Quantcast
Channel: UDAKU SPECIAL
Viewing all 104789 articles
Browse latest View live

Mjumbe Ukawa Atinga Bungeni, Posho Ya Laki Tatu Kwa Siku si Mchezo

$
0
0
Dodoma. Wakati wajumbe wa Bunge la Katiba wanaounda Umoja wa Katiba ya Wananchi (Ukawa) wakiendelea na msimamo wa kususia vikao vinavyotarajiwa kuanza leo mjini Dodoma, mmoja wa wajumbe wake jana aliripoti bungeni na kujiandikisha.

Mjumbe huyo, Clara Mwatuka ambaye pia ni Mbunge wa Viti Maalumu (CUF), alionekana katika Viwanja vya Bunge saa 6:30 mchana akiwa ameongozana na wabunge kadhaa wa CCM wakiwamo Livingstone Lusinde (Mtera) na Jerome Bwanausi (Lulindi).

CUF ni moja ya vyama vinavyounda Ukawa, pamoja na Chadema na NCCR Mageuzi na tayari viongozi wakuu wa vyama hivyo, Profesa Ibrahim Lipumba, Freeman Mbowe na James Mbatia wametangaza kwamba wajumbe wote wanaotokana na umoja wao hawatashiriki vikao vya Bunge hilo.

Mwatuka baada ya kujaza fomu maalumu za kujiandikisha, alielekea lango la Magharibi na kuingia kwenye gari la Bwanausi.

Awali, alipoulizwa kwenye Viwanja vya Bunge kuhusu kuwapo kwake Dodoma, alikataa kuzungumza lakini alikiri kujiandikisha bungeni

Shilole ni Mkulima wa Mpunga Anayeutaka Ubunge wa Igunga

$
0
0
Inawezekana kabisa Shilole akawa msanii ambaye ungedhani angewekeza zaidi kwenye duka la urembo, nguo ama hata madini kwa jicho la kawaida kama akitaka kufanya biashara mbali na muziki. Lakini kwa jicho la tatu usimchukulie hivyo.

Msanii huyo ambaye ni mzaliwa wa Igunga  panapofahamika zaidi kama kwa Rostam Aziz, mbunge aliyekaa muda mrefu madarakani kabla ya nafasi yake kuchukuliwa na Dr. Kafumu ambaye ni mbunge wa sasa, amepanga kuingia kwenye mchakato wa ubunge kwa lengo la kulitwaa jimbo hilo.

Shilole aliiambia Bongo Dot Home kuwa amefanya uamuzi wa kugombea katika jimbo hilo kwa kuwa anaona kuna baadhi ya mambo hayaendi sawa na yeye kama mzawa anaamini anaweza kuwasaidia zaidi wananchi wa Igunga.

“Ni kwa sababu ya matatizo yaliyopo. Nimekuwa nikienda naona matatizo kila siku yapo..ndio maana naona kama naweza kusimama na watu wengi sana wakanisikiliza kwa nini nisijitokeze kuwasaidia matatizo yao. Nimezaliwa pale mimi, nakijua kitongoji kimoja baadaya kingine.” Ameeleza.

“Nikipata ubunge kwanza kabisa nitadeal na akina mama, wafanyabiashara ndogondogo waweze kujikwamua vizuri. Pili vijana waweze kupata ajira kwa sababu sasa hivi naona vijana wa Igunga ajira zimekuwa ngumu kupatikana. Kuweka vitendea kazi ambavyo vitakuwa rahisi sana kuweza kufanya kazi na kutoa vijijini kupeleka mjini.” Alijinadi Shilole.

Akiwa kwenye kipindi cha The Jump Off cha 100.5 Times Fm, mwimbaji huyo alieleza kuwa mbali na muziki yeye ni mkulima wa mpunga na ana mashamba mengi ya mpunga huko Igunga

Diamond Vs Ali Kiba : Nay wa Mitego Atamani Kutembeza Kipigo Kikali Kukomesha

$
0
0
Ushindani kati ya Diamond na Ali Kiba ambao siku zote mimi nauita ‘ushindani usio rasmi’ huku wengine wakiutafsiri kama ‘beef’ umetengeneza mitazamo tofauti kati ya wadau wa muziki Tanzania.

