Quantcast
Channel: UDAKU SPECIAL
Viewing all 104809 articles
Browse latest View live

“Singida United Mmetuletea Kitu Kipya Katika Soka la Bongo”-Shaffih Dauda

$
0
0
Bila shaka kila mtu ni shahidi juu ya picha ya mafanikio waliyoibeba Singida United ndani na nje ya uwanja kwa muda mfupi ambao wamerejea ligi kuu Tanzania bara.

Singida United ipo nafasi ya nne kwenye msimamo wa ligi ikiwa na pointi 23 nyuma ya Simba na Azam ambao wana pointi 26 katika nafasi ya kwanza na ya pili. Wamecheza mechi 12 hadi sasa wameshinda mechi sita, sare tano na kupoteza mchezo mmoja.

Walichokifanya kwenye Mapinduzi Cup kila mmoja amekiona, katika mechi sita walizocheza wamepoyeza mchezo mmoja tu wa nusu fainali dhidi ya Azam mchezo ambao uliwafanya waondolewe kwenye mashindano hayo ambayo walishiriki kwa mara ya kwanza katika historia.

Imetoa wachezaji watano (5) pamoja na kocha bora wa kikosi cha mashindano ya Mapinduzi msimu huu lakini katika mechi sita walizocheza, wachezaji wa Singida United walitajwa kuwa man of the match katika mechi tano.

Siku za nyuma kulikuwa na mechi za aina tatu ambazo zilikuwa zinaonekana zina mvuto, kwa maana kwamba mechi ya Simba vs (timu nyingine), Yanga vs (timu nyingine) na Yanga vs Simba hizo ndio zilikuwa mechi zinazofuatiliwa sana na wadau wa soka na kuonekana zina mvuto, lakini inapofika mechi za (timu nyingine) vs (timu nyingine) hakuna watu wanaofuatilia kwa hiyo matokeo yake ilijenga ushindani wa timu mbili ambazo zilikuwa zinapokezana.

Walipoingia Azam wakaongeza kifurushi cha nne, kwa maana ya kwamba, Simba vs (timu nyingine), Yanga vs (timu nyingine), Simba vs Yanga halafu iliyoongezeka ikawa Simba vs Azam na Yanga vs Azam lakini wigo ukaendelea kuzizunguka Simba na Yanga.

Ushindani wa Azam ulipoingia kati yao (Simba na Yanga) ukaongeza mzuka lakini kwa bahati mbaya Azam pamoja na ubora wake mpaka leo bado hawana wigo mpana wa mashabiki kitu ambacho kinaongeza thamani ya profile ya klabu ukiachilia mbali kubeba mataji mbalimbali lakini bado haina wafuasi wengi.

Kwa hiyo inapokuja mechi ya Azam vs (timu nyingine) bado mechi inakosa mzuka mkubwa, utamu wa mechi ya Azam vs Simba au Yanga unatokana na ushindani ambao Azam wamekuja nao lakini ujio wa Singida United ni changamoto nyingine na tofauti.

Uwezo wa kumchukua kocha Hans van Pluijm ni mara chache sana kuona kocha mwenye ubora kama wa Hans kwenda kufundisha timu za nje ya Dar kwa sababu ni mara nyingi makocha wote wakali wanaishia Dar, wakitoka hapo wanarudi makwao.

Kitendo cha Singida United kumchukua Hans kiliwashtua wengi na kuanza kujiuliza kuhusu nguvu ya klabu hiyo, wakati wanajiuliza juu ya hilo, mfungaji bora wa Rwanda Danny Usengimana akatua pale, Singida wakaonesha jeuri ya kumchukua Deus Kaseke ambaye aliivimbia Yanga impe mkataba mnono kama hawataki yuko tayari kuondoka na sio kwamba aliachwa, walishindwa kukubalia lakini Singida ilifikia dau la mchezaji huyo na kumchukua.

Namna wanavyoendesha mambo yao, idadi ya wadhamini walioingia mikataba na Singida United kabla hata ligi kuanza ikafanya watu waanze kufuatilia kwa karibu kuona uwekezaji uliofanywa itakuwaje uwanjani, kwa bahati nzuri hadi sasa hawajawaangusha watu. Kwa hiyo sasa hivi Singida United wamengia kwenye kundi la timu zinazopigania ubingwa (Singida United, Azam, Yanga, Simba na Mtibwa) licha kwamba Mtibwa huleta changamoto mwanzoni lakni mwishoni mwa msimu wanakimbia.

Kutokana na mazingira yalivyo sasa hivi, mechi zenye mvuto kwenye ligi zimeongezeka, zamani zilikuwa Simba vs (timu nyingune), Yanga vs timu nyingine) na Simba vs Yanga, baadae walivyokuja Azam zikaongezeka kwa hiyo ujio wa Singida United nao umeongeza changamoto kwa sababu mechi ya Singida dhidi ya timu nyingine inafuatiliwa, halafu mechi ya Azam na timu nyingine pia inafuatiliwa kwa sababu mashabiki wanataka kujua nini kitatokea huko ili kupata picha ya ushindani kwenye mbio za ubingwa wa ligi.

