Quantcast
Channel: UDAKU SPECIAL
Viewing all 104799 articles
Browse latest View live

Punguza Unene Unaokusumbua Katika Mwili Kwa Kutumia Bidhaa za Edmark

$
0
0
Tumia Dawa za Edmark za Kupunguza uzito uliozidi Mwilini Mwako, Edmark ni Vurutubisho na Chakula Mbadala na Zimehakikiwa na TFDA...

Ni uhakika kwa afya yako,👉 kupunguza uzito na sumu mwilini, Mafuta Sehemu Mbaya, Kitambi na nyama uzembe na kutibu MAGONJWA Mbalimbali kwa msaada wako mfuate instagram: @afyayanguutajiriwangu @afyayanguutajiriwangu


Au Mtafute WhatsApp Huyu Dada kwa kutumia Namba +255783 566844

Pia Dawa za Edmark Zinaweza kupa Fursa ya Biashara Uweze pata Kipato Kirahisi kwa Kuwasaidia watu Kuimarisha Afya zao


Kilichomfanya Mbunge Akapiga Magoti Bungeni

$
0
0
Mbunge wa Ileje (CCM) Janeth Mbene amepiga magoti bungeni na kumshukuru Rais John Magufuli kwa kupeleka maendeleo kwenye wilaya yake anayodai ilisahaulika.

Mbene amefanya kitendo hicho jana bungeni Aprili 13, wakati akichangia bajeti ya ofisi ya Rais kwa mwaka wa fedha 2018/19.

Mara baada ya kuruhusiwa kuchangia bajeti hiyo, Mbene alisema wilaya ya Ileje ni ya miaka mingi lakini ilikuwa haina barabara ya lami lakini katika Serikali Awamu ya Tano, barabara imejengwa.

Katika kuonyesha kuwa jambo hilo limemfurahisha, mbunge huyo alipiga magoti, pembeni ya kiti anachoketi bungeni akimshukuru Rais Magufuli.

Uganda Kuwatoza Kodi Watumiaji wa Mtandao wa Kijamii

$
0
0
Uganda Kuwatoza Kodi Watumiaji wa Mtandao wa Kijamii
Serikali ya Uganda imeeleza mpango wake wa kutambulisha utaratibu wa kutoza kodi watumiaji wa mitandao ya kijamii kuanzia mwezi July ikiwa ni njia ya kuongeza mapato ya nchini.

Taarifa hii imetolewa na Waziri wa Fedha wa nchi hiyo Matia Kasaija hata hivyo suala hilo limepingwa na mwanaharakati wa haki za binadamu Rosebell Kagumire.

Mwanaharakati huyo ameeleza kuwa utaratibu huo unapelekea kupunguza uhuru wa kujieleza wa watu wa nchi hiyo.

Video ya Utupu ya Bilnass na Nandy Yaizima Kwangaru ya Daimond

$
0
0
Video ya Utupu ya Bilnass na Nandy Yaizima Kwangaru ya Daimond
Kwa wafuatiliaji wa mitandao ya kijamii nchini Tanzania, hususani kwa wale ambao wanamfuatilia Diamond Platnumz utagundua kuwa jana Aprili 12, 2018 aliahidi kuachia video ya wimbo wa ‘Kwa ngwaru’ ambayo amemshirikishwa na Harmonize lakini mpaka sasa hivi hakuna chochote kile walichofanya.

Mapadri Watatu wa Kanisa Katoliki Wafariki Ghafla

$
0
0
Mapadri Watatu wa Kanisa Katoliki Wafariki Ghafla
Mapadri watatu wa Kanisa Katoliki Jimbo la Same, wamefariki dunia ndani ya saa 72. Kanisa limesema vifo vya aina hiyo havijawahi kutokea.

Waliofariki wametajwa kuwa ni Padre Ubaldus Kidavuri, Padre Arbogast Mndeme na Michael Kiraghenja, wote wa jimbo hilo. Wawili kati ya hao walifariki ghafla usingizini.

Kwa mujibu wa taarifa kutoka ndani ya kanisa hilo, padre mmoja ndiye aliyekuwa akiumwa na alifariki akiwa katika Hospitali ya KCMC.

Taarifa ya vifo vyao ilitolewa jana na Askofu wa Jimbo la Same, Mhashamu Rogath Kimario.

Kwa mujibu wa taarifa hiyo, mapadri hao wanatarajiwa kuzikwa Aprili 17, katika Makaburi ya Mapadri Jimbo la Same.

Taarifa ilisema haijawahi kutokea vifo vitatu vilivyopishana kwa saa 24 katika jimbo moja.

“Jana nilionana na Padri Kidavuri na alikuwa akijiandaa kwa safari ya kwenda kuzika wenzie na nikampa pole pale St. Joseph, alikuwa mzima wa afya. Wapumzike kwa amani, amina,” alisema Padre Kimario.

Akithibitisha vifo hivyo jana, Katibu Mkuu wa Baraza la Maaskofu Katoliki Tanzania (TEC), Padre Raymond Saba, alisema kanisa limepokea kwa mshtuko mkubwa kufuatia vifo hivyo vya ghafla.