Hivi karibuni, G-Lover alitoa mtazamo wake kuhusu tofauti iliyopo kati yao huku akimpa credit kila mmoja.

Akiongea na Fadhili Haule  katika Sunrise ya 100.5 Times Fm, Nay wa Mitego yeye ameeleza jinsi asivyopenda kabisa malumbano yanayoendelea kudai kuwa angekuwa na uwezo angetembeza kipigo heavy.

“Ningekuwa na uwezo wa kuwapiga wote ambao yaani wanaendelea huu mchezo uliopo, nafikiri ningewapiga na ningewafunga ningekuwa na amri hiyo.” Nay wa Mitego ameiambia Sunrise.

“Coz unajua kuna watu wanatengeneza hivi vitu, wanataka kuwatia watu stress. Wanataka watu ifike time waje wauane. Kuna beef tunaona zinakuwaga beef tu za kawaida. Lakini huu mchezo wa Ali Kiba na Diamond ni Mchezo ambao naona kama watu wanaoufanya uwe serious sana. Mimi sipendi nachukia.” Ameongeza rapper huyo wa ‘Itafahamika’.

Amewashauri Ali Kiba na Diamond kuachana kabisa na kinachoendelezwa kati yao na kuendelea na muziki kwa kuwa itafikia hatua mbaya ambayo wataumizana na kushindwa kufanya muziki

Mlemavu Atumia Mguu Wake wa Bandia Kuuzia Madawa ya Kulevya Mitaani

$
0
0
Kamishna Suleiman Kova akionesha namna mguu huo wa mtu mwenye ulemavu unavyotumika kutunzia dawa za kulevya.
KIJANA mmoja ambaye ni mlemavu wa mguu, Said Tindwa (36), mkazi wa Vijibweni Kigamboni jijini Dar, anashikiliwa na Jeshi la Polisi Kanda Maalum ya Dar es Salaam kwa kutumia mguu wake wa bandia kwa ajili ya kutunzia na kuuza dawa za kulevya.

Akizungumza na waandishi wa habari, Kamishna wa Jeshi la Polisi Kanda Maalum, Suleiman Kova alisema mlemavu huyo alitiwa nguvuni Agosti 1 mwaka huu kufuatia mtego uliowekwa na jeshi hilo. 
Alisema uchunguzi wa awali unaonesha kuwa mtuhumiwa huyo amekuwa akitumia mbinu ya kuziuza dawa hizo kwa kuzificha kwenye mguu wake wa bandia. 
Aidha Kova alisema kuwa dawa alizokuwa akiziuza mlemavu huyo ni zile za viwandani kama vile cocaine, heroin na wakati mwingine bangi. 
“Katika mtego maalum uliowekwa na askari wa upelelezi ndipo mlemavu huyo alikamatwa akiuza dawa hizo kwa wateja wake baada ya kuzitoa alikozificha ambapo ni ndani ya mguu huo wa bandia” alisema Kova.

Kujichora Tattoo Kitu Gani Bwana Penzi la Shilole na Nuhu Mziwanda Kwishey..Kisa Hichi Hapa

$
0
0
Stori ya Nuh Mziwanda kujichora tatoo yenye jina la Shilole ilisambaa sana na wengi walikua wakijiuliza siku ikitokea wameachana itakuaje hasa upande wa Nuh ambaye ndiye aliyejichora tatoo hiyo.

Maelezo ya Nuh Mziwanda yamedai kuwa sababu zilizosababisha waachane ni msg ambayo aliikuta kwenye simu ya Shilole ambayo inasemekana ilitumwa na mwanaume,Nuh alipomwambia Shilole apige alionekana kunikanyanga.

Nuh Mziwanda kaongea na Soudy Brown kwenye You heard na kazungumza mambo mengi ambayo yametokea kwenye uhusiano wao.

