Quantcast
Channel: UDAKU SPECIAL
Viewing all 104809 articles
Browse latest View live

Kunguru Asababisha Ndege Iliyowabeba Wanajeshi Kutua Ghafla

$
0
0
Kunguru Asababisha Ndege Iliyowabeba Wanajeshi Kutua Ghafla
Kunguru mmoja amelazimu ndege iliokuwa imewabeba wanajeshi wa Amisom kutoka Burundi kutua kwa ghafla katika uwanja wa ndege wa Bujumbura nchini Burundi.

Ndege hiyo inadaiwa kumgonga kunguru huyo angani wakati ilipokuwa ikipaa , kabla ya rubani kuamua kutoendelea na safari ya kuelekea Somalia ambapo wanajeshi hao wanahudumu kulingana na vyanzo vya habari na wizara ya ulinzi katika uwanja huo.

Ndege hiyo ilisalia hewani kwa takriban saa moja kabla ya kutua.

Rais wa Burundi Pierre Nkurunziza ametangaza kuwa serikali yake inajiandaa Kuishtaki EU
Wanajeshi wa Burundi ni miongoni mwa wananjeshi wa Umoja wa Afrika wanaokabiliana na wapiganaji wa Al-Shabab nchini Somalia.


Afisa mkuu wa uwanja wa ndege wa Burundi Emmanuel Habimana amethibitisha kuwa ndege hiyo iligonga kunguru huyo mepama alfajiri.

Hatahivyo kulingana na afisa huyo hakukuwepo na tatizo lolote la kiufundi na ndege hiyo iliondoka tena.

Sijawahi Kubuti na Mwanaume Kwenye Mapenzi Huwa Naacha- Snura

$
0
0
Sijawahi Kubuti na Mwanaume Kwenye Mapenzi Huwa Naacha- Snura
MSANII wa filamu Bongo, Snura Mushi amesema kuwa, japo amekuwa akionekana kulalamika kuhusu masuala ya mapenzi, ukweli ni kwamba kinachomuuma ni kutompata mwanaume stahiki kwake, lakini hajawahi kuachwa, huwa anaacha.

Snura alifunguka hayo kutokana na kuibuka minong’ono ya mara kwa mara kuwa huenda anaongoza kwa kupewa vibuti kwenye mapenzi ndomana hachoki kulalamika kuwa na stress za mahusiano, jambo ambalo amelipinga vikali.

“Nani kakudanganya huwa naachwa hiyo haijawahi kutokea, nikiona mtu haeleweki huwa najiengua mwenyewe sisubiri anipasue kichwa changu, hivyo kinachoniliza ni kutopata mtu sahihi kwangu na siyo kuachwa na wanaume,”alisema.

Eti Inasemekana Ireni Uwoya Mjamzito!...... Ahamisha Makazi Ajificha Nyumbani kwa Masogange

$
0
0
Eti Inasemekana Ireni Uwoya Mjamzito!...... Ahamisha Makazi Ajificha Nyumbani  kwa Masogange
Baada ya kusambaa kwa madai kuwa muigizaji Irene Uwoya amenasa ujauzito, imeelezwa kuwa mrembo huyo amejificha nyumbani kwa Video Queen matata Bongo, Agnes Gerald ‘Masogange’ kukwepa kamera za mapaparazi.

Awali, mtoa ubuyu makini alilitonya Amani kuwa licha ya kuwa mrembo ‘aliigiza ndoa’ na msanii wa Bongo Fleva, Abdulaziz Chende ‘Dogo Janja’ lakini kiuhalisia wanabanjuka kweli penzini hivyo bwa’mdogo huyo ndiye mhusika wa ujauzito huo.

“Kweli ile ndoa ilikuwa ni ya kwenye Tamthiliya ya Sarafu lakini bwa’mdogo alikuwa anapiga kweli sasa nasikia ndiyo hivyo tena kampa ujauzito,” kilisema chanzo hicho.

Kikizidi kushusha ubuyu huo, chanzo hicho kilidai kuwa Uwoya amekuwa akikwepa mapaparazi kwani anaona kama litakuwa ni jambo la aibu kwani uhusiano wao hakupenda uwe wazi.

“Si unajua Uwoya tangu awali alikuwa hapendi kuonesha kwamba ana uhusiano na Dogo Janja na ndiyo maana alikuwa akisema kuwa hana uhusiano naye licha ya Dogo Janja kudai amemuoa kweli Uwoya,” kilisema.

Makachero wa OFM walifika nyumbani kwa Uwoya, maeneo ya Sinza Mori na kuambiwa na majirani kuwa siku za karibuni, hawajamuona mrembo huyo nyumbani hapo.


“Hebu jaribuni kwa Masogange maana nasikia ndiyo kajificha huko,” kilisema chanzo hicho ambacho kilisema hakikusikia habari hizo za kwamba ni mjamzito.

Mapema wiki hii, makachero wa OFM walifika nyumbani kwa Masogange, maeneo ya Makongo Juu na kumkuta mfanyakazi wa ndani ambaye alikiri kuwa Uwoya yupo.

Kachero: Nimemkuta Uwoya?

Dada wa kazi: Ndiyo yupo?

Kachero: Naomba uniitie.

Dada wa kazi: Nimwambie nani?

Kachero: Mwambie (anataja jina lake na chombo anachotoka).

Baada ya muda mchache, dada huyo wa kazi alirejea na kusema kuwa Uwoya amelala na hata alipoulizwa kuhusu Masogange naye akasema amelala.

