Quantcast
Channel: UDAKU SPECIAL
Viewing all 104789 articles
Browse latest View live

Rais Magufuli Ampa Kashkash Mbunge...Habari Zilizopo Katika Magazeti ya Leo Jumapili ya May 6

$
0
0


Rais Magufuli Ampa Kashkash Mbunge...Habari Zilizopo Katika Magazeti ya Leo Jumapili ya May 6

Serikali Kutumia Bilioni 131.47 Kutekeleleza Miradi Ya Kimkakati

$
0
0
Na Benny Mwaipaja, WFM,  Dodoma
Kwa mara ya kwanza katika historia ya nchi, Serikali imezindua Mkakati wa kuziwezesha Mamlaka za Serikali za     Mitaa kutekeleza miradi yenye kuchochea upatikanaji wa mapato ili ziweze kujitegemea.

 Mkakati huo umezinduliwa Jijini Dodoma na Naibu Waziri wa Fedha na Mipango, Dkt. Ashatu Kijaji, kwa niaba ya Waziri wa Fedha na Mipango, Dkt. Philip Mpango, ambapo amesema kiasi cha shilingi bilioni 131.47 kitatumika kutoa ruzuku ya utekelezaji wa miradi 22 kwa halmashari 17 zilizoko katika mikoa 10 nchini, katika mwaka wa fedha 2018/19.

 Ameitaja mikoa hiyo ambayo Halmashauri zake zimekidhi vigezo vya kunufaika na miradi ya kimkakati katika awamu ya kwanza ya mpango huo kuwa ni Dar es Salaam, Geita, Kigoma, Kilimanjaro, Lindi, Morogoro, Mtwara, Pwani, Simiyu na Songwe.

 Amesema kuwa lengo la Serikali ni kuhakikisha kuwa Halmashuri zinajenga uwezo wa kujitegemea kwa takribani asilimia 80 hadi 100 ifikapo mwaka 2025, badala ya hali ya sasa ambapo halmashauri hizo zinategemea ruzuku kutoka Serikali Kuu kwa zaidi ya asilimia 88.

Amezitaka halmashuri zitakazopata fedha za miradi hiyo kuhakikisha fedha hizo zinawekezwa kwenye miradi yenye tija, inayokuza ajira kwa wananchi na kuongeza mapato ya halmashauri.

Ametoa wito kwa Wakurugenzi wa Majiji, Manispaa na Halmashauri kubuni miradi ya kibiashara kwa ajili ya wananchi wanaowaongoza kwa kutengeneza ajira kwa kutumia rasilimali zilizopo katika maeneo yao.

Alionya kuwa hatua kali za kisheria zitachukuliwa kwa watendaji wanaosimamia miradi hiyo ikiwa watatumia fedha hizo kwa malengo tofauti na yaliyokusudiwa na kurejea kauli ya Rais Dkt. John Pombe Magufuli, kwamba kufuja fedha za Serikali katika kipindi hiki ni sawa na kunywa sumu.

Kwa upande wake Katibu Mkuu wa Wizara ya Fedha na Mipango Bw. Doto James, amesema kuwa Serikali inazo fedha za kutosha kufanikisha mkakati huo na kutoa wito kwa viongozi wa Mikoa husika kuchangamkia fursa hiyo kwa kuanisha miradi yenye tija ili ipatiwe fedha.

Alifafanua kuwa tayari Serikali imetumia kiasi cha shilingi bilioni 15 kwa ajili ya utekelezaji wa miradi mbalimbali ya kimkakati katika mkoa wa Dar es Salaam katika Halmashauri ya Jiji la Dar es Salaam, kwa kujenga Kituo cha Mabasi cha Mbezi Luis, Ujenzi wa Soko la Mburahati katika Manispaa ya Ubungo, Ujenzi wa Soko la Kisasa la Magomeni katika Manispaa ya Kinondoni na Ujenzi wa Soko la Kisasa la Kisutu, Ujenzi wa Machinjio ya Kisasa ya Vingunguti katika Manispaa ya Ilala.

Naye Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa- TAMISEMI Selemani Jaffo (Mb) amesema kuwa Ofisi yake itaanza kufuatilia na kupima utendaji kazi wa Wakurugenzi wa Halmashauri zote nchini ili kuona kama wanaendana na kasi ya Serikali ya Awamu ya Tano inayoongozwa na Mhe. Rais Dkt. John Pombe Magufuli.