“Vifo vimetushtua sana maana vimekuwa vya ghafla mno, tulikuwa nao na walikuwa wazima kabisa,” alisema Padre Saba.

Alisema wanatarajia mazishi yatafanyika Jumanne ijayo, Same.

DC Kasesela Awataka Bongo Movie Kuwekeza Kama Diamond

$
0
0
DC Kasesela Awataka Bongo Movie Kuwekeza Kama Diamond


Wasanii wa filamu nchini Tanzania, wakiongozwa na Jacob Stephan JB, Steve Nyerere, Jack Wolper, Aunt Ezekiel na wengine wengi wamewasili jana jioni Mkoani Iringa kwaajili ya tamasha la Amka Kijana litakalofanyika Jumamosi ya leo (April 14, 2018) katika Viwanja vya Mwembe Togwa.

Tamasha hilo lina lengo la kuwaelimisha vijana kuacha kukaa vijiweni na kuanza kuchangampia fursa mbalimbali ikiwemo kujiajiri kupitia vipaji vyao vya sanaa.

Akiongea na wasanii hao muda mchache baada ya kuwasili, DC wa Iringa Richard Kasesela amesema inasikitisha kuona tasnia ya filamu inashindwa kwenda mbele kwa kasi kubwa ambapo amewataka wasanii hao kuanza kujishughulisha na kazi nyingine nje ya sanaa zao ili kuwa na vyanzo vya mapato vya kutosha.

“Wasanii bila kufanya biashara lazima utayumba katika maisha yako, nyie wote hapa mnauwezo wa kuwa matajiri, ni jambo la kuamua tu nataka kufanya kitu fulani na mambo yakaenda,” alisema DC Kasesela.

Aliongeza, “mara ya kwanza nilitembelewa na Diamond hapa, nikamwambia tumia brand yako sasa kufanya biashara ili upate pesa, nimekaa muda nikasikia Diamond Karanga, juzi nimesikia ishu ya Wasafi TV haya ni mafanikio makubwa sana,”

DC huyo aliwataka wasanii hao kuwekeza mkoani Iringa kwa kununua mashamba na kupanda miti kwani biashara hiyo imewanufaisha wengi mkoani huyo.

Alimtolea mfano msaani Aslay kwamba ni mmoja kati ya wasanii ambao anawasiliana nae kwaajili ya kufanya biashara hiyo.

Hukumu ya Nabii Tito Kutolewa April 20

$
0
0
Hukumu ya kesi ya Tito Machibya (maarufu Nabii Tito), ambayo ilikuwa itolewe uamuzi jana, iliahirishwa hadi Aprili 20, mwaka huu kutokana na hakimu anayehusika na kesi hiyo kuwa na dharura.



Akitoa maelezo mahakamani hapo, Mwanasheria wa Serikali Judith Mwakyusa, mbele ya Hakimu Mfawidhi wa Mahakama ya Wilaya, Godfrey Pius, alisema kesi hiyo ilikuja mahakamani hapo kwa ajili ya kutolewa uamuzi mdogo.

Mwakyusa alisema kesi hiyo ilikuwa itolewe uamuzi jana mbele ya Hakimu Mkazi Mfawidhi wa Mahakama ya Wilaya ya Dodoma, James Karayemaha, lakini amepata dharura.

“Mheshimiwa Hakimu shauri hili limeletwa kwako kwa ajili ya kuahirishwa kutokana na Karayemaha kuwa na dharura,” alisema.Hakimu Mfawidhi wa mahakama hiyo, Godfrey Pius, aliahirisha kesi hiyo hadi Aprili 20, mwaka huu itakapoletwa tena kwa ajili ya uamuzi.

Pius alisema mtuhumiwa atarudishwa rumande hadi tarehe hiyo.

Aprili 5, mwaka huu Hakimu Karayemaha alisema wamepokea taarifa ya kitabibu kutoka taasisi ya magonjwa ya akili ya Isanga inayomhusu Mchibya na uamuzi ungetolewa jana.

Nabii Tito alidai ana matatizo ya akili yaliyosababisha kutaka kujiua na kuiomba mahakama kuamuru akachukuliwe vipimo ili kupata uhakika wa afya yake ya akili.

Katika kesi hiyo, anashtakiwa kwa kosa la kutaka kujiua kwa kujikata na wembe na kujijeruhi kwenye maeneo ya tumbo, Januari 25, mwaka huu katika mtaa huo wa Ng’ong’ona alipokwenda kukamatwa na polisi.

Katika Hili , Riyama Ally Ulitakiwa Kuchutama

$
0
0
NI ukweli usiopingika kwamba utakapowataja wasanii wa kike Bongo wanaofanya vizuri, jina la mwanadada Riyama Ally haliwezi kukosekana.

Binafsi namfahamu Riyama tangu kitambo kidogo, enzi hizo akiwa ndiyo kwanza anaanza kuchipukia kwenye filamu, akiwa bado kinda kisanii na kiumri! Namfahamu kuanzia kipindi hicho akiwa mahiri zaidi katika filamu za ma­jonzi na huzuni, tofauti na sasa ambapo anafiti zaidi kwenye nafasi za umcharu­ko, mwanamke wa Uswazi.



