Quantcast
Channel: UDAKU SPECIAL
Viewing all 104809 articles
Browse latest View live

Pata Dawa Bora ya Nguvu za Kiume na Maumbile Madogo ya Kiume ( Super Shafti)

$
0
0
DAWA BORA YA NGUVU ZA KIUME NA MAUMBILE MADOGO YA KIUME ( SUPER SHAFITI) NI DAWA YENYE UWEZO MKUBWA WAKUTIBU UPUNGUFU WA NGUVU ZA KIUME


 (SUPER SHAFITI ni dawa ya asili yenye uwezo mkubwa wa kuogeza nguvu za kiume maradufu
(1) itakufanya uwe na nguvu za ajabu ukiwa unafanya ntedo la ndoa
(2) inaogeza hamu ya kurudia ntedo la ndoa zaidi ya mara tatu bila kuchoka
( 3) itakufanya uchelewe kufika kileleni dani ya dk 30
( 4)  itaimalisha milija ya uume iliyo legea au kusinyaa
(5) lnarefusha na kunenepesha uume saizi utakavyo kuazia ichi 1-8 unene sm 2-4
 (6) itakupa nguvu za kusimamiasha uume wako barabara kama_ msumari wakati wa ntedo la ndoa
(7) inasaidia kusafisha mishipa. ya kwenye uume na hivyo kusaidia Katika kuongeza kasi ya msukumo wa damu kwenye mishipa ya uume
(8) usaidia kuurudisha nje uume ulioingia ndani
(9) inasaidia kuogeza manii nyingi ambazo vina viini vya uzazi
(10)usaidia kutibu madhara ya punyeto ,matumizi makali ya  madawa ya kizugu mirungi bangi na sigara

KWA NINI BAADHI YA WANAUME WENGI WANA UPUNGUFU WA NGUVU ZA KIUME NA KUWA NA MAUMBILE MADOGO YA KIUME NINI CHANZO CHAKE?

ni kutokana na magonjwa megi kuongezeka yakiwemo kisukari presha ya kupanda na kushuka upigaji wa punyeto wa mda mrefu magonjwa ya moyo ngiri ya kuviba korondani vidonda vya tumbo
Msongo wa mawazo  tumbo kuuguruma kujaa ngesi kutopata choo vinzuri maumivu ya mgongo kiuno na tumiaji wa madawa makali ya kizungu ya kuongeza nguvu za kiume kuzaliwa na chango linaloshabulia neva za ukuwaji wa uume utumiaji wa mirungi bangi sigara na nk  tunapenda kuwatangazia wasomaji, wa makala zetu kuwa tunazo dawa nzuri za asili ambazo hazina mazala na zinazotibu na kuponyesha matatizo ya upungufu wa nguvu za kiume na maumbile ya kiume

NA TUNATIBU MAGONJWA YOTE SUGU KAMA KISUKARI PRESHA AINA YOTE UGONJWA WA MOYO SITRUKO KWIKWI KICHOMI MINGUU KUFA NGAZI ASIMA NK MZEE ISAYA ANAPATIKANA MAGOMENI MIKUMI KARIBU NA KANISA  TUMAINI HEBRAST CLINI NDIYO JIBU NA SULULISHO YA MATATIZO YOTE

PIGA simu 0745495181 au 0682644040

Kwa watu wa mikoa huduma utatumiwa na watu wa nje ya nchi utazipata dsm kama huna nafasi ya kufika ofisini kwetu utaletewa popote ulipo

Kutana na Mtabibu Mwenye KUBRI kutoka kwa ALLAH issa simba said Mtabibu wa Nyota za Binadamu na Dawa za Asili

$
0
0
Kutana na Mtabibu Mwenye KUBRI kutoka kwa ALLAH issa simba said Mtabibu wa Nyota za Binadamu na Dawa za Asili ya Africa Mwenye UWEZO Kubaini tatizo lako Pindi tu Utakapo Fanya Mawasilino Kupitia Wasaa Husika..JE UNASUMBULIWA NA Mapenzi? (Umeachwa na Umpendae,Awe Mume,Mke na Bado unampenda?Na Umejaribu Sehemu nyingi Bila Mafanikio?Wasilina na Maalim Hussein Ujione muujiza wa Papo kwa Papo.. anauwezo WA KURUDISHA MAHUSIANO NA KUIMARISHA NDOA YAKO NDANI YA SAA 12 TU. Umekimbiwa na Mumeo,mkeo au Mpenzi na anaishi na mtu mwingine? Muone akutatulie Anauwezo wa Hali ya Juu wa Kusambalatisha Mahusiano yao Endapo utafata Atakacho kuelekeza.
Atamfanya Atimize Ahadi zote kwa Muda Mfupi.