Msikilize Hapa:

Picha Kali Ya Mchumba wa Ney wa Mitego..Siwema

$
0
0
 Siwema Mchumba wa Ney wa Mitego Katika Pozi....Shemejiiiiiiiiiiiiiiiiiiii

Msichana Aliyepigwa na Mtoto wa Obama Atoa Kauli ya Kushangaza

$
0
0
Mtoto wa rais wa kike wa Marekani, Malia Obama mwenye umri wa miaka 16 alimpiga/alimgonga kwa bahati mbaya msichana aliyefahamika kwa jina la Bridget Truskey walipokuwa katika tamasha kubwa la muziki la Lollapalooza nchini Marekani.  

Msichana huyo amewashangaza watu baada ya kuonesha kufurahishwa sana na tukio hilo  kutokana na umaarufu wa Malia Obama.

Truskey ametweet sentensi kadhaa kuonesha furaha yake huku maelezo yakionesha kuwa haamini kilichotokea.

“I got (accidentally) kicked by Malia Obama today at Lollapalooza. No lie. Malia. Obama. It was awesome. #lollapalooza.”

Ni kweli msichana huyo ana sababu ya kufurahi kwa kuwa amekuwa maarufu pia kupitia tukio hilo.
- See more at: http://langolajiji.blogspot.com/2014/08/msichana-aliyepigwa-na-mtoto-wa-obama.html#sthash.vQMNqcZo.dpuf

Mume Wangu Kampa MIMBA Mbwa Wetu......Nilimfumania Mimi Mwenyewe kwa Macho Yangu Akingonoka na Naye

$
0
0
Mwanamke mmoja aliyejitambulisha kwa jina la Cecilia Hamis (pichani), mkazi wa Majoe Mjimpya Relini jijini Dar es Salaam amemlalamikia mumewe aliyemtaja kwa jina la Hamis Juma kwamba ametembea na mbwa wao mweusi hadi kumpa mimba.

Akizungumza na Uwazi mwishoni mwa wiki iliyopita nyumbani kwake, mwanamke huyo alisema alibaini hilo wiki mbili zilizopita.

“Nililigundua hilo wiki mbili zilizopita. Nakumbuka ilikuwa usiku nikiwa nimelala, nikamsikia mbwa mmoja (kati ya wawili) analia. Niliamka kwenda kuangalia ili kujua sababu, kufika nikawasha tochi ya simu, nilishangaa sana kumwona mume wangu yuko naye anafanya  mapenzi.

“Nilimuuliza anachokifanya, akasema anammalizia shida zake kwa kuwa hakuna mbwa wa kiume wa kumsaidia,” alisema mwanamke huyo.

Akiendelea kumlalamikia mume wake kwa madai hayo mazito, mama huyo alisema:

“Siku iliyofuata usiku tena, nikiwa nimelala nilimsikia mbwa akilia, nikaamka. Safari hii niliambatana na watoto wangu, tukaenda nje, kufika tukamshuhudia mume wangu akifanya tukio kama la jana yake, nilipomuuliza akanipa majibu yaleyale kwamba anammaliza shida zake mbwa huyo.”
Akaendelea: “Hawa mbwa waliletwa wawili wakiwa wadogo kabisa na wote ni majike na tangu walipoletwa sijawahi kumwona mbwa dume hata siku moja kwani mara nyingi tunawafungia kwenye banda lao.

“Na tangu mume wangu aanze mchezo huo huyo mbwa mmoja mweusi (pichani) amenawiri kupita kiasi, naamini amempa mimba.”

Mwanamke huyo alisema kutokana na kukithiri kwa tabia hiyo, aliamua kuwaeleza majirani ambao nao walimshauri aende kuripoti kwa mjumbe wa eneo hilo.

Akizungumza na Uwazi, Mjumbe wa Shina Na. 26, Majoe Mjimpya, Mbaruka Nyamaishwa alikiri kupokea malalamiko hayo kutoka kwa mwanamke huyo akamshauri kuyapeleka kwenye Kituo cha Polisi cha Stakishari.

Habari zaidi zinawekwa wazi kwamba, majirani nao walipoona mwanamke huyo anachelewa kwenda polisi, wao walimsomba na kwenda naye ambapo walitoa taarifa katika Dawati la Jinsia.