Aliwapongeza Wakurugenzi walioonesha mfano katika kuendana na kasi ya Serikali ya Awamu ya Tano kwa kubuni miradi yenye tija na ya kimkakati iliyopewa Fedha na Wizara ya Fedha na Mipango na kuwataka watendaji wengine waige mfano huo.

Baadhi ya miradi itakaotekelezwa na Halmashauri zilizokidhi vigezo ni pamoja na Ujenzi wa Masoko ya Kisasa, Ujenzi wa Maegesho ya Malori, Ujenzi wa stendi za kisasa, Maghala ya kuhifadhi mazao, Masoko ya Kisasa, Machinjio na Ujenzi wa Viwanda.

Download Hapa Application Mpya ya Udaku Special Uweze Soma Vimbwanga na Udaku Mtaani Kila Siku

$
0
0
Mpendwa msomaji wetu, tunakukumbusha Kuidownload Upya Application yetu ya UDAKU SPECIAL Maana ile ya Zamani Tutaifuta.

Kuna Marekebisho Makubwa tumeyafanya ikiwa na tatizo la Notification kutatuliwa

NB: App mpya ina Icon Nyekundu

 Bonyeza Hapa Chini Kuinstall Upya:


==>>Unaweza Kuidownload << kwa Kubofya Hapa>>   

Wema Sepetu baada ya Heaven Sent, ‘kuna project za kutikisa mji’

$
0
0
Baada ya muigizaji Wema Sepetu kuachia filamu yake ya Heaven Sent, 2017 na kushinda tuzo, amefunguka kipi kinafuata kutoka kwake.

Mrembo huyo amesema kwa kushirikiana na timu yake kuna movie wanaandaa ambayo itakuja kubadili tasnia nzima, pia kuna event nyingine kubwa atafanya June mwaka huu.

“Heaven Sent imekuja imeshinda tuzo, so it good thing, tutegemee vitu vikubwa kama nilivyosema hapo awali kuna kitu kitatokea June kwa hiyo tukae mkao wa kula kitu kizuri kinakuja nadhani kitabadilisha tasnia ya filamu as a all, kuna project za kutikisa mji,” Wema ameiambia Bongo5.

Usiku wa April 01, 2018 filamu ya Heaven Sent ilimfanya Wema Sepetu kuwa mshindi wa tuzo mbili za Sinema Zetu International Film Festival Awards (SZIFF).

Michepuko Kwenye Mapenzi ni Kitu cha Kawaida – Young Killer

$
0
0

Rapper Young Killer mara baada ya kusikia aliyekuwa mpenzi wake ‘Halimaty’ kwa sasa ana ujauzito wa mtu mwingine, amevunja ukimya.

Young Killer akipiga stori na U-Heard, Clouds FM amesema jambo hilo halimuumizi kwani walishaachana na siku zote kila chenye mwanzo kina mwisho wake.

Soma Pia; Young Killer na Miss Hip Hop ndio basi tena

Pia Young Killer amekanusha taarifa kuwa kipindi cha mahusiano yao alikuwa akimnyanyasa mrembo huyo.

“Hapana, ni maneno ya watu hayo kwa sababu matatizo madogo madogo, sijui michepuko huwa ni vitu vya kawaida kwenye mapenzi, huwa havikosi, umenisoma?,” amesema Young Killer.

“Ni jambo la kheri, hapana siumii kwa sababu hakuna kitu kama kuona mtu ambaye mlikuwa mnapeana furaha anaendelea kufurahi,” ameongeza.


Kipindi cha mapenzi yao kabla ya kuchana

Young Killer ambaye anafanya muziki wake chini ya Wanene Entertainment kwa sasa anatamba na ngoma ‘Shots’ aliyomshirikisha rapper Khaligraph Jones kutokea nchini Kenya.

Video: Mimi nilikuwa Nabii wa Yanga, nimeacha historia TZ – Jerry Murro Ajitapa

$
0
0
Aliyekuwa afisa habari wa klabu ya Yanga, Jerry Muro amesema kuwa ndani ya timu hiyo alikuwa kama nabiina wala hakuajiriwa kili alilotamka lilikuwa likitimia kama alivyosema wataifunga Costi Union ya Tanga goli sita kwakuwa ilikuwa tarehe 6 na kweli yakatimia.