Issa simba said Anatumia Jina la Muhusika au Picha Kumaliza Tatizo lako..
Anatibu kwa Kutumia Vitabu vya QUR-AN Dawa za Asili za Africa,Dawa za Kiarabu na Majini.Anatafsiri Ndoto. Kushinda BAHATI NASIBU, KUSAFISHA NYOTA. Mvuto wa Mwili na BIASHARA, Kinga ya Mwili,ZINDIKO za Nyumba.MIGUU Kufa GANZI.Kufungua KIZAZI kwa wale walio fungwa kwa njia za KISHIRIKINA. Anakupa Jini la Mali kwa yule anaehitaji Utajiri BILA MASHARTI. Nguvu za KIUME, Humaliza Kesi zilishindika ndani ya siku 14 tu..na mengi zaidi

Wasiliana nasi  Kwa Numba Hizi +255 622588038 , 0679119679 , +255 764318107, 0656145170, 0762899488

CCM yatoa Sababu za Kutaka Mtulia Achaguliwe Tena

$
0
0
Kada wa CCM, Dk Mwigulu Nchemba ameeleza sababu za kuwaomba wapigakura wa Jimbo la Kinondoni kumchagua mgombea ubunge wa chama hicho, Maulid Mtulia.

Dk Nchemba aliyewahi kuwa naibu katibu mkuu wa chama hicho (Bara), alisema hayo jana wakati wa uzinduzi wa kampeni za CCM uliofanyika katika Viwanja vya Biafra jijini Dar es Salaam.

Mtulia alijiondoa CUF Desemba 2, mwaka jana hivyo kupoteza ubunge wa jimbo hilo na baadaye alijiunga na CCM ambayo imempitisha kuwania tena kiti hicho katika uchaguzi mdogo utakaofanyika Februari 17.

Dk Nchemba alikuwa mgeni rasmi katika kampeni hizo ambazo zilikuwa za aina yake licha ya kutokuwapo mjumbe yeyote wa sekretarieti ya chama hicho kama ilivyo kawaida.


Baadhi ya wajumbe wa NEC akiwamo Steven Wasira walinogesha kampeni hizo zilizokuwa na vikundi mbalimbali vya burudani kikiwamo cha TOT.

Dk Nchemba ambaye pia ni Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi alisema mgombea wa CCM ndiye mwenye uwezo wa kutatua matatizo ya wananchi kwa kuwa ilani inayotekelezwa ni ya chama hicho kilichopo madarakani.

Alisema kuchagua mgombea wa upinzani ni kujikosesha maendeleo kwa kuwa hawawezi kuzifikisha hoja za matatizo ya wananchi sehemu husika.

Huku akisindikizwa na vibwagizo vya nyimbo za TOT, Dk Nchemba ambaye pia ni mbunge wa Iramba Magharibi, alisema mgombea wa CCM ana uwezo wa kukutana na viongozi wa Serikali kuzungumzia matatizo ya wananchi tofauti na wagombea wa upinzani.

Alisema uchaguzi utakaofanyika licha ya kuitwa ni mdogo, lakini ni mkubwa kwa CCM na inauchukulia kwa uzito kwa kuwa ni jambo la kitaifa na ina masilahi nao. Alisema baada ya uzinduzi wa kampeni, kila mmoja awe meneja wa mgombea wa chama hicho.

Dk Nchemba alisema kwa kuangalia tathmini ya hali ya siasa, ajenda za kitaifa zinatekelezwa na CCM hivyo kuhoji mtu anabaki upinzani kufanya nini.

Alisema changamoto kubwa kwa mbunge ni kushindwa kutekeleza ajenda aliyowaahidi wananchi, hivyo akiona hana namna ya kutekeleza ni muhimu kuhama.

Wakati Dk Nchemba akiendelea kuhutubia, baadhi ya vikundi vya uhamasishaji navyo vilikuwa vikiendelea kuzunguka kwenye Uwanja wa Biafra kuhamasisha wananchi waliohudhuria mkutano huo.

“Siasa safi ni kuipongeza Serikali inapofanya vizuri, lakini kwa Tanzania Serikali ikifanya jambo jema kabisa mtu wa upinzani akasifia kesho yake ni kikao cha kuulizwa ni kwa nini unasifia na wakati mwingine wapinzani wanafanya kila namna kukwamisha mipango hiyo,” alisema.

Dk Nchemba alisema, “Wengine hata si wawakilishi, juzi mzee kaenda Ikulu kumsalimia, kesho yake kikao, anaulizwa kwa nini ulimsifia Rais.

“Hata bungeni mpinzani anaweza kwenda kwa waziri moja kwa moja, lakini akienda anaulizwa kwa nini ameenda upande mwingine.”

Alisema, “Mtulia aliangalia hasara ya mwezi mmoja na hasara ya miaka iliyobakia akaona bora ya mwezi mmoja ili baadaye awe mbunge bora.”

Dk Nchemba alisema Mtulia amefanya hesabu zitakazomsaidia kuacha kumbukumbu ya uongozi bora jimboni humo.

“Mipango yote inayotengewa fedha ni Ilani, hakuna mwingine mwenye sera au ilani yake atapangiwa fedha, ni sawa na kupigia kura kivuli, ili usipoteze muda wako, mpigie Mtulia mwenye ilani,” alisema.