Mkuu wa dawati hilo, Koplo Golbert aliongozana na walalamikaji hao hadi nyumbani kwa mdaiwa ambapo alimkagua mbwa huyo na kuwaamuru wanandoa hao kuripoti kwenye kituo hicho cha polisi bila kukosa jana Jumatatu saa 3 kuonana na mkuu huyo na uchunguzi kuendelea.

Uwazi lilimuuliza swali moja mwanamke huyo, ni kwa nini anasema aliamka na kutoka nje usiku bila kueleza mumewe anakuwa wapi muda huo kwani hakuonyesha kushangaa kutomwona kitandani?

Anajibu: “Tulitengana vyumba kwa sababu ya ugomvi wa kifamilia.”

Uwazi lilimgeukia mume wa mwanamke huyo na kumuuliza kuhusu madai mazito ya mkewe ambapo alisema:

“Mimi sijawahi kufanya kitendo hicho na mbwa ila nahisi mke wangu na hawa majirani wa hapa wananitengenezea hilo tukio ili nikafungwe jela maisha, halafu wao waweze kuchukuwa mashamba yangu kwani ndani ya ndoa yangu kumekuwa na ugomvi wa mara kwa mara.”

Uwazi lilitilia shaka uwezekano wa mbwa kunasa mimba ya binadamu, hivyo lilimsaka daktari mmoja wa Hospitali ya Taifa Muhimbili (MNH) na kumuuliza kuhusu madai ya mwanamke huyo.

Msikie: “Mh! Binadamu kumpa mimba mbwa haiwezekani. Binadamu anaweza kumpa mimba sokwe, kwa mbali sana nyani. Lakini si mbwa.

“Ila kama huyo mama anasema hivyo, mbwa akapimwe na ikibainika ni kweli basi yatakuwa maajabu ya dunia maana dunia ina mambo yake.”




Nitakuwa Rais wa Mwisho Kuongoza TZ Masikini - Jakaya Kikwete

$
0
0
Rais Kikwete amesema kuwa anataka na anatamani kuwa Rais wa mwisho wa Tanzania kuongoza nchi ambayo ni maskini na hivyo atatumia muda wake uliobakia katika uongozi kuelekeza nchi kwenye mwelekeo huo.

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mheshimiwa Jakaya Mrisho Kikwete amesema kuwa anataka na anatamani kuwa Rais wa mwisho wa Tanzania kuongoza nchi ambayo ni maskini na hivyo atatumia muda wake uliobakia katika uongozi kuelekeza nchi kwenye mwelekeo huo.
Aidha, Rais Kikwete amesema kuwa jambo la msingi kabisa la kama Watanzania watanufaika na ugunduzi wa gesi asili ama watabakia katika hali yao ya sasa ya umasikini ni aina ya uongozi ambao nchi hiyo itaupata, uongozi wenye uwezo wa kufanya maamuzi sahihi kwa kadri nchi inavyozidi kusonga mbele.
Rais Kikwete pia anasema kuwa Tanzania inatarajia kuanza kupokea mapato yake ya kwanza kutokana na raslimali ya gesi asilia katika miaka sita ijayo, kuanzia Mwaka 2020.
Rais Kikwete ameyasema hayo jana, Jumatatu, Agosti 4, 2014, wakati alipozungumza kwenye Kituo cha Kimataifa cha Maendeleo (Centre for Global Development) mjini Washington,D.C., Marekani, ambako alizungumzia Hali ya Baadaye ya Tanzania kufuatia Ugunduzi wa Gesi – Future of Tanzania following the Discoveries of Gas.
Rais Kikwete yuko nchini Marekani kwa ziara rasmi ya siku tisa ambako miongoni mwa mambo mengine atahudhuria Mkutano wa Kwanza wa Viongozi wa Marekani na Afrika ulioitishwa na Rais Barack Obama wa Marekani na unaoanza leo, Jumanne, Agosti 5, 2014.
Rais Kikwete ameuambia mkutano kwenye Kituo hicho kuwa anataka kufanya kila linalowezekana katika kipindi chake kilichobakia cha uongozi kuhakikisha kuwa anaanzisha na kuanza kujenga taasisi na kuweka kanuni sahihi za kuweza kusimamia raslimali ya gesi asilia .
“Nitafanya kila linalowezekana kuhakikisha kuwa Watanzania na nchi yao wananufaika kutokana na mapato ya raslimali kutokana na gesi asilia. Nataka na natamani kuwa Rais wa mwisho wa Tanzania kuongoza nchi masikini. Raslimali ya gesi inatoa nafasi na fursa kubwa kwa nchi yetu kuondokana na umasikini. Mimi nimeongoza nchi masikini, lakini nataka mrithi wangu kuongoza nchi yenye ustawi na utajiri,” amesema Rais Kikwete na kuongeza:
“Hivyo, dhamira na shughuli yangu kubwa kati ya sasa na mwisho wa kipindi changu cha uongozi ni kuiongoza nchi yetu kuelekea kwenye njia hiyo ambako gesi italeta ustawi na utajiri na maisha bora zaidi kwa wananchi wetu.”
Hata hivyo, Rais Kikwete amesema kuwa ili Watanzania wanufaike na mapato ya gesi ni muhimu kuwepo na uongozi imara ambao utakuwa tayari kuchukua maamuzi sahihi kwa kadri nchi inavyosonga mbele. “Jambo la kutia moyo ni kwamba Tanzania ni demokrasia, na ushiriki wa umma kutaja kujua nini kinaendelea uko juu sana.”
Tanzania imekuwa inatafuta gesi na mafuta tokea miaka ya 1950 na ugunduzi wa kwanza ulikuwa Mwaka 1974 katika Kisiwa cha Songo Songo kilichoko Mkoa wa Lindi na Mnazi Bay katika Mkoa wa Mtwara mwaka 1982.
Hata hivyo, ilikuwa kuanzia Mwaka 2010 wakati ugunduzi mkubwa wa gesi ulipofanyika kwenye eneo la bahari, ugunduzi ambao mpaka sasa umefikia futi za ujazo trilioni 50.5.