Siku iliyofuata, Masogange alipoulizwa kuhusu suala la kumficha Uwoya nyumbani kwake, alieleza jambo la tofauti na yule dada wa kazi aliyesema Uwoya kalala, akadai huwa anakwenda tu kumsalimia na kuondoka.

Alipotafutwa Dogo Janja ili kujua kama kweli mzigo ni wake, aliomba atafutwe Uwoya mwenyewe azungumzie suala hilo.

“Mimi niombe mumtafute Uwoya mwenyewe azungumze.”

Alipoulizwa Uwoya kuhusu suala la ujauzito na kujificha nyumbani kwa Masogange alikanusha na kusema si kweli kwani anaishi kwake.
Chanzo: Global Publishers

Msimbazi Vigogo Watofautiana Kisa Ujio wa Kocha Mpya

$
0
0
Msimbazi Vigogo Watofautiana Kisa Ujio wa Kocha Mpya
Sakata la kocha mpya wa kurithi mikoba ya Mcameroon, Joseph Omog limegubikwa na utata baada ya vigogo wa klabu hiyo kupishana kauli.

Klabu ya Simba imeanza mchakato wa kusaka kocha mpya baada ya kumtupia virago Omog na nafasi yake kujazwa na Mrundi Masoud Djuma.

Hata hivyo, utata umeibuka kuhusu nafasi ya Omog baada ya vigogo wa klabu hiyo kupigana kumbo kila mmoja akimtaja kocha anayeona anafaa kuinoa Simba.

Habari za ndani zimedokeza kuwa kumeibuka mvutano baina ya vigogo wa klabu hiyo kuhusu kocha sahihi wa kurithi nafasi ya Omog.

“Mvutano ni mkubwa kwasababu kila mmoja ana jina lake mfukoni, lakini ukweli ni kwamba Simba bado haijapata kocha rasmi wa kujaza nafasi ya Omog,”kilisema chanzo hicho.

Wakati Mjumbe wa Kamati ya Utendaji, Mohammed Nassoro akimtaja Mfaransa Hubert Velud kujaza nafasi ya Omog, Kaimu Rais wa Simba, Salim “Try Again” Abdallah amemkana kocha huyo.

Kauli ya Kaimu Rais

Abdallah alisema wanatafuta kocha mpya, lakini sio Velud aliyewahi kuzifundisha timu za TP Mazembe Englebert ya Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo (DRC) na Etoile du Sahel ya Tunisia.

Alisema kumekuwa na taarifa nyingi kuhusiana na kocha huyo, lakini akiwa ndiye kiongozi wa juu wa klabu hatambui ujio wake.

“Habari hizo si za kweli hazina maslahi ya klabu cha kushangaza taarifa zisizo rasmi zimekuwa nyingi, nimeamua kuweka wazi kuhusiana na suala hilo.

“Mimi sijui chochote kuhusiana na suala la kocha huyu anayetajwa sifahamu nani anamleta kwenye klabu yetu, labda kuna klabu nyingine tofauti na Simba. Kwa kifupi hatuna mpango na kocha huyo,” alisema Abdallah.

Akizungumza Dar es Salaam jana, Nassoro alisema Velud ndiye kocha mpya wa Simba na mchakato wa kumpa mkataba kabla ya kuanza kazi rasmi umeanza.

“Unaulizia mchakato wa kocha, umemalizika tupo katika maandalizi ya mkataba kwa ajili ya kuanza kazi, ”alisema kigogo huyo mwenye ushawishi ndani ya klabu hiyo kongwe nchini.

Mmoja wa viongozi wa juu wa Simba ambaye aliomba jina kuhifadhiwa, alisisitiza kuwa Mfaransa huyo ametua nchini na amefichwa kwa ajili ya kukamilisha utaratibu.

Kiongozi huyo alisema Velud aliwasili nchini siku tatu zilizopita kujiunga na Simba, lakini wameshindwa kumtambulisha kwa kuwa hana mkataba.

“Kocha yupo nchini lakini hatuwezi kumtangaza mpaka taratibu za mkataba zikamilike, kuna masuala mengi yanayohusiana na ajira kwa raia wa kigeni ngoja tumalize uongozi utatangaza rasmi,” alisema kiongozi huyo.

Dewji afunguka

Mwananchama mkongwe wa Simba ambaye pia ni Mjumbe wa Kamati ya Utendaji, Kassim Dewji alikataa kuzungumzia suala hilo kwa undani.

“Mimi sijui suala la kocha nilikuwa Kigali, Rwanda nimekuja kuona mechi ya Singida (kesho), kwa kweli sijui lolote wala chanzo chake japo najua klabu kwa sasa haina kocha mkuu,” alisema Dewji na kuomba suala hilo aulizwe Mohamed Nassoro.

Nuh Mziwanda na Nedy Music Wapewa Onyo Kali Watakiwa Kukaa Mbali na Shilole

$
0
0
Nuh Mziwanda na Nedy Music Wapewa Onyo Kali Watakiwa Kukaa Mbali na Shilole
Baada ya Shilole kufunga ndoa na mpenzi wake Uchebe, msanii Baba Levo amewataka Nuh Mziwanda na Nedy Music kukaa mbali na Shilole.

Nuh Mziwanda na Nedy Music waliwahi kutajwa kuwa katika mahusiano ya kimapenzi na Shilole kipindi cha nyuma.