“Hata uweke lugha nzuri kiasi gani vocha za Tigo haziingii Vodacom, kawaida kabisa unapoteza kura yako, mwenye ilani umemwona ni Mtulia.”

Dk Nchemba alisema kazi inayofanywa na Rais John Magufuli itabakia kwenye historia ya Tanzania.

“Zaidi ya Sh20 bilioni inatumika kupanua Bandari ya Dar es Salaam, mtu akisema anataka kujiunga na historia hiyo kuna kosa gani? Kuna watu wanalalamika vitu vidogo sana vinavyosemwa, ni mpito tu, eti pesa imeisha... Unatumia pesa ili upate pesa,” alisema.

Huku akishangiliwa na wananchi waliohudhuria, alisema “Huwezi kununua ndege, kujenga reli na kupanua bandari halafu fedha ibaki vilevile. Ukimaliza hayo ndiyo unaanza kushughulika na mishahara. Anachotengeza Rais ni kutaka kujitegemea, huwezi kupandisha mshahara kwa mikopo ya kuomba, kwa hiyo hakuna kosa kwa wale wanaokuja kujiunga na historia hii.

“Haiwezekani upeleke mtu ambaye kazi yake ni kutukana tu, hata sala hazikuwekwa kihasara. Zote ni sifa kwanza kabla ya kuomba (akitumia mfano wa sala ya Baba Yetu) ikishakolea ndiyo unapiga mizinga, sasa uchague mtu kazi yake kutukana?” alisema.

Waziri huyo wa Mambo ya Ndani alisema watazuia vurugu wakati wa kampeni na kuwataka wananchi kufanya kampeni kwa amani na utulivu huku akionya kuwa atakayefanya fujo atashughulikiwa.

Kabla ya kumleta mgombea jukwani kunadi sera zake, Dk Nchemba aliwapokea kwanza wanachama wa Chadema waliojiunga CCM akiwamo aliyekuwa diwani wa Kata ya Kimara, Pascal Manota.

Ikiwa imesalia takribani dakika tano kufika saa 12.00 jioni, Dk Nchemba alimkaribisha jukwaani Mtulia ambaye alianza kujinadi kwa kujiita mjanja kwa kwa kuthubutu kuacha kiinua mgongo bungeni.

Pia alijinadi kwa kuiweka hadharani familia yake wakiwamo mkewe, watoto na mama yake mzazi kwamba hiyo ni tofauti aliyonayo na wagombea wengine.

Akijinadi kwa wananchi, Mtulia alisema alizuia bomoabomoa iliyokuwa ikitekelezwa na Serikali jimboni humo.

Pia, alisema anampenda sana Rais Magufuli na kwamba, alipokuwa mbunge kwa miaka miwili hakuwa na namba (ya simu) ya kiongozi huyo mkuu wa nchi.

Alisema baada ya kuingia CCM, namba hiyo anayo, hivyo akaomba apewe ubunge ili akawatumikie kwa kumueleza Rais matatizo yao.

Mtulia ambaye kabla ya kuzungumza na wananchi alionyesha kadi yake ya CCM na kitambulisho cha mpiga kura, aliwaomba waliohudhuria mkutano huo kuwa mabalozi wake kwa kumuombea kura.

Akimnadi mgombea huyo, Wasira alisema wakazi wa Kinondoni na maeneo mengine yanayoongozwa na Chadema yalichukuliwa kwa makosa.

Alisema tuhuma kuwa Mtulia ameingia CCM kwa kununuliwa hazina mashiko.

“Alipotoka Nyalandu (Lazaro aliyekuwa mbunge wa Singida Kaskazini kwa tiketi ya CCM) nikawa nasubiri kusikia wao walitumia shilingi ngapi kumnunua, lakini kimya,” alisema.

Wasira alisema katika Uchaguzi Mkuu wa mwaka 2015, Chadema iliwadanganya wapiga kura jimboni humo kuwa itapeleka mabadiliko lakini haikuwa hivyo.

“Wananchi walidanganywa Mkoa wa Dar es Salaam kwa mabadiliko ya kuzungusha mikononi tu, sasa wamegundua makosa, kule Arusha wamejiondoa madiwani kumi na moja, Longido walijua mapema kwamba wasingeshinda sasa wamejileta Kinondoni, ndugu zangu naomba mtoe kura kwa Mtulia mapema kabisa,” alisema Wasira.

Mwananchi

''Kwa Hili CHADEMA Mnajisumbua'' Wananchi Hawawezi Kupigia Kivuli Kura Wakati Kuna Mtu

$
0
0
Mbunge wa Iramba Magharibi na Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Mwigulu Nchemba amesema atawashangaa sana kuona wananchi wa jimbo la Kinondoni wakimpigia kura mgombea wa CHADEMA Salum Mwalimu kwa madai Ilani inayofanya kazi ni moja tena ya CCM.