Kwa sasa ligi imetanuka na ushindani umeongezeka ukilinganisha na zamani, ushindani huu uachwe hivihivi ili timu inayostahili kuchukua ubingwa ichukue isijekufika sehemu yakafanyika magumashi na mizengwe ya kubadilisha mambo.

Zamani inapotajwa timu ya taifa, kuna wachezaji wakiitwa watu wote wanabaki kimya kwa sababu hakuna wengine zaidi ya hao walioitwa, lakini ligi ikiwa na ushindani ikitajwa timu ya taifa halafu hakuna jina la Habib Kiyombo, hakuna jina la Feisal Salum ‘Fei Toto’ watu lazima watahoji kwa sababu kuna wachezaji wengi wanye sifa za kuitwa na hiyo ndio inazua mijadala hata ukimuuliza kocha atakupa sababu kwa nini amemwita huyu akamwacha yule.

Kocha atakwambia kutokana na mechi tunayokwenda kucheza, tunahitaji kuwa na mchezaji wa aina fulani kulingana na mazingira ya mchezo lakini nimemuacha yule si kwa sababu ni mbaya bali hatofiti kwenye mechi ijayo. Kwa hiyo ushindani ukiwa mkubwa kwenye ligi inakuwa ni faida kwa nchi na si vilabu pekee.

Kutana na Mtabibu Wanyota Duniani Kote Maalim Fadhili Rashid Kutoka COMORO Kwa Sasa Yupo Tanzania

$
0
0
KUTANA NA MTABIBIBU WANYOTA DUNIANIKOTE MAALIM FADHILI RASHIDI KUTOKA COMORO KWA SASA YUPO TANZANIA NI BINGWA WAKUTIBU MARADHI SUGU KAMA VILE MIGUU KUUMA NA KUWAKA MOTO PRESHA KISUKARI VIDONDA VYA TUMBO PUMU

MAALIM FADHILI RASHIDI ANAJUWA UMEHANGAIKA SANA LAKINI HUJAFANIKIWA MUONE HARAKA AKUSAIDIE ANADAWA ZA KI COMRO DAWAZAKE HABAHATISHI MUONE HARAKA AKUSAIDIE TEZI NAUVIMBE TUMBONI ANAUWEZO WAKURUDISHA MTUALIE POTEA KIMAZINGIRA (MSUKURE) KUMFANYA MKE MUME MPENZI ASIKUSALITI DAWA YA (LIMBWATA) KUMTAWALA MPENZI WAKO UNAVYOTAKA KUMUONA MBAYA WAKO LIVE KWASABABI MALUM ANATOA PETE YA BAHATI INAYO ENDANA NA NYOTA YAKO ITAKAYO KULETEA MALI BILA YA MASHARITI NAKUMILIKI MALI ZAMAJINI DAWA YAKUONGEZA UUME ZAIZI UIPENDAYO DAWA YA NGUVU ZAKIUME PIA ANAYO DAWA YAKUONGEZA HIPS SHEPU KUWA NAUMBO BOMBA KAMA UMEIBIWA AMA KUDHULUMIWA UTARUDISHIWA MALIYAKO NDANI YA MASAA (24) ANAFUNGA KESI NAKUPATA HAKIYAKO DAWA YA MVUTO
WABIASHARA KUUZA MALIYAKO KWAHARAKA KUZUIYA CHUMAULETE KUSAFISHA NYOTA NAKUTOWA MIKOSI NA KUPANDISHWA CHEO KAZINI KARIBUNI WOTE TIBA NIKWADINI ZOTE UTAPATA HUDUMA POPOTE ULIPO DUNIANI

CALLING +255719362806/

WHATSAPP CALLING +255785786436/

Karibu Markson Beauty Wamezindua Products Mpya za Urembo za Kutengeneza Umbo, Ngozi na Nywele