Huyu Ndie Mjumbe Mdogo Kabisa Katika Bunge la Katiba Analipwa Laki Tatu Kwa Siku

$
0
0


Habari nzuri kuona kwamba katika bunge la katiba kuna mjumbe kijana kabisa ambaye ameteuliwa kwenda kuwakilisha vijana;Teddy Ladislaus Patrick (21), ndiye Mjumbe mdogo kulioko wote katika bunge maalum la katiba.

Utafiti Umebaini Polisi Inaongoza Kwa Rushwa Bongo..True or Not?

$
0
0
Utafiti uliofanywa na Shirika lisilo la kiserikali la Twaweza la nchini Tanzania unaonyesha kuwa Jeshi la Polisi nchini linaongoza kwa rushwa kwa asilimia 94 huku likifuatiwa na sekta za Siasa, Afya, Kodi na Elimu.

Akizindua utafiti huo leo jijini Dar es Salaam, Mtafiti wa Twaweza Elvis Mushi amesema wananchi wanamsukumo zaidi wa kutoa rushwa hata wasipoombwa wakati wanatafuta huduma muhimu zikiwemo Maji, Elimu na Afya huku ikionekana kutoa rushwa ni jambo la kawaida kutoa na kuombwa mara kwa mara.
Kwa upande wao, Mkurugenzi wa Kituo cha Sheria na Haki za Binadamu LHRC, Dkt. Helen Kijo-Bisimba amesema asilimia kubwa ya wananchi wanaamini rushwa haiwezi kumalizika kutokana na kutokuwa na mipango thabiti ya kuitokomeza.
Wakati huo huo, mtandao wa Wanafunzi nchini Tanzania (TSNP) umesema wanaokwamisha uundwaji wa Katiba mpya wanarudisha maendeleo ya nchi na kwamba mchakato huo haupo kwa ajili ya kuonesha misimamo ya kisiasa bali namna gani taifa litaongozwa na Katiba iliyotokana na mawazo yao.
Hayo yamesemwa leo jijini Dar es Salaam na Mkurugenzi wa Mtandao huo, Bw. Alphonce Lusako ambapo ameeleza kuwa endapo mchakato wa kupata katiba mpya utakwama itakuwa ni dhambi ya kihistoria ambayo haitaweza kufutika machoni pa watanzania.
Aidha, Lusako ameongeza kuwa kutofautiana ni demokrasia lakini demokrasia safi ni ile inayojenga muafaka, maridhiano na makubaliano na sio kubomoa na kuwataka wajumbe wa Bunge Maalum la Katiba watambue sheria kuu ndani ya bunge hilo ni kuboresha Katiba ya wananchi.