 Mhe. Mwigulu ameeleza hayo leo wakati wa akizindua kampeni hizo za uchaguzi mdogo katika Jimbo la Kinondoni ambapo upande wa CCM wamemsimamisha mgombea Mtulia Said Maulid ambaye hapo awali yeye ndiye alikuwa Mbunge wa Jimbo hilo kupitia CUF kabla hajajivua unachama wake na kuenda kumuunga mkono Rais Magufuli katika kujenga Taifa la Tanzania.

"Msije mkaenda kupiga kura ya uchaguzi mdogo kwa kiwango cha uchaguzi mdogo, twendeni tukapige kura kwa uzito ule ule kwamba ni jambo la msingi, la kitaifa na jambo la chama chetu lenye maslahi mapana nalo. Tutakapo tawanyika hapa kila mmoja awe kampeni meneja wa mgombea wetu na aje na wapiga kura siku hiyo ya kupiga kura", alisema Mwigulu.

Pamoja na hayo, Mwigulu amedai CCM inasababu zote za kushinda uchaguzi huo mdogo wa marudio kwa sababu Ilani inayotekelezwa ni moja ambayo ni CCM na itaishi mpaka 2020.

 "Leo hii ukifuata uhalisia sababu zote za msingi za ushindi tunazo sisi lakini wao watabaki na moja tu kwamba kwa nini Mtulia alihama. Ilani ya uchaguzi iliyochaguliwa ni ya CCM na itatekelezwa hadi mwaka 2020, asitokee mtu ambaye atawadanganya, kumpigia kura mtu wakati hana ilani inayotekelezeka ni sawa na kupigia kivuli wakati kuna mtu", alisisitiza Mwigulu.

Kwa upande mwingine, Mhe. Mwigulu amewasii wananchi wa jimbo hilo kuwa makini wasije kudanganywa na mtu yeyote kwamba ana sera nzuri kwa sababu hakuna sera nyingine inayotekelezwa zaidi ya CCM.

Wanamuziki Nandy na Ruby Hapatoshi..Waanza Kurushiana Vijembe Upya..Kisa Kugombania Number Clouds FM

$
0
0
Msanii wa muziki wa kike hapa bongo ambaye hivi sasa ndio gumzo kwenye game, Nandy, amesema kitendo cha Ruby kusema kuwa kwake kimya alikuwa anampisha, alikuwa ana tafuta kisingizio kwani bado alikuwepo kwenye game.

Akizungumza kwenye 5SELEKT ya East Africa Television, Nandy amesema kwa Ruby kusema hivyo ni kisingizio, kwani wakati yeye anaanza kufanya vizuri, Ruby alikuwa ana kazi alizoachia baada ya kugombana na uongozi wake wa awali.

 “Sio kweli kwa sababu nakumbuka wakati ambapo amegombana na uongozi wake, ana nyimbo tatu alizotoa, siamini kitu kama hicho, hapo alikuwa amepumzika au, ni kitu ambacho sio cha kweli, watu wengi wanajua Ruby alikuwa amegombana na uongozi wake na ndio akatoa hizo nyimbo, kwa hiyo kikawa kama kisingizio, alikuwa anatafuta kisingizio”, amesema Nandy.

Wasanii hao wawili inasemekana hawana maelewano mazuri tangu watu waibue hisia kwamba Nandy amekuja kuchukua nafasi ya Ruby kwenye uongozi wake wa awali, ambao ndio ulimuweka juu kwenye game.

“Kukaa Juu Namba Moja Juu ya Yanga Kuna Raha yake Bwana”-Haji Manara

$
0
0
Leo Jumapili Januari 28, 2018 Simba itacheza mchezo wa ligi kuu dhidi ya Majimaji kwenye uwanja wa taifa, kuelekea mechi hiyo afisa habari wa Simba Haji Manara amsema kukaa juu ya msimamo wa ligi kuna raha yake lakini haitakuwa na maana endapo watapoteza au kutaka sare kwenye mchezo wa leo.

“Wachezaji wetu wameahidi kujituma kuhakikisha tunapata pointi tatu ili kuendelea kukaa juu kwa uhuru zaidi, pale juu pana raha yake najua kwa matokeo yoyote ya mechi yetu na Majimaji tunaendelea kukaa juu, lakini haitakuwa na maana kama unakaa juu huku umefungwa au umetoka draw raha ya kukaa juu uwe umeshinda tena ushindi mzuri.”

Manara amesema majimaji ni timu nzuri wanaiheshimu kwa historia yake kwenye soka la bongo pamoja na rekodi yao nzuri ilipokutana na timu zinazofanya vizuri msimu huu.

“Ni timu nzuri yenye wachezaji wazuri na rekodi zao ni nzuri kwa timu ambazo zinafanya vizuri msimu huu Yanga, Singida United, Azam na hata Prisons hakuna timu iliyowafunga Majimaji kwa hiyo sisi hatuendi pale tukiwa tunawadharau, tunajua tunahitaji pointi tatu.”