$
0
0
MWAKA MPYA
MAMBO MAPYA
Katika kusherekea miaka kumi na nane (18) ya kampuni hii, @markson_beauty_pr imezindua bidhaa zake mpya. Bidhaa hizi mpya zimefanyiwa maboresho makubwa hivyo zina nguvu na matokeo ya haraka kuliko ilivyokuwa. Dawa zetu zimetengenezwa kwa mimea na matunda na hazina kemikali wala madhara. 100% ZIMETHIBITISHWA KIAFYA.
KWA WANAUME TUNATIBU👇👇
☆Kukosa hamu ya tendo.
☆Kuwahi kufika kileleni na kushindwa kurudia tendo.
☆Maumbile madogo ya uume.
☆Kuchoka sana wakati wa tendo na uume kusinyaa nk.
@markson_beauty_pr tumeandaa tiba bora kabisa kama ifuatavyo:-
1.HANDSOME UP ORIGINAL_ Inaongeza uume kwa size uipendayo na kuimarisha misuli (wiki 2) @250,000/=
2.SHARK POWER GELY_ Inaongeza uume inch 6 (wiki 4) @150,000/=
3VigRX CREAM_ Inaongeza uume inch 6.5 hadi 8 (wiki 2-3) @200,000/=
4.Vidonge maalum vya kuongeza nguvu na hamu ya tendo hata kwa wenye kisukari na BP @150,000/=
5. MAXMAN 2-Hii ni vidonge vinavyoongeza nguvu za kiume pamoja na uume @250,000/=
6.VIGA SPRAY OG_ Inaongeza uwezo ktk tendo na kuchelewesha kufika kileleni @150,000/=
PIA KWA WANAWAKE WANAOPENDA KUWA NA MUONEKANO MZURI ZIPO ZA👇👇👇
1.Kuongeza hips, makalio na mapaja @200,000/=
2.Kushepu mguu (CHUPA YA BIA) @150,000/=
3.Kuwa mweupe bila sugu kwa:-
(a)mafuta @150,000/=
(b) Vidonge @170,000
4.Kurefusha nywele na kuzuia kukatika ovyo @150,000/=
5.Kuongeza hips, makalio na mapaja kwa vidonge (YODI PILLS ORIGINAL) @250,000/=
6Kupunguza au kuongeza maziwa kuyasimamisha @150,000/=
7.Kubana uke na kuondoa uchafu ukeni @130,000/=
8.Kupunguza unene na manyama uzembe @150,000/=
9.Kufungua mirija ya uzazi na kupata ujauzito haraka @250,000/=
NB:Hakikisha unapata risiti yenye muhuri na garantii ili kukuhakikishia ubora na usalama wa bidhaa za MARKSON BEAUTY LTD

Wasiliana nasi Popote
ulipo duniani kwa (+255)
0767447444 au
0714335378
Bei hizi ni of a hadi tar 25/01/18

Wasiojulika Wachoma Nyumba Ya Kiongozi Wa CCM

$
0
0

Watu wasiojulikana wamedaiwa kuchoma moto nyumba ya Katibu wa Umoja wa Vijana Chama Cha Mapinduzi (CCM) wa Mkoa wa Iringa, Alphonce Muyinga iliyopo maeneo ya Kihesa njiapanda ya Kwabeda usiku wa kuamkia leo.


Kwa mujibu wa taarifa kikosi cha Zima Moto kilifanikiwa kufika katika nyumba hiyo na kujaribu kuzima moto huo ambao tayari ulikuwa umeshaleta athari ndani ya nyumba hiyo kwa mali mbalimbali zilizokuwepo ndani.

Mbali na hilo aliyekuwa Diwani wa kata ya Mwangata, Iringa kwa tiketi ya CHADEMA na baadaye kujiuzulu nafasi yake hiyo, Anjelus Mbogo naye amefanyiwa uharibifu katika nyumba ambayo alikuwa akijenga baada ya watu wasiojulikana kuibomoa nyumba hiyo.

"Kauli ya Mbunge ndiyo inaweza kuwa chanzo cha uchochezi kwa wananchi kuja kubomoa nyumba hizi kwa sababu yeye aliwaambia wananchi kama atajiuzulu wabomoe nyumba yake hata gari yake ichomwe moto nadhani wananchi wakachukua hilo kwani wananchi unapowashawishi ndivyo unavyomuaminisha kuja kufanya hivi huo ndiyo ukweli.

Na mimi sisemi mambo mengi kwa kuwa jambo hilo bado linaendelea na upelelezi lakini naamini wameniaminisha kuwa hatabaki mtu" alisema Anjelus Mbogo

Aliyejaribu Kuzuia Kupiga Chafya Apasuka Koo

$
0
0

Madaktari wameonya kwamba kuzuia kupiga chafya kwa kufunga pua na mdomo kunaweza kukusababishia madhara makubwa.

Hii inajiri baada ya madaktari mjini Leicester kumtibu mtu mwenye umri wa miaka 34 ambaye alipusuka koo kwa kujaribu kujizuia kupiga chafya.

Huku kukiwa hakuna nafasi ya hewa ya chafya hiyo kutoka, ililazimika kupasua tishu laini.

Licha ya kwamba kisa hicho sio cha kawaida, madaktari wameonya kwamba watu wengine wanafaa kujua kuhusu hatari hiyo.

Kuzuia kupiga chafya kunaweza kuharibu masikio mbali na kuathiri ubongo wameonya katika jarida la BMJ.

Mtu huyo anasema kuwa alihisi kuwashwa katika koo yake baada ya chafya hiyo na muda mchache baadaye akaanza kuhisi uchungu na akaanza kushindwa kula na kuzungumza.