Binafsi nilipokutana naye kwa mara ya kwanza na kufanya naye mahojiano am­bayo yalitoka gazetini, moyoni nilijiam­bia kwamba ipo siku Riyama atakuwa msanii mkubwa sana nchini. Niliiona ‘spirit’ kubwa ndani yake, mapenzi makubwa ya sanaa, hamu ya mafanikio na nidhamu iliyotukuka, si tu katika maisha yake ya kisanii bali hata katika maisha yake halisi.



Miaka kadhaa imepita sasa, Riyama amepiga hatua kubwa katika sanaa, japokuwa mimi niliamini kwamba atakuja kung’ara sana kwenye ‘scene’ za majonzi, mambo yamebadilika na anaonekana kung’ara zaidi kwenye nafasi za umapepe, mcharuko, maneno mengi na kuchambana!



Yote kwa yote, Riyama hivi sasa ni msanii mkubwa na bila unafiki nakiri kwamba anaweza kuwa miongoni mwa wasanii wachache wa kike ambao wanakamua kisawasawa, ukita­zama filamu kumi za Kibongo, unaweza kukuta tano au sita Riyama yupo ndani yake! Hata hivyo, kuna jambo ambalo limetokea siku chache zilizopita likimhusisha mwanadada huyo na ama kwa hakika ameonesha kile ambacho wengi hawakukitarajia kutoka kwake. Hilo limetokea katika hafla ya utoaji tuzo za Sinema Zetu zilizoandaliwa kwa mara ya kwanza tangu kuanza kusuasua kwa Bongo Muvi.



Kitendo cha Azam kuanzisha tu tuzo hizo, kwa mtu yeyote anayeitakia mema tasnia ya filamu nchini, ni jambo la kupongezwa sana kwa sababu sasa wasanii wetu watakuwa wakiumiza vichwa kufanya kazi bora, kila mmoja akitaka kung’ara kwenye tuzo hizo ambazo kwa mujibu wa waandaaji, zitakuwa zikitolewa kila mwaka.



Baada tu ya kutolewa kwa tuzo hizo, wasanii wengi walione sha kuchukizwa na kitendo cha mwanadada Wema Sepetu kuzoa tuzo mbili, ikiwemo ya mwigizaji bora wa kike. Mtego huu haukumuacha salama Riyama, naye akasikika katika vyombo vya habari akitoa mapovu ya kufa mtu, mpaka kufikia hatua ya kumwaga machozi hadharani.

Malalamiko yake ni kwamba hakupewa taarifa kwamba ameshindanishwa kwenye tuzo hizo na kwamba amekatishwa tamaa kwa sababu anaamini kwamba ana­fanya kazi kubwa sana pengine kuliko msanii mwingine yeyote wa kike. Kwa lugha nyepesi, Riyama anaamini yeye ndiye aliyes­tahili kupewa tuzo ya mwigizaji bora wa kike.



Waswahili wanao msemo kwamba muungwana akivuliwa nguo, huchuta­ma! Yawezekana vigezo vilivyotumika katika tuzo hizo siyo vile vilivyo­zoeleka na wengi, waandaaji ndiyo wanaojua vigezo zilivyotumika na wameshafafanua sana hili, sina haja ya kulirudia.Riyama unapaswa kufahamu kwamba hata kama unafanya kazi nzuri kiasi gani, haina maana kwamba umezifanya kwa ubora zaidi kuliko wengine.



Yawezekana ukawa bora kwenye eneo hili, lakini ni vizuri kutambua kwamba wapo wengine ambao pia ni bora kwenye eneo lingine, kwa hiyo ustaarabu siyo kuanza kutimua mbio ukilalama kila kona ilihali nguo imeku­dondoka, waungwana huchutama kwanza.



Tuzo zenyewe ndiyo kwanza zimeanza, sasa ukishaanza ‘uswahili’ kama huo unaouonesha, eti ukitaka uombwe radhi na waandaaji, unafikiri zikija tuzo nyingine itakuwaje? Hivi ungeshinda hiyo tuzo kweli un­geikataa kwa sababu hukuambiwa kwamba unashindanishwa? Unaposema yasiyofaa kusemwa na msanii mkongwe kama wewe, si tu unajishusha hadhi wewe mwenyewe, bali pia unawasononesha mashabiki wako ambao miaka nenda rudi wamekuwa wakikusapoti, hata pale ambapo tuzo hazikuwepo.

HASH POWER.
GPL

Nafasi za Ajira zilizotangazwa Leo

$
0
0

Niyonzima Anusurika Kifo Baada ya Kupata Ajali

$
0
0
Niyonzima Anusurika Kifo Baada ya Kupata Ajali
KIUNGO wa Simba, Haruna Niyonzima amenusurika katika ajali aliyoipata eneo la Mwenge jijini Dar es Salaam.

Niyonzima amepata ajali hiyo juzi baada ya gari lake kupiga bonde na kupoteza mwelekeo wakati akirejea nyumbani kwake.