Kuhusu presha ya Azam na Yanga ambazo zipo nyuma yao, Manara amesema, timu hizo haziwashughulishi wanachoangalia ni timu wanayokutananayo.

“Hawa wa nyuma tusishughulike nao sana, sisi tushughulike na na yule tunayecheza nae, tukishinda mechi zetu zote hawa wanyuma vyovyote itakavyokuwa hawatushughulishi. Lazima tuangalie anayekuja kucheza na sisi tusimwangalie Azam Yanga, Singida United hao tayari wapo nyuma yetu kama tutaendelea kushinda mechi zetu hata wafanye nini hawawezi kutufikia.”

Maneno ya Cannavaro Baada ya Ushindi wa Yanga vs Azam

$
0
0
Nahodha wa yanga Nadir Haroub ‘Cannavaro’ anadai kuwa, azam ni timu anayoikubali kwa hapa bongo na kupata ushindi dhidi kwenye uwanja wao si jambo dogo.

“Kushinda dhidi ya Azam si kitu kidogo, ni timu nzuri ambayo naikubali kwa Tanzania lakini nashukuru tumeweza kupata ushindi dhidi yao”-amesema Cannavaro ambaye ni mchezazi wa muda mrefu zaidi kwa sasa kwenye kikosi cha Yanga.

Licha ya kutocheza katika mchezo huo, Cannavaro anaamini matunda ya ushindi huo ni umoja uliopo kati ya wachezaji wanaocheza na wale wa nje ya uwanja.

“Nimefurahi kwa sababu yanga ni kama familia tunashukuru tumeweza kupata ushindi na watu wote wanaocheza na wasiocheza tumekuwa kitu kimoja na kuweza kupata pointi tatu ugenini.”

Mkongwe huyo amesema tayari kama wachezaji wameshakubalina kushinda kila mechi inayokuja mbelke yao: “Tumekubaliana kwamba ili tuweze kutetea ubingwa ni lazima tushinde mechi.

Licha ya ushindi dhidi ya azam kuifanya yanga ipunguze pengo la pointi, cannavaro bado anawaheshimu wapinzani wao wanaoongoza ligi kwa sasa.

“Bado ligi ni ngumu na tumeachwa na Simba, mpira wa kitanzania haujapishana sana ikiwa tutachanga karata zetu vizuri tunaweza kutetea ubingwa wetu vizuri.

Wassira: Nyalandu ameanza kuwapigia simu baadhi ya viongozi wa CCM.

$
0
0
Wakati akihutubia kwenye mkutano wa kumnadi mgombea wa CCM, Maulid Mtulia, Mzee Wassira alisikika akisema Lazaro Nyalandu ameanza kuwapigia simu baadhi ya viongozi wa CCM ili aongee nao kuhusu hatima yake ndani ya CHADEMA.

Wassira anamshangaa Nyalandu kwa kushindwa kufanya utafiti sahihi kuhusu CHADEMA kabla hajaamua kujiondoa CCM na kuhamia CHADEMA na amewashauri wamsikilize na kumuuliza alichokiona CHADEMA kwa muda mfupi mpaka kuanza kufikiria hatima yake ndani ya CHADEMA.

VIDEO:

Habari Njema: Tunatibu Busha, Korodani Kuvimba,Ngiri, Miguu Kufa Ganzi Pamoja na Matatizo ya Nguvu za Kiume

$
0
0

Ni Dawa ya nguvu za kiume inayorefusha na kunenepesha uume saizi uipendayo (Inch 1-7) kwa muda wa siku 6 tu.Dozi hii itakufanya uchelewe kufika kileleni kwa muda wa dakika 30, utarudia tendo la ndoa zaidi ya mara 4 bila hamu kuisha bila kujali umri na garantee ni miaka 60 baada ya kutibu tatizo.

Pia tunatibu Busha bila kufanyiwa Oparesheni, korodani moja kuvimba, ngiri, tumbo kujaa gesi na kuunguruma, kutopata choo vizuri, miguu kuwaka moto na kufa ganzi, chango la wanawake, kisukari na kutokwa na kinyama sehemu ya haja kubwa.

MIHAYO:
Inarudisha mke, mchumba, hawara na atakutimizia kila kitu unachotaka kutoka kwake ndani ya  saa 2 tu hata kama yupo mbali. atarudi na kumfunga asiwe na mwingine zaidi yako.

Umefukuzwa kazini? unataka kupandishwa cheo? Umepoteza pesa zako kwenye biashara bila kujua umepandikizwa chuma ulete? Njoo urudishe pesa zako. Unauza mali yako haiendi?