Baba Levo amesema wasanii hao wasijewakatumia hicho kama kigezo cha kuendelea kwa karibu na Shilole kwani sasa ni mke wa mtu na endapo watafanya hivyo wataambulia makofi kutoka kwa uchebe.

“Hiki kilichotokea sasa hivi naomba Nuh Mziwanda Nedy Music sasa watulie Uchebe amekomaa atakupiga kofi, mtagongwa makofi biashara itaisha,” amesema.

“Na kuanzia sasa hivi Shilole atulie amuheshimu mume wake ambaye amekubaliana naye kuendesha maisha,” amesisitiza.

Usiku wa January 14 mwaka huu ndipo ilifanyika sherehe ya ndoa ya Shilole na Uchebe ambapo Baba Levo alikuwa MC wa shughuli hiyo.

Yanga Yabanwa Mbavu na Mwadui Yakubari Sare Tasa

$
0
0
Yanga Yabanwa Mbavu na Mwadui Yakubari Sare Tasa
Mchezo wa ligi kuu soka Tanzania Bara baina ya mabingwa watetezi klabu ya Yanga dhidi ya Nwadui FC umemalizika Uwanja wa Uhuru kwa timu hizo kutoka sare tasa ya bila kufungana.

Kwa matokeo hayo Yanga SC inasalia katika nafasi yake ya tano kwakuwa na ponti 22 wakati Mwadui FC ikiwa na alama 13 na kuzishusha Kagera Sugar, Ndanda FC na Mbeya City.

Michezo mingine ya ligi kuu inatarajiwa kupigwa hapo kesho ambapo vinara wa ligi Simba SC itakuwa mwenyeji kwa kuwakaribisha Singida United inayoshika nafasi ya tatu wakati Majimaji itakuwa mwenyeji dhidi ya matajiri wa Dar es Salaam wanalambalamba Azam FC wanaoshika nafasi ya pili mechi itayopigwa uwanja wa Majimaji.

Babu Tale Afunguka Kuhusu Mjengo wa Diamond wa WCB TV, Radio “Hatuja Nunua Nyumba"

$
0
0
Babu Tale Afunguka Kuhusu Mjengo wa Diamond wa WCB TV, Radio “Hatuja Nunua Nyumba"
Baada ya Story ya mjengo mpya alioupost Diamond Platnumz kushika headlines katika mitandao na hata vijiwe vya stori huku wengine wakisema kanunua na wengine wakisema kapangisha Meneja wa Diamond Platnumz Babu Tale Aeleza Ukweli.

Babu Tale alipoulizwa swali kuhusu mjengo huo amesema kuwa watazungumza baada ya kukaa na BASATA.

Babu Tale amesema hawajanunua nyumba na wao kama uongozi hawajazungumzia hilo suala ila wanasubiri kukaa na BASATA halafu watakuja kuzungumza na kusema kama wamenunua au wamepangisha na tarehe ambayo  Radio yao itafunguliwa.

Viwanja Posta Vyaingia Mikononi Mwa Wajanja

$
0
0
Viwanja Posta Vyaingia Mikononi Mwa Wajanja
SHIRIKA la Posta Tanzania, limeokoa viwanja vyake 198 katika maeneo mbalimbali nchini, vilivyokuwa vimeingia kwenye mikono ya wajanja wachache kwa ajili ya kujimilikisha.

Aidha, shirika hilo limedhibiti matumizi mabaya ya fedha, kujimilikisha mali za shirika na ubadhilifu mwingine uliosababisha kujiendesha kwa hasara na mali zake kupotea ovyo kwa miaka tisa.

Mwenyekiti wa Bodi ya Shirika la Posta, Dk. Haroun Kondo, aliwaambia waandishi wa habari jana jijini Dar es Salaam, walipoingia mwaka jana walikuta vinavyoendelea ni wizi, rushwa na ubadhilifu, huku mali nyingi za shirika zikiwa hazijaorodheshwa kokote.

“Tuliamua kufanya ziara mikoani. Wapo waliolalamika kwamba tunasafiri sana, lakini hilo lilitusaidia kujua mali za shirika zimemilikishwa watu. Tulienda mahali tukakuta kuna kituo cha mafuta imejengwa kwenye kiwanja cha Posta na hawajui kwamba ni mali yao, hawajawahi kukusanya hata senti moja,” alisema.

Alisema waliingia kukiwa hakuna fedha benki na Sh. bilioni 4 zimetumika nje ya matumizi, madeni zaidi ya Sh. bilioni 16 hayajakusanywa na walipokusanya (Bodi) Sh. bilioni 10 zikaishia mifukoni mwa wajanja.

Kwa mujibu wa Mwenyekiti huyo, Posta ilikuwa na akaunti za benki zipatazo 120, jambo lililozua shaka na bodi iliamua kuzifunga.

Alisema pia walipitia upya mikataba na watoa huduma mbalimbali, ubia katika maeneo ya matengenezo ya magari na usafirishaji wa vifurushi na kubaini ubadhilifu mkubwa, hivyo kuamua kufuta baadhi ya mikataba na mingine inaendelea kupitiwa.

“Kutokana na hayo wapo watumishi walifukuzwa, walifikishwa mahakamani, walikabidhiwa Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa (Takukuru) na kuwanyang’anya mali za shirika walizojimilikisha pamoja na kuondoa wafanyakazi 95 kwa kosa la vyeti feki,” alisema.

Dk. Kondo ambaye pia ni Luteni Kanali mstaafu wa jeshi, alisema wamekuja na mkakati mpya wa kuijenga Posta mpya kwa kununua magari madogo sita, malori matano na mabasi matatu.