VIDEO:

Soma Nafasi za Ajira zilizotangazwa leo

$
0
0

Kutana na Mtaalam Sharif Hamad Kalala Mchambuzi wa Nyota za Binadamu na Tiba Asili

$
0
0
KUTANA NA SHARIF HAMAD KALALA NI SHARIFU MCHAMBUZI WA
NYOTA ZA BINAADAMU NA NI MWENYE UPEO MKUBWA KUTAFITI MATATIZO YAKO KABLA YA KUTOA USHAURI WAKE WA TIBA AlJALISHI MBALI ULIKO TIBA YAKE UMFIKIA YEYOTE MWENYE UITAJI POPOTE
DUNIANI.

 SHARIF HAMAD KALALA NI TABIBU MWENYE KUBRI TOKA KWA ALAH ANATIBU KWA NJIA YA VITABU VYA QUR-AN, DAWA ZA ASILI ZA MITI SHAMBA PAMOJA NA DAWA ZA KIARABU.

ANATIBU KWA NJIA YA SIMU KWA KUTOA
MAELEKEZO NAMNA YA MATUMIZI YA DAWA UKIWA NCHI YOYOTE MKOA WOWOTE KWA MATATIZO YAFUATAYO:-

 KUFANIKISHA NDOA KWA UNAYE MPENDA KWA HARAKA. KUMRUDISHA MPEZI NDANI YA MASAA 12 TU.
 ULIJALI (NGUVU ZA KIUME) NDANI YA /IKI MMOJA TU
MIGUU KUWAKA MOTO KUTAFSIRI NDOTO MFARAKANO WA WANANDOA MFARAKANO KAZINIKUPANDISHWA CHEO NDANI YA SIKU SABA 7 TU.
KUTOA PETE YA BAHATI KUTOA MAJINI MACHAFU IKIWA NI KWENYE MWILI WA BINADAMU MAJUMBANI NA KWENYE BIASHARA. KUPATA MAFANIKIO YA MALI BILA YA MASHARTI. KUPANDIKIZANYOTA YA KUBASHIRI KUFUNGUA UZAZI KWA WALIYO FUNGWA KWA NJIA YA USHIRIKINA KUTOA VIFUNGO VYOTE VILIVYO FUNGWA KWENYE BIASHARA. ANA UWEZO MKUBWA WA KUPANDIKIZA NYOTA YA KUMPATA YEYOTE UMPENDAYE KWA KUMUOA AU KUWA NAYE. ANAO UWEZO WA KUMRUDISHA ALIYE MBALI PIA ALIYE CHUKULIWA
KWA NJIA YAMSUKULE
NAO UWEZO WA KUUA KESI SUGU NA MPYA NDANI SIKU 7 TU.
MENGINEYO MENGI ZAID YALIYO KUWA SUGU PIGA KWA WALE WALIYO ANGAIKA SEHEMU MBALI MBALI SHARIF HAMAD KALALA NI SULUISHO. ENDAPO UTAMSIKILIZA KWA YALE ATAKAYO KUSHAURI NA KUKUPA
ELEKEZI.
 TIBA NI KWA DINI ZOTE POPOTE ULIPO NJE NA NDANI YA NCHI.

MOBILE +255 -673 025 376
WhatsApp +255-757 069 066

Shaffih Dauda Atoboa Siri ya Mafanikio Simba

$
0
0
Siku zote mafanikio hayaji yenyewe, yanatafutwa na nyuma ya mafanikio yoyote lazima kuwe kuna mtu au watu wanaopambana kuhakikisha mafanikio hayo yanapatikana.

Kwa sasa klabu ya Simba inaelekea kutwaa ubingwa wa VPL walioupoteza kwa kipindi kirefu lakini pia akuna mgongano wala mvutano ndani ya klabu, kila kitu ni shwari.

Shaffih Dauda anaamini hali hiyo inatokana na uongozi mzuri chini ya kaimu Rais wa Simba Bw. Salim Abdalla maarufu kama try again.

Shaffih ameenda mbali zaidi na kusema kuwa, endapo Bw. Salim ataamua kugombea nafasi ya urais ndani ya Simba bila shaka yoyote atamuunga mkono.

“Wapo wanachama wenye uwezo na nia wakasimama kwenye hivi vilabu vitasogea, mfano mzuri ni Simba ya sasa hivi watu hawajui mafanikio ya Simba ya sasa hivi yapo kwa nani.”

“Salim Abdallah ‘try again’ ni mtu ambaye amesimama amenyooka anasimamia misingi, hana janja-janja nina uhakika aina ya watu kama yeye wanaweza wakawa wanapigwa vita sana na baadhi ya wanachama ambao ni oyaoya.”

“Salim akichukua fomu ya kugombe uenyekiti Simba, mimi kama mpenda maendeleo ya michezo nitamuunga mkono.”