Taarifa zinaeleza Niyonzima raia wa Rwanda alikuwa mwenyewe kwenye gari na akiwa njiani wakati anarejea nyumbani, akakutana na majanga hayo.



Jana Championi lilifanya juhudi za kumpata Niyonzima aliyetua nchini kuichezea Yanga akitokea APR ya Rwanda na baada ya kumpata alithibitisha kupata ajali na kusema anamshukuru Mungu kwa kuwa haikuwa ajali kubwa.



“Gari lilipoteza mwelekeo wakati nikiwa njiani narejea nyumbani na kuingia kwenye msingi. Bahati nzuri sikuwa katika mwendo mkubwa na kuna mtu alikatiza ghafla, nilipojaribu kumkwepa nikapoteza mwelekeo wakati najitahidi kurudi barabarani, nikapiga bonde gari likanishinda nikaingia msingini.



“Haukuwa msingi mrefu, baadaye walikuja watu tukalitoa nikaondoka. Nashukuru sikuumia wala yule mtu sikumgonga hivyo hakuna aliyeumia. Gari ilipata mikwaruzo,” alisema.



Taarifa za Niyonzima kupata ajali zilisambaa jana mchana na kila mmoja alikuwa akieleza tofauti zikiwemo taarifa za kwamba aliumia na wengine wakisema alikuwa na rafiki zake.



Lakini Niyonzima alisisitiza alikuwa mwenyewe kwenye gari na taarifa hizo ziliifikia familia yake yeye akiwa nyumbani na baadhi ya watu walisema wamesikia ameumia sana, jambo ambalo halikuwa sahihi.



Niyonzima amejiunga na Simba akitokea Yanga lakini hakuwa na msimu mzuri baada ya kuumia na kulazimika kwenda kutibiwa India. Hivi karibuni ameanza kurejea taratibu akicheza mechi kwa dakika kadhaa, jambo ambalo limeamsha matumaini upya kwake.

Beki wa Simba Awangojea kwa Hamu Okwi, Bocco

$
0
0
Beki wa Simba Awangojea kwa Hamu Okwi, Bocco
BEKI wa kati wa Yanga, Abdallah Shaibu ‘Ninja’ amesema anawasubiri kwa hamu washambuliaji wa Simba, Emmanuel Okwi na John Bocco ili awaonyeshe kazi kuthibitisha ubora wake kwa sasa.



Simba inaongoza kwa pointi 55, nyuma ya Yanga wenye pointi 47 katika Ligi Kuu Bara na timu hizo zitakutana Aprili 29, mwaka huu kwenye Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam katika mchezo wa ligi hiyo.


Beki huyo ambaye muda mrefu hakuwa akipata nafasi kikosini Yanga, hivi karibuni alicheza mechi ya kwanza ya kimataifa ya Kombe la Shirikisho Afrika dhidi ya Wolaita Dicha ya Ethiopia.



Ninja pia katikati ya wiki hii alicheza mechi ya ligi kuu dhidi ya Singida United na kuifungia Yanga bao moja na kutoka sare ya bao 1-1.



Akizungumza na Championi Jumamosi, Ninja alisema; “Nimekuwa nikibezwa sana ila nafasi ya kucheza imeniongezea vitu na kunifanya nizidi kuwa bora japokuwa bado sijafikia katika kiwango changu.



“Nikipata nafasi ya kucheza dhidi ya Simba, nataka kuwaonyesha washambuliaji wao na zaidi mipira ya juu nitaicheza kwa ustadi mkubwa na naamini washambuliaji wao hawataleta madhara.”

Marekani, Ufaransa na Uingereza Zafanya Shambulizi Syria

$
0
0
Marekani, Ufaransa na Uingereza Zafanya Shambulizi Syria


Marekani, Ufaransa na Uingereza zimefanya shambulizi nchini Syria kumuadhibu rais wa nchi hiyo, Bashar al-Assad kwa shambulio la silaha za sumu dhidi ya raia na kuzuia kufanya hivyo tena.

Televisheni ya taifa nchini Syria imeripoti kuwamba vifaa vya ulinzi wa anga vya Syria, vilijibu shambulio hilo baada ya shambulio la Marekani na washirika wake kutulia.

Hatua hiyo ilijiri kufuatia tuhuma kwamba utawala wa rais Bashar al-Assad wa Syria, ulitumia gesi ya sumu kuwashambulia na kuwaua raia wake, wakiwemo watoto wachanga.

Katika hotuba yake kutoka White House jana Ijumaa mwendo wa saa tatu usiku saa za ukanda wa wa Mashariki mwa Marekani, Rais Trump alisema kuwa nchi hizo tatu zimeamua kuchukua hatua hiyo kama njia ya kuzima uwezekano ya mashambulizi mengine ya kutumia gesi ya sumu.

"Muda mfupi uliopita nimeamuru jeshi la Marekani kushambulia maeneo yaliyohusika na shambulizi la silaha za kemikali lililotekelezwa na utawala wa Bashar al-Assad," alisema Trump.