Huddah Ajuta ‘Natamani Ningekuwa Mweusi na Mwenye Makalio Makubwa

$
0
0

Mfanyabiashara na mwanamitandao Huddah Monroe, ameanza kuitamani ngozi nyeusi katika mwili wake. 
Mrembo huyo aliyeamua kujikita katika biashara za urembo wa vipodozi ametoa kauli hiyo kupitia mtandao wa kijamii wa Snapchat kwa kuandika “You all know my obsession with dark skin. If I died today and come back. I could come back super super dark skinned, talk and skinny.With a little bit of ass.”

Mrembo huyo ambaye aliwahi kuwa ex wa rapper Prezzo amekuwa akidaiwa kujichubua ngozi yake baada ya kuanza kupata pesa nyingi.

Nay wa Mitego Aendelea Kuwa na Balaa la Kukataliwa na Mademu...Mrembo Nini Nae Amkana

$
0
0

Msanii wa muziki Bongo, Nini amefunguka kuhusu ukaribu wake na Nay wa Mitego.

Muimbaji huyo ambaye anafanya vizuri na ngoma ‘Niwe Dawa’ alioshirikiana na Nay ameiambia The Playlist ya Times Fm kuwa hajawahi kuwa na mahusiano ya kimapenzi na rapper huyo.

Kauli ya Nini anakuja baada ya hapo awali kuwepo taarifa kuwa sababu ya kutimuliwa MJ Record ni kuwa na mahusiano na Nay.

“Sina mahusiano ya kimapenzi na Nay, halafu hata kama ningekuwa nayo, kiupande wangu I don’t real think hiyo ni sababu ambayo ingeweza kumfanya yeye afanye kile alichokifanya,” amesema.

“Seriously sidhani kama mahusiano ya kimapenzi yanaweza kuathiri muziki, sina uhakika may be according to me navyofikiria lakini sidhani kama hiyo it can be specific reason,” amesisitiza.

Walimu 28 Watimuliwa kwa Ubadhirifu

$
0
0

Zanzibar. Serikali ya Mapinduzi Zanzibar imewafukuza kazi walimu 28 baada ya kugundulika kufanya ubadhirifu wa zaidi ya Sh100.4 milioni.

Akizungumza na waandishi wa habari Ikulu Mjini Zanzibar leo Jumatano, Katibu Mkuu Kiongozi, Abdul-Hamid Yahya Mzee amesema pamoja na kufukuzwa kazi walimu hao waliokua wakichukua mishahara hewa lakini pia wanatakiwa kulipa fedha hizo serikalini.

Amesema uamuzi huo umekuja baada ya uhakiki katika wizara mbalimbali za Serikali ya Zanzibar na kubaini kasoro ambazo watendaji wake walionekana kufanya makosa hayo kwa makusdi.

Amesema sababu za kufukuzwa kwa walimu hao ni kuchukua fedha za mishahara bila ya kuwepo kazini kwa muda mrefu huku wakishindwa kabisa kutoa taarifa kwa wahusika.

Mzee amesema kwa mujibu wa takwimu zao katika uchunguzi huo zinaonyesha watumisihi 46 wa Wizara ya Elimu visiwani hapa wamekuwa wakilipwa mishahara bila ya kustahiki kulipwa fedha hizo.

“Kwa mujibu wa takwimu zetu zinaonyesha kuwa watendaji waliokosa kuripoti kazini kwa muda mrefu ni 20 wagonjwa 8 na 6 hawakujitokeza kabisa katika uhakiki huo huku wengine wakishikiliwa kwa makosa mbalimbali.’’




Watu 2,624 Waathirika na Mafuriko Dodoma

$
0
0

Dodoma. Mbunge wa Chemba (CCM), Juma Nkamia amewaomba watu wa kada mbalimbali kutoa msaada kwa wananchi wa kata ya Mrijo mkoa wa Dodoma walioathirika na mafuriko yaliyotokana na mvua zinazoendelea kunyesha.

Akizungumza na waandishi wa habari bungeni leo Januari 17, 2018, Nkamia amesema jana wananchi wengine 161 wamekosa makazi kutokana na nyumba zao kuzingirwa maji.

Amesema watu hao 161 wamefanya idadi ya wasio na makazi katika kata hiyo na kuhifadhiwa  na ndugu na katika shule kufikia 2624.

Amesema vijiji vilivyoathirika ni Mrijo Chini, Kaloleni na Olborot, “Lakini hadi sasa hakuna watu wanaohusika na maafa waliofika kutoa msaada kwa wakazi hawa. Waliotoa msaada ni msalaba mwekundu tu tena wachache.”

“Msaada unaohitajika ni wa mahema, vyakula na mahitaji mengine ya binadamu.”