Yanga wasema haya kuhusiana na hali yao kiuchumi

$
0
0
Uongozi wa Yanga kupitia kwa Msemaji wake, Dismas Teni, umeeleza kwa msisitizo kuwa ni kweli unapitia wakati mgumu hivi baada ya kuyumba kuyumba kiuchumi.

Ten ametoa kauli hiyo wakati akizungumzia maandalizi kuelekea mchezo wao wa leo dhidi ya USM katika Kombe la Shirikisho Afrika dhidi ya USM Alger huko Algeria.

Ofisa huyo wa Habari amesema Yanga hivi sasa ina tatizo la kuyumba kiuchumi, huku akieleza kuwa ni timu nyingi huwa zinapitia changamoto kama hizo na akiamini siku moja suala hilo litapita.

Yanga imekuwa haina matokeo mazuri msimu katika ligi na mashindano ya kimataifa ukilingana na msimu mmoja nyuma, sababu za kuyumba kwa uchumi zinaelezwa kuchangia pia kikosi kutokuwa imara.

Katika mchezo wa leo wa Kombe la Shirikisho, Yanga itakuwa inawakosa wachezaji wake kadhaa walio mhimili wa kikosi cha kwanza.

Hizi ndizo Dalili za awali za kuharibika kwa Mimba

$
0
0
Leo tumeamua kuzungumzia jambo hili ambalo huwakumba watu wengi sana katika familia zao, wengi wamekuwa wakitokewa na jambo hili katika mimba zao za kwanza na mimba zao zinazoendelea katika familia zao na kushindwa kupata watoto.

Kuna wengine wanapata watoto au mtoto mmoja na baadaye wanashindwa kupata mtoto kwa sababu ya mimba zao kuwa zinaharibika mara kwa mara.

Kwa kawaida kitabibu inaaminika kwamba asilimia 50 ya mimba zote huwa zinaharibika, najua watu wengi wanaweza wakashangaa lakini ni kweli tafiti za kitabibu zinasema hivyo isipokuwa watu wengi huwa hawaelewi au wanawake wengi huwa hawaelewi kama mimba zao zimeharibika kwani hutoka au huaribika kabla wao hawajagundua kama walikuwa wajawazito.

Isipokuwa wale ambao hujua kwamba walikuwa na ujauzito na umetoka hao wanaweza kuwa asilimia 10 hadi 20, na hizo asilimia zinazobaki kama 35 ni kwa wale ambao hawajui kama mimba zao zimeharibika au walikuwa wajawazito.

Kwa maana hiyo basi wewe ambaye unatafuta ujauzito kwa muda mrefu sasa na umekuwa haupati lakini unakuwa unaandamwa na matatizo ya hedhi kwa mara kadhaa halafu hedhi inakaa sawa basi kuna uwezekano mkubwa kwamba mimba zako zimekuwa zikiharibika pasipo wewe kujua.

Dalili za kuharibika kwa mimba

Ni vizuri kujua ni dalili zipi ambazo mtu akiziona basi kunakuwa na uwezekano wa kuharibika kwa mimba, kwani mimba huweza kuharibika hadi wiki ya 20 (miezi 5) kuanzia siku ya kwanza inapoingia, japo hasahasa hutokea katika miezi mitatu ya mwanzo (1st trimester) lakini huweza fika hadi wiki ya 20.

Na dalili hizo ni kama;

Damu nyepesi kutoka kwa mwanamke mwenye mimba.
pale mwanamke anapopata ujauzito basi ni vema kabisa kujua kwamba hatakiwi kabisa kupata hedhi au kutokwa na damu katika via vyake vya uzazi, kwa maana hiyo basi wewe mwanamke ambaye umepata ujauzito na bado unaona damu inatoka kidogokidogo basi ni vema kuwahi mapema kituo cha afya kabla tatizo halijawa kubwa kwani kutoka kwa mimba (miscarriage) huwa hakutokei ghafla tu huanza taratibu na dalili yake kubwa ni hii kutokwa na damu ilihali wewe ni mjamzito.

kutokwa na damu yenye mabonge mabonge na inakuwa nzito

Wakati mwingine  mwanamke anaweza akakumbwa na kutokwa na damu nyepesi na kabla hajatahamaki, damu ile nzito inaanza kutoka tena, na hii ni dalili mbaya sana ya kwamba ujauzito wako uko kwenye hatari zaidi na kuna uwezekano ujauzito ulionao ukatoka, kwa maana hiyo basi mwanamke anapopatwa na dalili ile ya kwanza ni vema zaidi kufuata ushauri wa daktari ili kuulinda ujauzito wako.