Wasiliana na mtaalam Challo kwa; 0714006521 

Dr Shein "Nitaondoka Nikimaliza Muda Wangu wa Kikatiba, Swala la Miaka 7 Nalisikia tu Mimi Halinihusu"

$
0
0
Rais wa Zanzibar Dr Shein amesema atatoka madarakani pindi atakapomaliza muda wake wa kikatiba na kwamba habari za kuongeza muda kuwa miaka 7 hata yeye amezisikia. Dr Shein amesema swala la kuongeza muda linajadiliwa na Baraza la Wawakilishi na kamwe hawezi kuwaingilia maana huenda wanajadili muhula wa Rais atakayemfuatia. Dr Shein ameyasema hayo akiwa airport mara baada ya kuwasili akitokea ziarani katika nchi za falme za kiarabu.

Source ITV habari!

‘Msishangae sisi Kuwataja CHADEMA Hapa, Hao ndio Mashetani Wetu Hapa’-Wasira

$
0
0
Chama cha Mapinduzi (CCM) kilifanya uzinduzi wa kampeni katika viwanja vya Biafra kwa ajili ya kumnadi mgombea Ubunge Jimbo la Kinondoni Maulid Mtulia, miongoni mwa waliopanda katika jukwaa hilo ni  aliyekuwa Waziri wa Kilimo, Chakula na Ushirika Stephen Wasira,

Wasira ameeleza sababu kwa nini wanakitaja Chama cha CHADEMA katika mikutano yao na kusema chama hicho ndio shetani wao kwa hiyo lazima wakitaje. Pia akakumbushia hotuba ya Mgombea Urais wa  CHADEMA katika uchaguzi wa mwaka 2015 na kusema ilikuwa fupi kuliko sala ya “Baba yetu uliye Mbinguni”

VIDEO: Alikiba Amtembelea mama mzazi wa Rais Magufuli nyumbani kwake wilaya ya Chato

$
0
0
Msanii wa muziki wa kizazi kipya Ali kina akiwa na kundi wametembela hospital mbali mbali na kuwaona wagonjwa , Kwa kuwa walipita chato wakaamua kumuona mama Magufuli nyumbani kwake

Kijana alikiba ni miongoni mwa wanamuziki wanaofanya vizuri na wanaotambua kazi ya muziki na umuhimu wake

VIDEO:

Wastara Amfungukia Mange Kimambi na Wanaomtuhumu Kuwa Tapeli

$
0
0
Msanii wa filamu wa bongo Wastara Juma ambaye hivi karibuni amepewa mchango wa milioni 15 na familia ya Rais Magufuli, amewajibu watu wanaomtuhumu kuwa tapeli kwani hana ugonjwa unaomsumbua.

Akizungumza na mwandishi wa www.eatv.tv Wastara amesema kabla ya kuomba michango alijitahidi sana kujitafutia mwenyewe hiyo pesa kwani hakutaka pesa ya mtu mwengine ije imsaidie, kwani alijiona anakuwa mzigo kwa jamii.

Kufuatia kauli hiyo Wastara amesema alishajaribu kujiingiza kwenye biashara ambazo amedai hazina faida, mpaka kufikia hatua ya kuanza kuuza vitu vya ndani, jambo ambalo msanii mwenzake Steve Nyerere alimkataza, na kumshauri aweke wazi matatizo yake iili watu wamsaidie.

Akiendelea kulalamikia kitendo cha watu kumdhihaki, amesema asilimia kubwa ya watu wanaomtuhumu hawajahi hata kwenda kumuona wakiwemo wasanii wenzake, ambao waliamua kumtenga baada ya yeye kuolewa na aliyekuwa Mbunge wa CCM Sadifa.

Baadhi ya wasanii wamesikika wakiongea chini chini kuwa Wastara anajidai kuumwa ili apate hela , pia Mwanadada Mange Kimambi amemlipua Wastara kupitia ukurasa wake wa Instagram

Dawa Bora za Nguvu za Kiume na Kukosa Hamu ya Tendo la Ndoa

$
0
0
DAWA BORA ZA NGUVU ZA KIUME NA KUKOSA HAMU YA TENDO LA NDOA
Baada ya utafiti wa muda mrefu juu ya matatinzo ya upungufu wa nguvu za kiume na ukosaji wa hamu ya tendo la ndoa ama kushindwa kurundia tendo kwa haraka Sasa inakuletea suluhisho juu ya matatizo haya kwa kutumia dawa za FULL POWER

Full Power dawa asili yenye vidonge inayotibu tatizo la upungufu au ukosefu wa nguvu za kiume dawa hii inamchanganyiko wa kutosha kuzalisha vichocheo vingi vya hernone za gestro gen zikiwemo vitamin b6 na b1 vitamin e pamoja na madini aina ya zinc

Itakufanya kuwa na nguvu na mzunguko mzuri wa damu na kuongeza hamu na uwezo wakufanya tendo la ndoa zaidi hatua nne au zaidi na kuchelewa kufika kileleni zaidi ya dakika 20/30 ZAT 50