Mwananchi

Ujauzito Wamzuia Giggy Money Kukutana na Waziri Shonza

$
0
0

Dar es Salaam. Mazungumzo kati ya Naibu Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo, Juliana Shonza na mwanamuziki Giggy Money kuhusu picha za nusu utupu na kufungiwa kujishughulisha na sanaa yamekwama baada ya wote wawili kuugua.

Waziri Shonza akizungumza na Mwananchi jana Jumanne jioni amesema ameshindwa kukutana na msanii huyo kama walivyopanga kutokana na matatizo ya kiafya lakini amesisitiza kuwa agizo lake lipo pale pale.

Amesema alimwagiza msanii huyo afike ofisini kwake na kwamba atakutana naye pale hali yake kiafya itakapokaa sawa.

Kwa upande wake Giggy Money ambaye jina lake halisi ni Gift Stanford amesema ameshindwa kufika ofisini kwa waziri huyo kutokana na matatizo ya kiafya yanayomkabili.

Giggy Money ambaye awali alifika Baraza la Sanaa la Taifa (Basata) badala ya ofisini kwa waziri huyo kama lilivyokuwa agizo, alisema alipanga kuonana naye wiki iliyopita lakini alishindwa kufanya hivyo kutokana na kusumbuliwa na maradhi ambayo hakuyaweka bayana.


Habari Njema: Tunatibu Busha, Korodani Kuvimba,Ngiri, Miguu Kufa Ganzi Pamoja na Matatizo ya Nguvu za Kiume

$
0
0
Ni Dawa ya nguvu za kiume inayorefusha na kunenepesha uume saizi uipendayo (Inch 1-7) kwa muda wa siku 6 tu.Dozi hii itakufanya uchelewe kufika kileleni kwa muda wa dakika 30, utarudia tendo la ndoa zaidi ya mara 4 bila hamu kuisha bila kujali umri na garantee ni miaka 60 baada ya kutibu tatizo.

Pia tunatibu Busha bila kufanyiwa Oparesheni, korodani moja kuvimba, ngiri, tumbo kujaa gesi na kuunguruma, kutopata choo vizuri, miguu kuwaka moto na kufa ganzi, chango la wanawake, kisukari na kutokwa na kinyama sehemu ya haja kubwa.

MIHAYO:
Inarudisha mke, mchumba, hawara na atakutimizia kila kitu unachotaka kutoka kwake ndani ya  saa 2 tu hata kama yupo mbali. atarudi na kumfunga asiwe na mwingine zaidi yako.

Umefukuzwa kazini? unataka kupandishwa cheo? Umepoteza pesa zako kwenye biashara bila kujua umepandikizwa chuma ulete? Njoo urudishe pesa zako. Unauza mali yako haiendi?

Wasiliana na mtaalam Challo kwa; 0714006521

Onyo la Mwisho la JPM..Habari Zilizopo Katika Magazeti ya Leo Alhhamisi ya January 18

$
0
0


Onyo la Mwisho la JPM..Habari Zilizopo Katika Magazeti ya Leo Alhhamisi ya January 18

Waziri Mkuu Amcharukia Mhandisi wa Maji baada ya kutoridhishwa na utendaji wake.

$
0
0
WAZIRI MKUU Kassim Majaliwa amemkabidhi Mhandisi wa Maji wa Halmashauri ya wilaya ya Rorya, Mhandisi Obetto Sasi kwa Naibu Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais-TAMISEMI, Bw. Josephat Kandege baada ya kutoridhishwa na utendaji wake.

Ametoa uamuzi huo jana jioni (Jumanne, Januari 16, 2018) wakati aliposimamishwa na umati wa wananchi kwenye mji Mdogo wa Shitari alipokuwa njiani kuelekea kwenye kijiji cha Bubombi wilayani Rorya.

“Hatuwezi kuwa na mtumishi wa aina hii ambaye kila eneo tunakutana na changamoto za maji huku kukiwa hakuna hatua zinazochukuliwa licha ya Serikali kutoa fedha, hivyo namuagiza Katibu Tawala wa Mkoa alete mhandisi mwingine wa maji.”

Pia Waziri Mkuu amemuagiza Katibu Mkuu wa Wizara ya Maji na Umwagiliaji Profesa Kitila Mkumbo kwenda wilayani Rorya na kukagua mradi wa maji katika mji Mdogo wa Shirati na kuona namna ya kuutekeleza.

Amesema kwa sasa Serikali inatekeleza Kampeni ya Rais Dkt. John Magufuli ya kumtua mama ndoo. Kampeni hiyo  inalenga kuwaondolea wananchi tatizo la upatikanaji wa huduma ya maji safi na salama, hivyo itawachukulia hatua wote watakaokwamisha miradi ya maji.