Uchovu na maumivu makali ya kiuno na mgongo.

kwa wewe mwanamke ambaye mimba bado ni changa na unapatwa na maumivu makali sana ya mgongo au kiuno au vyote kwa pamoja basi ni vema kuwahi kituo cha afya ili kuangalia ni jinsi gani unaweza kuzuia ujauzito wako usitoke au usikumbwe na tatizo hili la kutokwa na ujauzito (miscarriage).

Kama unapatwa na dalili kama hizi kutokwa na damu nyepesi au nzito ilihali wewe ni mjamzito basi ni vema kuwahi kituo cha afya au wasiliana nasi ili kukusaidia. Kwa ushauri vipimo na tiba dokta anapatikana kwenye vituo vyake vya Dar es Salaam, Tanga, Morogoro na Mwanza.

Kuwa na Ngozi Nyeupe Bila Kutumia Mkorogo

$
0
0

Wanawake wengi na baadhi ya wanaume wanatumia vipodozi vilivyo na kemikali ili waweze kuwa na ngozi nyeupe.

Ila leo nitakupa njia moja tu itakayoweza kukusaidia kuwa na rangi nyeupe bila kutumia kipodozi vyenye kemikali katika ngozi yako.

Ifuatayo ni njia itakayoweza kukusaidia.

Mahitaji:

1. Asali kijiko kimoja cha chai



2. Juisi (maji maji ya limau) kijiko kimoja cha chakula.

3. Maji ya uvuguvugu kiasi


Jinsi ya kutengeneza mchanganyiko wako:

1. Changanya juisi ya limau na asali katika chombo kimoja kisafi na uchanganye ukitumia uma au kijiko cha kawaida kwa dakika kadhaa.

Matumizi:

1. Osha uso vizuri ukitumia sabuni (kama unapata sabuni ya habbat soda inakuwa vizuri zaidi) na maji ya uvuguvugu kisha jifute na kitambaa kisafi.

2. Jipake mchanganyiko huo usoni na maeneo yote ya shingoni taratibu huku ukijipaka taratibu kwa dakika 10.

3. Osha uso kwa maji safi, mwisho jifute kwa taulo safi.



ZINGATIA: Fanya zoezi hili kwa wiki mara 1 mpaka mara 3.

Chanzo: Fadhil Paulo.

Pata Tiba ya Tatizo la Nguvu Za Kiume, Inasaidia Kukufanya Urudie Mara 5 na kuchelewa kwa Dakika 20

$
0
0
TATIZO LA UPUNGUFU WA NGUVU ZA KIUME NA MAUMBILE MADOGO LINATIBIKA.Baada ya utafiti wa mda mrefu juu ya matatizo ya upungufu wa nguvu za kiume na ukosaji wa hamu ya tendo la ndoa ama kushindwa kurudia tendo kwa haraka DR Magise imekuletea tiba ya matatizo hayo kwa kutumia dawa za:

GUMBA POWER:Ni dawa asili ya vidonge inayotibu tatizo la upungufu au ukosefu wa nguvu za kiume,dawa hii inamchanganyiko wakutosha wenyekuzalisha vichocheo vingi vya Hemone za Gestrogen vikiwemo vitamin B6&B1,vitamini E,pamoja na madini aina ya zinc vitakufanya kuwa na nguvu na mzunguko mzuri wa damu na kuongeza hamu na uwezo wa kufanya tendo la ndoa zaidi ya hatua nne au zaidi,na kuchelewa kufika kileleni zaidi dakka 20-30.

NTINJE:Inarutubisha maumbile ya uume yani kurefusha na kunenepesha nchi 4-7 upana cm3-4 standard kiafya haijalishi umri wako hata kwa wazee ukiitumia maumbile yako yatabaki kuwa hivyo siku zote,Pia tunatibu Presha,kisukari siku7,ngiri,chango la tumbo tumbo kujaa gesi,kutopata choo vizuri

 TUPO TZ DAR ES SALAAM   MBAGALA RANGI TATU.HUDUMA HII UTALETEWA POPOTE ULIPO .WASILIANA NAMI 0754741788, 0715741788, 0783741788

-DR MAGESA

Wananchi Wamkataa mganga wa zahanati wakimtuhumu kuiba dawa.