“Shirika lilishindwa kutoa huduma vizuri kutokana na uchakavu wa magari. Tumeingia makubaliano na Bohari Kuu ya Dawa (MSD) kusambaza dawa mikoani kwa kutumia magari yetu 10. Tunaomba serikali iendelee kutumia huduma zetu ili tupate kipato zaidi,” alibainisha.

Aidha, alisema wanajiendesha bila ruzuku ya serikali na kuiomba kuiona ni Posta mpya na iwapo serikali itatumia huduma zake kama kusafirisha vifurushi, itawawezesha kupata mapato na kuchangia pato la Taifa. Posta ‘Express’

 Alisema Shirika hilo limeanzisha huduma Posta haraka kwa huduma zote kupatikana eneo moja na kuiomba serikali kuruhusu huduma za pasi za kusafiria na leseni kutolewa kwenye eneo la Posta.

 Mtendaji Mkuu wa Shirika hilo, Hassani Mwang’ombe, alisema uwapo wa kituo cha posta ‘Express’ kutawezesha wananchi kupata huduma sehemu moja na iwapo huduma za leseni na pasi za kusafiria zitaongeza mapato ya posta.


Daktari wa Kienyeji Adakwa na Polisi Kwa Kuwalaghai Wanawake Wenye Tatizo la Kushika Mimba

$
0
0
Daktari wa Kienyeji Adakwa na Polisi Kwa Kuwalaghai Wanawake Wenye Tatizo la Kushika Mimba
Polisi nchini Guinea wanasema kuwa wamemkamata daktari mmoja wa kienyeji kwa kuwalaghai mamia ya wanawake na kuwafanya kuamini kuwa wao ni wajawazito.

N'na Fanta Camara aliwapa wanawake ambao hawakuwa na uwezo wa kuwa wajawazito , dawa ya kienyeji ambayo ilisababisha tumbo zao kufura na kuonekana kuwa wao ni wajawazito.

Kutokana na huduma hizo wagonjwa walilipa dola 33 kwenye nchi ambayo kipato cha kila mwezi kinakadiriwa kuwa dola 48.

Polisi wanaamini kuwa Bi Camara alipata maelfu ya dola kila mwezi licha ya yeye kusema kuwa alijaribu tu kusaidia.

Siku ya Jumanne zaidi ya wanawake 200 waliandamana nje ya kituo cha polisi kwenye mji mkuu wa Guinea Conakry ambapo Bi Camara alikuwa akizuiliwa.

Zaidi ya wanawake 700 walio na kati ya umri wa miaka 17 na 45 wanaamiwa kuathiriwa na matibabu ya Bi Camara.

Idadi hiyo kubwa inaashiria jinsi Guinea na nchi zingine za Afrika zinawategemea madaktari wa kienyeji

Mwaka 2006 shirika la afya duniani lilisema kuwa asilimia 80 ya waafrika walitumia matibabu ya kienyeji

Woman with swollen stomachHaki miliki ya pichaALHASSAN SILLAH
Image caption
Baadhi ya wanawake walisema kuwa walionekana kuwa wajawazito kwa kati ya miezi 12 na 16.
Wanawake hao walisema kuwa Bi Camara aliwashauri wasimuone daktari, na mara alipothibitisha kuwa wamekuwa wajawazito walistahili kumpa kuku na vitambaa kama njia ya kumshukuru.

Baadhi ya wanawake walisema kuwa walionekana kuwa wajawazito kwa kati ya miezi 12 na 16.

Uwezekano wa mimea ya msituni kutumiwa kupanga uzazi
Daktari aliyewachunguza 47 kati ya wanawake walioathiriwa alisema wako kwenye hatari ya kukumbwa na matatizo ya kiafya ya muda mrefu kutokana na matibabu hayo.

Bi Camara hata hivyo anasema kuwa hajafanya lolote baya.

"Ninafanya kazi ngumu sana kuwasaidia wanawake kuweza kutimiza ndoto zao lakini mengine yako mikononi mwa Mungu, aliwambia waandishi wa habari mjini Conakry.

Pata Tiba ya Tatizo la Nguvu Za Kiume, Inasaidia Kukufanya Urudie Mara 5 na Kuchelewa Kwa Dakika 20

$
0
0
TATIZO LA UPUNGUFU WA NGUVU ZA KIUME NA MAUMBILE MADOGO LINATIBIKA.Baada ya utafiti wa mda mrefu juu ya matatizo ya upungufu wa nguvu za kiume na ukosaji wa hamu ya tendo la ndoa ama kushindwa kurudia tendo kwa haraka DR Magise imekuletea tiba ya matatizo hayo kwa kutumia dawa za:


FULL POWER: Ni dawa asili ya vidonge inayotibu tatizo la upungufu au ukosefu wa nguvu za kiume,dawa hii inamchanganyiko wakutosha wenyekuzalisha vichocheo vingi vya Hemone za Gestrogen vikiwemo vitamin B6&B1,vitamini E,pamoja na madini aina ya zinc vitakufanya kuwa na nguvu na mzunguko mzuri wa damu na kuongeza hamu na uwezo wa kufanya tendo la ndoa zaidi ya hatua nne au zaidi,na kuchelewa kufika kileleni zaidi dakka 20-30.