Awali, Mkuu wa Mkoa wa Mara Bw. Adam Maliwa alimueleza Waziri Mkuu kwamba changamoto ya upatikanaji wa huduma ya maji safi na salama katika mkoa huo inatokana na watendaji wa idara hiyo kutokuwa na uwezo wa kutosha kiutendaji.

Wilaya ya Rorya inatekeleza miradi 11 ya maji ya bomba kupitia Programu ya Maji na Usafi wa Mazingira Vijijini (RWSSP) katika vijiji vya Kinesi, Randa, Utegi, Mika,Kirogo, Nyihara, Kisumwa,Nyamkonge, Nyambori, Gabimori na Marasibora.

IMETOLEWA NA:
OFISI YA WAZIRI MKUU

VIDEO: Msikilize Rais Magufuli Akipiga Marufuku Michango Yote Shuleni

$
0
0
Rais Dkt. John Magufuli leo Januari 17, 2018 amepiga marufuku aina yoyote ya michango katika shule za Serikali za msingi na Sekondari na kuwaagiza waziri Suleiman Jaffo na Waziri wa Elimu Profesa Joyce Ndalichako kusimamia hilo.

==Msikilize hapo chini

CCM Yazidi Kuwasomba Wapiinzani....Yazoa Wengine 36

$
0
0
Viongozi 17 wa ACT- WAZALENDO na 19 wa CHADEMA wa ngazi mbalimbali wakiwemo wajumbe wa Kamati kuu, Wenyeviti  na Makatibu wa mikoa, wilaya na kata kutoka mikoa mbalimbali wamevihama vyama vyao na kujiunga na CCM  tarehe 17 Januari 2018 katika  Mkutano wa Halmashauri  Kuu ya CCM Mkoa wa Kilimanjaro. Viongozi hao wamepokelewa na Katibu wa Halmashauri Kuu, Itikadi na Uenezi wa CCM Ndugu Humphrey Polepole.

Maamuzi ya viongozi hao yametokana na kile wanachodai kuwa vyama vyao vimehama kutoka kuwa taasisi za umma na kuwa kampuni za watu binafsi na wapambe wao, aidha, viongozi hao wamekiri kuridhishwa na kazi nzuri inayofanywa na serikali ya Chama Cha Mapinduzi (CCM) Awamu ya Tano na wameguswa na Mageuzi makubwa yanayofanywa na Chama Cha Mapinduzi (CCM) kipindi hiki.

Mmoja wa viongozi hao, aliyekuwa Mjumbe wa Kamati Kuu ya Chama cha ACT Wazalendo, Ndugu Kansa Mohammed Mbaruku amefafanua kuwa maamuzi hayo ya kukihama chama cha ACT na kujiunga na CCM ni kutokana kuwepo na  ugonjwa mkubwa sana uliyopo kwenye vyama vya upinzani, wa kutokutembea kwenye maneno na misingi yake, vinasema ni vyama vya kidemokrasia ila havina demokrasia kabisa na mambo mengi yanakwenda kinyume na misingi ya uanzishwaji wa vyama hivi na jambo hili linawakatisha tamaa wanachama wengi wa vyama hivi

Akizungumza kwa niaba ya wanachama wa Chadema waliohamia CCM, aliyekuwa Katibu Mwenezi wa Wilaya ya Siha, Ndg. Daniel Nkini amesema wamegundua Chama cha Mapinduzi katika masuala ya maendeleo hakibagui wananchi tofauti na ambavyo vyama vingine vimekuwa vikitenda.

Katibu wa Itikadi na Uenezi ambaye ndio alikuwa mgeni rasmi amewapokea viongozi hao waliokuwa wa vyama vya upinzani, amewahakikishia wamefanya uamuzi sahihi, wamechagua upande mzuri na washirikiane na wanachama wengine wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) kukijenga chama na nchi ya Tanzania.

Ndugu Polepole amewaapisha wanachama hao, Katika kiapo cha Imani na Ahadi za mwanachama wa CCM na akisisitiza umuhimu wa wanachama wapya na wale wazamani kujengeka kiitikadi na kiimani ya Chama na kuishi sawasawa na Imani, Itikadi na Ahadi za mwana CCM huku akinukuu usemi maarufu wa “Imani bila matendo imekufa”.

Huu ni muendelezo wa mamilioni ya watanzania wanaojiunga na CCM na mamia ya viongozi wa vyama vya upinzani kujiunga na Chama Cha Mapinduzi (CCM) katika awamu hii ya tano chini ya uongozi wa Ndugu John Pombe Joseph Magufuli Mwenyekiti wa CCM na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.

Imetolewa na,
IDARA YA ITIKADI NA UENEZI
CHAMA CHA MAPINDUZI (CCM)
MOSHI, KILIMANJARO

Waliopeperusha Bendera Ya Tanzania Bila Kibali Wapandishwa Kizimbani

$
0
0
WAKURUGENZI wawili wa Kampuni za Saha Limited  na Lucky Shipping Co.Ltd, wamefikishwa katika Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu wakikabiliwa na mashitaka mawili ya uhujumu uchumi ikiwemo kupeperusha bendera ya Tanzania bila kibali.