$
0
0
Zahanati ya Kijiji cha Izinga, Kata ya Wampembe wilayani Nkasi mkoani Rukwa, imefungwa kwa muda usiojulikana baada ya wakazi wa kijiji hicho kumkataa mganga wa zahanati hiyo wakimtuhumu kuiba dawa.

Mwenyekiti wa kijiji hicho, George Fataki alisema wananchi hao wamefikia uamuzi huo baada ya kukamata dawa zikiuzwa katika duka la dawa za binadamu kijijini hapo.

Alisema baada ya wananchi hao kumhoji mmiliki wa duka hilo alieleza kuwa dawa hizo aliuziwa na mganga huyo (jina tunalihifadhi).

Fataki alisema baada ya wananchi hao kupata taarifa hizo walimfuata mganga huyo na walipomhoji alikiri kumuuzia dawa mfanyabiashara huyo baada ya kuona zimekaa muda mrefu bila kutumika na muda wake wa kufikia mwisho wa matumizi ukikaribia.

Alisema Kaimu Mganga Mkuu wa Halmashauri ya Wilaya ya Nkasi, Hashim Mvogogo alifika kijijini hapo kwa ajili ya shughuli za kikazi na kukuta mgogoro huo.

Kwa mujibu wa Fataki, kaimu mganga huyo alizungumza na wananchi ili wamuache mganga huyo aendelee kutoa huduma katika zahanati hiyo.

Mkurugenzi wa Halmashauri ya Wilaya ya Nkasi, Misana Kwangula alikiri kuwapo kwa tukio la kufungwa kwa zahanati hiyo na kuongeza kuwa tayari muuguzi huyo alikwisha fikishwa katika mikono ya sheria.

Mzee Yussuf Afunguka Kulipua Bomu

$
0
0
Aliyewahi kuwa mwimbaji mahiri wa muziki wa Taarab nchini ambaye pia alikuwa Mkurugenzi wa kundi la Jahazi Modern Taarabu, Mzee Yusuph amefunguka na kusema kuwa hazitapita siku tatu lazima alipue bomu.

Mzee Yussuf amesema hayo baada ya moja ya mtu ambaye alifahamiana naye kwa masuala ya kidini lakini baadae amekuja kumbadilikia jambo ambalo amesema sasa limempa mafunzo ila lazima aliweke sawa ndani ya siku tatu hizi.

"Kinachouma ni pale Muislamu mweenzio kukujia kidini kisha kukugeukia mpaka unajiuliza huyu alikuja kwa ajili ya urafiki wa kidini lakini leo anakuulizaa na kukuambia maneno mpaka unajiuliza karitadi kwani? Kiuhalisia si kila mtu wa kumuamini na kuna watu huwezi kumjua mpaka uishi nae mda mrefu kidogo ili umsome na wengine washenzi mpaka huamini kama ni yeye lakini humjui ila mpaka ukae nae. Kweli usimdharau usiyemjua na pia usimuamini usiyemjua"

Baada ya kauli hiyo watu wengi walianza kumpa pole Mzee Yussuf huku wengine wakitamani kujua jambo gani ambalo limempata mpaka kutoa kauli kama hiyo ambayo inaonyesha wazi kabisa kuwa kuna jambo halipo sawa, ndipo hapo aliposema kuwa lazima aliweke sawa jambo hilo ndani ya siku tatu hizi.

"Mtanielewa tu Insha Allah ngoja bomu lilipuke, labda Allah aniokoe lakini siku hizi tatu kutoka leo hesabu tu lazima niweke wazi" alisema Mzee Yussuf .


Sir Alex Ferguson afanyiwa upasuaji kwenye kichwa

$
0
0
Kocha wa zamani wa klabu ya Manchester United, Sir Alex Ferguson jana Mei 05, 2018 amefanyiwa upasuaji mdogo kwenye kichwa.

Kwa mujibu wa taarifa iliyotolewa na ukurasa rasmi wa Twitter wa klabu ya Manchester United, imeelezwa kuwa upasuaji huo unahusisha ubongo na umeenda salama.

Hata hivyo, hakuna taarifa rasmi kuhusu tatizo linalomsumbua Mzee Ferguson hadi kufanyiwa upasuaji huo.

Kufuatia hali hiyo, Mtoto wa Sir Alex aitwaye Darren Ferguson ambaye pia ni kocha wa klabu ya Doncaster jana alishindwa kuhudhuria mechi kati ya kalbu yake dhidi ya Wigan.

Hata hivyo, baadhi ya wachezaji wametoa pole kwa mzee Ferguson kufuatia taarifa akiwemo Robin Van Persie, Pepe Reina, Diego Forlan, Bacary Sagna na wengineo.