NYAMVA: Inarutubisha maumbile ya uume yani kurefusha na kunenepesha nchi 4-7 upana cm3-4 standard kiafya haijalishi umri wako hata kwa wazee ukiitumia maumbile yako yatabaki kuwa hivyo siku zote,Pia tunatibu Presha,kisukari siku7,ngiri,chango la tumbo tumbo kujaa gesi,kutopata choo vizuri

 TUPO TZ DAR ES SALAAM   MBAGALA RANGI TATU.HUDUMA HII UTALETEWA POPOTE ULIPO .WASILIANA NAMI 0783741788/ 0715741788 -DR MAGISE

Simba vs Singida Utd: Mechi ya Mashambulizi, Wachezaji, Mfumo Kumbeba Hans?

$
0
0
KAIMU kocha mkuu wa Simba, Masoud Djuma ameweka wazi timu yake itacheza mchezo wa kushambulia ili kupata matokeo watakapoikabili Singida United. Mpinzani wake Hans van der Pluijm pia ameitengeneza timu yake katika ‘umbo’ la mashambulizi hivyo mitazamo ya makocha hao wawili kuelekea mchezo wa Alhamisi hii katikas uwanja wa Taifa, Dar es Salaam ni kucheza soka la kushambulia.

Simba wanaongoza msimamo wa ligi wakiwa na alama 26, pointi tatu zaidi ya Singida United walio nafasi ya nne.  Kiufungaji Simba wameonekana kuwa bora zaidi kwa kuwa wamefanikiwa kufunga magoli 25, wakati Singida wamefunga mara 12 tu katika michezo 12. Timu zote zimeonekana kuwa na beki imara kwa sababu zimeruhusu magoli sita-kila timu.

Wachezaji, mfumo, kumbeba Hans

Licha ya kucheza ugenini sitarajii kuona Hans akibadili stahili yake ya uchezaji. Ataendelea kuwapanga walinzi wake wane, Shafiq Matambuze,  Michel Rusheshangoga katika beki za pembeni, Malik Antri na Kenedy Juma katika beki ya kati.

Kwa vyovyote, Djuma atalazimika kuwaanzisha John Bocco na Emmanuel Okwi katika safu ya mashambulizi. kuwapanga Okwi na Bocco kama washambuliaji wawili-pacha kutaifanya Singida kulazimika kumtumia Ken Ally kama kiungo mlinzi zaidi ambaye atakuwa na jukumu la kuwasaidia walinzi wa kati.

Kutumia mfumo wa 3-5-2 kama alivyofanya katika mchezo dhidi ya Ndanda FC, Djuma atakuwa ameruhusu timu yake kuwa hatarini kwa maana Batambuze na Michel ni walinzi wenye uwezo mkubwa wa kupandisha mashambulizi timilifu wakitokea pembeni

Hans atawapanga viungo watano katikati ya uwanja. Kenny, Deus Kaseke akishambulia kutokea upande wa kulia, Mudathir Yahya akicheza zaidi na kupanga mashambulizi akitokea kati, Kiggy Makassy akishambulia kutokea upande wa kushoto, Tafadzwa Kotinyu akicheza nyuma kidogo ya mshambulizi Daniel Lyanga.

Ili Simba wafanikiwe kubalansi mechi, wanatakiwa pia kuchezesha viungo wane katika mfumo wa 4-4-2. Erasto Nyoni akicheza katika beki ya kulia atasaidia kuipandisha haraka timu kutokana na mipira yake mirefu inayofika, Asante Kwassi  anaweza kufanya vizuri na kumzima Kaseke kama atachezeshwa beki ya kushoto, Juuko Murshid na Yusuph Mlipili wanafaa kutengeneza beki inayoweza kuifanya timu kujilinda na kushambulia haraka.

Kuwapanga, James Kotei, Mohamed Ibrahim, Shiza Kichuya na Said Ndemla nyuma ya Okwi na Bocco kunaweza kumpa matokeo mazuri Djuma kwa sababu viungo hao wane si wachezaji wanaopoteza hovyo mpira. Simba watatakiwa kuwa makini kwa kuwa Singida wameonyesha nidhamu kubwa ya kimchezo. Wanacheza kitimu, wana nguvu na stamina ya kutosha hivyo hawapotezi hovyo mpira katikati ya uwanja kama wanavyofanya Muzamiru Yassin na Jonas Mkude.

Hii ni mechi ambayo Hans anaweza kushinda kutokana na aina ya mfumo wake na wachezaji alionao na jinsi wanavyojituma. Uzoefu wake dhidi ya Djuma unaweza kumpa matokeo kwa sababu kocha huyo wa Simba ameonyesha kuwa muoga huku akihangaika kujua ni mfumo gani unaifaa timu yake. Nini kitatokea? Ni soka la kasi, ufundi huku mbinu za walimu na uwajibikaji wa wachezaji vikitarajiwa kuamua mshindi.

Hans van Pluijm: Siwaogopi Simba, nawaheshimu, tutawashangaza

$
0
0
Na Baraka Mbolembole

KUELEKEA mchezo wa Alhamis hii dhidi ya vinara Simba, kocha mkuu wa timu ya Singida United, Hans van der Pluijm amesema anawachukulia mabingwa hao wa zamani kama washindani wake wengine katika ligi na atakiingiza kikosi chake katika uwanja wa Taifa, Dar es Salaam kwa ‘tahadhari’ kubwa licha ya ukweli haihofii timu hiyo iliyofunga magoli 12 katika michezo 12 iliyopita.