"Hatutakubali mashambulizi ya kemikali," aliongeza.

Trump aidha alilizishutumu Urusi na Iran kwa kile alichokiita "kushirikiana na uongozi wa Syria kufanya mashambulizi kwa raia wa Syria ambayo hayakubaliki."

Na akihutubia waandishi wa habari kwenye makao makuu ya kijeshi ya Marekani, Pentagon, waziri wa ulinzi Jenerali Jim Mattis alitoa maelezo zaidi kuhusu mashambulizi hayo, na kusema kuwa yalilenga vituo vitatu, kikiwemo kimoja cha utafiti na kingine cha kuhifadhi gesi ya sumu.

"Mashambulizi hayo ni makubwa zaidi ya mara mbili na yale tuliyoyafanya nchini Syria mwaka jana...na ni makubwa," alisema Mattis.

Kituo cha televisheni cha CNN kiliripoti Ijumaa usiku kwamba milipuko mikubwa ilisikika mjini Damascus punde baada ya rais Trump kutoa hotuba yake.

Katika hotuba yake, Trump aidha alieleza masikitiko yake kwamba licha ya rais wa Urus Vladmir Putin kuahidi kuchukua hatua za kuangamiza uwezo wa Syria wa kutumia silaha za kemikali, Russia bado haijafanya hivyo.

"Ni sharti Urusi iamue kama itaendelea kwenye barabara hiyo au itajiunga na nchi zinazotafuta amani," alisema rais huyo.

Yanga Kuondoka Kesho Ethiopia kwaajili ya Mechi ya Marudiano

$
0
0
Image result for yanga wakisafiri
Mabingwa wa soka nchini Tanzania Yanga SC wanatarajia kuondoka nchini Jumapili kwenda Hawassa Ethiopia tayari kwa mchezo wao wa marudiano wa mchujo wa kuwania kuingia hatua ya makundi ya Kombe la Shirikisho Afrika dhidi ya wenyeji Wolaita Dicha.

Yanga watakipiga na Wolaita Dicha Jumatano jioni kwenye Uwanja wa Hawassa mjini Hawassa. Klabu hiyo inaingia mchezoni ikiwa na mtaji baada ya kushinda 2-0 kwenye mchezo wa kwanza Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam Jumamosi iliyopita.

Kitu cha tofauti kuelekea kwenye mchezo huo, Yanga hawatakuwa na kocha wao Mkuu, Mzambia, George Lwandamina aliyeondoka mapema Jumanne kwenda kukamilisha mipango ya kurejea kwenye klabu yake ya zamani Zesco United.

Kwa sasa benchi la Ufundi la Yanga lipo chini ya walimu watatu waliokuwa wasaidizi wa Lwandamila, Mzambia mwenzake, Noel Mwandila na wazawa, Nsajigwa Shadrack na Juma Pondamali.

Okoa Ndoa yako Sasa...Umepungukiwa na Nguvu za Kiume na Unashindwa Kupanda Mlima Vizuri

$
0
0
OKOA NDOA YAKO SASA : JE UMEPUNGUKIWA NA NGUVU ZA KIUME AU UUME WAKO MDOGO AU MPENZI WAKO HAKUTIMIZII UTAKACHO:


Acha kujiona mpweke pale ukutanapo na mpenzi au mke wako kwa sababu ya kutokuwa na nguvu za kiume au Uume wako mdogo

Dawa YA MAPRO POWERA ndio dawa sahihi na tiba tosha kwa sasa Kutibu tatizo na kuponesha kabisa tatizo LA KUWAI KUFIKA KILELENI KABLA MWENZI WAKO BADO AJAKOJOA

KUSHINDWA KURUDIA TENDO LA NDOA NA MWILI KUCHOKA

UUME KUSINYAA NA KUWA LEGELEGE

KUUMWA NA TUMBO WAKATI UNAPOMALIZA KUFANYA TENDO

Dawa hii utumiwa ata na wazee wenye umri mkubwa na haina madhara yoyote

MAKAKANUA HII NI dawa ya maumbili madogo urefusha na kunenepesha saizi upendayo saiz 5-6-7-8 na unene sm 3-4-5 kwa mini huabiki kwa kuwa na UUME mdogo wai sasa upate tiba sahihi kabisa na ni tofauti na ulizowai kutumia :

Tunarudisha mke au mpenzi ndani ya masaa matatu tu zipo dawa za presha kisukali vidonda vya tumbo korodani iliyovimba dawa za uzazi tunapunguza matiti makubwa kitambi na mwili mkubwa dawa zipo FIKA OFISINI KWANGU MBAGALA ZAKHEMU KWA WATEJA AMBAO AMTAKUWA NA NAFASI YA KUJA OFISINI AU MLIO MKOANI MTALETEWA p

Piga simu 0743362017 au 0789234653

DR AGU

Huyu Hapa Binti Mwenye Ugonjwa wa Kutokunenepa

$
0
0
Binti Elizabeth Ann Velasquez ni raia wa Marekani na mkazi wa Austin Texas nchini humo. Ana umri wa miaka 29.