Chifu Kiumbe Ajibu Madai ya Kuuza 'Unga', Asema Sasa Ameamua Kumrudia Mungu

$
0
0
Mfanyabiashara maarufu ambaye amekuwa akitoa misaada mikubwa kwa wanamuziki na watu mbalimbali, Chifu Kiumbe amejibu tetesi zilizokuwa zikielezwa na baadhi ya watu kuwa anajihusisha na biashara ya dawa za kulevya.

Chifu Kiumbe amekanusha tetesi hizo katika kipindi cha ‘Mkasi’ na kueleza kuwa yeye hajawahi hata kuyaona madawa ya kulevya.

“Sijawahi kuuza madawa ya kulevya, wala sijawahi kuona unga unafanaje katika maisha yangu. Kwanza katika maisha yangu pombe sijawahi kugusa, sigara sijawahi kugusa wala kinywaji cha aina yoyote.” Amesema Chifu Kiumbe.

Amesema watu wengi katika jamii wana kasumba ya kumsema mtu kuwa anauza unga kwa sababu tu ana pesa nyingi kitu ambacho sio sahihi.

Katika hatua nyingine, Chifu Kiumbe ameeleza kuwa hivi sasa ameamua kumrudia Mungu baada ya kufanya mambo mengi na kwamba anataka kujikita katika kujenga misikiti.

“Nimeamua kurudi kwa mwenyezi Mungu. Nimefanya mengi katika hii dunia na hakuna ambacho sikijui katika hii dunia. Maisha ya kuishi duniani ni machache. Maisha mengi ni kwa mwenyezi Mungu kwa hiyo sasa nimeelekea kwa mwenyezi Mungu na hapa nilipo kiu yangu ni kufikiria jinsi gani ya kujenga misikiti.”

Akizungumzia kitu ambacho anakijutia katika maisha yake, amesema hana anachojutia zaidi ya kuwa na jina kubwa halafu anajikuta akiandikwa vibaya kwenye mitandao ya kijamii kwa habari zisizo za kweli.

Diamond Anunua Ekari 44 za Viwanja Maeneo ya Mapinga...Dogo Hela Anazo

$
0
0
Juzi nlikuwa nimeenda Mapinga Jirani na Bunju, Mpakani mwa Dar es Salaam na Bagamoyo kutizama viwanja japo nitafute pakuweka mgongo ila kuna sehemu nimeonyeshwa kiwanja kina ekari zinakaribia 44 naambiwa na madalali kuwa ni mali ya Yule msani wa wasafi. Tuacheni utani yule msanii ana hela tuweke chuki kando...Hongera Chibu

Mnaoishi Nje ya nchi Acheni Kupoteza Muda Kwenye Blogs na Kulaumu Wengine Kuhusu Uraia Pacha..Leteni Hoja

$
0
0
RAIS Jakaya Kikwete, amewataka Watanzania waishio nje ya nchi na wanaotaka kuona Tanzania inakubali kuanzisha mfumo wa uraia pacha, kutumia muda wao kujenga hoja za jambo hilo badala ya kupoteza muda kwenye mijadala ya ‘blogu’ na kulaumu watu wengine.

Pia, aliwataka watanzania hao kusema ili wasikike, kwa sababu kimsingi hoja ya uraia pacha haina nguvu miongoni mwa Watanzania wanaoishi Tanzania, bali inatokana zaidi na msukumo wa Watanzania wanaoishi nje, ambao kwa bahati mbaya hawafanyi jitihada za kutosha kutetea hoja yao.

Aliwaambia watanzania hao, kuacha kupoteza muda kujadili mambo yasiyokuwa na maana, badala yake kuelekeza nguvu zao katika kujenga hoja yenye nguvu zaidi ya uraia pacha, jambo ambalo ni moja ya mambo yatakayojadiliwa katika mchakato wa Katiba mpya.