Watu 15 wapandishwa Kizimbani kwa kukosa vyoo

$
0
0
WANANCHI 15 wakazi wa Kijiji cha Gebailumbwa wilayani Longido, wamepandishwa kizimbani katika Mahakama ya Wilaya hiyo wakikabiliwa na makosa matatu likiwemo la kutokuwa na vyoo na kusababisha mlipuko wa ugonjwa wa kipindupindu.

Akisoma mashtaka hayo juzi mbele ya Hakimu Mfawidhi wa mahakama hiyo, Aziza Temu, Mwendesha Mashitaka wa Jeshi la Polisi wilayani humo, Anzulimu Mihella, alidai kuwa shitaka la kwanza na la pili linawakabili washtakiwa wote kwa pamoja.

Washtakiwa hao ni Oleulei Losinigi (50), Kirusu Taitai (48), Kelepu Kesonyi (35) Lazaro Parteye (38), Joshua Metui (20) Kamete Lemomo (25) Kimare Lamama (38) Lemomo Kokoyo (25) na Zacharia Kabamngasi (33).

Wengine ni Paulo Lemomo (30), Kaika Ngatete (55) Thimotheo Kibangasi (37) na Moko Tataya (75)

Alisema mnamo mwaka 2016 na Aprili 30, mwaka huu, washtakiwa hao kwa pamoja walitenda kosa kwa kukaidi amri halali ya kuchimba vyoo, jambo ambalo ni kinyume cha Sheria ya Afya ya mwaka 2009.

Alisema kosa la pili mnamo mwaka 2016 na Aprili 30, mwaka huu katika nyakati tofauti washtakiwa hao wakiwa wakazi wa kijiji cha Gebailumbwa walikataa kutii amri halali ya Afisa Afya ya kujenga choo ili kuepuka mlipuko wa ugonjwa wa kipindupindu, kinyume na kifungu cha 111 (1,2) cha Sheria ya Afya ya mwaka 2009.

Kosa la tatu linamhusu mshtakiwa namba mbili, Kirusu Taitai (48) ambapo ilielezwa kuwa mshtakiwa huyo akiwa mkazi wa Kijiji cha Gibailumbwa, alishawishi wanakijiji kukataa kuchimba choo jambo ambalo ni kosa na ni kinyume kanuni ya adhabu, kifungu cha 390 cha sura ya 16 kama ilivyofanyiwa marejeo mwaka 2002.

Washtakiwa hao waliokuwa wakiongozwa na mwanasheria wao, Nicholaus Senteu, walikana mashtaka na hakimu Aziza, alidai dhamana ipo wazi kwa kila mshtakiwa kuwa na mdhamini mmoja ambaye ni mtumishi wa umma mwenye kusaini bondi ya sh milioni 10 kila mmoja.

Awali wakili, Senteu, aliiomba mahakama iwapatie dhamana wateja wake yenye masharti nafuu itakayowafanya wakidhi vigezo vya masharti.

Hata hivyo, washtakiwa hao walishindwa kutimiza masharti ya dhamana na kurudishwa rumande katika Gereza Kuu la Kisongo jijini Arusha hadi kesi hiyo namba 38/2018 itakapotajwa tena Mei 16, mwaka huu.

Kutana na Mtabibu Mwenye KUBRI kutoka kwa ALLAH issa simba said Mtabibu wa Nyota za Binadamu na Dawa za Asili

$
0
0
Kutana na Mtabibu Mwenye KUBRI kutoka kwa ALLAH issa simba said Mtabibu wa Nyota za Binadamu na Dawa za Asili ya Africa Mwenye UWEZO Kubaini tatizo lako Pindi tu Utakapo Fanya Mawasilino Kupitia Wasaa Husika..JE UNASUMBULIWA NA Mapenzi? (Umeachwa na Umpendae,Awe Mume,Mke na Bado unampenda?Na Umejaribu Sehemu nyingi Bila Mafanikio?Wasilina na Maalim Hussein Ujione muujiza wa Papo kwa Papo..

anauwezo WA KURUDISHA MAHUSIANO NA KUIMARISHA NDOA YAKO NDANI YA SAA 12 TU. Umekimbiwa na Mumeo,mkeo au Mpenzi na anaishi na mtu mwingine? Muone akutatulie Anauwezo wa Hali ya Juu wa Kusambalatisha Mahusiano yao Endapo utafata Atakacho kuelekeza.
Atamfanya Atimize Ahadi zote kwa Muda Mfupi.