Ni binti ambaye ana ugonjwa ambao unafanya mwili wake kutoongezeka uzito na kunenepa na kwamba hadi katika umri wake wa miaka 29 hajawahi kuwa na uzito uliozidi kilo 27.

Baada ya Kukutana na Rais Goodluck Gozbert Afunguka Haya "Nakumbukwa Kuchekwa"

$
0
0
Baada ya Kukutana na Rais Goodluck Gozbert Afunguka Haya
Msanii wa nyimbo za Injili nchini Goodluck Gozbert amefunguka na kusema kuwa kitendo cha kukutana na Rais John Pombe Magufuli na viongozi wengine akiwepo Rais Mstaafu Jakaya Kikwete inamkumbusha watu ambao walikuwa wakimkatisha tamaa katika kazi yake hiyo.


Goodluck amesema hayo baada ya kupata nafasi ya kwenda Ikulu na kuimba mbele ya viongozi hao katika uzinduzi wa taasisi ya Jakaya Mrisho Kikwete Foundation

"Nikukumbushe tu....sikuzaliwa kwenye familia yenye kujulikana au kuwa na heshima kokote kule, na wala sikuwahi kushika hata nafasi ya tano darasani, nakumbuka kuchekwa, kukatishwa tamaa, kuandikiwa ubaya, kunenewa uongo na kutabiriwa kushindwa kila nilipofikiri ningeweza, nakumbuka mengi mengine ya juzi tu. Ila hakuna kitu nakumbuka zaidi kama zile ahadi za Mungu kwangu, hakuna kitu nakumbuka kama huruma za huyu Yesu aliyenipenda nikiwa sijielewi. Kesho nitawaambia wanangu, Mungu aliyenitoa na kunifikisha pale ndiye atakayeenda pamoja nanyi" alisema Goodluck

Rais Magufuli mara kadhaa alionyesha hisia zake juu ya nyimbo za msanii huyo na kusema kuwa anavutiwa sana hasa zaidi na wimbo wake 'Hauwezi Kushindana' ambao ameutoa miezi  wa tatu mwaka huu.

SOMA PIA: Job Opportunity at East African Community, Internal Auditor

Video ya utupu ya Nandy na Bill Nass yawawekea uzibe Harmonize na Diamond Platnumz

$
0
0
Kwa wafuatiliaji wa mitandao ya kijamii nchini Tanzania, hususani kwa wale ambao wanamfuatilia Diamond Platnumz utagundua kuwa jana Aprili 12, 2018 aliahidi kuachia video ya wimbo wa ‘Kwa ngwaru’ ambayo amemshirikishwa na Harmonize lakini mpaka sasa hivi hakuna chochote kile walichofanya.

Diamond kupitia kupitia kurasa zake za mitandao ya kijamii jana aliahidi kuachia video ya Kwa ngwaru kwa kuahidi kuwa endapo angepata maoni (Comments) 10,000 kwenye posti yake aliyochapisha kwenye mtandao wa instagram, basi wangeachia video ya wimbo huo ambao umetokea kupendwa sana na mashabiki wa wakali hao lakini posti hiyo hadi sasa imefikisha comments elfu 13 na video hiyo bado haija achiwa.

Hii haina ubishi kuwa video ya utupu ya Nandy na Bill Nass imepoteza attention kwa mashabiki wengi wa muziki nchini Tanzania kutokana na ukubwa wa wasanii hao ambao kila Mtanzania alikuwa anaamini kuwa ndio zao jipya la wasanii wa kizazi kipya.

Hata hivyo, mpaka sasa hivi si Diamond wala Harmonize aliyetoa kauli yoyote ile kuhusiana na kuachia video hiyo ingawaje mashabiki wengi walitazamia kuona video hiyo kwa siku ya jana.

Kwa mujibu wa maelezo ya Nandy na Bill Nass kuhusu video yao ya utupu iliyovuja siku ya jana hadi sasa bado haijajulikana ni nani aliyevujisha kwani wamekuwa wakitupiana lawama kila mmoja.

SOMA PIA: Job Opportunity at East African Community, Security Officer

Kutana na Mtaalam Sharif Hamad Kalala Mchambuzi wa Nyota za Binadamu na Tiba Asili

$
0
0
KUTANA NA SHARIF HAMAD KALALA NI
SHARIFU MCHAMBUZI WA
NYOTA ZA BINAADAMU NA NI MWENYE UPEO MKUBWA KUTAFITI MATATIZO YAKO KABLA YA KUTOA USHAURI WAKE WA TIBA AlJALISHI MBALI ULIKO TIBA YAKE UMFIKIA YEYOTE MWENYE UITAJI POPOTE
DUNIANI.