“Ushauri wangu ni kwamba tumieni muda wetu kusaidia kusukuma hoja yenu hii muhimu ambayo kama mnavyojua imeingizwa katika rasimu kwa mapendekezo ya CCM kwa sababu suala hilo halikuwemo katika rasimu ya kwanza,” alisema.

Rais Kikwete, ameyasema hayo Agosti 2 mwaka huu, wakati alipokutana na Watanzania wanaoishi Marekani,  hasa katika maeneo ya Jiji la Washington D.C na majimbo ya Virginia, Maryland, New York na hata California katika mkutano uliyofanyika hoteli ya Marriot Washington mjini Washington D.C.

Rais yuko katika ziara ya siku tisa nchini Marekani, ambako miongoni mwa mambo mengine atahudhuria mkutano wa kwanza wa Marekani na Afrika ambao shughuli zake zimeanza jana.

Tundu Lissu: Sitaki Kuulizwa Tena Kuhusu Kumtukana Mwalimu Nyerere

$
0
0
Tundu Lissu ameyasema hayo katika maojiano na kituo kimoja cha radio jijini Dar - es - salaam. 

Alipo ulizwa swali kama yeye anadai makada wa CCM wanaitukana tume ya Warioba je na yeye anaweza kulitolea ufafanuzi suala la kumtusi Baba wa Taifa? Anasema "sitaki kuulizwa hili swali kuanzia leo nitatolea ufafanuzi kwa mara ya mwisho mimi sijawahi kumtukana mwalimu nilisema ukweli na wala CHADEMA haikuwahi kuomba radhi kama walivyosema watu. 

Sijawahi kukutana na Mama Maria Nyerere japo ningependa kumpa hata shikamoo" 

Pia alisema taarifa kuwa UKAWA yapasuka ni uongo mtupu na kuyatuumu magazeti ya Habari Leo Uhuru na Mzalendo kuandika propoganda.

Ameongeza na kusema Mbuge yeyote atakayerudi bungeni kukipata, na "hatarudi bungeni".

Mwisho alisema kuna mbunge mmoja wa mahakama ana elements za UKAWA maana anasema mpaka UKAWA warudi nami ndo nitarudi.

Ney wa Mitego: Nilishawahi Kushuhudia Mabinti wa Bongo Movies Wakijiuza kwa Wegeni Wanaotoka Nje ya Nchi

$
0
0
Stori: Shani Ramadhan

MKALI wa Bongo Fleva, Emanuel Elibariki maarufu kama Nay wa Mitego, amesema kuwa aliwahi kushuhudia staa mmoja wa filamu Bongo (jina tunalo) akijiuza kwa mgeni mmoja kutoka nje ya nchi na kwamba tukio kama hilo aliliona zaidi ya mara moja.

Akizungumza na gazeti hili mapema juzi, Nay mkali wa nyimbo za Nakula ujana na Muziki Gani, alisema mabinti wengi wanacheza filamu siyo kwa ajili ya kujikwamua kimaisha, bali wanafanya hivyo ili kuuza sura ambayo baadaye huitumia kwa ajili ya kujiuza ili kujiingizia kipato.

“Mimi kila kitu ambacho huwa ninakiimba huwa kina ukweli ndani yake na niko tayari kwa mtu ambaye atahisi nimemuonea tutafikishana popote pale, nilishawahi kushuhudia mabinti wa bongo movie wakinunuliwa na wageni wanaokuja kutoka nje ya nchi,” alisema Nay.

Rose Mhando Afunguka Asema Anamtamani Sana Mchungaji Gwajima

$
0
0
Stori: Shani Ramadhan na Gabriel Ngosha

NYOTA wa nyimbo za Injili nchini, Rose Muhando amesema anatamani sana kuhamia kanisa la Ufufuo na Uzima linaloongozwa na Mchungaji Josephat Gwajima kutokana na mahubiri yake mazuri.
“Natamani nihamie katika kanisa la Mchungaji Gwajima lakini mimi huwa napenda kumuita Askofu kwa sababu ya upako alionao, naomba ikiwezekana na mimi nihamie hapa,” alisema Rose.
Katika siku ambayo kulikuwa na sala ya shukurani kanisani kwa Gwajima Jumapili iliyopita Kawe jijini Dar es Salaam,  mchungaji huyo alimwambia Rose aliyealikwa kuimba, kwamba yupo tayari kumjengea kanisa Dodoma anakoishi na yeye mwenyewe alisimamie.