“Naichukulia Simba kama timu nyingine. Siwezi kuweka akili yangu yote kwao.” Anasema Hans nilipofanya naye mahojiano Jumanne hii. Inatakiwa tuwe makini na tucheze mchezo wetu kwa kujitambua na kuimarisha morali ya timu nzima. Inatakiwa tufanye kazi yetu vizuri katika kila nafasi na katika uchezaji wa mpira pia.”

Singida wamepanda daraja msimu huu lakini namna timu hiyo inavyoendeshwa imesaidia kwa  kiasi kikubwa kusajili wachezaji mahiri kutoka ndani na ng’ambo, ikiwemo kumtwaa kocha Hans ambaye aliipa Yanga mataji mawili mfululizo ya ligi kuu.

Mudathir Yahya, Ken Ally, Deus Kaseke, Kiggy Makassy, Daniel Lyanga, golikipa Peter Manyika ni baadhi ya nyota wazawa ambao wamesajiliwa na klabu msimu huu. Mzimbabwe, Tafadzwa Kutinyu, Mganda, Shafiq Batambuze,  Wanyarwanda, Michael Rusheshangoga, Danny Usengimana wamefanya kikosi hicho kuwa imara na ushindi wowote utawafanya kuwa pointi sawa na Simba.

Hans ni kocha mwenye uzoefu mkubwa sasa hadi katika soka la Tanzania. Amewahi kuishinda Simba katika michezo yote miwili ya ligi kuu msimu wa 2015/16 ameendeleza aina ya soka lake la kushambulia katika kikosi cha Singida. Atawavaa Simba kwa mara ya kwanza akiwa nje ya kikosi cha Yanga huku akiwa na kumbukumbu ya kupoteza mchezo mmoja tu vs Simba.

“Mpira hautabiriki. Kila kitu kinawezekana, Simba bado ni timu kubwa na nawaheshimu lakini siwaogopi. Tunajiandaa vizuri na timu ipo katika morali, natumaini tunaweza kuwashangaza siku ya mchezo. Hii mechi wachezaji wanatakiwa wawe makini wao wenyewe ili tupate matokeo mazuri. Ni mechi yetu muhimu.” Anasema Hans ambaye atamkosa mfungaji wake namba moja Usengimana.

Singida wamekusanya alama 23 katika michezo 12 iliyopita. Wakiwa nafasi ya nne ya msimamo pointi  tatu nyuma ya Simba, timu hiyo kutoka mkoani Singida imeonyesha mwanga kuwa huenda wakawa washindani wa kweli katika mbio za ubingwa msimu huu kutokana na uimara wa timu yao.

“Njia bado ngumu, chochote kinaweza kutokea muda wowote. Tunaichukulia ligi ‘mchezo kwa mchezo’ mwishoni tutajua tulipofika. Inatakiwa tufanye kazi yetu vizuri.” Anamaliza kusema Hans.

Kiwanja Cha Kujenga Nyumba Kinauzwa Eneo la Mapinga Karibu na Bunju B

$
0
0
Kiwanja cha Kujenga Nyumba Kinauzwa , Kina Size ya 20 Kwa 20 Mita, Kipo Eneo la Mapinga Karibu na Bunju B, Mita 100 Kutoka Barabara ya Lami
Shilingi Mil 8.5 Maongezi yapo Kidogo

Piga simu 0714604974 Kwa Mawasiliano zaidi

Lemutuz Aendelea Kuteswa na Video Aliyopigwa Akitoka Kuoga..Afunguka Mengine Asubuhi ya leo

$
0
0

From @lemutuz_superbrandtz - LIVE STRAIGHT TALK:- The Art of Forgiving Mungu anasema KUSAMEHE NI SHERIA YAKE MUHIMU SANA ...nimesema nimemsamehe aliyenirekodi na wala sina kinyongo naye isipokuwa tu SIMUHITAJI tena karibu yangu cause Shetani akishindwa haina maana amekubali kushindwa ila anakutegea tu ili aje akutege tena next time sasa kwa sababu kashindwa na kale kavideo NEXT TIME ATAKUJA NA SUMU KWENYE CHAKULA ndio maana simuhitaji yule msichana karibu yangu tena for the rest of my life wala hata ku communicate naye tena or anything to do with her LAKINI NIMEMSAMEHE STRAIGHT FROM MY HEART....
so guys nawakumbusha tu kwamba jifunze kutoka mfano wangu SAMEHE cause ningeweza nikamkaanga na Sheria Uwezo ninao na Nguvu ninayo lakini nilichagua kumuheshimu Mungu na kufuata amri yake ya KUSAMEHE .....cause Mungu anasema kama wewe hujui kusamehe usitegemee any Msamaha kutoka kwake Mungu NA INFACT MUNGU ANASEMA TUJIFUNZE KUSAMEHE MARA 70 .....isipokuwa Mungu hajasema ukishasamehe uwe rafiki na uliyemsamehe HAPANA ....ndio maana Mungu anasema "IKIWEZEKANA ISHI KWA AMANI NA KILA MTU" ......ni kwa sababu hata Mungu anajua kuwa HAIWEZEKANI ....lakini Mungu anasema KUSAMEHE cause anajua kuwa INAWEZEKANA......kama nilivyosema Guys AKILI KUBWAZZZ huwa tunajifunza kutokana na Makosa na huwa hatuna aibu kusema Ukweli cause ndio unaotuweka huru binadam....JIFUNZE KUSAMEHE TENA HASA INAPOKUTOKEA ISHU MBAYA SANA ....na kumbuka marafiki zangu wote mliokuwa mnalilia nimkamate yule Msichana nilikuwa nawacheka sana moyoni cause nyie ni kama wale marafiki wa Ayubu kwenye Biblia mlikuwa mnatumwa na Shetani ....hahahahaha....ndio you were nothing but Devil's agents so next time ukijiona unalilia mtu asisamehe ujue unatumika na Shetani .
....guys mimi sio Mlokole wala Mchungaji ila nimesoma Chuo Cha Bible Studies New York/USA kwa Miaka 2 niliamua kusoma Mwaka 2005/2007 kwa faida yangu binafsi nilitaka KUMJUA MUNGU na KUIJUA BIBLE kwa ajili ya maisha yangu binafsi it worked cause guys the ishu sio kwenda Kanisani tu isipokuwa kutumia Elimu ya Kanisani kwa faida yako binafsi ....so GUYS TUJIFUNZE KUSAMEHE! ....na muhimu ni kwa Binadam kutomuonyesha Shetani kuwa ana nguvu cause HANA! - le Mutuz