Washitakiwa hao ni Issa Haji au Salum (39) ambaye ni baharia na Mkurugenzi wa Kampuni ya Lucky Shipping pamoja na Abdullah Hanga (73) mfanyabiashara na Mkurugenzi wa Kampuni ya Saha ambaye ni mkazi wa Mbezi Beach.

Akisoma  mashitaka hayo jana mbele ya Hakimu Mkazi Mwandamizi, Victoria Nongwa, Wakili wa Serikali, Wankyo Saimon alidai washitakiwa walijihusisha na mtandao wa uhalifu kinyume na aya 4(1) C, jedwali la kwanza na kifungu cha 57(1) na 60 (2) cha Sheria ya Uhujumu uchumi.

Saimon alidai kuwa Julai 19, mwaka jana na Januari 16, mwaka huu jijini Dar es Salaam, walitoa ushauri, msaada na maelekezo katika kutenda kosa la jinai la mtandao wa uhalifu ambalo ni kupeperusha bendera ya Tanzania kwenye meli iitwayo Huihang 68 zamani ilijulikana kama Greko 02, bila kuwa na hati ya usajili kutoka kwa msajili wa meli nchini kwa lengo la kujipatia faida kutoka katika shughuli za uvuvi haramu.

Pia alidai kuwa Julai 19, mwaka jana na Januari 16, mwaka huu, katika jiji la Dar es Salaam washitakiwa hao huku wakifahamu kuwa ni kosa kisheria waliruhusu upeperushwaji wa bendera katika meli hiyo ya Huihang 68 au zamani ilijulikana kama Greko 02 bila kuwa na leseni kutoka kwa msajili wa meli kwa lengo la kuifanya ionekane kuwa ya Tanzania wakati sio kweli.

Hakimu Nongwa alisema washitakiwa hao hawatakiwi kujibu chochote kwa kuwa mahakama hiyo haina mamlaka ya kusikiliza shauri hilo.

Hata hivyo, Saimon alidai kuwa upelelezi wa shauri hilo upo katika hatua za mwisho kukamilika hivyo wanaomba tarehe nyingine kwa ajili ya kuieleza mahakama taarifa za upelelezi huo.

Wakili wa utetezi, Dismas Raphael aliiomba mahakama ijielekeze katika Katiba ambayo inawatambua washitakiwa hao kama watuhumiwa na kwamba iwatendee haki kwa kuwapatia dhamana.

Akijibu hoja hiyo, Saimon alidai kuwa Mkurugenzi wa Mashitaka nchini (DPP), amewasilisha hati ya kuzuia dhamana kwa washitakiwa hao kwani wakipewa dhamana wataingilia maslahi ya Taifa hivyo mahakama ijielekeze katika suala hilo.

Pia alidai Ibara ya 59 (B) ibara ndogo ya 3 inaainisha mamlaka ya DPP kuhusu masuala yote yanayolenga maslahi ya Taifa kama ilivyoainishwa kwenye Katiba.

“Kama upande wa utetezi wanalenga kuipinga hati ya kuzuia dhamana wanatakiwa wafuate taratibu nyingine katika mahakama za Kikatiba ambapo watakapowasilisha maombi yao, sisi tutayajibu ndipo mahakama itatoa maamuzi,” alidai Saimon.

Hakimu Nongwa alisema upande wa utetezi uwasilishe mapingamizi yao kuhusu hati hiyo na upande wa mashitaka ujibu na kwamba mahakama hiyo itatoa maamuzi kama hati hiyo ni sahihi au la.

Hata hivyo, aliahirisha kesi hiyo hadi Januari 22, mwaka huu kwa ajili ya kutajwa na kwamba washitakiwa hao wamerudishwa rumande.

Mwisho

Soma Nafasi za Ajira Zilizotangazwa Leo

Je Una Upungufu wa Nguvu za Kiume, Hamu ya Tendo la Ndoa au Maumbile Madogo ya Uume?

$
0
0

JE, UNA UPUNGUFU WA NGUVU ZA KIUME, HAMU YA TENDO LA NDOA AU MAUMBILE MADOGO YA UUME?
SOMA HAPA👇👇.
Tatizo la upungufu wa nguvu za kiume au ukosefu wa hamu ya tendo la ndoa limezidi kuongezeka kwa kasi duniani kote na limekuwa chanzo kikubwa cha ndoa nyingi na mahusiano kukosa uaminifu kutokana na wengi kutoka nje ya ndoa ili kupata mtu atakayemtosheleza na kumfikisha kileleni. Pia udogo wa maumbile ni tatizo kubwa na limekuwa likiwakosesha wanaume wengi uwezo wa kujiamini katika tendo na kusababisha tendo hilo kutokufanyika kwa usahihi. Hili pia huchangia kwa kiasi kikubwa wanawake wengi kwenda nje ya ndoa ( MAHUSIANO) kutafuta mbadala wake.
BAADHI YA DALILI ZA UPUNGUFU WA NGUVU ZA KIUME NI KAMA:-
☆Kukosa hamu ya tendo la ndoa
☆Uume kusimama kwa ulegevu
☆Kuwahi kufika kileleni
☆Uume kusinyaa katikati ya tendo
☆Kushindwa kurudia tendo kwa wakati
☆Kuchoka sana baada ya round ya kwanza na hata kukinai kabisa.