Inarundisha maumbile ya uume yaani kurefusha na kunenepesha nchi 3/7 na upana cm 3/4 standard.kiafya haijalishi umri wako hata kwa wazee ukitumia maumbile yatabaki kuwa hivyo siku zote pia anatibu matatizo mengine kama presha kisukari ngiri chango la tumbo kujaa gesi kutopata choo vizuri minguu kuwaka moto matatizo ya uzazi bawasili na magonjwa ya zinaa kama kisonono na kaswende

Tunapatikana Dar es Salaam  na mikoan wasiliana na DR Oshinda no 0755505099 au 0714126118  Karibuni kwa hunduma bora

Klabu ya Simba SC Haikamatiki...Yamchapa Mtu 4 Bila..Yanga Mlie tuu

$
0
0

Klabu ya Simba SC yaibuka na Ushindi wa mabao 4-0 dhidi ya Majimaji FC na kuendelea kujiimarisha kileleni mwa Ligi kwa alama 35
-
Magoli ya Simba SC yamefungwa na John Bocco dakika ya 12, 27 pamoja na Emmanuel Okwi aliyefunga dakika ya 52 na 68
-
Sasa Simba SC anaongoza Ligi Kuu Soka Tanzania Bara kwa tofauti ya alama 5

Dawa Bora za Nguvu za Kiume na Kukosa Hamu ya Tendo la Ndoa

$
0
0

DAWA BORA ZA NGUVU ZA KIUME NA KUKOSA HAMU YA TENDO LA NDOA
Baada ya utafiti wa muda mrefu juu ya matatinzo ya upungufu wa nguvu za kiume na ukosaji wa hamu ya tendo la ndoa ama kushindwa kurundia tendo kwa haraka Sasa inakuletea suluhisho juu ya matatizo haya kwa kutumia dawa za FULL POWER

Full Power dawa asili yenye vidonge inayotibu tatizo la upungufu au ukosefu wa nguvu za kiume dawa hii inamchanganyiko wa kutosha kuzalisha vichocheo vingi vya hernone za gestro gen zikiwemo vitamin b6 na b1 vitamin e pamoja na madini aina ya zinc

Itakufanya kuwa na nguvu na mzunguko mzuri wa damu na kuongeza hamu na uwezo wakufanya tendo la ndoa zaidi hatua nne au zaidi na kuchelewa kufika kileleni zaidi ya dakika 20/30 ZAT 50

Inarundisha maumbile ya uume yaani kurefusha na kunenepesha nchi 3/7 na upana cm 3/4 standard.kiafya haijalishi umri wako hata kwa wazee ukitumia maumbile yatabaki kuwa hivyo siku zote pia anatibu matatizo mengine kama presha kisukari ngiri chango la tumbo kujaa gesi kutopata choo vizuri minguu kuwaka moto matatizo ya uzazi bawasili na magonjwa ya zinaa kama kisonono na kaswende

Tunapatikana Dar es Salaam

Wema na Diamond Ndo Habari ya Mjini Leo..Waonekana Kwenye Sherehe Wakipeana Mahaba Motomoto

$
0
0
Wale wapenda ubuyu wenzangu tembeleeni kwa dada wa taifa kuna video mubashara kabisa ya Tz Sweetheart na kaka Abdul Naseeb. Mapenzi yamerudi kwa kasi ya ajabu sana. Zarina ni muda sasa aamue kuondoka akaelee au aendelee kubanana na Wema na kwa hali ilipofikia Diamond hawezi kumuacha tena Wema hata awe aoe Wema ataendelea kuwepo..

Tazama VIDEO:

Mkubwa Fella Atumbua Jipu "Nataka Diamond ufanye kolabo na Alikiba"

$
0
0
Meneja wa Diamond Platnumz, Mkubwa Fella amesema kuwa anataka kolabo ya Diamond na Alikiba ifanyike haraka kabla hajaaga dunia.

Tazama VIDEO:

Trump amjibu Jay Z kuhusu Afrika na ‘Wamarekani Weusi’

$
0
0
Rais wa Marekani, Donald Trump amemjibu rapa Jay Z kwa kile alichokisema kwenye mahojiano na CNN kuhusu matamshi ya kibaguzi yanayodaiwa kutolewa na kiongozi huyo.

Akizungumza katika mahojiano maalum kwenye kipindi cha The Van Jones Show wiki hii, rapa huyo nguli ambaye jina lake halisi ni Shawn Carter alikosoa vikali matamshi yanayodaiwa kuwa ya Trump akiizita nchi za afrika kuwa ni nchi chafu (nchi za shimo la choo).

“Ndiyo, inaumiza sana na inatuangusha. Kila mtu alisikia hasira. Baada ya hasira inaumiza kweli kama mtu anawadharau watu wote,” alisema na kuongeza kuwa ingawa amekanusha matamshi hayo, hivyo ndivyo watu humzungumzia.

Rapa huyo alienda mbali akimkosoa Trump kwa vitendo vya kibaguzi na kumuita kuwa ni mdudu aliyeshindikana kwa dawa (superbug).

Alipinga kauli kuwa Marekani sasa imeongeza idadi ya ajira hasa kwa nchi za Afrika kama inavyodaiwa na Serikali ya Trump.