Miujiza ya Sharifu Seif Mohamed..JE Umeachwa na Mme/Mke au Mpenzi, Umesongwa na Mitihani ya Maisha..Piga Simu Upate Muujiza Wako

$
0
0
SHARIFU SEIF MOHAMED ANAWASHUKURU WALE WOTE WANAOENDELEA KUPIGA SIMU, WENYE MATATIZO NA WALE WANAOTOA  SHUKRANI NA SHUHUDA JINSI TIBA ZAKE ZINAVYO WASAIDIA,

(Rudisha mahusiano yako ndani ya masaa 72 tu)

SHARIFU MOHAMED Ni  mtaalam na mnajimu maarufu wa nyota na kubashiri mambo yanayo watesa binadamu duniani kote na kupata ufumbuzi, Anatumia kitabu cha QUR'AN, Dawa za Asili, Dawa za Kiarabu na majini kwa kumtuliza mke/mme, mchumba au mpenzi ndani ya masaa 72 tu, na kutatua matatizo yote ya kimaisha,

Je Umeachwa na UMPENDAE awe Mme/Mke na bado unampenda? Je Umekimbiwa na Mmeo/ Mkeo n anaishi na mtu mwingine? Je Umejaribu sehemu nyingi bila mafanikio? Mpigie simu SHARIFU SEIF sasa hivi ujionee Muujiza wa Papo kwa Papo, Anauwezo wa hali ya juu wa kusambaratisha mahusiano yao na kumrejesha kwako haraka sana na Kumfanya Atimize Ahadi zote Ndani ya Muda Mfupi Endapo Utafwata Atakacho Kuelekeza

ANAZO DAWA ZA MAPENZI, NGUVU ZA KIUME, CHANGO NGIRI MAJI NA N.K, ZINDIKO LA NYUMBA NA BIASHARA, PETE ZA BAHATI, HUMALIZA KABISA TATIZO LA NGUVU ZA KIUME NA KUREFUSHA UUME KWA SAIZI UNAYOTAKA, HUZUIA CHUMA ULETE KWENYE BIASHARA, HURUDISHA MALI ZILIZOPOTEA, MAGONJWA SUGU, MIGUU KUWAKA MOTO AU KUFA GANZI, HUTIBU BUSHA BILA KUPASUA, ANAO UWEZO WA KUMRUDISHA ALIE MBALI AU ALIECHUKULIWA MSUKULE, KUPANDISHA NYOTA NA KUSHINDA BAHATI NA SIBU, KASAFISHA NYOTA NA KUKUPA MVUTO WA AJABU, KUTOA NUKSI NA VIFUNGO MBALIMBALI,  MAFANIKIO YA MAISHA NA UTAJIRI BILA MASHARI, NA MENGINE MENGI YA SIRI,

Je UMAHANGAIKA KUPATA MTOTO BILA MAFANIKIO? WASILIANA NA MTAALAMU HUYU KWANI YEYE HUFAULU PALE WOTE WALIPOSHINDWA, PIA UMALIZA KAZI ZILIZO SHINDIKANA NA WATAALAM WENGINE NDANI YA MASAA 24 TU,

(NA ANATIBU KWA NJIA YA SIMU UKIWA NCHI YOYOTE AU MKOA WOWOTE ENDAPO UTAFWATA MAELEKEZO YAKE)

Kwa ushauri na mawasiliano  zaidi Piga SIMU No:

Mobile +255 654-836970
WhatsApp +255 756-033670

Waombolezaji Watimua Mbio Baada ya Mtu Aliyedhaniwa Amekufa Kuibukia Msibani

$
0
0
Waombolezaji Watimua Mbio Baada ya Mtu Aliyedhaniwa Amekufa Kuibukia Msibani
Wakazi wa kijiji cha Marindi huko Kaunti ya Migori walipaniki na kuchanganyikiwa baada mwanaume wa miaka 35 ambaye aliaminika kuwa amefariki kuibukia msibani nyumbani kwake ghafla

Familia ya mwanaume huyo walikuwa wakimalizia mipango ya mazishi ndipo Okelo Nyamwaga alipojitokeza

Kufika kwake huko kusikotarajiwa kulileta hofu na furaha katika familia yake na marafiki na waombolezaji wengine kukimbia

Nyamwaga alikuwa amepotea kwa miezi miwili na familia yake ilipoteza matumaini ya kumpata akiwa hai

Wiki moja iliyopita marafiki wa Nyamwanga walisema mwili wake ukiwa umeharibika ulikuwa katika chumba cha kuhifadhia maiti cha Migori

Mwili huo uliokotwa mtoni ukiwa umeharibika na kupelekwa mochwari

Beki wa Liverpool Ahukumiwa Baada ya Kumpiga Mpenzi Wake

$
0
0
Beki wa Liverpool Ahukumiwa Baada ya Kumpiga Mpenzi Wake
Beki wa Liverpool ya England ambaye msimu wa 2016/2017 alikuwa akiichezea Burnley kwa mkopo Jon Flanagan amehukumiwa baada ya kukutwa na hatia ya kumpiga mpenzi wake.