Kitu kingine kilichomtokea Masogange ndani ya uwanja wa ndege

$
0
0
Video model Agnes Masogange mwaka jana alitawala vyombo vya habari baada ya kukamatwa na polisi huko South Africa akiwa na mwenzake Melisa Edward wakiwa na mzigo wa Crystal Methamphetamine wenye thamani ya Tsh bilioni 6.8.
Taarifa mpya kutoka kwa kamanda wa polisi kitengo cha kuzuia na kupambana na dawa za kulevya Gedfrey Nzowa inasema kikosi hicho kilimshikilia Masogange usiku wa juzi baada ya kurejea akitokea South Africa. Taarifa inasema kwamba Masogange alihojiwa kwa zaidi ya masaa 10 na kupekuliwa na baadae kuachiwa hutu bila masharti.
Masogange alivyotafutwa kwenye simu alijibu kwa kifupi na kusema,”Hilo unalosema siyo kweli na sipo tayari kuzungumzia. Siwezi kuzungumza na chombo cha habari kwa sasa, shida yako nini”.
Source : Mwananchi

Haya ni Maswali Mengine Yaliyoulizwa Kwenye Mazungumzo ya Rais Kikwete na Watanzania Waishio Marekani.

$
0
0
Rais wa Jamhuri ya Muungano Jakaya Kikwete Usiku wa Agosti 2 2014,alikutana na waTanzania katika hoteli ya Marriot iliyopo jijini Washington DC Baada ya hotuba yake,Rais Kikwete aliruhusu maswali kutoka kwa Watanzania hao.
Miongoni mwa maswali hayo ni yale yaliyotaka uthibitisho wa Rais juu ya taarifa aliyowahi kuitoa Katibu Mkuu wa Chadema Dr.Wilbroad Slaa kuhusu madai ya Ridhiwan Kikwete kukamatwa na madawa ya klulevya China.
Rais ametoa ufafanuzi kuhusu tuhuma hizo,yapo maswali mengi mengine ambayo Rais ameulizwa,Ripota wa Nguvu wa millardayo.com aliyepo nchini Marekani Mubelwa Bandio karekodi kila kitu na hiki ndicho kilichotokea.
Hizi ni dakika 30 za maswali hayo na majibu,
Bonyeza play kusikiliza

Kenyan Rapper Says Ray C And The Late Ngwair Sunk Him Deeper Into Drug Addiction

$
0
0
Kenyan hip hop rapper G rongi has revealed that Tanzanian artists such as Ray C and Mangwair got him to sink in deeper into drug addiction that almost killed his rap career.

G rongi who is now based in Paris , France says he lost everything he had and ended up roaming the streets as a homeless person in Mathare. It was then that his family traced him and took him to rehab.

The rapper who was speaking to Mzazi Willy M Tuva's Girongi revealed that he was in the same drug rings with the late Mangwair just one year before the Tanzanian rapper died. "I did drugs with big Tanzanian artists the likes of Ray C and rapper Mangwair who were all heavy consumers of hard drugs" adding that he was really affected when he learnt of his death.

G rongi now makes two the number of artists who have emerged from the dark past of drug addiction from the same drug ring. Ray C who was in the same crew recently left the rehab and has since started a foundation dealing with drug abuse.

The Fyatua rapper will be launching his new video "Mukurino" which is a kikuyu term that loosely translates to "who is the savior". According to G rongi the song is meant to provoke thoughts of people stuck in various predicaments, that they are their own saviors.

The Dandora bred rapper also revealed that he would jet back into the country in February 2015 to launch his album which he is going back to finalise in Paris
Viewing all 104789 articles
Browse latest View live




Latest Images

<script src="https://jsc.adskeeper.com/r/s/rssing.com.1596347.js" async> </script>
<script src="https://jsc.adskeeper.com/r/s/rssing.com.1596344.js" async> </script>