 SHARIF HAMAD KALALA NI TABIBU MWENYE KUBRI TOKA KWA ALAH ANATIBU KWA NJIA YA VITABU VYA QUR-AN, DAWA ZA ASILI ZA MITI SHAMBA PAMOJA NA DAWA ZA KIARABU.
ANATIBU KWA NJIA YA SIMU KWA KUTOA
MAELEKEZO NAMNA YA MATUMIZI YA DAWA UKIWA NCHI YOYOTE MKOA WOWOTE KWA MATATIZO YAFUATAYO:-

 KUFANIKISHA NDOA KWA UNAYE MPENDA KWA HARAKA. KUMRUDISHA MPEZI NDANI YA MASAA 12 TU.
 ULIJALI (NGUVU ZA KIUME) NDANI YA /IKI MMOJA TU
MIGUU KUWAKA MOTO KUTAFSIRI NDOTO MFARAKANO WA WANANDOA MFARAKANO KAZINIKUPANDISHWA CHEO NDANI YA SIKU SABA 7 TU.
KUTOA PETE YA BAHATI KUTOA MAJINI MACHAFU IKIWA NI KWENYE MWILI WA BINADAMU MAJUMBANI NA KWENYE BIASHARA. KUPATA MAFANIKIO YA MALI BILA YA MASHARTI. KUPANDIKIZANYOTA YA KUBASHIRI KUFUNGUA UZAZI KWA WALIYO FUNGWA KWA NJIA YA USHIRIKINA KUTOA VIFUNGO VYOTE VILIVYO FUNGWA KWENYE BIASHARA. ANA UWEZO MKUBWA WA KUPANDIKIZA NYOTA YA KUMPATA YEYOTE UMPENDAYE KWA KUMUOA AU KUWA NAYE. ANAO UWEZO WA KUMRUDISHA ALIYE MBALI PIA ALIYE CHUKULIWA
KWA NJIA YAMSUKULE
NAO UWEZO WA KUUA KESI SUGU NA MPYA NDANI SIKU 7 TU.
MENGINEYO MENGI ZAID YALIYO KUWA SUGU PIGA KWA WALE WALIYO ANGAIKA SEHEMU MBALI MBALI SHARIF HAMAD KALALA NI SULUISHO. ENDAPO UTAMSIKILIZA KWA YALE ATAKAYO KUSHAURI NA KUKUPA
ELEKEZI.
 TIBA NI KWA DINI ZOTE POPOTE ULIPO NJE NA NDANI YA NCHI.
MOBILE +255 -673 025 376
WhatsApp +255-757 069 066

Paul Makonda "Kuna Wanaume Wanaomba Dua Mvua iendelee Kunyesha ili Mambo Yaharibike"

$
0
0
Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam, Paul Makonda amewataka wanawake waliotelekezewa watoto kuwa na moyo wa uvumilivu katika kipindi cha mvua ili mradi kila mtoto apatiwe haki yake inayostahili kama alivyoahidi japokuwa anajua kuna wanaume wanaomba dua mvua iendelee kunyesha ili mambo yaharibike


Paul Makonda ametoa kauli hiyo leo Aprili 13, 2018 alipokuwa akizungumza na umati mkubwa wa mama ambao mpaka sasa hawajafanikiwa kupata namba ya kuingia ndani kusikilizwa shida zao na kuwasii wamama hao kuwa na subira  wapatiwe namba ili zoezi hilo liweze kuendelea kusudi kila mmoja apate haki yake.

"Furaha niliyonayo nikuona kuna watu wameshaanza kupata amani ya mioyo yao na hilo ndio lilikuwa lengo kubwa la serikali yenu na watumishi hawa waliojitolea ambako kiukweli siwalipi hata senti 5. Lakini zaidi ya yote ndio lengo la Mungu kuleta amani katika familia. Leo ni siku ya Ijumaa ambayo ilikuwa ya mwisho lakini ukitazama kuna watu hata namba hawajapata lakini kuna mambo mawili lazima muyapate", amesema Makonda.

Pamoja na hayo, Makonda ameendelea kwa kusema "jambo la kwanza ni lazima kila mtoto apate kile anachostahili, jingine ni kupata bima ya afya niliyoahidi kwa kila mtoto aliyekanyaga katika viwanja hivi. Kwasababu hizo niwaombe muwe wavumilivu leo wote ambao hamjapewa namba mtapewa. Vumilie mvua najua wakina baba huko walipo wanaombea mvua iendelee kunyesha ili mambo yaharibike lakin waambieni kama mliweze kuvumilia miezi tisa na matusi yote waliyowatukana sembuse mvua ? kwa hiyo tutaendelea kuvumilia mpaka haki itakapopatikana".

Kwa upande mwingine, Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam Paul Makonda amesema mpaka kufikia siku ya tano leo wameshasikilizwa takribani wamama 4,000 huku familia 205 kwa hesabu za siku ya jana (Alhamisi) yaani watoto 205 wameondokana na mfumo wa omba omba na sasa wanapatiwa huduma zote zinazostahili kwa baba na mama zao wakiwa pamoja.

Makala: Nandy Umetudanganya Watanzania, Umezidi Kumpa Ushindi Zari, Wimbo wa Sina Jambo Umekuumbua

$
0
0
Kwanza nitoe pole kwa Nandy na Bill Nass mara baada ya video yao ya faragha kuvuja mtandaoni, ni kitu ambacho unaweza kukichukulia kawaida ila usiombe yakukute.