Issa simba said Anatumia Jina la Muhusika au Picha Kumaliza Tatizo lako..
Anatibu kwa Kutumia Vitabu vya QUR-AN Dawa za Asili za Africa,Dawa za Kiarabu na Majini.Anatafsiri Ndoto.

Kushinda BAHATI NASIBU, KUSAFISHA NYOTA. Mvuto wa Mwili na BIASHARA, Kinga ya Mwili,ZINDIKO za Nyumba.MIGUU Kufa GANZI.Kufungua KIZAZI kwa wale walio fungwa kwa njia za KISHIRIKINA. Anakupa Jini la Mali kwa yule anaehitaji Utajiri BILA MASHARTI. Nguvu za KIUME, Humaliza Kesi zilishindika ndani ya siku 14 tu..na mengi zaidi

Piga simu +255 622588038 au 0679119679 au +255 764318107

NB: TIBA KWA DINI ZOTE NA IMANI ZOTE...

Waumini Wampiga Mawe Askofu...Habari Zilizopo Katika Magazeti ya Leo Jumatatu ya May 7

$
0
0


Habari Zilizopo Katika Magazeti ya Leo Jumatatu ya May 7

KIMENUKA..Msanii Ali Kiba Aburuzwa Mahakamani

$
0
0
Mfanyabiashara  wa mitumba Hadija Hassan amefungua kesi ya madai ya matunzo ya mtoto dhidi ya msanii nguli wa muziki wa kizazi kipya, Ali Kiba maarufu kama King Kiba.

Katika kesi hiyo, Hadija anadai jumla ya Sh. milioni 1.41, ikiwamo Sh. 950,000 za ada na Sh. 460,000 za matumizi ya mtoto wa miaka mitano (jina limehifadhiwa kwa sababu za kisheria na kimaadili).

Hadija ambaye ni mfanyabiashara wa mitumba amefungua kesi ya madai hayo katika Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu, jijini Dar es Salaam akidai matunzo kwa mlalamikiwa ambaye ni mzazi mwenzie -King Kiba.

Kwa mujibu wa hati ya madai iliyowasilishwa mahakamani hapo, mlalamikaji anadai kuwa Januari, 2013 katika Hospitali ya Mikocheni, jijini Dar es Salaam alizaa mtoto wa kike ambaye baba yake ni mlalamikiwa.

Alidai kupitia hati hiyo kwamba mlalamikiwa anatakiwa kumhudumia mtoto huyo kwa mahitaji yote muhimu ikiwamo chakula, nguo, elimu na matibabu.

"Kutokana na Sheria ya Watoto ya mwaka 2009, mdaiwa anatakiwa kutoa huduma kila mwezi, chakula Sh. 150,000, matunda Sh. 50,000, chakula cha ziada Sh. 50,000, michezo na burudani za watoto Sh. 100,000, nguo Sh. 60,000 na matibabu Sh. 50,000 ambapo jumla ni Sh. 460,000," alidai mlalamikaji kupitia hati hiyo.

Aidha mlalamikiwa anatakiwa kulipa ada ya shule kwa muhula Sh. 950,000, na anadaiwa aliacha kutoa matunzo hayo kwa mtoto tangu Januari, mwaka huu hivyo anaiomba mahakama imwamuru mdaiwa kutoa matunzo hayo ya Sh. 460,000 kila mwezi na ada.

Pamoja na mambo mengine, mlalamikaji anaomba malipo ya kwanza yatolewe mapema baada ya hukumu, na pia anaiomba mahakama imwamuru King Kiba kumsomesha mtoto, kumnunulia nguo na matibabu ikiwamo kumtafutia bima ya afya.

Pia mlalamikaji anaomba mahakama imwamuru Kiba kulipa gharama za matunzo Sh. 460,000 kuanzia Februari 2017 mpaka siku itakapotolewa hukumu na gharama za kesi ziwe kwa mdaiwa.

Mbali na maombi hayo, Hadija anaomba mahakama itoe amri nyingine yoyote itakayoona inafaa kwa manufaa yake. Kesi imefunguliwa kwa msaada wa Kituo cha Wanawake cha Msaada wa Kisheria (WLAC).

Ali Kiba, ambaye jina lake la kuzaliwa ni Ali Saleh Kiba amefunguliwa madai hayo ikiwa ni siku chache tangu afunge ndoa iliyopendeza mjini Mombasa Kenya.
Viewing all 104789 articles
Browse latest View live




Latest Images