Kwa kutumia mimea na matunda bila kemikali 🍇🍍🍓🌿🍉🍒🍎🍑 @markson_beauty_pr Tunakuletea suluhisho la matatizo hayo hata kwa wenye "KISUKARI NA PRESSURE" kwa:-
1.HANDSOME UP ORIGINAL:- kifaa chenye uwezo wa 99% kuongeza uume kwa size uipendayo na kuimarisha misuli ya uume iliyolegea @250,000/=
2.SHARK POWER ni gely ya kupaka inayoongeza uume kwa wastani wa inch 5.5 hadi 6 @150,000/=
3.VigRX CREAM:- ni gely iliyoboreshwa mahususi kwa ajili ya kuongeza maumbile kwa wastani wa inch 6.5 hadi 8 na kuimarisha misuli ya uume iliyolegea @200,000/=
4.Vidonge maalum kwa ajili ya kuongeza nguvu na hamu ya tendo la ndoa hata kwa wenye kisukari @150,000/=
5.Spray ya kuchelewesha kufika kileleni na kuweza kurudia tendo ×3. @150,000/=
BIDHAA HIZI HAZINA MADHARA KIAFYA NA ZIMETHIBITISHWA
NA SHIRIKA LA AFYA DUNIANI (WHO).
KWA BIDHAA HIZI NA NYINGINE NYINGI TEMBELEA UKURASA WETU WA INSTAGRAM :-
@markson_beauty_pr
@markson_beauty_pr
@markson_beauty_pr
WEB:www.markbeauty.org
Wasiliana nasi Popote
ulipo duniani kwa (+255)
0767447444 na
0714335378
UTAPATA HUDUMA
NB:Matokeo ni uhakika na garantii na hakikisha unapata risiti yenye muhuri halisi wa MARKSON CO pamoja na garantii ili kukuhakikishia kufanikiwa kwako.

Kamati ya Kuchunguza Madini ya Tanzanite Yaanza Kazi

$
0
0
Kamati ya Kuchunguza Madini ya Tanzanite Yaanza Kazi
Kamati iliyoundwa na Rais John Magufuli kuchunguza biashara ya madini ya Tanzanite imeanza kufanya mazungumzo na kampuni ya Tanzanite One.

Mwenyekiti wa kamati hiyo  Waziri wa Katiba na Sheria Profesa  Palamagamba Kabudi amesema mazungumzo hayo yaliyoanza jana  Januari 16 , 2018 yanalenga kuhakikisha Tanzania inanufaika ipasavyo na rasilimali ya madini hayo ambayo yanachimbwa nchini Tanzania pekee.

Profesa Kabudi amesema mazungumzo yameanza vizuri ambapo pande hizo mbili zinapitia matatizo yote yanayohusu biashara ya madini ya Tanzanite, utekelezaji wa sheria na kanuni mbalimbali za madini na mapato ya rasilimali hiyo, ili hatimaye zikubaliane namna bora itakayohakikisha Tanzania inanufaika ipasavyo.

Rais Magufuli Afanya Uteuzi Amteua Dkt. Mwinuka Kuwa Mkurugenzi Mtendaji wa Tanesco

$
0
0
Rais Magufuli Afanya Uteuzi Amteua Dkt. Mwinuka Kuwa Mkurugenzi Mtendaji  wa Tanesco
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. John Pombe Magufuli leo tarehe 17 Januari, 2018 amemteua Dkt. Titus Mwinuka kuwa Mkurugenzi Mtendaji wa Shirika la Umeme Tanzania (TANESCO).

Mnamo Januari 1, 2017 , Rais John Pombe Magufuli alitengua uteuzi wa aliyekuwa Mkurugenzi Mtendaji wa Shirika la Umeme Tanzania (TANESCO), Mhandisi Felchesmi Mramba na kumteua Dk Tito Esau Mwinuka kuwa Kaimu Mkurugenzi wa shirika hilo.

Kwa mwaka 2017 Mkurugenzi wa Tanesco, Mhandisi Felchesmi Mramba alikuwa mfanyakazi wa kwanza kutumbuliwa na Rais John Pombe Magufuli
Viewing all 104809 articles
Browse latest View live




Latest Images