Viatu walivyovaa Nandy na Bill Nass kwa sasa vinawapwaya katika miguu yao na pengine ni vizito, nitoe pole kwao kwa hilo lilowafika kwani ni tukio ambalo si vigumu kuja kufutika katika maisha yao kutokana na utandawazi uliopo sasa.

Fid Q katika ngoma yake August 13 alisema, ustaa ni mzigo wa mwiba, ukiubeba utaumia. Video ya Nandy na Bill Nass imesambaa kwa kasi kutokana na umaarufu wao, hivyo maumivu wanayopitia wanapaswa kuelewa ni kawaida katika tasnia yao ya burudani.

Nandy ameelewa hilo na ndio sababu hakuona aibu kuomba radhi kwa mashabiki wake kwa hicho kilichotokea. Kwa anayeelewa maana ya neno samahani atakuwa amemsamehe na maisha mengine kuendelea.

KWANINI NANDY

Baada ya video kusambaa, Nandy na Bill Nass kila mmoja amejitetea kwa upande wake. Nimzungumzie Nandy kwa ufupi; ameomba radhi na kueleza kilichotokea ila kuna jambo halipo sawa kwa upande wake.

Kwa mujibu wa post aliyoweka Bill Nass katika ukurasa wake wa Instagram jana na kuifuta baada ya muda mfupi alitupa lawama zake nyingi kwa Nandy kuhusu kuvuja kwa video hiyo. Ameeleza siku moja kabla, Nandy alimtafuta kumuomba picha za zamani kipindi wakiwa wapenzi ili azitumie katika kum-wish Happy Birth Day yake, hata hivyo alimueleza kuwa hana picha hizo.

Lakini baadaye alikuja kuona picha hizo mtandaoni kitu ambacho hakupendezwa nacho kutokana kwa sasa ana mahusiano mapya, hivyo Nandy alishindwa kuheshimu uamuzi wa mwenzake.

Katika Interview aliyofanya Nandy na MCL Digital alieleza kuwa walikuwa na mahusiano mwaka 2016, mahusiano yao walipanga kuwa private lakini ukifuatilia kwa makini kuna kitu ambacho hakipo sawa hapa.

Katika video iliyosambaa mtandaoni unasikika wimbo wa Bill Nass unaokwenda kwa jina la Sina Jambo. Wimbo huu ulitoka Augost 17, 2017, yaani miezi saba iliyopita.

Hivyo kueleza kuwa walikuwa na mahusiano mwaka 2016 na ndio video hiyo ilirekodiwa, bado haiingii hakilini kwa urahisi huo.

KUHUSU ZARI

Sikupenda kumhusisha mrembo huyo katika suala hili ila kutokana na ujumbe ambao ningependa kuutoa nalazimika kufanya hivyo. Nitangulize samahani kwa yeyote nitakayemkwanza.

March 28, 2018 mwaka huu Zari alipata dila la kuwa balozi wa kutangaza nepi za watoto za Soft Care. Baada ya hapo kulizuka mjadala kuwa ni kwanini mastaa wa kike Bongo hawajapewa dili hilo au kupata dili kama hizo.

Muigizaji Faiza Ally alihoji; ” how stupid Tanzanian can be, mastaa wote watanzania, watu wote Watanzania hamkuona hata mmoja anae stahili kupata dili zaidi ya Zari ? Ina maana uhitaji Bongo umeisha mpaka tuweke watu kutoka nje?.

Baada ya kauli hiyo Shamsa Ford alimjibu Faiza kwa kumueleza kuwa hakuna mfanyabiashara atayekubali kumchukua staa wa Bongo kisa uzalendo tu halafu apate hasara.

Aliongeza kuwa baadhi ya mastaa wengi wa Bongo wanajulikana kwa mambo ambayo si mazuri kitu ambacho si kizuri kwa brand za kibiashara.

“Maana kama jamii inakudharau hata hiyo bidhaa unayoibeba itadharaulika.kikubwa tujifunze, swala sio kujulikana ila swala ni kuwa unajulikana vipi!? Watu wanakutambua kwa lipi. Ni vizuri tumeumia sasa tujipange na kufukiaa mashimo yaliyotoboka ili na sisi tueshimike na kuthaminika,” alisema Shamsa.

Kwa mujibu wa posti ya Bill Nass, alieleza baada ya kumuuliza Nandy ni kwanini ametoa picha hizo za kitambo wakiwa katika mahusiano kwani ni kitu walipanga kuwa siri, Nandy alimjibiwa kuwa amepanga kiki yeye na team yake. Weka nukta hapo.

Twende pole pole; Kwa kile kilichotokea jana kwa Nandy naanza kuelewa kile alichoeleeza Shamsa Ford. Sielezi kwa kumhukumu Nandy, hapana!, ila ni ukweli ambao upo na utendelea kuishi. Hivyo maneno ya Shamsa yanasaidifu kile kilichotokea kwa asilimia kubwa na tukio lenyewe linatoa sababu ya kwanini Zari alistahili kupata dili lile. Asante.
Viewing all 104799 articles
Browse latest View live




Latest Images