Jon Flanagan amekutwa na hatia baada ya mahakama jijini Liverpool kujiridhisha na ushahidi, hivyo amehukumiwa saa 40 za kufanya kazi bila malipo na miezi 12 ya kufanya shughuli za kijamii.

Staa huyo mwenye umri wa miaka 25 alitenda kosa hilo kwa kumpiga Ms Wall ambaye ndio mpenzi wake December 22 wakiwa mtaa wa Duke jijini Liverpool.

Hii Hapa Zawadi Aliyoitoa Obama kwa Mkewe Kwenye Birthday Yake

$
0
0
Hii Hapa Zawadi Aliyoitoa Obama kwa Mkewe Kwenye Birthday Yake
Jumatano hii ya January 17 ilikuwa ni kumbukumbu ya siku ya kuzaliwa ya mke wa Rais wa 44 wa Marekani, Michelle Obama. Je unafahamu ni zawadi gani ambayo aliipokea kutoka kwa mumewe Barack Obama?

Kupitia mtandao wa Instagram Michelle amethibitisha kupokea zawadi ya maua kutoka kwa mumewe huyo.

Thank you @BarackObama for the beautiful flowers waiting for me in the office this morning. You’re my best friend, biggest fan, and getting notes and flowers from you will never get old. And to the many people from around the country who sent cards and posted on social media, you have no idea how much we love hearing from you. I know birthdays can sometimes be bittersweet (54!), but your messages of hope, generosity, and warmth have always reminded me how lucky and blessed we are.

Mbali na zawadi ya maua pia Obama amemuandikia mkewe huyo ujumbe unaosomeka, “Wewe sio tu mke wangu na mama wa watoto wangu, wewe ni rafiki yangu mzuri. Ninapenda nguvu zako, neema yako, na uamuzi wako. Na ninakupenda kila siku. Happy Birthday, @MichelleObama.”

Afande Sele: Muziki Umekosa Mtu wa Aina Yangu Mwenye Uzito wa Mashairi

$
0
0
Afande Sele: Muziki Umekosa Mtu wa Aina Yangu Mwenye Uzito wa Mashairi
Msanii Mkongwe wa Bongo Flava, Afande amefunguka sababu ya kukaa muda mrefu bila kutoa ngoma mpya.
Mkali huyo wa rhymes ameiambia Planet Bongo ya EA Radio yupo mbioni kutoa ngoma mpya kwani watu wake wanamuulizia sana kutokana na uzito wa mashairi yake.

“Mimi nina nyimbo nyingi zilizo bora isipokuwa nawaomba wanipe muda nafaikiri kabla ya Pasaka nitatoa wimbo mpya kwa ajili yao kwa sababu maombi yamekuwa mengi na nidhani wamekosa mawazo yangu na hakuna uzito wa mashairi kama yangu uliotokea katika taifa hili,” amesema Afande Sele.

Ameongeza kuwa muziki umekosa mtu wa aina yake na kilichomkimbiza katika game ni kushauriwa kufanya muziki wenye swag ambao yeye hauwezi.

Ngoma ya mwisho Afande Sele kutoa na kufanya vizuri inakwenda kwa jina Dini Tumeletewa ambayo alimshirikisha Belle 9.

Mambosasa Akanusha Tamko la Kuzuia Wanawake Kuvaa Vimini

$
0
0
Kamanda wa Polisi Kanda Maalum ya Dar es Salaam,  Lazaro Mambosasa amekanusha kutoa tamko la kuzuia wanawake kuvaa nguo fupi zisizo na heshima kwa maelezo kuwa  jambo hilo ni la kimaadili siyo sheria.

Amesema Jeshi la Polisi lina kazi ya kushughulikia makosa ya kisheria na si maadili.

Mambosasa ametoa kauli hiyo leo Januari 18, 2018 wakati akihojiwa katika kipindi cha 360 kinachorushwa na Redio Clouds, ikiwa ni siku mbili baada ya kunukuriwa katika mkutano wake na wanahabari kuwa amezuia uvaaji wa nguo fupi jijini Dar es Salaam.

 “Niliwaeleza wazi kuwa suala la mavazi bado halijatungiwa sheria hivyo polisi hatuhusiki nalo mtu anayevaa kimini katika maeneo kama kanisani au msikitini  ni ukiukwaji wa maadili,” amesema na kuongeza,

“Niliwaeleza  kuwa katika nyumba hizo za ibada kuna kamati ya ulinzi na usalama za eneo husika wao watakushughulikia lakini si polisi.”

Amesisitiza, “Nilikwenda mbali zaidi na kuwaeleza kuwa hivyo vimini kuna mahali vinahitajika kama ufukweni, sehemu za starehe. Ikitokea mtu amepigwa, amedhalilishwa au amekamatwa na askari kwa kuwa amevaa kimini ana haki ya kulalamika kuwa ameshambuliwa.”
Viewing all 104809 articles
Browse latest View live




Latest Images