Leo, Trump ametumia mtandao wa Twitter kama ilivyo kawaida yake na kumjibu Jay-Z akimtaja jina, akisisitiza kuwa tangu aingie madarakani idadi ya Wamarekani Weusi wasio na ajira imeshuka.

“Mtu mmoja amtaarifu Jay –Z tafadhali kwamba kwa sababu ya sera zangu, idadi ya watu weusi wasio na ajira wameripotiwa kuwa katika KIWANGO CHA CHINI KUWAHI KUTOKEA,” inasomeka tweet ya Trump.

Tanzania yaibuka kinara Afrika uchumi jumuishi....Watalaamu Waitabiria Makubwa Zaidi

$
0
0
Baada ya Tanzania kuibuka kinara wa Uchumi Jumuishi barani Afrika, baadhi ya Wataalamu wa masuala ya uchumi nchini wameelezea kuwa hatua zinazochikuliwa na Serikali kuwawezesha wanachi kuwekeza katika shughuli za kiuchumi na utoaji bora wa huduma za jamii vitaufanya uchumi wa Tanzania kuendelea kukua zaidi.

Wakitoa maoni yao juu ya dhana ya uchumi jumuishi, baadhi ya wataalamu hao wamesema kuwa madiliko ya sera na sheria zinawawezesha wananchi wengi kumiliki uchumi ni sehemu ya vigezo vya kuufanya uchumi kukua huku ukigusa maisha ya wananchi walio wengi.

Katibu Mtendaji wa Baraza la Taifa la Uwezeshaji Kiuchumi, Bi. Bengi Issa ameielezea dhana ya uchumi jumuishi kuwa ni ile ambayo shughuli za kiuchumi zinawajumuisha moja kwa moja wananchi na kwamba mabadiliko ya sheria katika sekta ya madini na katika umiliki wa makampuni ya simu yametoa fursa kwa watanzania wengi kushirikikatika uchumi.

Amesema kuwa utekelezaji wa sera ya elimu bure kuanzia shule ya msingi hadi kidato cha nne, kuimarishwa kwa huduma za afya, maji, umeme pamoja na mapambano dhidi ya rushwa, hifadhi ya jamii na utekelezaji wa miradi ambayo inawapa fursa wananchi kushirikikatika shughli a kiuchumi ni miongoni mwa sifa zinazoifanya Tanzania kushika nafasi ya juu.

“Serikali inaweka mazingira bora ya wananchi kushiriki shughuli za kiuchumi katika miradi mbalimbali. Tunahakikisha kila mradi unaoingia nchini basi wafanyabiashara wa Tanzania wanashiriki kikamilifu katika utekelezaji wa mradi huo”, alifafanua Bi. Bengi.

Amesema kwa upande wa Baraza la Taifa la Uwezeshaji Kiuchumi wamekuwa wakishiriki katika kuweka mipango na sera ili kuhakikisha Watanzania wengi wanashiriki shughuli zakiuchumi ikiwemo kumiliki ardhi ili iwasaidie katika kutafuta mitaji ya biashara.

Nae Mtaalam wa Uchumi wa Kilimo ambaye pia aliwahi kuwa Mkurugenzi wa Taasisi ya ESRF, Dkt. Hoseana Lunogelo anaeleza kuwa mfumo bora wa utawala nchini umewezesha Tanzania kuwa na Uchumi Jumuishi kutokana na wananchi kuanzia ngazi ya kijiji kushirikishwa katika kupanga mipango ya maendeleo jambo ambalo linawafanya waangalie vipaumbele muhimu katika maeneo yao.

Dkt. Lunogelo anataja mradi ya TASAF, kuongezeka kwa mikopo kwa wanafunzi wa  elimu ya juu, kuanzishwa kwa vikundi vya kuweka na kukopa (SACCOS) na kurahisishwa kwa huduma za kifedha ni miongoni mwa mambo yanaifanya Tanzania kuibuka kinara katika uchumi jumuishi.

Aidha, Dkt. Lunogelo anaeleza kuwa kutokana na kuendelea kuboreshwa kwa mifumo na juhudi za makusudi za Serikali za kuwasaidia Watanzania wengi zaidi kushiriki shughuli za kiuchumi kutaifanya Tanzania kung’ara zaidi katika suala la uchumi jumuishi ambao unafaidisha wananchi wengi.

“Uchumi jumuishi ndio msingi mkubwa wa kuleta amani na utulivu katika nchi kwani watu wanaguswa na matunda ya ukuaji wa uchumi”, alieleza Mtaalamu huyo wa Uchumi.

Dkt. Lunogelo anasisitiza kuendelea kufanya kuwashirikisha na kuwatafutia wananchi fursa zaidi za kiuchumi ili dhana hii ya Uchumi Jumuishi iwaguse Watanzania wengi zaidi.
Viewing all 104809 articles
Browse latest View live




Latest Images