHA MAHUSIANO NA KUIMARISHA NDOA YAKO NDANI YA SAA 12 TU. Umekimbiwa na Mumeo,mkeo au Mpenzi na anaishi na mtu mwingine? Muone akutatulie Anauwezo wa Hali ya Juu wa Kusambalatisha Mahusiano yao Endapo utafata Atakacho kuelekeza.
Atamfanya Atimize Ahadi zote kwa Muda Mfupi.

Maalim Hussein Anatumia Jina la Muhusika au Picha Kumaliza Tatizo lako..
Anatibu kwa Kutumia Vitabu vya QUR-AN Dawa za Asili za Africa,Dawa za Kiarabu na Majini.Anatafsiri Ndoto. Kushinda BAHATI NASIBU, KUSAFISHA NYOTA. Mvuto wa Mwili na BIASHARA, Kinga ya Mwili,ZINDIKO za Nyumba.MIGUU Kufa GANZI.Kufungua KIZAZI kwa wale walio fungwa kwa njia za KISHIRIKINA. Anakupa Jini la Mali kwa yule anaehitaji Utajiri BILA MASHARTI. Nguvu za KIUME, Humaliza Kesi zilishindika ndani ya siku 14 tu..na mengi zaidi

+255 629793352 au watsap
+255 679119679

Lissu Afunguka Kuhusu Wanaohama CHADEMA

$
0
0
Lissu Afunguka Kuhusu Wanaohama CHADEMA
Mbunge wa Singida Mashariki ambaye sasa Kenya akiendelea na matibabu kufuatia kupigwa risasi Septemba 7, 2017 amefunguka juu ya viongozi ambao wanasaliti CHADEMA na kusema jambo hilo lisiwatishe bali wao waendelee na kazi yao.

Tundu Lissu aliyasema hayo jana alipoonana Mwenyekiti wa Baraza la Vijana CHADEMA (BAVICHA) Taifa, Patrick Ole Sosopi ambaye alimtembelea Mhe Lissu hospitali jijini Nairobi jana kumjulia hali
"Ndugu zangu Mhe Lissu ameweza kunieleza mambo mengi sana na binafsi naamini ameniagiza kwa niaba ya Baraza la Vijana na tutayetekeleza kwa maslahi mapana ya nchi na chama chetu, hajasita kuniambia kwamba hali ya siasa yetu ndani ya nchi yetu kwa biashara inayoendelea kununua Viongozi uchwara na wenye tamaa wa chama chetu, amesema tusipate hofu CHADEMA hatujaanza kusalitiwa leo na hao wanaondoka, sio ajabu hata kidogo kwani mbona Yesu aliwahi kusalitiwa tena na mwanafunzi wake na hakuacha kazi yake" aliandika Ole Sosopi
Aidha Sosopi aliendelea kusema kuwa Tundu Lissu amemweleza kuwa hata watu ambao waliwahi kuisaliti CHADEMA kipindi cha nyuma hawajapata mafanikio yoyote katika maisha yao
"Wanaotusaliti hawajawahi kuwa na mafanikio katika maisha yao, tusikate tamaa mapambano yaendelee. Mwisho kabisa Mhe. Lissu ametuma salamu nyingi kwa Watanzania wote wanaoendelea Kumchangia na Kumuombea, ameendelea kuwasihi waendelee kumchangia na kumuombea, maana Bunge na serikali wamekataa kabisa kumtibia ili hali kwa mujibu wa sheria ni haki yake" alisema Ole Sosopi
Viewing all 104799 articles
Browse latest View live




Latest Images